Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano ya April 3


Waziri Wa Madini Uganda Afurahishwa Na Usimamizi Wa Sekta Ya Madini Nchini

$
0
0
Na Greyson Mwase, Geita
Waziri wa Madini Nchini Uganda, Peter Lokeris ames    ema kuwa amefurahishwa na usimamizi wa sekta ya madini nchini Tanzania na kusisitiza kuwa Uganda bado itaendelea kutuma wataalam wake pamoja na wachimbaji wadogo wa madini nchini Tanzania kwa ajili ya kujifunza namna bora ya uchimbaji na uchenjuaji wa madini.

Lokeris aliyasema hayo jana tarehe 02 Aprili, 2019 mara baada ya kutembelea migodi ya wachimbaji wadogo na wa kati ya madini iliyopo Wilayani Geita Mkoani Geita, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku nne nchini Tanzania yenye lengo la kujifunza namna Tanzania ilivyofanikiwa katika Sekta ya Madini kupitia Wizara ya Madini hususan katika kuwasaidia wachimbaji wadogo wa madini.

Akiwa ameongozana na  ujumbe wa maafisa waandamizi kutoka Serikali ya Uganda pamoja na wawakilishi wa wachimbaji wadogo aliwasili mkoani Geita na kupokelewa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Geita ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Geita pamoja na Naibu Waziri wa Madini Nchini Tanzania, Stanslaus Nyongo.

Ziara hiyo pia ilihusisha wataalam kutoka Wizara ya Madini. Tume ya Madini, vyombo vya ulinzi na usalama vya mkoa pamoja na waandishi wa habari.

Akielezea hali iliyopelekea nchi ya Uganda kuichagua nchi ya Tanzania kama sehemu ya kujifunza kuhusu Sekta ya Madini, Lokeris alisema kuwa, baada ya kutanya  utafiti katika nchi za Aftika Mashariki, walibaini kuwa nchi ya Tanzania ni nchi iliyopiga hatua kubwa kwenye usimamizi wa sheria na kanuni za madini hali iliyopelekea wananchi wengi kunufaika nayo hususan wachimbaji wadogo wa madini.

Aliendelea kusema kuwa, Sekta ya Madini Nchini Uganda ndio inaanza kukua, hivyo wameona ni vyema kuja Tanzania  kwa ajili ya kujifunza na kwenda kuimarisha Sekta ya Madini ili baada ya miaka kadhaa angalau iwe inakaribiana na nchi ya Tanzania.

Akielezea mikakati ya matumizi ya uzoefu mkubwa ujumbe huo ilioupata kutoka kwa nchi ya Tanzania, Waziri Lokeris alisema hatua ya kwanza itakayofanywa na Serikali ya Uganda kupitia Wizara yake ya  Madini ni kuhamasisha wachimbaji wadogo wa madini kuunda vikundi na kuwapatia leseni.

Aliongeza kuwa, mara baada ya kuwapatia leseni hatua itakayofuata itakuwa ni kuwaleta Tanzania kwa ajili ya mafunzo ambapo watajifunza kupitia wachimbaji wadogo wa madini wa Tanzania waliofanikiwa kwenye shugfhuli za uchimbaji na uchenjuaji wa madini.

Aliendelea kueleza kuwa, nia ya Serikali ya Uganda kupitia Wizara yake ya Madini ni kuhakikisha sekta hiyo inakua kwa kasi na kuanza kuzalisha dhahabu na kuuza nyingine nje ya nchi na kujipatia mapato makubwa.

“Tumefurahishwa na usimamizi mzuri kwenye sekta ya madini hususan kwenye eneo la uwezeshaji wa wachimbaji wadogo, tumeona namna wanavyochenjua madini huku wakizingatia sheria na kanuni za mazingira,”alisisitiza Waziri Lokeris.

Naye Naibu Waziri wa Madini Nchini Tanzania, Stanslaus Nyongo akielezea mafanikio ya sekta ya madini nchini alieleza kuwa, mafaniko yaliyopatikana ni pamoja na uboreshaji wa sheria mpya ya madini pamoja na kanuni zake inayotambua madini kama mali ya watanzania na kusisitiza kuwa wachimbaji wadogo wamekuwa wanufaika kwa kiasi kikubwa.

Aliongeza kuwa, Serikali kupitia Wizara ya Madini imeondoa tozo mbalimbali zisizo za lazima hali iliyopelekea wachimbaji wadogo kuzalisha madini kwa gharama nafuu na kulipa kodi na tozo mbalimbali serikalini.

Alieleza mafanikio mengine kuwa ni pamoja na uanzishwaji wa masoko nchini kama njia mojawapo ya kudhibiti utoroshwaji wa madini kwa kuhakikisha wachimbaji wa madini wanakuwa na soko la uhakika la kuuzia madini yao kwa bei yenye faida.

Naye mmiliki wa mgodi wa  dhahabu wa Blue Reef uliopo katika eneo la Rwamgaza Wilayani Geita mkoani Geita ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Wachimbaji wa Madini Mkoa wa Geita (GEREMA), Christopher Kadeo akizungumza na  ujumbe huo uliofanya ziara kwenye mgodi wake akielezea mchango wa mgodi wake katika jamii iliyopo jirani alisema mgodi wake tangu ulipoanzishwa mwaka 1991 mpaka sasa umefanikiwa kuajiri watumishi 160 na vibarua takribani  200.

Alieleza mafanikio mengine kuwa ni pamoja na uboreshaji wa huduma za jamii kama vile afya, elimu, ulinzi kupitia ujenzi wa vituo vya polisi na kusisitiza kuwa mgodi umekuwa ukishirikiana kwa karibu zaidi na Tasisi nyingine za Serikali kama vile Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Chuo cha Madini Dodoma (MRI), Chuo Cha Ufundi Dar es Salaam (DIT), Wizara ya Madini, Tume ya Madini na mashirika mengine ya kimataifa.

Aidha, aliongeza kuwa mgodi wake umewahi kupewa tuzo ya utunzaji bora wa mazingira na Rais wa Awamu ya Tatu ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin Mkapa.

Akielezea mikakati ya mgodi wake kwenye shughuli za uchimbaji wa madini  alisema mgodi wake unatarajia kufanya utafiti zaidi ili kugundua madini zaidi na kuunganisha leseni zake tano unazomiliki na kutoka kwenye uchimbaji wa kati hadi mkubwa.

Serikali Kuendelea Kuimarisha Upatikanaji Wa Maji Safi Na Salama Nchini

$
0
0
Na; OWM (KVAU) - SONGWE
Serikali imedhamiria kuimarisha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi waishio mijini kufikia asilimia 95 na vijijini asilimia 85 ifikapo 2020.

Kauli hiyo imetolewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mama Samia Hassan Suluhu wakati wa uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Aprili 2, 2019 zilizofanyika uwanja wa Kimondo – Forest Mlowo, Wilaya ya Mbozi, Mkoani Songwe.

Kauli mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu 2019 isemayo “Maji ni Haki ya kila Mtu, Tutunze Vyanzo Vyake na Tukumbuke Kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa”

Makamu wa Rais amesema kuwa dhamira ya Serikali inayoongozwa na Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ni  kuboresha huduma za jamii ikiwemo sekta ya elimu, afya, barabara,  umeme vijijini, usafiri wa anga, uvuvi, kilimo, viwanda na upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wote.

“Sera yetu ya Maji ya mwaka 2002 inasisitiza upatikanaji wa maji safi na salama ambayo ni muhimu kwa maisha ya kila mtu, shughuli za kiuchumi na ustawi wa mazingira,” alisema Makamu wa Rais.

Akizungumzia kuhusu upatikanaji wa maji safi, alieleza kuwa Serikali inaendelea kutekeleza ujenzi wa miradi mbalimbali ya maji nchini ikiwemo mabwawa ya kimkakati na kuboresha miundombinu ya uzalishaji na usambazaji maji safi.

Aidha, Makamu wa Rais alitoa wito kwa Wananchi kuhakikisha wanatunza vyanzo vya maji kwa kuacha kufanya shughuli za kibinadamu kando ya vyanzo hivyo.

Kupitia hadhara ya Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Makamu wa Rais, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi na kushiriki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao ni muhimu katika kuleta maendeleo ya watu na huduma za kijamii.

Awali Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama alisema kuwa Mwenge wa Uhuru ndio msingi mkubwa wa amani, Mshikamano, Uzalendo na Umoja tulionao katika Taifa.

“Tunu hii imekuwa ni kichocheo cha maendeleo kwa wananchi na wamekuwa wakihamasika kushiriki katika kuandaa na kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo ikiwemo ya kijamii na kiuchumi iliyopo katika maeneo yao,” alisema Mhagama.

Waziri Mhagama aliongeza kwa kuwashukuru wadau mbalimbali waliosaidia kufanikisha tukio hilo muhimu la Kitaifa.

Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Brigedia Jenerali (Mst.), Nicodemus Mwangela alishukuru Serikali kwa kuchagua Mkoa wa Songwe kuwa wenyeji wa Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa mwaka 2019.

Afikishwa Mahakamani Kwa Makosa Ya Kughushi Vyeti Vya Taaluma

$
0
0
Na Amiri kilagalila
Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoa wa Njombe,imemfikisha katika mahakama ya hakimu mfawidhi wilaya ya Makete Bi.HONORATHA MWINUKA katibu muhtasi halmashauri ya wilaya ya Makete na kumfungulia kesi na CC.11/2019 kwa makosa ya kughushi vyeti vya taaluma chini ya sheria ya kanuni ya adhabu kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kaimu mkuu wa Takukuru mkoa wa Njombe CHARLES MULEBYA  amesema kuwa mshtakiwa kwa lengo la kujipatia ajira kama katibu muhtasi alighushi vyeti vya taaluma akionyesha kuwa alisoma kozi ya ukatibu muhtasi katika chuo cha utumishi wa umma (TPSC) Dar es salaam.

Ambapo alihitimu na kupewa cheti cha kumaliza kozi hiyo na kile cha matokeo huku akijua hajawahi kujiunga na chuo hicho wala kuhitimu kozi ya ukatibu muhtasi.

Mulebya amesema kitendo cha mshtakiwa  kughushi vyeti ni kinyume na K/F cha 333,335(a)337 na 342 vyote vya sheria ya kanuni ya adhabu kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Aidha amesema kesi dhidi ya mshtakiwa ipo mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Makete Mh.Jonathan Mpitanjia.

Pierre Liquid atua Bungeni Dodoma

$
0
0
Peter Mollel maarufu Pierre Konki Liquid leo Jumatano April 3, 2019  yuko ndani ya ukumbi wa Bunge tayari kwa kushuhudia wabunge wakiendelea na kikao cha pili cha mkutano wa Bunge la Bajeti, jijini Dodoma leo.

Tazama hapo chini alivyopokelewa na Spika wa Bunge Job Ndugai na Naibu Spika Dr Tulia Ackson

LIVE: Rais Magufuli Akiendelea na ziara ya kikazi Mtwara

$
0
0
LIVE: Rais Magufuli Akiendelea na ziara ya kikazi Mtwara

Kauli ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Mussa Assad Baada ya Bunge Kugoma Kufanya Naye Kazi

$
0
0
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Mussa Assad amsema suala la Bunge kufikia uamuzi wa kutofanya naye kazi ni jambo zito ambalo linahitaji tathimini na kutazama athari zake.

Amesema kuwa maamuzi yakifanyika bila kuangalia athari zake yanaweza kuleta tatizo kubwa siku za baadaye.

Profesa Assad amesema hayo leo Jumatano Aprili 03, 2019 wakati akizungumza na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kwa njia ya simu.

“Nafikiri ni jambo zito sana hilo na kama nilivyosema tunahitaji tathimini kali kutazama athari zake ni zipi,” amesema na kuongeza “tukifanya maamuzi ambayo hatujatazama athari zake linaweza kuwa tatizo kubwa zaidi badala ya kupata solution,”

“Mi nafikiri tukae chini tutazame, halafu tuone athari ni zipi ili kuepuka matatizo ambayo tunaweza kuyasababisha… wasiwasi wangu ni kwamba huenda linaweza likaja kuwa tatizo kubwa zaidi kuliko linavyoonekana sasa hivi.”

Profesa Assad ametoa rai kuwa hansadi ya maswali na majibu kutoka katika mahojiano yake pamoja na Kamati ya Bunge ya Maadili iwekwe wazi ili kila Mtanzania ajue nini kilichozungumzwa baada ya kuitwa na kamati hiyo.

“Rai yangu ni kwamba ile hansadi ya Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge iwekwe wazi kwa kila mtu ili kila mtu ajue nimeulizwa kitu gani na nimejibu kitu gani,” amesema nakuongeza “ili kila Mtanzania aweze kuweka tathimini yake, halafu aweze kupima kuwa hili lilipofikiwa ni sawa au sio sawa.”

Creditr: Mwananchi

Jumla Ya Tsh.bilioni 10 Zimetumika Katika Ujenzi Wa Mabweni Mapya Udsm[magufuli Hostel]

$
0
0
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha, amelihakikishia Bunge kuwa ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yajulikanayo kama hosteli za Dk. John Magufuli uligharimiwa na serikali kwa Sh. bilioni 10.

Ole Nasha aliliambia Bunge jana alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Susan Lyimo, aliyetaka kujua ni kiasi gani kilitumika kujenga mabweni hayo.

Akijibu swali hilo, Ole Nasha, alisema mradi wa ujenzi wa mabweni hayo ulianza rasmi Julai mosi, 2016 na mabweni hayo yalikamilika na kukabidhiwa rasmi Aprili 15, 2017.

"Ujenzi huo ulifanywa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), kama mkandarasi na kusimamiwa na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa," alisema.

Katika swali lake la nyongeza, mbunge huyo alisema gharama hiyo iliibua mjadala na waliomba Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), afanye ukaguzi.

"Ni jengo gani la ghorofa nne linaweza kugharimu milioni 500 tu, nilitaka kujua baada ya miezi minne yalikuwa na nyufa nyingi, lakini nyufa zilianzia kwenye msingi hadi kwenye madirisha, ni kwanini yalikuwa na nyufa hizo," alihoji. Aidha, alihoji ni gharama kiasi gani imetumika.

Akijibu maswali hayo, Ole Nasha alisema, mkandarasi aliyejenga alifanya marekebisho ya nyufa hizo na hakuna fedha za ziada zilizotolewa.

"Nimhakikishie jengo limegharimu Sh. bilioni 10, sasa kama yeye anapingana na huu ukweli niliomweleza alete gharama zake, kwa kuwa hizi ni fedha za umma na zimetumika kwa utaratibu, hakuna fedha nyingine iliyotumika zaidi ya hizo," alisema.


Ahukumiwa Miaka 30 Jela Kwa Kumbaka Mwanafunzi na Kumpa Ujauzito

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mbeya, imemhukumu adhabu ya kifungo cha miaka 30 jela na kuchapwa viboko 12 mfanyabiashara Anthony Mandawa (58), baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka mwanafunzi na kumsababishia ujauzito.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mkoa wa Mbeya, Rashid Chengula, alisema Mandawa alitenda kosa hilo Februari mwaka jana na mahakama imeridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka.

Hakimu Chengula alisema mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo kwa kumbaka mwanafunzi wa kidato cha kwanza aliyekuwa akisoma shule ya Upili Samora na kumsababishia ujauzito huku akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Alisema Jamhuri kupitia mashahidi wake, akiwamo muathirika wa tukio hilo bila kuacha shaka, mfanyabiashara amefanya makosa yote mawili hivyo kumtia hatiani na kumpatia hukumu hiyo.

Awali katika utetezi wake, mshtakiwa Mandawa alikana kutenda kosa hilo, huku akikosoa mwenendo wa shauri hilo kwa madai kuwa muathirika alichelewa kutoa taarifa akidaiwa kuripoti baada ya siku 30.

Aidha, alidai kuwa yeye (mshtakiwa) ni muathirika wa ugonjwa wa Ukimwi na kujitetea kuwa mwanafunzi anayedaiwa kubakwa hajaathirika hivyo mahakama inathibitishaje kama kweli alimbaka.

Hata hivyo, mahakama ilisema utetezi wa mshtakiwa hauna mashiko ya kutomtia hatiani.

Shauri hilo lilikuwa likiendeshwa na mawakili wawili wa serikali, Davice Msanga ambaye aliiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali dhidi ya mshtakiwa ili iwe fundisho kwake na kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, mshtakiwa Mandawa, ambaye ni mfanyabiashara na mkazi wa Isanga, alishtakiwa na Jamhuri kwa makosa mawili ya kumbaka mwanafunzi wa kidato cha kwanza kinyume na kifungu namba 130 (2) e na 131 (1) ya kanuni ya adhabu.

Kosa la pili ni kumsababishia ujauzito mwanafunzi huyo, kinyume na kifungu namba 60 A (3) cha Sheria ya Elimu sura ya 353 na marekebisho yake kifungu namba 22 (3) cha sheria namba 2 ya mwaka 2016.

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Chengula, alisema mshtakiwa anahukumiwa kifungo cha miaka 30 jela na kuchapwa viboko 12 kwa kosa la kwanza ikiwa ni pamoja na kulipa faini ya Sh.milioni mbili.

Kosa la pili mtuhumiwa huyo alihukumiwa kutumikia jela miaka 30 kwa kosa la kumsababishia ujauzito mwanafunzi huyo, ambaye pia amemsababisha akatishe masomo yake na vifungo hivyo aliviamuru kwenda pamoja.

Jeshi La Polisi Mkoa Wa Kigoma Limefanikiwa Kuuwa Majambazi 24, Kukamata Silaha 14 Aina Ya Smg Na Risasi 350.

$
0
0
Jeshi la Polisi Tanzania limeendesha Operesheni sehemu mbalimbali za nchi ili kupambana na wahalifu waliokuwa wanavamia majumani na kuteka magari njiani kwa kutumia silaha za moto.

Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi Nchini  CP, Liberatus Sabas amesema operesheni hiyo iliyofanika katika Mkoa wa Kigoma imefanyika ndani ya miezi mitatu ambayo ilianza mwezi wa kwanza mpaka mwezi wa tatu mwaka huu na kufanikiwa kukamata silaha 14 aina ya SMG na risasi 350 pamoja na mafanikio hayo Jeshi la Polisi limefanikiwa kuua majambazi 24 katika majibizano ya kurushiana risasi na polisi ambapo katika mapambano hayo askari wawili walijeruhiwa na majambazi ila mpaka sasa wanaendelea na matibabu.

Aidha kamishna Sabas, amesema wahalifu hao wanaotoka nchi za jirani ambazo hazina utulivu wa kisiasa, huku akiwaonya wahalifu hao wanaotoka  nchini jirani kuwa wajue wataingia ila hawatatoka na wakae wakijua hakuna mwalifu atakaebaki salama pia akiwataka wale wanaoingia nchini kwa kutumia miamvuli ya wakimbizi na wao hawatakuwa salama kwani wakae wakijua Tanzania ni kisiwa cha amani.

Kamishna Sabas amewataka  wananchi kuendelea kutoa ushirikiano baina yao na Jeshi la Polisi ili kukabiliana na wahalifu wa ndani na wale wanaotoka nje ya nchi na kuwatumia salamu kuwa Tanzania si sehemu salama kwa wahalifu.

Rais Magufuli Akerwa na Wakandarasi Wasiofanya Kazi Zao Vizuri na Kwa Wakati

$
0
0
Rais John Magufuli amewajia juu wakandarasi wasiofanya kazi zao vizuri na kwa wakati na kuitaka Wizara ya Ujenzi kuwachukulia hatua za kisheria ikibidi wafukuzwe kazi kwani wameifanya Tanzania ni nchi ya majaribio.

Ametoa kauli hiyo leo jumatano Aprili 3, wakati akizungumza na wananchi katika ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani Mtwara ambapo ameweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa Barabara kutoka Mtwara -Newala – Masasi yenye urefu wa kilomita 210.

“Wakandarasi mliosajiliwa katika nchi hii mbadilike na wizara muendelee kutumia sheria namba 17 ya mwaka 1997 na wale wasiofanya kazi vizuri wafukuzwe Tanzania isiwe nchi ya majaribio, Oktoba nitatenga muda kuja kuangalia kama huu mradi umekamilika na ole wenu nikute haujakamilika tutazungumza lugha nyingine.

“Tunataka lami na nikuombe Waziri pamoja na kazi nzuri mnayoifanya katika bajeti ya mwaka huu muhakikishe mnatangaza kilomita nyingine 50 kwenda mbele na mwaka mwingine tena 50 au 100 itategemeana fedha tutakazokuwa nazo,” amesema

Aidha amewataka wananchi wa Mtwara kudumisha amani na mshikamamo kati yao na kuachana na tabia ya kubaguana ili waweze kusaidiana kukuza uchumi wa nchi kwa kufanya kazi kwa pamoja.

“Tukishakuwa na miundombinu mizuri, umeme na maji Mtwara patakuwa ni mahali ambapo kila mtu atataka kupakimbilia endeleeni kuwa na mshikamano msibagueni kwaajili ya vyama wala dini mimi ni rais wa wote lengo ni kupeleka maendeleo ya nchi mbele,” amesema

Rais Magufuli atoa onyo kwa Wakurugenzi

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amewaonya Wakurugenzi ambao watanaoesha nia kudai ushuru kufuatia uamuzi wa Serikali, kununua zao la korosho kwa bei elekezi ya shilini 3300, baada ya mvutano wa muda mrefu baina ya wakulima na wafanyabiashara wa korosho.
 
 Magufuli ametoa kauli hiyo akiwa mkoani Mtwara wakati akizungumza kwenye uzinduzi wa uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa barabara kutoka Mtwara kuelekea Newala na Masasi, ambapo amesema serikali haiwezi kuamua kuwasaidia wananchi halafu Halmashauri ijitokeze kutaka ushuru.
 

"Halmashauri mmeshindwa kusimamia korosho, baada ya kupewa bei nzuri wanapewa 1500, tukasema hapana tukakopa ili tuwalipe, nione Mkurugenzi ananiomba hizo hela, aone kama ataendelea kuwa Mkurugenzi, utaombea kijijini ukiwa unalima".
 

"Haiwezi Serikali imepanga bei ya korosho 3300, halafu ianze kulipia kodi kwenye Halmashauri ambayo ilishindwa kununua korosho, mkitaka ushuru msimamie vizuri bei ya korosho, siwezi nikakusanya hela mikoa mingine nije niwalipe nyinyi."Amesema Rais Magufuli

Rais wa Algeria Bouteflika atangaza kujiuzulu

$
0
0
Rais wa Algeria Bouteflika (82) ambae anatumia wheelchair kutembelea amejiuzulu wadhifa wake baada ya kukaa madarakani kwa miaka 20, hatua hiyo inakuja baada ya Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Algeria Ahmed Gaid Salah kumtaka Rais huyo ajiuzulu haraka iwezekanavyo.

Kulikuwa na shangwe na vifijo kwenye mji mkuu Algiers baada ya kutangazwa uamuzi huo jana usiku. Televisheni ya taifa ilitangaza kuwa Bouteflika alilishauri rasmi Baraza la Katiba kuwa anaachia madaraka kama Rais wa Algeria. 

Alisema uamuzi huo uliochukuliwa kwa dhati unalenga kuchangia katika kuituliza mioyo na fikra za Waalgeria, na kuwawezesha kuiongoza Algeria kuwa na mustakabali mzuri na ambao wana haki ya kuufanikisha. 

Video ilimuonyesha Bouteflika, akiwa kwenye kiti cha walemavu, akikabidhi barua yake ya kujiuzulu kwa mkuu wa Baraza la Kikatiba Tayeb Belaiz.

Waziri Mkuu Amuahidi tiketi ya ndege Pierre Konki Liquid kwenda kuishabikia Taifa Stars AFCON

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa Pierre Liquid ataambatana na Timu ya Taifa, Taifa Stars katika fainali za AFCON zitakazofanyika nchini Misri.

Amemhakikishia hilo wakati akizungumza naye katika Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma, ambapo Piere alikwenda kutembelea kwa mwaliko wa Spika wa Bunge, Job Ndugai.

Hayo yanajiri ikiwa zimepita siku kadhaa tangu Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda kutoa kauli ya kukosoa tabia ya watu kuvipa muitikio mkubwa vitu visivyo na msingi, akitolea mfano Mchekeshaji huyo aliyejizolea umaarufu kwenye vyombo vya habari pamoja na mitandao ya kijamii.

Katika hafla iliyoandaliwa na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo ambayo ilikuwa na malengo ya kutokomeza ziro katika wilaya hiyo, Makonda alisema kwamba watu wa 'hovyo' kama Pierre hawapaswi kupewa nafasi kwenye vyombo vya habari, hali iliyozua gumzo kubwa.

Spika Ndugai Aanika Madeni ya Mbunge Godbless Lema.....Amtimua Mbunge wa CHADEMA

$
0
0
Spika Job Ndugai ameagiza Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA), afike mbele ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge leo saa 8:00 mchana kujibu tuhuma zinazomkabili za kulidharau na kulidhalilisha Bunge

Spika amesema kuwa Bunge analoliongoza si dhaifu na yeyote atayeingia kwenye 18 zao anaalikwa kwenye mchezo huo.

Aidha, asemema huwa Mbunge huyo wa Arusha Mjini ana msongo wa mawazo kwani tangu aingie Bungeni, amekopa Tsh. Milioni 644.

 
“Yapo mambo ambayo hawasemi wacha tuseme kidogo amekopa Sh 644 milioni…Sasa hivi ameshalipa lipa zimefika Sh 419 milioni huu ni msongo wa mawazo ndio maana anafika mahali anajilipua tu na kadhalika,”amesema.

Katika hatua nyingine amemfukuza ndani ya Ukumbi wa Bunge, Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko(CHADEMA) baada ya kupiga kelele kumpinga kiongozi huyo kutaja deni la Lema.

Spika Ndugai kuwataja wabunge waliotelekeza watoto

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai, amesema anayo orodha ya baadhi ya wabunge waliotelekeza watoto hivyo amewataka wahusika kulimaliza suala hilo kabla hajawataja.

Spika Ndugai ametoa kauli hiyo bungeni leo wakati wa kipindi cha maswali na majibu mara baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola kujibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Tauhida Galloos (CCM), aliyetaka kujua Serikali ina mkakati gani juu ya raia wa kigeni wanaopewa vibali vya kuja kufanya kazi nchini kwa muda na kuwazalisha watoto.

Akijibu swali hilo Lugola amesema sheria tayari ipo hivyo aliwaomba kina mama ambao wamekimbiwa wafuate sheria.

“Sheria tayari tunayo, niwaombe kina mama wote ambao wameathirika na jambo hili kwa kuwa ni la jinai waende katika vituo ambavyo vipo jirani wafungue kesi ili serikali tutumie kesi hizi kuwarejesha nchini wajibu mashtaka,” amesema Lugola.

Baada ya kujibu swali hilo, Spika Ndugai alisem; “Nakubaliana kabisa na maneno ya Waziri wa Mambo ya Ndani kwa asilimia 100 na mimi nishuhudie ninayo mawasiliano kadhaa ya kina mama kutoka sehemu mbalimbali za nchi wakiwalalamikia wabunge wanaume kutelekeza watoto.

“Naomba kila anayehusika na jambo hili achukue hatua ipo siku hapa nitakuja na orodha patakuwa hapatoshi hapa,” amesema Spika Ndugai

Serikali Yasema Mzunguko wa Fedha Katika Soko Uko Imara

$
0
0
Na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Serikali imesema kuwa kwa sasa nchi haina tatizo la mzunguko mdogo wa fedha katika soko kutokana na hatua mbalimbali ilizozichukua kukabiliana na tatizo hilo ikiwemo kuongeza ukwasi kwenye uchumi.

Hayo yameelezwa leo Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Momba Mhe. David Silinde (Chadema), aliyetaka kujua sababu za mzunguko mdogo wa fedha.

Dkt. Kijaji alisema kuwa, katika kutatua changamoto ya kupungua kwa mzunguko wa fedha katika soko, Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ilichukua hatua  mbalimbali za kuongeza ukwasi kwenye uchumi ikiwemo kushusha riba ya Benki Kuu (discount rate) kutoka asilimia 16 kwa mwezi Machi, 2017 hadi asilimia 7, Agosti 2018.

“Benki Kuu ilipunguza kiwango cha kisheria cha sehemu ya amana kinachotakiwa kuwekwa Benki Kuu na mabenki ya biashara(Statutory Minimum Reserve Requirement, (SMR)) kutoka asilimia 10 hadi asilimia 8 mwezi April 2017 pamoja na kuruhusu mabenki kutumia asilimia 10.0 ya sehemu ya SMR kama chanzo kimojawapo cha kusaidia hali ya ukwasi kwenye uchumi”, alisema Dkt. Kijaji.

Alisema Benki Kuu ilianzisha utaratibu wa kutoa mikopo ya muda maalumu kwa mabenki pamoja na kununua fedha za kigeni kutoka kwenye soko la jumla la mabenki ili kuongeza ukwasi kwenye uchumi.

Alifafanua kuwa mzunguko wa fedha katika uchumi unaendana na malengo pamoja na mahitaji halisi ya shughuli za kiuchumi zizopo kwa sasa.

Aidha, Dkt. Kijaji alisema Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania inatekeleza Sera ya Fedha inayolenga kusimamia mzunguko wa fedha unaoendana na mahitaji halisi ya uchumi kwa lengo la kudumisha utulivu wa mfumuko wa bei na hivyo kuweka mazingira mazuri ya ukuaji wa uchumi.

Tamko la Rais Magufuli Latekelezwa....Wazabuni Walipwa Bilioni 199

$
0
0
Na Farida Ramadhani na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Serikali imeleeza kuwa imeshawalipa Wazabuni 2048 kiasi cha Shilingi 199bilioni tangu kutolewa kwa tamko la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 3 Januari, 2018 Ikulu Jijini Dar es Salaam la kutaka Wazabuni wote wanaoidai Serikali walipwe.

Hayo yameelezwa Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa (CCM), Mhe. Ritta Kabati, aliyetaka kujua baada ya tamko la Mhe. Rais kuhusu Wazabuni wote wanaoidai Serikali walipwe ni Wazabuni wangapi wameshalipwa.

Akijibu swali hilo Dkt. Kijaji alieleza kuwa kati ya Wazabuni 2048 waliolipwa na Serikali, Wazabuni 1,277 walihudumia Sekretarieti za Mikoa na 771 walihudumia Wizara, Taasisi na Wakala za Serikali.

Dkt. Kijaji alifafanua kuwa Shilingi 3,729,605,175 zimetumika kulipa Wazabuni waliotoa huduma kwa Sektretarieti za Mikoa na Shilingi 195,334,409,791.64 zimetumika kulipa Wazabuni wa Wizara, Taasisi na Wakala za Serikali.

“Ikumbukwe kuwa madeni yote haya yalilipwa baada ya uhakiki  kufanyika”, alisisitiza Dkt. Kijaji.

Aliongeza kuwa Serikali itaendelea kulipa madai mbalibmali ya wazabuni kulingana na upatikanaji wa fedha, sambamba na uhakika wa madai husika.

Dkt. Kijaji amesema kuwa  ili kukamilisha zoezi la uhakiki kwa wakati, wazabuni wote wanatakiwa kutoa ushirkiano, hususan kuwasilisha taarifa na vielelezo sahihi vya madai yao pindi wanapotakiwa kufanya hivyo.

Katika swali la nyongeza Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Kabati alitaka kujua vigezo vilivyotumika kuwalipa wazabuni hao.

Akijibu swali hilo la nyongeza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji alisema kuwa vipo vigezo vingi ambavyo Serikali imevitumia kulipa madeni hayo moja ikiwa umri wa deni, madeni ambayo yamekaa kwa muda mrefu na ambayo tayari yamehakikiwa ndiyo yanapewa kipaumbele katika malipo.

Aliongeza kuwa kigezo cha pili ni riba Serikali imekuwa ikitoa kipaumbele kwa madeni ambayo riba yake inakuwa kulingana na muda, ili Serikali isiendelee kuumia wala mwananchi asiendelee kuumia.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamis April 4

Makamu Wa Rais Kufungua Kongamano La Pili La Maadhimisho Ya Kumbukumbu Ya Hayati Sheikh Abeid Amani Karume Leo

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan leo Alhamisi tarehe 4, Aprili 2019 atakuwa mgeni rasmi katika Kongamano la Pili la Maadhimisho ya kumbukumbu ya Rais wa Kwanza wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Kwanza wa Baraza la Mapinduzi Hayati Sheikh Abeid Amani Karume. 
 
Mada kuu ya Kongamano hili ni “Uhai wa Fikra za Falsafa za Abeid Amani Karume katika Zanzibar ya leo”.
 
Kongamano hilo limeandaliwa na Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na litafanyika kwenye Kampasi ya Zanzibar Bubu ambapo baada ya Makamu wa Rais kufungua Kongamano hilo atatunuku zawadi kwa washindi wa Insha.
 
Aidha baada ya ufunguzi kutaendeshwa mada mbali mbali zitakazotolewa na Mhe.Dkt. Saada Mkuya Salum na Mhe.Ayoub Mohammed Mahmoud

Imetolewa na:
Ofisi ya Makamu wa Rais
Zanzibar
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>