Mwili wa Sista baada ya kupigwa risasi.
Majambazi watatu wamemuua kwa kumpiga risasi kichwani Mhasibu
wa Kanisa Katoliki, Usharika wa Makoka, jijini Dar es Salaam, Sista
Prisencia Kapuli na kisha kumpora fedha zinazokadiriwa kuwa zaidi ya Sh milioni
10 alizokuwa nazo.
Tukio hilo ni la jana saa 9 alasiri katika
eneo la Ubungo Riverside wakati Prisencia, mtawa mwenzake pamoja na dereva
Majambazi Yamuua Sista wa Kanisa Katoliki kwa Risasi jijini Dar na kisha Kupora Fedha
↧
↧
Mbowe avitaka Vyama Vinavyounda UKAWA Vijiimarishe Kivyake pasipo kutegemea nguvu ya chama kingine
Vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vikiwa na matumaini ya kuunganisha nguvu katika uchaguzi mkuu ujao, vimeambiwa kila kimoja kijiimarishe kivyake katika mapambano ya kisiasa.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe, amesema vyama hivyo, visitegemee nguvu ya umoja huo badala yake, vijiimarishe kuleta ushindani katika harakati zao za
↧
Sakata la Kanga Moko Kupigwa Risasi: Mama Mazazi wa Mabinti hao Asimulia mkasa Mzima
Mama mzazi wa binti aliyesababisha wasichana wawili kujeruhiwa kwa
kupigwa risasi na polisi baada ya kushiriki ngoma maarufu ya Kanga Moko
iliyopigwa marufuku, huko Mwananyamala Kisiwani jijini Dar es Salaam,
amefunguka na kusema kuwa hakukuwa na sherehe yoyote nyumbani kwake siku
hiyo ya tukio.
Mama huyo, Rehema Aziz alisema waliojeruhiwa walikuwa wakisherehekea
kuolewa kwa mwanaye
↧
Mikutano ya Nape Nnauye yapigwa Marufuku Mtwara.......Alalamika na kusema huko ni kubaka demokrasia
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye ameonja chungu
ya uamuzi wa Serikali wa kusitisha mikutano ya hadhara katika mikoa ya
Lindi na Mtwara baada ya kushindwa kufungua mashina ya chama hicho mjini
Mtwara.
Nape ambaye alikuwa mkoani Mtwara kwa ziara ya
siku moja, alijikuta akiishia kuwakabidhi bendera za chama hicho
viongozi wa matawi ili wakazipandishe wenyewe kimyakimya.
↧
Flora Mbasha na Mumewe Waanza Kusaka Suluhu ya Ugomvi wao baada ya kukubali kukutanishwa ili kumaliza Ugomvi
Kuna kila dalili kwamba mwimbaji maarufu wa muziki wa Injili
nchini, Flora Mbasha na mumewe Emmanuel Mbasha wanatamani kurudiana,
baada ya kuwapo mgogoro katika uhusiano wao wa ndoa, ulioingia katika
vyombo vya habari yapata mwezi mmoja sasa.
Kwa nyakati tofauti jana, kila mmoja wao
alimwambia mwandishi wetu kwamba yupo tayari kurudiana na mwenzake,
hatua ambayo inaweza kuondoa
↧
↧
Mchungaji Adaiwa Kumtorosha Mwanamke
Mchungaji mmoja wa kanisa la kiroho la Biblical
lililopo Kinondoni jijini Dar es Salaam (jina tunalo), anadaiwa
kumtorosha mwanamke aitwaye Catherine Paul (28) ambaye ni mfanyabiashara
wa duka Tegeta jijini Dar.
Habari zinadai kuwa, wakati akiendelea na biashara hiyo, Catherine alipata ugonjwa wa ajabu ambapo alionekana mnyonge.
“Tunasikia alimshirikisha rafiki yake wa karibu, Victor
↧
AJIRA: Haya ni Majina ya Walimu Wapya ( na vituo vya kazi ) waliohitimu vyuo vya Ualimu mwaka 2013 ambao hawakubahatika kupangiwa hapo awali
Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI imewapangia vituo vya kazi ya ualimu walimu waliohitimu Vyuo vya Ualimu Mwaka 2013 kuchukua nafasi za walimu ambao hawakuripoti katika vituo walivyopangiwa kwa ajira ya Machi 2014.
Baadhi ya waombaji hawakupangiwa vituo vya kazi kutokana na kutokuwa na sifa zinazostahili kuajiriwa katika utumishi wa umma kwa mfano:- umri na maombi kutoambatanishwa na
↧
Majina ya Wanafunzi waliomaliza Kidato cha Nne na Kuchaguliwa Kujiunga na Vyuo vya Ufundi 2014
Uchaguzi wa wanafunzi wa kuingia Kidato cha Tano katika shule za
Serikali na Vyuo vya Ufundi kwa mwaka 2014 umekamilika.
Uchaguzi
umefanyika kwa kuzingatia takwimu za matokeo ya watahiniwa waliofanya
Mtihani wa Kidato cha Nne Tanzania Bara mwaka 2013.
Yafuatayo ni Majina ya Wanafunzi waliomaliza Kidato cha Nne na Kuchaguliwa Kujiunga na Vyuo vya Ufundi 2014
----------
↧
Mauaji Mengine yawakuta Wakenya.....Watano wamevamiwa na kuuawa usiku wa kuamkia leo
Takriban watu watano wameuawa katika shambulizi jingine katika eneo la pwani ya Kenya usiku wa kuamkia leo.
Mauaji hayo yametokea karibu na eneo ambako
mashambulizi mengine yalifanyika wiki jana na kusababisha vifo vya watu
zaidi ya sitini
Maafisa wanasema kuwa kundi la watu waliokuwa wamejihami walivamia
kijiji cha Witu ambacho kiko umbali wa kilomita 15
↧
↧
Magazeti ya Leo Jumatano ya tarehe 25 June 2014
↧
Mwanamke aliyehukumiwa Kifo Baada ya kukubali kuolewa na Mkristo nchini Sudan Akamatwa tena ikiwa ni masaa machache tu baada ya kuachiwa huru
Meriam akiwa na mwanaye Maya,
kushoto ni mumewe Daniel Wani aliyempakata mtoto wao wa kiume Martin na
wadau waliopigania mama huyo kuachiwa huru kabla ya kukamatwa tena
***
Mwanamke Meriam Ibrahim aliyeachiwa huru juzi baada ya kuhukumiwa
kifo kwa kosa la kuolewa na mwanamume mkristo na kukana dini ya
kiisilamu amekamatwa tena akiwa na mumewe pamoja na watoto wawili katika
uwanja wa
↧
Polisi Yatangaza Msako Mkali kwa watu waliomuu Sista wa Kanisa Katoliki....Msako huo utahusisha Traffiki Wote,Askari wa doria, Wapelelezi na Askari wa kawaida
POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam imeanzisha msako mkali, kuwatafuta watu waliohusika na mauaji ya Mhasibu wa Kanisa Katoliki Parokia ya Makoka jijini Dar es Salaam, Sista Cresencia Kapuri (50), ambao utahusisha vikosi vyote vya Polisi. Vikosi hivyo ni Usalama Barabarani, askari wa doria wanaotumia pikipiki na magari, wapelelezi na askari Polisi wa kawaida.
Mauaji ya mtawa huyo,
↧
Serikali Yajibu hoja ya Ukosefu wa Ajira Nchini.....Yatumia Mawaziri wanne kujibu Mapigo, yawataka wapinzani kuacha Uchonganishi
SERIKALI imetoa ufafanuzi kuhusu tatizo la ajira nchini, huku wanasiasa waliozungumzia tatizo hilo kuwa ni bomu, wakitakiwa kutoa ushauri wa namna ya kulitegua au kupunguza athari zake kama likilipuka.
Mbali na ushauri huo, Serikali pia imewataka wanasiasa wanaotumia tatizo hilo kisiasa, kuonesha mfano wa kusaidia vijana katika majimbo yao kwanza, badala ya kusubiri siku wakipewa nchi.
↧
↧
Kajala Masanja: Sina hamu ya kuendelea kuishi Tanzania
Staa wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja amefunguka kuwa yuko Bongo
kwa kuwa ndipo nyumbani kwao lakini hana hamu ya kuendelea kuishi nchini
kutokana na kuzushiwa mambo kila kukicha.
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko wikiendi iliyopita, mwigizaji huyo
alisema anapenda awe na maisha ya furaha na wanawake wenziye kwa
kubadilishana mawazo ya hapa na pale lakini kwa sasa hana upendo huo
↧
CHADEMA yakumbwa na Majanga tena...Vigogo 82 wawatolea Uvivu Mbowe na Slaa, Madai ya Ufisadi kufikishwa kwa msajili wa vyama
BAADA ya kujaribu kuficha migogoro nyuma ya kichaka cha Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), hatimaye bundi wa migogoro ameibuka tena ndani ya CHADEMA.
Kwa muda mrefu sasa, kumekuwemo mvutano kutokana na kile kinachodaiwa ukiukwaji wa Katiba na matumizi mabaya ya madaraka na fedha za chama.
Hatua hiyo ilisababisha baadhi ya viongozi wakiwemo wa ngazi za juu kuvuliwa uanachama na
↧
Baby Madaha : "Wema Sepetu Tuachie Na Sisi Huyo Diamond Tumfaidi "
Star wa filamu na muziki wa Bongoflava Baby Madaha anadaiwa kuwewesekea
penzi la Diamond Platnumz na kumtaka Wema Sepetu awaachie na wao Diamond
a.k.a Sukari ya warembo ili wafaidi kama anavyojiachia.
Chanzo
kimoja kilicho karibu na Baby Madaha ambacho pia kinafanya juu chini
kuwika katika filamu kwa masharti ya kutotajwa jina lake kikizungumza na
Swahiliworldplanet wiki iliyopita
↧
Kitale akanusha kutoka Kimapenzi na Penny ambaye aliwai kuwa mpenzi wa zamani wa Diamond
Msanii wa filamu za vichekesho, Kitale, ambae kwa sasa anatambulika
zaidi kwa jina la ‘Mkude Simba’ amekanusha kuwa hajawai kuwa na
mahusiano ya kimapenzi na Vj Penny ambae aliwai kuwa mpenzi wa zamani
wa Diamond.
Kitale akizungumza Global TV hivi karibuni ,amekanusha uvumi huo,
ambao uliambatana na picha zinazo muonyesha Penny akimbusu
Kitale.
“Penny mimi sina
↧
↧
Mapacha wamjibu Lulu Michael baada ya kukana kuimba kwenye wimbo wao....Wasema 'Ametudharau'
Baada ya Elizabeth Michael kukana kushirikishwa na kundi la mapacha
kwenye wimbo wao mpya ‘Time For The Money’, Kundi la Mapacha limeeleza
jinsi lilivyoipokea taarifa hiyo.
Akiongea na Times Fm, Kulwa wa Mapacha amesema kitendo
alichokifanya Lulu ni dharau kubwa kwao na kwamba inawezekana ameona
hataki kusikika kwenye wimbo waliofanya wao.
“Sisi tuliamua kumtaja kwa respect kwa
↧
Batuli: Sijawahi kula hela ya mume wa mtu na kamwe siwezi kuugeuza mwili wangu kuwa mtaji
Staa wa kike anayefanya vizuri katika tasnia ya fillamu Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ amefunguka na kudai kuwa hajawahi kula hela ya mume wa mtu na kama watu wanamhisi hivyo basi watakuwa wanakosea sana.....
Batuli alitoa kauli hiyo ili kuwathibitishia mashabiki wake juu ya kauli mbovu za watu kuwa urembo wake unategemea mtaji wa mwili wake
↧
Tunaomba Radhi kwa Picha: Kikongwe auawa kinyama kwa kukatwa Shoka kichwani huko Kahama
Bibi mmoja Mkazi wa mtaa wa Nyahanga, wilayani Kahama Mkoani Shinyanga, Rebeka Sengasenga (82), ameuawa kwa kukatwa na Shoka kichwani kwa kile kinachohisiwa kuwa ni imani za Kishirikina.
Kwa mujibu wa majirani, tukio hilo limetokea jana asubuhi katika Mtaa wa Nyahanga, wilayani humo, ambapo Marehemu Rebeka alienda nyumbani kwa mtoto wake Bundala Sengasenga alikokuwa ameitwa na mke wa
↧
More Pages to Explore .....