Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mwanafunzi Darasa la Pili Aliwa na Mamba Ruvuma

$
0
0
Mwanafunzi wa darasa la pili katika Shule ya Msingi Makoteni Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, Bimwana Saleh (12) amekufa kwa kuliwa na mamba katika mto Ligoma wakati akifua nguo na mama yake.

Mkuu wa wilaya ya Tunduru, Mkoani Ruvuma, Juma Homera amemuagiza ofisa wanyamapori wa wilaya hiyo kumuua mamba huyo ili kuwanusuru wananchi na tishio la kundelea kujeruhiwa na kuuawa na mamba.

Homera amesema hayo wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Makoteni muda mfupi baada ya kuitembelea familia ya Mtoto Bimwana Salehe (12) aliyepoteza maisha baada ya kujeruhiwa na mamba na kutoa pole kwa wafiwa.

Aidha, Homera aliwataka wakazi wa kitongoji hicho kuchukua tahadhari na kujenga tabia ya kwenda wakiwa katika makundi wanapokwenda kuchota maji au kufua katika mto huo.

Alisema utaratibu wa kwenda watu wengi kwa pamoja mtoni utawasaidia kuokoana endapo ikitokea mmoja wao kuvamiwa.

Homera aliwataka wazazi na walezi katika kata hiyo kuacha taratibu za kuwatuma watoto wadogo kwenda kufanya shughuli zozote katika mto huo.

Mtendaji wa kijiji cha makoteni Ajili Mbemba alimueleza mkuu wa wilaya kuwa watu wawili wamekwishapoteza maisha na wengine watano walijeruhiwa kwa kushambuliwa na mamba katika eneo hilo katika kipindi cha Julai 2018 hadi Februari mwaka huu.

Kwa mujibu wa Mbemba waliopoteza maisha ni Furaha Mtindinganya (15) aliyekufa mwanzo mwa mwezi Januari mwaka huu na Bimwana Hashim aliyepoteza maisha Februari 26 mwaka huu.

Aidha Mbemba aliwataja waliojeruhiwa na mamba hao na kusababishiwa vilema vya maisha katika eneo la mto huo kuwa ni Shabilu Mohammed (8), Muhdini Dhabiti(29), Katrimu Juma (11), Saidi Issa (19) na merina Omari (15).

Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Diwani wa kata hiyo Abbas Ngajime walioomba serikali kuangalia uwezekano wa kuwapunguza mamba hao ili wananchi waweze kuishi kwa amani.

Akizungumzia hali hiyo Kaimu Ofisa Wanyamapori wa Wilaya ya Tunduru Limbega Ali pamoja na kukiri kuwepo kwa matukio hayo alisema kuwa tayari amekwishatuma askari wenye silaha kwa ajili ya kwenda kumsaka na kumuua mamba huyo ili asiendelee kuleta madhara kwa watu.

Kwanini Ukate Tamaa ....Rudisha Furaha Na Heshima ya Ndoa Yako sasa

$
0
0
KWANINI UKATE TAMAA ,RUDISHA FURAHA NA HESHIMA YAKO  kwa kutumia Dawa hii hiitwayo SUPER  MUMBl, kwa ajili ya nguvu za kiume na NYAMOLO 3 MIX ni kwaajili ya kuongeza maumbile

 Kwa mwanaume aliye kamilika anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara mbili au zaidi hapo utamlidhisha mpenzi wako.kiume .TIBA YA TATIZO LAKO NI; Dawa hiitwayo SUPER MUMBI,(huongeza homoni za kiume ziitwazo testosterone), dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge na unga wa asili ambavyo avina madhara kwa mtumiaji ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja;-

1).itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuchoka.
2).ltakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15 hadi 20 kwa tendo la kwanza.
3).lnaimarisha uume uliolegea na uliosinyaa na kuupa nguvu maradufu.

Je unamaumbile madogo pamoja na uume mfupi? NYAMORO 3 MIX ni suluisho la tatizo lako. Na ni dawa inayoboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi kuanzia inch. 5 hadi 8 kwa muda mfupi sana .Dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk.30 .

Pia ninatibu;- KISUKARI, PRESHA, MATATIZO YA UZAZI , NGIRI, PUMU, MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE ,BP, NK.

IGEMEJA, ni dawa ya mvuto wa biashara,  Pia humvuta mke,Mme,hawara ,mchumba

Pia ipo dawa ya kupunguza matiti,unene ,tumbo,na kitambi ,hupunguza mafuta ,kuondoa makovu,chunusi,michilizi mwilini na kuongeza hipsi, makalio na mguu wa bia nk. Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR,SHANGATA Anapatikana Dar es salaam-Mbagala

Simu no, 0756241666 au 0672186977
       Huduma hii utaipata popote ulipo,kwa wale mliopo nje ya Dar es salaam mtatumiwa kwa njia ya mabasi

Waziri Mkuu ataka Muswada kuunganishwa kwa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) na Shirika la Viwango nchini(TBS)

$
0
0
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amezitaka Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) na Shirikia la Viwango Tanzania (TBS) kuacha urasimu huku akimtaka Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu na Waziri wa Viwanda na Biashara Joseph Kakunda kuandaa muswada wa kuunganisha taasisi hizo na kuwasilisha bungeni ili sheria zake zifanyiwe mapitio upya.

Majaliwa aliyasema hayo juzi katika kikao chake na wafanyabiashara wa kati na wadogo uliofanyika kwenye ukumbi wa Anatoglo ambapo alionyesha kukasirishwa na urasimu wa taasisi hizo mbili na kuagiza pia wakurugenzi wa taasisi hizo kufanya mapitio ya utendaji wa watumishi wao. 

Alisema mamlaka hizo zikiunganishwa zitaweza kuondoa malalamiko kutoka kwa wafanyabiashara ambao wamekuwa wakilalamikia kuwepo kwa tozo nyingi na urasimu unaosababisha taifa kupoteza makundi makubwa ya wafanyabiashara na wateja.

“Sheria za TBS na TFDA zote zinafanana, ni maneno tu mnacheza nayo huku ubora, sijui viwango, vikiwa na viwango lazima vitakuwa bora, urasimu tu ndio uliokithiri TBS na TFDA, mizigo inakuja bandarini inakaa miezi miwili mitatu mnajifanya mnapima, mnapima nini?”alihoji Majaliwa. 

Aliongeza kuwa ukimwi wenyewe siku hizi unapimwa kwa dakika tano unapewa majibu yako na kuongeza kuwa typhoid unapima leo, kesho mtu anatakiwa kupewa majibu lakini akahoji kwa nini wao wanachukua siku 20.

“Kama mashine zenu mbovu kwa nini msiagize mashine nyingine nje, Mkemia mkuu yupo kwa nini msiende kupima huko, mnakaa na bidhaa za watu muda mrefu mpaka zinaoza ndio maana wakati mwingine TRA wanaruhusu mizigo itoke mnakuja baadae kusema bidhaa haina viwango… mawaziri wa wizara zote kaeni na taasisi zenu mbadilike, kama mashine yenu inachukua miaka mitano kutoa majibu basi nunueni zenye ubora, nimesikia TBS wanapima mpaka stuli za kukalia, hivi stuli unapima nini? “alihoji.

Waziri Majaliwa alizitaka taasisi hizo zitoe mwongozo kama kwenye soko bidhaa za thamani za ndani zinazotakiwa sio kusumbua wafanyabiashara.

 “TBS mnapima mpaka shati, nadhani kuna haja ya kufanya mapitio taasisi hii, kuna mtu mmoja alikuja ofisini kwangu kanunua vifaa vyake China vya ujenzi vya nyumbani madirisha, milango na masinki ya vyoo, kalipia kila kitu vimefika bandarini TBS imezuia miezi minne eti mwisho mnasema vipo chini ya kiwango, kila kitu kikitoka Italia wananchi wa Magomeni Mapipa watawaweza kumudu gharama?” aliuliza.

Majaliwa pia aliwataka wafanyabiashara wasikubali kutoa rushwa kwa chombo chochote na kuwataka watendaji kuacha lugha za dharau kwa wananchi na kuzitaka taasisi zote zinazohusika na masuala ya Bandari, TRA, TBS na TFDA kukaa jengo moja kuwaepusha wananchi na usumbufu wa nenda rudi.

“Bandarini kuna jengo moja kubwa sana pale limekaa kama meli, kuna vyumba vipo tupu, taasisi zote zinazousika zikae pale mtu akienda kulipia mizigo yake anamaliza kila kitu pale sio kupiga makitaimu mara bandarini, Ubungo achene urasimu, na nyie wananchi, rushwa si sehemu ya mkakati wa serikali, hivyo vita dhidi ya rushwa lazima iendelezwe na watu wote. Mafanikio tuliyoyapata ikiwa ni pamoja na kuimarika kwa huduma za afya, maji na barabara ni matokeo ya kupiga vita rushwa,” alisema.

Majaliwa aliwataka pia watumishi kuacha kukaa ofisini na badala yake wajenge tabia ya tabia ya kuwatembelea wafanyabiashara kwenye maeneo yao na kusikiliza kero zinazowakabili na kushirikiana nao ili kutafuta ufumbuzi.

“Kila mtendaji katika eneo lake atekeleze majukumu yake kikamilifu urasimu, dharau, lugha za ajabu zimeshamiri kwenye maeneo ya kutolea huduma jambo ambalo si sahihi. Badilikeni,” alisema. Alisema serikali imepanga mpango wa kulibadilisha utaratibu wa kufanya biashara katika eneo la Kariakoo ili kuwawezesha wafanyabiashara kufanya shughuli zao kwa saa 24 kama yalivyo masoko makubwa duniani.

Waziri Mkuu alisema lengo la mabadiliko hayo ni kukuza uchumi wa taifa na wa wafanyabiashara kwa ujumla. “Nchi yetu ina usalama na ulinzi wa kutosha hivyo hatuwezi kushindwa kufanya biasahara wakati wote.”

Katika mkutano huo aliouitisha kwa lengo la kusikiliza changamoto zinazowakabili wafanyabiashara hao, Waziri Mkuu alisema atakutana na viongozi wa mkoa wa Dar es Salaam ili kupanga namna ya kutekeleza utaratibu huo. Alisema jiji la Dar es Salaam moyo wa kitivo cha kibiashara nchini, hivyo serikali itahakikisha mwenendo wa biashara unaboreshwa pamoja na kutoa fursa kwa wafanyabiashara kufanya biashara zao wakati wote na bila usumbufu.

Hospitali Ya Rufaa Ya Kanda Ya Mbeya Yakabiliwa Na Changamoto Ya Mtambo Wa Kuteketeza Taka

$
0
0
Na Lulu Mussa, Mbeya
Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Mbeya imeagizwa kuja na mpango mkakati wa haraka wa kukarabati mtambo maalumu wa kuteketeza taka hospitalini hapo badala ya kutumia mfumo wa sasa wa kuchoma taka hizo katika shimo kitendo ambacho ni uchafuzi wa mazingira na kinahatarisha afya za wagonjwa na wakazi wa maeneo jirani kutoka na kukithiri kwa moshi.

Katika ziara yake Mkoani Mbeya yenye lengo la kukagua maeneo yenye changamoto za kimazingira katika sekta ya afya na namna ya uteketezaji wa taka pamoja na kuzitafutia ufumbuzi Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Mussa Sima ameshuhudia  kukosekana kwa mtambo maalumu wa kuteketeza taka Hospitalini hapo na uteketezaji wa taka kufanyika katika shimo ambalo si salama kiafya na kimazingira.

“Nimeshuhudia Hospitali ya Rufaa ya Mbeya haina Incinerator, taka hatarishi zinachomwa kwenye shimo bila tahadhari yoyoye, kuna madhara makubwa zaidi ya uchomaji wa taka katika eneo hilo. Kama hatua za haraka nimeagiza taka hizo ziteketezwe katika burning chambers na waanze kuweka mkakati wa kupata incinerator itakayokidhi mahitaji” Sima alisisitiza.

Waziri Sima amesema uchomaji wa taka hususan taka hatarishi bila kuzingatia taratibu   madhara yake ni makubwa hasa kwa jamii inayozunguka, ukizingatia hospitali hiyo inapakana na Shule ya Sekondari ya Loleza. Ameelekeza kusitishwa kwa uchomaji taka wa aina hiyo na badala yake uongozi wa Hospitali hiyo utumie kiteketezi taka maalumu “burning chambers” kama mkakati wa haraka ili kunusuru afya za watu na mazingira.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Mussa Sima ameshuhudia kiasi kikubwa cha taka ngumu ambazo hazijazolewa hospitalini hapo kwa kipindi kirefu na kusababisha hofu ya mlipuko wa magonjwa. Katika kutatua changamoto hii Naibu Waziri Sima ameagiza Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya na Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya kukaa pamoja na kuweka mkakati endelevu wa kuhakikisha taka zinaondolewa kwa wakati Hospitalini hapo.

Alipoulizwa juu ya hali hiyo Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda – Mbeya Dkt. Paul Lawala amekiri kuwa Hospitali hiyo inakabiliwa na changamoto ya uzoaji taka kwa wakati na kuainisha kuwa changamoto hizo zinafanyiwa kazi  ikiwa ni pamoja  kuanza kwa ukarabati wa ‘burning chamber’ na mkakati wa kupata mtambo maalumu wa kuteketeza taka utakaokidhi mahitaji halisi.

Mvutano wa Rwanda na Uganda Wachukua Sura Mpya.......Mpaka Wafungwa, Rwanda Yatoa Tahadhari Kwa Raia Wake

$
0
0
Serikali ya Uganda imemtaka Balozi wa nchi ya Rwanda nchini humo Meja Jenerali Frank Mugambage kueleza mvutano wa kidiplomasia kuhusu sintofahamu kati ya mpaka wa nchi hizo jirani.

Uganda pia inamtaka Balozi wake nchini Rwanda kupata maelezo ni kwanini mvutano huo unaendelea kushuhudiwa.

Hali ya wasiwasi imeshuhudiwa wiki hii baada ya serikali ya Rwanda kufunga mpaka wa Gatuna kwa kile ilichosema kuwa, ulikuwa unakarabatiwa na kulazimu magari ya mizigo kutoka Uganda kupitia mpaka mwingine wa Kagitumba, umbali wa Kilomita 114.

Serikali ya Rwanda, imewataka raia wake wanaokwenda nchini Uganda kuwa makini, kwa madai kuwa raia wake wanakamatwa na kurudishwa nyumbani kwa nguvu.

PICHA: Mwili wa Ruge Mutahaba watua Bukoba....Mamia wajitokeza kuupokea

$
0
0
Mamia ya wananchi wamefurika Uwanja wa Ndege Bukoba kushiriki mapokezi ya mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji wa Clouds Media Group Tanzania na aliyekuwa mhamasishaji mkubwa wa vijana katika matumizi ya vipaji na fursa, Ruge Mutahaba.

Magari mawili yatakayoongoza msafara tayari yameingia ndani huku 'plate number' zikiwa na maandishi ya R.I.P Ruge.

Pia magari yatakayohusika katika msafara yamepewa namba na kuandikwa neno 'msiba,na njiani kuna vibao vinavyoelekeza eneo la msiba kwenda Kijiji cha Kiziru Wilaya ya Bukoba.

Ndege ya ATCL iliyotua uwanjani hapo na baadaye kuondoka ilikuwa na abiria ambao wengi wao hawakuondoka na badala yake kujiunga na watu waliopo kiwanjani.

Baada ya mapokezi msafara utapita mitaa mbalimbali kuelekea Kiziru ambapo ataagwa kesho Jumatatu asubuhi viwanja vya Ghmkhana na mazishi kufanyika baadaye jioni.

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Marekani, Urusi zanyukana kuhusu Venezuela

$
0
0
SERIKALI za Marekani na Urusi zimeendelea kupambana vikali juzi kuhusiana na jinsi ya kuisaidia Venezuela iliyokumbwa na mzozo wa kisiasa, ambapo Urusi iliamua kutoa njia mpya za kutoa misaada kupitia Rais Nicolas Maduro wa Venezuela, lakini Marekani ikatangaza kuweka vikwazo vipya dhidi ya taifa hilo la Amerika Kusini.
 
Rais wa Venezuela Nicolas Maduro ameamuru ofisi za kampuni ya taifa ya mafuta zilizoko mjini Lisbon kuhamishiwa mjini Moscow, mnamo Urusi ikiapa kuendelea kumsaidia rais huyo ikiwa ni pamoja na kutuma misaada ya kiutu.

Makamu wa rais wa Venezuela Delcy Rodrigues amesema hii leo kuwa uamuzi huo wa kuzihamisha ofisi za kampuni ya taifa ya mafuta PDVSA ulilenga katika ulinzi wa mali za nchi hiyo. 

Aliyazungumza hayo kwenye mkutano wa pamoja na waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov, akisema Ulaya imeshindwa kuhakikisha usalama wa mali za Venezuela. 

Aidha alitolea mfano uamuzi wa Benki ya Uingereza kukataa kutoa dhahabu zake akisema sasa Caracas inazidisha ushirikiano na Urusi.

Ofisi ya kampuni ya mafuta ya Venezuela itapanua ushirikiano wa kiufundi katika uchimbaji mafuta na makampuni ya mafuta ya Urusi ya Rosneft na Gazprom. 

Naye waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov amesema Urusi imetuma msafara wa kwanza wa matibabu nchini Venezuela na pia itaisadia nchi hiyo na misaada ya ngano.

"Kama tunazungumzia hali ya kitu nchini Venezuela kwa ujumla, nafikiri usambazaji wa kiwango kikubwa cha ngano kimesaidia kutuliza hali. Kimesaidia serikali ya Venezuela kushughulikia matatizo yaliyopo.", alisema Lavrov.

Urusi imetuma jumla ya tani 64,100 za ngano nchini Venezuela hadi kufikia hivi sasa katika msimu wa soko la mwaka 2018/19. 

Lavrov ameongeza kwamba wamepokea maombi zaidi ya misaada kutoka Venezuela akiongeza kwamba nchi hizo mbili zitaendelea kushirikiana katika nyanja ya masuala ya kigeni. Pia inaituhumu Marekani kwa kujaribu kuchochea mapinduzi dhidi ya rais Maduro.

Urusi kama ilivyo China imekuwa mkopeshaji wa dakika ya mwisho wa Caracas, ikiipatia mabilioni ya dola wakati uchumi wake ukizidi kuporomoka. Pia imeipatia misaada ya kijeshi na katika sekta ya mafuta.

Ikiwa inakabiliwa na mgogoro wa kiuchumi Venezuela ilitumbukia katika mgogoro wa kisiasa wakati kiongozi wa upinzani Juan Guaido alipojitangaza kwa rais wa mpito mnamo mwezi Januari na kusisitiza kuwa Maduro si kiongozi halali. 

Marekani ilimtambua Guaido na kuongoza kampeni ya kuunga mkono uhalali wake.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Magonjwa yanayoababisha Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Ni Kama Vile, Kisukari ,presha, Ngiri Ya Kupanda Na Kushuka, Kiuno, Maumivu Ya Mgongo, Tumbo Kuuma Chini Ya Kitovu, Tumbo Kujaa Gesi. Yote Matatizo Yote Haya husababisha Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Kushindwa Kufanya Kazi Kwa Mwenza Wako  .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa Dar anapatikana mbagala Zakhem.  Songea ,bombambili, Shinyanga, Kahama ,mjini, Kwa ,maelezo, Zaidi , Piga Simu 0763172670/ 0715172670,/ ,Sema ,haloo, Dr Sitta... Wote  mnakalibishwa. 

Ufugaji wa nguruwe : Gharama na Faida Zake

$
0
0
 Utangulizi
Nguruwe ni mnyama amabaye hutumika kama chakula / mboga na pia ni zao la biashara kwa mfugaji, mjasirimali na mfanyabiashara.
 
NGURUWE HUTEGEMEA SANA MAMBO YAFATAYO
1 . Banda imara na rafiki kwake
2. Usafi ni muhimu sana katika banda la Nguruwe
3 Mchaganyo bora wa chakula
4. Tiba bora na kinga
5. Maji na Lishe ( access ya vyakula Muhimu kwake )
 
CHANGAMOTO
KATIKA UFUGAJI WA NGURUWE KUNACHAGAMOTO ZAKE LAKINI ZAWEZA KUTATULIWA KWA KUFATA MAMBO KADHAA.
Katika ufugaji wa nguruwe kunachagamoto ya vifo vya nguruwe wachanga ambao hupunguza faida ya biashara ya nguruwe kwa kupunguza idadi ya nguruwe wazima wa kuuzwa lakini utunzaji mzuri wa nguruwe wachanga huepusha vifo vinavyotokana na shida kama:
 
Matatizo ya kupumua
Ni kifo kinachosababishwa na mama anapomlalia nguruwe mchanga.chagamoto hii inaweza kutatuliwa kwa kuwatenga au kuwa na mabanda makubwa ya kulelea watoto.
 
Baridi
Nguruwe wachanga huathiriwa na baridi haswa katika majuma mawili au matatu ya mwanzo. Hii ni kwa kuwa wana kiwango kidogo cha utando wa mafuta wa kuwakinga.
 
Unashuriwa kuwaweka katika hali ya joto, wape matandiko na utumie vipasha joto kama vile kuwasha globu za joto kama utakuwa umewaweka kwenye mabanda ya kuta au nyumba yenye sakafu baridi.
 
Namna bora utunzaji wa nguruwe wachanga
Nguruwe moja wa kike ana uwezo wa kuzaa watoto 12. Namna ifuatayo itasaidia kupunguza idadi ya vifo vya nguruwe wachanga:
1.Pale nguruwe awapo na kidonda nyunyizia dawa ya ayodini 5% kwenye kovu ili kuzuia kuambukizwa kwa magonjwa.
2.Wawekee matandiko (nyasi kavu au maganda ya miti) mahali pa mapumziko ili wapate joto au utumie globu za joto.
3Wadunge sindano ya madini ya chuma (iron) siku ya tatu baada ya kuzaliwa ili kuzuia upungufu wa damu.
3. Yalainishe meno ya vichaga kabla ya masaa 24 ili kuzuia uharibifu wa matiti wakati wanaponyonya.
4. Watie vibandiko au utoboe masikio ili uwatambue na uhifadhi rekodi zao kama kuna umuhimu kama vile wafanyavyo wafugaji wa ng’ombe.
5. Wapime uzani wanapozaliwa na uhifadhi rekodi hiyo itakusaidia kujua ukuaji wao na maendeleo yao
6. Wahasi wale wa kiume juma la tatu, wale ambao hawafai katika kuendeleza kizazi kwa kutumia mtindo wazi (open method) kama unaona inafaa.
7. Wapatie dawa ya kuzuia minyoo pia zipo dawa za asili kama unga wa mkaa na majivu pia zipo za kitaalamu, wasiliana na wataalamu wa mifugo
8.Waachishe kunyonya katika juma la nane au wafikapo kilo 14 hadi 20 hii itasaidia kujitegemea na kukua kwa haraka.
 
Nguruwe Walioachishwa Kunyonya
1.Walioachishwa kunyonya wawekwe makundi ya 10 hadi 12 kulingana na uzito au ukubwa wao kwenye eneo ambalo watajitosheleza.
2.Watenganishe wakubwa kwa wadogo ili kuzuia kupigana.
3.Wakati wa kuwaachisha kunyonya mwondoe mama yao kutoka kwa watoto ili kupunguza usumbufu.
4Watoto wa nguruwe wa mama tofauti wasiwekwe pamoja maana hii husababisha mapigano kati yao na
5.Unapowachanganya watoto wa mama tofauti wapake mafuta ya gari yaliyotumika kwenye ngozi yao au mafuta ya kula ili kuiondoa harufu ya kutambulika ili wasipigane
 
FAIDA YA UFUGAJI WA NGURUWE
Faida kuu ya nguruwe ni zao la chakula lakini pia ni zao la kukuongezea kipato ukiwa kama mjasirimali / mfanyabiashara.
Lengo langu nikueleza namna unavyoweza kufuga na kutupa faida, Steps zifatazo ni muhimu kuzigatia.
 
JIPE MTAJI WA MILLION 4 / 3.5 KWA NGURUWE 50
UANDAAJI WA BADA WEKA MAKADILIO YA LAKI TANO (800,000/=) .
Hapo nazugumzia banda lenye heru U yenye mstatili ikiwa na kitako kirefu
Eneo lenye ukubwa wa mita 50 kwa 50 litafaa zaidi ili kuhakikisha usalama wa nguruwe wako na ukuaji bora.
1. Tafuta mabati used kwa bei ya 5000 mfano mabati 20 ya futi 10 /10 = 100,000/=
2. Tafuta mabazi ya futi 10 kwa 2000 kila moja utapata mabazi pic 100 = 200,000/=
3. Tafuta miti ya nguzo na kechi ya 1000 na 2000 miti ya 1000*70 na 2000*3 = 120,000/=
4. Tafuta chagalawe / moramu trip 10*3000 =30000/=
5. Cement mifuko kwa ajiri ya sakafu na mashimo ya kulishia 5 *18000 = 90,000/=
6. Misumari ya aina 4, nch 6 kg5,nch 3 kg5 nch 5 kg10 na nch4 kg10, Bawaba na komeo =100,000/=
7. Malipo ya fundi 75000 fundi uashi na 75000 fundi seremala =150,000
JUMLA HAPO INAKUWA 790,000/= MAKADILIO INAKUWA 800,000/=
 
UNUNUZI WA NGURUWE WA KUANZIA .
Nguruwe wadogo wadogo ni vinzuri zaidi kuanza nao kwa sababu watakuzalia watoto wengi na kwa muda mrefu . Chukua mfano MILLION 2.5 . Nguruwe wadogo wa dogo wanauzwa 50000 au 40000 inategemeana na mahala na maelewano . Milioni 2.5 inakupa vitoto 50 au 55 . Hivyo unawexa kuwa na vitoto jike 50 na vidume 5. baadaye ukaongeza madume matano ya kuazima au kukondi kwa ajiri ya kupandishia
 
MAANDALIZI YA CHAKULA
Mchaganyiko wa chakula cha nguruwe na gharama zake tunaweza ukadilia kujitosheleza kwa laki tatu kwa mwenzi mmoja kwa nguruwe hao 50, kwa 300,000/= , ambapo itajumuisha tiba / kinga, lishe, vyakula vya nguruwe vinaweza kuwa pumba ya mpunga ile laini,pumba ya mahindi, mashundu, mabaki ya magada ya vianzi amba mabaki ya chakula yaliyosalama
 
MALIPO YA MSIMAMIZI NA ENEO LA KUWEKEZA
Katika kipengele hiki makadilio ya juu ama ya chini kwa msimamizi wa kazi yako waweza mlipa 100,000/= ama chini yake pia kwa mwenye eneo huwa nimaelewano tu aunaweza pata kwa fair au kukakodi kwa laki tatu, 300,000/= kwa mika miwili.
 
HIVYO JUMLA YOTE YA GHARAMA ZA UAZISHAJI UWEKEZAJI WA NGURUWE 50 ZITAKUGHARIMU MILLION 4 AMA MILLION 3.5 KWA MAANA KUWA HAPO JUU NIMETUMIA MAKADILIO YA JUU NA UKIINGIA KWENYE UHALISIA KAMA MJASIRIMALI LAZIMA IPUNGUE NA KUFIKIA 3.5

KIPATO AU FAIDA YA UFUGAJI NGURUWE
Nguruwe wanafaida ya haraka na nimradi wa uhakika kabisa, ukipitiia mchanganuo hapo juu wa nguruwe 50 utatupa faida kama ifatavyo
 
Nguruwe huzaa Mara mbili kwa mwaka na huzaa watoto zaidi ya watanoyaani huzaa watoto 12 ama nane .
Basi chukua nguruwe 50 * vitoto 5 yaani ufanye kuwa nguruwe wako 50 wakupatie vitoto vitano vya uhakika
Nguruwe 50*5 = 250 ukijumlisha na wale 50 wa mtaji umakuwa nao 300 . Chukua zao la nguruwe la 250 na uza kwa 200000 kwa kila nguruwe yaan bei ya kawaida kabisa. Utapata Million 50.

Hivyo zao la kwanza ndani ya robo tatu ya mwaka inakutegenezea million 50 pia na mienzi sita ijayo inakupa tena 50 na zaidi ili kukamilisha uzao wa pili hii inkupa uhakika wa kutegeneza million 100 za uakakika ndani ya mwaka mmoja na nusu ama miaka miwili ukijipa timeframe work lakini kumbuka hapo tumefanya kwa hesabu ya uzao wa chini kabisa ambapo tumeangalia na hasara ya vifo kama vifo visipotokea na uzao ukawa mkubwa utakuwa na uhakika wa kutegeneza million 150 kwa miaka miwili.

Kwenye hesabu ya kuwale unaweza kuwaza sana kuwa itaongezeka na kukughalimu sana jibu ni hapana mpka kufikia kuuza hawatokugharimu zaidi ya million 7 je million 7 kwenye million 150 ni kitu kisicho nafaida ?
 
NB . jambo lolote linahitaji umakini naa dhamira ya dhati pia kushirikisha wataalamu na wenye uzoefu ili kufikia leng Ewe ndugu kila kitu kinawezekana UTAYARI WAKO / UTHUBUTU WAKO, UAMINIFU .NA MAAMZI YAKO.
 

Godbless Lema Atoa Povu Lowassa Kurudi CCM

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amefunguka kuhusu  uamuzi wa aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa kurejea CCM.

Lema amedai kuwa uamuzi wa Lowassa unadhihirisha kuwa ameweka mbele maslahi yake binafsi kuliko mabadiliko aliyokuwa anayahubiri alipoingia Chadema.

Alidai kuwa Lowassa alifikia uamuzi huo ili kulinusuru shamba lake linaloshikiliwa Mkoani Tanga, shamba lake la mifugo linaloshikiliwa Dodoma pamoja na kumnusuru mkwewe Sioi Sumari na kifungo dhidi ya kesi inayomkabili. 

Sumari anatuhumiwa kwa kula njama ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, kughushi pamoja na utakatishaji wa fedha.

“Mtu huyu alitaka kuwa Rais, hali ya kisiasa ilivyo sasa watu wapo magerezani, wanapata misukosuko ya kibiashara, hawana cha kuipa CCM ili wapate ahueni, lakini kwa sababu yeye anacho cha kuwapa CCM ilia pate amani. Hajaona gharama ya kufanya hivyo,” Lema amekaririwa na Gazeti la  Mwananchi 
 
“Chadema imepata baraka kuondokewa na mtu kama huyu. Alikuja kwa ajili ya kutaka urais na sio mabadiliko aliyokuwa akiyanadi. Nchi inataka demokrasia, katiba mpya, sheria mpya na inakabiliwa na ubanaji wa vyombo vya habari… mwanasiasa makini hawezi kuungana na CCM,” aliongeza.

Lowassa alijiunga na Chadema mwaka 2015 baada ya jina lake kuondolewa kwenye kinyang’anyiro cha watu waliokuwa wakiwania nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya CCM. Aligombea urais na kuleta ushindani mkubwa dhidi ya Dkt. John Magufuli wa CCM.

Juzi alipokewa na Dkt. Magufuli, Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Lowassa alieleza kwa ufupi kuwa amerejea nyumbani. Alipokewa katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.

Magonjwa 8 Yanayoshambulia KUKU Pamoja na Tiba Zake

$
0
0
Hivi Karibuni tuliona namna unavyoweza kuwa milionea kupitia ufugaji wa kuku. Tulisimulia namna unavyoweza anza na mtaji wa 250,000 tu na ndani ya miaka miwili tukaona unavyoweza  kujipatia milioni 390 kupitia ufugaji wa kuku wa kienyeji.

Leo tutazungumzia magonjwa yote yanayosumbua kuku ili sasa uyajue na ukabiliane nayo na hatimaye uweze kutimiza ndoto zako za kuwa milionea.

 1.Rangi ya kinyesi
==>>Mharo mweupe(pullorum bacilary diarrhoea)
ugonjwa huu huathiri zaidi vifaranga kabla ya wiki nne
huharisha mharo mweupe,

Tiba
Usafi  kwenye banda na kuepusha maji yasimwagike ovyo

2.Kipindupindu cha kuku(fowl cholera)
-Kinyesi cha kuku ni njano
-Tumia dawa za salfa, eg Esb3 au amprollium

3.Coccidiuosis
mwanzo kinyesi cha kijivu na baadae huharisha damu iliyochanganyika. Tumia dawa ya VITACOX au ANTICOX

4.Mdondo(Newcastle)
-kuku hunya kinyesi cha kijani (NB; sio kila kijani ni newcastle)
-HAKUNA TIBA. (Kuku wapewe  chanjo  tangu  vifaranga wa  umri wa  siku 3,  baada ya  wiki 3  – 4,  na baadaye  kila baada  ya miezi 3)

5.Typhoid
-Kinyesi cheupe
-kinagandia sehemu za nyuma au hulowana sehemu za haja
-dawa ni Eb3

6.Gumboro
-Huathiri zaidi vifaranga
-kinyesi huwa ni majimaji
-Dawa hakuna, tumia vitamini na antibiotic

7.Kideri
Ni ugonjwa unaosababishwa na virusi ambao hushambulia aina zote za spishi za ndege, ijapokuwa kuku ndio aina inayoathirika zaidi

Dalili
•Vifo vya ghafla bila kuonesha dallili zote
•Kuvimba kwa kichwa na shingo
•Kuhalisha uharo wa kijani
•Utagaji wa mayai kushuka kwa kiasi kikubwa au kusimama kabisa
•Kutetemeka, kichwa kugeuzwa upande mmoja
•Kupooza kwa mabawa na miguu.

Jinsi unavyoenea
•Chanzo cha maambukizi ni maji, chakula kill Hoxha fulls a na kinyesi cha kuku wagonjwa.
•Pia maambukizi huweza kupitia mfumo wa hewa ktoka kwa kuku wagonjwa
•Kuku, vifaa vya kazi na bidhaa zitokanazo na kuku ( nyama, mayai, manyoya na mbolea) kutoka mashamba yenye ugonjwa zinaweza kueneza ugonjwa
•Faranga anaweza kupata maambukizi kutoka vituo vya kutotolea vifaranga kutokana na maganda ya mayai yaliyochafuliwa
•Kuku kuzubaa na kuacha kula
•Kuku kukohoa, hupiga chafya na kupumia kwa shida

Matokeo Kwa Kuchunguza Mzoga Aliyeathirika
Ugonjwa huathiri zaidi mfumo wa hewa na njia ya chakula, hivyo mabadiliko yanayoonekana kwenye mzoga ni pamoja
•Madoa ya damu kwenye mfumo wa hewa
•Kamasi nzito zenye Tangu ya njano kwenye koromeo
•Utandu mweupe kwenye mfumo wa hewa
•Bandama kuvimba
•Uvimbe kwenye kichwa na eneo la shingo
•Madoa madogo madogo ya damu kwenye kifua, mafuta na utandu wa tumboni
•Damu kuvia kwenye mfumo wa usagaji chakula, juju, firigisi, tumbo na utumbo.

NB:
Haya matokeo yatakusaidia wakati pale kuku amekufa banda bila kujua nini tatizo, kabla ya kumtupa mchinje na kumkagua tatizo lilikuwa nini.

Kudhibiti
Kuna namna za kuchanja kuku wako dhidi ya ugonjwa wa kideriI.Kudondoshea tone moja jichoniII.Kwa kidonge

Kudondoshea tone moja jichoni
•Pata chanjo kutoka kwa wakala au duka la mifugo lililokaribu nawe. Chanjo inayopendekezwa ni chanjo ya kideri 1-2 (1-2 NEWCASTLE VASSINE)
•Kamata kuku kwa uthabiti huku ukiwagemeza upande
•Dondoshea tone moja la chanjo ya kideri kwenye jicho moja
•Subiri kuku achezeshe kope ndipo umuachie.
 
Kwa kidonge
•Pata chanjo kutoka wakala au duka la mifugo lililo karibu nawe, hakikisha hifadhiwa kwenye barafu ili isiyeyuke kabla ya kutumika
•Kidonge hicho kimoja kitatumika kwa kuwekwa kwenye kiasi cha maji Lita 20
•Ukisha changanya kidonge na maji, hakikisha inatumika ndani ya Masaa 2 baadaya masaa hayo kupita haitafaa tena kwa matumizi.

Muhimu:
Chanja kila baada ya miezi 3 kwa kuku umri zaidi ya miezi mitatu na kuendelea tofauti na vifaranga
Chanja kuku kwenye afya tuu. ( uki chanja mgonjwa atakufa)

Sababu za kuku kula mayai
Kuku hula mayai kwa sababu nyingi sana ambazo zingine au zote zinaweza kuzuilika,
1.Tabia yao tu- Hapa utakuta ndo uzao wao wanatabia ya kula mayai hivyo kuku hufanya muendelezo wa kula mayai,
2.Kuto kupata chakula cha kutosha- Hii ni moja ya sababu kubwa kabisa inayo pelekea kuku kula mayai.
3.Kukosa madini joto- Hii inaweza kuwa ndo sababu kuu ya kwa nini kuku wanakula mayai, kuku wakikosa madini joto ni lazima wale mayai na hata kulana wao wenyewe, na jua kwamba kwenye yai kuku huwa anatafuta lile ganda la juu pekee sema anapo donoa na kulipasua yai hujukuta anakula na ute na kiini ila yeye lengo lake hasa ni ganda la juu
4.Kuku kutagia sehemu nyeupe sana yenye mwanga mkari hupelekea kuku kula mayai.
5.Mayai kukaa muda mrefu bila kukusanywa baada ya kutaga- Hapa ni kwamba mayai yanapo kaa muda bila kukusanywa na kama yapo sehemu ya wazi sana hupelekea kuku waanze kutest na some time kushangaa nini hiki cheupe? katika kushangaa ni kitu gani hiki cheupe cha mviringo hujikuta wanatest kudonoa na matokea yake ni kupasua yai.
6.Lishe mbaya
7.Nafasi ndogo
8.Vyombo havitoshi
9.Kukosa shughuli
10.Banda chafu (Manyoya)
11.Ukoo

Namna ya kuzuia kuku kudonoana au kula mayai
1.Chakula cha kutosha ni muhimu sana, ili kuwafanya wasitake kula mayai ili kushiba.
2.Mayai yakusanywe mara tu anapo taga na usiyaache muda mrefu bandani.
3.Sehemu ya kutagia iwe na giza la kutosha ili kufanya kuku ashindwe kuona yai alilo taga.
4.Madini joto ni muhimu sana.
5.Kuku wenye tabia za kula mayai unaweza chinja au kuuza.
6.Kuweka idadi ya kuku inayolingana na sehem ulionayo.
7.Usizidishe mwanga.
8.Banda liwe safi.
9.Weka vyombo vya kutosha.
10.Wape lishe bora.
11.Wape kuku shughuli kwa kuwawekea bembea na sehemu ya uwazi kwa ajili ya mazoezi.
12.Kata midomo ya juu.
13.Epuka ukoo wenye tabia hizo.

Kuwa tajiri kwa mtaji wa laki 2 na Nusu tu kupitia ufugaji wa kuku wa kienyeji. Tazama Hapa

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, yawezekana umekuwa ukiwaza sana nini ufanye ili uweze kufanikiwa na kuondokana na adha za umaskini.  Kulalamika tu vyuma vimekaza haitakusaidia kitu kama hutaki kujiongeza ili uongeze kipato chako.

Yako mambo mengi ya kufanya ili kujikwamua kiuchumi. Usitegemee mshahara wako tu. Mimi nataka kukufungua macho kwa jambo moja tu tena kwa uchache. Jambo hili anaweza kulifanya mwenye mtaji mkubwa au mdogo.
 
Somo  ni dogo tu lakini naamini wapo watakaopata mafanikio makubwa sana.
 
Unaweza kuanza kwa mtaji wa Mil.1 mpaka laki tano au hata chini ya hapo.

==>>Mfano. Unaweza kutumia Tsh 250,000 kununua kuku 25 kwa bei ya Tsh 10,000 kwa kuku mmoja (kadirio la juu) Majogoo watakuwa 5 kwa uwiano wa 1:4.

Hii ina maana kuwa wakishaanza kutaga utakuwa na

vifaranga 20 x 10 = 200Watunze vizuri.

Wale vifaranga tunakadiria kuwa majike watakuwa 150 ambao ndani ya miezi 3 au zaidi nao wataanza kutaga.

Utakuwa na kuku 200 + 25( ulioanza nao) =225 ndani ya miezi 6. Miezi 6 inayofuata 225 - (majogoo 55) = 170 Hii ina maana kuwa 170 x 10= 1,700.

Ndugu msomaji, hayo niliyotoa ni makadirio ya chini sana hivyo mpaka mwisho wa mwaka utakuwa na kuku zaidi ya 2000. 

Mwaka utakaofuata utakuwa na kuku wangapi baada ya kuuza kuku baadhi  ili upate fedha ya kuwalisha ????

Ukiuza kuku 1000, utabaki na kuku 1000, kati yao tuseme majike ni 750. Ndani ya Miaka 2 maanake ni  750(majike) x 10 = kuku 7500 (uza wengine upate pesa ya kutumia kuwalisha) . 

Tuseme sasa utabakiwa na kuku jike  3000 x 10( jike moja ni mayai 10) = kuku 30,000. 

Hao kuku 30,000  ukiwauza wote utapata; 30,000x 13000( bei ya kawaida kbsa)= 390,000,000. Je, bado utakuwa masikini? Bado vyuma vitakuwa vimekaza?

Nina uhakika, mpaka mwisho wa mwaka huo wa pili utakuwa umefanikiwa sana kuukimbia UMASIKINI.

Kwenye hayo mamilioni, hata ukitoa milioni 100 kwamba  tuseme ndo zimetuka kuendeshea mradi wako, bado utakuwa ni milionea tu. Kumbuka huu ni mwongozo tu, fanya utafiti na ufuatilie zaidi.

NB: Ukiyapata hayo mamilioni ya pesa, kumbuka kutoa Zaka, sadaka na kusaidia masikini wasiojiweza ili ubarikiwe zaidi 


Super Majinjas :Ni Dawa Ya Nguvu Za Kiume Iliyoboleshwa Ipo Kwenye Kichupa Sipesho

$
0
0
Acha kusubilia mpaka mke au mpenzi wako akwambie mme wangu huniridhishi tuwepo kitandani unatakiwa ujitambue mapema

Kwa mwanaume aliyekamilika na mwenye nguvu za kutosha ili kumridhisha mke au mpenzi wake unatakiwa uwe na uwezo wa kufanya tendo zaidi ya mara tatu lakini kama unakomea moja au mbili hapo ujue umejiridhisha wewe 

Tumia sasa tiba bora ya nguvu za kiume ;SUPER MAJINJAS dawa hii itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu pia itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dakika 10-15 kwa tendo la kwanza pia  huimalisha uume uliolegea na kusinyaa kwa Wale ambao wamepiga punyeto kwa mda mrefu ...dawa hii ni tofauti na ulizowai kutumia ni vidonge na unga 

JE UNA UUME MFUPI NA MWEMBAMBA tumia dawa hii hapa MAKAKANUA NO 5 ;dawa hii huboresha uume saiz 5,6,7,na 8 na unene wa am 2,3,4,na 5 dawa hii ipo ya kunywa na kupaka pia husaidia zaidi kwa mwanaume aliyefanyiwa tohara ukubwani

 ISENYE NO 3; hii ni dawa ya kisukari hutibu kabisa ugonjwa huo pia ugonjwa wa kisukari ndio chazo kikubwa kwa wanaume kuishiwa nguvu za kiume 

NGWARUSA; hii ni dawa ya uzazi kwa mwanamke na mwanaume .Zipo dawa za vidonda vya tumbo,korodani kuvimba, kupunguza kitambi na minyama uzembe.

Ofisi ipo MBAGALA ZAKHEMU ...njoo mpaka KWENYE UKUMBI WA DAR LIVE ...morogoro yupo wakala na mwanza au piga simu 0744040721- DR BRUNNO   utaletewa popote ulipo uduma hizi

Je Kwanini Baadhi Ya Wanaume Wengi Wana Ukosefu Ama Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
JE KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UKOSEFU AMA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO ???

Pata sululisho la matatizo haya na  magonjwa mengine utapona kwa mda mfupi sana hatakama ulihangaika mpaka ukakata tamaaa 

GALIMBO 3 MIX  ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa aina mbili ili kukidhi mahitaji ya mtumiaji, imetengenezwa kwa muundo wa vidonge pamoja na unga kwaajili ya kuponesha tatizo moja kwa moja , huimalisha misuli ya uume iliyolegea wakato wa tendo la mdoa ,na kukufanya ucherewe kufika kileleni kwa mda wa dk ( 20 - 45 ) itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu nira hamu kuisha wara kuhisi kuchoka vilivile huzalisha viini vya uzazi ( manii ) 

YOLAN  hurefusha na kunenepesha  maumbile madogo ya uume na kuwa na uume kuanzia nchi (6-8) tiba kwa mda mfupi sana

Zipo sananu nyingi sana zinazosababisha matatizo hayo  km vile -:punyeto, kisukali,ngili,chango,vidonda vya tumbo,  tumbo kuunguluma na kujaa gesi maumivu ya mgongo ama kiume ,kolodani moja kuvimba ama kuingia ndani  presha nk 

Matatizo haya yote sio mageni, kigeni ni tiba sahihi ya kuponesha matatizo hayo

SUPER MBUKE -:  nidawa ya kuponesha tatizo la kisukali kwa mda mfupi sana , usihangaike wara kuteseka tumia dawa ya mitishamba kwaajili ya tatizo hili na upone kabisa

NTINJIWA  nidawa ya mvuto wa biashara,kazi, kupandishwa cheo,kumfanya mfanyakazi apendwe na bos wake

Pia ninadawa za kumvuta mme , mke,mchumba,hawara, au mtu yoyote unaemuhitaji katika maisha yako hata km yupo mbali na atatulia na kukutimizia cjovjote utakacho na kumfunga asiwe na mtu mwingime ,

Pata tiba za magonjwa mbalimbali ikiwemo miguu kuwaka moto, mgongo,bawasili ,kaswende ,gono na mengine mengi

KWAUSHAULI NA TIBA WASILIANA NA DR CHIKAGO    0759 208 637

Km huna nafasi ya kufika ofisini hudumahii utaletewa hapo ulipo , kwa wale wa mikoani natuma kwanjia ya basi

Mkuu wa Wilaya ya Newala Apata Ajali Mbaya ya Fari

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Newala, Aziza Mangosongo na watu wengine watatu wamenusurika kifo baada ya gari walilokuwa wamepanda kupata ajali na kupinduka.

Tukio limetokea eneo la Mandawa jana saa mbili usiku wilayani  Kilwa Mkoa wa Lindi  wakati mkuu huyo akiwa safarini kwenda Dar es Salaam.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Sokoine, Muhaji Mohamedi  amesema amepokea majeruhi wanne  ambao ni Aziza Mangosongo, Mwanahamisi  Naenda, mkazi wa Kitangali, Zaituni Lipau  na Jasiri Nguru.

Amesema wanatarajia kuwapa rufaa majeruhi kwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili  kwa matibabu  zaidi.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Renatus Chalya amethibitisha kutokea kwa tukio hilo akisema dereva Daudi  Kakulilo wa gari hilo la Serikali anashikiriwa  na polisi kwa mahojiano.

Audio:Gozbert Goodluck - Tutaonana Tena

$
0
0
Audio:Gozbert Goodluck - Tutaonana Tena

Picha 4: Msanii Diamond Platnumz Awasili Ukumbi wa Karimjee Kumuaga Ruge Mutahaba

$
0
0
Msanii Diamond Platnumz na Mama yake mzazi Bi Sandra, wamefika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam kuungana na watanzania waliojitokeza katika taratibu za kuuaga mwili wa Marehemu Ruge Mutahaba.

Waziri Ummy Mwalimu: Bima Ya Afya Ndiyo Suluhisho La Uhakika Wa Matibabu

$
0
0
Na WAMJW – Kilosa, MOROGORO.
Wananchi wametakiwa kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya ili kuwa na uhakika wa kupata matibabu wanapofika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Waziri Ummy Mwalimu ameyasema hayo leo alipokuwa ziarani Wilaya ya Kilosa Mkoa wa Morogoro akikagua hali ya utoaji wa huduma za afya katika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa.

“Ni muhimu kwa wananchi kuwa na bima ya afya ili waweze kuwa na uhakika wa kupata matibabu ikiwemo dawa bila ya kikwazo cha fedha” amesema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema kuwa matarajio ya wananchi mara baada ya kujiunga na bima ya afya ni kupata huduma bora za afya bila usumbufu huku wakiwa na uhakika wa kupata dawa kwa makundi yote ikihusishwa wale wa Bima ya Afya pamoja na Mfuko wa Bima ya Afya Ngazi ya Jamii (CHF) iliyoboreshwa.

“Mwananchi yeyote ambaye amekuja na bima ya afya, CHF iliyoboreshwa wanapaswa kupata huduma zote, kumwona daktari bure, vipimo bure, na dawa bure” amesema Waziri Ummy na kuongezea “Bila ya kufanya hivyo hakuna umuhimu wa kuwaambia wananchi kukata bima za afya.

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amewataka watoa huduma za afya nchini kutoa huduma bora kwa kuzingatia Mwogozo wa Taifa wa Matibabu na orodha ya dawa muhimu huku akiwataka kutoa huduma bora za matibabu kwa kutoa dawa kulingana na mwogonzo unavyobainisha.

“Badala ya kumwandikia unayoitaka wewe au mgonjwa, tumeweka utaratibu weka dawa ambayo ipo kwa mujibu wa mwongozo” alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy amesema kuwa lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha wananchi wanapata dawa katika vituo vya kutolea huduma kwani kumekuwa na malalamiko hapo zamani wagonjwa wakisema madaktari walikuwa waki waambia dawa hakuna huku ili hali dawa zipo.

“Hatutaki kuona wananchi wanalalamika dawa hakuna na kutuona tunadanganya wakati dawa zipo, na mwongozo unasema wazi kama hakuna dawa A mpe dawa B. Alisikika akisema Waziri Ummy.

Ka upande mwingine Waziri Ummy ameupongeza Uongozi wa Hospitali ya Wilaya ya Kilosa kwa kuhakikisha dawa zinapatikana kwa ufanisi muda wote na kuwataka mafanikio ambayo wameyapata wahakikishe waharudi chini.

“Serikali itaendela kuhakikisha inaboresha Sekta ya afya ili Taifa liweze kuwa na nguvu kazi yenye afya bora kazi yenu nyinyi ni kuhakikisha mnaendelea kutoa huduma bora na kuhakikisha dawa zinapatikana muda wote” amesema Waziri Ummy.

Naye Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Dkt. Halima Mangiri ameishukuru Serikali kwa kuuongeza bajeti ya dawa wilayani humo.

Dkt. Mangiri amesema kuwa bajeti ya dawa imekuwa ikiongezeka maradufu mwaka hadi mwaka huku akitolea mfano wa mwaka 2017/18 hali ya upatikanaji wa dawa ilikuwa ni asilimia 86, huku kwa mwaka 2018/19 hali ya upatikanaji dawa ikiongezeka na kufikia asilimia 96.

“Tunaishukuru Serikali, Kwa kweli hali sasa sii kama zamani, tunapata dawa na hali inaridhisha” alisema Dkt Mangiri.

Joseph Kusaga: Ruge aliniambia siku nikifariki , tafadhali msilie

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga, ameeleza kuwa alikutana na Ruge miaka 25 iliyopita wakati akifanya kazi za disko na wakati huo Ruge akiwa mwanafunzi nchini Marekani ambapo walianzisha urafiki kisha kukaa pamoja na kutengeneza wazo la kuanzisha redio.

Kusaga amesema hayo leo Jumamosi, Machi 2, 2019 katika Viwanja vya Karimjee wakati akitoa wasifu wa marehemu Ruge kabla ya kuagwa mwili wake.

“Ruge alipokuja miaka 25 iliyopita, biashara ya kupiga muziki ilikuwa uhuni..tuliiitwa wahuni…..wimbo wa kwanza kutengeneza pale Mawingu uliitwa ‘Oya Msela oooyaaa’…   Tulipopeleka kwenye redio tukaambiwa mnaona sasa wahuni hawa, wimbo gani unaitwa Msela?

“Ruge alitengeneza kina Ruge wengine wengi ambao wapo Clouds, na mimi binafsi kupitia Foundation itakayokuja hivi karibuni nitahakikisha tunaendeleza yale aliyokuwa akifanya Ruge Mutahaba,” alisema Kusaga.

Akielezea kwa utulivu wa majonzi miongoni mwa mambo aliyoambiwa na marehemu, Kusaga alisema kwamba Ruge alimwambia:  “Siku nikifa,  msilie, msherehekee, msifie yale mazuri mtakayoona niliyafanya…”

Kusaga alisema kwamba maneno hayo alimwambia wakati alipokwenda kumwona nchini India wakati wa matibabu yake ambapo alikwenda kwa kushtukiza na ambapo wawili hao walikumbatiana bila kujua kwamba ilikuwa ni mara yao ya mwisho kufanya hivyo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images