Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu Aridhishwa Na Hatua Za Ujenzi Wa Teminarl III katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA)

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea mradi wa ujenzi wa jengo la tatu la abiria katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA) na kusema ameridhishwa hatua iliyofikiwa.
 
Mradi wa ujenzi wa jengo hilo umefikia asilimia 95 na unatarajiwa kukamilika Mei 30, mwaka huu ambapo hadi sasa tayari maeneo mengi yamekamilika ikiwa ni pamoja na sehemu za abiria wanaowasili na kuondoka.

Waziri Mkuu ambaye ametembelea mradi huo jana (Alhamisi, Februari 28, 2019) amesema amefurahi kukuta michoro ya wanyama kama tembo, twiga, bahari, minazi na majahazi ambayo ni alama za nchi.

Kufuatia kukamilika kwa uwanja huo kwa asilimia 95, Waziri Mkuu ameitaka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) ianze kukamilisha  taratibu za kuutumia uwanja huo ili mkandarasi anapoukabidhi uanze kutumika.

Kadhalika, Waziri Mkuu ameipongeza kampuni inayojenga uwanja huo kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa sababu jengo ni zuri na linavutia. Pia amewapongeza Watanzania wanaofanya kazi kwenye mradi huo.

Awali, akisoma taarifa ya mradi huo, Mkurugenzi wa Walaka wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mhandisi Patrick Mfugale alimuelezwa Waziri Mkuu kuwa jengo hilo limekamilika kwa asilimia 95.

Mhandisi huyo alisema tayari wamefanya majaribio ya kwanza ya mifumo na vifaa mbalimbali na kwamba mkandarasi anatarajia kukabidhi mradi huo Mei 31 mwaka huu. Jengo hilo linauwezo kubeba abiria milioni sita.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Akabidhi Kompyuta 25 Ludewa Kuongeza Kiwango Cha Ufaulu Shule Za Sekondari

$
0
0
Na Amiri Kilagalila
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye amegawa kompyuta 25 kwa shule za sekondari za Wilaya ya Ludewa mkoani Njombe zenye thamani ya shilingi milioni 48 kwa lengo la kuwawezesha wanafunzi kujifunzia na waalimu kufundishia, kuongeza uelewa na kupata maarifa kwa kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) kwa kuunganisha kompyuta hizo na mtandao wa intaneti ili kuwawezesha wanafunzi wa Wilaya hiyo kuongeza kiwango cha ufaulu

Nditiye amekabidhi kompyuta hizo kwa Mbunge wa Ludewa, Deo Ngalawa kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Ludewa ili ziweze kutumika kwenye shule mbali mbali zilizopo Wilayani humo

“Nimeleta kompyuta 25 ili zigawiwe kwenye shule mbalimbali ili watoto wajifunze kutumia TEHAMA pamoja na waalimu waliopewa mafunzo ya TEHAMA na taasisi yetu ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF)”, amesema Nditiye. 

Kompyuta hizo zimetolewa na UCSAF ambayo inahusika na ufikishaji wa huduma za mawasiliano vijijini na maeneo yasiyo na mvuto wa kibiashara

Nditiye ameongeza kuwa Wilaya ya Ludewa inafahamika katika kipindi cha miaka ya nyuma kwa kuwa moja ya Wilaya saba nchini ambapo wanafunzi wake wana kipaji cha akili ukilinganisha na Wilaya nyingine zilizopo nchini ambapo ameona ni vema kuwapatia wanafunzi wa shule za Wilaya hiyo kompyuta hizo ili waweze kuongeza ufaulu, kujenga uelewa na kupata maarifa ili waweze kuwa wanafunzi vinara kama iliivyokuwa imezoeleka katika kipindi cha miaka ya nyuma. Pia, amesema kuwa Tanzania inaongoza katika matumizi ya TEHAMA katika Jumuiya ya Afrika Mashariki

Mara baada ya kupokea kompyuta hizo kwa niaba ya wananchi, Mbunge wa Ludewa, Deo Ngalawa alimuomba Mkuu wa Wilaya ya Ludewa, Andrea Tsere kuwa, kuwe na kituo kimoja cha kutunga mitihani Ludewa ili waalimu watunge mtihani wa aina moja na waweze kumaliza kufundisha masomo ya kiada na ziada kama walivyopanga kwa muhula husika wa masomo ili waweze kuwapima wanafunzi wote kwa pamoja

Naye Mkuu wa Wilaya hiyo, Andrea Tsere alimueleza Nditiye kuwa wataweka intaneti kwenye kompyuta hizo ili waalimu na wanafunzi waweze kupata notisi. Pia, amesema kuwa kompyuta hizo zitatumika kuinua kiwango cha elimu na zimefika muda muafaka

“Mmetusaidia sana, umeingia kwenye akili yangu ya kuinua kiwango cha elimu Ludewa,” amesisitiza Tsere wakati akimshukuru Nditiye kwa kuzipatia shule za Wilaya yake kompyuta 25. Tsere amewataka waalimu wakuu wa shule kuzitunza kompyuta hizo na kuzifanyia matengenezo pindi inapohitajika badala ya kuacha ziharibike na pasipo kuzipanga vizuri kwa sababu ni vifaa vya Serikali badala yake wanapanga lini wavichukue badala ya kuzitunza vizuri ili zisaidie wanafunzi wengi na kwa muda mrefu. Aidha, amesisitiza kwa waalimu hao kuwa kompyuta zikipotea na wao wapotee

Katika hatua nyingine, Nditiye amewaeleza wananchi hao kuwa, Wizara yake ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kupitia UCSAF imetoa ruzuku kwa kampuni ya simu ya Halotel na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) ili wajenge minara 11 kwenye maeneo ya mwambao kwa wananchi waishio Wilayani Ludewa kwa kuwa hawana mawasiliano.

“Tunahitaji Ludewa iwasiliane na dunia,” amesisitiza Nditye. Amefafanua kuwa minara tisa imejengwa na kampuni ya Halotel na miwili ni ya TTCL

Vile vile, ameongeza kuwa, ujenzi wa meli ya abiria waishio Ludewa kwa ajili ya usafiri wa Ziwa Nyasa umekamilika ambapo kwa sasa meli hiyo inafanyiwa majaribio kabla ya kuanza safari zake na Serikali inakamilisha ujenzi wa gati za kushusha na kupakia abiria kwenye mwambao wa ziwa hilo kwenye maeneo ya Manda, Lupingu, Nsele, Yiga na Nkanda ambapo meli hiyo inatarajiwa kuanza safari zake za kutoka Ludewa, Njombe hadi Kyela, Mbeya mwezi Aprili mwaka huu

“Tunataka Lupingu hadi Matema watu wapite kwa lami,” amefafanua Nditiye. Ameyasema hayo wakati akiongea na wananchi wa Ludewa mjini na kuwaeleza kuwa  azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha kuwa barabara ya Lusitu – Mawengi yenye urefu wa kilomita 50 inajengwa kwa kiwango cha zege kwa gharama ya shilingi bilioni 159 ambapo tayari mkandarasi wa kutoka nchi ya Korea yupo na anaendelea na ujenzi wa barabara hiyo ili iweze kupitisha madini ya Mchuchuma na Liganga

Ngalawa amewaeleza wananchi kuwa anamshukuru Nditiye kwa kuwa alifanya ziara kutoka Lupingu hadi Manda mwaka jana mwezi wa tatu akiwa na miezi minne tu tangu alipoteuliwa kuwa Naibu Waziri na kushuhudia ukosefu wa mawasiliano kwa wananchi waishio mwambao na sasa minara 11 imejengwa ambapo tayari minara mitatu ya Nkanda, Mawengi na Mahong’olo imewashawa na meli ya abiria pia itaanza safari zake

Tsere alimshukuru Ngalawa kwa kumleta Nditiye ambapo alisafiri na boti siku nzima Ziwani mwaka jana mwezi wa Machi na kushuhudia ukosefu wa mawasiliano kwa kuwa tangu dunia iumbwe wananchi wa mwambao hawajawahi kupata mawasiliano na sasa wanawasiliana.

Benki Ya Maendeleo Ya Afrika-AfDB Yaahidi Kuipatia Tanzania Mikopo Nafuu Kutekeleza Miradi Ya Maendeleo

$
0
0
Na Farida Ramadhani,  WFM, Abidjan
Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) imeahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maedeleo ikiwemo mindombinu ya barabara, umeme na ujenzi wa viwanja vya ndege hususan Kiwanja cha Msalato mkoani Dodoma.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na  Rais wa AfDB, Dkt. Akinwumi Adesina, wakati wa  Mkutano wa Mawaziri wa Fedha wa nchi za Afrika Mashariki, uliofanyika Abidjan nchini Ivory Coast.

Dkt. Mpango,  ambaye pia ni Gavana wa Benki ya Maendelo ya Afrika (AfDB), alisema Rais wa Benki hiyo amekubali ombi la Mhe. Rais, Dkt. John Pombe Magufuli la kuipatia Tanzania mkopo nafuu ili kuwezesha kuanza ujenzi wa kiwanja cha ndege cha Msalato mkoani Dodoma.

"Benki hii imekuwa ni ya msaada mkubwa sana na yapo maeneo mengi ambayo Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika amekubali kuendelea kushirikiana na nchi yetu",  alisema Mhe. Mpango.

Mhe. Mpango alieleza kuwa Dkt. Adesina ameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Magufuli, kwa juhudi zake za kupiga vita rushwa, ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma kwa vitendo, kufanya maamuzi magumu ya kulinda rasilimali za Taifa hususan madini, kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima Serikalini, kuimarisha ukusanyaji wa mapato na kudhibiti ukwepaji kodi.

Alisema kuwa Dkt. Adesina ameahidi kuendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano ambazo zimesababisha Tanzania kupata mafanikio makubwa katika maendeleo kwa kipindi kifupi.

Akizungumza wakati wa  Mkutano wa Mawaziri wa Fedha wa nchi za Afrika Mashariki, Mhe. Mpango aliishukuru  Benki ya Maendeleo ya Afrika kwa kuendelea kuipatia mikopo nafuu kwa ajili ya kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo.

Katika mkutano huo wa Mawaziri, Mhe. Mpango aliuomba  uongozi wa Benki kuharakisha maandalizi ya miradi inayotarajiwa kuanza kutekelezwa mwaka 2019 ikiwemo: Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Msalato (USD milini 200); Ujenzi wa Barabara ya Kuzunguka Jiji la Dodoma (USD  milioni 180).

Miradi mingine ni Mradi wa Kufua Umeme wa Maji (87 MW) wa Kakono (USD milioni 350); Ujenzi wa Barabara ya Bagamoyo-Tanga/Lungalunga-Mombasa-Malindi (USD milioni 158.2); na Awamu ya Pili ya Mpango wa Kuendeleza Utawala Bora na Maendeleo ya Sekta Binafsi (USD milioni 56).

Benki ya Maendeleo ya Afrika imeahidi kuiwezesha Tanzania kupata mikopo nafuu ili miradi hiyo iweze kuanza kutekelezwa mapema. Aidha, iliahidi kuwa mkataba wa Dola za Marekani milioni 256 kwa ajili ya ujenzi ya barabara ya Kabingo-Kasulu-Manyovu (km 260) kwa kiwango cha lami utasainiwa mapema mwanzoni mwa mwezi machi, 2019.

Kwa upande mwingine,  Mawaziri wa  Fedha wa nchi za Afrika Mashariki waliohudhuria mkutano huo, walimuahidi Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika kuwa wataendelea kuunga mkono kusudio la Benki hiyo la kuongeza mtaji ili kuziwezesha nchi wanachama kupata mikopo nafuu kwa ajili kutekeleza miradi ya maendeleo.

Mwisho.

Audio:Weusi X Mwana Fa X Ay - Jasiri

$
0
0
Audio:Weusi X Mwana Fa X Ay - Jasiri

Serikali Kutenga Bajeti Kwa Ajili Ya Uzalishaji Wa Pamba Mbegu Vipara

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Shinyanga
Serikali imeeleza kuwa imejipanga kuimarisha zao la Pamba ili kuongeza uzalishaji nchini kwani kufanya hivyo wakulima watanufaika katika uzalishaji wenye tija na kuimarisha biashara.

Ili kuongeza uzalishaji wa Pamba dhamira ya serikali ni kuanzisha Pamba mbegu vipara ili kuondokana na utumiaji wa pamba manyoya ambayo imezoeleka lakini tija yake ni ndogo katika uzalishaji kuliko Pamba Manyonya.

Naibu Waziri wa Kilimo ameyasema hayo  tarehe 28 Februari 2019 wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Muhunze kilichopo katika Wilaya ya Kishapu wakati wa ziara ya Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan Mkoani Shinyanga.

Alisema kuwa elimu itatolewa kuhusu matumizi ya Pamba mbegu vipara ili kuwajengea uelewa wananchi na serikali kufikia hatua ya kufungamanisha kilimo cha Pamba na uchumi wa viwanda.

Mhe Bashungwa aliongeza kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt JKohn Pombe Magufuli imejipanga kuhakikisha kuwa kilimo kinawakomboa wananchi ili kuimarisha uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla wake.

“Sisi kama Wizara tutakuwa na jukumu la kushawishi wawezaji ili kuwekeza kwenye viwanda vya Pamba nyuzi pamoja na viwanda vya nguo na kufanya hivyo tutakuwa tumetekeleza vyema maelekezo yaliyoainishwa kwenye ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi yam waka 2015-2020” Alikaririwa

Aidha, alisema kuwa Wizara ya Kilimo imejipanga vyema katika kutafuta masoko ya mazao ya wakulima ambapo kwa upande wa zao la mahindi tayari soko limepatikana kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) imesaini mkataba wa mauziano ya mahindi ya Tani 36,000 na Mpango wa Chakula Duniani (WFP).

Katika hatua nyingine alisema kuwa wakulima wa Wilaya ya Kishapu ni miongoni mwa wakulima wa zao la Mtama hivyo kupitia Mpango wa Chakula Duniani (WFP) serikali ya Tanzania inaendelea kujiridhisha uhitaji wa mtama nchini Sudani Kusini ili kuwaunganuisha wakulima na soko hilo.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri huyo ameiagiza Bodi ya Pamba kuhakikisha viuadudu (Viuatifu) vinapatika haraka katika Wilaya ya kishapu ili kuondoa haraka changamoto inayowakumba wakulima kwa kukosekana viuatilifu kwa wakati.

Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi Asikitishwa na Taasisi za Kimataifa Zinazoishutumu Serikali Kabla ya Kuifata Itoe Ufafanuzi

$
0
0
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Taasisi isiyo ya Kiserikali ya “Defend Defenders” Bw. Hassan Shire na Bw. Nicolas Agostini.

Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ubalozi wa Kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa, Geneva nchini Uswisi wakati wa Kikao cha 40 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kinachofanyika Mjini Geneva ambacho Prof. Kabudi anahudhuria.

Prof. Kabudi na viongozi wa Taasisi hiyo wamejadili masuala mbalimbali yanayohusu haki za binadamu nchini ambapo pia walimkabidhi Prof. Kabudi Ripoti yao ya mwaka 2018 ambayo iliishutumu Serikali kwa ukiukwaji wa masuala mbalimbali ya haki za binadamu.

Akizungumza na viongozi hao, Prof. Kabudi alieleza masikitiko yake kwa Taasisi hiyo na Taasisi nyingine kwa kuishutumu Serikali na kutoa ripoti na taarifa mbalimbali ambazo zinatoa shutuma dhidi ya Serikali bila kuwasiliana na Serikali ili kupata ufafanuzi wa shutuma hizo.

Alisema vitendo hivyo vinasababisha upotoshaji mkubwa wa hali halisi ya masuala ya haki za binadamu nchini na jitihada za Serikali katika kutekeleza wajibu wake wa kukuza, kulinda na kuheshimu haki za binadamu.

Prof. Kabudi alisisitiza umuhimu wa taasisi hiyo na taasisi mbalimbali kuishirikisha Serikali ili kupata maelezo kutoka  pande zote na kupata uelewa wa jambo kabla ya kutoa taarifa zao ambazo zinaishutumu Serikali.

Amesema Tanzania kama nchi nyingine inapata changamoto mbalimbali wakati inatekeleza jukumu yake la kulinda, kuheshimu na kukuza haki za binadamu nchini na pale inapoonekana kuwa haitekelezi ipasavyo wajibu iliyonao ni vizuri mashauriano yakafanyika na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kuboresha utekelezaji wa wajibu wa kulinda na kustawisha haki za binadamu kwani mawasiliano yangefanyika ripoti hiyo isingetoka hivyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo ya “Defend Defenders” alikiri kuwa hawakuwasiliana na Serikali kabla ya kutoa ripoti hiyo, na alimshukuru Prof. Kabudi kwa kuridhia kukutana nao na kwamba Taasisi hiyo imepokea ushauri ya Mhe. Waziri na kuahidi kuendelea kujadiliana na Serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria ambayo inasimamia masuala ya haki za binadamu.

Waziri Kabudi alitumia fursa hiyo kuukaribisha uongozi wa Taasisi hiyo Tanzania ili wapate ufafanuzi wa masuala mbalimbali ambayo yameripotiwa kuhusu Tanzania na kama ina maoni au mapendekezo kuhusu namna bora ya kuboresha haki za binadamu nchini wanakaribishwa kujadiliana na Serikali  kupitia Wizara ya Katiba na Sheria.

LIVE: Rais Magufuli, Waziri Mkuu Majaliwa, Kikwete Walivyofika Kumuaga RUGE, Karimjee

$
0
0
LIVE: Rais  Magufuli, Waziri Mkuu Majaliwa, Kikwete Walivyofika Kumuaga RUGE, Karimjee

Rais Mstaafu Jakaya kikwete Ampongeza Lowassa Kurudi CCM

$
0
0
Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt Jakaya Kikwete amempongeza Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kwa uamuzi wake wa kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM).
 
Lowassa alijiunga CHADEMA Julai 2015 baada ya jina lake kuenguliwa kwenye mchakato wa kutafuta mgombea wa urais ndani ya CCM.

"Karibu tena nyumbani, Hongera kwa uamuzi wa busara," ameandika Dkt. Kikwete kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Twitter.

Lowassa alitangaza hapo jana kurejea CCM katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo Lumumba Dar es Salaam na kupokelewa na Mwenyekiti wa CCM taifa, Rais John Magufuli.


Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Super Mbushi Power:ni Maalum Kwa Wenye Matatizo Ya Upungu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
Wanaume wengi wamekuwa na upungufu wa Nguvu za kiume na kuwa na maumbile madogo ya kiume .

Magonjwa kama Kisukari,Presha,Ngiri ya kupanda na kushuka,Tumbo kuunguruma chini ya kitovu,Kutokupata choo vizuri,Tumbo kujaa gesi,Unywaji wa pombe kupita kiasi Pamoja na msongo wa mawazo huchangia kwa kiasi kikubwa upotevu wa nguvu za kiume

Tumia dawa za mitishamba ambayo haina madhara kwa mtumiaji hata awe na miaka 70-85 inatibu na kumaliza matatizo hayo kwa mda mfupi tu.

SUPER MBUSHI POWER:Hii ni dawa yenye uwezo mkubwa wa kuongeza nguvu za kiume mara dufu; huanza kufanya kazi ndani ya dk kumi na tano(15)toka uitumie.
(1)Itakufanya uwe na NGUVU za ajabu ukiwa unafanya tendo la ndoa
(2)Inaongeza hamu ya kurudia tendo la ndoa bila kuchoka.(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 27 kwa tendo la pili nakuendelea bila kuchoka.

NKINDA:INAREFUSHA NA KUNENEPESHA MAUMBILE YA KIUME SAIZI INAYOKUBARIKA KIAFYA KUANZIA nch 3-71/2 NA UNENE CM 2-4.
(4)Itaimalisha mishipa ya uume uliolegea
(5)Inasaidia kusafisha mishipa ya kwenye uume na hivyo kuongeza kasi ya msukumo wa damu ndani yauume,na inasidia kuzarisha HORMONES ZA CETROGEN,Vile vile inazalisha kwa wingi mbegu za kiume yaani(manii)

NGUMO: Ni dawa inayotibu Kisukari kwa mda wa wiki mbili(14)tu nakuwa  nomo.

NGITO:Ni kwale waliochwa na mpenz,mke,hata kwa wewe unayetafuta mchumba majibu ni ndani ya masaa kumi na mbili(12)tu.

WASILIANA NA DR.SEMEKA 

TEL 0753-459433 -ANAPATIKANA MAGOMENI MAPIPA.

Kwanini Uhangaike Na Magonjwa Yanayowezekana Kupona?..........Tiba Sahihi Imewasili

$
0
0
Asilimia 60- 80 ya wanaume wameathilika kisaikologia baada ya kujiona wako tofaut na wengine kimaumbile na kupungukiwa nguvu za kiume , mwanaume aliekamilika kimaumbile anatakiwa awe na maumbile yasiyo pungua nchi 6-8 tofautina hapo anaupungufu ,

zipo sababu nyingi zinazosababisha mapungufu hayo ambazo ni :- upigaji wa punyeto ( mastervation) ,ngili,KISUKARI,vidonda vya tumbo,maumivu ya mgongo ama kiuno,unene(kitambi) tumbo kuunguluma na kujaa ges, matatizo haya huchangia kwa kiasi kikubwa sama kukosa nguvu za kiume vilevile maumbile kuwa madogo na kiingia ndani (kunywea)

GALIMBO 3 POWER :- hii nidawa kiboko kwa matatizo ya nguvu za KIUME,ni dawa ya Asili tuliyo jaaliwa na mwenyezi MUNGU huimarisha misuli ya uume wakati wa tendo la ndoa na kuzalisha viini vya uzazi (manii) vilevile utaludia tendo zaidi ya mara tatu bila ham kuisha pamoja na kuchelewa kufika kilele takiriban dk 20 - 45 kwatendo moja.

SUNUPER :- hii nidawa ya Asili Hurefusha na kune nepesha maumbire madogo ya UUME , hurefusha urefu wa nchi (6-8 )na unene wa sm( 3-4) huanza kufanya kazi masaa machache baada ya kuanza kuitumia,( tiba niyakudumu ikishakutibu,

Nina dawa ya kutokomeza KISUKARI na kupona kabisa hata kama kimekusumbua kwa mda mrefu mpaka ukajikatia tamaa  tiba ipo na utatumia vyakula vyote bila tatizo baada ya kupona ,

Pia ninadawa ya Vidonda vya tumbo,Ngiri, miguu kuwaka moto, mvuto wa mapenz ( kumvuta mke /mme/mpenzi/hawara/ama yoyote unaemuhitaji) dawa za biashara, uzazi kwa akina mama na akina baba (pande zote) pata dawa ya bawasili bila kufanyiwa upasuaji,

KWAMAELEZO NA MSAADA WASILIANA NA DR SILIMBA NAPATIKANA DAR ES SALAAM

 SM O620510598 / 0743543944

Nb km huna nafasi huduma hii inakufikia popote ulipo kwaware wa mikoani tunatuma kwa njia ya mabasi

Lipumba Amshangaa Lowassa Kurudi CCM Mbowe akiwa Gerezani

$
0
0
Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amesema anashangazwa na uamuzi wa Edward Lowassa kurejea CCM katika kipindi ambacho mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akiwa gerezani.
 
Akihojiwa na Gazeti la Mwananchi,  Profesa Lipumba, ambaye mwaka 2015 alijivua uenyekiti kutokana na CUF kuunga mkono Lowassa kugombea urais kwa mgongo wa vyama vinne, amesema hajashangazwa na hatua ya Lowassa kurejea CCM kwa kuwa alijua ingawa hakufahamu siku.

"Lowassa amerudi CCM bila aibu wakati Mbowe bado yupo gerezani. Hakufikiria wenzake anawaachaje," amesema Profesa Lipumba.
 
Lipumba amesema ni vyema wapinzani wakawa na msimamo na kwamba mapambano ya kudai haki yanahitaji muda mrefu si harakaharaka kama walivyofanya Chadema kumchukua Lowassa ili awasaidie kuchukua nchi.

"Niliwaambia Lowassa amekuja upinzani kwa ajili ya madaraka tu. Hiki cha leo ni dhambi ya usaliti waliomfanyia (katibu wa zamani wa Chadema, Willbrod) Dk Slaa inaanza kuwatafuna,” alisema

Waziri Mhagama Awahimiza Watanzania Kupima Virusi vya Ukimwi

$
0
0
JAMII imeshauriwa kupima afya zao mara kwa mara ili kubaini kama wana maambukizi ya VVU ili kupata huduma mapema na kuchukua hatua muhimu ya kunendelea kulinda afya za wasio na maambukizi.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu Mhe.Jenista Mhagama alipokuwa akizindua kituo cha kutolea huduma za tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI katika Mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara Machi1, 2019.

Waziri Mhagama aliwahimiza wananchi kupima VVU  ili kufanikisha mpango wa 90 tatu na kutoa hamasa kubwa kwa wanaume kuwa mstari wa mbele katika kupima afya zao,na wakina mama kisiwe kipimo chao.

“Ili kupunguza maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi nchini, asilimia 95 ya watanzania ambao hawana maambukizi ya Virusi vya UKIMWI inapaswa walindwe ili wasiambukizwe na kundi la wanaume wawe mstari wa mbele kujitokeza kupima afya zao,”alisema Mhagama.

Waziri aliongezea kuwa ni vyema jamii kuendelea kujilinda ili kuepuka maambukizi mapya yanayosababisha takwimu za maambukizi nchini kuongezeka badala ya kupungua.

“Pia asilimia tano ya watanzania ambao wana maambukizi ya virusi vya UKIMWI inapaswa walindwe ili asilimia hizo zisiongezeke kutokana na mpango wa 90 tatu”, alisisitiza Mhagama.

Alisema pia kwenye asilimia hiyo 90 watakaopima na kukuta wamepata maambukizi wanapaswa kutumia dawa za kufubaza virusi vya ukimwi ili kuhakikisha maambukizi mapya yanatokomezwa kabisa hapa nchini.

Aliwataka wananchi wa eneo hilo kutumia kituo hicho kwa kutunza afya zao na kuishi kwa furaha kwani kinawahusu wenye maambukizi na wale wanaohitaji kujua afya zao.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Manyara Mhe.Alexander Mnyeti alisema Mirerani ndiyo sehemu inayoongoza kwenye mkoa huo kwa kuwa na watu wengi wenye maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa kulinganisha maeneo mengine katika mkoa huo.

Alisema maambukizi ya VVU kwa mkoa wa Manyara ni asilimia 2.3 na kwenye mji mdogo wa Mirerani ni asilimia 16 hivyo eneo hilo pekee ndilo linasababisha mkoa huo kuwa na asilimia kubwa za maambukizi na kuwataka wananchi kuchukua hatua za dhati za kupambana kuanzia ngazi ya mtu mmoja mmoja kwa kuhamasisha kupima na kutumia dawa endapo unagundulika na maambukizi.

“Huu ugonjwa umekaa mahali pabaya mno, ningekuwa na jeshi kama lililojenga ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite ningetumia kuzuia UKIMWI lakini siwezi kufanya hivyo ila niwahimize mjitokeze kwa hiari kuja kupima katika kituo hiki,” alisisitiza Mnyeti.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Udhamini wa kudhibiti UKIMWI, Bw. Godfrey Simbeye alisema kituo hicho kimegharimu jumla ya shilingi Milioni 250 ambapo shilingi Milioni 200 ni kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la Kituo na Shilingi Milioni 50, ununuzi wa samani na vifaa tiba na litahudumia watu 49,802.

Simbeye ameiomba serikali isaidie mfuko kuhakikisha kinapatikana chanzo cha uhakika cha upatikanaji wa fedha kwani michango pekee haitoshelezi Mfuko huu .

Aidha amewaomba wadau wengine na wafanyabiashara kujitokeza kuchangia katika mfuko huo kupitia namba ya simu 0684 909090 ili kuendelea kudhibiti VVU na UKIMWI nchini.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Dkt. Leonard Maboko alisisitizia umuhimu wa wananchi kushiriki na kutumia kituo hicho kikamilifu kipima afya zao na kuanza dawa kwa kadri watakavyoelekezwa na wahudumu wa afya.

Mbunge wa jimbo la Simanjiro Mhe. James Ole Millya aliishukuru Serikali kwa kufanikisha ujenzi wa kituo hicho na kuwaasa wananchi kujikinga na maambukizi mapya ya VVU ili kuendelea kuwa na afya njema na kujiletea maendeleo yao.

Mwakilishi wa watu wanaoishi na VVU  Wilayani Simanjiro, Wariandumi Kweka alisema kituo hicho kitawasaidia kwani awali walikuwa wanakwenda umbali mrefu kufuata huduma hiyo na wengi kukatishwa tamaa na hali hiyo na kuendelea kuitaka jamii kubadili mitazamo hasi juu yao na kuwapa ushirikiano na kupinga imani potofu za baadhi ya madhehebu  yanayopinga matumizi ya dawa hizo kwa imani ya  kupona bila kutumia dawa za kufubaza virusi hivyo.

Mtoto wa Ruge Mutahaba amuombea msamaha baba yake

$
0
0
Familia ya Ruge Mutahaba wamesema wanatambua Ruge aliwahi kuwakosea watu kwa kuwa yeye ni binadamu hajakamalika.

Mtoto mkubwa wa Ruge aitwaye Mwachi  amesema Familia inaomba msamaha kwa niaba yake na imewasamehe wote waliomkosea pia.

“Ninamuombea msamaha baba yangu kwa wale wote aliowakosea enzi za uhai wake, nasi tunawasamehe wote waliomkosea baba,” amesema Mwachi wakati akisoma wasifu wa baba yake

Amesema baba yake alikuwa mtu aliyejitoa kwa wengine mpaka familia ilifikia wakati inaona watu wa nje wanamfaidi kuliko wao.

“Alitenga muda mwingi kusaidia kwa kuzingatia misingi ya utu, alipambana kwa hali zote kufanikisha mambo mengi katika jamii,” alisema huku akijitahidi kujizuia kutoa machozi.

Rais Dkt Magufuli Aongoza Maelfu Ya Waombolezaji Kuuaga Mwili Wa Marehemu Ruge Mutahaba Jijini Dar Es Salaam

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa heshima zake za mwisho kwa Marehemu Ruge Mutahaba alipoongoza maelfu ya waombolezaji kuuaga mwili wa marehemu ambaye aliyekuwa Mkurugenzi wa Uzalishaji na Vipindi wa Clouds Entertainment kwenye hafla iliyofanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam leo Jumamosi March 2, 2019


Kutana na Dr Majebele Kutoka Mwagala Ukoo wa Watemi .....Anatibu Busha, Nguvu za Kiume, Vidonda vya Tumbo, Presha

$
0
0
DR MAJEBELE KUTOKA MWAGALA UKOO WA WATEMI NI MTANZANIA HALISI.
**********************************
Anatoa tiba ya mitishamba iliyo na ubora asilia ya kienyeji.
🔖(1)Anatatua tatizo la nguvu za kiume linalowatesa wanaume wengi duniani_chanzo Cha tatizo hilo ni maelezo mafupi yafuatayo:
♦Kama uliwahi kuugua kichocho wakati yu mdogo mbeleni nguvu za kiume lazima zipungue.
♦Kama uliwahi kuwa na chango lolote nguvu za kiume lazima zipungue.
♦Vyakula vya kisasa, mafuta mengi, msongo wa mawazo, kukaa kipindi kirefu zaidi ya masaa 8,.
________________________________
📌MWAGALA 4 POWER,
NI dawa iliyochanganywa mizizi 66 .NI Bora na yenye kutoa tatizo la kutokua na  nguvu za kiume kwa kina baba pia inafanya kazi kwa haraka sana,okoa ndoa yako Sasa usitembee na aibu,kimoja kwa dakika 2 na huwez kurudia tena tiba Sasa yapatikanikal,usinywe dawa ya kuongeza nguvu kunywa dawa ya kuponyesha tatizo la nguvu miaka mingi,ni dawa ya mfumo wa   unga tu
🔸NI dozi ya siku 7🔸
Utakua umepona milele,pia unaruhusiwa kutumia kama Kinga inafanya kazi ndani ya masaa 2
MWAGALA 4 POWER Sasa ni suluhisho la nguvu za kiume.
________________________________
📌LUGOBHI na NGOLOLO ni   dawa ya kubadili maumbile yaliyosinyaa na kurefusha usilalamike uume mfupi tumia LUGOBHI utarefuka size uitakayo,tumia NGOLOLO kwa kuufanya uume uwe mnene size uitakayo dozi siku 7 
🔸mabadiliko ndani ya siku 2 ipo ktk mfumo wa unga tu.🔸
________________________________
📌UGOMOLA,
Ni mchanganyiko wa miti 8 wenye kutibu kisukari ulichosumbuka nacho kwa mda mrefu iwe ya kupanda au kushuka, dawa hii inaponesha kabisa dozi siku 18 na itakupa mabadiliko mazuri sana kabla ya siku 18,anaruhusiwa kutumia mwny umri wa miaka15_ na kuendelea.
🔸Ni mfumo wa unga tu.🔸

📌IDUNI,
Ni mchanganyiko wa miti 4 yenye kutibu presha kwa haraka sana.
🔸dozi siku 3 ina mfumo wa unga.🔸
________________________________
📌KOONYA,
Ni dawa ya mchanganyiko wa miti 10 inayotibu tezi dume kwa mda wa siku 14 haihitaji kulazwa unatumia na kuendelea kufanya mambo yako,
🔸NI mfumo wa unga tu🔸
________________________________
📌MALEMALE,
Hutibu busha bila operation na kusambaa kabisa kwa siku 20.
🔸Dawa hii IPO katika mfumo wa unga tu.🔸
________________________________
📌MWENDO WA YEGE,
Ni dawa yenye kufanikisha:
🔖Kumvuta umpendae aliyekuacha wakati bado unampenda pia
🔖Inafanya kazi kwa haraka sana.
🔸Matokeo ndani ya masaa 4,ina mfumo wa unga tu🔸
________________________________
📌KONDWAHULI,
NI dawa yenye uwezo mkubwa kuzuia CHUMAULETE, iwe:
🔖Nyumbani au katika
🔖Biashara pia
🔸Haina kikomo ni hadi milele🔸
________________________________
📌SALE,NI dawa ya kutibu miguu,kiuno magoti kuwaka Moto,
🔸Dozi siku 10, Mfumo wa unga.🔸
________________________________
📌MALELA,
NI dawa ya kutibu:
🔖Vidonda vya tumbo
🔖Tumbo kujaa gesi
🔖Minyoo tumboni
🔖Kilungulila au muungurumo tumboni.
🔸mfumo wa unga  dozi siku 5🔶
________________________________
📌SALIUNGU,NI dawa ya kuvutia wateja ktk biashara yako unayofanya..
________________________________

📌TOBO,NI dawa ya uzazi kwa akina mama waliohangaika  bila kupata watoto kwa mda mrefu,kutoa uvimbe tumboni,pia kupanga mayai yaliyo mbali na kumaliza chango lolote.dozi NI siku 12 na kupona kabisa,NI mfumo wa unga tu.
________________________________
📌NUNDANUNDA,ni dawa inayotibu kupooza/strock,msongo wa mawazo na uti wa mgongo.
________________________________
📍Kama una tatizo ambalo halijaorodheshwa hapo utanifahamisha,huduma kuanzia saa 1 asubuhi_1jioni.kama huwezi kufika nilipo nakuletea dawa mwenyewe unayohitaji..Nipo ktk mikoa miwili tu SHINYANGA &DAR ES SALAAM (kinondoni na temeke)..Piga namba
📞+255 753 928 576 (WhatsApp)
📞+255 716 608 959
----------------------------------------
For non tanzanian residents, please contact us through Whatsapp number
📞 +255 753 928 576
For the delivery of our services
______________________________
________________________________

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Magonjwa yanayoababisha Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Ni Kama Vile, Kisukari ,presha, Ngiri Ya Kupanda Na Kushuka, Kiuno, Maumivu Ya Mgongo, Tumbo Kuuma Chini Ya Kitovu, Tumbo Kujaa Gesi. Yote Matatizo Yote Haya husababisha Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Kushindwa Kufanya Kazi Kwa Mwenza Wako  .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa Dar anapatikana mbagala Zakhem.  Songea ,bombambili, Shinyanga, Kahama ,mjini, Kwa ,maelezo, Zaidi , Piga Simu 0763172670/ 0715172670,/ ,Sema ,haloo, Dr Sitta... Wote  mnakalibishwa. 

PICHA:Harmonize, Babu Tale Waungana na Waombolezaji Karimjee Kumuaga Ruge Mutagaba

$
0
0
Babu Tale ambaye ni mmoja wa mameneja wa mwanamuziki, Diamond Platnumz amefika katika viwanja vya Karimjee inapoendelea shughuli ya kumuaga aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji, Ruge Mutahaba.

Mbali na Babu Tale, Msanii Harmonuze naye keshafika kujumuika na waombolezaji kuuaga Mwili wa Ruge.

Uwepo wa Babu Tale na Harmonize katika viwanja hivyo umekuwa kivutio kutokana na uhasimu wa kibiashara uliopo baina ya Clouds Media Group na Wasafi Media.

Audio:Gozbert Goodluck - Tutaonana Tena

$
0
0
Audio:Gozbert Goodluck - Tutaonana Tena

Picha 4: Msanii Diamond Platnumz Awasili Ukumbi wa Karimjee Kumuaga Ruge Mutahaba

$
0
0
Msanii Diamond Platnumz na Mama yake mzazi Bi Sandra, wamefika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam kuungana na watanzania waliojitokeza katika taratibu za kuuaga mwili wa Marehemu Ruge Mutahaba.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images