Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Askari Watano Wapewa Zawadi Ya 1,500,000 Baada Ya Kukataa Rushwa Kutoka Kwa Wachina Wamiliki Wa Mashine Za Kamali

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni ,Dodoma.
Askari watano mkoani Dodoma wamepewa zawadi ya Tsh.Milioni Moja na Nusu kutoka kwa ofisi ya kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa baada ya kukataa rushwa ya Tsh.Milioni 1 Kutoka kwa Wamiliki wa Mashine za kuchezea kamali Raia wa China.
 
Akizungumza na waandishi wa habari Leo Februari 22,Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma Gilles Murroto  amewataja askari waliopewa Motisha hiyo ili waendelee kuchapa kazi zaidi ni Inspekta Ntilungila,F 3129 Coplo Edward,G 2856 D/C  Ahmed,G 1973 D/C Edward na wa tano ni askari mwenye No.G 6593 PC Stanley.
 
Raia wa Kichina waliokamatwa wakitaka kutoa hongo hiyo ni Chen Xian Wen[35],Chen Ji[21] na Mwingine ni Lin Bibi[30].
 
Kamanda Murroto ameendelea kufafanua kuwa ,Jeshi la polisi Mkoa wa Dodoma limefanikiwa kukamata jumla ya watuhumumiwa  wa makosa mbalimbali 49 pamoja na  mali mbalimbali za wizi zikiwemo mashine za kuchezea kamali 138.
 
Katika wilaya ya Dodoma, Zimekamatwa Jumla ya mashine  za kamali 77 na watuhumiwa 12  wakiwemo Raia wa china na kusema kuwa  Raia hao wa china ndio wamiliki  na wasambazaji wakuu wa mashine hizo ambapo wakati wanakamatwa  walikutwa na mashine  62 wakiwa wamezificha  baada ya kupata taarifa ya kuwepo msako mkali  wa mashine hizo.
 
Pia, Muroto amesema kuwa vijana wengi wamekuwa wakicheza michezo hiyo ambapo wao ndio nguvu kazi ambayo inatakiwa kuwa kazini na kuwataka Vijana kuchangamkia fursa zilizopo Jijini Dodoma na kuachana na Vitendo hivyo .
 
Aidha Kamanda Murroto amesema kuwa wamekamata mafurushi yenye nguo mbalimbali wanazotumia watalii kupandia Mlima Kilimanjaro .
 
Vifaa hivyo ni pamoja na makoti ambayo yaliiibwa Kilimanjaro na kuanza kusafirishwa kupitia Gari La Machame.
 
Vilevile Kamanda Muroto amesema  tarehe 20/2/2019 wilayani Chamwino Mkoani Dodoma alikamatwa Tumaini Makali [28]mkazi wa kijiji cha Mahama tarafa ya Chilonwa wilayani Chamwino akiwa na Dawa za kulevya  aina ya bhangi kete 93 yalikuwa yamehifadhiwa kwenye mfuko wa nailoni maarufu RAMBO  akiwa anauza nyumbani kwake.
 
Tukio jingine ni MICHAEL TANDALA na wenzake 8 wote wakazi wa kijiji cha Mvumi  wilayani Chamwino walikamatwa wakiwa na bangi kavu kg 2 pamoja na mbegu.
 
Kwa upande wake mkuu wa Mkoa Dodoma Dkt Binilith Mahenge amelipongeza jeshi la polisi la mkoa wa Dodoma linaloongozwa na kamanda muroto kwa kazi kubwa wanayo ifanya pamoja na kupiga marufuku kwa nyumba yeyote ya mtu Binafsi kuwa na mashine hizo.
 
Katika hatua nyingine Dkt Mahenge amewataka wazazi kuwafuatilia watoto wao ili wasijiingize katika vitendo ambavyo si salama kwao. 
 
Mbali na hilo Kamanda muroto amesema katika wilaya ya chamwino  Mkoani Hapa  amekamatwa  Tumaini  Makali (28) mkazi wa kijiji cha Mahama  Tarafa ya Chilonwa , Wilayani Chamwino akiwa na madawa ya kulevya yadhaniwayo kuwa ni Bhangi  kete 93 ambayo yalikuwa yamehifadhiwa  kwenye mfuko wa nailoni  maarufu kama Rambo, akiwa anayauza nyumbani kwake.     
 
Hatahivyo,  Kamanda Muroto amesema kuwa jeshi la polisi litawachukulia hatua wale wote watakao kamatwa kwa kushawishi  kutoa rushwa au kupokea rushwa kutoka kwa mtu yeyote Yule   

MWISHO.

Serikali Yasitisha Kuipatia Manispaa Ya Kinondoni Sh. Bilioni 38 Za Miradi Ya Kimkakati

$
0
0

Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam
SERIKALI KUU imezuia shilingi bilioni 38 zilizokuwa zielekezwe kwenye utekelezaji wa miradi mitatu ya Kimkakati ya kuijengea uwezo wa kimapato Manispaa ya Kinondoni, mkoani Dar es Salaam, baada ya kubainika kuwa utekelezaji wa mradi wa Soko la Kisasa la Magomeni uliopatiwa fedha zaidi ya shilingi bilioni 8.5, unasuasua.

Uamuzi huo umetolewa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, wakati akifanya majumuisho ya ziara yake ya siku tatu mkoani Dar es Salaam ambapo amekagua miradi kadhaa ya kimkakati iliyopewa ruzuku na Serikali na kubainika kuwa haitekelezwi kwa mujibu wa mikataba.

Miradi mitatu iliyoguswa na uamuzi huo wa Serikali ni Mradi wa uendelezaji wa Ufukwe wa Oyterbay wenye thamani ya shilingi bilioni 14.1, mradi wa Soko la Kisasa la Tandale wenye thamani ya shilingi bilioni 9.7 na mradi wa soko la Kisasa la Kibada wenye thamani ya shilingi bilioni 14, yote ikiwa katika Manispaa hiyo ya Kinondoni.

"Hatutaleta fedha hizi ambazo ni utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya awamu ya pili ambayo Manispaa ya Kinondoni ilipewa ruzuku na mikataba yake kusainiwa mwezi Februari 5, 2019 mpaka hapo tutakapo jiridhisha na utekelezaji wa mradi huo wa Soko la Kisasa la Magomeni kwa sababu watendaji wanaosimamia mradi huo ni wale wale ambao wangesimamia miradi hiyo mipya mitatu" alisema Dkt. Kijaji

Dkt. Kijaji amewataka wakuu wa Wilaya za Ilala, Kinondoni na Ubungo kuhakikisha kuwa wanaisimamia kwa karibu miradi yote ya kimkakati inayotekelezwa katika maeneo yao ili kutimiza dhamira ya Serikali ya Awamu ya tano ya Dkt. John Pombe Magufuli, ya kuziwezesha Mamlaka ya Serikali za Mitaa kujitegemea ili ziweze kutoa huduma bora kwa wananchi.

Vilevile Dkt. Kiaji ameonya kuwa miradi yote ya kimkakati inayoendelea kutekelezwa nchini isiingizwe siasa ndani yake kwa kuwa itaharibu maana yake ya kuwa miradi ambayo Serikali imeridhia kuipa fedha ili ianzishwe kwa ajili ya kuchochea maisha na uchumi wa wananchi.

Akiwa ziarani mkoani Dar es Salaam, Dkt. Ashatu Kijaji, alikagua utekelezaji wa miradi ya kimkakati ambayo ni sehemu ya miradi 22 ya awamu ya kwanza ambayo serikali ilitoa ruzuku ya zaidi ya shilingi bilioni 147 mwezi Mei, 2018, ukiwemo mradi wa soko la kisasa la Kisutu, Soko la Kisasa la Mburahati,  Soko la Kisasa la Magomeni, Ujenzi wa Kituo cha Mabasi Mbezi Louis, na Ujenzi wa machinjio ya Kisasa ya Vingunguti.

Akiwa katika Soko la Kisutu, Dkt. Kijaji alielezea kutoridhishwa kwake na kasi ya ujenzi wa soko hilo na kuutaka uongozi wa Wilaya na Manispaa ya Ilala kungeza kasi ya ujenzi wa soko hilo linalosubiriwa kwa hamu kubwa na wakazi wa Wilaya ya  Ilala.

Katika Soko la Magomeni, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, amezuia Sh. bilioni 5.5 ambazo zilipaswa kutumika kutekeleza mradi wa Kimkakati wa Soko la Magomeni, liliko wilaya ya Kinondoni, kutokana na kucheleweshwa kwa utekelezaji wa mradi huo licha ya kupewa sh. bilioni 3 za kianzio miezi kadhaa iliyopita lakini utekelezaji wake unasuasua.

Akiwa katika Soko la Kisasa la Vingunguti, ameinyang'anya Manispaa ya Ilala, mkoani Dar es Salaam shilingi bilioni 3 ilizoipatia kwa ajili ya kutekeleza mradi wa Kimkakati wa Machinjio ya Kisasa wa Vingunguti, baada ya Manispaa hiyo kushindwa kuanza kutekeleza mradi huo wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 8.5.

Dkt. Kijaji pia alitembelea ujenzi wa Mradi wa Kituo Kikuu kipya cha Mabasi yaendayo ndani na nje ya nchi cha Mbezi Louis ambacho ujenzi wake utagharimu shilingi bilioni 50.9 na kuelezea kuridhishwa kwa kiasi fulani na utekelezaji wake lakini akautaka uongozi wa Wilaya ya Ubungo kuongeza kasi ya ujenzi huo ambao kukamilika kwake kutaliwezesha Jiji la Dar es Salaam kuingiza mapato ya zaidi ya sh. bilioni 7 kwa mwaka.

Akiwa katika Soko la Mburahati, Wilaya ya Ubungo, Dkt. Kijaji alionya kuhusu mabadiliko yoyote ya michoro ama usanifu wa mradi huo unaotekelezwa kwa ubia kati ya Sekta Binafsi na Serikali wenye thamani ya shilingi bilioni 2 ambapo Serikali imetoa zaidi shilingi milioni 900, kwamba usije ukaongeza gharama za ujenzi kwa sababu Serikali haiko tayari kutoa fedha za nyongeza.

Mwisho

Makamu Wa Rais, Samia Suluhu Hassan Aongoza Mazishi Ya Mtoto Wa Waziri Kigwangalla

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan  ameongoza  shughuli za  mazishi  ya  Zulqarinain mtoto wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Hamisi Kigwangalla  yaliyofanyika leo Ijumaa Februari 22, 2019 saa kumi jioni katika kijiji cha Puge,  Nzega vijijini jimboni kwa Waziri Kigwangalla.

Mazishi hayo yamehudhuriwa na   viongozi mbalimbali wakiwemo baadhi ya Mawaziri, Manaibu Waziri Wabunge pamoja  na Watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii.

Marehemu Zul alifikwa na mauti  jana majira ya saa nne asubuhi   JAKAYA KIKWETE CARDIAC INSTITUTE katika hospitali ya taifa ya Muhimbili  alikokuwa   amelazwa   akiwa anasumbuliwa na tatizo la moyo.

#R.I.P Zul.

Inna lillahi wainna illaihi rajiuun

 

Wachimbaji madini watakiwa kuwa na Mpango wa Ufungaji Mgodi

$
0
0
Na Greyson Mwase, Pwani
Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amewataka wachimbaji wa madini  ya ujenzi aina ya kokoto katika mkoa wa Pwani kuwa na Mpango wa Ufungaji Mgodi utakaotumika kama mwongozo wa kuhakikisha mazingira yanaachwa yakiwa katika hali salama mara baada ya kumalizika kwa shughuli za uchimbaji wa madini hayo.

Profesa Kikula aliyasema hayo jana tarehe 21 Februari, 2019 katika nyakati tofauti alipofanya ziara yake katika migodi  inayojishughulisha na shughuli za uchimbaji wa madini ujenzi aina ya kokoto iliyopo katika Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani yenye lengo la kutembelea wachimbaji wa madini hayo pamoja na kusikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili.

Profesa Kikula katika ziara hiyo akiwa ameambatana na Kamishna – Tume ya Madini, Dkt. Athanas Macheyeki, wataalam kutoka Makao Makuu ya Tume ya Madini jijini Dodoma, Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Ofisi ya Afisa Migodi Mkazi wa Lugoba pamoja na waandishi wa habari, Profesa Kikula alitembelea migodi ya Sisti Mganga, Gulf Concrete Company Limited na  Yaate Company Limited iliyopo katika Wilaya ya Bagamoyo.

Akizungumza katika nyakati tofauti mara baada ya kutembelea migodi hiyo, Profesa Kikula aliwataka wamiliki wa migodi kuhakikisha wanakuwa na mipango ya ufungaji migodi mapema badala ya kusubiri mpaka shughuli za uchimbaji madini zinapomalizika hivyo kufanya zoezi la ufungaji wa migodi kuwa gumu huku wakiacha mazingira yakiwa hatarishi.

“Ninapenda kuwakumbusha kuwa suala la kuwa na Mpango wa Ufungaji wa Migodi ni la lazima kulingana na Sheria ya Madini pamoja na kanuni zake, hivyo ninawataka kuhakikisha mnakuwa na mpango ili kuhakikisha mashimo hayaachwi wazi,” alisema Profesa Kikula.

Awali akiwa katika mgodi unaomilikiwa na Sisti Mganga Profesa Kikula  alielezwa mafanikio ya mgodi huo ikiwa ni pamoja na kokoto za mgodi huo kutumika katika ujenzi wa daraja la Mto Wami uliopo mkoani Pwani,  reli ya kisasa ya standard gauge na utengenezaji wa marumaru kwa ajili ya soko la ndani ya nchi.

Katika hatua nyingine Mganga alitaja changamoto zinazoukumba mgodi huo kuwa ni pamoja na tozo kubwa kutoka katika halmashauri na tozo nyingine zinazotozwa na kijiji cha Kihangaiko  pasipo kuwa na risiti pamoja na ukosefu wa vifaa vya kisasa.

Profesa Kikula alisema kuwa, suala la tozo litafanyiwa kazi kwa kuliwasilisha mamlaka za juu kwa ajili ya kufanyiwa kazi na kusisitiza kuwa nia ya Serikali kupitia Tume ya Madini, ni kuhakikisha wachimbaji wa madini hususan wadogo wanafanya kazi katika mazingira mazuri yenye faida kubwa huku wakilipa kodi mbalimbali Serikalini pasipo vikwazo vyovyote.

Wakati huo huo, akiwa katika mgodi wa uzalishaji wa kokoto wa Gulf  Concrete Limited Profesa Kikula alitoa mwezi mmoja kwa uongozi wa mgodi huo kuhakikisha wanarekebisha kasoro ya mazingira kwa kuhakikisha vumbi linalotoka wakati wa shughuli za uchimbaji wa kokoto halisambai kwani linaathiri wananchi  wa vijiji vya jirani katika mgodi huo.

Alisema ni vyema wakazingatia Sheria ya Mazingira kwani vumbi mbali na kuathiri wananchi wanaoishi katika vijiji vya jirani linaweza kuathiri wafanyakazi wa mgodi huo.

Aidha, alituaka mgodi huo kuendelea kuhakikisha unatoa huduma kwa jamii inayozunguka mgodi huo na kutumia huduma za ndani ya nchi kama vile bidhaa pamoja na ajira kwa wazawa.

Katika hatua nyingine, Profesa Kikula akiwa katika mgodi wa kuzalisha kokoto wa Yaate Co. Limited, mbali na kuupongeza mgodi kwa kuaminiwa na kupewa kazi ya kusambaza kokoto kwenye mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa ya standard gauge unaotelekezwa na kampuni ya Yapi  Merkezi na kutoa huduma mbalimbali kwa jamii inayouzunguka mgodi huo pamoja na ajira, aliutaka mgodi huo kuendelea kununua bidhaa/huduma kutoka kwa wananchi.

“Kutoa huduma bora kwa wananchi wanaozunguka mgodi kunaboresha mahusiano na kupunguza migogoro ya mara kwa mara inayoweza kujitokeza.

Awali akielezea mafanikio ya mgodi, Mkurugenzi Mtendaji wa Yaate Co. Limited, Eugen Mikongoti alisema  mradi umenufaisha watanzania wengi kwa kuchangia maendeleo ikiwa ni pamoja na ulipaji wa zaidi ya shilingi bilioni 1.31 ambazo zimelipwa kama ushuru wa madini  kati ya kipindi cha mwezi Juni, 2018 hadi Januari, 2019 na shilingi milioni 338.8 zilizolipwa kama mrabaha.

Alieleza mafanikio mengine kuwa ni pamoja na utoaji wa fursa za ajira kwa watanzania hususan vijana wanaozunguka mgodi na kuziwezesha kampuni zinazomilikiwa na wazawa kushiriki katika miradi mikubwa  hivyo kuzijengea uwezo wa kitaalam na kupata fursa.

Mikongoti alitaja mafanikio mengine kuwa ni pamoja na kuwezesha maendeleo ya wanachi wanoishi karibu na mgodi kupitia huduma za jamii ambapo mpaka  sasa mgodi huo unaendelea na ujenzi wa nyumba za watumishi na kuhudumia wananchi katika zahanati iliyopo mgodini.

Katika hatua nyingine Mikongoti alipongeza kazi kubwa zinazofanywa na Tume ya Madini chini ya Mwenyekiti wake Profesa Kikula ikiwa ni pamoja na kuwatembelea, kuwapa elimu na kutatua changamoto mbalimbali.

Ujenzi Wa Viwanda Vya Dawa Kuokoa Mabilion Ya Shilingi Nchini

$
0
0
Na WAMJW – PWANI
WAZIRI Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu leo amefanya ziara ya kukagua Maendeleo ya ujenzi wa kiwanda vya Dawa cha Vista Pharma Ltd na Kairuki Pharmaceutical Ltd  vinavyoendelea kujengwa kwa kasi katika Mkoa wa Pwani.

Katika ziara hiyo Waziri Ummy alilenga kujionea na kutatua Changamoto zinazowakumba Wawekezaji nchini hususani katika Viwanda vya Dawa ili kuokoa kiasi kikubwa cha fedha kinachoendelea kupotea kutokana na kuagiza Dawa nje ya nchi.

Waziri Ummy amesema kuwa katika kila Shilingi 100 ambayo Serkkali inatumia kununua Dawa, Vifaa na Vifaa Tiba, Shilingi 94 inapotea nje ya nchi, ambapo kumalizika kwa Viwanda hivi kutasaidia pesa hiyo kubaki ndani ya nchi na kutumika katika shughuli nyingine za  Maendeleo kwa Wananchi.

“Katika kila Shilingi 100 ambayo Serikali inatumia kununua Dawa, Vifaa na Vifaa Tiba, Shilingi 94 tunaipeleka nje ya nchi kununua Dawa, Vifaa na Vifaa Tiba, na ndiomaana nimefanya ziara hii pamoja na viongozi wa Mkoa na kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara na Kituo cha uwekezaji ili kuokoa fedha hiyo inayopotea nje ya nchi” alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy aliendele kusema kuwa kumalizika kwa Viwanda hivi kutasaidia kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa Dawa za kutosha na kwa bei rahisi, jambo litalosaidia kuimarika kwa huduma za Afya nchini.

 ”Dawa kupatikana kwa wingi na kwa bei rahisi na kwa haraka zaidi, kwasababu kuagiza Dawa nje ya nchi MSD anatumia mpaka miezi 6  mpaka ifike Tanzania” alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy amewaagiza Tanesco ndani ya Mkoa kuhakikisha wanaleta huduma ya umeme ndani ya wiki moja ili hatua za mwanzo za ufungaji wa mashine katika Viwanda hivyo uanze Mara moja.

Pia, Waziri Ummy amewaagiza Mamlaka ya Maji Mkoani Mkoa wa Pwani kuhakikisha wanaleta huduma ya maji ndani ya Machi 15 katika eneo hilo la Viwanda ili kuharakisha shughuli za ujenzi.

Mbali na hayo, Waziri Ummy amewashukuru wawekezaji hao wa Ndani kwa maamuzi mazuri aliyochukua ya kuwekeza katika Viwanda vya Dawa ili kuisaidia Jamii ya Watanzania ambao Dawa bado imekuwa ni changamoto licha ya Jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali katika kukabikiana na changamoto hiyo.

#TunaboreshaAfya

Waziri Wa Kilimo Abainisha Jitihada Za Serrikali Kwenye Mapinduzi Ya Kilimo Nchini

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam
Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mheshimiwa Dr. John Pombe Joseph Magufuli, imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali katika kuweka mazingira bora ya kuleta mapinduzi katika kilimo.

Japokuwa Kilimo kinachangia karibu asilimia 30 ya Pato la Taifa, ukuaji wa Sekta ya Kilimo bado hauridhishi kutokana na changamoto zilizopo, japo kumekuwepo na mwelekeo chanya katika siku za karibuni. Kulingana na taarifa zilizopo za hivi karibuni ukuaji wa sekta ya kilimo umefikia asilimia 7.1

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameyasema hayo jana tarehe 21 Februari 2019 wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa wadau wa asasi zinazotoa huduma ndogo za fedha vijijini kwa Wajasiriamali Wadogo (TAMFI) katika ukumbi wa mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania – Dar es salaam.

Alisema kuwa kwa kutambua hilo, Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Wizara za Sekta ya Kilimo (ASLMs) kwa kushirikiana na wadau wa sekta inatekeleza Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo Awamu ya Pili (Agricultural Sector Development Programme Phase Two-ASDPII).
 
Lengo kuu la ASDP II ni kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo (mazao, mifugo na uvuvi) ili kuongeza uzalishaji na tija, kufanya kilimo kiwe cha kibiashara na kuongeza pato la wakulima wadogo kwa ajili ya kuboresha maisha na usalama wa chakula na lishe.
 
Alisema kuwa Utekelezaji wa lengo hilo ni kuhakikisha kuwa Taifa linaendelea kujitosheleza kwa chakula; kuimarisha uchumi; kuwa kichocheo cha kukua kwa viwanda; na kuongeza ajira. Ili kufikia malengo haya; Utekelezaji wa ASDP II utazingatia mnyororo wa thamani wa mazao ya kipaumbele ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
 
Alizitaja jitihada zingine katika kuleta mapinduzi ya kilimo ambazo ni Kuanzishwa kwa eneo maalum la kuboresha mnyororo wa thamani kwa mazao mbalimbali (yaani The Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania (SAGCOT), Kuanzishwa kwa Program ya Miundo Mbinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (yaani Marketing Infrastructure, Value Addition and Rural Finance Support Programme –MIVARF) ambao lengo lake kuu ni kusaidia nyanja mbalimbali muhimu katika kuendeleza kilimo cha kisasa nchini na Kuanzishwa kwa Benki ya Kilimo (yaani TADB) ili kurahisisha upatikanaji wa mikopo nafuu kwa wakulima na shughuli za kilimo nchini.
 
Alisema kuwa Jitihada za dhati zinahitajika kuwashawishi vijana kwa njia mbalimbali ili nao waingie katika biashara ya kilimo hasa katika uboreshaji wa mnyororo wa thamani kutokea shambani hadi kwa mlaji.

Kuwepo kwa huduma kama bima ya afya kwa wakulima na makazi bora kunaweza kuwa kichocheo kikubwa cha kuwafanya watu wengi zaidi haswa vijana kujihusisha na kilimo kwa njia za kisasa zaidi na usalama wa afya zao na makazi yao pia.

Allisema kuwa hiyo itakuwa njia bora ya kutatua mahitaji yao na kuwasaidia wakulima vijana kufanya shughuli za kilimo pamoja na kilimo biashara kwa ufanisi. “Umefika wakati sasa tuhamasishe kuwa na Kilimo cha mashamba makubwa na ya kati yatakayopelekea kuzalisha kwa wingi na kwa tija” Alikaririwa Mhe Hasunga
 
Mkutano huo utafanyika kwa siku mbili kuanzia leo tarehe 21 Februari 2019 mpaka kesho tarehe 22 Februari 2019 ukiwa na lengo la kujadili namna bora ya kuwajengea wakulima uwezo wa kustahimili matukio mbalimbali kwa kutumia huduma za fedha vijijini, namna ya kuwanufaisha wakulima na huduma za hifadhi ya jamii, bima ya afya, matumizi ya teknologia rafiki ya kuwafikishia huduma za fedha vijijini, makazi bora kwa wakulima pamoja na elimu ya fedha vijijini.

Mkutano huo umewajumuisha wadau mbalimbali wakiwemo maafisa kutoka serikalini, watoa huduma za kifedha vijijini, wataalam wa mambo ya kifedha, wakulima, na wawakilishi wa mashirika.

MWISHO

Video Mpya: Nini - Usiniendeshe

$
0
0
 Video Mpya: Nini - Usiniendeshe

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya February 23


Waziri Mkuu: Michezo ni Muhimu kwa Ustawi wa Afya

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema wanafunzi wanatakiwa washiriki katika michezo mbalimbali kwa sababu ina umuhimu mkubwa kwa ustawi wa afya ya binadamu pamoja na maendeleo ya nchi.

Ameyasema hayo jana (Ijumaa, Februari 22, 2019) wakati akizindua shule ya Sekondari Jumuishi ya Mtakatifu Amachius Inclusive katika wilaya ya Hai, Kilimanjaro. Amezindua shule hiyo kwa niaba ya Rais Dkt. John Magufuli.

“Lakini katika dunia ya leo michezo ni ajira na chanzo kikubwa cha mapato kwa vijana na Taifa kwa ujumla. Kwa kifupi michezo ni moja ya sekta muhimu kwa maendeleo ya Taifa, hivyo wazazi waruhusuni watoto washiriki.”

Alisema kutokana na umuhimu wa michezo, Serikali imetenga vipindi kwa ajili ya elimu ya michezo katika ratiba za masomo na kuendesha mashindano ya michezo shuleni yaani UMITASHUMTA na UMISSETA.

Waziri Mkuu alisema kuna wakati baadhi ya shule hususani za binafsi, dini na mashirika zimekuwa hazioni umuhimu wa kuwa na vipindi hivi au kushiriki katika mashindano.

“Hivyo, taasisi zetu zizingatie kuwashirikisha wanafunzi katika programu za ufundishaji michezo na kushiriki mashindano ili waweze kujenga afya ya mwili na akili, kukuza amani, ushirikiano, upendo na mshikamano kati ya yao.

Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuutaka uongozi wa shule ya Sekondari Jumuishi ya Mtakatifu Amachius Inclusive kuwa na walimu watakaofundisha vipindi vya michezo pamoja na kuwawezesha wanafunzi wao kushiriki mashindano ya michezo.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu Azitaka Benki Zipunguze Riba za Mikopo

$
0
0
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amezitaka benki nchini zipunguze viwango vya riba zinazotozwa kupitia mikopo mbalimbali wanayoitoa kwa wananchi.

Aliyasema hayo jana jioni (Ijumaa, Februari 22, 2019) alipozungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Bomang’ombe wilayani Hai.

Waziri Mkuu ambaye yuko mkoani Kilimanjaro kwa ziara ya kikazi alisema kitendo cha benki kutoza riba kubwa kinawaumiza wajasiriamali nchini.

Pia, Waziri Mkuu aliwataka wananchi hususani, vijana, wanawake na wenye ulemavu kuchangamkia fursa ya mikopo inayotolewa katika Halmashauri.

Alisema kila halmashauri inatakiwa itenge asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya kuwawezesha vijana, wanawake na wenye ulemavu kupata mitaji.

Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu amewataka wakulima wa kahawa wabadilike na kuondoa miti ya zamani na kupanda mipya ili waongeze tija.

Waziri Mkuu alisema wakulima hao wanaweza kuweka utaratibu wa kuondoa miche ya zamani kwa awamu na kupanda mipya, hivyo kupata mavuno mengi.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Salamu za Pole Kufuatia Ajali Iliyoua Watu 19 Songwe

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus E. Mwangela anatoa salamu za pole kwa niaba ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa ndugu, jamaa na marafiki wa wafiwa, kufuatia ajali ya gari iliyosababisha vifo 19 ikiwa wanaume ni 15 na wanawake wanne.

Brig. Jen. (Mst) Mwangela amesema kutokana na ajali hiyo iliyotokea usiku eneo la Senjele Wilayani Mbozi ikihusisha magari matatu yaliyokuwa yakielekea Mbeya kugongana, serikali Mkoani Songwe imetoa majeneza 19 pamoja na usafiri kwa ajili ya kuhifadhi miili ya marehemu.

“Rais Magufuli amenituma niwape pole na ametuelekeza kama Mkoa kusimamia Mamlaka za Usalama barabarani kufanya uchunguzi na hatua zinazo stahili kuchukuliwa, pia ameelekeza tujipange vizuri kukabiliana na matukio ya ajali za barabarani”, amesema Brig. Jen. (Mst) Mwangela.

Brig. Jen. (Mst) Mwangela amesema chanzo cha ajali hiyo kimetokana na gari la abiria aina ya coaster kugongwa na gari la mizigo lililokuwa nyuma yake kisha coaster kugonga gari la mizigo lililo kuwa mbele yake na kupelekea gari la abiria kubanwa katikati ya magari mawili ya mizigo.

Aidha ameliagiza Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe, kuweka utaratibu maalumu wa magari kupita kwa kupokezana katika maeneo yote yenye miteremko mikali, kuwepo ukaguzi wa magari kabla hayajaanza kushuka au kupanda mlima pamoja na kuweka ulinzi wa maeneo hayo.

“Mungu ametupa akili za kufanya kazi na akili hizi tuzitumie kuzuia ajali ndani ya Mkoa wa Songwe, hivyo nawasihi watumiaji wote wa vyombo vya moto kuhakikisha wanafuata sheria za usalama barabarani ili kuweza kuepuka ajali kama hizi”, amesisitiza Brig. Jen. (Mst) Mwangela.

Mapema jana Brig. Jen. (Mst) Mwangela amefika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Songwe ambapo miili ya marehemu ilikuwa imehifadhiwa ili kuwafariji wafiwa waliofika kutambua miili ya ndugu zao.

Uchaguzi Mkuu Nigeria kufanyika leo

$
0
0
Uchaguzi ulioahirishwa kwa wiki moja nchini Nigeria, unatarajia kufanyika hii leo Jumamosi, lakini baadhi ya watu wanahofu kubwa ya kujitokeza kwenye vituo vya kupigia kura kufuatia vitisho vya kushambuliwa na kundi la Boko Haram.

Rais Muhammadu Buhari amewataka wananchi wa Nigeria wajitokeze kwa wingi kweda vituoni kupiga kura leo Jumamosi na ameahidi kwamba usalama umeimarishwa katika maeneo yote ya nchi hiyo.

Katika uchaguzi huo ulioahirishwa wiki iliyopita Rais Buhari anapambana vikali na mfanyabiashara, Atiku Abubakar ambaye hapo awali alikuwa makamu wa Rais.

Aidha, tume huru ya uchaguzi nchini Nigeria wiki iliyopita iliahirisha uchaguzi huo wakati Wanigeria zaidi ya milioni 72 walipokuwa wanajitayarisha kwenda kupiga kura katika vituo mbalimbali nchini humo.

Akihutubia taifa kwenye televisheni Rais Buhari amewataka Wanigeria wasiwe na wasiwasi na wawe na imani kwamba tume ya uchaguzi itatimiza jukumu lake, huku mpinzani wake kiongozi wa chama kikuu cha upinzani PDP, Atiku Abubakar ametoa wito huo huo kwa wapiga kura.

Zaidi ya Wanigeria milioni 84 wameandikishwa kupiga kura kwenye taifa hilo lenye wakaazi milioni 190 la Magharibi mwa Afrika.

Nkoma: Tiba Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
NKOMA
_________________________
NKOMA Ni dawa bora ya nguvu za kiume  yenye mchanganyiko wa mitishamba (7) yenye maajabu yafuatayo/

🔖 (1) inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimalisha misuli ya uume uliolengea wakati wa tendo la ndoa/
🔖 (2) Kurefusha maumbile ya kiume yaliyorudi ndani kuazia nchi 5 - 9/
🔖 (3) kunenepesha uume cm 5 ya upana itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 - 20 kwa tendo la kwanza na utakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya 2-4 bila hamu kuisha/

📌 Na inatibu kabisa, unashauriwa uitumie dawa hii kama kinga ya magonjwa sugu./
 📌 Haijalishi umri hata kama una miaka 85 itumie huanza kufanya kazi dk 50 tu na haina madhara yoyote kwa mtumiaji/

📍📍📍📍📍📍📍📍📍
            MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA.
_________________________
🔖 (1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖 (2)Choo kama cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(4)Kaswende/
🔖(5)Gono/

📌Haya yote husababisha kuishiwa nguvu za kiume na kuwa na uume mdogo/
📌 Itumie leo, bado hujachelewa ni tofauti na nyingine.
_________________________
DR MAKOBA ANAPATIKANA DAR ES SALAAM, PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
___________________________
WASILIANA NA
Dr MAKOBA SIMU.
📞0754832349
📞0683490600
____________________________
*****************************

Kwanini Uhangaike Na Magonjwa Yanayowezekana Kupona?..........Tiba Sahihi Imewasili

$
0
0
Asilimia 60- 80 ya wanaume wameathilika kisaikologia baada ya kujiona wako tofaut na wengine kimaumbile na kupungukiwa nguvu za kiume , mwanaume aliekamilika kimaumbile anatakiwa awe na maumbile yasiyo pungua nchi 6-8 tofautina hapo anaupungufu ,

zipo sababu nyingi zinazosababisha mapungufu hayo ambazo ni :- upigaji wa punyeto ( mastervation) ,ngili,KISUKARI,vidonda vya tumbo,maumivu ya mgongo ama kiuno,unene(kitambi) tumbo kuunguluma na kujaa ges, matatizo haya huchangia kwa kiasi kikubwa sama kukosa nguvu za kiume vilevile maumbile kuwa madogo na kiingia ndani (kunywea)

GALIMBO 3 POWER :- hii nidawa kiboko kwa matatizo ya nguvu za KIUME,ni dawa ya Asili tuliyo jaaliwa na mwenyezi MUNGU huimarisha misuli ya uume wakati wa tendo la ndoa na kuzalisha viini vya uzazi (manii) vilevile utaludia tendo zaidi ya mara tatu bila ham kuisha pamoja na kuchelewa kufika kilele takiriban dk 20 - 45 kwatendo moja.

SUNUPER :- hii nidawa ya Asili Hurefusha na kune nepesha maumbire madogo ya UUME , hurefusha urefu wa nchi (6-8 )na unene wa sm( 3-4) huanza kufanya kazi masaa machache baada ya kuanza kuitumia,( tiba niyakudumu ikishakutibu,

Nina dawa ya kutokomeza KISUKARI na kupona kabisa hata kama kimekusumbua kwa mda mrefu mpaka ukajikatia tamaa  tiba ipo na utatumia vyakula vyote bila tatizo baada ya kupona ,

Pia ninadawa ya Vidonda vya tumbo,Ngiri, miguu kuwaka moto, mvuto wa mapenz ( kumvuta mke /mme/mpenzi/hawara/ama yoyote unaemuhitaji) dawa za biashara, uzazi kwa akina mama na akina baba (pande zote) pata dawa ya bawasili bila kufanyiwa upasuaji,

KWAMAELEZO NA MSAADA WASILIANA NA DR SILIMBA NAPATIKANA DAR ES SALAAM

 SM O620510598 / 0743543944

Nb km huna nafasi huduma hii inakufikia popote ulipo kwaware wa mikoani tunatuma kwa njia ya mabasi

Viongozi DRC wapigwa marufuku kuingia Marekani

$
0
0
Marekani imesema Ijumaa kuwa iko pamoja na watu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kufuatia zoezi la kihistoria la kukabidhiana madaraka na kutangaza katazo la kuingia Marekani kwa maafisa kadhaa kutoka tume huru ya uchaguzi (INEC), serikali na jeshi la nchi hiyo.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Mike Pompeo anaweka wazi kwamba, kutokana na kujihusisha katika ufisadi mkubwa unaohusiana na mchakato wa uchaguzi, watu wafuatao: Corneille Nangaa, Mwenyekiti wa Tume huru ya uchaguzi (CENI) ya DRC, Norbert Basengezi Katintima, Makamu mwenyekiti wa CENI; Marcellin Mukolo Basengezi, Mshauri wa Mwenyekiti wa CENI; Aubin Minaku Ndjalandjoko, Spika wa Bunge la Taifa la DRC; na Benoit Lwamba Bindu, Rais wa Mahakama ya Katiba DRC, na familia zao za karibu hawataruhusiwa kuingia nchini Marekani.

Taarifa hiyo ya wizara imesema kuwa Kifungu 7031 cha Sheria ya Wizara ya Mambo ya Nje, operesheni za nje ya nchi imempa madaraka wakati wowote Waziri wa Mambo ya Nje akiwa na taarifa za uhakika kuwa maafisa wa serikali za kigeni wamejihusisha na ufisadi mkubwa au kuvunja kabisa haki za binadamu, watu hao na familia zao wasiruhusiwe kuingia Marekani.

Waziri huyo wa Mambo ya Nje pia ameweka katazo la viza kwa maafisa wa uchaguzi na maafisa wa serikali na jeshi ambao wanasadikiwa kuwa wamehusika kwa kusaidia, au kujihusisha na uvunjifu wa haki za binadamu au unyanyasaji au ukandamizaji wa mchakato wa demokrasia nchini DRC.

Taarifa hiyo ya wizara imesema kuwa watu hawa wamejitajirisha kupitia ufisadi, wameamrisha au kusimamia uvunjifu wa amani dhidi ya raia, wakati wananchi hao walipokuwa wanatekeleza haki zao za kukusanyika kwa amani na uhuru wa kujielezea. Walikuwa wanaendesha mambo bila ya kujali kwamba wanawaathiri wananchi wa Congo na wamekuwa wakionyesha waziwazi kutojali kwao misingi ya demokrasia na haki za binadamu.

Wizara ya Mambo ya Nje imesisitiza kuwa hatua hii iliyotangazwa jana  inaelekezwa kwa maafisa maalum na siyo kwa wananchi wa Congo au serikali mpya iliyoingia madarakani.

Uamuzi huu unaonyesha nia ya Wizara ya Mambo ya Nje kuendelea kushirikiana na serikali mpya ya DRC katika kutekeleza ahadi zake za kutokomeza ufisadi na kuimarisha demokrasia na kuwajibika, na kuheshimu haki za binadamu.

Uchaguzi uliofanyika unaonyesha nia ya watu wa DRC kuleta mabadiliko na kuwa na taasisi za serikali zenye kuwajibika. Lakini hata hivyo kuna malalamiko ya kisheria juu ya mchakato wa uchaguzi jinsi ulivyoendeshwa na uwazi wake.

Credit: VOA

Ahukumiwa Miaka 30 Jela kwa Kumbaka Binti yake wa Kumzaa

$
0
0
Mkazi wa kijiji cha Msigalile, Masasi mkoani Mtwara, Ally Katambo (30) amehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kosa la kumbaka mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 11 (jina linahifadhiwa) baada ya kuelezwa na Mganga wa jadi kuwa kwa kufanya hivyo, atapata utajiri.

Hukumu hiyo ilitolewa jana katika Mahakama ya Wilaya ya Masasi baada ya mahakama kuridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na upande wa mashtaka.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi, Honorious Kando, alisema mshtakiwa alitenda kosa hilo kuanzia Juni Mosi hadi 29, mwaka jana akiwa nyumbani kwake kijiji cha Msigalile-Ndanda mjini Masasi.

Hakimu Kando alisema ushahidi ulitolewa na upande wa mashatka mahakamani hapo pamoja na mshtakiwa kukiri kufanya kosa hilo kwa madai kwamba ni kutokana na imani za kishirikina baada ya mganga wa jadi kwa lengo la kutaka utajiri na kutakiwa kufanya hivyo.

Alisema mahakama imemtia hatihani mshtakiwa na kumhukumu kifungo cha miaka 30 jela baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa.
 
Kando alisema mtuhumiwa alikiri kuwa baada ya kuelezwa na mganga wake kufanya kitendo hicho, alirudi nyumbani na kumbaka mtoto wake ili kutekeleza masharti aliyopewa kwa lengo la kufanikisha azma yake.

Alisema kwa mujibu ya kifungu cha 158 (1) ( 2 ) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu iliyofanyiwa makerebisho mwaka 2002, mahakama inamhukumu Katambo jela miaka 30 na kwamba hiyo itakiwa fundisho kwa jamii na watu wengine wanaofanya matukio kama hayo.

Katika kufikia uamuzi huo, Hakimu huyo alisema mahakama pia imejiridhisha na ushahidi wa vipimo vya kidaktari ambavyo vimeonyesha kuwa mtoto huyo amebakwa na kusababishiwa maumivu makali katika sehemu zake za siri, jambo ambalo pia limemwathiri kisaikolojia.

Baada ya hukumu, mahakama ilitoa fursa kwa mshtakiwa kujitetea na kuomba apunguziwe adhabu kwa vile kwa sasa ana watoto wawili wadogo na mke mmoja ambao wanamtegemea kimaisha.

Awali, mwendesha mashtaka wa polisi, Koplo Selemani, aliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshtakiwa ili iwe fundisho kwa wengine na jamii kwa ujumla, na kwamba kwa kumbumbuku za nyuma za mshtakiwa hakuwa na kosa lolote alilowahi kulifanya isipokuwa hilo la ubakaji.

VIDEO: Haitham Kim - Nimeyakanyaga

$
0
0
VIDEO: Haitham Kim - Nimeyakanyaga

Wimbo Mpya: Kayumba - Wasi Wasi

$
0
0
Wimbo Mpya:  Kayumba - Wasi Wasi

Mpina Agoma Kuhudhuria Makongamano Ya Vyama Vya Wafugaji....Asisitiza wafanye kazi waliyopewa na Mheshimiwa Rais

$
0
0
Na John Mapepele, Simiyu
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amepiga marufuku  makongamano ya wafugaji yenye lengo la kumpongeza Rais Dk John Magufuli kwa uamuzi aliochukua wa kuwasaidia badala yake ametaka watumie kipindi hiki kifupi walichopewa kuanisha maeneo ambayo yamepoteza sifa za uhifadhi yaweze kuchukuliwa  kwa ajili ya malisho ya mifugo.

Hivyo ametaka wafugaji kote nchini kujipanga na kupendekeza maeneo yaliyopoteza sifa za uhifadhi, mashamba yasiyoendelezwa ili wafugaji waweze kuyapata kwa ajili ya malisho ya mifugo yao kama sehemu ya kuunga mkono uamuzi uliotolewa wa kusaidia sekta hiyo.

Akizungumza katika mkutano wa kuwasilikiza wananchi waishio kando ya Hifadhi ya Pori la Akiba la Maswa wilayani Meatu mkoani Simiyu kwenye ziara ya Kamati ya mawaziri nane, Waziri Mpina alisema tangu mwaka 2000 tume zaidi ya 27 ziliundwa na Bunge na Serikali kushughulikia migogoro zaidi ya 1,095 lakini asilimia 99 ya mapendekezo ya tume hizo hayajatelezwa hadi leo.

Mpina alisema tume nyingi zilizoundwa miaka ya nyuma kushughulikia migogoro hiyo zilichakachuliwa hata kabla ya kukabidhi matokeo ya mambo waliyobaini kwa kuwa kwenye migogoro hiyo wako baadhi ya viongozi wa Serikali wako nyuma wana manufaa binafsi wanayopata ndio maana mapendekezo yaliyotolewa ya kutatua migogoro hiyo hayajawahi kutekelezwa hadi leo.

Alisema baadhi ya watendaji wa Serikali walilazimika hata kutoa rushwa ili kubadilisha maamuzi ya tume zilizokuwa zinaundwa kushughulikia migogoro hiyo kwa sababu wananufaika na migogoro hiyo.

“Mhe John Pombe Magufuli akasema hapana nitaunda tume ambayo haitapokea rushwa timu ya Lukuvi mnaiona ina sura ya kupokea rushwa? Vichwa vya kina Mpina unaweza ukawapa nini wakakubali, akasema wananchi wangu watahangaika mpaka lini, watauana mpaka lini mifugo mingi imedhulumiwa kwa kivuli cha uhifadhi, Mhe Rais akasema nitaunda tume ndio hii sasa ya mawaziri 8”alisema Mpina

Mpina aliwahakikishia wananchi kuwa mapendekezo yaliyotolewa na wananchi yatafika kwa Rais tofauti na tume zingine zilizotangulia zilikuwa hazina uwazi wa namna ya kuchukua maoni na namna ya kufikisha mapendekezo serikalini.

“Mhe Rais akasema nitaunda timu ambayo itaandaa waraka wa baraza la mawaziri ili waraka ule uamuliwe na Serikali hapo ndipo utaona huyo ndio Dk John Pombe Joseph Magufuli ambaye amejipambanua katika kuhakikisha kwamba matatizo ya wananchi yanashughulikiwa na yanamalizika”alisema Mpina

Kufuatia hali hiyo Waziri Mpina ameagiza wafugaji wote nchini kusitisha makongamano na maandamano ya kumpongeza Rais kwa sasa kwani Rais amewapa kazi wakulima, wafugaji, wavuvi kuangalia maeneo ambayo yamepoteza sifa yaweze kupendekezwa ili wafugaji wayapate.

“Sisi kama wafugaji tusipoteze muda wa makongamano na kumshangilia Mhe Rais wakati ametupa kazi kubwa ya kupendekeza maeneo hayo ili mwisho tuyapate, yafutwe tuweze kufanya shughuli kilimo, ufugaji”alisema

Hivyo Waziri Mpina amekataa kuhudhuria makongamano ya vyama vya wafugaji ambao wamemualika kuhudhuria sherehe hizo na kuwataka kujipanga vizuri kupendekeza ili kuitumia vizuri nafasi ya pekee waliyopewa na Rais Dk Magufuli.

“Hakuna kiongozi mwingine yoyote katika historia ya Tanzania ambaye amekuwa na mtizamo wa kutatua kero za wananchi wake kama Mhe Dk John Pombe Magufuli, Rais huyu historia itaandika ya Tanzania na hata ya dunia kwa mtazamo wake ambapo wananchi wengi wakitaka kupaza sauti zao wanazuiwa na watu wachache ambao walikuwa na masilahi katika mambo hayo sasa hayo yote yamefika mwisho”alisisitiza Waziri Mpina.

Akiwasilisha maelezo na mapendekezo ya wananchi waishio Kando ya Pori la Akiba la Maswa mmoja wa wananchi hao, Deus Martin alisema hadi sasa jumla ng’ombe 75 wanashikiliwa katika Kituo cha Buturi kwa zaidi ya mwaka mmoja na miezi 4 bila kuachiwa na kurudishiwa wenyewe.

Alisema mpaka uliopo sasa uliwekwa mwaka 1984 bila kuwashirikisha wananchi ambapo katika kipindi hicho wananchi walikuwa wanaishi zaidi ya kilomita 10 kutoka mpaka uliowekwa sasa hivyo wananchi walihamishwa kwa nguvu na kusababisha ukosefu wa malisho hadi sasa.

Hivyo wameomba kupewa maeneo hayo waliyoyaacha ndani ya hifadhi ili wayatumie kwa ajili ya malisho kwa kipindi cha kuanzia Novemba hadi Juni.Pia wameomba Sheria ya kuwazuia ndani ya mita 60 kutoka kwenye kingo za mito ifutwe ili waweze kutumia maeneo hayo kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Maalum na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi aliwahakikishia wananchi walioondolewa kupisha mita 500 warudi waendelee na shughuli zao kwani Rais Dk John Magufuli alishasitisha zoezi la kuwaondoa wananchi hao.

Lukuvi aliwahakikishia wananchi waishio pori la Akiba la Maswa kuwa mapendekezo waliyotoa ya kuomba kuongezewa eneo la malisho wamechukua na watayasilisha kwa Rais kama yalivyo kwa uamuzi zaidi.

Mawaziri wanaounda timu hiyo mbali na Mpina na Lukuvi ni pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Suleiman Jafo, Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamish Kigwangala, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi, Naibu Waziri wa Kilimo, Omary Mgumba na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira, Mussa Sima.

Uchaguzi TLS: Mawakili sita wajitokeza kuwania nafasi ya Fatma Karume

$
0
0

Inataarifiwa kuwa Mawakili sita wamepitishwa kugombea urais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) unaotarajiwa kufanyika Aprili mwaka huu.

Uchaguzi wa TLS umekuwa ukivuta hisia kali, tangu Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu alipowania na hatimaye kushinda nafasi hiyo Machi 2017. Hata hivyo, Lissu aliitumikia nafasi hiyo kwa miezi sita tu baada ya kushambuliwa kwa risasi jijini Dodoma na kutumia muda wake wote kwenye matibabu nje ya nchi.

Fatma Karume anayeshikilia nafasi hiyo na ambaye anamaliza muda wake sasa, awali alieleza nia yake ya kugombea tena nafasi hiyo lakini baadaye alibadili nia.

Taarifa iliyotolewa jana na kamati ya uchaguzi wa TLS na kuthibitishwa na mtendaji mkuu wa chama hicho, Kaleb Gamaya imewataja wagombea hao kuwa ni mkurugenzi wa chama cha wanasheria watetezi wa mazingira (Leat), Dk Rugemeleza Nshala na aliyewahi kuwa Rais wa chama hicho, John Seka, wengine ni Godfrey Wasonga, Gaspar Mwanalyeka, Godwin Ngwilimi na Charles Tumaini.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images