Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Viwanda 3,504 Vimeanzishwa Nchini

$
0
0
Na: Lilian Lundo – MAELEZO, Dodoma.
Jumla ya viwanda 3,504 vimeanzishwa nchini kutokana na juhudi za kujenga uchumi wa viwanda zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano tangu iingie madarakani hadi kufikia Desemba, 2018.

Hayo yameelezwa leo Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya alipokuwa  akijibu swali la mbunge wa Chumbageni, Mhe. Ussi Salum Pondeza juu ya viwanda vingapi vimeanzishwa tangu Serikali ya Awamu ya Tano ianze utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda.

“Kati ya viwanda hivyo 3,504 vilivyoanzishwa, vinajumuisha viwanda vidogo sana 2,500, viwanda vidogo 943, viwanda vya kati 51 na viwanda vikubwa 10,” amesema Mhandisi Manyanya.

Amesema wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina imekuwa ikifanya tathmini ya viwanda 156 vilivyobinafsishwa na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa kwa viwanda  68  ambavyo havijaendelezwa.

Aidha amesema, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ilijiridhisha na mapendekezo yaliyotolewa na kuiwezeshsa Ofisi ya Msajili wa Hazina kuchukuwa hatua.

Mhandisi Manyanya  amesema hatua iliyochukuliwa na Ofisi ya Msajili ni kuvirejesha viwanda 14 Serikalini na juhudi za kuvitafutia wawekezaji wengine walio tayari kuviendeleza zinaendelea.

Ameeleza kuwa, kwa mujibu wa hali ya uchumi ya mwaka 2017, mchango wa sekta ya viwanda katika Pato la Taifa ni asilimia 5.5 ikilinganishwa na asilimia 4.9 mwaka 2016, sawa na ongezeko la asilimia 0.6.

Kamati ya Bunge Yashauri Wafungwa waliooa Wajengewe vyumba private ili wapate tendo la ndoa

$
0
0
Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria imeishauri Serikali kuandaa na kutekeleza mpango mkakati chini ya Magereza kuwafanya wafungwa wanapata haki ya kutembelewa na wenza wao na kupata haki ya tendo la ndoa.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa kamati hiyo bungeni jijini Dodoma leo Ijumaa Februari 8, 2019 mwenyekiti wake, Mohamed Mchengerwa amesema hatua hiyo itapunguza maambukizi ya magonjwa kwenye magereza ikiwemo Ukimwi.

“Serikali iandae na kutekeleza mpango mkakati chini ya Magereza ambao utahakikisha wafungwa wenye ndoa wanawekewa mazingira yatakayohakikisha wanapata haki ya kutembelewa na wenzi wao na kupata haki ya tendo la ndoa kwa kuzingatia utaratibu utakaowekwa na mamlaka husika,” amesema.

Ikulu Yakanusha Taarifa za Kutumbuliwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani

$
0
0
Baada ya kusambaa mitandaoni kwa taarifa ya kutumbuliwa kwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Wilsoni Masilingi ikulu imetoa ufafanuzi wa kwamba barua hiyo siyo ya kweli.

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa amekanusha taarifa hiyo kupitia mtandao wake wa kijamii (Twitter) na kusema kwamba barua hiyo haina ukweli wowote.

"Imeghushiwa, tafadhali ipuuzeni. 'Fake, please ignore'".

Barua ya kutenguliwa kwa uteuzi wa Balozi Masilingi imeanza kusambaa ikiwa ni siku moja tangu kukutana na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu katika kituo cha utangazaji VOA nchini Marekani.

Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi azungumzia haki ya tendo la ndoa kwa wafungwa

$
0
0
Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amesema suala la kuwakutanisha wafungwa na wenza wao kwa Tanzania halina ulazima kwa kuwa halivunji haki za msingi.

Profesa Kabudi alitoa kauli hiyo leo jioni Ijumaa Februari 8, 2019 wakati akichangia taarifa za kamati za Bunge za Sheria na Sheria Ndogo kwa mwaka 2018.

Amesema Tanzania ilifanya utafiti na walibaini kuwa jambo hilo haliwezekani.

"Hata mataifa ya wenzetu huko si kwamba wenza wanakwenda magerezani hapana, bali wana utaratibu mwisho wa mwaka wafungwa wanaotembelea familia zao majumbani na kukaa hadi Januari 2 ndio wanarudi gerezani, " alisema Kabudi.

Amesema wenza wakienda magerezani hata faragha haitakuwepo kwani kila mmoja atajua wanachofanya hivyo usiri hautakuwepo huku akisisitiza uvumilivu kwani kuna wanaume rijali lakini wamekubali kuwa waseja.

Leo bungeni kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria imeishauri Serikali kuandaa na kutekeleza mpango mkakati chini ya Magereza kuwafanya wafungwa wanapata haki ya kutembelewa na wenza wao na kupata haki ya tendo la ndoa.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa kamati hiyo mwenyekiti wake, Mohamed Mchengerwa amesema hatua hiyo itapunguza maambukizi ya magonjwa kwenye magereza ikiwemo Ukimwi.

“Serikali iandae na kutekeleza mpango mkakati chini ya Magereza utakaohakikisha wafungwa wenye ndoa wanawekewa mazingira yatakayohakikisha wanapata haki ya kutembelewa na wenza wao na kupata haki ya tendo la ndoa kwa kuzingatia utaratibu utakaowekwa na mamlaka husika,” amesema.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya February 9

Kamishna Mkuu UNHCR aomba msaada wa kimataifa kwa Tanzania, inayohifadhi wakimbizi 330,000

$
0
0

Dar es Salaam, Februari 8, 2019; Kamishna Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Wakimbizi Duniani, Filippo Grandi amemaliza ziara yake ya kikazi ya siku nne nchini Tanzania kwa kuomba uwekezaji katika ulinzi wa mazingira na maendeleo ya kiuchumi katika maeneo ya Kaskazini-Magharibi mwa nchi ambako wakimbizi takribani 330,000 wanahifadhiwa. 

Ameitaja Tanzania kama “moja ya nchi muhimu zitoazo uhifadhi kwa wakimbizi Afrika,” Bw. Grandi ameelezea kuridhishwa kwake na hakikisho la serikali kwamba nchi itaendelea kuwa yenye ukarimu kwa wakimbizi.
 
Katika mkutano wake na Mheshimiwa Raisi, Dkt. John Joseph Magufuli, Bw. Grandi ameipongeza Tanzania kwa utamaduni wake wa muda mrefu wa kuwakaribisha wakimbizi wanaokimbia machafuko na mateso katika nchi zao, ikiwa ni pamoja na kuwapa uraia watu 162,000 waliokimbia kutoka Burundi mwaka 1972. Amesema ukarimu wa Tanzania na Watanzania uliodumu kwa miongo mingi kwa watu wanaotafuta hifadhi unastahili kutambuliwa kimataifa.

 Ameahidi kuendelea kukusanya misaada ya kibinadamu na ya maendeleo kwa nchi mwenyeji, kwa lengo la kuimarisha usalama katika maeneo ya makambi na kuendeleza miradi ya mazingira ikiwa ni pamoja na kutafuta nishati mbadala wa kuni. Pia, walijadili wazo la kuanzisha mfumo wa kikanda utakaojikita katika kutafuta suluhisho la kudumu kwa wakimbizi wa nchi za Burundi na Kongo.
 
Katika kikao chake na maafisa wa serikali, Bw. Grandi alisisitiza kwamba urejeshwaji wa wakimbizi wenye tija unatokea pale wakimbizi wanapoamini kuwa ni salama kurudi makwao na wakipokea misaada muhimu utakaowawezesha kujihudumia mara watakapofika katika nchi zao. Katika miaka miwili iliyopita, wakimbizi 57,865 kutoka Burundi wamesaidiwa kurudi kwa hiari kutoka Tanzania. 

Hata hivyo, baadhi ya wakimbizi wameripoti kuwa shinikizo kutoka kwa maafisa wa serikali linalojumuisha kuzuiliwa kutembea maeneo mengine na upatikanaji wa fursa za kuendesha maisha vimewafanya waamue kurudi makwao. Bw. Grandi amesema kwenye mkutano wake kwamba UNHCR iko tayari kufanya kazi pamoja na serikali katika kuwasaidia wale wote wanaoonyesha utayari wa kurudi nyumbani lakini kwa uzoefu wake, baadhi ya vikwazo vinaweza visiwe na manufaa na kwamba ni pale tu wakimbizi wanapoamini kuwa hali ni salama kwenye nchi zao ndipo watakapochagua kurudi kwa hiari yao.
 
“Katika nchi za Kongo na Burundi bado kuna hali ya sintofahamu,” Bw. Grandi amesema kwenye mkutano wake na vyombo vya habari kufuatia ziara yake katika Kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu wilayani Kasulu, huku akisema hata hivyo baadhi ya wakimbizi wako tayari kurudi na wanasaidiwa na UNHCR. “Ni muhimu urejeshwaji ubaki kuwa jambo la hiari na kwamba hakuna anayeshinikizwa kurudi.” Bw. Grandi ameomba msaada wa kimataifa ili kuhakikisha kuwa wakimbizi wanaorudi kwa hiari wanaweza kuanza upya maisha katika nchi zao za asili na kujitegemea, akisema msaada unaotolewa sasa pamoja na fedha havitoshelezi mahitaji ya wale wanaorudi Burundi.
 
Bw. Grandi amerejelea Tanzania kama nchi imara katika kanda isiyo na utulivu wa kisiasa na ameipongeza nchi kwa jukumu lake kama mtunza amani wa kanda, akiuhimiza uongozi wa Tanzania kuendeleza jitihada za amani. Katika mkutano wake Dar es Salaam na Rais mstaafu wa Tanzania, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa ambaye hivi karibuni alikuwa
 
Mwezeshaji mwakilishi wa Umoja wa Afrika ya Mashariki katika Mjadala wa Mazungumzo ya Mchakato wa amani wa Burundi, Bw. Grandi alielezea matumaini yake kuwa juhudi za usuluhishaji zitaendelea. Bw. Mkapa alionyesha wasiwasi kuwa mchakato huo umesimama na, ingawa kuna hatua ilipigwa katika eneo la usalama, kikwazo cha kisiasa kinabakia na majadiliano kati ya wadau ndiyo njia pekee ya kumaliza mgogoro wa sasa na katika kuwezesha uchaguzi huru, wa haki uliopangwa kufanyika mwaka 2020.
 
Asilimia 74 ya wakimbizi na watafuta hifadhi walioko Tanzania wanatoka Burundi, na asilimia 26 nyingine wanatoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Wengi wao wanaishi kwenye kambi karibu na maeneo ya mipaka, na wengi wao wamekuwa hapo kwa miongo mingi sasa.
 
Bw. Grandi aliisifu Tanzania kwa kuuunga mkono jitihada za Muungano wa Pamoja wa Kimataifa kwa Wakimbizi ambao utawezesha kuomba msaada mkubwa kutoka jumuiya za kimataifa kwa ajili ya kuzisaidia nchi wenyeji. Pia inaomba uwezeshaji wa wakimbizi katika kujitegemea kwa lengo la kukuza uchumi na kutoa fursa kwa wenyeji, alisema Bw. Grandi.

 Wakati wa ziara yake kwenye kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu, mkimbizi kutoka Kongo, Selemani Boaz, ambaye ni mfanyabiashara katika soko la pamoja lililoko nje ya kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu, alisema, “soko linatusaidia kuwasiliana na kuonana na watu tofauti tofauti, hata kutoka nje ya kambi, hasa Watanzania .... Tunapata kufahamiana na hii husaidia kutuunganisha.” Bw. Grandi pia alisikia kutoka kwa wakimbizi kuwa soko linawawezesha pia wakimbizi kupata vyakula vya aina mbalimbali, tofauti na mgao wa chakula wa Shirika la Chakula Duniani (WFP).
 
Katika mikutano yake na viongozi wa serikali ya Tanzania, Kamishna Mkuu pia alipata fursa ya kufafanua mkanganyiko wa hivi karibuni kuhusu nguo za msaada, ambapo asilimia ndogo ilitengwa na kukabidhiwa kwa mamlaka ya serikali kwa sababu zilikuwa na mtindo usiofaa. Aidha, ameihakikishia serikali ya Tanzania kuwa tahadhari kubwa itachukuliwa wakati mwingine ili kuepuka kujirudia.

Naibu Mawaziri watembelea Kituo cha kutoa huduma kwa pamoja cha Mtukula.

$
0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) amekutana na Naibu Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Uganda, Mhe. Julius Wandera Maganda katika Kituo cha kutoa huduma kwa pamoja mpakani cha Mutukula mpakani mwa Tanzania na Uganda Tarehe 7 Februari 2019.

Mara baada ya kukutana walipata fursa ya kutembelea na kujionea namna kituo cha kutolea huduma kwa pamoja mpakani cha Mtukula (OSBP) kinavyofanya kazi na kufanya Mkutano wa pamoja uliowashirikisha wadau mbalimbali kutoka Tanzania na Uganda. Mkutano huo umefanyia Mpakani mwa Tanzania na Uganda eneo la Mtukula.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Mhe. Dkt. Ndumbaro alisema lengo la ziara yao katika kituo hicho cha kutolea huduma kwa pamoja Mtukula ni pamoja na kujionea mafanikio na kubaini changamoto zinazokabili utendaji wa kazi na kuzipatia ufumbuzi.

Akiainisha mafanikio makubwa yaliyofikiwa na kituo hicho , Dkt. Ndumbaro alieleza namna mizigo mbalimbali ikipita kwa wakati kwa kuzingatia taratibu zote zilizopo pamoja na wafanyabiashara kati ya nchi hizi mbili wakifanya biashara zao bila vikwazo vyovyote vile.

Pamoja na mambo mengine Dkt. Ndumbaro alitumia fursa hiyo kuwajulisha wadau mbalimali waliohudhuria mkutano huo, kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeanzisha safari za Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), kutoka Dar es Salaam, Arusha mpaka Enttebe, Uganda. Mafanikio hayo yametokana na mahusiano mazuri ya kidiplomasia yaliyopo baina ya Tanzania na Uganda na pia kupitia Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kwa upande wake Mhe Maganda, alifurahishwa na hali ya kituo hicho namna huduma zinavyotolewa. Aidha, aliahidi kuwa Serikali ya Uganda itaongeza watendaji kazi kwenye kituo hicho ili kuwezesha upande wa Uganda kufanya kazi masaa 24 kama ilivyo kwa upande Tanzania. Pia alisisitiza nchi yake kuendelea kushirikiana na Tanzania katika masuala mbalimbali ya Ushirikiano.
   
Pia katika Mkutano huo wadau walitoa pongezi kwa viongozi wa Serikali za pande zote mbili kwa kuanzisha kituo hicho cha kutolea huduma kwa pamoja mpakani Mtukula, ambapo walisema kuanzishwa kituo hicho kumeongeza chachu ya maendeleo kwa wafanyabiashara wa pande zote mbili ambapo wamekuwa wakisafirisha bidhaa zao kwa wingi bila kupata changamoto kulinganisha na hapo awali kabla ya kuanzishwa kwa kituo hicho.

 Kadhalika wadau walitoa pongezi kwa watendeji waliopo kituoni hapo kwa upande wa Tanzania, kwa kutoa huduma nzuri kwa masaa 24 kwenye kituo hicho ambapo, imepelekea wafanyabiashara kutokupoteza muda mwingi wafikapo mpakani hapo.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
9 Februari 2019

Kiingilio Mechi ya Simba na Al Ahly ni 2000 tu

$
0
0
Uongozi wa Simba umetangaza bei ya kiingilio kwenye mchezo baina ya timu yao na Al Ahly, Jumanne ijayo ambacho kitakuwa ni Sh2000.

Uamuzi huo umelenga kupata idadi kubwa ya mashabiki watakaojitokeza uwanjani siku hiyo ili kuiunga mkono timu hiyo kwenye mechi hiyo ya hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa Afrika.

"Tulishawahi kuwafunga Zamalek hapa. Tulishawahi kuwafunga Enyimba hapa lakini hilo halitowezekana kama hatutopata sapoti ya mashabiki.

"Pamoja na kufanya vibaya kwenye mechi mbili zilizopita, naamini kama tukipata ushindi kwenye mechi zinazofuata, bado tuna nafasi ya kusonga mbele.

"Tumekaa kama bodi ya klabu na kuamua kiingilio kwenye mchezo huo kiwe Shilingi 2000. Tunajua kuwa tunahitaji fedha lakini matokeo ni ya muhimu zaidi," alisema mwenyekiti wa bodi ya klabu hiyo, Mohammed Dewji.


Ajali mbaya yatokea Hamugembe Manispaa ya Bukoba Mjini

$
0
0
Ajali mbaya imetokea usiku wa kuamkia leo Kata ya Hamugembe Manispaa ya Bukoba Mjini Mkoani Kagera na kusababisha vifo vya watu 4 waliokuwemo katika magari hayo.

Ajali hiyo imehusisha magari aina ya Toyota Hiace T- 869 CHT na Fuso T-223 ATK ambapo yaligongana uso kwa uso na kusababisha mlipuko mkubwa wa moto kutokea katika eneo hilo.

Hayo yamethibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Revocatus Malimi mara baada ya kufika katika eneo la tukio ambapo amesema kuwa mpaka sasa wameshaopoa maiti nne kutoka kwenye ajali hiyo.

Godbless Lema Asimulia Walivyomtorosha Zitto Kabwe

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Godbless Lema amesema kuwa  Jumatano Februari 6, 2019 walilazimika kumuondoa mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe baada ya kufuatiliwa na watu ambao hakuwataja.

Ameyasema hayo jana wakati akichangia taarifa ya Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria ambapo amesema kuwa kama Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikitawala kwa haki, kwa kufuata sheria na Katiba hana tatizo hata kikitawala milele.

“Leo mwenyekiti (Mussa Azzan Zungu), Zitto hayuko bungeni tumemuondoa juzi alikuwa anafuatiliwa usiku kwa kazi za kibunge, sio za kuuza madawa ya kulevya si za kubaka watoto ni kazi za kibunge.”alisema Lema

Lema aliongeza kwa kusema kuwa lengo lao ni kuona wanatawaliwa na CCM  kwa haki na ndio maana ya upinzani lakini leo hii chuki inajengwa na baadhi ya viongozi ambao wamekuwa wakitoa kauli tata dhidi ya upinzani.

Wakulima Wahamasishwa Kujiunga na Bima ya Kilmo

$
0
0
Na Erick Msuya – MAELEZO
Wakati serikali ya Awamu ya Tano ikiwahangaikia wakulima nchini katika kuwawezesha kimaendeleo, wakululima na wadau wake wenye viwanda vya kilimo wameanza kuhamasishwa kufungua Bima ya wakulima itakayo wasaidia katika mazao yao.
 
Zaidi ya asilimia 70 ya watanzania nchini ni wakulima na ndio tegemeo kutokana na kilimo kuwa uti wa mgongo kwa taifa, hivyo kuwa na bima katika kilimo ni jambo ili kuzuia majanga katika mchakato wa kilimo kwa kuepuka moto, mafuriko, magonjwa ya mazao na mengine kadhaa.
 
Tanzania Insurance Regulatory Authority (TIRA) ni wadau wanao wanaosimamia shughuli za bima nchini na hivyo kuwa na nafasi ya kushiriki katika sekta ya kilimo kwa wakulima kuwa na bima
 
Katika semina ya siku mbili; februari 7 – 8, iliyofanyika jijini Dar es S alaam kwa lengo la kuwainua wakulima kwa kufungua bima za mazao ili kuwaokoa kiuchumi, wadau mbalimbali wa kilimo, sekta binafsi pamoja na serikali zimewataka wakulima kujiungta na bima ili iwasaidie pindi wanapokutana na majanga.
 
Akizungumza na Maelezo, Mkurugenzi wa Leseni na Mwenendo wa Soko kutoka Mamlaka ya Bima Tanzania, Samweli Mwiru amewataka wakulima nchini wajiandae kwa ujio huo wa bima katika mashamba yao pia watambue bima ni kitu muhimu hasa katika mazao yao na kilimo kwa ujumla..
 
“Bima itasaidia endapo patatokea majanga yoyote katika kilimo na mazao, makampuni ya bima nchini yataweza kuwalipa hizo gharama ili kumfanya mkulima kutofilisika na kumfanya aendelee na shughuli zake za kilimo” alisema Samweli Mwiru
 
Sambamba na hilo, amesema bima hiyo ya kilimo itamlinda mkulima katika maeneo mengi tofauti tofauti ikiwa na majanga yatokanayo na hali ya hewa, mjanga yatokanayo na Magonjwa mbalimbali ya Mimea, hivyo akaongezea kuwa bima hiyo itakuwa mahususi kukinga majanga yatokanayo na hali ya hewa.
 
Naye Afisa Habari wa Mamlaka hiyo, Eyuke Faustin amesema asilimia 68 ya wakulima wadogo wadogo elimu yao ni ndogo juu ya uelewa wa bima hivyo amewataka wadau mbalimbali wa bima hizo ingefaa waandae mchakato wa bidhaa za bei rahisi zitakazo weza kujibu maswali na changamoto zitakazo weza kumkabili mkulima.
 
“Swala la bima kwa wakulima wadogo wadogo bado ni changamoto, kutokana na takwimu zilizopo zilizotolewa na Waziri wa kilimo, asilimia 68 ya wakulima wadogo wadogo elimu yao ni kuanzia elimu za msingi kampuni za bima ziandae bidhaa rahisi zitakazo eleweka vizuri kwa kujibu hoja ama maswali ya mkulima mdogo mdogo” alisema, Eyuke Faustin.
 
Katika siku ya mwisho ya seminahiyo, matumaini yao ni kuandaa hatua za kuchukua katika kuendeleza soko la bima za kilimo, kuundwa kwa kikosi kazi maalumu kitakachoweza kuandaa ripoti itakayopelekwa wizarani ili mikakati itakayoandaliwa iweze kusaidia Mamlaka ya Bima pamoja na taasisi mbalimbali zilizo wadau

Waziri Mkuchika Atoa ONYO Kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya Wanaowasweka Watu Rumande

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), George Mkuchika, amewaumbua baadhi ya wakuu wa Wilaya nchini wanaowaweka ndani watu kwa saa 48 wakati hakuna sheria inayowapa mamlaka hayo.

Mkuchika amewataka wakuu hao wa Wilaya kuacha kutumia mabavu kwenye utendaji wao wa kila siku kwa kuwa wakiendelea na tabia hiyo watakuwa wanahatarisha kazi yake ya uwaziri.

Aliyasema hayo juzi bungeni wakati akichangia na kueleza kuwa wakuu wa wilaya na mikoa wanapaswa kutumia busara katika kuwaweka ndani raia.

“Msiniponze. Mimi nataka Rais Magufuli asinibadili hapa, mimi nataka Rais Magufuli aseme mzee endelea, tuache masuala ya umwamba, nawaomba huko mliko msiniharibie kazi yangu. Mimi ndiye mwenye cheo cha utawala bora, mimi ndiye waziri mwenye dhamana ya utawala bora, ukiendesha mambo kinyume cha utawala bora unaniharibia kazi,” alisema Mkuchika.

Alisema madaraka ya wakuu wa wilaya kuwaweka ndani watu saa 24, lugha iliyotumika ni kwa usalama wake, maana yake mtu ameua mtu na jamaa zake wamekasirika wanataka kumpiga yule aliyeua na hapo ndipo dhana ya kumweka huyo mtuhumiwa ndani saa 24 inatumika kwa usalama wake.

Alisema mkuu wa wilaya akishamweka mtu huyo ndani ya saa 24 na muda huo ukamalizika, ikifika asubuhi ni lazima apelekwe mahakamani.

“Nataka niseme mahali popote mkuu wa wilaya kumweka ndani mtu saa 48 ni makosa kwa sababu sheria inampa saa 24 na mkuu wa mkoa amepewa saa 48,” alisema Mkuchika.

Aliongeza kuwa mkuu wa mkoa amepewa mamlaka ya saa 48 na akipenda anaweza kumweka mtuhumiwa ndani saa 24 na si lazima amweke mtu ndani.

“Kama ni kosa la jinai OCD (Mkuu wa Polisi wa Wilaya) yuko. Kama ni suala la uhamiaji mtu wa uhamiaji yupo, kama amekwepa kodi mtu wa TRA (Mamlaka ya mapato Tanzania) yupo, si lazima utamke wewe,” alisema Mkuchika.

Je Unaupungufu Wa Nguvu Za Kiume au Maumbile Mafupi na Membamba...Suluhu iko hapa

$
0
0
Acha kusubilia mpaka mke au mpenzi wako akwambie Mme wangu wewe ni dhaifu tuwepo kitandani,unatakiwa ujitambue mapema ,kwa mwanaume aliyekamilika  na mwenye nguvu za kutosha  ili kumridhisha mke au mpenzi wake anatakiwa awe na uwezo wa kurudia zaidi ya Mara mbili lakini kama unakomea moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe tu sio na yeye, ili uwe mwanaume mwenye uwezo kamili tumia dawa yako hii hapa

 SUPER MAJINJAS MIX; dawa hii ni tofauti na ambazo uliwai kutumia inamichanganyo ya miti na matunda zaidi ya saba ndio maana inakupa uwezo wa ,KURUDIA TENDO ZAIDI YA MARA TATU,NA ITAKUFANYA UCHELEWE KUFIKA KILELENI DAKIKA 10-15 KWA TENDO LA KWANZA,NA PIA HUIMALISHA MISULI ILIYOLEGEA NA KUSINYAA KWA WALE AMBAO WALIPIGA SANA PUNYETO,dawa hii ni ya vidonge na unga na haina madhara yoyote

MAKAKANUA NO 5 MPYA; dawa hii uboresha uume saizi upendayo UREFU WA INCHI 5,6,7,NA 8 NA UPANA WA CM 2,3,4 NA 5 dawa hii ipo ya kunywa na kupaka  na pia usahidia zaidi kwa mwanaume aliyefanyia tohara ukubwani,

ISENYE NO 3; hii ni dawa kwa wenye kisukari dozi siku 21 tatizo la kisukari na ndio chazo kikubwa cha kuishia nguvu za kiume,

NGWALUSA ; hii ni dawa ya uzazi ambayo ufungua milija ya uzazi ata kwa wale walifungwa uzazi,zipo dawa za busha,vidonda vya tumbo,miguu au viungo kufa gazi kupungza kitambi,minyama uzembe,na matiti makubwa 

TUNAPATIKANA DARES SALAAMU buguruni na MOROGORO YUPO WAKALA na MWANZA YUPO MTAA WA BIZA C, NA KAHAMA MJINI kwa mawasiliano zaidi piga simu 0744040721, 0683645920 DR BRUNO pia unaweza ukaletewa popote ulipo

Usikate Tamaa....Okoa Ndoa yako kwa Tiba Hii ya Asili

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

GALIMBO 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0620510598  / 0743543944

Dawa Mpya Asilia Ya Nguvu Za Kiume

$
0
0
Baada Ya Watu Kuhangaika Mda Mrefu Bila Kupata Dawa Ya Uhakika Ya Kumaliza Na Kuondoa Tatizo La Nguvu Za Kiume Sasa Dr.mbulana Ana Dawa Mpya Ya Mitishamba Ambayo Ni Komesha Kabisa Kwa Tatizo Sugu La Nguvu

SUPER MGUNO ;Ni dawa ya mitishamba inatibu kabsa tatizo la nguvu za kiume inakufanya uwe na uwezo wa kuchelewa kufika kileleni pia inakufanya uweze kufanya tendo mara 3 hadi 4 bila kuchoka

SUPER MGUNO2; Hi dawa ya mitishamba inayo nenepesha na kurefusha Uume mfupi ulio sinyaa na kuufanya uwe imara na inasafisha mirija ya uume na kuupa nguvu wakat wa tendo.

Dawa hii ni dawa inayo tibu mtu yeyote ambae amepata tatizo ili kutokana na sababu mbali mbali kama vile kupiga punyeto kwa mda mrefu,magonjwa kama vile kisukari,ngiri,vitonda vya tumbo n.k

Pia DR.MBULANA ANATIBU MAGONJWA KAMA KISUKARI,NGIRI,VIDONDA VYA TUMBO,UZAZI N.K

DR huyu anapatika DAR ES SALAAM PIA HUDUMA HII UNATUMIWA POPOTE ULIPO NA MIKOANI TUNATUMA KWA NJIA YA MABASI

MAWASILIANO
DR.MBULANA
0714092127

Msigwa Ampongeza Waziri Mkuchika Kwa Kuwakemea Wakuu wa Mkoa Wanaotumia Madaraka Yao Vibaya

$
0
0
Mbunge wa Iringa Mjini kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mch. Peter Msigwa amesema kuwa baadhi ya vingozi hasa wakuu wa mikoa wanaongoza kwa mihemko ya kisiasa kitu ambacho kinapunguza ufanisi  katika utendaji kazi kwa watumishi umma.

Ameyasema hayo Jijini Dodoma wakati akichangia kwenye mjadala juu ya utawala bora ambapo amedai kuwa baadhi ya wateule mkoani kwake wanatumia vibaya mamlaka yao ya kisheria.

“Mara nyingi tumeambiwa kwamba hatusifu ila nimeamua kutoa sifa zifuatazo, kwanza nampongeza Mkuchika kutoa semina ya utawala bora Mkoa wa Iringa, na ninashangaa kuona viongozi wengine wakiendelea kutofuata utaratibu wa Mkuchika.

"Wakuu wa Mikoa wengine wanapagawa sana wanafika hawamjali mtu yeyote ikiwezekana Waziri Mkuu na TAMISEMI muendelee kuwalea hawa vijana kwa sababu haya mambo ya kuwaweka watu ndani yanashusha ari ya kufanya kazi”, alisema Msigwa.

Wakati Mbunge Msigwa akisema hayo, Mbunge wa Chemba Juma Nkamia alibainisha kuwepo kwa tatizo kama hilo wilayani Chemba ambapo zaidi ya watumishi 30 alidai waliomba kuhamishwa kwa sababu viongozi wao kuwa na matumizi mabaya ya madaraka.

Mali za Vigogo Waliokopa SUMA JKT Kuanza kupigwa Mnada

$
0
0
Watu mbalimbali waliokopa matrekta Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT), wakiwamo wabunge na mawaziri, sasa matumbo joto baada ya serikali kutangaza mali zao kukamatwa na kupigwa mnada.

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Hussein Mwinyi, alisema jana bungeni jijini hapa kuwa shirika hilo limepanga kuuza kwa mnada wa mali za vigogo waliokopa matrekta katika shirika hilo.

Dk. Mwinyi alisema hayo alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Ruth Mollel, alilouliza kwa niaba ya Mbunge wa Same Mashariki (Chadema), Naghenjwa Kaboyoka.

Aidha, alisema tangu Rais John Magufuli kuagiza wakopaji wa matrekta kulipa madeni yao, jumla ya Sh. bilioni 2.9 zimekusanywa.

Dk. Mwinyi alisema SUMA JKT imeziandikia mamlaka za ajira za viongozi waliokopa ambao mpaka sasa hawajalipa mikopo yao, wakiwemo wabunge, wakuu wa wilaya na mikoa.

Katika swali lake, Mbunge huyo alitaka kujua mkakati wa kukusanya madeni ya fedha zilizokopwa katika idara mbalimbali kutoka SUMA JKT na wale waliokopa matrekta huku akitaka watangazwe magazetini.

Akijibu swali hilo, Waziri huyo alisema SUMA JKT lilikopesha idara zake Sh. bilioni tano na mpaka sasa Sh. bilioni mbili zimelipwa sawa na asilimia 45.

“Tunaamini fedha hizi zitalipwa kutokana na kuwa idara zilizokopa zinafanyia biashara,” alisema.

Alisema Sh. bilioni 2.9 zimekusanywa na wanajipanga kupiga mnada mali za waliokopa ambao watashindwa kulipa madeni yao katika kipindi hiki cha kukusanya madeni.

“Tayari orodha ya wadaiwa sugu wa matrekta ilishatolewa na kwa sasa wameziandikia mamlaka za ajira kwa viongozi wakiwamo wabunge ambao mpaka sasa hajalipa madeni haya,” alisema.

Dk. Mwinyi alisema orodha ilishatolewa kwenye vyombo vya habari na Spika alishakabidhiwa orodha ya wabunge wanaodaiwa.
 
Katika swali la nyongeza, Mbunge wa Kuteuliwa, Abdallah Bulembo, alitaka kuwekwa orodha ya viongozi wa serikali wakiwamo wabunge na kutangaziwa ili wafahamike.

Awali, katika swali la msingi, Kaboyoka alisema SUMA JKT idara ya zana za kilimo ilikopesha Sh. 5,355,153,000 kwa idara mbalimbali.

“Taarifa ya CAG za mwaka zimeonesha kuwa hadi Juni 30, 2016 ni kiasi cha Sh. 534,785,000 ambayo ni chini ya asilimia 10 ndicho kimerejeshwa, Je, ni kiasi gani hadi sasa kimerejeshwa kwenye idara ya zana za kilimo?” alihoji.

Alihoji pia serikali itakubaliana naye kwamba uzembe wa kutohakikisha mikopo ya fedha za serikali inarudishwa kwa wakati ili wakulima wengine nao waweze kukopeshwa kumechangia kukwamisha juhudi za kupunguza umasikini Tanzania.

“Serikali inachukua hatua gani kuwawajibisha waliohusika na utoaji huo wa mikopo bila kuhakikisha inarudishwa kwa wakati,”alihoji.

Akijibu maswali hayo, Dk. Mwinyi alisema hadi Januari 31, mwaka huu, Sh. 2,389,082,000 zimerejeshwa na Sh. 2,966,071,000 bado hazijarejeshwa.

VIDEO: Fid Q ft Isha Mashauzi, Rich Mavoko & Big Jahman – BAM BAM

$
0
0
VIDEO: Fid Q ft Isha Mashauzi, Rich Mavoko & Big Jahman – BAM BAM

Rudisha heshima yako Kwa Mpenzi Wako, Mke Wako...Tumia Tiba Hii ya Asili

$
0
0
Rudisha heshima yako sasa kwa kutumia Dawa hii iitwayo SUPER GAFINA, kwa ajili ya nguvu za kiume na NKOLOMIJE ni kwaajili ya kuongeza maumbile.

Kwa mwanaume aliye kamilika anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara mbili ,ila ukiwa unapiga moja tena kwa shida wewe ujue  unamatatizo ya upungufu wa nguvu za kiume.

TIBA YA TATIZO LAKO NI; Dawa iitwayo SUPER GAFINA, dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge na unga wa asili ambavyo havina madhara kwa mtumiaji ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja;-

1).itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuchoka.

2).ltakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15 hadi 20 kwa tendo la kwanza.

3).lnaimarisha uume uliolegea na uliosinyaa na kuupa nguvu maradufu.

Je unamaumbile madogo pamoja na uume mfupi? NKOLOMIJE ni suluisho la tatizo lako. Na ni dawa inayoboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi kuanzia inch. 5 hadi 8 kwa muda mfupi sana .Dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk.30 ukisha tumia guarantee miaka 50  ikishakutibu.

Pia ninatibu;- KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU, MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE ,BP, NK.

IGULYATI, ni dawa ya mvuto wa biashara, kazi,kupandishwa cheo na humfanya mfanyakazi kupendwa na mwajiri wake. Pia humvuta mke,Mme,hawara ,mchumba unae muitaji utampata kwa dk.30 tu na atatulia na kumfunga asitoke nje ya ndoa, Pia natoa Pete za bahati ambazo zimetajirisha wengi.

Pia ipo dawa ya kupunguza matiti,unene ,tumbo,na kitambi ,hupunguza mafuta ,kuondoa makovu,chunusi,michilizi mwilini na kuongeza hipsi, makalio na mguu wa bia nk. 

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR,HOSUTWA .Anapatikana Mbagara

Simu no, 0756241666 na 0672186977.

       Huduma hii utaipata popote ulipo

Kutana na Bingwa wa Kutibu Tatizo Sugu la Nguvu za Kiume, Vidonda vya Tumbo kwa Tiba Asili

$
0
0
Ninatibu gonjwa lililosumbua  kwa muda mrefu yaani NGUVU ZA KIUME kwa dawa iitwayo MWAGALA NUNDANUNDA POWER Hutibu na kupona kabisa na kufanya kuongeza hamu ya tendo la ndoa na utaweza kurudia tendo zaidi na zaidi mpaka uchoke mwenyewe,.

Ii kupona kabisa tumia dawa mpaka umalize dozi, dozi yake Ni siku 6 tu,Ni ya miti shamba iliyoboreshwa kwa mfumo wa vidonge na unga.

MMALE;komesha ya maumbile madogo .Kama tatizo limeanzia utotoni huchukua siku 6.

MMEGELE; Ni mixer ya miti 48 kwa kutibu ugonjwa wa kisukari kupanda na kushuka,na kupona kabisa dawa huu hutumika kwa siku 14, kisukari kwako inabaki historia.

SEESE,Ni dawa ya Uzazi kwa wasiofanikiwa kupata watoto awe baba au mama haijalishi una umri gani tumia SEESE uone mafanikio

ITULA,Ni dawa ya kutibu ngiri na Busha bila kufanyiwa operation,dozi ya Busha siku 21 dozi ya ngiri siku 4 na kuuma kwa korodani dozi siku 4.

CHAVAGI,Ni dawa ya heshima sehem za kazi na biashara na kusikilizwa uyasemayo mbele za watu au mitafaruko ndani ya nyumba.

NANGANANGUMU MIXER,Ni dawa ya kutibu tezi dume bila kufanyiwa operation tiba ya tezi dume ipo mlangoni kwako kwa mda wa siku 7 na kupona kabisa..

MUHALE NANSELYA,Ni dawa ya miguu kufa ganzi,kuuma kuwaka moto,magoti,dozi siku 8..

GEMBE,Ni dawa ya kuondoa michirizi,nyama uzembe,chunusi pia kutengeneza shape nzuri.

SUNGURURU,Ni dawa ya kutibu vidonda vya tumbo na kilungulia dozi siku 4.

KASELA NA TALIGURA,Ni dawa ya kukupa utajiri,Pete ya bahati,

HUDUMA ZANGU MASAA 12 PIA NASAFIRISHA KWA WATU WA MBALI NIPO DAR NA SHINYANGA 
 
NO.0753 928 576
 YOUR WELCOME.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images