Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali ya Tanzania na Misri kusainiana mkataba wa makubaliano wa kuanzisha mashamba makubwa ya ngano, mpunga na pamba

$
0
0
Serikali ya Tanzania na Misri zinatarajia kusainiana mkataba wa makubaliano wa kuanzisha mashamba makubwa ya pamoja kwa lengo la kuinua kilimo cha ngano, mpunga na pamba

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Kilimo, Japhet Hasunga mara baada ya kufanya mazungumzo na timu ya Wataalamu wa kilimo kutoka Misri wakiongozwa na Waziri wa Kilimo na Ardhi wan chi hiyo, Dk Ezzidine Abu Stiet.

Mhe. Hasunga amesema katika mazungumzo hayo wamekubaliana kushirikiana katia Sekta ya Kilimo husan katika mazao ya mpunga, ngano na pamba ambapo tande zote mbili zitakuwa na mashamba ya pamoja.

“Kama mnavyojua Misri wamepiga hatua katika kilimo hususani kilimo cha umwagiliaji na tekinolojia hivyo tumekubaliana mafaniko hayo yahamie hapa nchini.”

Waziri Hasunga aliongeza: “Baada ya mazungumzo ya kina na makubaliano katika maeneo ya ushirikiano, tumepeana miezi miwili ili ifikapo mwezi Mei mwaka huu, tutasaini mkataba wa makubaliano na kuanza utekelezaji.

Amesema eneo lingine ambapo wamekubaliana ni kuimarisha Vituo vya Utafiti wa mazao ili kupata mbegu bora na namna bora ya kuzitumia mbegu hizo na pia kuhamisha ujuzi na zana kutoka Misri ambao utasidia kuinua kilimo hapa nchini.

Waziri Hasunga alisema kwa sasa Wataalam wa kilimo wa nchi hizo mbili watatumia muda huu wa miez miwili kutembelea maeneo mbalimbali ili kubainisha maeneo ambayo yanafaa kwa kilimo.

“Mfano tuliwaza kupeleka kilimo cha ngano wilayani Misenyi mkoani Kagera lakini wamesema eneo hilo ni dogo, hivyo wataalamu wa Misri na wale wa Tanzania watapita maeneo mbalimbali kuangalia maeneo yanayofaa na baadaye tusainiane mkataba wa makubaliano,” alisema.

Naye Waziri wa Kilimo na Ardhi wa Misri, Stiet alisema wamekuwa na mazungumzo mazuri na yenye mafanikio na kukubalianakushirikiana katika mafunzo, utafiti na tekinolojia katika sekta ya kilimo ili kuboresha mazao ya kimkakati ya pamba, mbunga na ngano..

“Makubaliano hayo yanaongeza wigo wa ushirikiano kati ya nchi hizi mbili ambayo ni ya muda mrefu, tumekubaliana kuinua kilimo katika mazao matatu kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania. Baada ya kusainiana mkataba tunategemea utekelezaji wa haraka,” alimalizia.

Super Mkuyati: Tiba Sahihi ya Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
ASILIMIA 45-88 YA WANAUME WAPO TOFAUTI NA WENGINE KUTOWATIMIZIA NYEMA WAKE ZAKE ZAO AU WAPENZI WAO SUPER MKUYATI NI TIBA YA MARADHI YAKO
------------------
SUPER MKUYATI; nidawa  iliyo katika mfumo wa vidonge  na  unga , inapambana  na magonjwa sugu  yakina baba.  dawahii inaNguvu  (3) inafanya kazi kwa pamoja (1) inaongeza nguvu zakiume ( 2) itakufanya kuchelewa kufika kileleni  kwa muda wa dk 10-15(3)inazalisha homoni  kwa wingi na kuku fanya uwe na mbegu nyingi zenye vimeleo vingi nya uzazi vilivokomaa
------------------
MDINGO POWER nidawa inayo lefusha na kunene pesha maumbile madogo yaliyosinyaa kunzia nchi
6-8 upana 3-4     dawa hizi hazina madhara hata kwa wazee    TUMIA LEO UONE MAJABU YAKE TIBA HIZI NIZAKUDUMU
------------------
DR GATUNDU anazo dawa zakutibu mangonjwa sugu kama vile kisukali presha henia ngili ya kushuka bila upasuji vidonda vya tumbo kuondoa sumu mwilini  kushikwa na ganzi mwilini
------------------
DR GATUNDU ANA PATIKANA DAR-ES SAALM  WALE WAMIKOANI WATA TUMIWA KWA NJIA YA MABASI PASIPO NA MASHAKA TIBA NI WITO NYOTE MNA KALIBISWA
 DR GATUNDU📞 0716 948950

Rudisha heshima yako Kwa Mpenzi Wako, Mke Wako...Tumia Tiba Hii ya Asili

$
0
0
Rudisha heshima yako sasa kwa kutumia Dawa hii iitwayo SUPER GAFINA, kwa ajili ya nguvu za kiume na NKOLOMIJE ni kwaajili ya kuongeza maumbile.

Kwa mwanaume aliye kamilika anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara mbili ,ila ukiwa unapiga moja tena kwa shida wewe ujue  unamatatizo ya upungufu wa nguvu za kiume.

TIBA YA TATIZO LAKO NI; Dawa iitwayo SUPER GAFINA, dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge na unga wa asili ambavyo havina madhara kwa mtumiaji ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja;-

1).itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuchoka.

2).ltakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15 hadi 20 kwa tendo la kwanza.

3).lnaimarisha uume uliolegea na uliosinyaa na kuupa nguvu maradufu.

Je unamaumbile madogo pamoja na uume mfupi? NKOLOMIJE ni suluisho la tatizo lako. Na ni dawa inayoboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi kuanzia inch. 5 hadi 8 kwa muda mfupi sana .Dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk.30 ukisha tumia guarantee miaka 50  ikishakutibu.

Pia ninatibu;- KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU, MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE ,BP, NK.

IGULYATI, ni dawa ya mvuto wa biashara, kazi,kupandishwa cheo na humfanya mfanyakazi kupendwa na mwajiri wake. Pia humvuta mke,Mme,hawara ,mchumba unae muitaji utampata kwa dk.30 tu na atatulia na kumfunga asitoke nje ya ndoa, Pia natoa Pete za bahati ambazo zimetajirisha wengi.

Pia ipo dawa ya kupunguza matiti,unene ,tumbo,na kitambi ,hupunguza mafuta ,kuondoa makovu,chunusi,michilizi mwilini na kuongeza hipsi, makalio na mguu wa bia nk. 

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR,HOSUTWA .Anapatikana Mbagara

Simu no, 0756241666 na 0672186977.

       Huduma hii utaipata popote ulipo

Waziri Mkuu: Zaidi Ya Sh. Bil. 500 Zimelipwa Kwa Wakulima Wa Korosho

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema zaidi ya sh. bilioni 500 zimelipwa kwa wakulima wa korosho kati ya sh. bilioni 700 zinazotarajiwa na kwamba malipo hayo bado yanaendelea kulipwa kwa wakulima wengine waliosalia.

Amesema tamko la Rais Dkt. John Magufuli la kwamba Serikali itanunua korosho kwa bei ya sh. 3,300 ni kwa ajili ya korosho za daraja la kwanza  na bei ya korosho za daraja la pili ni asilimia 80 ya zile za daraja la kwanza.

Ametoa kauli hiyo leo asubuhi (Alhamisi, Februari 7, 2019) Bungeni jijini Dodoma katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu wakati akijibu swali la Mbunge wa Liwale, Zuberi Kuchauka.

Mbunge huyo alitaka kupata kauli ya Serikali kuhusu malipo kwa wakulima wa korosho ambao walikuwa wakilipwa sh. 2,600 kwa kilo wakati Rais Dkt.  Magufuli alisema Serikali itanunua kilo moja ya korosho kwa sh. 3,300.

“Malipo yanaendelea na sehemu kubwa ni kwa wakulima wenye kilo zaidi ya 1,500, Serikali itanunua korosho zote kama ilivyoelezwa. Taratibu zinazofanyika ni kuhakikisha anayelipwa ni muhusika. Wananchi endeleeni kuiamini Serikali yenu.”

Waziri Mkuu amesema ilikuwa ni lazima kwa Serikali ifanye uhakiki kwa wakulima hususani wale wenye kilo zaidi ya 1,500 ili kujiridhisha kama ni wakulima, hivyo baada ya kuhakikiwa wakulima wote watalipwa fedha zao.

Amesema Januari 27, 2019 alitoa maagizo kwa Wizara ya Kilimo pamoja na Bodi ya Mazao Mchanganyiko wahakikishe hadi Februari 15 mwaka huu wawe wamekamilisha zoezi la uhakiki na kuwalipa wakulima wote wa zao la korosho.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo wakati akizungumza na wadau wa zao la korosho kwenye kikao kilichofanyika mkoani Mtwara, lengo la kikao hicho ilikuwa ni kupata taarifa juu ya mwenendo mzima wa bidhaa hiyo kwa msimu wa mwaka 2018/2019.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amesema Serikali haijakiuka sheria kuhusu suala la watumishi kupandishwa mishahara na kwamba ina nia njema ya kuhakikisha wanalipwa mishahara na posho nzuri.

Ameyasema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Mbozi, Pascal Haonga aliyedai Serikali imekiuka sheria ya utumishi kwa kutopandisha mishahara, ambapo Waziri Mkuu amesema  Serikali haikukiuka sheria, bali iliamua kushughulikia suala hilo kwa kuanza na uhakiki wa watumishi.

Waziri Mkuu amesema baada ya kufanya uhakiki na kubaini uwepo kwa watumishi hewa pamoja na waliokuwa wakitumia vyeti vya kugushi, iliwaondoa na sasa Bodi ya Mishahara na Maslahi ya Watumishi wa Umma inafanya mapitio ya mishahara baada ya kubaini tofauti, hivyo watumishi waendelee kuwa watulivu.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Super Mkongo: Kiboko ya Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- uume kusimama kwa kulegea
- uume kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Pia kuna MCONGO POWER Kiboko ya uume mdogo inaboresha maumbile ya uume kwa kurefusha na kunenepesha kwa saizi uipendayo haijalishi umri hata kwa walioathirika na upigaji punyeto.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume na uume mdogo.
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________
Kwanini uhangaike? Kwanini uhuzunike?
Hii ni spesho kwa waliotumia madawa mengi bila kufanikiwa hakika hautajuta kuitumia. _______________________________
WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia
_______________________________
********************************

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Kesi ya Kitilya na Wenzake yatinga Mahakama ya Uhujumu Uchumi

$
0
0
Upande wa Jamhuri umeshawasilisha jalada la kesi ya  Mahakama Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitillya na wenzake.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 58 yakiwamo 49 ya kutakatisha fedha.

Jalada hilo limewasilishwa katika mahakama hiyo jana likiwa na taarifa ya maelezo ya mashahidi na kupokelewa kisha kurejeshwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa hatua za mwisho ili ianze kusikilizwa.

Washtakiwa wanasubiri kuitwa na Mahakama ya Kisutu kwa tarehe itakayopangwa kwa ajili ya kusomewa maelezo ya mashahidi kisha jalada lirudi Mahakama Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi kwa ajili ya kuanza kusikiliza ushahidi.

Washtakiwa katika kesi hiyo ni, Kitilya, Kamishna wa Sera ya uchambuzi wa Madeni kutoka Wizara Fedha na Mipango, Bedason Shallanda, msaidizi wake Alfred Misana na maofisa wa benki ya Stanbic, Shose Sinare na Sioi Solomon.

Taarifa Kwa Umma Ya Wito Wa Wadau Kwa Ajili Ya Kutoa Maoni Kuhusu Muswada Wa Sheria


Nkoma: Tiba Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
NKOMA
_________________________
NKOMA Ni dawa bora ya nguvu za kiume  yenye mchanganyiko wa mitishamba (7) yenye maajabu yafuatayo/

🔖 (1) inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimalisha misuli ya uume uliolengea wakati wa tendo la ndoa/
🔖 (2) Kurefusha maumbile ya kiume yaliyorudi ndani kuazia nchi 5 - 9/
🔖 (3) kunenepesha uume cm 5 ya upana itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 - 20 kwa tendo la kwanza na utakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya 2-4 bila hamu kuisha/

📌 Na inatibu kabisa, unashauriwa uitumie dawa hii kama kinga ya magonjwa sugu./
 📌 Haijalishi umri hata kama una miaka 85 itumie huanza kufanya kazi dk 50 tu na haina madhara yoyote kwa mtumiaji/

📍📍📍📍📍📍📍📍📍
            MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA.
_________________________
🔖 (1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖 (2)Choo kama cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(4)Kaswende/
🔖(5)Gono/

📌Haya yote husababisha kuishiwa nguvu za kiume na kuwa na uume mdogo/
📌 Itumie leo, bado hujachelewa ni tofauti na nyingine.
_________________________
DR MAKOBA ANAPATIKANA DAR ES SALAAM, PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
___________________________
WASILIANA NA
Dr MAKOBA SIMU.
📞0754832349
📞0683490600
____________________________
*****************************

Rais Magufuli Akutana Na Kaimu Balozi Wa Eu Nchini, Mjumbe Maalumu Wa Rais Wa Zimbabwe Ikulu Jijini Dar Es Salaam

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 07 Februari, 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Mjumbe Maalum wa Rais wa Zimbabwe ambaye ni Waziri wa Ardhi, Kilimo, Maji, Mazingira na Makazi Vijijini Mhe. Pretence Shiri.

Mazungumzo hayo yamefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam ambapo Mhe. Shiri amekabidhi barua kutoka kwa Rais wa Zimbabwe Mhe. Emmerson Mnangagwa.

Mhe. Shiri ameishukuru Tanzania kwa mchango mkubwa ilioutoa kwa Zimbabwe wakati wa kupigania uhuru uliopatikana mwaka 1980, na amebainisha kuwa Wazimbabwe wanaichukulia Tanzania kuwa ni nyumbani.

“Tunafurahi sana kuwa hapa Tanzania, tunajisikia ni nyumbani kwetu, bila Tanzania Zimbabwe isingepata uhuru mwaka 1980, ingechukua muda mrefu sana, lakini tunafurahi kuwa Watanzania walijitolea kwa kiasi kikubwa kuhakikisha Zimbabwe inakuwa nchi huru” amesema Mhe. Shiri.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Jumuiya ya Ulaya Bw. Charles Stuart na baada ya mazungumzo hayo Bw. Stuart amesema mazungumzo baina yao yalikuwa mazuri na yamehusu uhusiano wa muda mrefu wa Tanzania na Umoja wa Ulaya na dhamira ya umoja huo kuisadia Tanzania.

“Uhusiano wa Tanzania na Umoja wa Ulaya umekuwa imara siku zote, na kumekuwa na maeneo mengi ya uhusiano yenye maslahi muhimu kwa pande zote na kwa miaka mingi” amesema Mhe. Stuart.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam

07 Februari, 2

Je Kwanini Baadhi Ya Wanaume Wengi Wana Ukosefu Ama Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
JE KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UKOSEFU AMA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO ???

Pata sululisho la matatizo haya na  magonjwa mengine utapona kwa mda mfupi sana hatakama ulihangaika mpaka ukakata tamaaa 

GALIMBO 3 MIX  ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa aina mbili ili kukidhi mahitaji ya mtumiaji, imetengenezwa kwa muundo wa vidonge pamoja na unga kwaajili ya kuponesha tatizo moja kwa moja , huimalisha misuli ya uume iliyolegea wakato wa tendo la mdoa ,na kukufanya ucherewe kufika kileleni kwa mda wa dk ( 20 - 45 ) itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu nira hamu kuisha wara kuhisi kuchoka vilivile huzalisha viini vya uzazi ( manii ) 

YOLAN  hurefusha na kunenepesha  maumbile madogo ya uume na kuwa na uume kuanzia nchi (6-8) tiba kwa mda mfupi sana

Zipo sananu nyingi sana zinazosababisha matatizo hayo  km vile -:punyeto, kisukali,ngili,chango,vidonda vya tumbo,  tumbo kuunguluma na kujaa gesi maumivu ya mgongo ama kiume ,kolodani moja kuvimba ama kuingia ndani  presha nk 

Matatizo haya yote sio mageni, kigeni ni tiba sahihi ya kuponesha matatizo hayo

SUPER MBUKE -:  nidawa ya kuponesha tatizo la kisukali kwa mda mfupi sana , usihangaike wara kuteseka tumia dawa ya mitishamba kwaajili ya tatizo hili na upone kabisa

NTINJIWA  nidawa ya mvuto wa biashara,kazi, kupandishwa cheo,kumfanya mfanyakazi apendwe na bos wake

Pia ninadawa za kumvuta mme , mke,mchumba,hawara, au mtu yoyote unaemuhitaji katika maisha yako hata km yupo mbali na atatulia na kukutimizia cjovjote utakacho na kumfunga asiwe na mtu mwingime ,

Pata tiba za magonjwa mbalimbali ikiwemo miguu kuwaka moto, mgongo,bawasili ,kaswende ,gono na mengine mengi

KWAUSHAULI NA TIBA WASILIANA NA DR CHIKAGO    0759 208 637

Km huna nafasi ya kufika ofisini hudumahii utaletewa hapo ulipo , kwa wale wa mikoani natuma kwanjia ya basi

Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii Yaitaka BASATA Iache Kufungia Nyimbo za Wasanii

$
0
0
Kamati ya  Bunge ya Maendeleo ya Jamii imelitaka Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) kuacha kufungia nyimbo za wasanii na badala yake kutekeleza jukumu la kuwalea na kuwashauri kuandaa nyimbo zinazoendana na maudhui.

Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za kamati hiyo bungeni jijini Dodoma leo Alhamisi Februari 7, 2019 makamu mwenyekiti  wa kamati hiyo, Juma Nkamia amesema mojawapo ya kazi ya Basata ni kutoa ushauri na misaada ya kiufundi kwa wasanii na wadau.

Amesema hivi karibuni kumekuwa na wimbi la kufungia nyimbo za wasanii na matamasha mbalimbali.

Amesema wasanii hao wamekuwa wakipata mapato mengi kutokana na ‘Hits’ wanazopata kupitia mitandao ya kijamii kama Youtube, Serikali haipati chochote kutokana na mahusiano yasiyoridhisha.

Nkamia amesema kamati inapendekeza Basata kutekeleza jukumu lake la kuwalea pamoja na kuwashauri kuandaa nyimbo zinazoendana na maudhui na kuwaonya pale wanapokosea.

Amesema kamati inashauri kuboresha mahusiano na wasanii ili kufaidika na mapato yatokanayo na hits za mitandao ya kijamii.

Ester Bulaya amsababishia Halima Mdee kushindwa kufika Mahakama

$
0
0
Mbunge wa Kawe (CHADEMA), Halima Mdee ameshindwa kufika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa sababu anamuuguza Mbunge mwenzie wa Bunda Ester Bulaya.

Mdee alishindwa kufika mahakamani hapo katika kesi inayomkabili ya kutoa lugha chafu dhidi ya Rais John Magufuli.

Hayo yameelezwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba na mdhamini wa Mdee, Faris Lupomo wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa.

Lupomo alidai kuwa aliwasiliana na Mbunge huyo na kumueleza kuwa atashindwa kufika mahakamani kwa kuwa anamuuguza Mbunge mwenzie Bulaya mjini Dodoma.

“Niliwasiliana naye jana (juzi) akanijulisha kuwa anamuuguza Mbunge mwenzie Ester Bulaya ambaye anaishi naye Dodoma nyumbani kwake na anamuuguzia hospitali ya Bunge Dodoma, “ alidai shahidi huyo.

Wakili wa Utetezi Hekima Mwasipu naye alikiri kuwa mshtakiwa huyo hayupo Mahakamani na amepewa taarifa na mdhamini huyo kuwa anamuuguza Bulaya mjini Dodoma.

Baada ya maelezo hayo, Hakimu Simba alisema kuwa sababu zilizotolewa na mdhamini huyo kuhusiana na kushindwa kufika kwa mshtakiwa kufika zinaleta ukakasi na kubainisha kuwa zina lengo la kuifanya kesi hiyo isimalizike kwa wakati.

“Mdhamini ulichokiongea kinaleta ukakasi wa kutosha, kwa sababu wapo Madaktari na Wabunge wengine wanawake ambao wanaweza kumuuguza, sasa tukiruhusu haya yaendelee tutashindwa kumaliza kesi”

“Kiukweli jambo hili linakwaza na linatia wasiwasi kama hii kesi tutaweza kumaliza kwa mwendo huu, tunakubali sababu hiyo ya kuuguza lakini kwa shingo upande, “ Alisema Hakimu Simba

Baada ya maelezo hayo, Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi, Februari 28, 2019 kwa ajili ya kesi hiyo kuendelea na ushahidi.

Mpaka sasa mashahidi watatu wamekwisha kutoa ushahidi katika kesi hiyo akiwemo Mkuu wa Kituo cha Polisi Urafiki, Mrakibu wa Polisi Batseba Kasanga.

Mdee anadaiwa kutenda kosa hilo Julai 3, mwaka jana maeneo ya Ofisi za CHADEMA zilizopo Mtaa wa Ufipa Wilayani Kinondoni, DSM ambapo alimtukana Rais Dk John Magufuli kwamba “anaongea hovyohovyo anatakiwa afunge break”, kitendo ambacho kingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Kanuni bora za ufugaji wa kuku wa kienyeji(kuku Asili)....Soma Hapa Uwe Tajiri

$
0
0
Ufugaji wa kuku wa asili ni nyenzo muhimu katika kupambana na wimbi la umasikini kwa kuongeza kipato cha kaya. 

Hata hivyo, pamoja na soko la uhakika, bado ufugaji kuku haujaweza kutumika ipasavyo kupambana na umaskini unaowakabili Watanzania wengi.

 Ni mazoea kwa jamii nyingi hapa Tanzania kufuga kuku wa asili kama sehemu ya mila na desturi zao. Kuku wa asili amekuwa akifugwa bila ya kupatiwa huduma muhimu kama makaazi bora, chakula cha ziada, tiba, kinga za magonjwa mbali mbali. 

Muhtasari huu unatoa muongozo wa ufugaji wa kuku wa asili ili uweze kuzalisha na hatimae kukuza kuku kwa wingi.

Usafi wa vyombo na mazingira ya kuku
Uchafu ni mama wa magonjwa, hivyo zingatia haya;
1.  Vyombo vya chakula na maji visafishwe mara kwa mara kwa maji safi na sabuni.

2. Pumba au chakula kilicholowana na kuchanganyika na kinyesi cha kuku kitolowe na kufukiwa.

3.  Choma moto au zika kwenye shimo refu kuku waliokufa kwa ugonjwa.

4.  Usifuge kuku na ndege wa jamii nyingine kwa mfano bata katika banda moja.

5.  Ondoa mbolea mara kwa mara kutoka katika banda la kuku.

6.  Tumia dawa za kuulia vimelea kusafishia banda na upake chokaa angalau mara moja kwa mwaka.

7.Ziba matundu yote yanayoweza kuruhusu panya na wanyama wakali kama vicheche kuingia katika banda la kuku.


Magonjwa na kinga kwa kuku wote

1.Ndui ya kuku
Huathiri sana vifaranga wanaokua na ujitokeza kwa wingi wakati wa mvua za muda mrefu. Husababisha vivimbe katika uso/ kishungi na hata sehemu nyengine zisizo na manyoya.

2.Mdondo/kideri
Mdondo, au kwa majina mengine lufuo, au kideri ni ugonjwa hatari katika magonjwa ya kuku wa asili. Ni ugojwa wa virusi ambao huathiri kuku wa rika zote, huweza kuangamiza kuku wote kijijni.

3.Ukosefu wa vitamini A
Ugonjwa huu husababisha macho kuvimba na kutoa uchafu mziito kama sabuni iliyolowana. Kuku wenye dalili hizi hawaponi na hata kufa. Ugonjwa hujitokeza baada ya kipindi kirefu cha kiangazi kwa ajili ya ukosefu wa majani mabichi.

4.Kosidiosisi
Huathiri kuku wa umri wowote lakini huuwa zaidi vifaranga na kuku wanaokua. Kuku hudhoofika, manyoya huvurugika na kuku huwa kama wamevaa koti. Kuku huarisha damu au kinyesi cha kahawia na huzubaa na kuonekana kama wamevaa koti.

5.Viroboto, chawa na utitiri
Hawa ni wadudu wa nje wanaoshambulia ngozi. Huweza kusababisha ugonjwa kutokana na kunyonya damu. Viroboto hushambulia kichwa na kunata huku wakinyonya damu. Viroboto huuwa vifaranga. Chawa na utitiri hughasi kuku hadi wakashindwa kutaga na kuatamia.

6.Minyoo
Minyoo huweza kudhofisha kuku na kuwafanya waweze kuugua maradhi mengine kirahisi. Muone mtaalaam ukihisi kuku wako wana minyoo.


Chakula cha ziada
1.Wapatie vifaranga nyongeza ya protini kwa kuwachanganyia vumbi la dagaa au vichwa vya dagaa vilivyotwangwa kwenye pumba za mahindi.

2.Changanya kikombe kimoja cha vumbi la dagaa na vikombe vitano vya pumba za mahindi (tumia kikombe kidogo cha chai).

3.Mchwa na wadudu wengine wanaweza kutumika kama nyongeza ya protini.

4.Vuna mchwa kwenye vichuguu au tengeneza mchwa katika njia za mchwa.

5. Kutengeneza mchwa: changanya kinyesi cha ng’ombe na majani makavu, mabua ya mahindi au maranda ya mbao katika chungu au ndoo ya zamani.

6Mwagia maji hadi kila kilichomo kilowane kisha weka katika chombo kama ndoo au chungu. Weka chombo chako katika njia ya mchwa ukikigeuza juu chini na subiri hadi kesho yake asubuhi, kisha beba vyote vilivyomo na uwamwagie kuku mahali walipo.

Utotoleshaji wa vifaranga
Chagua jogoo bora na tetea bora kuzalisha kuku.

Sifa za jogoo bora
1.  Awe na umbo kubwa, awe ukiko mzuri na usioangukia upande mmoja.

2.  Apende kuwa na himaya yake. Ukimpata jogoo mwenye sifa hizi mueke yeye na matetea kumi. Hivyo ukiwa na matetea ishirini jogoo wawili wanatosha.

Sifa za tetea bora
Tetea bora ni yule mwenye umbo kubwa, mwenye uwezo wa kutaga mayai ya kutosha, kuatamia na hatimaye kutotoa vifaranga.

Uhifadhi wa mayai
1.  Weka mayai mahali safi na penye hewa ya kutosha.

2.  Tumia kasha lililokatwa na kujaza mchanga mkavu na safi au kasha la kuhifadhia mayai.

3.  Weka sehemu butu ya yai iwe upande wa juu na ile iliyochongoka itizame chini.

4.  Andika namba au tarehe katika siku lilipotagwa.

5.  Mayai yakishatagwa yatolewe na kuhifadhiwa na moja liachwe kwenye kiota ili kumuita kuku kuja kutaga kesho yake.

Kuatamiza mayai
1.  Kuku awekewe mayai yatakayokuwa na uwezo wa kuyaatamia na kuyatotoa yote.

2.  Mayi 10 hadi 12 yanatosha kuatamia.

3.  Mayai ya kuatamiza yasizidi wiki 2 toka kutagwa.

4.  Yai la mwisho kutagwa liwe la kwanza kuchaguliwa hadi yapatikane mayai 10 mpaka 12, na apewe kuku wa kuyaatamia.

5.  Mayai ya kuatamiza yasafishwe kwa kitambaa kikavu na safi au kilichowekwa spiriti

Kutotolesha vifaranga wengi kwa wakati mmoja
1.  Kama unataka kuku zaidi ya mmoja watamie na kutotoa kwa mpigo fanya yafuatayo;

2.  Kuku wa kwanza akianza kuatamia muwekee mayai yasiyo na mbegu mfano mayai ya kuku wa kisasa au kuku asiye na jogoo.

3.  Rudia zoezi hilo hadi utakapofikisha kuku watano kisha wawekee kuku wote mayai yenye mbegu.

Matunzo ya vifaranga ili kuzuia vifo
Vifaranga wengi hufa kabla ya kufikisha miezi miwili kutokana na magonjwa, baridi na kuliwa na wanyama wengine. Ili kupunguza vifo vya vifaranga wa siku 1 hadi miezi miwili zingatia yafuatayo;

Ulinzi dhidi ya mwewe na wanyama wengine
1.  Weka vifarang kwenye tega na kuwafunika ili wasiende mbali wakati wa mchana. Wape maji na chakula. Hakikisha hawapigwi jua wala kunyeshewa mvua. Wakati wa usiku walale na mama yao.

Chanjo ya mdondo kideri/lufuo
Kama tetea alichanjwa kabla ya kuanza kutaga vifaranga wanaoanguliwa huwa na kinga ya mdondo ya kuwatosha kwa wiki 3 za kwanza za maisha yao. Wachanje vifaranga hao dhidi ya mdondo wafikishapo umri wa siku 18.

Vifaranga ambao historia ya chanjo ya mama haijulikani, wapewe chanjo ya mdondo siku tatu baada ya kuanguliwa, rudia hadi wakifikisha wiki tatu kisha uchanje kila baada ya miezi 3

Kinga dhidi ya kosidiosisi
Kinga ya kosidiosisi kwa vifaranga, itolewe hata kama ugonjwa haujajitokeza.

1.  Wape dawa ya amprolium kwa muda wa siku tatu mfululizo mara wafikishapo siku saba tokea waanguliwe kama kinga ya kosidiosisi.

2.  Dawa inaweza kutolewa hata kama wamevuka umri huo. Fuata maelekezo ya mtaalam juu ya kiasi cha dawa kinachopaswa kuchanganwa katika maji au pumba

3.  Kama vifaranga wadogo wataonesha dalili za kuzubaa kama kuvaa koti wapewe dawa ya amprolium kwenye maji kwa utaratibu ufuatao;

Dawa siku tatu mfululizo: usiwape kwa siku mbili; gawa tena kwa siku tatu

Hitimisho
1.  Hakikisha banda na vyombo vya chakula cha kuku ni visafi kuepusha magonjwa.

2.  Usichanganye kuku na bata katika banda moja

3.  Lisha chakula cha ziada hasa kwa vifaranga.

4.  Kideri, kosidiosisi, ndui na upungufu wa vitamini A ni vyanzo vikuu vya vifo vya kuku wako. Kumbuka kukinga kuku wako dhidi ya magojwa haya.

5.  Kumbuka kuchagua mayai ya kuatamiza kama ilivyoelekezwa ili kuepuka kupata mayai viza.

6.  Vifaranga wadogo hadi wiki nane huhitaji matunzo mazuri, fuata maelezo kuzuia vifo.

7.  Kumbuka ukiuza kuku wengi kwa mpigo utaongeza mapato yako, jitahidi kuzalisha vifaranga kwa wingi ili upate kuku wengi baadae.

8.  Muone mtaalam wa mifugo ulie karibu nae kwa ushauri zaidi.

Ondoa Kibamia Na Tibu tatizo la Nguvu Za Kiume Kwa Dawa Hii Ya Mitishamba

$
0
0
JILO HERBAL CLINIC

ONDOA KIBAMIA NA ONGEZA NGUVU ZA KIUME KWA DAWA HII YA MITISHAMBA AMBAYO NI KOMESHA KWA TATIZO SUGU LA NGUVU ZA KIUME

SUPER MBONGOSHI; Ni dawa ya mitishamba ambayo inatibu tatizo la nguvu za kiume inakufanya kuchelewa kufika kileleni na kuongeza hamu ya kuendelea kufanya tendo.
 
SUPER MBONGOSHI2 Ni dawa ya mitishamba ambayo ina nenepesha na kurefusha maumbile mafupi au yaliyosinyaa na kuufanya kuwa imara dawa hii inasafisha mishipa ya Uume ambayo imedhurika na matatizo mbali mbali kama vile kupiga punyeto kwa mda mrefu,ngiri,kisukari,vidonda vya tumbo na mengine mengi.
 
DR.JILO Pia anatibu magonjwa mengine kama vile kisukari,ngiri,ugumba,pressure n.k

KWA HUDUMA ZA JILO HERBAL CLINIC WASILIANA NA DR.JILO SASA UPATE DAWA HII .UTATUMIWA POPOTE PALE ULIPO PIGA SIMU
0752723508

Waziri Mkuu: Watumishi wa Umma Kuweni na Subira Ongezeko la Mishahara

$
0
0
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa, amewataka watumishi wa umma kuwa na subira kwa sababu Serikali inaendelea na mchakato wa kuwatambua watumishi wa umma halali na kufanya ulinganifu wa mishahara katika kada mbalimbali ili watumishi hao waanze kulipwa mishahara stahiki.

Waziri Mkuu Majaliwa ameyazungumza hayo leo Jijini Dodoma wakati alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mbozi, Mhe Pascal Haonga, lililohoji juu ya ongezeko la mishahara kwa watumishi wa umma chini ya Sheria ya Utumishi wa Umma.

Mhe. Majaliwa amefafanua kuwa mwanzoni nchi ilikuwa na idadi kubwa ya wafanyakazi hewa ambapo wote kwa pamoja walikuwa wakilipwa mishahara na posho mbalimbali hivyo, ili kuwatambua watumishi halali Serikali iliamua kufanya uchunguzi na kuwagundua watumishi hao hewa.

Pia, Serikali ilifanya uchunguzi mwingine wa kuwatambua watumishi wenye vyeti stahiki vya kufanya kazi mbalimbali Serikalini kwa mujibu wa Kanuni za Utumishi wa Umma.

Mhe. Majaliwa ameongeza kuwa baada ya kumaliza utambuzi wa watumishi halali, Rais Dkt. Magufuli aliunda Tume ya Mishahara na Motisha kwa ajili ya kufanya mapitio ya kada zote za Utumishi wa Umma na viwango vya mishahara ili kutambua ulinganifu kati ya stahiki ya mshahara na kada husika.

“Lengo la Rais Magufuli kuunda tume hiyo ni kufanya tathmini nzuri ili kutambua weledi wa kazi, uwajibikaji na tija inayopatikana mahala pa kazi, hivyo baada ya kukamilika Serikali itatoa taarifa,” alisema Mhe. Majaliwa.

Aidha, Mhe. Majaliwa ametoa rai kwa Watumishi wa Umma kuendelea kuiamini serikali kwani ina nia ya dhati kuhakikisha watumishi wote wanapata haki zao stahiki vile vile mpaka sasa mjadala kati ya Serikali na Vyama vya Wafanyakazi unaendelea vizuri.

Serikali imejiandaa Vyema Kunufaika na Ujio wa Mashindano ya AFCON

$
0
0
Na Anitha Jonas – WHUSM,Dodoma.
Serikali kwa kushirikiana na taasisi zote muhimu imejiandaa kupokea wageni wote watakao shiriki mashindano ya AFCON yanayotarajia kufanyika nchini hivi karibuni .

Kauli hiyo imetolewa leo bungeni jijini Dodoma na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kilolo Venance Mwamoto (CCM) wakati wa maswali ya papo kwa papo ya wabunge.

“Serikali inatambua maandalizi yanayofanyika na Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo  kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) pamoja na wadau mbalimbali na tunatambua kuwa tutapokea wageni wengi akiwemo Rais wa Shirikisho la Mpira Duniani (FIFA)”,alisema Mhe.Waziri Mkuu Majaliwa.

Aidha,Mheshimiwa Waziri Mkuu aliendelea kusema kuwa kupitia mashindano hayo serikali imehamasisha Mikoa ya jirani kujipanga kunufaika na mashindano hayo na jumla ya viwanja vitatu vitatumika  na nijukumu la watanzania wote kushirikiana ili kuhakikisha tunanufaika kwa ujio huu mkubwa.

Pamoja na hayo Mheshimiwa Majaliwa aliendelea kuwasisitiza TFF kuimarisha maandalizi ya timu hiyo itayoshiriki ili taifa liweze kuibuka kidedea,vilevile aliwasihi watanzania wote   kuonyesha uzalendo kwa timu yao ili kuweza kuwatia moyo kwa kuwa na imani kuwa timu hiyo itaweza kushinda.

Nae Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza ametoa majibu ya swali la Mbunge wa Konde Mhe.Khatibu Haji (CUF) lilihoji kuhusu mgao wa fedha zinazotolewa na FIFA kwa TFF kuwa ni kiasi gani zimekwisha pelekwa kwa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) kwa kusema kuwa kuwa kufuatia changamoto TFF kutokukidhi vigezo vya utawala bora na uwazi katika matumizi ya fedha kwa zaidi ya miaka mitatu wamekuwa hawapati mgao na FIFA ila kwa kuanzia mapema mwaka huu wanatarajia kuanza kupata mgao huo baada ya kutatua changamoto hizo.

Halikadhalika katika swali la nyongeza Mhe.Naibu Waziri Shonza alijibu kuwa si kweli kuwa ZFA haijawahi kupatiwa msaada wa TFF kwani wameshawahi kupatiwa msaada wa miradi moja wapo ni ujenzi wa ukarabati wa uwanja wa Gombani Pemba na kufafanua kuwa ZFA ni sehemu ya TFF hivyo fedha zinazoletwa na FIFA kwa TFF hugawiwa  kwa mashirikisho yote na ZFA hawaletewi fungu lao peke yao kwani ZFA siyo mwanachama FIFA wala CAF.

Watu Wanne Watiwa Mbaroni Jijini Mbeya Kwa Kuingiza Bidhaa Nchini Kinyemela Bila Kulipia Ushuru

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu wanne pamoja na gari moja aina ya Toyota Coaster kwa kosa la kuingiza bidhaa nchini kinyume cha sheria.

Ni kwamba mnamo tarehe 06.02.2019 majira ya saa 22:00 usiku huko katika kizuizi cha barabarani kilichopo eneo la Kayuki, Kata ya Mpuguso, Tarafa ya Pakati, Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi wakiwa Doria waliwakamata watu wanne [04] ambao ni:-
  1. MARY ANDEMBWISYE [30] Mfanyabiashara na Mkazi wa Ghana Mbeya
  2. TUMPE ANDEMBWISYE [32] Mfanyabiashara na Mkazi wa Ghana Mbeya 
  3. . ISSA KIBONA [47] Dereva na Mkazi wa Kyela na
  4.  YOHANA ADAM [25] Kondakta na Mkazi wa Rungwe Mission
Watuhumiwa walikamatwa wakiwa wanaingiza bidhaa nchini bila kulipia ushuru ambazo ni bello 26 za mitumba kutoka nchi jirani ya Malawi. Mzigo huo ulikuwa umepakiwa kwenye gari yenye namba za usajili T.350 DDR aina ya Toyota Coaster.

Watuhumiwa watafikishwa Mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Ofisi Ya Rais-Utumishi Yafanya Ufuatiliaji Wa Utekelezaji Wa Waraka Wa Mavazi Kwa Watumishi Wake

$
0
0
Idara ya Ukuzaji  Maadili, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kushirikiana na Kamati ya Uadilifu ya ofisi hiyo, imefanya ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Waraka wa Mavazi Na. 3 wa Mwaka 2007 kwa watumishi wa ofisi hiyo kwa lengo la kujiridhisha na kiwango cha utekelezaji wake, ikiwa ni pamoja na kuhimiza watumishi wa umma nchini kuzingatia waraka huo mahala pa kazi.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Ukuzaji Maadili, Sehemu ya Ufuatiliaji Uzingatiaji wa Maadili, Bibi Janeth Mishinga mara baada ya kukamilika kwa zoezi la ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Waraka huo kwa watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambao unawaelekeza watumishi wa umma aina ya mavazi wanayostahili kuyavaa mahala pa kazi.

Bibi Mishinga amesema, Ofisi ya Rais-Utumishi ni msimamizi wa miongozo mbalimbali ya kiutumishi ikiwemo Kanuni za Maadili ya Utendaji katika Utumishi wa Umma ambapo kanuni ya kwanza inaelekeza utoaji wa huduma bora na kuongeza kuwa moja ya kigezo cha watumishi wa umma kutoa huduma bora ni pamoja na kuvaa mavazi  yenye staha.

Bibi Mishinga amefafanua kuwa, zoezi hilo la ukaguzi katika ofisi ya Rais-Utumishi limebaini kuwa asilimia 95 ya watumishi wameonekana kutekeleza vema waraka huo wa mavazi ikiwemo kuwahi kazini na asilimia tano ya watumishi waliobainika kutotekeleza waraka huo wamekumbushwa kuuzingatia.

Aidha, Bibi Mishinga ametoa wito kwa wasimamizi wa taasisi zote za umma nchini  kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa waraka huo na kuwahimiza watumishi walio chini yao  kuwahi kazini kwa ili kutoa huduma bora na kwa wakati kama ambavyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli anavyohimiza.

Bibi Mishinga  amesisitiza kuwa, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora  ikiwa ndio msimamizi wa waraka huo wa mavazi itaendelea kufanya ukaguzi na ufuatiliaji  katika taasisi zote za umma nchini na haitosita kuwachukulia hatua za kinidhamu watumishi wote wa umma watakaobainika kuukiuka.

Mbunge Ataka Mashine ya Kuwapima Wanaume Wasiotahiriwa Bungeni

$
0
0
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Jackline Ngonyani ametaka wabunge ambao hawajafanyiwa tohara kuchunguzwa na wakibainika wafanyiwe, akibainisha kuwa hiyo ni mbinu mojawapo kupambana na maambukizi ya Ukimwi.

Jackline ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Februari 7, 2019 bungeni jijini Dodoma katika mjadala wa taarifa ya kamati ya Bunge ya masuala ya Ukimwi.

Amesema kwa utafiti ambao umefanyika unaonyesha wanaume ambao hawajatahiriwa wamekuwa wakiambukiza magonjwa mbalimbali, ukiwemo Ukimwi kwa asilimia 60.

Mbunge huyo alikatishwa na mbunge wa Rombo (Chadema), Joseph Selasini aliyempa taarifa kwamba hata Bunge la Kenya liliweka wataalam mbele ya mlango wa Bunge,  wale waliobainika hawajatahiriwa walipata tiba.

“Ni sahihi kabisa Spika unaweza kuchukua utaratibu huo ili kuepuka maambukizi ya Ukimwi,” amesema Selasini.

Baada ya taarifa hiyo, Jackline aliendelea kuzungumza akibainisha kuwa zoezi hilo ni vyema lianzie kwa wabunge na watakaobainika hawajatahiriwa wafanyiwe tohara mara moja.

Amesema pia wasiofanyiwa tohara wamekuwa wakiambukiza kansa ya kizazi kwa wanawake.

Mbunge wa Mtwara Vijijini (CCM),  Hawa Ghasia alimpa taarifa Jackline kuwa wakati akitoa hoja ya wabunge wanaume wapimwe mikono sweta, hawakuwepo ndani ya ukumbi wa Bunge ili waweze kuunga mkono hoja hiyo.

Ghasia amesema jambo la kusikitisha wasiofanyiwa tohara wanakwenda kuambukiza magonjwa wanawake.

Hata hivyo, mbunge wa Geita (CCM),  Joseph Kasheku ‘Musukuma’ alitoa taarifa akisema si jambo jema kutaka wabunge wasiofanyiwa tohara waweze kutambulika na kufanyiwa.

“Lakini pia takwimu zinaonesha kuwa hata wanawake waliokeketwa pia wanachangia maambikizi ya Ukimwi. Hivyo tuwekewe mashine ili wakati tunapima wanaume wasiotahiriwa basi tupime na wanawake waliokeketwa,” amesema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images