MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
Tukaingia kwenye godauni hili lenye ukimya huku kofia yangu nyeusi nikiwa naimeivaa vizuri kichwani mwangu na kuficha kabisa sura yangu. Kwa mavazi haya meusi niliyo yavaa si rahisi kwa mtu kuweza kunitambua kwamba ni mimi.
Tukaingia katika chumba ambacho amemning’iniza mzee huyu kichwa chini miguu juu huku akiwa amemvua nguo zote na kumbakisha na boksa tu na usoni mwake amemfunga kitambaa cheusi ambacho si rahisi kwa mzee huyu kuweza kuniona. Nikamtazama mzee huyu na wazo la kuweza kumchafua mzee Poul Mkumbo taratibu likaanza kunijaa kichwani mwangu na nikaona muda huu ndio mzuri wa kuweza kutekeleza kile nilicho kikusudia kukifanya.
ENDELEA
“Simu yako ina rekodi vizuri?”
Nilizungumza kwa kumnong’oneza Roman.
“Ndio mkuu”
“Nipatie”
Roman akatoa simu yake, nikamuomaba aniwekee upende wa kamera na akafanya hivyo.
“Ulinimpiga?”
“Kiasi kidogo ila kwa sasa amepoteza fahamu ila kama unahitaji nimuamshe basi ninaweza kufanya hivyo.”
“Fanya hivyo”
Roman akachukau wanya mrefu wa umeme ambao umekatwa kwa mbele. Akachukua ndoo ya maji ya baridi.
“Kabla ya kumuasha, hakikisha kwamba anajibu maswali haya”
Nikayaandika maswali hayo kwenye simu yangu na kumkabidi Roman. Taratibu akaanza kusoma swali moja baada ya jengine. Akatingisha kichwa akimaanisha kwamba ameelewa. Alipo hakikisha kwamba kila kitu alicho kihitaji kipo vizuri akafunika uso wake na ni ngumu sana kwa mtu kuweza kumtambua. Akamwagia maji mzee huyu na kumfanya aanze kujitishisha tingine. Akamfungua kitambaa chake usoni.
“Ohoo nipo wapi, eheee?”
Mzee huyu alizungumza kwa kukoroma. Roman akachukua waya huu wa umeme, akamgusisha mzee huyu eneo la kifuani na kumfanya atetemeshwe sana huku akipiga kelele za maumivu.
“Kwa nini unahitaji boksi jeusi?”
“Pumbavu wewe unahisi nitazungumza”
Roman akamgandamiza kwa nguvu mzee huyu waya huo wa umeme na kumfanya azidi kupiga kelele kwa maumivu makali sana.
“Nani kakutuma?”
Roman alizungumza kwa sauti nzito na iliyo jaa mikwaruzo mingi, tofauti kabisa na sauti anayo itumia katika kuzungumza. Kazi yangu kubwa ni kuendelea kurekodi kila tukio. Roman alio ona mzee huyu ni mbisha sana akamvua boksa yake na kichana na akabaki kama alivyo zaliwa. Roman akabadika waya huu wa umeme kwenye ume wa huyu mzee na kumfanya alie kama mtoto mdogo kwani shoti anayo ipata hapo sio ndogo kwa kweli.
“Nas…em…a”
Mzee huyu uzalendo ulimshinda kwani huku ni kwenda kupoteza uwanaume wake.
“Ni nai?”
“Ni….ni.ni…mimi mwenyewe. Nilihitaji kulipata hilo boksi kwa manufaa yangu mimi.”
Roman akanitazama, nikampa ishara yakuendelea kumuuliza maswali.
“Kwahiyo wewe ni msaliti?”
“Hahaaaa….haa…haa…hahaa….pana”
Nikampa ishara Roman ya kupiga shoti nyingine mzee huyu. Akatii amri yangu na kuendelea kumpiga shoti mzee huyu aliye endelea kulia kwa uchungu sana ila hakuna mtu wa kuweza kumsaidia.
“Ni mipango gani ya chama chako”
“Najua wewe ni mtu wa Mkumbo, ila sinto kwenda kukueleza kitu cha aina yoyote kwangu juu ya chama changu ninacho kipigania usiku na mchana”
Hapa ndipo nilipo kuwa nina pahitaji. Roman akaendelea kumpa mateso makali mzee huyu, ila kila mateso yanavyo zidi kuendelea ndivyo jinsi anavyo mtaja bwana Mkumbo kwamba hata akimuua basi hato weza kushinda kiti cha uraisi. Hali iliyo kuwa mbaya zaidi kwa mzee huyu, nikamuamuru Roman ampige risasi mzee huyu na kummalizia kabisa.
Romani akampiga risasi za kichwa, kisha akamfungua katika eneo alilo mfunga. Akachukua dungu la mafuta ya petroli na kuumwagika mwili huu kisha akaanza kumwaga mafuta yaka katika chumba hichi kisha tukatoka nje. Akatupia njiti ya kiberiti ndani ya chumba hicho na kukifanya kianze kuwaka moto huku mwili wa mzee huyo ukiwemo ndani. Tukatoka ndani ya godauni hili tukaingia ndani ya gari la kuianza safari ya kuondoka eneo hili kwa kasi pasipo mtu yoyote kutuona.
“Bosi video umeipata vizuri?”
“Yaaa”
Nilizungumza huku nikiifungua video hiyo, nikaanza kuitazama na kila jambo limekwenda kama vile nilivyo kuwa nimepanga.
“Kuna ushahidi mzuri mwengine ambao unaweza kumuweka Mkumbo katika hali mbaya”
“Ushahidi gani?”
Roman akatoa simu nyingine na kuniwekea mazungumzo ambayo kwa kuyasikiliza vizuri ni mazungumzo ya mzee huyu tuliye muua na mzee Poul Mkumbo.
“Wewe mwana haramu unasambaza chuki juu ya wafuasi wangu si ndio”
Nilisiikia sauti ya baba yangu mkwe, mzee Poul Mkumbo akifoka sana.
“Huna jipya mzee wewe. Wewe na chama chako jiandaeni kuangukia pua uchaguzi huu”
“Hahaaa….hata kwa kuiba kura ni lazima nishinde uchaguzi huo”
“Nchi ya miaka ileee sio ya sasa. Sasa wewe jidanganye tu na utaona cha mtema kuni mukifanya ujinga wenu”
“Eti eheee?”
“Ndio maana yake. Dalili ya mvua ni mawingu Mkumbo”
“Pumbavu wewe nitaakikisha nina muua mmoja baada ya mwengine shenzi nyinyi. Tena wewe uanjidai afisa mwenezi wa chama chako. Nitakwenda kukuchoma moto huo mwili wako”
“Hahaaa jaribu uone. Nimejipanga mzee, na tena usinitishe kwa maana wewe bado kwangu ni mtoto mdogo sana.”
“Leo huimalizi”
“Hahaaa, utaona”
Mazungumzo hayo yakaishia hapa na kujikuta nikumtazama Roman usoni mwake ambaye analiendesha gari hili kwa mwendo wa kasi sana.
“Umeyapatia wapi?”
“Niliweza ku hack system za simu zote za mzee Poul Mkumbo ili niweze kujua mpango wake. Bahati nzuri alicho kizungumza ndicho nilicho kifanya. Nilianda kila kitu alicho kizungumza na nilimteka mzee huyu kabla ya watu wake kuweza kufanikisha mpango wao kwa maana leo alikuwa anatekwa kweli na kwenda kuuwawa”
“Kazi nzuri sana Roman. Sasa hii video inabidi tuiachie kwenye mitandao ya kijamii?”
“Kwa sasa bado mapema mkuu na ni watu wengi sana wanaweza kuitafuta hiyo accont na kidogo italeta msako makali sana na kumbuka kwamba mataifa makubwa duniani yana tazama huu uchaguzi hivyo wanaweza kuleta wapelelezi wao na itapelekea kukamatawa kwetu”
“Unashaurije sasa kwa maana mimi kwenye mambo hayo ya kiusalama. Sina ninalo lijua sana”
“Nitakuonyesha nini cha kufanya mkuu”
“Sawa”
Tukafika hotelini na Roman akaniacha kisha yeye akendelea na safari yake huku akiwa na simu yake niliyo rekodia tukio hilo. Nikaingia chumbani kwangu huku nikiwa na mawazo mengi sana kichwani mwangu kwani hili tukio la leo ni la kikatili sana kwa mimi kuweza kulishuhudia kwenye maisha yangu. Sikupata usingizi hadi kuna pambazuka. Nikajiandaa na kuelekea kazini kwangu guku nikikodi bajaji, nikashuka kwenye bajaji na kumlipa dereva huyu na kila mfanyakazi aliye niona nimo kwenye bajaji hii hakusita kunishangaa na wengine walitamani hata kuniuliza.
“Mbona unshangaa sana”
“Mkurugenzi imekuwaje umepanda bajaji?”
Kijana mmoja mchangamfu aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.
“Foleni kubwa barabarani, ndio maana nimepanda bajaji”
“Ahaa sawa mkurugenzi, sisi tukahisi labda kuna tatizo”
“Hakuna, kazi njema”
“Nawe pia mkurugenzi”
Nikaelekea ofisini kwangu. Baada ya kama dakika kumi hivi Biyanka akaingia ofisini kwangu huku akiwa amevaa na kupendeza sana. Japo mimi na Biyanka tuna matatizo binafsi ila kusema kweli ni mwanamke mmoja mzuri sana na aliye jaliwa uzuri wa aina yake. Kwa takribani dakika tano nikabaki nikiwa nimeduwaa nikimtazama.
“Ethan, Ethan”
“Na..anaaammm”
“Mbona nina kuita dakika zote hizo. Hunisikii mpenzi wangu”
“No umependeza”
Nilijikuta nikiropoka maneno hayo na kumfanya Biyanka atabasamu kidogo huku akinitazama usoni mwangu. Taratibu akanisogelea na kuniinamia hapa kwenye kiti changu nilicho kikalia, kwa macho yaliyo mlegea, akazikutanisha lipsi zake na zangu na taratibu akaanza kuninyonya midomo yangu na kuufanya mwili wangu kusisimka sana.
Nikapitisha mkono wangu wa kulia kiunoni mwake, kiganja changu taratibu kikaanza kukitomasa tomasa kiuno chake na baadae uzalendo ukanishinda na kujikuta tukipeana haki yetu.
“Ohooo asante mume wangu”
Biyanka alizu gumza huku akinigeukia na kakanikumbatia kwa nguvu.
“Asante nawe pi”
Nilizungumza huku nikihema. Taratibu tukaachinaa na Biyanka huku kila mtu akivaa nguo zake.
“Vipi mkutano wa jana?”
Nilimuuliza Biyanka huku nikiufunga mkanda wa suruali yangu vizuri.
“Umekwenda poa sana. Watu walijitokeza wengi sana”
“Ohoo safi”
Nimemueleza baba na mama kwamba umerudi. Wamefurahi kusikia kwamba umerudi na wameniomba nikuambia kwenye mkutano mwengine wa kesho wanaomba tuongozane wote Dodoma.
“Dodoma!!?”
“Ndio mume wangu. Kidogo nawe ukatembee tembee nchini ukaione nchi”
“Mmmm sawa na wewe si unakwenda?”
“Ndio nitakwenda”
“Poa utaniandalia mazingira”
“Usijali mume wangu ninakupenda sana na kama huto jali twende ukulele kwangu leo kwa maana tutaondoka asubuhi sana”
“Sawa”
Biyanka akanibusu kwa furaha, kisha akajiweka sawa shati lake alilo livaa na kutoka ndani humu na kuniacha peke yangu. Nikaokota mafaili yaliyo anguka na nikaendelea na majukumu yanug ya kiofisi. Nikawajulisha Qeen, Latifa na Roman juu ya safari yangu ya kesho wote wakakubaliana na jambo hilo.
“Mkuu utahitaji ulinzi wangu?”
“Ndio ila uwe wa pembeni sana. Isitokee mtu akafahamu juu ya uwepo wako”
“Sawa mkuu”
Muda wa mchana tukaondoka ofisini hapa na Biyana na kuelekea nyumbani kwake kwa ajili ya kijiandaa na safari ya kesho. Biyanka akaniomba msamaha kwa yale yote yaliyo jitokeza.
“Nimekusamehe mke wangu”
“Nashukuru sana mume wangu. Nakuapia na kukuhakikishia kwamba sinto rudia tena kuenenda kinyume na wewe mume wangu”
“Nimekuelewa”
Siku iliyo fwata alfajiri na mapema tukaanza safari ya kuelekea katika mkoa wa Dodoma huku gari letu nalo likiwa miongoni mwa magari ya msafara wa mgombea uraisi wa chama tawala. Sikuona ajabu ya mimi kuvaa tisheti ya sare ya chama hichi cha baba mkwe pasipo wao kujua kwamba mimi ndio adui yao namba moja ninaye wapiga kimya kimya. Tukafika kwenye moja ya mji na wananchi wakasimamisha msafara huu.
“Hapa ni wapi baby?”
“Chalinze”
Mzee Poul Mkumbo akahutubia watu wa haba walio kusanyika kumsikiliza na baada ya hapo tukaendelea na msafara huu. Kuna baadhi ya miji miwili wananchi nao walijitokeza kumzuia mzee Poul Mkumbo na walipo ridhika kwa sera za mgombea huyu tukaendelea na safari. Majira ya saa sita mchana tukafika katika mji wa Dodoma na kupokelewa kwa shangwe kubwa sana huku mabango mengi barabarani yakiwa yamebandikwa sura ya mzee Poul Mkumbo.
“Baba mkwe ana wafuasi ehee?
Nilimuambia Biyanka huku nikiwatazama wamama walio valia sare za chama hichi jinsi walivyo kusanyika barabarani.
“Ndio mume wangu”
Tukafika katika moja ya hoteli tukapata chakula cha mchana na baada ya hapo tukaelekea katika uwanja mkubwa wa mpira ambapo nikakuta watu wengi sana wakiwa wamekusanyika hadi wakaanza kunitisha kwani sidhani kama wapinzani wana watu wengi kiasi hichi. Burudani mbalimbali zikaanza kutolewa kisha wakaongea viongozi baadhi wa chama hichi huku wakimnadi mgombea huyu. Ukafika muda na wakati wa bwana mkumbo kuzungumza. Taratibu Biyanka akanishika mkono wangu wa kulia huku tukiwa tumekaa kwenye viti vya hili jukwaa kuaa.
“Dodomaaa Hoyeeeeeeeeeeeeee”
Watu wote wakaitikia kwa shangwe sana. Gafla spika za eneo hili zikaanza kusikika mazungumzo ya bwana mkumbo na mzee tuliye muua jana usiku jambo lililo tufanya sisi sote kushangaa kwani sikutarajia kama Roman anaweza kumwaga mchele kwenye kuku wengi namna hii.
==>>ITAENDELEA KESHO