Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Super Mkongo: Kiboko ya Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- uume kusimama kwa kulegea
- uume kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Pia kuna MCONGO POWER Kiboko ya uume mdogo inaboresha maumbile ya uume kwa kurefusha na kunenepesha kwa saizi uipendayo haijalishi umri hata kwa walioathirika na upigaji punyeto.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume na uume mdogo.
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________
Kwanini uhangaike? Kwanini uhuzunike?
Hii ni spesho kwa waliotumia madawa mengi bila kufanikiwa hakika hautajuta kuitumia. _______________________________
WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia
_______________________________
********************************

Nkoma: Tiba Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
NKOMA
_________________________
NKOMA Ni dawa bora ya nguvu za kiume  yenye mchanganyiko wa mitishamba (7) yenye maajabu yafuatayo/

🔖 (1) inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimalisha misuli ya uume uliolengea wakati wa tendo la ndoa/
🔖 (2) Kurefusha maumbile ya kiume yaliyorudi ndani kuazia nchi 5 - 9/
🔖 (3) kunenepesha uume cm 5 ya upana itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 - 20 kwa tendo la kwanza na utakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya 2-4 bila hamu kuisha/

📌 Na inatibu kabisa, unashauriwa uitumie dawa hii kama kinga ya magonjwa sugu./
 📌 Haijalishi umri hata kama una miaka 85 itumie huanza kufanya kazi dk 50 tu na haina madhara yoyote kwa mtumiaji/

📍📍📍📍📍📍📍📍📍
            MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA.
_________________________
🔖 (1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖 (2)Choo kama cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(4)Kaswende/
🔖(5)Gono/

📌Haya yote husababisha kuishiwa nguvu za kiume na kuwa na uume mdogo/
📌 Itumie leo, bado hujachelewa ni tofauti na nyingine.
_________________________
DR MAKOBA ANAPATIKANA DAR ES SALAAM, PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
___________________________
WASILIANA NA
Dr MAKOBA SIMU.
📞0754832349
📞0683490600
____________________________
*****************************

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 67

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   
       
Tukaingia kwenye godauni hili lenye ukimya huku kofia yangu nyeusi nikiwa naimeivaa vizuri kichwani mwangu na kuficha kabisa sura yangu. Kwa mavazi haya meusi niliyo yavaa si rahisi kwa mtu kuweza kunitambua kwamba ni mimi.

 Tukaingia katika chumba ambacho amemning’iniza mzee huyu kichwa chini miguu juu huku akiwa amemvua nguo zote na kumbakisha na boksa tu na usoni mwake amemfunga kitambaa cheusi ambacho si rahisi kwa mzee huyu kuweza kuniona. Nikamtazama mzee huyu na wazo la kuweza kumchafua mzee Poul Mkumbo taratibu likaanza kunijaa kichwani mwangu na nikaona muda huu ndio mzuri wa kuweza kutekeleza kile nilicho kikusudia kukifanya.
                                                                                                      
ENDELEA
“Simu yako ina rekodi vizuri?”
Nilizungumza kwa kumnong’oneza Roman.
“Ndio mkuu”
“Nipatie”
Roman akatoa simu yake, nikamuomaba aniwekee upende wa kamera na akafanya hivyo.
“Ulinimpiga?”
“Kiasi kidogo ila kwa sasa amepoteza fahamu ila kama unahitaji nimuamshe basi ninaweza kufanya hivyo.”
“Fanya hivyo”
Roman akachukau wanya mrefu wa umeme ambao umekatwa kwa mbele. Akachukua ndoo ya maji ya baridi.
“Kabla ya kumuasha, hakikisha kwamba anajibu maswali haya”
 
Nikayaandika maswali hayo kwenye simu yangu na kumkabidi Roman. Taratibu akaanza kusoma swali moja baada ya jengine. Akatingisha kichwa akimaanisha kwamba ameelewa. Alipo hakikisha kwamba kila kitu alicho kihitaji kipo vizuri akafunika uso wake na ni ngumu sana kwa mtu kuweza kumtambua. Akamwagia maji mzee huyu na kumfanya aanze kujitishisha tingine. Akamfungua kitambaa chake usoni.
“Ohoo nipo wapi, eheee?”
Mzee huyu alizungumza kwa kukoroma. Roman akachukua waya huu wa umeme, akamgusisha mzee huyu eneo la kifuani na kumfanya atetemeshwe sana huku akipiga kelele za maumivu.
 
“Kwa nini unahitaji boksi jeusi?”
“Pumbavu wewe unahisi nitazungumza”
Roman akamgandamiza kwa nguvu mzee huyu waya huo wa umeme na kumfanya azidi kupiga kelele kwa maumivu makali sana.
“Nani kakutuma?”
Roman alizungumza kwa sauti nzito na iliyo jaa mikwaruzo mingi, tofauti kabisa na sauti anayo itumia katika kuzungumza. Kazi yangu kubwa ni kuendelea kurekodi  kila tukio. Roman alio ona mzee huyu ni mbisha sana akamvua boksa yake na kichana na akabaki kama alivyo zaliwa. Roman akabadika waya huu wa umeme kwenye ume wa huyu mzee na kumfanya alie kama mtoto mdogo kwani shoti anayo ipata hapo sio ndogo kwa kweli. 
 
“Nas…em…a”
Mzee huyu uzalendo ulimshinda kwani huku ni kwenda kupoteza uwanaume wake.
“Ni nai?”
“Ni….ni.ni…mimi mwenyewe. Nilihitaji kulipata hilo boksi kwa manufaa yangu mimi.”
Roman akanitazama, nikampa ishara yakuendelea kumuuliza maswali.
“Kwahiyo wewe ni msaliti?”
“Hahaaaa….haa…haa…hahaa….pana”
Nikampa ishara Roman ya kupiga shoti nyingine mzee huyu. Akatii amri yangu na kuendelea kumpiga shoti mzee huyu aliye endelea kulia kwa uchungu sana ila hakuna mtu wa kuweza kumsaidia.
 
“Ni mipango gani ya chama chako”
“Najua wewe ni mtu wa Mkumbo, ila sinto kwenda kukueleza kitu cha aina yoyote kwangu juu ya chama changu ninacho kipigania usiku na mchana”
Hapa ndipo nilipo kuwa nina pahitaji. Roman akaendelea kumpa mateso makali mzee huyu, ila kila mateso yanavyo zidi kuendelea ndivyo jinsi anavyo mtaja bwana Mkumbo kwamba hata akimuua basi hato weza kushinda kiti cha uraisi. Hali iliyo kuwa mbaya zaidi kwa mzee huyu, nikamuamuru Roman ampige risasi mzee huyu na kummalizia kabisa.
 
Romani akampiga risasi za kichwa, kisha akamfungua katika eneo alilo mfunga. Akachukua dungu la mafuta ya petroli na kuumwagika mwili huu kisha akaanza kumwaga mafuta yaka katika chumba hichi kisha tukatoka nje. Akatupia njiti ya kiberiti ndani ya chumba hicho na kukifanya kianze kuwaka moto huku mwili wa mzee huyo ukiwemo ndani. Tukatoka ndani ya godauni hili tukaingia ndani ya gari la kuianza safari ya kuondoka eneo hili kwa kasi pasipo mtu yoyote kutuona.
“Bosi video umeipata vizuri?”
“Yaaa”
Nilizungumza huku nikiifungua video hiyo, nikaanza kuitazama na kila jambo limekwenda kama vile nilivyo kuwa nimepanga. 
 
“Kuna ushahidi mzuri mwengine ambao unaweza kumuweka Mkumbo katika hali mbaya”
“Ushahidi gani?”
Roman akatoa simu nyingine na kuniwekea mazungumzo ambayo kwa kuyasikiliza vizuri ni mazungumzo ya mzee huyu tuliye muua na mzee Poul Mkumbo.
“Wewe mwana haramu unasambaza chuki juu ya wafuasi wangu si ndio”
Nilisiikia sauti ya baba yangu mkwe, mzee Poul Mkumbo akifoka sana.
“Huna jipya mzee wewe. Wewe na chama chako jiandaeni kuangukia pua uchaguzi huu”
“Hahaaa….hata kwa kuiba kura ni lazima nishinde uchaguzi huo”
“Nchi ya miaka ileee sio  ya sasa. Sasa wewe jidanganye tu na utaona cha mtema kuni mukifanya ujinga wenu”
 
“Eti eheee?”
“Ndio maana yake. Dalili ya mvua ni mawingu Mkumbo”
“Pumbavu wewe nitaakikisha nina muua mmoja baada ya mwengine shenzi nyinyi. Tena wewe uanjidai afisa mwenezi wa chama chako. Nitakwenda kukuchoma moto huo mwili wako”
“Hahaaa jaribu uone. Nimejipanga mzee, na tena usinitishe kwa maana wewe bado kwangu ni mtoto mdogo sana.”
“Leo huimalizi”
“Hahaaa, utaona”
Mazungumzo hayo yakaishia hapa na kujikuta nikumtazama Roman usoni mwake ambaye analiendesha gari hili kwa mwendo wa kasi sana.
 
“Umeyapatia wapi?”
“Niliweza ku hack system za simu zote za mzee Poul Mkumbo ili niweze kujua mpango wake. Bahati nzuri alicho kizungumza ndicho nilicho kifanya. Nilianda kila kitu alicho kizungumza na nilimteka mzee huyu kabla ya watu wake kuweza kufanikisha mpango wao kwa maana leo alikuwa anatekwa kweli na kwenda kuuwawa”
“Kazi nzuri sana Roman. Sasa hii video inabidi tuiachie kwenye mitandao ya kijamii?”
“Kwa sasa bado mapema mkuu na ni watu wengi sana wanaweza kuitafuta hiyo accont na kidogo italeta msako makali sana na kumbuka kwamba mataifa makubwa duniani yana tazama huu uchaguzi hivyo wanaweza kuleta wapelelezi wao na itapelekea kukamatawa kwetu”
 
“Unashaurije sasa kwa maana mimi kwenye mambo hayo ya kiusalama. Sina ninalo lijua sana”
“Nitakuonyesha nini cha kufanya mkuu”
“Sawa”
Tukafika hotelini na Roman akaniacha kisha yeye akendelea na safari yake huku akiwa na simu yake niliyo rekodia tukio hilo. Nikaingia chumbani kwangu huku nikiwa na mawazo mengi sana kichwani mwangu kwani hili tukio la leo ni la kikatili sana kwa mimi kuweza kulishuhudia kwenye maisha yangu. Sikupata usingizi hadi kuna pambazuka. Nikajiandaa na kuelekea kazini kwangu guku nikikodi bajaji, nikashuka kwenye bajaji na kumlipa dereva huyu na kila mfanyakazi aliye niona nimo kwenye bajaji hii hakusita kunishangaa na wengine walitamani hata kuniuliza.
 
“Mbona unshangaa sana”
“Mkurugenzi imekuwaje umepanda bajaji?”
Kijana mmoja mchangamfu aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.
“Foleni kubwa barabarani, ndio maana nimepanda bajaji”
“Ahaa sawa mkurugenzi, sisi tukahisi labda kuna tatizo”
“Hakuna, kazi njema”
“Nawe pia mkurugenzi”
Nikaelekea ofisini kwangu. Baada ya kama dakika kumi hivi Biyanka akaingia ofisini kwangu huku akiwa amevaa na kupendeza sana. Japo mimi na Biyanka tuna matatizo binafsi ila kusema kweli ni mwanamke mmoja mzuri sana na aliye jaliwa uzuri wa aina yake. Kwa takribani dakika tano nikabaki nikiwa nimeduwaa nikimtazama.
 
“Ethan, Ethan”
“Na..anaaammm”
“Mbona nina kuita dakika zote hizo. Hunisikii mpenzi wangu”
“No umependeza”
Nilijikuta nikiropoka maneno hayo na kumfanya Biyanka atabasamu kidogo huku akinitazama usoni mwangu. Taratibu akanisogelea na kuniinamia hapa kwenye kiti changu nilicho kikalia, kwa macho yaliyo mlegea, akazikutanisha lipsi zake na zangu na taratibu akaanza kuninyonya midomo yangu na kuufanya mwili wangu kusisimka sana. 
 
Nikapitisha mkono wangu wa kulia kiunoni mwake, kiganja changu taratibu kikaanza kukitomasa tomasa kiuno chake na baadae uzalendo ukanishinda na kujikuta tukipeana haki yetu.
 
“Ohooo asante mume wangu”
Biyanka alizu gumza huku akinigeukia na kakanikumbatia kwa nguvu.
“Asante nawe pi”
Nilizungumza huku nikihema. Taratibu tukaachinaa na Biyanka huku kila mtu akivaa nguo zake.
 
“Vipi mkutano wa jana?”
Nilimuuliza Biyanka huku nikiufunga mkanda wa suruali yangu vizuri.
“Umekwenda poa sana. Watu walijitokeza wengi sana”
“Ohoo safi”
Nimemueleza baba na mama kwamba umerudi. Wamefurahi kusikia kwamba umerudi na wameniomba nikuambia kwenye mkutano mwengine wa kesho wanaomba tuongozane wote Dodoma.
 
“Dodoma!!?”
“Ndio mume wangu. Kidogo nawe ukatembee tembee nchini ukaione nchi”
“Mmmm sawa na wewe si unakwenda?”
“Ndio nitakwenda”
“Poa utaniandalia mazingira”
“Usijali mume wangu ninakupenda sana na kama huto jali twende ukulele kwangu leo kwa maana tutaondoka asubuhi sana”
“Sawa”
 
Biyanka akanibusu kwa furaha, kisha akajiweka sawa shati lake alilo livaa na kutoka ndani humu na kuniacha peke yangu. Nikaokota mafaili yaliyo anguka na nikaendelea na majukumu yanug ya kiofisi. Nikawajulisha Qeen, Latifa na Roman juu ya safari yangu ya kesho wote wakakubaliana na jambo hilo.
“Mkuu utahitaji ulinzi wangu?”
“Ndio ila uwe wa pembeni sana. Isitokee mtu akafahamu juu ya uwepo wako”
“Sawa mkuu”
Muda wa mchana tukaondoka ofisini hapa na Biyana na kuelekea nyumbani kwake kwa ajili ya kijiandaa na safari ya kesho. Biyanka akaniomba msamaha kwa yale yote yaliyo jitokeza.
 
“Nimekusamehe mke wangu”
“Nashukuru sana mume wangu. Nakuapia na kukuhakikishia kwamba sinto rudia tena kuenenda kinyume na wewe mume wangu”
“Nimekuelewa”
    Siku iliyo fwata alfajiri na mapema tukaanza safari ya kuelekea katika mkoa wa Dodoma huku gari letu nalo likiwa miongoni mwa magari ya msafara wa mgombea uraisi wa chama tawala. Sikuona ajabu ya mimi kuvaa tisheti ya sare ya chama hichi cha baba mkwe pasipo wao kujua kwamba mimi ndio adui yao namba moja ninaye wapiga kimya kimya. Tukafika kwenye moja ya mji na wananchi wakasimamisha msafara huu.
 
“Hapa ni wapi baby?”
“Chalinze”
Mzee Poul Mkumbo akahutubia watu wa haba walio kusanyika kumsikiliza na baada ya hapo tukaendelea na msafara huu. Kuna baadhi ya miji miwili wananchi nao walijitokeza kumzuia mzee Poul Mkumbo na walipo ridhika kwa sera za mgombea huyu tukaendelea na safari. Majira ya saa sita mchana tukafika katika mji wa Dodoma na kupokelewa kwa shangwe kubwa sana huku mabango mengi barabarani yakiwa yamebandikwa sura ya mzee Poul Mkumbo.
 
“Baba mkwe ana wafuasi ehee?
Nilimuambia Biyanka huku nikiwatazama wamama walio valia sare za chama hichi jinsi walivyo kusanyika barabarani.
“Ndio mume wangu”
Tukafika katika moja ya hoteli tukapata chakula cha mchana na baada ya hapo tukaelekea katika uwanja mkubwa wa mpira ambapo nikakuta watu wengi sana wakiwa wamekusanyika hadi wakaanza kunitisha kwani sidhani kama wapinzani wana watu wengi kiasi hichi. Burudani mbalimbali zikaanza kutolewa kisha wakaongea viongozi baadhi wa chama hichi huku wakimnadi mgombea huyu. Ukafika muda na wakati wa bwana mkumbo kuzungumza. Taratibu Biyanka akanishika mkono wangu wa kulia huku tukiwa tumekaa kwenye viti vya hili jukwaa kuaa.
 
“Dodomaaa Hoyeeeeeeeeeeeeee”
Watu wote wakaitikia kwa shangwe sana. Gafla spika za eneo hili zikaanza kusikika mazungumzo ya bwana mkumbo na mzee tuliye muua jana usiku jambo lililo tufanya sisi sote kushangaa kwani sikutarajia kama Roman anaweza kumwaga mchele kwenye kuku wengi namna hii.

==>>ITAENDELEA KESHO

Jaji Mkuu Aagiza sheria zote kuwekwa mtandaoni Ili Wananchi Wazisome na Kuzijua

$
0
0
Jaji Mkuu Profesa Ibrahimu Juma, amemtaka Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuweka sheria zote mtandaoni ili Watanzania wote wapate kuzifahamu.

Amesema hatua hiyo itawasidia Watanzania kufahamu sheria kabla ya kufungua mshahauri mahakamani na mambo mengihne yanayohusu sheria.

Jaji Mkuu amesema hayo leo Jumatano Februari 6, katika kilele cha siku ya maadhimisho ya Sheria zilizofanyikia jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais John Magufuli.

Amesema wananchi wasiwaache wanasheria wabaki peke yao, wanatakiwa kufahamu sheria hasa kwenye mirathi kabla ya kufungua shauri hilo.

“Kabla ya kuanza kesi inabidi mwananchi ahakikihse anafahamu hatua zote ambazo kesi yake itapitia.

“Huhitaji elimu ya sheria angalau kujua hatua za kuchukua katika kupata haki,” amesema Jaji Mkuu.

Pamoja na mambo mengine, amesema mfumo Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), italeta mapinduzi iwapo itashirikisha wadau na wanasheria wote.

“Mfumo wa kielektroniki wa kusajili mashauri kwa njia ya kielektroniki kwa mfano kufungua sheria benki ya kuhifadhi hukumu zinazotolewa, kurahisisha wananchi kusoma hukumu zinazotolewa, mfumo wa kusajili mawakili na mfumo wa utambuzi wa kimahakama,” amesema.

Harmonize Ajisalimisha Polisi Central Sakata la dawa za kulevya

$
0
0
Mwanamuziki Harmonize anashikiliwa kwa zaidi ya saa tano katika Kituo cha Polisi Central, jijini Dar es Salaam alipokwenda kujisalimisha akituhumiwa kuvuta bangi alipokuwa nchini Ghana .

Muimbaji huyo ameitikia wito wa RC Makonda, ambaye alimtaka akifika nchini achunguzwe kuhusiana na matumizi ya dawa za kulevya aina ya bangi baada ya kuonekana akivuta kitu chenye moshi mkubwa kinachodaiwa kuwa ni bangi.

Makonda alisema alimwagiza Gavana  wa kule amchunguze alichokuwa akivuta na kama ikithibitika kilikuwa na kilevi angemwajibisha.

Harmonize leo alijisalimisha katika kituo hicho  akiwa amejifunika kichwani kwa kuvaa sweta jeusi na miwani. Alipofika kituoni hapo alitimua mbio huku akiwafurusha waandishi waliokuwa wakijaribu kumpiga picha.

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Chalaani mauaji ya muumini Itigi

$
0
0
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimesema   kimesikitishwa na tukio la mauaji ya Peter Chambalo.

Chambalo anadaiwa kuuawa na askari wa wanyamapori wakiwa na Mkurugenzi wa Wilaya ya  Itigi mkoani Singida ndani ya Kanisa la Sabato.

Taarifa iliyotolewa jana na LHRC na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa kituo hicho, Paul Mikongoti ilieleza kwamba kitendo hicho  ni uvunjifu wa haki ya kuishi kinyume na ibara ya 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano 1977 inayoainisha haki ya kuishi kama haki ya msingi ya binadamu.

“Pia ni ukiukwaji wa ibara ya 6 ya Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Raia na Siasa, 1966 unaoainisha haki ya kuishi   na kuweka jukumu la kulinda haki hiyo katika sheria. “kila mtu ana haki ya kuishi”

“Kanuni ya utawala wa sheria inaweka sharti la kutumia utaratibu maalamu kwa mtu yeyote, uliowekwa kisheria katika kutekeleza majukumu bila kujali cheo, hadhi au nasaba ya mtu. Kitendo cha kuingia kanisani kimeingilia uhuru wa kuabudu pamoja na faragha ya kanisa hilo wakati wa kuabudu.

“Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kinalaani na kinakemea tukio hilo lililotweza utu pamoja na kuondoa haki ya kuishi ya mtu huyo.

“Kituo kinalaani tukio hilo kwani lilifanyika kwa ukatili na kutia hofu na taharuki wakazi wa eneo hilo waliokuwa wamekusanyika kwa amani wakifanya ibada siku ya Sabato,” alisema Migongoti katika taarifa hiyo

Alisema LHRC inatoa rai kwa viongozi na watendaji wa Serikali kuzingatia misingi ya Katiba na sheria zilizopo katika kutekeleza majukumu yao.

Kaimu Mkurugenzi huyo alisema wanafutiliwa kwa  karibu tukio hilo na kinatoa wito kwa vyombo vya dola kuendelea kuchunguza na kuwachukulia hatua stahiki wale wote wanatuhumiwa kwa mauaji haya.

Kituo pia kinatoa wito kwa uongozi wa Mkoa wa Singida na Wilaya ya Ikungi kuwahakikishia wananchi wa Itigi usalama wa maisha na mali zao na na kuhakikisha haki ya kuishi inalindwa kwa mujibu wa sheria za nchi.

Ondoa Kibamia Na Tibu tatizo la Nguvu Za Kiume Kwa Dawa Hii Ya Mitishamba

$
0
0
JILO HERBAL CLINIC

ONDOA KIBAMIA NA ONGEZA NGUVU ZA KIUME KWA DAWA HII YA MITISHAMBA AMBAYO NI KOMESHA KWA TATIZO SUGU LA NGUVU ZA KIUME

SUPER MBONGOSHI; Ni dawa ya mitishamba ambayo inatibu tatizo la nguvu za kiume inakufanya kuchelewa kufika kileleni na kuongeza hamu ya kuendelea kufanya tendo.
 
SUPER MBONGOSHI2 Ni dawa ya mitishamba ambayo ina nenepesha na kurefusha maumbile mafupi au yaliyosinyaa na kuufanya kuwa imara dawa hii inasafisha mishipa ya Uume ambayo imedhurika na matatizo mbali mbali kama vile kupiga punyeto kwa mda mrefu,ngiri,kisukari,vidonda vya tumbo na mengine mengi.
 
DR.JILO Pia anatibu magonjwa mengine kama vile kisukari,ngiri,ugumba,pressure n.k

KWA HUDUMA ZA JILO HERBAL CLINIC WASILIANA NA DR.JILO SASA UPATE DAWA HII .UTATUMIWA POPOTE PALE ULIPO PIGA SIMU
0752723508

Je Kwanini Baadhi Ya Wanaume Wengi Wana Ukosefu Ama Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
JE KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UKOSEFU AMA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO ???

Pata sululisho la matatizo haya na  magonjwa mengine utapona kwa mda mfupi sana hatakama ulihangaika mpaka ukakata tamaaa 

GALIMBO 3 MIX  ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa aina mbili ili kukidhi mahitaji ya mtumiaji, imetengenezwa kwa muundo wa vidonge pamoja na unga kwaajili ya kuponesha tatizo moja kwa moja , huimalisha misuli ya uume iliyolegea wakato wa tendo la mdoa ,na kukufanya ucherewe kufika kileleni kwa mda wa dk ( 20 - 45 ) itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu nira hamu kuisha wara kuhisi kuchoka vilivile huzalisha viini vya uzazi ( manii ) 

YOLAN  hurefusha na kunenepesha  maumbile madogo ya uume na kuwa na uume kuanzia nchi (6-8) tiba kwa mda mfupi sana

Zipo sananu nyingi sana zinazosababisha matatizo hayo  km vile -:punyeto, kisukali,ngili,chango,vidonda vya tumbo,  tumbo kuunguluma na kujaa gesi maumivu ya mgongo ama kiume ,kolodani moja kuvimba ama kuingia ndani  presha nk 

Matatizo haya yote sio mageni, kigeni ni tiba sahihi ya kuponesha matatizo hayo

SUPER MBUKE -:  nidawa ya kuponesha tatizo la kisukali kwa mda mfupi sana , usihangaike wara kuteseka tumia dawa ya mitishamba kwaajili ya tatizo hili na upone kabisa

NTINJIWA  nidawa ya mvuto wa biashara,kazi, kupandishwa cheo,kumfanya mfanyakazi apendwe na bos wake

Pia ninadawa za kumvuta mme , mke,mchumba,hawara, au mtu yoyote unaemuhitaji katika maisha yako hata km yupo mbali na atatulia na kukutimizia cjovjote utakacho na kumfunga asiwe na mtu mwingime ,

Pata tiba za magonjwa mbalimbali ikiwemo miguu kuwaka moto, mgongo,bawasili ,kaswende ,gono na mengine mengi

KWAUSHAULI NA TIBA WASILIANA NA DR CHIKAGO    0759 208 637

Km huna nafasi ya kufika ofisini hudumahii utaletewa hapo ulipo , kwa wale wa mikoani natuma kwanjia ya basi

Naibu Waziri wa Fedha: Utaratibu Ufuatwe Ili Kufungua Kituo Cha Forodha Manda

$
0
0
Na. Saidina Msangi, WFM, Dodoma
Serikali imemtaka Mbunge wa Ludewa kushirikiana na uongozi wa mkoa wa Njombe kuandaa andiko la kuwasilisha Serikalini katika hatua ya kufungua Kituo kipya cha forodha katika bandari ya Manda iliyopo katika Ziwa Nyasa.

Maelekezo hayo yametolewa na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji, Bungeni Jijini Dodoma, wakati akijibu swali la msingi la Mbunge wa Ludewa Mhe. Deogratias Ngalawa, aliyetaka kujua ni lini Serikali itaanzisha Kituo cha Forodha katika bandari ya Manda, ili kurahisisha huduma kwa wananchi wanaokwenda nchi jirani hasa kwa shughuli za biashara.

Dkt. Kijaji alisema kuwa, utaratibu wa kufungua kituo kipya cha forodha unatakiwa kuzingatia Sheria ya Forodha ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Mwaka 2004, ambayo inaitaka nchi mwanachama kuwasilisha kwenye Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki maombi ya idhini ya kuanzisha kituo kipya cha forodha na hatimaye kutangazwa kwenye gazeti la Jumuiya ya Afrika Mashariki ili kupata nguvu ya kisheria.

“Mchakato wa ndani wa kuwasilisha maombi ya kufungua kituo kipya cha forodha unaanza katika ngazi ya mkoa ambapo mkoa unatakiwa kuwasilisha maombi ya kufungua kituo kipya cha forodha katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki”, alisema Dkt. Kijaji.

Alisema kuwa baada ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kujiridhisha itamfahamisha Kamishna Mkuu Mamlaka ya Mapato Tanzania ili kufanyia kazi maombi husika kwa kuzingatia sheria ya forodha ya afrika ya mashariki na hatimaye kuwasilisha maombi hayo kwenye sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mwisho.

Serikali Yatoa Rai Kwa Waendesha Bodaboda Kote Nchini Kujiunga Katika Vikundi Ili Kupatiwa Mikopo

$
0
0
Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
 Serikali  imetoa rai kwa waendesha bodaboda kote nchini kujiunga katika vikundi hali itakayowawezesha kutambulika vizuri na kupatiwa mikopo.

Rai hiyo imetolewa leo Februari 6 Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu,Ajira na vijana ,Antony Mavunde wakati akijibu swali la mbunge wa Lushoto Shaban Shekilindi aliyehoji kwa kuwa bodaboda imetoa ajira kwa vijana wengi,kuna mpango gani wa serikali kuwawezesha  mikopo vijana wa bodaboda.

Naibu waziri Mavunde amesema serikali inashirikiana na serikali za mitaa ili vijana kujiunga katika vikundi na kutengeneza katiba ya vikundi husika  ili waweze kupatiwa mikopo na amesisitiza kuwa serikali hutoa mikopo kama vikundi vya bodaboda vitaonesha utayari huo

Mbunge wa viti maalum  [CHADEMA]Suzan Lyimo  naye amehoji licha ya bodaboda kutambuliwa kama kazi maalum kwanini serikali imekuwa ikiwakataza kufanya shughuli katika miji yenye misongamano mikubwa ya watu hususan katikati ya jiji la Dar  es Salaam na   eneo la chuo kikuu cha Dar  es Salaam.

Katika majibu yake Mhe.Mavunde amesema kuwa suala la kuwazuia bodaboda  lilikuwa ni suala la kiusalama  na msongamano lakini serikali inafanya namna ya kuwasaidia hususan kwa kutambua vituo rasmi vya maegesho.

Katika Bunge la 11 ,mkutano  wa 14 kikao cha 8 ,Jumla ya Maswali 16 yameulizwa pamoja na hati mbili za taarifa kuwasilishwa bungeni ambazo ni taarifa ya kamati ya Nishati na Madini  ya mwaka 2018/2019 na taarifa ya kamati ya mambo ya nje ,ulinzi na Usalama ya mwaka 2018/2019.

Kuwa tajiri kwa mtaji wa laki 2 na Nusu tu kupitia ufugaji wa kuku wa kienyeji. Tazama Hapa

$
0
0
Mpendwa msomaji wetu, yawezekana umekuwa ukiwaza sana nini ufanye ili uweze kufanikiwa na kuondokana na adha za umaskini.  Kulalamika tu vyuma vimekaza haitakusaidia kitu kama hutaki kujiongeza ili uongeze kipato chako.

Yako mambo mengi ya kufanya ili kujikwamua kiuchumi. Usitegemee mshahara wako tu. Mimi nataka kukufungua macho kwa jambo moja tu tena kwa uchache. Jambo hili anaweza kulifanya mwenye mtaji mkubwa au mdogo.
 
Somo  ni dogo tu lakini naamini wapo watakaopata mafanikio makubwa sana.
 
Unaweza kuanza kwa mtaji wa Mil.1 mpaka laki tano au hata chini ya hapo.

==>>Mfano. Unaweza kutumia Tsh 250,000 kununua kuku 25 kwa bei ya Tsh 10,000 kwa kuku mmoja (kadirio la juu) Majogoo watakuwa 5 kwa uwiano wa 1:4.

Hii ina maana kuwa wakishaanza kutaga utakuwa na

vifaranga 20 x 10 = 200Watunze vizuri.

Wale vifaranga tunakadiria kuwa majike watakuwa 150 ambao ndani ya miezi 3 au zaidi nao wataanza kutaga.

Utakuwa na kuku 200 + 25( ulioanza nao) =225 ndani ya miezi 6. Miezi 6 inayofuata 225 - (majogoo 55) = 170 Hii ina maana kuwa 170 x 10= 1,700.

Ndugu msomaji, hayo niliyotoa ni makadirio ya chini sana hivyo mpaka mwisho wa mwaka utakuwa na kuku zaidi ya 2000. 

Mwaka utakaofuata utakuwa na kuku wangapi baada ya kuuza kuku baadhi  ili upate fedha ya kuwalisha ????

Ukiuza kuku 1000, utabaki na kuku 1000, kati yao tuseme majike ni 750. Ndani ya Miaka 2 maanake ni  750(majike) x 10 = kuku 7500 (uza wengine upate pesa ya kutumia kuwalisha) . 

Tuseme sasa utabakiwa na kuku jike  3000 x 10( jike moja ni mayai 10) = kuku 30,000. 

Hao kuku 30,000  ukiwauza wote utapata; 30,000x 13000( bei ya kawaida kbsa)= 390,000,000. Je, bado utakuwa masikini? Bado vyuma vitakuwa vimekaza?

Nina uhakika, mpaka mwisho wa mwaka huo wa pili utakuwa umefanikiwa sana kuukimbia UMASIKINI.

Kwenye hayo mamilioni, hata ukitoa milioni 100 kwamba  tuseme ndo zimetuka kuendeshea mradi wako, bado utakuwa ni milionea tu. Kumbuka huu ni mwongozo tu, fanya utafiti na ufuatilie zaidi.

NB: Ukiyapata hayo mamilioni ya pesa, kumbuka kutoa Zaka, sadaka na kusaidia masikini wasiojiweza ili ubarikiwe zaidi 


Taarifa Kwa Umma Kuhusu Uteuzi Wa Wajumbe Wa Bodi Ya Wakurugenzi Wa Shirika La Kuhudumiaviwanda Vidogo (SIDO)

$
0
0
Kufuatia Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kumteua Prof. Elifas Tozo Bisanda kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya SIDO, Mheshimiwa Joseph George Kakunda (Mb), Waziri wa Viwanda na Biashara, kwa Mamlaka aliyopewa kwa mujibu wa Ibara ya 1(b) ya Jedwali la Sheria ya SIDO ya mwaka 1973, amewateua Wajumbe sita (6) wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO). 

Wajumbe hao walioteuliwa ni:-
  1. Bw. Maduka Paul Kessy (Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma);
  2.  Prof. Bashira Alli Majaja (Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam);
  3.  Bi. Seraphia Robert Mgembe (Mratibu wa MKURABITA);
  4. Mhandisi Peter Daud Chisawilo (Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya Intermech Engineering Ltd na Mhandisi Mkuu Mstaafu wa Shirika la Mzinga);
  5. Bw. John Mihayo Cheyo (Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Ofisi ya Rais TAMISEMI); na
  6.  Mhandisi Gilman Kasiga (Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa Kampuni ya Kimataifa ya General Electric – GE).
Uteuzi huu ni wa miaka mitatu (3) kuanzia tarehe 3 Februari 2019.

Kauli ya Serikali kuhusu Mauaji na Utekaji wa Watoto Mkoani Njombe

$
0
0
Serikali imesema si vyema kuhusisha mauaji ya watoto yaliyojitokeza mkoani Njombe na itikadi za aina yoyote au shughuli za uzalishaji mali na biashara kwani kwa kufanya hivyo inaweza kuwahusisha wasiohusika.
Hayo yamesemwa leo Jumatano Februari 6, 2019 bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola wakati akitoa kauli za mawaziri.

Kauli hiyo ilikuja baada ya mbunge wa Lupembe (CCM), Joram Hongoli kuomba Bunge liahirishwe  Februari 4, 2019 ili wabunge waweze kujadili mauaji yanayoendelea mkoani Njombe.

Amesema watu 29 waliokamatwa ni wananchi wa kawaida usioweza kuwanasibisha na udini, siasa au biashara.

“Nashauri tutulie wakati Serikali kupitia wizara yangu tunaendelea kufuatilia na kudhibiti hali hii,” amesema.

Lugola amesema Serikali itawakamata wote waliosambaza taarifa za kuzua taharuki mitandaoni na kuwafikisha mahakamani ili wakajifunze kutumia uhuru wao wa kujieleza vizuri.

Pia amewaasa Watanzania kuacha kuanzisha na kusambaza taarifa za uzushi kwa nia yoyote  kwenye mitandao.

Serikali Yasema Haijanunua Kahawa kwa Wakulima Kama Ilivyonunua Korosho

$
0
0
Naibu Waziri wa Kilimo, Omary Mgumba amesema kuwa Serikali haijanunua kahawa kutoka kwa wakulima kama ilivyo katika korosho.

Mgumba alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Kuteuliwa (CCM) Abdallah Bulembo bungeni leo, Alhamisi Februari 6 mwaka 2019.

“Wakulima wana shida, kahawa yao iko katika maghala hawajalipwa hadi leo. Kwa nini Serikali isifanye kama ilivyofanya katika korosho?” Amehoji Bulembo.

Akijibu swali hilo, Mgumba amesema Serikali haijanunua kahawa ya wakulima na kwamba wakulima waliamua wenyewe kupitia vyama vyao vya ushirika kuuza kahawa yao mnadani Moshi.

Amesema kutokana na kuyumba kwa soko la dunia na kuongezeka kwa uzalishaji bei ya zao hilo imepungua.


Taarifa Kwa Umma Kuhusu Maadhimisho Ya Siku Ya Kimataifa Ya Kupinga Ukeketaji Duniani

$
0
0
Maadhimisho ya kupinga ukeketaji kwa wanawake na watoto uadhimishwa kila ifikapo tarehe 6 Februari kila mwaka. Historia ya siku hii ilianza mwaka 2003 Jijini Adis Ababa Ethiopia kwenye mkutano wa kimataifa ambao ulitoa tamko la kutenga siku maalum ya kikomo cha uvumilivu kwa ukeketaji wa wanawake na watoto wa kike.

Baraza la Umoja wa Mataifa lilifikia uamuzi huu baada ya kutathimini na kuona athari kubwa zitokanazo na vitendo vya ukeketaji kwa mtoto wa kike. Madhumuni ya maadhimisho haya ni kupinga ukeketaji ambao ni kitendo cha kikatili na kinyume na sheria lakini pia kinyume na  haki za binadamu.Tanzania kama nchi mwanachama wa umoja huo inaungana na nchi nyingine duniani kuadhimisha siku hii ya kupinga ukeketaji.

Pamoja na jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali, Mashirika na Taasisi mbalimbali bado ukeketaji umeendelea kutekelezwa katika baadhi ya jamii hapa nchini.

Kwa mujibu wa Takwimu za Taarifa ya Demographia na Afya ya 2015/16 zinaonyesha kuwa pamoja na jitihada za kutokomeza vitendo hivyo, bado kuna mikoa mitano inayoongoza kwa ukeketaji nchini ikiongozwa na Manyara wenye asilimia (58) ukifuatiwa na Dodoma (47), Arusha (41), Mara (32) na Singida yenye asilimia (31),Tanga( 14), kilimanajaro (10), Mororgoro (9), Iringa (8) na Njombe (7).

Ziko sababu nyingi zinazosababisha, kuendelea kwa ukeketaji moja kati ya hizo ni usiri mkubwa uliopo katika jamii husika. Jamii kwa kuamini kuwa kukeketa ni mila na desturi zao, wameendelea kuhifadhi na kutunza siri za wale wanaoendeleza vitendo hivyo, ili kuwaepusha wahusika na mkono wa dola. Hali hii hupelekea watoto wa kike na wanawake kuendelea kunyanyasika bila msaada.

Mwaka huu wa 2019 maadhimisho haya ya siku ya kupinga ukeketaji yanafanyika katika mikoa yote Tanzania kulingana na mazingira husika Kauli mbiu ya mwaka huu ni: Acha mila zenye madhara: tokomeza ukeketaji”.

Kauli mbiu hii imezingatia Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030 inayolenga kuondoa umaskini, kukuza mafanikio ya kiuchumi, maendeleo ya kijamii na ustawi wa watu.

Aidha kauli mbiu hii imejikita zaidi katika lengo namba 5 linalosisitiza suala la kutokomeza ukatili na ubaguzi dhidi ya wanawake na wasichana. Katika utekelezaji wa Malengo ya maendeleo Endelevu jamii ina wajibu wa kulinda haki na utu wa mwanamke kwa kupinga ukatili  na vitendo vyovyote vinavyodhalilisha utu wa mwanamke na mtoto wa kike.

Yapo madhara mengi yanayosababishwa na ukeketaji; madhara hayo yanaweza kuwa ya kiafya au hata kisaikolojia. Madhara yanayosababishwa na ukeketaji yanaweza kuwa ya papo kwa papo kama maumivu makali wakati wa ukeketaji, mshtuko, homa kali, kumwaga damu nyingi na mara nyingine hata kupelekea kifo, kuambukizwa magonjwa kama Virusi Vya UKIMWI na msongo wa mawazo. Yapo pia madhara ya muda mrefu kama vile; kuathirika kisaikolojia, ulemavu/kovu la kudumu katika uke, fistula, kupata shida wakati wa kujifungua na muda mwingine kupelekea kupata ugumba.

Wizara naiomba jamii kuhakikisha inashiriki kikamilifu katika utoaji taarifa wa matukio ya ukeketaji yanayofanywa katika maeneo yenu lakini pia familia hasa wazazi/walezi kuwa mstari wa mbele kupinga wanawake na watoto wa kike kufanyiwa vitendo vya ukeketaji.

Serikali imeendelea kufanya jitihada mbalimbali katika kushugulikia tatizo la ukatili  kwa wanawake na watoto kwa kuandaa Mpango kazi wa Kitaifa wa kutokomeza Ukatili kwa Wanawake na Watoto 2017/18-2021/22, uliozinduliwa mwaka 2016 na kupitia mpango kazi huu serikali imedhamiria kupunguza vitendo vya ukatili ikiwemo ukeketaji kutoka asilimia 15 ya mwaka 2010  kufikia asilimia 7 ifikapo 2022.

Serikali imeanzisha jumla ya kamati za ulinzi wa mama na mtoto 10,988 katika ngazi mbalimbali kwa lengo la kulinda wanawake na watoto dhidi ya ukatili nchini.Aidha serikali imeanzisha madawati ya jinsia  na watoto katika vituo vya polisi kutoka 417 mwaka 2015 hadi 600 mwaka 2017.

Serikali imeendelea kuboresha sheria na sera mbalimbali ili kupanua wigo wa adhabu kwa wale wanaoendelea kutekeleza kitendo hicho cha kikatili. Kwa mfano mabadiliko ya Sheria ya Mtoto (2009) yamelenga pamoja na mambo mengine kupanua adhabu na kutengeneza mnyororo mpana wa washiriki. Maboresho ya Sheria ya Kanuni ya Adhabu (2002) nayo yamepanua uwanda wa kutoa adhabu na kubaini kipimo cha ushiriki wa mtuhumiwa katika kufanya ukeketaji.

Sera mbalimbali za kitaifa ikiwemo Sera ya Elimu ya 2015 inapinga kila aina ya unyanyasaji kwa mtoto wa kike na inaweka na kutambua misingi ya haki na usawa kwa watoto wote wa kike na wa kiume. Sera hii pia imelenga kuondoa ubaguzi na unyanyasaji kwa mtoto wa kike.

Mtuhumiwa Kesi ya Wizi wa Milioni 7 kwa dakika Asomewa Mashitaka Mapya 506

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jana imewafutia mashtaka mfanyabiashara maarufu,  Mohamed Yusufali na mwenzake Arital Maliwala.

Hata hivyo, washtakiwa hao baada ya kufutiwa kesi hiyo na kutoka katika chumba cha mahakama, walikamatwa tena na kusomewa mashitaka mapya 506
likiwamo la kuisababishia serikali hasara ya mabilioni ya shilingi, huku kesi yao ikisajiliwa kwenye Mahakama Kuu Divisheni ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, maarufu Mahakama ya Mafisadi.

Wakati hali ikiwa hiyo, upande wa Jamhuri umemuunganisha Meneja wa Benki ya I&M Tawi la Kariakoo, Sameer Khan, kwenye kesi hiyo.

Awali, Yusufali aliyedaiwa na Rais John Magufuli kuiba Sh. milioni saba kwa dakika, pamoja na mfanyakazi wake, Arifali Maliwalla, walikuwa wakikabiliwa na mashtaka 601 likiwamo kutakatisha Sh. bilioni 14.

Hata hivyo, Upande wa Jamhuri jana ulibadilisha hati ya mashtaka kutoka mashtaka 601 hadi 506 na kumuunganisha Khan katika kesi hiyo yenye namba za usajili 8/2019 na kusomwa mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustine Rwizile.

Katika kesi hiyo, Upande wa Jamhuri uliongozwa na Wakili wa Serikali Mwandamizi Patrick Mwita akisaidiana na Mawakili wa Serikali, Esther Martin na Leornad Swai.

Wakili Mwita alidai kuwa, washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 506, yakiwamo ya utakatishaji fedha, kuisababishia serikali hasara, kula njama, kutoa taarifa za uongo Mamlaka ya Mapato (TRA) na kughushi.
 
Baada ya kusomewa mashtaka hayo, Wakili Mwita alidai kuwa upelelezi umekamilika na wapo katika hatua ya mwisho ya kuwasilisha taarifa Mahakama Kuu Divisheni Maalum ya Uhujumu Uchumi na Rushwa.

Hakimu Rwizile alisema kesi hiyo itatajwa Februari 28, mwaka huu na washtakiwa wote wapelekwe mahabusu.

Mashamba ya Mo Dewji, Sumaye Yaibua Mjadala Bungeni

$
0
0
Serikali imesema mashamba sita yanayomilikiwa na mfanyabiashara Mohamed Dewji ‘Mo’ yapo chini ya uangalizi na kama atashindwa kutekeleza masharti watayafuta.

Akijibu hoja za wabunge jana walizozitoa katika mjadala wa taarifa ya kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi alisema awali mfanyabiashara huyo alipewa onyo katika mashamba 12 kati ya 21 aliyokuwa akimiliki.

Alisema Serikali tayari imefuta hati za mashamba sita bado sita ambayo yapo kwenye uangalizi na kubainisha kuwa Tanzania ina mashamba makubwa 2000 ya kilimo na ufugaji.

“Haijatokea nikapata agizo kutoka kwa Rais kuwa nifute hati ya shamba la mtu,”alisema Lukuvi.

Alisema zoezi hilo ni utatuzi wa kero zilizotolewa na wabunge baada ya kuwapa dodoso la kuandika kero zao.

Alisema asilimia 60 ya kero zilizoandikwa na wabunge zilihusiana na mashamba pori na migogoro ya ardhi.

Lukuvi alisema kwa kipindi cha miaka mitatu wamefuta mashamba 46 katika maeneo mbalimbali ambayo yameshindwa kutimiza masharti.

Alisema katika utafiti waliofanya wamebaini mashamba hayo yametumika kama rehani ambazo zimewawezesha kupata zaidi ya Sh1 trilioni.

Lukuvi alisema kiasi hicho cha fedha kimeenda kuwekezwa katika miradi mingine na si kilimo ambapo kama wangewekeza fedha zote kungekuwa na mabadiliko kwenye sekta hiyo.

“Mheshimiwa Msigwa (mbunge wa Iringa Mjini-Chadema) hakuna uhalali wa kuunda kamati kwa sababu mambo haya yamefanyika kwa kufuata sheria. Nendeni mkahangaike na majimbo yenu,” alisema Lukuvi.

Awali, Wabunge wa Upinzani na  wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), waliingia katika mvutano na gumzo  kuhusu taratibu zilizotumika kuyafuta, huku Spika wa Bunge, Job Ndugai, akilazimika kuzima mjadala huo, akisema anadhani suala la  Sumaye liko mahakamani, hivyo si jambo jema kuendelea kulijadili bungeni.

Kabla ya Spika Ndugai kuzima mjadala huo usiendelee, Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Peter Msigwa, alisema haoni shida ya unyang’anywaji wa mashamba hayo, lakini taratibu zinazofanyika siyo sahihi.

Akichangia, Msigwa alisema pamoja na mambo mengine, kamati haikuweka baadhi ya mapendekezo yake katika taarifa ambayo ni kuitaka serikali kuunda kamati ya kuchunguza unyang’anywaji wa mashamba hayo.

Kutokana na kauli hiyo ya Msigwa, Mbunge wa Simanjiro (CCM), James Ole Millya,  alisimama na kuomba kumpa taarifa mzungumzaji huyo akisema: “Mheshimiwa Spika, naomba nimpe taarifa mbunge, mimi natoka Jimbo la Simanjiro, takribani mwezi mmoja uliopita, Waziri alifuta mashamba zaidi ya 200 na nina hakika mashamba haya yote yalikuwa hayajafuata utaratibu na wala asipende kumchafua waziri.”

Alipomaliza kutoa taarifa hiyo, Msigwa alimshangaa Millya akisema: “Mimi nadhani unaenda haraka, mimi sijamchafua sasa ni wapi namchafua, nimezungumza, nimesema sina tatizo kabisa na mashamba makubwa kunyang’anywa kwa mujibu wa sheria na kufuatwa utaratibu.”

“Nimetoa mfano moja, Mheshimiwa Sumaye alikuwa na shamba lake, alilipata kihalali na ameliendeleza mpaka wanachukua shamba lake, alikuwa na ng’ombe 200 kwenye shamba lake, alikuwa na kondoo 350, nyumba kubwa ya umwagiliaji, kisima na ghala la mazao, anaambiwa hajaendeleza, mimi nasema unyang’anyaji huu siyo sahihi.”

Alisema anafahamu kwamba Rais kubadilisha hati, anayo mamlaka hiyo na kwamba mpaka sasa  ukiangalia hali ilivyo, ukiangalia akina Mo (Mohamed Dewji) wamenyanganywa mashamba yao ni lazima kamati ya uchunguzi iundwe ili kuangalia unyang’anywaji unavyoenda.

Suala hilo lilimwinua kitini Mbunge wa Ulanga (CCM), Goodluck Mlinga, na kutoa taarifa kwa mzungumzaji huyo kwamba kinachoonekana kupigiwa kelele ni shamba la Sumaye.

Mlingwa amesema: “Hapa linalopigiwa kelele ni suala la shamba la Mheshimiwa Sumaye, ambaye taarifa zake ni hizi, alikuwa na shamba la ekari 326, amekaa nalo miaka 15, ameendeleza ekari sita, amejenga kibanda kimoja kina watu watatu.

“Katika shamba la Sumaye, kulikuwa na miembe mitatu, miche ya mahindi 76, mnazi mmoja, ng’ombe watatu, mbuzi 11, bata sita na kuku tisa.”

CCM Njombe Yaadhimisha Miaka 42 Kwa Kupanda Chai

$
0
0
Na   AMIRI KILAGALILA
Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Njombe jana kimeungana na wananchi wa kijiji cha uliwa kata ya Ihungilo mkoani Njombe katika zoezi la upandaji wa miche ya chai ili kukuza na kuendeleza zao hilo la kimkakati mkoani humo pamoja na kuadhimisha miaka 42 ya chama hicho tangu kilipozaliwa.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo, katibu wa siasa na uenezi wilaya ya Njombe HITLA BENJAMINI MSOLA amesema kuwa chama hicho kimeamua kufanya maadhimisho hayo kwa kushirikiana na wananchi wa kijiji hicho ili kuakisi ukombozi wa uchumi wa Tanzania.

“kwanza tumefikisha miaka 42 ya chama cha mapinduzi, na huko nyuma tulikuwa tukiadhimisha kwa ngonjera na nyimbo lakini kwa sasa tuko na ccm mpya inayofanya kazi kwa vitendo na tumeamua kufanya hivi na kufanya kazi ambazo zinaakisi ukombozi wa uchumi kwa mtanzania mmoja mmoja na Tanzania kwa ujumla,na chai itakwenda kulisha viwanda vyetu na ukiangalia zao hili la chai ni miongoni mwa zao la kimkakati hususani katika mkoa wetu na katika eneo hili ni zao ambalo linastawi vizuri”alisema MSOLA

DENIS MSIGWA ni mwenyekiti wa kikundi cha Mapinduzi kinachomiliki shamba hilo anasema kuwa,watu wengi katika kijiji chao walikuwa na hamasa ndogo katika kilimo cha chai hivyo kupitia hamasa hiyo anaimani zao la chai litalimwa kwa wingi katika kijiji chao ukilinganisha na vijiji vingine vilivyopo katika tarafa ya IGOMINYI.

“kwa kweli tumehamasika kwa kuona viongozi wetu tuko nao pamoja hapa, na hamasa itakuwa kubwa kwa kuwa watu awali walidhani kilimo hiki hakina tija lakini kwa kuja kwa viongozi hawa tunauhakika sasa wananchi wamehamasika zaidi ya kipindi cha mwanzo licha ya elimu tuliyokuwa tukiipata”alisema DENIS MSIGWA.

Kwa upande wake afisa kilimo wa halmashauri ya ya mji wa Njombe ELNEST NGAPONDA amewataka wakulima wa chai kuonyesha juhudi katika kilimo hicho kwa kuwa kitakuwa na uhakika wa kipato ukilinganisha na mazao mengine ya viazi na mahindi.

“kwasababu soko lipo na bei nzuri ipo inatolewa na kiwanda cha Uniliver wakulima watakuwa na uhakika wa kipato na ukiangalia wataalamu watakaotoa maelekezo ya kitaalamu wapo kwa kufanya hivyo ni lazima tu wakulima hawa watakuwa na kipato kizuri kuliko kutegemea mazao ya mahindi na viazi yanayoathiliwa na bei kila wakati, muhimu wakulima wajiunge katika vikundi ili serikali iweze kuwawezesha baadhi ya pembe jeo”alisema Ngaponda

Naye meneja wa kampuni ya NOSC  PHILBET KAVIA wadau wakubwa wa zao la chai mkoani Njombe amesema kuwa wataendelea kumsaidia mkulima wa chai kwa kila Njia licha ya kuwepo kwa changamoto mbali mbali ikiwemo ubovu wa miundombinu.

“lengo letu Nosc ni kuinua kipato kwa mkulima maskini mmoja mmoja ambao ukiangalia ni mtizimo wa serikali na serikali hii inaongozwa na chama cha mapinduzi sasa kuja kwa viongozi hawa maeneo haya hawa wananchi wanapata faraja na nguvu ya kufanya kazi kupitia serikali yao,lakini changamoto kubwa tulizonazo ni barabara na unajua mashamba hayapo vijijini kwenye village centre  na hazipo chini ya Tarula, na hapa kikubwa ni kuona jinsi gani hizi barabara zinaboreshwa ili kupunguza gharama kwa mkulima na hata kwa kampuni na kufikisha pembejeo kwa urahisi mashambani”alisema KAVIA

Zaidi ya miche 500 ya chai imepandwa na viongozi mbali mbali wa chama na wananchi katika shamba la moja ya kikundi cha wakulima kijijini hapo katika maadhimisho ya miaka 42 ya chama cha mapinduzi yaliyofanyika kiwilaya katika kata ya Ihungilo.

Kampuni Ya Uturuki Yaonesha Nia Kuwekeza Katika Sekta Za Uchukuzi, Utalii, Nishati, Usafiri Wa Anga Na Ujenzi

$
0
0
Na. OWM, DODOMA.
Kampuni ya MNG Group of Companies ya nchini Uturuki imeonesha nia ya kufanya uwekezaji mkubwa nchini katika sekta mbalimbali; zikiwemo sekta za Uchukuzi, Utalii, Nishati na Usafiri wa Anga.

Uwekezaji huo umebainishwa na Mwenyekiti wa Bodi ya MNG Group of Companies, Mehmet Gunal, wakati alipokutana na  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Mhe. Angellah Kairuki (Mb), jijini Dodoma, tarehe 5 Januari 2019.

Waziri Kairuki amebainisha kuwa nia ya serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha uwekezaji wenye tija nchini, na kwa kutumia mfumo wa sera ya  Ushirikiano baina ya sekta Binafsi na Umma inahakikisha inavutia wawekezaji zaidi nchini.

“Tunazo fursa na miradi inayohitaji mitaji ya uwekezaji hapa nchini, jukumu letu ni kuhakikisha wawekezaji mnapata mazingira wezeshi katika fursa na miradi mnayotaka kuwekeza ili nchi iweze kupata tija kutokana uwekezaji huo” Amesisitiza  Mhe. Kairuki.

Akiongea katika kikao hicho mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya MNG Group of Companies, Mehmet Gunal, amefafanua kuwa , Kampuni hiyo iko tayari kuwekeza nchini katika Sekta mbalimbali, kwa kuwa wamevutiwa na mazingira ya uwekezaji ya hapa nchini.

Aidha, Gunal alifafanua kuwa wamejipanga kutumia  fursa na miradi yenye kuhitaji uwekezaji nchini ili kuweza kufanya uwekezaji mkubwa , pia alisema kampuni yake ipo tayari kuwekeza hata kwa mfumo wa sera ya ushirikiano baina ya Sekta ya Binafsi na Umma au kuwekeza wao wenyewe.

Kampuni ya MNG Group of Companies inao uzoefu katika masuala ya uwekezaji kwa miaka 42 katika mabara matatu Duniani, ikiwa  imejikita katika uwekezaji  kwenye sekta sita na tayari hadi hivi sasa imetekeleza miradi zaidi ya mia mbili  katika mabara hayo.

Baadhi ya Miradi ambayo imetekelezwa na Kampuni hiyo ni pamoja na , Bwawa la kufua Umeme la Chief Dam la nchini Algeria,  Ujenzi wa uwanja wa Ndege wa Kimataifa  KOTOKA (terminal III),  wa  nchini Ghana, Ujenzi wa makao makuu  ya na Benki ya Halk nchini Uturuki.

Kikao hicho kilihudhuriwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi, Isack Kamwelwe, Wataalamu wa masuala ya Uwekezaji na maendeleo ya Sekta Binafsi   wa Ofisi ya Waziri Mkuu, pamoja na wataalam kutoka   Kituo cha Uwekezaji nchini.

MWISHO. 

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamis ya February 7

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images