Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mbaroni kwa Kumbaka Mtoto wa Miaka 6

$
0
0
Polisi mkoani Tabora wanamshikilia mkazi wa kitongoji cha Utemini kata ya Ushokola wilayani Kaliua, Amos Zakaria kwa tuhuma za kumbaka mtoto wa miaka sita.

Akizungumza leo Jumatatu Februari 4, 2019 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Emmanuel Nley amesema tukio hilo limetokea jana saa sita mchana.

Amesema mtuhumiwa alimvizia binti huyo wakati anapita na kumvutia bafuni kisha kumbaka.

Amesema polisi walimkamata na baada ya kukamilisha maelezo atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Je Kwanini Baadhi Ya Wanaume Wengi Wana Ukosefu Ama Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
JE KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UKOSEFU AMA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO ???

Pata sululisho la matatizo haya na  magonjwa mengine utapona kwa mda mfupi sana hatakama ulihangaika mpaka ukakata tamaaa 

GALIMBO 3 MIX  ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa aina mbili ili kukidhi mahitaji ya mtumiaji, imetengenezwa kwa muundo wa vidonge pamoja na unga kwaajili ya kuponesha tatizo moja kwa moja , huimalisha misuli ya uume iliyolegea wakato wa tendo la mdoa ,na kukufanya ucherewe kufika kileleni kwa mda wa dk ( 20 - 45 ) itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu nira hamu kuisha wara kuhisi kuchoka vilivile huzalisha viini vya uzazi ( manii ) 

YOLAN  hurefusha na kunenepesha  maumbile madogo ya uume na kuwa na uume kuanzia nchi (6-8) tiba kwa mda mfupi sana

Zipo sananu nyingi sana zinazosababisha matatizo hayo  km vile -:punyeto, kisukali,ngili,chango,vidonda vya tumbo,  tumbo kuunguluma na kujaa gesi maumivu ya mgongo ama kiume ,kolodani moja kuvimba ama kuingia ndani  presha nk 

Matatizo haya yote sio mageni, kigeni ni tiba sahihi ya kuponesha matatizo hayo

SUPER MBUKE -:  nidawa ya kuponesha tatizo la kisukali kwa mda mfupi sana , usihangaike wara kuteseka tumia dawa ya mitishamba kwaajili ya tatizo hili na upone kabisa

NTINJIWA  nidawa ya mvuto wa biashara,kazi, kupandishwa cheo,kumfanya mfanyakazi apendwe na bos wake

Pia ninadawa za kumvuta mme , mke,mchumba,hawara, au mtu yoyote unaemuhitaji katika maisha yako hata km yupo mbali na atatulia na kukutimizia cjovjote utakacho na kumfunga asiwe na mtu mwingime ,

Pata tiba za magonjwa mbalimbali ikiwemo miguu kuwaka moto, mgongo,bawasili ,kaswende ,gono na mengine mengi

KWAUSHAULI NA TIBA WASILIANA NA DR CHIKAGO    0759 208 637

Km huna nafasi ya kufika ofisini hudumahii utaletewa hapo ulipo , kwa wale wa mikoani natuma kwanjia ya basi

Spika Ndugai aitaka Serikali kutoa kauli mauaji ya watoto Njombe

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai ameiagiza Serikali kutoa kauli kuhusu mauaji ya watoto yanayoendelea mkoani Njombe kabla ya kuahirishwa kwa mkutano wa Bunge Ijumaa Februari 8, 2019.

Ametoa kauli hiyo bungeni jijini Dodoma leo Jumatatu Februari 4, 2019 kufuatia mwongozo ulioombwa bungeni na mbunge wa Lupembe (CCM), Joram Hongole aliyetaka Bunge kuahirisha shughuli zake za leo ili kujadili mauaji hayo.

Mbunge huyo amesema taharuki imezuka mkoani Njombe na shughuli za uchumi zimesimama baada ya mauaji ya watoto chini ya miaka 10 wapatao saba.

“Kumezuka taharuki kubwa na shughuli za uchumi hazifanyiki, wakinamama wanatakiwa kuwapeleka watoto wao shuleni na kuwarudisha jioni,” amesema.

Amesema hali ni mbaya katika mkoa wa Njombe na kwamba kuna watu wanachochea hasira kwa kutuma picha za kuonyesha mauaji mkoani humo.

Mbunge wa Makambako (CCM) Deo Sanga amesema hali ya Njombe ni tete na baadhi ya watu wageni wanaonekana wamekuja kuteka na kuua.

Amesema wafanyabiashara wakubwa 10 wenye watumishi zaidi ya watu 200 wamekamatwa na hivyo shughuli za uchumi zimesimama.

Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama amesema jambo hilo ni zito na linachukua taswira nzito ndani ya Taifa.

Akijibu mwongozo huo, Spika Job Ndugai amesema ni jambo kubwa linalohuzunisha na kusikitisha na kuagiza kabla Bunge kuahirishwa wanataka kupata maelezo ya juu ya nini kinachoendelea mkoani humo na kisha kuangalia nini cha kufanya.

Mahakama Yaamuru Wadhamini Kesi ya Tundu Lissu Wafike Mahakamani February 25

$
0
0
Mahakama  ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru wadhamini wa Mbunge wa Singida Mashariki kupitia tiketi ya Chama cha Chadema, Tundu Lissu kufika Mahakamani hapo Februari 25, 2019 kueleza maendeleo ya afya yake.

Amri hiyo,  imetolewa  leo Februari 4, 2019 baada ya Wakili wa serikali Mwandamizi Patrick Mwita kudai mahakamani hapo,  Mbele ya  Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa na kwamba hadi sasa hawajajua hali ya mshtakiwa wa nne, ambae ni Lisu inaendeleaje.

"Mheshimiwa, Kesi hii leo imekuja kwaajili ya kuendelea kusikilizwa lakini hadi sasa hatuna taarifa ya hali ya mshtakiwa wa nne,tunaamini hata Mahakama hii haina rekodi ya Maendeleo yake" amedai  Wakili Mwita

Hakimu Simba amesema, kwa kuwa mahakama hiyo haina rekodi ya taarifa ya hali ya Lisu hivyo Februari 25 wadhamini wafike Mahakamani ili kueleza maendeleo ya afya yake.

Kesi hiyo ambayo ipo katika hatua ya usikilizwaji wa ushahidi wa upande wa mashtaka, inamkabili Lissu na wenzake Simon Mkina, Jabir Idrisa na Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehbooh.

Kwa pamoja, wanakabiliwa na mashtaka matano likiwamo la kuandika habari za uchochezi kinyume na Sheria ya Magazeti ya Mwaka 2002.

Inadaiwa, Januari 12 hadi 14, 2016 jijini Dar es Salaam, washtakiwa Jabir, Mkina na Lissu, waliandika na kuchapisha taarifaza uchochezi zenye kichwa cha habari kisemacho, ‘Machafuko yaja Zanzibar.’

Katika shtaka la pili wanadaiwa kuwa Januari 14, 2016 walichapisha habari hizo ili kuleta chuki kwa wananchi wa Zanzibar.

Mshtakiwa Mehboob anadaiwa kuwa Januari 13 ,2016 katika jengo la Jamana lililopo Manispaa ya Ilala, alichapisha gazeti la Mawio lililokuwa na taarifa za uchochezi.

Inadaiwa kuwa mshtakiwa huyo pia alichapisha gazeti hilo bila ya kuwasilisha hati ya sheria ya kiapo kwa Msajili wa Magazeti.

Serikali Yanunua Tani 214,269.7 za Korosho Ghafi Kufikia Januari 30

$
0
0
Na: Lilian Lundo - MAELEZO, Dodoma.
Hadi kufikia Januari 30 mwaka huu Serikali imenunua tani 214,269.7 za korosho ghafi zenye thamani ya shilingi 707,089,957,200.00 sawa na asilimia 89.3 ya lengo la uzalishaji wa msimu wa korosho wa mwaka 2018/2019.

Hayo yameelezwa leo Bungeni, Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe Omari Mgumba alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kawe, Mhe. Halima Mdee kuhusu tani ngapi zimenunuliwa na Serikali mpaka sasa na wakulima wangapi na vyama vingapi vya msingi vimelipwa na vingapi bado havijalipwa.

"Ununuzi wa korosho unafanywa na Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ambapo malipo yaliyolipwa na kuingizwa kwenye akaunti za wakulima hadi tarehe 30 Januari, 2019 ni kiasi cha shilingi 424,849,405,110 zilizotokana na korosho za wakulima kiasi cha tani 134,535.9," alisema Mhe. Mgumba.

Ameendelea kusema, jumla ya wakulima 390,466 wamelipwa hadi kufikia tarehe 30 Januari, 2019. Aidha vyama vya msingi 603 vimelipwa kati ya vyama vya msingi 605 vilivyohakikiwa.Aidha amesema, zoezi la operesheni korosho linaenda vizuri na linatarajia kukamilika ifikapo tarehe 15 Februari mwaka huu.

Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ni taasisi ya kibiashara yenye lengo la kupata faida na mtaji wake unatokana na ruzuku kutoka Serikalini na mikopo kutoka taasisi za Fedha kama Benki ya Maendeleo ya Kilimo - TADB, NMB na CRDB.

Mnamo Novemba, 2018 Serikali iliungana na msimamo wa wakuliwa wa kukataa bei zilizotolewa na kampuni za ununuzi wa korosho, ambapo zilitangaza kununua korosho kwa bei ya kati ya shilingi 2,717 na shilingi 1,900 kwa kilo ikiwa imeshuka kutoka zaidi ya shilingi 3,600 ya msimu uliopita.

Aidha, Mhe. Rais Dkt. Magufuli alitangaza Serikali kununua korosho hizo kwa shilingi 3,300 badala ya shilingi 3,000.

Vannesa Mdee Akanusha Kuongeaza Matiti.

$
0
0
Mwanadada anaetamba na kufanya vizuri kwa sasa na wimbo wa thats for me,  Vannesa mdee amefunguka na kukanusha taarifa kuwa amefanya surgery na kuongeza sehemu ya mwili wake hasa upande wa matiti.

Akiongea na refresh ya wasafu tv, Vanesa aliulizwa swala la kizushi kuhusu mwili wake kuwa sehemu kubwa ya maziwa yake kwa sasa imeongezeka na sio kama ilivyokuwa hapo awali, mwanadada huyo alisema kuwa habari hizo sio za kweli na kwamba hajafanya kitu kama icho.

Akiongea kwa kujiamini, Vanesa anasema kuwa katika maisha yake hajawahi kufanya upasuaji kwa ajili ya kuongeza kitu chochote katika mwili huo na hata swala la maziwa watu wamekuwa wakimwangalia kwa wasiwasi lakini hajafanya chochote.

==>>Sikiliza Full Interview hapo chini

Kiongozi wa upinzani DRC, Martin Fayulu akataa mwito wa maridhiano wa Tshisekedi

$
0
0
Kiongozi  wa  upinzani nchini DRC, Martin Fayulu amekataa juhudi za Rais mpya,  Felix Tshisekedi za kutaka maridhiano, baada ya uchaguzi mkuu wa kwanza wa kidemokrasia kumalizika.

Mwito huo wamaridhiano ulitoleawa na Rais huyo  mpya katika jitihada za kutafuta maridhiano ya kisiasa nchini hapa.

Hata hivyo jitiahada hizo za Rais Tshisekedi zinaonekana kugonga mwamba baada ya  Fayulu kusema kuwa  pale unapopewa mkono ambao ni mchafu, hupaswi kuupokea.

Kauli ya Fayulu imekuja siku chache baada ya Rais  Tshisekedi kusema katika hotuba yake aliyoitoa baada ya kuapishwa kwamba  nchi yake haitakuwa ni ya upande mmoja ama ukabila, huku akisisitiza kuwa tayari kukutana na wapinzani ili waweze kushirikiana kujenga Congo imara.

“Tunataka kujenga Congo imara  katika utamaduni wake. Tutakuza maendeleo  kwa amani na usalama. Congo ni ya kila mmoja  ambapo kila mtu ana nafasi yake mwenyewe, “alisema Tshisekedi.

Fayulu alitoa kauli hiyo juzi katika mkutano wake wa kwanza  tangu aliposhindwa kwenye uchaguzi wa rais uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana wakati akiwahutubia  mamia ya wafuasi wake waliokusanyika mjini hapa.

Hata hivyo pamoja na kukataa wito huo wa maridhiano, kiongozi huyo aliwataka wafuasi wake wasifanye fujo wakati anapoendelea kupinga uchaguzi anaodai ulikumbwa na udanganyifu.

“Hakuna haja ya kufanya vurugu ila tutaendelea kupaza  sauti zetu katika jumuiya za kimataifa ili haki ipatikane,”alisema kiongozi huyo.

 Aliuhimiza Umoja wa Mataifa (UN) na wa Afrika (AU) kutopokea maagizo kutoka kwa mtu anayedai kuwa Wakongo hawakumchagua

Wimbo wa Kumtukuza Mungu: Niongozwe Nawe- Doreen Lifard

$
0
0
MWIMBAJI Wa Nyimbo za  Injili, Doreen Lifard ameachia video ya wimbo wake  uitwao Niongozwe Nawe. Utazame Hapo chini upate kubarikiwa Weekend hii

Sheria ya uvuvi kufumuliwa....Waziri Luhaga Mpina Afunguka

$
0
0
Serikali imeamua kuifumua Sheria ya Uvuvi Namba 22 ya mwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2009 ili kuondoa vikwazo vya kibiashara na uwekezaji katika sekta ya uvuvi.

Pia kwenda na kasi ya mabadiliko ya Serikali ya awamu ya tano inayolenga kujenga Tanzania ya viwanda, kuwatetea na kuwalinda wanyonge.

Akizungumza katika uzinduzi wa ukusanyaji maoni ya wadau kuhusu rasimu ya Sheria ya Uvuvi na Sheria ya Ukuzaji viumbe kwenye maji jijini Dar es Salaam, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina, alitaja sababu nyingine zilizosababisha kuwapo mabadiliko hayo.

Sababu ya kwanza pamoja na kutoa ulinzi madhubuti wa rasilimali za uvuvi, kuongeza uzalishaji na kuwa na masoko ya uhakika sambamba na kudhibiti utoroshwaji na uingizaji holela wa mazao ya uvuvi nchini.

Aidha, Mpina alisema sheria hiyo mpya inatakiwa iendane pia na mabadiliko na matumizi ya sayansi na teknolojia katika uvuvi na ukuzaji viumbe kwenye maji ili kwenda sambamba na mahitaji pamoja na kuwapo mwamko mkubwa wa ufugaji wa samaki kwenye maji uliojitokeza miongoni mwa wananchi.

Alisema pamoja na rasimu ya sheria hizo mbili pia Serikali iko kwenye hatua za mwisho za kuzifanyia marekebisho Sheria ya Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu Namba 29 ya mwaka 1994 na Kanuni zake za mwaka 2009 na Sheria ya Bahari Kuu Cap 388 na Kanuni zake za mwaka 2007 na 2016.

Hivyo Waziri Mpina aliwasihi wananchi kutoa maoni yasiyofungamana na upande wowote na kuacha tabia ya kila mmoja kuvutia upande wake ili kuwezesha kutunga sheria madhubuti.

Aidha Waziri Mpina alieleza utajiri wa kipekee wa rasilimali za uvuvi nchini ikiwamo kuwa na eneo kubwa la maji lenye kilomita za mraba 346,337 sawa na asilimia 36.7 ya eneo lote la nchi, fukwe ndefu na za kuvutia, kuwapo kwa samaki na viumbe vingine ambavyo vimetoweka na vingine vikiwa kwenye tishio la kutoweka duniani.

Pia kuwapo kwa mito, mabwawa na maziwa yenye sifa za kipekee ikiwemo Ziwa Victoria ambalo ni la pili kwa ukubwa duniani na Ziwa Tanganyika ambalo ni la pili kwa kina duniani na la kwanza kwa ujazo wa maji duniani.

Alisisitiza kuwa wakati nchi inakwenda kutunga sheria hiyo mpya ya uvuvi, ni muhimu kama Taifa kujiuliza maswali kadhaa ikiwamo matumizi sahihi ya rasilimali hizo.

"Lazima tujiulize tunapata wapi uhalali wa kuagiza samaki kutoka nje ya nchi?, tujiulize kwa nini tumeshindwa kulihudumia soko la ndani na la nchi jirani, Afrika na dunia?, kwa nini tuzidiwe uzalishaji na mauzo na nchi ambazo tunazizidi kwa mbali kwa rasilimali?,.

"Vilevile Kwanini tuwe na wavuvi masikini tena ambao hawana zana bora za uvuvi, kwanini biashara, uwekezaji na ujenzi wa viwanda ni wa kusuasua ? haya ndio maswali tunayopaswa kujiuliza kama Taifa," alihoji Mpina.


Hivyo Waziri Mpina alisema kutokana na ugumu wa maswali
hayo ndio maana wizara yake ikaamua ni bora kuifumua Sheria ya Uvuvi Namba 22 ya mwaka 2003 na Kanuni zake za mwaka 2009 ili kusaidia kupata majawabu ya namna gani kama taifa litatoka kwenye mkwamo huo.

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Siku Ya Wanawake Duniani 2019

$
0
0
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto) inapenda kuwajulisha wadau wa maendeleo ya jinsia na wanawake pamoja na Watanzania kwa ujumla kuwa Tanzania itaungana na Nchi Nyingine Wanachama wa Umoja wa Mataifa kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa tarehe 8, Machi ya kila mwaka.

Kaulimbiu ya Kitaifa ya Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa mwaka 2019 inasema:“Badili Fikra Kufikia Usawa wa Kijinsia kwa Maendeleo Endelevu”.

Kwa mwaka huu, Maadhimisho yataendelea kufanyika katika ngazi ya Mkoa ili kutoa wigo mpana kwa wanawake, wadau mbalimbali na kila Mtanzania kutathmini hatua tulizofikia kama Taifa katika masuala ya usawa wa kijinsia na uwezeshaji wanawake na wasichana. 

Aidha, Maadhimisho haya ni fursa ya kujadiliana namna ya kukabiliana na changamoto katika kufikia Maendeleo jumuishi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne ya February 5

Waziri wa Kilimo: Wakulima wa Pamba watarajie mabadiliko makubwa

$
0
0
Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga amewaambia Waheshimiwa Wabunge wa maeneo yanayolima pamba kuwa Wizara ya Kilimo imedhamiria kumkomboa Mkulima wa pamba na kwa kuanza imeanzisha zoezi la kuwasajili Wakulima wote nchini wakiwemo Wakulima wa pamba ambapo Serikali imetengeneza mfumo maalumu wa kuwatambua kwanza Wakulima, maeneo wanayotoka, mashamba yao yapo wapi na yana ukubwa gani.

Mhe. Hasunga ameyasema hayo wakati wa kikao maalumu na Waheshimiwa Wabunge hao katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo Jijini, Dodoma  Jumatatu tarehe 4 Februari, 2019.

Kikao hicho kilikuwa na lengo la kufanya maboresho kwa ajili ya kujiandaa na msimu ujao wa mauzo ya pamba ambao unatarajia kuanza Mwezi Aprili mwaka huu.

Mhe. Hasunga amesema moja ya mambo ambayo Wizara ya Kilimo itahakikisha inayashughulikia ipasavyo, sambamba na kuwatambua Wakulima wa pamba ni pamoja na kuupitia upya mfumo wa Ushirika katika ununuzi wa pamba, mfumo wa uagizaji na uingizaji wa viuatilifu vya pamba pamoja na masoko ya zao hilo.

Waziri Hasunga amesema katika kipindi hiki kifupi amekuwa akipata malalamiko mengi kutoka kwa Wakulima wa mazao mbalimbali kuhusu udhaifu wa mfumo wa uagizaji wa uingizaji wa pembejeo za kilimo yakiwemo madawa na mbegu hafifu.

“Napenda nikiri kuwa tuna tatizo katika mfumo wa uagizaji na uingizaji wa pembejeo za kilimo, bado haujakaa vizuri lakini baya zaidi ni viuatilifu hafifu. Serikali kamwe haiwezi kutazama Wakulima wakionewa na Wajanja wachache na huu ni uhujumu uchumi lazima wanaofanya mambo haya wachukuliwe hatua kali za kisheria”. Amekaririwa Waziri Hasunga.

Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya Wabunge wameshauri kuwa muda wa kupeleka pembejeo za kilimo kama mbegu bora na madawa uwe mapema zaidi kuliko ilivyo sasa. Mhe. Kiswaga Boniventura Mbunge wa Magu ameishauri Serikali kuwa wakati wa zoezi la ununuzi wa pamba ghafi zoezi hilo liendane na zoezi la kuwapelekea Wakulima mbegu bora za pamba na kuongeza kuwa litaokoa fedha za Umma kwa kuwa fedha za usafirishaji itatumika mara moja tu.

Naye Mbunge wa Itilima Mhe. Njalu Silanga amesema kuna haja kubwa ya kupitia mfumo mzima wa Vyama vya Ushirika vinavyonunua pamba, akitoa mfano katika msimu wa pamba uliopita wa mwaka 2018/2019 Wakulima wa pamba walikuwa wakikatwa shilingi 100 katika kila kilo moja kwa ajili ya kugharamia ununuzi wa viuatilifu (Madawa ya pamba) katika msimu ujao wa kilimo.

Mhe. Njalu amesema kuna maeneo mengi ambayo Wakulima wengi wanafikisha zaidi ya kilo mia tano (500) na anapokatwa kiasi hicho cha fedha makusanyo yanakuwa makubwa hadi kufikia shilingi elfu hamsini (50,000/=) wakati thamani halisi ya pembejeo ambazo atapewa na Chama chake cha Ushirika hakizidi shilingi elfu kumi (10,000/=).

Mhe. Waziri Hasunga amekiri kuwa jambo hilo linaweza kuwepo na kuna haja ya kuufanya maboresho makubwa mfumo mzima ununuzi wa pamba kabla ya kuanza msimu mpya wa ununuzi wa pamba ambao unataraji kuanza mapema Mwezi Aprili, 2019

Waziri wa Kilimo Mhe. Japhet Hasunga amewaambia Waheshimiwa Wabunge wa maeneo yanayolima pamba kuwa Wizara ya Kilimo imedhamiria kumkomboa Mkulima wa pamba na kwa kuanza imeanzisha zoezi la kuwasajili Wakulima wote nchini wakiwemo Wakulima wa pamba ambapo Serikali imetengeneza mfumo maalumu wa kuwatambua kwanza Wakulima, maeneo wanayotoka, mashamba yao yapo wapi na yana ukubwa gani.

Mhe. Hasunga ameyasema hayo wakati wa kikao maalumu na Waheshimiwa Wabunge hao katika ukumbi wa Wizara ya Kilimo Jijini, Dodoma leo Jumatatu tarehe 4 Februari, 2019.

Kikao hicho kilikuwa na lengo la kufanya maboresho kwa ajili ya kujiandaa na msimu ujao wa mauzo ya pamba ambao unatarajia kuanza Mwezi Aprili mwaka huu.

Mhe. Hasunga amesema moja ya mambo ambayo Wizara ya Kilimo itahakikisha inayashughulikia ipasavyo, sambamba na kuwatambua Wakulima wa pamba ni pamoja na kuupitia upya mfumo wa Ushirika katika ununuzi wa pamba, mfumo wa uagizaji na uingizaji wa viuatilifu vya pamba pamoja na masoko ya zao hilo.

Waziri Hasunga amesema katika kipindi hiki kifupi amekuwa akipata malalamiko mengi kutoka kwa Wakulima wa mazao mbalimbali kuhusu udhaifu wa mfumo wa uagizaji wa uingizaji wa pembejeo za kilimo yakiwemo madawa na mbegu hafifu.

“Napenda nikiri kuwa tuna tatizo katika mfumo wa uagizaji na uingizaji wa pembejeo za kilimo, bado haujakaa vizuri lakini baya zaidi ni viuatilifu hafifu. Serikali kamwe haiwezi kutazama Wakulima wakionewa na Wajanja wachache na huu ni uhujumu uchumi lazima wanaofanya mambo haya wachukuliwe hatua kali za kisheria”. Amekaririwa Waziri Hasunga.

Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya Wabunge wameshauri kuwa muda wa kupeleka pembejeo za kilimo kama mbegu bora na madawa uwe mapema zaidi kuliko ilivyo sasa. Mhe. Kiswaga Boniventura Mbunge wa Magu ameishauri Serikali kuwa wakati wa zoezi la ununuzi wa pamba ghafi zoezi hilo liendane na zoezi la kuwapelekea Wakulima mbegu bora za pamba na kuongeza kuwa litaokoa fedha za Umma kwa kuwa fedha za usafirishaji itatumika mara moja tu.

Naye Mbunge wa Itilima Mhe. Njalu Silanga amesema kuna haja kubwa ya kupitia mfumo mzima wa Vyama vya Ushirika vinavyonunua pamba, akitoa mfano katika msimu wa pamba uliopita wa mwaka 2018/2019 Wakulima wa pamba walikuwa wakikatwa shilingi 100 katika kila kilo moja kwa ajili ya kugharamia ununuzi wa viuatilifu (Madawa ya pamba) katika msimu ujao wa kilimo.

Mhe. Njalu amesema kuna maeneo mengi ambayo Wakulima wengi wanafikisha zaidi ya kilo mia tano (500) na anapokatwa kiasi hicho cha fedha makusanyo yanakuwa makubwa hadi kufikia shilingi elfu hamsini (50,000/=) wakati thamani halisi ya pembejeo ambazo atapewa na Chama chake cha Ushirika hakizidi shilingi elfu kumi (10,000/=).

Mhe. Waziri Hasunga amekiri kuwa jambo hilo linaweza kuwepo na kuna haja ya kuufanya maboresho makubwa mfumo mzima ununuzi wa pamba kabla ya kuanza msimu mpya wa ununuzi wa pamba ambao unataraji kuanza mapema Mwezi Aprili, 2019

Spika Ndugai Apigilia Msumari Bima ya Afya Kwa Kila Mtanzania

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai, ameagiza serikali kufanyia kazi kwa haraka suala la kuanzisha bima ya afya moja ili wananchi wote wapate huduma pindi wanapohitaji kama ilivyo kwa nchi ya Ghana na Rwanda.

Ndugai alitoa agizo hilo jana bungeni baada ya majibu ya serikali kuhusu mchakato wa kuanzisha bima hiyo.

Spika alisema Bunge lilishawatuma wabunge kutembelea nchi hizo ili kujifunza namna wanavyotumia mfumo huo na kuomba suala hilo lipewe msukumo na serikali ili Watanzania wapate huduma.

“Fanyeni kazi usiku na mchana ili ipatikane bima kwa Watanzania wote kwa kuwa lina umuhimu mkubwa,” alisema.

Awali, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulile, alisema wizara hiyo imeandaa mapendekezo ya kuanzisha bima ya afya moja na kuwasilishwa katika ngazi mbalimbali za maamuzi serikalini.

“Wizara inaendelea na maandalizi ya utaratibu wa kuhakikisha wananchi wote wanakuwa katika mfumo wa bima ya afya na hivyo kuwa na uhakika wa kupata huduma wakati wowote wanapohitajika bila kuwa na kikwazo cha kifedha,” alisema.

Alisema pindi serikali itakaporidhia mapendekezo hayo suala hilo litawasilishwa bungeni na endapo Bunge litapitisha muswada huo kutakuwa na ulazima wa wananchi wote kujiunga na bima.

“Matarajio ni kuanza kutekelezwa mwaka huu wa 2019, kwa sasa wizara inaendelea kutekeleza mikakati na kuhamasisha wananchi kujiunga na Bima ya Taifa ya Afya na Bima ya Afya ya Jamii (CHF) iliyoboreshwa,” alisema.

Alisema kuwa licha ya Watanzania asilimia 34 kuwa kwenye mfumo wa bima ya afya bado uwezo wa wananchi kuchangia matibabu ni changamoto.

Alitoa rai kwa wabunge kuendelea kuwahimiza wananchi kujiunga na bima za afya zilizopo wakati wanasubiri muswada huo kupitishwa.

Dk. Ndugulile alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kiteto Koshuma, aliyehoji ni lini serikali italeta sheria ya kuwataka wananchi wote kujiunga na mifuko ya taifa ya bima ya afya.

Chanjo Ya Mlango Wa Kizazi Haihusiani Na Uzazi Wa Mpango- Waziri Ummy Mwalimu

$
0
0
Na WAMJW – DOM
WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu amewatoa hofu Wananchi kwa kusisitiza kuwa chanjo ya kuwakinga wasichana na Saratani ya Mlango wa kizazi haihusiani na uzazi wa mpango wala kumzuia msichana kuja kupata uja uzito baadae.

Ameyasema hayo jana  wakati akiongea na Waandishi wa Habari katika siku ya Saratani Duniani, iliyofanyika katika Ukumbi wa Idara ya Habari Bunge jijini Dodoma, huku kauli mbiu ya mwaka huu ikiwa ni “NITAFANYA JITIHADA ZOTE KUPUNGUZA JANGA LA SARATANI DUNIANI”.

Waziri Ummy amesema kuwa Chanjo ya Mlango wa kizazi ni salama na imethibitishwa na Shirima la Afya Duniani kwaajili yakuwakinga Wasichana dhidi ya maambulizi ya Saratani ya Mlango wa kizazi.

” Chanjo ya kuwakinga wasichana na saratani ya mlango wa kizazi haihusiani na uzazi wa mpango, ni chanjo ambayo imethibitishwa na Shirika la Afya Duniani kwaajili yakuwakinga wasichana dhidi ya maambukizi ya Saratani ya mlango wa Kizazi” Alisema Waziri Ummy

Waziri Ummy amesema kuwa katika kila wagonjwa wa Saratani 100, takribani wagonjwa 31 ni wanawake wa Saratani ya Mlango wa kizazi, hivyo amewahasa wazazi na walezi nchini kuhakikisha wasichana wanaostahili kupata chanjo hii, wanaipata bila vikwazo vyovyote ili kutokomeza kabisa Saratani hii nchini.

“Katika kila wagonjwa wa Saratani 100, Wagonjwa takribani 31 ni wanawake wa Saratani hii ya Mlango wa kizazi, kwahiyo hatuna haja ya kuiogopa chanjo hii kwasababu ndio itayowakinga watoto wetu na maambukizi ya Saratani ya mlango wa kizazi” alisema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Tafiti za Saratani (IARC), zinaonyesha kwamba kwa Tanzania kunatokea mgonjwa 1 wa Saratani kwa kila watu 1000, hivyo Tanzania inakua na wagonjwa wapya wa Saratani 55,000 kwa mwaka na takribani wagonjwa 28,610 hufariki kwa mwaka, ambapo ni vifo asilimia 52 ya wagonjwa wapya.

Aliendelea kusema kuwa Taarifa kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road zinaonesha kwamba kumekuwa na ongezeko la wagonjwa wa Saratani mwaka hadi mwaka, huku akisema kuwa Mwaka 2015 wagonjwa wapya 5,764, huku mwaka 2016 wagonjwa wapya 6,338, na mwaka 2017 wagonjwa wapya 7,091, pia mwaka 2018 wagonjwa wapya 7,649.

Kwa upande mwingine Waziri Ummy amedai kuwa Serikali imeanzisha huduma kwenye vituo 624 vilivyopo katika Halmashauri mbalimbali nchini ambapo jumla ya wanawake 375,522 walifanyiwa uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi na saratani ya matiti mnamo mwaka 2017, ukilinganisha na wanawake 416,841 waliofanyiwa uchunguzi huo mwaka 2018. Kati ya hao, wanawake 16,147 waligundulika kuwa na mabadiliko ya awali mwaka 2017, na wanawake 18,341 mwaka 2018.

Nape Nnauye ajiuzulu uenyekiti wa kamati ya Bunge

$
0
0
Katibu wa Bunge, Ndugu Stephen Kagaigai amethibitisha kupokea barua ya mbunge wa Mtama Mh. Nape Nnauye kujiuzulu nafasi ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii.
 
Kagaigai amesema jana Jumatatu Februari 04, 2019 Nape aliandika barua kwenda kwa Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai ya kujiuzulu nafasi hiyo na tayari spika amempatia nakala ya barua hiyo.

''Ni kweli nimeiona barua aliyomwamndikia Spika na mimi nimepata nakala yangu kwahiyo ni kweli amejiuzulu labda awe na mawazo mengine'', amesema.
 
Machi mwaka 2017, Nape aling’olewa kwenye nafasi ya Uwaziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambayo sasa ipo chini ya Waziri Harrison Mwakyembe.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Itigi Atiwa Mbaroni Kwa Tuhuma za Mauaji Kanisani

$
0
0
Watu watano, akiwamo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Itigi, Pius Luhende, wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Singida, wakituhumiwa kusababisha kifo cha mfugaji Peter Chambalo, anayedaiwa kupigwa risasi akiwa kanisani.
 
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Ahmed Msangi, amesema tukio hilo limetokea juzi na kueleza kuwa mpaka sasa, wanaoshikiliwa ni watu  watano akiwamo mkurugenzi huyo.

Msangi alitaja watuhumiwa wengine wanaoshikiliwa kuwa ni askari wanyamapori wawili, mmoja kutoka Mamlaka ya Wanyamapori (Tawa) na mwingine kutoka Halmashauri ya Ipigi, mwanasheria na mtendaji wa kata.

“Ni kweli tukio limetokea, lakini siyo kweli kuwa askari wa Jeshi la Polisi wamehusika na tukio hilo," Amesema Msangi.

"Waliokuwapo ni askari wanyamapori, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Itigi, mwanasheria wake na mtendaji wa kata. Kilichotokea ni kwamba, walipofika katika kijiji cha Kazikazi, Kata ya Kitaraka, Tarafa ya Itigi, kulitokea kutoelewana, hivyo kusababisha vurugu," alisema.

Aliongeza kuwa, wakati wa vurugu hizo, inadaiwa askari walifyatua risasi na kumjeruhi mtu huyo ambaye alifariki dunia.

Tamko la Waziri wa Afya Katika Maadhimisho ya Saratani Duniani

$
0
0
Siku ya Saratani Duniani huadhimishwa kila Tarehe 4 mwezi Februari. Siku hii, ambayo ilianza kuadhimishwa mwaka 2000 mjini Paris, Ufaransa wakati wa mkutano wa Dunia wa Saratani, ni siku maalumu ya kutafakari na kuuelezea ulimwengu hasa wananchi kuhusu janga la Saratani. 

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya Siku ya Saratani Duniani kwa mwaka huu wa 2019 ni:Ni Mimi, nitafanya (I am, I will) Binafsi, nitafanya jitihada zote kupunguza janga la Saratani Duniani.
 
Ujumbe huu unaeleza kwamba, kila mtu binafsi ana wajibu wa kushiriki kikamilifu katika kupambana na janga la saratani kwa kuelimisha jamii, kuwa na mtazamo chanya, kupima afya yake, kujikinga na vitu vyote vyenye kusababisha saratani, kusaidia wagonjwa wa saratani na kwa Hospitali zote zinazotoa huduma ya saratani kuhakikisha zinatoa huduma bora, ili kupunguza janga la saratani na athari zake zote.

Saratani ni ugonjwa ambao unaathiri watu wa rika na jinsia zote; watoto, watu wazima, wake kwa waume. Takwima mpya za Shirika la Kimataifa la Utafiti wa Saratani (International Agency for Research on Cancer – IARC) na Shirika la Afya Duniani (WHO) zilizotolewa Septemba 2018, zinaeleza kwamba kila mwaka duniani kote kunatokea wagonjwa wapya wa saratani wanaokadiriwa kufikia milioni 18.1, na kati ya hao, zaidi ya wagonjwa milioni 9.6 hufariki kutokana na ugonjwa wa saratani kila mwaka. 

Aidha, watu zaidi ya millioni 43.8 wanaishi na saratani duniani kote na kama hatua madhubuti za kinga, uchunguzi wa mapema na tiba stahiki hazitachukuliwa haraka, tatizo la saratani litaongezeka na kufikia makadirio ya wagonjwa wapya milioni 24 ifikapo mwaka 2035, huku ongezeko kubwa likiwa katika ukanda wa nchi zinazoendelea kama Tanzania.

Nchini Tanzania, tatizo la saratani limekuwa likiongezeka na kukua siku hadi siku. Takwimu za Shirika la Umoja wa Mataifa la Tafiti za Saratani (IARC), zinaonyesha kwamba kwa Tanzania kunatokea mgonjwa 1 wa Saratani kwa kila watu 1000; hivyo Tanzania inakua na wagonjwa wapya wa Saratani 55,000 kwa mwaka na takribani wagonjwa 28,610 hufariki kwa mwaka, ambapo ni vifo asilimia 52 ya wagonjwa wapya. 

Takwimu za hospitali za mwaka 2018, zinaonyesha wagonjwa wapya wa saratani waliohudumiwa ni 14,028 ambayo ni sawa na asilimia 25.5 ya wagonjwa wote wanaokadiriwa kuwepo nchini. 

Wagonjwa waliohudumiwa walifika kupata huduma katika hospitali za Ocean Road (7,649), Bugando (2,790), KCMC (1,050), Muhimbili (1,321), na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (218). Aidha takribani wagonjwa wapya 1,000 walipata huduma katika hospitali binafsi za Agakhan, Hindu Mandal, Hubert Kairuki, Besta, Rabininsia na mikoani. 

Aidha, Wagonjwa wengi takribani asilimia 75 walifika katika Hospitali wakiwa katika hatua za juu za ugonjwa (hatua ya 3 na ya 4) hali ambayo hupunguza uwezekano wa wagonjwa kupona maradhi yao. Hili ni tatizo kubwa ambalo tunaweza kuondokana nalo endapo tutakuwa na tabia ya kupima afya zetu mara kwa mara ili ugonjwa uweze kugundulika katika hatua za mwanzo na hivyo kutibika kwa urahisi.

Taarifa kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road zinaonesha kwamba kumekuwa na ongezeko la wagonjwa wa Saratani mwaka hadi mwaka. Mfano Mwaka 2015 wagonjwa wapya 5,764; mwaka 2016 wagonjwa wapya 6,338; mwaka 2017 wagonjwa wapya 7,091; na mwaka 2018 wagonjwa wapya 7,649.

Aidha kwa mujibu wa Taarifa kutoka Taasisi ya Saratani ya Ocean Road za mwaka 2018, aina za Saratani zinaoongoza hapa nchini ni kama ifuatavyo:

1. Saratani ya mlango wa kizazi (Cervical cancer) – 31.2%
2. Saratani ya matiti (Breast cancer) – 12.9%
3. Saratani ya koo (Cancer of the oesophagus) – 9.8%
4. Saratani ya ngozi (Kaposis Sarcoma) – 9.3%
5. Saratani za kichwa na shingo (Head and Neck) – 6.8%
6. Saratani ya matezi (Lymphoma) – 5.3%
7. Saratani ya damu (Leukemia) – 4.7%
8. Saratani ya tezi dume (Prostate cancer) – 3.9%
9. Saratani ya kibofu (Urinary Bladder cancer) – 2.8%
10. Saratani ya ngozi (Skin Cancer) – 2.6%

Mwaka 2018, Saratani ya Koo (Cancer of the Oesophagus) imejitokeza sana na kuwa Saratani ya 3 (9.8%) kati ya Saratani kubwa 5 kwa kuathiri watanzania wengi; kwa miaka ya nyuma ilikua saratani ya 4.

Kwa upande wa Wanaume, Saratani zinazoongoza ni:
Saratani ya Ngozi (Kaposi Sarcoma) (20.3%)
Saratani ya Koo (Esophageal Cancer) (18.7%)
Saratani ya Tezi Dume (Prostate Cancer) (16%)
Saratani ya matezi (Lymphoma) (13%)

Kwa upande wa wanawake, wengi wanaumwa Saratani:
1. Saratani ya Mlango ya Kizazi (Cervical Cancer) (56.5%)
Saratani ya Ngozi (Kaposis Sarcoma) (14%)
Saratani ya Matiti (Breast Cancer) (17%)
Saratani ya Koo (Esophageal Cancer) (11%)

Vyanzo vikubwa vya saratani vipo vinne;
Maambukizi (infection) – Maambukizi yamegawanyika katika sehemu kuu tatu;
Virusi – Kirusi ya Human Papilloma (Human Papiloma Virus) vinavyosababisha Saratani ya Mlango wa kizazi, na Kirusi cha Hepatitis B (Hepatitis B Virus) huweza kusababisha Saratani ya Ini.
Maambukizi ya Bakteria – Mfano Helicobacter Pyroli vinaweza kusababisha Saratani ya Tumbo.
Parasaiti (Parasites) – Kwa mfano vimelea vya kichocho vinaweza kusababisha Saratani ya Kibofu cha mkojo.

Kutokuzingatia Mtindo bora wa maisha (unhealthy Life Style), kama vile matumizi ya tumbaku na bidhaa zake, kula vyakula ambavyo si salama au kula vyakula ambavyo havikuhifadhiwa vizuri, kutokula matunda na mbogamboga, kunywa pombe kupitiliza, matumizi ya dawa za kulevya na kutokufanya mazoezi. 

Mfano, matumizi ya Tumbaku ni kisababishi kikubwa cha magonjwa ya Saratani ya matiti, mdomo, koo pamoja na magonjwa ya moyo. Unywaji wa vilevi uliopitiza huchangia kwenye kusababisha magonjwa ya saratani za matiti, ini, utumbo mpana, pamoja na saratani nyingine.

Madhara kutokana na Mazingira (Exposures) – Mfano miale ya jua ambayo inaathiri ngozi haswa kwa watu wanaoishi na ualbino huweza kusababisha saratani ya ngozi kwa jamii hii; vumbi la asbestos kutoka viwandani kusababisha saratani ya mapafu; kemikali za benzene katika mafuta ya mitambo kusababisha saratani ya damu; sumu kuvu kutoka katika nafaka kusababisha Saratani ya koo; n.k.

Urithi katika familia (vinasaba-Genetics) – Kwa mfano Saratani ya Matiti, Utumbo mpana, na tezi dume huweza kusababishwa na vinasaba kwenye ukoo mtu anaotokea.

Serikali inaendelea na utekelezaji wa Sera ya Afya ya mwaka 2007, ambayo inapitiwa upya pamoja na mengineyo lengo likiwa ni kuhakikisha afua mbalimbali za afya zinajielekeza katika kutoa huduma bora zaidi na za kisasa kwa magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwemo Saratani. 

Aidha, Serikali, inaendelea kushirikiana na Mashirika ya Kimataifa, Mashirika yasiyo ya kiserikali na Sekta binafsi, kuandaa na kurekebisha Sheria, Kanuni na taratibu ili kuimarisha uzuiaji na udhibiti wa magonjwa yasiyo ya kuambukiza.

Kwa upande wa kinga dhidi ya saratani, Serikali imeanza kutoa chanjo ya kukinga wasichana na virusi vinavyosababisha saratani ya mlango wa kizazi (HPV Vaccine) kuanzia mwezi Aprili 2018.

 Chanjo hii inatolewa kwa wasichana walio shuleni na kwenye jamii kuanzia umri wa miaka 9 hadi miaka 14. Hata hivyo kutokana na changamoto ya upatikanaji wa dozi za kutosha za chanjo hii kutoka kwa wazalishaji, Serikali iliamua kuanza kutoa chanjo hii kwa wasichana wa umri wa miaka 14 ambapo tulilenga kuwafikia wasichana wapatao 625,452 kwa mwaka 2018. 

Kwa takwimu za awali, mpaka kufikia Desemba, 2018 wasichana wapatao 412,016 (66%) walipatiwa dozi ya kwanza na wasichana 125,362 (53%) ndiyo walikuwa wamekwishapatiwa dozi ya pili ya chanjo hii. Kutokana na chanjo kuanza kutumika mwezi Aprili 2018, lengo la mwaka litakamilika ifikapo mwishoni mwa mwezi Machi, 2019. 

Ninapenda kuwahimiza wazazi, walezi na walimu kuhakikisha wasichana wanaostahili kupata chanjo hii wanaipata bila vikwazo vyovyote. Hatua hii ya kuwapatia wasichana chanjo ya HPV itasaidia sana kupunguza au kutokomeza kabisa Saratani ya mlango wa kizazi hapa nchini kwetu.

Kwa upande wa kugundua mapema na kutibu mapema (Early detection and Early treatment), Serikali imeanzisha huduma kwenye vituo 624 vilivyopo katika Halmashauri mbalimbali nchini ambapo jumla ya wanawake 375,522 walifanyiwa uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi na saratani ya matiti mnamo mwaka 2017, ukilinganisha na wanawake 416,841 waliofanyiwa uchunguzi huo mwaka 2018. Kati ya hao, wanawake 16,147 waligundulika kuwa na mabadiliko ya awali mwaka 2017, na wanawake 18,341 mwaka 2018.

 Aidha wanawake 3,254 walidhaniwa kuwa na saratani ya mlango wa kizazi (suspicious cervical cancer) mwaka 2017, kulinganisha na wanawake 4,487 mwaka 2018 na hivyo kupatiwa rufaa Hospitali za ngazi za juu kwa ajili ya kuthibitisha kama ni saratani ili wapatiwe matibabu stahiki. 

Hata hivyo licha ya kupewa rufaa, wanawake wengi bado hawaendi Hospitali kwa ajili ya ugunduzi na matibabu. Nitoe rai kwa wanawake kujenga utamaduni wa kuchunguza afya zao ikiwemo Saratani ya Mlango wa Kizazi na Saratani ya Matiti angalau mara moja kwa mwaka, na wakigundulika na mabadiliko ya awali ya saratani, basi wasiache kwenda kupatiwa matibabu. Saratani ya mlango wa kizazi ikigundulika mapema, inatibika kwa asilimia 100.

Hivyo ninarudia tena kuwataka Waganga Wakuu wa Mikoa/Wilaya na Waganga Wafawidhi kuhakikisha Vituo vyote vya Afya (Health Centres) na Hospitali za umma nchini zinakuwa na siku maalum kila mwezi kwa ajili ya upimaji wa Saratani ya mlango wa kizazi na saratani ya matiti. Ugunduzi wa mapema wa saratani huokoa maisha.

Kwa upande wa matibabu, Serikali ya Awamu ya tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais, Dkt John Pombe Magufuli, kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na kwa kushirikiana na wadau wengine wa Maendeleo imehakikisha upatikanaji wa matibabu ya Saratani kwa wagonjwa wote kwa ufanisi zaidi. Mwaka 2018, Wizara ilinunua mashine mbili za kisasa za tiba ya Saratani aina ya LINAC zenye thamani ya shilingi bilioni 9.4 na kuzifunga katika Taasisi ya Saratani Ocean Road. 

Mashine hizi zilianza kufanya kazi mwezi Septemba 2018. Hadi kufikia Desemba 2018, jumla ya wagonjwa 109 wametibiwa kwa kutumia mashine hizi na kati ya wagonjwa hawa, wagonjwa 70 wangepelekwa nje ya nchi kwa matibabu endapo mashine hizi zisingekuwepo nchini kwa gharama za wastani wa Shilingi Milioni 50 kila mgonjwa.

Utumiaji wa mashine mpya za LINAC umeokoa Shilingi Bilioni 3.5 katika kipindi cha Septemba hadi Desemba 2018 tu. Pamoja na kuokoa fedha, pia muda wa kusubiri kuanza tiba za mionzi kwa wagonjwa umepungua hadi kuwa chini ya wiki 4; na tunategemea utakuwa chini ya wiki 2 ifikapo Aprili 2019. Mwaka 2015, muda wa kusubiri tiba mionzi ulikuwa wiki 12 na sasa tumeweza kuupunguza hadi kufikia wiki 4.

Serikali katika Mwaka wa fedha wa 2018/2019 imeendelea kuhakikisha upatikanaji wa dawa za tiba ya Saratani kwa kuweka bajeti ya Shilingi bilioni 10, kutoka shilingi milioni 700 mwaka 2015/16 Kutokana na ongezeko hili la fedha, kiwango cha upatikanaji wa dawa za Saratani katika Taasisi ya Saratani Ocean Road ni asilimia 92 kutoka asilimia 4 mwaka 2015. Aidha, mgao wa dawa za Saratani unapelekwa pia katika Hospitali za Bugando na KCMC.

Aidha, Serikali iko kwenye taratibu za kununua mashine ya kisasa ya upimaji wa Saratani aina ya PET Scan kwa thamani ya shilingi bilioni 14 ambayo itafungwa katika Taasisi ya Saratani Ocean Road. Upatikanaji wa kipimo hiki nchini utapunguza gharama zitokanazo na kupeleka wagonjwa nje ya nchi hasa India kwani takriban asilimia 80 ya wagonjwa wa saratani walikuwa wanapelekwa nje ya nchi kwa ajili ya kipimo hiki. 

Hivyo, Serikali itaokoa takriban Shilingi bilioni 5 kwa mwaka zilizokuwa zinatumika kwa ajili ya kulipia wagonjwa kwenda nje kwa kipimo hiki. 

Wastani ya watanzania 500 huenda nje ya nchi kila mwaka kwa ajili ya kipimo cha PET/CT Scan ambapo gharama kwa mgonjwa mmoja inafikia mpaka shilingi 10,000,000 ikijumlisha gharama za safari, malazi, huduma hospitali na kipimo.

Katika jitihada zetu za kuhakikisha upatikanaji wa matibabu ya saratani kwa wananchi wengi zaidi, Serikali imeongeza wigo wa upatikanaji wa matibabu ya Saratani kutoka Hospitali ya Saratani Ocean Road na sasa huduma za matibabu ya Saratani zinapatikana Hospitali ya Kanda Bugando ambayo imefunga mashine ya tiba mionzi ambapo wagonjwa wa Kanda ya Ziwa wanapata huduma za tiba ya mionzi (radiotherapy) Hospitalini hapo sambamba na huduma za matibabu kwa njia ya dawa (Chemotherapy). 

Aidha, Hospitali ya Kanda ya KCMC, Kilimanjaro na Hospitali ya Kanda Mbeya zinatoa huduma ya tiba ya Saratani kwa dawa (Chemotherapy); ambapo hatua inayofuata ni kujenga jengo maalum kwa ajili ya kusimika mashine za mionzi katika Hospitali ya KCMC.

Ili kuwa na mipango bora ya upatikanaji wa fedha za kutoa huduma za saratani hapa nchini, takwimu sahihi zinahitajika. Kuanzia mwezi Juni, mwaka 2018, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeanza kuchukua taarifa za saratani katika hospitali za Ocean Road, KCMC, Bugando, Mbeya na Benjamin Mkapa kwa mfumo uitwao Population-based cancer registry. Mfumo huo utawezesha kutupatia taarifa ya aina na ukubwa wa saratani ya aina fulani, inawapata zaidi jinsia gani, na ipo katika Kanda au Mkoa gani. 

Aidha, mfumo huu utatupa takwimu za uhakika zaidi kuhusu idadi ya watu wanaofariki kila mwaka. Hii itasaidia Serikali katika mipango ya kupambana na saratani.

Saratani haibagui jinsi wala hali ya mtu. Ni vyema kila mmojawetu akapima afya yake mara kwa mara ili kutambua hali yake ya kiafya. 

Endapo mtu atatambuliwa kuwa ana ugonjwa wa Saratani ninamuhimiza kutumia huduma za afya kulingana na ushauri atakaopewa na wataalam wa afya. Kwa wale ambao wameshajitambua kuwa na matatizo ya Saratani lakini hawatumii huduma za afya ipasavyo, nawaasa watumie huduma za afya zilizopo kwa manufaa ya afya zao na kuepusha athari zinazotokana na ugonjwa wa Saratani.

Tunao Mkakati wa Kitaifa wa Kupambana na Saratani (National Cancer Control Strategy wa mwaka 2013-2022, Mkakati wa kisera wa Tiba shufaa wa mwaka 2013 (Palliative Care Policy Guidelines) na Mwongozo wa Kitaifa wa Tiba ya Saratani wa mwaka 2018 (National Cancer Treatment Guidelines) ambao umekamilika na utazinduliwa hivi karibuni.

 Mikakati hii na Mwongozo ni Dira katika kuimarisha huduma za Saratani katika kukinga, kugundua mapema, kutibu, kutoa tiba shufaa na hasa kupanga manunuzi ya Dawa za Saratani kwa kuzingatia hali halisi ya Nchi yetu.

Katika maadhimisho haya ya Siku ya Saratani Duniani, napenda kuchukua fursa hii kuhimiza Watanzania wote kwenda kwenye vituo vya afya kufanya uchunguzi wa Saratani hasa Saratani ya mlango wa Kizazi, Saratani ya Matiti, Tezi dume na saratani nyingine mapema. Kuchelewa kufika Hospitalini huchangia ongezeko la vifo vya saratani. Kwa upande wetu Serikali tutaendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kuhakikisha kuwa huduma za Afya ya saratani zinaboreshwa na zinapatikana karibu zaidi na wananchi. 

Mwaka huu 2019 tutazindua Mwongozo wa Kitaifa wa Tiba ya magonjwa ya Saratani (National Cancer Treatment Guidelines) ambao ndio utatumika nchi nzima kuanzia Zahanati, ikihusisha zaidi huduma za Kinga, hadi kwenye ngazi ya Hospitali za Mikoa na Kanda ambapo huduma za uchunguzi na tiba za saratani zinapatikana na kufikia Hospitali za Kitaifa ambapo huduma za kibingwa za saratani zinapatikana. 

Nachukua fursa hii pia kuwashukuru wadau wote wanaoshirikiana na Serikali katika jitihada za kudhibiti ugonjwa wa Saratani hapa nchini. Ni matarajio yetu kuwa wataendelea kushirikiana nasi katika kudhibiti tatizo la saratani nchini.

Ni Mimi, nitafanya (I am, I will) Binafsi, nitafanya jitihada zote kupunguza janga la Saratani Duniani.

LIVE : Kipindi Cha Maswali Na Majibu Kutoka Bungeni Leo

$
0
0
LIVE :  Kipindi Cha Maswali Na Majibu Kutoka Bungeni  Leo

Rudisha heshima yako Kwa Mpenzi Wako, Mke Wako...Tumia Tiba Hii ya Asili

$
0
0
Rudisha heshima yako sasa kwa kutumia Dawa hii iitwayo SUPER GAFINA, kwa ajili ya nguvu za kiume na NKOLOMIJE ni kwaajili ya kuongeza maumbile.

Kwa mwanaume aliye kamilika anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara mbili ,ila ukiwa unapiga moja tena kwa shida wewe ujue  unamatatizo ya upungufu wa nguvu za kiume.

TIBA YA TATIZO LAKO NI; Dawa iitwayo SUPER GAFINA, dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge na unga wa asili ambavyo havina madhara kwa mtumiaji ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja;-

1).itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuchoka.

2).ltakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15 hadi 20 kwa tendo la kwanza.

3).lnaimarisha uume uliolegea na uliosinyaa na kuupa nguvu maradufu.

Je unamaumbile madogo pamoja na uume mfupi? NKOLOMIJE ni suluisho la tatizo lako. Na ni dawa inayoboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi kuanzia inch. 5 hadi 8 kwa muda mfupi sana .Dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk.30 ukisha tumia guarantee miaka 50  ikishakutibu.

Pia ninatibu;- KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU, MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE ,BP, NK.

IGULYATI, ni dawa ya mvuto wa biashara, kazi,kupandishwa cheo na humfanya mfanyakazi kupendwa na mwajiri wake. Pia humvuta mke,Mme,hawara ,mchumba unae muitaji utampata kwa dk.30 tu na atatulia na kumfunga asitoke nje ya ndoa, Pia natoa Pete za bahati ambazo zimetajirisha wengi.

Pia ipo dawa ya kupunguza matiti,unene ,tumbo,na kitambi ,hupunguza mafuta ,kuondoa makovu,chunusi,michilizi mwilini na kuongeza hipsi, makalio na mguu wa bia nk. 

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR,HOSUTWA .Anapatikana Mbagara

Simu no, 0756241666 na 0672186977.

       Huduma hii utaipata popote ulipo

Je Unaupungufu Wa Nguvu Za Kiume au Maumbile Mafupi na Membamba...Suluhu iko hapa

$
0
0
Acha kusubilia mpaka mke au mpenzi wako akwambie Mme wangu wewe ni dhaifu tuwepo kitandani,unatakiwa ujitambue mapema ,kwa mwanaume aliyekamilika  na mwenye nguvu za kutosha  ili kumridhisha mke au mpenzi wake anatakiwa awe na uwezo wa kurudia zaidi ya Mara mbili lakini kama unakomea moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe tu sio na yeye, ili uwe mwanaume mwenye uwezo kamili tumia dawa yako hii hapa

 SUPER MAJINJAS MIX; dawa hii ni tofauti na ambazo uliwai kutumia inamichanganyo ya miti na matunda zaidi ya saba ndio maana inakupa uwezo wa ,KURUDIA TENDO ZAIDI YA MARA TATU,NA ITAKUFANYA UCHELEWE KUFIKA KILELENI DAKIKA 10-15 KWA TENDO LA KWANZA,NA PIA HUIMALISHA MISULI ILIYOLEGEA NA KUSINYAA KWA WALE AMBAO WALIPIGA SANA PUNYETO,dawa hii ni ya vidonge na unga na haina madhara yoyote

MAKAKANUA NO 5 MPYA; dawa hii uboresha uume saizi upendayo UREFU WA INCHI 5,6,7,NA 8 NA UPANA WA CM 2,3,4 NA 5 dawa hii ipo ya kunywa na kupaka  na pia usahidia zaidi kwa mwanaume aliyefanyia tohara ukubwani,

ISENYE NO 3; hii ni dawa kwa wenye kisukari dozi siku 21 tatizo la kisukari na ndio chazo kikubwa cha kuishia nguvu za kiume,

NGWALUSA ; hii ni dawa ya uzazi ambayo ufungua milija ya uzazi ata kwa wale walifungwa uzazi,zipo dawa za busha,vidonda vya tumbo,miguu au viungo kufa gazi kupungza kitambi,minyama uzembe,na matiti makubwa 

TUNAPATIKANA DARES SALAAMU buguruni na MOROGORO YUPO WAKALA na MWANZA YUPO MTAA WA BIZA C, NA KAHAMA MJINI kwa mawasiliano zaidi piga simu 0744040721, 0683645920 DR BRUNO pia unaweza ukaletewa popote ulipo
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images