Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

PICHA:Rais Magufuli Ahudhuria Mkutano Wa Kawaida Wa 20 Wa Jumuiya Ya Afrika Mashariki Jijini Arusha

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongozana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Liberat  Mfumukeko na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo wakati alipowasili katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) kuhudhuria Mkutano wa Kawaida wa 20 wa Viongozi wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha leo Ijumaa Februari 1, 2019.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akisalimiana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Burundi Mhe. Gaston Sindimo alipowasili katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) kuhudhuria Mkutano wa Kawaida wa 20 wa Viongozi wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha leo Ijumaa Februari 1, 2019.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudani ya Kusini Mhe. Barnaba Marial Benjamin akiwa na Balozi wa Nchi hiyo nchini Mhe. Mariano Deng Ngor wakati alipowasili katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) kuhudhuria Mkutano wa Kawaida wa 20 wa Viongozi wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha leo Ijumaa Februari 1, 2019.
  Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akilakiwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Liberat Mfumukeko na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo wakati alipowasili katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) kuhudhuria Mkutano wa Kawaida wa 20 wa Viongozi wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha leo Ijumaa Februari 1, 2019.
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwa na Rais Paul Kagame wa Rwanda wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) muda mfupi kabla ya kuanza kwa  Mkutano wa Kawaida wa 20 wa Viongozi wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha leo Ijumaa Februari 1, 2019.
   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akisalimiana na Rais wa Kenya Mhe. Uhuru Kenyatta alipowasili katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) kabla ya kuanza kwa  Mkutano wa Kawaida wa 20 wa Viongozi wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha leo Ijumaa Februari 1, 2019.
   Rais wa Uganda Mhe. Yowweri Kaguta Museveni akilakiwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Liberat Mfumukeko na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo wakati alipowasili katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) kuhudhuria Mkutano wa Kawaida wa 20 wa Viongozi wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha leo Ijumaa Februari 1, 2019.
  Sehemu ya Ujumbe wa Tanzania katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC) wakihudhuria Mkutano wa Kawaida wa 20 wa Viongozi wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki jijini Arusha leo Ijumaa Februari 1, 2019. Picha na IKULU

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

Usiteseke Tena na Matatizo ya Nguvu za Kiume.....Tumia Tiba Hii ya Asili

$
0
0
SUPER MKUNYATI MIX; ni dawa bora ya mitishamba iliyopo katika mfumo wa vidonge na unga yenye uwezo wa kutibu na kumaliza matatizo yote ya ukosefu wa nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile:-

  -kuwai kufika kileleni ndani ya dakika chache tu.
 -Kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa muda mrefu.
 -Kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu(punyeto) husababisha kuishiwa au kupungukiwa na nguvu za kiume.
 -Uume kusimama kwa kulegea au katikati ya tendo la ndoa unalala na kushindwa kusimama.

Epuka matatizo haya kwa kutumia dawa bora ya asili ya SUPER MKUNYATI MIX ni kiboko ya matatizo haya yanayowasumbua baadhi ya wanaume wengi.

Pia kuna dawa ya kutibu Presha,miguu kufa ganzi, tumbo kuuma chini ya kitovu, kisukari,ngiri, chango aina zote na nk, matatizo haya nayo uchangia matatizo haya ya ukosefu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile madogo na uume mfupi.

KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA MAUMBILE MADOGO NA UUME MFUPI?  Usikate tamaa ondoa maradhi yako  hayo maana matatizo haya yamekuwa yakiathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti na sana na wanaume wengine kwa kushindwa kumlizisha mwanamke.


MDINDADINDA MIX, ni dawa ambayo inarefusha na kunenepesha maumbile na itakufanya uwe na uume saizi uipendayo.Dawa hizi za asili za mitishamba zipo katika mfumo wa vidonge na unga na hazina madhara kwa mtumiaji.

JABABILA;- ni dawa ya mvuto wa mapenzi ,mchumba, mke, mume aliyekuacha atakurudia ndani ya siku moja tu na atakutimizia utakacho.

ITALIGULA;- ni dawa ya biashara  na hata kama umezurumiwa utalipwa mapema ,kupata kazi, kupanda cheo. Ofisi zetu zinapatikana DAR ES SALAAM, SONGEA - BOMBAMBILI, SHINYANGA - KAHAMA MJINI. na pote pale ulipo utaipata huduma hii,kama huna nafasi utaletewa hulipo.Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR. MACHIMKENDA simu no ,0717 339771

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 64

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA
       
Akanikabidhi simu yake ya kiganjani.
“Ya nini?”
“Zungumza na huyu mtu”
Nikaiweka simu yangu sikioni.
“Nashukuru sana kwa kurudi Ujerumani. Ulihisi unaweza kulikimbia ili. Tunahitaji BOKSI JEUSI haraka iwezekanavyo kabla ya hatujaharibu msiba wa mama yako”
Maneno ya mwanaume huyu yakanistua sana, jamaa huyu aliye simama eneo hili taratibu akafungua koti lake na kunionyesha bastola aliyo ichomeka kiunoni mwake akiashiria kwamba nikifanya jambo lolote la kijinga anaweza kuniua hapa hapa.

ENDELEA
Nikashusha pumzi taratibu huku nikimtazama jamaa huyu usoni mwake. Kwa ishara ya macho akaanza kunionyesha wingi wa vijana alio ambatana nao kwenye nyumba hii. Wingi wa vijana hawa wanaweza kumua mtu yoyote humu ndani.  Nikamuona Camila akija eneo nililo simama kwa kasi, jamaa huyu akaliweka sawa koti lake ili bastola yake isiweze kuonekana.
 
“Nimekuelewa, nitajitahidi kukupatia. Nipeni muda”
“Sawa sawa bwana Ethan. Tunamuona mrembo wako anakuja hapo. Angalia usije ukampoteza”
Mwnaaume huyo aliendelea kuzungumza jambo lilio nifanye nizidi kupatwa na wasiwasi.
“Sawa sawa usijali katika hilo”
Simu ikakatwa na nikamkabidhi kijana huyu na akaondoka.
“Ulikuwa unazungumza na nani mume wangu?”
“Ahaa, kuna mfanya biashara mmoja alikuwa akinipa pole sasa ametuma wawakilishi wake hapa nyumbani”
Nilizungumza huku nikiwa na wasiwasi mkubwa sana.
“Mbona kama una wasiwasi mume wangu?”
 
“Hakuna”
“Kuna hii video mume wangu. Huwezi amini kumbe yule Dany ni gaidi yule ambaye nilisha wahi kumsikia sikia kwenye historia ya magaidi wa dunia”
Camila alizungumza huku akinionyesha video hii inayo muonyesha Dany tuliye muacha nchini Tanzania na alikuwa ni msaada mkubwa sana kwetu hadi baadhi ya mazoezi amemfundisha mke wangu. Maneno ya vitisho anayo yazungumza Dany juu ya nchi ya Marekani yakaniacha mdomo wazi.
 
“Mbona hata haonekani kama ni gaidi?”
“Hata mimi mume wangu sielewi. Yaani huwezi kuamini kama ni gaidi, kuishi nasi vizuri kutusaidia kumbe ndio yule Dany halisi”
“Oooh Mungu wangu hali ya dunia inakwenda kuwa mbaya mke wangu”
“Ni kweli, sijui hili tatizo tunaweza kulitatua vipi kwa maana hii ni vita mume wangu”
Nikajikuta nikiguna huku nikimtazama Camila usoni mwake. Nikatamani kujizuia kumuambia Camila kuhusiana na vitisho ambayo nilipewa na mtu nisiye mfahamu ila nikajikuta nikizungumza tu.
“Mke wangu tuta tatizo?”
“Tatizo gani?”
“Eneo zima hili la hapa nyumbani. Limezungukwa na watu ambao wanahitaji kutuangamiza, usiangalie nyuma kwa maana wana tufwatilia”
Nilimzuia Camila kugeuza shingo yake ili kuweza kutazama watu hao walipo.
 
“Kutuangamiza kwa nini?”
“Wanahitaji boksi jeusi. Hili sekeseka la Dany na Marekani nina imani kwamba linaweza kuwasukuma watu hawa kuzidi kutushinikiza kuhakikisha kwamba tunalitoa boksi hilo jeusi”
“Ohoo Mungu wangu. Kwani boksi hilo jeusi wewe unalifahamu?”
“Sijawahi kuliona kwenye maisha yangu, ila mwanasheria alisha wahi kuniambia kwamba baba ameliacha sehemu na kuna maelekezo ambayo yapo kwenye mwili wangu na unakumbuka ulisha wahi kunichana ila ukakosa?”
 
“Ndio”
Camila alinijibu kwa unyonge kwani tukio hilo alilifanya kwa uadui mkubwa kati yangu mimi na yeye.
“Mambo ndivyo jinsi yalivyo mpenzi wangu, mimi wewe, Mery ndani huko sote hatupo salama”
“Hiyo kazi naomba uweze kuniachia mimi”
“Kazi gani?”
“Kazi ya kushuhulika na hao watu.”
“Utawafahamu vipi?”
“Dany alinifundisha uwezo mkubwa sana wa kuweza kuwafahamu maadui zangu. Nina imani kwamba nitawafahamu mmoja baada ya mwengine taratibu. Jambo la kufanya hakikisha kwamba huonyeshi wasiwasi wowote kwa mtu wa aina yoyote kwamab kuna jambo baya limepangwa kufanywa hapa nyumbani”
 
“Sawa mke wangu”
“Ngoja nijaribu basi kumtafuta Dany kama nitaweza kuzungumza naye nitamuomba aweze kusitisha mpango wake wa kwenda kuishambulia Marekani”
“Sawa mke wangu”
Camila akanibusu mdomoni kisha akaondoka eneo hili, nikarudi eneo walipo kina Frenando na nikaendelea kuzungumza nao mambo mawili matatu kisha nikachukua kombe walilo niletea na kuelekea ndani. Nikiwa ninapandisha ngazi za kuelekea gorofani, Camila akanifwata kwa nyuma na tukaingia kwa pamoja ndani huku akionekana ana habari anayo hitaji kunieleza.
“Tumewapata maadui wote”
“Wapo wangapi?”
 
“Hapa nyumbani wapo ishini na mbili”
Camila alizungumza huku akianza kunionyesha picha za watu hao. Nilamuamini sana juu ya upelelezi wake mara ya kumuona kijana ambaye amenikabidhi simu nizungumze na bosi wake.
“Eeehe tunafanyaje juu ya hawa watu?”
“Tunamuangamiza mmoja baada ya mwengine tena kimya kimya. Kisha yule kijana ndio atakuwa wamwisho yeye atatupeleka walipo wenzake”
“Hili swala inabidi uwe makini sana mpenzi wangu”
“Usijali, nina jiamini na nina uwezo mkubwa zaidi ya unavyo fikiria. Ila sijajua kwa upende wangu wewe mwenzangu”
 
“Unapnaje tukamueleza baba yako?”
“Ethan hili ni jambo la sisi wawili. Hakuna kumuambia mtu. Hapa ninasimama kama mke wako, baab yeye naye anamajukumu yake bwana”
“Nimekuelewa mke wangu”
Camila akanisogelea taratibu na kunibusu mdomoni mwanngu. Tukatazamana kwa sekunde kadhaa huku kila mmoja akisikilizia msisimko wa mwenzake. Tukaanza kunyonyana midomo yetu huku taratubu nikirudi nyuma nyuma na tukaingia bafuni kwani kufanya mapenzi katika chumba chetu kunaweza kuwafanya watu watakao pita nje ya mlango wetu kuweza kusikia kelele zetu za mahaba.
 

 

Camila alizungumza huku akikizungusha kiuno chake, unaweza kuhisi si mtoto wa Kijerumani vile na ni mswahili halisi aliye zaliwa katika kabila la wadigo ama wazaramo.
 
Tukajikuta kwa pamoja tukiimaliza safari yetu ya mapenzi, huku kila mmoja akisikilizia utamu wa viungo vyake.
“Ahaa…nilikuwa na hamu na wewe mume wangu”
“Hata mimi mke wangu”
“Sasa hapa kiu kidogo imepungua, nina imani kwamba ninaweza kwenda kufanya jambo sasa juu ya hawa washenzi”
Camila alizungumza huku  akijichomoa taratibu kwenye jogoo wangu. Akakaa kwenye choo hichi cha kukaa, akachukua toilet paper na kuanza kujifuta taratibu
 
Tulipo hakikisha kwamba viongo vyetu vipo salama. Kila mmoja akajiweka sawa nguo yake, tukatoka bafuni humu, tukajipulizia perfume kisha tukaendelea na mipango ya mazishi ya bi Jane Klopp. Wachezaji wa zamani ambao walicheza na mzee Klopp nao wakazidi kufika katika msiba huu kutoa pole ya kuondokewa na mama yetu.
 
Majira ya saa moja kasoro usiku, Camila akaniomba tuelekea kwenye moja ya chumba cha chini ya ardhi katika hii nyumba yetu. Nikaongozana naye na kuingia kwenye chumba hicho, sikuamini macho yangu mara ya kuwakuta watu wote ambao alinionyesha wakiwa wamelala chini.
 
“Umewaua hawa?”
“Hapana hakuna niliye muua. Ila kuna sumu fulani ya kisindano Dany alinifundisha nimeweza kuwashoma mmoja baada y mwengine na nimeweza kuwaleta hapa”
“Ehee huyu ndio kijana ambaye ameniletea simu yake nizungumza na bosi wake.”
“Simu yake hii hapa ninayo na nimeweza kuangalia muda ule ni nani aliweza kumpigia nimeweza kupata ni nani uliye zungumza naye”
“Ni nani?”
Camila akanionyesha picha ya mwanaume mmoja ambaye kwa haraka sana niliweza kumfahamu kwani ni miongoni mwa watu nilio kutana nao kikao cha siri nilicho fanya na viongozi wa chama cha upinzani nchini Tanzania.

==>>ITAENDELEA KESHO

Dalili za Mimba Kuharibika

$
0
0
Kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha mama mjamzito mimba yake kuharibika. Sababu kuu huwa ni magonjwa kama vile ugonjwa hatari wa malaria, ugonjwa unaotokana na zinaa kama vile kaswende na kisonono na U.T.I, dawa fulani fulani mfano Albendazole, Misoprostol, Metronidazole na kadhalika.

Lakini pia mjamzito akifanya kazi za kutumia nguvu nyingi anaweza kusababisha mimba yake kuharibika. Lakini kuna sababu nyingi ambazo zinasababisha mimba kutoka huweza kuzuilika kwa kwenda kliniki mapema yaani pale tu unapohisi una mimba hata kama ni wiki mbili na kufuata ushauri wa wataalamu.

Ukweli ni kwamba kuna wanawake wengi mimba zao huharibika na wao hushindwa kugundua mapema na matokeo yake anakaa na mtoto mfu hata miezi kadhaa bila kujua.

DALILI ZA MIMBA KUHARIBIKA
Zipo dalili ambazo husababisha mimba kuharibika kama tutakavyoona leo hapa. Dalili hizo ni hizi zifuatazo:

KUTOKA DAMU NYINGI SEHEMU ZA SIRI
Mjamzito akitokwa na damu nyingi sehemu za siri ni dalili kwamba mimba imeanza kuachia na mlango wa uzazi umeanza kufunguka, na hiyo inaashiria kwamba kuna mambo mawili yameshatokea kwanza inawezekana mtoto ameshafia tumboni au bado hajafa, lakini kama damu imetoka kwa wingi inaashiria kuwa mtoto huyo aliye tumboni atakufa tu.

MTOTO KUACHA KUCHEZA TUMBONI
Ikiwa mtoto ataacha kucheza tumboni ni tatizo kubwa kwani kwa kawaida mtoto huanza kucheza akiwa na wiki ya 18 mpaka 20 kwa wanawake ambao hawajawahi kubeba mimba na wiki ya 16 mpaka 20 kwa wanawake ambao wameshawahi kuzaa. Ikitokea mtoto aliye tumboni ameshawahi kucheza lakini ghafla akawa hachezi au muda huo umepitiliza na bado kimya kuna uwezekano mkubwa ikawa mtoto huyo amefia tumboni, hivyo haraka sana wahi hospitali kumuona daktari.

KUPOTEA KWA DALILI ZA UJAUZITO
Kupotea kwa dalili za ujauzito ni tatizo lingine baya kwa mama mjamzito. Mara kwa mara mwanamke akiwa na ujauzito anakuwa na dalili nyingi kama vile kuwa na kichefuchefu, kukosa hamu ya kula baadhi ya vyakula, kutapika, kulamba vitu vichachu kama vile limao, ndimu, wengine hula udogo na wengi hubadilika sana tabia, hivyo basi dalili zote hizo za mimba zikisimama ghafla basi ujue mimba imeharibika. 

MIMBA KUTOKUA 
Ikiwa mimba itaacha kuongezeka au kukua ni dalili nyingine ya mimba kuharibika. Kila mtu aliye mjamzito anategemea mimba iwe inakua kila siku  na iwe kubwa kulingana na umri unavyozidi kwenda mbele, ikiwa mimba iko vilevile kwa miezi kadhaa, yaani haikui au ukubwa wa tumbo haubadiliki ujue kwamba mimba hiyo imeharibika, ili kupata uhakika wahi hospitali kupimwa.

TUMBO KUWA NA MAUMIVU MAKALI
Ikiwa mjamzito atakuwa ana maumivu makali ya tumbo wakati ni mjamzito hiyo pia ni dalili mbaya. Kwa kawaida maumivu makali ya tumbo hasa kwa mimba kubwa ya miezi zaidi ya mitano au mimba ndogo kama mwezi mmoja, basi kuna uwezekano mkubwa kondo imeanza kujiondoa kwenye kizazi kwa mimba kubwa au mimba ndogo imeshindwa kuendelea kukua na moja kwa moja hiyo inaweza kuwa dalili ya kuwa mimba imeharibika.

KUTOKA VIPANDE VYA NYAMA SEHEMU ZA SIRI
Ikiwa mama mjamzito atakuwa akitokwa na vipande vya nyama sehemu za siri ni dalili mbaya sana. Kutokwa na vipande vya nyama sirini ni kuashiria kwamba kuna mtoto ameharibika tumboni. Hali hiyo ya hatari ikitokea mjamzito anatakiwa asafishwe kuondoa masalio yaliyobaki.

Kangi Lugola: Hakuna Atakayesalimika Mauaji ya Wazee Nchini

$
0
0
Na Mwandishi wetu Dodoma
Waziri Mambo ya Ndani Kangi Lugola ametoa wito kwa vijana wote nchini kuachana na tabia ya mauaji ya vikongwe na Wazee Nchini na kutoa onyo kwamba hakuna muuaji hata mmoja atakaye salimika na kukwepa mkono wa sheria.

Amesema hayo leo jijini Dodoma katika hotuba yake ya ufunguzi wa kikao kazi kilichowakutanisha wazee makamanda wa jeshi la polisi na maofisa Ustawi wa Jamii kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa kujadiliana kwa pamoja kuhusu mbinu mpya za kutokomeza mauaji hayo kwa kutumia Mkakati mpya wa miaka 5 wa  Kutokomeza Mauji ya Wazee na Vikongwe Nchini.

Mkakati huo uliozinduliwa rasmi na Waziri Mkuu wa Tanzania tarehe 29, January 2019 wakati wa Mkutano wa Mwaka wa Maafisa Ustawi wa Jamii Nchini uliofanyika Jijini Dodoma.

Aidha Waziri Lugola amewataka vijana kutambua kuwa kijana wa leo ni Mzee wa Kesho hivyo atambue kuwa machungu ya mauaji ya wazee wanayoyapata leo naye ayatarajie baadae kwa kuwa kila mtu atazeeka.

Kufuatia hali hiyo Waziri Lugola aliwataka Vijana  kutunza wazee wao kwasasababu machozi ya wazee wanayolia kila siku kwa kwa kukosa matunzo ya watoto wao yanapelekea wazee wengi kuwa na macho mekundu yanayoplekea watu wenye imani potofu  kuwapoteza maisha yao kwa imani za kishirikina.

Aliongea kuhusu Mkakati wa Kutokomeza Mauaji ya Wazee Waziri Nchini Lugola alisema lengo la mkakati huu ni kuhakikisha tunashirikiana ili ifikapo mwaka 2023 mauaji ya wazee yawe yamekomeshwa kabisa.

”Hatutakua na sababu yoyote ya kueleza tukishindwa kutekeleza wajibu huu muhimu wa kulinda uhai wa kundi hili tete. Naomba muongeze kasi ili tufikie lengo hili, tena ikiwezekana mapema zaidi kwani tutapimwa kwalo 2023’’. Aliongeza Mhe. Lugola.

Alitoa wito kwa vyombo vya dola hasa Jeshi la polisi kuendelea kufuatilia kwa ukaribu sababu na vichocheo vya mauaji haya ikiwa ni pamoja na kuwabaini wahusika wanaopanga na kutekeleza mauaji haya ili wafikishwe kwenye vyombo vya Sheria, na pale inapothibika wahusika wachukuliwe hatua kali ili tukomesha kabisa vitendo hivi vya kikatili. 

Wakati huo huo Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Idara Kuu Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu aliwaambia wajumbe wa Mkutano kuwa mahuaji ya vikongwe yalianza tangu miaka ya 1960 na serikali imekuwa ikipambana nayo lakini yamekuwa yakiendelea.

Dkt. Jingu aliongeza kuwa jughudi za serikali kupitia Jeshi la Polisi zimefanikiwa kupunguza mauaji haya lakini hayajakwisha kwasababu bado kuna watu wengi wenye Imani potofu katika Jamii hivyo ni lazima mapambano dhidi yao yaendelee.

Alisema kuwa Mkakati wa Kutokomeza Mauaji dhidi ya Wazee unalenga kuwa na Taifa linaloazingatia haki na ustawi wa wazee kwa kupiga vita imani za kushirikina, ubaguzi, ukatili na mauaji.

Aidha Dkt. Jingu aliongeza kuwa tafiti zilizopo zinaonesha  mauaji na ukatili dhidi ya Wazee yanachochewa na Imani za kishirikina pamoja na migogoro ya ardhi hivyo serikali kwa kushirikiana na wadau imeandaa Mkakati wa Kutokomeza Mauaji ya Wazee Nchini kwa lengo la kutokomeza kabisa mauaji haya.

Je Kwanini Baadhi Ya Wanaume Wengi Wana Ukosefu Ama Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
JE KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UKOSEFU AMA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO ???

Pata sululisho la matatizo haya na  magonjwa mengine utapona kwa mda mfupi sana hatakama ulihangaika mpaka ukakata tamaaa 

GALIMBO 3 MIX  ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa aina mbili ili kukidhi mahitaji ya mtumiaji, imetengenezwa kwa muundo wa vidonge pamoja na unga kwaajili ya kuponesha tatizo moja kwa moja , huimalisha misuli ya uume iliyolegea wakato wa tendo la mdoa ,na kukufanya ucherewe kufika kileleni kwa mda wa dk ( 20 - 45 ) itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu nira hamu kuisha wara kuhisi kuchoka vilivile huzalisha viini vya uzazi ( manii ) 

YOLAN  hurefusha na kunenepesha  maumbile madogo ya uume na kuwa na uume kuanzia nchi (6-8) tiba kwa mda mfupi sana

Zipo sananu nyingi sana zinazosababisha matatizo hayo  km vile -:punyeto, kisukali,ngili,chango,vidonda vya tumbo,  tumbo kuunguluma na kujaa gesi maumivu ya mgongo ama kiume ,kolodani moja kuvimba ama kuingia ndani  presha nk 

Matatizo haya yote sio mageni, kigeni ni tiba sahihi ya kuponesha matatizo hayo

SUPER MBUKE -:  nidawa ya kuponesha tatizo la kisukali kwa mda mfupi sana , usihangaike wara kuteseka tumia dawa ya mitishamba kwaajili ya tatizo hili na upone kabisa

NTINJIWA  nidawa ya mvuto wa biashara,kazi, kupandishwa cheo,kumfanya mfanyakazi apendwe na bos wake

Pia ninadawa za kumvuta mme , mke,mchumba,hawara, au mtu yoyote unaemuhitaji katika maisha yako hata km yupo mbali na atatulia na kukutimizia cjovjote utakacho na kumfunga asiwe na mtu mwingime ,

Pata tiba za magonjwa mbalimbali ikiwemo miguu kuwaka moto, mgongo,bawasili ,kaswende ,gono na mengine mengi

KWAUSHAULI NA TIBA WASILIANA NA DR CHIKAGO    0759 208 637

Km huna nafasi ya kufika ofisini hudumahii utaletewa hapo ulipo , kwa wale wa mikoani natuma kwanjia ya basi

Mchungaji atuhumiwa kufanya mapenzi na mtoto wa Mchungaji Mwenzake

$
0
0

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mjini Richard Kasesela amelishauri Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT Dayosisi ya Iringa kumuondoa kutomfumbia macho aliyekuwa Msaidizi wa Askofu wa Dayosisi hiyo mchungaji Yusto Kinyori kwa tuhuma za ya kufanya mapenzi na mtoto wa mchungaji mwenzake kwenye gari.

Kasesela amesema hayo kwenye Mkutano Mkuu wa kumchagua Msaidizi wa Askofu wa kanisa hilo uliofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania KKKT usharika wa Ipogolo ambapo amesema kuwa anayo video clip ikionesha mchungaji huyo akifanya mapenzi kwenye gari na mtoto wa mchungaji mwenzake.

Kasesela amesema kuwa kinachomuuma zaidi viongozi wa dini ndiyo wanaotumwa kwenda serikali kuwawakilisha baadhi ya viongozi au kutoa matamko mbalimbali kwa niaba ya kanisa lakini kiongozi huyo amekengeuka kwa sababu ya kitendo alichokifanya na kushauri kanisa limuondoe haraka kwa sababu analiaibisha kanisa.

Kwa upande wake Askofu wa Kanisa hilo Dayosisi ya Iringa Mchungaji Blastone Gavile amesema mkutano huo maalumu umefanyika kutokana na vikao vilivyofanyika mwishoni mwa mwakajana kujadili ofisi ya msaidizi wa askofu kutokana na tuhuma zilizokuwa zikimkabili.

Mara baada ya kufanya uchaguzi huo walimpata msaidizi wa askofu Askari Mgeyekwa ambaye alikuwa mkuu wa KKKT usharika wa Kihesa na ameibuka kidedea kwa kupata kura 480.

Je, ni sahihi kufanya mapenzi wakati mkeo akiwa na MIMBA?. Je, mimba yaweza kutoka? Vipi kuhusu afya ya mtoto tumboni..BOFYA HAPA NIKUPEKULIE

$
0
0
Ni kawaida kwa mwanaadamu aliye mzima kupenda kuwa na mtoto, na kwa namna ya upekee katika kuumbwa kwa mwanaadamu, hakuna njia nyingine yoyote ile ambako mtoto anaweza kupatikana bila ya maingiliano ya kimwili baina ya watu wa jinsia mbili tofauti (ukiachilia mbali instances chache ambapo mambo ya test tube na artificial insemination hutumika).

Kifupi ni kwamba, kama mwanamke atataka kubeba ujauzito ni lazima akubali kuingiliwa, Vivyo  hivyo kama mwanaume anataka kumbebesha mwenza wake ujauzito ni lazima ahakikishe kuwa amemwiligilia mke

Hata hivyo, licha ya ukweli wa kuwa ili ujauzito upatikane ni lazima kuwe na kufanya mapenzi, kumekuwa na mkanganyiko sana juu ya tendo hili la kufanya mapenzi  pindi inapotokea mwanamke ameshashika ujauzito.

Je, ni sahihi kufanya mapenzi wakati mwanamke ni mjamzito?
Je, ni hadi muda gani kabla ya kujifungua, ambapo mwanamke mjamzito anaweza kuwa anaingiliwa kimwili na mwenza wake?

Kwa maswali haya na mengine kadhaa, hebu twende pamoja mdogo mdogo kama ifuatavyo:-

(1).  Je, ni sahihi kufanya mapenzi ikiwa mwanamke ni mjamzito?
Ndio, hakuna tatizo lolote kwa mwanamke kuendelea kufurahia maisha ya kutiana na mumewe au mpenzi wake wakati anapokuwa yu mjamzito. 
 
 Wataalamu wanaeleza kuwa, ikiwa ujauzito ulioubeba haukupi shida yoyote ile na unajisikia uko poa, basi hakuna hatari yoyote ile ikiwa utataka kufanya.

Tatizo pekee ambalo huwa linawakumba wengi wa wanawake wakiwa wajawazito ni kuwa, huwa wanapoteza hamu ya tendo lenyewe wanapokuwa katika hali hii, au kushindwa kumudu kutokana na kujisikia uchovu muda mwingi.

Ingawa pia wapo wanawake ambao wakiwa katika hali hii ndio kwanza, wanakuwa wanajisikia kukereketwa kupita maelezo, na wanatamani muda wote wafanye mapenzi.

Wapo baadhi ya wanawake ambao wanakuwa wako normal kimwili, lakini kisaikolojia wanakuwa na ile hofu ya kuwa kufanya kunaweza kuwaharibia mimba zao, fikra ambazo huwatoa kabisa katika mstari wa kufurahia tendo hili.

Kwa hiyo, ikiwa mwili wako uko poa, na madaktari wamekwambia kiumbe kinakua bila shaka, na unaweza kwenda kazini, huna haja ya kujibania utamu wa mumeo au kumbania mumeo.

(2). Je, kufanya wakati wa ujauzito kunaweza kusababisha ujauzito kuharibika?
Hili pia ni miongoni mwa maswali na hali ambazo zimekuwa zikiwachanganya watu wengi, waume kwa wanawake.
Ila ukweli ni kwamba, kufanya hakuhusiani na kuharibika kwa mimba au kujifungua kabla ya wakati muafaka.

 Kwa kawaida, kuharibika kwa mimba hutokana na sababu zingine tofauti kabisa, ikiwa ni pamoja na kizazi cha mwanamke kuwa na matatizo hasa katika kuhimili ukuaji wa kiumbe tumboni na sababu zingine za kimazingira.

Wala sio kwa sababu ya kitu ambacho unakifanya au hukifanyi.

(3). Je, kufanya wakati wa ujauzito kunaharibu au kumdhuru mtoto?
Kiumbe kilicho tumboni wakati wa ujauzito huwa kinakingwa na ute maalum unaojulikana kitaalamu kwa jina la "amniotic fluid" ndani ya mji wa uzazi, pamoja na kuta za mji wenyewe wa uzazi.

Hakuna namna ambavyo muhogo unaweza kupita na kufika mahali mtoto anapokuwa anakua huko ndani, au zile mbegu kuwa zitapita moja kwa moja na kwenda kumdhuru mtoto.

 Kumekuwa na ule msemo wa kuwa kufanya wakati wa ujauzito ni kulea mimba, watu wakiamini kuwa mbegu huwa zinakwenda moja kwa moja kwenye kiumbe.

 Dhana hii ni potofu. Kama kilivyo chakula cha kawaida mtu anapokula, ndivyo ambavyo mbegu nazo huwa hivyo.

Kila kitu kwanza lazima kiingie katika mfumo wa kawaida wa usafirishaji wa virutubisho vilivyo sahihi kuelekea kwenye kiumbe husika.

 Hii ikimaanisha kuwa mbegu nazo huingia katika mfumo huo huo, huchujwa na kile kinachoonekana kuwa ni kirutubisho kitasafirishwa kwenda kulea kiumbe, ilhali yale makapi lazima yatatoka.

 Tofauti pekee hapa ni kuwa, "mbegu  za kiume  zina protini  nyingi", hii ikimaanisha kuwa sehemu kubwa ya kile kinachomwagwa kwenye uke wa mjamzito, kina nafasi ya kutumika kwa ajili ya kuongeza rutuba kwa kiumbe kinachokuaa ndani ya tumbo.

 Na nyingine zinaweza kutoka tu zenyewe bila matatizo yo yote.

(4). Ni mikao ipi (staili) ambayo ni mizuri zaidi kuitumia kufanya wakati wa ujauzito?
Hakuna mkao maalum. Ujauzito sio ulemavu kwamba mnalazimika kujipanga upya namna ya kuridhishana, wala sio ugonjwa pia.

 Ikiwa mwanamke unajihisi uko fresh kuendelea kutumia staili ya mwanzo ambayo mlikuwa mnaitumia na unafikishwa na mwenzio, huku huyo mwenzio naye akiwa yuko ok kuitumia staili hiyo na anaimudu hata unapokuwa na tumbo lako, hakuna  shida

 Jichumishe mboga, jifanye mbuzi ulogoma kwenda, jifanye namna yoyote ile unayoona uko poa, na mambo yatakuwa vizuri.

(5). Kuna umuhimu wa kutumia kondomu?
Kama nilivyodokeza hapo awali, wakati wa ujauzito uch** wa mwanamke unakuwa sensitive zaidi kwa magonjwa.
 Unaweza tu kuguswa na mwenzako ambaye hakuwa amenawa mikono uzuri na ikakusababishia tatizo fulani, hivyo basi, inashauriwa kutumia kondomu ikiwa:
  1. mwenza wako aliwahi au ana maradhi ya maambukizi
  2.  uko kwenye mahusiano na zaidi ya mtu mmoja
  3. umeamua kungonoka na king'asti kipya wakati wa ujauzito
(7). Je, kukojoa au ku-squi*t mara kwa mara kunaweza haribu mimba?
Hapana. Licha ya ukweli kuwa wakati wa ujauzito uke huzalisha kemikali ambazo ni mahususi kwa ajili ya kumkinga mjamzito na uvamizi wa bakteria wowote wanaoweza kuwa tishio kwa ujauzito wake, na kwamba kemikali hizi wakati mwingine huweza kuhitilafiana na lile bao analopiga mwanamke na hivyo kumletea hali fulani ya kukwaza, kwa ujumla wake hakuna baya linaloweza kusababishwa na kukojoa au kufika kileleni .

Na wala kufanya mapenzi hakuwezi kuathiri kwa namna yoyote ile muda wako wa kujifungua (kuuchelewesha au kuuwahisha)

(7). Je, ni wakati gani mwanamke mjamzito anatakiwa kuacha kufanywa?
Ijapokuwa wapo wanawake wengi ambao wanaweza kabisa kuendelea kufurahia kufanywa hadi siku wanakwenda kujifungua , kuna baadhi ya nyakati mshauri wako wa afya anaweza kukushauri kuacha ngono kutokana na moja au yote kati ya yafuatayo:
  1. umekuwa na tatizo la kujifungua kabla ya muda muafaka kabla ya ujauzito ulio nao
  2. umetokewa na tatizo la kutokwa na damu kwenye uke
  3. umekuwa ukitokwa na ute fulani ambao wataalamu wanauita kwa jina la "amniotic fluid"
  4. umekuwa na tatizo la kwenye mlango wa uzazi, ambalo kitaalamu linajulikana kama cervical incompetence
  5.  kondo la nyuma limesambaa na kuziba kabisa mlango wa uzazi na kuanza kujitokeza kwa nje (placenta previa)
(8). Je, kuna tatizo lolote ikiwa huhitaji kufanya?
Hapana, na hii ni hali ya kawaida sana kwa baadhi ya wanawake wanapokuwa wajawazito, ama kutokana na hofu inayokuwa vichwani mwao kuwa atapata madhara kwa kufanya hivyo, au kutokana tu na aina ya homoni zinazozalishwa mwilini wakati huo.

Kuna mengi mnaweza kufanya bila kuhusisha maingiliano ya kimwili na ambayo yanaweza kumfanya mwanamke kuridhika anapokuwa katika hali hiyo.

(10). Ni baada ya muda gani toka kujifungua mwanamke anaweza kuendelea kufanyana?
Iwe kwa njia ya upasuaji au kwa njia ya kawaida, inaeleweka wazi kuwa baada ya kujifungua, mwanamke anakuwa na hali fulani ya mwili kuchoka, hali ambayo ni ya kawaida.

 Ingawa wapo ambao wanaweza kujihisi wanamudu kushiriki tendo la ndoa kabla, lakini wataalamu wanashauri kuwa wakati mzuri wa kurejea kufanyana na mwenzio baada ya kujifungua, inakuwa ni baada ya kupita wiki sita.

Tupe Maoni Yako Hapo chini.....

Kagame Ateuliwa kuwa mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)

$
0
0
 Rais wa Rwanda, Paul Kagame leo Ijumaa Februari Mosi, 2019 ameteuliwa kuwa mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Rais Kagame amechukuwa nafasi ya Rais wa Uganda, Yoweri Museveni aliyemaliza muda wake.

Akizungumza leo jioni baada ya kutangazwa kwake katika mkutano wa wakuu wa nchi za jumuiya hiyo unaofanyika jijini Arusha nchini Tanzania, Kagame amesema ataitumikia vyema jumuiya hiyo.

Kagera Yatengewa Hekta 58,000 Kwa Ajili Ya Viwanda

$
0
0
Na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Serikali imeeleza kuwa mikakati inayoendelea kutekelezwa na kuratibiwa katika Mkoa wa Kagera  ni pamoja na kutenga maeneo ya uwekezaji yenye ukubwa wa hekta 58,000 kwa ajili ya kuanzisha viwanda vya kusindika na kuongeza thamani ya mazao ya kilimo (Agro Processing Industries) hususani viwanda vya kusindika nyama, maziwa, asali, ndizi, miwa, kahawa na samaki.

Hayo yameelezwa Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji, alipokua akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalaum Mhe. Halima Bulembo, aliyeuliza mkakati wa Serikali wa kuwa na miradi maalum ya kuondoa umasikini kwa Watu wa Kagera ambao ndio Mkoa pekee unaopakana na nchi nyingi zaidi za EAC na hivyo kuufanya kuwa Mkoa wa kimkakati kibiashara.

Alivitaja baadhi ya viwanda hivyo kuwa ni Kagera Fish Co. Ltd na Supreme Perch Ltd vinavyosindika minofu ya samaki, Kagera Sugar Co. Ltd na Amir Hamza Co. Ltd vinavyosindika miwa na kahawa, na Kiwanda cha Mayawa kinachosindika Mvinyo ya Rosella na juisi.

” Kampuni ya Josam imepatiwa eneo lenye ukubwa wa hekta 500 katika ranchi ya Kikulula na tayari imejenga bwawa kwa ajili ya kuvuna maji pamoja na kuanza ufugaji wa ng’ombe wa maziwa wapatao 100 hadi sasa” aliongeza Dkt. Kijaji

Dkt. Kijaji alieleza kuwa mkakati wa kutekeleza miradi maalum ya kuondoa umasikini katika Mkoa wa Kagera imeainishwa kwenye Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016/2017 – 2020/2021, Mpango Mkakati wa Mpango wa utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo na Mipango ya Mkoa wa Kagera kwa ujumla.

“ Miradi yote ya kiuchumi na kijamii inayotekelezwa na Serikali na Sekta Binafsi katika mkoa wa Kagera, na mikoa mingine ni kwa ajili ya kuondoa  umaskini na kuboresha maisha ya wananchi”, alisema Dkt. Kijaji.

Aidha, aliainisha baadhi ya mikakati inayoendelea kutekelezwa na kuratibiwa na Serikali katika mkoa huo kuwa ni pamoja na  kuimarisha usafiri wa majini kwa kukamilisha ujenzi wa meli kubwa itakayotoa huduma ya usafiri na usafirishaji kati ya Bukoba na Mwanza.

Dkt. Kijaji aliongeza kuwa Serikali imeendelea kuimarisha miundombinu ya barabara kama vile barabara kwa kiwango cha lami ya Kyaka – Bugene (km 59.1), Kagoma – Lusahunga (Km. 154), Ushirombo – Lusahunga (Km. 50).

Alizitaja barabara nyngine zinazojengwa katika ukanda huo kuwa ni barabara ya Nyakanazi – Kibondo (km 50), ambayo ujenzi wake umefikia asilimia 40 pamoja na barabara ya Kyamyorwa – Buzirayombo (km 120).

“Kitaanzishwa kiwanda cha kuchakata madini ya bati katika wilaya ya Kyerwa ifikapo Juni, 2021 ambapo Kampuni ya Tanzaplus Minerals na African Top Minerals ltd zimeonesha nia ya kuwekeza katika sekta hiyo na tayari zimeanza kuleta mitambo ya uchenjuaji” aliongeza Dkt. Kijaji

Aliutaja mradi mwingine wa sekta ya madini kuwa ni uendelezaji na uwekezaji wa madini ya Nikeli Kabanga katika Wilaya ya Ngara ifikapo Juni mwaka 2021.

Mbunge wa Ilolo Mhe. Venance Mwamoto, aliuliza  mpango wa Serikali wa kukarabati barabara za mkoa wa Kagera kwakuwa una viwanda vingi  ili viweze kufikika kwa urahisi na kurahisisha biashara ndani na nje ya nchi.

Akijibu swali la nyongeza Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhe.  Atashasta Nditiye alisema kuwa Serikali imeshapeleka fedha katika mkoa huo na tayari imetoa tangazo la kutafuta Wakandarasi kwa ajili ya ukarabati wa barabara hizo.

LIVE | Kipindi cha Maswali na Majibu Bungeni Dodoma

$
0
0
LIVE | Kipindi cha Maswali na Majibu Bungeni Dodoma

Chadema wamjibu Spika Ndugai juu ya matibabu ya Tundu Lissu

$
0
0
Ndugu wanahabari na watanzania wote, bila shaka mmemsikia Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Job Ndugai tarehe 31 /01/2019 akitoa taarifa bungeni au kile alichakuwa akikiita kuwa ni ufafanuzi juu ya malalamika ya malipo ya matibabu ya Mh Tundu Lissu (MB) wa Singida Mashariki na Mnadhimu mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni.

CHADEMA tunalazimika kumjibu Spika Ndugai kwa kuwa bila haya na kwa makusudi ameamua kuliangopea Bunge na umma wa Watanzania. Mh Tundu Lissu ametibiwa na Chama chake  CHADEMA, wanachama  mmoja mmoja,mashirika mbalimbali ya  ndani na nje ya nchi, watanzania waishio ndani na nje na sambamba na hilo wabunge mmoja mmoja walichangia takribani Tsh 43 millioni kutoka katika posha zao kama walivyofanya watanzinia wengine.

Mh Lissu ni Mbunge halali wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa mujibu wa sheria ya bunge anastahili kulipwa mshahara wake wa kibunge na posha mbalimbali na pia kutibiwa na Bunge. 

Takribani Tsh. 207 million alizopatiwa Mh Lissu ni stahikl zake halali za kibunge na si pesa ya Matibabu kama Spika alivyoliongopea bunge na umma wa Watanzania. 

Spika amedai kuwa anazo nyaraka za uthibitisho wa malipo ya matibabu tunamtaka atoe hizo nyaraka hadharani .
 
Sisi Chama,Familia na Mh Lissu mwenyewe wote tuna nyaraka zote za Matibabu kwa kila hatua. Tunalitaka Bunge kulipia Matibabu ya Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa ni haki yake kisheria na si huruma kama anavyojaribu kuonyesha

Waajiri watakiwa kuwahisha michango mifumo ya jamii

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenister Mhagama, ameitaka mifuko yote ya hifadhi ya jamii kuhakikisha kuwa waajiri wanafikisha michango ya wafanyakazi katika mifuko hiyo baada ya kuwakata katika mishahara yao.

Mhagama alisema hayo bungeni jana, alipokuwa akitoa jibu la nyongeza kwa Mbunge wa Viti Maalum, Catherine Magige (CCM), ambaye alitaka kujua ni lini serikali itawalipa wafanyakazi 545 wa Kilitex-Arusha na wale wa hoteli ya Sabasaba ambao bado wanadai pensheni baada ya mwajiri wao kutowasilisha michango yao kwenye mfuko wa PPF.

Alisema bado tatizo la malipo ya pensheni kwa wafanyakazi ni tatizo kutokana na baadhi ya waajiri kutofikisha michango ya wafanyakazi kwenye mifuko kwa wakati.

Akizungumzia suala la wafanyakazi wa KILTEX na wa hoteli ya Sabasaba ambao wafanyakazi wake hawalipwa pensheni, Mhagama aliwataka viongozi watendaji wa mifuko inayohusika na wafanyakazi hao kukaa pamoja kutatua tatizo hilo.

Awali akijibu swali la msingi la mbunge huyo, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Ashatu Kijaji, alisema kwa mujibu wa kumbukumbu na nyaraka zilizoko na taratibu za ufilisi ulikamilika na wafanyakazi wa KILTEX walilipwa stahili zao.

Kijaji alisema hata hivyo, baadhi ya wafanyakazi walilipwa mafao yao ya kiinua mgongo kwa mkupuo na wengine walirejeshewa michango yao kadri walivyochangia.

Alisema utaratibu huo wa malipo ulifanyika baada ya mfilisi kushindwa kulipa riba, adhabu na malimbikizo ya michango kwenye mfuko wa pensheni wa PPF.

“Uamuzi huo ulifikiwa kutokana na ukweli kwamba, mauzo ya mali za kiwanda yalikuwa ni madogo ikilinganishwa na jumla ya madai na gharama halisi za ufilisi,” alisema.

Jeshi laapa kuilinda Serikali ya Bashir dhidi ya Wanaoipinga kwa Maandamano

$
0
0
Jeshi la Sudan limesema halitakubali kuiona Serikali ya nchi hiyo ikianguka kutokana na maandamano yanayoendelea yanayotaka Rais Omar al-Bashir ajiuzulu.

Mkuu wa Majeshi, Jenerali Kamal Abdul Maarouf amesema kupitia taarifa ya jeshi hilo kwa umma kuwa hawataruhusu Serikali kuangukia mikononi mwa watu wasiojulikana.

Jenerali Maarouf alisema kuwa watu wanaoandamana kupinga Serikali ni wasaliti wa Taifa wanaoipaka tope taswira ya nchi hiyo.

Jeshi limetoa taarifa hiyo ikiwa ni siku chache tangu Rais Al-Bashir azuru Misri na nchi washirika, akitafuta msaada wa kuokoa uchumi wa nchi yake.

Waandamanaji walianza kufanya maandamano ya kupinga Serikali kufuatia tangazo la kupanda kwa bei ya mafuta pamoja na chakula.

Al-Bashir ameiongoza nchi hiyo kwa kipindi cha takribani miaka 30 tangu alipoingia madarakani kupitia mapinduzi yasiyomwaga damu mwaka 1989.

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya February 2

Serikali Kusimamia Makubaliano Na Taasisi Ya Bill And Melinda Gates Ili Kukuza Sekta Ya Mifugo

$
0
0
Na. Edward Kondela
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amemuagiza Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel kufanya ufuatiliaji wa karibu kuhakikisha mikakati ambayo serikali imekubaliana na Taasisi ya Bill and Melinda Gates katika sekta ya mifugo inatekelezwa kama walivyokubaliana.

Naibu Waziri Ulega amesema hayo jana (01.02.2019) jijini Dodoma alipotembelewa na ujumbe kutoka Taasisi ya Bill and Melinda Gates katika ofisi za wizara hiyo na kubainisha kuwa serikali inahakikikisha Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Mifugo Tanzania unatekelezwa na kuishukuru taasisi hiyo kwa kutoa mchango mkubwa katika mpango huo.

“Sisi tuko pamoja na nyinyi na tunathamini makubaliano yetu na hatuwezi kuvunja makubaliano yetu ninawahakikishia kuwa nitamuagiza katibu mkuu afanye ufuatiliaji wa karibu sana kuhakikisha kwamba sisi tuna mikakati yetu tunayoifanya  lakini hii mikakati yote inaenda sambamba na kile tulichokubaliana.” Alisema Mhe. Ulega

Naibu Waziri Ulega pia amesema serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekuwa ikifanya ufuatiliaji wa karibu katika sekta za mifugo na uvuvi kwa kulinda rasilimali za nchi kwa kutumia Operesheni Nzagamba na Operesheni Sangara ili kuondoa mambo yaliyokuwa yakifanywa bila utaratibu na kuisababishia serikali hasara.

“Tunafanya ulinzi wa rasilimali na kuondoa ule uholela na kuhakikisha kuwa zile sheria, taratibu na kanuni zinafuatwa sana kwa sababu hata masoko ya kimataifa yalitaka uholela usiwepo, mambo yawe katika utaratibu wa kisheria na kanuni zinazoongoza sekta.” Alisema Mhe. Ulega

Aidha Mhe. Ulega amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi, inahakikisha katika operesheni hizo sheria, kanuni na taratibu za sekta za mifugo na uvuvi zinafuatwa ili sekta hizo ziweze kusonga mbele kwa kumuwekea mazingira mazuri mwananchi ili aweze kufaidika na nchi iweze kuongeza pato la taifa.

Akizungumza katika kikao hicho ambacho kimehudhuriwa pia na wakuu wa idara kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amebainisha baadhi ya mambo ambayo yanapaswa kusimamiwa ikiwemo elimu ili wafugaji waweze kunufaika kupitia sekta hiyo.

“Ningependa katika ushirikiano wetu huu tuzidi kushirikiana katika kutoa elimu kwa wafugaji wetu tuwe na ufugaji wenye tija, lakini eneo lingine la pili ni usimamizi dhidi ya magonjwa, la tatu ni kuwawezesha wafugaji wetu kiuchumi lakini la nne ni utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Maendeleo ya Mifugo Tanzania.” Alisema Prof. Gabriel

Prof. Gabriel pia ameainisha mambo mengine kuwa ni umuhimu wa kufanyika kwa tafiti, usimamizi na uhakikishaji wa uzalishaji bora wa mifugo ili sekta ya mifugo iweze kuwa na maendeleo endelevu.

Akizungumza kwa niaba ya Afisa Programu Mwandamizi wa Taasisi ya Bill and Melinda Gates katika Ukanda wa Afrika ya Mashariki Bibi Mercy Karanja, Mshauri Mwelekezi kutoka taasisi hiyo nchini Tanzania Prof. Marcellina Chijoriga amesema Taasisi ya Bill and Melinda Gates bado itaendelea kufanya kazi nchini kwa kufuata mpango wa serikali.

Aidha Prof. Chijoriga ameshukuru uongozi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambao umekuwa ukitoa ushirikiano mkubwa kwa taasisi hiyo na kutoa ombi kwa uongozi wa wizara kuendelea kushirikiana na Taasisi ya Bill and Melinda Gates ili iweze kuleta matokeo chanya kwa wafugaji nchini.

Serikali Yaelekeza Kusimamishwa Kazi Mkuu Wa Idara Ya Utawala Na Utumishi Wa Manispaa Ya Ilala

$
0
0
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Laurean Ndumbaro ametoa maelekezo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kumsimamisha kazi Mkuu wa Idara ya Utawala na Utumishi wa Manispaa hiyo, Bi. Benadeta Mwaikambo na kuwachukulia hatua za kinidhamu maofisa wanaohusika na Mfumo Shirikishi wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara (HCMIS) kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu.

Dkt. Ndumbaro ametoa maelekezo hayo jana wakati akizungumza na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) ofisini kwake jijini Dodoma, kufuatia utafiti uliofanywa kuhusu malalamiko ya watumishi ambao ulibaini Halmashauri ya Manispaa ya Ilala kuongoza kwa kuwa na malalamiko mengi ya watumishi ikifuatiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.

Dkt. Ndumbaro amefafanua baadhi ya malalamiko hayo kuwa, ni pamoja na kutopandishwa vyeo kwa watumishi kutokana na kutokuwa na taarifa sahihi za watumishi, uhakiki wa vyeti, kuwepo kwa upendeleo katika masuala ya kiutumishi, ushughulikiaji usioridhisha wa masuala ya kiutumishi, uwasilishaji wa madai ya malimbikizo ya mishahara Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora yakiwa hayana usahihi na yenye mapungufu kutokana na uzembe.

Dkt. Ndumbaro ametoa mfano wa madai ya malimbikizo ya mishahara yaliyowasilishwa Ofisi ya Rais-Utumishi ya walimu wastaafu 40 ambapo kati ya hayo, madai 24 yalikuwa sahihi  na 16 yalikuwa hayana taarifa sahihi ikiwemo kutogongwa mhuri wa mwajiri kuthibitisha madai hayo na kuongeza kuwa licha ya Manispaa ya Ilala kurejeshewa madai hayo kwa ajili ya marekebisho takribani miezi saba iliyopita lakini hadi sasa ni madai ya wastaafu wawili tu yaliyowasilishwa.

Sanjari na hilo, Dkt. Ndumbaro ameelekeza kuhamishwa kwa Maofisa Utumishi walio chini ya Idara ya Utawala na Utumishi ya Manispaa hiyo kwenda katika halmashauri ambazo hazihudumii watumishi wengi ili waweze kumudu majukumu yao kikamilifu.

Dkt. Ndumbaro ametoa wito kwa watumishi wa umma nchini hususan maofisa wanaoshughulikia masuala mbalimbali ya kiutumishi kufanya kazi kwa weledi, uadilifu na kutatua changamoto za watumishi kwa wakati na kuongeza kuwa ofisi yake itaendelea kufanya ufuatiliaji kwa taasisi zote zinazolalamikiwa.

Jaji Mkuu Awataka Wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye Maonesho ya Wiki ya utoaji wa Elimu ya Sheria

$
0
0
Na Lydia Churi-Mahakama, Dodoma
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amewataka wananchi wa mkoa wa Dodoma na Maeneo ya jirani kujitokeza kwa wingi kwenye Maonesho ya Wiki ya utoaji wa Elimu ya Sheria na kutumia nafasi hiyo kujifunza masuala mbalimbali yanayohusu Mahakama.

Akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kutembelea maonesho hayo leo, Jaji Mkuu pia amewataka wananchi wenye malalamiko na maoni kuhusu utendaji kazi wa Mahakama ya Tanzania kujitokeza na kutoa hizo ili ziweze kujibiwa na watumishi mbalimbali wa Mahakama walioko kwenye Maonesho hayo.

Jaji Mkuu pia ameto wito kwa wananchi wa Dodoma kufika na kuiuliza maswali Mahakama hasa juu ya ucheleweshwaji wa kesi zao na kuahidi kuwa maswali hayo yatajibiwa kwa lengo la hakikisha wanapata haki kwa wakati.

“Nawakaribisha wananchi wenye nafasi kufika kwenye viwanja vya Nyerere Square ili waweze kuona Mahakama ya Tanzania inavyofanya kazi zake kwa kushirikiana na wadau, ni wakati mzuri wa kutathmini utendaji wa Mahakama katika kipindi cha mwaka moja yaani tangu 2018” alisema Jaji Mkuu.

Alisema katika kipindi cha mwaka mmoja, Mahakama ya Tanzania imepiga hatua hasa kutokana na matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) katika kesi.  Aliongeza kuwa kupitia Maonesho ya Wiki ya Sheria, wananchi watajifunza kuwasilisha kesi katika ngazi mbalimbali za Mahakama.

Akizungumzia mashauri kukaa kwa muda mrefu Mahakamani, Jaji Mkuu alisema Mahakama imekuwa ikilaumiwa kuchelewesha kesi lakini wakati mwingine kesi zimekuwa zikichelewa kwa kuwa ni lazima kesi ishughulikiwe na baadhi ya Taasisi wadau huku akitoa mfano kuwa kesi hupepelezwa na polisi lakini huendeshwa na Mwendesha Mashtaka.

Wiki ya Sheria imeanza jana Januari 31 jijini Dodoma na itamalizika Februari 5 ambapo siku ya Sheria nchini itaadhimishwa Februari 6, 2019 katika viwanja vya Chimala jijini Dar es salaam.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images