Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Msanii Harmonize Matatani...RC Makonda Aagiza Achungwe Kama Anavuta Bangi

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Paul Makonda ameagiza vyombo vya usalama kumchunguza msanii  Harmonize kama anatumia bangi au lahh! ili achukuliwe hatua za za kisheria.

Makonda ameyasema hayo leo Alhamisi Januari 31,2019  wakati akizungumza na wasanii katika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam.

Amesema katika mtandao wa Instagram ameona picha ikimuonyesha Harmonize anayetamba na wimbo Paranawe akivuta kitu hicho hivyo ameomba ichunguzwe kama ni bangi au lah.

“Nimemuagiza Gavana wa huko  achunguze ile ni bangi au nini na ikigundulika ni bangi atakapotua tu hapa ni pingu na kupelekwa lock up, Vizuri namlea mwenyewe na mtoto anapokosea lazima umshikishe adabu bila kujali unampendaje,” amesema Makonda.



Spika Wa Bunge Akimuaga Mhe. Kitwanga Uwanja Wa Ndege Jijini Dodoma Wakati Akipelekwa Jijini Dar Es Salaam Kwa Matibabu Zaidi

$
0
0
 Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai (katikati) akiagana na Mbunge wa Misugwi Mhe. Charles Kitwaga katika Uwanja wa Ndege wa Jijini Dodoma kabla ya kusafirishwa kwenda Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa  matibabu zaidi. Kulia kwa Spika ni Naibu wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula na kushoto kwa Spika ni Katibu wa Bunge Ndg. Stephen Kagaigai.
PICHA NA BUNGE

Waziri Mkuu Majaliwa Amwakilisha Rais Magufuli Katika Mazishi Ya Mke Wa Mufti Wa Tanzania

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli katika mazishi ya mke wa Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Aboubakary Bin Zubeir yaliyofanyika Kwamndolwa, Korogwe mkoani Tanga.

Akitoa salam kwa niaba yake amesema “Rais Dkt. Magufuli aliweka nia ya dhati kushiriki mazishi haya ila kwa bahati mbaya leo ana mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika jijini Arusha ambapo yeye ni Mwenyekiti.”

“Mheshimiwa Rais amenituma nije nikupe pole wewe, watoto, familia na wote walioguswa na msiba huu. Mheshimiwa Rais anawaombea kwa Mungu ili mpate utulivu katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na nguzo katika familia. Haya yote ni mapenzi ya Mwenyezi Mungu.”

Waziri Mkuu ameshiriki mazishi hayo ya mke wa Mufti, Bibi Hidaya Omar leo (Alhamisi, Januari 31, 2019).

Kadhalika, Waziri Mkuu amewasihi wafiwa na waombolezaji wote waendelee kuwa watulivu na kumuombea marehemu kila mmoja kwa imani yake ili Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema.

Kwa upande wake, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhad Mussa Salum akizungumza kwa niaba ya familia amemshukuru Rais Dkt. Magufuli kwa kumtuma Waziri Mkuu amuwakilishe katika mazishi hayo. Pia amewashukuru watu wote waliojitokeza kwa ajili ya kuifariji familia kutokana na msiba walioupata.

Viongozi wengine waliohudhuria mazishi hayo niWaziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Mhe. Ummy Mwalimu, Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo, Mhe. Salma Kikwete, Mhe. Hawa Ghasia, Mhe. Mary Chatanda ,Mhe. Mkuu wa Mkoa wa TangaMartine Shigelana Masheikh wa Mikoa.

Homa ya uchaguzi mkuu yaanza kupanda Bungeni

$
0
0
Ikiwa imebaki miezi kadhaa kuelekea uchaguzi mkuu, baadhi ya wabunge wameonyesha kuwa na hofu juu ya kuchelewa kwa marekebisho ya daftari la wapiga kura.

Mbunge wa viti maalumu (Chadema), Cecilia Pareso leo aliuliza swali Bungeni kutaka kujua ni namna gani katika kipindi kilichobaki Serikali inaweza kutoa haki kwa Watanzania wenye sifa ya kujiandikisha ili watumie haki yao mwakani kupiga kura.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na wenye Ulemavu, Anthony Mavunde  amesema: "Mheshimiwa Spika, mchakato wa kuboresha daftari la wapigakura ulianza mwezi Agosti 2018, kwa kuhuisha kanzidata ya daftari la kudumu la wapigakura na kuboresha mifumo ya uandikishaji na utunzaji wa kumbukumbu za daftari."

Mavunde amesema kwa mujibu wa kifungu cha 15(5) cha Sheria ya Uchaguzi, sura ya 343, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iko katika hatua za mwisho za kufanya maandalizi ya uboreshaji wa daftari kwa majaribio katika baadhi ya mikoa. 


==>>Msikilize hapo chini

Spika Ndugai: Zitto Kabwe Hawezi Kuwa Rais wa Nchi Hii....Haiwezekani

$
0
0
Spika wa Bunge Job Ndugai amesema kuwa Mbunge wa Kigoma Mjini hawezi kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kufafanua kauli yake au kutaja sababu hasa itakayopelekea kiongozi huyo na chama chake kushindwa kushika dola.
 
Kauli hiyo ya Spika ameitoa Bungeni Jijini Dodoma wakati wa kujadili muswada wa vyama vya siasa nchini ambapo aliingilia kati uchangiaji Waziri wa zamani wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa George Simbachawene ambaye alikua akichangia.

Katika mchango wake Simbachawene alitolea mfano kiongozi huyo wa ACT - wazalendo kuwa Rais wa nchi lakini akihoji itakuaje kama akishuhudia wapinzani wake wakiendesha shughuli za maandamano.

Wakati Simbachawene akizungumza ghafla Spika wa Bunge Job Ndugai aliingilia kati na kusema, "mheshimiwa Simbachawene bahati nzuri Zitto hawezi kuwa Rais wa nchi haiwezekani."

Kupitia ukurasa wake wa Twitter kujibu kauli hiyo Zitto ameandika, "namuomba sana Mungu ampe uhai Job Ndugai na pia anipe uhai na kama kuna kheri ndani yake anipe nafasi ya kusaidiana na wenzangu kuongoza nchi yetu, hakuna ajuaye ya kesho isipokuwa Mungu tu".

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Ufaransa Yazitaka nchi za Umoja Wa Ulaya kuisusia Uingereza

$
0
0
Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amezitaka nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya (EU) kususa kufanya mazungumzo mapya na Uingereza kuhusu makubaliano ya kujiondoa kutoka umoja huo, maarufu kama Brexit.

Alisema licha ya hayo zinapaswa kujiandaa kwa uwezekano wa kutokea hali ngumu baada ya Uingereza kujitoa kutoka Umoja wa Ulaya Machi mwaka huu.

Akizungumza kwenye mkutano wa tano wa kilele wa Ulaya Kusini uliofanyika Nicosia nchini Cyprus, aliitaka Uingereza ijikite katika makubaliano ya awali ili kuepuka kujitoa EU bila makubaliano.

Taarifa iliyotolewa na mkutano wa kilele wa Ulaya Kusini imesema, Umoja wa Ulaya utajitahidi kuifanya Uingereza ijitoe kwenye Umoja huo kwa utaratibu.

Lengo la kufanya hilo ilisema ni kuhakikisha uthibitisho wa raia na kampuni pamoja na kuharakisha maandalizi ili kukabiliana na changamoto zitakazotokana na ondoko la Uingereza umojani humo.

Kauli hiyo inakuja baada ya Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May kujipanga kurudi kwenye umoja huo katika jitihada za kujadili tena vipengele muhimu vya mpango wake kuhusu mchakato wa Brexit.

Uamuzi wa May unakuja baada ya wabunge wa Uingereza kupiga kura juu ya mapendekezo saba yaliyochaguliwa na Spika wa Bunge yaliyolenga kuleta mabadiliko katika mchakato wa awali wa Brexit.

Wabunge hao walipitisha mabadiliko yanayoitaka serikali kuepusha uwezekano wa Uingereza kuondoka Umoja wa Ulaya bila ya mkataba ifikapo Machi 29.

Lakini ishara zote zinaonyesha May atakuwa katika malumbano mapya na EU baada ya kuahidi kubadili makubaliano yaliyofikiwa awali kuhusu mchakato huo.

Mpango huo alioufanikisha baada ya mwaka mmoja na nusu wa majadiliano na EU, hata hivyo ulikataliwa na wabunge wa Uingereza, waliotaka mabadiliko katika vipengele fulani.

Katika kujaribu kuyafufua mazungumzo ya Brexit yaliyokwama, May amepewa jukumu na Bunge la nchi yake la kurudi kwenye makao makuu ya Umoja wa Ulaya ili kuzungumzia tena makubaliano aliyoafikiana na EU.

May anapanga kujadili na EU juu ya kipengele kinachohusu suala lenye utata la mpaka wa Ireland kilichokwisha kutiwa saini na nchi 27 wanachama wa Umoja wa Ulaya ambacho sasa Uingereza inataka kibadilishwe.

Hata hivyo, viongozi wa nchi za Umoja wa Ulaya wamesisitiza kuwa kipengele hicho hakiwezi kubadilishwa.

Msemaji wa Rais wa Baraza la Umoja wa Ulaya, Donald Tusk amesema suala hilo la mpaka wa Ireland ni sehemu ya mkataba juu ya Uingereza kujiondoa EU na kwamba haliwezi kujadiliwa upya.

Binafsi May anatambua kuwa Umoja wa Ulaya hauna hamu wala hautaki kuubadilisha mpango wa Brexit uliopo sasa, lakini ameahidi kwenda mjini Brussels na kutafuta mabadiliko makubwa na ya kisheria kuhusu mkataba huo.

Kanisa Katoliki laondoa msimamo wake DRC

$
0
0
Kanisa  Katoliki nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), limeondoa msimamo wake wa awali wa kutotambua matokeo ya uchaguzi wa urais.

Kanisa hilo, ambalo lilikuwa na maelfu ya waangalizi wa uchaguzi wakati wa uchaguzi mkuu wa Desemba 30 mwaka jana, linaamini Rais Felix Tshisekedi hakushinda uchaguzi huo.

Limesema kuwa kufuatia kuapishwa kwa Felix Tshisekedi kuwa rais wiki iliyopita, halitaunga mkono maandamano ya kumpinga.

Mmoja wa wapinzani wa Tshisekedi, Martin Fayulu, anasisitiza kuwa aliporwa ushindi, kutokana na takwimu za Kanisa hilo kuonesha ameshinda kwa kishindo.

Lakini wachambuzi wa mambo wanasema Fayulu hawezi kufika mbali katika madai yake bila uungwaji mkono wa Kanisa la Katoliki, ambalo lina nguvu na ushawishi nchini humo.

Kanisa hilo lilikuwa muhimu katika mandamano makubwa ya kumpinga Rais Joseph Kabila, ambaye ameondoka baada ya kuwa madarakani kwa miaka 18.

Kitendo chake cha kumkabidhi Tshisekedi madaraka ya urais, kilikuwa uhamishaji wa kwanza wa madaraka kwa njia ya amani nchini humo katika kipindi cha karibu miaka 60.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya February 1

Viwanja Vikubwa Vinauzwa: Bunju na Mapinga (Baobab sec)

$
0
0
Viwanja Vikubwa Vinauzwa: Bunju na Mapinga (Baobab sec)

Viwanja viko Mingoi, ni mpakani mwa Bunju na Mapinga. Viko umbali wa km 2 kutoka Darajani (Bagamoyo Road). Viwanja viko sehemu nzuri inayofaa kwa Makazi, Biashara na Ufugaji.

Viko Viwanja vya size tofauti:
20/20 (sqm 400) bei milion 5
20/30 (sqm 600) bei milion 8
20/40 (sqm 800) bei milion 10
Robo eka (32/32) bei milion 12
Nusu eka (32/64) bei milion 24
Eka nzima (64/64) bei milion 48

Ruksa kulipa kwa awamu 2, kianzio ni 75% na luksa kujenga mara tu baada ya kulipa awamu ya kwanza.

Biashara hii haina dalali/udalali. Mpigie Mhusika: call 0758603077, whatsap 0757489709

Ukipata ujumbe huu, mjulishe ndugu/jamaa/rafiki.

Wapinzani Waibuka na Sakata la Korosho

$
0
0
Kambi rasmi ya upinzani bungeni imeishauri serikali kutowabagua wakulima wa korosho kwa kuwalipa wakulima wote pesa zao ili kuwaokoa wanafunzi walioshindwa kuanza shule pamoja na kulipa mikopo.

Hayo yamesemwa na Waziri Kivuli wa Kilimo ambaye pia ni mbunge wa Mbozi, Pascal Haonga wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa habari jijini Dodoma.

Mh. Haonga amesema serikali inatakiwa kuacha kuwabagua wakulima wa korosho pamoja na kutakiwa kuzilipa ushuru halmashauri zote ambazo zina wakulima wa korosho ambao asilimia kubwa zinategemea ushuru kupitia zao hilo.


Haonga ameitaka serikali iwe inaanzisha haraka minada ya zao la korosho ili kuepusha uuzaji holela wa zao hilo ambalo katika siku za hivi karibuni soko lake limekuwa likisuasua.

"Mwenendo wa kununua zao la korosho unakatisha tamaaa wakulima na wafanyabiashara kwa ujumla kwani kwani wakati mwingine wanatakiwa waonyeshe mashamba yao ndipo walipwe fedha zao," alisema

Haonga ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mbozi mkoa wa Songwe alisema kuwa iwapo serikali itaanzisha mapema minada ya korosho, itawapa ahueni wakulima wa zao hilo.

"Ikiwa minada itaanza mapema walau mwezi wa nane badala ya mwezi wa kumi mwishoni utaepusha uuzaji holela kwa kuwa kuna maeneo kama vile wilaya ya Lulindi, Nachunyu na Mvuleni ambapo maeneo hayo korosho zinakuwa tayari zimekomaa," alisema

Taarifa Kwa Umma Toka Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Kuhusu Huduma za Kubadilisha Fedha za Kigeni

Kikosi Cha IGP Siro Chatua Njombe Kuwasaka Wauaji Wa Watoto

$
0
0
Ikiwa siku moja imepita tangu naibu waziri wa mambo ya ndani ya nchi amuagize IGP Siro kutuma kikosi maalumu cha kiintelinsia kuongeza nguvu katika uchunguzi wa watekaji na wauaji wilayani Njombe , Hatimae hii  jana kikosi hicho kimewasili mkoani Njombe kikiongozwa na Kamisha wa operesheni na mafunzo wa jeshi la polisi nchini Nsato Marijani.

Akizungumza katika mkutano wa dharura na wananchi katika kituo kikuu cha mabasi mkoani Njombe mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Olesendeka wakati akitamburisha kikosi hicho kilichosheheni wataalamu mbalimbali kutoka vyombo mbalimbali vya ulinzi na usalama nchini amewataka wananchi kutoa ushirikiano ili kuwabaini wahusika wamaovu hayo huku akidai hakuna mtu atakae achwa salama kama amehusika na mauaji.

Katika mkutano huo pia Olesendeka amemuagiza kamanda wa polisi mkoa wa Njombe RPC Rennata Mzinga kumkamata mara moja aliyekuwa mratibu wa tiba mbadala na asilia mkoa wa Njombe Matias Gambishi ambaye pia ni afisa afya wa mkoa huo baada ya kulalamikiwa na waganga wataalamu wa tiba asili na mbadala kuwa amekuwa chanzo cha kusababisha migogoro katika chama chao pamoja kufanya usajiri holela wa waganga hao.

Nae kamanda wa kikosi hicho maalumu Nsato Marijani ambaye ni  Kamisha wa operesheni na mafunzo wa jeshi la polisi nchini alisema kikosi hicho kimekuja kwa kazi ya kuwasaka wahusika wa mauaji na kwamba kitawasaka popote walipo kwa heri ama shari.

Kwa upande wananchi wanapongeza serikali kwa kuchukua hatua za haraka za kukabiliana na vitendo hivyo vya ukatili dhidi ya watoto.

EU yamtambua Mpinzani Juan Guaido kama rais wa Venezuela

$
0
0
Mgogoro wa kisiasa unaoendelea kuikabili Venezuela umechukua sura mpya Alhamisi mara baada ya bunge la Umoja wa Ulaya kutangaza kuwa linamtambua rasmi Juan Guaido wa Venezuela, kama rais wa muda wa nchi hiyo.

Bunge hilo limesema kuwa litaendelea kumtambua Guaido kama kiongozi wa Venezuela hadi pale nchi hiyo itakapofanya uchaguzi huru na wa haki. huku wajumbe 429 wakipiga kura kuunga mkono hatua hiyo wakati wa kikao maalum mjini Brussels, Ubelgiji.

Aidha, hatua hiyo, inaendelea kuongeza changamoto zinazomkabili rais Nicolas Maduro anayeegemea mlengo wa Kisocialisti, na ambaye anakabiliwa na mzozo mkubwa wa kisiasa tangu uchaguzi ulioibua utata mwaka jana.

Marekani na baadhi ya washirika wake wa Ulaya, zimetangaza pia kwamba zinamtambua Guaido, ambaye alikuwa kiongozi wa bunge la nchi hiyo, kama kaimu rais, hatua ambayo imepingwa vikali na Russia, China na Uturuki, kati ya nchi zingine, ambazo viongozi wao ni washirka wa karibu wa Nicholas Maduro.

Hata hivyo, wakati Venezuela ikiendelea kukabiliwa na migogoro ya kiuchumi na kisiasa, Umoja wa Ulaya tayari umeiwekea nchi hiyo vikwazo vya silaha na pia vya kibiashara, kuwazuia baadhi ya maafisa wa serikali ya Maduro kushirikiana kwa vyovyote vile na nchi wanachama wa muungano huo wa EU.

Chadema wamjibu Spika Ndugai juu ya matibabu ya Tundu Lissu

$
0
0
Ndugu wanahabari na watanzania wote, bila shaka mmemsikia Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Job Ndugai tarehe 31 /01/2019 akitoa taarifa bungeni au kile alichakuwa akikiita kuwa ni ufafanuzi juu ya malalamika ya malipo ya matibabu ya Mh Tundu Lissu (MB) wa Singida Mashariki na Mnadhimu mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni.

CHADEMA tunalazimika kumjibu Spika Ndugai kwa kuwa bila haya na kwa makusudi ameamua kuliangopea Bunge na umma wa Watanzania. Mh Tundu Lissu ametibiwa na Chama chake  CHADEMA, wanachama  mmoja mmoja,mashirika mbalimbali ya  ndani na nje ya nchi, watanzania waishio ndani na nje na sambamba na hilo wabunge mmoja mmoja walichangia takribani Tsh 43 millioni kutoka katika posha zao kama walivyofanya watanzinia wengine.

Mh Lissu ni Mbunge halali wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa mujibu wa sheria ya bunge anastahili kulipwa mshahara wake wa kibunge na posha mbalimbali na pia kutibiwa na Bunge. 

Takribani Tsh. 207 million alizopatiwa Mh Lissu ni stahikl zake halali za kibunge na si pesa ya Matibabu kama Spika alivyoliongopea bunge na umma wa Watanzania. 

Spika amedai kuwa anazo nyaraka za uthibitisho wa malipo ya matibabu tunamtaka atoe hizo nyaraka hadharani .
 
Sisi Chama,Familia na Mh Lissu mwenyewe wote tuna nyaraka zote za Matibabu kwa kila hatua. Tunalitaka Bunge kulipia Matibabu ya Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa ni haki yake kisheria na si huruma kama anavyojaribu kuonyesha

Wimbo Mpya: Ray C Ft. Salmin Swaggz – Your Woman

$
0
0
Wimbo Mpya: Ray C Ft. Salmin Swaggz – Your Woman

LIVE | Kipindi cha Maswali na Majibu Bungeni Dodoma

$
0
0
LIVE | Kipindi cha Maswali na Majibu Bungeni Dodoma

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati

$
0
0
Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara, Msanii wa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo Dawa na PETE za Bahati zenye uwezo mkubwa wa kuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.

Kutana na Dokta Mkwambas. Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki.

 Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. 

Dokta Mkwambas ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA- Dokta Mkwambas  Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na Nje ya nchi.

Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nayasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.

Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudishaa aliepotea, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizopotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi,   kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMBA, GARI..)na mengine mengi (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET)

*{لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّهُ بِاللَّغْوِ فِي أيْمَانِكُمْ وَلَٰكِنْ يُؤَاخِذُكُمْ بِمَا عَقَّدْتُمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِمَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ }* ﴿٨٩﴾

✨Wabillahhi Tawfiq Asallam  Alaikum

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa

nambari ya simu
+255 717 163 789
+255 716 261 577

Whatsapp :  0752 388 329

Waajiri watakiwa kuwahisha michango mifumo ya jamii

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenister Mhagama, ameitaka mifuko yote ya hifadhi ya jamii kuhakikisha kuwa waajiri wanafikisha michango ya wafanyakazi katika mifuko hiyo baada ya kuwakata katika mishahara yao.

Mhagama alisema hayo bungeni jana, alipokuwa akitoa jibu la nyongeza kwa Mbunge wa Viti Maalum, Catherine Magige (CCM), ambaye alitaka kujua ni lini serikali itawalipa wafanyakazi 545 wa Kilitex-Arusha na wale wa hoteli ya Sabasaba ambao bado wanadai pensheni baada ya mwajiri wao kutowasilisha michango yao kwenye mfuko wa PPF.

Alisema bado tatizo la malipo ya pensheni kwa wafanyakazi ni tatizo kutokana na baadhi ya waajiri kutofikisha michango ya wafanyakazi kwenye mifuko kwa wakati.

Akizungumzia suala la wafanyakazi wa KILTEX na wa hoteli ya Sabasaba ambao wafanyakazi wake hawalipwa pensheni, Mhagama aliwataka viongozi watendaji wa mifuko inayohusika na wafanyakazi hao kukaa pamoja kutatua tatizo hilo.

Awali akijibu swali la msingi la mbunge huyo, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Ashatu Kijaji, alisema kwa mujibu wa kumbukumbu na nyaraka zilizoko na taratibu za ufilisi ulikamilika na wafanyakazi wa KILTEX walilipwa stahili zao.

Kijaji alisema hata hivyo, baadhi ya wafanyakazi walilipwa mafao yao ya kiinua mgongo kwa mkupuo na wengine walirejeshewa michango yao kadri walivyochangia.

Alisema utaratibu huo wa malipo ulifanyika baada ya mfilisi kushindwa kulipa riba, adhabu na malimbikizo ya michango kwenye mfuko wa pensheni wa PPF.

“Uamuzi huo ulifikiwa kutokana na ukweli kwamba, mauzo ya mali za kiwanda yalikuwa ni madogo ikilinganishwa na jumla ya madai na gharama halisi za ufilisi,” alisema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images