Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Nkoma: Tiba Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

0
0
NKOMA
_________________________
NKOMA Ni dawa bora ya nguvu za kiume  yenye mchanganyiko wa mitishamba (7) yenye maajabu yafuatayo/

🔖 (1) inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimalisha misuli ya uume uliolengea wakati wa tendo la ndoa/
🔖 (2) Kurefusha maumbile ya kiume yaliyorudi ndani kuazia nchi 5 - 9/
🔖 (3) kunenepesha uume cm 5 ya upana itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 - 20 kwa tendo la kwanza na utakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya 2-4 bila hamu kuisha/

📌 Na inatibu kabisa, unashauriwa uitumie dawa hii kama kinga ya magonjwa sugu./
 📌 Haijalishi umri hata kama una miaka 85 itumie huanza kufanya kazi dk 50 tu na haina madhara yoyote kwa mtumiaji/

📍📍📍📍📍📍📍📍📍
            MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA.
_________________________
🔖 (1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖 (2)Choo kama cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(4)Kaswende/
🔖(5)Gono/

📌Haya yote husababisha kuishiwa nguvu za kiume na kuwa na uume mdogo/
📌 Itumie leo, bado hujachelewa ni tofauti na nyingine.
_________________________
DR MAKOBA ANAPATIKANA DAR ES SALAAM, PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
___________________________
WASILIANA NA
Dr MAKOBA SIMU.
📞0754832349
📞0683490600
____________________________
*****************************

Upelelezi wa kesi ya kughushi saini ya Waziri January Makamba Bado Haujakamilika

0
0
Upelelezi wa kesi ya kughushi saini ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba inayowakabili  maofisa sita wa  Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (Nemc), bado haujakamilika.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka sita, likiwemo la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kusababisha hasara ya Sh160 milioni, katika kesi ya uhujumu uchumi namba 81/2018, iliyopo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Wakili wa Serikali, Jenipher Masue ameeleza hayo, leo, Jumatano Januari 30, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustina Mmbando, wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa.

Hata hivyo, mshtakiwa wa kwanza katika kesi hiyo, Magori Wambura (38) ambaye ni ofisa mazingira, hakuwepo mahakamani hapo wakati shauri hilo linatajwa.

Wakili Masue alidai kuwa taarifa aliyopewa na magereza ni kwamba, Wambura alipelekwa Mahakama Kuu, kwa sababu wana kesi nyingine.

Hakimu Mmbando baada ya kusikiliza maelezo hayo, aliahirisha kesi hiyo hadi Februari 13, mwaka huu itakapotajwa.

Washtakiwa watano wapo nje kwa dhamana baada ya kupata kibali cha dhamana kutoka Mahakama Kuu, huku mshtakiwa Wambura akiendelea kusota rumande baada ya kushindwa kuwasilisha maombi ya dhamana Mahakama Kuu.

Usiteseke Tena na Matatizo ya Nguvu za Kiume.....Tumia Tiba Hii ya Asili

0
0
SUPER MKUNYATI MIX; ni dawa bora ya mitishamba iliyopo katika mfumo wa vidonge na unga yenye uwezo wa kutibu na kumaliza matatizo yote ya ukosefu wa nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile:-

  -kuwai kufika kileleni ndani ya dakika chache tu.
 -Kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa muda mrefu.
 -Kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu(punyeto) husababisha kuishiwa au kupungukiwa na nguvu za kiume.
 -Uume kusimama kwa kulegea au katikati ya tendo la ndoa unalala na kushindwa kusimama.

Epuka matatizo haya kwa kutumia dawa bora ya asili ya SUPER MKUNYATI MIX ni kiboko ya matatizo haya yanayowasumbua baadhi ya wanaume wengi.

Pia kuna dawa ya kutibu Presha,miguu kufa ganzi, tumbo kuuma chini ya kitovu, kisukari,ngiri, chango aina zote na nk, matatizo haya nayo uchangia matatizo haya ya ukosefu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile madogo na uume mfupi.

KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA MAUMBILE MADOGO NA UUME MFUPI?  Usikate tamaa ondoa maradhi yako  hayo maana matatizo haya yamekuwa yakiathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti na sana na wanaume wengine kwa kushindwa kumlizisha mwanamke.


MDINDADINDA MIX, ni dawa ambayo inarefusha na kunenepesha maumbile na itakufanya uwe na uume saizi uipendayo.Dawa hizi za asili za mitishamba zipo katika mfumo wa vidonge na unga na hazina madhara kwa mtumiaji.

JABABILA;- ni dawa ya mvuto wa mapenzi ,mchumba, mke, mume aliyekuacha atakurudia ndani ya siku moja tu na atakutimizia utakacho.

ITALIGULA;- ni dawa ya biashara  na hata kama umezurumiwa utalipwa mapema ,kupata kazi, kupanda cheo. Ofisi zetu zinapatikana DAR ES SALAAM, SONGEA - BOMBAMBILI, SHINYANGA - KAHAMA MJINI. na pote pale ulipo utaipata huduma hii,kama huna nafasi utaletewa hulipo.Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR. MACHIMKENDA simu no ,0717 339771

Rais Magufuli afanya uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa DSFA

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Islam Seif Salum Mchenga kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu (Deep Sea Fishing Authority – DSFA).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Dkt. Mchenga umeanza tarehe 01 Desemba, 2018 na kwamba kabla ya uteuzi huo alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi - Zanzibar.

Wakati huo huo Rais Magufuli amemteua Dkt. Emmanuel Andrew Sweke kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu (DSFA).

Uteuzi wa Dkt. Sweke umeanza tarehe 01 Desemba, 2018 na kabla ya uteuzi huo alikuwa Afisa Utafiti wa Uvuvi Mwandamizi na Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti wa Uvuvi Tanzania (Tanzania Livestock Research Institute - TAFIRI) – Kigoma.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais Magufuli amemteua Prof. Sebastian W. Chenyambuga kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Utafiti wa Mifugo (TALIRI).

Uteuzi wa Prof. Chenyambuga umeanza tarehe 26 Januari, 2019.

Pia amemteua Prof. Justinian Rwezaula Ikingura kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (Geological Survey of Tanzania - GST).

Taarifa Kutoka Jeshi La Polisi Mkoani Mbeya Leo

0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea na jitihada za makusudi za kupiga vita wapiga ramli chonganishi @ lambalamba ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa wakisababisha madhara makubwa kwa jamii ikiwemo kuongezeka kwa matukio ya mauaji, kulipa kisasi na kuchochea chuki baina ya mtu na mtu au jamii na jamii.

Ikumbukwe kuwa, upigaji wa ramli chonganishi ni kinyume cha sheria ya tiba asili na mbadala namba 23 ya mwaka 2002. Wapiga ramli chonganishi @ lambalamba wengi wao hawana vibali vya kufanya shughuli hiyo, hivyo kukiuka sheria za nchi na kufanya matendo ambayo ni kinyume na haki za binadamu.

Kwa mujibu wa ibara ya 19 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 imekataza mtu mmoja au jamii kuingilia uhuru wa mtu mwingine katika imani, hivyo kutokana na baadhi ya watu kutokuwaamini wapiga ramli chonganishi jamii imekuwa ikihusika kwa kiasi kikubwa kuvunja sheria hii ya haki ya kuabudu.

Kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Desemba, 2018 jumla ya wapiga ramli chonganishi waliokamatwa ni 78 kati yao wanaume ni 67 na wanawake 11.
  1. Jumla ya kesi zilizofikishwa Mahakamani [Fresh Case] – 29.
  2. Jumla ya kesi zilizoshinda Mahakamani [Conviction] – 10.
  3. Jumla ya kesi zilizoshindwa Mahakamni [Acquited] – 04.
  4. Kesi zilizo chini ya upelelezi [Progress Investigation] 02.
  5. Kesi zinazoendelea kusikilizwa Mahakamani [Preliminary Hearing] – 09.
Aidha Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya linaendelea na mikakati mbalimbali ya kuzuia vitendo hivi visiendelee ikiwa ni pamoja na:-
 
Kupitia sera ya Polisi Jamii, kutoa elimu kwa wananchi kuhusu madhara ya imani potofu za kishirikina.
 
Kuendelea kushirikiana na Chama cha Waganga wa tiba asilia ili kuwabaini na kuwakamata wapiga ramli chonganishi hasa katika maeneo ambayo mara kwa mara vitendo hivi vimekuwa vikiripotiwa na kusababisha madhara kwa jamii husika.

Sambamba na hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa rai kwa wazazi na walezi kuongeza uangalizi kwa watoto wao hasa katika kipindi hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha hapa nchini kadhalika na kuweka uangalizi wa kutosha hasa kutokana na mkoa jirani wa Njombe kuripotiwa kwa matukio ya kupotea kwa watoto na hata wengine kupatikana wakiwa wamekufa kutokana na kinachodaiwa ni kuwepo kwa imani za kishirikina.
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linaendelea kutoa wito kwa wananchi kutoa taarifa za mtu au watu wanaowatilia mashaka katika maeneo yao ili uchunguzi zaidi uweze kufanyika dhidi yao. Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limechukua tahadhari kwa kufanya doria katika maeneo mbalimbali pamoja na kuunda dawati maalum la ulinzi wa mtoto kwa kushirikiana na idara nyingine za serikali ili kuhakikisha watoto wanapata ulinzi wakati wote.
 
Imetolewa na:
[ULRICH OMATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Je Kwanini Baadhi Ya Wanaume Wengi Wana Ukosefu Ama Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

0
0
JE KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UKOSEFU AMA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO ???

Pata sululisho la matatizo haya na  magonjwa mengine utapona kwa mda mfupi sana hatakama ulihangaika mpaka ukakata tamaaa 

GALIMBO 3 MIX  ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa aina mbili ili kukidhi mahitaji ya mtumiaji, imetengenezwa kwa muundo wa vidonge pamoja na unga kwaajili ya kuponesha tatizo moja kwa moja , huimalisha misuli ya uume iliyolegea wakato wa tendo la mdoa ,na kukufanya ucherewe kufika kileleni kwa mda wa dk ( 20 - 45 ) itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu nira hamu kuisha wara kuhisi kuchoka vilivile huzalisha viini vya uzazi ( manii ) 

YOLAN  hurefusha na kunenepesha  maumbile madogo ya uume na kuwa na uume kuanzia nchi (6-8) tiba kwa mda mfupi sana

Zipo sananu nyingi sana zinazosababisha matatizo hayo  km vile -:punyeto, kisukali,ngili,chango,vidonda vya tumbo,  tumbo kuunguluma na kujaa gesi maumivu ya mgongo ama kiume ,kolodani moja kuvimba ama kuingia ndani  presha nk 

Matatizo haya yote sio mageni, kigeni ni tiba sahihi ya kuponesha matatizo hayo

SUPER MBUKE -:  nidawa ya kuponesha tatizo la kisukali kwa mda mfupi sana , usihangaike wara kuteseka tumia dawa ya mitishamba kwaajili ya tatizo hili na upone kabisa

NTINJIWA  nidawa ya mvuto wa biashara,kazi, kupandishwa cheo,kumfanya mfanyakazi apendwe na bos wake

Pia ninadawa za kumvuta mme , mke,mchumba,hawara, au mtu yoyote unaemuhitaji katika maisha yako hata km yupo mbali na atatulia na kukutimizia cjovjote utakacho na kumfunga asiwe na mtu mwingime ,

Pata tiba za magonjwa mbalimbali ikiwemo miguu kuwaka moto, mgongo,bawasili ,kaswende ,gono na mengine mengi

KWAUSHAULI NA TIBA WASILIANA NA DR CHIKAGO    0759 208 637

Km huna nafasi ya kufika ofisini hudumahii utaletewa hapo ulipo , kwa wale wa mikoani natuma kwanjia ya basi

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 63

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   
   
“Tumefika Ujerumani?”
Camila aliniuliza huku akinitazama usoni mwagu”
“Nahisi mke wangu”
Camila akarudi kwenye siti yake na kufunga mkanda, nikafungua kijipazia kidogo cha dirisa na kuchungulia nje, nikaanza kuona baadhi ya majengo marefu ya nchi hii ya Ujerumani, nikashusa pumzi kwani safari hii imetuchukua masaa mengi na sijui ni kwanini tumelala sana. Ndege ikatua uwanja wa ndege, hatukuhitaji kupoteza muda, tukakodi helicopter hadi katika hospitali aliyo lazwa bi Jane Klopp. Da Mery akatupokea, huku akilia kwa uchungu sana, nikakumbatiana naye huku nikihiataji kufahamu ni nini kinacho endelea kwa mama yetu.

ENDELEA
“Mama ana endeleaje?”
Nilimuuliza da Mery huku nikiwa na wasiwasi mkubwa sana. Da Mery hakunijibu jambo lolote zaidi ya kuendelea kumwagikwa na machozi, kwa ishara akanionyesa chumba cha mama alicho lazwa, nikamuachia nami nikaingia ndani ya chumba hicho na kumkuta bi Jane akiwa amezungukwa na madaktari huku wakihangaika  katuka kapandisha mapigo yake ya moyo kwa mashine maalumu za umeme. Zoezi hili hata mimi likaufanya mwili wangu kuzizima, hali ya uchungu na majonzi ikaanza kunitawala, nikajikaza huku nikiendelea kutaza zoezi hili. 

Mashine inayo onyesha asilimia za mapigo ya moyo jinsi yanavyo fanya kazi, taratibu ikaanza kupandisha asilimia hizo kutoka tano hadi kufika asilimia themanini na sita. Madaktari wote wakajawa na furaha kwa maana bi Jane amepunyuka punyuka kwenye kifo.
“Naweza kuzungumza na mama yangu?”
Nilimuuliza mmoja wa madaktari.
 
”Hapana kwa sasa muache apumzike kidogo, akiwa sawa unaweza kuzungumza naye”
“Sawa sawa ninashukuru dokta, ila hali yake ipo vipi?”
“Kama unavyo muona, yupo hapa ICU”
Madaktari walizungumza huku wakinitazama usoni mwangu. Nikwajibu kwa kutingisha kichwa nikimaanisha kwamba nime waelewa. Tukatoka nje ya chumba hichi, da Mery pamoja na Camila wakanyanyuka na kunitazama usoni, tabasamu langu nililo liweka kidogo likawafanya wapate matumaini.
“Vipi mama hali yake?”
“Mapigo ya moyo yameweza kupanda na amerudi katika hali yake ya kawaida”
“Ohoo asante Mungu”
 
Camila alizungumza kwa furaha huku akimkumbatia wifi yake. Tukaendelea kukaa hapa hospitalini na Camila akawasiliana na wazazi wake na kuwajulisha  juu ya uwepo wake hapa nchini Ujerumani. Haikupita lisaa moja, walinzi wa raisi walio ambatana na wazazi wa Camila wakafika hospitalini hapa. Furaha ya kuto kuonana nao kwa kipindi cha muda mrefu ikatawala katikati yetu.
“Mume kua”
Mama Camila alizungumza kwa kututania na kutufanya sote tucheke. Kutokana na majukumu ya kiserikiali baba Camila na mke wake wakaondoka hapa hospitalli na kurudi ikulu huku hapa hospitali ikiwa chini ya ulinzi mkali. “Ethan hivi unatambua kwamba waandishi wa habari wameweka kambi  huko nje?”
“Weeee?”
“Ndio wanahitaji kutuhoji, sasa tutaongea nini kwa maana baadhi nahisi wana amani kwamba tulitekwa kabla ya uchaguzi?”
 
“Usijali tutazungumza nao, ila kwa sasa ngoja tuangalie hali ya mama kwanza”
Daktari mmoja ambaye kichwani mwake ana uwalaza, akaingia ndani ya chumba cha mama, baada ya muda akatoka na kwaishara akaniomba niweze kuingia katika chumba cha mama. Nikanyanyuka kwenye kiti ambacho nilikuwa nimekalia. Nikaingia ndani ya chumba hichi ambacho ni mlio wa mashine ya kuhesabu mapigo ya moyo ndio inasikika kwa sauti ya chini kidogo. Nilipo kisogelea kitanda cha mama, taratibu akatabasamu huku mwili wake ukionekana kudhohofika sana. Nikasimama pemben yake, kwa ishara ya mkono akaniomba niweze kuinama ili anibusu. Nikatii hivyo, taratibu akanibusu mashavuni mwangu, kisha akabalizia busu la upendo kwenye paji la uso wangu.
“Nimerudi mama”
Nilizungumza kwa unyonge sana huku nikimtazama mama usoni mwake. Akatabasamu sana, anaonekana ni mtu anaye hitaji kuzungumza maneno mengi ila anashindwa kutokana na hali yake, akakishika kiganja cha mkono wangu wa kulia na kukiweka kifuani mwake.
 
“Ni…na..k..upe…nda Etha….n”
Bi Jane alizungumza kwa shida kidogo ila niliweza kumuelewa.
“Ninakupenda pia mama”
Nilizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwangu.
“Mli…nde….M…e….ry. A….sij…e aka…p…a…twa na maba…ya”
“Sawa sawa maam nitafanya hivyo”
“Ca…amm…i….la yu….p…o w..p”
“Yupo hapa nje, ngoja nimuite”
Nikatoka ndani humu na kumuita Camil, tukaingia wote ndani ya chumba hichi na Camila na tukasimama pembeni ya bi Jane. Taratibu akavishika viganja vyetu na kuviweka juu ya kifua chake huku machozi yakimwagika usoni mwake.
 
“Pen…da…neni”
“Sawa mama”
“Sawa mama”
Kila mtu alijibu kwa muda wake huku tukiwa na huzuni.
“Ny…ny…I nd..io  ndug…u wa Mery mulio…oo. Sa..lia”
Bi Jane alizungumza huku akihema kwa shida kidogo, japo anapewa msada wa kuhema kwa mashine.
“Mu…pate wa….to….to”
“Tunashukuru sana mama”
“Me…ry….mu…ite”
Camila kwa haraka akatoka ndani humu na baada ya sekunde kadhaa wakaingia na Mery na moja kwa moja wakatudwata hapa kitandani na wakasimama pembeni yangu.
 
“Me…ry”
“Ndio mama”
“Pe…nda neni na E….THAN….ata…kul…inda”
“Sawa mama, nina mpenda sana Ethan”
“N…dio….naj…ua. Ha…ta yey…..e ana….kupe…nd…a”
Bi Jane aliendelea kuzungumza kwa tabu sana huku maneno yake yakiwa ni ya kukata kata.
“Nimekuelewa maama”
“Na….m…fwa..ta mu…me wangu sa…sa. Namuona ana….n…ii..ita”
Wote tukabaki na kigugumizi huku macho yakitutoka, tukabaki tukimuangalia bi Jane na kushindwa kuzungumza chochote.
 
“Nawape…nda. NATAKA KULALA SASA”
Bi Jane mara baada ya kuzungumza hivyo, akatabasamu, kisha akayafumba macho yake taratibu. Mlio wa mashine ya kuhesabu mapigo ya moyo ikaanza kutoa sauti kubwa huku mapigo ya moyo yakianza kushuka chini kwa kasi sana. Kundi la madaktari likaingia ndani humu na wakatuomba tusogee pembeni ya kiitanda hichi. 

Wakaanza kuhakikisha kwamba wana yapandisha mapigo ya moyo, ila kila wanali lifanya, hali ilizidi kuwa mbaya zaidi, kwani pagigo ya moyo yanaendela kushuka. Nikashuhudia sifuri mbili zenye rangi nyekunduhuku mstari mmoja mrefu wa kijani ukionekana kwenye mashine hii. 

Da Mery akaanguka kilio kizito na kuwafanya baadhi ya manesi kumdaka kabla hata ya kuanguka chini. Mwili na akili kwa ujamla vikawa kama vimegandishwa, sikuweza kuelewa ni nini kinacho fanywa zaidi ya kuona heka heka ndani ya chumba hichi. 
 
“ETHAN, ETHAN, ETHAN”
Sauti ya Camila ndio ikanistua kutoka katikwa dibwi la bumbuwazi hili. Nikamtazama huku nikiwa nimemtolea macho makali sana.
“Ehhh”
Nilizungumza, Camila akanikumbatia kwa nguvu huku akilia kwa uchungu sana. Nikamshudia daktari akimfunika bi Jane shuka usoni mwake, nikamuachia Camila na kisogea kilipo kitanda, nikataka kumfunua bi Jane shuka hili ila madaktari wakaniwahi kunikamata, kwa maana wana amani kwamba si akili yangu inayo fanya hivyo.
 
“Nataka kumuoana mama yangu”
Nilizungumza huku nikilia na kujitahidi kujitoa mikononi mwa madaktari hawa. Madaktari wakaongezeka kunishika na kunitoa ndani ya chumba hichi.
“Ethan kazi ya Mungu haina makosa, tumejitahidi kadri ya uwezo wetu ila tumeshindwa kabisa”
Daktari mmoja alizungumza huku akinitazama, sikumjibu kitu cha aina yoyote kwani akili yangu haina hata uwezo wa kufikiria kwa sasa. Wakaniingiza kwenye chumba cha kupumzikia, nikaka kwenye moja ya kiti huku nikiendelea kushangaa shangaa na kutafakari imekuwaje bi Jane amekufa. Nikamuona Ethan akiwa amesimama mbele yangu huku akiwa amevalia mavazi meupe na usoni mwake akiwa na unyonge mwingi, akakaa pembeni yangu pasipo mtu wa aina yoyote kuweza kumuona.
 
‘Hei’
Ethan alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.
‘Jikaze, mama ndio ameondoka hivyo. Yupo kwenye maisha ya furaha kwa sasa’
“Furaha?”
Nilizungumza kwa sauti kubwa na kuwafanya madaktari waliomo ndani humu kunishangaa. Ethana akawatazama madaktari hawa kisha akanishika kifuani mwangu. Mwili ukazidi kunilegea, giza totoro likanitawala machoni mwangu na mwishowe nikajikuta nikilala usingizi fofofo.
                                                                                                          ***
    Nikafumbua macho yangu na kujikuta nikiwa nipo chumbani kwangu katika jumba la mzee Klopp. Nikaa kitako kitandani huku nikisikilizia mziki mlaini unao tumika katika sehemu za misiba, ukisikika kutokea nje ya chumba changu. Nikashuka kitandani kwangu huku nikiwa na boksa tu mwili mwangu, nikaanza kutembea kuelekea mlangoni kabla sijaufikia mlango, mlango ukafunguliwa na akaingia Camila huku akiwa amevalia gauni kubwa jeusi.
“Umeamkaje mume wangu?”
“Nimefikaje hapa?”
 
“Ulipoteza fahamu kwenye chumba cha kupumzikia ambacho madaktari walikuingiza. Nikawashauri waweze kukurudisha nyumbani. Hivyo ni jana ndio umerudishwa nyumbani”
“Sasa hivi saa ngapi?”
“Ni saa mbili asubuhi, tayari maandalizi ya msiba yamefanyika na baadhi ya ndugu na marafiki wamesha kusanyika katika eneo hili”
Camila alizungumza huku akifungua kabati, akatoa suti moja nyeusi pamoja na shati jeusi.
“Inabidi uweze kuingia bafuni mume wangu. Oga uvae kisha upendeze”
“Maiti ya mama imesha letwa hapa nyumbani?”
“Hapana bado ipo hospitalini?”
“Yupo wapi Mery?”
“Sebleni, yupo na baadhi ya marafiki zake wana mfariji”
“Sawa”
 
Nikaingia bafuni, nikauweka sawa mwili wangu ambao bado una uchuvu chovu kidogo. Nikarudi chumbani na kuvaa nguo hizi huku Camila akinisaidia kunifunga vifungo vya shati langu. Tulipo maliza zoezi hili tukatoka chumbani humu na moja kwa moja tukaelekea sebleni, watu wakaanza kunipa pole kwa kufikwa na mama. Nikawashukuru kwa kuja, kisha nikaka eneo alipo kaa da Mery ambaye bado yupo kwenye majonzi mazito sana.
“Hei umepata kifungua kinywa?”
Nilimuuliza da Mary kwa sauti ya chini.
“Hapana”
“Kwa nini?”
“Ethan sijisikii kula chochote”
Da Mery alizungumza kwa msisitizo huku akinitazama usoni mwangu. Sikuona haja ya kumlazimisha kupata kifungua kinywa kwa maana hata mimi kwa upande wangu sijapata kifungua kinywa. Nikamuona Frenando akiwa amesimama pembezoni ya mlango wa kuingilia ndani humu, nikambusu da Mery kwenye shavu la kushoto kisha nikanyanyuka na kumfwata Frenando rafiki yangu wa muda mrefu sana katuka kusoma kwangu. Frenando akanikumbatia huku akiwa na furaha sana ya kuonana nami.
“Niambie rafiki yangu?”
“Poa kaka, pole sana nilisikia juu  ya swala la msiba wa mama nikastuka sana”
 
“Nashukuru ndugu yangu vipi masomo?”
“Kaka tumesha maliza mbona. Umesahau?”
“Akili yangu haipo sawa”
“Twende huku”
Frenando alizungumza huku akinishika mkono wangu wa kulia tukatoka nje na nikakutana na wachezaji wa timu yangu ya shule. Nikasalimiana nao kwa furaha sana huku nikikumbatiana na kila mmoja.
“Nashukuru kwa kuja sana rafiki zangu, hii ni surprise ambayo sikuitarajia kuiona kwa muda kama huu”
“Tupo pamoja ndugu yetu”
“Vipi lile kombe mulilichukua?”
“Ndio tulifanikiwa kupambana hadi dakika ya mwisho na tukafanikiwa kulichukua”
 
“Hongereni sana”
Mchezaji mmoja akaingia kwenye basi kubwa ambalo wamekuja nalo. Akatoka ndani ya basi na kombe ambalo tulikuwa tunaligombania na kunikabidhi jambo lililo nifanya nizidi kujawa na mshangao.
“Tumekuletea kombe hili kapteni ikiwa kama zawadi kwako kwa maana umetufanya tung’are. Yaani hadi tumavyo zungumza hivi sasa, kila mmoja hapa amepata mkataba katika kabla kubwa za hapa Ujerumani na nje ya Ujerumani”
“Weeee”
“Ndio. Mimi Ethan nasubiria jibu lako ni wapi niweze kujiunga kwa maana nimesha tumia ofa na klabu kubwa tatu. Liverpool, Real Madrid na Man Chester City”
Frenando alizungumza kwa furaha huku akinionyesha email za ofa alizo tumiwa na timu hizo.
“Tutalizungumza hilo maswala ya msiba yakiisha”
“Sawa sawa kaka”
“Ethan samahani”
 
Jamaa mmoja mwenye asili ya kijerumani alizungumza huku akiwa amesimama pembeni yangu. Nikamkabidhi Frenando kombe hili kisha tukasogea pembeni kidogo na kuzungumza.
“Ndio”
Akanikabidhi simu yake ya kiganjani.
“Ya nini?”
“Zungumza na huyu mtu”
Nikaiweka simu yangu sikioni.
“Nashukuru sana kwa kurudi Ujerumani. Ulihisi unaweza kulikimbia ili. Tunahitaji BOKSI JEUSI haraka iwezekanavyo kabla ya hatujaharibu msiba wa mama yako”
Maneno ya mwanaume huyu yakanistua sana, jamaa huyu aliye simama eneo hili taratibu akafungua koti lake na kunionyesha bastola aliyo ichomeka kiunoni mwake akiashiria kwamba nikifanya jambo lolote la kijinga anaweza kuniua hapa hapa.
 
==>>ITAENDELEA KESHO

Tamko La Wizara Ya Afya Kulaani Mauaji Ya Watoto 10 Mkoani Njombe

0
0
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inalaani na kukemea vikali vitendo vya mauaji ya watoto kumi (10) vilivyotokea katika wilaya ya Njombe ndani ya kipindi cha mwezi Desemba 2018 hadi Januari 2019; na hivyo kusababisha  taharuki kubwa kwa familia, jamii na Taifa kwa ujumla. Vitendo hivi havikubaliki kabisa katika jamii yetu na vinakiuka Sheria za nchi yetu.

Wizara inachukua nafasi hii kuzikumbusha familia zote katika jamii kuhakikisha zinaimarisha ulinzi na usalama wa watoto. Familia zinahimizwa kuwaangalia watoto na kujiridhisha wakati wote kuwa watoto wako wapi, wako na nani, wanacheza maeneo gani ili kuhakikisha wakati wote wanakuwa salama.

Aidha, Wizara inaikumbusha jamii na wazazi wote kwa ujumla kuzingatia jukumu la kuimarisha ulinzi na usalama wa watoto ndani ya maeneo yao. 

Sheria ya Mtoto kifungu cha 95 inamtaka kila mwanajamii ambaye ana ushahidi au taarifa kwamba haki za mtoto zinakiukwa au ziko hatarini kukiukwa atoe taarifa mara moja kwa vyombo vya ulinzi na usalama katika eneo husika ili kuzuia uwezekano wa vitendo viovu kutokea. 

Hivyo Wizara inatoa wito kwa wanajamii wote na kamati za Ulinzi na Usalama wa Mtoto kuhakikisha wanachukua hatua haraka na kutoa taarifa katika vituo vya polisi, Ofisi za Serikali za Mitaa na Mamlaka husika.

Wizara inatoa rai kwa uongozi wa Halmashauri zote Mikoani kuendelea kuanzisha na kuimarisha Kamati za Ulinzi na Usalama wa Wanawake na Watoto. 

Wizara ina imani na inalishukuru kwa dhati Jeshi la Polisi mkoani Njombe kwa juhudi wanazofanya kuhakikisha inawatia nguvuni watuhumiwa wa mauaji haya na kuwachukulia hatua kali za kisheria.

Wizara inatoa pole kwa wazazi, walimu na ndugu wote walioguswa na msiba wa watoto wetu wapendwa, na kwa pamoja tunaomba Mwenyezi Mungu awape nguvu na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.

Halmashauri ya jiji la Dodoma Yaandaa Viwanja 161,069

0
0
Halmashauri  ya jiji la Dodoma imeandaa michoro 245 yenye viwanja 161,069 kwa kipindi cha mwezi Mei, 2017 hadi Januari 2019,.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa idara ya Ardhi, Mipango Miji, na Maliasili Joseph Mafuru alipokuwa akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za sekta ya Ardhi kwa mwaka wa fedha 2017/2018 na nusu ya mwaka 2018/2019 kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika ukumbi wa halmashauri ya jiji la Dodoma jana.

Mafuru alisema kuwa, katika kipindi cha kuanzia mwezi Mei 2017 hadi Januari, 2019, Halmashauri hiyo katika utekelezaji wa mipango kina iliandaa michoro 245.

“Michoro hiyo ina jumla ya viwanja 161,069, ambapo upangaji huu unajumuisha michoro ya maeneo mapya, maeneo ya urasimishaji, na upangaji uliotekelezwa na Halmashauri” alisema Mafuru.

Ongezeko hilo ni kubwa ikilinganishwa na michoro 148 yenye viwanja 69,353 wakati wa miaka 44 ya Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu kwa kipindi cha kuanzia mwaka 1973 hadi mwezi Mei, 2017, aliongeza.

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi Mhe Dkt Angelina Mabula alifanya ziara ya kikazi ya siku moja katika halmashauri ya jiji la Dodoma kukagua utekelezaji wa shughuli za sekta ya Ardhi na kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Serikali kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Waziri Mkuu Majaliwa Amjulia Hali Mbunge Wa Misungwi, Charles Kitwanga

0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimjulia hali Mbunge wa Misungwi, Charles Kitwanga ambaye amelazwa katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma kwa matibabu, Januari 30, 2019.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimpa pole, Mkuu wa wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Mkunda ambaye anamuuguza mwanae, Tunu Kikula aliyelazwa katika hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma kwa matibabu, Januari 30, 2019.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya madaktari na wauguzi wa Kitengo cha Kusafisha Damu katika hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma wakati alipowajulia hali wagonjwa  hospitalini hapo, Januari 30, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu: Serikali Inahitaji Madaktari na Wauguzi

0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali inawahitaji madaktari na wauguzi ili waende kutoa huduma katika hospitali, vituo vya afya na zahanati.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Januari 30, 2019) alipozungumza na wanafunzi wa mwaka wa tano wanaosomea udaktari Chuo Kikuu cha Dodoma.

Waziri Mkuu amewataka wanachuo hao wasome kwa bidii ili waweze kufaulu masomo yao na kuapata sifa zitakazowawezesha kuajiriwa au kujiajiri.

Waziri Mkuu  amekutana na wanafunzi hao katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, alipokwenda kumjulia hali Mbunge wa Misungwi, Charles Kitwanga.

Akiwa hospitalini hapo, pia Waziri Mkuu alimjulia hali Mkuu wa wilaya ya Bahi, Mwanahamisi Makunda ambaye anamuuguza mtoto wake, Tunu Kikula.

Wengine aliowajulia hali ni pamoja na Mbunge wa Viti Maalum, Sabrina Sungura ambaye amelazwa  hospitalini hapo pamoja na wagonjwa wengine.

Kwa upande wake, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu amewapongeza madaktari hao ambao ni wanafunzi.

Amesema madaktari hao wamekuwa wakitoa msaada mkubwa kwa madaktari bingwa katika kuwahuduma  wagonjwa wanaofika hospitalini hapo.

 (mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

BREAKING: Aliegundua madini ya Tanzanite Mzee Jumanne Ngoma Afariki Dunia

0
0
Mzee Jumanne Ngoma ambaye aligundua Madini ya Tanzanite amefariki dunia leo January 30, 2019 katika Hospital ya Taifa Muhimbili alipokuwa anapatiwa matibabu.

Akithibitisha kifo cha Mzee Ngoma, Mtoto wake ambaye ni Mtangazaji wa Clouds TV Hassan Ngoma amesema Mzee amefariki leo akiwa anapatiwa matibabu na taratibu za mazishi zitatolewa baada ya kikao cha familia

Aprili 6 mwaka jana, Rais John Magufuli akizindua ukuta wa mgodi wa Tanzanite, Mirerani mkoani Manyara alimzawadia Sh100 milioni kama shukrani kwa mchango wake kwa kugundua madini hayo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya January 31

Spika Ndugai, Zitto Kabwe Mahakamani Leo

0
0
 Kesi ya kikatiba kuhusu kinga ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kwa mujibu wa Katiba ya Nchi na Mamlaka ya Bunge katika kuwaita na kuwahoji watu mbalimbali, leo inatajwa rasmi mahakamani.

Kesi hiyo ya Kikatiba namba 01/2019 imefunguliwa Mahakama Kuu, Masjala Kuu na mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe dhidi ya Spika wa Bunge, Job Ndugai.

Mahakama hiyo imetoa wito kwa wadau wote (mdai- Zitto na mdaiwa-Spika) ikiwataka kufika mahakamani leo kesi hiyo itakapotajwa kwa mara ya kwanza.

Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa na jopo la majaji watatu wakiongozwa na Firmin Matogolo, Dk Benhajj Masoud na Elinaza Luvanda.

Katika kesi hiyo, Zitto ambaye pia ni Kiongozi wa Chama cha ACT- Wazalendo anaiomba Mahakama Kuu itoe tafsiri ya kinga ya CAG iliyopo kikatiba na tafsiri ya Sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge katika kushtaki watu wanaosemekana kulidharau Bunge.

Zitto alifungua kesi hiyo baada ya Spika kupitia kwenye vyombo vya habari na baadaye kumwandikia barua CAG, Profesa Mussa Assad akimtaka afike mbele ya kamati ya Bunge kuhojiwa kutokana na kauli aliyoitoa akiwa Marekani kuwa Bunge ni dhaifu.

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Mkutano Maalum Wa 38 Wa Baraza La Mawaziri EAC

0
0
Mkutano Maalum wa 38 wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unafanyika jijini Arusha kwa lengo la kujadili na kukubabaliana na agenda mbalimbali zitakazowasilishwa kwenye Mkutano wa 20 wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya hiyo utakaofanyika tarehe 1 Februari, 2019.
 
Mkutano huo ambao unaongozwa na Mwenyekiti kutoka Jamhuri ya Uganda ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Kirunda Kivejinja utajadili agenda mbalimbali muhimu ambazo ni pamoja na ripoti ya utekelezaji wa maamuzi mbalimbali yaliyofikiwa na Baraza hilo kwenye vikao vilivyopita; taarifa kutoka Ofisi ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, taarifa kuhusu masuala ya miundombinu, forodha na biashara na ripoti ya kamati ya utawala na fedha.

Agenda zingine ni taarifa ya Baraza kwa Wakuu wa Nchi kuhusu utekelezaji wa maamuzi mbalimbali yanayofiwa kwenye mikutano ya Wakuu hao wa Nchi na Kalenda ya Matukio ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Juni 2019.

Mkutano huo wa Mawaziri ulitanguliwa na vikao vya Maafisa Waandamizi kutoka nchi wanachama kilichofanyika tarehe 28 Januari kikifuatiwa na kikao cha Kamati ya Uratibu chini ya Makatibu Wakuu kutoka nchi wanachama kilichofanyika tarehe 29 Januri 2019.

Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo  unaongozwa na Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na kuwahusisha pia Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (Mb), Waziri wa , Katiba
na Sheria, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), Waziri Fedha na Mipango, Mhe. Kapt. Mstaafu George Mkuchika (Mb), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Mhe. Joseph Kakunda (Mb), Waziri wa Viwanda na Biashara na Mhe. Innocent Bashungwa, Naibu Waziri wa Kilimo.

Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo inaundwa na nchi sita za Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda na Sudan Kusini imeendelea kuhakikisha wananchi katika nchi hizo wananufaika na Jumuiya hiyo hususan katika nyanja za biashara, ulinzi na usalama, viwanda, kilimo, miundombinu na huduma za kijamii.
 
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Arusha.
30 Januari 2019

IGP Sirro Aagizwa Kuunda Tume ya Kuchunguza Mauaji ya Watoto Njombe

0
0
Naibu  Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni, amemtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Simon Sirro, kuunda timu kutoka makao makuu itakayokwenda kushirikiana na wapelelezi wa Mkoa wa Njombe kuchunguza matukio ya mauaji dhidi ya watoto 10 mkoani humo.

Masauni alitoa agizo hilo jana, akiwa wilayani Njombe baada ya kukutana na waganga wa kienyeji kuzungumzia matukio ya mauaji dhidi ya watoto, yaliyohusishwa na imani za kishirikina.

Alisema timu ya IGP inatakiwa kuchunguza matukio yote ya mauaji mkoani humo na kuhakikisha wahusika wanakamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

“Agizo la pili IGP ahakikishe timu itakayotoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, inachunguza tukio la jana (juzi), lililosababisha polisi kutumia nguvu kwa kupiga mabomu ya machozi ili kutawanya wananchi, uchunguzi ujikite kubaini kiini na uwiano wa nguvu iliyotumika kuhusu uhalisia wa tukio," Masauni aliagiza.

Juzi, wakati naibu waziri huyo akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Njombe kwenye Viwanja vya Turbo, ghafla kulisikika milio ya mabomu ya machozi jirani na mkutano huo, kitendo ambacho kilisababisha taharuki na kusimama kwa mkutano huo.

Taarifa mbili zilizotolewa kwa Masauni kuhusu tukio hilo zilikinzana na kumfanya naibu waziri huyo kutaka uchunguzi ili kama amedanganywa, polisi wawajibike.

Katika agizo lake la tatu jana, Masauni alilitaka Jeshi la Polisi Mkoa wa Njombe kuongeza operesheni katika maeneo yote hususani kwenye mapori na misitu na kuhakikisha linakusanya taarifa za kiintelijensia ili kukomesha matukio hayo.

Kiongozi huyo wa serikali pia aliwataka Watanzania kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo, ili kukomesha vitendo vya uhalifu kwenye maeneo yao.

Ester Matiko atoa bati 1324 akiwa gerezani

0
0
Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini Mhe Esther N. Matiko ameamua kununua Bati zipatazo 1324 kwa ajili ya kuezeka Vyumba vya Madarasa 21, Ofisi 3 za Walimu na Vyoo 2 vyenye jumla ya Matundu 16. Mhe Esther N. Matiko ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini yuko Gerezani kwa muda wa siku 72 tangu kufutiwa dhamana na Mahakama ya Kisutu Jijini Dar es salaam.

Mhe Esther N. Matiko ameamua kuchukua maamuzi hayo baada ya idadi kubwa ya wanafunzi wa Darasa la 7 waliofaulu kujiunga na kidato cha kwanza wapatao *2046* kati ya hao ni Wanafunzi *416* tu walipata nafasi ya kuanza kidato cha kwanza na Wanafunzi *1630* wamekosa nafasi ya kujiunga kidato cha kwanza sababu tu ya upungufu wa vyumba vya Madarasa katika Shule za Sekondari Tarime Mjini.

Matiko ameamua kununua Bati hizo kupitia fedha za Mfuko wa Jimbo ambazo ni Tsh *31,000,000/=* ili kuwezesha uezekaji wa Madarasa hayo na kutoa fulsa kwa watoto hao kupata Haki yao ya Msingi ya kupatiwa Elimu.

Bati hizo zilizonunuliwa na Mhe Bashiri Abdalah Suleiman (Sauti) ambaye amekaimu nafasi ya Mhe Matiko mgawanyo wake ni kama ifuatavyo.

(1) Shule ya Sekondari Sabasaba Mabati 440 kuezeka Madarasa 7 na Ofisi 1 ya Walimu na Matundu 8 ya vyoo

(2) Shule ya Sekondari Nyamisangura Mabati 240 kuezeka Madarasa 4 na Ofisi 1 ya Walimu

(3) Shule ya Sekondari Nyandoto Mabati 120 kuezeka Madarasa 2

(4) Shule ya Sekondari Kenyamanyori Mabati 142 kuezeka Madarasa 2

(5) Shule ya Sekondari Tagota Mabati 250 kuezeka Madarasa 4 na Ofisi 1 ya Walimu na Choo cha Matundu 8

(6) Shule ya Sekondari Nkende Mabati 190 kuezeka Madarasa 3

(7) Shule ya Sekondari Rebu Mabati 60 kuezeka Darasa 1.

Kukamilika kwa vyumba hivyo vya Madarasa kutakuwa kumetoa fulsa kubwa sana kwa Wanafunzi walioachwa kujiunga na elimu ya Sekondari ikiwa ni haki yao ya Msingi.

Ofisi ya Mbunge Jimbo la Tarime Mjini inapenda kuwaambia Wananchi wote wa Tarime Mjini kuwa Bati hizo zote zilizopelekwa kwenye Shule wanazojenga zimetolewa na Mhe Esther N. Matiko na sio Mtu yeyote .

Mhe Esther N. Matiko anapenda kuwahasa Wananchi wote na watendaji waliopokea Bati hizo zitumike kwa Matumizi yaliyopangwa tu na sio jambo lingine.

Tarime Yetu Mshikamano Kwa Wote
Rasirimali Zetu Kwa Maendeleo Yetu

Imetolewa na:-
Peter Magwi Michael
Katibu wa Mbunge
Jimbo la Tarime Mjini

Tanzania yapata mnunuzi wa tani laki moja ya Korosho kutoka Kenya

0
0
Serikali ya Tanzania kupitia Bodi ya Taifa ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko imesaini mkataba wa mauzo ya korosho ghafi kiasi cha tani laki moja kwa Kampuni ya Kenya ya ENDO Power Solutions kwa malipo ya Shilingi bilioni 418.

Mkataba huo umesainiwa jijini Arusha tarehe 30 Januari 2019 kati ya Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo Dkt. Hussein Mansoor kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Bw. Brian Mutembei, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya ENDO Power Solutions ya nchini Kenya.

Tukio hilo la kihistoria lilishuhudiwa na Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Joseph Kakunda, Waziri wa Viwanda na Biashara, Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Innocent Bashungwa, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florence Luoga, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt.

Viongozi wengine walioshuhudia ni Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Dan Kazungu, Prof. Sifuni Mchome, Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Prof. Joseph Buchweshaija, Katibu Mkuu wa Viwanda na Biashara, Prof. Siza Tumbo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Edwin Rutaberuka, Mkurugenzi wa TanTrade, Maafisa Waandamizi kutoka Serikalini na Waandishi wa Habari.

Awali wakizungumza kabla ya kusainiwa kwa Mkataba huo Mawaziri hao wakiongozwa na Prof. Kabudi, kwa pamoja walipongeza kwa dhati uamuzi wa Mhe. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Serikali kununua korosho kutoka kwa wakulima ili kuepusha wakulima hao kuuza korosho zao kwa bei ya chini kwa watu wasio kuwa na nia njema kwa wakulima. 

Itakumbukwa kuwa, mwezi Novemba 2018, Mhe. Rais Magufuli alitoa maelekezo kwa Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo waratibu zoezi  la ununuzi wa korosho kutoka kwa wakulima kwa shilingi 3,300 kwa kilo moja.

Kwa upande wake Prof. Kabudi alisema kuwa anampongeza  Mhe. Rais Magufuli kwa uamuzi huo wa Serikali kununua korosho yote ili wakulima wapate bei inayolingana na jasho lao ambao hatimaye umezaa matunda kwa faida na maendeleo ya nchi.

Naye Mhe. Kakunda alieleza kuwa Bw. Mutembei ni mnunuzi wa kwanza kati ya wengi ambao walikuwa kwenye mazungumzo na Serikali kuhusu ununuzi wa korosho hizo. 

Mhe. Kakunda alisema katika majadiliano Serikali iliangalia kufanya biashara ya faida ambayo itawezehsa kulipa gharama mbalimbali ikiwemo gharama za upakiaji na upakuaji, malipo kwenye Serikali za Mtaa na michango mingine ya kijamii kwa mujibu wa makubaliano. 

Hivyo aliwataka watanzania na wenye viwanda kutokuwa na wasiwasi kwani Serikali ina nia njema ya kuwaletea maendeleo wananchi hususan kupitia sekta ya kilimo cha korosho.

“Wakulima wa Korosho wanatakiwa kumshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa uamuzi wake ambao unalinda maslahi ya mkulima na umewawezesha kuuza korosho zao kwa faida. Nawakaribisha wafanyabiasha makini kuja nchini kwani Serikali ipo tayari kuwasikiliza watu wa aina hiyo na kufanya nao biashara” alisema Mhe. Kakunda.

Kwa upande wake, Mhe. Bashungwa alieleza kuwa katika msimu wa korosho wa mwaka 2018/2019 tayari zimekusanywa tani 213,159 ambazo kati ya hizo tani 126,194 zimehakikiwa na tayari  wakulima wa mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma na Pwani wamelipwa fedha zao kwa zaidi ya asilimia 95.5. Mhe. Bashungwa aliongeza kuwa, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha Wakulima wote kulipwa fedha zao hadi kufikia tarehe 05 Februari 2019.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Kazungu alisema kuwa kusainiwa kwa mkataba huo ni faraja kubwa kwake katika historia ya mahusiano kati ya Tanzania na Kenya ambayo yanaendelea kuimarika siku hadi siku. 

Aidha, alieleza kuwa mkataba huo ni mfano mzuri wa kuimarika kwa mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki hususan katika masuala ya kilimo na biashara.

Kwa upande wake, mnunuzi wa korosho hizo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Endo Powers Solutions, Bw. Mutembei alisema amekuja kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais Magufuli za kumwinua mkulima wa Tanzania na kwamba anawataka wale wote wanaobeza jitihada hizo za Mhe. Rais Magufuli kuacha mara moja huku akilaani kitendo cha baadhi ya wafanyabiashara kuendelea kuwakandamiza wakulima kwa kununua mazao yao kwa bei ndogo wanazopanga wao huku wakijua wazi kuwa wakulima hao wametumia gharama kubwa katika uzalishaji wa mazao hayo.

Pia aliwataka wafanyabiashara kufuata taratibu na sheria katika kufanya biashara kama Serikali zinavyoelekeza na kuacha kuchanganya biashara na siasa.

Naye Mkurugenzi wa Bodi ya Nafaka, Dkt. Mansoor alieleza kufurahishwa na tukio hilo ambalo limekuja wakati mwafaka wakati nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki zikijiandaa na Mkutano wa Wakuu wa Nchi utakaofanyika jijini humo hivi karibuni. 

Aidha alisema kuwa, kwa kiasi kikubwa tukio hilo limeiinua Bodi yake na kwamba anatoa wito kwa wafanyabiasha wengine wa ndani na nje ya Tanzania kuja nchini na kushirikiana na Bodi hiyo ili kuwakomboa wakulima wengi Zaidi.

Mkataba huo umesainiwa wakati baadhi ya Mawaziri na Makatibu Wakuu wa Tanzania wakiwa jijini Arusha kwa ajili ya kuhudhuria vikao vya maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika kwenye Kituo cha  Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC) tarehe 1 Februari 2019.

Taarifa Kwa Umma: Tanzania Ina Akiba Ya Kutosha Ya Fedha Za Kigeni,

Spika Ndugai: Zitto Kabwe Hawezi Kuwa Rais wa Nchi Hii....Haiwezekani

0
0
Spika wa Bunge Job Ndugai amesema kuwa Mbunge wa Kigoma Mjini hawezi kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kufafanua kauli yake au kutaja sababu hasa itakayopelekea kiongozi huyo na chama chake kushindwa kushika dola.
 
Kauli hiyo ya Spika ameitoa Bungeni Jijini Dodoma wakati wa kujadili muswada wa vyama vya siasa nchini ambapo aliingilia kati uchangiaji Waziri wa zamani wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa George Simbachawene ambaye alikua akichangia.

Katika mchango wake Simbachawene alitolea mfano kiongozi huyo wa ACT - wazalendo kuwa Rais wa nchi lakini akihoji itakuaje kama akishuhudia wapinzani wake wakiendesha shughuli za maandamano.

Wakati Simbachawene akizungumza ghafla Spika wa Bunge Job Ndugai aliingilia kati na kusema, "mheshimiwa Simbachawene bahati nzuri Zitto hawezi kuwa Rais wa nchi haiwezekani."

Kupitia ukurasa wake wa Twitter kujibu kauli hiyo Zitto ameandika, "namuomba sana Mungu ampe uhai Job Ndugai na pia anipe uhai na kama kuna kheri ndani yake anipe nafasi ya kusaidiana na wenzangu kuongoza nchi yetu, hakuna ajuaye ya kesho isipokuwa Mungu tu".
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images