Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kesi ya Zitto Kabwe Yapigwa Kalenda

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeshindwa kuanza kusikiliza ushahidi wa upande wa mashtaka katika kesi ya uchochezi inayomkabili, Kiongozi wa ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kwa sababu shahidi aliyetakiwa kuanzakutoa ushahidi wake Leo amepata dharura.

Kesi hiyo ilipangwa kuanza kusikilizwa leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi lakini Wakili wa Serikali, Nassoro Katuga ameiomba mahakama kuipangia kesi hiyo tarehe nyingine Kwani shahidi amepata dharura.

“Kwa jinsi  upande wa mashtaka tulivyokuwa tumejipanga tulitaka tuanze na ushahidi leo na shahidi tuliyekuwa tumemuandaa amepata matatizo ya kifamilia tunaomba kuahirishwa kwa muda,” amesema Katuga.

Wakili wa utetezi,  Jebra Kambole amedai mshtakiwa alikuwa amejiandaa kwa ajili ya kuanza kusikilizwa lakini pia ana majukumu mengine  kuomba tarehe za mwishoni.

Hakimu Shahidi baada ya kusikiliza maelezo hayo ameahirisha kesi hiyo hadi Februari 27, 2019  kwaajili ya kuanza kusikiliza mashahidi wa upande wa mashtaka.

Katika kesi ya msingi,  Zitto anadaiwa kutenda makosa hayo   Oktoba 28, 2018 katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ofisi za  makao makuu ya chama cha ACT Wazalendo.

Alifikishwa katika mahakama hiyo na kushtakiwa kwa mashtaka matatu ya uchochezi.

Aliyekuwa Mkurugenzi NIDA Afikishwa Mahakamani Tena

$
0
0
Aliyekuwa  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho (NIDA), Dickson Maimu na wenzake sita leo Jumanne Januari 29, 2019 wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Maimu na wenzake hao jana Jumatatu Januari 28, 2019 walifutiwa mashtaka na mahakama hiyo lakini muda mfupi baadaye washtakiwa hao walikamatwa tena na polisi.

Wamefikishwa mahakamani hapo leo asubuhi na kupelekwa moja kwa moja katika chumba cha mahabusu kilichopo mahakama hapo.

Hata hivyo,  haijajulikana watapandishwa mahakamani saa  ngapi na kujibu mashtaka gani.

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Askari wa JWTZ afariki akijiokoa kubakwa na fundi

$
0
0
Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) kambi ya Tabora, Esther Gway amefariki wakati akijiokoa katika tukio la ubakaji lililotekelezwa na kijana aliyedaiwa kuwa ni fundi ujenzi.

Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora, Emmanuel Nley amesema tukio hilo limetokea juzi Jumapili Januari 27, 2019 saa moja usiku katika eneo la Kariakoo mjini humo.

Kamanda Nley amesema kwamba mtuhumiwa alimvizia mwanajeshi huyo akiwa nyumbani kwake muda huo na kumkaba shingo kisha kumuangusha chini na katika purukushani za kutaka kumbaka huku akimkaba shingoni alisababisha kifo chake.

"Fundi huyo inadaiwa alikuwa akijenga nyumba ya marehemu eneo la Kariakoo katika manispaa ya Tabora, tayari anashikiliwa na Jeshi la Polisi na tunaendelea na uchunguzi, tayari mwili wa marehemu upo katika uchunguzi pia hospitalini", amesema Kamanda Nley.

Akizungumzia taratibu za maziko ya marehemu amesema kuwa baada ya uchunguzi, mwili wa marehemu utakabidhiwa kwa ndugu pamoja na Jeshi ili taratibu za mazishi ziendelee.

Usiteseke Tena na Matatizo ya Nguvu za Kiume.....Tumia Tiba Hii ya Asili

$
0
0
SUPER MKUNYATI MIX; ni dawa bora ya mitishamba iliyopo katika mfumo wa vidonge na unga yenye uwezo wa kutibu na kumaliza matatizo yote ya ukosefu wa nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile:-

  -kuwai kufika kileleni ndani ya dakika chache tu.
 -Kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa muda mrefu.
 -Kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu(punyeto) husababisha kuishiwa au kupungukiwa na nguvu za kiume.
 -Uume kusimama kwa kulegea au katikati ya tendo la ndoa unalala na kushindwa kusimama.

Epuka matatizo haya kwa kutumia dawa bora ya asili ya SUPER MKUNYATI MIX ni kiboko ya matatizo haya yanayowasumbua baadhi ya wanaume wengi.

Pia kuna dawa ya kutibu Presha,miguu kufa ganzi, tumbo kuuma chini ya kitovu, kisukari,ngiri, chango aina zote na nk, matatizo haya nayo uchangia matatizo haya ya ukosefu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile madogo na uume mfupi.

KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA MAUMBILE MADOGO NA UUME MFUPI?  Usikate tamaa ondoa maradhi yako  hayo maana matatizo haya yamekuwa yakiathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti na sana na wanaume wengine kwa kushindwa kumlizisha mwanamke.


MDINDADINDA MIX, ni dawa ambayo inarefusha na kunenepesha maumbile na itakufanya uwe na uume saizi uipendayo.Dawa hizi za asili za mitishamba zipo katika mfumo wa vidonge na unga na hazina madhara kwa mtumiaji.

JABABILA;- ni dawa ya mvuto wa mapenzi ,mchumba, mke, mume aliyekuacha atakurudia ndani ya siku moja tu na atakutimizia utakacho.

ITALIGULA;- ni dawa ya biashara  na hata kama umezurumiwa utalipwa mapema ,kupata kazi, kupanda cheo. Ofisi zetu zinapatikana DAR ES SALAAM, SONGEA - BOMBAMBILI, SHINYANGA - KAHAMA MJINI. na pote pale ulipo utaipata huduma hii,kama huna nafasi utaletewa hulipo.Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR. MACHIMKENDA simu no ,0717 339771

Hakimu kortini tuhuma za kupokea rushwa 710,000/

$
0
0
Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo ya Ukonga jijini Dar es Salaam, Dickson Mwasenga (46), amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala na kusomewa mashtaka matatu ya kupokea rushwa ya jumla ya Sh. 710,000.

Akisomewa mashtaka hayo jana na Mwendesha Mashtaka wa Mahakama hiyo, Devota Mihayo, mbele ya Hakimu Samuel Obasi, ilidaiwa mshtakiwa alipokea rushwa hiyo ili kufanya upendeleo katika kesi ya jinai namba 352 ya mwaka 2017 iliyokuwa inamkabili ofisa wa Benki ya CRDB, Ngomoi Mmbaga (42).

Katika shtaka la kwanza, ilidaiwa kuwa Februari 22, 2017, mshtakiwa huyo alipokea Sh. 210,000 kutoka kwa Ngomoi Mmbaga kupitia Tigo Pesa ili kumpa upendeleo ofisa huyo wa benki katika kesi ya jinai namba 352 ya mwaka 2017.

Katika shtaka la pili, ilidaiwa kuwa Aprili 14, 2017, mshtakiwa alipokea Sh. 100,000 kutoka kwa Ngomoi Mmbaga, kupitia Tigo Pesa ili kumpa upendeleo ofisa huyo wa benki katika kesi ya jinai namba 352 ya mwaka 2017.

Katika shtaka la tatu, ilidaiwa kuwa Mei Mosi, 2017, mshtakiwa alipokea Sh. 400,000 kutoka kwa Ngomoi Mmbaga kupitia Tigo Pesa ili kumpa upendeleo katika kesi ya jinai namba 352 ya mwaka 2017.

Mihayo alidai mahakamani hapo kuwa, kufanya hivyo ni kinyume cha Sheria ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 Kifungu 15(1) ya Mwaka 2017.

Mwendesha mashtaka huyo pia alisoma mashtaka matatu dhidi ya Mmbaga ya kutoa rushwa, ili kupewa upendeleo katika kesi ya jinai namba 352 ya mwaka 2017 katika mahakama hiyo ya mwanzo.

Katika shtaka la kwanza, ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, Februari 22, 2017, mshtakiwa Ngomoi Mmbaga alituma Sh. 210,000 kwenda kwa Dickson Mwasenga kupitia Tigo Pesa, ili kupewa upendeleo katika kesi ya jinai namba 352 ya mwaka 2017.

Katika shtaka la pili, ilidaiwa kuwa Aprili 14, 2017, mshtakiwa huyo alituma Sh. 100,000 kwenda kwa Dickson Mwasenga kupitia Tigo Pesa, ili kupewa upendeleo katika kesi ya jinai namba 352 ya mwaka 2017.

Katika shtaka la tatu, ilidaiwa kuwa Mei Mosi, 2017, mshtakiwa Ngomoi Mmbaga, alituma Sh. 400,000 kwenda kwa Dickson Mwasenga kupitia Tigo Pesa ili kupewa upendeleo katika kesi ya jinai namba 352 ya mwaka 2017.

Mihayo alidai mahakamani hapo kuwa, kwa kufanya hivyo ni kinyume cha Kifungu cha 15(1) cha Sheria ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya mwaka 2017.

Washtakiwa wote walikana mashtaka na kesi hiyo kupangwa kutajwa tena Februari 19, mwaka huu.

Naibu Waziri Mabula Achochea Kasi Ya Ujenzi Shirika La Nyumba Katika Mji Wa Serikali Mtumba

$
0
0
Na Munir Shemweta, DODOMA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amechochea kasi ya ujenzi wa ofisi za serikali katika eneo la Mtumba mkoani Dodoma unaofanywa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Kasi hiyo inatokana na ziara za mara kwa mara zinazofanywa na Naibu Waziri huyo wa Ardhi katika eneo hilo kwa nia ya kuhakikisha ujenzi wake unakamilika katika muda uliopangwa.

Akiambatana na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa .Dkt Sophia Kongela pamoja na Mkurugenzi wa Shirika Dkt Maulid Banyani jana, Naibu waziri Mabula alijionea maendeleo makubwa ya ujenzi huo ambapo sasa umefikia hatua ya kuezeka.

Mbali na kufikia hatua hiyo, kazi nyingi katika ujenzi huo zinaenda kwa pamoja kama vile kuweka njia za umeme, tiles, utengenezaji madirisha ya nondo pamoja na mashimo ya choo  jambo linaloonesha Shirika limejipanga kukamilisha kazi mapema tofauti na makampuni mengine ya ujenzi yanayofanya kazi kwenye eneo la Mtumba.

Kampuni ya Ujenzi ya Shirika la Nyumba la Taifa katika eneo hilo la Mtumba inajenga majengo ya ofisi nne za Wizara ya Ardhi Nyumba na Maenendeleo ya Makazi, Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Nishati pamoja na Wizara ya Fedha na Mipango.

Akizungumza  baada ya kukagua kwa mara ya pili ujenzi wa ofisi hizo, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Mabula alisema kasi inayooneshwa na Shirika la NHC katika ujenzi huo ni ishara tosha kuwa shirika hilo kupitia kampuni yake ya ujenzi lina uwezo mkubwa wa kujenga majengo kwa haraka na yenye viwango.

Alisema, hata kama ujenzi wa ofisi zinazosimamiwa na shirika hilo katika eneo la Mtumba utachelewa kidogo lakini ucheleweshaji huo utatokana na MHC kutaka kujenga majengo ya uhakika na yenye ubora unaotakiwa.

Dkt Mabula ameendelea kutoa sifa kwa Ofisi ambazo majengo yake yanasimamiwa na shirika la Myumba la Taifa kutokana na ukaribu inaouonesha katika kipindi chote cha ujenzi kwa nia ya kuwa na majengo yanayokidhi mahitaji ya Wakala wa Ujenzi Tanzania (TBA) na ofisi husika kwa kuwa mawazo ya pande zote yatakuwa yamejumuishwa katika kutekeleza ujenzi huo.

Je Kwanini Baadhi Ya Wanaume Wengi Wana Ukosefu Ama Upungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
JE KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA UKOSEFU AMA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO ???

Pata sululisho la matatizo haya na  magonjwa mengine utapona kwa mda mfupi sana hatakama ulihangaika mpaka ukakata tamaaa 

GALIMBO 3 MIX  ni dawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa aina mbili ili kukidhi mahitaji ya mtumiaji, imetengenezwa kwa muundo wa vidonge pamoja na unga kwaajili ya kuponesha tatizo moja kwa moja , huimalisha misuli ya uume iliyolegea wakato wa tendo la mdoa ,na kukufanya ucherewe kufika kileleni kwa mda wa dk ( 20 - 45 ) itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu nira hamu kuisha wara kuhisi kuchoka vilivile huzalisha viini vya uzazi ( manii ) 

YOLAN  hurefusha na kunenepesha  maumbile madogo ya uume na kuwa na uume kuanzia nchi (6-8) tiba kwa mda mfupi sana

Zipo sananu nyingi sana zinazosababisha matatizo hayo  km vile -:punyeto, kisukali,ngili,chango,vidonda vya tumbo,  tumbo kuunguluma na kujaa gesi maumivu ya mgongo ama kiume ,kolodani moja kuvimba ama kuingia ndani  presha nk 

Matatizo haya yote sio mageni, kigeni ni tiba sahihi ya kuponesha matatizo hayo

SUPER MBUKE -:  nidawa ya kuponesha tatizo la kisukali kwa mda mfupi sana , usihangaike wara kuteseka tumia dawa ya mitishamba kwaajili ya tatizo hili na upone kabisa

NTINJIWA  nidawa ya mvuto wa biashara,kazi, kupandishwa cheo,kumfanya mfanyakazi apendwe na bos wake

Pia ninadawa za kumvuta mme , mke,mchumba,hawara, au mtu yoyote unaemuhitaji katika maisha yako hata km yupo mbali na atatulia na kukutimizia cjovjote utakacho na kumfunga asiwe na mtu mwingime ,

Pata tiba za magonjwa mbalimbali ikiwemo miguu kuwaka moto, mgongo,bawasili ,kaswende ,gono na mengine mengi

KWAUSHAULI NA TIBA WASILIANA NA DR CHIKAGO    0759 208 637

Km huna nafasi ya kufika ofisini hudumahii utaletewa hapo ulipo , kwa wale wa mikoani natuma kwanjia ya basi

Ofisa wa TRA anayedaiwa kumiliki mali za Milioni 721 Kusomewa Maelezo ya Awali February 20

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu  imepanga Februari 20, 2019, kumsomea maelezo ya awali ofisa wa forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania ( TRA), Godfrey Mapuga anayekabiliwa na shtaka moja la kumiliki mali zenye thamani ya Sh721milioni zisizoendana na kipato chake cha sasa na cha zamani.

Uamuzi huo umetolewa leo Jumanne Januari 29, 2019 na hakimu mkazi, Salum Ally baada ya upande wa mashtaka kudai upelelezi wa shauri hilo umekamilika.

Wakili wa Serikali mwandamizi,  Vitalius Peter amedai kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi wa shauri hilo umeshakamilika.

Baada ya maelezo hayo hakimu Ally ameahirisha kesi hiyo hadi Februari 20, 2019 siku ambayo upande wa mashtaka utamsomea maelezo ya awali mshtakiwa.

Katika kesi hiyo ya jinai namba 13/2019, Mapunga amedaiwa kumiliki viwanja vitatu pamoja nyumba  moja ya ghorofa, ambavyo haviendani na kipato chake.

Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, anadaiwa kutenda kosa hilo kati ya Aprili  Mosi, 2011 na Julai 19, 2016 eneo la  Ubungo.

Mapuga akiwa mtumishi wa umma, anadaiwa kumiliki nyumba  moja ya ghorofa iliyopo Goba manispaa ya Ubungo yenye thamani ya Sh698.9milioni  ambayo haiendani na kipato chake.

Pia katika kipindi hicho, mshtakiwa anadaiwa kumiliki kiwanja kimoja ambacho hakijasajiliwa kilichopo eneo la  Mbezi Juu, manispaa ya Ubungo chenye thamani ya Sh 7milioni.

Vile vile, anadaiwa kumiliki ardhi ambayo haijasajiliwa iliyopo eneo la Kigamboni yenye thamani ya Sh 6milioni.

Mapuga anadaiwa kumiliki kiwanja ambacho hakijasajiliwa kilichopo Goba chenye thamani Sh 9.5miloni na kufanya idadi ya mali anazodaiwa kumiliki ambazo haziendani na kipato chake cha sasa na cha zamani kufikia Sh721.4milioni.

Mshtakiwa ambaye anatetewa na wakili,  Mluge Fabian  baada ya kusomewa mashtaka yanayomkabili alikana ya yupo nje kwa dhamana.

Dkt Ndungulile: Serikali Itaweka Utaratibu Wa Bima Ya Afya Kwa Kila Mtanzania

$
0
0
NAIBU Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Dkt faustine Ndungulile asema serikali itaweka utaratibu wa bima ya Afya kwa watanzania wote na hilo litakuwa ni takwa la kisheria kwa kila mtu kuwa na bima

Dkt Ndungulile aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati akizundua Zanahati ya St .Marrys iliyopo Kijiji cha Mivumoni Kata ya Bushiri wilayani Pangani inayomilikiwa na Watawa wa Cappucion.

Alisema watafanya hivyo kwa lengo nzuri kutokana na kwamba hivi sasa serikali inafanya uwekezaji mkubwa na hatua hiyo inaweza kuwaondoa wananchi baadhi ya changamoto wanazokumbana nazo wakati wanapougua wakiwa hawana fedha za kuweza kupata matibabu

“Sasa hivi tutakuja utaratibu wa bima ya Afya kwa watanzania wote na hilo litakuwa ni Takwa la kisheria utake usitake kwa watanzania wote lazima wawe na bima ya Afya hivi tunafanya uwekezaji mkubwa sana lakini changamoto ambayo ninayoipata kama Naibu Waziri nyingi sana kila simu anayopata ni mtu anasema maiti yake imezuliwa,mgonjwa wake amepona anashindwa kutoka Hospitalini”

“Lakini kwa sababu anadaiwa fedha pia nimekuwa hakimu wa kusuluhisha migogoro kati ya hosipitali na wananchi hivyo ili kuweza kuondokana na hili tutoke hapo tuende kwenye bima ya Afya kwa kila mtanzania”Alisema Naibu Waziri huyo.

Aidha pia alisema pamoja na uwekezaji huo mkubwa ambao umefanywa lakini gharama za matibabu zinazidi kukua na jamii za wananchi wengi bado ni maskini hivyo wakaona waboresha mifumo ya bima za afya nchini kwa kuja na CHF iliyoboreshwa

“Kwani tunaweza kujenga kituo cha Afya lakini wananchi wakashindwa kupata matibabu kwa sababu ya gharamu serikali wameliona hilo na ndio maana tumeona tuboreshe mifumo ya bima za Afya kwa kuja CHF iliyoboreshwa “Alisema.

Naibu Waziri huyo alisema CHF hiyo itakuwa ni mtu na mwenza wake na wategememzi wannne watapata huduma za afya kuanzia ngazi ya zahanati mpaka hospitali za mikoa kwa sh.30,000 huduma za upasuaji na za kawaida.

Naye kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah alisema kwamba uwepo wa zahanati hiyo umekuwa ni chachu kubwa kwa wananchi kwani utasaidia kuboresha huduma za afya kwenye tarafa yao ya Madanga.

Alisema pia utasaidia kuwaepusha wakina mama kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya ambako walikuwa wakikumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo kujifungulia njiani.

“Tunashukuru sana kwa uwekezaji huu ambao utakuwa chachu kubwa kwa kuwaondolea changamoto za upatikanaji wa huduma za Afya kwa wananchi “Alisema.

Naye Kwa upande wake Askofu wa Jimbo Katoliki la Tanga Mhashamu Anthony Banzi alisema kanisa linapotoa huduma kwa jamii linaongozwa na mwanzilishi wake Bwana Yesu Kristo kutokana na kwamba ukisoma kwenye injili utaona jinsi alivyowaponya watu.

Alisema pia viongozi wa dini tunafurahi sana kushirikiana na viongozi wa serikali katika kuwahudumia watu mbalimbali kwa awamu ya tano kila mmoja anasisimuka na hari kubwa ya kutaka kushirikiana nayo.

Alisema kwa sababu imeonyesha lengo lake na jinsi inayofanya kazi kutaka kumkomboa na kumuendeleaza mtanzania wa hali ya chini hasa maskini.

Waajiri 19 Kortini kwa kukiuka sheria za kazi.

$
0
0
Katika kipindi cha mwaka 2016/17 Serikali imewafikisha mahakamani waajiri 19 kwa kukiuka sheria za kazi.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumanne Januari 29, 2019 bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Anthony Mavunde wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalumu, Munira Khatibu.

Mbunge huyo ametaka kujua Serikali ina kauli gani juu ya manyanyaso yanayofanywa na kampuni binafsi kwa watumishi wake ikiwemo muda wa kazi, kutowapa chakula, na kuwalipa mshahara mdogo.

"Ni wajibu wa mwajiri kutii matakwa ya sheria kwa kumlipa mfanyakazi wake mshahara na maslahi stahiki," amesema Mavunde.

Amesema mwajiri anayekiuka matakwa ya sheria hiyo, anastahili adhabu kulingana na Sheria ya Bunge ya mwaka 2016 sheria ya kazi namba 7 ya mwaka 2004.

Bundi Azua Kizaazaa Bungeni....Spika Awatoa Hofu Wabunge

$
0
0
Katika hali isyo ya kawaida Ndege aina ya bundi ameonekana Bungeni akiwa juu kabisa. 

Spika wa bunge, Job Ndugai, amemshuhudia Bunge huyo laivu na kusema alipomuona alichanganyikiwa kidogo na kisha akawatoa hofu Wabunge kuwa kwa Dodoma kumuona ndege huyo mchana si tatizo isipokuwa ukimuona usiku ndio unaweza kuogopa.

Watumishi wa Bunge waliingia ndani ya jengo hilo kwa ajili ya ukaguzi na kumuona ndege huyo juu ya paa la ukumbi wa Bunge.

Ndege huyu hakutoka licha ya maofisa hao kutaka kumtoa, aliruka kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Hata hivyo, haikujulikana  muda aliotoka na mahali alikoelekea lakini Spika Job Ndugai akasema ni mambo ya kawaida kwa Dodoma.

"Waheshimiwa wabunge, asubuhi tumeanza kumwona Bundi ndani ya jengo hili, lakini kwa Dodoma Bundi wa mchana hana madhara kwa hiyo ni mambo ya kawaida kabisa," amesema Ndugai.

==>>Msikilize spika hapo chini

VIDEO: Muswada wa Vyama Vya Siasa Ulivyowasilishwa Bungeni Leo

$
0
0
Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya vyama vya Siasa wa mwaka 2018  umewaasilishwa bungeni leo Jumanne Januari 29, 2019 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama.

Mhagama amesema pamoja na mambo mengine muswada huo unalenga kumpa Msajili wa Vyama vya Siasa kuhakiki chama cha siasa wakati wowote.

==>>Msikilize Hapo chini

Taarifa MUHIMU Toka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais IKULU

Dawa Bora na Imara ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
Kifaru vidonge asilia hurefusha maumbile ya kiume nchi 6-8 dk 60 garantii mika 30- 40 .itakupa nahamu ya kufanya tendo la ndoa mara 4- 5 bila kuchoka au hamu kuisha, ina imalisha misuri  ya uume  na haina madhara kwa mtumiaji

Malelemba; inatibu presha kisukari, ngili, busha bila uperesheni, kiuno, kutopata choo vizuri, vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto, kisosono

Jirumba; kumvuta mume mke mpenzi mchumba kwa masaa 3 yoyote unae mtaka  uta mpata ..acha kuumiza roho bure hatakama una fanya nae kazi sehemu moja ila unaogopa kumuanza au muone mzee jirumba atakusaidia

Fika mbagara kwa wa mikoani shinyanga kahama mwanza kwa mawasiano piga 0713560943 /0762540447 dr jirumba

Rais Magufuli Akerwa na Vitendo vya Wakuu wa Wilaya Kuwaweka Watu Mahabusu

$
0
0
Rais John Magufuli amewaasa wakuu wa wilaya kutotumia vibaya sheria na mamlaka walizopewa ikiwamo za kuweka watu ndani na kuwatoa wakidai wamejifunza bila kupelekwa mahakamani.

Magufuli ameyasema hayo leo wakati wa kuwaapisha majaji 15 wa Mahakama Kuu na sita wa Mahakama ya Rufani.

Amesema siyo haki na viongozi wengi wamezungumza kuhusu suala hilo na yeye anarudia kwa sababu kama mkuu wa wilaya ana mamlaka hayo na mkuu wa mkoa akiamua kuweka watu ndani itakuwa ni vurugu, huku akibainisha kuwa mambo mengine yanahitaji kutolewa maelekezo tu.

Rais  Magufuli amesema ameamua kumtoa katika uongozi aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Mwanga, Aaron Mbogho na kumhamishia katika kitengo cha wadudu kwa sababu yeye ni mtaalamu wa eneo hilo.

Amesema yaliyokuwa yakitokea wilaya ya Mwanga ya kuwaweka watendaji wa Serikali ndani akiwamo katibu tawala, mkurugenzi kila mmoja alikuwa akiyaona huku vurugu zote zilikuwa zikianzia kwa kiongozi huyo.

“Hata katika mazungumzo yake amekuwa akisema yeye ni mtaalamu pekee wa wadudu Tanzania hakuna kama yeye hivyo nikaamua kumpeleka huko huenda atafanya vizuri...” amesema Magufuli.

Akizungumzia wilaya ya Tarime Rais Magufuli amesema kuna changamoto nyingi ndiyo maana aliamua kumuweka  (Charles Kabeho aliyekuwa kiongozi wa mbio za mwenye mwaka 2018) kwa sababu alikuwa akiona jinsi anavyokemea mabaya na kukataa kufungua baadhi ya majengo yaliyo chini ya kiwango.

“Nikaona ngoja nimpeleke huko kwa Wakurya akawakatalie, kwa wakurugenzi kulikuwa na nafasi zilizokuwa wazi na wengi mlikuwa mnakaimu tumeona kazi zenu nzuri hivyo kasimamieni kafanyeni kazi nzuri, kasimamieni mapato,”

“Nchi inahitaji mapato ya kwenda mbele, msiende mkaanze tena mabishano ya mkurugenzi na mkuu wa wilaya, nimeshazungumza kwa baadhi ya halmashauri ambazo kila siku mabishano nimewaacha kwanza nimewaambia wajirekebishe wameanza kufanya hivyo,” amesema

Akitolea mfano wa maeneo hayo kuwa ni Dodoma na Nyasa huku akisema uongozi ni pamoja na kushirikiana.

Uingereza Yaahidi Kuendelea Kushirikiana na Tanzania....Benki ya Dunia Yatoa Ushauri Namna ya Kuwekeza Kwenye Viwanda

$
0
0
Waziri Kakunda akiwa na Balozi wa Uingereza, Sarah Cooke
**
Timu ya wataalam elekezi wa Benki ya Dunia (WB) wameishauri Tanzania kuwekeza kwenye viwanda vya kuchakata mazao ili kuongeza thamani ya kilimo kwa lengo kumkomboa Mtanzania.

Watalaam hao jana Jumatatu Januari 28, 2019 wamekutana na waziri wa viwanda na Biashara, Joseph Kakunda na kumueleza kuwa ipo haja ya kuongeza nguvu katika eneo hilo ambalo kwa sasa linaonekana bado halikufanyiwa kazi vya kutosha.

Waziri Kakunda amekiri udhaifu huo na kueleza kuwa kumekuwa na changamoto lukuki zinazokwamisha uchakataji wa mazao nchini kubwa ikiwa ni ukosefu wa malighafi jambo linalosababisha viwanda vya aina hiyo visiwepo.

Alisema kwa sasa uchakataji wa mazao umekuwa wa kusuasua kutokana na upatikanaji wa mazao hivyo Serikali inafungua milango kwa wawekezaji kuja kuwekeza kwenye viwanda vya aina hii ili kuchakata mazao hapa na bidhaa kuuzwa nje.

 “Wametushauri vitu vingi kubwa likiwa ni kutuhamasisha kuweka nguvu kwenye uanzishwaji wa viwanda vya kuchakata mazao. Inatakiwa tuwe tunauza nje ya nchi bidhaa ambayo imeshatengenezwa si malighafi,” alisema.

“Tukiboresha mazingira ya biashara tupata wawekezaji wengi na kuongeza mapato kwa Serikali kwa sababu watu wengi watahitaji kufanya biashara Tanzania,” alisema.

Katika hatua nyingine Waziri Kakunda amekutana na Balozi wa Uingereza, Sarah Cooke ambaye alimueleza kuwa nchi yake imedhamiria kuendelea kuhamasisha wawekezaji kutoka Uingereza kuja Tanzania.

Balozi huyo ameeleza Uingereza itaongeza nguvu katika elimu ya ufundi stadi ili kuzalisha wataalam wengi watakaofanya kazi kwenye viwanda.

Kwa upande wake, Waziri Kakunda amemueleza Cooke kuwa  Serikali itaviwezesha viwanda vinavyomilikiwa na Waingereza ili viendelee kufanya kazi na kutoa ajira kwa Watanzania na kuzalisha bidhaa zitakazobeba nembo ya Tanzania.

Lulu Michael Agoma Kuzungumzia Taarifa za Kupigwa na Mchumba Wake

$
0
0
Mwigizaji Elizabeth Michael maarufu Lulu amesema taarifa za kuwa amepigwa na mchumba wake hataki kuzizungumzia kwa kuwa anaona zinalenga kumtoa katika njia yake anayotaka kwenda kwa sasa.

Akizungumza leo Januari 29 katika kipindi cha Joto la Asubuhi kinachorushwa na kituo cha redio E FM, amesema habari hizo zilianza kuenea baada ya kutangaza kampeni yake ya Save my Valentine wiki iliyopita.

“Kama umeshawahi kutazama filamu za mapigano mwishoni utaona adui anavyojaribu kufanya vitu vya kumhadaa sterling, hivyo ndivyo nilivyochukulia maneno haya,” amesema.

Ameongeza kuwa utakapofika wakati sahihi atalizungumzia hilo na kwamba kwa wakati huu angependa kuendelea na kampeni yake ya kusaidia wasiojiweza.

Akizungumzia kampeni hiyo ya kusaidia wenye uhitaji amesema itaendeshwa kwa fedha anazopata katika mauzo ya nguo zake lakini amewaomba watu binafsi na mashirika wanaotaka kushirikiana naye wajitokeze.

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Abdallah Mtolea Aapishwa Bungeni Leo

$
0
0
Mbunge wa Temeke (CCM), Abdallah Mtolea leo Jumanne Januari 29,2019 ameapishwa bungeni jijini Dodoma.

Mtolea ameapishwa baada kupita bila kupingwa kutokana na wagombea wa vyama vingine kukosa vigezo.

Alikuwa mbunge wa jimbo hilo kwa tiketi ya CUF na alijiuzulu Novemba 15, 2018 na kujiunga CCM.

Hata hivyo,  kiapo cha Mtolea leo kilikuwa tofauti na viapo vya wabunge wengine waliohamia CCM kutokea upinzani kutokana na kutokuwa na mbwembwe zilizozoeleka.

Mtolea aliingia akisindikizwa na wabunge wachache wa CCM. Mara baada ya kuapishwa na Spika, Job Ndugai alikwenda moja kwa moja kusalimiana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Profesa Adelardus Kilangi na  Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenister Mhagama.

Wakati Mtolea akiapishwa wabunge wa upinzani waliokuwepo bungeni ni wa CUF upande wa mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images