Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri awataka wakuu wa shule kuanzisha Club za vijana mashuleni

$
0
0
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewataka walimu wakuu wa Shule za Sekondari Nchini kushirikiana na Shirika la FEMA Hip kuanzisha club za vijana katika shule zao ili kutoa fursa za vijana mashuleni kupata elimu ya Afya ya uzazi na kujitambua.

Waziri Ummy alisema hayo juzi wakati wa maadhimisho ya miaka 20 tangu kuanzishwa kwa shirika hilo ambalo kwasasa lina uwezo wa kuwafikia vijana 15,000 kila mwezi na kuwalimisha masuala mbalimbali ya kiafya ikiwemo kujikinga na maabukizi ya ukimwi.

Aidha Waziri Ummy aliongeza kuwa yeye amekuwa mdau mkubwa katika kuhakikisha vijana Nchini wanapata elimu ya uzazi nchini ikiwezekana hata mtoto wa darasa la tano na kuwafanya kutambua angalau kulinda mwili wao kwani siku hizi watoto wanapevuka katika umri mdogo.

Aliongeza kuwa mwelekeo wa Serikali ni kuwa na uchumi wakati lakini hatuwezi kufikia hapo kama bado kati ya wasichana 100 wasichana 27 wanapata mimba katika umri mdogo hivyo kuwa na mzunguko wa umasikini usio kwisha.

Aliwapongeza FEMA kwa kuanza kupunguza masuala ya elimu ya Afya na uzazi nakuanza kujielekeza katika masuala ya uwezeshaji wa wa vijana kiuchumi kwani kama utampatia elimu bila kuwawezesha kiuchumi matatizo yao yanabaki palepale.

Amelitaka shirika hilo kuanzisha pia masuala ya elimu ya lishe kwa kuwa Tanzania kwasasa inakabiliwa na tatizo la udumavu ambapo kila watoto 100 watoto 34 wenye umri chini ya miaka 5 wamedumaa.

Shirika la FEMA limitimiza miaka 20 tangu kuanzishwa kwake na limekuwa likijihusisha na utoaji na uhamasishaji vijana kujikinga na ukimwi, kuwapa matumaini wa wathirika wa ugonjwa wa ukimwi, kutoa elimu ya Afya uzazi kwa vijana, kuwawezesha vijana kubuni namna bora za kujiwezesha kiuchumi kupitia club za FEMA Hip mashuleni lakini pia kwa kupitia vyombo vya habari.

Usiteseke Tena na Matatizo ya Nguvu za Kiume.....Tumia Tiba Hii ya Asili

$
0
0
SUPER MKUNYATI MIX; ni dawa bora ya mitishamba iliyopo katika mfumo wa vidonge na unga yenye uwezo wa kutibu na kumaliza matatizo yote ya ukosefu wa nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile:-

  -kuwai kufika kileleni ndani ya dakika chache tu.
 -Kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa muda mrefu.
 -Kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu(punyeto) husababisha kuishiwa au kupungukiwa na nguvu za kiume.
 -Uume kusimama kwa kulegea au katikati ya tendo la ndoa unalala na kushindwa kusimama.

Epuka matatizo haya kwa kutumia dawa bora ya asili ya SUPER MKUNYATI MIX ni kiboko ya matatizo haya yanayowasumbua baadhi ya wanaume wengi.

Pia kuna dawa ya kutibu Presha,miguu kufa ganzi, tumbo kuuma chini ya kitovu, kisukari,ngiri, chango aina zote na nk, matatizo haya nayo uchangia matatizo haya ya ukosefu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile madogo na uume mfupi.

KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA MAUMBILE MADOGO NA UUME MFUPI?  Usikate tamaa ondoa maradhi yako  hayo maana matatizo haya yamekuwa yakiathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti na sana na wanaume wengine kwa kushindwa kumlizisha mwanamke.


MDINDADINDA MIX, ni dawa ambayo inarefusha na kunenepesha maumbile na itakufanya uwe na uume saizi uipendayo.Dawa hizi za asili za mitishamba zipo katika mfumo wa vidonge na unga na hazina madhara kwa mtumiaji.

JABABILA;- ni dawa ya mvuto wa mapenzi ,mchumba, mke, mume aliyekuacha atakurudia ndani ya siku moja tu na atakutimizia utakacho.

ITALIGULA;- ni dawa ya biashara  na hata kama umezurumiwa utalipwa mapema ,kupata kazi, kupanda cheo. Ofisi zetu zinapatikana DAR ES SALAAM, SONGEA - BOMBAMBILI, SHINYANGA - KAHAMA MJINI. na pote pale ulipo utaipata huduma hii,kama huna nafasi utaletewa hulipo.Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR. MACHIMKENDA simu no ,0717 339771

Kesi ya Polisi Wanaotuhumiwa Kusindikiza Dhahabu za Mabilioni ya Pesa Jijini Mwanza Yapigwa Kalenda

$
0
0
Shauri namba 1/2019 la uhujumu uchumi, rushwa na kutakatisha fedha dhidi ya watu 12 wakiwemo askari polisi wanane katika mahakama ya hakimu mkazi Mwanza limetajwa leo Jumatatu Januari 28, 2019 na kuahirishwa hadi Februari 11, 2019 kwa kuwa upelelezi haujakamilika.

Wakili wa Serikali, Castus Ndamugoba ameiambia Mahakama kuwa upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na kuomba tarehe nyingine ya kutajwa.

Kwa mara ya kwanza, washtakiwa walifikishwa mahakamani Januari 11, 2019 wakidaiwa kuhusika na sakata la kilo 319.59 za dhahabu yenye thamani ya zaidi ya Sh27.018 bilioni na fedha taslim Sh305 milioni zilizokamatwa zikisafirishwa kutoka Mwanza kwenda Geita.

Mbele ya hakimu mkazi, Gwai Sumaye, mawakili watatu wa Serikali, Castus Ndamugoba, Robert Kidachi na Jackaline Nyantoro waliieleza mahakama kuwa washtakiwa walitenda makosa hayo kati ya Januari 4 na 5, 2019.

Wanaokabiliwa na shauri hilo ambao hawakutakiwa kujibu lolote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na uwezo kisheria wa kusikiliza shauri hilo ni aliyekuwa mkuu wa operesheni mkoani Mwanza, mrakibu mwandamizi wa polisi, Morice Okinda, E. 6948 D/CPL. Kasala, F. 1331 PL. Matete, G. 6885 D/C Alex na G. 5080 D/C Maingu.

Wengine ni G. 7244 D/C Timothy, G. 1876 D/C Japhet, H. 4060 D/C David Kadama, Hassan Saddiq, Emmanuel Mtemi, Kisabo Nkinda ambaye pia anafahamika kwa jina la Paulo Nkinda na Sajid Hassan.

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

PICHA: Spika Ndugai Aongoza Kikao Cha Kamati Ya Uongozi Jijini Dodoma.

$
0
0
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha kamati ya uongozi cha kujadili ratiba za shughuli za Bunge katika Mkutano wa kumi na nne (14) kilichofanyika leo tarehe 28 Januari, 2019 katika ofisi ya Bunge jijini Dodoma, ikiwa ni maandalizi ya Mkutano wa kumi na nne (14) wa Bunge la 11 unaotegemewa kuanza kesho tarehe 29 Januari, 2019 Bungeni Jijini Dodoma.

Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson akizungumza  na wajumbe wa kamati ya uongozi wakati wa kikao cha kujadili ratiba za shughuli za Bunge katika Mkutano wa kumi na nne (14) kilichofanyika leo tarehe 28 Januari, 2019 katika ofisi ya Bunge jijini Dodoma. Ikiwa ni maandalizi ya Mkutano wa kumi na nne (14) wa Bunge la 11 unaotegemewa kuanza kesho tarehe 29 Januari, 2019 Bungeni Jijini Dodoma.
Wajumbe kamati ya uongozi wakiwa kwenye kikao cha kujadili ratiba za shughuli za Bunge katika Mkutano wa kumi na nne (14) kilichofanyika leo tarehe 28 Januari, 2019 katika ofisi ya Bunge jijini Dodoma,  ikiwa ni maandalizi ya Mkutano wa kumi na nne (14) wa Bunge la 11 unaotegemewa kuanza kesho tarehe 29 Januari, 2019 Bungeni Jijini Dodoma.

Wawekezaji kutoka Austria wavutiwa na mazingira ya uwekezaji nchini

$
0
0
Afisa mwandamizi wa Ubalozi wa Austria wenye makazi yake Nairobi, Kenya. Bw. Kurt Muellauer akifungua Kongamano la Biashara lililoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Chama cha Wafanyabiashara, Wakulima na Wenyeviwanda Tanzania (TCCIA) na Ubalozi wa Austria. 

Kongamano hilo nimwendelezo wa jitihada za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania nchini Ujerumani ambao unawakilisha pia nchini Austria na wadau mbalimbali katika kutekeleza diplomasia ya uchumi. 

Pamoja na mambo mengine kampuni 8 kati 16 zinatarajiwa kufanya ziara jijini Dodoma tarehe 29 Januari kwa lengo la kukutana na Mawaziri wa Kilimo; Nishati; Fedha na Mipango; Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto na Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. 

Kongamano hilo limefanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi wa Uhamasishaji Uwekezaji wa TIC, Bw. John Mnali, pamoja na wadau wengine wakimsikiliza kwa makini Bw.Muellauer (hayupo pichani). 


Baadhi ya wawekezaji kutoka Austria nao wakifuatilia kongamano hilo.

Tanzania na Uganda zakubaliana kumaliza majadiliano ya Bomba la Mafuta mwezi Juni mwaka huu

$
0
0
 Na Teresia Mhagama, Kampala
Serikali za Uganda na Tanzania zimekubaliana kuwa, majadiliano mbalimbali yanayohusu utekelezaji wa mradi wa Bomba la mafuta Ghafi kutoka Hoima Uganda hadi Tanga Tanzania yakamilike ifikapo mwezi Juni mwaka huu  ili kuendelea na hatua ya ujenzi wa bomba hilo.

Hayo yalielezwa kwa nyakati tofauti jijini Kampala na Waziri wa Nishati wa Tanzania, Dkt Medard Kalemani na Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini wa Uganda, Irene Muloni mara baada ya kufanyika kikao cha Mawaziri mbalimbali kutoka Uganda na Tanzania wanaohusika na mradi huo.

“ Kwa ujumla tumejipanga kuwa, majadiliano yote ya mradi na maandalizi mengine ya mradi kati ya pande zote mbili  yakamilike mwezi Juni mwaka huu ili ujenzi wa mradi pia uanze mwezi Juni  na tunataka kukamilisha mradi huu ndani ya miezi 36 mara baada ya ujenzi kuanza,” alisema Dkt Medard Kalemani.

Dkt Kalemani alisema kuwa,  kwa ujumla, mradi ulishaanza kutekelezwa kwa kufanyika kazi za awali ikiwemo tathmini ya mazingira  ambayo kwa upande wa Tanzania imekamilika na upatikanaji wa eneo kutapojengwa matenki matano yatakayohifadhi mafuta lita laki tano kila moja  mkoani Tanga ambapo taratibu za ujenzi zinaendelea.

 Aliongeza kuwa, mradi huo unatekelezwa hatua kwa hatua hivyo kuna kazi zinazoendelea kufanyika wakati  majadiliano yakiendelea ikiwemo kazi za utafiti wa kijiokemia, kijiolojia na kijiotekniko na kuna kazi zitakazofuata baada ya majadiliano kukamilika.

Vilevile alisema kuwa, mara baada ya kumalizika kwa majadiliano kati ya Serikali ya Tanzania na Uganda, hatua itakayofuata ni majadiliano ya kimkataba kati ya Serikali ya Tanzania na wawekezaji wa mradi ambao ni kampuni ya Total E&P  ya Ufaransa, Tullow Oil ya Uingereza na CNOOC ya China na pia  Serikali ya Uganda itafanya  majadiliano husika na wawekezaji hao.

Akizungumzia kikao hicho cha Mawaziri, Dkt Kalemani alisema kuwa, mara baada ya kusainiwa kwa mkataba wa mradi huo mwaka 2017, kulikuwa na masuala mengi ya kujadili lakini katika vikao mbalimbali vya ngazi ya Mawaziri, wameendelea kukubaliana katika masuala mengi yatakayowezesha mradi kusonga mbele.

Kwa upande wake, Waziri wa Nishati na Maendeleo ya Madini wa Uganda, Irene Muloni alisema kuwa  mazungumzo kati ya pande hizo mbili yamefanyika vizuri na yale waliyokubaliana, kila pande unaenda kuyawasilisha katika uongozi wa juu wa nchi kabla ya kuendelea na hatua nyingine za majadiliano.

“Kwa ujumla kuna majadiliano mbalimbali yaliyo mbele yetu ikiwemo majadiliano kuhusu ubia wa kampuni (shareholding agreement) ambayo tunatarajia yakamilike mwezi Juni ili kuweza kuanza ujenzi wa mradi,” alisema Muloni.

Vilevile alisema kuwa, Timu za Majadiliano ya Kitaifa kutoka Uganda na Tanzania (GNT) bado zina kazi kubwa ya kufanya na wanaamini kuwa wataendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha kuwa wananchi wa Uganda na Tanzania wanafurahia mradi huo muhimu.

Mawaziri kutoka Tanzania waliohudhuria kikao hicho ni Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Paramagamba Kabudi,  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba.

Serikali yamlilia Mama Abdul....Tazama Hapa Alichokisema Waziri Mwakyembe


Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Mvuto Wa Mapenzi

$
0
0
*************************
KIBOKO YA  MATATIZO YA  NGUVU  ZA  KIUME MAUMBILE MADOGO MVUTO  WA  MAPENZI .
MAGONJWA SUGU
*************************
Wanaume  wengi wana  upungufu wa  nguvu  za kiume nakuwa  na  maumbile madogo  ya kiume magonjwa kama  kisukari, presha, ngiri  korodani kuvumba, busha, tumbo kuunguruma na kujaa  gesi  na  kutopata  choo  vizuri, punyeto  NK.
___________________________
Huchangia kwa  kiasi kikumbwa upotevu  wa nguvu  za kiume tumia dawa nzuri ya  mitishamba ambayo haina madhara kwa mtumiaji ata uwe  na  miaka 80 inatibu na kumaliza matatizo  hayo:

 SUPER SHAFT 
********'****************
HII NI DAWA  YENYE  UWEZO  MKUBWA WA  KUOGEZA  NGUVU ZA KIUME MARA  DUFU NA MAUMBILE MADOGO  YA KIUME
************************
(1) Itakufanya uwe  na nguvu za  ajabu ukiwa unafanya tendo la ndoa.
___________________________
(2 ) Inaongeza hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi  ya mara  tatu bila kuchoka.
___________________________
(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni ndani ya dk 30 nakukupa nguvu ya ajabu.
___________________________
(4) Pia itakupa nguvu za kusimamisha uume wako barabara kama msumari wakati wa tendo la ndoa.
___________________________

NYATI POWER
*****************
INAREFUSHA NA KUNENE PESHA MAUMBILE YA KIUME  SAIZI UTAKAVYO kuazia Inchi 1 -8 unene sm 2-4.
*************************
(5) Itaimarisha mirija ya uume iliyolegea au kusinyaa.
___________________________
(6)lnasaidia kisafisha mishipa ya kwenye uume na hivyo kusaidia kuogeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume.
___________________________
(7) Usaidia kuurudisha nje uume ulioingia ndani.
___________________________
(8) Inasaidia kuogeza  manini  nyingi abazo vinaviini vya  uzazi.
___________________________
(9)Husaidia kutibu  madhara ya punyeto.
___________________________
Matumizi makali ya madawa  ya kizungu mirungi, bangi na  sigara.
*************************
TUNATIBU MAGONJWA YOTE SUGU, NGIRI, KORODANI KUVIMBA,  BUSHA BILA KUFANYIWA OPARESHENI, TEZI DUME, KISUKARI, PRESHA AINA ZOTE, UGONJWA WA MOYO STROKU. KWIKWI, KICHOMI MIGUU KUFA NGAZI NK
*************************
ANAPATIKANA MAGOMENI MIKUMI, KARIBU NA  KANISA KATOLIKI, TUMAINI HEARST CLINC NDIYO  SULUHISHO LA MATATIZO YOTE
*************************
PIGA  SIMU
📞0745495181 AU
📞0682644040 
*************************
WOTE  MNAKARIBISHWA
*************************
Kama huna nafasi ya kufika ofisini  kwetu  huduma  hii  utaletewa mahali  ulipo na wa mikoani  mtaipata kirahisi.
KWA MENGINEYO INGIA HAPA
*************************

Nkoma: Tiba Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
NKOMA
_________________________
NKOMA Ni dawa bora ya nguvu za kiume  yenye mchanganyiko wa mitishamba (7) yenye maajabu yafuatayo/

🔖 (1) inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimalisha misuli ya uume uliolengea wakati wa tendo la ndoa/
🔖 (2) Kurefusha maumbile ya kiume yaliyorudi ndani kuazia nchi 5 - 9/
🔖 (3) kunenepesha uume cm 5 ya upana itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15 - 20 kwa tendo la kwanza na utakuwa na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya 2-4 bila hamu kuisha/

📌 Na inatibu kabisa, unashauriwa uitumie dawa hii kama kinga ya magonjwa sugu./
 📌 Haijalishi umri hata kama una miaka 85 itumie huanza kufanya kazi dk 50 tu na haina madhara yoyote kwa mtumiaji/

📍📍📍📍📍📍📍📍📍
            MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA.
_________________________
🔖 (1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖 (2)Choo kama cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(4)Kaswende/
🔖(5)Gono/

📌Haya yote husababisha kuishiwa nguvu za kiume na kuwa na uume mdogo/
📌 Itumie leo, bado hujachelewa ni tofauti na nyingine.
_________________________
DR MAKOBA ANAPATIKANA DAR ES SALAAM, PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
___________________________
WASILIANA NA
Dr MAKOBA SIMU.
📞0754832349
📞0683490600
____________________________
*****************************

Jeshi La Polisi Jijini Mbeya Lakamata Watuhumiwa Mbalimbali wa Makosa ya Wizi, Kuingiza Bidhaa Nchini Kinyemela...Tazama Hapa

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu wanne [04] kutokana na tuhuma mbalimbali kama ifuatavyo:-
 
KUINGIZA BIDHAA NCHINI BILA KULIPIA USHURU.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia mtu mmoja dereva Bodaboda na Mkazi wa Boda Matenkini Wilayani Kyela aitwaye MUSA MAULID [23] akiwa ameingiza nchini bidhaa aina ya Uyoga – Soya Gold paketi 750 na mifuko laini ya rambo bello tatu [03] toka nchini Malawi bila kulipia ushuru.
 
Mtuhumiwa alikamatwa Januari 24, 2019 saa 06:45 asubuhi huko katika Road Block Kayuki iliyopo Kata ya Ilima, Tarafa ya Pakati, Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya. Mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika. Bidhaa zilizokamatwa zimekabidhiwa idara ya forodha kwa hatua zaidi za kisheria.

KUINGIZA BIDHAA NCHINI BILA KULIPIA USHURU.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia mtu mmoja Mkazi wa Lwangwa – Busokelo Wilayani Rungwe aitwaye BAHATI KASUNGULA [35] akiwa na vitenge doti 36 toka nchini Malawi akiviingiza nchini bila kulipia ushuru.

Mtuhumiwa alikamatwa Januari 25, 2019 saa 16:30 jioni huko katika Road Block Kayuki iliyopo Kata ya Ilima, Tarafa ya Pakati, Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya. Bidhaa zilizokamatwa zimekabidhiwa idara ya forodha kwa hatua zaidi za kisheria.

KUPATIKANA NA MALI IDHANIWAYO KUWA NI YA WIZI.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia mtu mmoja JUHUDI KASYUPA [25] Mkazi wa Majengo Wilayani Chunya akiwa na mali mbalimbali zinazodhaniwa kuwa ni za wizi.
 
Mtuhumiwa alikamatwa Januari 27, 2019 saa 13:30 mchana katika msako uliofanyika huko katika Kijiji cha Majengo, Mtaa wa Pili, Kata ya Nkung’ungu, Tarafa ya Kipembawe, Wilaya ya Chunya, Mkoa wa Mbeya. Vitu alivyokamatwa navyo mtuhumiwa ni:-
  1. Box moja la Daftari ndogo,
  2. Radio moja muundo wa sub woofer aina Aborder na Spika zake mbili, spika moja aina ya sony,
  3. Deki moja aina ya Samsung,
  4. Betri moja ya Sola aina Sundar,
  5. Screen moja ya Computer Dell,
  6. T.V moja aina Tandar,
  7. Kopo moja la rangi Cream,
  8. Stablizer moja,
  9. Solar inveter moja,
  10. Waya wa cable mmoja,
  11. Solar panel moja aina ya oceanic wat 4o
Aidha baada ya mtuhumiwa kupekuliwa alikutwa na vifaa mbalimbali vya kuvunjia ambavyo ni nondo, bisibisi moja vitu vyote hivyo vilikutwa ndani kwake Mtuhumiwa alipohojiwa kuhusu umiliki wake alishindwa kuelezea. Upelelezi unaendelea.

KUPATIKANA NA MALI IDHANIWAYO YA WIZI.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la JUMA ADAMSON [23] Mkazi wa Mbozi Mkoa wa Songwe akiwa na copper plate tatu [03] mali idhaniwayo ni ya wizi.
 
Mtuhumiwa alikamatwa Januari 27, 2019 saa 10:00 asubuhi katika msako uliofanyika huko mlima Reli, Kata ya Utengule Usongwe, Tarafa ya Usongwe, Wilaya ya Kipolisi Mbalizi, Mkoa wa Mbeya. Baada ya mahojiano imebainika kuwa mtuhumiwa ni kati ya wahalifu sugu wanaofanya wizi wa kushusha mizigo katika milima Songwe, Iw ambi, na mlima nyoka pindi magari ya mizigo yanapokuwa yakipanda mlima kwa mwendo mdogo. Upelelezi wa ushauri hili unaendelea na mara baada ya kukamilika mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani.
 
Imetolewa na:
[ULRICH O. MATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 62

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   
Wakanishusha kwenye moja ya kituo waendesha bajaji na pikipiki, nikangia kwenye moja ya bajaji na kuondoka eneo hili na safari ya kurudi hotelini ikaanza majira haya ya saa tatu kasoro usiku. Simu yangu ikaanza kuita, nikaitazama na kukuta ni namba kutoka nchini Ujerumani. Nikaipokea kwa haraka na kuiweka sikioni mwangu.
“Ethan”
Niliisikia sauti ya Mery akiniita huku akilia lia.
“Naam”
“Mama hali yake mbaya na kama inawezekana rudi Ujerumani, anahitaji kukuambia neno la mwisho kabla ya kukata roho”
Mwili mzima ukahisi kuzizima na viungo vyote vikafa ganzi, nikajikuta mapigo ya moyo yakinienda kasi hadi jasho likaanza kunitiririka mwilini mwangu.

ENDELEA
“Ethan unanisikia?”
“Ndio ninakusikiliza dada”
Nilizungumza kwa kujikaza tu.
“Fanya uje, ninaogopa nipo peke yangu huku”
“Sawa ngoja niangalie maswala ya usafiri”
“Sawa”
Simu ikatwa, nikashusha pumzi nyingi sana huku nikifikiria ni kitu gani ninacho weza kukifanya mtu. Mtu wa kwanza kunijia kichwani mwangu ni Camila mwanamke ninaye mpenda kuliko kitu chochote kwenye maisha yangu. Nikaitafuta namba yake kwenye simu yangu kwa haraka na nikaipata, nikaipga na kuiweka sikioni mwangu, simu yake ikaita baada ya sekunde kadha ikapokelewa.
“Ndio mume wangu”
“Upo wapi?”
“Nipo nyumbani baby, tunapata chakula cha usiku”
“Inabidi twende Ujerumani leo hii hii”
“Leo!! Kuna tatizo gani mume wangu?”
“Hali ya mama ni mbaya sana na anahitaji hospitalini. Hivyo pakiza kili kitu chako nina imani usiku huu utaweza kufika Dar, hapa nitashuhulikia maswala ya ndege ya kukodi”
“Sawa mume wangu”
 
Camila alinijibu kwa sauti ya unyonge kisha nikakata simu. Nikaingia kwenye mtandoa wa google, nikatafuta ni shirika gani ambalo lina ndege za kukodi, kwa habati nzuri nikapata shirika moja liitwalo THRIPPLE P AIR WAYS. Nikaangalia baadhi ya ndege zao ambazo ni private jet. Nikaridhika nazo, nikachukua namba yao ya simu na kuwapigia.
“Karibu Tripple P Air Ways, unazungumza na Liliana, nani mwenzangu”
Niliisikia sauti ya kike nzuri sana ambayo kidogo ikanita hata ujarisi wa kuzungumza kama mweume mwenye pesa zake.
“Mimi ni Ethan, ninahitaji ndege ya kukodi kuelekea nchini  Ujerumani”
“Karibu sana, unahitaji kwa lini”
“Nahitaji kwa leo, nimeona ndege moja aina ya Gulfstreem N60983. Nina imani kwamba ipo nchini Tanzania”
“Ndio muheshimiwa inapatikana. Kutoka hadi Tanzania hadi Ujerumani, itakugarimu kiasi cha dola laki sita na nusu”
“Sawa niwekeeni, nafanya malipo ya awali kwenye akaunti yenu sasa hivi na nikifika hapo uwanja wa ndege kwenye ofisi zenu nitafanya malipo mengine ya mwisho”
“Sawa karibu sana na akaunti namba yetu ndio hiyo iliyopo kwenye tovuti yetu”
 
“Ninashukuru sana”
Nikakata simu na kwa mara kadhaa dereva huyu bajaji macho yake yote anayaelekezea kwangu.
“Kaka wewe ndio yule Ethan, huku tumezoea kukuita Messi?”
“Ndio”
“Aisee tukifika tunapo kwenda ninaomba tuweze kupiga picha japo moja”
“Sawa”
Tukafika hotelini. Dereva akatoa simu yake, akasimama pembeni yangu na kuanza kupiga picha kadhaa huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana. Nikamkabidhi kiasi cha pesa ambacho hata sikuzihesabu. Nikakimbilia ndani ya hoteli, nikaingi kwenye lifti na kuelekea juu gorofani. Nikaingia chumbani kwangu, kwa haraka nikavua nguo zangu zote nilizo zivaa. 

Nikafungua laptop yangu na kuingia kwenye akaunti yangu ya benki ya Bacrays na kuhamisha kiasi cha dola laki tatu na nusu kwenye akaunti ya shirika hili la ndege kisha nikaingia bafuni, kwa haraka nikaoga kisha nikarudi chumbani. 

Nikaweka begi langu juu ya kitanda na kuanza kuweka nguo zangu kadhaa. Nikampigia Camila simu yake, kwa bahati mbaya sikuweza kuipata hewani. Nikaumbuka kwamba kuna watu wa kuwaga. Nikampiagia simu Qeen kisha nikaiunganisha na Latifa.
 
“Jamani nina habari sio nzuri”
“Habari gani tena mkuu?”
“Hapa ninapo zungumza nipo kwenye harakati za kuelekea nchini Ujerumani, mama yangu ana umwa sana hivyo ninaondoka usiku huu na nimesha kodisha ndege moja ya kutupeleka huko”
“Ya kuwapelekea huko na nani?”
“Mimi na mke wangu”
“Unataka kusema kwamba unakwenda na Biyanka?”
“Nani aliye waambia Biyanka ni mke wangu, ninakwenda na mke wangu halisi”
“Mmm tuyaache na hayo pole sana Ethan”
“Nashukuru Latifa”
“Pole sana boss’
 
“Asante Qeen. Ila mipango yetu ipo pale pale hakuna jambo lililo haribika mume nielewa?”
“Tumekuelewa mkuu”
“Kitu kingine hakikisheni kwamba hamtoi siri hii kwa mtu yoyote”
“Tumekuelewa mkuu”
“Nashukuru”
Nikakata simu na kumpigia tena simu Camila huku nikimalizia kulifunga begi langu. Simu yake ikaanza kuita, nikaiweka simu yangu loud speaker na kuiweka kitandani na kuendelea kuvaa nguo haraka haraka.
 
“Mume wangu?”
“Mbona simu nakupigia haipatikani?”
“Tupo njiani na Dany, kuna sehemu nyingine hazina mtandao”
“Mumefikia wapi?”
“Sijajua ni wapi?”
“Hembu  mpe simu Dany”
“Ethan”
“Ndio, mume fika wapi?”
“Kwasasa tupo sehemu inaitwa Mkata, ila kama baada ya lisaa moja hivi na nusu tutafika hapo”
“Sasa nakuomba muje moja kwa moja uwanja wa ndege kwa maana mimi huko ndipo ninapo elekea kwa sasa, kuna mambo ninakwenda kuyamalizia kuyakamilisha kwa ajili ya safari”
“Sawa”
 
Nikakata simu, nikajiweka vizuri suti hii  ya rangi ya kaki niliyo ivaa. Nikaangaza huku na huku kwenye hichi chumba, nikaingiza laptop yangu kwenye begi langu la mgongoni kisha nikalivaa. Nikabeba begi langu hili la nguo na nikatoka chumbani humu. Moja kwa moja nikaeleka hadi mapokezi, nikawakabidhi kadi yao ya kufungulia mlango.
 
“Akija mke wangu muta mkabidhi hii kadi sawa”
“Una safiri?”
“Acha maswali mengi dada. Mkabidhi hii kadi umenielewa”
“Sawa”
Nikatoka nje na kuingiza begi kwenye gari langu hili. NIkawasha gari na kuanza safari ya kuelekea uwanja wa ndege. Picha ya sura ya mtoto Clara ikanijia kichwani mwangu, wasiwasi  wa kuondoka pasipo kuweza kumuaga ikanijaa moyoni mwangu.
 
‘Nitarudi’
Nilijifariji huku nikiogeza mwendo kasi wa gari langu. Kuna baadhi ya maeneo iliniladhimu kusimama kutokana na foleni za magari. Simu ikaanza kuita na nikaitazama na kuona ni namba ya Biyanka, moyo wangu ukaendelea kujawa na wasiwasi kwa mana sijamueleza juu ya hili swala la mimi kuondoka.
“Ndio mke wangu”
“Samahani mume wangu, tumeshindwa kupata ndege ya kundoka, hivyo tutarudi kesho asubuhi na kikao pia hakuna kwa usiku wa leo”
 
“Sawa, ila samahni mke wangu. Mama anaumwa nchi Ujerumani amelazwa na yupo mahututi na ana hitaji kuniona haraka iwezekanavyo”
“Ohoo Mungu wangu, ni nini tena kinamsumbua?”
“Madaktari bado hawajananiweka bayana. Hivyo sasa hivi ninaelekea uwanja wa ndege, nimepata moja ya tiketi kwenye shirika la ndege la  fly Emirates. Hivyo ninaondoka Tanzania usiku huu”
Nilimuongopea Biyanka.
“Jamani mume wangu nina kuoena huruma. Ningekuwepo tungeondoka na ndege ya baba”
“Usijali, tutawasiliana, yaani kichwa changu hapa kimevurugika sana, hadi nimesahau kukufahamisha”
“Natambua kwa habari kama hiyo ni lazima kichwa kichanganyikiwe mume wangu. Sawa, nitamueleza mama na baba na tunazidi kukuombea uweze kurudi salama”
 
“Nashukuru. Kampuni, ninakutegemea mpenzi wangu”
“Usijali mume wangu, nitasimama imara na hakuna ambacho kitakwenda vibaya”
“Sawa ninashukuru kusikia hivyo”
“Ukipanda ndege, samahani nina omba uweze kunifahamisha”
“Sawa”
Nikakata simu na kuendelea na safari yangu ya kuelekea uwanja wa ndege. Nikafanikiwa kufika uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Nikashuka kwenye gari langu na kuelekea moja kwa moja kwenye shirika la Thipple P Air ways,  nikapokelewa vizuri sana na muhudumu niliye zungumza naye.
 
“Tumeweza kupokea kiasi ulicho kituma. Ndege ipo tayari ni wewe kuweza kufanya malipo ya mwisho ili uweze kuondoka”
“Sawa”
Nikalipia kiasi cha mwisho cha pesa ambacho kimesalia. Tukaandikishana mkataba wa safari hii na endepo kutaotokea tatizo lolote ama ajali ya angani basi kampuni hii italipa familia yangu fidia ya asilimia hamsini ya kile kiasi nilicho lipia.
 
“Kama unahitaji kwenda kukagua ndege inaweza kuongozana na wataalamu wetu”
Lilian alizungumza mara baada ya kumaliza kulipa kiasi hichi cha pesa.
“Sawa, hili begi langu si ninaweza kuliacha hapa?”
“Ndio unaweza kuliacha tu hapa”
Nikaondoka na mainjinia wawili wa shirika hili, tukafika katika ndege hii, wakaanza kunionyesha sehemu moja baada ya nyingine. Ni ndege nzuri sana.
 
“Hii spidi mita yake ni kilomita 900 kwa lisaa moja. Sifa yake nyingine inaweza kwenda umbali wa kilomita 8, 000 bila ya kuongezwa mafuta, hivyo boss hapa upo salama”
Injinia huyu alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.
“Hivi hizi viwandani zinauzwa kiasi gani?”
“Mmmm inategemea na kile kitu unacho hitaji kutengenezewa na kiwanda husika.”
“Nashukuru nitalifwatilia hilo”
 
Tukarudi ofisini kwao. Simu yangu ikaanza kuita, nikaitoa mfukoni na kukuta ni Camila ndio anaye piga, nikaipoke.
“Tumefika uwanja wa ndege mume wangu njoo unichukue nje”
“Sawa”
Nikatoka hadi nje na kuwakuta Camila na Dany wakiwa wamesimama kwenye maeneo ya maegesho ya magari. Camila akanikumbatia kwa nguvu na kuanza kuninyonya lipsi zangu, alipo ridhika tukaachiana na nikasalimiana na Dany.
“Nashukuru kwa kumleta mke wangu”
“Usijali, ila poleni sana kwa mama kuumwa”
“Nashukru Dany, kuna gari ile BMW, kidogo ilipata itilfu ipo kwenye gereji moja hapa mjini”
 
Nikamuelekeza Dany gereji hiyo sehemu ilipo na akanielewa. Nikamkabidhi funguo ya gari langu hili jipya na kumuomba alipeleke kwenye kampuni jengo la kampuni yangu na funguo aikabidhiwe kwa mkurugenzi msaidizi ambaye ni Biyanka. Nikamtumia meseji Biyanka ya kumfahamisha kwamba gari atalikuta ofisini kwetu. Tukaagana na Dany kisa nikabeba mabegi mawili ya Camila na kuelekea kwenye ofisi za Tripple P air ways.
 
“Tupo tayari kwa safari”
“Sawa na marubani tayari wapo ndani ya ndege”
Lilian alizungumza huku akitutazama.
“Nashukuru”
Tukasaidiwa na vijana wabeba mizigo wa kampuni hii hadi ilipo ndege. Baada ya kuhakikisha kwamba mizogo  yote imepakizwa kwenye ndege, tukaingia kwenye ndege hii ya kifahari na safari ikaanza taratubu, baada ya ndege kuwa hewani Camila akafungua mkanda wa siti yake na kunifwata sehemu nilipo kaa, akanikalia mapajani mwangu huku akinitazama usoni mwangu.
 
“Nina hamu na wewe mume wangu”
“Hata mimi nina hamu na wewe mke wangu, ila tupo angani kwa sasa hatuwezi kufanya chochote”
Nilizungumza kwa unyonge huku nikizichezea chezea nywele nyingi za Camila. Taratibu akakilaza kichwa chake kifuani mwangu na ndani ya muda mchache usingizi ukaanza kumpiti, nami usingizi ukaanza kunipitia, nikajikaza nisilale, ila nikashindwa kujizuia na nikalala usingizi fofofo.Sauti ya rubabi akituomba tuweze kufunga mikanda, ndege ikataka kutua ikatustua kutoka usingizini. 
 
“Tumefika Ujerumani?”
Camila aliniuliza huku akinitazama usoni mwagu”
“Nahisi mke wangu”
Camila akarudi kwenye siti yake na kufunga mkanda, nikafungua kijipazia kidogo cha dirisa na kuchungulia nje, nikaanza kuona baadhi ya majengo marefu ya nchi hii ya Ujerumani, nikashusa pumzi kwani safari hii imetuchukua masaa mengi na sijui ni kwanini tumelala sana. Ndege ikatua uwanja wa ndege, hatukuhitaji kupoteza muda, tukakodi helicopter hadi katika hospitali aliyo lazwa bi Jane Klopp. Da Mery akatupokea, huku akilia kwa uchungu sana, nikakumbatiana naye huku nikihiataji kufahamu ni nini kinacho endelea kwa mama yetu.

==>.ITAENDELEA KESHO

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218,0789289945. TUNAPATIKANA MBAGALA ZAKIEM STENDI ya musanga

Ugonjwa wa Zinaa wa Kisonono (gonorrhea) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga

$
0
0
Kati ya magonjwa yanayoathiri watu wengi sana duniani ni magonjwa ya zinaa. Haya ni magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kupitia vitendo vya ngono. 

Vitendo hivi vya ngono vinaweza kuwa kujamiana, kupiga denda (kissing), vitendo vya ngono kwa kutumia mdomo (oral genital sex), kujamiana kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) iwe kwa mwanamume na mwanamke au kati ya wanaume wenyewe na hata wale wanaotumia vifaa vya kufanyia ngono (vibrators). 

Magonjwa ya zinaa huathiri sana watu walio katika umri wa miaka 15 – 24 lakini hata kwa watu wengine ambao wana umri chini au zaidi ya huu niliotaja pia yanaonekana kwa wingi.

Kuna magonjwa ya zinaa zaidi ya ishirini yanayotambulika duniani, baadhi ya magonjwa ya zinaa ni
  1.  Kisonono (Gonorrhoea – “Gono” kama wengi wanavyopenda kuita kwa kifupi).
  2.     Chlamydia
  3.     Kaswende (Syphillis)
  4.     Human papilloma virus (HPV)
  5.     HIV/AIDS (Ukimwi/Upungufu wa kinga mwilini)
  6.     Hepatitis B, C, A
  7.     Herpes virus
  8.     Trichomoniasis
  9.     Bacteria Vaginosis
  10.     Pubic lice (chawa kwenye nywele za kinena)
  11.     Chancroid
Magonjwa mengi ya zinaa yanatibika lakini kuna baadhi ambayo hayana tiba ya uhakika kama HPV, Hepatitis B na C, na HIV. Mengine yameanza kuwa sugu kutokana na matumizi ya dawa za antibiotics bila mpangilio, magonjwa hayo ni kama gono (gonorrhoea) na nk.
 
Visababishi vya magonjwa ya zinaa
  1. Vitendo vya ngono kama nilivyoeleza hapo awali
  2. Kuanza vitendo vya ngono mapema au wakati wa umri mdogo
  3. Kuwa na wapenzi wengi
  4. Kufanya mapenzi ambao sio salama
  5. Maambukizi kupitia michibuko au sehemu zilizokatika kwenye ngozi kwa kugusana na majimaji ya aina yoyote yanayotoka kwa mtu mwenye ugonjwa wa zinaa kama damu, shahawa nk. Hii inaweza kutokea bila mtu kujua kwani mara nyingi dalili za magonjwa ya zinaa zinakuwa hazionekani kwa wanawake na hata baadhi ya wanaume.
Watu wengi huhisi kitendo cha kula denda (kissing) ni salama lakini si kama wanavyofikiria kwani baadhi ya magonjwa kama kaswende, herpes nk, yanaweza kuambukizwa kupitia njia hii. 

Soma pia:Tatizo la Kutokwa na usaha Wakati wa Kukojoa 

Kondomu husaidia kupunguza maambukizi ya magonjwa ya zinaa kama gono, Chlamydia lakini sio kinga muafaka dhidhi ya magonjwa ya zinaa kama kaswende, genital herpes, genital warts, na magonjwa ya upungufu wa kinga mwilini (AIDS).

Kisonono (gonorrhea) ni nini?
Kisonono ni ugonjwa kati ya magonjwa ya zinaa unaosababishwa na bakteria aina ya Neisseria gonorrhoeae, bakteria ambao hukuwa na kuzaliana kwa haraka katika sehemu zenye unyevunyevu na joto mwilini kama kwenye shingo ya kizazi kwa wanawake (cervix), mirija ya kupitisha mkojo au shahawa (urethra), mdomoni na kwenye puru. Maambukizi mengi kwa wanawake hutokea kwenye shingo ya kizazi (cervix). 

Asilimia 75 ya ugonjwa wa gono hutokea kwa watu wenye umri wa miaka 15 – 29, wanawake walio katika umri wa miaka 15 -19 na wanaume walio katika umri wa miaka 20 – 24 wako kwenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa huu.
 
Ugonjwa huu huambukizwa vipi?
Ugonjwa huu huambukizwa kupitia vitendo vya ngono kupitia uke, njia ya haja kubwa (anus), kupitia mdomoni (oral sex). Ugonjwa unaweza kujitokeza kwenye sehemu za kujamiana, kwenye mdomo na kwenye puru (rectum). 

Soma Pia: Ugonjwa wa Zinaa wa Kaswende (Syphilis) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga 

Ugonjwa wa gono huonekana sana kwa vijana, watu wenye maisha duni kiuchumi, watu wanaoishi mijini, watu weusi na watumiaji madawa ya kulevya.
 
Dalili za ugonjwa wa kisonono
Dalili za ugonjwa wa kisonono huanza kujitokeza kuanzia siku ya 2 hadi ya 7 baada ya mtu kupata maambukizi na huweza kuchelewa kwa wanawake. Dalili ni kama zifuatazo

Kwa wanaume
  1. Kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa (burning sensation)
  2. Kutokwa na majimaji ya njano au meupe au ya kijani kutoka kwenye uume yanayoambatana na maumivu makali sana
  3. Wakati mwengine maumivu au kuvimba kwa korodani (swollen testicles)
  4. Maambukizi yakiwa kwenye puru (rectum) huambatana na maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa, kuwashwa sehemu za haja kubwa, na hata haja kubwa inaweza kutoka ikiambatana na damu, hii inatokea kwa wanaume na wanawake.
Kwa wanawake
Dalili kwa wanawake huwa si nyingi lakini wanawake wengi hawaonyeshi dalili zozote
  1. Maumivu au kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa
  2. Kuongezeka kwa kutoka majimaji kutoka kwenye tupu ya mwanamke ambayo ni ya njano au yamechanganyika na damu
  3. Kutokwa na damu kupitia tupu ya mwanamke kabla ya hedhi kufika.
  4. Kutokwa na damu baada ya kujamiana au baada ya tendo la ndoa
  5. Kichefuchefu
  6. Homa (fever)
  7. Kutapika
Vipimo vya ugonjwa wa kisonono
  1. Swab for culture – Kipimo hiki hufanyika maabara kwa kupandikiza bakteria baada ya kufuta sehemu za siri kwa kutumia swab ili kuona kama kuna bakteria wanaosababisha gono.
  2. Polymerase Chain Reaction (PCR)– Kipimo cha kuangalia vina saba (DNA) ya bakteria, ni ghali sana.
Tiba ya ugonjwa wa kisonono ni nini?
Tiba ya gono inahusisha na tiba ya ugonjwa wa Chlamydia kwani mara nyingi magonjwa haya huambatana kwa pamoja.Tiba hutegemea na umri wa mgonjwa na kama mtu ni mjamzito au la. 

Tiba ya gono ambayo sio sugu iliyo kwenye shingo ya kizazi (cervix), urethra na puru, dawa zinazotumika ni aina za cephalosporin dozi moja pamoja na dawa za aina ya macrolide antibiotics (mfano azithromycin) na za jamii ya penicillin (mfano doxycyclin) ili kutibu ugonjwa wa chlamydia. Mara nyingi kwa wale chini ya miaka 18 na wanawake wajawazito, hutibiwa kwa kuchomwa sindano.

Soma Pia: Saratani ya tezi dume : Madhara Yake, Dalili Zake, Chanzo na Tiba Yake

Fuata ushauri wa daktari kabla ya kutumia dawa hizi kwani dawa nyingi zina madhara kwa wajawazito (mfano doxycyclin). Ushauri nasaha hutolewa kwa wapenzi wote wawili na ni vizuri wapenzi wote wawili kutibiwa hata kama mmoja hana dalili za ugonjwa huu.
 
Madhara ya ugonjwa wa kisonono
  1. Kutoweza kuzaa kwa mwanamke (tasa) au kutoweza kutungisha mimba kwa mwanamume (infertility)
  2. Huweza kuathiri moyo (heart valves), ubongo,ngozi nk ambayo ni hatari sana kwa mtu yoyote.
  3. Madhara kwenye sehemu za maungio au jointi (joint inflammation)
  4. Kwa wanawake wale ambao hawajatibiwa wanaweza kupata ugonjwa wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) ambao huongeza asilimia ya mwanamke kuwa tasa.
  5. Wale wanawake ambao ni wajawazito na wameambukizwa gono wako kwenye hatari ya mimba kutoka au kuzaa mapema kabla mimba haijatimiza umri wake (preterm labor).
  6. Kwa wale wanaoambukizwa gono kipindi cha kukaribia kujifungua, wanaweza kuwaambukiza watoto wao na hivyo watoto kupata ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), kuwa kipofu (blindness), homa ya mapafu (pneumonia) na ugonjwa wa mifupa (septic arthritis).
Kinga ya kisonono
  1. Kutumia kondomu wakati wa kujamiana
  2. Kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu
  3. Kuacha vitendo vya ngono kama matumizi ya vifaa vya ngono hasa kwa wanawake mfano vibrators nk.
  4. Kwa wanawake wajawazito – Hakikisha unahudhuria kliniki mapema ili upate kuchunguzwa na kupatiwa tiba muafaka kama utagundulika na ugonjwa wa gono au ugonjwa mwengine wowote.
  5. Wanawake wajawazito wanashauriwa kujifungulia hospitali ili kama mtoto ameathirika na gono apate matibabu ya haraka baada ya kuzaliwa kuepusha kuwa kipofu.
  6. Epuka kufanya ngono na mtu aliyeambukizwa gono.

Jamhuri yakata rufaa kupinga Tido Mhando kuachiwa huru

$
0
0
Upande wa Jamhuri katika kesi ya matumizi mabaya ya madaraka na kusababisha serikali hasara ya Sh.milioni 887.1, umekata rufaa Mahakama Kuu kupinga uamuzi wa kuachiwa huru Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando.

Mahakama hiyo ilimwachia huru Mhando na Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi ambaye alisema sababu za kumwachia huru kuwa ni mikataba minne aliyoingia haikuwa na nguvu ya kisheria kwani haikusainiwa na wahusika akiwamo Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Hata hivyo, Wakili wa Serikali Leonard Swai alidai kuwa Jamhuri haujaridhika na hukumu hiyo kwamba pamoja na kwamba mikataba inadaiwa kuwa haikufuata sheria lakini mawakili walilipwa fedha,hasara  ambayo imesababishwa na na mshtakiwa.

Rufaa hiyo inasubiri kupangiwa jaji na tarehe ya kusikilizwa.

Katika kesi hiyo Tido alikuwa anakabiliwa na mashtaka manne ya kutumia madaraka vibaya na moja la kuisababishia Serikali hasara ya Sh milioni 887.1.

Kilichoendelea Leo Mahakamani Katika Kesi ya Wema Sepetu Kusambaza Video ya Ngono

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Jumatatu Januari 28, 2019 imeutaka upande wa mashtaka kuhakikisha upelelezi wa kesi inayomkabili mlimbwende wa Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu unakamilika kwa wakati.

Wema anakabiliwa na shtaka moja la kuchapisha video ya ngono na kusambaza katika mitandao ya kijamii.

Uamuzi huo umetolewa leo na Hakimu Mkazi, Maira Kasonde, baada ya upande wa mashtaka kudai kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Awali, wakili wa Serikali, Mosia Kaima amedai kuwa kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wake bado haujakamilika.

Aliiomba mahakama ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi wa shauri hilo utakuwa umekamilika ama la.

Baada ya wakili huyo kueleza hayo, wakili wa Wema, Ruben Simwanza aliieleza mahakama kuwa kesi hiyo imeshatajwa mara nne mahakamani hapo huku upelelezi wake ukiwa bado.

"Naomba upande wa mashtaka ujitahidi kukamilisha upelelezi kwa wakati kwa sababu shauri hili limeshatajwa kwa mara ya nne sasa, bila upelelezi wake kukamilika," amedai Wakili wa Utetezi.

Hakimu Kasonde baada ya kusikiliza hoja za pande zote ameahirisha kesi hiyo hadi Februari 13, 2019 itakapotajwa tena na kuwataka upande wa mashtaka kuhakikisha wanakamilisha upelelezi wao kwa wakati.

Katika kesi ya msingi, Wema anadaiwa kuwa Oktoba 15, 2018 katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam alichapisha video ya ngono na kuisambaza katika mtandao wa kijamii wa Instagram.

Mahakama Yamwachia Huru Aliyekuwa Mkurungenzi Mkuu Wa NIDA Na Wenzake Sita

$
0
0
Mahakama  ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuachia huru aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho (NIDA), Dickson Maimu na wenzake 6 waliokuwa wakikabiliwa na kesi  ya uhujumu uchumi na kusababisha hasara ya Sh.Bilioni 1.16 kwa sababu Mkurugenzi wa Mashtaka' (DPP) hana nia ya kuendelea  na mashtaka dhidi ya washtakiwa

Washtakiwa hao wameachiwa chini ya kifungu cha 91(1) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai sura 20 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Hata hivyo,  mara baada ya vigogo hao kuachiwa  huru na kutoka nje ya chumba cha mahakama, walikamatwa tena na kuwekwa chini ya ulinzi na polisi na baadae kupelekwa katika kituo cha polisi cha Kati.

Mkutano Wa 14 Wa Bunge La 11kuanza Kesho Jijini Dodoma

Wakuu Wa Mikoa Wakabidhiwa Awamu Ya Pili Ya Vitambulisho Vya Wafanya Biashara Ndogo Ndogo

$
0
0
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi leo jumatatu ya Januari 28,2019 amekabidhi vitambulisho milioni moja na laki moja vya awamu ya pili kwa ajili ya wafanyabiashara wadogowadogo ambavyo viliasisiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.

Balozi Kijazi amekabidhi vitambulisho hivyo kwa wakuu wa mikoa yote nchini Ikulu jijini Dar es salaam na kuwataka wakuu wa mikoa hiyo kuhakikisha vitambulisho hivyo vinatolewa kwa wahusika na kwa wakati  na kuongeza kuwa tayari kuna taarifa za baadhi ya watumishi wa halmashauri ambao wanaviuza vitambulisho hivyo kwa zaidi ya bei elekezi iliyotolea na Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na kuwataka wakuu hao wa mikoa kuwachukulia hatua za kinidhamu wale wore wanaokiuka agizo hilo.

Amewataka wakuu hao wa mikoa kusimamia kikamilifu zoezi hilo la ugawaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo wadogo huku akitaja idadi ya vitambulisho ambavyo kila mkoa utakabidhiwa

Amchinja mwanaye kisa wivu wa mapenzi

$
0
0
Mwanamke mmoja aliyetambulika kwa jina la Cecilia Paschal mkazi wa Kisimani wilayani Simanjiro Mkoani Manyara anadaiwa kumuua mtoto wake mdogo mwenye umri wa miezi sita baada ya kuibuka ugomvi kati yake na mumewe uliosababishwa na wivu wa mapenzi.

Inadaiwa kuwa Cecilia alitekeleza tukio hilo la kumchinja mwanaye kwa kisu na kitu kinachodhaniwa kuwa ni kisu, kisha kutaka kujiua mwenyewe kwa kumeza dawa za aina mbalimbali.

Akithibitisha tukio hilo, Kamanda wa polisi Mkoa wa manyara, Augustino Senga alipozungumza na waandishi wa habari amesema kuwa tukio hilo lilitokea Januari 20, majira ya saa 12 jioni.

“Chanzo cha tukio hili ni wivu wa kimapenzi kwa sababu kabla ya tukio, inaelezwa alikuta namba ya simu ya mwanamke katika simu ya mumewe, baada ya kuona namba ya simu ya mwanamke huyo ikitumika kuwasiliana na mumewe kila wakati, Januari 19, ndipo ukatokea ugomvi kati yao,’ alisema Kamanda Senga.

Kwa mujibu wa Kamanda Senga, mume wa Cecilia aliamua kuondoka nyumbani mpaka alipojulishwa madai ya mwanaye kuchinjwa ndipo akarejea nyumbani. 

Alisema  kuwa Mwili wa mtoto huyo umehifadhiwa katika Hospitali ya wilaya ya Hai kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images