Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

VIDEO | Pradetha - Nipepee

0
0
VIDEO | Pradetha - Nipepee

Wapinzani Warishishwa na Marekebisho yaliyofanyika Katika Muswada wa Vyama vya Siasa

0
0
Vyama 15 vya upinzani vya siasa 15 vilivyokuwa vikipinga muswada wa marekebisho ya sheria ya vyama vya siasa vimesema vimeridhishwa na marekebisho yaliyofanywa na Kamati ya Bunge ya Sheria na Katiba licha ya kasoro chache walizoomba zifanyiwe kazi.

Akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya vyama, leo Jumapili Januari 27, 2019 jijini Dar es Salaam, naibu katibu mkuu wa Chadema (Zanzibar), Salum Mwalimu amesema baada ya kutoa maoni yao mbele ya kamati hiyo hivi karibuni bungeni Dodoma, hoja nyingi walizopigia kelele zimesikilizwa.

"Tulipigia kelele suala la mafunzo na adhabu zake. Kamati baada ya kupitia hoja zetu, kwanza imepunguza adhabu kutoka Sh1 milioni hadi Sh500,000 na jela kutoka miezi 6 hadi mitatu," amesema Mwalimu.

Hata hivyo, amesema bado kuna utata umebaki wa kuchanganya elimu ya uraia na kujengeana uwezo ndani ya chama.

"Jambo kubwa ni kipengele kuamua utoaji wa elimu ya uraia, kimeondolewa. Yeye anazungumzia capacity building, tunaiomba kamati iangalie hili."

Amekitaja kipengele cha 3b kilichosema msajili anaweza kuomba taarifa kutoka kwa mwanachama yeyote na sasa kinasema ataomba taarifa kwa kiongozi yeyote.

"Bado tunaiomba kamati irekebishe iseme mawasiliano yafanywe kwa katibu mkuu kwa kuwa yeye ndiye 'contact person' tunaona nia mbaya ya msajili kuvuruga vyama," amesema.

Hata hivyo, amesema kuna mambo ambayo yamebaki bila kufanyiwa kazi, akiwaomba wabunge kuendelea pale kamati hiyo ilipoishia.

"Yapo mambo ya msingi kabisa tuliyajengea hoja yamefanyiwa kazi, lakini kuna vipengele ambavyo bado havijafanyiwa kazi, tunaomba vifanyiwe na ikishindikana vifafanuliwe na Bunge, asiyeshukuru kwa kidogo hawezi kushukuru kwa kikubwa," alisema Mwalimu.

Jeshi la Polisi Mbeya Lakanusha Habari ya Wahudumu wa Gesti Kuvamiwa na Kubakwa

0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linapinga vikali taarifa iliyotolewa na gazeti la Nipashe katika toleo Na.0579824 la Januari 26, 2019 yenye kichwa cha habari “Unyama wa kutisha” Majambazi wavamia gesti, wabaka wahudumu na kupora fedha….baada ya kuwapa vinywaji na biskuti zenye….

Ni kwamba Januari 24, 2019 saa 06.00 asubuhi iliripotiwa taarifa kuwa huko katika Bar na nyumba ya kulala wageni ijulikanayo kwa jina la Malema iliyopo maeneo ya Makunguru, Kata ya Manga, Tarafa ya Sisimba, Jiji na Mkoa wa Mbeya watu watatu waliofahamika kwa majina ya LUCY MWAPASI [36] Mhudumu na mkazi wa Mwanjelwa, CHRISTINA KIPESI [37] Mkazi wa Ituha na DICKSON ALLY [22] Mlinzi na Mkazi wa Makunguru waligundua kuibiwa simu zao za mkononi tano [05] na fedha taslimu za mauzo ya Bar na nyumba ya kulala wageni kiasi cha shilingi 701,000/= na watu wawili wanaowafahamu kwa sura.

Inadaiwa kuwa watu hao walifika katika nyumba hiyo ya kulala wageni na mmoja wapo alichukua chumba namba 11 ambapo aliishi hapo kwa siku tatu [03] hivyo kujenga mazoea ya karibu na wahudumu hao.

Januari 23, 2019 saa 23:30 usiku muda wa kufunga Bar ulipofika, walibaki wahudumu wawili huku mmoja akiwa wa Bar na mwingine wa nyumba ya kulala wageni na mlinzi ndipo watu hao walitoka chumbani kwao na kuwaambia wale wahudumu kuwa wanataka kuwapa offer ndipo walikubali na kuwanunulia juice ya azam na biskuti wahudumu hao, vitu ambavyo vinadaiwa kuwa na madawa yadhaniwayo ya kulevya na baada ya kula wote walianza kulegea na kulala na kupoteza fahamu na kisha watu hao kutekeleza adhima yao ya wizi.

Wahanga walipata msaada toka kwa wasamaria wema majira ya saa 09:00 asubuhi ambapo walipelekwa Hospitali ya Rufaa Mbeya kwa matibabu. Kwa mujibu wa mganga wa zamu aliyewafanyia uchunguzi na kugundua kuwa wahanga hao watakuwa wamekula/kunywa chakula chenye sumu au kinywaji chenye sumu hivyo aliwapatia matibabu kuondoa sumu mwilini na baada ya siku moja waliruhusiwa kutoka Hospitalini baada ya kupata nafuu.

Baada ya tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lilifanya upelelezi wa shauri hili na kubaini kuwa wahudumu hao hawakubakwa kama ilivyoripotiwa katika gazeti tajwa hapo juu. Aidha uchunguzi wa kitabibu uliofanywa na daktari wa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya unaonyesha kuwa wahanga wa tukio hili hawakubakwa.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linapinga vikali taarifa hiyo iliyotolewa na gazeti la Nipashe na kulitaka gazeti hilo kuomba radhi na kukanusha kupitia gazeti hilo taarifa waliyochapisha kwenye toleo Na. 0579824 la Januari 26, 2019 kwani ni kinyume na kifungu cha sheria ya “Media Service Act 36 (12) ya mwaka 2016 na kifungu cha sheria ya Media Service Act 50 (12) (1) (a) – (f) na (2) (a) – (c) ya mwaka 2016.

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Ziara Ya Kampuni Kubwa Za Uwekezaji Kutoka Austria Na India

0
0
Ujumbe wa Makampuni 16 makubwa ya uwekezaji kutoka Austria utafanya ziara ya kikazi hapa nchini kuanzia tarehe 28 hadi 30 Januari, 2019.

Ziara ya ujumbe huo nchini ni mwendelezo wa jitihada za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania nchini Ujerumani ambao unawakilisha pia nchini Austria na wadau mbalimbali katika kutekeleza diplomasia ya uchumi.  Pamoja na mambo mengine, diplomasia ya uchumi inalenga kwenye kutafuta na kuleta wawekezaji wenye nia ili wawekeze katika maeneo mbalimbali hapa nchini kwa lengo la kukuza uchumi na kuinua kipato cha wananchi.

Makampuni hayo ya Austria yana nia ya kuangalia fursa za uwekezaji hapa nchini katika sekta mbalimbali ikiwemo afya, mawasiliano ya simu, umeme wa kutumia maji na usafirishaji.

Ukiwa nchini, ujumbe wa Kampuni 8 umeomba kuonana na kufanya majadiliano na viongozi wa Wizara mbalimbali tarehe 29 Januari, 2019 jijini Dodoma akiwemo Mhe. Japhet Ngailonga Hasunga (Mb.), Waziri wa Kilimo; Mhe. Dkt. Medard Kalemani (Mb.), Waziri wa Nishati; Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb.), Waziri wa Fedha na Mipango; Mhe. Ummy Mwalimu (Mb.), Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto na Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Lengo la ujumbe huo kukutana na Mawaziri hao ni kutaka kufahamu kuhusu kazi na miradi mbalimbali inayosimamiwa na kutekelezwa na wizara hizo ili waone namna ya kuwekeza katika maeneo hayo.

Aidha, ujumbe huo utashiriki kwenye Kongamano la Biashara lililoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Chama cha Wafanyabiashara, Wakulima na Wenyeviwanda Tanzania (TCCIA) na Ubalozi wa Austria. Kongamano hilo litafanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam tarehe 28 Januari 2019.

Serikali ya Tanzania na Austria zina mahusiano ya kidiplomasia ya muda mrefu tangu uhuru ambapo Austria imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali kupitia mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) hapa nchini hususan katika sekta ya kilimo, afya na kuwajengea uwezo wanawake. Ziara ya ujumbe wa makampuni hayo ni dalili njema za kuanza kuimarika zaidi kwa mahusiano kati ya Tanzania na Austria.

Wakati huohuo, Ujumbe wa wawekezaji kutoka Kampuni ya Bureau Facility Services Pvt Ltd (CISB) ya India utafanya ziara hapa nchini kuanzia tarehe 29 Januari hadi 05 Februari 2019. Ziara hiyo ina lengo la kukamilisha utaratibu wa kuwekeza katika maeneo kadhaa ikiwemo ujenzi wa kiwanda cha madawa, kutafuta fursa ya kuwekeza kwenye miundombinu kama vile barabara na madaraja na ujenzi wa nyumba na hoteli. Wajumbe hao wanatarajia kukutana na kufanya mazungumzo na Mawaziri na Viongozi Wakuu Waandamizi wa sekta husika.

Ujumbe huo wa watu watatu utaongozwa na Bw. Alban Rodricks kutoka CISB ambaye alishafanya ziara hapa nchini mara kadhaa. Aidha, Ujumbe huo unatarajiwa kukutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Hamisi Kigwangala (Mb.), Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Ummy A. Mwalimu (Mb.), Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto na Mhe. Mhandisi Isack Kamwelwe (Mb.), Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano pamoja na Mhe. Angellah Kairuki (Mb), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji.

Katika ziara yao hiyo fursa mbalimbali za kiuwekezaji zinatarajia kuibuliwa pamoja na kujadiliana namna bora ya kushirikiana kati ya Tanzania na India.

Askofu Kakobe Akana Kumiliki Kadi ya CHADEMA....Awataka Wanaotukana Viongozi wa Dini Wakatubu

0
0
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe amesema yeye na kanisa hilo si wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Pia, amewataka viongozi wa Chadema waliotukana viongozi wa dini watubu hadharani, wasipofanya hivyo, chama chao kitatumbukia kwenye shimo refu zaidi, hawataweza kuinuka tena.


"Baada ya kumalizika kwa mkutano kati ya Rais Magufuli na viongozi wa dini, kuna baadhi ya viongozi wa siasa wa CHADEMA tena walioko katika baraza kuu waliwatukana viongozi wa dini kupitia mitandao ya kijamii, wajue viongozi wa dini wana nguvu katika nchi hii kuliko wao wanavyodhani.

" Viongozi ambao wamewatukana viongozi wa dini kwenye mitandao ya kijamii wanapaswa kutubu haraka sana, wakikaidi agizo hilo chama chao kitatumbukia kwenye shimo refu ambalo hakitainuka tena, kuwatukana viongozi wa dini kwa sababu hawakuzungumza yale mliyotaka kuyasikia ni utovu wa nidhamu ni kiburi", amesema Askofu Kakobe.

Kiongozi huyo wa FGBF ametoa kauli hiyo leo Jumapili Januari 27, 2019 jijini Dar es Salaam wakati wa ibada kufuatia siku za hivi karibuni kuonekana mara kadhaa kwenye hafla za Rais John Magufuli na kupewa nafasi ya kuomba.

Hata hivyo, amesema aliwahi kuhudhuria mkutano mmoja tu wa Chadema uliofanyika Mlimani City na kwamba katika mkutano huo alihudhuria si kama mwanachama bali kama baba ambaye anaweza kualikwa na watoto wengi.

"Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, sijawahi kuwa na mazungumzo naye; iwe kanisani au nyumbani au mahali popote. Hata katika mkutano ule nilipokelewa na viongozi wengine kabisa," amesema Askofu Kakobe.

Amesema hajawahi kuonana wala kuzungumza kwa simu na mbunge wa jimbo la Ubungo (Chadema), Saed Kubenea ambaye anaongoza eneo ambalo kanisa lake lipo.

"Kama hamjui, nimehudhuria mikutano mingi zaidi ya CCM kuliko Chadema. Nakumbuka wakati mmoja niliwahi kuhudhuria mkutano wa wazee kumuaga Rais Benjamin Mkapa, nilialikwa na Yusuph Makamba. Wakati ule nilihudhuria mikutano mingi kwa sababu Makamba ni rafiki yangu sana," amesema.

Askofu Kakobe amesema kuhudhuria kwake mikutano ya Rais Magufuli kumeibua mitazamo tofauti, wengine wakisema ameahidiwa ubunge na wengine wakisema amenunuliwa. Hata hivyo, amekanusha madai hayo.

Serikali Yatoa Mwezi Kwa Wizara, Bodi Ya Mazo Mchanganyiko hadi Februari 5 Wawe Wamekamilisha Uhakiki Na Malipo Kwa Wakulima Wa Korosho

0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Kilimo pamoja na Bodi ya Mazao Mchanganyiko wahakikishe hadi Februari 5 mwaka huu wawe wamekamilisha uhakiki na kuwalipa wakulima wote wa zao la korosho.

Pia amesema Serikali inaendelea kufuatilia mwenendo wa mazao makuu ya biashara kuanzia hatua ya uzalishaji hadi masoko yake likiwemo zao la korosho kwa lengo la kuwapatia tija wakulima.

Amesema zao la korosho ambalo awali soko lake halikwenda vizuri kutokana na utaratibu uliokuwa ukitumiwa na wafanyabiashara kwa kutenda bei ndogo na wakulima wenyewe kugomea bei hiyo.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Januari 27, 2019) wakati akizungumza na wadau wa zao la korosho mkoani Mtwara, lengo likiwa ni kupata taarifa juu ya mwenendo mzima wa bidhaa hiyo kwa msimu wa mwaka 2018/2019.

Amesema Serikali ilitoa nafasi kwa wafanyabishara kufanya    marekebisho ili waweze kununua bidhaa hiyo kwa bei nzuri bila mafanikia hali iliyopelekea Serikali kuamua kununua korosho zote ili wakulima wapate tija.

Naibu Waziri wa Kilimo Omary Mgumba amesema kuwa, taarifa iliyotolewa na timu ya uhakiki ilisema msimu wa 2018/2019 matarajia yalikuwa ni kuvuna tani 150,000 kutokana na kushuka kwa uzalishali.

“Lakini kwa kazi nzuri iliyofanywa na timu nzima ya Wizara, wilaya na mkoa na timu ya uhakiki hadi sasa korosho tulizozipokea ambazo ziko katika maghala ni zaidi ya tani laki mbili.”

Amesema zoezi hilo limewapa tija kubwa katika zao hilo tofauti na taarifa zilizowafikia hapo awali, ambapo wanatarajia baada ya zoezi hilo kumalizika watafikisha zaidi ya tani 200,000 ikiwa ni nyongeza zaidi ya tani 100,000.

Amesema, Wilaya inayoongoza kwa uzalishaji mkubwa hapa nchini ni Tandahimba amabpo wamefikia asilimia 96 ya uhakiki hadi kufikia jana huku zoezi la malipo kwa korosho zote zilizohakikiwa kwa mkoa wa Mtwara yamefikia asilimia 83.

Hata hivyo, Waziri huyo amesema kuwa fedha za kununulia korosho hizo zipo kwa kuwa Serikali imejipanga vizuri. Jumla ya sh bilioni 700 zimetengwa kwa ajili ya zoezi hilo ambapo hadi sasa zaidi ya sh. bilioni 400 zimeshalipwa wakulima waliohakikiwa hadi juzi.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Rais Magufuli afuta kodi ya ardhi kwa madhehebu ya dini

0
0
Rais wa Tanzania, John Magufuli amefuta kodi ya ardhi kwa madhehebu ya dini nchini kuanzia mwaka wa fedha ujao 2019/2020.

Hatua hiyo imetangazwa leo Jumapili Januari 27, 2019 na waziri wa Ardhi, William Lukuvi jijini Mbeya wakati wa ibada ya kuwawekea wakfu viongozi wa Jumuiya Kuu ya Kanisa la Kibaptisti Tanzania (BCT).

Lukuvi amesema Rais Magufuli ameiagiza wizara hiyo kutoyatoza kodi madhehebu ya dini kwa sehemu ambazo zimeandaliwa kwa ajili kutoa huduma za maombi.

"Rais ameagiza kuanzia Julai mosi mwaka wa fedha ujao madhehebu ya dini yasilipe kodi ya ardhi kwa maeneo ambayo huduma za maombi zinatolewa si sehemu ambazo kuna miradi ya kuingiza fedha ambayo tunajua madhehebu mengi yameanzisha," amesema Lukuvi.

Lukuvi amefafanua maagizo hayo tayari yametolewa kwa makamishna wa ardhi wa kanda na mikoa pamoja na maofisa ardhi wa majiji, manispaa na halmashauri nchi nzima.

Hata hivyo, Lukuvi ametoa nafasi ya kukutana na viongozi wa dini ambao wana migogoro ya ardhi kwenye maeneo ambayo wanatoa huduma.

"Najua kuna migogoro mingi kwenye maeneo ambayo mnatoa huduma hivyo nawakaribisha ofisini kwangu Dodoma na kama migogoro itakuwa mikubwa nitafika mpaka eneo la mgogoro," amesema Lukuvi.

“Wizara yangu imepewa jukumu la kutatua migogoro ya ardhi kabla ya mwaka 2020 na tusipotatua migogoro ya dini inaweza kupelekea uvunjifu wa amani nchini hivyo hatutaki kuifuga migogoro iliyopo,” amesema.

Awali, askofu wa kanisa la Baptisti nchini, Arnold Manase amesema kanisa lake ni moja ya madhehebu yanayoongoza kuwa na migogoro ya ardhi na baadhi ya waumini wa kanisa hilo.

"Kwa kuwa waziri mwenye dhamana upo naomba nafasi nije ofisini kwako nikueleze migogoro iliyopo ndani ya kanisa langu ili uangalie namna ya kuitatua maana migogoro imekithiri mpaka kufikia hatua ya kujenga makundi miongoni mwa waumini," amesema Manase.

BREAKING: Rais Magufuli atumbua Wakuu wa Wilaya wawili, ateua Majaji 21

0
0
Rais wa Tanzania, John Magufuli ametengua uteuzi wa wakuu wa wilaya za Tarime na Mwanga huku akiteua majaji 15 wa Mahakama Kuu na sita wa Mahakama ya Rufani.

Pia Rais Magufuli amewateua wakurugenzi 10 ili kuziba nafasi zilizoachwa wazi kwenye halmashauri za mikoa mbalimbali nchini.

Taarifa ya Rais Magufuli iliyosomwa leo Jumapili Januari 27, 2019 kwa vyombo vya habari na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi imeeleza kiongozi huyo ametengua uteuzi wa wakuu wa wilaya za Tarime, Glorious Luoga na Aaron Mbogho wa Mwanga.

“Nafasi ya Luoga imechukuliwa na Charles Kabeho aliyekuwa kiongozi wa mbio mwenge mwaka jana. Wakati nafasi ya Mbogho imechukuliwa na Thomas Apson,” amesema Balozi Kijazi.

Balozi Kijazi amewataja majaji wa Mahakama ya Rufani walioteuliwa ni Dk Rehema Sameji, Dk Mary Levira, Ignas Kitusi, Winnie Korosso, Lugano Mwandambo  na Sahel Barke.

Majaji wa Mahakama Kuu ni Cyprian  Mkeha, Dustan Ndunguru, Seif  Kulita,  Dk Mtemi Kilikamajenga, Zeferine Galeba, Dk Juliana Masabo,  Mustafa Ismail,  Upendo  Madeha, Willbard  Mashauri,  Yohanne Masara,  Dk Lilian Mongella,  Fahamu  Mtulya,  John Kahyoza, Athuman Kirati na Suzan Mkapa.

Balozi Kijazi amewataja wakurugenzi wapya walioteuliwa kuwa na halmashauri zao kwenye mabano ni Isaya Mbenje (Pangani) Dk Fatuma  Mganga (Hai) Regina Bieda (Tunduma) Jonas  Malosa (Ulanga) Ali Juma Ali (Njombe) Misana Kangura (Nkasi) Diocres Rutema (Kibondo) Neto Ndilito (Mufindi) Elizabeth Gumbo (Itilima) Stephen Ndaki (Kishapu).

Majaji hao watapishwa Jumanne Januari 29, 2019 Ikulu jijini Dar es Salaam na Rais John Magufuli. Pia, Ma DC na Wakurugenzi watapaswa kuhudhuria shughuli hiyo.


Asasi zataka muswada vyama vya siasa urekebishwe

0
0
Asasi za Kiraia zimesema licha ya muswada wa Sheria wa vyama vya siasa kuwa na baadhi ya vipengele vizuri, kuna haja ya vile vyenye upungufu kufanyiwa marekebisho kabla ya Bunge kuupitisha.

Viongozi wa asasi za kiraia walisema juzi Dar es Salaam kuna haja ya wabunge kuupa muswada muda wa kutosha kuuchambua kwa kina kabla ya kuupitisha kwani waathirika ni wao, wanasiasa na jamii.

 Fulgen Masawe kutoka Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) alisema baadhi ya maeneo mazuri kwenye muswada huo uliosomwa bungeni kwa mara ya kwanza Novemba 16 mwaka jana una kipengele cha kukataza vyama vya siasa kuanzisha vikundi vya ulinzi, kutoa mafunzo ya aina yoyote ya kijeshi, kiulinzi au yanayofanana na hayo kuepusha vitendo vya uvunjifu wa amani kwa siku za baadaye.

Pia wamesifu uwazi katika matumizi ya fedha, mapato na matumizi na uwazi katika maamuzi ya vyama vya siasa kwa kuzingatia maamuzi yanatolewa na viongozi wa ngazi ya juu bila kushirikisha wanachama. 

Akiorodhesha upungufu kwenye muswada huo, Masawe alisema kifungu cha 5A kinataka Msajili kupewa taarifa kimaandishi na taasisi yoyote ya ndani ama ya nje ya Tanzania itakapotaka kutoa mafunzo ya kiraia ya kujenga uwezo kwa chama cha siasa na kutaja wahusika, malengo na nyenzo zitakazotumika.

Msajili anayo nguvu ya kutoa kibali ama kukataa kufanyika kwa mafunzo hayo na endapo yatafanyika bila kibali, taasisi hiyo inaweza kupigwa faini ya mpaka Sh milioni 30 na watu watakaokutwa na hatia ya kwenda kinyume na kifungu hicho wanaweza kufungwa kati ya miezi sita mpaka mwaka mmoja gerezani. 

Kifungu cha 5B cha muswada kinampa nguvu, Msajili wa Vyama vya siasa nchini Tanzania kuomba na kupewa taarifa ya chama chochote cha siasa. 

“Ofisa wa chama cha siasa ambaye ataenda kinyume, yaani kutokutoa taarifa husika atakuwa ametenda kosa na akikutwa na hatia atapigwa faini ya Sh 1,000,000 mpaka Sh milioni 10 au kifungo kisichopungua miezi sita na kisichozidi miezi 12,”alisema Masawe.

Alisema hata baada ya adhabu hiyo, ofisa huyo au chama hicho kitatakiwa kutoa taarifa zilizohitajika na iwapo taarifa itaendelea kuminywa, basi chama hicho kinaweza kusimamishwa ama kufutiwa usajili. 

Akinyumbulisha zaidi vipengele hivyo, Mkurugenzi wa Twaweza, Aidan Ayakuze alisema Msajili ni mteule wa Rais ambaye analipwa mshahara na serikali hivyo ni vigumu kutofungamana na upande mmoja. 

“Nchi ilikuwa na maslahi kipindi cha chama kimoja lakini tangu vyama vingi, wabunge wanaangalia maslahi yao na vyama vyao kuliko umma, wanaangalia hoja imetolewa na upande gani wanapinga.

“Kifungu cha 6 cha muswada kinamlinda Msajili na wanyakazi wa ofisi yake dhidi ya kufunguliwa mashtaka: “Shauri halitafunguliwa dhidi ya Msajili, Naibu Msajili, Mkurugenzi au maafisa wengine chini ya Msajili kwa lolote watakalolifanya au kutolifanya kwa nia njema chini ya sheria hii,” alisema.

 Rais wa Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS), Fatma Karume alisema “Wabunge wa CCM wanadhani wanalindwa na muswada huu, wanasahau sheria ni msumeno, wanaenda kwenye uchaguzi, wanapaswa kujua kuna kura za maoni ni rahisi kukatwa watu wasiopendwa bila demokrasia hivyo wawe makini,” 

Wakati asasi hizo za kiraia zikiendelea kukazia msimamo wake wa kutaka kufanya marekebisho kwenye muswada huo, tayari CCM kupitia kwa Katibu Mwenezi, Humphrey Polepole wameuunga mkono.

Trump Asalimu Amri....Serikali ya Marekani Yafunguliwa

0
0
Rais wa Marekani, Donald Trump ametangaza kufunguliwa kwa idara za serikali kuu ambazo zilifungwa kwa zaidi ya mwezi mmoja, baada ya kufikia makubaliano na kamati ya pamoja ya bunge.

Makubaliano yaliyofikiwa Ijumaa yataruhusu idara za serikali kuu kufunguliwa kwa kipindi cha wiki tatu mpaka Februari 15 wakati ambapo majadiliano yataendelea kufanyika kuhusu suala kuu la ulinzi wa mpaka.

Vyanzo vya habari katika Bunge la Marekani - Congress vinasema kuwa .Makubaliano yaliyofikiwa hayajumuishi fedha za ujenzi wa ukuta kwenye mpaka wa Marekani na Mexico.

Rais Donald Trump amesaini makubaliano ya kufungua tena serikali ya Marekani kwa kipindi cha wiki tatu; baada ya kuvunja rikodi ya kufungwa idara hizo za serikali kuu kwa muda mrefu kuliko wakati wowote.

Rais Trump amesema kuwa mkataba huo uliofikiwa utaiwezesha serikali kuendesha shughuli zake hadi Februari 15.

Amesema kuwa wafanyakazi wa serikali kuu watalipwa mshahara wao wote "kwa haraka iwezekanavyo."

Akizungumza akiwa White House, Rais Trump amesema makubaliano yamebainisha kuwa wanaweza kuelewana kwa ajili ya maslahi ya taifa la Marekani na watu wake.

Amesisitiza umuhimu wa ulinzi wa mpaka ili kuzuia uhamiaji haramu pamoja na uingiaji wa madawa ndani ya ardhi ya Marekani.

Trump amesema wajibu na kipaumbele chake cha juu ni kuilinda nchi na kulinda wamarekani wasiingiliwe na watu ambao ni wabaya na kuongezea kuwa Marekani inapenda kukaribisha wageni kutoka kile pembe ya dunia, lakini waingie kwa utaratibu unaotakiwa.

Mamia ya Watu Wahofiwa Kufa Baada ya Bwawa Kuvunja Kingo Zake Brazili

0
0
Takribani watu 200 hawajulikani waliko baada ya bwawa la maji kuvunja kingo zake katika mgodi wa kampuni ya chuma Kusini Mashariki mwa nchi ya Brazil.
 
Katika tukio hilo inadaiwa takribani watu tisa wamefariki dunia huku uongozi ukisema huenda idadi ya waliofariki ikaongezeka kwa kuwa karibu watu 200 bado hawajulikani walipo.
 
Maporomoko hayo yamewazika watu wengine waliokuwa katika kantini wakila chakula kwa kuwa ulikuwa muda ya mchana.
 
Inaelezwa kuwa mgodi huo unamilikiwa na kampuni ya uchimbaji madini ya Vale inayomilikiwa na Serikali ya Brazil.
 
Miaka mitatu iliyopita watu 19 walifariki kutokana na maporomoko mengine yaliyotokea kwenye mgodi unaomilikiwa na kampuni hiyo. Hadi leo eneo hilo bado linakabiliana na changamoto za kimazingira zilizotokana na maporomoko hayo.
 
Taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari nchini Brazil vimesema kuwa maji yaliyochanganyika na matope yaliwafunika mamia ya wafanyakazi wa shirika hilo na watu wengine.
 
Shughuli ya kuwatafuta manusura inaendelea karibu na mji wa Brumadinho, katika Jimbo la Minas Gerais.
 
Gavana wa jimbo hilo, Romeu Zema, amesema kuna hofu huenda watu wengi wamefariki katika tukio hilo.
 
Baadhi ya watu waliokwama kwenye matope, waliokolewa kwa kutumia helikopta baada ya barabara kuharibiwa.
 
Watu wengine wamehamishwa kutoka makazi yao kutokana na sababu za kiusalama.
 
Kwa mujibu wa Ofisa mkuu mtendaji wa Kampuni ya Vale, Fabio Schvartsman, theluthi moja ya wafanyakazi karibu 300 hawajulikani waliko.

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatatu ya January 28

Mkuu Wa Operesheni Maalum Za Jeshi La Polisi Nchini Ateta Na Kikosi Cha Kupambana Na Uhalifu Mkoa Wa Ruvuma

0
0
Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Nchini Naibu Kamishna DCP Liberatus Sabas, akizungumza na kikosi Maalum cha kupambana na uhalifu katika viwanja vya Kikosi cha kutuliza Ghasia mkoani Ruvuma, baada ya kuwasili katika ziara yake ya kikazi. (Picha na Jeshi la Polisi) 

 Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Nchini Naibu Kamishna DCP Liberatus Sabas katikati kulia kwake ni Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Ruvuma Kamishna Msaidizi ACP Pili O. Mande na kushoto kwake ni Mkuu wa Kikosi cha kutuliza Ghasia Mkoa wa Ruvuma ACP Omar K. Omari wakiwa katika picha ya pamoja na kikosi maalum cha kupamban na uhalifu mkoani humo. 

Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Nchini Naibu Kamishna DCP Liberatus Sabas, akishiliki mazoezi ya pamoja na kikosi maalum cha kupamba na uhalifu Mkoa wa Ruvuma baada ya kuwasili katika ziara yake ya siku moja mkoani humo. 


(Picha na Jeshi la Polisi)

Ugonjwa Wa Ukoma Hauna Uhusiano Na Imani Za Kishirikina

0
0
Na WAMJW -Mvomero, Morogoro.
“Ugonjwa wa ukoma hausababishwi na imani za kishirika bali ni vimelea vya magonjwa ambavyo huingia ndani ya mwili na kusababisha ukoma”

Hiyo ni kauli ya Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alipokuwa akizungumza na waathirika wa ugonjwa wa ukoma pamoja na wananchi katika maadhimisho ya siku ya Ukoma Duniani, wilayani Mvomero, katika Mkoa waMorogoro.

Dkt. Ndugulile amewaasa wananchi kuachana na imani za kishirikina kwa kuamini kuwa ya kwamba ugonjwa huo unahusika moja kwa moja na imani hizo za giza.

“Dhana ya kwamba ugonjwa huu ni wa kurogwa siyo kweli, ugonjwa wa ukoma hausababishwi na mtu kulogwa wala kutupiwa jini bali ni vimelea ambavyo huingia mwilini na kusababisha ugonjwa wa ukoma, ni watu kama mimi na wewe” anasema Dkt Ndugulile.

Aidha Dkt Ndugulile ametumia nafasi hiyo kuwaelimisha wananchi kuwa ugonjwa wa ukoma unatibika na kusema kuwa dawa za kutibu ugonjwa huo zipo na kuwaondolea hofu ya kuwa ugonjwa huo kutotibika. Hata hivyo Dkt. Ndugulile ametoa rai kwa wananchi wote kujitokeza mapema katika vituo vya kutolea huduma za afya kupata huduma za matibabu pindi wanapohisi kuwa na dalili za ugonjwa wa ukoma.

“Mtu yeyote ambaye anaanza kuona mabadiliko kwenye ngozi yake, anapata mabaka ambayo hayaelewi au kupoteza hisia pindi unapojigusa ni muda wa kwenda hospitalini kufanya uchunguzi na kama utagundulika kuwa na vimelea vya ugonjwa wa ukoma utapewa matibabu” alisisitiza Dkt. Ndugulile.

Dkt. Ndugulile amewataka wananchi kuwa mabalozi wa kuwaelimisha watu wengine juu ya dalili na athari za ugonjwa wa ukoma. “Niwaombe ndugu wananchi tuendelee kutoa elimu kuhusiana na ugonjwa huu ni ugonjwa ambao tunaweza tukauzuia na tusiwe na athari kwenye jamii na tusingependa kuona kwenye zama hizi watu wanapata athari za kudumu na wanapoteza viungo, hisia katika sehemu za miili yao au kuharibika ngozi kwa sababu ya kutopata matibabu mapema” alifafanua Dkt Ndugulile.

Naibu Waziri huyo wa Afya amesema kuwa Serikali ipo katika hatua nzuri za kutokomeza ugonjwa wa ukoma nchini licha ya changamoto ambazo zipo katika baadhi ya maeneo sugu ambayo ugonjwa huo umeonekana kuwa ni tatizo. 

“Takwimu zinaonyesha kuwa takribani watu 1993 huugua ugonjwa wa ukoma kila mwaka huku mikoa ya Lindi, Rukwa, Mtwara, Pwani, Tanga, Geita, Dodoma, Tabora, Kigoma na Mkoa wa Morogoro ikiwa na idadi kubwa ya wagonjwa” alisema Dkt. Ndugulile.

Sasa hivi tumepiga hatua kubwa, tunajua jinsi gani ugonjwa unaambukizwa, na namna ya kuutibu pamoja na kujikinga dhidi ya maambukizi mapya, naamini kwa mikakati iliyopo tunaweza kuutokomeza ugonjwa huu.

Akizungumiza mikakati iliyopo Dkt Ndugulile amesema kuwa pamoja na elimu ambayo wamekuwa wakiitoa, Serikali imehamishia nguvu kwenda kwenye jamii moja kwa moja kuwabaini wagonjwa wa ukoma. “Hatusubiri watu watufate, tumewekeza nguvu nyingi kwenye jamii na kuwafikia huko huko maeneo wanayoishi” alisema Dkt Ndugulile.

Kwa upande mwingine, Dkt Ndugulile amezindua Mpango wa Kingatiba ya Ugonjwa wa Ukoma mahususi kwa wale ambao wamekuwa wakiishi na wagonjwa wa ukoma ili waweze kujikinga kutopata ugonjwa huo na kutoa rai kwa wananchi wote ambao wamekuwa wakiishi na wagonjwa wa ukoma kujitokeza katika vituo vya huduma za afya kumeza dawa hizo za kujikinga na ukoma.

“Mtu mwenye ukoma na ambaye amekunywa dawa za kingatiba hawezi kusambaza ugonjwa huu na tunaweza kuishi na kushirikiana naye kufanya shughuli mbalimbali kimaendeleo” alisema Dkt Ndugulile na kuwaasa wananchi kuacha tabia za kuwanyanyapaa wenye ukoma.

Dkt Ndugulile ameipongeza taasisi ya GLRA kutoka Ujerumani inayojihusisha na kuwatunza watu wenye ukoma kwa kuwaanzishia miradi ya ujasiriamali na kuwaunganisha wahanga wa ugonjwa huo na jamii pamoja na kuwapongeza pia wagonjwa wa ukoma kujishughulisha na shughuli za uzalishaji kipato kuliko kuwa omba omba barabarani.

Awali akitoa salamu zake Rais wa Taasisi ya GLRA Bw. Patric Meisen amesema kuwa anafuraha kuona Tanzania na Ujerumani zikiwa na mahusiano mazuri na kuahidi kuendelea kuwasaida waathirika wa ugonjwa ukoma nchini.

“Tumekuwa tukifanya kazi na wataalam wa afya katika kuwatunza waathirika waugonjwa wa ukoma, hatujaishia hapo tuu, tumewasaidia waathirika wa ugonjwa huu kwa kuwapatia mitaji itakayowasaidia kujiongezea kipato ambacho kitawasaidia” alisema Bw. Meisen.

Siku ya Ukoma Duniani huadhimishiwa kila jumapili ya mwisho wa mwezi Januari, ambapo kwa mwaka huu 2019, maadhimisho hayo kitaifa yamefanyika Wilayani Mvomero, Mkoa wa Morogoro yakiwahusisha wadau mbalimbali wa Sekta ya afya huku kauli mbiu ikiwa ni “Tutokomeze Ubaguzi, Unyanyapaa na Chuki dhidi ya Waathirika wa Ukoma”

Wimbo Mpya: Hanstone - Acha Lipite

0
0
Wimbo Mpya: Hanstone - Acha Lipite

Wimbo Mpya wa Lava Lava - Tukaze Roho

0
0
Wimbo Mpya wa  Lava Lava - Tukaze Roho

Waziri wa Mifugo Awabana Wawekezaji Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU)

0
0
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina, ametoa mwezi mmoja kwa wawekezaji walioingia mikataba ya uwekezaji kwenye Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu (MPRU) kulipa deni la shilingi milioni 331.2 wanalodaiwa vinginevyo Serikali itavunja mikataba na wahusika wote watakamatwa na kutaifishwa mali zao.

Waziri Mpina ametoa agizo hilo alipokuwa akizungumza katika ziara ya kutembelea Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu kwenye Visiwa vya Mbudya na Bongoyo ambapo ilibainika kuwa baadhi ya wawekezaji waliopewa maeneo kwenye hifadhi hizo kushindwa kuyaendeleza kwa mujibu wa mikataba sambamba na kushindwa kulipa tozo stahili za Serikali zilizowekwa kwa mujibu wa sheria.

Alisema Serikali haiwezi kukubali kuchezewa na wawekezaji ambao hawajajipanga na kuchelewesha uendelezaji wa fukwe na maeneo mengine ya urithi wa nchi yetu sambamba na kukwamisha ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

Waziri Mpina alisema Hifadhi ya Bahari na Maeneo Tengefu ina utajiri na urithi mkubwa wa Tanzania kwa kuwa na fukwe ndefu na nzuri za kipekee duniani, makaburi yenye historia ya kuvutia, mazalia ya samaki, matumbawe yenye mvuto wa kipekee na ndege wa aina za kipekee ambao hawapatikani maeneo mengine duniani.

Mpina alisema pamoja na kuwapo vivutio hivyo vya kipekee, bado kitengo hicho hakijaweza kuvitangaza vivutio hivyo kikamilifu ambapo hadi sasa hakuna mabango kwenye malango ya kuingia nchini ikiwamo viwanja vya ndege, bandarini na mipakani na mikoani, hakuna matangazo kwenye vyombo vya habari, hivyo kuchangia wananchi kutofahamu urithi huo na kuwapo kwa idadi ndogo ya watalii wa ndani na nje ya nchi wanaotembelea hifadhi hizo.

Kutokana na hali hiyo, aliagiza kuandaliwa mkakati wa kutangaza vivutio hivyo ili viweze kujulikana, idadi ya watalii kuongezeka pamoja na kukuza mapato ya Serikali, huku akisisitiza kuwa mkakati huo uwasilishwe wizarani kwake Februari 28, mwaka huu.

Katika hatua nyingine, alionesha kushangazwa na taasisi hiyo kushindwa kujiendesha na kuendelea kutegemea ruzuku ya Serikali licha ya kuwapo fursa nyingi na vyanzo vingi vya mapato, hivyo alitoa mwezi mmoja kuandaliwa mkakati wa kuongeza ukusanyaji wa mapato na kuifanya taasisi hiyo kujitegemea kuanzia mwaka ujao wa fedha wa 2019/2020.

Kuhusu kile kinachodaiwa kuwapo baadhi ya viongozi kuingilia na kuhujumu majukumu ya kitengo hicho kwa kuwaeleza uongo wananchi, Mpina amewataka watumishi wa taasisi hiyo kushikilia msimamo wa Sheria iliyoanzisha taasisi na kwamba kama kuna maelezo na mawazo ya kisera basi malalamiko hayo yawasilishwe kwa viongozi wakuu wa wizara.

Aidha, aliwahimiza watendaji wa kitengo hicho kubuni miradi mingine ya kiuchumi hasa katika maeneo ambayo zamani yalikuwa yakitumika kwa shughuli za uvuvi ili kuwawezesha wananchi wa maeneo hayo kujiongezea kipato na kuona thamani ya uwapo wa hifadhi hizo.

Pia aliagiza kufanyike tathmini ya ubora wa miundombinu na vifaa muhimu katika shughuli ya uhifadhi ili kuboresha utendaji kazi wa kitengo hicho. Vile vile ameagiza kuandaliwa kwa mpango biashara utakaowezesha kitengo kujiendesha kibiashara zaidi.

Kwa upande wake Meneja wa MPRU, John Komakoma, alimhakikishia Waziri kuwa maagizo yote aliyoyatoa atayasimamia kikamilifu kuona yanatekelezwa kwa wakati ili kuiwesha taasisi hiyo kutoa mchango unaostahili kwa pato la Taifa.

Komakoma alisema ili kuleta ufanisi wa kazi kitengo hicho kiko kwenye hatua ya mwisho ya mapitio ya Sheria ya Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu Namba 29 ya mwaka 1994 ili kuiwezesha taasisi hiyo kuhifadhi maeneo tengefu yaliyoko kwenye mito mikubwa, mabwawa na maziwa kote nchini .

Pia alisema katika kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018 kitengo hicho kimepokea watalii 45,000 ambapo kati ya hao 26,000 ni watalii wa ndani 19,000 ni wa nje na kuingiza kiasi cha wastani wa shilingi bilioni 1.6 kwa mwaka ambapo idadi ya watalii na mapato yanatarajia kuongezeka katika kipindi cha mwaka 2018/2019.

Utunzaji Majalada Ya Ardhi Chamwino Wamvuruga Naibu Waziri Mabula

0
0
Na Munir Shemweta, DODOMA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amekasirishwa na jinsi halmashauri ya wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma inavyotunza majalada ya Ardhi katika halmashauri hiyo.

Dkt Mabula alikutana na kadhia hiyo mwishoni mwa wiki alipotembelea masijala ya ardhi katika halmashauri hiyo akiwa katika mfululizo wa ziara zake kutembelea halmashauri mbalimbali nchini kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya ardhi.

Dkt Mabula alisema, utunzaji wa majalada ya ardhi katika halmashauri ya Chamwino hauzingatii taratibu za kutunza majalada jambo linaloweza kutoa nafasi kwa baadhi ya nyaraka kupotea na wakati mwingine watumishi wasiokuwa waaminifu kuyahujumu

Wakati wa ukaguzi wa majalada ya ardhi katika halmashauri ya wilaya ya Chamwino Dkt Mabula alibaini majalada mengi yakiwa hayana maelekezo kutoka kwa afisa mmoja kwenda kwa mwingine jambo linaloonesha kuwa utendaji kazi katika sekta hiyo hauna maelekezo yoyote.

‘’mawasiliano ya ofisi lazima yaonekane kutoka kwa ofisa mmoja kwenda kwa mwingine na hapa kuna index namba lakini haitumiki na huwezi kujua aliyepokea nyaraka kwa mara ya kwanza nani hapo lazima migogoro isiishe.’’ Alisema Mabuila.

Dkt Mabula alisema, utunzaji majalada ya ardhi usiozingatia taratibu kwa kiasi kikubwa ndiyo chanzo cha migogoro mingi ya ardhi katika maeneo mbalimbali kwa kuwa ni rahisi kucheza na majalada kwa nia ya kufanya udanganyifu.

Naibu waziri wa Ardhi alitoa maagizo kwa Mkuu wa Idara ya Ardhi Christopher Sanga na Afisa Ardhi Mteule wa halmashauri hiyo ambaye anahudumu pia wilaya ya Kongwa Letare Shoo kuhakikisha upungufu uliopo katika majalada ya ardhi yanarekebishwa kabla mwezi machi mwaka huu na ukifika muda huo atarajea kuona kama maagizo yake yametekelezwa.

Aidha, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ameagiza kufikia machi mwaka huu 2019 viwanja vyote vya halmashauri ya Chamwino viwe vimepimwa na kupatiwa hati na Mkurugenzi wake ahakikishe halmashauri inalipa kodi ya pango la ardhi kwa viwanja inavyomiliki.

Pia ameitaka halmashauri ya Chamwino kuhakikisha wadaiwa wote wa kodi ya pango la ardhi wanapelekewa ilani za madai na watakaoshindwa kutii wafikishwe kwenye mabaraza ya ardhi na kusisitiza kuwa suala hilo halitakiwi kufanywa kisiasa ili kuja na matokeo chanya.

Katika hatua nyingine Dkt Mabula aliitaka idara ya ardhi katika halmashauri wilaya ya Chamwino kuhakikisha hakuna mmiliki wa kiwanja anayejenga katika halmashauri hiyo bila kuwa na kibali cha ujenzi ili kuepuka ujenzi holela.

Naibu Waziri Mabula alisema anataka halmashauri ya Chamwino kuwa na mji uliopangika na mfano kwa halmashauri nyingine na kusisitiza anachotaka ni wengine kujifunza kwenye halmashauri hiyo hasa ikizingatiwa Ikulu iko Chamwino.

Katika kutekeleza hilo amewataka watumishi wa sekta ya ardhi katika halmashauri hiyo kuwa na maadili katika kazi zao ili kuepuka utoaji kiwanja kimoja kwa zaidi ya mtu mmoja jambo linalotokea kwa baadhi ya halmashauri na kuleta migogoro.

Tiba Asili Kwa Wenye Matatizo ya Nguvu za Kiume,UTI Sugu,Tezi Dume,Miguu Kuwaga Moto

0
0
SIX(6) power; Ni dawa ya Nguvu za kiume inayofanya kuchelewa kufika kileleni dkk 30 Hadi 46 unaweza kupiga ndani kwa ndani na kurudia tendo utakavyo,pia inarutubisha mbegu za kiume kwa wasio na sifa ya kupata mtoto,dozi Ni siku sita mabadiliko masaa manne.Tumia six(6) power ndio kiboko wa yote usisubiri kuhadithiwa.

SHOOLA 4 POWER;Wenye maumbile madogo (KIBAMIA) inanenepesha na kurefusha ,kama tatizo Ni la kuzaliwa siku 12 Kama Ni la ukubwani siku 6.ni vidonge na unga.

MBUKE; Dawa ya Uzazi kwa aliyefungwa na kutofanikiwa kupata mtoto,kwa asie pata hedhi kwa mpangilio mzuri tatizo huisha kabisaa..Ni ya unga.

LYONGO,dawa ya mvuto wa mapenzi Kama umeachwa yote yatakwisha aliembali atakuhudumia mwenza wako atarejea ndani ya SAA 12 hata Kama yupo mbali.

HOLAZA,Ni dawa ya kumaliza matatizo mengi mengi Kama dhuluma,kushindwa kuuza eneo nyumba na Kama biashara haziendi.

TALIGULA,dawa ya kufungua kitu kilichofungwa kuchawi,kimizimu,majini wabaya kuoa au kuolewa na Safari zilizofungwa

DR.Mjukuu wa kushosha asema kwanini usumbuke na maradhi mwilini wakati tiba zipo?? ,Amini tiba asilia Sasa maradhi yako yatakwisha .
 
Je,wewe una maradhi gani mwilini mwako??
(1)Sukari ya kupanda na kushuka(TUNDWA)Ni ya unga inayochemshwa na vidonge dozi Ni siku 20.
(2)Presha ya kupanda na kushuka(NGADA) ni dawa ya vidonge na unga dozi siku 14
(3)maleria sugu(NINJIWE) dozi siku 8 unapona kabisa
(4)U.T.I sugu(GUMO)Dozi siku 4 habari kwisha kabisa.
(5)Typhoid sugu(IKWATA) Dozi siku 3
(6)Kifua kubana,moyo,Figo(LUGALA)dozi siku 7
(7)Tezi dume(Dozi siku 8 vidonge na unga),ngiri,busha bila operation (SALIUNGU)dozi siku 14
(8)Miguu kuwaka moto (JIMYA)dozi siku 6
(9) kilungulia,kwikwi(INJACHI)dozi masaa 6.
(10)msongo wa mawazo.

HIZO NDIZO HUDUMA ZITOLEWAZO NA NYINGINE NYINGI,USITUME MESEJI WALA KUBIP,.OFISI ZIPO KATIKA MIKOA MIWILI SHINYANGA WILAYA YA KAHAMA NA DAR ES SALAAM WILAYA YA ILALA..SEHEMU ZINGINE NASAFIRISHA..NIULIZE KWA MAWASILIANO YAFUATAYO...
     0753 928 576
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images