Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Dr Sandala: Mtaalamu wa Tiba Bora za Mitishamba...Tezi Dume, Vidonda vya Tumbo..Mimba Kutoka, Nguvu za Kiume

0
0
DR SANDALA: ANAKUHABARISHA KUHUSU TIBA BORA YA MITI SHAMBA(100%)

  NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo     kupooza/kuparalazi  kupoteza  fahamu  

KALALA; hutibu  kisukari , uti  wa  mgongo,  Chango,.. pumu, busha bila operation, kaswende, kifua  kikuu, muwasho  sehemu  ya siri kwa mda wa siku 60. : 

THREE POWER MIX; Ni  dawa  ya  nguvu za kiume na  kuweka heshima ndani ya nyumba kwa akina baba wasio na uwezo ktk tendo la ndoa na kupona kabisa na tatizo kutokurudia tena ,okoa Ndoa yako sasa na three power mix dozi yake ni mda wa siku sita(6)na utachelewa kufika kileleni kwa mda wa dakika 29-32 

 MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2tu,atakurudia na kukuhudumia hata akiwa mbali ipate na ukomeshe asie heshim mahusiano.

NSASI, kupunguza vitambi(nyama uzembe),  maziwa makubwa,michirizi, makovu makubwa, chunusi sugu. Nk

SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo regea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4tu

GASELA:-ni dawa ya maajabu (10) yaliyoshindikana.    (1)-Kisukari siku 14 na kuwa normal na kupona kabisa na kutorithisha wanao, vidonda vya tumbo,kutoa gesi na kupona kabisa dozi siku 7, tezi dume ukitaka kupona tezi dume wasiliana nami nikushauri kwani n8 gonjwa sugu a kwangu utapona,dawa ya uzazi hujawahi kupata mtoto na unataka kupata mtoto tiba yake ipo je? unabeba mimba zinatoka ?na unahitaji uitwe mama? tumia dawa ya mapacha 1-4 ,busha bila oparesheni siku 60,na kuendelea kufanya kazi zako. 

Haya yote yana wezekana kwa DR SANDALA popote ulipo ukiniitaji nafika napatikana DAR ES SALAAM, PWANI BAGAMOYO ,SHINYANGA KAHAMA,MOSHI KILIMANJARO NA MBEYA.mawasiliano   simu namba     0753 928 576.

                

Atiwa Mbaroni Kwa Kumbaka na Kumuweka Kinyumba Mwanafunzi Darasa la Nne

0
0
Mkazi wa kijiji cha Kateka, Kalambo mkoani Rukwa, Linus Mayaya (35) ametiwa matatani kwa kudaiwa kumbaka mwanafunzi wa darasa la nne kisha kumweka kinyumba.
 
Linus ameingia kwenye wakati mgumu kutokana na tuhuma hizo baada ya kumfuatilia kwa muda mrefu mwanafunzi huyo huku akimpatia fedha za chipsi na soda ili kuweka mazingira ya kumsogeza karibu ili kutimiza azma yake.

Tukio hilo la kusikitisha na kushangaza jamii, limetokea baada ya mama mzazi wa mwanafunzi huyo, kutoa taarifa polisi kutokana na mtoto wake kuachishwa masomo na kijana huyo kumweka kinyumba akimfanya mke hali akifahamu kuwa anastahili kupata haki yake ya elimu.

Oliver Edita, mama mzazi wa mtoto huyo, alisema baada ya kutomwona mwanawe kwa siku mbili, alimtafuta huku na kule kisha juzi akabaini kuwa amewekwa kinyumba na mtuhumiwa huyo.

Alisema baada ya kugundua hilo, alitoa taarifa kwa serikali ngazi ya tarafa na polisi ambao walimkamata mtuhumiwa akiwa na mwanafunzi ndani mwake.

George Kyando, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, amethibitisha kuwapo kwa tukio hilo na kusema jeshi lake limemnasa mtuhumiwa huyo ambaye anaendelea kuhojiwa katika kituo kikuu cha polisi wilaya na atafikishwa mahakamani pindi uchunguzi utakapokamilika.

Video: Billnas ft Roma - Funga Geti

0
0
Video: Billnas ft Roma - Funga Geti

Waitara Amsimamisha Kazi Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa,

0
0
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mwita Waitara, ameagiza kumsimamisha kazi Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, ili kupisha uchunguzi wa fedha zilizotumika katika ujenzi wa mabweni mawili ya wasichana katika Shule ya Sekondari Isimila.
 
Waitara alichukua uamuzi huo jana akiwa mkoani Iringa, baada ya kukagua ujenzi wa mabweni hayo yaliyojengwa chini ya kiwango kulinganisha na fedha zilizotumika. Ujenzi huo umegharimu Sh. milioni 184 huku majengo yakiwa hayajamalizika yakiwa yanahitaji fedha zingine ili kukamilika.

Kutokana na hali hiyo, Waitara alionyesha kukerwa na ujenzi huo ambao umetumia fedha za serikali na nguvu za wananchi na umesimama kutokana na kutokamilika.

Alimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Robert Masunya, kumsimamisha kazi mhandisi huyo, Nestory Chacha, mpaka uchunguzi utakapofanyika ili hatua za kinidhamu zichukuliwe.

‘’Naona ninyi mnaichezea serikali, haiwezekani serikali itoe fedha kujenga mabweni ili watoto wetu waepukane na vitendo vya kikatili vikiwamo ubakaji na mimba za utotoni wasome katika mazingira mazuri na hatimaye kufikia ndoto zao. Sasa leo (jana) ninaagiza mhandisi apewe adhabu kali na ifikapo Februari 5, taarifa ya uchunguzi iwe imeshanifikia,’’ alisema.

Aidha, aliwataka wakuu wa wilaya mkoani hapa kuhakikisha wanasimamia miradi ya maendeleo inayotekelezwa na fedha za serikali ili kukamilika kwa wakati huku ikiwa na kiwango kinachostahili.

Pia alionyeshwa kusikitisha na taarifa ya shule hiyo kuhusu wanafunzi 43 ambao wameshindwa kuanza kidato cha kwanza mwaka huu kutokana na utoro.

Waitara alisema pamoja na serikali kuipa kipaumbele sekta ya elimu, kumekuwa na utoro wa wananfunzi waliochanguliwa kuanza masomo. Aliutaka uongozi wa shule na wilaya kufuatilia kwa makini ili wale waliochaguliwa waanze masomo mara moja.

Wimbo Mpya: Darassa Ft. Marioo - Chanda Chema

0
0
Wimbo Mpya: Darassa Ft. Marioo - Chanda Chema

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

Makanga 3 Power, Dawa Bora Za Nguvu Za Kiume

0
0

Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.

Tupo dar es salam Buguruni

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348.

Majambazi Yavamia Nyumba ya Kulala Wageni...Yabaka na Kupora Fedha

0
0
Watu wanaodaiwa kuwa majambazi, wamevamia nyumba ya kulala wageni ya Malema Lodge katika mtaa wa Sinde jijini Mbeya, inayomilikiwa na Diwani Viti Maalumu (CCM), Mary Malema, kisha kufanya ubakaji kwa wahudumu na mlinzi na hatimaye kupora fedha.

Unyama huo waliufanya usiku wa kuamkia jana baada ya kuwapa ofa ya vinywaji na biskuti zinazodaiwa kuwa na dawa za kulevya.

Shuhuda wa tukio hilo (jina linahifadhiwa), alisema watu watatu waliingia ndani ya baa hiyo wakiwa kama wateja na kuanza kutoa ofa za vinywaji na biskuti na kwamba yeye aliondoka baada ya muda kufika na kwamba alipata taarifa kuwa baada ya kula vitu hivyo, walilala wakiwa hoi.

Alisema baada ya kuzidiwa kutokana na kulewa, watu hao watatu walianza kuwabaka wanawake hao hata kufikia hatua kuwaingilia kinyume cha maumbile kisha kupora fedha ambazo thamani yake haijafahamika na kwamba asubuhi alipokuwa anapita, aliona msamaria mwema amewabeba na kuwapeleka hospitali akipitia polisi.

Malema, mmiliki wa nyumba hiyo, alisema ilikuwa usiku wa saa tano waliingia watu watatu kama wateja na mlinzi alifunga geti kutokana na muda kuwa ulikwisha, hivyo walianza kunywa pombe na kuwapa ofa wahudumu pamoja na mlinzi ambaye alipewa soda na biskuti.

Alisema baada ya hapo, wahudumu walilala fofofo, ndipo watu hao wakafanya unyama huo na kwamba hajafahamu kama walibakwa au la kwa kuwa bado wamelazwa katika Hospitali ya Rufani ya Mkoa wa Mbeya wakiwa hawajitambuhi wakipumulia mashine.

Malema ambaye pia ni diwani wa viti maalumu katika kata ya Manga, alisema wakati anapita aliona msamaria mwema anawabeba ndipo katika kuchunguza akabaini kuwa vijana wake waliingiliwa na watu hao. Alisema alikwenda polisi akapewa barua kwa ajili ya matibabu.

Alisema alipofika baa alikuta fedha zote zimechukuliwa na zikiwamo pia na za upande wa gesti na kwamba hajajua kiasi cha fedha kwa kuwa hawakufunga hesabu. Aliliomba jeshi la polisi kufuatilia kwa kina suala hilo kwa kuwa vijana wake (majina yanahifadhiwa) wamelazwa hospitalini pamoja na mlinzi aliyemtaja kwa jina la Dickson.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei, alisema hajapelekewa taarifa juu ya tukio hilo na mkuu wa polisi wilaya na kwamba atahitaji apate taarifa hizo ili kujua undani wake sambamba na kuweka mikakati ya watuhumiwa ili wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya dola.

Credit: Nipashe


Video Mpya: Gigy Money X Nass Bugatti - Alamba

0
0
Video Mpya:  Gigy Money X Nass Bugatti - Alamba

Jaji Mkuu Nchini Nigeria Atimuliwa Kazi...Wanasheria, Wapinzani Watoa Tamko

0
0
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari amemsimamisha kazi jaji mkuu wa nchi hiyo, na kuanzisha mgogoro wa kikatiba katika nchi hiyo yenye idadi kubwa kabisa ya watu barani Afrika

Mpinzani mkuu wa Buhari katika uchaguzi huo, aliyekuwa makamu wa rais Atiku Abubakar, alimtuhumu rais kwa kitendo hicho alichokiita kuwa cha "kidikteta" na kisichokuwa halali .Nacho Chama cha Wanasheria nchini Nigeria kikiilaani kwa kusema kuwa ni "jaribio la mapinduzi" dhidi ya katiba.

Buhari ambaye alikuwa kiongozi wa kijeshi katika miaka ya 1980 na kuchaguliwa madarakani mwaka wa 2015, atagombea kwa muhula wa pili katika uchaguzi wa Februari 16. Kuachishwa kazi kwa Walker Nkanu Samuel Onnoghen kumekuja wakati jaji huyo mkuu alikuwa akijiandaa kuwaapisha majaji wa mahakama za kesi za uchaguzi.
 
Jaji Mkuu Onnoghen anatuhumiwa kwa ufisadi
Onnoghen anakabiliwa na kesi ya madai ya kushindwa kutangaza mali za fedha za kigeni kama wanavyotakiwa kufanya maafisa chini ya sheria ya Nigeria.

Madai hayo yaliibuka wiki mbili zilizopita. Idara ya mahakama na jaji mkuu watatekeleza jukumu muhimu ikiwa kutatokea utata katika uchaguzi.

Buhari amesema hatua hiyo ya kusitishwa kazi itaendelea hadi pale kesi dhidi yake itakapokamilika. Hii ni mara ya kwanza kwa jaji mkuu kushtakiwa nchini Nigeria,ambako ufisadi umekithiri. Onnoghen anahoji kuwa mashitaka hayo hayana msingi.

Waangalizi tayari wameonya kuwa uchaguzi huo huenda ukasababisha machafuko – uchaguzi wa Buhari mwaka wa 2015 lilikuwa tukio la nadra la kukabidhi madaraka kwa njia ya amani katika nchi hiyo yenye utajiri wa mafuta – na wanadiplomasia wamewaomba wagombea wakuu kusaini ahadi ya kudumisha amani.

Taarifa ya Buhari imesema kuwa mbali na mashitaka hayo ya Onnoghen, mashirika ya usalama yamegundua biashara nyingine inayotilishwa shaka ya mabilioni ya dola kwenye akaunti zake za benki.

Jaji Ibrahim Tanko Muhammed atachukua wadhifa wa kaimu jaji mkuu. 

Muhammed  anatokea upande wa kaskazini wenye Waislamu wengi, wakati Onnoghen anatokea kusini ambako kuna Wakristo wengi.

Credit:DW

Malipo ya kazi za wasanii, mawakala na kampuni za simu sasa asilimia 50 kwa 50

0
0
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imewaagiza wasanii walioingia mikataba na kampuni za simu au mawakala kwa ajili ya kutumia kazi zao kama miito ya simu ambao hawajalipwa stahiki zao, wawasilishe madai yao katika ofisi hizo kwa ajili ya kupatiwa haki zao.

Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James Kilaba, aliyaeleza hayo, muda mfupi baada ya kumaliza kikao na wasanii na mawakala waliokuwa wakijadili kuhusu kutokuwapo na mgawanyo sawa wa malipo ya miito ya simu baina ya wasanii wa muziki, kampuni za simu na mawakala wanaotumia kazi za wasanii.

Katika kikao hicho, walikubaliana malipo kuwa kwa kipindi cha miezi sita yakutafuta suluhu ya kudumu, malipo ya kazi za wasanii, mawakala, kampuni za simu na mtoa huduma yawe asilimia 50 kwa 50 kabla ya kuja na mfumo rasmi.

Aliongeza kuwa wamekubaliana kuwapo uwezekano wa msanii kusaini makubaliano ya kazi zake kutumika kama miito ya simu katika kampuni husika ya simu moja kwa moja na endapo atataka kutumia wakala afanye hivyo.

Pia walikubaliana kuwa kampuni za simu ziwasilishe TCRA mgawanyo halisi wa gharama za utayarishaji wa kazi hizo za wasanii ambazo hutumika kama miito ya simu.

Mhandisi Kilaba, alitaja azimio lingine ni TCRA kuangalia uhalisia wa mikataba inayoingiwa baina ya kampuni za simu na mawakala au wasanii kuona kama ni rafiki katika mazingira ya biashara ya miito ya simu.

Rais Nkurunziza aishtaki televisheni ya Ufaransa

0
0
Mahakama nchini Ufaransa imeanza kusikiliza kesi iliyofunguliwa na Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza dhidi Televisheni moja ya nchini Ufaransa, Mwanasheria wa Ubelgiji na Mwandishi wa Habari wa Burundi, David Gakunzi, kwa makosa ya kuikashifu nchi yake na hadhi yake.

Rais Nkurunziza anadai kuwa Televisheni hiyo ya Ufaransa miaka miwili iliyopita ilionyesha picha za video za mauaji ya kimbari kwa madai kuwa chama tawala cha Burundi ndicho kilichohusika.

Aidha, amesema kuwa picha hizo za video zilizoonyeshwa na televisheni ya Ufaransa, Channel 3, zinadai mauaji hayo ya watu wengi yalifanyika katika viunga vya makazi ya Rais Nkurunziza, jambo linalokanushwa na ambalo kwa sasa limefikishwa mahakamani.

Kwa mujibu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Rais Nkurunziza amekanusha vikali kwamba picha hizo wala si za ndani ya Burundi, bali zinavyoonekana ni kama zilichukuliwa mahali fulani katika nchi za Afrika Magharibi.

Televisheni hiyo ya Channel -3 ya Ufaransa ilizirusha picha hizo mwaka 2016, wakati wa uchaguzi mkuu wa Burundi, ulioandamana na vurugu.

Video hizo katika matangazo kupitia televisheni ya France Channel 3, zilionyesha mauaji ya watu wengi, yanayodaiwa kutekelezwa na wafuasi wa Rais Pierre Nkurunziza.

Picha hizo za video zimepewa jina la ‘Proof of acts of violence in Burundi”, ikimaanisha ‘Ushahidi wa vitendo vya machafuko ya Burundi.”

Ndani ya picha hizo pia baadhi ya watu wanaonekana wakizungumza lugha ya Kihausa, lugha ambayo haiongelewi nchini Burundi.

Mshitakiwa Bernard Maingai, ambaye ni mwanasheria, anatuhumiwa kwamba ndiye aliyepeleka video hiyo ili ichezwe katika runinga, wakati mwandishi wa habari, David Gakunzi, yeye anashitakiwa na Rais Nkurunziza kwa tuhuma za mahojiano aliyoyafanya kwenye runinga, akizungumzia picha hizo.
 
Serikali ya Burundi imekuwa ikipata vikwazo kutoka kwa jumuiya za kimataifa, kwa madai ya kukiuka haki za binadamu na kwamba chama tawala nchini humo kina kundi la vijana linaloitwa Imbonerakure. Hata hivyo, Serikali ya Burundi imekuwa ikipinga madai hayo.

Mvutano kati ya Rais Trump na Wabunge wa wademocrat unaendelea....Je, Atatangaza sheria ya hali ya hatari?

0
0
Majadiliano yameanza upya Marekani kati ya chama cha upinzani cha Democrat na kile kinachotawala cha Republican kwa lengo la kutafuta ufumbuzi wa muda wa mvutano wa bajeti uliopelekea watumishi wengi wa serikali kulazimika kubaki nyumbani mwao kwa kuwa shughuli za serikali zilifungwa kutokana na kukwama bajeti ya kuendesha.

Gazeti la Washington Post jana limeripoti kuwa, mpango uliopendekezwa na Rais Donald Trump na ule mbadala uliopendekezwa na Chama cha Democrat ili kukwamua mzozo wa bajeti haukusaidia kuungwa mkono vya kutosha katika Baraza la Seneti.

Kwa zaidi ya mwezi sasa, wabunge na Rais Trump wanazozana kuhusiana na suala la ujenzi wa ukuta ambao Rais Trump anataka kuujenga katika mpaka wa Marekani na Mexico, ili kukabiliana na wahamiaji kinyume cha sheria.

Waliutaja mpango huo kuwa haulingani na manufaa yanayoweza kupatikana na zaidi kuliko yote hauna maana. Wabunge wa chama cha Democrat wanapinga moja kwa moja kutengwa dola bilioni 5.7 ili kuugharimia ujenzi huo.

Wabunge hao wanapendekeza mpango mbadala wa ulinzi wa mpakani. Matokeo yake tangu Desemba 22 mwaka jana takribani watumishi 800,000 wa serikali na watumishi wengine kadhaa wanalazimika kubaki nyumbani bila malipo.

Juhudi za chama cha Republican hazikufaulu, kwakuwa pendekezo lake lililowasilishwa kupigiwa kura kwa mara ya kwanza juzi lingesaidia kugharimia shughuli za serikali hadi mwezi wa Septemba mwaka huu na linajumuisha pia fedha za kugharimia ukuta.

Chama cha Republican ndicho kinachodhibiti Baraza la Seneti, lakini kwa vile wanadhibiti viti 53 kati ya 100, walihitaji kuungwa mkono na wabunge wa Democrat ili kujipatia asilimia 60 zinazohitajika ili pendekezo la Rais Trump liweze kufikishwa katika zoezi la mwisho la kupigiwa kura. Hata hivyo, hawakufanikiwa kuwashawishi Democrat.

Mara baada ya malumbano makali,  viongozi wa Republican na Democrat katika Baraza la Seneti wakakutana kujaribu kuikwamua hali ya mambo.

Ikulu ya Marekani ilikubali kuwaachia wajadiliane kuhusu sheria ya kugharimia kwa muda wa wiki tatu kwa masharti kwamba gharama hizo zinajumuisha sehemu kubwa ya fedha za kujenga ukuta.

“Wakiniletea makubaliano ya maana nitayaunga mkono. Bila ukuta, hatuwezi kudhibiti usalama wetu,” alisema Rais Trump, alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu kadhia hiyo.

Hata hivyo, Trump amebakiwa na karata moja, kutangaza sheria ya hali ya hatari.

Ufumbuzi wowote inabidi upitie katika Baraza la Wawakilishi ambalo linadhibitiwa na Democrats.

Kwa upande wake, Spika wa Baraza hilo, Nancy Pelosi, ameshasema hakubaliani na bajeti ya kugharimia ukuta.

Bado haijulikani kwa hivyo mzozo utafumbuliwa vipi. Kutokana na kutofikiwa maridhiano, Rais Trump amelazimika kuahirisha hotuba yake kwa taifa aliyokuwa aitoe wiki ijayo.

Credit: DW

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

Habari Njema Kwa Wenye Matatizo Ya Nguvu za Kiume, vitambi, nyama uzembe

0
0
HABARI NJEMA KWA MLIOATHIRIKA NA MAGONJWA YA MWILI NA AKILI.
Sasa dokta MBALU ana uwezo mkubwa wa kutibu magonjwa yaliyoshindikana,Kama umehangaika kwa muda mrefu bila mafanikio DK.MBALU Ni kiboko kabisaa.

TIBA ATOAZO NI:- (a)Vidonga vya tumbo,kilungulia,Tumbo kujaa gesi.
 (b)Kifua kikuu(TB),Pumu(ATHMA) na Rovu
(c)Miguu kuwaka moto,nyama za magoti kuuma,kiuno na mgongo.
(d)Uzazi na chango.
 (e)Nguvu za kiume,kurefusha na kunenepesha uume,busha,mshipa wa ngiri na tezi dume.
(f)Elimu mwanafunzi kuwa na uwezo mkubwa darasani na kufanya vizuri katika mitihani yake, kupandishwa cheo kazini, kulipwa madeni au mafao yako.
(g) kutoa ushauri nasaha kwa wenye matatizo ya kisaikolojia.

      AINA ZA DAWA.
NINJIWE:-,Hutibu vidonda vya tumbo,tumbo kujaa gesi,na kilungulia,vidonge 16 kwa muda wa siku nne na ya unga.
MPALAMA:-,Hutibu Kifua kikuu (TB), Pumu (ATHMA),na wenye tatizo la uvimbe katika koromeo yaani (ROVU),Huisha na kutorudi Tena.,dozi siku 6.

NKOLA:-,Hutibu miguu kuwaka moto,nyama za goti kuuma,kiuno na mgongo dozi siku 10.
MWATYA:-,Hutibu Uzazi au chango,dozi siku 30,na tatizo kupona kabisa.

LYONGO POWER:-,Hii ni dawa ya heshima kwa akina baba yenye uwezo wa kurefusha na kunenepesha uume kwa wale wenye maumbile madogo yaani (KIBAMIA).

NENGONENGO(4)POWER:-,Hutibu Nguvu za kiume na kuleta hamu ya tendo hivyo kuchelewa kufika kileleni na kuweza kurudia tendo zaidi ya mara (4),ina Nguvu mno Kama Ni muhanga wa tatizo hili   tumia NENGONENGO (4)POWER Ipo aina ya vidonge na unga dozi Ni siku 5 unapona kabisaa wahi Sasa.

NTUNDWA:-,Hutibu busha,mshipa wa ngiri na tezi dume,Busha dozi Ni siku (30),bila kufanyiwa operation,Mshipa wa ngiri dozi siku (4) na tezi dume dozi siku (10).

GWATA:-,kuuwa kesi na shauri kupangiwa tarehe za karibu zaidi na baadae kesi kufutiliwa mbali kabisaa.
NUGWANO:-, Humfanya mtu kuheshimika na kupandishwa cheo kazini pia kulipwa madeni au mafao kwa wakati muafaka.

NKOMA:-, Hurudisha mke,mme,hawara, mchumba ndani ya siku mbili atatimiza mahitaji yote hata Kama yupo mbali na kumfunga asiwe na mtu mwingine..

  Huduma zinatolewa ndani ya masaa 12,Saa moja asubuhi Hadi kumi na mbili jioni,DAR ES SALAAM NA KAHAMA wa mikoani unapata huduma kwa njia ya kusafirisha..na huduma yetu inakufikia ukiwa ofisini au nyumbani kwako..,


CONTACTS;   0716608959 au 0767171773

 OUR SERVICES ARE EASY.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

0
0

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.


Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Ugonjwa wa Zinaa wa Kaswende (Syphilis) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga

0
0
Ugonjwa wa kaswende ni ugonjwa wa zinaa unaosababishwa na bakteria aina ya Treponema pallidum. Ugonjwa wa huu ni kati ya magonjwa ya zinaa yanayoongoza kwa kusababisha madhara mengi. 

Maambukizi ya kaswende wakati wa ujauzito huleta madhara mengi sana kama kujifungua kiumbe mbacho kimeshakufa, mtoto kuathirika na ugonjwa huu wakati wa kuzaliwa, mtoto kupata matatizo wakati wa ukuaji wake, degedege na kuongezeka kwa vifo vya watoto wachanga nchini. 

Ugonjwa wa kaswende huathiri zaidi ya mimba millioni moja duniani kote kila mwaka na huchangia theluthi mbili ya vifo vya watoto wale wanaozaliwa tayari wameshakufa katika nchi za maeneo ya jangwa la sahara. 
 
 Asilimia 30 ya mimba zinazoathiriwa na kaswende huishia watoto kufariki wakati wa kuzaliwa. Asilimia nyengine 30 ya mimba zinazoathiriwa na kaswende husababisha watoto kuzaliwa na ugonjwa huu wa  kaswende, kupata matatizo ya ukuaji wao, degedege na kuongeza vifo vya watoto kwa asilimia 50. 
 
Ugonjwa wa ukimwi na kaswende mara nyingi huambatana pamoja. Ugonjwa wa kaswende huongeza uwezekano wa mtu kupata ugonjwa wa ukimwi.

Visababishi vya ugonjwa wa kaswende

Kama tulivyosema awali, kaswende husababishwa na bakteria aina ya Treponema pallidum. Njia za maambukizi za ugonjwa huu ni kama zifuatavyo;
  • Kupitia kujamiana bila kutumia kinga na mtu aliyeambukizwa kaswende
  • Kujamiana kupitia njia ya haja kubwa (anal sex)
  • Kujamiana kupitia njia ya mdomoni (oral sex)
  • Mama aliyepata ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito anaweza kumuambukiza mtoto wake wakati wa ujauzito.
  • Kuambukizwa kupitia michibuko au mipasuko kwenye ngozi wakati wa kujamiana au wakati mwengine wowote pale mtu anapogusana na mtu mwenye kaswende ikiwa wote wawili wana mipasuko kwenye sehemu mbalimbali za ngozi zao. Sio rahisi mtu kutambua kama ana michibuko au la kwenye ngozi kwani mengine inakuwa midogo sana isipokuwa ile ambayo inaweza kuonekana kwa macho.
Dalili na Viashiria vya ugonjwa wa kaswende
Dalili na viashiria vya ugonjwa wa kaswende hutegemea na aina ya ugonjwa wa kaswende wenyewe. Kuna aina tano za ugonjwa wa kaswende ambazo ni;
  • Ugonjwa wa kaswende wa awali (Primary syphilis)
  • Ugonjwa wa kaswende wa pili (Secondary syphillis)
  • Kaswende iliyojificha (Latent syphilis)
  • Kaswende ya baadae (Tertiary syphilis)
  • Kaswende ya kurithi (Congenital syphilis)
Kaswende ya awali (primary syphilis)
Dalili ya kwanza ya aina hii ya kaswende ni kutokea kwa kidonda kidogo cha mviringo (chancre kama kinavyojulikana kitaalamu) katika sehemu ambayo bakteria wameingilia na hutokea kati ya siku 10 hadi miezi mitatu (kwa kawaida kuanzia wiki 2 hadi 6) baada ya mtu kupata maambukizi ya kaswende. Kidonda hiki kinaweza kutokea kwenye sehemu ya haja kubwa, shingo ya kizazi kwa wanawake (cervix), mdomoni (lips), uume (penis), ulimi, vulva, tupu ya mwanamke (vagina) na sehemu nyengine mwilini. Tezi (lymph nodes) ambazo zipo karibu na sehemu iliyotokea kidonda hiki kawaida huwa zinavimba baada ya siku 7 hadi 10. 


Kidonda hiki hakiambatani na maumivu na kwa kuwa kinaweza kutokea katika sehemu zilizojificha kama kwenye shingo ya kizazi, sio rahisi mtu kutambua kama na aina hii ya kaswende. Kidonda hiki kinaweza kuwepo kwa muda wa wiki 3 hadi 6 kama mtu hatapata tiba na kinatoweka chenyewe bila tiba au baada ya kupata tiba. 

Robo tatu ya wale ambao hawapati tiba huishia kuingia kwenye kundi la kaswende ya aina ya pili (Secondary syphilis).
 
Kaswende aina ya pili (Secondary syphilis)
Aina hii hutokea wiki 4 hadi 10 baada ya mtu kupata kaswende ya awali. Dalili za aina hii ya kaswende ni;
  • Vipele ambavyo haviwashi katika viganja vya mikono au nyayo za miguu. Vipele hivi pia vinaweza kutokea mwili mzima au sehemu mbalimbali za mwili.
  • Uchovu
  • Kuumwa kichwa
  • Homa (fever)
  • Kunyofoka nywele
  • Vidonda vya koo (sore throat)
  • Kuvimba kwa matezi mwili mzima
  • Maumivu ya mifupa (joint pain)
  • Kupungua uzito
Kaswende ya aina hii inakuwepo kwa wiki kadhaa na hupotea hata bila kupata tiba kwa mtu aliyeathirika. Pia inaweza kujirudia rudia katika kipindi cha mwaka mmoja hadi miwili na mtu huingia kwenye kundi la aina ya tatu ya ugonjwa wa kaswende (latent syphilis) baada ya miaka miwili.
 
Kaswende iliyojificha (Latent syphilis)
Hii inajulikana kama kaswende ambayo inaweza kuthibika tu kwa kutumia vipimo vya maabara (serological test). Imegawanyika katika makundi mawili:
i. Early latent syphilis (kaswende iliyojificha ya awali) – Hii ni ile ambayo hutokea ndani ya kipindi cha mwaka mmoja baada ya muathirika kuugua kaswende aina ya pili (secondary syphilis). Aina hii huwa na dalili zinazojirudia kama za kaswende ya pili (secondary syphilis)
ii. Late latent syphilis (kaswende iliyojificha ya kuchelewa) – Hii hutokea baada ya mwaka mmoja wa kuugua kaswende ya aina ya pili (secondary syphilis). Wakati wa kuugua aina hii, muathirika anakuwa hana dalili wala viashiria vyovyote vile na uwezo wake wa kuambukiza mtu mwengine unakuwa chini au hawezi kabisa kumuambukiza kaswende mtu mwengine.

 
Kaswende ya baadae (Tertiary syphilis)
Asilimia 30 ya wagonjwa wa kaswende ambao hawakupata tiba hapo awali huingia kwenye kundi hili na hutokea miaka 15 – 30 baada ya maambukizi ya kaswende hapo awali. 


Aina hii inaweza kuathiri viungo kama macho, ubongo, mishipa ya fahamu (Neurosyphilis), jointi au viunganishi vya mifupa, uti wa mgongo, moyo, mishipa ya damu na hivyo kusababisha madhara makubwa kama;
  • Upofu
  • Magonjwa ya moyo – Aortic dissection type B, syphilitic aortitis
  • Magonjwa ya akili
  • Magonjwa ya mishipa ya fahamu
  • Mtu kuwa kiziwi
  • Kupungukiwa na kumbukumbu (Memory loss)
  • Kifo
Pia aina hii ya kaswende inaweza kuathiri mfumo wa chakula (abdominal organs), mfumo wa kupumua (respiratory system) na mfumo wa uzazi (reproductive system).
 
Kaswende ya kurithi (Congenital syphilis)
Aina hii hutokea wakati wa ujauzito au baada ya mtoto kuzaliwa. Robo mbili ya wototo wanaozaliwa hawaonyeshi dalili zozote. Nusu ya watoto wenye maambukizi ya kaswende hufariki muda mfupi kabla ya kuzaliwa au baada ya kuzaliwa. Dalili za aina hii ya kaswende kwa mtoto mchanga zinaweza kutokea baada ya kuzaliwa au wiki 2 hadi miezi 3 baada ya kuzaliwa;
  • Kutoongezeka uzito au kushindwa kukua
  • Homa
  • Kukasirika haraka (irritability)
  • Kutochongoka kwa pua, pua inakuwa bapa (no bridge to nose or saddle nose)
  • Vipele kwenye viganja vya mikono na kwenye nyayo
  • Vipele vya rangi ya madini ya shaba kwenye uso, viganja vya mikono na nyayo
  • Vipele kwenye mdomo, sehemu za siri na sehemu ya haja kubwa
  • Kutokwa na majimaji puani
  • Kuongezeka ukubwa wa ini na bandama (hepatosplenomegally)
  • Ngozi kuwa ya njano (jaundice)
  • Upungufu wa damu mwilini (anemia)
Dalili kwa mtoto mkubwa
  • Kuathirika meno (Hutchinson teeth)
  • Maumivu ya mifupa
  • Upofu
  • Kupungua uwezo wa kusikia au mtoto kuwa kiziwi
  • Ukungu kwenye mboni za macho (Clouding of cornea)
  • Vidonda rangi ya kijivu kwenye sehemu ya haja kubwa na kwenye tupu ya mwanamke (vagina)
  • Ngozi kuwa na mabaka meusi kwenye mdomo, sehemu za siri na sehemu za haja kubwa
  • Maumivu kwenye mikono na miguu
  • Kuvimba jointi za mifupa
Ugunduzi wa ugonjwa wa kaswende
Ugunduzi wa ugonjwa wa kaswende huusisha utambuzi wa dalili na viashiria vya ugonjwa huu (hii hufanywa na daktari) kupitia historia ya mgonjwa, vipimo vya damu na vipimo vya kugundua bakteria aina ya Treponema pallidum. 

 
a. Utambuzi wa dalili na viashiria vya ugonjwa wa kaswende
  1. Hufanywa na daktari
  2. Huusisha historia ya mgonjwa
b. Vipimo vya damu
Vipimo hivi vinahusisha utambuzi wa chechembe za antibodies dhidhi ya bakteria Treponema pallidum. Majibu yanaweza kuwa false positive (Wale ambao vipimo vimeonyesha wana kaswende lakini hawana ugonjwa huu,hii hutokea kwa wale ambao waliugua kaswende awali na hali hii inaweza kuwepo hadi miezi mitatu baada ya kupona ugonjwa huu au wale wenye ugonjwa wa kifua kikuu, malaria, wajawazito, measles, endocarditis, connective tissue disease nk.) au false negative (Wale ambao wameathirika na kaswende lakini vipimo vinaonyesha hawana kaswende). Mara nyingi ni vigumu sana kuthibitisha uwepo wa ugonjwa huu, hivyo vipimo hurudiwa ili kupata uthibitisho.
  • RPR (Rapid plasma reagin) test
  • VDRL (Veneral Disease Research Laboratory)
  • The microhemagglutination assay [MHA-TP] Hufanywa kuthibitisha ugonjwa wa kaswende
  • Fluorescent-treponemal-antibody absorption [FTA-ABS, enzyme-linked immunosorbent assay ELISA]) Hufanywa kuthibitisha ugonjwa wa kaswende
  • PCR (Polymerase Chain Reaction) – Kipimo cha kuangalia vina saba (DNA) vya Treponema pallidum.
  • Complete Blood Count - Kipimo cha kuangalia wingi wa damu na aina tofauti za chembechembe za damu
c. Vipimo vya kugundua bakteria
Hufanywa kwa kutumia hadubini ( Dark field microscopy).
d. Vipimo kwa wale wenye madhara ya kaswende
  • Picha ya X-ray ya kifua, uti wa mgongo
  • Vipimo vya moyo – ECG, transesophageal echocardiogram,aortic angiography, doppler ultrasonography, chest MRI, cardiac CT scan (contrast), CT angiography.
  • CT scan ya kichwa, mfumo wa chakula (abdominal CT)
  • MRI ya kichwa, uti wa mgongo, brainstem
  • Bone scan (Vipimo vya mifupa)
  • Vipimo vya macho
  • Vipimo vya masikio
  • Lumbar puncture – Kipimo cha kuangalia bakteria kwenye maji ya uti wa mgongo
  • Cerebral angiogram – Kipimo cha kuangalia mishipa ya damu kwenye ubongo
  • Nerve conduction tests
Tiba ya ugonjwa wa kaswende
Tiba ya ugonjwa wa kaswende inahusisha matumizi ya dawa za antibiotic za kundi la penicillin. Dawa nyengine ni aina ya polyketides antibiotics (doxycyline nk.) lakini hizi hazitumikia kwa wajawazito. Kwa wale ambao wanapata madhara baada ya kutumia penicillin ni bora kumjulisha daktari mapema. 


Tiba kwa wale wenye kaswende iliyoathiri mishipa ya fahamu ni penicillin inayotolewa kupitia kwenye mishipa ya damu na wanahitaji kulazwa hospitali kwa matibabu zaidi. Wale ambao wameathiriwa na kaswende kwenye viungo vya mwili, madhara hayo sio rahisi kurekebishika na mengine hayarekebishiki.
 
Tiba ya upasuaji
Tiba ya upasuaji kwa wale wenye madhara ya ugonjwa wa kaswende kama kwenye moyo na nk.
Wagonjwa wa syphilitic aortitis wanaweza kutibiwa kwa angiography/angioplasty lakini kama wana magonjwa mengine ya moyo kama coronary heart disease basi tiba hii haifanyiki. 

 
Madhara ya ugonjwa wa kaswende
  • Magonjwa ya moyo
  • Magonjwa ya akili
  • Mtu kuwa kiziwi
  • Upofu
  • Magonjwa ya mishipa ya fahamu
  • Kupungukiwa kumbukumbu (memory loss)
  • Upungufu wa damu mwilini
  • Mimba kutoka wakati wa ujauzito
  • Kuzaa mtoto ambae ameshafariki
  • Madhara kwenye mifupa
  • Vifo vya watoto
Jinsi ya kujikinga na ugonjwa wa kaswende
  1. Kufanya ngono salama kwa kutumia kondomu, njia sahihi ni kuepuka kabisa ngono
  2. Wale walioathirika kuacha kufanya ngono na wenza wao hata kama wameanza tiba mpaka vidonda vipone
  3. Kwa wajawazito, kuhudhuria kliniki mapema ili kama ukigundulika kuwa na kaswende hivyo kupata tiba haraka.
  4. Epuka kugusana na majimaji yoyote yanayotoka kwa mtu aliyeathirika kwa ugonjwa huu.

Usiteseke Tena na Matatizo ya Nguvu za Kiume.....Tumia Tiba Hii ya Asili

0
0
SUPER MKUNYATI MIX; ni dawa bora ya mitishamba iliyopo katika mfumo wa vidonge na unga yenye uwezo wa kutibu na kumaliza matatizo yote ya ukosefu wa nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile:-

  -kuwai kufika kileleni ndani ya dakika chache tu.
 -Kukosa hamu ya tendo la ndoa kwa muda mrefu.
 -Kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu(punyeto) husababisha kuishiwa au kupungukiwa na nguvu za kiume.
 -Uume kusimama kwa kulegea au katikati ya tendo la ndoa unalala na kushindwa kusimama.

Epuka matatizo haya kwa kutumia dawa bora ya asili ya SUPER MKUNYATI MIX ni kiboko ya matatizo haya yanayowasumbua baadhi ya wanaume wengi.

Pia kuna dawa ya kutibu Presha,miguu kufa ganzi, tumbo kuuma chini ya kitovu, kisukari,ngiri, chango aina zote na nk, matatizo haya nayo uchangia matatizo haya ya ukosefu wa nguvu za kiume na kuwa na maumbile madogo na uume mfupi.

KWANINI BAADHI YA WANAUME WENGI WANA MAUMBILE MADOGO NA UUME MFUPI?  Usikate tamaa ondoa maradhi yako  hayo maana matatizo haya yamekuwa yakiathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti na sana na wanaume wengine kwa kushindwa kumlizisha mwanamke.


MDINDADINDA MIX, ni dawa ambayo inarefusha na kunenepesha maumbile na itakufanya uwe na uume saizi uipendayo.Dawa hizi za asili za mitishamba zipo katika mfumo wa vidonge na unga na hazina madhara kwa mtumiaji.

JABABILA;- ni dawa ya mvuto wa mapenzi ,mchumba, mke, mume aliyekuacha atakurudia ndani ya siku moja tu na atakutimizia utakacho.

ITALIGULA;- ni dawa ya biashara  na hata kama umezurumiwa utalipwa mapema ,kupata kazi, kupanda cheo. Ofisi zetu zinapatikana DAR ES SALAAM, SONGEA - BOMBAMBILI, SHINYANGA - KAHAMA MJINI. na pote pale ulipo utaipata huduma hii,kama huna nafasi utaletewa hulipo.Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR. MACHIMKENDA simu no, 0658102596,au 0621998653.

Wakuu Wote wa Mikoa Waitwa Dar Jumatatu

0
0
Wakuu wa mikoa wote nchini Tanzania wameitwa jijini Dar es Salaam kupeana mbinu mbalimbali kuhusu ugawaji vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo.

Imeelezwa kuwa vitambulisho hivyo vilivyotolewa na Rais John Magufuli ugawaji wake katika mikoa mbalimbali nchini ni wa kusuasua.

Kauli hiyo imetolewa leo Jumamosi Januari 26, 2019 mjini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Seleman Jafo katika ufunguzi wa mkutano wa siku moja kwa ajili ya mikakati ya uanzishwaji wa masoko ya madini.

Washiriki wa mkutano huo walikuwa maofisa na wafanyakazi wa wizara ya madini, wakuu wa mikoa na makatibu tawala mikoa.

Akizungumza mbele ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Jafo amesema kuna mikoa inasuasua zaidi katika zoezi hilo licha ya kuwa baadhi ya mikoa imeshafikia hadi asilimia 94.

Bila kuitaja mikoa iliyofanya vizuri na ambayo inasuasua, amesema kitendo hicho hakifurahishi kwani kinarudisha nyuma juhudi za Rais Magufuli.

"Niwatangazie kuwa  Jumatatu tunatakiwa Dar es Salaam na Rais kwa ajili ya maelekezo zaidi na mbinu za kufanya katika kazi hii," amesema Jafo.

Ufugaji wa nguruwe : Gharama na Faida Zake

0
0
 Utangulizi
Nguruwe ni mnyama amabaye hutumika kama chakula / mboga na pia ni zao la biashara kwa mfugaji, mjasirimali na mfanyabiashara.
 
NGURUWE HUTEGEMEA SANA MAMBO YAFATAYO
1 . Banda imara na rafiki kwake
2. Usafi ni muhimu sana katika banda la Nguruwe
3 Mchaganyo bora wa chakula
4. Tiba bora na kinga
5. Maji na Lishe ( access ya vyakula Muhimu kwake )
 
CHANGAMOTO
KATIKA UFUGAJI WA NGURUWE KUNACHAGAMOTO ZAKE LAKINI ZAWEZA KUTATULIWA KWA KUFATA MAMBO KADHAA.
Katika ufugaji wa nguruwe kunachagamoto ya vifo vya nguruwe wachanga ambao hupunguza faida ya biashara ya nguruwe kwa kupunguza idadi ya nguruwe wazima wa kuuzwa lakini utunzaji mzuri wa nguruwe wachanga huepusha vifo vinavyotokana na shida kama:
 
Matatizo ya kupumua
Ni kifo kinachosababishwa na mama anapomlalia nguruwe mchanga.chagamoto hii inaweza kutatuliwa kwa kuwatenga au kuwa na mabanda makubwa ya kulelea watoto.
 
Baridi
Nguruwe wachanga huathiriwa na baridi haswa katika majuma mawili au matatu ya mwanzo. Hii ni kwa kuwa wana kiwango kidogo cha utando wa mafuta wa kuwakinga.
 
Unashuriwa kuwaweka katika hali ya joto, wape matandiko na utumie vipasha joto kama vile kuwasha globu za joto kama utakuwa umewaweka kwenye mabanda ya kuta au nyumba yenye sakafu baridi.
 
Namna bora utunzaji wa nguruwe wachanga
Nguruwe moja wa kike ana uwezo wa kuzaa watoto 12. Namna ifuatayo itasaidia kupunguza idadi ya vifo vya nguruwe wachanga:
1.Pale nguruwe awapo na kidonda nyunyizia dawa ya ayodini 5% kwenye kovu ili kuzuia kuambukizwa kwa magonjwa.
2.Wawekee matandiko (nyasi kavu au maganda ya miti) mahali pa mapumziko ili wapate joto au utumie globu za joto.
3Wadunge sindano ya madini ya chuma (iron) siku ya tatu baada ya kuzaliwa ili kuzuia upungufu wa damu.
3. Yalainishe meno ya vichaga kabla ya masaa 24 ili kuzuia uharibifu wa matiti wakati wanaponyonya.
4. Watie vibandiko au utoboe masikio ili uwatambue na uhifadhi rekodi zao kama kuna umuhimu kama vile wafanyavyo wafugaji wa ng’ombe.
5. Wapime uzani wanapozaliwa na uhifadhi rekodi hiyo itakusaidia kujua ukuaji wao na maendeleo yao
6. Wahasi wale wa kiume juma la tatu, wale ambao hawafai katika kuendeleza kizazi kwa kutumia mtindo wazi (open method) kama unaona inafaa.
7. Wapatie dawa ya kuzuia minyoo pia zipo dawa za asili kama unga wa mkaa na majivu pia zipo za kitaalamu, wasiliana na wataalamu wa mifugo
8.Waachishe kunyonya katika juma la nane au wafikapo kilo 14 hadi 20 hii itasaidia kujitegemea na kukua kwa haraka.
 
Nguruwe Walioachishwa Kunyonya
1.Walioachishwa kunyonya wawekwe makundi ya 10 hadi 12 kulingana na uzito au ukubwa wao kwenye eneo ambalo watajitosheleza.
2.Watenganishe wakubwa kwa wadogo ili kuzuia kupigana.
3.Wakati wa kuwaachisha kunyonya mwondoe mama yao kutoka kwa watoto ili kupunguza usumbufu.
4Watoto wa nguruwe wa mama tofauti wasiwekwe pamoja maana hii husababisha mapigano kati yao na
5.Unapowachanganya watoto wa mama tofauti wapake mafuta ya gari yaliyotumika kwenye ngozi yao au mafuta ya kula ili kuiondoa harufu ya kutambulika ili wasipigane
 
FAIDA YA UFUGAJI WA NGURUWE
Faida kuu ya nguruwe ni zao la chakula lakini pia ni zao la kukuongezea kipato ukiwa kama mjasirimali / mfanyabiashara.
Lengo langu nikueleza namna unavyoweza kufuga na kutupa faida, Steps zifatazo ni muhimu kuzigatia.
 
JIPE MTAJI WA MILLION 4 / 3.5 KWA NGURUWE 50
UANDAAJI WA BADA WEKA MAKADILIO YA LAKI TANO (800,000/=) .
Hapo nazugumzia banda lenye heru U yenye mstatili ikiwa na kitako kirefu
Eneo lenye ukubwa wa mita 50 kwa 50 litafaa zaidi ili kuhakikisha usalama wa nguruwe wako na ukuaji bora.
1. Tafuta mabati used kwa bei ya 5000 mfano mabati 20 ya futi 10 /10 = 100,000/=
2. Tafuta mabazi ya futi 10 kwa 2000 kila moja utapata mabazi pic 100 = 200,000/=
3. Tafuta miti ya nguzo na kechi ya 1000 na 2000 miti ya 1000*70 na 2000*3 = 120,000/=
4. Tafuta chagalawe / moramu trip 10*3000 =30000/=
5. Cement mifuko kwa ajiri ya sakafu na mashimo ya kulishia 5 *18000 = 90,000/=
6. Misumari ya aina 4, nch 6 kg5,nch 3 kg5 nch 5 kg10 na nch4 kg10, Bawaba na komeo =100,000/=
7. Malipo ya fundi 75000 fundi uashi na 75000 fundi seremala =150,000
JUMLA HAPO INAKUWA 790,000/= MAKADILIO INAKUWA 800,000/=
 
UNUNUZI WA NGURUWE WA KUANZIA .
Nguruwe wadogo wadogo ni vinzuri zaidi kuanza nao kwa sababu watakuzalia watoto wengi na kwa muda mrefu . Chukua mfano MILLION 2.5 . Nguruwe wadogo wa dogo wanauzwa 50000 au 40000 inategemeana na mahala na maelewano . Milioni 2.5 inakupa vitoto 50 au 55 . Hivyo unawexa kuwa na vitoto jike 50 na vidume 5. baadaye ukaongeza madume matano ya kuazima au kukondi kwa ajiri ya kupandishia
 
MAANDALIZI YA CHAKULA
Mchaganyiko wa chakula cha nguruwe na gharama zake tunaweza ukadilia kujitosheleza kwa laki tatu kwa mwenzi mmoja kwa nguruwe hao 50, kwa 300,000/= , ambapo itajumuisha tiba / kinga, lishe, vyakula vya nguruwe vinaweza kuwa pumba ya mpunga ile laini,pumba ya mahindi, mashundu, mabaki ya magada ya vianzi amba mabaki ya chakula yaliyosalama
 
MALIPO YA MSIMAMIZI NA ENEO LA KUWEKEZA
Katika kipengele hiki makadilio ya juu ama ya chini kwa msimamizi wa kazi yako waweza mlipa 100,000/= ama chini yake pia kwa mwenye eneo huwa nimaelewano tu aunaweza pata kwa fair au kukakodi kwa laki tatu, 300,000/= kwa mika miwili.
 
HIVYO JUMLA YOTE YA GHARAMA ZA UAZISHAJI UWEKEZAJI WA NGURUWE 50 ZITAKUGHARIMU MILLION 4 AMA MILLION 3.5 KWA MAANA KUWA HAPO JUU NIMETUMIA MAKADILIO YA JUU NA UKIINGIA KWENYE UHALISIA KAMA MJASIRIMALI LAZIMA IPUNGUE NA KUFIKIA 3.5

KIPATO AU FAIDA YA UFUGAJI NGURUWE
Nguruwe wanafaida ya haraka na nimradi wa uhakika kabisa, ukipitiia mchanganuo hapo juu wa nguruwe 50 utatupa faida kama ifatavyo
 
Nguruwe huzaa Mara mbili kwa mwaka na huzaa watoto zaidi ya watanoyaani huzaa watoto 12 ama nane .
Basi chukua nguruwe 50 * vitoto 5 yaani ufanye kuwa nguruwe wako 50 wakupatie vitoto vitano vya uhakika
Nguruwe 50*5 = 250 ukijumlisha na wale 50 wa mtaji umakuwa nao 300 . Chukua zao la nguruwe la 250 na uza kwa 200000 kwa kila nguruwe yaan bei ya kawaida kabisa. Utapata Million 50.

Hivyo zao la kwanza ndani ya robo tatu ya mwaka inakutegenezea million 50 pia na mienzi sita ijayo inakupa tena 50 na zaidi ili kukamilisha uzao wa pili hii inkupa uhakika wa kutegeneza million 100 za uakakika ndani ya mwaka mmoja na nusu ama miaka miwili ukijipa timeframe work lakini kumbuka hapo tumefanya kwa hesabu ya uzao wa chini kabisa ambapo tumeangalia na hasara ya vifo kama vifo visipotokea na uzao ukawa mkubwa utakuwa na uhakika wa kutegeneza million 150 kwa miaka miwili.

Kwenye hesabu ya kuwale unaweza kuwaza sana kuwa itaongezeka na kukughalimu sana jibu ni hapana mpka kufikia kuuza hawatokugharimu zaidi ya million 7 je million 7 kwenye million 150 ni kitu kisicho nafaida ?
 
NB . jambo lolote linahitaji umakini naa dhamira ya dhati pia kushirikisha wataalamu na wenye uzoefu ili kufikia leng Ewe ndugu kila kitu kinawezekana UTAYARI WAKO / UTHUBUTU WAKO, UAMINIFU .NA MAAMZI YAKO.
 
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images