Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya January 18


Wimbo Mpya wa Ben Pol - Wakuone

Video Mpya ya Nay Wa Mitego - Mbele Kwa Mbele

$
0
0
Video Mpya ya Nay Wa Mitego - Mbele Kwa Mbele

Wizara ya Madini Kuweka Msukumo Miradi Ya Liganga, Mchuchuma

$
0
0
Na Asteria Muhozya, Ludewa
Wizara ya Madini imesema itashirikiana na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kupitia Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC) kuweka msukumo ili kuhakikisha  kwamba miradi ya Makaa ya Mawe Mchuchuma na ule wa Chuma Linganga inaanza kutekelezwa.

Kauli hiyo ilitolewa Januari 16 na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za madini mkoani Njombe  na kuona namna ya kutatua changamoto zinazohusu Wizara ya Madini katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Alisema miradi hiyo ni moja ya miradi ya kimkakati ambayo Taifa linatarajiwa kunufaika kwa kiasi kikubwa, hivyo kutokana na umuhimu wake, wizara ya madini itashirikiana na wizara hiyo kuhakikisha hatua zaidi zinapigwa ili hatimaye miradi hiyo ianze kutekelezwa kwa kuwa imechukua muda mrefu.

Aliongeza kuwa, ni miradi mikubwa ambayo taifa linatarajiwa kunufaika nayo  kupitia ajira na kuongeza pato la nchi huku akiyataja madini ya chuma kuwa moja ya malighafi muhimu kwa uchumi  wa Tanzania ya viwanda na kusema kuwa, kama taifa, linautolea macho mradi huo na kwamba serikali imedhamiria kuutekeleza.

Aliongeza kwamba, katika Serikali ya Awamu ya Tano, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli anayo imani kubwa  kuwa miradi hiyo itaanza huku serikali ikitegemea kupeleka maendeleo kwa wananchi kupitia miradi husika.

“Wizara yetu ndiyo inatoa leseni za madini na tayari tulishatoa leseni ya Makaa ya mawe mchuchuma kwa hiyo nimefika kuangalia changamoto ambazo ziko upande wa wizara yetu kuweza kuzitatua ili tutoke hapa. Miradi hii tumeisikia miaka mingi ni wakati sasa tunataka ianze.” alisisitiza Nyongo.

Aliongeza kuwa, ikiwa wizara ndiyo inatoa leseni za madini,  inaowajibu wa kujua yule aliyepewa leseni kama anaifanyia kazi na kuongeza, “Sisi tuliotoa leseni lazima tuangalie tuliyempa leseni amekwama wapi  lakini pia tujue miradi hii inaanza lini? Makaa ya mawe na chuma vyote vinahitajika kwa taifa. Tunatambua makaa ya mawe ni madini ambayo yana tija kwa uchumi kwa nchi,” alisema Nyongo.

Akifafanua zaidi kuhusu miradi hiyo alisema kuwa, mradi wa Makaa ya Mawe unatarajiwa kuzalisha umeme ambao mbali ya kuuza kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), umeme huo unatarajia kutumika katika kuzalisha madini ya Chuma Liganga.

“ Mpango ni Liganga kutumia megawati 250 kwa shughuli zake za kuzalisha chuma na megawati 350 zitauzwa Tanesco kuzalisha umeme,” aliongeza.

Akifafanua sababu za kuchelewa kwa miradi hiyo, alisema ni kutokana na changamoto za kimkataba ambazo bado ziko katika majadiliano katika ngazi za juu na kuitaja baadhi ya mikataba hiyo kuwa ni  kuwa ni pamoja na mikataba ya upunguzaji wa kodi.

Aliongeza kuwa, wizara ya madini ikiwa ni wizara ambayo inasimamia Sheria ya Madini, imelenga kuhakikisha kwamba miradi hiyo mikubwa inaanza ili hatimaye iweze kuwanufaisha watanzania na taifa.

Akielezea suala la fidia kwa wananchi waliopisha miradi hiyo, alianza kwa kumpongeza Mkuu wa Wilaya ya Ludewa kwa kutenganisha suala la miradi hiyo na fidia  ambapo alisema kwamba taratibu za juu zikikamilika, wananchi watalipwa fidia na hivyo kuwataka kuwa na subira na kuwa tayari kupisha utekelezaji wa miradi hiyo.

Awali,  Mkuu wa Mkoa wa Njombe , Christopher Ole Sendeka alimweleza waziri umuhimu wa wizara ya madini kujielekeza  kwenye kupata taarifa halisi kuhusu tafiti zilizofanyika awali kuhusu akiba iliyopo ya madini ya chuma Liganga na Makaa ya Mawe mchuchuma.

Aidha, aliongeza kuwa, mbali na chuma na makaa ya mawe mkoa huo unayo madini mbalimbali ikiwemo dhahabu ambayo bado haijachimbwa kwa kiasi kikubwa.

Miradi ya Makaa ya Mawe Mchuchuma na Chuma Liganga, inatekelezwa kwa ubia kati ya Serikali ya Tanzania kupitia Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na kampuni ya Sichuan Hongda Group Ltd, ya China.

Pia, akiwa mkoani humo, Naibu Waziri alitembelea mgodi wa Kokoko Kokoto wa Nyakamtwe Quary, ambapo alitoa changamoto kwa mmiliki wa mgodi huo kuongeza kasi ya uzalishaji na kuwa wabunifu kutumia fursa  za miradi mikubwa ya ujenzi inayotekelezwa na serikali ikiwemo ya ujenzi wa reli ili kokoto hizo ziweze kutumika.

Kilosa Wataka Mabwawa Kupunguza Athari Za Mafuriko

$
0
0
Wilaya ya Kilosa imekuwa ikiathiriwa na mafuriko ya mara kwa mara kutokana na  mvua nyingi zinazonyesha nchini na kusababisha kujaa kwa maji katika mito mikubwa inayopita katika wilaya hiyo ambayo ni mto Mkondoa na Mkundi. Kutokana na hali hiyo Kamati ya Wilaya ya Usimamizi ya Maafa Kilosa imeliomba Baraza la Taifa la Usimamizi wa Maafa kuzielekeza wizara za kisekta kukamilisha mpango wa kufufua na kujenga mabwawa wilayani humo, ili kupunguza kasi ya maji yanayo jaa katika mito hiyo.

Akiongea wilayani Kilosa wakati wa kufuatilia hatua za urejeshaji hali kutokana na athari za maafa ya mafuriko yaliyotokana na mvua zilizonyesha, Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kanali, Jimmy Matamwe ameeleza kuwa wamelipokea ombi hilo ambalo ni muhimu kutekelezwa kwa ajili ya kupunguza athari za maafa wilayani humo.

“Mvua zinaponyesha na tukawa na utaratibu mzuri wa kuyavuna maji hayo, matokeo ya mvua hizo huwa zinachochea shughuli za maendeleo hasa kilimo, lakini bila kuyavuna maji yanaweza kusababisha maafa kama  mafuriko. Kwa kulitambua hili, tutaratibu wizara husika kuhakikisha mabwawa yanafufuliwa ili kuhifadhi maji na kupunguza maji mengi yanayoingia mto Mkondoa” Alisisitiza Kanali, Matamwe.

Kanali Matamwe amewataka wananchi wa kilosa kutoendeleza shughuli za kibinadamu kando ya mto huo kutokana na kuwa serikali imetumia gharama kubwa za kujenga tuta la mto Mkondoa kwa lengo la kupunguza athari za maafa yaliyokuwa yanatokea baada ya mto huo kujaa.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati ya Wilaya ya Maafa Bw. Asajile Mwambambale, amefafanua kuwa ipo haja ya kuharakisha ujenzi wa bwawa  la Kidete ili kuweza kupunguza kasi ya maji ma wingi wa maji yanayo ingia mto Mkondoa, ambapo athari zake za mafuriko huathiri watu, mali na miundombinu ya Kilosa.

“Pamoja na kuwa tungependa utafiti wa kina ufanyike kuanzia kwenye chanzo cha mto Mkondoa  ili kuweza kuelewa tabia ya mto huu, niliombe Baraza la Taifa la Usimamizi wa maafa, litusaidie kuzielekeza hizi wizara za kisekta, ikiwemo wizara ya maji, zikamilishe mipango ya kufufua  na kujenga mabwawa ambayo yatasaidia kuhifadhi maji na kupunguza wingi wa maji yanaoyoingia katika mto Mkondoa” alisema Mwambambale.

Mwambambale amefafanua kuwa wilaya ya kilosa imeendelea kutekeleza mpango wa Kujiandaa na Kukabiliana na mafuriko kwa kutoa mchanga kwenye mto Mkondoana Mkundi, ili kuongeza kina cha mito hiyo. Pia zoezi la Upandaji wa miti na matete kando ya  mto Mkondoa limefanyika. Aidha Kamati za maafa za kata na vijiji pamoja na timu za uokoaji na kutoa misaada kwa waathirika wakati wa maafa zimejengewa uwezo.

Wilaya ya Kilosa ni miongoni mwa wilaya 7 za mkoa wa Morogoro ambayo imekuwa ikiathiriwa na mafuriko ya mara kwa mara kutokana na mvua zinazonyesha mikoa ya jirani ya Dodoma na Manyara hususani Wilaya za Mpwapwa, Kongwa na Kiteto, maji ya mvua hizo hupita wilayani Kilosa kupitia mto Mkondoa na Mkundi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya January 19

Sekta ya Afya Nchini Yaendelea Kukua Kwa Kasi

$
0
0
Na WAMJW – DOM
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa Sekta ya Afya nchini yaendelea kukua kwa kasi, kutokana na Serikali kuendelea kuboresha Huduma kwa Wananchi zikiwemo upatikanaji wa Dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi, huduma za chanjo, huduma za afya ya uzazi na mtoto na Huduma za Dharura.

Waziri Ummy ameyasema hayo wakati akitoa tamko mbele ya Waandishi wa Habari na baadhi ya viongozi wa Wizara, kuhusu hali ya Huduma za Afya mwaka 2018, katika ukumbi wa Wizara ya Afya jijini Dodoma.

Waziri Ummy amesema kuwa Katika mwaka 2018, jumla ya wajawazito 2,086, 930 walihudhuria na kuandikishwa Kliniki, ikilinganishwa na wajawazito 2,009,879 Mwaka 2017, huku mwongozo wa utoaji huduma za afya ya uzazi na mtoto unaelekeza wajawazito kuanza huduma mapema kabla ya majuma 12 ya ujauzito na kuhudhuria kliniki angalau mara nne katika kipindi cha ujauzito.

Mbali na hayo Waziri Ummy amesema kuwa, Katika kipindi cha mwaka 2018 jumla ya watoto 1,568,832 walizaliwa ikilinganishwa na Watoto 1,498,488 mwaka 2017, huku wakipatiwa huduma mbalimbali za chanjo ili kuzuia magonjwa yanayowaathiri Watoto ikiwemo ugonjwa Kupooza, Kuharisha, Pepopunda, Pneumonia, homa ya ini na Surua.

“Katika kipindi cha mwaka 2018 hali ya chanjo kwa Watoto nchini imeendelea kuwa katika kiwango cha juu zaidi ya asilimia 85 ya kiwango kilichowekwa na Shirika la Afya Duniani kama inavyoonyeshaa katik hapa chini” Alisema Waziri Ummy.

Hata hivyo nWaziri Ummy amesema mwaka 2018 kumetokea jumla ya vifo 20,087 ikilinganishwa na vifo 19,693 mwaka 2017, huku Katika kipindi cha miaka yote miwili 2017 na 2018, homa ya mapafu imeongoza kwa kusababisha vifo, ambapo kwa mwaka 2017, imechangia asilimia 18.2 ya vifo vyote na mwaka 2018 imechangia kwa asilimia 12.9 ya vifo vyote.

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa Mwaka 2018, ugonjwa usio wa kuambukiza (shinikizo la damu) umejitokeza katika magonjwa 10 yanayoongoza kwa kusababisha vifo ambapo umechangia vifo kwa asilimia 1.9 ya vifo vyote.

Kwa upande mwingine, Waziri Ummy amesema kuwa Hali ya upatikanaji wa Dawa muhimu katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini imeendelea kuimarika, hii ni kutokana na Serikali kuongeza bajeti ya dawa kutoka Shilingi Milioni 31 mwaka 2015/16 hadi kufikia Shilingi milioni 251 mwaka 2016/17 na Shilingi 270 mwaka 2018/19.

Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa hali ya upatikanaji wa Damu Salama ambapo katika kipindi cha mwaka 2018, huku jumla ya chupa za damu salama 307,835 sawa na asilimia 85.5 ya lengo zilikusanywa ikilinganishwa na chupa 233,933 mwaka 2017, huku akiwahasa Wananchi kujitokeza kuchangia damu ili kuendelea kuokoa maisha ya wahitaji.

“Chupa zote 307,835 zilizokusanywa zilipimwa makundi ya damu pamoja na magonjwa makuu manne ambayo ni Ukimwi (HIV,) Homa ya Ini B na C (HBV, HCV) na Kaswende (Syphilis). Jumla ya chupa 262,283 sawa na asilimia 85.3 zilikuwa salama na kusambazwa katika hospitali kwa ajili ya wagonjwa wenye uhitaji wa damu.” Alisema Waziri Ummy.

Hata hivyo Waziri Ummy amesema kuwa, katika mwaka 2018 jumla watu 47,967 waligundulika kuwa na vijidudu vya Kifua kikuu ikilinganishwa na wagonjwa 44,714 waliogunduliwa mwaka 2017., huku akisisitiza kuwa tatizo la ugonjwa wa Kifua Kikuu limeendelea kuwepo takribani mikoa yote nchini.

kwa upande mwingine, Waziri Ummya amesema kuwa, hadi kufikia Desemba 2018, jumla ya vituo vya kutolea huduma za Afya vilifikia 7,768 kutoka vituo 7,435 mwaka 2017 sawa na ongezeko la vituo 333 kwa mwaka, amedai kuwa Serikali ilikuwa inamiliki asilimia 71 ya vituo vya kutolea huduma; Mashirika ya dini asilimia 12, Taasisi za Serikali asilimia 3 na vituo binafisi asilimia 15.

Sambamba na hilo, waziri Ummy amesema kuwa, hadi kufikia Desemba mwaka 2018, Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ulikuwa na jumla ya wanachama 899,654 na ikihudumia jumla ya wanufaika 4,219,192 sawa na asilimia 8 ya Watanzania wote.

Wanne Watia Mbaroni Jijini Arusha kwa Kutengeneza Fedha Bandia

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha limewakamata watuhumiwa sita kwa makosa mbalimbali.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Ramadhani Ng'anzi amesema jana Ijumaa Januari 18, 2019 kuwa watuhumiwa wanne ambao hakuwataja majina yao kwa sababu za kipelelezi wanajihusisha na utengenezaji wa fedha bandia.

Amesema mtuhumiwa wa kwanza alikutwa na noti bandia za dola za Marekani  zenye thamani ya dola 500 (zaidi ya Sh 1.1 milioni).

"Huyu mtuhumiwa wa kwanza aliwapeleka askari wetu nyumbani kwake eneo la Daraja Mbili ambako zilikutwa fedha bandia za mataifa mbalimbali," alisema Ng'anzi

Fedha hizo ni dola za Marekani, fedha za Umoja wa Ulaya (Euro), Kenya, Malawi, Zambia, Rwanda na Sudan.

Alisema watuhumiwa wanashikiliwa kwa ajili ya mahojiano na upelelezi ukikamilika watafikishwa mahakamani.

Katika tukio jingine, Ng'anzi amesema kuwa watuhumiwa wengine wawili ambao ni Kennedy Mbilinyi na Richard Loishiye wamekamatwa kwa kuiba gari aina Harrier lenye namba za usaili T 241 DKC na kujaribu kulivusha mpaka wa Namanga kuelekea nchi jirani ya Kenya.

Alichokisema Zitto Kabwe Baada ya Spika Ndugai Kusema Anamuumiza Sana Kichwa

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo) Zitto Kabwe amesema kuwa si kweli kwamba yeye ndiye Mbunge anayemsumbua zaidi Spika Job Ndugai kama alivyodai kwani amekuwa akifuata taratibu na kanuni bila kuvunja sheria.

Zitto ambaye pia ni Kiongozi wa ACT-Wazalendo ametoa kauli hiyo  baada ya kuulizwa kuhusu maoni yake kufuatia kauli ya Spika aliyoitoa jana akidai kuwa Zitto ni mbunge anayempa tabu kutokana na kauli zake.

"Sijui kwanini Spika amesema vile kwani mimi simpi tabu, nasimamia haki na Spika afuate kanuni tu”, amesema Zitto.
 
Januari 17 katika mkutano wake na wanahabari, Spika Ndugai amesema amekuwa akishindwa kumfukuza bungeni mbunge huyo wa Kigoma Mjini kwa kuwa ndiye pekee anayekiwakilisha chama cha ACT- Wazalendo.

"Ni kweli Zitto Kabwe ananisumbua sana lakini, ukisema umtoe Bungeni unawaza mtu mwenyewe yuko peke yake ukimsimamisha atawakilishwa na nani?. Unamuacha tu lakini wale wengine nafukuza tu maana wako wengi akikosekana kwenye mjadala atawakilishwa na wenzake, hebu nisaidieni Zitto nimfanyeje?, alihoji Spika Ndugai.

Kigwangalla Aivunja Bodi ya Utalii (TTB)

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangalla amevunja bodi ya wakurugenzi ya Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) kuanzia jana Ijumaa na kutoa miezi mitatu kwa menejimenti kujirekebisha kinyume na hapo ataifumua.

Waziri huyo ametangaza kuunda bodi mpya ya wakurugenzi ambayo itakuwa na wajumbe vijana watakaokwenda na kasi katika kazi hiyo ya kutangaza vivutio.

Dk Kigwangalla amefikia uamuzi huo kwa kile alichoeleza kuwa TTB imeshindwa kutekeleza maelekezo yake yenye lengo la kutangaza vivutio vya utalii.

Akitoa uamuzi huo jana Ijumaa Januari 18, 2019 mbele ya waandishi wa habari Dk Kigwangalla ameeleza kutotangazwa kwa vivutio vya utalii kunaifanya Serikali inyooshewe kidole na kuonekana haifanyi kazi.

Amesema kwa kipindi cha mwaka mmoja ametoa maelekezo zaidi ya 15 lakini hayajafanyiwa kazi jambo linalosababisha yeye kutukanwa.

“Serikali ikitukanwa kwenye sekta ya maliasili na utalii maana yake natukanwa mimi naonekana sitoshi kwenye nafasi hii, “ amesema Dk Kigwangalla.

Miongoni mwa maelekezo ambayo hayajafanyiwa kaiz ni pamoja na TTB kutoweka mabango ya kutangaza utalii katika miji mikubwa ikiwemo Dar es Salaam kuanzia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA)

Jingine ni kushindwa kuwatumia watu maarufu na wasanii kutangaza vivutio vya utalii, kushindwa kutangaza vivutio kwenye michezo, kutotengenezwa kwa video na filamu fupi zinazojumuisha vivutio na nyingine nyingi.

Rais Magufuli: Changamoto Zilizopo Sasa Zisipotatuliwa, Sidhani Kama Ajaye Atazitatua

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amesema hana uhakika endapo mrithi wake ataweza kutekeleza mambo anayoyafanya katika uongozi huu wa awamu ya tano.

Magufuli ameyasema hayo jana  Ijumaa Januari 18, 2019 katika hafla ya makabidhiano ya mfumo wa kusimamia uwazi katika mawasiliano ya simu (TTMS) wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Alisema katika safari ya kutatua changamoto anakutana na magumu mengi na ndiyo maana amekuwa akihitaji nguvu za Mungu kutekeleza majukumu yake.

“Viongozi wa dini endeleeni kuliweka Taifa hili kwenye mikono ya Mungu. Hii ni vita kama ilivyo nyingine na vita ya uchumi inahitaji maombi sana, bila maombi kazi hii haiwezi kufanyika,” alisema.

“Hao wanaokaa gizani hauwezi kujua ana kisu, ana panga au ameweka nyoka mfukoni lakini huko gizani huwa wanatolewa kwa maombi, yatawapumbaza huko gizani wasitake kufanya walichokusudia.”

Alisema kufanya hivyo kutawafanya viongozi wa nchi kusimamia misingi ya uadilifu na upendo wa kweli katika kulitumikia Taifa tajiri, lenye changamoto nyingi zinazohitaji kutatuliwa.

Zitto Kabwe Adai Kutishiwa Kuuawa Dodoma .....Amwandikia Barua Spika wa Bunge

Wimbo wa Kumtukuza Bwana: Niongozwe Nawe - Doreen Lifard

$
0
0
MWIMBAJI Wa Nyimbo za  Injili, Doreen Lifard anakukaribisha Weekend hii ujumuike naye katika kumtukuza Mwenyezi Mungu kupitia Wimbo wake Uitwao Niongozwe Nawe. Utazame Hapo chini

Super Mkongo: Kiboko ya Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
********************************
SUPER MKONGO MPYA,
_______________________________
********************************
Ni dawa bora ya kutibu na kumaliza matatizo yote ya nguvu za kiume na sababu zake zote kama vile,

- kuwahi kufika kileleni dakika moja ushakojoa
- maumbile kusinyaa na kulegea wakati wa tendo
- kukosa hamu ya tendo la ndoa
- kushindwa kurudia tendo la ndoa
- uume kusimama kwa kulegea
- uume kulegea katikati ya tendo
- kuathirika kwa kujichua kwa muda mrefu
- kuishiwa nguvu kutokana na punyeto.

Epuka aibu hii leo kwa kutumia SUPER MCONGO MPYA, kiboko ya matatizo haya.
_______________________________
Pia kuna MCONGO POWER Kiboko ya uume mdogo inaboresha maumbile ya uume kwa kurefusha na kunenepesha kwa saizi uipendayo haijalishi umri hata kwa walioathirika na upigaji punyeto.
_______________________________
Kwanza fahamu sababu zinazopelekea kuwa na upungufu wa nguvu za kiume na uume mdogo.
_______________________________
(1) kujichua (punyeto) kwa muda mrefu maana hupelekea misuli ya uume kulegea.
(2) ngiri
(3) kuugua chango la uzazi kwa muda mrefu.
(4) kupungukiwa hormone za testosterone.
(5) ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na visivyo na virutubisho  vya kutosha.
(6) kutokufanya mazoezi na mwenendo wa maisha.
(7) kisukari.
(8) tumbo kuunguruma na kujaa gesi.
(9) maumivu ya kiuno nk.
_______________________________
Kwanini uhangaike? Kwanini uhuzunike?
Hii ni spesho kwa waliotumia madawa mengi bila kufanikiwa hakika hautajuta kuitumia. _______________________________
WASILIANA NA:
DR. MCONGOMANI
SIMU NO:
📞0658816558
📞0682323682
Popote ulipo huduma hii inakufikia
_______________________________
********************************

Tambua Dalili Za Kupungikiwa Nguvu Za Kiume Na Chanzo Chake

$
0
0
Tambua Dalili Za Kupungikiwa Nguvu Za Kiume Na Uume Kuwa Mdogo Na Chanzo Chake;dalili za mwanaume kupungukiwa nguvu za kiume ni kama vile 1. mwanaume mpaka amwambie mke au mpenzi wake naomba ushike  ili usimame 2. ,kushindwa kurudia tendo,3.  kusimama na kuwa legelege 4,kuisha nguvu au kuanguka ukiwa ndani ya tendo 5,kuwai kukojoa kabla  ya mke au mpenzi wako .

NI NINI CHAZO CHA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME,1,magonjwa ya moyo,presha,kisukari 2,usongo wa mawazo 3, utumiaji holela wa madawa  4 uume kukosa vichocheo ambavyo usababisha damu isiwe na mzunguko mzuri

NI NINI KINASABISHA UUME KUWA MFUPI? 1 unene kupita kiasi 2 kuumwa na chango hasa chini ya kitovu 3 kuvaa nguo za kubana sanasana ni wakati wa usiku,4 kufanyiwa tohara ukubwani,

SUPER MAJINJAS; ni dawa ya nguvu za kiume ambayo itakufanya urudie tendo zaidi ya Mara tatu pia itakufanya uchelewe kufika kilele dakika 10-15 kwa tendo la kwanza 

MANGUNGU NO 5 MPYA; dawa hii uboresha uume saizi upenda ichi 5,6,7,na 8 kwa urefu na unene wa sm 1-5 za upenyo dawa zetu ni ukweli na uhakika ni tofauti na ulizowai kutumia ni dawa za miti shama za vidonge unga na maji ,

ISENYE; ni dawa ya kisukari ambayo utibu kabisa tatizo dozi yake siku 21 pia ipo dawa ya uzazi 

FIKA OFISINI KWANGU BUGURUNI MALAPA morogoro yupo wakala maeneo ya stendi kuu mwanza yupo mtaa wa biza c mbeya yupo mbalizi ,na kahama mjini piga simu 0744040721. 0683645920 Dr BRUNO na utaletewa popote ulipo

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Mvuto Wa Mapenzi

$
0
0
*************************
KIBOKO YA  MATATIZO YA  NGUVU  ZA  KIUME MAUMBILE MADOGO MVUTO  WA  MAPENZI .
MAGONJWA SUGU
*************************
Wanaume  wengi wana  upungufu wa  nguvu  za kiume nakuwa  na  maumbile madogo  ya kiume magonjwa kama  kisukari, presha, ngiri  korodani kuvumba, busha, tumbo kuunguruma na kujaa  gesi  na  kutopata  choo  vizuri, punyeto  NK.
___________________________
Huchangia kwa  kiasi kikumbwa upotevu  wa nguvu  za kiume tumia dawa nzuri ya  mitishamba ambayo haina madhara kwa mtumiaji ata uwe  na  miaka 80 inatibu na kumaliza matatizo  hayo:

 SUPER SHAFT 
********'****************
HII NI DAWA  YENYE  UWEZO  MKUBWA WA  KUOGEZA  NGUVU ZA KIUME MARA  DUFU NA MAUMBILE MADOGO  YA KIUME
************************
(1) Itakufanya uwe  na nguvu za  ajabu ukiwa unafanya tendo la ndoa.
___________________________
(2 ) Inaongeza hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi  ya mara  tatu bila kuchoka.
___________________________
(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni ndani ya dk 30 nakukupa nguvu ya ajabu.
___________________________
(4) Pia itakupa nguvu za kusimamisha uume wako barabara kama msumari wakati wa tendo la ndoa.
___________________________

NYATI POWER
*****************
INAREFUSHA NA KUNENE PESHA MAUMBILE YA KIUME  SAIZI UTAKAVYO kuazia Inchi 1 -8 unene sm 2-4.
*************************
(5) Itaimarisha mirija ya uume iliyolegea au kusinyaa.
___________________________
(6)lnasaidia kisafisha mishipa ya kwenye uume na hivyo kusaidia kuogeza kasi ya msukumo wa damu kwenye mishipa ya uume.
___________________________
(7) Usaidia kuurudisha nje uume ulioingia ndani.
___________________________
(8) Inasaidia kuogeza  manini  nyingi abazo vinaviini vya  uzazi.
___________________________
(9)Husaidia kutibu  madhara ya punyeto.
___________________________
Matumizi makali ya madawa  ya kizungu mirungi, bangi na  sigara.
*************************
TUNATIBU MAGONJWA YOTE SUGU, NGIRI, KORODANI KUVIMBA,  BUSHA BILA KUFANYIWA OPARESHENI, TEZI DUME, KISUKARI, PRESHA AINA ZOTE, UGONJWA WA MOYO STROKU. KWIKWI, KICHOMI MIGUU KUFA NGAZI NK
*************************
ANAPATIKANA MAGOMENI MIKUMI, KARIBU NA  KANISA KATOLIKI, TUMAINI HEARST CLINC NDIYO  SULUHISHO LA MATATIZO YOTE
*************************
PIGA  SIMU
📞0745495181 AU
📞0682644040 
*************************
WOTE  MNAKARIBISHWA
*************************
Kama huna nafasi ya kufika ofisini  kwetu  huduma  hii  utaletewa mahali  ulipo na wa mikoani  mtaipata kirahisi.
KWA MENGINEYO INGIA HAPA
*************************

Alichokisema Spika Ndugai Sakata la Zitto Kabwe Kutishiwa Kuuawa

$
0
0
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai, ametoa kauli yake baada ya Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Zuberi Kabwe kulalamika kutishiwa uhai na mtu wa usalama wa Taifa ndani ya viwanja vya Bunge siku ya jana Januari 18, mpaka kufikia hatua ya kumuandikia Spika Barua.

Spika Ndugai amesema kwamba barua hiyo haijamfikia rasmi mezani kwake ingawa kaiona mitandaoni, hivyo hawezi kuifanyia kazi mpaka pale itakapofika mezani kwake.

“Barua haijanifikia, unajua baadhi ya matatizo tunayapata siku hizi tunayakimbizia kwenye mitandao, inatakiwa niipate rasmi kama ni ya kweli tutayafanyia kazi”, amesema Spika Ndugai.

Akiendelea kuzungumzia suala hilo Spika Ndugai amesema licha ya taarifa hizo usalama wa Wabunge uko 'guaranteed”, ingawa taarifa hizo sio za kuzipuuzia.

“Usalama wa wabunge uko 'guaranteed', wabunge wako salama kabisa, kumbuka Wabunge wote kwa ujumla wetu tuko 363, na tuna watumishi pale bungeni zaidi ya 300, kwa hiyo kuna 'community' ya watu mia sita, ukisikia mtu mmoja analalamika, wawili kwenye kundi kubwa kiasi hicho, unatakiwa ulifikirie hilo jambo, sio la kudharau hata kidogo, lakini halimaanishi kwamba hapo mahali usalama haupo, pako salama sana”, amesema Spika Ndugai.

Licha ya hayo Spika Ndugai amekanusha tuhuma za kuwazima wabunge wa upinzani pale wanapotaka kuibua hoja ya msingi kuhusu muswada wa vyama vya siasa, na kusema kwamba wakati huu wadau (wananchi) ndio wanatoa maoni yao, na wao utakapofika muda wao wataruhusiwa kutoa maoni yao, hivyo wawaache wananchi wautumie muda wao.

“Hakuna wabunge wa upinzani wanaozimishwa, kwa sababu kinachoendelea sasa hivi Kamati inasikiliza wadau, Watanzania wanakuja pale kwenye Bunge wanatoa maoni yao kuhusu ule muswada, Wabunge wanapoingia mule ndani na kuanza kuleta fujo maana yake nini wakati hii sio zamu yao wao!? Zamu yao itakuja kwenye bunge mule, sasa wao wanakuja wanaanza kuleta fujo”, amesema Spika Ndugai.

Credit:Eatv

Shambulizi la Kigaidi Kenya :Washukiwa sita wafikishwa mahakamani

$
0
0
Washukiwa sita, akiwemo raia wa Canada, wamefikishwa mahakamani Ijumaa nchini Kenya, kuhusiana na shambulizi la kigaidi kwenye hoteli moja mjini Nairobi na kusababisha vifo vya watu 21.

Watuhumiwa hao wametajwa kuwa Joel Ng’ang’a Wainaina, Oliver Kanyango Muthee, Gladys Kaari Justus, Osman Ibrahim, Hussein Muhamed na Guleid Abdihakim ambaye ni raia wa Canada.

Jaji wa mahakama alikubali ombi kutoka kwa upande wa mashtaka kutaka watuhumiwa hao wanne na mwanamke mmoja kubaki chini ya ulinzi kwa siku 30 wakati uchunguzi ukiendelea. Mtuhumiwa wa sita atafikishwa mahakamani wiki ijayo.

Watuhumiwa wanashutumiwa kuhusu ‘uwezekano wa kuhusika’ katika shambulizi la takriban saa 20 kwenye hoteli ya Dusit D2 na jengo la ofisi ambalo mshambuliaji bomu wa kujitoa mhanga na watu wanne walio kuwa na silaha waliuawa na majeshi ya usalama, nyaraka iliyotolewa mahakamani imesema.

“Uchunguzi kuhusiana na suala hili una mambo mengi na ni wa kimataifa na huenda ukahitaji muda zaidi na rasilimali ili kubaini mtandao mzima wa kihalifu,” taarifa kutoka kwa mkurugenzi wa mashtaka, Noordin Haji imesema.

Washukiwa 11 walikamatwa Jumanne baada ya shambulizi, hata hivyo uchunguzi kuhusiana na washukiwa wengine bado unaendelea.

Mtuhumiwa Wainaina anadaiwa ni dereva wa taxi ambaye aliwapatia usafiri washambuliaji mara kadhaa sehemu mbali mbali mjini, na Muthee ni dereva mwingine ambaye aliwapeleka baadhi ya washambuliaji kwenye eneo la tukio.

Mwanamke pekee katika kundi hili la watuhumiwa Gladys Justus anachunguzwa kwa kuhusika katika kutuma fedha, wakati raia wa Canada, Guleid Abdihakim anachunguzwa kwasababu ya mawasiliano yake na baadhi ya watuhumiwa.

Ibrahim anadaiwa kuwa alikutana na mmoja wa washambuliaji Januari 8.

Muhamed simu yake ilionyesha mawasiliano na baadhi ya wanamgambo wa kiislamu na atafikishwa mahakamani wiki ijayo siku ya Jumatano.

Washukiwa wawili bado hawajafikishwa mahakamani, Ali Salim Gichunge na Violete Kemunto Omwoyo ambayo wana kadi za simu ambazo zinaonyesha walikuwa na mawasiliano ya mara kwa mara na baadhi ya namba nchini Somalia, nyaraka za mahakama zimeonyesha.

Shambulizi ambalo inadaiwa lilifanywa na kundi la wanamgambo wa kiislamu la al-Shabaab la Somalia, lenye uhusiano na al-Qaeda limehusika kuilenga Kenya mara kwa mara katika mashambulizi.

Mwaka 2013 kundi hilo lilifanya shambuliz kwenye eneo la maduka la Westgate mjini Nairobi na kusababisha watu 67 kupoteza maisha, wakati mwaka 2015 kundi hilo liliua watu 18 katika chuo kikuu cha Garissa, mashariki mwa Kenya.

Credit: VOA

Tiba Asilia ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Kifaru vidonge asilia hurefusha maumbile ya kiume nchi 6-8 dk 60 garantii mika 30- 40 .itakupa nahamu ya kufanya tendo la ndoa mara 4- 5 bila kuchoka au hamu kuisha, ina imalisha misuri  ya uume  na haina madhara kwa mtuaji

Malelemba; inatibu presha kisukari, ngili, busha bila uperesheni, kiuno, kutopata choo vizuri, vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto, kisosono

Jirumba; kumvuta mume mke mpenzi mchumba kwa masaa 3 yoyote unae mtaka  uta mpata ..acha kuumiza roho bure hatakama una fanya nae kazi sehemu moja ila unaogopa kumuanza au muone mzee jirumba atakusaidia

Fika mbagara kwa wa mikoani shinyanga kahama mwanza kwa mawasiano piga 0713560943 /0762540447 dr jirumba

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images