Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Tambua Dalili Za Kupungikiwa Nguvu Za Kiume Na Chanzo Chake

$
0
0
Tambua Dalili Za Kupungikiwa Nguvu Za Kiume Na Uume Kuwa Mdogo Na Chanzo Chake;dalili za mwanaume kupungukiwa nguvu za kiume ni kama vile 1. mwanaume mpaka amwambie mke au mpenzi wake naomba ushike  ili usimame 2. ,kushindwa kurudia tendo,3.  kusimama na kuwa legelege 4,kuisha nguvu au kuanguka ukiwa ndani ya tendo 5,kuwai kukojoa kabla  ya mke au mpenzi wako .

NI NINI CHAZO CHA KUISHIWA NGUVU ZA KIUME,1,magonjwa ya moyo,presha,kisukari 2,usongo wa mawazo 3, utumiaji holela wa madawa  4 uume kukosa vichocheo ambavyo usababisha damu isiwe na mzunguko mzuri

NI NINI KINASABISHA UUME KUWA MFUPI? 1 unene kupita kiasi 2 kuumwa na chango hasa chini ya kitovu 3 kuvaa nguo za kubana sanasana ni wakati wa usiku,4 kufanyiwa tohara ukubwani,

SUPER MAJINJAS; ni dawa ya nguvu za kiume ambayo itakufanya urudie tendo zaidi ya Mara tatu pia itakufanya uchelewe kufika kilele dakika 10-15 kwa tendo la kwanza 

MANGUNGU NO 5 MPYA; dawa hii uboresha uume saizi upenda ichi 5,6,7,na 8 kwa urefu na unene wa sm 1-5 za upenyo dawa zetu ni ukweli na uhakika ni tofauti na ulizowai kutumia ni dawa za miti shama za vidonge unga na maji ,

ISENYE; ni dawa ya kisukari ambayo utibu kabisa tatizo dozi yake siku 21 pia ipo dawa ya uzazi 

FIKA OFISINI KWANGU BUGURUNI MALAPA morogoro yupo wakala maeneo ya stendi kuu mwanza yupo mtaa wa biza c mbeya yupo mbalizi ,na kahama mjini piga simu 0744040721. 0683645920 Dr BRUNO na utaletewa popote ulipo

Theresa May agonga mwamba kujitoa Umoja Ulaya

$
0
0
Waziri Mkuu wa Uingereza ameshindwa vibaya katika kura ya kujitoa katika Umoja wa Ulaya – maarufu kama Brexit – katika bunge la Uingereza baada ya wabunge kupinga mswaada wake kwa kura 432 kwa 202.

Mara baada ya kipigo hicho, May amesema kuwa kutokana na wingi wa kura za kupinga mswaada huo serikali yake itaruhusu mswaada wa kutokuwa na imani kujadiliwa bungeni.

Aidha, wakati anarudi kukaa chini, kiongozi wa chama cha upinzani cha Leba, Jeremy Corbyn mara moja alithibitisha kuwa amewasilisha kura ya kutokuwa na imani na serikali ya May, mswaada ambao utajadiliwa Jumatano.

Hata hivyo, May alikuwa amewasilisha mbele ya bunge mpango mzima wa jinsi Uingereza itakavyojitoa katika Umoja wa Ulaya suala ambalo liliidhihirishwa katika kura ya maoni mwaka 2016.

RPC Wankyo awatangazia kiama Trafiki wala rushwa

$
0
0
Askari wa Usalama Barabarani Mkoa wa Pwani, wametakiwa kufanya kazi zao kwa weledi na kuacha kuomba na kupokea rushwa.

Hayo yamesemwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Kamishina Msaidizi Mwandamizi, Wankyo Nyigesa wakati akizungumza na askari wa kikosi cha usalama barabarani wilayani Kibaha mkoa wa Pwani.

Amesema kuwa kumekuwepo na malalamiko kwa baadhi ya askari wa usalama barabarani kujihusisha na vitendo vya kuomba na kupokea rushwa jambo ambalo limekuwa likichafua taswira ya Jeshi la Polisi.

“Katika kipindi cha uongozi wangu nitakuwa mkali na sitosita kuchukua hatua kwa askari yeyote atakayebainika kuomba na kupokea rushwa kutoka kwa madereva,”amesema Wankyo

Aidha Wankyo, amewataka askari hao kuzingatia utoaji wa huduma bora kwa wateja wanaowahudumia kila siku na kuacha vitendo vya malumbano na majibu yasiyozingatia utu kwa wale wanaowahudumia katika barabara.

Hata hivyo, amewaasa madereva wanaoingia ndani ya mkoa wa Pwani kuzingatia sheria za usalama barabarani na wale watakaokaidi kutii sheria hizo watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Taarifa Kwa Umma Kutoka Kwa Mwenyekiti Wa Kamati Ya Uchaguzi Ya Tff Kuhusu Uchaguzi Wa Yanga

$
0
0
Ndugu Wana-habari, Ijumaa iliyopita niliwatangazia kusogezwa mbele kwa muda uchaguzi mdogo wa klabu ya Yanga kufuatia taarifa za wimbi la (tulioamini kuwa wana-Yanga) kufungua kesi sehemu mbalimbali nchini kuzuia uchaguzi huo usifanyike na kwamba baadhi ya Mahakama zilishatoa amri hiyo.  
 
Kwa kuheshimu mamlaka ya ki-Katiba ya Mahakama nchini na kwamba nchi yetu inaheshimu na kufuata utawala wa sheria, Kamati yangu ya Uchaguzi haikuwa na njia nyingine ya kufanya bali kuusogeza mbele kwa muda uchaguzi wa Klabu ya Yanga uliopangwa ufanyike siku mbili baadaye, yaani Jumapili ya tarehe 13/01/2018. 
 
Kwa upande wa pili, Kamati ilijikuta na deni kubwa kwa wana-Yanga, deni la kuelezea kilichojiri, kuelezea msingi wa kesi hizo mahakamani zilizosababisha kusogezwa mbele kwa muda uchaguzi katika klabu yao. 
 
Hivyo kuanzia Ijumaa jioni, yaani mara tu baada ya kutangaza kusogezwa mbele kwa muda kwa uchaguzi huo, Kamati ilitumia njia mbalimbali kuwafikia wale wote waliofungua kesi ili kujua msingi wa malalamiko yao na uhalali wao kusimama mahakamani dhidi ya Klabu hiyo ya Yanga kwa mujibu wa Katiba ya Yanga.  
 
Tumejiridhisha kuwa malalamiko yote yamejikita kwenye maeneo makuu matatu: (i) mosi, uhalali wa wanachama wenye kadi za zamani, kadi za CRDB na kadi za Benki ya Posta kupiga kura; (ii) pili, kukataliwa majina ya wanachama katika baadhi ya matawi ya Yanga kuingizwa kwenye rejista ya wanachama wa Yanga; na (iii) tatu, sintofahamu ya nafasi ya Mwenyekiti wa Yanga hivyo kusababisha baadhi ya wanachama wenye sifa za uongozi, kuwa na mashaka kujitokeza.  
 
Kamati ya Uchaguzi, mbali na kuchambua sifa ya uanachama ya walalamikaji hao (ambapo Kamati imebaini kuwa walalamikaji wote kasoro mmoja, si wanachama hai wa Yanga), imepitia malalamiko yote hayo kwa kina na kuwapelekea ujumbe ufuatao walalamikaji wote kwamba: (i)  uanachama wao Yanga una hitilafu ki-Katiba, hivyo hawakuwa na sifa (locus) kupeleka malamamiko yao popote pale kwa kivuli cha uanachama wa klabu hiyo; (ii) Katiba za Yanga, TFF, CAF na FIFA haziruhusu wanachama wao kupeleka malalamiko mahakamani, hivyo utaratibu huo hauna tija mbali na kuiondolea klabu sifa ya kuheshimu taratibu (compliance); (iii) malalamiko yao yote waliyoainisha yanatatulika kwa taratibu zilizopo ndani ya shirikisho, hivyo hawana budi kuondoa kesi hizo mahakamani mara moja.  
 
Napenda kuwataarifu kuwa walalamikaji wote wametuelewa na wamekubali kuondoa kesi zao zote mahakamami na hivyo, kuruhusu Kamati yangu kuwasilisha TFF malalamiko yote tuliyoainisha ili yafanyiwe kazi ndani ya siku 7 kuanzia jana na baada ya hapo Kamati itatangaza ratiba ya kukamilisha uchaguzi mdogo wa Yanga.  
 
Naomba vilevile nisisitize kwamba uchaguzi huu ni uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi zilizoachwa wazi. 
 
Hivyo viongozi wa Yanga tunaowachagua sasa ni wa kipindi kifupi kilichobaki cha takriban mwaka mmoja, kabla ya mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa Yanga kuanza. 
 
 Nihitimishe taarifa yangu kwa kuwashukuru Watanzania na wana-Yanga wote kwa utulivu na uvumilivu mkubwa mliouonesha baada ya uchaguzi wenu mdogo kusogezwa mbele kwa muda. 
 
Aidha nawaomba wana-Yanga wote wakiongozwa na Wajumbe wa Baraza la Wadhamini, Sekreterieti na Wajumbe waliobaki wa Kamati ya Utendaji, wasichoke maana tumekaribia mwisho wa zoezi hili lenye afya kwa ustawi na maendeleo ya klabu hii kongwe Afrika ya Mashariki na Kati. Timu bora inategemea uongozi bora unaowajibika kwa wanachama.   
 
AHSANTENI KWA KUNISIKILIZA
Malangwe Ally Mchungahela
Mwenyekiti Kamati ya Uchaguzi ya TFF

Waziri Lukuvi Atoa Hati Miliki Za Kimila Kwa Wananchi Wa Kijiji Cha Mapogolo

$
0
0
NA FREDY MGUNDA,IRINGA
ZAIDI ya Kaya 200 za wafugaji wa kabila la Wamasai na Wamang’ati wamemilikishwa ardhi katika kijiji cha Mapogolo wilayani Iringa, hatua iliyoelezwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kwamba “itamaliza migogoro ya wakulima na wafugaji na kukuza utanzania.”

Kaya hizo zilikabidhiwa hatimiliki za ardhi za kimila juzi katika hafla iliyohusisha ugawaji wa jumla ya hati 2,404 za mashamba kwa wananchi wa kijiji hicho kinachopakana na Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

Hati hizo zimetolewa kupitia mradi wa Urasimajishaji Ardhi Vijijini (LTA) unaotekelezwa kupitia  mpango wa Kupunguza Njaa na Utapiamlo (Feed The Future) kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID).

“Leo tumeshuhudia makabila mbalimbali, wakiwemo ndugu zetu wamasai na wamang’ati wakipata ardhi katika ardhi ya wahehe. Hii ndio Tanzania, haina ubaguzi, mtu yoyote ana uwezo wa kufanya shughuli yoyote ya kimaendeleo mahali popote ili mradi havunji sheria,” alisema.

Alisema watanzania hawatarajii tena kusikia ugomvi baina ya wakulima na wafugaji katika kijiji hicho kwani mradi huo umeyawezesha makundi hayo kumiliki ardhi watakayoitumia kwa maendeleo yao endelevu katika jamii.

Mmoja wa wafugaji wa kabila la wamasai aliyemilikishwa ardhi katika kijiji hicho, Liwau Shang’ali aliwashukuru wenyeji wa kijiji hicho kwa kuikaribisha familia yake kijijini hapo akisema; “kama isingekuwa hivyo nisingewe kupata na kumiliki kisheria zaidi ya ekari saba za ardhi.”

Baada ya kupata shamba hilo, alisema hatarajii  kuepeleka mifugo yake kwenye mashamba ya watu wengine kwa kuwa shamba alilonalo linaweza kukidhi mahitaji ya mifugo yake kama ataliendeleza na kufuga kisasa baada ya kupata elimu.

Pamoja na kupata kipande hicho cha ardhi aliishukuru serikali ya kijiji kwa kupitia mradi huo kutenga eneo kubwa la malisho kwa ajili ya wafugaji akisema uamuzi huo unaongeza usalama wa mifugo yao, utalinda mashamba ya wakulima na hatimaye kukuza amani na ushirikiano miongoni mwao.

Awali Mkurugenzi wa LTA, Tressan Sulivan alisema mpango wa matumizi bora ya ardhi na upimaji ardhi una manufaa makubwa katika kupunguza umasikini na njaa katika jamii hasa za vijijini.

Alisema wakulima, wafugaji, wafanyabiashara, wanawake na wanaume wana haki ya kupata, kutumia, kumiliki na kugawa ardhi ili mradi wafuate sheria na taratibu zilizowekwa.

Sullivan alisema kwa kupitia mradi huo uelewa wa haki za wanawake na jamii katika kumiliki ardhi umeongezeka na umesaidia kuwahamasisha kutumia nafasi waliyopewa kuomba ardhi ambayo ni rasilimali muhimu katika kukuza kipato chao.

Katika kijiji hicho alisema mradi uliwezesha uandaaji wa mpango wa matumizi bora ya ardhi na kukarabati masijala ya ardhi na kutoa mafunzo juu ya haki za ardhi na matumizi ya rasilimali ardhi kiuzalishaji ili kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Alisema waliopata hatimiliki za kimila wanaweza pia kuzitumia kama dhamana mahakamani na katika taasisi za fedha kupata mikopo itakayowawezesha kushughulikia changamoto walizonazo.

Alisema jumla ya vijiji 36 kati ya vijiji 133 vya wilaya hiyo vimenufaika na mradi huo ulioanza kutekelezwa mwaka 2015 na ambao utakamilika mwakani, 2019.

Mmoja wa wanawake walionufaika na mpango huo, Sakina Mlelwa alisema wanafurahi kuona mila na desturi zilizokuwa zikiwanyima haki ya kumiliki ardhi katika jamii zao zinapoteza nguvu zake mbele ya sheria mbalimbali za ardhi. 

“Tumeelimishwa jinsi sheria hizo zinavyoondoa tofauti za umiliki wa ardhi baina ya mwanamke na mwanaume, jamii inajua na imeanza kuuona umuhimu wa mwanamke kutobaguliwa katika umiliki wa ardhi,” Mlelwa alisema.

Alisema tatumia kipande chake cha ardhi chenye ukubwa wa heka tatu kutafuta mikopo atakayoitumia kuwekeza katika shughuli za kilimo na ufugaji.

Rudisha heshima yako Kwa Mpenzi Wako, Mke Wako...Tumia Tiba Hii ya Asili

$
0
0
Rudisha heshima yako sasa kwa kutumia Dawa hii iitwayo SUPER GAFINA, kwa ajili ya nguvu za kiume na NKOLOMIJE ni kwaajili ya kuongeza maumbile.

Kwa mwanaume aliye kamilika anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara mbili ,ila ukiwa unapiga moja tena kwa shida wewe ujue  unamatatizo ya upungufu wa nguvu za kiume.

TIBA YA TATIZO LAKO NI; Dawa iitwayo SUPER GAFINA, dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge na unga wa asili ambavyo havina madhara kwa mtumiaji ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja;-

1).itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuchoka.

2).ltakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15 hadi 20 kwa tendo la kwanza.

3).lnaimarisha uume uliolegea na uliosinyaa na kuupa nguvu maradufu.

Je unamaumbile madogo pamoja na uume mfupi? NKOLOMIJE ni suluisho la tatizo lako. Na ni dawa inayoboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi kuanzia inch. 5 hadi 8 kwa muda mfupi sana .Dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk.30 ukisha tumia guarantee miaka 50  ikishakutibu.

Pia ninatibu;- KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU, MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE ,BP, NK.

IGULYATI, ni dawa ya mvuto wa biashara, kazi,kupandishwa cheo na humfanya mfanyakazi kupendwa na mwajiri wake. Pia humvuta mke,Mme,hawara ,mchumba unae muitaji utampata kwa dk.30 tu na atatulia na kumfunga asitoke nje ya ndoa, Pia natoa Pete za bahati ambazo zimetajirisha wengi.

Pia ipo dawa ya kupunguza matiti,unene ,tumbo,na kitambi ,hupunguza mafuta ,kuondoa makovu,chunusi,michilizi mwilini na kuongeza hipsi, makalio na mguu wa bia nk. 

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR,HOSUTWA .Anapatikana Mbagara

Simu no, 0756241666 na 0672186977.

       Huduma hii utaipata popote ulipo

Tiba Asilia ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Kifaru vidonge asilia hurefusha maumbile ya kiume nchi 6-8 dk 60 garantii mika 30- 40 .itakupa nahamu ya kufanya tendo la ndoa mara 4- 5 bila kuchoka au hamu kuisha, ina imalisha misuri  ya uume  na haina madhara kwa mtuaji

Malelemba; inatibu presha kisukari, ngili, busha bila uperesheni, kiuno, kutopata choo vizuri, vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto, kisosono

Jirumba; kumvuta mume mke mpenzi mchumba kwa masaa 3 yoyote unae mtaka  uta mpata ..acha kuumiza roho bure hatakama una fanya nae kazi sehemu moja ila unaogopa kumuanza au muone mzee jirumba atakusaidia

Fika mbagara kwa wa mikoani shinyanga kahama mwanza kwa mawasiano piga 0713560943 /0762540447 dr jirumba

Utomvu Wa Kunenepesha Na Kurefusha Maumbile Ya Kiume Yaliyosinyaa Kisa Kujichua

$
0
0
Je una maumbile ya kiume yaliyo sinyaa na kunywea kwa sababu ya kufanya punyeto kwa muda mrefu? Umejaribu tiba mbalimbali bila mafanikio?

Unataka kupata tiba ya uhakika ya tatizo lako ?
Kama jibu lako  ni NDIO basi HII NI HABARI NJEMA SANA KWAKO.

Neema Herbalist ni wauzaji wa DAWA mbalimbali za.asili.

Tunapenda kuwataarifu wateja wetu kwamba tunao utomvu wa asili ambao unasaidia kunenepesha na kurefusha maumbile ya kiume yaliyo sinyaa kwa sababu ya kufanya punyeto kwa muda mrefu.

Utomvu huu wa asili ambao unatumika kwa kunywa unasaidia kunenepesha na kurefusha maumbile ya kiume yaliyo sinyaa kwa punyeto ndani ya siku thelathini.

Mbali na kusaidia katika kunenepesha na kurefusha maumbile ya kiume yaliyo sinyaa kwa sababu ya punyeto utomvu huu pia unasaidia kuwatibu wanawaume wenye tatizo la kutoa mbegu chache .

Vile vile utomvu huu unasaidia pia KUONGEZA uteute kwenye joints mbalimbali mwilini.

Kupata tiba hii fika katika duka letu lililopo UBUNGO jijini DAR ES SALAAM jirani na SHULE YA MSINGI UBUNGO NATIONAL HOUSING nyuma ya jengo la UBUNGO PLAZA.

WASILIANA NASI KUPITIA SIMU NAMBA 0693 005 189.

NA KWA TAARIFA ZAIDI KUHUSU HUDUMA ZETU TUTEMBELEE KUPITIA BLOGU YETU:


CHADEMA yapata pigo Jijini Mbeya

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Mbeya Mjini, kimepata pigo baada ya Katibu wake, Raphael Mwaitege, kutangaza kujivua nyadhifa zake zote ndani ya chama hicho pamoja na uwanachama akidai kuwa anataka kupumzika siasa.
 
Akizungumza na wandishi wa habari jijini humo, Mwaitege amesema kuwa amefikia uamuzi huo ili kuokoa maisha yake kutokana na vitisho alivyokuwa anavipata kutoka kwa wanachama wenzake wa chama hicho ambao walikuwa wanamtishia maisha.

Naye Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Mbeya Mjini, Agustino Mwadalu amesema chama hicho kiko tayari kumpokea mwanachama yeyote wa upinzani ambaye ni msafi na anataka kuhamia katika chama hicho kwa ajili ya maendeleo.

"Ninamkaribisha ndugu yangu Katibu wa Chama wa CHADEMA, awe huru, aje kwenye chama ambacho kina sera, chama ambacho kina upendo na kwenye chama ambacho kimechukua dhamana ya kuwaongoza Watanzania, chama kinachoishi na Watanzania na kinachoongoza kwa m,ujibu wa sheria", amesema Katibu huyo wa CCM.

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Lugola atengua uteuzi wa Makamanda wa Polisi katika mikoa 3

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ametengua uteuzi wa Makamanda wa Polisi katika mikoa 3 ya kipolisi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo makamanda hao kushindwa kutekeleza majukumu yao.

Waziri Kangi Lugola ametoa uamuzi huo akiwa Jijini Dodoma, ambapo ametengua uteuzi wa makamanda wa polisi wa mikoa mitatu akiwemo Salum Hamduni aliyekuwa Ilala, kwa kosa la kushindwa kusimamia mianya ya rushwa na utoaji wa dhamana kwa watuhumiwa.

Kamanda mwingine aliyetenguliwa kwenye nafasi yake ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Emmanuel Lukula ambaye naye ametenguliwa kwa makosa hayo ya kushindwa kusimamia mianya ya rushwa na utoaji wa dhamana.

Akitangaza uamuzi huo mbele ya waandishi wa habari, Waziri Lugola ameeleza pia kumtengua kwenye nafasi yake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng'azi.

Aidha Waziri huyo amemtaka Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Fortunatus Muslimu kujitafakari na kujipima kama anatosha katika nafasi hiyo.

Bunge Lasitisha Kufanya Kazi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)

$
0
0
Spika wa Bunge Job Ndugai, amesema kwa sasa Bunge limesitisha kufanya kazi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad.

Kutokana na hali hiyo, amewatawanya wajumbe wa Kamati za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC) na ile ya Hesabu za Serikali za Tawala za Mikoa na Mitaa (LAAC) kufanya kazi katika kamati nyingine.

Hatua ya usitishaji huo inatokana na kauli ya Profesa Assad aliyoitoa Desemba mwaka jana katika mahojiano na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa, Arnold Kayanda.

Mtangazaji huyo alimuuliza CAG kuwa ni vipi ofisi yake imekuwa ikijitahidi kila mwaka kufanya ukaguzi na kutoa ripoti zenye kuonesha kuna ubadhirifu, lakini baada ya hapo wananchi hawaoni kinachoendelea.

Katika majibu yake CAG alisema; “Hilo ni jambo ambalo kimsingi ni kazi ya Bunge. Kama tunatoa ripoti zinazoonyesha kuna ubadhirifu halafu hatua hazichukuliwi, huo kwangu ni udhaifu wa Bunge.

“Bunge linatakiwa kusimamia na kuhakikisha pale panapoonekana kuna matatizo basi hatua zinachukuliwa.

 “Sisi kazi yetu ni kutoa ripoti. Na huu udhaifu nafikiri ni jambo lenye kusikitisha. Lakini ni jambo ambalo muda si mrefu huenda litarekebishika, ni tatizo kubwa ambalo tunahisi Bunge linashindwa kufanya kazi yake kama inavyotakiwa.”

Spika Ndugai jana alisema suala hilo si la utani kama baadhi ya wanasiasa wanavyolichukulia.

“Hili jambo sio la utani utani kama hao kina Zitto (Mbunge wa Kigoma Mjini) wanacheza huko Dar es Salaam, sisi hili jambo lililotokea limetusikitisha sana kiukweli.

“Huwezi kutuita sisi dhaifu halafu wewe ni mtu unatakiwa kufanya kazi na sisi.

“Sisi hatutegemei utuite dhaifu yaani kama mazezeta, hiyo ni kuonyesha kwamba si kwamba tumevunja hizo kamati. Ila kwa sasa tumesitisha kazi ya hizo kamati kwa muda. Kwa hiyo wabunge kama wabunge watafanya kazi kupitia kamati nyingine.

“Tumesitisha kwa muda ili hili jambo la huyu ambaye ni mshirika wetu (CAG Profesa Assad) katika kufanya kazi, kwanza afike mbele ya Kamati ya Bunge aeleze kama sisi ni wadhaifu ama laa. Vinginevyo hatuna haja ya kufanya naye kazi ili atafute hao ambao ni ‘strong’ (wenye nguvu) afanye nao kazi.

“Yaani hili si suala la magazeti kama mnavyoandika ushabiki, hatuwezi kujenga nchi ya watu wa kudharaulianauliana, ‘no’ (hapana), haiwezekani.

“Haiwezekani watu mnafanya kazi zenu, watu na heshima zenu mnajitahidi kufanya mnavyoweza, lakini kwa hili acha aje kwanza tumsikilize nini atajibu kwenye kamati, na majibu yake ndani ya kamati mapendekezo yao tutayatoa kwa umma.

“Na kuhusu kamati, ningependa kwanza tubakie huko   maana hili sasa tayari lipo kwenye Kamati ya Maadili, sipendi sana kulirudiarudia, tunataka afike tarehe 21 (Januari) na baada ya hapo mapendekezo yao tutayatoa ‘public’ (kwa umma).

“Kiuweli kuhusu hili la kamati za Bunge tumesitisha kwa sasa shughuli za kamati hizo mbili (PAC na LAAC) mpaka jambo hili litakapokaa vizuri,” alisema Spika Ndugai.

Credit: Mtanzania

Lugola Aunda Kamati Ya Kuchunga Malalamiko Ya Rushwa Kwa Polisi Wa Usalama Barabarani

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola amemuagiza katibu mkuu wa wizara hiyo aunde kamati ya kuchunguza vitendo na mianya ya rushwa kwa jeshi la polisi na msisitizo mkubwa kwenye kitengo cha usalama wa barabarani.

Akizungumza leo Jumatano Januari 16 2019, Lugola pia amemtaka kamanda wa kikosi cha usalama wa barabarani kujitafakari, kujipima kama anatosha katika nafasi hiyo.

"Nimemwelekeza katibu mkuu aunde timu ambayo itapewa miezi mitatu kuchunguza vitendo na mianya ya rushwa na msisitizo mkubwa kwenye usalama wa barabarani na tume hiyo itanipa hatua za kuchukua," amesema.

Amesema kumekuwa na malalamiko mengi yanayohusu ubambikiaji wa makosa ya barabarani kwa madhumuni ya kutaka rushwa na unyanyasaji wa madereva bodaboda.

Ameongeza kwamba licha ya kuwapo makamanda wa trafiki wa mikoa lakini bado kumekuwa na malalamiko juu ya utendaji  wa polisi na hivyo ameamua kuchukua hatua dhidi ya vitendo hivyo.

Amesema tume itachunguza kitengo hicho na kumpelekea majibu ili aweze kuchukua hatua.

Ndege za ATCL Zatafutiwa Fursa ya Kusafirisha Samaki

$
0
0
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe ameanza kutafuta fursa za ndege za Serikali ambazo zimekodishwa kwa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kwa kufanya ziara katika viwanda vya uzalishaji mabondo na kuchakata minofu ya samaki jijini Mwanza.

Akizungumza baada ya kufika ofisi za kanda rasilimali za uvuvi jijini hapa leo Jumanne Januari 15, 2019, Waziri Kamwelwe amesema lengo la ziara yake ya siku moja ni kuangalia mzigo unaozalishwa na viwanda hivyo ili kuandaa mazingira mazuri kwa ajili ya kusafirisha bidhaa hizo nje ya nchi kupitia usafiri wa anga kwa kutumia shirika la ndege la ATCL.

"Juzi tarehe 12 Waziri Luhaga Mpina (mifugo na uvuvi) alinipigia simu akanieleza kwamba kuna mzigo mkubwa wa minofu na mabondo, hivyo nimekuja kujionea viwanda vilivyopo na uwezo wake wa kuzalisha mzigo,” amesema.

Waziri huyo amesema pia atatamani kuangalia na machinjio ya mbuzi kuona kiwango kinachozalishwa.

Amesema kila baada ya siku saba huwa anatembelea Bandari ya Dar es Salaam ambapo hushushwa makontena 7,000 kutoka nje ya nchi lakini hurudi yakiwa matupu bila mzigo hivyo wanataka kuondoa hali hiyo.

"Baada ya ziara yangu Mwanza nitaenda Kanda ya Mbeya kuangalia uzalishaji wa mbogamboga kisha nitaenda kanda za Arusha na Kilimanjaro kuangalia mashamba ya maua,” amesema.

Naye ofisa mfawidhi rasimali za uvuvi Ziwa Victoria, Didas Mtambalike amesema wameandaa viwanda tisa vinavyozalisha minofu na mabondo atakavyotembelea.

Bodi ya mikopo ya wanafunzi yatangaza utaratibu mpya wa Kulipa Mikopo

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, HESLB imekuja na mfumo mpya wa kielektoniki wa ulipaji madeni ya waliyokuwa wanufaika wa mikopo, ambapo mfumo huo utajulikana kwa jina la 'Goverment Electronic Payment Getway' (GEGP).

Akitagaza mfumo huo, Mkurugenzi wa bodi ya mikopo nchini, Abdulrazack Badru amesema mfumo utarahisisha uwazi wa kwenye ukusanyaji wa fedha hizo, utamfanya mdaiwa kulipa mahali popote alipo pamoja na kutoa fursa ya kuongezeka kwa mapato ya bodi hiyo.

"Tumekamilisha utaratibu mfumo wa serikali wa kukusanya mapato (GEPG), mwajiri na wanufaika watatakiwa kujiunga kwenye mfumo huu mpya wa GEPG ili kulipa madeni wanayodaiwa na serikali," amesema Badru

Aidha amesema, "waajiri ambao watashindwa kulipa madeni ya wafanyakazi ambao walikuwa ni wanufaika, tutawaanzishia operesheni maalumu ya kupitia maofisini kwao ili kuwabaini wasiolipa mikopo ya bodi".

Akifafanua mfumo huo mpya mtaalamu wa GEPG, Baziri Bajunia  amesema, "mfumo huu umekuwa ukitumika sasa hivi na taasisi nyingi ambazo zinafanya malipo kwa taasisi za serikali, ni utaratibu ambao hata taasisi nyingine za kifedha wanautumia".

BREAKING: Rais Magufuli Asitisha Zoezi La Kuondoa Vijiji Na Vitongoji Vilivyopo Ndani Ya Maeneo Ya Hifadhi

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ameagiza kusitishwa mara moja kwa zoezi la kuviondoa vijiji na vitongoji vinavyodaiwa kuwepo katika maeneo ya hifadhi na amewataka viongozi wa wizara zote zinazohusika kukutana ili kubainisha na kuanza mchakato wa kurasimisha maeneo ya vijiji na vitongoji hivyo.

Mhe. Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 15 Januari, 2019 Ikulu Jijini Dar es Salaam alipokutana na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamis Kigwangallah, Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi John Kijazi, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamhanga na Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Bi. Dorothy Mwanyika.

Pamoja na agizo hilo Mhe. Rais Magufuli ametaka viongozi wa wizara husika kubainisha maeneo ya hifadhi za wanyamapori na misitu ambayo hayana wanyamapori ama misitu ili yagawiwe kwa wafugaji na wakulima ambao kwa sasa wanataabika kupata maeneo ya kufugia wanyama na kuzalisha mazao.

Mhe. Rais Magufuli pia ameitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kuangalia upya zoezi la uwekaji wa mipaka ya hifadhi na makazi, na kutumia busara katika uwekaji wa mawe ya mipaka hiyo ili kutowaondoa wananchi katika maeneo ambayo hayana ulazima wa kuwaondoa.

“Mimi sifurahii kuona wafugaji kila mahali wanafukuzwa, kama kuna eneo ambalo tunafikiri lilikuwa hifadhi ya wanyama lakini halitumiki, tutabadilisha sheria, tunalimega na tunaligawa kwa wafugaji, vivyo hivyo hata kwa wakulima kama kuna eneo tunaona ni hifadhi lakini halina msitu wala wanyamapori, na lina rutuba, na wakulima wanataka kulima nalo tunalimega tunawapa wakulima.

Baadaye tutajua kabisa eneo hili ni la hifadhi, hili ni la mifugo, hili ni la wakulima, hili ni la makazi. Kwa hiyo nyinyi Mawaziri na Makatibu Wakuu mkakae mkatangulize maslahi ya hawa tunaowaongoza ambao ni wakulima, wafugaji, wavuvi nakadhalika, lakini pia tunahitaji wanyamapori, sijasema sasa hifadhi zote za wanyama tunazimaliza, hapana, hifadhi za wanyama lazima tuzihifadhi” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli ameagiza vijiji vyote 366 vilivyoainishwa kuwepo ndani ya maeneo ya hifadhi hapa nchini visiondolewe katika maeneo hayo na badala yake ametoa mwezi mmoja kwa viongozi wa wizara zote zinazohusika kubainisha maeneo ya vijiji hivyo na kuanzisha mchakato wa mabadiliko ya sheria ili yawasilishwe katika kikao kijacho cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amefafanua kuwa ni lazima Serikali ifanye maamuzi haya sasa kwa kuwa idadi ya Watanzania imeongezeka hadi kufikia Milioni 55, idadi ya mifugo imeongeza hadi kufikia Milioni 35 na hivyo kuna ongezeko kubwa la mahitaji ya maeneo ya ardhi ikilinganishwa na wakati nchi inapata uhuru ambapo Watanzania walikuwa Milioni 9 na mifugo ilikuwa Milioni 10.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameagiza sheria ya vyanzo vya maji pia iangaliwe upya ili kutowazuia Watanzania wanaozalisha mazao kandokando mwa mito na ameelezea kutofurahishwa kwake na vitendo vya kufyeka mazao ya wakulima kwa madai kuwa wamelima ndani ya mita 60.

Halikadhalika Mhe. Rais Magufuli ameipongeza Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuwasilisha kwake mapendekezo ya kufutwa kwa mashamba ambayo hayajaendelezwa na ameagiza wizara hiyo iendelee kumpelekea mapendekezo ya mashamba yote yaliyotelekezwa ili ayafute na wananchi wagawiwe kwa ajili ya kuyatumia kwa uzalishaji wa mazao na mifugo.

Hata hivyo Mhe. Rais Magufuli amesema maagizo hayo hayana maana kuwa sasa wananchi waruhusiwe kuvamia maeneo ya hifadhi, na ametaka zoezi la uwekaji wa mipaka lifanyike haraka na kwa uwazi.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
15 Januari, 2019 .a

Mtoto Wa Tembo Aliyetumbukia Shimoni Aokolewa Pori La Akiba Lwafi

$
0
0
Mamlaka ya Usimamizi wanyamapori Tanzania, inapenda kuwataarifu wananchi wote kuwa mnamo tarehe 11/01/2019 majira ya saa kumi kamili jioni (10:00) Ungozi wa Pori la Akiba Lwafi Mkoani Katavi walipokea taarifa kutoka kwa Bw.Salum Summy ambaye ni  mmiliki wa shamba la Msipazi linalopakana na pori hilo kuhusu kunasa kwa mtoto wa tembo kwenye tope  aliyetumbukia ndani ya chimo eneo la china ndani ya pori hilo.

Bw. Salum alipata taarifa hizo kutoka kwa wafanyakazi wake waliyokuwa jirani baada ya kusikia tembo wakipiga kelele kwa sauti zaidi ya saa moja, na baada ya kufuatilia wakaona kundi kubwa la tembo wakijitahidi kumtoa mtoto wao kwenye shimo. Kwa vile tembo walikuwa wengi watu hao hawakuweza kuwasogelea, hivyo waliamua kuwasiliana na uongozi wa Pori la Lwafi kuhusu tukio hilo . Waliwasiliana na  Mkuu wa Kanda ya Lwafi Bw. Asubuhi T. Kasunga,na kumueleza taarifa hiyo, Bw. Asubuhi bila kuchelewa aliondoka akiongozana na askari  4 wakiwa na siraha na mahema kuelekea eneo la tukio, walifika majira ya saa 5:00 usiku na kupata taarifa ya awali toka kwa mashuhuda  wa tukio hilo,

 Kwa vile ilikuwa usiku sana  na kuhofia kuwepo kwa tembo wengine jirani  walisubiri hadi kupambazuke hadi tarehe 12/1/2019 majira ya saa 12:00 asubuhi walifuatana na wafanyakazi wa shamba pamoja na  wanakijiji jumla walikuwa 11 walifika  eneo la tukio na kumkuta mtoto wa tembo mwenye umri chini ya wa mwaka mmoja  akiangaika kutoka shimoni. Jitihada za kumuokoa zilifanyika baada ya kupanga mawe ndani ya shimo bila kumdhuru mtoto,na hatimaye walimtoa mtoto.

Baada ya kumtoa walimpelea hadi kambi ya Shamba la Msipazi. Waliwahoji wafanyakazi kujua  tembo wanaonekana muda gani kusudi waweze kumrudisha mtoto kwenye kundi, walidai kawaida wanapita majira ya saa nne usiku walisubiri siku nzima hadi muda huo lakini  hawakuonekana.  Tembo hao.

Muda wote  walikuwa wakiwasiliana na Dakitari wa tiba za wanyamapori toka Shirika la Uhifadhi liitwalo (Wildlife Conservation Society-WCS) Bi. Elizabert Stigmaier  kutoa ushauri wa chakula cha kumlisha mtoto huyo maana alionekana amechoka. Wakaelezwa wampatie Glucose aina ya DNS na aliwaeleza jinsi ya kumpa ilia pate nguvu.

Tarehe 13/1/2019  Ofisi yangu iliwasiliana na wataalamu wa Taasisi ya Utafiti wa wanyamapori (TAWIRI ). Idara ya wanyamapori,na WCS na kufikia uamuzi wa  tumsafirishe kwa ndege ya kampuni ya Northen Air Transport No. 5G-DEB  ambayo ilitolewa na Rusell Hastings wa Shirika la Uhifadhi liitwalo ‘ Freidkin Conservation’ hadi Arusha majira ya saa 10: 00 jioni na kupelekwa kwenye kituo cha kupokea Wanyamapori yatima kiitwacho ‘ Makoa farm Vertinary Clinic’ iliyopo Machame Wilaya ya Hai.Mtoto huyo wa tembo anaendelea vizuri.

LIMETOLEWA NA
Dkt. JAMES WAKIBARA  (KAMISHNA MHIFADHI-TAWA)

Mahakama ya ICC Yamwachia huru Gbagbo

$
0
0
Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC), imemwachia huru rais wa zamani wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo, baada ya upande wa mashitaka kushindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yake.

Gbagbo alifikishwa mbele ya mahakama hiyo mwaka 2011 kutokana na vurugu za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ambao ulishuhudia akishindwa mbele ya mpinzani wake, Alassane Ouattara.

Katika uamuzi wao, majaji wa ICC, waliamuru Rais Gbagbo kuachiwa huru kwa kuwa upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha shitaka hata moja kati ya yale aliyoshitakiwa mbele ya mahakama hiyo.
Gbagbo alishitakiwa kwa madai ya kuhusika na vurugu zilizosababisha mauaji ya watu 3,000 huku wengine 500,000 wakiyakimbia makazi yao.

Kwa mujibu wa rekodi za ICC, Gbagbo ni kiongozi mkuu wa kwanza wa zamani wa nchi kupandishwa mbele ya mahakama hiyo. Kukamatwa kwake kulitekelezwa na vikosi vilivyokuwa vikiungwa mkono na Umoja wa Mataifa (UN) na Ufaransa.

Mbali na Gbagbo, mke wake Simone Gbagbo, naye alitiwa hatiani na mahakama za nchi hiyo kwa kuhusika na makossa mbalimbali ikiwemo kuratibu makundi ya ujambazi.

Serikali ya Ivory Coast ilikataa kumkabidhi Simone kwa ICC ikisema itamshitaki na kumhukumu katika mahakama za ndani.

Alihukumiwa kutumikia kifungo cha miaka 20 jela baada ya kutiwa hatiani kwa makossa mbalimbali ikiwamo ya uvunjifu wa sheria za nchi, kuvuruga usalama wa nchi na makossa dhidi ya ubinadamu.
Simone alinufaika na msamaha wa Rais Ouattara mwaka jana ambaye alisema ameamua kumsamehe ili kufungua milango ya majadiliano na maridhiano kwa mustakbali wa taifa hilo linaloongoza kwa kilimo cha kakao duniani.

Maafisa watano wa TFDA kizimbani kwa tuhuma za kuisababishia Mamlaka hiyo hasara ya sh. milioni 58

$
0
0
Maofisa wanne wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) wamepandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na shtaka moja la kusababisha hasara ya Sh58,390,000 kwa kuidhinisha malipo mara mbili kwa wafanyakazi wa mamlaka hiyo.

Waliosomewa hati ya mashtaka ni Raymond Wigenge, Ezekiel Mubito, Adelard Mtenga, Abdalah Juma na mshtakiwa wa kwanza, Chary Ugullum ambaye hata hivyo hajafikishwa mahakamani.

Akisoma hati ya mashtaka Wakili wa Takukuru, Leonard Swai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustino Rwezile alidai kuwa washtakiwa kwa pamoja wanashtakiwa katika kesi ya uhujumu uchumi.

Wakili Swai alidai kuwa kati ya Mei na Desemba mwaka 2016 washtakiwa hao wakiwa katika ofisi ya TFDA kwa uzembe waliisababishia hasara ya kiasi cha Sh58,390,000 kwa kuidhinisha posho maalumu kwa wafanyakazi ambao walishalipwa na kufanya walipwe mara mbili jambo ambalo ni kosa la kisheria.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo washtakiwa walikana shtaka hilo na upande wa Jamhuri walidai kuwa upelelezi umekamilika na waliomba mahakama hiyo ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kuwasomea hoja za awali.

Hakimu Mkazi Mwandamizi, Rwezile alisema dhamana kwa washtakiwa hao ipo wazi hivyo wanatakiwa wadhamini wawili wawe na kitambulisho cha Taifa (Nida) na barua za utambulisho.

Pia kati yao mmoja awasilishe fedha taslimu Sh5.8 milioni au hati yenye thamani ya Sh5.8 milioni.

Hata hivyo washtakiwa walishindwa kutimiza masharti ya dhamana hivyo wote wamerudishwa mahabusu.

Hakimu Rwezile aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 28, 2019 itakapokuja kwa ajili ya kusikiliza hoja za awali.

Naibu Waziri Masauni Ayaonya Makampuni Binafsi Ya Ulinzi Kujihusisha Na Uhalifu

$
0
0
Serikali imeziasa Kampuni Binafsi za Ulinzi kutoshiriki katika matukio ya uhalifu baada ya kuripotiwa mara kwa mara kwa walinzi wa kampuni hizo kupatikana na hatia ya uhalifu katika mahala pao pa kazi ikiwemo kuwaazima silaha wahalifu kwenda kufanya matukio ya uhalifu.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu wa Chama cha Sekta ya Ulinzi Tanzania (TSIA), uliofanyika leo jijini Dodoma.

Amesema kampuni zinatakiwa kuongea na walinzi wao sambamba na kuongeza maslahi kwa walinzi hao ili wasiingie katika vishawishi hali itakayopelekea kutoshiriki katika matukio ya uhalifu sehemu zao za kazi.

“Baadhi ya walinzi wa kampuni mnazozisimamia wamekua wakishiriki katika uhalifu, wengine wameenda mbali zaidi kwa kuwaazima silaha wahalifu kwenda kufanyia uhalifu, jambo hili halikubaliki, sasa naziagiza kampuni zenye walinzi wa namna hii kuhakikisha vitendo hivi vinakoma mara moja,” alisema Masauni

Akizungumza kwa niaba ya Jeshi la Polisi, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Narcis Misama alisema wao kama jeshi wanawahakikishia wanachama hao wa sekta ya ulinzi ushirikiano utakaowasaidia kutimiza majukumu yao huku akiweka wazi jeshi kama jeshi haliwezi kuyafikia maeneo yote kwa wakati

“Nawashukuru sana kwani mmekua msaada muhimu kwa jeshi la polisi hasa pale uhalifu unapotokea maeneo mnayolinda, tumeweza kuwapata watuhumiwa wa matukio mbalimbali kupitia taarifa zenu pindi tu uhalifu unapotokea, nawaahidi ushirikiano kwa siku zijazo  zaidi ya mnaoupata kutoka kwa jeshi,” alisema SACP Misama

Akizungumza kwa niaba ya wanachama Mwenyekiti wa Chama cha Sekta ya Ulinzi Tanzania, Felix Kagisa aliiomba serikali ipitishe sharia zinazoongoza sekta ya ulinzi binafsi ili waweze kufanya kazi zao kwa mujibu wa sheria na taratibu  za nchi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images