Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ajali ya Hiace Yaua Watu Wawili

$
0
0
Watu  wawili wamefariki dunia papo hapo baada ya gari aina ya Totota Hiace walilokuwa wamepanda kuacha njia na kupinduka.

Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa, George Kyando, alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi majira ya alasiri. Aliwataja watu waliofariki katika ajali hiyo ni Augenia Masumbuko (53) mkazi wa Isale, na Nestory Kayumba mkazi wa Kalambo.

Kamanda huyo alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni dereva aliyekuwa akiendesha gari lenye namba za usajili T 795 CVA aina ya Toyota Hiace kushindwa kulimudu katika mteremko, hivyo kuacha njia na kupinduka.

Katika ajali hiyo watu wawili pia walijeruhiwa ambao ni Akoba Kung'ombe (40) mkazi wa Bangwe na mwingine ambaye hajafahamika ambaye ni mwanaume mwenye umri kati ya miaka 25-30.

Kamanda Kyando alisema miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika kituo cha afya Namanyere, na majeruhi wamelazwa katika Zahanati ya Myula kwa ajili ya matibabu.

Kwa mujibu wa Kamanda Kyando, dereva wa gari hilo alikimbia baada ya ajali hiyo na kwamba Jeshi la Polisi linaendelea kumsaka ili afikishwe mahakamani.

Aliwaasa madereva mkoani humo kwa makini wawapo barabarani na kufuata sheria za usalama barabarani, ili kuepuka vifo na majeruhi kutokana na ajali zinazoweza kuepukika.

Waitara Azipiga Marufuku Shule binafsi kufukuza wanafunzi wasiolipa ada

$
0
0
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mwita Waitara amepiga marufuku wanafunzi wa shule binafsi ambao hawajamaliza ada kusimamishwa au kufukuzwa shule.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Alhamisi Januari 10, 2019, jijini Dar es Salaam, Waitara amesema kuanzia kesho Ijumaa ataanza kupokea taarifa kutoka kwa katibu tawala wa mikoa, wakurugenzi wa halmashauri na wadhibiti ubora wa shule ambazo zimewafukuza au kuwarudisha wanafunzi.

Amesema ni marufuku mwanafunzi kusimamishwa au kufukuzwa shule kwa sababu ya kutolipa ada bila kujali anasoma shule ya umma au binafsi.

Waitara amesema jambo jingine ambalo Serikali haikubaliani nalo ni la wazazi kulazimishwa kulipa ada kwa mkupuo na iwapo hawajafanya hivyo wanafunzi hawataendelea na masomo hata kama mwaka uliopita walifanya hivyo.

"Nina sms (ujumbe mfupi wa maandishi) nilizotumiwa na wazazi wa shule ambazo zimerudisha wanafunzi nyumbani kwa kukosa ada na malipo mengine ya kiholela kama vile kulazimishwa kununua sare za shule shuleni, for figer, rim na madaftari ya ganda gumu (counter book),” amesema Waitara.

“Nataka maofisa elimu, wakurugenzi na makatibu tarafa kwenda kwenye hizi shule (anazitaja shule) hadi kufikia kesho niwe na majibu yanayoonyesha kupatikana ufumbuzi."

Waitara pia amewataka wazazi ambao watoto wao wamerudishwa kwa ajili ya kutolipa au kukamilisha ada wafike kwenye ofisi alizozitaja au Tamisemi kwa ajili ya kupatiwa  ufumbuzi.

Uongozi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Wajibu Tuhuma za Msanii Ray Kigosi Kuibiwa Vitu Vyake

$
0
0
Uongozi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) umewataka abiria wanaodhani wamepoteza vitu vyao wakati wanasafiri kwa kutumia Uwanja huo watoe taarifa mapema ili waweze kusaidiwa kupata vitu vilivyopotea.

Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Paul Rwegasha amesema iwapo mtu atapata tatizo lolote ni vyema akawasiliana na uongozi badala ya kuandika kwenye mitandao ya kijamii kwani atakuwa anaichafua nchi.

Rwegasha amelazimika kutoa ufafanuzi huo baada  Msanii Maarufu wa Filamu nchini, Vincent Kigosi ‘Ray’ kuandika kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram akieleza aliibiwa vifaa vyake akiwa anaelekea Dubai.

“Wiki iliyopita mliniibia raba pamoja na pafyumu ( mafuta ya manukato), sasa swali langu? Kwa nini uongozi hauwachukulii hatua kali hao wafanyakazi wenu wenye tabia ya udokozi wanaoharibu sifa ya uwanja wa ndege huu wa kimataifa?” Aliandika Ray Kigosi

Mmoja wa wachangiaji ambaye ni msanii mwenzake mwenye jina la @Gabozingamba aliandika ;“Wakati tunakwenda Kigali (Rwanda) nilikuambia wameniibia laptop (kompyuta mpakato) na manukato wamezuia ukaniambia tulia dogo ndiyo ukubwa. Basi na wewe utulie kaka ndiyo uzee huo kumradhi.”

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Dr Hindu: Bingwa Wa Tiba Asili .....Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR HINDU popote ulipo . Muone  DR HINDU,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46. Dar es salaam, Mbagala Tanzania. ,..Dr. HINDU 0744,92,29,82 / 0716608959...You are welcome. Yuko pia Khahama Mjini

Huna Sababu ya Kuabika Tena, Jipatie Dawa Bora ya Nguvu za Kiume, Maumbile Madogo na Mvuto wa Mapenzi

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiathiri watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine ....kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapungufu katika mwili wake.

Kuna sababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huathiri misuli ya uume, 


Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0620510598  / 0743543944

Mume wa AMBER RUTTY Adondoka Mahakamani

$
0
0
Msanii na 'video queen' kwenye video za wasanii, Amber Rutty ameeleza sababu iliyopelekea mume wake, Said Mtopali kudondoka ghafla mahakamani kuwa ni kutokana na hali ya kizunguzungu aliyokuwa akijisikia.
 
Amber Rutty amesema kwamba hali ya mume wake haikuwa nzuri tangu walipotoka gereza la Segerea kwa kuwa walikumbwa na maradhi.

Amber Rutty amesema kwamba kwa sasa mume wake ameshapatiwa huduma ya kwanza na tayari amepatiwa 'drip'mbili za maji.

"Hali yake haikuwa nzuri sana tangu tulipotoka magereza. Wote tuliondoka kule na magonjwa, ila yeye alikuwa akiumwa sana. Namshukuru Mungu kwa sasa anaendelea vizuri", amesema Amber Rutty.

Leo Hakimu Mkazi Kisutu, Janeth Mbando ameahirisha kesi inayowakabili wanandoa hao kwa kusambaza video chafu mitandaoni hadi Februari 11, 2019 baada ya Wakili Neema Mbwana kusema upelelezi haujakamilika.

Wanandoa hao wapya ambao wamefunga ndoa wiki iliyopita wamedai baada ya matatizo yao kwisha watafanya sherehe ili kusherehekea ndoa yao.

Zitto amwandikia barua Katibu Mkuu CPA sakata la Spika Ndugai, Profesa Assad

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, amemwandikia barua Katibu Mkuu wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola (CPA) kumtaka kuingilia kati sakata la Spika wa Bunge, Job Ndugai na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Profesa Mussa Assad.

Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya spika Ndugai kumtaka Profesa Assad kwenda mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kinga, Maadili na Madaraka ya Bunge Januari 21, kwa kitendo cha kuliita Bunge kuwa ni dhaifu wakati akihojiwa na Radio ya Umoja wa Mataifa nchini Marekani hivi karibuni, ambapo amesema akishindwa kufika mwenyewe atafuatwa na pingu.

Katika barua hiyo, Zitto pia ametuma nakala kwa maspika wa mabunge yote ya Afrika kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola na Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara (SADC), na Wadhibiti na Wakaguzi Wakuu wa Hesabu za Serikali wote wa Jumuiya ya Madola, kuwataka kuzungumza na Spika Ndugai kuachana na kitendo hatari cha kudidimiza misingi ya uwajibikaji nchini.

“Kwa kuwa Bunge la Tanzania ni mwanachama wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola (CPA), naomba uingilie kati kutatua kidiplomasia kwa kuzungumza na Spika wa Bunge la Tanzania, ukimueleza hatari za uamuzi wake.

“Naamini kuwa suala hilo linaweza kutatuliwa kwa urahisi na kuboresha uhusiano kati ya taasisi hizo mbili muhimu yaani Bunge na Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, ambayo hutegemeana,” imesema sehemu ya barua hiyo ya Zitto.

Ndege Nyingine Mpya ya Serikali aina ya Airbus A220-300 Kutua Nchini Kesho Ijumaa Mchana

$
0
0
Ndege nyingine mpya ya Serikali aina ya Airbus A220-300 iliyopewa jina la Ngorongoro inatarajia kuwasilini nchini kesho Ijumaa mchana, ambapo itafanya idadi ya ndege zilizonunuliwa na Serikali kufikia sita.

Ndege hiyo ambayo tayari inanakshi za Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL)  itafanya jumla ya ndege za ATCL kufikia 7, ikijumlishwa na ndege yao ya zamani aina ya Bombardier Q300 ambayo sasa ipo katika matengenezo.

Ndege inayotarajiwa kutua kesho ni ya pili ya aina hiyo, kwani Desemba 23 iliwasili ya kwanza ambayo ilipewa jina la Dodoma. 

Ndege nyingine zinazomilikiwa na shirika hilo ni Bomberdier Q400-8 tatu na Boeing 87-8 (Dreamliner) moja.

Mke wa Mzee Yussuf aendelea vizuri....Ni Baada ya Kujeruhiwa na Majambazi Usiku

$
0
0
Hali ya mke wa Mzee Yussuf, Leyla Rashid, inaendelea vizuri baada ya kujeruhiwa maeneo mbalimbali ya mwili na majambazi waliovamia nyumbani kwake, Chanika, jijini Dar es Salaam, juzi usiku.

Leyla amesema baada ya kupata majeraha hayo alikimbizwa hospitali na kupatiwa matibabu na sasa ameruhusiwa kurudi nyumbani na hali yake inaendelea vizuri.

“Nashukuru kwa sasa naendelea vizuri nimetoka hospitali nipo nyumbani kwangu Chanika, nimegundua vitu ambavyo nimeibiwa vinafika thamani ya shilingi 5,000,000, nashukuru ndugu na jamaa waliojitokeza wakati wa tukio,” amesema Leyla.

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 48

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   
Biyanka akanijibu kwa heshima zote, kiburi na dharua zote alizo kuwa akinifanyia jana usiku zote zimemuisha. Tukarudi hotelini na Jojo huku tukiwa na furaha kubwa sana kwani mpango wetu umekwenda kama vile tulivyo panga.
“Hongera”
“Nashukuru Jojo, nakushukuru sana kwa kile ulicho nifanyia”
“Usijali, huyu binti amesha nipatia namba yake”
“Waoo sasa muda wa kwenda kuwaangusha maadui zangu hivi sasa umewadia. Umeona jinsi dharau zake zilivyo muisha”
“Yaa sasa kama unafanya kweli kweli mapenzi hakikisha kwamba unafanya kweli na ukimpata hakikisha ana kupenda kupitiliza na akisha kolea hakikisha kwamba una mpa pigo kubwa sana yeye na baba yake naamini kwamba huo ndio utakuwa anguko lao umenielewa”
“Nimekuelewa nanitafahanya hivyo kuhakikisha kwamba ninawaangusha chini yeye na familia yake.”

ENDELEA           
Nilizungumza huku nikiwa nimejawa na tabasamu  pana sana usoni mwangu. Jojo akampigia Dany na kumpa habari hii.
“Camila anahitaji kuzungumza nawe”
“Sawa sawa”
Nikaipoke simu hii na kuingia bafuni.
“Niambie mke wangu”
“Safi ehee niambie ni nini kinacho endelea?”
“Mipango inakwenda vizuri na hadi ninavyo zungumza hivi sasa nimenunua kampuni moja ya simu inaitwa ZAiartel”
“Wooo kweli mume wangu?”
 
“Ndio na kupitia hi kampuni sasa nitaanza kumsogelea adui yangu na nikimtia mikononi basi nitahakikisha kwamba anajutia kwa yale yote ambayo amenifanyia kwenye maisha yangu”
“Sawa mume wangu nina kuamini sana nina imani kwamba huto niangusha”
“Usijali mpenzi wangu nitahakikisha kwamba, tunarudi Ujerumani tukiwa na ushindi mkubwa sana, sawa mama”
“Sawa mume wangu”
 
“Nitakufahamisha kila jambo ambalo litatokea”
“Sawa mume wangu, nakupa muda na uhuru wa kuweza kufanya jambo lolote ili mradi uhakikishe kwamba una fanikisha kile kitu ambacho unakihitaji kukifanya”
“Nashukuru mke wangu”
Tukamaliza kuzungumza na Camila na kukata simu. Jioni ikawadia na Jojo akawasiliana na Biyanka na kumpa maelekezo ya wapi anaweza kutukuta. Tukajianda ana kueleeka katika hoteli nyingine ambayo nayo ina hadhi ya nyota tano. Biyanka akafika katika eneo hili la hoteli akiwa ameongozana na walinzi wake wa kike, nikamkaribisha kwa furaha pasipo kuonyesha kwamab niliweza kuchukizwa na tabia yake ya kunidharau jana jioni.
 
“Pole kwa kuweza kukusumbua”
“Usijali mkuu ni jukumu langu nami nakuomba msamaha kwa yale yote ambayo nilikufanyia jana. Kichwa changu kidogo hakikuwa sawa ndio maana yakatoka yale yaliyo tokea”
“Nimekusamehe, ehee kampuni sasa ipo mikononi mwangu, niambie biashara inakwenda vipi na changamoto ni zipi kwa wafanyakazi walipo hivi sasa?”
“Biashara kwa sasa imeweza kuyumba kidogo kwa nchi yetu ya Tanzania. Uchaguzi kidogo umeyumbisha uchumi, ila nina imani raisi ajaye anaweza kufanya mambo mazuri sana na kusimamisha tena uchumi wa hii nchi”
 
“Ni kweli, japo sipo Tanzania kwa miaka mingi kidogo ila naipenda sana nchi yangu”
“Nafurahi sana kuweza kusika hivyo mkuu”
“Ehee ni nini ambacho natakiwa kuongeza na nini natakiwa kupunguza katika kuhakikisha kwamba ninadumisha kampuni yangu?”
“Kwa haraka haraka mkuu unachotakiwa kukifanya ni kujali maslahi ya wafanyakazi, kwani kwa miezi ya hivi karibuni, kampuni iliweza kupunguza wafanyakazi kutokana na kuyumba. Pili ushindani katika soko, wenzetu wenye mitandao wanajua jinsi ya kupangilia ofa zao. Kupangilia matangazo yao, ila sisi tulishindwa kutokana na kuyumba kiuchumi”
 
“Ohoo sawa hili nitalitazamia kwa jicho la umakini. Ehee jambo jengine?”
“Kitu kingine ni kuwa karibu na serikali, hususani mgombea anaye gombani kiti cha uraisi kwa chama tawala.”
“Ambaye ni baba yako…..”
“Ohoo kumbe umesha mfahamu?”
“Ndio nimemfahamu na mimi ni shabiki yake namba moja na kama atahitaji nimuunge mkono, kwangu haito kuwa shida kabisa nitahakikisha kwamba anashinda kwa kishindo”
“Ohoo asante sana mkuu”
 
“Niite Ethan, mkuu ni Mungu pekee ila sisi wote tusimame kwa majina yetu”
“Sawa sawa”
Biyanka alizungumza kwa furaha kubwa sana huku moyoni mwangu nikijiapiza kwamba furaha hiyo itakuw ani huzuni na mateso makubwa sana kwake pale nitakapo hakikisha kwamba nimemuweka mikononi baba yake aliye nipotezea wazazi  wangu.
“Kesho naomba uitishe kikao na wafanyakazi wote, hata wale wa hali ya chini namaanisha wale wafagizi, nahitaji kuzungumza nao kisha baada ya hapo tutajua nini cha kufanya”
 
“Sawa sawa Ethan”
“Kitu kingine, kumbuka kwamba mimi ni kijana mdogo sana. Hivyo mambo yangu nayapeleka kasi sana. Uvivu na uzembe ni adui mkubwa sana kwangu. Kama atakuwepo mtu mwenye asili  hiyo katika kampuni yangu basi nitahakikisha kwamba ninamtoa mara moja kwenye kazi yangu”
“Usijali bosi kila jambo litakwenda kama vile unavyo hitaji”
“Nafasi yako haito kuwa na mabadiliko yoyote”
“Nashukuru sana Ethan, nitahakikisha kwamba nina ifanya kazi hii kwa uwezo wangu wote hadi pale utakapo nichoka”
“Siwezi kukuchoka”
Nilizungumza huku nikimtazama vizuri Biyanka usoni mwake, ni binti mzuri, anaye jipenda na ana vigezo vyote vya kuitwa mwanamke mzuri, taratibu nikamshika kiganja chake cha mkono wa kulia na kuanza kuupapasa na kidole changu gumba.
 
“Eth…”
“Ohoo samahani”
Nilizungumza huku nikimuachia kiganja chake.
“Hapana ila kidogo nimejawaliwa aibu”
“Hahaa….vipi shemeji anasemaje?”
“Hapana sina mwanaume Ethan”
“Kwa nini?”
“Bado sijamuona mwanaume wa kuwa naye”
“Mmmmm”
“Kweli wanaume wengi ni wadanganyifu na mimi huwa nina linda heshima yangu na usichana wangu”
 
“Hongera sana”
“Ahaa kawaida”
Tukazungumza mambo mengi sana katika usiku huu, hadi majira ya saa tano nikamruhusu Biyanka na akaondoka na walinzi wake. Hatukuona sababu ya kuendelea kuwemo hapa hotelini, tukaanza safari ya kurudi katika hoteli yetu.
“Vipi umefanikiwa?”
Jojo aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.
“Asilimia sabini na tano hizo ishirini na tano nitazimalizia siku kadhaa zijazo”
“Kazi nzuri, ila angalia usije ukamsahau Camila kwa maana nimekuona umejiachia sana kwake”
“Hahaa usijali siwezi kumsahau mpenzi wangu, Camila nimekua naye toka tupo watoto dogo sana”
“Sawa”
                                                                                                          ***
    Alfajiri na mapema tukafika ofisi, nikamkuta Biyanka pamoja na wafanyakazi kadhaa, nikasalimiana nao na Biyanka akaanza kunitembeza kwenye jengo hili zima la kampuni hii niliyo inunua. Hadi inatimu saa mbili asubuhi tukawwa tumemaliza kulitembea jengo hili. Kama nilivyo agiza ndivyo jinsi Biyanka alivyo fanya. Wafanyakazi wote hadi wafagizi wa hii kampuni wakakusanyika katika ukumbi mkubwa wa kampuni hii. 

Biyanka akaanzisha kikao cha kampuni hii huku akinitambulisha kuwa ndio mmiliki mpya wa kampuni hii. Wasaa wa mimi kuzungumza ukawadia, taratibu nikasimama kwenye kiti nilicho kikalia na kusimama eneo lenye kipaza sauti. Nikawatazama wafanyakazi hawa kwa sekunde kadhaa kisha nikatabasamu kidogo.
 
“Habari za asubuhi”
Wafanyakazi wote wakaitikia salamau yangu. Kitu nilicho kigundua kwa haraka juu ya wafanyakazi hawa ni hali  ya woga pamoja na kukatishwa tamaa na kazi ambayo wanaifanya.
“Nashukuru kwa uwepo wenu hapa. Machache ambayo nitahitaji kuyazungumza ni mshikamano, umoja, upendo na kufanya kazi kwa juhudi ndio kitu muhimu katika kuhakikisha kwamba maisha yanu yanakuwa mazuri”
 
“Nitahakikisha kwamba ninapitia mikataba ya kila mfanyakazi mmoja mmoja na wale ambao hawajapewa mikataba nao tutawapa mikataba yao na nitaongeza mshahara ndani ya mwezi ujao.”
Wafanyakazi wote wakapiga makofi huku wakiwa na furaha kubwa sana.
“Napenda kuhakikisha kwamba ndani ya miezi michache kampuni yetu inakuwa ni namba moja kwa mauzo hapa nchini Tanzania, ila mukinipa ushirikiano wenu nina imani kwamba tutafikia malengo hayo ambayo nimewaeleza hivi sasa. Nashukuru sana kwa muda wenu na ninaomba tuendelee na majukumu yetu”
 
Nilipo maliza kuzungumza wafanyakazi wakaanza kuondoka huku wakiwa na furaha kubwa sana, tukaongozana na Biyanka hadi ofisini kwangu.
“Nani ni mkurugenzi wa waajiriwa?”
“Yupo”
“Basi muambie ahakikishe kwamba mikataba ya wafanyakazi wote inapitiwa upya nikiwa ninaidhibitisha au fanya hivi nahitaji mikataba ya wafanyakazi wote ofisini kwangu”
“Sawa Ethan, ila kuna jambo moja ambalo umelizungumza pale na sasa tupo mwanzoni mwa mwenzi je hadi mwenzu ujao kweli litakuwa limekamilika?”
 
“Jambo gani?”
“Juu ya kuwaongezea mishahara wafanyakazi?”
“Usijali nitajua ni jinsi gani nitavyo hakikisha kwamba hili swala linakwenda kwenye mstari na hivi benki muna kiasi gai kama kapuni hivi sasa?”
“Pesa ziliszo acha na mmiliki aliye pita ni milioni mia mbili za Kitanzania”
“Hayo ni mauzo ya muda gani?”
“Sio mauzo ya muda, ni pesa alioyo iacha kwenye kampuni ili mmuliki mwengine atakapo kuja aweze kuziendelezea katika kuendesha kampuni”
 
“Sawa nimekuelewa fanya nilicho kuambia”
“Sawa Ethan”
Biyanka akatoka chumbani humu na kuniacha ofisini kwangu, baada ya dakika kumi, mkurugenzi anaye shuhulika na maswala ya waajiriwa akafika ofisini kwangu akiwa na mikataba ya wafanyakazi wote. Nikamsalimia mwana mama huyu kisha akaanza kunionyesha mikataba ya wafanyakazi wa ngazi za juu ikiwemo wakurugeni wa vitengo vyote.
“Nashukuru mama yangu, niwekee hapo nitaipitia leo”
“Sawa mkuu”
 
“Niite tu Ethan mama yangu”
“Sawa mimi ninaitwa Bi Agatha Kimaro”
“Ahaa nashukuru mama Kimaro”
“Naweza kuzungumza nawe kidogo?”
“Ndio kuwa huru tu mama yangu”
“Hakika nimependa kile ulicho kizungumza, ni ndani ya dakika mbili ila umezungumza vitu vyenye poiti kubwa na nisikufiche, umenipa moyo wa kuitumikia hii kampuni. Naomba maneno yako yasimame mwanangu katika kile kitu ulicho kusuida kufanya juu yetu na Mungu akubariki mwanangu”
 
“Nashukuru sana mama, naamini mutazidi kunisaidia”
“Wala usijali katika hilo mama yangu, nipo pamoja nanyi”
Mama Kimaro akatoka ofisini kwangu. Nikaendelea kupitia taarifa kadhaa za kampuni hii, hadi inafika muda wa wafanyakazi kutoka ofisini hapa sikuweza kumaliza kazi nilizo kusudia kumaliza hapa na kunilazimu kuongeza muda wa ziada katika kuifanya kazi. Nikamruhusu Jojo kurudi hotelini na kumpa maagizo ya kuja kunichukua saa tatu usiku. Mida ya saa moja usiku mlango wa ofisi kwangu ukagongwa, nikamruhusu anaye gonga mlango aweze kuingia ndani.
 
“Ethan kumbe bado hujaondoka?”
Biyanka alizungumza huku akiingia ofisini kwangu. Nikamsindikiza kwa macho hadi kwenye kiti alicho kikalia. Taratibu nikasimama na kuzunguka kwenye meza hii kubwa ya hapa ofisini kwangu, nikakaa juu ya meza huku nikimtazama Biyanka kwa macho makali, taratibu nikamshika kidevu chake kwa kiganja cha mkono wangu wa kulia kisha nikamnyanyua uso wake na tukatazama. Biyanka akasimama taratibu akasimama na mikono yake akaiweka juu ya mapaja yangu huku tukitazamana na midomo yake akianza kuing’ata ng’ata akiashiria kwamba ana haja ya kuhitaji kile nilicho kikusudia kumfanyia na sasa ndege niliye mtega anaanza kuingia kwenye tundu bovu.

==>>ITAENDELEA KESHO

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 180 na 181 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA      
 
“Endeleni kusonga mbelee”
Raisi Sound akili zake wala sijui zipo vipi, kwani alicho kizungumza sikielewi kabisa, nikamtazama Ester sikumpa ishara yoyote.
“Siwaui marubani wako, sasa wewe ndio utawaua kwani mashambulizi sasa hivi yatakuja kwako hapo Washington D.C ulipo, jiandae muheshimiwa raisi”
Viongozi  wote wakaanza minong’ono wengi wakionekana kugopa sana kwa kile kitakacho kwenda kutokea hapo baada ya muda mchache. Ester na wezake ambao kwa sasa ndio wana uwezo wa kuziongoza ndege hizo wakafanya kile nilicho kizungumza, na ndege hizo zikageuzwa badala ya kueleke Pakistani zikaanza kueleke Marekani kwenye mji wa Washington D.C na zikifika hapo nilazima zifanye mashambulizi za kulichangua jengo hilo la serikali alipo raisi Sound na viongozi wengine wote na inchi itakosa kiongozi wa kisiasa kwani nilazima wafe.
   
ENDELEA   
“Kimya”   
Raisi Sound alizungumza na kuwafanya viongozi walio anzisha mijadala kunyamaza mara moja. Raisi akaka kimya huku akinitazama mimi, kichwani mwake anaonekana kwamba ana mawazo mengi sana.
“Meli zao za kivita zipo ngapi zilizo ondoka?”
Nilizungumza huku nikimtazama Ester, jambo lililo zidi kuzua taharudi kwa viongozi hawa wa Marekani, kwa ishara ya vidole Ester akanionyesha ni meli nne.
“Kila ndege itapiga meli moja”
Ester akatingisha kichwa akimaanisha kwamba emenilewa nilicho kizungumza.
“Nimebadilisha mawazo yangu, meli zako zitakwenda kushambuliwa na kuteketea, je mimi na wewe nani ni raisi wa Marekani?”
Viongozi wote wakamgeuki raisi huyu aliye chukua madaraka kwani yeye ndio muhusika anaye paswa kujibu swala ambalo nimemuuliza.
“Mimi ndio raisi wa Marekani”
“Basi amuru  meli zako  zishambulie hizo ndege ambazo zitafika eneo hilo baada ya dakika……”
Nikamgeukia Ester, akaniambia kwa sauti ya chini sana ambayo haisikiki.
“Dakika kumi na tisa kuanzia hivi sasa, kwa hiyo ukihitaji vita hii iishe, kubali kuniomba msamaha kuhusiana na makosa aliyo yafanya raisi aliye pita, kisha usahau kwamba kuna mtu anaitwa Dany”
“Siwezi kumsujudi gaidi tena muafrika, nitahakikisha kwamba ninakuangusha”
“Sawa subiri kitakacho tokea”
Nilizungumza huku nikijilaza taratibu katika kiti hichi cha kuzunguka, nikawatazama marubani hawa wanao jitahidi kadri ya uwezo wao kuongoza ndege zao ila wanashindwa kabisa kwani hata mimi mwenyewe sifahamu Ester na wezake wamefanyaa kitu gani hadi kuwadhibiti hizi ndege. Viongozi hawa wakaanza kujadiliana kuna ni jinsi gani wanaweza kumshawishi raisi aweze kufwata kile nilinicho muambia.
“Dakika tano zimebaki”
Nilizungumza na kuwafanya viongozi baadhi kunitazama, huku wengi wao wakiwa wamejawa na wasiwasi mwingi sana.
“Dakika mbili zimebaki muheshimiwa raisi”
Viongozi wakaonekana kuchoka kwani raisi wa sasa hashauriki.
“Puuuuuuu”
Nilizungumza huku nikiitazama Tv ya namba tato ambayo inaonyesha video hizo jinsi zinavyo anza kufanya mashambulizi kwenye meli hizi kubwa za kivita na wanajeshi waliopo kwenye meli hizo wakajikuta wakishindwa kufanya chochote kwa moja ni ndege za nchi yao na mbili ni ndege ambazo zina uwezo mkubwa wa kivita na tatu shambulizi limetokea kwa kustukiza sana. Mashambulizi yakaendelea zaidi ya dakika kumi na kuziteketeza meli hizo zote za kivita.
“Wanajeshi wako wameteketea na wamekufa kutokana na ubishi wako. Ndege zako ninaziteketeza sasa”
Ester na wezake kazi yao ni kufanya kile nilicho waeleza, ndege moja baada ya nyingine ikalipuka na baada ya muda kidogo mabaki ya ndege hizo zikaangukia kwenye bahari.
“Tutaonana baadaye baada ya kuhakikisha kwamba mke wangu munamuachia”
Nikachukua rimoti na kuzima tv zote, nikawageukia watu walipo humu ofisini, kila mmoja yupo kimya akinisikiliza ni kitu gani ninacho kwenda kukizungumza.
“Vita sasa imeanza, ninacho kihitaji wote humu ni kuhakikisha kwamba kila mmoja anakuwa jasiri katika kila kitu kinacho jitokeza mbele yetu”
“Munaweza kukaa”
Livna alizungunza, Martin na wezake wakaanza kukaa kila mmoja kwenye kiti alichokuwa amekikalia.
“Kwa sasa mtu ambaye tunamgeukia ni K2, kifo cha Lucy siwezi kukiacha kipite bure, ninahitaji watu ambao watakwenda kumteka mtoto wa K2”
“Samahani Dany, labda mtoto wa K2 yupo wapi?”
“Ester unaweza kunitafutia huyo kijana”
“Si yule kibonge?”
Ester aliniuliaza huku akinitazama usoni mwake.
“Ndio”
Livna alimjibu, Ester akaanza kuifanya kazi hiyo.
“Kwa sasa mtoto wa K2 yupo nchini China ambapo ndipo anapo soma kwenye shule moja ya Kung Fu. Inaitwa Shing Ku Fu.”
Ester alizungumza huku akitutazama mimi na Livna.
“China nina watu ambao wanaweza kuifanya hiyo kazi”
“Hao watu wanahisiana na kikundi hichi?”
“Ndio wanahisiana na kikundi hichi”
“Basi ninaomba uwasiliane nao, ninahitaji kumuumiza K2 zaidi ya alivyo muumiza waziri mkuu”
Livna akawasiliana na watu hao  alio sema wanaweza kuifanya hiyo kazi, akawapatia maelekezo na watu hao wakaahidi kwamba wanaweza kuifanya hiyo kazi siku hii hii.
“Baada ya muda gani munaweza kuikamilisha”
Livna alizungumza huku akiwa ameiweka simu yake mezani na watu wote ndani ya hichi chumba tunayasikia mazungumzo ya Livna na msichana huyo.
“Baada ya lisaa moja mkuu nitakupigia ni wapi nipo na mtoto huyo”
“Sawa Sara, kuwa makini na hakikisha kwamba kila kitu kinakwenda sawa”
“Usijali mkuu unafahamu kwamba mimi sifeli kwenye kila kazi unayo nipatia”
“Nakuaminia ndio maana nikakukabidhi wewe”
“Basi usiwe na mashaka”
Livna akakata simu na kuirudisha mfukoni mwake.
“Mtoto wa K2 nina imani kwamba atakuwa amepatiwa ulinzi mmoja mkubwa sana”
Winy alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama Livna.
“Yaaa, ila huyu ni professional killer, ana uwezo mkubwa japo nimempiga ila tupo vizuri sana”
“Hapa tusubirie matokeo”
“Ila inanibidi niende kumpokea, nje ya hii meli kwa mana yeye afahamu ni wapi ninapo jificha”
“Nitakwenda na wewe”
Martin alizungumza na kunitafanya nimtazame.
“Unajiweza Martin kwa maana ni hatari huko tunapo kwenda, dunia nzima inamtamani huyu jamaa na sisi tayari tumesha husishwa katika swala la kumsaidia, sasa je utaweza shuhuli?”
“Nitaweza niamini Livna”
“Sawa, Ester niandalie vijana wawili, baada ya lisaa wawe tayari”
“Sawa mkuu”
“Na wewe Martin ujiandae katika hili tunalo kwenda kulifanya. Logate hakikisha kwamba ulinzi unakiwa juu yetu kila tunapo kwenda muhakikishe kwamba munatulinda”
“Usijali mkuu”
“Dany wewe ndio ninakuacha hapa, nina imani ni mgeni ila una uwezo mkubwa wa uongozi, hakikisha kwamba ulinzi unakuwa imara”
“Usijali, mimi nitaendelea kudili na hawa wajinga”
“Sawa”
Livna akanyanyuka kwenye kiti hichi na kutoka humu chumbani huku akimuita Martin. Winy naye akaondoka humu ndani na nikabaki na Babyanka pamoja na Logate.
“Dany”
“Naam”
“Mtoto wa K2 unahitaji kumfanya kitu gani?”
Babyanka aliniuliza kwa sauti ya upole sana, nikamtazama usoni mwake kwa sekunde kadhaa huku nikiwa natafakari cha kumjibu.
“Nakuomba usimuue”
“Bayanka umekuwaje, mbona una roho ya huruma sana, au umekoka?”
“Hapana sio kuokoa, ninajia Dany hujapata mshauri mzuri mimi ndio mshauri wako kwa sasa”
“Unanishauri pumba muda mwengine, hivi hujawahi kuona picha za familia yangu ehee?”
“Nimesha wahi kuzioana”
“Sasa unacho kihitaji ni nini, unahitaji kumuacha K2 andelee kuishi kwa furaha na asipate machungu kama ninavyo upata mimi?”
“Najua una mamumivu makubwa moyoni mwako. Ila Dany leo umea watu wengi, ingia basi hata likizo ya kuua hawa watu”
“Nisipo waua wao, watania mimi. Kwanza nenda kamtazame Hawa anaendeleaje”
“Sawa”
Babyanka alizungumza huku akishasha pumzi nyingi sana. Akatoka chumbani humu na kuniacha mimi na Logate.
“Huyu dada ni mpole sana hadi sauti yake”
“Huyo alikuwa ni mlnzi mwenzangu”
“Mlinzi kivipi?”
“Tulikuwa tunamlinda raisi aliye pita nchini Tanzania kabla ya K2”
“Kumbe ulikuwa mfanyakazi muaminifu kwa raisi?”
“Ndio, ila alinibadilika na kuniwinda, wakaniuliza familia yangu na mwisho wa siku nikamuaa kubadilika mazima”
“Masikini wee, familia yako wanaitwa nani?”
Nikamtajia Logate jina la mama yangu, akalitafuta kwenye laptop yake, nikamuona akiziba mdomo wake kwa kile alicho kiona.
“Picha ndio hizi?”
Logate alizungumza huku akinigeuzia laptop yake, nikazitazama picha ya mama yangu akiwa amechinhwa kikatili sana, pambeni ya picha hiyo kuna mwanangu wa kike, pamoja na mdogo wangu. Kwa hasira na maumivu niliyo nayo moyoni mwangu, nikajikuta machozi yakinilenga lenga usoni mwangu.
“Ndio hao”
“Masikini jamani pole sana kaka Dany”
“Shukrani”
Livna akaingia humu ndani akiwa amebadilisha nguo, Logate akaigeuzia laptop yake upande wake. Livna naye akatazama picha zilizopo kwenye laptop ya Logate kisha akanitazama usoni mwangu.
“Dany”
Livna alizungumza hukku akikaa pembeni ya kiti kilichopo pembeni yangu, taratibu akanisogelea na kunitazama uosni mwangu.
“Ninakuomba usikumbuke machungu haya, una safari ndefu kwenye maisha yako, ninakuomba uzidi kuwa jasiri”
“Niahidi kitu”
“Zungumza tu”
“Niahidi unarudi na mtoto wa K2 hapa”
“Usijali, hapa ninasubiria simu ya Sara, akinijulisha tu basi nitaondoka hapa na kwenda kumchukua”
“Unamuamini huyo Sara?”
“Sina mashaka naye kabisa, ni mtu ambaye amefanya kazi zangu nyingi kubwa sana”
“Sawa kuwa makini?”
“Usijali mutakuwa munatufwatilia kila tunacho kifanya kupitia hizi tv”
“Poa”
Ester akaingia akiwa na wasichana wawili warefu kiasi, sura zao zote zinafanana ikimaanisha kwamba ni mapacha.
“Hizi ni mashine zangu, ni pacha wapo vizuri kishenzi”
“Sawa”
“Wamefanana kusema kweli, kikubwa kuweni makini nanawahitaji muwee kufanya kitu kikubwa ambacho K2 hato kisahau kwenye maisha yake.”
“Ninatambua uchungu ambao upon aye, nitakuletea unacho kihitaji.”
Simu ya Livna akaita kisha akaitoa kwenye mfuko wa suruali yake.
“Sara”
“Nimefanikiwa mkuu, tuonane wapi?”
“Nipigie imo, nahitaji kumuona huyo mtoto”
“Poa”
Livna akakata simu baada ya muda simu yake ikaita tena, akapokea na kuiweka mbele yake. Nikaitazama video hiyo na nikamuona Sara huyo, ni binti mwenye asili ya kiafrika.
“Kibonge ninaye kwenye gari”
Sara alizungumza huku akionyesha video ya mtoto wa K2 ambaye nilisha wahi kumtibu kipindi nilipo pandikiza virusi vilivyo sababisha watu kuweza kupata mapunye miilini mwao nchini Tanzania.
“Nimemuona, hakikisha kwamba unachukua boti na kukutana kwenye kisiwa tunacho kutana kila siku”
“Sawa mkuu”
“Dany ninaianza safari”
“Unatumia usafiri gani?”
“Boti, ambayo hakuna satelaiti inayo weza kuinasa zaidi ya satelaiti yetu tu”
Martin akaingia huki naye akiwa amevaa nguo za jeshi.
“Martin mlinde Livna”
“Sisi tutamlinda yeye”
Msicha mmoja kati ya hawa mapach alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.
“Sawa”   
Kila mmoja akavaa kifaa maalumu cha mawasiliano, hadi mimi nikavaa ili niweze kuzungumza nao moja kwa moja pale pale wanapokuwa mbali nasi. Livna na watu wake wakaondoka humu ofisini na kutuacha na Ester pamoja na wezake, wakaziwasha Tv hizi na tukaanza kuwaona jinsi wanavyo ianza safari hii, ambayo itawachukua muda. Tukaendelea kuwafwatilia hadi wakafika katika kisiwa walicho panga kukutana, wakasimamisha boti hiyo pembeni, na wakashuka, kisiwa hichi sio kikubwa kwa maana tuna kiona kwa juu. Galfa kisiwa mlipuko mkubwa wa bomu ukatokea katika kisiwa hichi na kutufanya watu wote tuliopo humu ndani kustuka sana na nikajikuta nikisimama, sikuona mtu yoyote zaidi ya moto mwingi unao endelea kuteketeza eneo hili la hichi kisiwa.
“LIVNA LIVNA LIVNAAAAAAAAAAAA………………..”
Niliita kwa sauti ya juu, sikuitikiwa zaidi ya kusikia kimlio kikali sana kilicho tuumiza masikio na kujikuta sote tukivua vifaa hivi vya mawasiliano masikioni mwetu huku mapigo ya moyo yakinienda mbio kwani sijui shambulizi limetokea wapi.
                                                                         
AISIIIII……….U KILL ME 181

 Ukimya ukatawala ndani ya chumba hichi huku kila mtu kiwa na wasiwasi mwingi sana.
“Hembu vuta karibu hiyo video”
Nilizungumza kwa haraka huku nikimtazama Ester usonii mwake. Kwa haraka akaanza kuisogeza karibu video ya kisiwa hichi kwani tulikuwa tuinaitazama kwa juu sana. Ikafika karibu, tukawaona wote wanne wakiwa wamelala chini, huku pacha mmoja akiwa amelala juu ya Livna. Nikajikuta nikiwa nimsehika mdomo wangu kwani hadi sasa hakuna anaye fahamu kama wapo hai japo tumewaona wamelala.
Tukaona boti mbili zikija kwa kasir karibu ya kisiwa hichi.
“Ni kina nani hao?”
“Sijafahamu mkuu”
Ester alizungumza huku akizivuta karibu sura za watu hawa. Sote tukawaona ni wazungu walio valia bukta na mashati waliyo yaacha wazi.
“Hawa ni wavuvi, ila pia niwatalii”
Ester alizungumza huku sote tukiwatazama jinsi wanavyo shuka kwenye boti zao, kisha kwa haraka wakakimbilia hadi sehemu walipo anguka Livna na wezake, wakaanza kuwageuza huku wakiwatazama.
“Wanawakagua kama wapo hai?”
“Hii ni hatari, Ester tuma vinaja wakawachukuee”
“Hatuto wawahi, kwa maana ni sehemu ya mbali sana kutoka hapa walipo, ngoja tuangalie mwisho wao utakuwa ni wapi?”
“Na mlipuko umetokea wapi?”
“Ni bomu la kutegewa ardhini, nahisi kuna mmoja wao atakuwa amelikanyaga pasipo kujua ndio likalipuka”
Wazungu hao wakawaingiza kwa haraka Livna kwenye boti yao na kuondoka kwa kasi katika eneo hilo.
“Hakikisheni kwamba hawawapotei hadi sehemu ya mwisho watakapo kwenda”
“Sawa kuna kisiwa kikubwa kama maili sita kutoka kisiwa hichi, ninaimani kwamba hapo ndipo wanapo kwenda”
“Ni lazima tukawachukue”
“Kama watafikia hapo basi ulinzi utakuwa ni wa uhakika kwa maana ni kisiwa wanacho ishi watalii pamoja na wenyeji”
“Wenyeji ni watu gani?”
“Ni Waafrika”
Tukaendelea kutazama boti zilizo wapakiza Livna na wezake jinsi zinavyo zidi kwenda kwa kasi, baada ya saa moja wakafanikwia kufika kweli kwenye kisiwa hicho kikubwa, wakawashusha Livna na wezake na kuwaingia kwenye magari na moja kwa moja wakawapeleka hadi kwenye hospitali iliyopo katika eneo hilo.
“Andaa vijana waweze kwenda”
“Sawa mkuu, ngoja nikawatangazie”
Ester akatoka chumbani humu na kuniacha na Logate.
“Logate tazama Sara yupo wapi, ninahitaji kwenda mimi mwenyewe kumchukua mtoto wa K2”
“Kwenda wewe mwenyewe?”
“Ndio, ninahitaji kwenda mimi mwenywe?”
“Hapana ni bora kuagiza watu waende kumchukua ila si wewe kwa maana ukiondoka wewe tunakosa kiongozi ikiwa kiongozi wetu mkubwa ndio kama hivyo yupo hospitalini”
“Kipindi sijafika nani alikuwa kiongozi?”
“Ester”
“Basi atachukua madaraka na mamlaka niliyo nayo, sawa”
Nilizungumza kwa msisitizo hadi Logate akatingisha kichwa akikubaliana na kile nilicho muagiza. Ester akaingia na kusimama mbele yangu.
“Tayari nimesha andaa vijana watano watakao kwenda kwenye hicho kisiwa na nimesha wapo maelezo ya kutosha, pia wasicha wote nimwafahamisha kwamba kiongozi wetu yupo kwenye hatari.”
“Vizuri na mimi niandalie boti ninahitaji kwenda kuonana na Sara, ninahitaji kumchukua mtoto wa K2 na kurudi naye hapa”
“Unataka kwenda kuonana na Sara!!!?”
“Ndio”
“Hapana Dany, hicho kitu siwezi kukiruhusu kabisa. Dunia nzima unatafutwa, satelaiti zaidi ya maelfu zinakutafuta wewe, unahisi kwamba inaweza kuwa ni rahisi wewe kupiga hatua hata ya kutoka usawa wa hii meli. Huwezi, tulia humu ndani hilo swala la kumpokea mtoto wa K2 nitawapa kazi watu wengine sawa”
Ester alizungumza kwa msisitizo huku akiwa amenyang’ata meno yake, ikiasihiria kwamba kile anacho kizungumza amekidhamiria kutoka moyoni mwake.
“Nitaendelea kuishi humu ndani hadi lini?”
“Ishu si kuishi humu ndani, hii ndio sehemu ya wewe kuwa salama, nimepokea jukumu la kuhakikisha kwamba unakuwa salama, basi ni lazima uwe salama siwezi kuenenda kinyume na kakuli ya mkuu wangu Livna, sawa”
Ester aliendelea kuzungumza kwa jazba huku akiwa amenisogelea karibu yangu akionekana kuto kuniogopa kabisa.
“Logate, mtafute Sara, kisha mtumie Carin hiyo picha ya wapi alipo Sara na mtumie namba za mawasiliano kwa maana nimesha muweka tayari kwa hilo”
“Nimesha mpata Sara anakaribia kufika kisiwani hivi sasa”
“Nitumie namba yake nimpigie imo”
“Sawa mkuu”
Logate akafanya alicho agizwa, Ester akatoa simu yake mfukoni baada ya meseji kuweza kuingia. Akampigia Sara, huku akivaa earphone sikioni mwake.
“Habari yako dada Sara”
“Ninaitwa Ester ni msaidizi wa Livna”
“Nashukuru kama unanifahamu, nina imani unampigia Livna na umeshindwa kupata mawasiliano naye?”
“Basi amepata tatizo katika hicho kisiwa kuna mabomu kadha ambayo yalitegwa kwa kipindi kirefu sana cha nyuma, mmoja ya watu alio ongozana na Livna ameweza kukanyaga bomu hilo na kulipuka, ninamuagiza kijana mwengine kuweza kuja kumchukua huyo kijana”
“Yeye kwa sasa amechukuliwa na wavuvi ambao ni watu salama, na yupo katika kisiwa cha Bama, na kwa sasa wapo hospitalini”
“Basi utakutana na vijana wengine huko”
“Shukrani”
Ester akakata simu yake aliyo ipiga kwa mfumo wa video, akanitazama usoni mwake.
“Pasipo kukuvunjia heshima, ninakuomba tuendelee kushirikiana kuhakikisha kwamba mkuu na wengine wanakuwa salama katika sehemu walipo”
Ester alizungumza kwa sauti ya upole, sikuwa na jambo la kuzungumza zaidi ya kukubaliana naye. Nikaka kwenye kiti nilichokuwa nimekalia huku nikiwa nia wasiwasi mwingi sana.
“Hakuna aliye kanyaga bomu”
Logate alizungumza huku akianza kurudisha vidoe ya muda mchache ulio pita.
“Kuna mnyama huyu nguruwe pori, alikanyaga bomu na kulipuka na mlipuko huo  wa galfa ndio ulio pelekea mkuu na wezake kupoteza fahamu”
Logate alizungumza huku akituonyesha nguruwe aliye lipuliwa upande wa pili wa hichi kisiwa, japo sio mbali sana kutoka sehemu na walipokuwa Livna na wezake.
“Kwa hiyo kuna uwezekano mkubwa, mkuu kuwa salama”
Logate aliendelea kusisitiza na kidogo akafufua matumini na furaha kwa mbali ndani ua moyo wangu.
“Sara naye amebadilisha mawazo anaelekea walipo Livna nina imani kwamba yeye ndio atawai kufika kuliko kina Carini”
“Si wemesha anza safari?”
“Ndio wamesha anza”
“Watafika hapo baada ya muda gani?”
“Kama saa moja na nusu”
“Poa ninikuja”
Nilizungumza huku nikinyanyuka katika kiti nilicho kalia, nikatoka ndani humu na kuwaacha Ester na Logate wakinitazama. Moja kwa moja nikaelekea katika chumba alipo Babyanka na Hawa, nikawakuta wakizungumza huku wakicheka sana.
“Mbona unaingia bila kubisha hodi jamani ungetukuta tupo uchi ingekuwaje?”
Babyanka alizungumza kwa utani.
“Kwani kuna ubaya kuwakuta mupo uchi?”
“Mmmmm”
Hawa akaguna, nikaka pembeni yake huku nimshika shika tumbo lake.
“Mtoto tumtarajie lini?”
“Mmmm bado. Babyanka amenisimulia kwamba kuna ndege za Marekani umezilipua?”
“Ndio”
“Unajisikia raha kuua eheee?”
“Utasikia raha na wewe nikiuliwa eheeee?”
Nilizungumza kwa sauti ya ukali huku nikimtazama Hawa usoni mwake.
“Lengo langu si kukukasirisha baba yangu”
“Kwenye swala la uongozi sinto hitaji kuona mtu yoyote ananishauri kitu ambacho atahisi kwamba kipo kinyime nami sawa?””
“Sawa baba nisamehe kwa maana mimi mwenyewe ninasubiria kifo changu baada ya kujifungua huyu mtoto”
Hawa alizungumza kwa sauti ya upole, kwa jinsi walivyo nichefua kwa maneno yao nikatoka chumbani humu na kupanda juu  kabisa ya hii meli kubwa sana. Huku napo kuna wasichana wanao fanya mazozi, pia kuna kiwacha cha helicopter ambacho kinaweza kupoteka helicopter zaidi ya tano kwani ni kikubwa sana.
“Shikamoo”
Msichana mmoja alinisalimia nikamgeukia na kumtazama usoni mwake.
“Marahaba”
“Naomba nijipime na wewe”
“Ujipime?”
“Ndio mazoezi”
“Una umri gani?”
“Miaka ishirini na mbili”
“Tutapambana kesho sawa”
“Sawa kaka Dany”
“Nenda kaendelee na mazoezi”
Msichana huyu akaondoka na kuniacha nikimuangalia makalio yake yaliyo banwa vizuri na suruali iliyo mbana sana. Sikuhitaji kuendelea kumfwatilia msichana huyu kwani sihitaji kumjengea matamanio ya kimapenzi. Nikaitazama mikono yangu hii miwili, nikajikuta machozi yakinilenga lenga kwani ni mikono ambayo imejaa damu za watu wengi sana ambao wengine nimewaua wakiwa na hatia huku wengine nikiwa nimewaua wakiwa hawana hatia kabisa.
‘Mungu wangu ninakuomba unisamehe’
Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga kwani sidhani hata siku ikitokea nimefariki, ninaweza kuridhi ufalme wa mbinguni kama vile tunavyo amini katika imani zetu za kidini.
“Dany Dany”
Niliisikia sauti ya Logate akiniita, nikageuka nyuma yangu na kumtazama.
“Kuna kitu unatakiwa kukiona huku”
Logate alizungumza huku akiwa na wasiwasi mwingi, kwa haraka tukaanza kukimbia kuelekea katika chumba cha mawasiliano. Tukafanikiwa kufika kwa haraka, tukafungua mlango na kumkuta Ester akiwa amesimama mbele ya Tv huku akitazama mapambo kwenye kisiwa ambacho Livna na wezake wamepelekwa na watalii.
“Wamarekani wametuma jeshi na wanaendelea kushambulia katika hospitali”
“Wanapambana na nani?”
“Wanapambana na Sara, yupo peke yake na amefanikiwa kufika eneo hilo”
“Ulio  waagiza bado hawajafika?”
“Bado hawajafika, ila wamebakisha dakika kama kumi na tano kuweza kufika”
Tukamuona jinsi Sara anavyo endelea kushambuliana na wanajeshi wa Marekani walio fika katika hospitali hiyo. Kusema kweli Sara ana uwezo mkubwa wa kuttumia mwili wake katika kufanya mashambulizi ya silaha na hata mapigano ya kawaida.
“Unaweza kumpigia?”
“Hapana siwezi kumpigia na wala hawezi kupokea simu kwani simu yake alisha iangusha mbali na hapo hospitalini”
“Mtoto bado anaye?”
“Ndio anaye?”
Nikashusha pumzi nyingi huku nikimtazama dada wa watu jinsi anavyo pambana.
“Ohoo Mungu wangu”
Logate alizungumza mara baada sisi sote kuona malori mawili yalio jaa wanajeshi yakisimama nje ya hospitali hiyo. Wanajeshi wakaanza kushuka kwa kasi huku kila mmoja akiwa na silaha yake.
“Waelezee wezako ulio  watuma juu ya hili linalo endelea”
“Nmesha wasiliana nao na wanazidi kuongeza mwendo kasi boti yao kuweza kufika kisiwani hapo”
“Hatuwezi kufanya mashambulizi yoyote ya kuweza kuwazuia hawa wanajeshi kuingia ndani ya hii hospitali?”
“Hapana na tukisema tufanye mashambilizi ya juu, tujue tunaharibu eneo  zima na tutawapoteza watu wetu muhimu”
“Wamefika”
Logate alizungumza huku akituonyesha wasichana walio agizwa na Ester wakisimamisha boti yao kisiwani, wote wakashuka na kukimbilia kwenye moja ya gari lililopo barabarani, wakaondoka kwa kasi walipo fika eneo la tukio, wala hawakuuliza maswali, wakanaza kushambulia.
“Carin hakikisheni mkuu anakuwa salama”
Ester alizungumza huku akiwa ameishika vizuri earphone aliyo ivaa sikioni mwake.
“Muweke loudspeaker”
Ester akafanya hivyo, akaminya moja ya simu za mezani na tukaanza kusikia milio ya risasi jinsi inavyo endelea kurindima katika eneo hilo. Wanajeshi wa Marekani wakazidi kuongezeka jambo ambalo ni hatari sana kwa vijana Livna.
“Mkuu tumezidiwa tunaomba msaada, narudia tena tumezidiwa tunaomba msaada”
Tuliisikia sauti ya Carin alizungumza jambo lililo tufanya sote kutazamana, kwani hata tukituma wasichana wengine ili kuweza kufika eneo hilo watachukua muda mrefu njiani na wanaweza kukuta kila kitu kimekwisha, jambo ambalo ni hatari sana kwetu.
 
 ITAENDELEA
‘Haya Wamarekani wameamua kuhakikisha kwamba wanamkamata Livna na kumuokoa mtoto wa K2 hali inazidi kuwa tete kwa wale walipo eneo la tukio je nini kitakacho endelea? Usikose sehemu inayo fwata ya hadithi hii ya kusisimua kutoka kwa muandishi mahiri Eddazaria G.Msulwa”

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya January 11

Ufaransa Yapinga Matokeo ya Urais DRC

$
0
0
Ufaransa imepinga matokeo ya uchaguzi wa rais nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ikisema ushindi uliotangazwa kwa kiongozi wa upinzani, Felix Tshisekedi haulingani na matokeo ambayo mpinzani wake mkubwa, Martin Fayulu anaonekana kuupata.

Katika tamko lililotolewa jana baada ya matokeo ya awali kutangazwa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Jean-Yves Le Drian alisema Fayulu, ambaye alitangazwa kushika nafasi ya pili, ndiye aliyetakiwa kutangazwa mshindi.

"Kwa kweli inaonekana matokeo yaliyotangazwa, hayaendani na matokeo halisi," alisema alipozungumza na kituo cha televisheni cha CNews.

"Kwa kuangalia (matokeo halisi), Fayulu ndiye kiongozi aliyepatikana katika uchaguzi huu. "

Alisema Kanisa Katoliki, ambalo lina wafuasi wengi na ambalo lilituma waangalizi 40,000, linajua nani hasa aliyehinda na maoni yao yanaonyesha mshindi ni Fayulu.

"CENCO ilifanya ukaguzi na kutangaza matokeo ambayo yalikuwa tofauti," alisema akimaanisha baraza la maaskofu la Kanisa Katoliki.

Dawa Za Nguvu Za Kiume Na Kukosa Hamu Ya Tendo La Ndoa

$
0
0
Asilimia 45-80 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kutowatimizia vyema wake au wapenz wao na kuwasababishia kutoka nje ya mahusiano yao. 

NINI CHANZO CHA HAYO? Kupiga punyeto,Ngiri, Vidonda vya tumbo, Korodani moja kuvimba, Msongo wa mawazo, Presha, Magonjwa ya zinaa, Kufanyiwa tohara ukiwa na umri mkubwa, Kisukari. 

DR. LUTAJA Sasa anakuletea tiba sahihi ya tatizo la Nguvu za kiume. 

NTOMBO :Hii hutibu na kuponya kabisa tatizo la Nguvu za kiume, utakuwa na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kafika kileleni kwa mda wa dk 20-45. Dawa hii imechanganywa na miti 18,Hata wazee wenye umri mkubwa wa zaidi ya miaka 85 wanapona kabisa okoa mahusiano yako, ndoa yako sasa. 

SUNGURURU MIX:Ndio tiba sahihi kwa wale wenye maumbile madogo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo nchi 3-8 na unene cm 2-5,dawa hii ipo katika mfumo wakupaka nakunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji :Hii ni tiba tofauti kabisa nazile ambazo umekwisha wahi kutumia. 

Pia tunadawa za Kupandisha nyota , Uzazi, Pumu, Malaria sugu, miguu kuwaka moto, Kaswende, Kisonono pamoja na mvuto wa mpenzi.

 DR. LUTAJA ANAPATIKANA DAR-ES-SAALAM Simu 0713-821823 kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote ulipo.

Waziri wa Kilimo Ashuhudia Hafla Ya Utiaji Saini Mikataba Ya Ubanguaji Korosho Tani 7500

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Mtwara
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) jana Tarehe 10 Januari 2019 ameshuhudia hafla ya utiaji saini mikataba ya ubanguaji korosho kati ya Bodi ya nafaka na Mazao Mchanganyiko Tanzania na wenye viwanda vya ndani.

Mkurugenzi wa Bodi ya nafaka na Mazao Mchanganyiko Tanzania Dkt Hussein Mansoor ndiye ametia saini kwa niaba ya serikali na Kampuni nne zimesaini mikataba ya awali kuanza kazi hiyo ambazo ni kampuni ya Hawte Investment Co. Ltd, Micronix Mtwara, Korosho Afrika, na Micronix-Newala.

Kampuni hizo zimeingia mikataba ya Jumla ya Tani 7500 ambapo kampuni ya Hawte Investment Co. Ltd yenye uwezo wa kubangua Tani 2000 kwa mwaka imesaini mkataba wa Tani 1500.

Kampuni ya Micronix ya mjini Mtwara yenye uwezo wa kubangua Tani 2400 kwa mwaka imeingia mkataba wa Tani 1200. Kampuni ya Korosho Afrika ya Mjini Tunduru Mkaoni Ruvuma yenye uwezo wa kubangua Tani 5000 kwa mwaka imeingia mkataba wa kubangua Tani 2400 ilihali Kampuni ya Micronix ya Wilayani Newala yenye uwezo wa kubangu Tani 5000 kwa mwaka imeingia mkataba wa kubangua Tani 2400.

Akizungumza katika hafla hiyo ya utiaji saini Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amesema kuwa serikali imepitia vifungu vyote vya kisheria kabla ya kuanza kuingia makubaliano na kampuni hizo kwa ajili ya ubanguaji wa Korosho.

Alisema kuwa zoezi la ubanguaji tayari lilikuwa limeanza kupitia Shirika la Kushughulikia viwanda vidogo vidogo (SIDO) ambalo tayari limeajiri wafanyakazi 160.

Alisema kuwa Shirika la Kushughulikia viwanda vidogo vidogo (SIDO) pamoja na majukumu mengine lakini lilikuwa na kazi mbili ambazo ni kuhakikisha wanatengeneza vipuli na mashine mbalimbali ambazo zimeharibika. Vileviele kuhamasisha wabanguaji wadogo wadogo na kuwasajili.

“Baada ya kuwasajili mtatakiwa kuingia nao mikataba kwa kiasi cha korosho wanachokihitaji kwa ajili ya ubanguaji” Alikaririwa Mhe Hasunga

Mhe Hasunga alisema kuwa serikali ina matumaini makubwa kuwa mikataba ya ubanguaji iliyosainiwa itazingatiwa kwa kufuata taratibu na masharti yote kwa mujibu wa sheria.

Alisisitiza kuwa serikali inaingia mikataba na viwanda ambavyo vimekuwa vikibangua kwa muda mrefu hivyo haina mashaka na ubora wa ubanguaji.

Aidha, Alisema kuwa viwanda hivyo vitakuwa na uhakika wa kufanya kazi usiku na mchana kutokana na malighafi nyingi iliyopo tofauti na miaka iliyopita ambapo malighafi ilikuwa haipatikani kutokana na korosho kubanguliwa nje ya nchi.

Mhe Hasunga amesisitiza kuwa serikali imeamua kubangua korosho zote nchini ili kuongeza wigo wa ajira kwa wananchi sambamba na kuongeza thamani ya korosho inayozalishwa nchini ili iweze kuuzwa kwa jina la Tanzania. Ambapo Wizara ya Kilimo itaweza kuchangia kwa ufasaha katika uchumi wa nchi.

MWISHO

RC Makonda Awahimiza Wananchi Kujiunga Na Rais Magufuli Kuipokea Ndege Ya Sita Ya Serikali Airbus A220-300 LEO Mchana

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda anawaalika Wananchi wote Wapenda maendeleo kujiunga na Mtekelezaji namba moja wa Ahadi Rais Dkt. John Magufuli kwenye mapokezi ya Ndege ya Sita ya Serikali (Airbus A220-300) itakayowasili Nchini leo January 11 Saa sita Mchana ikitokea Nchini Canada.

Hafla ya mapokezi itafanyika kwenye Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere.

Rais Magufuli aliahidi na sasa anatekeleza

WANANCHI WOTE MNAKARIBISHWA

Rudisha heshima yako Kwa Mpenzi Wako, Mke Wako...Tumia Tiba Hii ya Asili

$
0
0
Rudisha heshima yako sasa kwa kutumia Dawa hii iitwayo SUPER GAFINA, kwa ajili ya nguvu za kiume na NKOLOMIJE ni kwaajili ya kuongeza maumbile.

Kwa mwanaume aliye kamilika anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara mbili ,ila ukiwa unapiga moja tena kwa shida wewe ujue  unamatatizo ya upungufu wa nguvu za kiume.

TIBA YA TATIZO LAKO NI; Dawa iitwayo SUPER GAFINA, dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge na unga wa asili ambavyo havina madhara kwa mtumiaji ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja;-

1).itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuchoka.

2).ltakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15 hadi 20 kwa tendo la kwanza.

3).lnaimarisha uume uliolegea na uliosinyaa na kuupa nguvu maradufu.

Je unamaumbile madogo pamoja na uume mfupi? NKOLOMIJE ni suluisho la tatizo lako. Na ni dawa inayoboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi kuanzia inch. 5 hadi 8 kwa muda mfupi sana .Dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk.30 ukisha tumia guarantee miaka 50  ikishakutibu.

Pia ninatibu;- KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU, MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE ,BP, NK.

IGULYATI, ni dawa ya mvuto wa biashara, kazi,kupandishwa cheo na humfanya mfanyakazi kupendwa na mwajiri wake. Pia humvuta mke,Mme,hawara ,mchumba unae muitaji utampata kwa dk.30 tu na atatulia na kumfunga asitoke nje ya ndoa, Pia natoa Pete za bahati ambazo zimetajirisha wengi.

Pia ipo dawa ya kupunguza matiti,unene ,tumbo,na kitambi ,hupunguza mafuta ,kuondoa makovu,chunusi,michilizi mwilini na kuongeza hipsi, makalio na mguu wa bia nk. 

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR,HOSUTWA .Anapatikana Mbagara

Simu no, 0756241666 na 0672186977.

       Huduma hii utaipata popote ulipo

Mwalimu Atekwa....Anyweshwa Sumu na Kufariki Dunia

$
0
0
Mwalimu Nocka Mwaisango (28) wa Shule ya Sekondari Kibwe, jijini Dodoma, amefariki dunia baada ya kunyweshwa sumu na watu wasiofahamika.

Alikufa wakati akitokea mkoani Dodoma kwenda kijijini kwao mtaa wa Mtakuja, Mbalizi Wilaya ya Mbeya Vijijini kwa lengo la kumuoa mchumba wake wa muda mrefu.

Baba mzazi wa mwalimu huyo, Oddy Mwaisango, alisema alipigiwa simu Desemba 20, mwaka jana na mtoto wake huyo kuwa anatarajia kwenda Mbeya kwa mapumziko ya sikukuu na kwamba atatumia mapumziko hayo kumuoa mchumba wake wa muda mrefu.

Alisema baada ya kupigwa simu hiyo, alishangaa kuona muda mrefu unapita bila kumuona na wiki moja baadaye alipigiwa simu na watu wasiofahamika waliotumia namba ya simu ya mtoto wake wakisema kuwa wanamshikilia kwa kazi maalum.
 
Alisema baada ya kauli hiyo aliamua kwenda Kituo cha Polisi Mbalizi, kuripoti tukio hilo.

Alisema siku iliyofuata mama yake alienda Dodoma katika shule aliyokuwa akifundisha kukutana na Mwalimu Mkuu ambaye alimjibu kuwa mtoto wake hakumuaga alipoondoka.

Alisema, ilibidi aende kuripoti Polisi Dodoma na Kitengo cha Uchunguzi wa Mawasiliano mkoani humo kiligundua kuwa mwalimu huyo yuko mkoani Morogoro.

“Ilibidi mama yake asafiri hadi Morogoro na aliripoti kituo cha polisi na kukabidhiwa mtu wa uchunguzi wa mitandao ndipo katika kuchunguza wakabaini wahalifu hao na mwalimu huyo wako mkoani humo, lakini ghafla wakawa hawaonekani kwenye mtandao,” alisimulia.

Alisema baadaye wahalifu hao walimpigia simu (baba) wakihitaji Sh. 5,000,000 kama kikombozi, lakini kwa sababu hakuwa na fedha aliwatumia Sh. 500,000 ili wamwachie.

Aliongeza kuwa siku iliyofuata mtoto wake aliwapigia simu mwenyewe na kuwaambia kuwa yuko kituo cha daladala cha Tazara Mbeya na walipoenda kumfuata walikuta hajitambui.

Aidha, alisema waliamua kumkimbiza hospitali ya Ifisi iliyoko Wilaya ya Mbalizi na baadaye walimhamishia Hospitali ya Rufani Mbeya.

Alisema akiwa wodini aliongezewa maji ya kutosha, lakini alikuwa analalamika kuumizwa kwenye koo na kifuani na katika uchunguzi wa madaktari ilibainika amenyweshwa sumu.

Alisema siku iliyofuata mwalimu huyo alifariki akiwa hajawataja waliomfanyia unyama huo huku chanzo cha kifo kikitajwa kuwa ni dawa aina ya ‘Asphxia Due Mothorax’ aliyonyweshwa.

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kibwe, Dodoma, Mwasiti Msokola, alikiri kupata taarifa za kifo cha mwalimu wake na kwamba suala hilo linashughulikiwa na mkurugenzi ambaye ndiye mwajiri wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Credit:Nipashe

Naibu Waziri Aweso Atoa Onyo Kali Kwa Mkandarasi Muleba

$
0
0
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso ametoa onyo kali kwa Mkandarasi anayefanya kazi ya ujenzi wa Mradi wa Maji Katoke, Wilaya ya Muleba DC, mkoani Kagera baada kubaini changamoto mbalimbali katika mradi huo.

Mradi huo ambao umegharimu kiasi cha zaidi ya Shilingi milioni 476, umeonekana kuwa na kasoro mbalimbali licha ya kukamilika kwake, jambo lililomfanya Naibu Waziri kukasirishwa na Mkandarasi.

Naibu Waziri Aweso amemtaka Mkandarasi huyo awepo kwenye eneo la mradi, atakapofika kuukagua mradi huo, ambaye licha ya kuandikiwa barua tano zikimtaka kufanya marekebisho, bado amekuwa hafiki eneo la mradi na kufanya marekebisho stahiki.

Amesema ni lazima mkandarasi huyo afike na kueleza ni kwanini mradi huo una matatizo, pamoja na kuwa umekamilika unakosa thamani halisi ya fedha (value for money) zilizotumika kujenga mradi huo.

Ikibainika kuna ubadhirifu wa fedha hatua kali zitachukuliwa ikiwemo kuwafukuza wote kazi Mkandarasi na Mhandisi wa Wilaya, pamoja na kuwafikisha katika vyombo vya sheria kwa ajili ya kuchukuliwa hatua.

“Niwaonye watendaji wa Sekta ya Maji, hakikisheni mnawapa kazi wakandarasi wenye uwezo ambao watafanya kazi nzuri na kisha kuidai Serikali malipo yao; sio wakandarasi wajanja ambao wamekuwa wakila fedha za Serikali kiholela bila matokeo kuonekana”, alionya Aweso.

“Ndio maana nimefika Kagera kujionea fedha ambazo wizara inazitoa kama zinaleta matokeo na sio kuchezewa, huku kilio cha wananchi cha huduma ya majisafi na salama kikiendelea. Jambo hilo halina nafasi  kwenye Serikali ya Awamu ya Tano na Wizara ya Maji kwa sasa”, alisisitiza Aweso.

Akatoa tahadhari kwa kusema kuwa tunapoelekea kuanzisha Wakala wa Maji Vijijini (RUWA) wahandisi wababaishaji hawatakuwa na nafasi. Wizara itahakikisha inafanya utaratibu wa kuhakiki uwezo wa wahandisi wote wa maji na kuondoa wazembe na wanaokosa uadilifu.

Naibu Waziri Aweso atakua ziarani Kagera kwa siku tano kukagua miradi ya maji na kutatua changamoto.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images