Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power

$
0
0
Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power Kwaajili Ya Nguvu Za Kiuume Na Promix Kwaajili Ya Kuongeza Maumbile;

Kwa mwanaume aliyekamilika na mwenye Afya njema ili kumridhisha mke au mpenzi anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara mbili hapo utamridhisha mpenzi wako ila ukiwa unapiga moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe 

Tiba Ya Tatizo Lako Ni Dawa Hiitwayo Simpo Power No, 1; dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge vya miti shamba na unga ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja :-1 itakufanya urudie tendo zaidi ya mara tatu 
2 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-20 kwa tendo la Kwanza 
3 huimarisha uume uliolegea na kusinyaa 

Je Una Mke Au Mpenzi Aliyebalikiwa Kuwa Na Kario Kubwa Au Mwili Mnene Na Wewe Mume Wake Una   Maumbile Mafupu?; tumia sasa dawa ya PROMIX dawa itakufanya umfikishe shemu nyeti maana inaboresha maumbile saizi upendayo.

Dawa zangu haziina madhara yoyote kwa mtumiaji 

MARKSU; ni dawa ya kisukari dozi siku 21 
MWARU; ni dawa ya uzazi,hufungua milija ya uzazi ata kwa Wale waliofungiwa uzazi  
MTUNDUU; ni dawa ya busha bila kupasua 
MAZANZA; ni dawa ya kisukar zipo dawa za miguu Kuuma,tumbo,kupunguza Matiti,kutoa minyama uzembe ngiri,vidondo vya tumbo  

FIKA OFISINI KWANGU BUGURUNI MALAPA KARIBU NA KOTA ZA POLISI AU PIGA  SIMU ULETEWE MAHALI ULIPO SIMU NO : 0783185060 au 0752348593  -DR AGU

Uwoya, Dogo Janja Watupiana Maneno

$
0
0
Ndoa ya mastaa wawili bongo, Mwanamuziki Abdulaziz Chende 'Dogo Janja' na Muigizaji Irene Uwoya inaonekana kuzidi kuchafuka zaidi kutokana na wanandoa hao kuweka maneno ya vijembe kwenye kurasa zao za kijamii huku zikitafsiriwa kwamba wanatupiana.

Usiku wa kuamkia leo katika ukurasa wa Instagram wa Msanii Dogo Janja, aliandika bora uonekane kwamba huna hela kuliko kutumia hela nyingi ili kuwaonyesha kwamba uko vizuri.

Katika muendelezo wa ujumbe wake, 'hit maker' wa Banana amerusha jiwe gizani kwa kutoa ushauri kwa mtu huyo anayedhaniwa kuwa ni mkewe, kwamba aache kuishi maisha ya kuigiza.

"Acha Kufake Fake Life. Its better to live your real life  hujazaliwa kufrahisha kila mmoja, Komaaa" - Dogo Janja.
Mashambulio hayo ya gizani ya Dogo Janja yanatafsiriwa kwa haraka kuwa yanakwenda kwa muigizaji Uwoya kutokana na aina yake ya maisha anayoishi na kwamba inadaiwa ni msanii anayeishi maisha ghali sana tofauti na biashara ya sanaa ilivyo kwa sasa nchini.

Hata hivyo baada ya ujumbe huo wa Dogo Janja, Uwoya amerudisha mapigo yanayodhaniwa kwamba ni dongo kwa mume wake kwamba amegeuka mwimba taarabu.

"Kutoka kufanya hiphop mpaka taarab. ohhh shame" ameandika Uwoya.

Kuwa Wakwanza Kupokea Habari Zetu....Download App Yetu Kwa Kubonyeza Hapa, Huhitaji tena kuwa na Computer

$
0
0
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa urahisi kabisa kupitia simu yako ya mkononi muda wowote hata usiku wa manane au ukiwa kazini...

Pata kurasa za mbele Magazetini, habari za kitaifa, matukio yote ya kisiasa, burudani na udaku   kupitia simu yako ya mkononi.

Huhitaji tena kuwa na Computer. Ingia Play Store, pakua App yetu  tukuhabarishe masaa 24.

AY afunguka mwanzo mwisho kuhusu historia ya maisha yake na Jinsi Alivyolala Kwente Kontena Dar

$
0
0
Msanii Ambwene Yesaya ’AY’ kwa mara ya kwanza ameonyesha kontena alilokuwa akitumia kulala alipofika jijini Dar es Salaam kutafuta maisha akitokea mkoani Morogoro.

Katika ukurasa wake wa Instagram leo Jumapili Januari 6, 2019 alipiga picha mbele ya kontena hilo lililopo Upanga karibu na klabu maarufu ya zamani ya muziki iliyoitwa California Dreamer.

Picha hiyo ya AY ambaye amesimama mbele ya kontena hilo, imeambatana na maneno akisema “Heri ya mwaka mpya ndugu zangu. Leo ngoja niwaambieni stori kwa ufupi jinsi Ambwene baadaye akawa AY alivyokuja kupambana na maisha Jijini Dar Es Salaam.”

“Nilikuja Dar mwaka 1999 kutoka nyumbani Morogoro kwa msukumo wa ndugu yangu @gzingalize ambaye tulikuwa tunasoma wote Ifunda Technical School Iringa.”

“Nilikuja Dar nikiwa na ndoto moja tu ya kufanikiwa kupitia kipaji changu cha muziki. Nilipofika sehemu niliyoanza kuishi ni kwenye Container hili hapo nyuma, lipo Upanga baada ya mataa ya California Dreamer kama unaenda mjini,” anaeleza.

“Ndio sehemu nilikaa kwa kipindi kirefu kabla sijapewa hifadhi kwa familia ya @gzingalize halafu nikahamia kwa kina @kingcrazy_gk,” amesema AY.

Alieleza Container hilo lilikuwa linatumiwa na mafundi wa kushona nguo hivyo kila siku ilikuwa ni lazima amke saa 12:00 asubuhi kabla mafundi hawajafika.

Pia katika kuoga ilibidi kutembea mpaka Mnazi Mmoja kwenye mabafu ya Jumuiya ambayo ni ya kulipia.

“Mwisho wa siku ilikuwa lazima ndoto itimie bila kujali mazingira husika. Ni muhimu kushukuru kwa kila jambo Mungu analokubariki nalo na kuweka bidii kwenye ndoto zako, period!!.,”aliandika AY.



Heri ya Mwaka Mpya Ndugu zangu. Leo ngoja niwaambieni story kwa ufupi jinsi Ambwene baadaye akawa AY alivyokuja kupambana na maisha Jijini Dar Es Salaam. Nilikuja Dar mwaka 1999 kutoka nyumbani Morogoro kwa msukumo wa Ndugu yangu @gzingalize ambaye tulikuwa tunasoma wote Ifunda Technical School IRINGA. Nilikuja Dar nikiwa na ndoto moja tu ya kufanikiwa kupitia kipaji changu cha Muziki. Nilipofika sehemu niliyoanza kuishi ni kwenye Container hili hapo nyuma lipo Upanga baada ya mataa ya California Dreamer kama unaenda mjini na ndio sehemu nilikaa kwa kipindi kirefu kabla sijapewa hifadhi kwa familia ya @gzingalize halafu nikahamia kwa kina @kingcrazy_gk. Container hili lilikuwa linatumiwa na mafundi wa kushona nguo. Hivyo kila siku ilikuwa ni lazima niamke saa kumi na mbili asubuhi kabla Mafundi hawajafika. Pia ilibidi kuoga ilikuwa kutembea mpaka MNAZI MMOJA kwenye mabafu ya Jumuiya yaliyoko pale ya kulipia. Mwisho wa siku ilikuwa lazima ndoto itimie bila kujali mazingira husika. NI MUHIMU KUSHUKURU KWA KILA JAMBO MUNGU ANALOKUBARIKI NALO NA KUWEKA BIDII KWENYE NDOTO ZAKO PERIOD!!.. 📸 @shaffieweru #Safari 😊
A post shared by A.Y (@aytanzania) on

Mrema Akumbushia Alivyong'olewa Vunjo na Mrema

$
0
0
Mwenyekiti wa bodi ya Parole nchini na Mwenyekiti wa Chama Cha Tanzania Labour Party (TLP), Agustino Mrema amelalamikia kufanyiwa hujuma kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 na vyama vya upinzani kwa kile alichokidai kulifanyika njama ili aweze kuondolewa kwenye jimbo la Vunjo.

Mbunge wa sasa Jimbo la Vunjo ni James Mbatia ambaye alishika nafasi hiyo baada ya kuungana na vyama vingine vya upinzani ikiwemo CUF, Chama Cha Demiokrasia na Maendeleo CHADEMA, pamoja na NLD.

Mrema amedai James Mbatia alihamia Vunjo kwenye ngome ya upinzani, kwa lengo la kumuondoa yeye, lakini si kupambana kwenye majimbo ambayo CCM inaongoza.

"Vyama hivi vya UKAWA ndiyo niliviona Vunjo mimi nikiwa mpinzani wakanikataa na wakanichangia kama mpira wa kona, badala ya kupambana na CCM wakapambana na mimi, na walimleta Mbatia agombee Vunjo ili kuning'oa na kunimaliza kisiasa na wamefanikiwa" - Mrema.

"Huwezi kuhamia Vunjo kwa lengo la kunitoa mimi ambaye ni mpinzani mwenzako halafu ukiangalia historia yangu ni kubwa sana kwenye nchi hii, badala ya kuona ni namna gani ya kushirikiana na mimi lakini walining'oa" amesema Mrema.

Agustino Mrema alishawahi kuwa Waziri wa mambo ya ndani ya nchi ambaye alikuwa maarufu kwa namna ya utendaji kazi wake na kumfanya kwenye uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995 kuwa Mgombea Urais wa chama cha upinzani nchini ambaye alipata kura zaidi ya milioni 1.

Rudisha heshima yako Kwa Mpenzi Wako, Mke Wako...Tumia Tiba Hii ya Asili

$
0
0
Rudisha heshima yako sasa kwa kutumia Dawa hii iitwayo SUPER GAFINA, kwa ajili ya nguvu za kiume na NKOLOMIJE ni kwaajili ya kuongeza maumbile.

Kwa mwanaume aliye kamilika anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara mbili ,ila ukiwa unapiga moja tena kwa shida wewe ujue  unamatatizo ya upungufu wa nguvu za kiume.

TIBA YA TATIZO LAKO NI; Dawa iitwayo SUPER GAFINA, dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge na unga wa asili ambavyo havina madhara kwa mtumiaji ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja;-

1).itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuchoka.

2).ltakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15 hadi 20 kwa tendo la kwanza.

3).lnaimarisha uume uliolegea na uliosinyaa na kuupa nguvu maradufu.

Je unamaumbile madogo pamoja na uume mfupi? NKOLOMIJE ni suluisho la tatizo lako. Na ni dawa inayoboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi kuanzia inch. 5 hadi 8 kwa muda mfupi sana .Dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk.30 ukisha tumia guarantee miaka 50  ikishakutibu.

Pia ninatibu;- KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU, MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE ,BP, NK.

IGULYATI, ni dawa ya mvuto wa biashara, kazi,kupandishwa cheo na humfanya mfanyakazi kupendwa na mwajiri wake. Pia humvuta mke,Mme,hawara ,mchumba unae muitaji utampata kwa dk.30 tu na atatulia na kumfunga asitoke nje ya ndoa, Pia natoa Pete za bahati ambazo zimetajirisha wengi.

Pia ipo dawa ya kupunguza matiti,unene ,tumbo,na kitambi ,hupunguza mafuta ,kuondoa makovu,chunusi,michilizi mwilini na kuongeza hipsi, makalio na mguu wa bia nk. 

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR,HOSUTWA .Anapatikana Mbagara

Simu no, 0756241666 na 0672186977.

       Huduma hii utaipata popote ulipo

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Italia yamkana balozi wa Korea Kaskazini

$
0
0
Serikali ya Italia imekana kupokea ombi lolote la hifadhi kutoka kwa balozi wa Korea Kaskazini, Jo Song Gil mjini Rome ambaye anaripotiwa kuingia mafichoni nchini humo.

Kwa mujibu wa chanzo kimoja cha habari kutoka ndani ya wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa ya Italia, kimeliambia shirika la habari la AFP kuwa hawana taarifa juu ya ombi la aina hiyo na kuongeza kuwa kile ambacho wizara hiyo ilipokea ni ombi la kuijaza nafasi ya balozi huyo, ambaye Korea Kusini imesema anaitwa Jo Song Gil.

Hata hivyo, duru hiyo imesema haijulikani aliko balozi huyo wa Korea Kaskazini na kwamba aliyechukua nafasi yake tayari amewasili Rome.

Shirika la ujasusi la Korea Kusini liliwafahamisha jana wabunge kuhusu hatima ya balozi huyo baada ya gazeti moja kuripoti kuwa Jo Song Gil, mwenye umri wa miaka 47, aliomba hifadhi yeye pamoja na familia yake katika nchi moja ya Magharibi ambayo haikutajwa.

Huna Sababu ya Kuabika Tena, Jipatie Dawa Bora ya Nguvu za Kiume, Maumbile Madogo na Mvuto wa Mapenzi

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiathiri watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine ....kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapungufu katika mwili wake.

Kuna sababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huathiri misuli ya uume, 


Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0620510598  / 0743543944

Fid Q amshauri AY Alinunue Kontena Alilokuwa Akilala Dar

$
0
0
Baada ya msanii wa Hip Hop Bongo AY' kuweka wazi alivyoanza harakati zake za muziki jijini Dar es salaam kwa kuishi kwenye Kontena, msanii mwenzake Fareed Kubanda maarufu Fid Q amemshauri alinunue Kontena hilo.

Fid Q ambaye bado yupo kwenye fungate la 'Honey Moon' baada ya kufunga ndoa wiki hii, amemshauri mkongwe mwenzake huyo alinunue Kontena hilo kisha atengeneze Studio kwaajili ya wasanii wanaotoka mikoani.

''Nimemshauri AY alinunue lile Kontena kisha aligeuze studio na kijiwe maalum kwa ajili ya wasanii wote wanaotoka mikoani na kuja dar Kwa ajili ya kuendeleza harakati zao za sanaa'', ameeleza Fid Q.

Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii AY ameweka wazi kuwa alikuja Dar es salaam mwaka 1999 kwaajili ya kuendeleza kipaji chake lakini hakuwa na pakufikia ikabidi awe analala kwenye Kontena moja maeneo ya Upanga.

Wajasiliamali Wadogo Mihambwe Wamshukuru Rais Magufuli

$
0
0
Na Emmanuel Shilatu, Mihambwe
Wajasiliamali wadogo wa Kata ya Kitama wamemshukuru Rais Magufuli kwa Kuja na majawabu ya changamoto zao hususani suala la kutozwa Kodi kubwa isiyoendana na mitaji wala mauzo yao.
 
Wajasiliamali hao wameyasema hayo mbele ya Afisa Tarafa Mihambwe, Gavana Emmanuel Shilatu wakati alipoenda kutoa elimu na hamasa juu ya vitambulisho vya Wajasiliamali wadogo.
 
”Naomba Afisa Tarafa utufikishie salamu zetu kwa Rais Magufuli, mueleze sisi Wajasiliamali wadogo hatuna cha kumlipa kutokana na kuendelea kutupigania tufanye biashara zetu kwa amani na kwa faida. Hivi vitambulisho tumevipokea kwa mikono miwili maana ni mkombozi wetu” alisema Mjasiliamali mdogo mmojawapo.
 
Akizungumza kwenye mkutano huo Gavana Shilatu alipiga marufuku Wafanyabiashara wakubwa ama Watu wasio wajasiliamali kuchukua vitambulisho hivyo.
 
”Hivi vitambulisho havitolewi kwa Wafanyabiashara wenye mitaji mikubwa zaidi ya Tsh. Milioni 4 ama kwa Watu wasio wajasiliamali, Ni marufuku kabisa. Hivi vitambulisho tuwaachie wajasiliamali wadogo wenye mitaji midogo ili nao wapate fursa ya kukua wawe wajasiliamali wakubwa” alisema Gavana Shilatu.
 
Jana Jumamosi Januari 5, 2019 Gavana Shilatu alitoa elimu na hamasa kwa Wajasiliamali wadogo wachukue vitambulisho hivyo kwa kata za Kitama na Miuta na mwitikio ulikuwa mkubwa sana.

Dhahabu Ya Mamilioni Ya Pesa Yakamatwa Ikitoroshwa Jijini Mwanza

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza limekamata kilo 323.6 za Dhahabu na fedha taslimu kiasi cha shilingi Milioni mia tatu na Milioni tano (305,000,000) jana  zikisafirishwa kuelekea mkoani Geita, ambapo watu watatu wanashikiliwa mpaka sasa kwa kosa la kusafirisha Dhahabu hizo kinyume na utaratibu.

Akizungumza baada ya kushuhudia tukio hilo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, amewaonya Askari wasaliti au yeyote yule aliyeshiriki katika matukio hayo kwani ni sawa na msaliti wa nchi na kutoa maagizo kwa Jeshi la Polisi mkoani humo kuhakikisha wahusika wote wanapatikana.

Waziri Wa Kilimo Azitaka Nfra Na Bodi Ya Nafaka Na Mazao Mchanganyiko Kuwa Na Mkakati Wa Kununua Nafaka Za Wakulima Nchini

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Songea
Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) pamoja na Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko zimetakiwa kuandaa mikakati ya haraka kuanisha jinsi watakavyo nunua mazao ya wakulima nchini.


Wakati NFRA imetakiwa kuainisha namna ya kununua nafaka za wakulima kwa upande wa Bodi ya Nafaka na Mazao mchanganyiko yenyewe imetakiwa kujikita katika ununuzi wa mazao mbalimbali ya wakulima ikiwa ni pamoja na kutafuta masoko ya mazao ndani na nje ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa jana tarehe 5 Januari 2019 na Mhe Japhet Hasunga (Mb) Waziri wa Kilimo, wakati akizungumza na wafanyakazi wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula (NFRA) mara baada ya kutembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa maghala na vihenge vya kisasa.

Alisema kuwa Wizara yake imekuwa ikihamasisha wakulima nchini kuzalisha kwa wingi mazao kwa ajili ya chakula na biashara lakini inapofika hatua ya kuuza bei zinakuwa ndogo jambo ambalo serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli haitalifumbia macho kamwe.

Pamoja na mambo mengine waziri Hasunga ameupongeza Uongozi wa wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula NFRA kwa ujenzi wa Maghala na Vihenge vya kisasa (Silos) katika maeneo nane ya kanda saba za wakala ambapo ujenzi huo utaongeza uwezo wa kuhifadhi mahindi kutoka Tani251,000 za sasa hadi Tani 700,000 ifikapo mwaka 2025.

Mradi huo wa kuongeza uwezo wa kuhifadhi umeanza kujengwa katika Manispaa ya Songea (Ruvuma), Dodoma, Mpanda (Katavi), Makambako (Njombe), Mbozi (Songwe), Sumbawanga (Rukwa), Shinyanga Mjini (Shinyanga), na Babati (Manyara) ambapo Serikali ya Tanzania na Serikali ya Poland zilisaini mkataba wa mkopo wa masharti nafuu Septemba 2015 wa Dola milioni 55 sawa na sh. bilioni 124, kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo, ambao utaongeza uwezo wa hifadhi ya chakula.

Mhe Hasunga amesema kuwa pundi utakapokamilika ujenzi wa maghala na vihenge hivyo utapunguza gharama mbalimbali zilizokuwa zinatumika kwa ajili ya kununua madawa ya kufukiza mahindi sambamba na gharama za kununua magunia ya kuhifadhia mahindi.

Katika hatua nyingine Waziri huyo amemtaka Kaimu Mtendaji Mkuu wa wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Bi Vumilia L. Zikankuba kuweka msisitizo zaidi wa kununua nafaka ya mahindi kwani katika kipindi chake serikali haitotoa hela kwa ajili ya ununuzi wa mahindi badala yake NFRA ijipange kibiashara ili iweze kununua nafaka nyingi na kujiendesha.

Alisema kuwa huu sio muda wa NFRA kusubiri kupewa mtaji na serikali badala yake kufikiria tofauti na kuanza kufanya biashara ili kufikia walau ununuzi wa nafaka kwa Tani zaidi ya 300,000.

Vilevile, ameutaka Wakala wa majengo Tanzania (TBA) kusimamia kwa weledi mradi wa ujenzi wa maghala na vihenge vya kisasa ili kuhakikisha kuwa mradi huo unakamilika kwa wakati ili kuwanufaisha wananchi.

MWISHO.

Waziri Wa Kilimo:ifikapo Juni 2019 Wakulima Wote Watakuwa Wamesajiliwa Na Kuwa Na Vitambulisho

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo; Tunduru-Ruvuma
Wizara ya Kilimo imeanza kuandikisha wakulima nchini kwa lengo la kuwatambua ili kuwarahisishia huduma mbalimbali zikiwemo uhitaji wa pembejeo za kilimo.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameyasema hayo wakati akizungumza na Wenyeviti na makatibu wa Vyama vya Msingi kwenye kikao kazi  kilichofanyika leo tarehe 6 Januari 2019 katika Ukumbi wa Claster Mjini Tunduru katika Mkoa wa Ruvuma.

Akiwa katika ziara ya siku moja Wilayani Tunduma Waziri huyo amesema kuwa kumekuwa na upotoshaji mkubwa wa taarifa zinazohusu uandikishwaji wa wakulima kuwa una lengo baya, hivyo amewataka wakulima hao kutosikiliza propaganda hizo zisizo na tija kwani utambuzi wa wakulima ni jambo la kawaida kufanya utambuzi.

Alisema kuwa kuandikisha kwa wakulima ni njia pekee ya kuwa na takwimu sahihi kwa kutambua idadi ya wakulima, vijiji na Kata wanazolima ikiwa ni pamoja na kutambua ukubwa wa mashamba yao kwani kufanya hivyo serikali itakuwa na urahisi wa kuwahudumia wakulima hao.

Katika hatua nyingine Mhe Hasunga amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe Juma Homera kwa kusimamia vyema sakata la korosho kwa kusikiliza kesi 11 huku zikifikishwa mahakamani kwa ajili ya kutafutiwa ufumbuzi.

“Nakupongeza sana Mhe Homera kwa usimamizi madhubuti katika kudhibiti kangomba nilipata taarifa kuwa Kg 17,679 za korosho mmezikamata pamoja na zingine Kg 2,779.2 jambo hilo ni zuri endeleeni kusimamia vyema majukumu ya serikali ikiwa ni utekelezaji wa ilani ya CCM yam waka 2015-2020” Alikaririwa Mhe Hasunga

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe Juma Homera aliipongeza Wizara ya Kilimo kwa kuanza kuwalipa wasafirishaji wa korosho kutoka maghala ya vyama vya msingi, kuwalipa gharama za uendeshaji kwa vyama vya masingi, kuwalipa watunza maghala na magunia sambamba na kuondoa mzigo kwa wakati kutokana na ghala kuezuliwa na upepo lililokuwa na jumla ya Tani 536.

Pamoja na pongezi hizo pia Homera amezitaja changamoto mbalimbali katika Oparesheni korosho kuwa ni pamoja na kuchelewa kwa malipo ya wananchi waliofanyiwa uhakiki, utaratibu wa upatikanaji wa miche ya korosho kwa msimu wa mwaka 2018/2019, na mkanganyiko wa upatikanaji wa mapato ya Halmashauri 3% ya bei ya korosho.

MWISHO

Katibu Mkuu CCM Dkt Bashiru Awaonya Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya Walioanza Kutafuta Ubunge Kabla Ya Wakati

$
0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu
Katibu Mkuu wa Chama cha Mpinduzi (CCM) Taifa Dkt. Bashiru Ally amewaonya baadhi ya Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, na Wakuu wa Taasisi na Mashirika ya Umma, ambao wameanza kukaa vikao kwa ajili ya kutafuta majimbo kabla ya wakati wa Chama hicho kutangaza mchakato wa kutafuta wagombea wapya wa ubunge na udiwani.

Dkt. Bashiru ameyasema hayo Januari 05, 2019 wakati akizungumza na viongozi na wanachama wa CCM pamoja na Viongozi na watendaji wa Serikali katika wilaya ya Bariadi na Itilima wakati akiwa katika ziara yake mkoani Simiyu.

Dk Bashiru amesema ikiwa viongozi hao wataendelea kufanya hivyo atawataja hadharani na akasisitiza kuwa ni vema wakaridhika na nafasi walizopewa na Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwani kushindwa kufanya hivyo ni kumdharau aliyewateua.

“Wapo wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, Makatibu tawala wa mikoa, wakurugenzi wa halmashauri, na wakuu wa taasisi na mashirika ya umma, wameanza kukaa vikao kwa ajili ya kutafuta majimbo, CCM hatujatangaza mchakato wa kutafuta wabunge au madiwani wapya, uko wakati nitawatangaza hadharani, mridhike na nafasi zenu mlizopewa na Mhe. Rais” alisema

Katika hatua nyingine Dkt. Bashiru amesema kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika mwaka huu 2019 Viongozi wa CCM wajipange katika kuhakikisha viongozi wa Vijiji na Mitaa wanachaguliwa katika misingi ya demokrasia kwa kuzingatia sifa zao na si fedha zao(rushwa).

“ Katika mwaka huu wa kumuenzi Mwalimu Nyerere baada ya miaka 20 tunataka kufanya mchakato wa kusimamia uchaguzi uwe tofauti, wakati wa kuteua tuzingatie sifa na tuwapime viongozi kwa maisha yao na vitendo vyao......” alisema Dkt. Bashiru.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi ameishukuru Serikali ya awamu ya tano  kwa kutoa zaidi ya shilingi bilioni 26 katika kipindi cha miaka mitatu, kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya  maendeleo.

 Naye Mbunge wa Jimbo la Itilima Mhe.Njalu Silanga, ameishukuru Serikali kwa kuboresha miundombinu ya barabara ambapo amebainisha kuwa kupitia Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) barabara katika jimbo hilo zimetengenezwa zinapitika na zipo ambazo zinaendelea kufanyiwa matengenezo.

Naye Katibu wa CCM Mkoa, Bw. Donald Magesa  akitoa taarifa ya Chama, utekelezaji wa Ilani ya CCM mkoani humo umefanyika vizuri huku akisisitiza kuwa Viongozi wa Chama na Serikali wamejipanga kwa kushirikiana na wananchi kukamilisha maboma yaliyojengwa ili kila mwanafunzi aliyefaulu darasa la saba mwaka 2018 aweze kuanza kidato cha kwanza.

Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Bashiru Ally yuko Mkoani Simiyu kuanzia Januari 05,2019 kwa ziara ya kikazi ya siku mbili yenye lengo la kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM mkoani humo.

MWISHO.

 

Diwani CHADEMA Avuliwa Uanachama

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jimbo la Ukonga kimemvua uanachama diwani wa viti maalum manispaa ya Ilala, Dorcus Lukiko kwa madai ya kukihujumu chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania.

Akizungumza na vyombo vya habari leo Jumapili Januari 6, 2018 mwenyekiti wa Chadema jimbo la Ukonga, Omary Sweya amesema Lukiko amevunja kanuni na katiba ya chama kwa kutoshiriki vikao mbalimbali vya chama na kutosimamia sera zake kama katiba inavyoelekeza.

Amesema Lukiko ambaye pia mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Guluka Kwalala, amedhihirika kukihujumu chama hicho wakati wa uchaguzi mdogo katika jimbo hilo, uliofanyika Septemba 16, 2018.

"Ameonekana pia baada ya uchaguzi mdogo akimzungusha maeneo mbalimbali aliyekuwa mgombea wa CCM kwa lengo la kuwashukuru wananchi kwa ushindi alioupata bila kujali hujuma alizopata mgombea wetu na chama kwa ujumla," amesema Sweya.

Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa Lukiko amekuwa akiwadhalilisha na kuwatuhumu viongozi wa chama bila kufuata taratibu na kanuni za chama kama zinavyoelekeza.

Amesema alitumiwa barua ya kuitwa mbele ya kamati tendaji ya jimbo lakini kwa dharau alitupa barua hiyo na kutoa maneno ya kejeli kwa viongozi na chama kwa ujumla.

"Kwa niaba ya kamati tendaji ya jimbo iliyoketi kikao Januari 5, napenda kuwataarifu kwamba kuanzia sasa ninapozungumza,  Dorcus Lukiko si mwanachama wa Chadema. Tunatoa tahadhari kuwa kazi zozote zitakazofanywa na yeye, Chadema isihusishwe kwa namna yoyote ile," amesema.

Jux Na Mbosso Wasikilizwa Zaidi 2018.

$
0
0
Application ya Boomplay inafahamika kuwa chanzo kikubwa cha ukuaji wa muziki katika bara la Afrika na mnamo mwaka 2017 boomplay app iliweza kujinyakulia tuzo ya application bora ya muziki barani Afrika kupitia kipengele cha “App Afrika award” ikiwa imewafikia watu million 38 ulimwenguni kote na million 3 kwa Tanzania tu.

Kwa wapenzi wa muziki Application ya boomplay inapatikana kiuraisi ikiwa imepakuliwa katika simu za Android kama vile TECNO, Infinix na itel au unaweza kupakua kupitia google play store.
Application ya boomplay imeweza kusaidia wapenzi wa muziki kupakua/kusikiliza nyimbo mpya kwa wepesi zaidi lakini pia imeweza kulinda masilahi ya wasanii wetu kwa kuweza kutambua kiasi cha fedha msanii alichoingiza kupitia mauzo ya nyimbo katika kipindi Fulani.

Na kwa mwaka 2018 boompay imezalisha nyimbo million 833 na takribani nyimbo 30,000 zikiwa mbioni kuingia katika application ya boomplay kutoka kwa wasanii mbalimbali na kupitia takwimu za boomplay inaonyesha wasanii kama Vanessa Mdee, Nandy, Jux, Aslay, Mbosso, rayvanny, Harmonize kuwa miongoni mwa wasanii waliosikilizwa zaidi barani Afrika.

Boomplay mpaka sasa imefanikiwa kufanya kazi na makampuni mengine kama vile Universal music, Kudos, Tunicore na Africori na iko mbioni kuzindua application ya iOS.


Baraza la Taifa la Mitihani (Necta) lawafutia matokeo wanafunzi kwa kuandika matusi

$
0
0
Baraza la Taifa la Mitihani (Necta), limetangaza matokeo ya mitihani ya taifa ya darasa la nne na kidato cha pili iliyofanyika kuanzia Novemba 23, mwaka jana na limewafutia matokeo wanafunzi tisa baada ya kuandika matusi.

Akizungumza jijini hapa jana, Katibu Mtendaji wa Necta, Dk. Charles Msonde, alisema ufaulu wa watahiniwa umeongezeka kulinganisha na mwaka juzi.

Pia alisema katika matokeo hayo hakuna shule ya Serikali iliyojitokeza katika shule 10 bora zilizofanya vizuri.

Huku katika matokeo ya kidato cha pili, jumla ya wanafunzi 47 walifutiwa matokeo yao yote kutokana na udanganyifu, kati yao tisa kutokana na kuandika matusi katika karatasi zao za majibu.

“Kwa hawa wanafunzi tisa walioandika matusi kwenye skripti zao tumeziagiza bodi za shule wanakotoka wawachukulie hatua za kinidhamu ili tukio hilo lisijirudie tena kwa sababu bodi za shule ndizo zenye mamlaka ya kutoa adhabu kwa wanafunzi,” alisema Msonde.

Pia alisema limewafutia matokeo kwa mujibu wa kifungu cha 17(1) kinachokataza mwanafunzi kuandika matusi katika karatasi yake ya majibu.

Alisema jumla ya watahiniwa 506,235 wa kidato cha pili walisajiliwa kufanya mtihani sawa na asilimia 92.87 huku wanafunzi 38,842 sawa na asilimia 7.13 hawakufanya mtihani kutokana na ugonjwa na utoro.

Alisema matokeo ya mtihani huo yanaonyesha kuwa jumla ya wanafunzi 452,273 sawa na asilimia 89.68 wamepata alama za ufaulu zitakazowawezesha kuendelea na masomo ya kidato cha tatu huku 52,073 sawa na asilimia 10.32 wameshindwa kupata alama za kuwawezesha kuendelea na masomo ya kidato cha tatu.

“Mwaka 2017 wanafunzi 433,453 sawa na asilimia 89.32 walipata alama za kuwawezesha kuendelea na masomo ya kidato cha tatu, hivyo ufaulu wa jumla umeongezeka kwa asilimia 0.36,” alisema.

Alizitaja shule kumi zilizofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha pili kuwa ni St Francis Girls ya Mbeya, Thomas More Machrina ya Dar es Salaam, Bright Future Girls ya Dar es Salaam, St. Monica Moshono Girls ya Arusha, Bethel Sabs Girls ya Iringa, Centennial ya Pwani, St. Augustine-Tagaste ya Dar es Salaam, Anwarite Girls ya Kilimanjaro, St. Mary’s Ulete ya Iringa na St. Aloysius Girls ya Pwani.

Huku shule 10 za mwisho kitaifa kuwa ni Ocean ya Mtwara, Mdando ya Tanga, Kwashemshi ya Tanga, Miteja ya Lindi, Thaqalain ya Dar es Salaam, Korona ya Arusha, Imbafi ya Dodoma, Magindu ya Pwani, Mashindei ya Tanga na Luagala ya Mtwara.

Katika matokeo ya darasa la nne, alisema kati ya watahiniwa 1,302,461 sawa na asilimia 95.58 waliofanya mtihani huo na kufaulu kwa kupata daraja A, B, C, na D ni 1,213,132 sawa na asilimia 93.16 huku 89,093 sawa na asilimia 6.84 wamepata daraja E lenye ufaulu usioridhisha.

“Hata hivyo, jumla ya watahiniwa 151 wamefutiwa matokeo yao yote baada ya kubainika kufanya udanganyifu katika upimaji wa kitaifa kwa mujibu wa kifungu 32 (2) (b) cha kanuni za mitihani.

“Baraza limezishauri mamlaka zinazohusika kuwachukulia hatua wale wote waliohusika kwa namna moja au nyingine kusababisha kutokea kwa udanganyifu katika upimaji wa darasa la nne kwa mujibu wa kanuni za utumishi na sheria za nchi,” alisema.

Pia alisema ufaulu umeongezeka kulinganisha na mwaka 2017 kwa kuwa matokeo ya jumla ya upimaji wa kitaifa wa darasa la nne kwa mwaka 2018, yanaonyesha wanafunzi wamefanya vizuri kutokana na takwimu za matokeo zinaonyesha kuwa ufaulu wa watahiniwa kwa masomo yote uko juu ya wastani.

Pia alisema ubora wa ufaulu umezidi kuimarika kwa kuwa watahiniwa waliofaulu kwa daraja la A, B, na C wameongezeka kwa asilimia 0.03 ukilinganisha na mwaka 2017.

Kanisa Katoliki lafichua jina la mshindi wa urais DRC

$
0
0
Baraza Kuu la Maaskofu wa Kanisa Katoliki (Cenco), lenye ushawishi mkubwa  nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, limesema linafahamu aliyeshinda uchaguzi wa rais ambao ulifanyika Desemba 30 mwaka jana na kuomba Tume ya Uchaguzi (CENI) kutangaza matokeo katika mazingira huru, haki na ukweli.

Baraza hilo limetoa baada ya tume ya uchaguzi kutangaza kwamba italazimika kuchelewa kutangaza matokeo ya awali ya uchaguzi uliofanyika Jumapili iliyopita kutokana na hitilafu za kimitambo.

Kanisa hilo limesema sampuli ya wawakilishi ilichapishwa katika vituo vya kupigia kura ambavyo vinawaruhusu kujua jina la rais aliyechaguliwa. Sampuli hiyo ni ya vituo zaidi ya 23,000 kati ya vituo 70,000 vilivyowekwa na Ceni nchini humo.

Akizungumza na vyombo vya habari nchini humo, msemaji wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki, Padri Donatien Nshole, amesema si jukumu lao kutangaza matokeo, bali wao ni waangalizi lakini wanafahamu nani aliyechaguliwa na wananchi.

“Ni muhimu kusisitiza kuwa kasoro zilizojitokeza haziwezi kuathiri kwa kiwango kikubwa chaguo la wananchi wa DRC walioonyesha wazi katika uchaguzi wa urais wa Desemba 30. Cenco imeitaka Tume ya Uchaguzi (Ceni) kama taasisi inayounga mkono demokrasia kutangaza matokeo ya uchaguzi kwa heshima ya ukweli na haki,” amesema Padri Nshole.

Msemaji huyo amekuwa anawasilisha ripoti ya awali ya ujumbe wa waangalizi wa Uchaguzi wa Tume ya Haki na Amani ya Cenco, ambayo inasema kuwa ilikuwa na waangalizi 40,000 siku ya uchaguzi mkuu.

Uchaguzi huo utapelekea kumpata mrithi wa Rais Joseph Kabila, ambaye hakuruhusiwa kuwania muhula wa tatu kulingana na Katiba.

Mwanzoni mwa wiki hii Tume ya Uchaguzi, Ceni ilisema itatangaza matokeo ya awali Januari 6, mwaka huu, kabla ya siku chache baadaye kubadili kauli kuwa huenda zoezi hilo litaahirishwa.

Raia nchini DRC bado wanasubiri kutangazwa matokeo ya uchaguzi huo. Hali ya wasiwasi bado inaendelea, huku huduma ya intaneti ikiendelea kufungwa na mitambo ya radio ya kimataifa ikizimwa. Wakati huo Ceni imesema tayari imehesabu asilimia 20 tu ya kura zilizopigwa.

Kwa upande wake Serikali ya Marekani imeiomba Ceni kutangaza matokeo sahihi na kusema yeyote atakayekwenda kinyume na demokrasia ya nchi hiyo atawekewa vikwazo. Marekani pia imeitaka Serikali ya Congo kufungua mtandao wa intaneti na kuondoa vikwazo kwa vyombo vya habari.

Shirika la utangazaji la Ufaransa, RFI, ambalo lina wasikilizaji wengi katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, linasema mwandishi wake, Florence Morice, alilazimika kuondoka nchini humo baada ya kibali chake cha kufanya kazi kufutiliwa mbali.

Uongozi wa DRC kupitia Waziri wa mawasiliano, Lambert Mende, unalituhumu shirika hilo kwa kuleta utata baada ya kutangaza matokeo yasiyo rasmi madai ambayo shirika lenyewe limekanusha.

“Ni muhimu kufahamu kwamba chini ya sheria za Congo, ni Ceni pekee yenye mamlaka ya kuandaa uchaguzi na kutangaza matokeo,” alisema Mende.

Nalo Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa jana lilitarajiwa kufanya mkutano wa faragha kujadili uchaguzi wa DRC. Mkutano huo umeitishwa na Serikali ya Ufaransa, wakati ambapo mataifa yenye nguvu duniani yanasubiri matokeo ya uchaguzi huo.

Tume ya uchaguzi imepanga kutangaza matokeo kamili Januari 15 na rais aliyechaguliwa ataapishwa siku tatu baadaye.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya January 7

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images