Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kesi kupinga muswada wa Vyama vya Siasa yaahirishwa hadi saa 8 mchana huu

$
0
0
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam leo Januari 4, 2019, imeahirisha kesi No. 31 ya mwaka 2018, ambayo imefunguliwa na Kiongozi wa ACT Wazalerndo, Zitto Kabwe na wenzake wawili dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakiitaka mahakama kuzuia kusomwa bungeni mara ya pili kwa muswada wa sheria ya vyama vya siasa.

Katika kesi hiyo ambayo vyama 10 vya upinzani vimeungana kufungua jalada hilo mahakamani hapo huku walalamikaji wakiwa ni Zitto, Joran Lwehabula Bashange na Salim Abdallah Rashid Bimani wote wa Chama cha Wananchi (CUF) imeahirishwa hadi saa 8 mchana leo ambapo Mahakama hiyo itatoa uamuzi.

Akitoa maelezo mahakamani hapo, wakili wa Serikali ameiomba Mahakama kuongezewa muda wa siku 21 ili kuwasilisha utetezi wao lakini mawakili wa upande wa utetezi wameomba wapewe siku chache zaidi sababu muswada utawasilishwa bungeni Januari 15, mwaka huu.

Mawakili hao wamesema ili kuzuia muswada kupelekwa bungeni mahakama itoe muda mchache zaidi, na endapo siku 14 zitatolewa basi mahakama imeombwa kutoa zuio kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupeleka muswada huo bungeni sababu serikali ndiyo inayomiliki muswada. .

Kutokana na hoja hizo na nyingine zilizotolewa mahakamani hapo, Mahakama imepanga kutoa maamuzi saa 8 mchana wa leo.

Katika shauri hilo la kikatiba namba 31 la mwaka 2018, waombaji wanapinga kifungu cha 8 (3) cha Sheria ya Utekelezaji wa Haki za Msingi, kinachoeleza kuwa muswada wowote hauwezi kupingwa mahakamani.

Pia wanapinga muswada huo pamoja na mambo mengine wakidai unakiuka haki za kisiasa za binadamu, kwa kuwa unaharamisha shughuli za kisiasa na kumpa mamlaka makubwa Msajili wa Vyama vya Siasa kuingilia mambo ya ndani ya vyama vya siasa, yakiwemo ya uongozi.

Tazama Hapa Alichokiongea Rais Magufuli Leo Wakati wa utiaji saini wa mkataba wa mauziano ya mahindi na Shirika la Chakula Duniani (WFP)

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 04 Januari, 2019 ameshuhudia utiaji saini wa mkataba wa mauziano ya mahindi kati ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) na Shirika la Chakula Duniani (WFP) uliofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Mkataba huo umetiwa saini na Kaimu Mtendaji Mkuu wa NFRA Bi. Vumilia Zikankuba na Mwakilishi na Mkurugenzi Mkazi wa WFP hapa nchini Bw. Michael Danford, ambapo WFP itanunua tani 36,000 zenye thamani ya shilingi Bilioni 21 kutoka NFRA.

Baada ya kutia saini mkataba huo Bw. Michael Danford amesema mahindi hayo ni sehemu ya tani 160,000 za chakula zenye thamani ya shilingi Bilioni 132.2 zilizonunuliwa na WFP nchini Tanzania katika mwaka 2018, ikiwa ni ongezeko la kutoka shilingi Bilioni 63.6 zilizotumika kununua chakula katika mwaka 2017.

Bw. Michael Danford amebainisha kuwa kutokana na uhusiano mzuri wa Tanzania na WFP uliodumu kwa miaka 40 sasa, mwaka 2017 shirika hilo liliweka mpango mkakati unaoendana na Mpango wa Maendeleo wa Tanzania, ambapo limeamua kuwa mnunuzi mkubwa wa mazao ya chakula nchini Tanzania kwa ajili ya kusaidia wakimbizi na nchi jirani zenye matatizo ya chakula na kwamba WFP inatarajia kuendelea kuongeza kiwango cha chakula kitakachokuwa kikinunuliwa kutoka Tanzania.

Ameahidi kuwa WFP itaendelea kufanya kazi kwa karibu na NFRA na taasisi zingine zinazohusika katika ununuzi wa chakula ikiwemo Shirika la Reli Tanzania (TRC) ambako imetoa msaada wa kuliboresha ili kuhakikisha usafirishaji wa mazao unafanyika vizuri.

Pamoja na kushuhudia utiaji saini wa mkataba huo Mhe. Rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za Serikali zikiwemo Jeshi la Polisi, Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Shirika la Reli Tanzania (TRC) na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) kuhakikishia wanaondoa urasimu na kuharakisha ununuzi wa mazao yanayonunuliwa na WFP (ikiwemo tani hizo 36,000 za mahindi) ili wakulima wa Tanzania wanufaike na fursa hiyo.

Mhe. Rais Magufuli ameipongeza WFP kwa uamuzi wake wa kununua chakula kutoka Tanzania kwa ajili ya kusaidia wakimbizi na nchi zenye matatizo ya chakula na ameitaka NFRA kutoa tani zote 45,000 za mahindi ambazo WFP waliomba kununua, ili fedha zitakazopatikana zitumike kununua mahindi mengine kutoka kwa wakulima.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli ameitaka NFRA kujipanga vizuri katika shughuli zake ili kuondokana na utaratibu wa kuwa inapatiwa fedha kutoka Serikalini kila mwaka kwa ajili ya kununua mazao ya hifadhi ya chakula, ilihali mazao yaliyopo hifadhini yakiuzwa kiujanjaujanja kwa wafanyabiashara tena kwa bei ya kutupa.

“Nyinyi NFRA wapeni hawa WFP tani zote 45,000 wanazozihitaji, na hata wakihitaji tani 100,000 wapeni au hata 200,000 wapeni, mkipata hizo fedha nendeni mkanunue mazao ya wakulima wanaohangaika na soko. Lakini pia punguzeni matumizi makubwa ya fedha za kugharamia zoezi la ununuzi wa mazao” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Pia Mhe. Rais Magufuli amewataka wafanyabiashara kuacha kulalamika na badala yake wafanye biashara zao kwa uwazi na kwamba Serikali itawaunga mkono.

Mapema Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Innocent Bashungwa amesema wizara imechukua hatua kadhaa za kuimarisha mazingira kwa WFP kununua mahindi na mazao mengine hapa nchini, na kwamba jambo hilo linafanywa sambamba na mkakati wa kufungamanisha kilimo na viwanda na kuimarisha ushirika ili kupanua zaidi uwigo wa soko la mazao ya wakulima.

Hafla ya utiaji saini mkataba huo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Omary Mgumba, Naibu Waziri wa Ujenzi Mhe. Elias Kwandikwa, Makatibu Wakuu, viongozi wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama na wakuu wa taasisi mbalimbali.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
04 Januari, 2019

Kesi Kupinga Mswada Vyama vya Siasa: Mahakama Yatoa Siku 7 Serikali Ijieleze

$
0
0
Mahakama Kuu Tanzania imeipa siku saba Serikali kuwasilisha utetezi wake katika shauri la maombi ya kupinga muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa, tofauti na muda uliowekwa kisheria wa siku 14.

Kesi hiyo imefunguliwa na Kiongozi wa Chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe na wenzake wawili, Joran Bashange na Salim Biman wa CUF kwa niaba ya muungano wa wanachama wa vyama 10 vya upinzani, dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG).

Uamuzi huo umetolewa leo mchana Ijumaa Januari 4, 2019 na kiongozi wa jopo la majaji watatu wanaosikiliza shauri hilo, Jaji Barke Sahel.

Ametoa uamuzi huo baada ya kukubaliana na maombi ya waombaji katika shauri hilo la kupunguza muda wa Serikali kuwasilisha utetezi wake kutoka siku 14 zinazoelekezwa kisheria.

Awali Serikali kupitia kwa mwanasheria wa Serikali mkuu, Mark Mulwambo iliomba kuongezewa muda kutoka siku 14 za kisheria mpaka siku 21 kwa madai ya kufanya mashauriano baina ya Serikali na taasisi zake nyingine.

Akisoma uamuzi huo, Jaji Sahel amesema mahakama haikushawishika na maombi ya Serikali ya kuongezewa muda kwa lengo la kushaurina.

“Kwa kuzingatia kwamba shauri hili limewasilishwa chini ya hati ya dharura na kwa kuwa lina maslahi kwa umma na kwa kuzingatia kwamba muswada huu umepangwa kusomwa bungeni kwa mara ya pili Januari 15, 2019 mahakama inatoa amri zifuatazo,” amesema.

“Mjibu maombi atawasilisha majibu yake akiambatanisha na hati ya kiapo ndani ya siku saba tangu siku ya kupewa nyaraka za shauri hili, yaani atawasilisha utetezi wake kabla au Januari 9, 2019. Usikilizwaji wa shauri hili utafanyika Januari 11 saa 3 asubuhi.”

Katika shauri hilo la Kikatiba namba 31 la mwaka 2018, waombaji wanapinga kifungu cha 8 (3) cha Sheria ya Utekelezaji wa Haki za Msingi kinachoeleza kuwa muswada wowote hauwezi kupingwa mahakamani.

Zitto na wenzake wanapinga muswada huo pamoja na mambo mengine wakidai kuwa unakiuka haki za kisiasa za binadamu kwa kuwa unaharamisha shughuli za kisiasa na kumpa mamlaka makubwa Msajili wa Vyama vya Siasa kuingilia mambo ya ndani ya vyama vya siasa, yakiwemo ya uongozi.

Lugola Ataka Askari Wapandishwe Vyeo, Warekebishiwe Mishahara, Walipwe Fedha Za Uhamisho Na Likizo

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, MOHA-Karagwe.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewataka viongozi Wakuu wa Jeshi la Polisi nchini wahakikishe wanawapandisha vyeo pamoja na kuwarekebishia mishahara askari wote wanaostahili.

Lugola amesema kuna idadi kubwa ya askari wanaostahili kupandishwa vyeo na kurekibishiwa mishahara hivyo askari hao wana haki kwa mujibu wa sheria.

Akizungumza katika kikao cha Baraza la Askari na Watumishi wa Wizara yake, mjini Missenyi na Karagwe Mkoani Kagera, leo. Lugola alisema alitoa agizo kuwa ifikapo  mwezi Agosti mwaka jana agizo hilo liwe limefanyiwa kazi, lakini mpaka umefika mwaka mpya bado halijafanyiwa kazi.

“Kwanini bado hamjapanda vyeo na kubadilishiwa mishahara yenu mpaka sasa wakati nilishatoa maelekezo mpandishwe, nitahakikisha nalifuatilia hili mapema zaidi ili nijue tatizo ni nini.” Alisema Lugola.

Pia Lugola alizungumzia kuhusu ukosefu wa nyumba za makazi ya askari, kuwa licha ya Rais Dkt. Magufuli anatoa mchango mkubwa kwa kulisaidia Jeshi, lakini bado kuna upungufu mkubwa wa nyumba hizo.

“Pamoja na fedha kidogo tunazopata lakini bado tuna tatizo la ukosefu wa makazi wa nyumba za askari, lakini bado Serikali inatafuta fedha ili kuhakikisha changamoto hiyo inaisha,” alisema Lugola.

Pia lugola alisema changamoto nyingine inayowakabili askari wa vyombo vyake ni kutopata fedha za kuhamishwa na atahakikisha madai yote ya askari hao yanafanyiwa kazi.

Lugola alisema jambo ambalo linamuumiza kichwa ni kuhusu madai ya askari na watumishi wa wizara yake ambayo anasema kama wafanyakazi hawatalipwa haki zao na utendaji wa kazi utapungua.

Waziri Lugola yupo mkoani Kagera kikazi na jana alimaliza ziara Wilaya ya Bukoba, na leo anaanza ziara Wilaya ya Misenyi, inafuata Karagwe, Kyerwa, Ngara, Biharamulo na Januari 8, 2019 atamalizia ziara yake Wilaya ya Muleba ambapo katika Wilaya hizo pia atazungumza na wananchi pamoja na watumishi waliopo ndani ya Wizara yake ambao ni Jeshi la Polisi, Idara ya Uhamiaji, Jeshi la Magereza, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, pamoja na Idara ya Probesheni ambayo jukumu lake kuu ni kupunguza msongamano gerezani na kusimamia wafungwa waliopewa adhabu mbadala na Mahakama au wafungwa waliopata msamaha kupitia sheria ya huduma kwa jamii na kutumikia kifungo chao nje ya Gereza.

Hatimaye Abdul Nondo arejeshwa chuoni UDSM

$
0
0
Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo, amerejeshwa chuoni katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), alikokuwa akisoma.

Nondo amepokea barua ya kurejeshwa chuoni hapo leo Ijumaa Januari 4, baada ya kusimamishwa masomo mwaka jana kutokana na kesi ya kudanganya kutekwa na kuchapisha taarifa za uongo mitandaoni iliyokuwa ikimkabili, ambapo kwa mujibu wa sheria za chuo hicho uongozi ulilazimika kumsimamisha masomo hadi atakapomaliza kesi hiyo.

“Barua hii imethibitisha mimi kurudishiwa sifa ya kuwa mwanafunzi wa UDSM kuanzia tarehe 6/1/2019 ambapo nitakuwa na haki ya kufanya maandalizi na kufuatilia taratibu zote za kujiandaa kuendelea na masomo semista ya pili kuanzia Machi 2019.

“Ikumbukwe mimi nilibakiza semista ya pili tu ya mwaka wa tatu ndiyo naanza kufuatilia taratibu za kumalizia semista hiyo hapo mwezi wa tatu baada ya mimi kupata barua hii ya kurejeshewa sifa yangu (status) ya uanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam. ni muda wa kujipanga kumalizia masomo yangu, hili ni jambo la msingi sana,” amesema Nondo katika taarifa yake.

Nondo alishinda kesi hiyo na kuachiwa huru Novemba 5, mwaka jana baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa kushindwa kumtia hatiani na upande wa jamhuri kushindwa kuthibitisha makosa aliyoshtakiwa nayo.

Wizara ya Kilimo kuja na Mwarobaini wa mazao ya Wakulima yanayoozea mashambani

$
0
0
Naibu Waziri wa Kilimo Innocent Bashungwa amesema Wizara yake imepanga kuja na miundombinu itakayowasaidia wakulima kuondokana na adha ya mazao kuozea mashambani.

Ameyasema hayo leo Ijumaa Januari 4,katika utaiji tiaji saini wa mkataba wa makubaliano ya mauziano ya mahindi kati ya wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) na Shirika la Chakula Duniani (WFP) uliofanyika Ikulu jijini Dar ES Salaam.
 
Bashunga amesema mkakati huo una nia ya kuboresha kilimo kwani mbali na kupata changamoto hiyo lakini pia wana changamoto za masoko ya mazao ya kimkakati hivyo kupitia mkataba huo pia wataongea na WFP ili wanunue na mazao megine tofauti na mahindi.

“WFP wanasambaza chakula katika nchi nyingi sana tunataraji kuongea nao ili waje kununua mazao mengine kutoka hapa nchini na kufanya hivyo wakulima watakuwa wamepata soko la uhakika,

“Huu mkataba unaosainiwa leo ni matokeo ya jitihada za wizara yetu kufata maelekezo ya Rais na tunafanya kazi kwa ukaribu na wadau wa kilimo na taasisi za serikali nchini kuhamasisha kilimo cha tija nchini na kuhakikisha wakulima wetu wanapata masoko ya uhakika kwani ndio mkombozi wao,” Naibu waziri wa kilimo Innocent Bashungwa.

Aidhaamaetoa rai kwa viongozi wa vikundi vya wakulima na Bodi za mazao hapa nchini kaucha kujifikiria wao na badala yake wawafikiria wakulima amba ndo wanatumia muda wao na fedha kuwekeza katika kilimo.

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Kuanza Kwa Vikao Vya Kamati Za Bunge, Januari 2019

Taarifa Kwa Umma Kutoka Wizara Ya Mambo Ya Nje Na Ushirikiano Wa Afrika Mashariki

$
0
0
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Sekretarieti ya Shirika la Kuzuia Silaha za Kemikali (Secretariat of the Organization for the Prohibition of Chemical Weapons- OPCW) imetangaza nafasi za kazi za Afisa Mwandamizi wa Masuala ya Umma na Afisa wa Masuala ya Umma (Public Affairs Officer P-4 and Public Affairs Officer P-2). 

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inawahimiza Watanzania, hususan wanawake kuchangamkia nafasi hizo ambapo mwisho wa kufanya maombi kwa nafasi ya Public Affairs Officer P-4 ni tarehe 24 Januari 2019 na ile ya Public Affairs Officer P-2 ni tarehe 9 Januari 2019. 

Maombi yafanywe kwa njia ya mtandao kupitia tovuti www.opcw.org ambayo pia ina maelezo zaidi kuhusu nafasi hizo.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
4 Januari 2019

Watu Wawili Wafariki Dunia Kwa Kugongwa na Gari la Polisi

$
0
0
Watu wawili wamefariki dunia baada ya pikipiki waliyokuwa wamepanda kugongwa na gari la polisi wilayani Monduli mkoani Arusha.

Tukio hilo limetokea jana jioni Januari 3, 2019 eneo la Meserani Duka Bovu wilayani Monduli.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Ramadhani Ng'azi alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

"Ni kweli kuna hiyo ajali lakini mkuu wa upelelezi mkoa amekwenda eneo la tukio ndio atatupa taarifa sahihi ya kilichotokea,” amesema.

Kamanda Ng'azi amesema taarifa sahihi za tukio hilo ikiwepo majina ya marehemu zitatolewa baada ya uchunguzi kukamilika.

Pikipiki hiyo ilikuwa ikitoka kuweka mafuta katika kituo cha mafuta kilichopo pembezoni mwa barabarani ya Arusha- Dodoma na kukutana na gari hilo lililokuwa likipita barabara kuu.

Washtakiwa kesi ya bomba la mafuta waendelea kusota rumande

$
0
0
Jalada la kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili mfanyakazi mstaafu wa Shirika la Mafuta Tanzania na Zambia (Tazama), Samwel Nyakirang'ani (63) na wenzake 11, lipo katika ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kwa ajili ya kuchambuliwa.

Washtakiwa hao wanaendelea kusota rumande kwa muda wa miezi 11 na siku 18 sasa, kutokana na upelelezi wa shauri hilo kutokamilika.

Kwa mara ya kwanza, washtakiwa hao walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Januari 16, 2018 kujibu mashtaka matatu likiwemo la kujiunganishia isivyo halali bomba la mafuta mali ya Mamlaka ya Bandari Tanzania ( TPA),  lakini hadi sasa upelelezi wake bado haujakamilika.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Patrick Mwita amedai leo  Januari 4, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi, Janeth Mtega, kuwa shauri hilo lilikuja kwa ajili ya kutajwa.

Mwita ameeleza kuwa jalada la shauri hilo lipo ofisi ya DPP kwa ajili ya kuchambuliwa na kulitolea maamuzi  hivyo anaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Hakimu Mtega baada ya kusikiliza maelezo hayo ameahirisha  kesi hiyo hadi Januari 16, 2019 itakapotajwa.

Washtakiwa wote wapo rumande kutokana DPP kuwasilisha hati ya kuzuia dhamana.

Mbali na Samweli, washtakiwa wengine katika kesi hiyo namba 1/2018 ni Nyangi Mataro (54) ambaye ni mwalimu wa Shule ya Msingi Ufukoni.

Wengine ni mfanyabiashara, Farijia Ahmed (39), Malaki Mathias (39), Kristomsi Angelus (25), Pamfili Nkoronko (40) na Henry Fredrick (38), Audai Ismail (43), Chibony Emmanuel, Roman Abdon, Amina Shaban na Zubery Ally.

Kwa pamoja wanadaiwa kati ya mwaka 2015 hadi Januari 8, 2018 katika eneo la Tungi Muungano wilayani Kigamboni, washtakiwa wanadaiwa kujiunganishia bomba la mafuta ya dizeli lenye upana wa inchi moja kutoka katika bomba lenye upana wa inchi 24, bila kuwa na kibali.

Katika shtaka la pili ambalo ni kuharibu miundo mbinu, inadaiwa siku hiyo ya tukio, washtakiwa walitoboa bomba la hilo ambalo lilikuwa likitumika kusafirisha mafuta mali ya TPA.

Pia wanadaiwa kuharibu bomba la mafuta mazito lenye upana wa inchi 28, ambalo lilikuwa likitumika kusafirisha mafuta ghafi, mali ya TPA.

Waziri Mkuu: Rais Amedhamiria Kufungua Milango La Maendeleo Nchini

$
0
0
*Ni ile iliyokuwa imejifunga kwa muda mrefu kwenye mikoa mbalimbali

RAIS Dkt. John Magufuli amedhamiria kufungua milango na fursa za maendeleo iliyokuwa imejifunga kwa muda mrefu kwenye mikoa mbalimbali nchini ukiwemo mkoa wa Ruvuma.

Hayo yamesemwa leo (Ijumaa, Januari 4, 2019) na Waziri MKuu Kassim Majaliwa apozungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji Nyoni, Mbinga.

Waziri Mkuu ambaye yuko mkoani Ruvuma kwa ziara ya kikazi ya siku nne amesema Serikali itahakikisha milango ya maendeleo katika maeneo yote nchini inafunguka.

Amesema miongoni mwa miradi inayotekelezwa na Serikali ambayo inalenga kufungua milango na fursa ya maendeleo ni pamoja na ujenzi wa miundombinu ya barabara.

Waziri Mkuu ametolea mfano wa barabara inayojengwa kutoka Mbinga hadi Mbamba bey kwamba itafungua fursa za kiuchumi kwa wananchi pamoja na Taifa kwa ujumla.

Kadhalika, Waziri Mkuu amezungumzia suala ya utendaji kwa watumishi wa umma, ambapo amewataka watekeleze majukumu yao ipasavyo na hayo ndio matakwa ya Serikali.

“Lazima watumishi wa umma wawajibike kwa kuwatumikia wananchi ipasavyo na wazingatie wajibu wao. Serikali haitawavumilia watumishi wazembe, wala rushwa.”

Pia Waziri Mkuu amewasisitiza watumishi wa umma kwenda kwa wananchi kusikiliza kero na changamoto mbalimbali zinazowakabili ili kushirikiana nao katika kuzipatia ufumbuzi.

Amesema kitendo cha wananchi kuwasilisha malalamiko yao kupitia mabango kwenye mikutano ya viongozi kinaonesha kwamba watumishi hawaendi kwa wananchi.

“Watumishi wa Mbinga acheni kukaa ofisini na badala yake tengeni siku tatu kwa wiki na kwenda vijijini kwa ajili ya kuwasikiliza wananchi na kutatua kero zinazowakabili.”

Mkutano huo ulihudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenister Mhagama na Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga, Naibu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso.

Wengine ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro, Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhandisi Stella Manyanya, Naibu Waziri OR-TAMISEMI Joseph Kandege, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme na maafisa wengine wa Serikali.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya January 5

RC Makonda Ataka Watendaji Kuongeza Kasi Ya Makusanyo Ya Kodi Pasipo Kuwasumbua Wananchi

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amewataka watendaji kuhakikisha wanasimamia ipasavyo makusanyo ya kodo ikiwa ni pamoja na kubuni mbinu mpya na rafiki za ukusanyaji pasipo kuwatisha wala kuwabugudhi wananchi.

RC Makonda ametoa kauli hiyo wakati wa kikao mkakati baina yake ya mamlaka za ukusanyaji wa kodi ambapo amesema mwaka huu jiji hilo limedhamiria kuongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato ili kuendelea kuwa kinara.

Aidha RC Makonda amewataka watendaji kubuni vyanzo vipya vya mapato, kuongeza idadi ya walipa kodi, kufanya mabadiliko ya sheria kandamizi zilizopitwa na wakati pamoja na kuanzisha mfumo wa malipo kwa kadi Kama ilivyo kwa mataifa mengine.

Pamoja na hayo RC Makonda ameshauri kuanzisha kwa kitengo cha ushauri kwa wafanyabiashara jambo litakalowajengea wananchi hamasa ya kulipa kodi na kuondoa dhana ya kuonekana ni watu wa kukusanya mapato pekee.

RC Makonda anaamini kuwa wananchi wapo tayari kulipa kodi serikalini endepo watawekewa mazingira rafiki ya kuwawezesha kulipia ikiwa ni pamoja na wafanyabiashara kuwekwa katika data base moja.

Kikao hicho kimehusisha wakuu wa wilaya, makatibu tawala, TRA, BOT, TIC, NBS, Wizara ya fedha na kamati za ulinzi na usalama.

Waziri Mkuu Aridhishwa na kasi ya Ujenzi Barabara ya Mbinga

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amekagua mradi wa ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mbinga kwenda Mbamba bey yenye urefu wa kilomita 69 itakayogharimu sh. bilioni 129.3.

Amekagua barabara hiyo jana (Ijumaa, Januari 4, 2019) wakati akielekea wilayani Mbinga akiwa katika siku ya tatu ya ziara yake ya kikazi ya siku nne mkoani Ruvuma.

Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi wa mradi huo wa barabara inayojengwa na kampuni ya Chico ya nchini China, ambapo ameuagiza uongozi wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kusimamia vizuri mradi huo.

“Kazi hii inafanywa kwa uhogari mkubwa, naipongeza kampuni ya Chico kwa hatua waliyoifikia na ninaamini kwamba barabara hii inayotarajiwa kukamilika Januari 2021 itakamilika mapema zaidi.”

Kwa upande wake, Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Christina Mndeme amesema kukamilika kwa barabara hiyo kutachochea ukuaji wa uchumi kwa wananchi na mkoa kwa ujumla kwani itarahisisha usafiri kwa watu pamoja na usafirishaji wa mizigo.

Amesema pia barabara hiyo itakuza sekta ya utalii na uvuvi katika mkoa wa Ruvuma kwa sababu itawezesha watalii na wafanyabiashara kufika kwa urahisi katika wilaya ya Nyasa ambako ni kuingo cha biashara kati ya nchi jirani na mikoa inayopitiwa na ziwa Nyasa.

Mkuu huyo wa mkoa ametumia fursa hiyo kuushukuru uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli kwa kuwapelekea fedha za ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwemo ya hospitali, vituo vya afya, shule, nishati na maji.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Agizo Latolewa Kwa Wanaojenga Jengo La Wizara Ya Mifugo Na Uvuvi Kuendelea Kulipwa Kwa Wakati

$
0
0
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, amemtaka mkandarasi SUMA JKT anayejenga jengo la wizara hiyo katika Mji wa Serikali Jijini Dodoma, kuhakikisha anaendelea kuwalipa wafanyakazi wanaojenga jengo hilo kwa wakati pamoja na kuhakikisha ubora wa jengo hilo unaendana na thamani hali pesa.

Mhe. Ulega amesema hayo jana (04.01.2019) mara baada ya kufika katika mji huo uliopo Kata ya Mtumba, kwa ajili ya kufanya tathmini ya maendeleo ya ujenzi wa jengo la awali la Wizara ya Mifugo na Uvuvi na kuonesha kuridhishwa na kasi ya ujenzi inavyoendelea na kumtaka mkandarasi kukamilisha ujenzi huo kwa wakati.

“Unamlipa mtu kabla jasho lake halijakauka palepale unakuwa tayari umeshampa ndiyo dini inavyosema, ni jambo jema sana maana hawa mafundi wanasema wanalipwa kwa wakati, sisi muda wowote tutakuwa tunakuja hapa tunataka hii kazi imalizike kwa wakati na kwa viwango” Amesema Mhe. Ulega.

Mhe. Ulega amefafanua kuwa siyo jambo jema endapo kutatokea taarifa mara baada ya kumalizika kwa mradi wa ujenzi wa jengo la Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kuwa wafanyakazi waliokuwa wakijenga jengo hilo wanamdai mkandarasi ilhali wizara imemlipa pesa zote mkandarasi huyo SUMA JKT ili aweze kufanya kazi kwa wakati.

Kwa upande wake Mkandarasi Msimamizi wa SUMA JKT Injinia David Pallangyo ambaye anasimamia ujenzi wa jengo la Wizara ya Mifugo na Uvuvi amesema ujenzi wa jengo hilo unaenda kwa kufuata mpangilio wa ratiba wa shughuli kwa kila tarehe na kwamba hadi kufikia mwisho wa mwezi Januari mwaka huu jengo litakuwa katika hatua za mwisho.

Ziara ya Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega kufanya tathmini ya ujenzi wa jengo la wizara katika Mji wa Serikali jijini Dodoma ni mwendelezo wa ziara za viongozi wa juu wa wizara zenye lengo la kuhakikisha jengo hilo la awali la wizara ambalo limetengewa Shilingi Bilioni Moja kutoka serikali kuu linakamilika kwa wakati na kuanza kutumika.

MWISHO

Imetolewa: Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
                     Wizara ya Mifugo na Uvuvi

Kigwangallah Amsimamisha Kazi Mkuu wa Kikosi dhidi ya Ujangili Kanda ya Arusha

Jipatie Dawa ya Asili ya Kupunguza Maziwa, Kupunguza Tumbo,Kuongeza Unene, Kuongeza Maumbile ya Kiume na Kuondoa Chunusi

$
0
0
Anza mwaka 2019 na mambo mapya kutoka kampuni ile ile inayofanya vizuri TANZANIA na nchi za NJE ambayo ni @natural_beauty_prod.

           BADO TUNATOA OFFA KAMA IVI👇👇👇
1. SHARK POWER--Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza uume urefu na upana mpaka nchi 7.5 ilikua inapatikana kwa @170,000/= sasa ni @160,000/= tu

2.VIGA 84000---Hii dawa ya kuspray yenye uwezo mkubwa wa kuchelewesha wakati wa tendo la ndoa ilikua ni  @160,000/=. Sasa ni 150,000/= tu

3. HANDSOME UP ORIGINAL-- Hichi ni kifaa cha kuongeza maumbile kwa size uipendayo wewe pamoja na kuimalisha misuli kifaa hichi kilikua kinapatikana kwa @230,000/=. Sasa ni 210,000/= tu

4. MAXMAN CAPSULE--- Hii ni dawa ya vidonge ya kuongeza uume urefu na upana pamoja na kuongeza nguvu za kiume kwa wiki mbili ilikua inapatikana kwa @200,000/=. Sasa ni 180,000/= tu

5. VIG RX---- Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza uume urefu na upana mpaka nchi 10 ilikua inapatikana kwa @190,000/=. Bei ya sasa ni 170,000/=

6. BODY BOOSTER---Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri ilikua inapatikana kwa @150,000/=. Sasa ni 140,000/=

7. BOTCHO MULT PLUS-- Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza (hips mapaja na makalio) kwa size uipendayo ilikua inapatikana kwa @200,000/=. Sasa ni 180,000/=

8. WHITE COLLECTION---- Ni vidonge vya kuwa mweupe mwili mzima pamoja na kuwa soft ilikua inapatikana kwa @150,000/= Sasa ni @140,000/= tu

9. BOTCHO HOLOGRAM CREAM--- Hii ni dawa ya kuongeza hips na makalio ilikua inapatikana kwa@180,000/= Sasa ni@160,000/=       

N.K

Wasiliana nasi kwa simu
NO:. +255 759029968  AU +255 659618585
Popote ulipo utapata huduma zetu.

Pia hakikisha unapatiwa risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ununuapo bidhaa kampuni hii.
               WELCOME ALL

Habari Njema Kwa Wenye Matatizo Ya Nguvu za Kiume, vitambi, nyama uzembe

$
0
0
NAUHABARISHA ULIMWENGU TIBA BORA YA MITI SHAMBA..

  Ninatibu magonjwa 1-100 dawa ninazo Sasa.

KOLA; ni dawa ya kisukari dozi siku 14 ata kama unajihisi itumie kwa kinga zaidi

  THREE(3) POWER MIX,inatibu Nguvu za kiume Ni dawa iliyo Bora na Humfanya mume kuchelewa kufika kileleni dkk 40_47 bila kuchoka.Inaanza kufanya kazi ndani ya door 80 na inatibu kabisa ndani ya siku 6 tu,hutatumia Tena dawa ya Nguvu za kiume three power mix Ni kiboko kabisa,hata Kama unahisi una tatizo unaruhusiwa kutumia kwa ajili ya Kinga baadae.

 DUDUMA MIX 4 POWER,hunenepesha na kurefusha uume na kukomaza uume uliosinyaa kwa mda mfupi,tumia siku 4 na kupona kabisa.

  SHOOLA,Ni dawa ya kutibu tezi dume na kupona kabisa ni ya miti shamba hutumika kwa kunywa bila upasuaji ndani ya siku 14 haina madhara.

 NENGONENGO,dawa ya kutibu Uzazi kwa akina mama walioshindwa kubeba mimba kwa mda mrefu ukitumia utaweza kupata mimba na kujifungua salama.

  KAMINGO,Ni dawa inayotibu Busha bila kufanyiwa operation na aliyevimba korodani inatibu kabisa dozi Ni siku 7 na inaubora wa Hali ya just na unapona kabisa.

  IKUMBIJA,Ni dawa ya kumvuta mpenzi aliekuacha na mwenye ahadi za uongo kukutimizia,na kumkomesha mtu asiwe na mtu mwingine pia atakurudia ndani ya masaa 6.

   MALAMALA,Ni dawa ya vidonda vya tumbo na tumbo kujaa gesi, kilungulia na inafanya kazi kwa haraka zaidi na kupona kabisa ndani ya siku 6.
 

SAALA,Ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto,kiuno,mgongo,magoti na viungo vyote mwilini na joints,Sasa tiba yake Ipo kwangu.

   HALALA MIX,Ni dawa mix ya miti 100 inayotibu matatizo yote,Kama majini,kesi,biashara,kazi,mitego na kupoteza kumbukumbu. no

TUNAFANYA KAZI SIKU ZOTE PIA NAKUFIKIA POPOTE ULIPO KWA HARAKA,NAPATIKANA DAR ES SALAAM NA KAHAMA,PIA NINA MAWAKALA MIKOANI SIMIYU,SHINYANGA,MOSHI NA MBEYA.


     KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA: 0784 475946
           0744 922982
    DR,SANDALA.

Rudisha heshima yako Kwa Mpenzi Wako, Mke Wako...Tumia Tiba Hii ya Asili

$
0
0
Rudisha heshima yako sasa kwa kutumia Dawa hii iitwayo SUPER GAFINA, kwa ajili ya nguvu za kiume na NKOLOMIJE ni kwaajili ya kuongeza maumbile.

Kwa mwanaume aliye kamilika anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara mbili ,ila ukiwa unapiga moja tena kwa shida wewe ujue  unamatatizo ya upungufu wa nguvu za kiume.

TIBA YA TATIZO LAKO NI; Dawa iitwayo SUPER GAFINA, dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge na unga wa asili ambavyo havina madhara kwa mtumiaji ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja;-

1).itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuchoka.

2).ltakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15 hadi 20 kwa tendo la kwanza.

3).lnaimarisha uume uliolegea na uliosinyaa na kuupa nguvu maradufu.

Je unamaumbile madogo pamoja na uume mfupi? NKOLOMIJE ni suluisho la tatizo lako. Na ni dawa inayoboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi kuanzia inch. 5 hadi 8 kwa muda mfupi sana .Dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk.30 ukisha tumia guarantee miaka 50  ikishakutibu.

Pia ninatibu;- KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU, MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE ,BP, NK.

IGULYATI, ni dawa ya mvuto wa biashara, kazi,kupandishwa cheo na humfanya mfanyakazi kupendwa na mwajiri wake. Pia humvuta mke,Mme,hawara ,mchumba unae muitaji utampata kwa dk.30 tu na atatulia na kumfunga asitoke nje ya ndoa, Pia natoa Pete za bahati ambazo zimetajirisha wengi.

Pia ipo dawa ya kupunguza matiti,unene ,tumbo,na kitambi ,hupunguza mafuta ,kuondoa makovu,chunusi,michilizi mwilini na kuongeza hipsi, makalio na mguu wa bia nk. 

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR,HOSUTWA .Anapatikana Mbagara

Simu no, 0756241666 na 0672186977.

       Huduma hii utaipata popote ulipo

Video Mpya ya Dully Sykes - Samba

$
0
0
Video Mpya ya Dully Sykes - Samba
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images