Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Wanaoanza kidato cha kwanza mwaka huu watakiwa kwenda na kiti na meza

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, Kayombe Lyoba amewaagiza wazazi na walezi wenye watoto wanaotarajia kujiunga kidato cha kwanza  mwaka huu kuhakikisha wanakwenda na kiti  na meza ili waweze kuingia darasani.

Hali hiyo imekuja baada ya halmashauri hiyo kuongeza kasi kwenye ujenzi wa vyumba vya madarasa ili kila mwanafunzi aliyechaguliwa kuingia kidato cha  kwanza  apate fursa ya kuanza masomo.

“Tunawaomba wazazi na walezi wawezeshe watoto wao kuja na kiti na meza pindi wanapokuja kuanza masomo Januari 7, kwani tayari tumeshaongeza jitihada kuhakikisha vyumba vya madarasa vinakuwepo vya kutosha ili asikose kuingia mwanafunzi hata mmoja,” alisema  Lyoba.

Alisema jumla ya wanafunzi 4,136 wamepokewa na halmashauri iwemeweza kujenga vyumba vya madarasa 87 na kubakiwa na upungufu wa vyumba 32.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Kibena Kingo alisema mbali na jitihada za kujenga maabara katika shule zao kuna changamoto ya uhaba wa walimu wa masomo ya sayansi.

“Halmashauri yetu ina upungufu wa walimu 41 wa kufundisha masomo ya sayansi, hivyo tunamwagiza Ofisa Elimu Sekondari kulifuatilia suala hilo kwa ukaribu ili tuweze kuondokana na changamoto hiyo,” alisisitiza Kingo.

Aidha Ofisa Elimu Sekondari, Hatujuani Ally alisema Serikali ndiyo inayopanga walimu na hadi sasa imeweza kuleta walimu wa sayansi katika Shule ya Sekondari Nelson Mandela, Matombo, Kibogwa na Mvuha na matarajio ni kuongeza walimu wengi zaidi kwenye shule ambazo zina uhitaji mkubwa.

Ally aliongeza kwamba Wilaya ya Morogoro kwa sasa ina jumla ya walimu wa kufundisha masomo ya sayansi 42 huku mahitaji yakiwa ni walimu 83 katika shule 28 zilizopo.

Mawakili wa Mbowe Wahoji Kuhusu Rufaa Iliyokatwa na Serikali....Kesi Imepigwa Kalenda Hadi January 17

$
0
0
Wakati Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko wakiendelea kusota mahabusu, Wakili anyewatetea Profesa Abdallah Safari amehoji katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuhusu rufaa iliyokatwa na upande wa mashtaka katika Mahakama ya Rufani.

Mbowe na Matiko wanasota mahabusu baada ya Mahakama ya Kisutu kuwafutia dhamana yao November 26,2018 kwa kukiuka masharti ya dhamana, ambapo waliamua kukata rufaa Mahakama Kuu lakini iliwekewa pingamizi baada ya upande wa mashtaka kukata rufaa Mahakama ya Rufani.

Profesa Safari alihoji swali moja kuhusu rufaa hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri baada ya Wakili wa Serikali Mkuu, Paul Kadushi kueleza kuwa shauri hilo limeitishwa kwa ajili ya kutajwa.

Profesa Safari alimuuliza  Wakili Kadushi kama rufaa waliyoikata ilikuwa chini ya hati ya dharura na kama hawakufanya hivyo ni kwa nini...? 

Katika majibu yake Wakili Kadushi ameeleza kuwa hakuna uhalali wa kisheria kuhusu swali hilo mahakamani hapo, labda lingeulizwa Mahakama Kuu au Mahakama ya Rufaa.

Kutokana na hatua hiyo, Hakimu Mashauri ameahirisha kesi hiyo hadi January 17, 2019 huku akisema swali hilo la rufaa wakalihoji Mahakama Kuu.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ya jinai namba 112/ 2018 ni wabunge wa Chadema, Mchungaji Peter Msigwa (Iringa Mjini), John Mnyika (Kibamba),  John Heche (Tarime Vijijini), Halima Mdee (Kawe) na Ester Bulaya (Bunda Mjini).

Pia wamo, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji na Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar), Salum Mwalimu.

Kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 13 ikiwemo kula njama,  kufanya mkusanyiko wenye ghasia, kuhamasisha hisia za chuki, kushawishi hali ya kutoridhika, uchochezi na kushawishi utendaji wa kosa la jinai kati ya Februari Mosi na 16, 2018 maeneo ya  Dar es Salaam.

Vyama vya Upinzani Vyafungua Kesi Mahakamani Kuupinga muswada wa vyama vya siasa

$
0
0
Vyama  10 vya  upinzani nchini Tanzania kupitia muungano wao vimefungua kesi Mahakamani Kuu ya Tanzania kupinga muswada wa sheria ya vyama vya siasa kujadiliwa na Bunge kwa ajili ya kuupitishwa kuwa sheria.

Kesi hiyo imefunguliwa Desemba 20,2018 ikitarajiwa kuanza kusikilizwa kesho Ijumaa Januari 4,2019 huku mlalamikiwa akiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Akisoma tamko la umoja huo leo Alhamisi Januari 03, 2019, Kiongozi wa ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe amesema muswada huo unakinzana na Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 hivyo ni muhimu kwao kuupinga.

“Serikali imepeleka bungeni muswada wa sheria ya vyama vya siasa unaohalalisha agizo la Rais Magufuli alilolitoa mkoani Singida mwaka 2016 kuzuia mikutano ya vyama vya siasa. Muswada huu unafanya shughuli za kisiasa kuwa suala la jinai.

“Tumefungua kesi katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar chini ya hati ya dharura kupinga Muswada wa Sheria ya Vyama vya Siasa kujadiliwa na Bunge kwa minajiri ya kuupitisha kuwa sheria kwa sababu unakinzana na katiba ya nchi. 


"Hatuwezi kwenda kuujadili Bungeni, mnajua kuna wabunge wengi wa CCM, baadhi yao ni wazuri na tumekuwa tukijadiliana nao, lakini wengine ni makasuku.  Kuna wabunge wengine wa CCM wanapenda sifa, siyo kwamba utakuwa mbaya tu lakini utatoka mbaya zaidi.

“Muswada huo unalenga kumfanya Msajili wa Vyama vya Siasa kuwa na Mamlaka ya Usimamizi (Regulatory Authority), kuwa na mamlaka ya kuingilia shughuli za kiutawala na maamuzi ya ndani ya vyama vya siasa ikiwemo kusimamisha/ kumfukuza mtu uanachama,” amesema Zitto Kabwe.

Rudisha heshima yako Kwa Mpenzi Wako, Mke Wako...Tumia Tiba Hii ya Asili

$
0
0
Rudisha heshima yako sasa kwa kutumia Dawa hii iitwayo SUPER GAFINA, kwa ajili ya nguvu za kiume na NKOLOMIJE ni kwaajili ya kuongeza maumbile.

Kwa mwanaume aliye kamilika anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara mbili ,ila ukiwa unapiga moja tena kwa shida wewe ujue  unamatatizo ya upungufu wa nguvu za kiume.

TIBA YA TATIZO LAKO NI; Dawa iitwayo SUPER GAFINA, dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge na unga wa asili ambavyo havina madhara kwa mtumiaji ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja;-

1).itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuchoka.

2).ltakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15 hadi 20 kwa tendo la kwanza.

3).lnaimarisha uume uliolegea na uliosinyaa na kuupa nguvu maradufu.

Je unamaumbile madogo pamoja na uume mfupi? NKOLOMIJE ni suluisho la tatizo lako. Na ni dawa inayoboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi kuanzia inch. 5 hadi 8 kwa muda mfupi sana .Dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk.30 ukisha tumia guarantee miaka 50  ikishakutibu.

Pia ninatibu;- KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU, MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE ,BP, NK.

IGULYATI, ni dawa ya mvuto wa biashara, kazi,kupandishwa cheo na humfanya mfanyakazi kupendwa na mwajiri wake. Pia humvuta mke,Mme,hawara ,mchumba unae muitaji utampata kwa dk.30 tu na atatulia na kumfunga asitoke nje ya ndoa, Pia natoa Pete za bahati ambazo zimetajirisha wengi.

Pia ipo dawa ya kupunguza matiti,unene ,tumbo,na kitambi ,hupunguza mafuta ,kuondoa makovu,chunusi,michilizi mwilini na kuongeza hipsi, makalio na mguu wa bia nk. 

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR,HOSUTWA .Anapatikana Mbagara

Simu no, 0756241666 na 0672186977.

       Huduma hii utaipata popote ulipo

VIDEO: Katibu Mkuu CCM, Dkt Bashiru Ally aanika ubadhilifu kiwanda cha TANICA

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM, Dkt Bashiru Ally ameeleza kusikitishwa na ubadhirifu unaoendelea kwenye kiwanda cha usindikaji wa kahawa cha TANICA kilichopo Bukoba.

==>>Msikilize Hapo Chini

Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power

$
0
0
Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power Kwaajili Ya Nguvu Za Kiuume Na Promix Kwaajili Ya Kuongeza Maumbile;

Kwa mwanaume aliyekamilika na mwenye Afya njema ili kumridhisha mke au mpenzi anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara mbili hapo utamridhisha mpenzi wako ila ukiwa unapiga moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe 

Tiba Ya Tatizo Lako Ni Dawa Hiitwayo Simpo Power No, 1; dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge vya miti shamba na unga ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja :-1 itakufanya urudie tendo zaidi ya mara tatu 
2 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-20 kwa tendo la Kwanza 
3 huimarisha uume uliolegea na kusinyaa 

Je Una Mke Au Mpenzi Aliyebalikiwa Kuwa Na Kario Kubwa Au Mwili Mnene Na Wewe Mume Wake Una   Maumbile Mafupu?; tumia sasa dawa ya PROMIX dawa itakufanya umfikishe shemu nyeti maana inaboresha maumbile saizi upendayo.

Dawa zangu haziina madhara yoyote kwa mtumiaji 

MARKSU; ni dawa ya kisukari dozi siku 21 
MWARU; ni dawa ya uzazi,hufungua milija ya uzazi ata kwa Wale waliofungiwa uzazi  
MTUNDUU; ni dawa ya busha bila kupasua 
MAZANZA; ni dawa ya kisukar zipo dawa za miguu Kuuma,tumbo,kupunguza Matiti,kutoa minyama uzembe ngiri,vidondo vya tumbo  

FIKA OFISINI KWANGU BUGURUNI MALAPA KARIBU NA KOTA ZA POLISI AU PIGA  SIMU ULETEWE MAHALI ULIPO SIMU NO : 0783185060 au 0752348593  -DR AGU

Mkurugenzi APANGUA Tuhuma za Katibu mwenezi wa CCM, Humphrey Polepole Kushusha Mapato

$
0
0
Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji Mkoani Kigoma imeshindwa kufikia lengo la kukusanya mapato ya Shilingi Milioni 200.8 kwa mwezi kutokana na utendaji mbovu wa Watendaji, kushindwa kusimamia vyema ukusanyaji huo na sio Katibu mwenezi wa CCM, Humphrey Polepole kama inavyosemekana.

Akizungumza na Waandishi wa habari Mkoani Kigoma Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Mwailwa Pangani amesema licha ya Manispaa hiyo kushindwa kufikia lengo hilo lakini kila mwezi mapato yamekuwa yakiongezeka na hivyo kuahidi kufikia lengo hilo hivi karibuni.

Mwailwa amesema kuwa taarifa zilizoandikwa na moja ya chombo cha habari nchini, hakuhusika nazo yeye na kuomba msamaha kwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole kwakuhusishwa kwenye mgogoro usiohusika.

"Hizi taarifa zilizozagaa mimi sikuwa Mkurugenzi kwa wakati huo, hivyo natumia fursa hii mbele yenu waandishi wa habari kumuomba radhi Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, kwa kashfa hii aliyozushiwa na pia nakiomba chama cha mapinduzi radhi kwakuwa kimechafuliwa", amesema Mkurugenzi huyo.

Kufuatia kufanya vibaya kwa manispaa hiyo katika ukusanyaji mapato, Ofisi ya CAG imeipa manispaa hiyo hati chafu kwa miaka mitatu mfululizo.

Polepole alifanya ziara mkoani Kigoma mwezi Machi, 2018 ambapo pamoja na mambo mengine alisikiliza kero za wafanyabiashara wa masoko yaliyopo Manispaa ya Kigoma Ujiji waliokuwa wakilalamikia kupanda kwa tozo za vizimba kutoka shilingi 15,000 hadi shilingi 50,000.

Rais Mstaafu Jacob Zuma kuingia studio kurekodi albam

$
0
0
Rais mstaafu wa Afrika Kusini Jacob Zuma, anakusudia kuingia studio hivi karibuni, kurekodi albam ambayo itakuwa na nyimbo za mapambano.

Uongozi wa mji wa Durban, mji mkuu wa jimbo lake la KwaZulu-Natal, umetangaza kuwa utafadhili gharama za kurekodi albamu hiyo.

Mkuu wa kitengo cha burudani na utamaduni wa mji huo, Thembinkosi Ngcobo amesema  kuwa wazo hilo lilifikiriwa miaka mitatu iliyopita.

“Tulikuwa tunatafuta wasanii wa nyimbo za aiana hii, ilikuwa ngumu , tulijaribu kutafuta hata video fupi fupi, lakini hatukupata kitu katika jumba la makumbusho, hapo ndipo kama Idara tukamkumbuka Zuma kwenye suala la kuimba

”Hivi karibuni tulikuwa na Mazungumzo na Zuma, tulienda nyumbani kwake, tukajadili, alianza kuongelea mengine lakini kabla hatujaondoka, alisema amefurahi kuwa sehemu ya 'ptoject' hiyo, hivyo tutaangalia namna ya yeye kufanya mazoezi na kwaya hivi karibuni".ameeleza Ngcobo.

Polisi Yatoa Kauli kuhusu Watoto Wawili Waliokufa Maji Mtwara Huku Mwingine wa Tatu Akiuawa Kwa Kipigo

$
0
0
Watu wawili ambao ni wanafunzi wa shule ya Msingi Mgao Mkoa wa Mtwara wameokotwa wakiwa wamefariki Dunia pembezoni mwa mwambao wa Bahari ya Hindi.
 
Uchunguzi wa Daktari imebainisha kuwa vifo hivyo vimetokana na kukosa hewa baada ya kuzama kwenye maji.

Kamanda wa Polisi mkoani Mtwara, Kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi Blasius Chatanda amesema tukio la wanafunzi hao kuzama majini limetokea Januari Mosi katika kijiji cha Mgao ambapo uchunguzi wa awali unaonyesha watoto hao hawakuwa na wasimamizi walipokwenda kuogelea.

"Watoto hao tumeweza kuwatambua, wa kwanza alikuwa anaitwa Rajab Athman mwenye umri wa miaka 12 ambaye ni mwanafunzi wa darasa la nne, wa pili alikuwa anaitwa Salum Hamza ambaye alikuwa na miaka 8. Walikwenda kuogelea kwenye fukwe na bahati mbaya maji yaliwazidi na wakapoteza maisha," amesema Kamanda Chatanda.

Katika hatua nyingine siku hiyo ya Januari Mosi Amri Nayope ambae ni mwanafunzi wa shule ya Sekondari alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitari ya Wilaya ya Newala akidaiwa kushambuliwa kwa kupigwa na watu ambao hawakufahamika kisha kutelekezwa jirani na Nyumbani kwao.

Kufuatia taarifa hiyo baadhi ya wakazi mkoani hapa wameitaka jamii hususani wazazi na walezi kuongeza umakini katika kuwasimamia watoto wao.

Kamanda Chatanda amesema msako mkali unaendelea kuwabaini waliohusika katika shambulio lililopelekea kifo cha mwanafunzi huyo wa sekondari huku miili ya wanafunzi wa shule za msingi tayari imesha kabidhiwa kwa ndugu baada ya uchunguzi wa Daktari ili kuendelea na taratibu za mazishi.

Jeshi la Polisi Dar Lakanusha Taarifa ya Panya Road Kulitikisa Jiji Hilo Mwaka Mpya

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema Jiji hilo liko shwari na hakuna tukio lolote la uvunjifu wa amani ambalo linahusishwa na uwepo wa 'Panya road'.

Akizungumza leo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Lazaro Mambosasa amewahakikishia wananchi wa Jiji hilo kuwa hali ni shwari na hakuna tukio ambalo limetokea hasa kwenye siku ya mkesha wa mwakya mpya wa 2019.

"Tumeona moja ya gazeti likisema 'Panya road watikisa Dar'.Ukweli hakuna tukio limehusisha panya road siku ya mkesha wa mwaka mpya.Dar iko salama sana , hivyo taarifa hizo hazina ukweli wowote,"amesema Kamanda Mambosasa na kusisitiza Jeshi la Polisi Kanda Maalum limejipanga kuhakikisha usalama upo wa kutosha.

Amefafanua katika siku ya mkesha wa mwaka mpya kulikuwa na makundi ya watu mbalimbali wakiwamo wanaosheherekea mwaka mpya,makundi ya watu waliotoka Kanisani na maeneo mengine, hata hivyo hakukuwa na tukio ambalo limefanywa na hao wanaodaiwa kuwa panya road kwani hakuna panya road .

"Tupo kwa ajili ya kuhakikisha hali ya usalama inakuwa salama,hivyo asitokee mtu mmoja kwa utashi wake akawatia hofu wananchi kwa kudai kuna panya road wakati hakuna," amesema Kamanda Mambosasa na kuongeza kuwa wananchi wasiwe na hofu na kuwatataka waendelee na shughuli zao kama kawaida za ujenzi wa uchumi wao na Taifa kwa ujumla kwa mwaka huu wa 2019.

Harmonize atoa msaada kwa walemavu Dar

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka lebo ya WCB iliyochini ya Diamond Platnumz, Harmonize alimaarufu Kondeboy ameamua kutoa msaada kwa walemavu jijini Dar Es Salaam maeneo ya Kariakoo.

Msanii huyo ameamua kurudisha shukrani hizo kwa mashabiki zake ambao wana matatizo mbalimbali hasa walemavu wa miguu na katika kipindi hiki ambapo tumeingia mwaka mwingine.

Mbali na kutoa msaada huo msanii huyo ameandika ujumbe mrefu sana kweny ukurasa wake wa Instagram akitoa shukrani zake kwa wale wote walioweza kwa namna moja ama nyingine kuusapot muziki wake. na Ukumbe mwenyewe ndio huu hapa:-

“HERI YA MWAKA MPYA….!!! NDUGU ZANGU …!!! NINGEPENDA KUTOA SHUKRANI ZANGU ZA DHATI KWA WAANDISHI WA HABARI PAMOJA NA MEDIA ZOTE AMBAZO ZIMEKUWA SAMBAMBA NAMI BILA KUWASAHAU DJ’S WOTE DUNIANI KWA KUUNGANA NAMI NA KUNI SUPPORT KUSOPPORT MUZIKI WANGU AMA KWA HAKIKA BILA NYINYI BASI PASINGEKUWA NA HARMONIZE HATA MUZIKI WENYEWE HUWENDA USINGEKUWEPO 


MWAKA 2018 UMEKUWA MWAKA WENYE KUONYESHA MWANGA AMA NURU YA MUZIKI KWANGU NAAMINI MAZURI MENGI YAPO MBELE NINGEOMBA MUENDELEE NA MOYO HUWO HUWO WA UPENDO NA IMANI KUNIVUMILIA NINAPOKOSEA KWANI MIMI SIJAKAMILIKA HASA UKICHANGANYA NA UJANA…!!!! 

LAKINI PIA NIWATAKIE HERI YA MWAKA MPYA SHABIKI ZANGU AMBAO MUPO BEGA KWA BEGA NAMI KUHAKIKISHA TUNALIKAMILISHA KILA TULIPANGALO KWA UWEZO WA MUNGU….!!!!! HAKIKA NYINYI NDIO HARMONIZE MWENYEWE….!!! LAMWISHO NIOMBE KUWASILISHA HILI DOGO KWA WAMILIKI WA MEDIA WATANGAZAJI PAMOJA NA DJ’S WOTE….!!!

 KAMA UNGEPENDA MIMI NIKUPIGIE JINGLE AU TANGAZO LA REDIO YAKO BASI UNACHOTAKIWA KUFANYA NI KUCHUKUA NUMBER HI..! 👉 +255658135762 KISHA TUMA MAELEKEZO YAKO MFANO MIMI NI DJ FULANI KIPINDI FULANI YANI TUMA MAELEKEZO YAKO YOTE KUPITIA WHTSP NADHANI WATU WA MEDIA WASHANIELEWA NINACHO MAANISHA KISHA MWISHO WEKA EMAIL YAKO NAMI NITARECORD NA NITAKUTUMI KATIKA EMAIL YAKO HI NI KWA MEDIA WATANGAZAJI DJ’S WOTE DUNIANI……!!! LET’S GO…….!!!!!!!!!!”

Msanii huyo amekuwa sio mara ya kwanza kwenda kutoa msaada Kariakoo sehemu ambayo inaaminika ndio yalikuwa makazi ya msanii huyo kwani alishawahi kufanya kazi hapo ya kuuza maji kabla ya kuwa msanii.

Kikwete Amvaa Kingwangallah kwa Kushindwa Kurangaza Utalii

$
0
0
Mbunge wa Chalinze (CCM) Ridhiwani Kikwete amesema bado Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangala hajafanya kazi yake vilivyo katika kutangaza vivutio vya utalii nchini.

Ridhiwani ameyasema hayo leo Alhamisi Januari 3, 2019 katika uzinduzi wa redio ya kutangaza utalii ya 'Hakuna Matata'.

Amesema hivi karibuni alimuona Dk Kigwangalla akipiga picha katika moja ya mbuga za wanyama kama moja ya njia ya kuhamasisha kutembelea vivutio vya utalii.

"Nilipoiona picha ile, nilimkosoa kwa kweli na kumwambia bado hajaweka nguvu kubwa kwenye ushawishi, ingekuwa vizuri kama angetumia wasanii  ambao wana watu wengi wanaowafuatilia kwenye mitandao ya kijamii," amesema Mbunge huyo

Kuhusu ujio wa redio hiyo, Ridhiwani amesema ni jambo zuri ukizingatia kuwa ni ya mtandaoni ambako dunia imehamia huko.

Awali akieleza lengo la kufungua , Mkurugenzi wa redio hiyo, Beatrice Ndungu, amesema  moja ya sababu ni kutangaza utalii na pia kuzalisha ajira kwa vijana.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wasanii mbalimbali akiwemo Miss Tanzania, Elizabeth Makune, Mzee Chilo na  Monalisa,.

Seth, Rugemarila Kyendelea Kysota rumande

$
0
0
Washtakiwa katika kesi ya Uhujumu Uchumi, Habinder Seth na James Rugemarila, wanaendelea kusota rumande kutokana na upelelezi wa shauri hilo kutokukamilika.

Washtakiwa hao walifikishwa kwa mara ya kwanza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Juni 2017, kujibu mashtaka 12 yakiwemo ya utakatishaji fedha.

Rugemarila ambaye ni Mkurugenzi wa VIP na mmiliki mwenza wa zamani wa IPTL na Sethi ambaye ni Mwenyekiti Mtendaji wa PAP, wanadaiwa kutenda makosa hayo katika Jiji la Dar es Salaam na nchi za Afrika Kusini, Kenya na India.

Wakili wa Takukuru, Leonard Swai amedai leo Alhamisi Januari 3, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi, Wanjah Hamza kuwa, kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi wake bado haujakamilika, hivyo anaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Hakimu Hamza ameahirisha kesi hiyo hadi Januari 17, 2019 itakapotajwa tena, washtakiwa wamerudishwa rumande.

Wafanyakazi Dar waandamana kumpongeza Rais Magufuli kwa Kufuta Kikokotoo Kipya

$
0
0
Wafanyakazi jijini Dar es salaam wameandamana kwa lengo la kumpongeza Rais Dkt. John Magufuli kwa uamuzi wake wa kufuta kikokotoo kipya cha mifuko ya hifadhi za jamii na kurejesha cha zamani.

Maandamano hayo yamefanyika leo, Januari 3,2019 ambapo yameanzia ofisi za Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), Mnazi Mmoja jijini humo hadi viwanja vya Mnazi Mmoja wakiwa na mabango yenye ujumbe wa kumpongeza Rais Magufuli, yamepokewa na Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaviva.

Akizungumza na waandamanaji hao, Lyaviva ametoa rai kwa wafanyakazi wa umma nchini kufanya kazi kwa uadilifu na kuwahudumia wananchi bila upendeleo. Amesema wapo baadhi ya watumishi wa serikali wanaochelewesha huduma kwa wananchi kwa makusudi hali inayosababisha malalamiko.

“Zingatieni nidhamu ya utumishi na utendaji, bahati nzuri kila taasisi ina mfumo wake wa utendaji kazi zingatieni hiyo mifumo, furaha hii ya kikokotoo haimanishi mjisahau katika kuwahudumia wananchi,” amesema.

Akizungumzia kuhusu tamko la Rais Magufuli la kusitisha kikokotoo walichokiita kandamizi amesema uamuzi huo uwe chachu ndani ya mioyo ya wafanyakazi hao kwa kufanya kazi kwa bidii na kujituma zaidi.

Akisoma risala iliyoandaliwa na wafanyakazi hao, Katibu wa kamati za wanawake wa TUCTA, Jenijely James amesema kikokotoo hicho kilichorejeshwa kina mafao bora katika sekta ya umma.

Desema 28, 2018, Rais Magufuli alikutana na TUCTA, viongozi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) na wadau wengine Ikulu jijini Dar es salaam na kusitisha kikokotoo kipya na kurudisha cha zamani ambacho kitatumika hadi 2023.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya January 4


Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH....Anatoa Pete za Bahati, Anasafisha Nyota, Anazuia Chuma Ulete na Mengine

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam Shariff,  Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
 
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Adam Shariff Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. 

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Mawasiliaono: +255715971688  au +255756914036
 
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Katibu Mkuu Wa CCM Dkt. Bashiru Ally Atembelea Kaburi La Baba Wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM Dkt.Bashiru Ally amepokelewa Mkoa wa Mara baada ya kumaliza ziara yake ya kikazi Mkoani Kagera

Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally atafanya ziara ya siku mbili kuimarisha Chama Mkoa wa Mara ikiwa ni pamoja na kutembelea Wilaya ya Butiama alikozikwa mwasisi wetu Mwl. Julius kambarage Nyerere

Aidha, Ndg. Bashiru Ally amesema katika ziara yake hii ni kukijenga chama nakukiimarisha katika Misingi iliyowekwa na Mwasisi wetu Mwl.Nyerere

Ndg. Bashiru Ally ameyasema hayo Mbele ya wananchi na viongozi wa Chama na serikali wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama Mkoa Ndg. Samweli Kiboye  wakikagua kituo cha Afya jimbo la Bunda

Katika ziara hiyo ameshiriki kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Butiama.

Katika kikao hicho Dkt.Bashiru Ally ametoa salamu za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mh. John Pombe Magufuli kwa wana Mara na kuwambia anawahakikishia kuwa miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa Hospitali ya Mkoa na Uwanja wa ndege wa kisasa Musoma itatekelezwa.

Katibu Mkuu wa CCM amehitimisha kikao hicho kwa kusisitiza Umoja kwa watumishi wa Chama na Serikali, kwani kwa kufanya hivyo tutakuwa tunaendeleza misingi iliyo asisiwa na Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

Waziri Mkuu Afungua Soko La Mazao Songea

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amefungua mradi wa maghala ya kuhifadhi nafaka na soko la mazao la OTC-Lilambo katika Halmashauri ya Songea uliogharimu sh. bilioni 1.5.

Amesema Rais Dkt. John Magufuli ameazimia kuwawezesha wakulima kuwa na mahala pa uhakika pa kuhifadhia mazao yao na sehemu ya kufanyia biashara ili kuwaongezea tija.

Amefungua soko hilo jana (Alhamisi,  Januari 3, 2019) akiwa katika siku ya pili ya ziara yake ya kikazi ya siku nne ya kukagua shughuli za maendeleo mkoani Ruvuma.

Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na ujenzi wa soko hilo pamoja na maghala kwani umezingatia viwango. Maghala hayo mawili yana uwezo wa kuhifadhi tani 5,000 za nafaka.

“Licha ya soko hili kuwapa wakulima wetu fursa ya kupata masoko ya kuuzia mazao yao, pia  watapata mafunzo ya namna ya kuhifadhi bidhaa zao pamoja na taarifa za masoko.”

Kadhalika, Waziri Mkuu ameiagiza bodi ya soko hilo kuhakikisha inatoa matangazo katika vyombo mbalimbali vya habari ili wakulima waweze kupeleka mazao yao sokoni hapo.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amewataka wananchi kutumia vizuri mvua zinazoendelea kunyesha nchini kuandaa mashamba, kupanda mazao mbalimbali ya chakula na biashara.

“Nawaagiza viongozi wa kata na vijiji hakikisheni wananchi katika maeneo yenu wanaandaa mashamba na kupanda kwa wakati, tunataka tuwe na chakula  cha kutosha na ziada tuuze.”

Awali, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Songea, Martin Mtani ameiomba Serikali iwapatie mashine itakayowawezesha kupanga madaraja ya mazao ya nafaka mbalimbali.

Mkurugenzi huyo ameomba soko hilo liwekwe kwenye mpango wa kujengewa vihenge vyenye uwezo wa kukausha mazao kwa viwango vya kimataifa ili kutatua tatizo la unyaufu.

Pia Mkurugenzi huyo ameiomba Serikali iwasaidie katika kuliunganisha soko hilo na TMX ili waweze kuuza mazao ya nafaka ndani na nje ya nchi .

Ufunguzi huo umehudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenister Mhagama na Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga.

Wengine ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Christina Mndeme na maafisa wengine wa Serikali.

Jipatie Dawa ya Asili ya Kupunguza Maziwa, Kupunguza Tumbo,Kuongeza Unene, Kuongeza Maumbile ya Kiume na Kuondoa Chunusi

$
0
0
Anza mwaka 2019 na mambo mapya kutoka kampuni ile ile inayofanya vizuri TANZANIA na nchi za NJE ambayo ni @natural_beauty_prod.

           BADO TUNATOA OFFA KAMA IVI👇👇👇
1. SHARK POWER--Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza uume urefu na upana mpaka nchi 7.5 ilikua inapatikana kwa @170,000/= sasa ni @160,000/= tu

2.VIGA 84000---Hii dawa ya kuspray yenye uwezo mkubwa wa kuchelewesha wakati wa tendo la ndoa ilikua ni  @160,000/=. Sasa ni 150,000/= tu

3. HANDSOME UP ORIGINAL-- Hichi ni kifaa cha kuongeza maumbile kwa size uipendayo wewe pamoja na kuimalisha misuli kifaa hichi kilikua kinapatikana kwa @230,000/=. Sasa ni 210,000/= tu

4. MAXMAN CAPSULE--- Hii ni dawa ya vidonge ya kuongeza uume urefu na upana pamoja na kuongeza nguvu za kiume kwa wiki mbili ilikua inapatikana kwa @200,000/=. Sasa ni 180,000/= tu

5. VIG RX---- Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza uume urefu na upana mpaka nchi 10 ilikua inapatikana kwa @190,000/=. Bei ya sasa ni 170,000/=

6. BODY BOOSTER---Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri ilikua inapatikana kwa @150,000/=. Sasa ni 140,000/=

7. BOTCHO MULT PLUS-- Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza (hips mapaja na makalio) kwa size uipendayo ilikua inapatikana kwa @200,000/=. Sasa ni 180,000/=

8. WHITE COLLECTION---- Ni vidonge vya kuwa mweupe mwili mzima pamoja na kuwa soft ilikua inapatikana kwa @150,000/= Sasa ni @140,000/= tu

9. BOTCHO HOLOGRAM CREAM--- Hii ni dawa ya kuongeza hips na makalio ilikua inapatikana kwa@180,000/= Sasa ni@160,000/=       

N.K

Wasiliana nasi kwa simu
NO:. +255 759029968  AU +255 659618585
Popote ulipo utapata huduma zetu.

Pia hakikisha unapatiwa risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ununuapo bidhaa kampuni hii.
               WELCOME ALL

Rayvanny Ataja sababu ya kubadili muonekano wake wa nywele

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Rayvanny ameeleza sababu ya kubadili muonekano wake wa nywele.

Muimbaji huyo kutokea WCB akizungumza na Wasafi TV amesema kwa kawaida msanii anatakiwa kuwa na muonekano wa tofati tofauti na ndicho alichokifanya kwa sasa.

"Muda mwingine msanii unatakiwa uwe unabadilika sio panki kila siku. Mtaanza matusi yenu toa, toa, sitoi huo ndio muonekano wangu," amesema Rayvanny.

Kwa sasa Rayvanny anafanya vizuri na wimbo 'Paranawe' ambao ameshirikishwa na Harmonize.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images