Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya January 2


Rais Magufuli Ashika Nafasi ya Pili ya Viongozi Barani Afrika Waliofanya Vizuri 2018

$
0
0

Rais John Magufuli ameshika nafasi ya pili kati ya marais watano bora Afrika kwa mwaka 2018 kutokana na kazi aliyoifanya ndani ya miaka mitatu ya utawala wake, jarida la mtandaoni la Africa54 limebainisha.

Jarida hilo lilifanya utafiti wake kwa kuuliza wasomaji wake nani ni Rais bora kwa mwaka wa 2018, kiongozi ambaye hafanani na viongozi wengine wa Afrika; ufanisi wake katika kazi, msimamo, ujasiri na uongozi na matokeo makubwa.

Africa54 limebainisha kwamba, Rais Magufuli amefanya maajabu katika muda wa miaka mitatu ambao amekaa madarakani kuliko kiongozi mwingine. Ameweza kutoa elimu bure, amefufua shirika la ndege na kununua ndege saba, ameanza kujenga reli ya kisasa (SGR) na ameongeza upatikanaji wa huduma za afya. Pia anafahamika kwa kupiga vita rushwa na ufisadi.

Nafasi ya kwanza kwa mujibu wa utafiti huo imechukuliwa na Rais wa Botswana, Ian Khama. Jarida hilo limeandika Rais Khama ni kiongozi mtulivu ambaye ameleta mabadiliko makubwa ya kijamii na kiuchumi ikiwamo kuboresha miundombinu, upatikanaji wa huduma za jamii na upatikanaji wa ajira nchini kwake.

Limesema licha ya kuwa kiongozi huyo amestaafu Aprili mwaka huu, bado Waafrika wengi wanamuona kama kiongozi bora ambaye hana mfano barani Afrika.

Nafasi ya tatu imekwenda kwa Waziri Mkuu wa Ethiopia, Abiy Ahmed ambaye aliingia madarakani Aprili mwaka huu inaonyesha kuwa alipendwa ghafla na wananchi wengi nchini humo.

Africa54 limesema kiongozi huyo amefanikiwa kuibadilisha Ethiopia kuwa nchi ya kidemokrasia zaidi na jamii iliyo huru.

Ghulib-Fakim wa Mauritius anachukua nafasi ya nne miongoni mwa marais bora wa Afrika. Jarida hilo linabainisha licha ya kuondolewa madarakani kwa kashfa ya kadi ya malipo, alisimamia haki na maendeleo ya watu katika nchi yake.

Nafasi ya tano inakwenda kwa Rais Paul Kagame wa Rwanda. Limesema licha ya kiongozi huyo kuminya demokrasia, Waafrika wengi wanampenda kwa sababu amefanikiwa kulibadilisha Taifa lake kuwa kitovu cha uchumi Afrika Mashariki.

Credit: Mwananchi

Video Mpya ya Patoranking - Everyday

$
0
0
Muimbaji kutoka nchini Nigeria, Patoranking anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake unaokwenda kwa jina la Everyday. Itazame hapa.

Fid Q na mpenzi wake wafunga ndoa

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Fid Q amefunga ndoa na mpenzi wake jana. Hatua hiyo ikuja zikiwa ni siku chache zimepita tangu Fid Q alipomvisha pete ya uchumba mpenzi wake huyo.

Waziri Lukuvi: Misimamo ya Rais Magufuli Kuhusu Kulinda Rasilimali za Nchi Haijawafurahisha Wazungu

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya  Makazi, William Lukuvi, amesema chanzo cha baadhi ya nchi wahisani kugomea kutoa misaada kwa Tanzania kunatokana na msimamo wa Rais Dk. John Magufuli kuhusu kulinda rasilimali za nchi.

Kwa mujibu wa Lukuvi msimamo huo haujazifurahisha nchi hizo na kuamua kuweka masharti magumu katika misaada yao kwa Tanzania.

Waziri Lukuvi, alitoa kauli hiyo usiku wa kuamkia jana, wakati wa mkesha wa kukaribisha mwaka mpya  wa 2019, uliofanyika Kariakoo, Dar es Salaam ambapo alimwakilisha Rais Magufuli.

Waziri Lukuvi, alisema pamoja na hali hiyo, bado Serikali imeendelea kuwa imara na kuhakikisha inakusanya kodi za ndani ili kuweza kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo ikiwamo ya umeme wa maji wa Rufiji (Stiegler’s Gorge). 

“Leo (jana) tupo kwenye mkesha hapa, hakika nawaomba endeleeni kumwombea kwa dhati Rais Magufuli ili Mungu azidi kumpa nguvu na baraka za kuliongoza Taifa letu.

“Mnakumbuka hivi karibuni Tanzania kupitia Bunge, ilipitisha sheria ya kulinda rasilimali zetu za nchi (Sheria ya Madini ya mwaka 2017),baada ya kuanza kutumika mabwana wakubwa (wahisani) imewauma, sasa tunahitaji kujenga nchi inayokwenda kwa kasi kwa maendeleo na leo haya yote yanaonekana chini ya Rais Magufuli,” alisema Lukuvi.

Alisema pamoja na misimamo ya wahisani, bado Taifa linaendelea kupiga hatua kwa kasi ikiwamo kujenga miradi mkubwa kama wa reli ya kisasa (SGR).

Akizungumzia kero ya maji, alisema kwa sasa utekelezaji wa miradi ya maji kwa wananchi hali imekuwa ni nzuri huku lengo la Serikali ni kutaka kuona Watanzania wote wanapata huduma hiyo wakati wote.

Licha ya hali hiyo, alisema amekuwa akifanya mambo mengi makubwa  ambapo alitangaza kuanzia jana halmashauri zote zitaanza kutoa leseni za makazi kwa waliojenga kwenye maeneo ambayo hayajapangwa.

“Kuanzia kesho (jana) halmashauri zote ninaziagiza zianze kutoa leseni za makazi kwa wale waliojenga kwenye maeneo ambayo hajapimwa. Leseni hizo zitakuwa za miaka mitano na baada ya muda maeneo hayo yatapimwa na kupewa leseni. Lakini hata ukipewa leseni nenda kalipe kodi ya ardhi.

“Nami ninaawaambia Watanzania endeleeni kumwombea Rais Magufuli, maana hata sisi wasaidizi wake tumekuwa tukipata faraja kutokana na namna kiongozi wetu  anavyojitoa kwa ajili ya Watanzania.

“Tangu tumeingia madarakani, pale wizara ya ardhi hakuna migogoro mipya zaidi ile ya zamani ambayo ilikuwa inatengenezwa na watu wachache kwa masilahi yao.

“Tumuunge mkono Rais Magufuli tunataka nini, kila siku amekuwa akiweka mambo sawa sasa wafanyabiashara nchi nzima wamepewa vitambulisho aliyetenegeza ni Rais Magufuli twendeni tumuunge mkono kiongozi wetu kwa ajili ya Taifa letu,” alisema.

Akijibu hoja ya kuzuiwa kufanya maombi  Uwanja wa Taifa, Lukuvi alisema analichukua suala hilo na kulifikisha kwa Waziri wa Habari, Michezo, Sanaa na Utamaduni, Dk. Harrison Mwakyembe.

Awali akiendesha dua maalumu kwenye mkesha huo ,mwenyekiti wa mkesha mkubwa kitaifa, Askofu Dk. Godfrey Malassy wa Tanzania Fellowship of Churches, alishukuru serikali kwa upendo wake kwa Watanzania.

Pamoja na hali hiyo, waliwaombea viongozo mbalimbali, ikiwamo Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge, Job Ndugai pamoja na Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma.

Wengine waliombewa kwenye mkesha huo mawaziri, wabunge, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, wakuu wa mikoa na wilaya, viongozi wa dini pamoja na Watanzania wote.

UVCCM Wataka Muungano Wetu Ulindwe

$
0
0
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) umetoa mwito kwa Rais John Magufuli na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, kuhakikisha hakuna chokochoko dhidi ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
 
Hayo yamesemwa na Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa,
Tabia Mwita, wilayani Tarime, Mara kwenye kikao cha Baraza Kuu la umoja huo wilayani hapa.
 
Amesema waasisi wa Muungano, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Sheikh Abeid Aman Karume, wanapaswa kuenziwa kwa kuulinda muungano. Amesema amani ya nchi ndiyo daraja la maendeleo.
 
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Tanzania uliasisiwa Aprili 26, 1964.
 
Mwita amesema migogoro sharti ipatiwe suluhu. “Mfano, hapa Tarime kuna migogoro mingi ya ardhi…viongozi wa serikali wapo, lakini haiishi. Sasa nakwenda kumwambia Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,” amesema.
 
Kuhusu ajira, amesema ni kilio cha dunia nzima. “Shirika la Kazi Duniani (ILO), limesema changamoto ya ajira ni ya dunia nzima. Kazi na ajira ni vitu viwili tofauti. 

Kazi maana yake mtu anafanya kazi yoyote bila kujali ameajiriwa ili kujipatia kipato. Ajira ni mtu anayesubiri aajiriwe ndipo afanye kazi,” amesema.
 
Amewataka vijana na wananchi kwa jumla kuongeza juhudi katika kufanya kazi badala ya kusubiri ajira.
 
Amesema wakati viongozi wakuu wa serikali wakipambana kukuza uchumi, vijana wana wajibu kuhakikisha chama hicho kinashinda uchaguzi, akisema ushindi ni lazima. 
 
Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Tarime, Godfrey Francis, amesema wanajiandaa kuingiza basi litakalokuwa kitega uchumi cha umoja huo.
 
“Pia tunatafuta mbia atujengee jengo la kitega uchumi la ghorofa tano hapa Tarime. Hatutaki mchezo,” alisema Francis na kuongeza;
 
“Lakini ni fursa wenyeviti wa vijana na viongozi wote, mtu yeyote anayemkosoa vibaya Mwenyekiti wetu wa CCM Taifa, mimi nafikiri hakuna haja ya kupeleka kesi polisi. Sisi tupige, wao ndio wakashtaki wenyewe.
 
“Ndiyo kazi kubwa sisi tunayo. Kama kiongozi wetu anadhalilishwa sisi tupo viongozi tunamuangalia tu, maana yake sisi pia tunamuunga huyo mkono.”
 
Kikao hicho kilihudhuriwa na Mbunge wa Viti Maalumu ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Agnes Marwa.
 
Wengine ni Katibu wa UVCCM Mkoa wa Mara, Hassan Moshi, Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Musoma, Emmanuel Nestory, Mhasibu mstaafu wa CCM Tarime, John Gimunta, na viongozi wengine kadhaa.

Bei ya Petrol, Dizel na Mafuta ya Taa nchini Yashuka

$
0
0
Bei ya mafuta nchini imeshuka kwa kati ya Sh140 hadi zaidi ya Sh230 kwa lita moja katika maeneo mengi.

Taarifa ya kila mwezi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), inaonyesha unafuu huo kwa watumiaji wa petroli, dizeli na mafuta ya taa.

Pia yale yanayouzwa bei ya jumla yameshuka kwa viwango karibu na ya rejareja.

Taarifa iliyosainiwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Ewura, Nzinyangwa Mchany inaonyesha kuwa kuanzia leo, bei ya rejareja ya petroli imeshuka kwa Sh141 wakati ile ya dizeli ikipungua kwa Sh212 na mafuta ya taa Sh167 kwa kila lita. Bei hizo ni kwa mafuta yanayopitia Bandari ya Dar es Salaam.

Hali ikiwa hivyo kwa mafuta yanayopitia Dar es Salaam, Bandari ya Tanga na ukanda wa kaskazini kwa ujumla nao bei ya rejareja ya petroli imepungua kwa Sh237 na ile ya dizeli kwa Sh138 wakati ya mafuta ya taa yakipanda kwa Sh4.

Mwezi uliopita hakuna mzigo ulioshushwa katika Bandari ya Mtwara inayohudumia mikoa ya kusini ya Lindi, Mtwara na Ruvuma itakayolazimika kuagiza nishati hiyo kutoka jijini Dar es Salaam.

Bei ya mafuta kwenye mikoa hiyo, ripoti ya Ewura inasema itakuwa sawa na Dar es Salaam ukijumlisha na gharama za usafirishaji.

Kuhusu kutotumika kwa Bandari ya Mtwara, Msemaji wa Ewura, Titus Kaguo alisema hakuna mfanyabiashara aliyepitishia mafuta yake katika bandari hiyo na mamlaka hiyo haina uwezo wa kuwalazimisha waagizaji waitumie.

Mamlaka hiyo imevitaka vituo vyote vya mafuta kubandika bei za bidhaa wanazouza sehemu ya wazi ili kila mtu aweze kuziona huku ikiwakumbusha wateja kupiga *152*00# kujua bei ya mahali walipo.

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH....Anatoa Pete za Bahati, Anasafisha Nyota, Anazuia Chuma Ulete na Mengine

$
0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam Shariff,  Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
 
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Adam Shariff Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. 

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Mawasiliaono: +255715971688  au +255756914036
 
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Habari Njema Kwa Wenye Matatizo Ya Nguvu za Kiume, vitambi, nyama uzembe

$
0
0
NAUHABARISHA ULIMWENGU TIBA BORA YA MITI SHAMBA..

  Ninatibu magonjwa 1-100 dawa ninazo Sasa.

KOLA; ni dawa ya kisukari dozi siku 14 ata kama unajihisi itumie kwa kinga zaidi

  THREE(3) POWER MIX,inatibu Nguvu za kiume Ni dawa iliyo Bora na Humfanya mume kuchelewa kufika kileleni dkk 40_47 bila kuchoka.Inaanza kufanya kazi ndani ya door 80 na inatibu kabisa ndani ya siku 6 tu,hutatumia Tena dawa ya Nguvu za kiume three power mix Ni kiboko kabisa,hata Kama unahisi una tatizo unaruhusiwa kutumia kwa ajili ya Kinga baadae.

 DUDUMA MIX 4 POWER,hunenepesha na kurefusha uume na kukomaza uume uliosinyaa kwa mda mfupi,tumia siku 4 na kupona kabisa.

  SHOOLA,Ni dawa ya kutibu tezi dume na kupona kabisa ni ya miti shamba hutumika kwa kunywa bila upasuaji ndani ya siku 14 haina madhara.

 NENGONENGO,dawa ya kutibu Uzazi kwa akina mama walioshindwa kubeba mimba kwa mda mrefu ukitumia utaweza kupata mimba na kujifungua salama.

  KAMINGO,Ni dawa inayotibu Busha bila kufanyiwa operation na aliyevimba korodani inatibu kabisa dozi Ni siku 7 na inaubora wa Hali ya just na unapona kabisa.

  IKUMBIJA,Ni dawa ya kumvuta mpenzi aliekuacha na mwenye ahadi za uongo kukutimizia,na kumkomesha mtu asiwe na mtu mwingine pia atakurudia ndani ya masaa 6.

   MALAMALA,Ni dawa ya vidonda vya tumbo na tumbo kujaa gesi, kilungulia na inafanya kazi kwa haraka zaidi na kupona kabisa ndani ya siku 6.
 

SAALA,Ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto,kiuno,mgongo,magoti na viungo vyote mwilini na joints,Sasa tiba yake Ipo kwangu.

   HALALA MIX,Ni dawa mix ya miti 100 inayotibu matatizo yote,Kama majini,kesi,biashara,kazi,mitego na kupoteza kumbukumbu. no

TUNAFANYA KAZI SIKU ZOTE PIA NAKUFIKIA POPOTE ULIPO KWA HARAKA,NAPATIKANA DAR ES SALAAM NA KAHAMA,PIA NINA MAWAKALA MIKOANI SIMIYU,SHINYANGA,MOSHI NA MBEYA.


     KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA: 0784 475946
           0744 922982
    DR,SANDALA.

Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power

$
0
0
Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power Kwaajili Ya Nguvu Za Kiuume Na Promix Kwaajili Ya Kuongeza Maumbile;

Kwa mwanaume aliyekamilika na mwenye Afya njema ili kumridhisha mke au mpenzi anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara mbili hapo utamridhisha mpenzi wako ila ukiwa unapiga moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe 

Tiba Ya Tatizo Lako Ni Dawa Hiitwayo Simpo Power No, 1; dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge vya miti shamba na unga ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja :-1 itakufanya urudie tendo zaidi ya mara tatu 
2 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-20 kwa tendo la Kwanza 
3 huimarisha uume uliolegea na kusinyaa 

Je Una Mke Au Mpenzi Aliyebalikiwa Kuwa Na Kario Kubwa Au Mwili Mnene Na Wewe Mume Wake Una   Maumbile Mafupu?; tumia sasa dawa ya PROMIX dawa itakufanya umfikishe shemu nyeti maana inaboresha maumbile saizi upendayo.

Dawa zangu haziina madhara yoyote kwa mtumiaji 

MARKSU; ni dawa ya kisukari dozi siku 21 
MWARU; ni dawa ya uzazi,hufungua milija ya uzazi ata kwa Wale waliofungiwa uzazi  
MTUNDUU; ni dawa ya busha bila kupasua 
MAZANZA; ni dawa ya kisukar zipo dawa za miguu Kuuma,tumbo,kupunguza Matiti,kutoa minyama uzembe ngiri,vidondo vya tumbo  

FIKA OFISINI KWANGU BUGURUNI MALAPA KARIBU NA KOTA ZA POLISI AU PIGA  SIMU ULETEWE MAHALI ULIPO SIMU NO : 0783185060 au 0752348593  -DR AGU

Naibu Waziri Shonza Awataka Wasanii Kujijengea Tabia Ya Kujiwekea Akiba

$
0
0
Na Vero Ignatus, Arusha
Naibu waziri wa Habarui, sanaa utamaduni na michezo Mhe. Juliana Shonza amewataka wasanii wa Injili kjijengea tabia ya kujiwekea akiba ili punde wapatapo matatizo waweze kuyatatua kwa urahisi.

Ameyasema hayo hivi karibuni alipokuwa akizindua mfuko wa Tagoane LoanFund Jijini Arusha ambapo amepongeza uongozi wa Tagoane kufikia hatua hiyo. Ameyataka mashirikisho yote ya muziki wa Injili nchini Tanzania kuiga mfano nzuri wa Tagoane ili waweze kuwa na mashirikisho ambayo ni hai na yanayoleta mshindo kwenye jamii.

Amesema yeye kama mlezi wa wasanii wote nchi amewaomba waamke wachangamkie fursa na wasiwe wavivu kujifunza kutoka kwa wenzao waliofanikiwa .Amewataka wasanii kukaa kwa pamoja Kuonyeshe Uzalendo kwa nchi yao wajadili changamoto mbalimbali wanazozipitia na kutafuta namna ya kutazua changamoto zinazowakabili.

Kwa upande wake Rais wa Tagoane Taifa Dkt. Godwin Maimu amesema kuwa wanedhamiria kuanzisha mfuko wao wa Tagoane Loan Fund ambapo mpaka sasa umekuwa na wanachama ambao wameshachangia akiba zao zipatazo shilingi milioni kumi.Amesema mfuko huo unatarajiwa kuanza kutoa mikopo kwa wanachama wavhqngiaji kuanzia 2 januari 2019

Maendeleo kama vijana hayawezi kuendelea ukiwa na jitihada za mtu mmoja mmoja bali balintunapounganisha nguvu zetu kwa pamoja mwisho wa siku tunapata kitu cha kuweza kutusaidia. Alisema Dkt Maimu

Amesema lengo la mfuko huo ni kuwakwamua wasanii watakaokuwa na miradi ya uwekezaji, makampuni makubwa, na watakaoweza kutoa fursa na ajira kwa vijana hapa nchini na kulipa kodi kama wananchi wengine

Aidha tamasha hilo lililoshorikisha wasanii mbalimbali wakiwemo wajasiriamali, wachoraji, wachongaji, sanaa za ubunifu ni fursa ambayo Tagoane wameileta na kuwataka wasanii waitumie kwaajili ya kujikwamua kiuchumi na kuoata maendeleo katia jamii nzima

Tamasha hilo la Tukuza festival lilizinduliwa rasmi mwaka 2017 likiwa linafanyika kwa mara ya pili limebeba kauli mbiu isemayo toto yatima haihitaji chakula a mavazi peke yake ila awezeshwe nyenzo za kutimiza malengo yake.

Ujumbe wa Mwaka Mpya Alioutoa Katiku Mkuu CHADEMA Dkt. Vicent Mashinji

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Deokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Vicent Mashinji amewataka  watanzania pamoja na dunia kujiandaa kuipokea serikali mpya chini ya chama anachokiongoza.
 
Dkt. Mashinji ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter, akisisitiza wananchi kuielewa na kuipokea sera mbadala ya chama hicho.

"Pokeeni Sera Mbadala na jiandaeni kuipokea Serikali mpya inayoongozwa na CHADEMA baada ya October 25, 2020," amesema  Dkt. Mashinji.
Aidha kiongozi huyo ametoa ujumbe kwa watu wasiopenda siasa kwa kuwakumbusha kwamba siasa ni utaratibu mzima wa kufanya maaamuzi katika jamii hivyo waipende na wasiichukie.

"Wasiopenda siasa, waambieni hivi “siasa ni utaratibu mzima wa kufanya maamzi katika jamii au kundi fulani la watu ikiwemo familia, na pili, ni matumizi ya mamlaka katika kutekeleza maamzi hayo. Tafadhari Watanzania wenzangu tuipende, tuifanye na tuiishi Siasa" Dkt. Mashinji.

Tamko La Wizara Ya Afya Kulaani Vitendo Vya Ukatili Wa Watoto Majumbani

$
0
0
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inalaani na kukemea vikali vitendo vya ukatili dhidi ya watoto vinavyoendelea kujitokeza nchini. Vitendo hivi vinafanywa na kuhusisha ndugu na walezi wa karibu wa wataoto hivyo kuzua hofu kubwa kwa watoto na jamii kwani vinaathiri malezi na makuzi ya awali ya watoto kwa kutozingatia haki zao za msingi.

Mapema wiki hii, imeripotiwa  mwalimu wa shule ya msingi jijini Dodoma  (jina limehifadhiwa) ambaye anatuhumiwa kumfungia mtoto mdogo ndani ya kabati kwa kipindi kirefu na kusababisha afya ya mtoto huyo kudhohofika. Mwalimu huyo anatuhumiwa pia kumfanyia vitendo vya ukatili mama mzazi wa mtoto  huyo kwa kumpiga na kumsababishia maumivu mwilini yaliyopelekea binti huyo na mtoto wake kulazwa.

Kipekee, Wizara inawapongeza wanajamii wote walioibua tukio hili na kuwezesha Jeshi la Polisi kumkamata mtuhumiwa kwa ajili ya uchunguzi ili Sheria iweze kuchukua mkondo wake. TunaaminiJeshi la Polisi watafanya upelelezi wa tukio hili kwa weledi mkubwa ili hatua stahiki za kisheria ziweze kuchukuliwa.

Matukio ya ukatili wa watoto yanapotokea majumbani yanarudisha nyuma jitihada za Serikali za kulinda na kuendeleza haki na ustawi wa watoto katika ngazi ya familia ambayo ndio kitovu cha jamii wakiwemo na watoto.

Kufuatia kitendo hicho kilichofanywa na mwalimu wa shule ya msingi ambaye ni mlezi wa watoto, Wizara inawataka wazazi, walezi na jamii kuzingatia wajibu wa ulinzi wa watoto ili kuwahakikishia usalama wao katika maeneo ya majumbani, shuleni, mtaani, njiani na katika jamii kwa ajili ya kutekeleza lengo la kupunguza matukio ya ukatili kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2021/2022.

Aidha, Wizara inatoa rai kwa jamii na wananchi wema kuwa makini na matumizi ya mitandao ya kijamii ili kuepuka makosa ya kisheria yanayoweza kutokea kwa kusambaza, kuchapisha na kupiga picha za watoto ambao ni wahanga wa ukatili na kuziweka wazi kinyume na Sheria ya Mtoto Na. 21 ya Mwaka 2009.

Wizara inatoa pole kwa wazazi, ndugu, marafiki na familia ya mtoto aliyefanyiwa ukatili huo. Tunawaomba wanajamii kuendelea kutoa ushirikiano katika kufichua vitendo vyote vya ukatili dhidi ya watoto vinavyojitokeza katika maeneo yao. Aidha, katika kipindi hiki ambapo uchunguzi unaendelea kufanyika tunaomba pawe na utulivu na uvumilivu ili kutoa nafasi kwa vyombo vya dola kufanya uchunguzi kwa makini na Sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Imetolewa na
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto
(Idara Kuu Maendeleo ya Jamii)
02/01/2019

Rudisha heshima yako Kwa Mpenzi Wako, Mke Wako...Tumia Tiba Hii ya Asili

$
0
0
Rudisha heshima yako sasa kwa kutumia Dawa hii iitwayo SUPER GAFINA, kwa ajili ya nguvu za kiume na NKOLOMIJE ni kwaajili ya kuongeza maumbile.

Kwa mwanaume aliye kamilika anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara mbili ,ila ukiwa unapiga moja tena kwa shida wewe ujue  unamatatizo ya upungufu wa nguvu za kiume.

TIBA YA TATIZO LAKO NI; Dawa iitwayo SUPER GAFINA, dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge na unga wa asili ambavyo havina madhara kwa mtumiaji ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja;-

1).itakufanya urudie tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuchoka.

2).ltakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dk.15 hadi 20 kwa tendo la kwanza.

3).lnaimarisha uume uliolegea na uliosinyaa na kuupa nguvu maradufu.

Je unamaumbile madogo pamoja na uume mfupi? NKOLOMIJE ni suluisho la tatizo lako. Na ni dawa inayoboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi kuanzia inch. 5 hadi 8 kwa muda mfupi sana .Dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk.30 ukisha tumia guarantee miaka 50  ikishakutibu.

Pia ninatibu;- KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU, MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE ,BP, NK.

IGULYATI, ni dawa ya mvuto wa biashara, kazi,kupandishwa cheo na humfanya mfanyakazi kupendwa na mwajiri wake. Pia humvuta mke,Mme,hawara ,mchumba unae muitaji utampata kwa dk.30 tu na atatulia na kumfunga asitoke nje ya ndoa, Pia natoa Pete za bahati ambazo zimetajirisha wengi.

Pia ipo dawa ya kupunguza matiti,unene ,tumbo,na kitambi ,hupunguza mafuta ,kuondoa makovu,chunusi,michilizi mwilini na kuongeza hipsi, makalio na mguu wa bia nk. 

Kwa maelezo zaidi wasiliana na DR,HOSUTWA .Anapatikana Mbagara

Simu no, 0756241666 na 0672186977.

       Huduma hii utaipata popote ulipo

Waziri wa Kilimo: Tanzania ina ziada ya Tani 3,013,515 za mazao ya chakula

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Kwa mliganisho wa mahitaji na uzalishaji nchi ina ziada ya tani 3,013,515 na imejitosheleza kwa asilimia 123 na 120 mtawalia ambapo uzalishaji katika msimu wa 2016/2017 na 2015/2016 ulikuwa tani 15,900,864 na 16,172,841 mtawalia ambapo mahitaji ya chakula yanayoendana na uzalishaji huo ni tani 13,159,326, na 13,300,034 kwa mwaka wa ulaji 2017/2018 na 2016/2017 mtawalia.

Uzalishaji wa mazao ya chakula katika msimu wa uzalishaji wa 2017/2018 ulifikia tani 16,981,974 zikiwemo tani tani 9,537,857 za mazao ya nafaka na tani 7,354,117 mazao yasiyo nafaka, kiwango ambacho kimeiwezesha nchi kutosheleza mahitaji yake ya chakula ya tani 13,569,285 katika mwaka 2018/2019 kwa kiwango cha utoshelevu (Self Sufficiency Ratio-SSR) cha asilimia 124.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameyasema hayo tarehe 2 Januari 2019 wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano maarufu kama Kilimo IV Jijini Dodoma.

Alisema Uzalishaji wa mahindi katika msimu wa 2017/2018, 2016/2017 na 2015/2016 ulikuwa ni tani 6,273,150; 6,680,758 na 6,148,699 mtawalia,wakati mahitaji yanayoendana na uzalishaji huo ni tani 5,462,390; 5,407,499 na 5,202,405 katika miaka ya ulaji ya 2018/2019, 2017/2018 na 2016/2017, Ambapo ziada ya tani 810,760(2018/2019); 1,273,259(2017/2018)  na 946,284(2016/2017) zilipatikana.

Uzalishaji wa mchele katika msimu wa 2017/2018, 2016/2017 na 2015/2016 ulikuwa ni tani 2,219,628; 1,593,609; na 2,229,071 mtawalia,mahitaji yanayoendana na uzalishaji huo ni tani 990,044; 924,435; na 976,925 katika miaka ya ulaji ya 2018/2019, 2017/2018 na 2016/2017,Ziada ya tani 1,229,583(2018/2019); 669,175(2017/2018) na 1,252,146(2016/2017) zilipatikana.

Mhe Hasunga alisema kuwa kutokana na ziada hizo za uzalishaji nchi imeendelea kuwa ghala la chakula kwa nchi jirani. Kwa mfano, kulingana na takwimu za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), katika kipindi cha mwezi Juni 2017 hadi Juni 2018 jumla ya tani 64,477.95 za Mahindi zenye thamani ya shillingi billioni 90.6 na Maharage tani 99,434.45 zenye thamani ya shillingi bilioni 222.0 ziliuzwa katika nchi za DRC, Rwanda, Burundi, Kenya, Uganda, Sudan ya Kusini na Uarabuni.

Hasunga aliongeza kuwa Kati ya mwaka 2015/2016 na 2017/2018 uzalishaji wa mazao ya Asili ya Biashara umeongezeka kwa viwango tofauti tofauti, ambapo zao la korosho kwa sasa linalimwa katika mikoa 17 na Halmashauri 90 hapa nchini baada ya kuanza kwa mpango wa kuongeza uzalishaji wa zao la korosho mnamo mwaka 2013/2014 kupitia uhamasishaji wa kilimo hicho katika mikoa mipya.

Amesema kuwa Mikoa ya asili inayoongoza kwa kilimo cha zao la korosho ni Mtwara, Lindi, Ruvuma, Pwani na Tanga. Katika miaka ya hivi karibuni mikoa mingine mitano nayo imeanza kuzalisha korosho kwa kiasi kidogo ambayo ni Singida, Dodoma, Morogoro, Mbeya na Njombe.

Alisema kuwa taarifa ya uhakiki na malipo kwa wakulima mpaka kufikia tarehe 29 Desemba 2018 tayari Vyama vilivyohakikiwa na kulipwa ni 450.

Malipo yaliyohakikiwa na kuwasilishwa benki ni tsh 231,937,341,674, Malipo yaliyolipwa katika akaunti za Wakulima ni tsh 210,485,753,571, Korosho iliyolipiwa ni Kilo 70,284,043, Kiasi cha Korosho iliyokusanywa katika maghala makuu ni Tani 195,175.844, na Kiasi cha Korosho iliyosombwa na kupelekwa katika maghala ya Hifadhi ni Tani 35,175.844

Katika taarifa yake na waandishi wa habari Mhe Hasunga ameeleza kuwamatumizi ya mbegu bora za pamba yameongezeka kutoka tani 14,500mwaka 2015/2016 hadi tani 18,500 mwaka 2017/2018 na matarajio ni kufikia tani 25,000 msimu wa 2018/2019. Mpaka sasa kiasi cha mbegu tani 27,769 zimesambazwa na ni asilimia 37 zaidi ya kiasi kilichoombwa na Wilayaambacho kilikuwa tani 20,284.

Aidha, Uzalishaji wa chai kavu umeongezeka kutoka tani 32,628 mwaka 2015/2016 hadi kufikia tani 34,010 mwaka 2017/2018. Matumizi ya mfumo wa ushirika umeongeza bei ya kilo moja ya majani mabichi kutoka wastani wa Shilingi 251 mwaka 2015/16 hadi  shilingi 314 mwaka 2017/18. Thamani ya mauzo ya chai nje ya nchi imeongezeka kutoka Dola za kimarekani51,794,854.00 mwaka 2015/2016 hadi kufikia Dola za kimarekani62,167,167.00 mwaka 2017/2018.

Kuhusu zao la Mkonge uzalishaji umeongezeka kutoka tani 39,393 mwaka 2015/16 hadi tani 43,279 mwaka 2017/18. Bei ya tani moja ya Katani daraja la UG mwaka 2015/2016 ilikuwa Shilingi 2,200,000 na mwaka 2017/2018 imefikia Shilingi 3,330,000 sawa na asilimia 50. Thamani ya mauzo ya singa nje ya nchi ni kutoka dola za Kimarekani 35,991,161 mwaka 2015/16 hadi dola za Kimarekani 45,835,845 mwaka 2017/18.

Akieleza kuhusu zao la Sukari Waziri Hasunga amesema kuwa Serikali imeimarisha udhibiti wa uingizaji holela wa sukari kutoka nje hali iliyoimarisha soko la sukari nchini.

Udhibiti huo umechochea ongezeko la uzalishaji wa sukari kutoka tani 293,075 mwaka 2015/2016 hadi takriban tani 307,431.14 mwaka 2017/2018. Aidha, uzalishaji wa sukari unatarajiwa kuongezeka na kufikia tani 352,600 mwaka 2018/2019.

Vilevile, Serikali imeratibu uanzishwaji wa mashamba mapya ya miwa ya Mkulazi I (Ngerengere), Mkulazi II (Mbigiri) na Shamba la Bakhresa –Bagamoyo Sugar (Makurunge).  Sekta ya Sukari kwa ujumla inatoa ajira isiyo ya moja kwa moja kwa watu 57,000 pamoja na kutoa fursa ya ajira kwa watu wengine takriban 75,000 ambao wanahusika na shughuli zinazotoa huduma kwenye mnyororo wa thamani wa uzalishaji wa sukari nchini.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Waziri wa Nishati autaka Mgodi wa GGM kutumia umeme wa gridi ili walipe kodi stahiki.

$
0
0
Na Veronica Simba, Geita
WAZIRI Nishati Dk. Medard Kalemani amesema kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa mtambo wa kupoza umeme unaotarajiwa kujengwa Geita, kutawezesha serikali kupeleka umeme wa gridi ya taifa katika Mgodi wa Dhahabu wa Geita (Geita Gold Mine – GGM) na kuondoa sababu ya wao kutokulipa kodi stahiki kwa serikali kwa kigezo cha kutumia mafuta katika uzalishaji.
 
Akikagua eneo utakapojengwa mtambo huo, nje kidogo ya mji wa Geita, Desemba 31 mwaka huu, Waziri Kalemani alisema mtambo huo utafua umeme wa megawati 100 hivyo pamoja na kuwanufaisha wananchi wa Geita na maeneo jirani; utatosheleza pia mahitaji ya mgodi husika ambayo ni takribani megawati 25.
 
“Ni matumaini yangu, kufikia Desemba 2019, GGM watakuwa wameanza kutumia umeme wa gridi ya taifa ili waanze kulipa kodi stahiki kwa serikali. Waache kupata msamaha wa kodi wanaopata sasa kutokana na kuingiza mafuta wanayotumia kuendeshea shughuli zao mgodini,” alisema Waziri.
 
Waziri Kalemani aliongeza kwamba, kuwaunganisha GGM na umeme wa gridi, kutakamilisha azma ya serikali kuwaunganishia umeme wachimbaji wa madini wakubwa wote nchini kwani kwa sasa ni mgodi huo pekee uliobaki.
 
Alimtaka Meneja wa TANESCO Mkoa wa Geita, Mhandisi Joackim Ruweta kuwapa taarifa uongozi wa mgodi huo ili waanze kufanya maandalizi ya kuupokea umeme kwenye miundombinu yao.
 
Akizungumzia kuhusu mradi wenyewe, Waziri Kalemani alieleza kuwa serikali imetoa takribani shilingi bilioni 23 kwa ajili ya kuujenga ili kuboresha hali ya upatikanaji umeme kwa wananchi wa Geita na maeneo jirani.
 
Alisema mradi unahusisha kusafirisha umeme mkubwa kutoka Bulyanhulu, umbali wa kilomita 55 hadi Geita.
 
Aidha, alisema kuwa taratibu zote za maandalizi zimekamilika hivyo akamtaka mkandarasi atakayetekeleza mradi huo, ambayo ni kampuni ya CAMC Engineering kutoka China kuanza mara moja shughuli za ujenzi, ambao kwa mujibu wa mkataba utakamilika ndani ya kipindi cha miezi 17.
 
“Pamoja na kuwa mkataba unabainisha muda wa kukamilisha ujenzi ni miezi 17 lakini tumekubaliana na mkandarasi ajitahidi kukamilisha ndani ya miezi 12,” alifafanua Waziri.
 
Akizungumzia majukumu ya mkandarasi kwa mujibu wa mkataba, Waziri Kalemani alisema yanajumuisha ujenzi wa mtambo wenyewe wa kupoza umeme katika eneo la Mpomvu, nje kidogo ya mji wa Geita, ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Bulyanhulu hadi eneo la mtambo, umbali wa kilomita 55 pamoja na kazi ya kusambaza umeme kwenye vijiji 11 vinavyopitiwa na mradi vikiwemo vya Nyantororo na Buyagu.
 
Waziri aliagiza mambo kadhaa yafanyike katika utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo ambayo ni pamoja na kujenga uzio kuzungushia eneo husika kwa sababu za kiusalama pamoja na kuepusha watu kuvamia eneo husika na kujenga makazi.
 
Pia, aliagiza kuanza mara moja kwa kazi za kusafisha eneo husika pamoja na kutoa elimu kwa wananchi ambako mradi unapita ili wajue namna ya kujiandaa kuupokea mradi husika.
 
Waziri Kalemani alikuwa katika ziara ya kazi kukagua utekelezaji wa miradi ya umeme ambapo mbali na kukagua eneo utakapojengwa mtambo huo, aliwasha umeme Katoro na Buseresere katika vijiji kadhaa pamoja na kuzungumza na wananchi.

Mtoto wa Miaka 15 Amuua Mwenzake wa Miaka 16 Kwa Panga

$
0
0
Mwanafunzi wa kidato cha pili Shule ya sekondari Naisinyai wilayani Simanjiro Mkoa wa Manyara Godfrey Otieno (16) amefariki dunia kwa kukatwa panga kichwani na rafiki yake baada ya kumtania kwa kumwita albino.

Watoto hao ambao ni marafiki na majirani walikuwa pamoja wakisubiria kushangilia mwaka mpya wa 2019 ambao uligeuka kuwa kilio.

Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Manyara, Agostino Senga amesema tukio hilo limetokea Desemba 31, 2018 saa tatu usiku katika kitongoji cha Songambele kata ya Mirerani wilayani Simanjiro.

Amemtaja anayedaiwa kufanya mauaji hayo ni George Damas (15) mwanafunzi aliyemaliza shule ya msingi hivi karibuni na kufaulu, alikuwa akisubiri kupangiwa shule ya sekondari.

Ametaja chanzo cha kifo hicho ni utani kwani Otieno alimtania mwenzake kwa kumwita albino ndipo akakasirika na kuchukua panga na kumkata kichwani.

Amesema wanamshikilia Damas huku wakiendelea na uchunguzi wa tukio hilo kabla ya kumfikisha mahakamani.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza Lakamata Bhangi Kilo 110

$
0
0
Jeshi la Poliisi Mkoa wa Mwanza kwa kutumia kikosi chake kabambe chenye uweledi uliotukuka tumefanikiwa kuwakamata watu watatu kwa kosa la kupatikana na dawa za kulevya aina ya bhangi kiasi cha kilogramu 110, huko mtaa wa Ngumo “A”, Wilayani Kwimba.

Tukio hilo limetokea tarehe 01.01.2019 majira ya saa 21:00hrs, hii ni baada ya kikosi hicho mahiri cha askari wakati kikiwa doria na misako kilipokea taarifa toka kwa wasiri kwamba katika mtaa wa Ngumo ”A” na Safari club wapo watu wanaojihusisha na utumiaji na uuzaji wa dawa za kulevya. Ndipo askari walifanya ufuatiliaji na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao watatu wakiwa na kiasi hicho cha dawa za kulevya aina ya bhangi.

Watuhumiwa waliokamatwa na dawa hizo za kulevya aina ya bhangi ni;

Consolatha Elias, miaka 52, mkazi Ngumo “A”, huyu amekamatwa na dawa za kulevya aina ya bhangi kiasi cha kilogramu 100.

Emmanuel Lucas, miaka 21, mkazi wa kijiji cha Manguluma, na Rehema Joseph, miaka 27, mkazi wa Chato, hawa wawili wamekamatwa na dawa za kulevya aina ya bhangi kiasi cha kilogramu 10.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza tunaendelea na mahojiano na watuhumiwa wote watatu ili kuweza kubaini watu wanaoshirikiana nao katika uuzaji, utumiaji na usafirishaji wa dawa hizo za kulevya aina ya bhangi. Aidha pindi uchunguzi ukikamilika watuhumiwa wote watatu watafikishwa mahakamani ili hatua stahiki za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, tunatoa onyo kwa baadhi ya wananchi waojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya kuwa waache kwani ni kinyume na sheria na endapo mtu atabainika hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa dhidi yake. Vilevile tunawaomba wananchi waendelee kutupa ushirikiano kwa kutupa mapema taarifa za uhalifu na wahalifu ili waweze kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Imetolewa na;
Jonathan Shanna – ACP
Kamanda wa Polisi (M) Mwanza.
02 January, 2019.

Sakata la Kikokotoo Lawaibua Tena CHADEMA....Tazama hapa Alichokisema Bulaya

$
0
0
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetaka suala la kikokotoo liwasilishwe bungeni na lijadiliwe kwa hati ya dharura ili iwe sheria itakayomnufaisha kila mstaafu.

Akizungumza na waandishi wa Habari katika ofisi za Makao makuu ya Chama hicho Waziri Kivuli ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira, Vijana na watu wenye Ulemavu Mh Ester Bulaya amesema pamoja na Rais wa Tanzania Dr John Magufuli kurudisha kikokotoo cha awali lakini bado haijawa sheria rasmi hali inayosababisha ubaguzi wa mafao kwa wastaafu.

Desemba 28, 2018 Rais Magufuli aliagiza kurejeshwa kwa utaratibu wa zamani wa wastaafu serikalini wa kupewa mafao ya mkupuo ya asilimia 50 badala ya asilimia 25 yaliyopendekezwa katika kanuni hizo mpya.

Akizungumza na waandishi wa habari Bulaya ambaye ni mbunge wa Bunda (Chadema), amesema alichokifanya Rais ni kama kutoa huduma ya kwanza kwa majeruhi wa ajali na uamuzi wake huo ukitungiwa sheria ni sawa na kutoa matibabu.

"Rais ametoa huduma ya kwanza kwa mgonjwa sasa anahitaji matibabu ili asife. Serikali inapaswa kupeleka bungeni marekebisho ya sheria kwa hati ya dharura kwa ajili ya kipindi cha mpito, isipofanyika hivyo hiki kitakuwa kicheko cha muda tu," amesema Bulaya.

Amesema sheria hiyo itatoa ufafanuzi wa mambo mengi kama fao la kujitoa lakini pia suala ambalo wafanyakazi walilalamikia la kuwa na uwakilishi mdogo katika bodi inayofanya uamuzi.

Bulaya amesema hatua kadhaa zinapaswa kuchukuliwa kuhusu suala la mafao ikiwamo Serikali kulipa madeni yake yote katika mifuko ya hifadhi za jamii, watumishi waliohusika na uwekezaji mbovu katika mifuko hiyo kuchukuliwa hatua.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images