Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu Majaliwa Atembelea Mradi Wa Uendelezaji Miji Ya Kimkakati Katika Jiji La Dodoma

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea Mradi wa Uendelezaji  wa Miji ya Kimkakati katika jiji la Dodoma na kukagua ujenzi wa maegesho ya malori makubwa  katika eneo la Nala na uboreshwaji wa mandhari ya eneo la kupumzikia la Chinangal ijijini Dodoma.

Pia amemuagiza Mkurugenzi wa jiji la Dodoma, Godwin Kunambi andelee kutenga maeneo ya mapumziko ili wananchi wapate sehemu za kukutana na kubadilishana mawazo baada ya kumaliza kufanya kazi.

Waziri Mkuu amekagua maeneo hayo leo (Jumamosi, Desemba 29, 2018) ambapo ameupongeza uongozi wa jiji la Dodoma kwa kubuni wazo hilo na kusema kwamba ni muhimu kwa miji mikubwa kutenga maeneo ya kwa ajili ya mapumziko.

Amesema lazima jiji la Dodoma lipangwe kisasa  na amewataka wahandisi wahakikishe maeneo ya mapumziko yatengwa na yanatumika kama ilivyokusudiwa. Pia amemtaka Mkurugenzi wa Jiji, Kunambi aendelee kusimamia ujenzi wa kimkakati ndani ya jiji hilo.

”Hatuwezi kuwa tumejaza nyumba kila eneo, watu hawana mahali pa kupumzika na kukutana na marafiki zao plan ya Chinangali Park ni nzuri, Jiji la Dar es Salaam plan ya awali kulikuwa na maeneo ya mapumziko lakini watu wa Idara ya Ardhi waliyauza.”

Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu amekagua utekelezaji wa agizo alilolitoa Oktoba 21, 2018  kwa uongozi wa jiji la Dodoma la kubomoa uzio wa mabati uliojengwa kwenye eneo la wazi lililotengwa  kwa ajili ya kuchezea watoto na kuziba barabara ya tisa  katika Mtaa wa Mji Mpya Kata ya Madukani jijijini Dodoma. 

 Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na utekelezwaji wa agizo lake baada ya kutembelea eneo hilo na kukuta uzio umebomolewa na sasa kuna bustani iliyojengwa kwa ajili ya mapumziko na pia barabara imefunguliwa na wananchi wanaendelea kuitumia kama ilivyokuwa awali.

 Uzio huo ambao mbali na kujengwa katika eneo la wazi lililotengwa kwa ajili ya kuchezea watoto kwenye mtaa wa Mji Mpya kata ya Madukani pia uliziba barabara ya tisa, hivyo kusababisha usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa barabara hiyo.

Waziri Mkuu ameendelea kusisistiza uongozi wa jiji kutenga ardhi na kupima viwanja kwa ajili ya matumizi mbalimbali yakiwemo ya biashara, makazi, taasisi, huduma za jamii, viwanda pamoja na maeneo ya wazi kwa ajili ya mapumziko.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma amesema jiji la Dodoma ni miongoni mwa majiji manane nchini yanayotekeleza mradi wa uboreshaji wa miji ya kimkakati unaofadhiliwa na Serikali kupitia mkopo wa Benki ya Dunia.

Amesema katika jiji la Dodoma mradi huo unahusisha ujenzi wa miundombinu ya barabara katika maeneo ya Kikuyu, Chidachi, Kinyambwa, Itega, Njedengwa, Mapinduzi, Ilazo, Ipagala, Chamwino, Kilimani, Majengo, Mlezi pamoja na maingilio na stendi kuu ya mabasi na soko kuu zenye jumla ya urefu wa kilomita 26.6.

Mkurugenzi huyo amesema barabara hizo zinajengwa kwa kiwango cha lami, pia zitawekwa taa za barabarani takriban 925 zinazotumia mfumo wa umeme wa jua. Hata hivyo mradi huo utahusisha ujenzi wa kituo cha maegezo ya malori makubwa takribani 300 katika eneo la Nala.

Ameongeza kuwa mradi huo unahusisha ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi na soko kuu katika eneo la Nzuguni, ujenzi wa vituo sita vya watembea kwa miguu, ujenzi wa vizimba saba vya kukusanyia taka ngumu, uboreshaji wa mandhali ya eneo la kupumzikia katika eneo la Chinangali na ujenzi wa mtaro wa maji ya mvua wenye urefu wakilomita 6.5 katika eneo la Ipagala.

PICHA: Watumishi Jijini Mwanza Waandamana Kuunga Mkono Agizo La Rais Magufuli Kuhusu Kikokotoo

0
0
Waandamanaji hao wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbalimbali wakipita katika barabara ya Kenyatta wakielekea kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ili kufikisha ujumbe wao wa kumpongeza Rais John Magufuli baada ya kuiagiza mifuko ya hifadhi kuendelea kulipa malipo ya waastafu kwa kutumia utaratibu wa zamani wakati wadau wakiendelea na majadiliano hadi 2023.

Watumishi mbalimbali wa umma wakiimba wimbo wa mshikamano baada ya kuhitimisha maanandamano yao ya kuunga mkono agizo la Rais John Magufuli la kuiataka mifuko ya hifadhi ya jamii kuendelea na utaratibu wa zamani kulipa mafao ya wastaafu badala ya kutumia kikokotoo kipya. Picha zote na Daud Magesa
Waandamani hao wakiingia kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza jana kuunga mkono agizo la Rais John Magufuli kwa mifuko ya hifadhi ya jamii kuendelea kuwalipa watumishi waliostaafu mafao yao kwa kutumia utaratibu wa zamani.

CCM Arusha wakutana kumpongeza Rais Magufuli kwa Kufuta Kikokotoo

0
0
Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa Arusha kimempongeza Rais John Magufuli kwa utendaji wake mzuri katika kipindi cha miaka mitatu ikiwemo kurejesha kikokotoo cha zamani cha mafao ya wafanyakazi.

Wakitoa tamko lao leo Jumamosi Desemba 29, 2018 katika mkutano uliofanyika ukumbi wa CCM mkoa wa Arusha na kuwashirikisha wanaccm kutoka wilaya zote tano za mkoa wa Arusha, wamesema Rais John Magufuli ndiye mzalendo wa kweli.

Akitoa salamu kwa niaba ya wabunge wa mkoa Arusha, Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha ambaye pia ni mbunge wa Ngorongoro amesema katika kipindi cha miaka mitatu Rais Magufuli amefanya kazi ya mfano.

Ole Nasha amesema ndani ya miaka mitatu, Rais Magufuli amenunua ndege, amejenga madarasa na vivuko, ameanza ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Dar es salaam hadi Dodoma.

"Sio haya tu Rais wetu ameanza mradi mkubwa wa umeme wa Stiglers Gorge na jana amefanya kubwa kutetea wafanyakazi kurejesha kikokotoo cha zamani," alisema.

Mkuu wa wilaya ya Arusha, Gabriel Daqaro amesema, kazi alizofanya Rais ni kubwa na inawahakikishia CCM ushindi mwaka 2020.

Katika mkutano huo uliokuwa unaongozwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha, Loota Sanare pia ulihudhuriwa na mkuu wa mkoa Arusha Mrisho Gambo, wabunge na madiwani.

Katibu Mkuu CHADEMA Na Viongozi Wengine Wakamatwa Kwa Kufanya Mkusanyiko Bila Kibali

0
0
Jeshi la Polisi wilayani Hai, mkoani Kilimanjaro, linawashikilia Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vincent Mashinji na viongozi wengine watatu wa chama hicho mkoani humo kwa tuhuma za kufanya mkusanyiko usio halali.

Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Hai ambaye ni mkuu wa wilaya hiyo, Lengai Ole Sabaya amesema viongozi hao wamekamatwa mchana.

"Ni kweli tumemkamata Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Mashinji, katibu wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema, mwenyekiti wa halmashauri ya Hai, Helga Mchomvu na msaidizi wa mbunge wa Hai, Freeman Mbowe, Irine Lema kwa kufanya mkusanyiko usio halali," amesema.

Sabaya amesema viongozi hao, leo mchana wamekutwa wakifanya mkusanyiko katika eneo la Boma bila ya kuwa na kibali jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

"Naomba nitoe wito kwa wanasiasa kuheshimu sheria na taratibu, kama mnataka mkutano kuna taratibu hamuwezi kuvamia na kufanya mikutano kiholela," amesema.

Sabaya amesema katika wilaya yake ya Hai kwa sasa hataruhusu mikutano isiyo halali ambayo inalenga kuwapotosha wananchi kuhusu kazi nzuri ambazo zinafanywa na Rais john Magufuli.

"Waiache serikali ifanye kazi zake, kama wanataka siasa zao wasubiri kwenye kampeni, Hai tunataka maendeleo," amesema.

Mbowe Atuma Ujumbe Toka Gerezani

0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Seif Sharif Hamad, ameweka wazi mipango ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo, Freeman Mbowe baada ya kutoka gerezani ni kuungana na vyama vingine vya upinzani.

Katibu Mkuu huyo ameyasema  hayo baada ya kutumia siku ya Jumamosi ya leo kuwatembelea viongozi Mwenyekiti Mbowe pamoja na Mbunge Esther Matiko katika gereza la Segerea baada ya kufutiwa dhamana.

"Nimeitumia fursa ya kuonana na Mhe. Freeman Mbowe na Mhe. Esther Matiko kuwaeleza kuhusu  Azimio la Zanzibar na mikakati ya vyama sita vya siasa kurudisha demokrasia Tanzania. Mhe. Mbowe amenambia yuko pamoja na sisi na akitoka tu gerezani ataungana nasi kuendeleza atakapopakutia" Amesema Maalim Seif

Aidha kiongozi huyo amebainisha kwamba viongozi hao wawili bado wapo imara na wana imani kwamba haki itatendeka juu yao.

Mawaziri wakutana Mbeya kumpongeza Rais Magufuli

0
0
Mawaziri wameungana kumpongeza Rais John Magufuli kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali nchini kwa kasi kubwa.

Pongezi hizo zimetolewa leo Jumamosi Desemba 29, 2018 jijini Mbeya katika kongamano la Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi (UWT) lililofanyika kitaifa jijini humo.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amesema Rais Magufuli amefanya kazi kubwa kuhakikisha elimu inapatikana kwa wote bila kujali hali zao kiuchumi.

"Mheshimiwa Rais ameweza kusaidia kutolewa kwa elimu bure jambo lililopelekea ongezeko la watoto wanaoandikishwa katika shule zetu," amesema Profesa Ndalichako.

Naye Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angellina Mabula amesema Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli imesaidia kwa kiasi kikubwa kutatua migogoro mbalimbali ya ardhi.

"Serikali inaandaa mfumo ambao utasaidia kuondokana na tatizo la ardhi kumilikiwa na mtu zaidi ya mmoja," amesema Mabula.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Maji, Juma Aweso amesema miradi iliyotakiwa kutekelezwa katika awamu hii ni 1,810 lakini mpaka sasa miradi 1,659 imekwisha kutekelezwa.

Utabiri Uliotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) Kuanzia Usiku Huu

Afisa uhamiaji Afariki Dunia Baada yaunywa Pombe Kupita Kiasi

0
0
Na. John Walter-Babati
Afisa uhamiaji Mkoani Manyara aliefahamika kwa jina la Peter Kambanga (35- 40)  amepoteza maisha usiku wa alhamisi Disemba 27 kwa kile kinachoelezwa kunywa pombe kupita kiasi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara Agustino Senga amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba jeshi hilo lilifika katika chumba alichopanga marehemu, mjini Babati na kukuta kimefungwa kwa ndani na kuwalazimu kuvunja ndipo walipoukuta mwili huo.

Kamanda Senga amesema kuwa chanzo cha kifo hicho ni unywaji wa pombe kupindukia na kukosa hewa  na kuongeza kuwa  alikuwa akiishi mwenyewe katika chumba alichokuwa amepanga.

Aidha Senga amesema mwili wa Marehemu umesafirishwa leo Jumamosi Disemba 29,2018  kwenda wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma kwa ajili ya taratibu za Mazishi.

Kamanda Senga ametoa wito kwa wakazi wa Manyara kuishi pamoja na ndugu au familia zao pindi wanapokuwa mbali kikazi.

Sambamba na hilo jeshi la polisi mkoani Manyara limewasishi wananchi kunywa pombe kistaarabu na kuendesha magari kwa uangalifu huku likizidi kuimarisha ulinzi katika maeneo mbalimbali ya mkoa huu katika kipindi hiki cha siku kuu za mwisho wa mwaka.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya Disemba 30

Lugola Atoa ONYO Kwa Wanaotumia Misikiti na Makanisa Kuvuruga Amani ya Nchi

0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema Serikali haitawavumilia wanaotumia taasisi za dini ikiwamo misikiti na makanisa kuvuruga amani.
 
Alisema hayo juzi kwa niaba ya Rais John Magufuli wakati wa chakula cha jioni kilichoandaliwa na Kamati ya Amani ikiwa ni kusheherekea Sikukuu ya Krismasi.
 
Waziri huyo alisema bado kuna viashiria vya mtu mmoja mmoja na vikundi vya watu wanaotaka kuvuruga amani, vitendo ambavyo Serikali haitavivumilia.
 
Mwenyekiti wa Kamati ya Amani Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Musa Salum alisema ni mara ya kwanza kwa Waislamu kualikwa na kukaa pamoja katika kusheherekea Sikukuu ya Krismasi.
 
“Pamoja na kuwapo kwa mahusiano mazuri kati ya Wakristo na Waislamu nchini bado kumekuwa na shida kwa baadhi ya watu pale tunapokaa pamoja katika sikukuu hizi na kushindwa kutofautisha kusherehekea na kutambua,” alisema.
 
Naye Askofu wa Kanisa la Ufufuo, Paul Bendera alisema siku zote amani inatoka kwenye moyo wa mtu. 

“Haiwezekani tunakakaa pamoja akatokea mtu akatugawa, ili kuendeleza amani iliyopo tunapaswa kuthamini viongozi wetu na kutii mamlaka zao.”

Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally Atoa Maagizo MAZITO Kwa Naibu Waziri wa Kilimo

0
0
Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally amemwagiza Naibu Waziri wa Kilimo, Innocent Bashungwa kutafuta fedha za kuwalipa wakulima wa zao la kahawa mkoani Kagera kwa bei inayoridhisha kulingana na gharama watumiazo katika uzalishaji.
 
Dk Bashiru alitoa agizo hilo juzi mbele ya wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa huo wanaotoka wilaya za Ngara Kyerwa na Karagwe alipokutana nao mjini hapa.
 
Katibu mkuu huyo wa CCM alitoa agizo kwa Bashungwa ambaye ni Mbunge wa Karagwe (CCM) aliyekuwapo kwenye
kikao hicho kwenda kuhakikisha bei inaboreshwa ili kuwavutia wakulima wa zao hilo.
 
Alisema licha ya Serikali kuzuia magendo ya kahawa kutoka Kagera kuingia Uganda lakini inanunuliwa kwa kificho kisha inasafirishwa na kuwekwa katika kasha au kopo la robo kilo hadi nje ya nchi ikiwa na thamani kubwa hasa China.
 
“Waganda wananunua kahawa kwa magendo wanaikaanga na kuifunga kwa kuweka picha ya mwanamke mrembo wa Kiganda, wanaisafirisha hadi China kupitia bandari yetu inauzwa kakopo Sh40,000 iweje mkulima apatiwe Sh1,000?” alihoji Dk Bashiru.
 
Pia alimuagiza Mkurugenzi Halmashauri ya Ngara, Aidan Bahama kutowanyang’anya wananchi ardhi kwa madai ya kuwagawia wawekezaji kutoka Korea Kusini.
 
“Nilikupigia simu kukuzuia sasa nakupa ‘live’ sitaki kusikia wawekezaji wa nje wanapewa ardhi bila kufuata utaratibu wa kuridhiwa kwanza na mkutano mkuu wa vijiji,” alisema.
 
Mkuu Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali, Marco Gaguti alisema katika kupambana na biashara ya magendo ya kahawa wilaya ya Misenyi imekamata magari 12 yenye tani zaidi ya 60 na pikipiki zilizokuwa zikisafirisha Uganda.

Serikali Yakaribisha Wafanyabishara Wanaotaka Kubangua Korosho

0
0
SERIKALI  kupitia kwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Joseph Kakunda imewakaribisha wafanyabiashara kununua korosho na kuzibangua.
 
Mbali na uamuzi huo, Waziri Kakunda amesema Serikali  bado inaendelea kuingia mikataba na wabanguaji ili kupunguza mzigo wa korosho.

Kakunda ametoa kauli hiyo wakati taarifa ya timu ya pamoja ya wataalamu kuhusu hali ya utekelezaji wa operesheni korosho iliyotolewa Novemba 27 ikionyesha kuwa itachukua muda mrefu  kubangua korosho za msimu huu.
 
Novemba 12, Rais John Magufuli alitangaza Serikali kununua korosho yote kutoka kwa wakulima msimu huu kwa bei ya Sh3,300 kwa kilo.
 
Licha ya Waziri Kakunda kusema haina shida kwa ubanguaji kuchukua muda mrefu, amewataka wafanyabiashara wanaoweza kubangua wenyewe wakae meza moja na Serikali ili wauziwe korosho.
 
“Kama mtu anatokea popote iwe ndani au nje akasema mimi nataka ninunue korosho nikabangue mwenyewe, labda ana bei nzuri aje tuzungumze. Ije mvua, lije jua korosho ziko kwenye maghala, kuna tatizo hapo? Zitabanguliwa tu muda wowote,” alisema.
 
Alisema ubanguaji unaendelea baada ya Serikali kuingia mkataba na baadhi ya kampuni.
 
“Leo (juzi) ilikuwa niende kuzindua ubanguaji wa kule Mtwara, kwa hiyo siyo tumekaa tunasubiri wateja, tunaendelea kubangua.
 
“Sido (Shirika la Viwanda Vidogo) ambao ni wabanguaji wadogo, wameshabangua tani sita. Bado kuna viwanda tulikuwa tunaingia navyo mkataba, hadi jana (juzi) tumeingia mikataba minne na bado tutaingia mingine zaidi ya 12,” alisema.
 
Inaelezwa kuwa kuna jumla ya viwanda 23 vya kubangua korosho na ambavyo uwezo wake uliosimikwa sasa ni kubangua jumla ya tani 42,200. Hata hivyo, uwezo wa mashine kwa kiwanda kimoja ni tani 11,142 kwa mwaka sawa na asilimia 26 tu ya uwezo uliosimikwa wa viwanda hivyo.
 
Taarifa hiyo ya timu ya pamoja ya wataalamu inaonyesha matarajio ya uvunaji wa korosho kwa msimu wa mwaka 2018/19 kufikia jumla ya tani 275,191 na kama viwanda vinane vinavyofanyakazi vingebangua korosho kwa kiwango kinachotakiwa cha tani 127,200 kwa mwaka, kazi hiyo itafanyika kwa miaka miwili.
 

Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Taifa Muhimbili Aonya Kuhusu Rushwa, Lugha Chafu

0
0
MKURUGENZI  Mtendaji  wa  Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Prof. Lawrence  Museru  amesema  uongozi  wa  hospitali  hiyo  utachukua   hatua    za    kinidhamu    mtumishi    atakayejihusisha   na   vitendo   vya   rushwa  na  kutoa  lugha  chafu  kwa  wateja.

Haya    aliyasema    jjini    Dar  es Salaam juzi wakati akifungua mkutano  mkuu  wa  mwaka  wa  Chama  cha Wafanyakazi wa Afya Serikalini (TUGHE), tawi la Muhimbili.
 
Alisema,   kuwa   mtumishi   wa   umma    anapaswa    kuwa    mfano    katika  kutoa  huduma  bora  na  kuzingatia nidhamu.

Prof.   Museru   alisema   endapo   itabainika  kwamba  mtumishi  kujihusisha na vitendo hivyo hatua kali zitachukuliwa   dhidi   yake   ili   iwe   fundisho kwa wengine.
 
“Jina    la    Muhimbili    liendelee    kuwa  safi  tusikubali  watu  wachache    watukwamishe    ni    lazima    tushirikiane   katika   kuwafichua watu  hao  ili  hatua  stahiki  ziweze  kuchukuliwa   dhidi   yao,”   alisema   Prof. Museru.
 
Aliongeza  kuwa,  hospitali  hiyo  imekua      ikiendelea      kuboresha      huduma  zake  na  kufanikiwa  kuanzisha huduma za kibingwa ambazo awali zilikua hazifanyiki nchini.
 
“Tumeanzisha huduma ambazo zamani  ilikua  ni  lazima  mgonjwa  aende   kutibiwa   nje   ya   nchi,   na   vilevile   tunatoa   huduma   ya   tiba   radiolojia      (Interventinal Radiology),   nia   yetu   ni   kuhakikisha   huduma hizi zinaendelea ili Watanzania wengi wazipate,” alisema.

Alieleza   kuwa      sasa   huduma   hizo  wanaitoa  Muhimbili,  ambapo  wanatoa  huduma  ya  kupandikiza  figo ambapo mpaka sasa wagonjwa 28 tayari wamepandikizwa, watoto 21 wamewekewa vifaa vya kusaidia kusikia (Cochlear Implant).

Mbali   ya   huduma   hizo,   Mkurugenzi  huyo  alifafanua  kuwa  kwa    sasa  wanafunga  MRI  mpya  ili  kuipumzisha iliyopo ambayo imefanya kazi kwa muda mrefu.

Kwa     upande     wake     Katibu     wa  TUGHE  Mkoa  wa  Ilala,  Tabu  Mambo   aliupongeza   uongozi   wa   Muhimbili  kwa  utendaji  bora  wa  kazi  na  kueleza  kuwa  chama  hicho  kinatambua     mchango     mkubwa     unaotolewa na hospitali hiyo katika kuhakikisha   wananchi   wanapata   huduma bora.

Mkutano   huo   ulibeba   ajenda   mbalimbali  ikiwemo  kutoa  taarifa  za  utendaji  kazi  wa  chama  pamoja  na   kutoa   taarifa   ya   mapato   na   matumizi kwa mwaka

Juliana Shonza Atoa Mashart TBC

0
0
Na Anitha Jonas – WHUSM – Tarakea,Rombo
Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza ameutaka uongozi wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kuhakikisha wanaboresha usikivu wa matangazo kwa Wilaya ya Rombo katika maeneo ambayo hayana usikivu kabla ya bunge la bajeti.

Mheshimiwa Shonza ameyasema hayo jana katika kijiji cha Tarakea Wilayani Rombo Mkoani Kilimanjaro alipotembelea mitambo ya TBC iliyopo katika eneo la mpakani mwa Tanzania na Kenya kwa lengo la kutaka kufahamu kwanini  usikivu wa matangazo ya TBC bado unachangamoto japo kuwa wamefunga mitambo hiyo eneo la karibu na mpakani.

“Kero ya usikivu katika eneo hili la mpakani ni lazima lifanyiwe kazi kwa haraka kwani kikubwa hapa ilikuhakikisha mnamaliza kero hii ni mkafunge minara yenu katika eneo lenye mlima mrefu ili mawimbi yenu yaweze kwenda mbali bila kukutana na kizuizi na ili muweze kufanikiwa katika utafiti wenu wa eneo bora ni vyema muwashirikisheni wazawa wa eneo hilo katika kuwashauri eneo zuri lililopo juu zaidi,”alisema Mhe.Shonza.

Akiendelea kuzungumza katika ziara hiyo Naibu Waziri huyo ameusisitiza uongozi wa Kanda ya Kaskazini TBC kuhakikisha wanakamilisha zoezi la kuboresha usikivu huo kwani pesa kwa ajili ya maboresho hayo ilikwisha toka na sivyema pesa hiyo ikatumika vibaya kwa kusimika mitambo hiyo katika maeneo ambayo hayatatatua kero hiyo ikaja kuwalazimu kuhamisha tena mitambo hiyo, kwani kwa kufanya hivyo hayo yatakuwa ni matumizi mabaya ya fedha za umma hivyo ni vyema kuliangalia hilo.

Kwa upande wa Meneja wa TBC Kanda ya Kaskazini Bw.Gerald Uisso alieleza  kuwa ofisi yake ilikuwa imekwisha fanya utafiti katika eneo la Mlima Hakwe ila kabla ya kusimika mitambo hiyo watafanya utafiti na kwa maeneo mengine kwa kuzingatia maelekezo.

“Mchakato wa kusimika mitambo katika eneo hilo ilikuwa ni baada ya kumaliza ujenzi wa kusimika mitambo katika eneo la Longido ambao unaendelea kwa sasa,”alisema Bw.Uisso.

Pamoja na Hayo nae Mkuu wa Wilaya ya Tarakea Bibi.Agness Hokororo alimweleza Naibu Waziri huyo kuwepo kwa changamoto kubwa ya wakazi wa eneo hilo kupata habari sahihi naza uhakika kwani Radio wanazosikiliza wakazi waeneo hilo niza kutoka nchi ya jirani na hiyo imekuwa changamoto kubwa kwao katika kupata taarifa za mafanikio ya utekelezaji wa shughuli za serikali.

Halikadhalika Mheshimiwa Shonza aliwasisitiza uongozi wa TBC kukumbuka kuwa Shirika hilo nila umma hivyo linawajibu wa kuhakikisha linafikisha matangazo yake kila mahali  pasipo kuwa na changamoto yoyote.

Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power

0
0
Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power Kwaajili Ya Nguvu Za Kiuume Na Promix Kwaajili Ya Kuongeza Maumbile;

Kwa mwanaume aliyekamilika na mwenye Afya njema ili kumridhisha mke au mpenzi anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara mbili hapo utamridhisha mpenzi wako ila ukiwa unapiga moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe 

Tiba Ya Tatizo Lako Ni Dawa Hiitwayo Simpo Power No, 1; dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge vya miti shamba na unga ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja :-1 itakufanya urudie tendo zaidi ya mara tatu 
2 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-20 kwa tendo la Kwanza 
3 huimarisha uume uliolegea na kusinyaa 

Je Una Mke Au Mpenzi Aliyebalikiwa Kuwa Na Kario Kubwa Au Mwili Mnene Na Wewe Mume Wake Una   Maumbile Mafupu?; tumia sasa dawa ya PROMIX dawa itakufanya umfikishe shemu nyeti maana inaboresha maumbile saizi upendayo.

Dawa zangu haziina madhara yoyote kwa mtumiaji 

MARKSU; ni dawa ya kisukari dozi siku 21 
MWARU; ni dawa ya uzazi,hufungua milija ya uzazi ata kwa Wale waliofungiwa uzazi  
MTUNDUU; ni dawa ya busha bila kupasua 
MAZANZA; ni dawa ya kisukar zipo dawa za miguu Kuuma,tumbo,kupunguza Matiti,kutoa minyama uzembe ngiri,vidondo vya tumbo  

FIKA OFISINI KWANGU BUGURUNI MALAPA KARIBU NA KOTA ZA POLISI AU PIGA  SIMU ULETEWE MAHALI ULIPO SIMU NO : 0783185060 au 0752348593  -DR AGU

Habari Njema Kwa Wenye Matatizo Ya Nguvu za Kiume, vitambi, nyama uzembe

0
0
NAUHABARISHA ULIMWENGU TIBA BORA YA MITI SHAMBA..

  Ninatibu magonjwa 1-100 dawa ninazo Sasa.

KOLA; ni dawa ya kisukari dozi siku 14 ata kama unajihisi itumie kwa kinga zaidi

  THREE(3) POWER MIX,inatibu Nguvu za kiume Ni dawa iliyo Bora na Humfanya mume kuchelewa kufika kileleni dkk 40_47 bila kuchoka.Inaanza kufanya kazi ndani ya door 80 na inatibu kabisa ndani ya siku 6 tu,hutatumia Tena dawa ya Nguvu za kiume three power mix Ni kiboko kabisa,hata Kama unahisi una tatizo unaruhusiwa kutumia kwa ajili ya Kinga baadae.

 DUDUMA MIX 4 POWER,hunenepesha na kurefusha uume na kukomaza uume uliosinyaa kwa mda mfupi,tumia siku 4 na kupona kabisa.

  SHOOLA,Ni dawa ya kutibu tezi dume na kupona kabisa ni ya miti shamba hutumika kwa kunywa bila upasuaji ndani ya siku 14 haina madhara.

 NENGONENGO,dawa ya kutibu Uzazi kwa akina mama walioshindwa kubeba mimba kwa mda mrefu ukitumia utaweza kupata mimba na kujifungua salama.

  KAMINGO,Ni dawa inayotibu Busha bila kufanyiwa operation na aliyevimba korodani inatibu kabisa dozi Ni siku 7 na inaubora wa Hali ya just na unapona kabisa.

  IKUMBIJA,Ni dawa ya kumvuta mpenzi aliekuacha na mwenye ahadi za uongo kukutimizia,na kumkomesha mtu asiwe na mtu mwingine pia atakurudia ndani ya masaa 6.

   MALAMALA,Ni dawa ya vidonda vya tumbo na tumbo kujaa gesi, kilungulia na inafanya kazi kwa haraka zaidi na kupona kabisa ndani ya siku 6.
 

SAALA,Ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto,kiuno,mgongo,magoti na viungo vyote mwilini na joints,Sasa tiba yake Ipo kwangu.

   HALALA MIX,Ni dawa mix ya miti 100 inayotibu matatizo yote,Kama majini,kesi,biashara,kazi,mitego na kupoteza kumbukumbu. no

TUNAFANYA KAZI SIKU ZOTE PIA NAKUFIKIA POPOTE ULIPO KWA HARAKA,NAPATIKANA DAR ES SALAAM NA KAHAMA,PIA NINA MAWAKALA MIKOANI SIMIYU,SHINYANGA,MOSHI NA MBEYA.


     KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA: 0784 475946
           0744 922982
    DR,SANDALA.

TSNP Yawaangukiwa TAKUKURU Rushwa ya Ngono Vyuoni

0
0
Mtandao  wa   Wanafunzi   Tanzania    (TSNP)    imeitaka    Taasisi    ya    Kuzuia    na    Kupambana    na    Rushwa (Takukuru) kuongeza jitihada  zaidi  za  kuwajengea  uwezo 
wanafunzi     na     wahadhiri     juu     ya   masuala   ya   rushwa   hasa   ya   ngono kwa lengo la kupunguza au kumaliza kabisa tatizo hilo vyuoni.

TSNP  umesema  kuwa  rushwa  ya   ngono   kwa   sasa   imeshamiri   katika   vyuo   mbalimbali   nchini   hivyo  inapaswa  kukemea  kwani  inaharibu   maisha   ya   wanafunzi   ambao      wanategemewa      kuwa      viongozi wa baadae.

Akizungumza    na    waandishi    wa   habari   jijini   Dar   es   Salaam   hivi   karibuni,   Katibu   wa   TSNP,   Joseph  Marekela  alisema  rushwa  ya  ngono  vyuoni  ni  changamoto  kubwa  hasa  kwa  wanafunzi  wa  kike  hivyo  jitihada  za  makusudi  zinahitajika  ili  kuhakikisha  kuwa 
hakuna    mtu    anayepoteza    haki    yake ya msingi kwa kukataa kutoa rushwa   hiyo   ambayo   si   tu   inapoteza utu wa mtu bali ni kinyume na haki za binadamu.

Alisema   mfumo   wa   upimaji   uwezo    uliyopo    sasa    umempa    mamlaka  makubwa  mhadhiri  ya  kuamua   hatma   ya   mwanafunzi   kitaaluma    jambo    ambalo    lina
sababisha  uwepo  wa  mianya  ya  rushwa  ya  ngono  kwa    wahadhiri  wasio  na  maadili  ambao  wanatumia  nafasi  yao  kuminya  haki  ya  mwanafunzi.

“Kwakuwa      tatizo      hili      ni      kubwa   na   limeathiri   wanafunzi   wengi  chuoni    tunatoa  wito  kwa  Takukuru waongoze jitihada zaidi kwa  kuwajengea  uwezo  taasisi  za 
Takukuru  vyuoni  ili  kupambana  na  tatizo  hili  kikamilifu,  pia  vituo  vya jinsia na Serikali za wanafunzi ziwajibike ipasavyo ili kuhakikisha kuwa   hakuna   anaepoteza   haki   yake ya msingi kwa kukataa kutoa rushwa hiyo ya ngono,” alisema.

Hata     hivyo     mtandao     huo     umesema  kuwa  ukosefu  wa  taulo  za   kujisitiri   wanafunzi   wa   kike   hasa  wa  vijijini  kipindi  cha  hedhi  inaathiri maendeleo ya wanafunzi
hao kitaaluma.

Kutokana      na      hali      hiyo,      Marekela   alisema   wanatoa   wito   kwa  Serikali  kupitiaWizara  yenye  dhamana  kulitazama  upya  suala  kwa  kugawa  bure  taulo  hizo  kwa 
wanafunzi  wa  kike  hasa  waliopo  maeneo   ya   vijijini   ili   kunusuru   ndoto zao walizojiwekea.

Aidha alisema suala la mikopo kwa  wanafunzi  wa  elimu  ya  juu  bado ni changamoto kwani wengi wao  wameshindwa  kuendelea  na  masomo kwa kukosa mikopo hiyo

Rais Magufuli Aungana Na Waumini Wengine Wa Kanisa La Mtakatifu Petro Parokia Ya Oysterbay Jijini Dar Es Salaam Kuadhimisha Sherehe Ya Familia Takatifu Ya Yesu

0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mkono wa Amani na Masista wa kanisa katoriki na waumini wengine wakati wa Ibada ya jumapili ya Maadhimisho ya sherehe ya Familia Takatifu ya Yesu iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay Jijini Dar es Salaam.Desemba 30,2018.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na watoto wa kanisa katoriki wakati wa Ibada ya jumapili ya Maadhimisho ya sherehe ya Familia Takatifu ya Yesu iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili kanisani kwa ajili ya kushiriki Misa ya Maadhimisho ya sherehe ya Familia Takatifu ya Yesu iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay Jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Paroko msaidizi Padre Asis Mendokta mara baada ya kuungana na waumini wengine katika Misa ya Maadhimisho ya sherehe ya Familia Takatifu ya Yesu iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay Jijini Dar es Salaam.Picha zote: IKULU

Taarifa Kwa Umma Kuhusu Akaunti Halali Za Mitandao Ya Kijamii Ya Instagram Na Twitter Za Kangi Lugola, Waziri Wa Mambo Ya Ndani Ya Nchi

0
0
Baada ya kuwepo kwa akaunti feki ya Mtandao wa Kijamii wa Instagram ambao ulikua unatoa taarifa mbalimbali kwa jamii kuhusu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Wizara kwa ujumla, kuanzia leo Disemba 30, 2018, Wizara inatangaza rasmi kwa jamii, akaunti halali zilizosajiliwa kwa jina la Mheshimiwa Waziri Kangi Lugola, kama ifuatavyo;

    officialkangi_lugola (Instagram)
    @kangi_lugola (Twitter)

Taarifa zote zitakazotolewa katika kurasa za akaunti hizi zitakua sahihi.

Kwa hatua hiyo, Wizara inaendelea kutoa onyo kali kwa mtu yeyote atakayejihusisha kwa kutumia jina la Kangi Lugola kusajili akaunti yoyote na kutoa taarifa za Waziri huyo kupitia akaunti feki hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Aidha, Wizara inawaomba Watanzania waendelee kupata taarifa zake zaidi kupitia tovuti yenye anuani; www.moha.go.tz na twitter ya Wizara kwa akaunti ya Msemaji Mambo ya Ndani.  

PICHA:Rais Magufuli Amjulia Hali Mama Yake Mzazi Bibi. Suzana Magufuli Anayepatiwa Matibabu Jijini Dar Es Salaam

0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Wasaidizi wake wakimuombea Mama yake Mzazi Bibi. Suzana Magufuli anayepatiwa Matibabu  Jijini Dar es Salaam Desemba 30, 2018. 

Bibi Suzana Magufuli anasumbuliwa na ugonjwa wa Kiharusi ambapo amekuwa akipatiwa matibabu kwa takribani miezi mitatu sasa.PICHA NA IKULU
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images