Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Wananchi Wakimbia Kijiji Kukwepa Msako wa Vyoo

$
0
0
Wananchi wa vitongoji vilivyopo kijiji cha Muungano, wilayani Momba, wameyakimbia makazi yao wakihofia kukamatwa baada ya kuwapo kwa msako wa kuwakamata wasiokuwa na vyoo.
 
Kata ya Kamsamba ni miongoni mwa kata wilayani Momba ambayo imekumbwa na ugonjwa wa Kipindupindu na watu zaidi ya 100 kuugua na kusababisha serikali kuweka mikakati ya kudhibiti ugonjwa huo.
 
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kamsamba, Gerad Makwasa, alisema viongozi ngazi ya wilaya wakiwa na askari mgambo, walifika katika bonde la Kamsamba kuendesha doria kuwasaka wasiokuwa na vyoo, hali iliyowalazimu wakazi wa kijiji hicho kukimbilia kusikojulikana. 

Ofisa Tarafa ya Kamsamba, Zakayo Mwasomola, alisema juzi walikaa kikao na Mganga Mfawidhi wa kituo cha afya cha Kamsamba kujadili hali hiyo ambapo alisema kata zilizokumbwa zaidi ni ugonjwa huo ni Ivuna wagonjwa 35, Samang’ombe 35 na Kamsamba 34 na aliyefariki dunia ni mmoja.
 
Alisema ugonjwa huo uliibuka Novemba 11 mwaka huu na jitihada zinafanyika kudhibiti hali hiyo.
 
Alisema wamekuwa wakihamasisha watu kuweka hali ya usafi wa mazingira,kujenga vyoo bora,kuchemsha maji ya kunywa na kunawa kwa sabuni pindi watokapo chooni.
 
“Ni kweli wananchi karibu wote wa kijiji cha Muungano wameyakimbia makazi yao wakihofia kukamatwa, lakini tumeandika majina yao, tunafahamu kuwa watarejea tu kwani wameacha familia zao wengine wake zao ni wajawazito,’’alisema Mwasomola.
 
Mwenyekiti wa kamati ya Maafa,Juma Irando, alisema hiyo ni
operesheni endelevu ya kuhakikisha kila kaya inakuwa na choo bora ambacho kitakuwa kinatumika.
 
Irando ambaye pia ni Mkuu wa wilaya hiyo, alisema kata hiyo imekumbwa na Kipindupindu kutokana na watu wengi kutokuwa na vyoo na walitoa muda wa kujenga kwa hiyari kuanzia Novemba 30 mwaka huu hadi Desemba 30 mwaka huu.
 
Alisema huo ulikuwa ni mkakati wa kimkoa ambapo tayari
siku zimekwisha na sasa wapo katika utekelezaji.
 
Alisema kwamba kitendo cha wanakijiji hao kukimbia sio dawa ya kumaliza tatizo, kwani operesheni hiyo ni endelevu.

Vijiji Vyote Nchini Kupata Umeme

$
0
0
Na Mathias Canal, Songwe
Serikali imesema hakuna kijiji nchini kitakachoachwa bila ya kuunganishiwa umeme katika awamu ya tatu ya mradi unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (Rea).

Aidha,  Serikali imetenga Sh1 trilioni kwa ajili ya kusambaza umeme katika vijiji 8,000 ambavyo bado havijaunganishiwa na nishati hiyo huku ikiendela na uwekaji wa umeme katika vijiji zaidi ya 13400.

Mbunge wa Jimbo la Vwawa Mkoani Songwe Mhe Japhet Hasunga amewahakikishia wananchi kuhusu upatikanaji wa umeme katika jimbo hilo hivyo wananchi wanapaswa kuondoa wasiwasi na serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli.

Mhe Hasunga ameyasema hayo wakati wa mikutano yake katika kijiji cha Igale na Iyula A vilivyopo katika kata ya Iyula akiwa katika ziara ya kikazi jimboni humo.

Alisema kuwa upatikanaji wa umeme katika jimbo lake utasaidia kuongeza upatikanaji wa huduma mbalimbali za kijamii na kuwa chachu ya maendeleo kwa wananchi na Taifa kwa ujumla wake.

Alisema kuwa utekelezaji wa Miradi hiyo ya umeme katika Jimbo la Vwawa unaenda sambamba na lengo la Serikali ya awamu ya Tano ya kuwa na uchumi wa kati kupitia viwanda ifikapo 2025.

Mhe Hasunga amewataka wananchi hao kutumia fursa mbalimbali zitakazotokana na utekelezaji wa miradi katika sekta ya gesi na mafuta ili kujiongezea kipato na kuiwezesha nchi kutimiza malengo yake kuelekea kuwa nchi ya uchumi wa kati.

Kuhusu malalamiko ya wananchi dhidi ya gharama kubwa za pembejeo za kilimo, Mhe Hasunga ambaye ni Waziri wa Kilimo amewahakikishia wananchi kuwa wizara yake imejipanga kuhakikisha kuwa mbolea zinapatikana kwa wakati ili wakulima wa mazao mbalimbali ya chakula na biashara waweze kunufaika na pembejeo hizo.

Alisema kuwa kumekuwa na malalamiko mengi nay a muda mrefu kuhusu mbolea hivyo serikali itapitia upya utaratibu wa uuzaji wa mbolea ili kutafuta namna bora ya kurahisisha huduma hiyo kwa wakulima nchini.

MWISHO. 

Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), China Kutangaza Vivutio vya Utalii Nchini

$
0
0
Tanzania  kupitia Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) na Serikali ya Watu wa China, zimedhamiria kutangaza vivutio mbalimbali nchini na kukuza biashara kati ya nchi hizo.
 
Akizungumza na wanahabari juzi Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo, alisema lengo kuu la ziara iliyofanyika nchini China katika Jiji la Shanghai, Guangzhou, Hong Kong, Chengdu na Beijing Novemba 12- 20, ilikuwa ni kwa ajili ya kutangaza utalii.
 
Alisema wametumia fursa hiyo kuhakikisha Tanzania inaongeza sehemu ya umiliki wa soko kwenye soko la utalii kwa kutangaza vivutio vya utalii na fursa za uwekezaji zikizopo nchini ikiwamo na safari za ndege za ATCL kwenda China.
 
Jaji Mihayo, alisema katika safari hiyo ya nchini China, wameweza kusaini mkataba na Kampuni ya Touchroad Group na TTB na wamekubaliana kuwa kampuni hiyo italeta watalii 10,000 kutoka China hadi kufi kia mwaka 2019.
 
“Kundi la kwanza la watalii wanatarajiwa kuwasili nchini Januari na Februari 2019, watakuwa nchini kwa muda wa siku tatu na Touchroad wameonesha nia ya kuwekeza katika
huduma ya malazi zenye hadhi ya nyota tano na tayari wanazo hoteli nne,” alisema Jaji Mihayo.
 
Katika ziara waliyoifanya ya Jiji la Beijing, wawakilishi wa Shirika la Utangazaji la China (CCTV), walikutana na maofisa wa MNRT na wakatoa mapendekezo ya kutengeneza makala za dakika 30 za zamadam kisha kutoa filamu kama
ya Jurassic Park, ili kurushwa kwenye televisheni yao.
 
“Pia, CCTV4 wameafiki kushirikiana na Wakala wa Misitu
Tanzania (TFS), kupiga picha katika hifadhi za asili za misitu wakati wa sherehe za maadhimisho ya mwaka mpya wa China mnamo mwezi Februari 2019,” alisema.
 
Mwenyekiti huyo wa TTB alisema kwa takwimu inaonesha Tanzania kwa mwaka 2017 imeweza kupokea watalii 29,224 kutoka nchini China wakitembelea vivutio tofauti nchini.
 
Kwa upande wake, Meneja Mauzo na Usambazaji wa ATCL,
Edward Nkwabi, alisema katika ziara hiyo walipokea maombi kutokakwa viongozi wa miji ya Hong Kong, Beijig, Chengdu na Shanghai, kuanzishwa kwa safari za moja kwa moja kutoka Tanzania hadi kwenye miji hiyo.
 
Alisema jambo hilo liliwafanya kuingia makubaliano na kampuni moja ya uwakala ambayo itatangaza na kuuza tiketi za safari za ndege za ATCL. 

Alisema safari za moja kwa moja kuelekea nchini China zitaanza mapema mwakani kwa ajili ya kuimarisha sekta ya utalii nchini na lengo kuu ni kuwapa fursa ya kuja moja kwa moja kutoka China hadi Tanzania.

Waziri Mhagama: Kilimo biashara kuwakomboa vijana Kiuchumi

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Jenista Mhagama, amesema serikali imedhamiria kuwezesha vijana kiuchumi kupitia kilimo biashara ili kuchochea ongezeko la ajira na kipato.

Ofisi ya Waziri Mkuu chini ya Baraza la Taifa la Biashara (TNBC), kupitia Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji, wilayani Kigoma wameanza kutekeleza mradi unaolenga kuwezesha vijana kushiriki katika shughuli za uchumi kupitia mafunzo ya ujuzi na ujasiriamali kwenye kilimo na ufugaji.

Akizungumza katika ziara yake mkoani Kigoma wakati wa kukagua shughuli za utekelezaji za TNBC, Mhagama alisema vyombo hivyo vimeanza utekelezaji wa mradi huo kwa kushirikiana na Chuo cha Maendeleo Kihinga.

“Nitoe wito watendaji wa halmashauri na ngazi ya mkoa wa Kigoma waendelee kuwaunga mkono vijana hawa wanaoshiriki katika mradi huu wa kilimo biashara. Nawataka mtambue haya yote yanafanyika kwa sababu ya jitihada zinazofanywa na serikali, hivyo ufadhili wa mradi huu unaunga mkono jitihada zake za kuwezesha vijana,” alisema.

Naye Mratibu wa Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara na Uwekezaji (masuala ya majadiliano ya sekta ya umma na binafsi), Andrew Mhina, alibainisha kuwa katika kuhakikisha unawawezesha vijana kuwa na ujuzi wa kilimo na ufugaji utakaowawezesha kujiajiri, wameanza ufadhili wa awali kwa kutoa Sh.  milioni 53 ambazo zimetumika katika ujenzi wa mabwawa ya samaki, ukarabati wa mabanda ya kufugia kuku na kuandaa shamba darasa.

 Mradi wa kuwezesha vijana kushiriki katika Kilimo Biashara wilayani Kigoma, unasimamiwa na kutekelezwa na Ofisi ya Rais (Tamisemi) kupitia Manispaa ya Kigoma, Chuo cha Maendeleo Kihinga, Chuo cha Uvuvi Kigoma, Mradi wa LIC na Baraza la Biashara la Wilaya ya Kigoma.

SSRA Yawatoa Hofu Wastaafu......Yaendelea kupokea maoni kuhusu mafao

$
0
0
Mamlaka ya Udhibiti wa Mifuko ya Jamii (SSRA) inaendelea kupokea maoni mbalimbali kutoka kwa wadau na wananchi ambayo yatasaidia kuboresha kanuni na miongozo itakayoendelea kumnufaisha zaidi mstaafu kupitia mafao yake.
 
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es salaam jana, Mkurugenzi Mkuu wa SSRA, Dk. Irene Isaka, alisema lengo la mamlaka hiyo ni kuendelea na maboresho ya kanuni na miongozo, kwani dirisha la maoni lipo wazi kwa watanzania kuleta mawazo yao yatakayosaidia
kuboresha mfumo wa mafao kwa wastaafu.
 
“Milango ipo wazi kwa wananchi na wadau mbalimbali kuleta maoni yao, ili tuboreshe sheria na kanuni zinazoongoza mifuko ya jamii na kuongeza tija katika mafao ya wastaafu,’’ alisema Dk. Isaka.
 
Alieleza kuwa kanuni zinazotumika sasa zimetokana na ushirikishwaji wa wadau mbalimbali wakiwemo wafanyakazi, waajiri na kwa ujumla katika kutoa maoni na mapendekezo yamesaidia kupatikana kwa sheria na kanuni ambazo zimeleta neema kwa wastaafu kwa kupata mafao stahiki na kwa wakati.
 
“Taratibu za mafao zinampa mstaafu nafasi ya kupata mkopo
katika baadhi ya benki nchini kutokana na uhakika wa pensheni yake kwa kipindi cha kustaafu kwake na kumfanya aweze kuendelea kufanya miradi mbalimbali ya maendeleo,” alisema.
 
Dk.Isaka alisema tofauti na miaka ya nyuma pensheni za wastaafu zilikuwa na ukomo wa muda wa miaka 10 mpaka miaka 12, lakini kwa kanuni za sasa pensheni ya mstaafu atapokea kwa kipindi chote cha maisha yake ya kustaafu, hii inampa uhakika wa kupata mkopo na kuendelea kufanya shughuli mbalimbali za maendeleo.
 
“Moja ya majukumu ya SSRA ni kulinda na kutetea maslahi ya mwanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii hivyo tutaendelea kupokea maoni ili mwanachama anufaike zaidi kupitia michango yake atakapostaafu,” alisema.
 
Alisema SSRA itaendelea kuwaelimisha wanachama na wananchi kwa ujumla juu ya kanuni mpya ya ukokotoaji na faida zake kwa wanachama pale atakapo staafu, kwani imeonekana uelewa wa hii kanuni mpya haijawafikia watu wengi nchini na hata wale wachache waliofikiwa na taarifa hiyo wengi wao wamepotoshwa.
 
“SSRA tumejipanga kuwafikia wanachama wote nchini na
kuwapa elimu juu ya kanuni hii mpya ya ukokotoaji wa mafao ili kuwaondoa katika hofu ambayo imejengeka miongoni mwao kutokana na maneno ya baadhi ya watu wasio na uelewa wa kutosha juu ya kanuni mpya ya Ukokotoaji mafao,” alisema Dkt. Isaka.
 
Alisema madhumuni ya mamlaka hiyo ni kumuondoa mstaafu katika hali mbaya ya kiuchumi baada ya kumaliza mafao yake ya mkupuo ya asilimia 25, kwa kumpatia asilimia zilizobaki kama pensheni ya kila mwezi kwa kipindi chote cha maisha yake.

Habari Njema Kwa Wenye Matatizo Ya Nguvu za Kiume, vitambi, nyama uzembe

$
0
0
NAUHABARISHA ULIMWENGU TIBA BORA YA MITI SHAMBA..

  Ninatibu magonjwa 1-100 dawa ninazo Sasa.
  THREE(3) POWER MIX,inatibu Nguvu za kiume Ni dawa iliyo Bora na Humfanya mume kuchelewa kufika kileleni dkk 40_47 bila kuchoka.Inaanza kufanya kazi ndani ya door 80 na inatibu kabisa ndani ya siku 6 tu,hutatumia Tena dawa ya Nguvu za kiume three power mix Ni kiboko kabisa,hata Kama unahisi una tatizo unaruhusiwa kutumia kwa ajili ya Kinga baadae.

 DUDUMA MIX 4 POWER,hunenepesha na kurefusha uume na kukomaza uume uliosinyaa kwa mda mfupi,tumia siku 4 na kupona kabisa.

  SHOOLA,Ni dawa ya kutibu tezi dume na kupona kabisa ni ya miti shamba hutumika kwa kunywa bila upasuaji ndani ya siku 14 haina madhara.

 NENGONENGO,dawa ya kutibu Uzazi kwa akina mama walioshindwa kubeba mimba kwa mda mrefu ukitumia utaweza kupata mimba na kujifungua salama.

  KAMINGO,Ni dawa inayotibu Busha bila kufanyiwa operation na aliyevimba korodani inatibu kabisa dozi Ni siku 7 na inaubora wa Hali ya just na unapona kabisa.

  IKUMBIJA,Ni dawa ya kumvuta mpenzi aliekuacha na mwenye ahadi za uongo kukutimizia,na kumkomesha mtu asiwe na mtu mwingine pia atakurudia ndani ya masaa 6.

   MALAMALA,Ni dawa ya vidonda vya tumbo na tumbo kujaa gesi, kilungulia na inafanya kazi kwa haraka zaidi na kupona kabisa ndani ya siku 6.
 

SAALA,Ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto,kiuno,mgongo,magoti na viungo vyote mwilini na joints,Sasa tiba yake Ipo kwangu.

   HALALA MIX,Ni dawa mix ya miti 100 inayotibu matatizo yote,Kama majini,kesi,biashara,kazi,mitego na kupoteza kumbukumbu. no

TUNAFANYA KAZI SIKU ZOTE PIA NAKUFIKIA POPOTE ULIPO KWA HARAKA,NAPATIKANA DAR ES SALAAM NA KAHAMA,PIA NINA MAWAKALA MIKOANI SIMIYU,SHINYANGA,MOSHI NA MBEYA.


     KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA: 0784 475946
           0744 922982
    DR,SANDALA.

Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power

$
0
0
Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power Kwaajili Ya Nguvu Za Kiuume Na Promix Kwaajili Ya Kuongeza Maumbile;
Kwa mwanaume aliyekamilika na mwenye Afya njema ili kumridhisha mke au mpenzi anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara mbili hapo utamridhisha mpenzi wako ila ukiwa unapiga moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe 

Tiba Ya Tatizo Lako Ni Dawa Hiitwayo Simpo Power No, 1; dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge vya miti shamba na unga ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja :-1 itakufanya urudie tendo zaidi ya mara tatu 
2 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-20 kwa tendo la Kwanza 
3 huimarisha uume uliolegea na kusinyaa 

Je Una Mke Au Mpenzi Aliyebalikiwa Kuwa Na Kario Kubwa Au Mwili Mnene Na Wewe Mume Wake Una   Maumbile Mafupu?; tumia sasa dawa ya PROMIX dawa itakufanya umfikishe shemu nyeti maana inaboresha maumbile saizi upendayo.

Dawa zangu haziina madhara yoyote kwa mtumiaji 

MARKSU; ni dawa ya kisukari dozi siku 21 
MWARU; ni dawa ya uzazi,hufungua milija ya uzazi ata kwa Wale waliofungiwa uzazi  
MTUNDUU; ni dawa ya busha bila kupasua 
MAZANZA; ni dawa ya kisukar zipo dawa za miguu Kuuma,tumbo,kupunguza Matiti,kutoa minyama uzembe ngiri,vidondo vya tumbo  

FIKA OFISINI KWANGU BUGURUNI MALAPA KARIBU NA KOTA ZA POLISI AU PIGA  SIMU ULETEWE MAHALI ULIPO SIMU NO : 0783185060 au 0752348593  -DR AGU

Polisi Wafanya Ziara ya Kushtukiza Kisiwa cha Mbudya

$
0
0
Kikosi cha Polisi cha Wanamaji jana kilifanya ziara ya kushtukiza katika kisiwa cha Mbudya na kukuta madudu kibao ikiwemo kutokuwepo kwa vifaa vya uokoaji na usalama.
 
Lengo la kufanya ziara hiyo, ni kuangalia usalama uliopo hasa katika kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka, ambapo Kamanda wa kikosi hicho, ACP Evans Mwijage alisema wamefanya ziara hiyo ili kuangalia shughuli zinazoendela na hawajafanya kwa kisiwa cha Mbudya, bali visiwa vyote vilivyopo kwenye bahari ya hindi.
 
Alisema wamefanya ziara hiyo ili kujihakikisha usalama kwenye visiwa hivyo, ambapo wanaamini changamoto walizoziona watazifanyia kazi ikiwemo kuhakikisha ajali za mara kwa mara zinazuiwa zisiweze kutokea na kuwepo kwa boti ya usalama mara kwa kisiwani hapo.
 
Uamuzi huo, umetokana na hali ya usafiri kuelekea kisiwani hapo kuwa sio salama na mamlaka husika kutakiwa kuchukua hatua madhubuti kudhibiti matukio ya ajali za mara kwa mara majini, imeelezwa.
 
Taarifa za kiuchunguzi  zinaarifu  kuwa ajali za boti kwenda kisiwani humo, zinatokea mara kwa mara lakini zingine zinakuwa haziandikwi kutokana na vifo vya watu hao, kutojumuisha watu maarufu na inapotokea mtu maarufu ndio inaripotiwa kwenye vyombo vya habari.
 
Mbudya ni Moja ya visiwa vilivyopo katika pwani ya Kaskazini mwa jiji la Dar Es Saalam, Maeneo ya Kunduchi.

Ni eneo ambalo ni tengwa kwa lengo la kulinda na kuhifadhi viumbe wa baharini wanaopatikana eneo hilo. Hata hivyo, eneo hilo wageni hawazuiliwi kwenda na kupumzika kisiwani hapo. 


Watu wengi hivi sasa wamekuwa wakikitumia kisiwa hiki kama eneo la mpumziko ya weekend na siku nyingine za wiki huku wengine wakienda mbali hadi kupiga kambi ndani ya kisiwa.

Kipo chini ya Wizara ya Uvuvi (Sio Utalii na Maliasili). Kimsingi kuna njia moja kuu ya kuweza kufika hapo ambayo ni kwa njia ya Boti.

Rais Magufuli Akabidhiwa Majina ya Vigogo Serikalini Waliokatiwa Tiketi za Ndege Lakini Hawakusafiri

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege la Tanzania ATCL Ladislaus Matindi, ameeleza tayari ameshamkabidhi Rais Magufuli orodha ya majina ya viongozi ambao walikatisha safari zao za ndege katika shirika hilo licha ya kukatiwa tiketi za serikali.
 
Akizungumza Jijini Dar es salaam, Mkurugenzi Mkuu wa ATCL, Ladislaus Matindi, amedai wameshatekeleza agizo hilo la Rais Magufuli ambalo alilitoa kwenye hafla ya upokeaji wa ndege mpya ya Tanzania A220-300 aina ya Airbus.

"Majina ya vigogo husika tumeshayakabidhi kwa Rais, tangu tumeelekezwa tulifanyia kazi maelekezo hayo na kisha tukayakabidhi sehemu husika.

“Siwezi kutaja ni vigogo wa kada gani, ukitaka kujua, wasiliana na Ofisi ya Rais wataweza kuwa na majina pamoja na Idara au Taasisi wanazotoka, sisi tumepeleka orodha,” ameongeza Luhindi.

Disemba 23, mwaka huu, alipokuwa akipokea ndege mpya ya tano aina ya Airbus A220-300, Rais Magufuli, aliagiza mishahara ya vigogo wa serikali wanaokadiriwa kufikia 100, ambao wamekuwa wakikatiwa tiketi za ndege na hawasafiri, ikatwe ili kufidia hasara iliyopatikana.

Tanzania kuuza mazao kwa Muda wa Miezi Minne bila kodi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)

$
0
0
Jitihada zilizofanywa na uongozi wa Serikali Mkoa wa Songwe, umefanikisha wafanyabiashara wa Tanzania kupata kibali cha kuuza mazao ya chakula katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), kwa muda wa miezi minne bila kutozwa ushuru.
 
Taarifa ya Chemba ya Biashara Nchini (TCCIA), iliyotolewa
jana kwenda kwa wafanyabiashara ilieza kuwa wamepokea barua kutoka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kwamba, Ofisi ya RAS-Songwe kwa kushirikiana na TCCIA walifanyia kazi fursa ya kuuza mazao ya chakula huko DRC kwa upendeleo maalum na kufanikiwa.
 
“Kwamba katika uongozi wa Mkoa wa Songwe, umefikia makubaliano na uongozi wa Jimbo la Haut-Katanga na jimbo hilo limetoa Kibali cha miezi minne (4), kuanzia Desemba 1, 2018 hadi Machi 31, 2019 kwa wafanyabiashara wa Tanzania kuuza chakula katika jimbo hilo kwa kiwango chochote walichonacho pasipo kulipa ushuru,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.
 
Aidha, makubaliano hayo yameeleza kuwa baada ya kipindi hicho hawataruhusiwa kuuza kwa utaratibu wa kawaida ikiwa ni pamoja na kulipa ushuru.
 
Pia kwa makubaliano hayo, tani moja ya mahindi itauzwa kwa Dola za Kimarekani 350 sawa na zaidi ya Sh 700,000 za kitanzania na unga wa mahindi utauzwa kwa kiasi cha tani moja pia utauzwa kwa Dola 400 sawa na zaidi ya Sh 800,000.
 
Maharage na mchele kwa tani moja itauzwa kwa Dola 1,120 sawa na zaidi ya Sh Milioni 2.4 za kitanzania
 
Vilevile, taarifa ilieleza kuwa bei hizo ni pamoja na gharama za uchukuzi .na kwamba wafanyabiashara wote wameshauriwa kutumia fursa hiyo.
 
Mara kadhaa nchi ya DRC imekuwa ikikumbwa na uhaba wa mara kwa mara wa chakula kutokana na mapigano ya serikali na vikundi vya waasi hali inayofanya wananchi wasiweze kulima kwa ufasaha.

RC Makonda Atoa Ujumbe Mzito Kwa Viongozi wa Dini....Kakobe Afunguka Sakata la Kuitwa Mkosoaji

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amesema anatamani kuwa kiongozi wa dini kuliko kazi ya Ukuu wa Mkoa.
 
Makonda alitoa kauli hiyo ijini Dar es Salaam jana, alipozungumza na viongozi wa dini wa madhehebu mbalimbali na kuongeza kuwa wakati akiwa chuoni aliandaa semina za dini ambazo zilihudhuria na wanafunzi wengi.
 
“Ukiniiuliza kazi gani ninayoipenda nadhani nitakwambia hii ya kuwa kiongozi kwa dini kuliko ya Ukuu wa mkoa. Napenda kukaa katika nyumba ya bwana siku zote za maisha yangu,”alisema Makonda.
 
Alisema kitendo cha kukusanyika kwa viongozi hao wa dini kutoka madhehebu mbalimbali kwake ni utukufu kutoka kwa Mungu.
 
“Nimeona nianzishe utamaduni wa kukutanisha viongozi wa dini. Mwaka 2012 mkutano nilifanya mkutano wangu wa mwisho wa 18 na Mchungaji Christopha Mwakasenge katika viwanja vya vyuo vya Ushirika ambapo uwanja mzima ulijaa,”alisema.
 
Naye Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe, alisema wengi wanajua kwamba yeye ni mkosoaji lakini hawajui kuwa pia ni msifiaji.
 
“Nampongeza Makonda kwa wito huu na alitaka kufahamu kuwa kama nitakuja au la, nilimwambia kusudi la hafla hii ni kuujenga mwili wa Kristo, sasa kama ni mtumishi wa Mungu sitaki kujenga mwili wa Mungu nitajenga kitu gani,”alisema.
 
Alisema kuwa amekuwa katika huduma kwa miaka 30, hajawahi kuona kusanyiko la watumishi wa Mungu kutoka madhehebu mengi mbalimbali jijini Dar es Salaam.
 
Alisema kuwa kukusanya watumishi wa Mugu kutoka madhehebu mbali mbali ni jambo linalohitaji upako.

Mkuu wa mkoa wa Pwani Awatangazia Kiama MAFATAKI Waliowapa Mimba Wanafunzi 16

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Pwani, mhandisi Evarist Ndikilo amewaagiza wakuu wa wilaya katika mkoa huo kuhakikisha wanawapa misukosuko na kuwakamata waliohusika kuwapa mimba wanafunzi 16 na kusababisha kushindwa kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi.
 
Ndikilo alisema serikali haiwezi kuvumilia watu hao waendelee kutamba mitaani wakati wameharibu maisha ya wasichana wadogo, huku akiwataka wazazi na walezi kuacha kumaliza kesi za mimba za utotoni majumbani.
 
Alisema wazazi kwa kiasi wanachangia watoto wao kuharibika kwa kuwa wamekuwa tayari kurubuniwa kwa fedha ili kuwaachia huru wanaobainika kuwapa mimba watoto wao wa kike.
 
Kuhusu kushuka kwa ufaulu Ndikilo alisema wanafunzi 223 ambao ni sawa na asilimia 0.74 hawakufanya mtihani wa kumaliza darasa la saba, kutokana na utoro 149,mimba 16 ,ugonjwa 15,vifo tisa na sababu nyingine 34.
 
Alitaja tatizo jingine kuwa ni utoro,mdondoko suala ambalo linachangia kushusha taaluma.
 
“Tuna kazi ya ziada kukabiliana na mdondoko mashuleni, tunalea watoto kuacha shule, wilayani Mkuranga mdondoko ulikuwa 67,Kibiti 36,Chalinze 36,”

“Kisarawe wanne, Bagamoyo 12,Mafia wanne, Kibaha Mjini tisa na Kibaha Vijijini wanne “alifafanua Ndikilo.
 
Awali katibu tawala mkoani hapo, Theresia Mbando alieleza, idadi ya wahitimu waliosajiliwa kufanya mtihani ,walikuwa 30,010 kati yao wavulana 14,304 na wasichana 15,706 ambapo waliofanya mtihani huo ni watahiniwa 29,787 wakiwemo wavulana 14,182 na wasichana 15,605 sawa na asilimia 99.26.
 
Ofisa elimu mkoa Abdul Maulid alisema, halmashauri ya Chalinze waliopata mimba ni Tisa, Mkuranga wanne ,Bagamoyo mmoja, Kisarawe mmoja na Rufiji mmoja.
 
Alieleza kuwa licha ya hali hiyi matokeo yanaonyesha kupanda kwa ufaulu kimkoa kutoka asilimia 66.9 mwaka jana hadi asilimia 77.79 mwaka huu.

Kutana Na Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Yanayosumbua Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume

$
0
0
Kutana Na Bingwa Wa Magonjwa Yote Sugu Yanayosumbua Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha, Nguvu Za Kiume, Kisukari, Mivuto Yote, Kusafisha Nyota, Kurudisha Mali, Nk.


Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:

KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni NYASOSE MIX, Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1. MKEBE NO.1 Hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa    dk 20 hadi 40 tendo la kwanza bila kuchoka naitakufanya uwe na hamu ya kuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

MHESHA POWER
MKEBE NO 2 ni dawa ya kuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu,
KISUKARI, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ITINYA,
Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,hupandisha cheo humfanya mfanyakazi apendwe na mwajiri wake, humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa pia ana pete za bahati ambazo zimetajilisha wengi.

SUPER POWER,
Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL/KANISANI

SIMU NO 0652 102 152/0755 684 297/0788 330 105.

HUDUMA HII UNAWEZA KUIPATA/KULETEWA MAHALI POPOTE NCHINI

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

Bondia Francis Cheka Afunguka Baada ya Kupewa Kipigo Kizito na Dullah Mbabe

$
0
0
Bondia Francis Cheka amekubali yaishe kwa Abdallah Pazi (Dullah Mbabe)  baada ya kuchapwa kwa Knock Out raundi ya sita ya pambano lililokuwa la raundi 12 la kuwania ubingwa wa mabara wa WBF kwenye uzani wa super middle.
 
"Sijui kilichotokea,  Nilijikuta tu niko chini raundi ya sita na sikuendelea tena na pambano, " alisema Cheka.
 
Katika pambano hilo lililopigwa kwenye ukumbi wa PTA, Sabasaba mashabiki wa Cheka waliduwazwa na kipigo hicho.
 
"Sina namna zaidi ya kukubaliana na matokeo, Nimepigwa kihalali, sijui nilipatwa na nini kwani sikuwa natembea ulingoni,  Muda mwingi nilicheza kwenye kamba wakati si kawaida Yangu,.
 
Cheka alidai kipigo chake hakijasababishwa na umri au kiwango chake kushuka isipokuwa mpinzani wake alimuotea tu na kushinda.
 
"Hadi sasa sijui nimepotezaje pambano hilo, lakini pamoja na kupoteza siwezi kustaafu ngumi kwa sasa, " alisema.
 
Hata hivyo Dullah Mbabe ametamba kwamba kipigo hicho kwa Cheka si cha kubahatisha alijiandaa kumnyamazisha bondia huyo bingwa wa zamani wa dunia wa WBF.

Huna Sababu ya Kuabika Tena, Jipatie Dawa Bora ya Nguvu za Kiume, Maumbile Madogo na Mvuto wa Mapenzi

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiathiri watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine ....kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapungufu katika mwili wake.

Kuna sababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huathiri misuli ya uume, 


Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0620510598  / 0743543944

Vigogo Mabasi ya Mwendokasi Waachiwa Kwa Dhamanaa Baada ya Kukaa Mahabusu Siku 60

$
0
0
Wafanyakazi saba wa Kampuni ya Uda-Rapid Transit (UDART), akiwamo kigogo wa idara ya fedha, wanaodaiwa kuhusika katika mtandao wa uhujumu wa mapato ya mabasi ya mwendokasi kwa kuchapisha tiketi feki kwa abiria wameachiwa kwa dhamana.

Hatua hiyo imekuja baada ya kushikiliwa kwa zaidi ya siku 60 na Jeshi la Polisi huku wakiendelea kusubiri uamuzi wa jalada lao ambalo lipo kwa mwanasheria mkuu wa Serikali, likisubiri hatima yao kama kufikishwa mahakama ama laa.

Pamoja na kuachiwa, wafanyakazi hao ambao awali walikuwa wanane wametakiwa kuripoti Kituo Kikuu cha Polisi mara kwa mara huku upelelezi wa kesi yao ukiendelea.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa jana alisema tuhuma zinazowakabili wafanyakazi hao ni za kughushi na kuhujumu mapato ya mradi wa mabasi ya mwendokasi, hivyo upelelezi wake unachukua muda mrefu ili kuhakikisha wanapata mtandao mzima.

Alisema awali Jeshi la Polisi lilikuwa linawashikilia wafanyakazi wanane, lakini upelelezi ulipokuwa unaendelea, walilazimika kuwaongeza wafanyakazi wengine watatu.

“Tumelazimika kuwaachia kwa dhamana kwa sababu upelelezi wa kesi yao bado unaendelea, awali walikuwa wafanyakazi wanne, lakini tumelazimika kuongeza wengine watatu na kufikia saba,” alisema.

Mambosasa alisema jalada la watuhumiwa hao lipo mikononi mwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) ili aweze kulikagua na kuangalia taratibu za kisheria zinazopaswa kuchukuliwa ili kufikishwa mahakamani.

Alisema upelelezi umechukua muda mrefu kutokana na tuhuma za kughushi zinazowakabili ambazo zimehusisha mtandao wa kihalifu.

Mambosasa alisema Jeshi la Polisi litaendelea kuwakamata na kuwafikisha kwenye mikono ya sheria wale wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vya kihalifu pamoja na kwenda kinyume na sheria za nchi.

Wafanyakazi wanane wa Udart walikaa mahabusu zaidi ya miezi miwili baada ya kukamatwa wakidaiwa wanajihusisha na mtandao wa tiketi za kughushi huku wengine 18 wakiachiwa kwa dhamana.

Awali, Kamanda Mambosasa alidai kuwa watuhumiwa hao wamefanya kosa la kuhujumu mradi wa Serikali ambao ni wa kitaifa na kimataifa kwa kutaka kufifisha jitihada za Serikali.

Tundu Lissu Akubali Kugombea Urais 2020 Kama Atapitishwa na Chama Chake

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu amesema yupo tayari kugombea urais ikiwa vyama vya upinzani vitampa ridhaa hiyo.

Lissu ambaye yupo nchini Ubelgiji akipatiwa matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi zaidi ya 30, Septemba 7 mwaka jana akiwa Dodoma na watu wasiojulikana, amesema hayo jana katika mahojiano na na gazeti la Mwananchi

Mwanasiasa huyo alisema yeye ni mwanachama wa Chadema na hawezi kufanya jambo pasi na kuridhiwa na chama chake au vyama washirika wa Chadema kwani kufanya hivyo ni kinyume cha taratibu na maadili.

Kauli ya Lissu kuhusu kugombea urais mwaka 2020 imetokana na swali aliloulizwa kutokana na kuwa miongoni mwa wanasiasa wa upinzani wanaotajwatajwa, “Wakikaa katika vikao na kunipa bendera, nitakubali kubeba msalaba huo mzito kwa mikono miwili.”

Pia aliulizwa, ikiwa hataombwa na chama atajitosa mwenyewe kuwania nafasi hiyo? Rais huyo wa zamani wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) alisema, “Maadili yangu, unaambiwa ukiwa katika chama lazima upewe fursa kwa hiyo nitasubiri fursa hiyo.”

Kuhusu afya yake, Lissu ambaye ni mnadhimu mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni alisema anatarajia kuanza mwaka akiwa hana vyuma alivyowekewa Julai 9 katika mguu wake wa kulia ili kuunganisha mifupa.

“Desemba 31 nitafanyiwa upasuaji wa mwisho wa kuondoa hii antena ambayo nimekaa nayo kwa miezi sita tangu Julai 9 na nimeelezwa na madaktari kuwa mfupa uliokuwa uunge umeunga na mfupa uliotakiwa kuota unaendelea vizuri,” alisema Lissu na kuongeza:

“Yaani Jumatatu (Desemba 31) nitahitimisha kazi ya kitabibu na nitaanza mwaka mpya (2019) na mguu mpya ambao hauna chuma.”

Lissu alisema baada ya kuondolewa kwa vyuma, kitakachofuata ni mazoezi ya kutembea na taratibu ataachana na magongo.

Baada ya hapo, Lissu alisema ataanza kuhudhuria vikao mbalimbali ambayo amealikwa katika mataifa ya Ulaya.

Alisema Januari 14 amealikwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) na Umoja wa Ulaya (EU) Brussels, Ubelgiji na Februari mwakani amepata mwaliko wa wiki moja huko Washington Marekani.

“Huko kote nakwenda kuzungumzia kile kilichonitokea Septemba 7 (mwaka jana) lakini kile ambacho kinaendelea nyumbani (Tanzania) na mambo mengine,” alisema.

Alipoulizwa kwamba kuanza wake kusafiri nchi mbalimbali bila shaka ni wakati wake wa kurejea nyumbani, mwanasheria mkuu huyo wa Chadema alisema, “Katikati ya mwakani naweza kurejea. Kuanza mazoezi hakutanizuia kurejea kwani naweza kurudi nyumbani na nikawa nakuja huku (Ubelgiji) kwa madaktari.”

Hata hivyo, Lissu alisema hilo la kurejea nchini litafanikiwa baada ya kufanya mazungumzo na watu mbalimbali ikiwamo viongozi wenzake wa kisiasa pamoja na Serikali.

“Serikali itapaswa kunieleza usalama wangu utakuwaje baada ya kurejea, ingawa jukumu la Serikali ni kulinda raia wake na mimi ni miongoni mwao hasa ukizingatia kile kilichonitokea,” alisema.

Akigusia harakati zake za kupigania demokrasia, Lissu alisema , “Kama nilivyowahi kusema, sitarudi nyuma na mapambano ya kupigania demokrasia si ya wanasiasa pekee, bali makundi mbalimbali kama madaktari, waandishi wa habari, wakulima, wavuvi, bodaboda na wengine.”

Credit: Mwananchi

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania AKANUSHA Tuhuma za Fastjet Kuzuiwa Kuingiza Ndege Nchini

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania Hamza S. Johari  leo Disemba 27, 2018 amezungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Kampuni ya Fastjet  kuzuiwa kuingiza ndege hapa nchini pamoja na tuhuma kibao walizozitoa wakidai AirTanzania inapendelewa.

==>>Hapo chini kuna nukuu ya mambo machache aliyoyasema.

1.FastJet hawakuwa na ndege hata moja hivyo kama mamlaka ya TCAA hatuna budi kuwazuia, wanamadeni ya 6 billion  japo wamelipa kidogo, lakini sheria inawataka walipe yote, hivyo kama wao wanahitaji kufanya biashara wafuate masharti na walipe madeni. 

2.Tulipata taarifa kupitia vyombo vya habari kwamba tarehe 22 Disemba 2018  wangeleta hizo ndege zao, lakini mamlaka haikuwa na taarifa hizo na wao utaratibu wa kuingiza ndege nchini wanaujua.

3.Ilipofika Tarehe 24 Disemba 2018  saa 6 mchana ndo wakatuma email  ya maombi ya kuleta ndege  hizo zenye usajili wa Afrika Kusin. 

4.Ikumbukwe kwamba, tarehe 25 ilikuwa ni sikukuu na tarehe 26 ilikuwa ni Boxing Day hivyo sote hatukuwa ofisini. Wanaposema et tumewazuia kuzileta ni waongo. 

5.Katika notisi ya siku 28 tuliyowapa, tuliwataka Fastjet walete andiko la kudhibitisha uwezo wa kufedha ili kuona kama wanajiweza na pia walete Meneja Mwajibikaji mwenye utaalamu na mambo ya ndege. Fastjet hawakuletea hivyo vitu

6.Badala yake Tar 24.12.2018  ndo sasa wakaleta  maombi na barua ya mkurugenzi mtendaji wa Fastjet  Lawrence Masha  wakitujulisha kuwa Lawarence Masha amejiteua mwenyewe  kuwa accountable manager. 
 
7.Fastjet waache mzaha. FastJet itakufa kwasababu zao wenyewe maana wanamatatizo mengi, TCAA tunasimamia sheria ili kulinda usalama wa abiria, kulinda maslahi ya watoa huduma (supplies). Habari zote zilizoelezwa si za kweli ni upotishaji mtupu.
 

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images