Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Wimbo Mpya wa Linex - Kaa nami


Video Mpya ya Young Killer Msodoki Ft. Dela - Wakipekee

$
0
0
Video Mpya ya Young Killer Msodoki Ft. Dela - Wakipekee

Waziri Luhaga Mpina Aibua Kashifa ya Kuingizwa Nyama Mbovu Nchini.....Asema Kamwe Tanzania Haiwezi Kugeuzwa Dampo

$
0
0
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amesema Serikali haitakubali Tanzania kugeuzwa kuwa dampo la bidhaa za mifugo zilizokwisha muda wa matumizi na kuua uwekezaji kwa manufaa ya watu wachache.
 
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Saalam juzi, wakati wa kutoa matokeo ya ‘Operesheni Nzagamba’ iliyoendeshwa kwa vipindi viwili tofauti, Waziri Mpina alisema kilo 26,295 za bidhaa za nyama na maziwa zimekamatwa,baada ya kuingizwa nchini kutoka nje bila vibali, kulipiwa ushuru wala kuhakikiwa ubora wake.
 
Pia kilo 2,376 za bidhaa za nyama na maziwa yaliyokwisha muda wa matumizi nazo zikikamatwa zikiuzwa maeneo mbalimbali na kuhatarisha afya za walaji na kuingia katika hatari ya kupata magonjwa makubwa ikiwemo saratani.
 
“Hatutakubali kuua uwekezaji, viwanda na ajira za Watanzania kwa manufaa ya watu wachache, hatutakubali kuziweka rehani afya za watanzania eti kwa sababu ya uwekezaji operesheni hizi zitaendelea hadi pale wahalifu hao watakapoacha mchezo huu mchafu,” alisema Mpina.

Alisema hivi karibuni kwenye mitandao ya kijamii kuliibuka taharuki juu ya hatua zinazochukuliwa na Serikali dhidi ya wahalifu katika operesheni inayoendelea katika maeneo mbalimbali nchini.
 
Alisema operesheni hiyo, inayoendeshwa kwa mujibu wa sheria ina lengo la kudhibiti uingizaji holela wa mazao ya mifugo nchini, kudhibiti uuzaji wa mazao ya mifugo, pembejeo na chakula cha mifugo kilichokwisha muda wa matumizi na utoroshaji wa mifugo na mazao yake nje ya nchi. 

Alisema kilo 17,712 za pembejeo za mifugo zilizokwisha muda wa matumizi zilikamatwa, huku kilo 880 za nyama na maziwa ambazo hazina lebo wala taarifa yoyote katika vifungashio pamoja na usajili kutoka mamlaka husika nazo zikikamatwa.
 
Alisema tani 25,423 za chakula cha mifugo zilikamatwa zikisafirishwa kwenda nje ya nchi bila vibali ambapo katika uhakiki wa hesabu za ulipaji ushuru kwa kampuni chache zilizofanyiwa uhakiki katika kipindi cha mwaka wa fedha 2017/18, ilibainika Sh bilioni 4.25 zilikwepwa kulipwa


Alisema ng’ombe 40,954, mbuzi na kondoo 165,115 nazo
zilikamatwa zikiwa zinatoroshwa kwenda nje ya nchi bila vibali na bila kulipa ushuru wa aina yoyote huku zaidi ya ng’ombe 50,000 zilikamatwa zikiwa zimeingia nchini bila vibali
 
Katika operesheni hiyo,vifaranga 21,100 na mayai 21,480 yalikamatwa yakiingia nchini bila vibali ambapo yalitaifi shwa na Serikali kisha kuketetezwa.
 
Alisema licha ya bidhaa zinazoingizwa nchini bila vibali na huku Tanzania ikiwa na mifugo mingi, uagizaji wa bidha za mifugo kutoka nje ya nchi ni mkubwa nchini ambapo uagizaji wa bidhaa za nyama nchini umefi kia thamani ya wastani wa sh. bilioni 10 huku maziwa ikiwa ni wastani wa sh bilioni 30 kwa mwaka.
 
Waziri Mpina ametaja baadhi ya madhara ya uingizaji holela wa bidhaa hizo nchini ikiwemo kuathiri afya za wananchi kunakoweza kusababisha maradhi sugu ikiwemo saratani.

Sikukuu Ya Krismasi Yawa Chungu Kwa Machangudoa Singida, Zanzibar

$
0
0
Wamikili wa nyumba saba  Zanzibar ambazo ni maarufu kwa kufanyiwa biashara ya ukahaba ‘machangudoa’ wametakiwa kuripoti kwa Kamanda wa Polisi, Mjini Magharibi, Zanzibar ifikapo kesho.

Hatua hiyo kwa wamiliki wa nyumba hizo visiwani humo kunatokana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa huo kufanya operesheni ya kudhibiti biashara hiyo ambapo watu 22 wanaofanya biashara hiyo walikamatwa katika nyumba hizo zilizoko katika maeneo ya mkoa huo.

Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Ayoub Mohammed Mahmoud, alitoa agizo hilo baada ya operesheni hiyo.


Akizungumza baada ya operesheni hiyo, Mkuu wa mkoa huyo, alisema wamiliki wa nyumba hizo wanatakiwa kuripoti ifikapo saa nne asubuhi na atakayekaidi agizo hilo atachukuliwa hatua.

Alizitaja nyumba hizo ni zilizoko katika maeneo ya Raha Leo, Mwembe Shauri, Miembeni, Kikwajuni Juu na Kilimani na kwamba kamati ya ulinzi na usalama imejiridhisha kwenye nyumba hizo zinafanywa biashara za ukahaba.


Alisema biashara hiyo si halali, hivyo aliwataka wanaofanya biashara hiyo kuacha na watafute shughuli nyingine ya kujipatia kipato halali.


Wakati wamiliki wa nyumba hizo Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar wakitakiwa kuripoti polisi kesho, Polisi mkoani Singida imefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 11 wakiwemo wanawake 10 na mwanaume kwa tuhuma za kujihusisha na kufanya biashara ya ukahaba mjini Singida.

Kamanda wa Polisi, Mkoa wa huo , Sweetbert Njewike, alisema watuhumiwa hao walikamatwa kutokana na misako wa kubaini vitendo vya uhalifu na wahalifu wa makosa mbalimbali katika Mji wa Singida na viunga vyake.

Alisema msako huo ulifanyika Desemba 18 na 19, mwaka huu, katika maeneo ya Serengeti, kata ya Majengo na kufanikiwa kuwatia mbaroni watuhumiwa hao.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

Huna Sababu ya Kuabika Tena, Jipatie Dawa Bora ya Nguvu za Kiume, Maumbile Madogo na Mvuto wa Mapenzi

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiathiri watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine ....kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapungufu katika mwili wake.

Kuna sababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huathiri misuli ya uume, 


Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0620510598  / 0743543944

Shirika la Madini la Taifa (Stamico) lakabidhiwa mtambo wa kisasa kuchoronga miamba

$
0
0
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Prof. Simon Msanjila, amelitaka Shirika la Madini la Taifa (Stamico) kutumia mtambo wa kuchoronga miamba kwa ufanisi ili kuliletea tija taifa.

Prof. Msanjila aliyasema hayo juzi wakati wa hafla fupi ya kuukabidhi rasmi mtambo huo kwa Stamico kwa ajili ya kuanza kuutumia rasmi.

Alisema ununuzi wa mtambo huo ni uwekezaji mkubwa ambao serikali imeufanya kwa Stamico, hivyo shirika hilo halina budi kuutumia vyema ili kuleta tija.

Kuhusu gharama za mtambo huo, Prof. Msanjila, alisema umegharimu Dola za Kimarekani milioni 1.3, ambazo akiwa mtendaji mkuu wa wizara anaona ni deni kubwa kwake, hivyo kuahidi kuusimamia ipasavyo ili kuhakikisha unazalisha faida na kuwa chachu ya kununua mitambo mingine kama hiyo ili kukuza sekta ya madini nchini.

Pia alilitaka shirika hilo kujitangaza vyema ili wananchi, hususan wadau wa madini wanaojihusisha na shughuli za uchimbaji na utafutaji, kufahamu uwepo wa mtambo huo ili utumike hata kwa kampuni binafsi ili kujiongezea kipato na pia kuwasaidia wachimbaji wadogo wa madini.

“Kwa zabuni nilizozisikia mpaka sasa mtambo huu utazalisha pesa za kutosha,” alisema.

Prof. Msanjila pia aliitaka Stamico kuwasilisha taarifa za mapato na matumizi ya mtambo huo kila robo ya mwaka, ili kufanya tathmini endapo mtambo unatumika kwa faida.

Pia aliliagiza shirika hilo kuhakikisha mtambo huo unawezesha ununuzi wa mtambo mwingine mpya kila mwaka, ili ndani ya miaka mitano shirika limiliki mitambo mitano na kurahisisha utekelezaji wa shughuli za uchimbaji na utafutaji wa madini.

Orodha ya wasanii watakaoperform katika show ya funga mwaka na King Kiba

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya  Ali Salehe Kiba alimaarufu Alikiba ameweka wazi orodha ya wasanii watakaoperform katika show yake ya funga mwaka na king kiba.

Katika Orodha hiyo wamo Mr Blue, Mwana Fa,Barnaba classic, Nuh Mziwanda, The Mafikh, Billnas, na kundi lake la The Kings music, na wengineo wengi ambapo show hii itafanyika katika ukumbi wa Next door Arena Masaki jijini Dar Es Salaam.

Kiba amewasisitiza watu kuwahi kwa ajili ya kwenda kupata burudani nyingi hasa kutoka kwa mkongwe wa Bongo fleva Mwana Fa. Alikiba aliandika hivi kuhusu Mwana Fa:-

“Labda siku nyingi hujamuona @mwanafa kwenye jukwaa. Unahitaji kusikia mashairi yake ya kitambo na ngoma kali za hapo juzi kati kama #AsanteniKwaKuja#Sielewi#DumeSurualina nyingine.

Kiu ya burudani za Falsafa itakatwa Jumamosi hii pale Next Door Arena kwenye #FungaMwakaNaKingKiba. Hakikisha unanunua tiketi yako mapema.

Bila shaka unyunyu wa @fynbyfalsafautapatikana pale pia.
#mofayabyalikiba
#FungaMwakaNaKingKiba
#KingKiba”

Msako Mkali wa Silaha Kuanza Zanzibar....Wanaozimiliki Kinyume na Utaratibu Wapewa Siku 5 Kuzisalimisha

$
0
0
Jeshi  la Polisi Zanzibar, limetoa siku tano kuanzia jana kwa watu wanaomiliki silaha kinyume na utaratibu wazisalimishe katika vituo vya polisi visiwani humu.
 
Limesema baada ya kipindi hicho, litafanya operesheni ya kuwatafuta wamiliki hao na kuwachukulia hatua.
 
Kauli hiyo ilitolewa na Kamishna wa Polisi Zanzibar, Mohamed Haji Hassan na kusema kwa upande wa Zanzibar, silaha zilizoruhusiwa kutumiwa ni shotgun na gobore huku bastola zikiwa zimeruhusiwa kutumika Tanzania Bara.
 
Kamishna huyo aliwataka wanaomiliki bastola ambazo hufanya mipango kwa Tanzania Bara na kuingia nazo Zanzibar kutokana na sababu mbalimbali, kuzisalimisha kwenye vituo vya polisi.
 
“Kwa wanaomiliki bastola ambazo wamefanya mipango yao huko Tanzania Bara wanatakiwa kuzisalimisha na hawatakiwi kubaki nazo nyumbani kwani kwa kufanya hivyo ni uvunjifu wa sheria,” alionya Kamishna huyo.
 
Alisema Jeshi la Polisi limepata taarifa ya kuwepo kwa watu wanaomiliki silaha hizo kutojasajiliwa, hivyo aliwataka wale ambao silaha zao hazijasajiliwa wazisalimishe Makao Makuu ya Polisi Zanzibar katika kipindi hicho.
 
Alisema endapo kuna mtu anayetaka kuingia Zanzibar na bastola lazima akaisalimishe polisi na ataruhusiwa kuondoka nayo atakapoamua kurejea Tanzania Bara, kinyume na hivyo atakuwa anatenda kosa.
 
Kamishna Hassan aliongeza kuwa kwa mujibu wa sheria namba 2 ya mwaka 2015 ya Zanzibar kifungu cha 31 (1) kinachohusu udhibiti wa silaha za moto na milipuko, Kamishna wa Polisi ana mamlaka ya kufanya usajili wa silaha ndogo kwa matumizi binafsi.
 
Alisema silaha zilizoainishwa katika sheria kwa ajili ya matumizi au uwindaji wanyama waharibifu wa mazao shambani na si kwa matumizi mengine.
 
“Lengo la kuzuia silaha hizo ni kuimarisha ulinzi kwa raia na mali zao ambapo wapo baadhi ya watu ambao hutumia silaha hizo vibaya na kusababisha uvunjifu wa amani,”alisema

PICHA:Mapokezi ya wasanii wakaofanya ' Show ya Wasafi Festival Kenya

$
0
0
Wasanii watakaofanya show leo Jumatato  katika Tamasha la Wasafi Festival nchini Kenya kutoka Tanzania wamepokewa kwa shangwe kubwa na Wakenya hapo jana.

Awali show hiyo iliingiwa na sitofahamu baada ya msanii Diamond na Rayvanny kutoruhusiwa kufanya onesho nje ya nchi baada ya kufungiwa na BASATA kwa kosa la kuimba wimbo Mwanza ambao ulifungiwa na baraza hilo.

Lakini juzi baraza hilo lilitoa ruhusa kwa waimbaji hao ya kufanya enesho kwa madai adhabu ya kufungiwa ilikuja kwa wawili hao wakati tayari wameshaingia makubaliano ya enesho la Kenya.

Baada ya team hiyo kuwasili nchini Kenya, Rais wa WCB Diamond Platnumz aliwataka mashabiki kukaa mkao wa kula kwaajili ya enesho hilo la aina yake.

Mvutano waendelea ujenzi wa ukuta nchini Marekani

$
0
0
Pande zote mbili za kisiasa nchini Marekani bado zinavutana kuhusu ujenzi wa ukuta anaotaka kujenga Rais Donald kwenye mpaka na Mexico hazijapata ufumbuzi jinsi fedha zitakavyotumiwa katika kuujenga ukuta huo.

Katika taarifa ya pamoja, viongozi wa chama cha Demokratik seneta Chuck Schumer na mwenzake, spika Nancy Pelosi, wamemlaumu rais Donald Trump kwa mkwamo huo katika shughuli za serikali na pia kwa kuitumbukiza nchi kwenye matatizo. Wamesema Trump alitaka shughuli za serikali zikwame lakini kwa sasa anaonekana hajui vipi atajiondoa kwenye sakata hilo.

Kwa upande wake Trump alijisifu kwamba angeweza kuzikwamisha shughuli za serikali kwa ajili ya kupigania ujenzi wa ukuta, lakini sasa anawalaumu wanachama wa Demokratik kwa kukataa kuiunga mkono kura iliyohitajika kupitisha muswada wa bunge juu ya kuridhia Dola bilioni 5.7 anazotaka kwa ajili ya kujengea ukuta huo. Viongozi hao wa chama cha Demokratik wameelezea hasara kubwa iliyotokea kwenye soko la hisa la Wall Street pamoja na uharibifu uliosababishwa na hatua ya Trump ya kumuachisha kazi waziri wake wa ulinzi.

Ni mpaka hapo Trump, ambaye anataka kuujenga ukuta huo baina ya Marekani na Mexico, na wanachama wa chama cha Demokratik, ambao wanaipinga hatua yake hiyo watakapokubaliana, sehemu ya shughuli za serikali ya Marekani zitaendelea kufungwa.

Jana ilikuwa siku ya Krismasi na mkwamo huo umeingia katika siku yake ya nne na wala hakuna dalili kuwa hali hiyo itafikia mwisho wake hivi karibuni.

Wabunge wengi wameondoka kutoka kwenye jiji la Washington kwenda kujiunga na familia zao wakati ambapo kusherehekea Krismasi, rais Trump amebakia katika ikulu baada ya kuahirisha mipango ya sherehe za Krismasi katika makazi yake ya Florida.

Trump aliwaambia waandishi wa habari katika ikulu siku ya Jumatatu aliposhiriki kwenye mahojiano ya simu ambao ni utamaduni unaofanyika kila mwaka unaowashirikisha watoto na safari hii sana walitaka kujua ni lini baba Krismasi atawafikia waliko?. Trump amesema hakuna chochote kipya isipokuwa anachojua ni kwamba Marekani inahitaji usalama katika mpaka wake.

Trump alikutana Jumatatu na waziri wake wa ulinzi Kirstjen Nielsen na viongozi wengine wa idara ya usalama huku mazungumzo yakiendelea nyuma ya pazia kati ya wawakilishi wa serikali pamoja na wa vyama vya Republican na Demokratik.

Habari Njema Kwa Wenye Matatizo Ya Nguvu za Kiume, vitambi, nyama uzembe

$
0
0
HABARI NJEMA KWA MLIOATHIRIKA NA MAGONJWA YA MWILI NA AKILI.
Sasa dokta MBALU ana uwezo mkubwa wa kutibu magonjwa yaliyoshindikana,Kama umehangaika kwa muda mrefu bila mafanikio DK.MBALU Ni kiboko kabisaa.

TIBA ATOAZO NI:- (a)Vidonga vya tumbo,kilungulia,Tumbo kujaa gesi.
 (b)Kifua kikuu(TB),Pumu(ATHMA) na Rovu
(c)Miguu kuwaka moto,nyama za magoti kuuma,kiuno na mgongo.
(d)Uzazi na chango.
 (e)Nguvu za kiume,kurefusha na kunenepesha uume,busha,mshipa wa ngiri na tezi dume.
(f)Elimu mwanafunzi kuwa na uwezo mkubwa darasani na kufanya vizuri katika mitihani yake, kupandishwa cheo kazini, kulipwa madeni au mafao yako.
(g) kutoa ushauri nasaha kwa wenye matatizo ya kisaikolojia.

      AINA ZA DAWA.
NINJIWE:-,Hutibu vidonda vya tumbo,tumbo kujaa gesi,na kilungulia,vidonge 16 kwa muda wa siku nne na ya unga.
MPALAMA:-,Hutibu Kifua kikuu (TB), Pumu (ATHMA),na wenye tatizo la uvimbe katika koromeo yaani (ROVU),Huisha na kutorudi Tena.,dozi siku 6.

NKOLA:-,Hutibu miguu kuwaka moto,nyama za goti kuuma,kiuno na mgongo dozi siku 10.
MWATYA:-,Hutibu Uzazi au chango,dozi siku 30,na tatizo kupona kabisa.

LYONGO POWER:-,Hii ni dawa ya heshima kwa akina baba yenye uwezo wa kurefusha na kunenepesha uume kwa wale wenye maumbile madogo yaani (KIBAMIA).

NENGONENGO(4)POWER:-,Hutibu Nguvu za kiume na kuleta hamu ya tendo hivyo kuchelewa kufika kileleni na kuweza kurudia tendo zaidi ya mara (4),ina Nguvu mno Kama Ni muhanga wa tatizo hili   tumia NENGONENGO (4)POWER Ipo aina ya vidonge na unga dozi Ni siku 5 unapona kabisaa wahi Sasa.

NTUNDWA:-,Hutibu busha,mshipa wa ngiri na tezi dume,Busha dozi Ni siku (30),bila kufanyiwa operation,Mshipa wa ngiri dozi siku (4) na tezi dume dozi siku (10).

GWATA:-,kuuwa kesi na shauri kupangiwa tarehe za karibu zaidi na baadae kesi kufutiliwa mbali kabisaa.
NUGWANO:-, Humfanya mtu kuheshimika na kupandishwa cheo kazini pia kulipwa madeni au mafao kwa wakati muafaka.

NKOMA:-, Hurudisha mke,mme,hawara, mchumba ndani ya siku mbili atatimiza mahitaji yote hata Kama yupo mbali na kumfunga asiwe na mtu mwingine..

  Huduma zinatolewa ndani ya masaa 12,Saa moja asubuhi Hadi kumi na mbili jioni,DAR ES SALAAM NA KAHAMA wa mikoani unapata huduma kwa njia ya kusafirisha..na huduma yetu inakufikia ukiwa ofisini au nyumbani kwako..,


CONTACTS;  0744922982  au  0716, 608  ,959 au 0784475946

 OUR SERVICES ARE EASY.

Uchaguzi Ndani ya CHADEMA Waendelea Kutimua Vumbi

$
0
0
Vumbi la uchaguzi ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) limeanza kutimka katika maeneo mbalimbali ya nchi huku kikiwa kimepanga safu ya viongozi kwenye maeneo hayo kwaajili ya kusimamia chaguzi.

Uchaguzi huo unahusisha viongozi wa matawi, Kata, majimbo, mikoa na ngazi ya Kitaifa ulianza mapema mwezi huu ambapo wabunge wa Chadema wamegawana maeneo mbalimbali ya kusimamia.

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chadema John Mrema amesema kuwa, uchaguzi huo unaenda sambamba na vikao vya ndani kwaajili ya wagombea kupata nafasi ya kujinadi.

Amesema kutokana na kuzuiwa kwa mikutano ya hadhara nchini uchaguzi huo unatumia vikao vya ndani ambavyo hatahivyo katika baadhi ya maeneo vimekuwa kaa la moto huku chama kikiwatumia viongozi wenye ushawishi mkubwa wakiwemo wabunge kuongoza zoezi hilo.

"Huu ni mwaka wa uchaguzi ndani ya Chama na ndio maana tuko nchi nzima, tumesambaa kwa ajili ya kusimamia ili tuweze kuapata viongozi wazuri kuanzia ngazi ya msingi", amesema Mrema.

Mbunge wa Kibamba, John Mnyika ameshika majimbo ya Momba, Tunduma, Vwawa, Mbeya Mjini na Vijijini wakati Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa akisimamia majimbo yote ya mkoa wa Rukwa.

Mbunge wa Mbeya mjini, Jospeh Mbilinyi maarufu kama ‘Sugu’ anasimamia jimbo la Njombe Mjini.

Desemba 16, 2018 Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA -Zanzibar, Salum Mwalimu alikamatwa na Jeshi la Poilisi akiwa mjini Mafinga mkoani Iringa alikokwenda kushiriki moja ya kikao cha ndani akitokea Kanda ya Nyasa, ambapo kiongozi huyo ni moja ya safu iliyopangwa kusimamia chaguzi hizo katika majimbo ya Makambako, Makete, Ismani na Iringa Mjini.

Ndege za kivita za Israel za shambulia Syria

$
0
0
Inadaiwa kuwa ndege za kivita za Israel zimefyatua makombora kuelekea maeneo ya karibu na mji mkuu wa Syria Damascus jana usiku, na kulipiga ghala la silaha na kuwajeruhi wanajeshi watatu

Shirika la habari la Lebanon liliripoti kuwa ndege za kivita za Israel ziliruka katika anga ya kusini mwa Lebanon. Shirika la haki za binaadamu la Syria limesema mashambulizi ya angani ya Israel yaliyalenga maeneo matatu kusini mwa Damascus ambayo ni maghala ya silaha ya kundi la wanamgambo wa Hezbollah wa Lebanon na wanajeshi wa Iran.

Kwa mujibu wa Shirika la habari la Deutsche Welle (DW) Shambulizi hilo ni la kwanza tangu Rais wa Marekani Donald Trump alipotangaza wiki iliyopita kuwa Marekani itawaondoa wanajeshi wake wote 2,000 nchini Syria, hatua ambayo itaacha wazi udhibiti wa upande wa mashariki mwa Syria wenye utajiri wa mafuta. Hakujawa na taarifa yoyote kutoka kwa jeshi la Israel kuhusu shambulizi nchini Syria.

Mashambulizi hayo yanayoshukiwa kufanywa na Israel yamekuja siku mbili baada ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kusema kuwa kuondolewa kwa wanajeshi 2,000 wa Marekani kutoka kaskazini mashariki mwa Syria hakutoibadili sera ya Israel ya kuwalenga wanajeshi wa Iran nchini Syria. “Tutaendelea kuchukua hatua dhidi ya jaribio la Iran kuwa na uwepo wake kijeshi nchini Syria, na kama patakuwa na haja, tutatanua shughuli zetu nchini humo”. Alisema Netanyahu.

Israel imekuwa ikifanya mashambulizi kadhaa ya angani katika maeneo yanayoshukiwa kuwa ya jeshi la Iran na wapiganaji wa Hezbollah nchini Syria, ambako wanaunga mkono utawala wa Rais Bashar al-Assad.

Hata hivyo, Israel imewekewa kizuizi cha kufanya mashambulizi nchini Syria tangu Oktoba wakati Urusi iliipa Syria mfumo wa ulinzi wa anga aina ya S-300 ambao unayaharibu makombora yanayofyatuliwa na adui. Hilo lilijiri mnamo Septemba 17 wakati ndege ya kijeshi ya Urusi ilipoangushwa na mfumo wa ulinzi wa anga wa Syria wakati wa shambulizi lililofanywa na Israel.

Tukio hilo lilizusha mvutano kati ya Urusi na Israel, ambazo kawaida huwa na mahusiano mazuri na zina kiwango fulani cha ufahamu kuhusu Syria. Mashambulizi ya anga ya Israel yanachukuliwa na Urusi kuwa yanayoweza kuiyumbisha Syria ambako Urusi inalenga kuuyalinda mafanikio ambayo utawala wa Assad umepata katika vita vya vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo. wakati huo huo, wachambuzi wanasema Urusi inafahamu wasiwasi wa usalama ambao Israel iko nao kuhusu mpango wa Iran wa urutubishaji wa madini ya urani

CUF Upande wa Lipumba Wadai Maalim Seif Anampango wa Kuhamia ACT Wazalendo

$
0
0
Chama cha Wananchi (CUF) upande wa mwenyekiti wa chama hicho anayetambuliwa na ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba umedai Maalim Seif Sharif Hamad anajiandaa kuhamia ACT-Wazalendo.

Kimesema Maalim Seif ambaye ni katibu mkuu wa chama hicho kwa sasa yuko mbioni kutimkia ACT.

Akizungumza leo Jumatano katika mkutano na waandishi wa habari katibu wa kamati ya ulinzi na usalama wa CUF, Khalifa Suleiman Khalifa amedai vyama sita vya upinzani vilivyokutaka Zanzibar wiki iliyopita moja ya ajenda yao ilikuwa namna gani Maalim Seif atakubaliana na ACT-Wazalendo.

Amesema miongoni mwa makubaliano ni upande wa Maalim Seif uachiwe nafasi zote za uongozi upande wa Zanzibar na Zitto Kabwe ambaye ni kiongozi wa ACT, wachukue uongozi wa Tanzania Bara.

Amedai kuwa hata kama Maalim Seif ataondoka CUF, wataendelea kuwa imara huku akiwataka wote watakaoambatana na katibu mkuu huyo kwenda ACT kutosita kwa sababu uamuzi wao utaheshimiwa.

Mgogoro ndani ya CUF ulianza baada ya Lipumba kurejea katika uongozi mwaka 2016, ikiwa ni takribani mwaka mmoja tangu alipojiuzulu.

 Jambo hilo liliibua mgogoro wa uongozi baada ya ofisi ya msajili kutangaza kumtambua Lipumba kama mwenyekiti na kusababisha pande hizo mbili kukimbilia mahakamani na kufungua kesi kadhaa ambazo zinaendelea.

Diwani Ajinyonga Kwa Mtandio

$
0
0
Diwani wa zamani wa kata ya Nyerere, Unguja  Asha Ali Abei amejinyonga hadi kufa usiku wa kuamkia leo Jumatano Desemba 26, 2018.

Akizungumza leo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja, Kheri Musa amesema marehemu ambaye kwa miaka ya nyuma alikuwa diwani, alikutwa amekufa kwa kujinyonga akitumia mtandio alioufunga katika dirisha, tukio lililotokea katika shehia ya Magomeni.

Baadhi ya majirani wa marehemu walisema kwamba walipata taarifa za kifo hicho asubuhi baada ya mtoto wa marehemu kupiga kelele.

Sheha wa shehia ya Magomeni, Rajab Ali Ngauchwa amesema si vyema wananchi kuchukua hatua za haraka katika mambo yanayowachanganya

Amesena ni vyema  familia kukutana na kujadili ili kupata ufumbuzi wa tatizo kuliko watu kuchukua uamuzi kama huo wa kujitoa uhai.

Simba Wapigwa na Mashujaa 3-2.... Watupwa Nje Kombe la Shirikisho

$
0
0
Klabu ya soka ya Simba imeng'olewa katika michuano ya
shirikisho (Azam Sports Federation Cup) baada ya kupokea kichapo kutoka kwa Mashujaa FC .

Simba walikuwa wa kwanza kuandika bao dakika ya 18 kupitia kwa Paul Bukaba akimalizia shuti lililotemwa na mlinda mlango wa Mashujaa baada ya kutema shuti lililopigwa na Said Ndemla.

Kipindi cha pili Mashujuaa walisawazisha bao dakika ya 48 kupitia kwa Said Hamisi, bao la pili wakaandika dakika ya 57 kupitia kwa Jeremiah Josephat na msumari wa mwisho ukikomelewa na Rashid Athumani dakika ya 90 na mabao yote hayo ni kutokana na uzembe wa safu ya ulinzi na mlinda mlango Deogratius Munish 'Dida'.

Bao la pili la Simba liliandikwa dakika ya 60 baada ya faulo iliyopigwa na Clytous Chama aliyeingia dakika ya 60 akichukua nafasi ya Abdallah Seleman na kufungwa na Paul Bukaba dakika ya 80.

Mlinda mlango wa Mashujaa amekuwa ni shujaa kwa kuokoa mashuti ya washambuliaji wa Simba ambao mpaka mpira unaisha  wamecheza kona 10, huku mashuti mawili ya Rashid Juma na Mzamiru Yassin yakigoga mwamba.

Kikosi cha Simba kilikuwa na sura nyingi mpya ambazo zimekuwa hazipati nafasi kwenye kikosi cha kwanza ikiwa ni pamoja na kinda Abdallah Seleman, Asante Kwasi, Deogratius Munish.

 
Simba imeondolewa katika michuano hiyo kwa msimu wa pili mfululizo, ambapo msimu uliopita iliondolea katika hatua hii kwa kufungwa na Green Warriors kwa mikwaju ya penati 4-3.

Inabakiza nafasi mbili pekee za kupata tiketi ya kushiriki michuano ya kimataifa msimu ujao, ambazo ni Ligi Kuu Tanzania Bara endapo itaibuka bingwa pamoja na michuano ya Klabu Bingwa Afrika endapo itashinda ubingwa huo.

Hali Bado Tete Fastjet....Lawrance Masha Asema Serikali Imemzuia Kuingiza Ndege Nchini

$
0
0
Mwenyekiti mtendaji wa Shirika la Ndege la Fastjet Tanzania, Lawrance Masha amesema Serikali imemzuia  kuingiza ndege za shirika hilo nchini humo.

Waziri huyo wa zamani wa Mambo ya Ndani ametoa kauli hiyo leo Jumatano Desemba 26, 2018 wakati akizungumza na  na gazeti la Mwananchi, kubainisha kuwa ana matumaini kuwa baada ya kumalizika kwa sikukuu ya Krismasi huenda mambo yakawa mazuri.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Hamza Johari amesema kesho atazungumza na waandishi wa habari ili kufafanua yote yanayoendelea baina ya mamlaka hiyo na Fastjet.

Katika maelezo yake Masha amesema Serikali haimpi ushirikiano wa kutosha katika mkakati wake wa kulifufua Shirika la Fastjet.

Amesema wamemzuia kuingiza ndege aina ya Boeing 737-500 baada ya iliyokuwepo kuzuiliwa kuruka kwa madai kuwa inapata hitilafu mara kwa mara na shirika halina meneja mwajibikaji.

Desemba 19, 2018 akizungumza katika kipindi cha 360 kinachorushwa na televisheni ya Clouds, Masha alisema ndege hiyo ingewasili Tanzania Jumamosi iliyopita Desemba 22, 2018 lakini hadi leo saa sita mchana ndege hiyo ilikuwa haijafika.

Leo amebainisha kuwa ikiwa ataruhusiwa ndege hiyo itafika Tanzania ndani ya muda mfupi kwa maelezo kuwa kila kitu kipo tayari, “safari kutoka Afrika Kusini ilipo hiyo ndege hadi Tanzania ni mwendo wa masaa matatu tu.”

Amesema ndege iliyozuiwa ilikuwa imelipiwa tayari kwa kuruka ikiwa na wafanyakazi wote, hivyo kitendo cha kuizuia ni hasara.

“TCAA inasema ili niweze kuingiza ndege hiyo nimalize kwanza madeni yote, baadhi ya madeni tayari yamelipwa na Fastjet Plc mengine Fastjet Tanzania,” amesema.

“Tayari tumemaliza lakini fedha imeisha, kwa kuwa tayari fedha nyingine tulizitumia kutimiza matakwa yao, wangeniruhusu nifanye kazi ili nipate fedha ya kulipa yaliyobaki.”

Credit:Mwananchi

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya Disemba 27

Mwanamke Ajinyonga Hadi Kufa Ruvuma

$
0
0
Mkazi wa Kijiji cha Nakayaya, wilayani Tunduru mkoani Ruvuma Awetu Makunula (44), amejinyonga hadi kufa kwa madai ya kuchoka kusumbua wanafamilia kutokana na hali ya afya yake.

Taarifa za tukio hilo zinaeleza kuwa Makunula alikutwa akining`inia juu ya mti wa mkorosho jirani na nyumba ya wazazi wake, mjini hapa.

Mume wa marehemu Makunula, Salum Namtikwe, alisema kuwa usiku walilala wote na kabla ya tukio hilo aliamka majira ya saa 11 alfajiri na kumuaga kuwa anatoka nje kwa ajili ya kufagia nje ya nyumba yao ili amalize shughuli hiyo mapema na kwenda shambani.

Alisema baada ya kupewa maelezo hayo yeye aliendelea kulala, lakini baadaye alishangaa kupata taarifa za mkewe kukutwa akiwa amejinyonga hadi kufa baada ya kujining`iniza katika mti uliopo jirani na nyumbani kwa wazazi wake.

Alisema baada ya kupatiwa taarifa hizo aliamka na kwenda eneo la tukio na kumtambua marehemu na baadaye walitoa taarifa kwa viongozi wa serikali kwa ajili ya taratibu za kuuondoa mwili huo katika eneo hilo.

Aidha, akisimulia maisha ya mkewe, alisema kabla ya tukio hilo alikuwa akisumbulia na maradhi mbalimbali mara kwa mara jambo ambalo lilikuwa likimnyima amani wakati wote.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, ASCP Gemin Mushy, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo na kusema polisi inaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha kifo hicho.

Kamanda Mushy, alisema katika tukio hilo mwanamke huyo alijinyonga kwa kutumia mtandio alio jifunga shingoni na upande mwingine kuufunga juu ya mti wa mkorosho.

Aidha, kamanda Mushy aliwataka wananchi ambao wana taarifa za chanzo cha tukio hilo, kujitokeza ili kulisaidia jeshi hilo kukamilisha uchunguzi wake mapema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images