Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

Kutana Na Dr Chikago Bingwa Na Mwokozi Kwa Waliosumbuka Na Magonjwa Bila Mafanikio

$
0
0
Ninauwezo wa kumrudisha mume, mke ,mchumba, hawara, mtu unaempenda ndani ya masaa mawili tu (2) na kumfunga asiwe na mtu mwingine zaidi yako na kumfanya akutimizie kilakitu unachokihitaji kutoka kwake hata km yupo mbali na atatulia kabisa

GALIMBO 3 MIX;  nidawa ya mitishamba iliyitengenezwa kwa kwa utabibu wa hali ya juu kwakuchanganya miti na matundatiba , Huogeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15 -85 ) , inakomaza zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakat wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaid ya Mara tatu bila ham kuisha wara kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-40.

YOLANI :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inch (6-8) na unene wa sm (3-4)

Matatizo haya husababishwa na mambo mbalimbali km upigaji wa punyeto, kisukali,  vidonda vya tumbo, tumbo kuunguluma na kujaa gesi, ngili, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani, maumivu ya mgongo ama kiuno, namengineyo mengi  (nk )

SUPER MBUKE :- nidawa inayotatua tatizo la kisukali na kupona kabisa Kwa mda mfupi sana na utakuwa na uwezo wakula chakula chochote chenye sukali baada ya kupona,

vilevile ninadawa ya uzazi kwa akina Mama na akina Baba, kurudisha mali iliyopotea kwamda mfupi sana, vidonda vya tumbo, kaswende,presha,chango la uzazi, gono,nyama uzembe, kusafisha nyota, kuzuia majini wachafu, kinga ya mwili, kuuza vitu bila kununuliwa, dawa za biashara, pesa nyingi (utajili)  mambo ya kes nk

Kwa huduma n msaada wasiliana na Dr CHIKAGO atakusaidia hatakama ulikata tamaa utarudisha furaha yako

Napatikana Dar es salaam  sm no 0743543944   /0620510598

Nb :km huna nafasi ya kufika ofisin huduma hii itakufikia popote ulipo kwawatu wa mkoani tunatuma kwanjia ya mabasi.

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 176 na 177 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA  

Wanajeshi wawili wakasimama nyuma ya mzee huyu huku wakiwa wamemshikilia mtu aliye valishwa kigunia cheusi kichwani mwake. Wanajeshi hawa wakamvua mtu huyo, moyo ukanistuka, mapigo ya moyo yakaanza kwenda kasi huku jasho jingi likinimwagika usoni mwangu, kwani mtu waliye mkamata ni Yemi msicha ambaye hadi leo ninaishi na upendo wake moyoni mwangu na pete yake ya ndo bado ipo kidoleni mwangu, mzee huyu akasogea pembeni taratibu na hapo ndipo nikaona tumbo la Yemi ambalo limevimba kidogo, ikiashiria kwamba ni mwanamke mjamzito.
“Huyu ni mke wako wa ndoa, ni mjamzito sasa. Chagua kati ya mke na mtoto au kujisalimisha mbele ya jeshi la Kimarekani”
Sikujibu kitu chochote zaidi ya kutetemeka mwili mzima, maumivu ya moyo ninayo yasikia kusema kweli hayana mfano, kwani nilimuacha Yemi aende akaishia maisha yake salama salimin kwani ninatambua maisha yangu ni maisha ya hatari sana kwa kila ninaye ingia naye kwenye mahusiano ya kimapenzi.
   
ENDELEA
Nikajiikuta nikiifunika lapto hii taratibu huku nikimtazama Livna usoni mwake.
“Wanahitaji nini?”   
“Wamemkamata Yemi”
“Mmmmmm, Ester wamepata vipi mawasiliano nasi?”
“Waliniomba kupitia mtandoa nilio  post video zile”
“Wamefahamu ni wapi tulipo?”
 
“Hapana, hawajaweza kufahamu”
“Muda mwengine usiwakubalie pasipo kunifahamisha mimi kwanza”
“Sawa mkuu”
“Dany twende”
Livna alizungumza huku tukirudi kwenye chumba tulipo waancha Erick na wezake. Kila aliye nitazama nina imana anahisi kwamba kuna kitu ambacho kimetokea.
“Mkuu vipi?”   
Martin aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.
“Kuna tatizo limetokea”
Livna alizungumza huku akiwatazama kwenye nyuso zao.
“Tatizo gani?”
Winy naye aliuliza huku akiwa amejawa na shauku ya kuhitaji kufahamu ni kitu gani ambacho kimetokea.
“Yemi amekamatwa na Wamarekani, wanamlazimisha Dany kujisalimisha mikononi mwao la sivyo wanamuua Yemi na mbaya zaidi ni kwamba Yemi ni mjamzito”
“Oooohooo Mungu wangu!!”
Babyanka alizungumza huku akinitazama kwa macho yaliyo jaa masikitiko mengi.
 
“Hii ni vita, siwezi kujisalimisha mikononi mwao. Sihitaji kuonyesha udhaifu kisa mke na mtoto. Nilisha itoa sadaka famili yangu, mke wangu pamoja na mwanangu. Ninahitaji kuionyesha Marekani kwamba nina weza kufanya kitu”
“Sasa mkuu utaifanya nini Marekani ikiwa hatuna uwezo  wa kwenda kupambana nao, isitoshe wana vifaa vingi vya kivita, wana majeshi makubwa sana. Tuna fanyaje hapo?”
“Uwezo wa kumpiga Mmarekani tunao, tutampiga kwa silaha zao wao wenyewe”
Livna alizungumza kwa msisitizo huku  akinitazama usoni mwangu.
“Sasa mutaipiga Marekani na Yemi akiwa ndani yake?”
“Hatuna jinsi Babyanka, wanatulazimisha kufanya hivyo”
“Ila kuna kitu pia ninakifikiria?”
“Kitu gani Livna?”
 
“Nina mifumo mizima ya kuendeshea mabomu ya nyuklina yaliyopo Korea Kusini, munaonaje tukatumia mabomu hayo tukaipiga Marekani, na sisi tukajiweka pembeni pale watakapo anza kufumuana kwa maana Korea Kusini na Marekani ni sawa na panya na paka”
Sote tukamtazama Livna huku tukiwa tunashangaaa, hadi yeye mwneyewe akajistukia.
“Maana yangu sio mbaya kuzungumza hivyo, ila ninacho kisema hapa ni kuangalia ni jinsi gani sisi tunaweza kumuokoa Yemi pamoja na kiumbe elicho kuwa nacho tumboni na nina imani kwamba Yemi hayupo Marekani,  yupo Afrika hii hii”
Livna alizidi kunyoosha maelezo yake.
“Sasa Wakorea Kusini hawato tugeukia sisi?”
“Hapana, kila kitu tunacheza na code za kijeshi zinazo weza kuruhusu mabomu hayo kweza kushambulia Marekani na nina imani kwamba hakuna siku hata moja Mmarekani akakaa meza moja na Mkorea Kusini”
“Basi kama ni hivyo inabidi tufanye hili na tutazame ni nini kitakacho tokea”
“Jamani sio kama nina pinga hayo maamuzi, ila inabidi kujua ni wapi alipo Yemi, tumuokoe yeye na mtoto wake aliyopo tumboni?”
 
“Sawa Babyanka hilo halina shida vijana wangu watalishuhulikia kikamilifu”
“Hapo sawa, kwa maana mwenzenu nina roho ndogo sana kuona mwanamke mwenzangu tena mjamzito anaingia kwenye matatizo”
“K2 je?”
“Winy K2 huyo kwa sasa anapambana na aibu aliyo ipata, hadi akikaa sawa sisi tutakuwa tumesha maliza hili swala”
“Poa”
“Ila nina wazo”
Martin alizungumza na kutufanya sote tumtazame.
“Munaonaje Dany ukazungumza tena na Wamarekani ili kuwatishia kumuachia Yemi kabla ya wewe hujachukua maamuzi mazito kwa maana hili tunalo kwenda kulifanya ni vita ya tatu ya Dunia”
“Kweli hata mimi naunga mkono hilo swala. Dany hembu hili swala tuliweke mezani jamani na tulifikirie kwa umakini. Kuna wamama, kuna watoto wadogo, hawa wote ni mabilioni wa watu katika hizi nchi mbili. Je watakwenda kufa kwa ajili ya Yemi?”
 
Babyanka naye alizungumza huku akitutazama usoni mimi na Livna ambao tayari tumesha amua kufanya maamuzi magumu.
“Hilo nalo neno”
Winy naye akatilia ujazo wa maoni, jambo lililo tufanya mimi na Livna kutazamana.
“Basi hilo tuliweke ni Plan B, haya sasa tufikirieni Plan A, tutamuokoa vipi Yemi, na sasa hivi Wamarekani wana hasira kuliko kitu chochote wakimshika mmoja wetu hapa ninaimani kwamba hato pona”
Livna alizungumza na kufanya ukimya wa zaidi ya dakika mbili kutawala katika eneo hili.
“Na isitoshe Dany hawezi kujisalimisha mikononi mwao”
“Tukijua ni wapi alipo Yemi alipo mimi nitakwenda kumuokoa”
Martin alizungumza.
 
“Acha kutafuta kifo kisicho na sababu Martin”
“Hata nikifa sababu ipo, nitakuwa nimekufa nikijaribu kumuokoa mke wa mkuu wangu isitoshe hata kwenye harusi niliwasimamia mimi”
“Hakuna kitu kujaribu hapa ni kufanya”
“Martin unakumbuka namba yoyote ya meja?”
“Meja ndio nani?”
Livna aliuliza huku akinitazama usoni mwangu.
“Alikuwa ni mkuu wa kambi ya jeshi nchini Somalia, ni rafiki yangu na yeye ndio aliye andaa harusi yangu na Yemi”
“Una muamini, kwa maana hawa watu hawaaminiki kabisa”
“Alinisaidia katika mengi hata kuniokoa mikononi mwa Wamarekani walivyo nikamata kwa mara yangu ya kwanza”
“Ndio ninakumbuka namba yake ya mkononi alisha wahi kunipatia”
“Livna unaweza kuniazima simu ambayo nilimpigia nayo K2?”
“Ndio”
“Ninaomba unisaidie”
Livna akatoa simu yake mfukoni na kunikabidhi. Martin akaanza kunitajia namba moja baada ya nyingine. Nikaipiga namba hii huku nikiiweka simu hii sikioni mwangu, taratibu ikaanza kuita, baada ya sekunde kadhaa kikapokelewa.
 
“Haloo”
Niliisikia sauti ya Meja, nikameza fumba la mate huku nikishusha pumzi taratibu.
“Habari yako meja”
“Dany”
“Ndio meja”
“Habari za masiku”
“Salama”
“Aissee Dany nimejaribu kukutafuta siku zote sijakupata. Ninaiona kazi yako jinsi ilivyo kwenda vizuri”
“Nimejitahidi kwa kiasi chake meja”
“Sio kwa kiasi chake, umfanya kazi nzuri sana Dany, sikutegaema kama unaweza kuwa na roho ya ujasiri kiasi hicho”
“Shukrani sana meja, ila ninatatizo”
“Tatizo gani?”
“Yemi amekamatwa na Wamarekani”
“Ila Yemi si ulisha achana naye, yeye wa nini tena?”
“Ana ujauzito wangu na pia ni mke wangu wa ndoa. Bado nina mpenda na pete yake ninayo”
 
Ukimya wa sekunde ukatawala
“Sasa Dany unahitaji hapo nikusaidiaje rafiki yangu”
Meja alizungumza kwa sauti ya chini sana.
“Ninakuomba unisaidie kumpata mke wangu. Wamarekani wakimuua, basi hali ya dunia itakwenda kubadilika meja. Wewe ndio mtu wa pekee unaye weza kuzuia hali ya dunia kutochafuka, kama ilivyo anza kuchafuka kwa Wamarekani”
“Sawa nitaomba unipigie baada ya lisaa moja tutafute ni wapi alipo”
“Ninashukuru sana Meja”
“Ila upo wapi?”
“Usijali meja nitakuambia ni wapi nilipo baada ya hiyo kazi kuisha”
“Sawa”
Nikakata simu na kumrudishia Livna simu yake.
“Tuna lisaa moja la kusubira kuweza kupata jibu ni wapi Yemi alipo”
“Kwa hiyo nisiwaambie wasichana wangu kuto kufanya chochote?”
“Wakae tayari”
“Sawa”
“Samahani. Dany wakae tayari katika nini?”
“Katika vita, kama walimuweza Osama mwaka 2002, hawato niweza mimi”
 
Baada ya kumaliaza kuzungumza maneno haya nikasimama na kuanza kueleka mlangoni, Livna akaanza kunifwata kwa nyuma huku akiwa ameongozana na Martin.
“Dany huyu mtu unamuamini sana kwa maana kumbuka kwamba Wamarekani wana uzalendo mkubwa na nchi yao na isitoshe amelitumiakia jeshi lake kwa muda mrefu?”
“Akienenda kinyume nami ninamuua”
“Ila kweli mkuu alicho kizungumza Livna”
“Nimesema meja akinisaliti, nitamuua. Kuna swali?”
Nilizungumza kwa msisitizo huku nikiwa nimejawa na hasira ambayo haiitaji kusikia maswali ya mtu yoyote. Martin akatingisha kichwa akionyesha kwamba hana swali jengine, nikarudi chumbani kwangu huku nikiwa nimeongozana na Livna na Martin alirudi katika chumba tulichokuwepo mara baada ya kuona sipo sawa. Livna akaufunga mlango kwa ndani na kunisukumia kitandani, kisha akanikalia kiunoni mwangu huku akinitazama.
 
“Hivi umemua kunisaidia kutoka moyoni mwako?”
“Ndio Dany, ninakuomba uniamini sana, nimefanya hili swala kutoka moyoni mwangu sinto weza kukusaliti hadi kufa kwangu”
Baada ya Livna kuzungumza maneno haya akaanza kuninyonya midomo yangu taratibu, nikakishika kiuno chake na kuanza kukiminya minya.
Hisia za mapenzi zikaanza kutupanda huku kila mmoja akiwa na hamu ya kupata burudani hii, japo tupo katikati ya matatizo makubwa. Tukavuana nguo zetu, pasipo hata kuandaana sana

Baada ya kumaliza Livna alishuka kitandani, akaanza kutembea kueleka bafuni huku akipepesuka sana. Nikashuka kitandani na kumfwata kwa nyuma, nikamsaidia kumshika mkono na kuingia naye bafuni, tukaoga kwa pamoja na kutoka humu, kila mtu akavaa nguo zake yeye mwenyewe kama desturi ya waafrika tukimaliza kufanya tendo la ndoa kila mmoja anavaa nguo zake japo mwanzo tunajifanya kuvuana nguo.
“Lisaa moja litakuwa tayari ehee?”
“Yaa inabidi nimpigie”
“Chukua simu”
Livna akanipigia simu, nikampigia meja, simu ikaita baada ya muda ikapokelwa.
 
“Dany”
“Ndio”
“Sijafanikiwa kufahamu ni wapi Yemi alipo, kwani unahitaji kufanya nini?”
Nikajikuta nikisimama huku nikimtazama Livna usoni mwake.
“Halooo”
“Meja  niambie ukweli hujampata kabisa Yemi?”
“Niambie kwanza ni nini unataa kukifanya kwa Wamarekani nami nitakuwa tayari kukusaidia kumpata mke wako”
Upande mmoja wa roho yangu inaniambia nisimuambie meja mpango ninao kwenda kuufanya juu ya nchi yake pendwa aliyo itumikia kwa miaka mingi katika kitengo cha jeshi. Ila upande wa pili wa roho yangu unanishawishi kumueleza mpango mzima ili mradi anisaidie kumpata mke wangu wa ndoa mwenye ujauzito unao sadikika kwamba ni wangu.

AISIIIII……….U KILL ME 177

“Meja ukimpata Yemi nitakuambia ni nini ambacho nimekipanga, ila kwa sasa sinto weza kukuambia hilo. Samahani sana”
Baada ya kumaliza kuzungumza hivi nikakata simu na kumtazama Livna.
“Anahitaji nimueleze ni nini nitakacho kwenda kukifanya kwa Mmarekani”
“Ni vizuri ulivyo kataa kumuambia, ila ngoja wasichana wangu wanaweza kufanya kazi ya kumtafuta Yemi. Twende kwenye chumba cha mawasiliano”
Tukaongozana na Livna hadi kwenye chumba hichi cha mawasiliano, akamuita Ester pamoja na wasichana wengine wawili.
 
“Umeweza kumpata Yemi alipo?”
“Bado mkuu”
“Na haukujua  video ile waliyo hitaji kuzungumza na Dany ilitokea wapi?”
“Yaa nao waliweza kufunga mitambo yao na hatujajua ni wapi walipo”
“Wapigieni tena nizungumze nao”
“Dany”
“Naomba wafanye hivyo”
Livna akanitazama kwa muda usoni mwangu.
“Sawa”
Livna alizungumza, akamkabidhi Ester kazi kuwasiliana na mkuu wa jeshi la Marekani.
“Njoo kwenye chumba hichi”
Tukaingia kwenye chumba hichi ambacho kuna Tv kubwa tatu. Livna akawasha Tv moja ya katikati. Baada ya muda kidogo ikamuonyesha mkuu wa jeshi niliye zungumza naye masaa machache nyuma.
 
“Una masaa machache ambayo unaweza kujisalimisha mikononi mwa vikosi vya Marekani”
“Mzee sijakuja kukuomba wala sijakuja kukubembeleza. Ninakuamrisha ndani ya dakika kumi na tano muachie mke wangu. La sivyo  wananchi wa nchi yako watakwenda kulia kilio cha kusaga meno kwa kile ambacho kinakwenda kutokea”
Tv hii ikagawanyika katika picha mbili huku moja ikimuonyesha mkuu huyu wa jeshi na nyingine ikiwaonyesha viongozi walio kaa kwenye meza moja kubwa.
“Dany unazungumza na makamo wa raisi wa Marekani. Thomas Sound”
Nikaka kimya huku nikimtazama kiongozi huyu, ambaye sio mara yangu ya kwanza kumuona.
 
“Tunahitaji kuingia makubaliano nawe je upo tayari”
Nikamtazama Livna aliye simama pembeni na yeye haonekani kwenye hii Tv. Livna akatingisha kichwa kukubaliana na anacho kizungumza makamu huyu wa raisi aliye ichukua nafasi ya raisi Donald Bush niliye idhibitishia dunia kwamba mimi ndio niliye muua.
“Zungumza”
“Tunahitaji kumuachia mke wako, endapo pale utakapo jisalimisha mikononi mwa serikali yangu ya Marekani”
“Akili zenu ni moja, munazungumza kitu kimoja. Sasa nimewaambia ndani ya dakika kumi na tano ninahitaji mumuachie mke wangu. Zikipita kunzia hivi sasa. Mamilioni ya Wamarekani itakwenda kuwalaumu kwa maamuizi ya kijinga unayo yafanya na hao watu wako walio kuzunguka.”
“Mpumbavu wewe ni nani anaye kupa ruhusa ya kumuita raisi wetu mpumbavu”
Mzee mmoja alizungumza kwa sauti ya kukwaruza sana, huku hasira ikiwa inaonyesha dhairi kwamba imempanda.
“Munadakika kumi na tano”
Nikanyanyuka kwenye kiti nilicho kikalia, na Livna akazima tv hii.
“Dakika hizo kumi na tano una mpango wa kufanya nini?”
“Ninahitaji kutumia mpango ambao ulihitaji sisi kuweza kuufunya”
“Kutumia silaha za Korea Kusini kumshambulia Mmarekani?”
“Ndio”
“Ngoja kwanza, tulipua visima vyake kumi vya nyuklia, nina imani kwamba itakuwa ni fundisho kubwa kwao”
 
“Sawa waite vijana wako wanao weza kuifanya hiyo kazi”
Livna akatoka katika chumba hichi, hazikupita hata dakika mbili akarudi akiwa amongozana na wasichana watatu akiwemo na Ester, akawalezea ni nini wanatakiwa kufanya. Kazi ikaanza mara mmoja, ndani ya dakika kumi, wakawa wamefanikiwa kufahamu namba za siri ambazo zinaweza kutumika katika kulipua visima vya kuzalshia mabomu ya nyuklia ambayo duniani yanasifika kwa uhatari wa hali ya juu.
“Ukihitaji kulipua unaminya batani hii”
Ester alizungumza huku akinikabidhi laptop aliyokuwa anafanyia kazi.
“Nikiminya vinalipuka kwa muda mmoja?”
“Ndio kwa pamoja vinalipuka”
“Shukrani binti, wapigieni tena”
“Ila dakika kumi na tano bado hazijafika”
“Zimebaki ngapi?”
“Dakika tatu”
Livna alizungumza huku akitazama saa iliyopo ukutani mwake.
“Hizi tv si zinaweza kuonyesha chaneli kama BBC, CNN?”
“Ndio”
“Ziwasheni”
Livna akawasha tv hizi mbili na kuweka sauti ya chini sana ambayo haitoweza kuingiliana kabisa na mazungumzo ambayo ninakwenda kuyafanya na viongozi wa Marekani. Zilipo timia dakika kumi na tano Tv hii ninayo itumia kufanya mawasiliano Wamarekani ikawashwa na kuwakuta wakiwa kwenye kikao chao.
 
“Dakika kumi na tano nina imani zimesha fika, je munamuachia Yemi au hamumuachii?”
Makamu wa raisi pamoja na mkuu wa jeshi wakaka kimya kwani wao ndio wahusika wakubwa ninao zungumza nao.
“Munamuachia Yemi au hamumuachiii?”
“Hivi huyu nguruwe anajimini nini hadi kututisha kiasi hichi”
“Waziri wa ulinzi nyamaza”
Makamu wa raisi alizungumza kwa ukali huku akimtazama mzee huyo. Taratibu mkono wangu nikausogeza kwenye batani hii  ya kulipulia visima hivi vya nyuklia.
“Dany”
Makamo wa raisi alizungumza na kunifanya nisitishe zoezi la kuminya batani hii.
“Tutamuachia Yemi ila kwa makubaliano ya kubadilishana”
“Kubadilishana na nani?”
“Tunamuhitaji mke wa raisi, bi Hawa”
“Hawa alikuwa ni mpenzi wangu, raisi wenu alinipokonya na kuhitaji kuniua. Nina imani nyinyi nyote muliweza kujua ni mchango gani niliutoa kwa ajili ya kuliondoa kundi la Al-Shaba. Ila serikali yenu ikanigeuka na kuhitaji kunia, kisa raisi wenu amemchukua mpenzi wangu. Sasa makubaliano hayo musahau, Sawa”
Viongozi wote wakaka kimya huku wote wakinitazama usoni mwangu.
 
“Ninawauliza kwa dakika ya mwisho je mutamuachia Yemi na kuwapa maelekezo ni wapi apelekwe au?”
“Nchi yangu haiingii makubaliano na gaidi, ninakuhakikishia kwamba tutakutafuta, iwe ni angani au nchi kavu nilazima serikali yangu ikutafute na kukuua”
“Sawa tuanze kutafutana sasa”
Nikaminya batani ambayo nimeelekezwa na Ester. Nikawatazama viongozi  hawa wa Wamarekani huku nikitabasamu. Nikamuona msichana mmoja akimsogezea makamu wa raisi, akaonekana kustuka sana, kwa ishara akamuomba kijana mmoja kuwasha Tv kubwa iliyopo nyuma ya kiti chake. Nikataupia macho yangu kwenye Tv ya pembeni. Vituo vya habari vikaanza kuonyesha taarifa ya dharura inayo husiana na milipuko ya visima ya nyuklia.
“Huo ndio mwanzo, mukishindwa kumuachia, kitakacho fwata ni mara kumi ya hicho mulicho  kiona hapo”
Nikanyanyuka kwneye hiti hichi huku nikiwaachia mtihani mkubwa viongozi hawa wa kimarekani. Tv zikazima na tikatoka katika chumba hichi.
 
“Ester hakikisheni ulinzi unaimarishwa, kwa maana tumesha ingia kwenye vita”
“Sawa mkuu”
Tukaondoka katika eneo hili. Sikuzungumza kitu chochote zaidi tulipo ingia kwenye chumba ambacho wasichana wadogo wenye umari wa miaka mitano kwenda juu wanafundishwa jinsi ya kupambana.
“Hawa watoto wazuri”
Watoto hawa wakasimama kwenye mistari minne iliyo nyooka, wakatoa heshima yao kwa kuinamisha vichwa vyao chini. Livna akaipokea heshima hiyo kwa kuinamisha kichwa chake na yeye chini, kisha akawaruhusu waendelee na mazoezi yao.
“Yaa sasa hawa wakifikia miaka kumi na tano tunaaza kuwakabidhi kazi nchini mbali mbali”
“Kwa hiyo maisha yao yote wanaishi kujifunza kupambana?”
“Yaaa wanaishi kwa kupambana”
Simu ya Livna ikaita, akaitoa mfukoni akaitazama kisha akanikabidhi na kukuta namba ya meja ndio inayo piga. Taratibu nikaipokea na kuiweka sikioni.
“Dany wewe ndio umehusika katika kulipua visima vya nyuklia?”
 
Meja aliniuliza huku akiwa na wasiwasi mwingi sana.
“Kwa nini unaniuliza hivyo?”
“Kama ni wewe Dany kwa nini unahusisha matatizo kwa raia ambao hawana hatia yoyote. Kumbuka nina dhamira yangu ya kwenda kuiongoza Marekani, ninahitaji kuwa raisi wa hiyo nchi. Ni kwa nini umefanya hiyvo?”
“Meja unazungumza na kunishutumu mimi bure, kwa nini?”
“Dany nimepata taarifa kutika Washinton D.C na wewe ndio umehusika katika ulipuaji wa visima vya nyuklia, kama upo karibu na Tv hembu tazama ni jinsi gani raia walivyo fariki”
“Kosa sio langu, kosa ni la viongozi wa nchi yako. Ni hivi waambie kwamba wamuachie Yemi la sivyo kabla ya giza halijatawala anga, nitakwenda kuigeuza Marekani magodauni kama walivyo fanya kwa nchi za Iraque na Pakistani”
Nikakata simu na kumrudishia Livna. Baadhi ya watoto wakabaki wakiwa wananitazama kwa macho ya kunishangaa hadi nikajisikia aibu kwa kuzungumza vitu vizito mbele yao.
Nikatoka chumbani humu huku Livna naye akinifwata kwa nyuma. Tukarudi katika chumba cha mawasiliano na kuingia kwenye chumba chenye Tv. Nikawasha tv hizi na kuangalia taarifa za habari. Nikaona uharibifu mkubwa wa majengo, ulio fwanya na visima hivi vya nyuklia ambavyo nimevilipua.
“Mmmmm”    
 
Livna aliguna huku akitazama taarifa hizi.
“Nini?”
“Tuwapigie tena na kuwapa onyo, wamuachie Yemi”
“Acha kwanza walie lie, hembu mpigie K2”
“K2 utamuua kwa presha bwana”
“Lengo letu ni wafe. Wakati wao umeisha sasa niwakati wangu kuwaendesha umefika”
“So unahitaji kuhack kamera zao”
“Hapana ninahitaji kuzungumza naye kwa video call kama tulivyo fanya kwa Wamarekani”
“Sawa”
Livna akatoka chumbani humu. Nikabaki nikitazama taarifa hizi za habari, nikaona jinsi watu wengi walivyo fariki kwa milipuko wa visima hivi vya nyuklia.
‘Mungu ninakuomba unisamehee kwa maana hawakujua walitendalo’
 
Nilizungumza kimoyo moyo, mlango ukafunguliwa na akaingia Livna na wasichana wake wa mara ya kwanza huku kila mmoja akiwa na laptop yake mkononi mwake.
“Tumesha mpigia K2 anakusubiria uwashe Tv hiyo ya kati.”
Nikachukua rimoti  iliyopo pembeni yangu na kuisha tv hii. Nikamuona K2 akiwa amekaa kweye kiti cha ofisini kwake huku nyuma yake kukiwa na nembo ya taifa, ya mwanaume na mwanamke na imetawaliwa na rangi ya kijani.
“Nina imani umeona kilicho wapata Wamarekani, je upo tayari na wewe nikupige?”
K2 akaka kimya huku akinitazama, nikaitazama midomo yake jinsi inavyo cheza cheza kwa hasira kali.
“Usiteteshe midomo yako K2, je unahitaji na wewe nikubamize?”
“Huyo malaya ndio amekupa nguvu ya kuwa jeuri mbele yangu si ndio?”
Hata kabla sijazungumza chochote Livna akasimama nyuma yangu.
“Malaya mimi au wewe?”
“Wewe ndio malaya, umenisaliti kwa ajili ya huyo msen**”
“Hahahaaa, hivi unajua hichi kikundi ni wapi kilipo tokea au una ropoka?”
 
“Mbwa wewe, ninajipanga nikija ninakutumbua tumbua na hao panya wako”
“Nyooo jaribu uone, wewe mwenyewe unanijua mimi ni nani. Tena usinifanye nikabadilisha mawazo yangu nikakufwata wewe. Bado nina hasira ya vijana wangu wawili ulio watoa sadaka. Yaani laiti ingekuwa si kuijua vizuri Tannia, ningekubamiza kenge wewe”
Livna na K2 wakarushiana maneno ya kike, nikamzuia Livna, akaondoka nyuma yangu huku akiwa amenuna kwa hasira kali.
“K2 unatambua fika kwamba sina woga juu yako kwa maana ninakujua kinaga ubaga. Nina damu ya raisi mmoja mikononi mwangu, sasa hivi sihitaji kukuua ukiwa ni raisi, achia madaraka basi.”
“Siwezi kuachia madaraka kwamwe, si wewe wala si viongozi wa kisiasa wanao nilazimisha mimi kuachia madaraka. Nitahakikisha kwamba ninakuua”
“Na wewe unanitisha, K2 achia madaraka na mkabidhi waziri wako mkuu madaraka ambaye hukuona thamani yake ukahitaji nimuue.”
 
“Kenge wewe tena ngoja”
K2 kwa ishara akamuita mlinzi wake mmoja, akamnong’oneza, kisha mlinzi huyu akaondoka. Tukaka kimya huku tukitazamana na K2,  huku nikisubiria kuona ni nini atafanya. Baada ya muda akaingizwa Lucy aliye chakaa kwa mateso makali. K2 akamshika kichwa Lucy na kukilaza kwa lazima kwenye meza. Akamnyooshea mkono mlinzi wake, akachomoa bastola na kukabidhi, K2 akaiweka bastola hii kwenye sikio la Lucy huku akinitazama kwa macho makali.
“Ninamuua huyu malaya wako uliye mtoa bikra na kukukaribisha nchini kwangu, sasa utajua kwamba nina uwezo wa kukufanya wewe chochote.”
Baada ya K2 kuzungumza maneno hayo, pasipo na huruma akafyatua risasi iliyo ingia sikioni mwa Lucy na kusababisha damu nyingi kusambaa kwenye meza yake jambo lililo nifanya nifumbe macho yangu kwa hasira kali na kujikuta nikijilaumu  ni kwa nini nimemuacha K2 hai kipindi nilipo pata nafasi ya kumuua.
 
ITAENDELEA
‘Haya sasa K2 amemua Lucy mbele ya Dany ambaye kwa sasa anaogopwa Duniani kote hii ni kutokana na watu walio simama nyuma yake wakihakikisha wanamsaidia. Je Dany atamfanya nini K2? Usikose sehemu inayo fwata ya hadi hii ya kusisimua kutoka kwa muandishi mahiri Eddazaria G.Msulwa”

LIVE: Rais Magufuli Akizundua Ujenzi wa Daraja la Salender Dar

$
0
0
LIVE: Rais Magufuli Akizundua Ujenzi wa Daraja la Salender Dar

Kiumbe wa ajabu apewa jina la Rais wa Marekani Donald Trump

$
0
0
Kiumbe anayeweza kuishi baharini na katika nchi kavu amepewa jina la Rais wa Marekani Donald Trump, ingawa huenda kiongozi huyo asitake kuhusishwa na kiumbe huyo kutokana na sifa zake.

Amfibia huyo huwa anafukia na kuficha kichwa chake mchangani anapokabiliwa na hatari, jambo ambalo pengine limewashawishi wahusika kumpa kiumbe huyo jina la Trump kutokana na kiongozi huyo kukana kwamba shughuli za viwanda na za kibinadamu zinachangia mabadiliko ya tabia nchi. Kiumbe huyo pia ni kipofu, hawezi kuona.

Kwa mujibu wa Shirika la habari la BBC,The Guardian , The Nation na vyombo mbalimbali vya habari, Mnyama huyo ambaye amepewa jina Dermophis donaldtrumpi, aligunduliwa katika eneo la Panama, na alipewa jina hilo na mkuu wa kampuni ya EnviroBuild ambaye alikuwa amelipa $25,000 (£19,800) kwenye mnada kupata fursa ya kumpa jina kiumbe huyo.

Kampuni hiyo imesema inataka kuhamasisha watu kuhusu mabadiliko ya tabia nchi.

“[Dermophis donaldtrumpi] huathiriwa sana na mabadiliko ya tabia nchi na kwa hivyo ni kiumbe aliye katika hatari ya moja kwa moja ya kuangamia kutokana na sera ya somo wake kuhusu mazingira,” mwanzilishi mwenza wa EnviroBuild, Aidan Bell, amesema kupitia taarifa.
EnviroBuild, kampuni iliyopata haki yakumpa kiumbe huyo jina, iliongeza nywele bandia kwenye kiumbe huyo jambo lililomfanya kuwa na muonekano unaokaribiana na wa Trump

Kiumbe huyo mdogo ni wa aina ya caecilian, ambao ni viumbe watelezi wanaofanana na minyoo au nyoka, na huishi sana chini ya ardhi.

Bw Bell amesema tabia za kiumbe huyo zinashabihiana sana na za Trump.

“Kupuuza mambo (sawa na kuficha kichwa mchangani) humsaidia Donald Trump kukwepa maafikiano kuhusu madhara ya mabadiliko ya tabia nchi,” amesema.
Pesa zilizopatikana kutokana na kupiga mnada nafasi ya kumpa kiumbe huyo jina zitakabidhiwa shirika la Rainforest Trust

Wanasayansi duniani wanakubaliana kwamba mabadiliko ya tabia nchi yanasababishwa na shughuli za kibinadamu.

Lakini Bw Trump, ambaye utawala wake umekuwa ukiendeleza matumizi ya mafuta yanayotokana na kaboni, amewatuhumu wanasayansi hao kwa kuwa na “ajenda ya kisiasa” na kutilia shaka kwamba binadamu wanahusika katika ongezeko la joto duniani.

Marekani kuondoa wanajeshi wake Syria

$
0
0
Rais wa Marekani Donald Trump amesema Jumatano kwamba wanajeshi wa Marekani wataanza kuondoshwa nchini Syria na kurejeshwa nyumbani, kwavile wameshafanikiwa kulitokomeza kundi linalojiita Dola la Kiislam (IS).

Rais wa Marekani Donald Trump amesema Jumatno kwamba wanajeshi wa Marekani wataanza kuondoshwa nchini Syria, kwavile wamefanikiwa kutimiza lengo lao la kulitokomeza kundi linalojiita Dola la Kiislam (IS) na sasa hawahitajiki tena nchini humo.

"Tumekuwa tukipambana kwa muda mrefu sana nchini Syria. Nimekuwa rais kwa zaidi ya miaka miwili. Tumejitahidi sana na tumelishinda kundi la IS. Tumewashinda na tumewashinda vibaya sana. Tumewapokonya ardhi waliokuwa wanidhibiti. Na sasa ni wakati wa wanajeshi wetu kurudi nyumbani," amesema Donald Trump wakati akitangaza uamuzi wake huo.

Uamuzi huo wa kuondoa kabisa wanajeshi wa Kimarekani nchini Syria, umethibitishwa pia na maafisa wa Marekani na unatarajiwa kutekelezwa katika miezi ijayo. Lakini kuondoka kwao huko kunaweza kukafanya vigumu kupambana na kundi hilo iwapo litapata tena nguvu.

Na Marekani pia itapoteza ushawishi wake katika eneo hilo, na kuhujumu juhudi zake za kidiplomasia za kutaka kumaliza vita vya Syria vya wenyewe kwa wenyewe, ambavyo vimeingia mwaka wake wa nane.

Maseneta wakosoa uamuzi wa Trump
Uamuzi huo wa Trump umekosolewa na Maseneta pamoja na baadhi ya wanachama wenzake wa chama cha Republican, ambao wanadai kwamba kuondoka kutazipa nguvu Urusi na Iran, ambazo zinamuunga mkono Rais wa Syria Bashar Assad. Maseneta hao wa Marekani ikiwa ni pamoja na wa chama cha Republican Jumatano usiku walimsisitizia Rais Donald Trump kutafakari upya uamuzi wake huo wa kuondoa majeshi ya Marekani kutoka Syria.

Uamuzi huo pia unaweza kuliathiri kundi la muungano wa wanamgambo wa Kikurdi na Kiarabu unaojulikana kama SDF. Kundi hilo limekuwa mstari wa mbele katika kupambana na kundi la IS, lakini sasa linakabiliwa na kitisho kutoka Uturuki, kwa vile taifa hilo linatafakari kufanya mashambulizi nchini Syria.

Makamanda wa jeshi la Marekani waliopo Syria, ambao wamekuwa na uhusiano mzuri na viongozi wa kundi la SDF wameeleza wasiwasi wao juu ya uamuzi huo wa Trump na jinsi utakavyohatarisha vikosi vinavyoungwa mkono na Marekani.

Lakini Trump amesema kwake yeye operesheni ya Syria imemalizika, kwavile wanamgambo wa kundi la IS wameshapoteza maeneo waliokuwa wakiyadhibiti.

Maafisa wa Marekani wamesema wanajeshi wataanza kuondolewa Syria katika siku 60 hadi 100 zijazo na kwamba Wizara ya Mambo ya Nje itaanza kuondoa wafanyakazi wake kutoka Syria katika kipindi cha masaa 24.

RC Makonda Adai Mnyika na Saed Kubenea Wameomba Kuhamia CCM

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amesema amepokea maombi ya kujiunga Chama Cha Mapinduzi kutoka kutoka kwa wabunge wawili wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea na wa Ubungo, John Mnyika.

Paul Makonda ametoa kauli hiyo Jijini Dar es salaam, wakati akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa uwekaji la jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la kisasa la Selander na barabara unganishi jijini Dar es salaam.
 

 "Kilichotokea Temeke ni toba, Ukonga ni toba, kilichotokea Kinondoni ni toba na huku kwenye kata kuna toba nyingi sana zinafanyika, kwa ungwana walipoingia wamegundua hakuna ilani ya chama inayotekelezwa."Amesema Makonda na kuongeza;
 

 "Wengi wameniomba kujiunga CCM, wapo madiwani na wabunge wa Ubungo na Kibamba walikuwa wanasema kama deadline (tarehe ya mwisho) imeshatoka itakuaje? nikawaambia ngoja tuangalie kama kuna usajili wa dirishani Katibu Mkuu akiruhusu tuone itakuaje."

Awali akiwatambulisha Makonda amesema " mheshimiwa Rais nawatambua Meya wa Ilala, na Naibu Meya wa Ilala, pia tumesajili Naibu Meya yuko CCM, alitoka upande mwingine na nafikiri Meya anamtegemea Naibu Meya natumai ipo siku Meya ataweza kuona namna ya kutuunga mkono."

Rais Magufuli Ahoji Ufukwe wa Coco (Coco Beach) kutokuwa na Choo

$
0
0
Rais John Magufuli ameshangazwa na ufukwe wa Coco (Coco Beach) pembezoni mwa Bahari ya Hindi jijini Dar es Salaam kutokuwa na choo wakati eneo hilo zinakusanywa fedha kila siku.

Akizungumza leo Alhamisi Desemba 20, 2018 kabla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la  Selander jijini Dar es Salaam, Rais amedai magari yanayoegeshwa kando ya fukwe hiyo hulipiwa Sh2,000.

“Coco Beach panatia aibu. Ifike wakati tuzizungumzie aibu zetu pale hakuna hata choo, ndio nasikia wanajenga sasa,” amesema.

“Wanakusanya mapato kila siku hatujui hizo hela zinakwenda wapi na wanashindwa hata kujenga mabanda yaliyoboreshwa.”

Hata hivyo, amesema Jiji la Dar es Salaam limebadilika na kuwa na sifa ya kuwa jiji la kibiashara, kwamba anafurahi kuhamia Dodoma akiacha Dar es Salaam ikiwa katika hali hiyo.

Rais Magufuli Asema Tanzania Itaendelea kushirikiana na Wadau wa Maendeleo

$
0
0
Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli anasema kuwa Tanzania iko tayari kushirikiana na wadau wa maendeleo katika utekelezaji wa ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo  barabara na madaraja hatua inayolenga kuboresha maisha ya watanzania.

Akizungumza leo jijini Dar es salaam, Rais wa Jamhuri ya Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati akiweka jiwe la msingi katika ujenzi wa daraja jipya la Selander lenye urefu  wa kilomita 1.03 na barabara unganishi zenye urefu wa kilometa 5.2, upana wa mita 20 na njia nne za magari pamoja na njia ya waenda kwa miguu yenye upana wa mita 2.5, alisema kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na wadau  wa maendeleo katika kuwaletea watanzania maendeleo.

“Tanzania itaendelea kushirikiana na wadau wa maendeleo ili kuwaletea maendeleo watanzania sambamba na kuhakikisha malengo na matumaini ya watanzania ya kuleta maendeleo tunayafikia kikamilifu” alisema Rais Magufuli

Pia, Rais Magufuli aliwataka watanzania kufanyakazi kwa bidii ili kufikia kiwango cha maendeleo cha nchi ya Korea ya kusini ambayo, katika miaka ya 1960 kiwango cha maendeleo kilikuwa sawa kati ya nchi hizo mbili.

“Tulikuwa tunalingana kiuchumi na nchi ya Korea ya kusini ambayo ina idadi ya watu milioni 51 na Tanzania  milioni 55,huku Tanzania ikiwa na eneo kubwa zaidi ya nchi ya Korea ya Kusini, lakini wao walijifunga mkanda na mpaka sasa wameweza kujitegemea kiuchumi kwa kufanyakazi kwa bidii na kujiletea maendeleo makubwa” alisema Rais Magufuli

Aidha, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mhandisi Patrick Mfugale alisema kuwa daraja hilo  jipya la Selander litajengwa kwa fedha za mkopo nafuu kutoka nchi ya Korea kusini pamoja na fedha za ndani, ambapo litagharimu dola za kimarekani milioni 112.8 ambapo Korea ya kusini  itachangia dola za kimarekani milioni 91.03 na Tanzania itachangia dola za kimarekani milioni 21.822.

Vilevile, daraja hilo  litakuwa na urefu wa kilomita 1.03 na  barabara unganishi zenye urefu wa kilometa 5.2, upana wa mita 20 na njia nne za magari pamoja na njia ya waenda kwa miguu yenye upana wa mita 2.5, lengo likiwa ni kupunguza  msongamano wa magari katika barabara ya Ally Hassan Mwinyi.

Mhandisi Mfugale aliongeza kuwa daraja hilo litaweza kudumu kwa zaidi ya miaka 100 na linaweza kubeba uzito wa tani 180 kwa wakati mmoja.

Kwa upande wake, Mwakilishi Mkuu wa Benki ya Exim  nchini Tanzania, Hyon –Jong Lee alisema kuwa uhusiano wa Tanzania na Korea ya Kusini ulioanza miaka 26 iliyopita umezidi kuimarika, na kupitia Mfuko wa Shirika la Maendeleo la Korea kusini (ECDF), Korea imefadhili miradi ya Ujenzi wa chuo cha Mloganzila, daraja la Kikwete pamoja na Kituo cha kuchakata data cha Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Naye, Balozi wa Japan nchini Tanzania Cho Tae-ick alisema kuwa nchi ya Korea kusini inafurahishwa na jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali ya Tanzania katika kujiletea maendeleo

“Serikali ya Korea ya kusini inaangalia kwa makini fursa zilizopo Tanzania ikiwa ni nchi yenye uchumi unaokuwa kwa asilimia 7 na yenye sera kuelekea nchi ya viwanda, na hivyo Serikali Korea ya Kusini ina  nia ya dhati ya kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuleta maendeleo”

Rais Magufuli Ataka Daraja la Selander Libadilishwe Jina na Kuitwa Tanzanite

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 20 Desemba, 2018 ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja jipya la Selander linalounganisha eneo la Aga Khan na Coco Beach Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kupunguza msongamano wa magari katika barabara ya Ali Hassan Mwinyi.

Daraja hilo lenye urefu wa meta 1,030 na upana  wa meta 20.5 litakuwa na njia 4 za magari na njia 2 za watembea kwa miguu, na litajengwa pamoja na barabara unganishi zenye jumla ya kilometa 5.2.

Sherehe za uwekaji jiwe la msingi katika mradi huo zimefanyika katika eneo la Aga Khan na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Mke wa Rais Mhe. Mama Janeth Magufuli, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Spika wa Bunge Mhe. Job Yustino Ndugai, Mawaziri, Wabunge, Mabalozi wa nchi mbalimbali, viongozi wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi wa Dini, viongozi wa vyama vya siasa na viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Paul Makonda.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mhandisi Patrick Mfugale amesema ujenzi wa daraja hilo utakaochukua muda wa miezi 30 kuanzia tarehe 23 Julai, 2018 utagharimu shilingi Bilioni 256 zilizotolewa kwa mkopo nafuu kutoka Jamhuri ya Korea kupitia Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Kiuchumi (EDCF) na Serikali ya Tanzania.

Mhandisi Mfugale ameongeza kuwa daraja hilo litadumu kwa muda wa miaka 100 na litajengwa bila kuathiri nyumba zilizopo kando ya barabara za Kenyatta na Toure ambazo miongoni mwake wanaishi Mabalozi.

Mhe. Rais Magufuli ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Korea kwa kufadhili ujenzi wa daraja hilo na amemuomba Balozi Mteule wa Jamhuri ya Korea hapa nchini Mhe. Cho Tae-ick kufikisha ujumbe wake kwa Rais wa Jamhuri ya Korea Mhe. Moon Jae-in kuwa Tanzania itaendeleza na kukuza zaidi uhusiano na ushirikiano wake na nchi hiyo hususani wakati huu ambapo inaendelea kufanya mapinduzi makubwa ya kiuchumi.

“Jamhuri ya Korea ni marafiki wetu wa kweli, wametusaidia kujenga daraja la Kikwete katika mto Malagarasi na wametusaidia kujenga Hospitali ya Taaluma na Sayansi ya Tiba Mloganzila na miradi mingine, tunawashukuru sana, naomba na sisi Watanzania tubadilike, tuchape kazi, tuwe wazalendo, tuwahimize vijana wetu waje wafanye kazi kwenye mradi huu” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli ameitaka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kutafuta jina la daraja jipya la Selander na amependekeza lipewe jina la Tanzanite linaloakisi Utanzania.

Aidha, ametoa wito kwa Watanzania wote kuchapa kazi kwa juhudi na maarifa huku wakitanguliza uzalendo, kudumisha amani na upendo na kutokukatishana tamaa ili Tanzania ifanikiwe kupiga hatua za kimaendeleo kama ilivyofanya Jamhuri ya Korea ambayo uchumi wake ulikuwa sawa na Tanzania miaka ya 60 wakati Tanzania ikipata uhuru.

Mhe. Rais Magufuli amempongeza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe kwa juhudi zake za kusimamia ukusanyaji wa mapato ya Serikali ikiwemo kuhakikisha mabasi yote 49,000 yaliyopo nchini yanaanza kutoa tiketi za kielekroniki, kuongeza tija katika ukusanyaji wa mapato ya usafirishaji kwa njia ya reli na kufuatilia meli moja kubwa iliyonunuliwa kwa ushirikiano wa Tanzania na China ili ianze kuja nchini na kuinufaisha Tanzania.

Mapema katika salamu zake Balozi Mteule wa Jamhuri ya Korea Mhe. Cho Tae-ick ameishukuru Tanzania kwa uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati yake na Jamhuri ya Korea ambapo katika kipindi cha miaka 26 ya uhusiano huo, Jamhuri ya Korea imetoa ufadhili wenye thamani ya zaidi ya shilingi Trilioni 1 na hivyo kuifanya Tanzania kuwa nchi inayoongoza kwa ufadhili wa nchi hiyo Barani Afrika.

Nae mwakilishi wa EDCF Mhe. Hyon-jong Lee amesema kwa umuhimu wa kipekee wa uhusiano ya Tanzania na Jamhuri ya Korea, Serikali za nchi hizo zinaendelea na majadiliano ya ufadhili wa miradi yenye thamani ya shilingi Bilioni 687.6 itakayotekelezwa nchini Tanzania katika kipindi cha kuanzia mwaka 2018 hadi 2020.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
20 Desemba, 2018

Kubenea Amkana Makonda....Asema Hana Mpango wa Kuhamia CCM

$
0
0
Mbunge wa Ubungo (CHADEMA) Saed Kubenea amesema kuwa kitendo cha Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda kusema kuwa yeye na Mbunge wa Kibamba John Mnyika walitaka kujiunga na CCM, si kweli.

Kubenea amesema kuwa hawakuongea vile na Rais bali walikuwa wakizungumza mambo mengine, na Makonda amesema yale ili kuwafurahisha wanachama wa chama cha mapinduzi waliokuwepo kwenye hafla ile.

Kubenea amesema kuwa uchaguzi ujao watahakikisha kuwa wanashinda kwa kishindo hadi serikali inayoongozwa na CCM ishangae.

"Nataka nimwambie tu RC Makonda kwamba katika uchaguzi unaokuja upinzani tutashinda zaidi kuliko ilivyo kawaida, na ataondoka kwa aibu", amesema Kubenea.

Kubenea ameongeza, "Nchi yetu inajenga matabaka, mtu akionekana anaikosoa serikali wanasema huyu mpinzani na siku hizi wametupatia jina jipya wanatuita mawakala wa mabeberu".

Kubenea amesema kuwa, wale wanaomuunga mkono Rais Magufuli wengi wao ndio wanaompinga kimya kimya wakishirikiana na wanachama wengine ndani ya chama ambao wanajiandaa kumpinga katika uchaguzi ujao.

Hayo yamejiri baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda, kudai kuwa, amepokea maombi ya wanachama mbalimbali wanaotaka kujiunga na CCM, wakiwemo wabunge wawili wa CHADEMA, Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea na wa Kibamba, John Mnyika, wakati akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la kisasa la Selander na barabara unganishi jijini Dar es salaam.

Mrema Agoma Kurudi CCM

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour Party TLP na Mwenyekiti wa bodi ya Parole, Agustine Mrema amesema kuwa hawezi kumuunga mkono Rais John Pombe Magufuli kwa kumfuata ndani ya chama chake bali atafanya hivyo akiwa upinzani.

Mrema ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na kituo cha EATV  ambacho kilitaka kupata maoni yake juu ya hamahama ya waliokuwa wabunge wa vyama vya upinzani ambao walieleza sababu kuu ya kufanya hivyo kuwa ni kumuunga mkono Rais Magufuli.

Mrema amesema, "sina sababu ya kurejea CCM, na ningetaka kurudi CCM hakuna wa kunizuia, ila narudi kufanya nini kwa sababu Rais aliniona nikiwa TLP, nirejee CCM kutafuta nini kama kazi nimepata na nawatumikia watanzania."

"Kuhusu kumuunga mkono Rais mimi nilimuunga mkono akiwa hajachaguliwa licha ya wenzangu wa upinzani walikuwa wamenitenga, kwa hiyo sirudi CCM kwa sababu Rais wangu hajaniambia nirudi CCM," ameongeza.

"Siamini kumfuata Rais CCM ndiyo kumuunga mkono, mbona mimi niko TLP na namuunga mkono, nampenda nitaendelea kuwaambia watanzania wamchague," amesema Mrema.

Mrema alishawahi kuwa Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi akiwa ndani ya Chama Cha Mapinduzi ambaye alijibebea umaarufu kwa utendaji kazi wake lakini pia alishawahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Vunjo ambapo mwaka 2015 kiongozi huyo alienguliwa na Mbunge wa sasa James Mbatia.

CHADEMA Waendelea na Msimamo Wao wa Kususia Uchaguzi

$
0
0
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimeendelea na msimamo wake wa kutoshiriki chaguzi mbalimbali za marudio hapa nchini, kwa kile walichokidai kutofanyiwa haki, pamoja na kuminywa kwa demokrasia.

Msimamo huo wa CHADEMA umedhihirishwa kwenye chaguzi mbalimbali za marudio za hivi karibuni, ikiwemo uchaguzi katika jimbo la Singida Kaskazini, ambako alijiuzulu mwanachama wao wa sasa Lazaro Nyalandu.

Chaguzi nyingine ambazo CHADEMA ilitangaza kutoshiriki ni majimbo ya Ukerewe, Serengeti, Babati Mjini, Simanjiro, Liwale ambapo kwa sasa pia wametangaza kutoshiriki tena uchaguzi wa marudio wa Jimbo la Temeke.

Akizungumza Jijini Dar es salaam, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Mambo ya nje CHADEMA, John Mrema amebainisha kuwa msimamo wao ni ulele na haujabadilika.

"Msimamo wetu haujabadilika na tulishatangaza kutoshiriki uchaguzi mdogo kwa sababu tume ya uchaguzi haitutendei haki lakini leo tuna kikao ili kujua kwa mtu ambaye atashiriki uchaguzi huo tumchukulie hatua gani," amesema John Mrema.

Juzi Desmemba 18 kupitia Katibu Mkuu, Dkt Bashiru Ally, Chama Cha Mapinduzi CCM kilipitisha jina la Abdallah Mtolea kuwa mgombea Ubunge wa jimbo la Temeke.

Jana Disemba 19, 2018 mgombea huyo alichukua fomu ya kuwania ubunge wa Jimbo hilo na leo Desemba 20, 2018 ndiyo mwisho wa kurejesha fomu hizo.

Lowassa, Zitto Kabwe na Maalim Seif kutinga mahakamani kesho

$
0
0
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ni miongoni mwa viongozi watakaokwenda Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kesho Ijumaa Desemba 21, 2018 kusikiliza kesi inayowakabili vigogo wa Chadema, akiwemo mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe.

Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi Desemba 20, 2018 na mbunge wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea na kuthibitishwa na Mkurugenzi wa Mambo ya Nje, Itifaki, Mawasiliano wa Chadema, John Mrema inaeleza kuwa Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye naye atakuwepo.

Mrema amesema viongozi watakaokuwepo mahakamani ni wa vyama sita vilivyofanya mkutano juzi visiwani Zanzibar na kutoa maamuzi mawili mazito.

Mkutano huo ulioratibiwa na CUF chini ya Maalim Seif, vyama hivyo viliazimia kuanza kufanya mikutano ya hadhara kwa kuwa ni haki yao kwa mujibu wa sheria na Katiba ya nchi.

Pia, vilitangaza rasmi kwamba wanasiasa wote waliopo jela kwa tuhuma za kisiasa hao ni ‘Wafungwa wa kisiasa’ na kuanzia sasa wataitangazia dunia hivyo.

Maamuzi hayo ya Zanzibar yalisainiwa na Maalim Seif, mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia; mwenyekiti wa NLD, Oscar Makaidi; naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), Salum Mwalimu; mwenyekiti wa Chaumma, Hashim Rungwe na Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe.

Kesi hiyo ya jinai inayowakabili viongozi hao itatajwa kesho mahakamani hapo wakati Mbowe na mhazini wa Baraza la Wanawake la Chadema (Bawacha), Esther Matiko wakisubiri hatima ya rufaa yao.

Mbowe na Matiko wako gereza la Segerea, baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwafutia dhamana Novemba 26, 2018 kwa kukiuka masharti ya dhamana ikiwemo kutoka nje ya nchi bila kibali.

Washitakiwa wengine kwenye kesi hiyo ni Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vicenti Mashinji; manaibu katibu mkuu Salum Mwalimu (Zanzibar) na John Mnyika (Bara).

Wengine ni mbunge wa Kawe, Halima Mdee; mbunge wa Bunda, Ester Bulaya; mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa;  mbunge Tarime Vijijini,  John Heche.

Mbowe na wenzake, wanakabiliwa na mashtaka 12 ikiwemo kuandamana bila kibali, mkusanyiko usiokuwa wa halali pamoja na kutoa lugha za uchochezi.

Abdallah Mtolea Kapita Bila Kupingwa....Mkurugenzi Kamtangaza Kuwa Mbunge Temeke

$
0
0
Abdallah Mtolea, aliyepitishwa na CCM kuwania Ubunge wa Temeke,  leo Alhamisi Desemba 20, 2018 amepita bila kupingwa baada ya wagombea waliokuwa wamechukua fomu kuwania nafasi hiyo  kukosa sifa.

Mtolea aliyekuwa mbunge wa Temeke kwa tiketi ya CUF hadi Novemba 2018 alipojiunga na CCM na kupitishwa kuwania ubunge, leo Alhamisi Desemba 20, 2018 ametangazwa na msimamizi wa uchaguzi, Lusubilo Mwakabibi kuwa mshindi.

Katika hati ya kuchaguliwa kuwa mbunge ambayo Mpekuzi imeiona inaeleza kuwa kwa mujibu wa kifungu cha 81 (b) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi sura ya 343, Mtolea amechaguliwa kuwa mbunge wa Temeke katika uchaguzi uliofanyika leo.

Kifungu cha 45 (2) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, na kile cha 44 cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, vinasema endapo mgombea aliyeteuliwa katika uchaguzi ni mmoja tu, mgombea huyo atahesabika amechaguliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya Disemba 21

Waziri Ummy Apeleka Gari Ya Wagonjwa Ruangwa.

$
0
0
Na Bakari Chijumba, Lindi
Serikali imeahidi kukipatia kituo cha afya cha Luchelengwa wilayani Ruangwa, gari la kubebea wagonjwa pamoja na mashine ya kisasa ya Xray kabla ya Aprili 2019, lengo likiwa ni kuboresha  huduma za afya kwa wananchi.

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu, ametoa ahadi hiyo alipofika kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa na  kupokea taarifa ya Afya ya Wilaya hiyo jana 20 Desemba 2018.

Waziri Ummy amefikia uamuzi huo baada ya Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Hashim Mgandilwa, kutaja changamoto zinazosabababisha kusuasua kwa upatikanaji wa huduma ya afya ya uhakika.

"Mwezi wa tatu mwakani nitakabidhi gari la kubebea wagonjwa kituo cha Afya luchelengwa na mwezi  wa pili nitakabidhi machine ya mionzi ya kisasa " amesema Waziri Ummy

Aidha Waziri amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, kuanza ujenzi mara moja wa chumba cha kisasa cha kuhifadhia machine ya mionzi katika hospital ya Wilaya, ili iwe rahisi kukabidhi mashine hizo kwa wakati.

Katika hatua nyingine waziri Ummy, amepongeza kitendo cha Hospitali ya Wilaya kuwa na dawa zote muhimu zinazotakiwa kupatikana hospital na hiyo ni baada ya kukagua na kuona stoo ya dawa zilizopo hospitalini hapo.

"Nimefurahishwa na uwingi wa dawa uliopo hospitalini, niwatake muendele hivi hivi kuwa na dawa za muhimu za kutosha ili tupunguze suala la wananchi wetu kununua dawa kwenye maduka ya nje ya watu binafsi" amesema Mheshimiwa Ummy.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Hashim Mgandilwa  ametoa shukurani kwa serikali  kwa kuahidiwa kupatiwa Gari la wagonjwa na mashine ya mionzi (XRAY).

Mgandilwa amewataka madaktari kuhakikisha kila siku asubuhi wanabadili chati ya dawa ili iwe rahisi katika utendaji wao na kujua dawa ipi ipo kwa siku hiyo na ipi haipo.

" Mara nyingi nimekuwa nikipita naona hamfanyi mabadiliko ya chati ya dawa hii inasababisha wagonjwa kuandikiwa dawa zisizokuwepo, kuweni na taratibu kila siku asubuhi kubadilisha itawasaidia sana katika utendaji wenu" amesema Mgandilwa

MWISHO

Wakili Akwamisha Kesi ya Utakatishaji Mabilioni TRA

$
0
0
Upelelezi wa kesi ya kuisababishia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) hasara ya Bilioni 188.9  kupitia mashine ya risiti za kielekroniki (EFD)  inayomkabili  mfanyabiashara Mustapha Kambangwa (34), bado haujakamilika.

Kambangwa, mkazi wa Mbagala Kongowe anakabiliwa na mashtaka manne Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, likiwemo la  kutakatisha fedha .

Kwa mara ya kwanza, Kambangwa  alifikishwa mahakamani hapo Desemba 7, 2018  kujibu mashtaka manne  katika kesi ya uhujumu uchumi namba 19/ 2018.

Wakili wa Serikali, Ester Martin amedai jana Alhamisi Desemba 20, 2018 mbele ya Hakimu Mkazi, Janeth Mtega kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na upande wa utetezi kuwasilisha hoja za kupinga shitaka dhidi ya mshtakiwa.

Hata hivyo,  hoja hizo hazikuwasilishwa mahakamani hapo baada ya Ester kudai  kwamba wakili mwenzake Christopher Msigwa, ambaye ndio mwenye jalada halisi la kesi hiyo ameshindwa kufika mahakamani kwa sababu ni mgonjwa.

Baada ya upande wa mashtaka kueleza hayo, wakili wa utetezi Shamo Shadrack, alidai ofisi ya waendesha mashitaka ina  mawakili wengi na kuhoji sababu za  kuumwa kwa mtu mmoja kuzuie kesi kuendelea.

" Kuumwa kwa mtu mmoja kusizuie kuendelea kwa kesi, kwani mawakili wote wanafanya kazi ofisi moja hivyo tunaomba tarehe ijayo ambayo ni Desemba 24, 2018 tuweze kuwasilisha hoja zetu, " alidai Shadrack.

Baada ya kusikiliza hoja za pande zote, Hakimu Janeth aliwataka upande wa mashitaka kuhakikisha shauri hilo linaendelea hata kama yule wa  awali bado anaumwa aendeshe mwingine.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba 24, 2018 na mshtakiwa kurejeshwa rumande.

Radi Yaua Watu Watatu Ruvuma

$
0
0
Watu watatu wa familia moja wamefariki dunia kwa kupigwa na radi katika kijiji cha Majimaji, wilayani Tunduru, mkoani Ruvuma.

Taarifa za tukio hilo zilizothibitishwa na Mtendaji wa Kata ya Majimaji, Neema Mahujilo, zinaeleza kuwa, radi hiyo iliambatana na mvua kubwa ya upepo iliyonyesha Desemba 14, saa 12. 30 hadi saa 1.40 jioni.

Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Jemini Mushy, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo na kwamba Polisi inaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha vifo hivyo.

Kamanda Mushy aliwataja watu waliopoteza maisha kuwa ni Zenna Hamadi Ismail (50), Yusuph Abdalah Alli (25) na Zamila Abdalah Abbilahi (3).

Mganga Msaidizi wa Hospitali ya Wilaya ya Tunduru, Edger Ngauje, aliyeifanyia uchunguzi miili ya marehemu, alisema kuwa chanzo cha vifo hivyo ni kuunguzwa na shoti ya umeme uliosababishwa na radi hiyo.

China Yatangaza Neema Kwa Wakulima wa Karanga,Ufuta na Maharage......Inataka Tani 10,000 za Mazao Hayo

$
0
0
Ubalozi wa Tanzania Beijing, China umebainisha kuwa kampuni moja nchini China imewasilisha ombi la kununua ufuta, karanga na maharage ya soya kutoka Tanzania.

Taarifa iliyotolewa jana Alhamisi Desemba 20, 2018 na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade) na kusainiwa na mkuu wa kitengo cha mawasiliano wa mamlaka hiyo, Theresa Chilambo inaeleza kuwa kampuni hiyo inalenga kununua bidhaa hizo kwa vigezo.

Kampuni hiyo inahitaji ufuta tani 3,000 kwa mwezi, karanga tani 2,000 kwa mwezi na maharage ya soya tani 5,000 kwa mwezi

Theresa amesema ufuta unaotakiwa ni wa ubora wa Taifa daraja la pili.Amebainisha kuwa hata karanga na maharage ya soya yanayohitaji  nayo ni katika kiwango hicho cha ubora.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images