Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Makanga 3 Power, Dawa Bora Za Nguvu Za Kiume

$
0
0

Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.

Tupo dar es salam Buguruni

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

Fastjet Wajipanga Kuingiza Ndege Mbili....Moja Itatua Nchini Jumamosi Hii

$
0
0
Mwenyekiti mtendaji wa Shirika la Ndege la Fastjet Tanzania, Lawrance Masha amesema wamejipanga kuingiza ndege aina ya Boeing 737 na Bombardier. Amesema Boeing itaingia  Tanzania Jumamosi Desemba 22, 2018.

Akizungumza leo Jumatano Desemba 19, 2018 katika kipindi cha 360 kinachorushwa na Clouds Televisheni, Masha amesema  ndege ya shirika hilo aina ya Boeing 737 ambayo ilizuiliwa kuruka na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kutokana na hitilafu za kiufundi, sasa iko imara.

“Kuanzia Jumamosi tukakuwa na ndege mbili aina ya Boeing 737 (pamoja na iliyopo sasa) ambazo zitakuwa tayari kufanya kazi. Hii  itasaidia kuondoa kero ya kusitishwa kwa safari,” amesema Masha.

“Ndege zote zitakuwa na usajili wa Tanzania na kutokana na mahitaji na msimu,  hivi karibuni tunaweza kuongeza ndege nyingine moja au mbili aina ya Bombardier.”

Amesema ana imani shirika litainuka na kuwa imara zaidi na juhudi zinazofanyika sasa ni kuzungumza na mamlaka ili kuwaruhusu kuanza kuuza tiketi.

Amesema tayari baadhi ya matakwa ya mamlaka hiyo yametimizwa au kujibiwa ingawa bado mazungumzo yanaendelea.

“Tunatarajia kurejesha safari zetu za Nairobi na Afrika Kusini kuanzia Februari 2018 na kuanza kwenda Songea, Dodoma, Bukoba na Arusha mjini endapo TCAA wataturuhusu kwakuwa tutakuwa na ndege ndogo ambazo zina uwezo wa kutua katika viwanja hivyo,” amesema Masha.

Juzi, TCAA ilitangaza kuwa Fastjet imepoteza sifa ya kufanya biashara nchini na ndege yao moja imezuiwa kuruka kutokana na matatizo iliyonayo na kukosekana kwa meneja mwajibikaji wa shirika. Ilitoa notisi ya siku 28 ikikusudia kuifuta leseni ya shirika hilo.

Katibu mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally Agoma Kuzungumzia Sakata la Membe

$
0
0
Katibu mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally amegoma kuzungumzia sakata la waziri wa zamani, Bernard Membe ambaye alimwita kuzungumza naye kabla yakufanyika kwa kikao cha NEC .

Jana Jumanne Desemba 18, 2018 Kikao  hicho cha Halmashauri Kuu ya CCM  kiliketi ambapo pamoja na mambo mengine, kiliwasamehe na kuwarejeshea uanachama  waliokuwa wenyeviti wa mikoa wa chama hicho huku kikimpitisha Abdallah Mtolea kuwania ubunge wa Temeke.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari baada ya kikao hicho, Dk. Bashiru alisema hawezi kujibu swali lolote linalohusu suala la Membe katika mkutano huo kwa kuwa anatekeleza kile alichotumwa na mwenyekiti wake, kutoa taarifa ya yale waliyokubaliana katika mkutano wa NEC ulioanza juzi na kumalizika jana.

Dk. Bashiru alipokuwa katika mikutano yake mjini Bukombe, Geita Desemba 1, alimwita Membe ambaye pia aliwahi kuwa miongoni mwa waliowahi kuwania kuteuliwa kuwa mgombea wa urais kupitia CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, kufuatia taarifa alizodai kuwa zinazagaa katika mitandao ya kijamii, zikieleza nia yake ya kuwania kumpinga Rais Magufuli katika uchaguzi mkuu ujao.

Alisema tangu alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM hajawahi kuonana wala kuwasiliana na Membe, lakini sasa anachukua uamuzi wa kumwita iliazungumze naye kwa kuwa katika kipindi cha nyuma chama hicho kiliumizwa sana na makundi, fitina, uongo na nguvu ya pesa, mambo ambayo kwa sasa hawezi kuyaendeleza.

Hata hivyo, baada ya kuendelea kwa majibizano na taarifa mbalimbali kutokana na hatua hiyo, Dk. Bashiru alimtaka Membe kufika ofisini kwake kabla ya kikao cha NEC kilichofanyika juzi na jana.

Hata hivyo, hakuna taarifa yoyote iliyotolewa baada ya hapo, iwapo Membe alionana na Dk. Bashiru au laa, japo kuwa alisema mlango ukowazi kufanya majadiliano maalumu kuhusu mambo mengine ambayo hayahusiani na maamuzi ya NEC jana.

Dk. Bashiru pia alikanusha taarifa zilizokuwa zikizagaa katika mitandao ya kijamii kuwa mjumbe wa NEC kutoka Mara, Stephen Wassira alizuiwa kuingia katika kikao hicho jana asubuhi.

Alisema Wassira alihudhuria kikao hicho na alikuwa miongoni mwa watu waliochangia kwa kujiamini na alitoa mchango mkubwa.

Kutana Na Dr Chikago Bingwa Na Mwokozi Kwa Waliosumbuka Na Magonjwa Bila Mafanikio

$
0
0
Ninauwezo wa kumrudisha mume, mke ,mchumba, hawara, mtu unaempenda ndani ya masaa mawili tu (2) na kumfunga asiwe na mtu mwingine zaidi yako na kumfanya akutimizie kilakitu unachokihitaji kutoka kwake hata km yupo mbali na atatulia kabisa

GALIMBO 3 MIX;  nidawa ya mitishamba iliyitengenezwa kwa kwa utabibu wa hali ya juu kwakuchanganya miti na matundatiba , Huogeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15 -85 ) , inakomaza zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakat wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaid ya Mara tatu bila ham kuisha wara kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-40.

YOLANI :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inch (6-8) na unene wa sm (3-4)

Matatizo haya husababishwa na mambo mbalimbali km upigaji wa punyeto, kisukali,  vidonda vya tumbo, tumbo kuunguluma na kujaa gesi, ngili, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani, maumivu ya mgongo ama kiuno, namengineyo mengi  (nk )

SUPER MBUKE :- nidawa inayotatua tatizo la kisukali na kupona kabisa Kwa mda mfupi sana na utakuwa na uwezo wakula chakula chochote chenye sukali baada ya kupona,

vilevile ninadawa ya uzazi kwa akina Mama na akina Baba, kurudisha mali iliyopotea kwamda mfupi sana, vidonda vya tumbo, kaswende,presha,chango la uzazi, gono,nyama uzembe, kusafisha nyota, kuzuia majini wachafu, kinga ya mwili, kuuza vitu bila kununuliwa, dawa za biashara, pesa nyingi (utajili)  mambo ya kes nk

Kwa huduma n msaada wasiliana na Dr CHIKAGO atakusaidia hatakama ulikata tamaa utarudisha furaha yako

Napatikana Dar es salaam  sm no 0743543944   /0620510598

Nb :km huna nafasi ya kufika ofisin huduma hii itakufikia popote ulipo kwawatu wa mkoani tunatuma kwanjia ya mabasi.

Mnyika Ampongeza Rais Magufuli....Ataka Busara Itumike Kuwalipa Fidia Waliokumbwa na Bomoabomoa

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Kibamba kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (CHADEMA), John Mnyika amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli kwa kuweza kuamua kujenga barabara ya njia nane.

Amesema kuwa Watanzania wamemuombea asiwe na kiburi, huku akisema Wananchi wana malalamiko juu ya Bomoabomoa ambapo amemuomba kutanguliza utu, wa Mwl. Nyerere mbele.

Aidha, Mnyika ameongeza kuwa maendeleo ni ya vitu lakini maendeleo zaidi ni ya watu huku akimtaka atafakari kuwalipia fidia Wananchi waliopisha ujenzi huu.

“Kuna hili suala la bomoabomoa tunaomba ubinadamu utumike kwa kuwalipa fidia wananchi ili kuondoa malalamiko yaliyopo,” amesema.

Mbali na suala hilo la bomoabomoa,  Mnyika pia amemuomba Rais Magufuli kuondoa vikwazo vinavyoikabili demokrasia nchini.

”Demokrasia na Maendeleo ni mapacha, tunakuomba Rais unapofanya kazi za Miradi ya Maendeleo vilevile ukatumia fursa hii kuzungumzia kuondoa vikwazo vinavyoikabili Demokrasia ya Nchi ambayo tunaamini vitasaidia Nchi kusonga mbele,”amesema Mnyika

Pia ameongeza kuwa kuna mambo matano yanatoka kwa mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ambayo anawaomba Watanzania na Rais kwa ujumla kuweza kuyatafakari kwa muda huu tunapoelekea mwaka 2019.

Hata hivyo, Mnyika amesema kuwa akisikia Wafanyakazi wa Umma wanalilia kikokotoo, wengine wamepandishwa madaraja hawajapandishwa mishahara, Wafanyabiashara wanalia Mtaani, na kumuomba akipata nafasi ya kuzungumza pamoja na uzinduzi utatoa matumaini ya Taifa kwa 2019 na 2020″

Kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Salum Hapi Baada ya Kuzushiwa Kulala MAKABURINI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Salum Hapi ameonesha kushangazwa na madai ya kujikuta amelala kwenye makaburi mkoani Iringa, kitendo ambacho kinahusishwa na imani za kishirikina.

Kupitia mtandao wake wa Twitter Hapi ameandika ujumbe ulioashiria kuwa analichukulia tukio hilo ni la mzaha ambapo aliambatananisha na picha yenye maneno yanayodai kufanyiwa kitendo hicho.

Aidha katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa ameamuru mtumiaji huyo wa mitandao ya Kijamii, Hilda Newton kwenda kujisalimisha kwa Mkuu wa Polisi Iringa kwa ajili ya kutoa maelezo kabla ya disemba 21 mwaka huu,

”Aliyetunga na kusambaza uzushi huu akajisalimishe yeye Mwenyewe kwa RPC Bwire Iringa kabla ya tar 21.12.2018 saa 2:00 asb. Nasikia ni Katibu wa BAVICHA,”ameandika RC Hapi katika ukurasa wake wa Twitter

Kupitia ukurasa wa twitter wa mtu ambaye alisomeka kwa jina la Hilda Newton, aliandika,”Naambiwa mwezi mmoja uliopita, alikuwa amelala nyumbani kwake ilipofika alfajiri alijikuta amelala makaburini,”

Saed Kubenea Ammwagia Sifa Rais Magufuli kwa Ujenzi wa Barabara na Ukuaji wa Uchumi

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Ubungo kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Saed Kubenea ameunga mkono juhudi za Rais Magufuli katika ujenzi wa barabara, ukuaji wa uchumi huku akisema anaunga mkono kwa asilimia 200%.

Ameyasema hayo leo Jumatano 19 Disemba 2018 katika uzinduzi wa barabara ya kilomita 19. 2 unaoanzia Kimara jijini Dar es salaam mpaka Kibaha mkoani Pwani, ambapo amesema uzinduzi huo ni wa kihistoria na wao kama wapinzani wanaunga mkono.

”Kwakweli kwa juhudi hizi mheshimiwa rais Magufuli tunakuunga mkono kwa asilimia 200%, tumeona namna unavyokuza uchumi, sisi tukuhakikishie kuwa tuko pamoja,”amesema  Kubenea na kuongeza;

"Jambo dogo linalotutatiza wananchi hawa wana manunung'uniko yanayotokana na fidia, uangalie wananchi wote waliobomolewa wapate fidia zao. "

Rais Magufuli Asema Waliobomolewa Nyumba Zao eneo la Kimara, Mbezi Hawatalipwa Fidia

$
0
0
Rais John Magufuli amesema waliobomolewa nyumba kupisha upanuzi wa barabara ya Morogoro eneo la Kimara hadi Mbezi jijini Dar es Salaam hawatalipwa fidia kwa kuwa walijenga katika eneo la hifadhi ya barabara.

Rais Magufuli ametoa ufafanuzi huo leo Jumatano Desemba 19, 2018 katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi la upanuzi wa barabara hiyo inayofanyika eneo la Kimara Stop Over.

Huku akirejea mara tatu kusema "hakuna fidia", Magufuli amesema hata wakienda mahakamani hakuna fidia.

“Niwambie tu wananchi kuwa ukisogelea barabara madhara yake ni umasikini, hata mimi sijafurahishwa na hii bomoabomoa kwa kuwa wapo ndugu zangu nyumba zao zimebomolewa,” amesema.

"Ni vyema kuwaambia ukweli kesi hii hata wakienda wapi hawawezi kushinda."

Maadhimisho Krismasi kitaifa kufanyika Jijini Mwanza

$
0
0
Wakati zikiwa zimesalia siku sita tu kuelekea Sikukuu ya Krismasi, maadhimisho ya Sikukuu hiyo Kitaifa yatafanyika katika Jimbo Kuu Katoliki Mwanza.

Taarifa ya Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) iliyotolewa na Mratibu wa Kurugenzi ya Mawasiliano, Pascal Mwanache imesema maadhimisho hayo yatatanguliwa na mkesha wa Krismasi utakaofanyika katika Kanisa Kuu la Epifania Bugando.

Misa ya mkesha itaongozwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Bunda ambaye pia ni msimamizi wa Kitume wa Jimbo Kuu Katoliki Mwanza, Mhashamu Renatus Nkwande.

“Aidha misa takatifu ya Krismasi Desemba 25, 2018 itakayoanza saa nne kamili asubuhi itafanyika katika kanisa la Epifania Bugando na pia itaongozwa na Askofu Renatus Nkwande,” imesema taarifa hiyo.

Baraza hilo limewaalika waumini wa dini hiyo kuungana katika kuadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo ambaye ni mkombozi wa ulimwengu.

Mke wa Mugabe Kukamatwa

$
0
0
Polisi nchini Afrika Kusini imetoa amri ya kukamatwa kwa Grace Mugabe, mke wa aliyekuwa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ambaye anatuhumiwa kumshambulia na kumjeruhi mwanamitindo wa Afrika Kusini, Gabriella Engels, mwaka 2017.

Mwanasheria anayefanya kazi na shirika la kutetea haki za binadamu la AfriForum la huko Afrika Kusini, Garrie Nel amesema amethibitishiwa na Polisi kuhusu kutolewa kwa amri hiyo, na kuongeza kuwa ikiwa Bi. Mugabe atakanyaga kwenye ardhi ya Afrika Kusini atakamatwa.

Mwanasheria huyo vile vile ametaka mchakato wa kumtia mbaroni Grace Mugabe na kumsafirisha hadi Afrika Kusini uanze sasa.

Grace Mugabe anatuhumiwa kumpiga na kumjeruhi mwanamitindo Gabriella Engels kwenye hotel moja mjini Johannesburg Agosti mwaka 2017, lakini hakushtakiwa kwa sababu alikuwa na kinga ya kidiplomasia.

Waziri Mwakyembe Apokea majina 8 ya wanaokwamisha uchaguzi Yanga

$
0
0
Waziri wa Habari Sanaa Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwanyembe amepeleka majina nane ya wanachama wa klabu ya Yanga kwenye vyombo vya usalama kwaajili ya kuwachunguza.
 
Akisoma taarifa ya Waziri Mwakyembe kwa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa Ufundi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Yusuph Singo amesema Mh. Mwakyembe hafurahishwi na vitendo vya wanachama hao.

Waziri Mwakyembe ameeleza kuwa wanachama hao wanaoongozwa na Bakili Makele, wanahamasisha wanachama wengine kupinga uchaguzi wa Yanga uliopangwa kufanyika Januari 13, 2019.

Taarifa hiyo imesema kuwa wanachama hao wakiongozwa na Bakili wanahamasisha wanachama kususia uchaguzi wakishinikiza kuwa Mwenyekiti wao Yusuph Manji bado yupo madarakani.

Wanachama hao ni:-
  1. Bakili Makele
  2. Mustaph Mohammed
  3. Said Bakari
  4. Shaban Mgonja
  5. Kitwana Kondo
  6. Boaz Kupilika
  7. David Sanare
  8. Edwin Kaisi.
Bakili ambaye alikuwa Mwenyekiti wa matawi ya Yanga huku Boaz akiwa Katibu wake walifungiwa kujihusisha na soka miaka mitano na faini ya milioni mbili na Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) kwa kosa hilo hilo wiki kadhaa zilizopita.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Disemba 20

Jipatie Dawa ya Asili ya Kupunguza Maziwa, Kupunguza Tumbo,Kuongeza Unene, Kuongeza Maumbile ya Kiume na Kuondoa Chunusi

$
0
0
NATURAL BEAUTY PROD.
🍋🥑🍒OFFER ya X MAS na MWAKA MPYA🍉🍇

 Ofa hii itaisha tareh. 22/12/2018 wahi sasa jipatie bidhaa original kwa punguzo la bei.

 %%Bidhaa hizi zimetengenezwa kwa mimea na matunda hazina chemical wala madhara yoyote kwa mtumiaji.             Ukinunua bidhaa kuanzia mbili utapatiwa offer ya bidhaaa nyingine yoyote uipendayo wewe bureeee.

1. SHARK POWER--Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza maumbile ya kiume urefu na upana mpaka nchi 7.5 ilikua inapatikana kwa @170,000/= sasa ni @160,000/= tu

2. VIGA 84000---Hii dawa ya kuspray yenye uwezo mkubwa wa kuchelewesha wakati wa tendo la ndoa ilikua ni  @160,000/=. Sasa ni 150,000/= tu

3. HANDSOME UP ORIGINAL-- Hichi ni kifaa cha kuongeza maumbile kwa size uipendayo wewe pamoja na kuimalisha misuli kifaa hichi kilikua kinapatikana kwa @230,000/=. Sasa ni 210,000/= tu

4. MAXMAN CAPSULE--- Hii ni dawa ya vidonge ya kuongeza maumbile ya kiume urefu na upana pamoja na kuongeza nguvu za kiume kwa wiki mbili ilikua inapatikana kwa @200,000/=. Sasa ni 180,000/= tu

5. VIG RX---- Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza uume urefu na upana mpaka nchi 10 ilikua inapatikana kwa @190,000/=. Bei ya sasa ni 170,000/=

6. BODY BOOSTER---Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri ilikua inapatikana kwa @150,000/=. Sasa ni 140,000/=

7. BOTCHO MULT PLUS-- Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza (hips mapaja na makalio) kwa size uipendayo ilikua inapatikana kwa @200,000/=. Sasa ni 180,000/=

8. WHITE COLLECTION---- Ni vidonge vya kuwa mweupe mwili mzima pamoja na kuwa soft ilikua inapatikana kwa @150,000/= Sasa ni @140,000/= tu

9. BOTCHO HOLOGRAM CREAM--- Hii ni dawa ya kuongeza hips na makalio ilikua inapatikana kwa@180,000/= Sasa ni@160,000/=       

N.K

Wasiliana nasi kwa simu

NO:. +255 759029968  AU +255 659618585

Popote ulipo utapata huduma zetu.

Pia hakikisha unapatiwa risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ununuapo bidhaa kampuni hii.

WELCOME ALL

Wajumbe wa CAF Wawasili Tanzania.....Ratiba Ya Michuano Ya Afcon U17 Mwaka 2019 Itakayofanyika Tanzania Kupangwa Leo Mlimani City

$
0
0
Shirikisho la soka Afrika CAF Leo Alhamisi ya Disemba  20 2018 katika ukumbi wa Mlimani City Dar es Salaam watapanga Makundi ya michuano ya mataifa ya Afrika AFCON 2019 kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 ambapo michuano hiyo inachezwa Tanzania wakiwa wenyeji.

Afisa Habari na Mawasiliano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Clifford Mario Ndimbo amesema kwamba maandalizi yote yamekamilika kuelekea zoezi hilo.
 
Ndimbo amesema kwamba Rais wa TFF, Wallace Karia tayari amepokea ugeni kutoka Shirikisho la Soka Afrika (CAF) ambao upo nchini kwa upangaji wa ratiba.

Amesema ujumbe huo wa CAF ukiwa hapa nchini umetembelea kukagua uboreshaji wa miundo mbinu ya viwanja unaoendelea na Karia amesema baada ya kutazama maendeleo ya Viwanja watashauri zaidi kulingana na walivyoona maendeleo hayo.
 
Ndimbo amesema mbali na Viwanja ujumbe huo wa CAF umetembelea Hoteli na Hospitali na leo utahudhuria upangaji wa ratiba ya fainali hizo utakaofanyika kuanzia saa 12:00 jioni na Dunia itapata kushuhudia upangaji huo moja kwa moja kwenye Televisheni.
 
Wajumbe wa CAF waliopo nchini ni Samson Adamu,Yasmin Hossam Eldin El Ehwany,Amri Ali Sadek,Mohamed Bakeer,Fayrouz Mahml,Mohamed Alaa El Shizy,Dina Medat,Moses Magogo anayewakilisha Kamati y Utendaji ya CAF wakati Leodger Tenga Mjumbe wa Kamati ya Utendaji CAF atakua mwenyeji wao.
 
Timu zilizofuzu kushiriki AFCON U17 Mei mwakani pamoja na wenyeji, Tanzania nyingine ni Morocco, Senegal, Guinea, Nigeria, Cameroon, Uganda na Angola.


Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power

$
0
0
Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power Kwaajili Ya Nguvu Za Kiuume Na Promix Kwaajili Ya Kuongeza Maumbile;
Kwa mwanaume aliyekamilika na mwenye Afya njema ili kumridhisha mke au mpenzi anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara mbili hapo utamridhisha mpenzi wako ila ukiwa unapiga moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe 

Tiba Ya Tatizo Lako Ni Dawa Hiitwayo Simpo Power No, 1; dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge vya miti shamba na unga ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja :-1 itakufanya urudie tendo zaidi ya mara tatu 
2 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-20 kwa tendo la Kwanza 
3 huimarisha uume uliolegea na kusinyaa 

Je Una Mke Au Mpenzi Aliyebalikiwa Kuwa Na Kario Kubwa Au Mwili Mnene Na Wewe Mume Wake Una   Maumbile Mafupu?; tumia sasa dawa ya PROMIX dawa itakufanya umfikishe shemu nyeti maana inaboresha maumbile saizi upendayo.

Dawa zangu haziina madhara yoyote kwa mtumiaji 

MARKSU; ni dawa ya kisukari dozi siku 21 
MWARU; ni dawa ya uzazi,hufungua milija ya uzazi ata kwa Wale waliofungiwa uzazi  
MTUNDUU; ni dawa ya busha bila kupasua 
MAZANZA; ni dawa ya kisukar zipo dawa za miguu Kuuma,tumbo,kupunguza Matiti,kutoa minyama uzembe ngiri,vidondo vya tumbo  

FIKA OFISINI KWANGU BUGURUNI MALAPA KARIBU NA KOTA ZA POLISI AU PIGA  SIMU ULETEWE MAHALI ULIPO SIMU NO 0783185060,  0752348593  -DR AGU

Mvua Yaacha Kilio Tanga....Nyumba 300 Zamezwa na Maji

$
0
0

Mvua kubwa inayoendelea kunyesha jijini Tanga, imesababisha zaidi ya nyumba 300 kuzama maji baada ya kukumbwa na mafuriko katika Kata ya Magaoni, hivyo kusababisha wakazi wake kuhama makazi yao.

Tukio lilo lilitokea usiku wa kuamkia jana majira ya saa 7:00 usiku 
baada ya mvua kubwa kunyesha usiku kucha.

Mwenyekiti wa Kata ya Magaoni, Kassim Abdallah, ambaye pia nyumba yake 
imezama, alisema kuwa mvua iliyonyesha usiku wakuamkia jana,
imeacha hasara kubwa kwa wakazi wa kata hiyo kutokana na kuzingirwa na maji, huku mali mbalimbali zikiharibika.


Alisema mvua hiyo ilianza kunyesha wakati huo mpaka saa 2:00 asubuhi, hivyo kusababisha idadi kubwa ya wananchi kukosa mahali pa kuishi, hivyo kuhamia katika shule na wengine kuhifadhiwa kwa ndugu na jamaa zao.


Abdallah alisema kata hiyo ni mpya kwa kuwa mwanzo ilikuwa sehemu ya kata ya Mabawa kabla ya kugawanywa. 

Alisema sababu kubwa ya mafuriko hayo ni kukosekana kwa mifereji ya kutosha, hivyo kushindwa kuruhusu maji kutiririka kwa urahisi.



Mwenyekiti huyo alisema Diwani wa Kata hiyo, 
Mohamed Rajabu, baada ya kuchaguliwa mwaka 2015 alijitahidi kuhakikisha mifereji inajengwa lakini iliyopo haitoshelezi mahitaji ndiyo maana imekuwa rahisi kutokea mafuriko.


Kutokana na athari hiyo, aliiomba Halmashauri ya Jiji la Tanga kutenga fedha kwa
ajili ya mifereji, vinginevyo maafa yanaweza kuwa makubwa zaidi.

Naye Diwani Rajabu alisema mvua hiyo imesababisha 
mafuriko makubwa na kwamba mpaka sasa wananchi hawana mahali
pa kuishi na wamezikimbia nyumba zao huku vyombo vyote vikiwa vimeharibika.



Alisema kuwa ili kuondoa tatizo hilo, alisema ni lazima Halmashauri
ya Jiji la Tanga ipange bajeti kwa ajili ya kutengeneza mifereji ya
kupitisha maji katika kata hiyo, vinginevyo kunawezekana kutokea maafa makubwa
 zaidi.

Rais Magufuli Alivyopangua Kauli ya John Mnyika Kuhusu Demokrasia na Vyuma Kukaza

$
0
0
Rais John Magufuli amemjibu mbunge wa Kibamba (Chadema), John Mnyika baada ya mbunge huyo kuhoji kuhusu demokrasia, vyuma kukaza na kuomba waliovunjiwa nyumba zao kupisha upanuzi wa barabara ya Morogoro kulipwa fidia.

Magufuli alitoa kauli hiyo jana Jumatano Desemba 19, 2018 muda mfupi kabla ya kuweka jiwe la msingi la upanuzi wa barabara ya Morogoro jijini Dar es Salaam katika eneo la Kimara Stop Over.

“Nilitegemea atakaposimama hapa angesema asanteni sana CCM, demokrasia ya namna gani anaitaka, hata kufunika midomo usiongee nayo ni demokrasia. Demokrasia siyo fujo, watu wafanye fujo mitaani wabomoe maduka halafu tuwaache eti kisa ni demokrasia? Haiwezekani. Demokaria ya kweli imehamia bungeni.

“Napenda kuwaambia ndugu zangu wa eneo hili la Kimara kuwa, ukivamia sehemu ya barabara ujue kabisa umetafuta umaskini, hivyo anayewaambia kua kuna fidia, mimi ninawaambia fidia haipo, narudia tena fidia haipo, fidia haipo.

Awali Mnyika alimuomba Rais Magufuli kuwalipa fidia wananchi waliyobomolewa nyumba zao katika eneo la Kimara kupisha upanuzi wa barabara hiyo, lakini Rais amesisitiza kuwa serikali haitalipa fidia kwa watu waliobomolewa nyumba zao kwa kuwa walikuwa wamejenga ndani ya hifadhi ya barabara.

“Wapo wanasema vyuma vimekaza, vitakaza kweli, asiyefanya kazi na asile, lazima tuwaambie ukweli hii ya vyuma vimekaza ni watu wanazushazusha. Wananchi wa Ubungo muache kulalamika vyuma vimekaza, mkatafute kazi ya hata ya kuchimba mtaro hivyo vyuma havitabana.

“Ninawaomba Watanzania wote, hebu tujiamni basi angalau kwa miaka mitano, nikishaondoka muache kujiamini, mfanye mnavyotaka. Kwa nchi inayojitambua hatuwezi kusubiri misaada, mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe, nchi hii sio katili. 

"Tuheshimu Sheria zetu, nafahamu Sheria ni ngumu na ndiyo maana unakuta hata sheria za Mussa hatuziheshimu, usitamani mwanamke wa mtu unakuta kila mtu anatamani tu.

“Kuna watu wanasema eti ni kodi zetu, kwani zamani mlikuwa hamlipi kodi? Mmbona hazikujengwa? Kwa nini msiseme tu kuwa ni juhudi za Rais Magufuli? 

"Watu wamefariki kwa kushindwa kuwahi Muhimbili kwa ajili ya msongamano wa barabara hii, ndoa zimevunjika mtu anatumia sababu ya msongamano anarudi nyumbani usiku kumbe alikuwa pembeni anasema msongamano kumbe jamaa analiwa,” alisema Magufuli.

Jeshi La Polisi Dodoma Lakamata Watuhumiwa 64 Wakiwemo Wezi, Makahaba na Wauza Madawa ya Kulevya

$
0
0
Jeshi la Polisi Jijini Dodoma linaendelea na misako katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo ambapo limefanikiwa kukamata watuhumiwa 64 wakiwemo Wezi, Makahaba na Wauza Madawa ya kulevya.
 
Akizungumza jana na waandishi wa habari jijini Dodoma  kuhusu kukamatwa kwa watuhumiwa 64 kati yao wakiwamo 11 wa ukahaba, Kamanda wa Polisi mkoani humo, Gilles Muroto, alisema kuwa jeshi hilo litaendelea kuwakamata watu hao kwa kuwa wanachafua taswira ya jiji hilo.

Kamata kamata ya watu wanaofanya biashara hiyo, ilianza Oktoba 9, mwaka huu na kukamata makahaba 22, wanaume watano waliokuwa wakiwanunua pamoja na wamiliki wanne wa maeneo yanayoruhusu biashara hizo.

Aidha, Oktoba 31, mwaka huu, jeshi hilo liliwakamata watu wengine 17 wanaotuhumiwa kufanya biashara hiyo.

"Watuhumiwa hawa wote watafikishwa mahakamani na jeshi letu litaendelea na msako wa kuwakamata makahaba wote jijini Dodoma, Waziri Mkuu Majaliwa ndiye balozi wetu wa kupinga maambukizi mapya ya Ukimwi,hivyo hatuwezi kuendelea kuwavumilia hawa watu," alisema Muroto.

Alisema kumekuwa na ongezeko la biashara hiyo kwa kasi, hivyo ni vyema watu wakachukua tahadhari kujiepusha na ongezeko la maambukizi ya ugonjwa huo.

Alisema kuwa watuhumiwa hao wote wamekamatwa katika msako uliofanywa na jeshi hilo katika maeneo mbalimbali. 

Alisema kuwa msako huo ulihusisha pia ukamataji wa mali za wizi na wapokea mali hizo pamoja na wavunjaji wa nyumba za watu na kuiba.

Katika tukio jingine, Muroto alisema wamekamatwa watuhumiwa sita na dawa za kulevya aina ya bangi misokoto 420 ya majani ya bangi, pamoja na kilo tatu za majani ya bangi kinyume cha sheria.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Christopher Edward (25), mkazi wa Chang'ombe, Hafidhu Mohamed (32), mkazi wa Ntyuka na Cosmas Ndalu, mkazi wa Maili Mbili. 

Pia walikamatwa watuhumiwa wengine watatu Asha Omary, mkazi wa Chamwino, Tatu Shabani na Ashirafu Hassan, wakazi wa Chang'ombe wakiwa na pombe haramu ya gongo.

Muroto aliongeza kuwa jeshi hilo limemkamata Mkazi wa Chamwino Msafiri Stephano (32) akiwa na mafuta aina ya dizeli lita 100 zinazodaiwa kuwa za wizi.

Katika tukio jingine wamekamatwa watuhumiwa saba kwa makosa ya kuvunja na kuiba wakiwa na mali za wizi mbalimbali 

Kadhalika, Muroto aliwataka wananchi wa mkoa huo katika kipindi hiki cha sikukuu kila mtu achukue tahadhali za kuhakikisha usalama katika maeneo yao.

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 46

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588 
ILIPOISHIA
“Kwani wenyeji wako ni kina nani?”
“Wapo kule juu”
Nilizungumza huku nikiwatazama Dany, Jojo na Camila sehemu walipo kaa.
“Sawa naomba uzungumze nao”
“Sawa jamani kwa herini”
Nikaondoka eneo hili huku wachezaji wakiwa wamejawa na furaha kunwa sana. Nikajimuika na wezangu huku nao wakionekana kunisifia hususani Dany. Tukaondoka katika eneo hili na kuelekea katika hoteli nyingine kwa ajili ya chakula cha usiku. Tukaagizia chakula tunacho kihitaji na baada ya muda muhudumu akatuletea chakula hicho. Moyo ukanistuka kwa mara nyingine mara baada ya kumuona mwanaume ambaye ameniuliza wazazi wangu katika taarifa ya habari, akiwa ni miongoni mwa wagombea walio tangaza nia ya kogombania kiti cha uraisi katika nchi hii ya Tanzania.

ENDELEA
Nikajikuta nikisimama kwenye kiti nilicho kikalia na  kuanza kutembea hadi hadi karibu na tv hii jambo lililo wafanya Camila na watu wengine kushangaa sana. Nikamtazama mwanaume huyu huku kifua changu kikiwa kimejawa na hasira kali sana.
“Ethna”
Nilistuka mara baada ya Camila kunishika begani mwangu. Nikamtazama usoni mwake huku nikishusha pumzi nyingi sana.
 
“Vipi mume wangu”
“Huyu mwanaume”
“Amefanyaje?”
“Ndio aliye niulia wazazi wangu”
Camila macho yakamtoka huku akijiziba mdomo wake kutoka na an mshanagao mkubwa ulio mpata.
“Kama kweli yupo hapa Tanzania lazima nami nimuue”
“Ethan zungumza kwa sauti ya chini kidogo si unajua kuna watu wengi”
Camila alizungumza huku akinishika mkono na kurudi tulipo  kuwa tumekaa.
“Vipi?”
Dany aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.
“Yule mwanaume pale ndio aliye niulia wazazi wangu”
Dany na Jojo wakastuka kidogo huku wakinitazama usoni mwangu.
 
“Unasema kweli?”
“Sina haja ya kuwaongopea, ninacho kizungumza ni kitu cha ukweli na ninamkumbuka vizuri sana”
Ukimya ukatawala huku Dany na Jojo wakiitazama taarifa hii ya habari. Sikuweza hata kuendelea kupata chakula hichi, nikanyanyuka na kuelekea sehemu ya maegesho ya magari.
‘Fu* Fu*”
Nilizungumza huku nikipiga piga tairi  la gari tulilo jia.
“Ethan utajiumiza mume wangu usiwe hivyo bwana”
Camila alizungumza huku akinikumbatia kwa nyuma.
“Najua una hasira mume wangu, ila nina kuomba sana mpenzi wangu uwe mvumili, tutahakikisha tunamfungulia mastka na atashtakiwa kwa mujibu wa sheria za nchi hii”
“Nchi hii, unahisi mtu ana nguvu  ya kwenda kugombania urahisi, unahisi atashtakiwa ehee?”
 
“Ethna”
“Sio Ethan Camila. Hii sio Ujerumani, huku ni barani Afrika. Bara la watu weusi, hakuna haki, mwenye nguvu ana nguvu na asiye na nguvu hato kuwa na nguvu mke wangu”
Nilizungumza huku nikimwagikwa na mchozi usoni mwangu.
“Sasa mume wangu unahitaji tufanye nini?”
“Nahitaji alipe kwa kila baya alilo lifanya juu ya maisha yangu na wazazi wangu”
“Nitahakikisha  mume wangu nina kuwa nawe bega kwa bega kuhakikisha kwamba una fanikiwa katika kazi yako hii ya kulipiza kisasi sawa mume wangu?”
 
“Nashukuru mke wangu”
Jojo na Camila wakatufwata sehemu tulipo na tukaondoka eneo hili. Ndani ya gari sikuzungumza kitu chochote hadi tukafika nyumbani.
“Ethan nahitaji kuzungumza nawe”
Dany alizungumza huku akishuka kwenye gari, nikaanza kumfwata hadi nyuma ya nyumba hii, akafungua geti kubwa na kuingia ndani ya ukumbi mkubwa sana ambao  umejaa vitu vingi, ikiwemo silaha kubwa kubwa ambazo sikuwahi kuziona kwenye maisha yangu.
“Kaa hapo”
Dany aliniambia huku akinionyesha moja ya kiti cha kuzunguka kilichomo pembeni ya meza kubwa. Nikaka kwenye hichi kiti huku naye akizunguka kwenye meza hii na kukaa kwenye kiti kingine. Dany akaminya minya batani ya laptop iliyopo mezani mwake kisha akanigeuzia.
 
“Ni huyu”
Dany alinionyesha picha ya mzee ambaye ameniulia wazazi wangu. Nikafumba macho kwa sekunde kadhaa kisha nikafumbua na kumtazama tena.
“Ndio ni yeye”
“Anaitwa Poul Mkumbo, kabila lake ni Mnyiramba. Ana uwezo wa asilimia sabini na tano ya kuwa raisi wa nchi hii na ana nguvu katika jamii  kwa maana alijitengenezea nafasi ya kugombania uraisi zaidi ya miaka kumi na mbili kwa sasa”
“Nitampataje?”
“Unahitaji kumuua?”
“Nahitaji alipe kwa yale yote ambayo amenitendea kwenye maisha yangu”
“Kulipa kupo kwa aina nyingi, moja ni kumuua je hiyo ya pili una hitaji kumfanya nini?”
“Kwanza nahitaji  ngome yak e aliyo ijenga kwa miaka yote hiyo kuiangusha na ninahitaji kurudisha kila kitu alicho kichukua kwa wazazi wangu ana kirudisha”
 
“Alichukua nin na nini?”
Kumbukumbu zangu zikanirudisha kipindi nipo na wazazi wangu katika shamba letu moja kubwa la migomba. Katika harakati za wazazi wangu kupalilia migomba hii huku nami nikiwa nina cheza cheza pembeni ya moja ya mgomba huku nikichimba chimba chini, nikaona jiwe moja kubwa kiasi likiwa ni tofauti kabisa na mawe ambayo nilisha wahi kuyaona kwenye maisha yangu. Nikamkimbilia baba yangu na kumuonyesha jiwe hili, baba na maam wakaanza kutazama jiwe hili na kuniuliza ni wapi nilipo litoa.
Nikawaonyesha sehemu ambayo tumelitoa jiwe hili, baba akaanza kuchimba katika eneo hili na kuona jiwe jengine linalo fanania na jiwe hili.
 
“Hii ni dhahabu”
Maneno ya baba niliyakumbuka vizuri sana huku  akiwa na furaha kubwa sana huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.
“Eneo hili lina dhahabu, hii ni mali mke wangu tumesha kuwa matajiri”
Baba aliendelea kuzungumza kwa furaha kubwa sana, kutokana hapa shambani si mbali sana na nyumbani, akaniagiza niweze kwenda  nyumbani kuleta moja ya kibegi ambacho hukitumia sana pale anapo kwenda mjini kuuza mikungu ya ndizi.
Kumbukumbu zangu zikazidi kusonga mbele hadi pale nilipo fika nyumbani, nikatafuta kibegi hicho, japo ilinichukua muda mwingi sana kuweza kuwapata, ila niliweza kufanikiwa kukiona. 
 
Nilipo rudi shambani, nikamkuta baba pamoja na mzee mmoja ambaye ni rafiki yake huku wakiwa wanachimba eneo hilo ambalo lina mawe haya ya dhabu. Nikakumbuka kibegi hicho kilijaa mawe hayo yanayo ng’aa sana na kururahisha unapo yatazama. Usiku wa siku hii ndipo tulipo vamiwa na kundi la vijana pamoja na mzee huyu bwana Mkumbo na hapo ndipo yalipo kuwa ni matatizo yangu na familia yangu.
“Utajiri wake mkubwa umetokea kwenye mgoni wa dhahabu huko Arusha ana umiliki”
Maneno ya Dany yakanistua sana na akaanza kunionyesha picha nyingine za mgodi mkubwa sana ambao unamilikiwa na bwana Mkumbo jambo ambalo limenifanya nizidi kuchanganyikiwa na kushikwa na hasira sana.
 
“Huu mgodi upo kwenye eneo ambalo ni mali ya wazazi wangu, ninahitaji kuuchukua”
“Hilo unalo lizungumza sio jambo rahisi sana”
“Nina akili na nina uwezo wa kufanya kila kitu na nitahakikisha kwamba ninafanikiwa”
“Etthan”
“Ninaomba unipatie taarifa zake na mali zake zote anazo zimiliki nitaanza kushuhulika na moja baada ya jingine”
“Unahisi njia hiyo unayo hitaji kuitumia ni sahihi kuweza kupata hizo mali?”
“Ndio”
“Sawa”
“Nitakapo hitaji msaada wako nitakujulisha na kesho nahitaji kwenda jijini Dar es Salaam, naamini huko ndipo nitakapo kwenda kufanya mipango yangu ili iweze kwenda”
“Dar es Salaam?”
“Ndio””
Dany akakaa kwa sekunde kadha kisha akatingisha kichwa ikiwa ni ishara ya kunikubalia kile nilicho muomba. Dany akafungua droo ya hii meza na kutoa moja ya simu na kunikabidhi.
 
“Utaitumia hii na ina kila aina ya habari za mgombea uraisi bwana Mkumbo. Utazipitia usiku kucha kisha kesho nitapanga safari ya wewe kuelekea jijini Dar es Salaam”
“Sawa”
Nikatoka ndani humu na kurudi chumbani kwangu na kumkuta Camila akiwa amekaa kitandani akinisubiria.
“Vipi kuna kitu gani kinacho endelea?”
“Nahitaji kupambana sasa”
“Kivipi mpenzi wangu?”
Nikaanza kumuelezea Camila juu ya mzee huyu. Nikamueleza na historia nzima ya maisha yangu na ya wazazi wangu, katika umri huu sasa ndipo nilipo weza kufahamu kwamba baba na mama yangu walikuwawa na mzee Poul Mkumbo kwa ajili mgodi wa madini.
“Kesho nitakwenda Dar es Salaam na wewe utabaki hapa sawa”
 
“Dar es Salaama unakwenda kufanyaje tena mume wangu”
“Nalianzisha hili swala, nitakuhitaji ubaki hapa sawa”
“Ethan hapana, siwezi kukuacha wewe uende peke yako. Kumbuka kwamba hili jambo  ni letu wote tafadhali mume wangu”
Camila alizungumza huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake.
“Hapana sihitaji nikuweke matatizoni Camila. Kumbuka kwamba hii vita ni yangu, wewe kaa kama silaha yangu ya siri, siwezi kuingia vitani na silaha zangu zote za maangamizi kwa maana mtu ambaye ninakwenda kupambana naye sifahamu ana uwezo gani, sijui ana weza kutumia nguvu gani na kumbuka ninakwenda kumuangusha raisi ambaye anakwenda kuingia madarakani huku nyuma akiwa na dhambi na damu za watu ambao amewapokonya haki zao. Umenielewa?”
 
Nilizungumza kwa msisitizo na kumfanya Camila kukaa kimya huku akiendelea kumwagikwa na machozi usoni mwake.
“Nakupenda Camila nakuhitaji mke wangu. Ila acha nifanye hii kazi. Nina muda mfupi sana ila nakuomba mpenzi wangu unielewe sawa”
Camila akajibu kwa kutingisha kichwa akimaanisha  kwamba amenielewa kile nilicho mueleza.
“Nitakujulisha kila kila kitu ambacho kitakuwa kinaendelea katika katika kazi yangu sawa”
“Nimekuelewa mume wangu”
Tukakumbatiana na Camila kwa nguvu sana huku kila mmoja akiwa amejawa na huzuni pamoja na uchungu mwingi sana. Usiku huu, tukapeana penzi zito kana kwamba hatuto peana tena kwenye maisha yetu ya baadae.
                                                                                                                        ***
Tukaanza safari ya kuelekea jijini Dar es Salaam, tukiwa tumeongozana na Jojo, huku Dany akimsisitizia Jojo aweze kunilinda kwa kila namna. Safari ya kufika jijini Dar es Salaam ikatuchukua takribani masaa saba kwani nakumbuka ni sehemu moja tu ndio tulisimama ili kuweza kupata chakula cha mchana. Tukafika katika hoteli moja ya kifahari yenye hadhi ya nyota tano, Serena Hotel. Nikawasiliana na Camila na kumueleza kwamba tayari nimesha fika jijini Dar es Salaam na akanitakia kila la heri katika kuhakikisha kwamba nina ianzisha vita yangu ambayo haito mwaga damu ila itajaa uchugu na mateso makubwa sana kwa mzee Poul Mkumbo.
“Nakusikiliza Ethan, mpango wako wa kwanza ni upi?”
Camila aliniuliza huku akiwa ameweka nne kwenye sofa alilo kalia ndani ya chumba hichi tulicho fikizia.
 
“Katika meelezo nimeona mzee huyu ana mtoto wake wa kike na anafanya kazi katika shirika moja la simu si ndio?”
“Ndio”
“Nahitaji kuanza na huyo mwanaye wa kike”
“Unataka kumteka au kumfanya nini?”
“Ndio ninahitaji kumteka hisia zake, kupitia yeye nitaweza kuingia ndani kabisa katika familia ya mzee Mkumbo”
“Mmmm ni wazo zuri ila je umemuelewesha Camila juu ya jambo hili, isije tukapigana vita ambayo itaturudia sisi wenyewe?”
“Anaelewa kila kitu na nilisha muelez akia aina ya mbinu ambayo ninakwenda kuitumia kuifanya. Kikubwa ni kuhakikisha tunamuangusha mzee huyu”
“Sawa kama ni hivyo basi kila kitu kina wezekana”
“Nitahitaji kufahamu kwa sasa biti huyo yupo wapi ili tujue ni nini anacho kipanga”
“Sawa”
Jojo akafungua laptop tuliyo kuja nayo na kuanza kumtafuta binti huyo kupitia mtandao. 
 
“Sasa hivi namuona hapa anaelekea katika jengo la kibiashara Mlimani City”
“Ndio wapi?”
“Utafadhamu kama ukiamua twende”
“Sawa, linalo wezekana hivi sasa lisingoje baadae”
“Poa, je nibadilishe mavazi haya au?”
Nikamtazama Jojo jinsi alivyo vaa gauni lake refu lililo mpendeza.
“Una suti yoyote labda ulio kuja nayo?”
“Ndio”
“Vaa hiyo basi”
Camila akavaa suti nyeusi iliyo mfanya dhairi aonekane ni mlinzi wangu. Nikavaa koti langu la suti nililo livua muda nilipo kuwa tuna ingia ndani humu. 

Tukapanda kwenye gari letu tulilo kuja nalo aina ya BMW X6, nikakaa siti ya nyuma huku Jojo akiwa amekaa siti ya mbele kama dereva na nywele zake ndevu akiwa amezibana kwa nyuma huku baadhi ya nywele akiwa ameziachia eneo la usoni mwake na kufunika jicho lake la upande wa kulia. 

Nikaitazama hii saa ya dhahabu aliyo nikabidhi Dany asubuhi, kwa haraka haraka mtu akinitazama ni lazima atagundua kwamba mimi ni kijana mwenye pesa zangu tena sio chache ni nyingi sana. Nikaanza kupitia sura ya binti huyu wa Poul Mkumbo, ni binti mzuri kwa kukadiria ana umri kama miaka ishirini na tano au na kuendelea hivi, ila kutokana Mungu amenipa umbo kubwa kiasi sio rahisi kunidhania kwamba mimi ni kijana wa miaka kumi na nane. 
 
Tukafika katika jengo la kibiashara la Mlimani City. Jojo akashuka kwenye gari na kunifungulia mlango wa siti ya nyuma ya gar hili,i kisha tukaanza kutembea kuelekea ndani ya jengo hili, kabla ya kufika katika mlango mkubwa wa kuingia ndani ya jengo hili, tukamuona binti wa Poul Mkumbo akitoka huku akiwa ameongozana na walinzi wanne huku wawili wakiwa ni wa kiume huku wengine wawili ni wakike. Wakihakikisha wana mpa ulinzi mkubwa msichana huyu asiweze kusogelewa na mtu wa aina yoyote ile.

ITAENDELEA KESHO
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images