Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Disemba 16


Jipatie Dawa ya Asili ya Kupunguza Maziwa, Kupunguza Tumbo,Kuongeza Unene, Kuongeza Maumbile ya Kiume na Kuondoa Chunusi

$
0
0
NATURAL BEAUTY PROD.
🍋🥑🍒OFFER ya X MAS na MWAKA MPYA🍉🍇

 Ofa hii itaisha tareh. 22/12/2018 wahi sasa jipatie bidhaa original kwa punguzo la bei.

 %%Bidhaa hizi zimetengenezwa kwa mimea na matunda hazina chemical wala madhara yoyote kwa mtumiaji.             Ukinunua bidhaa kuanzia mbili utapatiwa offer ya bidhaaa nyingine yoyote uipendayo wewe bureeee.

1. SHARK POWER--Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza maumbile ya kiume urefu na upana mpaka nchi 7.5 ilikua inapatikana kwa @170,000/= sasa ni @160,000/= tu

2. VIGA 84000---Hii dawa ya kuspray yenye uwezo mkubwa wa kuchelewesha wakati wa tendo la ndoa ilikua ni  @160,000/=. Sasa ni 150,000/= tu

3. HANDSOME UP ORIGINAL-- Hichi ni kifaa cha kuongeza maumbile kwa size uipendayo wewe pamoja na kuimalisha misuli kifaa hichi kilikua kinapatikana kwa @230,000/=. Sasa ni 210,000/= tu

4. MAXMAN CAPSULE--- Hii ni dawa ya vidonge ya kuongeza maumbile ya kiume urefu na upana pamoja na kuongeza nguvu za kiume kwa wiki mbili ilikua inapatikana kwa @200,000/=. Sasa ni 180,000/= tu

5. VIG RX---- Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza uume urefu na upana mpaka nchi 10 ilikua inapatikana kwa @190,000/=. Bei ya sasa ni 170,000/=

6. BODY BOOSTER---Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri ilikua inapatikana kwa @150,000/=. Sasa ni 140,000/=

7. BOTCHO MULT PLUS-- Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza (hips mapaja na makalio) kwa size uipendayo ilikua inapatikana kwa @200,000/=. Sasa ni 180,000/=

8. WHITE COLLECTION---- Ni vidonge vya kuwa mweupe mwili mzima pamoja na kuwa soft ilikua inapatikana kwa @150,000/= Sasa ni @140,000/= tu

9. BOTCHO HOLOGRAM CREAM--- Hii ni dawa ya kuongeza hips na makalio ilikua inapatikana kwa@180,000/= Sasa ni@160,000/=       

N.K

Wasiliana nasi kwa simu

NO:. +255 759029968  AU +255 659618585

Popote ulipo utapata huduma zetu.

Pia hakikisha unapatiwa risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ununuapo bidhaa kampuni hii.

WELCOME ALL

Waziri wa Kilimo: Bilioni 133.2 Zimekwishalipwa Kwa Wakulima Wa Korosho

$
0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Mtwara
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) amesema kuwa mpaka kufikia jana tarehe 14 Disemba 2018 wakulima 130,163 wamelipwa jumla ya shilingi 133,259,933.855

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga ametoa takwimu hizo tarehe 15 Disemba 2018 wakati akizungumza kwenye mkutano wa wabanguaji uliofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.

Alisema kuwa katika Mkoa wa Mtwara wananchi ambao wamekwishalipwa ni 77,055 huku jumla ya fedha iliyolipwa ni Bilioni 80,098,982,060 

Katika mkoa wa Lindi tayari wakulima 41,564 wamekwishalipwa kiasi cha Bilioni 42,502,635,227 huku katika mkoa wa Ruvuma wakulima 11,463 wamekwishalipwa kiasi cha Bilioni 10,557,222,943

Aidha, Mhe Hasunga amesema kuwa katika mkoa wa Pwani Milioni 101,091,960 zimekwishalipwa kwa wakulima 81

Alisisitiza kuwa vyama vilivyohakikiwa ni 461 na vilivyolipwa ni 451, ambapo jumla ya Kilo 40,381,798

MWISHO

Msekwa Awajibu Waliponda Baada ya Kuteuliwa na Rais Magufuli Kuwa Mkuu wa Chuo MUST

$
0
0
Spika wa  Bunge Mstaafu, Pius Msekwa amesema uteuzi wake wa kuwa mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia (MUST) uliofanywa na Rais John Magufuli Desemba 6 ,2018 hakukosea na kwamba anatambua utendaji wake na uzoefu alionao kwa kuongoza baadhi ya vyuo vikuu nchini Tanzania kikiwapo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udsm).

Alisema hayo jana Jumamosi Desemba 15, 2018 alipokuwa akizungumza katika mahafali ya sita ya chuo hicho, ambapo alikuwa kivutio kutokana na staili yake ya kutumia vifungu vya biblia na kutoa mifano ya namna alivyokuwa akiliendesha Bunge.

"Kwanza kuna kila sababu ya kumshukuru Rais kwa kuniona mimi nafaa kuvaa kiatu hiki kwani kuna watu wengi serikalini lakini kaona mimi ndiye sahihi zaidi, nitaitumia fursa hii kuboresha elimu ya sayansi na teknolojia sambamba na kuongeza udahili kwa mwaka 2019/2020," alisema.

Msekwa alisema kupitia nafasi hiyo atahakikisha chuo hicho kinakuwa chachu ya kuzalisha wataalamu wa nyanja mbalimbali na kwamba amekuwa na bahati ya kuteuliwa kwa awamu ya tatu sasa kuongoza vyuo vikuu nchini.

Naye mwenyekiti wa baraza la chuo hicho, Zakia Meghji alishauri uongozi wa chuo hicho kufanya tafiti katika nyanja mbalimba ili kuchochea maendeleo ya uchumi wa viwanda.

Alisema mafanikio ya chuo hicho yanatokana na jitihada za Serikali kutatua changamoto zinapojitokeza.

Makamu mkuu wa chuo hicho, Profesa Joseph Msambichaka alisema wana mikakati ya kuanzisha mfuko kwa ajili ya kusomesha wanafunzi wa  kike sambamba na kujenga maabara ya kisasa itakayochukua wanafunzi 2,000 kwa wakati mmoja.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

Wimbo Mpya: Alicios - Christmas Njema

$
0
0
Wimbo Mpya: Alicios - Christmas Njema

Kagame Apangua Tuhuma za Rwanda Kutaka Kuipindua Serikali ya Burundi

$
0
0
Rais Paul Kagame amesema nchi yake haitajiingiza katika kile alichoelezea kuwa ni uchokozi unaofanywa na Burundi na akaongeza kwamba kufanya hivyo ni "kuwapa kile wanachotaka."

"Tumekuwa na aina zote za uchokozi kutoka Burundi na hatujaangukia ndani. Kadhalika hatujahangaishwa na aina hizo za uchokozi kwa sababu hiyo itakuwa kuwapa kile wanachotaka, kuthibitisha hoja yao kwamba hawana tatizo jingine lolote isipokuwa Rwanda," amenukuliwa Kagame akiwaambia waandishi wa habari kando ya mkutano wa Majadiliano ya Kitaifa ya 2018.

Katika taarifa iliyochapishwa kwenye Twitter rasmi ya Rais wa Rwanda, Kagame aliwaambia waandishi wa habari kwamba Rwanda ilijiunga katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa hiari.

"Kwa Rwanda kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki ilikuwa hiari yetu lakini pia ilikuwa haki yetu. Haikuwa juu ya mtu yeyote kutufanyia upendeleo. Tulipojiunga na EAC hatukupiga magoti, kuwainamia watu watupatie upendeleo. Jitihada zozote za mtangamano zinahitaji kanuni ya toa na chukua. Kila nchi ina mamlaka huru lakini unapochagua ushirikiano, unaelewa kwamba baadhi ya mambo yatasitishwa. Watu wanakuja pamoja na kuunda kitu ambacho ni kikubwa zaidi kuliko mamlaka huru ya kila taasisi," alisema.

Kauli ya Kagame imekuja saa kadhaa baada ya kuchapishwa taarifa kwamba Rais Yoweri Museveni wa Uganda na mwenzake wa Burundi Pierre Nkurunziza, katika kipindi cha wiki moja, walitumiana barua zenye maneno makali zikionyesha wazi mgawanyiko unaotokota kati ya nchi za wanachama wa EAC.

Katika barua ya Desemba 4, 2018 kwa Museveni kama mwenyekiti wa sasa wa EAC, Rais Nkrunziza aliomba uitishwe mkutano wa dharura wa viongozi wa kikanda kutatua kile alichokiita "uvamizi" wa Rwanda dhidi ya nchi yake.

"Mbali na ukweli kwamba Rwanda iliandaa na kusimamia mapinduzi ya serikali ya mwaka 2015, wahusika wa uhalifu na wahalifu wengine wameweka makazi huko Rwanda ambako wanapata msaada wa kushambulia Burundi, kuvuka mpaka wa Rwanda-Burundi au kupitia mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, pamoja na kupata msaada na hati za kusafiria ili kuwawezesha kuzunguka katika ukanda huu na hata Ulaya," aliandika Nkurunziza.

Hata hivyo, Kagame alibainisha kuwa Rwanda ndiyo imekuwa ikikabiliwa na uvamizi kutoka nchi za jirani.

Wimbo Mpya: Nikki wa Pili - Massage

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Nikki wa Pili kutoka kundi la Weusi ameachia wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Massage. Usikilize hapa.

Mambo Yamekamilika....Wataalamu Kuzifuata Ndege Zetu za Airbus 220-300 Canada Muda Wowote Kuanzia Sasa

$
0
0
Ndege mbili mpya aina ya Airbus 220-300 zilizotegemea kuwasili nchini Desemba mwaka huu, moja imeshakamilika na kufanyiwa majaribio ya kuruka, ambayo yameleta matokeo mazuri.

Kinachosubiriwa sasa ni timu ya makabidhiano kutoka Tanzania kufika Canada kwa ajili ya kuzipokea na kuzileta. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), Ladslaus Matindi alisema siku chache zilizopita ndege moja kati ya hizo mbili, ilifanya majaribio ya kuruka na kuleta matokea mazuri, hivyo kinachosubiriwa ni timu ya makabidhiano kuwasili nchini humo.

“Ndege mpya mbili tunazotarajia kuzipokea hivi karibuni, moja tumepata maendeleo yake imefanyiwa majaribio ya kuruka juzi na matokeo ni mazuri sana, timu ya wataalamu wetu inaondoka wiki ijayo kwenda Canada kwa ajili ya makabidhiano na kuzileta,”alisema Matindi.

Aliongeza, ndege ya pili nayo iko kwenye hatua za mwisho za uundwaji na iko vizuri na kwamba timu ya wataalamu kutoka Tanzania, ilishawasili nchini humo kwa ajili ua ukaguzi na kutoa ripoti yao ya maendeleo ya ndege hizo.

Matindi alisema baada ya ndege ya kwanza kuwa tayari, timu hiyo wataalamu na makabidhiano, itasubiri ndege ya pili ifanyiwe majaribio, kisha kuangalia vitu vyote kama viko sawa na hatua ya mwisho ni kuzisafirisha kuja nchini.

Akizungumzia ndege hizo, ambazo awali zilipaswa kuwa tayari na kuwasili nchini Novemba mwaka huu, Matindi alisema walipokea maombi kutoka kwa watengenezaji wa ndege hizo, kampuni ya Airbus nchini Canada ya kusogeza mbele tarehe ya kuzikabidhi ili kumalizia mambo madogo ya matengenezo yaliyosalia.

 “Ni kweli awali tulikuwa tuzipokee ndege hizo Novemba mwaka huu, lakini watengenezaji wametuomba na ni kitu cha kawaida, kusogeza mbele muda wa kuzikabidhi ili tuzipokee wakati wowote kuanzia sasa,”alisema Matindi.

Ndege hizo mbili kila moja ina uwezo wa kubeba abiria 132, ambapo daraja la kwanza ni abiria 12 na daraja la kawaida ni abiria 120. 

Awali, ndege hizo zilijulikana kwa jina la Bombardier C Series, na Julai mwaka huu kampuni ya Airbus iliingia mkataba wa ununuzi na kuzibadilisha jina na kuziita A220-100/300 .

Kutana Na Dr Chikago Bingwa Na Mwokozi Kwa Waliosumbuka Na Magonjwa Bila Mafanikio

$
0
0
Ninauwezo wa kumrudisha mume, mke ,mchumba, hawara, mtu unaempenda ndani ya masaa mawili tu (2) na kumfunga asiwe na mtu mwingine zaidi yako na kumfanya akutimizie kilakitu unachokihitaji kutoka kwake hata km yupo mbali na atatulia kabisa

GALIMBO 3 MIX;  nidawa ya mitishamba iliyitengenezwa kwa kwa utabibu wa hali ya juu kwakuchanganya miti na matundatiba , Huogeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15 -85 ) , inakomaza zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakat wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaid ya Mara tatu bila ham kuisha wara kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-40.

YOLANI :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inch (6-8) na unene wa sm (3-4)

Matatizo haya husababishwa na mambo mbalimbali km upigaji wa punyeto, kisukali,  vidonda vya tumbo, tumbo kuunguluma na kujaa gesi, ngili, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani, maumivu ya mgongo ama kiuno, namengineyo mengi  (nk )

SUPER MBUKE :- nidawa inayotatua tatizo la kisukali na kupona kabisa Kwa mda mfupi sana na utakuwa na uwezo wakula chakula chochote chenye sukali baada ya kupona,

vilevile ninadawa ya uzazi kwa akina Mama na akina Baba, kurudisha mali iliyopotea kwamda mfupi sana, vidonda vya tumbo, kaswende,presha,chango la uzazi, gono,nyama uzembe, kusafisha nyota, kuzuia majini wachafu, kinga ya mwili, kuuza vitu bila kununuliwa, dawa za biashara, pesa nyingi (utajili)  mambo ya kes nk

Kwa huduma n msaada wasiliana na Dr CHIKAGO atakusaidia hatakama ulikata tamaa utarudisha furaha yako

Napatikana Dar es salaam  sm no 0743543944   /0620510598

Nb :km huna nafasi ya kufika ofisin huduma hii itakufikia popote ulipo kwawatu wa mkoani tunatuma kwanjia ya mabasi.

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 45

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588 
ILIPOISHIA

Jojo akatufwata hapa tulipo simama huku akiwa na sura ya tabasamu.
“Ethan”           
“Mmmm”
“Huna kumbukumbu yoyote na wazazi wako?”
“Ndio”
“Unahitaji kufahamu ni kitu gani kilicho wapata?”
“Ndio”
Jojo akanisogelea na kunishika kichwani mwangu, nikahisi ubaridi mkali ambao taratibu katika ufahamu wangu wa akili nikaanza kuona ngurumo za radi huku mvua nyingi ikinyesha. Kumbukumbu zangu zikazidi kusonga mbele na kumuona mzee mmoja akiwa amezungukwa na kundi kubwa la vijana huku  wakimshambulia kwa kumpiga kwa magongo pamoja na mateke huku wakihitaji afariki dunia.

ENDELEA
Nikamuona mama yangu akiwa amejificha kwenye migomba pamoja nami huku akilia. Radi iliyo piga yenye mwanga mkubwa, ikanifanya niweze kumuona mwanaume mmoja ambaye baada ya kuiona sura yake nikajikuta nikistuka sana.
“Vipi?”
Dany aliniuliza hukua kinitazama usoni mwangu. Nikashindwa kulijibu swali lake kwani mapigo yangu ya moyo yananienda kasi huku jasho likinimwagika usoni mwangu.
“Kuna nini kinacho endelea hapa”
Camila alizungumza mara baada ya kufika hapa tulupo simama. Nikawatazama watu wote hawa kisha nikaondoka na kuanza kuelekea kwenye gari tulipo liacha.
“Ethan, Ethan”
Camila aliniita, sikuweza kumuita zaidi ya kuzidi kusonga mbele. Nikajaribu kufungua mlango wa gari ila haukufunguka.
“Ethna mume wangu kuna kitu gani kinacho endelea?”
Camila alizungumza huku akinishika mkono.
“Nimemuona”
“Umemuoan nani?”
“Mtu aliye niulia baba na mama yangu”
Camila macho yakamtoka kwa maana hakuamini kama ninaweza kukumbuka  vitu hivi kwa muda huu.
“Ni nani?”
 
“Simfahamu jina lake, ila nimeikumbuka sura yake”
“Ohoo jamani mpenzi wangu, tulia kidogo”
Camila alizungumza huku akinikumbatia mwilini mwangu. Dany na Jojo wakanifwata sehemu hii tulipo simama.
“Ethan umeona nini?”
Jojo aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.
“Nimemuona mtu aliye niulia baba na mama yangu”
“Una uhakika?”
“Ndio”
“Twendeni ndani jamani”
Dany alishauri na kutufanya mimi na Jojo kumtazama. Dany akaanza kuongoza kuelekea ndani, nasi tukaanza kumfwata kwa nyuma. Tukaelekea eneo lenye kiwanja kikubwa cha mpira. Tukakutatimu ya vijana chini ya miaka kumi na nane wakifanya mazoezi katika eneo hili. Baadhi ya watu nao wamejumuika katika kuitazama timu hii. Tukakaa katika moja ya sehemu ambayo tunaweza kuona mazoezi yao vizuri sana.
“Ethan”
“Naam”
“Mtu huyo anafananiaje?”
Nikamtazama Jojo huku nikijaribu kuvuta kumbukumbu yake, kitu kilicho nishangaza, sikuweza kuipata kumbukumbu yake tena.
 
“Mbona simkumbuki”
“Humkumbuki?”
“Ndio”
“Ngoja”
Jojo alizungumza huku akinishika kichwani mwangu, nikaanza kuoana jinsi mwanaume huyo alivyo toa amri ya sisi kukimbizwa pamoja na mama yangu. Mama akajitahidi kukimbia kwa kuchechemea huku akiniongelesha kwa lugha ya kichaga kwamba tukimbie. Kutokana na utoto wangu nikakimbia hadi kwenye migomba mingi ila nikashindwa kuendelea na kukimbia, nikarudi sehemu alipo mama yangu na kukuta akitaka kubakwa na vijana walio kuwa akitukimbiza. Vijana wawili wakaninyanyua juu juu na kunipeleka hadi kwenye korongo. Kitendo cha kujigonga kichwa changu kwenye jabali nikakurupuka tena huku nikishika kichwa changu upende ambao nilijibamiza kwenye korongo.
 
“Vipi umeona nini?”
Nikashusha pumzi taratibu huku nikimtazama Jojo usoni mwake.
“Nimeona jinsi mama alivyo kuwa akibakwa na mimi nikapigwa na kusukumia kwenye korongo”
“Hujamuona tena huyo mtu?”
“Hapana”
“Ukimuona picha je utamkumbuka?”
“Nahisi, ila kumuelezea kwamba yupo vipi siwezi kwa kweli”
“Chukua muda wa kutosha ukimkumbuka basi utanifahamisha sawa”
“Sawa”
Camila akanisogelea karibu yangu na kunishika mkono wangu na kukiegemesha kichwa chake karibu yangu.
“Unajisikiaje mume wangu?”
 
“Sasa nimejitambua mimi ni nani?”
“Kivipi?”
“Jina langu sio Ethan mpenzi wangu”
“Mmmmmm?”
“Yaa jina langu sio Ethan, jina hilo nimepewa ila sio lile nililo pewa na wazazi wangu”
Camila akabaki akiwa na mshangao mkubwa sana huku akinitazama usoni mwangu.
“Jina lako halisi ni lipi?”
“Naitwa LOLE, hilo ndio jina langu katika kabila langu la Kichaga”
“Wachaga ni watu wa wapi?”
“Moshi”
Camila akaka kimya huku akinitazama usoni mwangu akionekana kutafakari haya mambo niliyo mueleza.
“Lole sinto kuita Ethan tena sawa mume wangu?”
“Nashukuru mke wangu”
Nikamkumbatia taratibu Camila, tukaendelea kutazama mazoezi ya wachezaji hawa, japo wana kocha ila yamejaa udhaifu mkubwa sana.
“Natamani nikawaelekeze kidogo mke wangu”
“Mazoezi!?”
 
“Ndio”
“Ohoo mume wangu wasije wakahitaji kukuchukua, kumbuka mambo yaliyo tutokea Ujerumani”
“Nawaelekeza kidogo, kidogo tu”
“Mmmm haya”
Nikamuachia Camila na kuanza kushuka ngazi na kuelekea uwanjani. Walinzi wanao linda wachezaji  hawa wakanizuia kuingia.
“Samahani kuna machache nahitaji kuzungumza na kocha, tafadhali ninaomba munisaidie katikahilo”
Mmlinzi mmoja akanikazia macho sana, kisha baada ya muda kidogo akatabasamu.
“Kama sijakosea wewe ni Ethan Klopp?”
“Yaa ndio mimi”
“Pita pita”
Mlinzi huyo alizungumza kwa furaha kubwa sana na kuwafaya wezake nao wajawe na furaha kwa maana hapo awali hawakuweza kunifahamu. Nikafika katika sehemu walipo simama makocha wawili mmoja akiwa ni kocha wa kizungu. Nikasalimiana nao kwa heshima sana, kwa bahati nzuri wakaweza kunifahamu kwa haraka sana.
 
“Ohoo Ethan upo Tanzania?”
Kocha huyu wa kizungu alizungumza huku akiwa amejawa na mshangao sana.
“Ndio nina siku ya pili sasa japo nimekuja Tanzania kwa siri sana”
“Ohoo karibu sana yaani nilikuwa ninatamani sana kukuita kwenye kikosi changu ila sikuweza kufahamu ni wapi nitakupata”
“Nimekuja kwenye mapumziko mafupi, ila nitaandoka”
“Oohoo sasa unataka kuniambia kwamba huto kuwepo kwenye fainali zinazo endelea Ujerumani?”
“Yaa sinto kuwepo kwenye kikosi, naamini kama ni mfwatiliaji wa mambo utaweza kugundua ni kitu gani ambacho kimetokea kwenye wiki za hivi karibuni”
“Yaa nafwatilia”
 
“Ndio maana nipo hapa. Kuna mambo kadhaa ambayo naomba niweze kuwaelekeza timu yako. Nimekaa juu kule nikaona mapungufu kadhaa. Sijui unaweza kunipa nafasi japo dakika kumi na tano nikafundisha vijana wako”
“Kwa nini usiingie ukacheza ndani?”
“Hapana, labda siku nyingine, ila leo nahitaji kutoa maelekezo madogo madogo ili tumu iwe vizuri”
“Sawa darasa ni lako”
Kocha akapiga  filimbi na wachezaji wote wakakusanyika sehemu tulipo simama sisi. Nikasalimiana na wachezaji hawa ambao nao wakaonekana kufurahi sana kwangu.
“Mimi ni Mtanzania kama nyinyi tena ni mchaka. Hivyo naomba musiwe na ile hali ya kuhisi labda mimi ni mtu maarufu au nimetokea Ujerumani, hivyo mukajihisi unyonge kwenye mioyo yao. Mimi sifahamu mengi sana kwenye mpira, ila kwa yale machache niliyo nayo, nimeona ni vyema tukabadilisha yote katika yote ni kuweza kuijenga timu yetu si ndio”
 
“Ndio ndio”
Nikaanza kuwapa mbinu washambuliaji pale wanapo kuwa uwanjani. Nikagawa timu hii mara mbili kisha nikasimama kama refarii. Wakaanza kucheza mpira kama vile nilivyo walekeza, ndani ya dakika kumi thelathini, wakacheza kwa kiwango cha hali ya juu hadi watu hawa walio kuja kushuhudia mazoezi haya wakaanza kushangilia kana kwamba wanatazama mechi ya wapinzani. Kutokana tayari imesha kuwa jioni, nikapiga kipenga cha kumaliza mpira huu. Kila mchezaji akanifwata na kunipa pongezi kwa maelezo mazuri ambayo nimewapa.
“Kwa nini usibaki na sisi ukawa mchezaji?”
Mchezaji mmoja alizungumza huku tukiwa tunatembea kutoka uwanjani hapa.
“Hapana rafiki yangu kila jambo linawakati wake, wakati wangu wa kucheza hapa Tanzania ukifika basi nitacheza”
“Sawa, ila hakika wewe ni kocha bora kwa kweli, yaani huyu mzungu hapa anakula pesa za serikali yaani anatufundisha kawaida sana”
 
“Ngoja niwaambie kitu kimoja”
“Kitu gani?”
“Siri ya kuwa timu bora sio kocha. Nyinyi wachezaji munatakiwa kuwa upande kati yenu na mujue kwamba nyinyi ni kama familia ya baba mmoja. Mukipambana hakikisheni kwamba munapambana kama familia, musiangalie eti yule ana uwezo au yule hana uwezo. Mukishikamana hakika kocha yeye kazi yake itakuwa ni kusimama tu nje ya uwanja, ila nyinyi mutajua ni nini munafanya”
“Kweli kaka unacho zungumza ni kitu cha kweli kabisa. Unajua tatizo letu sisi huwa tumetolewa kila mtu kwenye timu yake hivyo tukikuatana hapa utakuta huyu  anacheza hivi huyu anacheza hivi yaani ni tabu tu?”
“Hiyo sio sababu ya maana. Muna muda gani toka muweke kambi?”
“Leo siku ya tatu?”
“Katika masaa mawili nyuma mulikuwa muna chezaje?”
“Kawaida?”
 
“Sasa toeni ukawaida, hakikisheni kwamba munacheza kwa kujituma na upendo, acheni kuweka matabaka. Kapteni ni nani?”
“Ni mimi”
“Ohoo kumbe nipo na timu kapteni. Sasa wewe ndio wa kuyafanyia kazi kama vile nilivyo kuelekeza sawa kaka”
“Sawa”
Tukafika sehemu walipo makocha hawa wawili, tukakusanyika kwa pamoja.
“Jamani mumeona mulicho cheza leo. Sasa nataka iwe hivi hivi kwenye mashindano ya kombe la dunia ambayo tunaiendea”
Kocha alizungumza huku akiwa amejawa na furaha sana. Wakanipongeza sana huku wakiniomba kesho niweze kurejea ili nizidi kuungana na makocha hawa katika kuhakikisha tunakinoa kikosi hichi cha vijana.
“Nitazungumza na wenyeji wangu kama wataniruhusu kufika hapa kila siku”
“Kwani wenyeji wako ni kina nani?”
“Wapo kule juu”
Nilizungumza huku nikiwatazama Dany, Jojo na Camila sehemu walipo kaa.
 
“Sawa naomba uzungumze nao”
“Sawa jamani kwa herini”
Nikaondoka eneo hili huku wachezaji wakiwa wamejawa na furaha kunwa sana. Nikajimuika na wezangu huku nao wakionekana kunisifia hususani Dany. Tukaondoka katika eneo hili na kuelekea katika hoteli nyingine kwa ajili ya chakula cha usiku. Tukaagizia chakula tunacho kihitaji na baada ya muda muhudumu akatuletea chakula hicho. Moyo ukanistuka kwa mara nyingine mara baada ya kumuona mwanaume ambaye ameniuliza wazazi wangu katika taarifa ya habari, akiwa ni miongoni mwa wagombea walio tangaza nia ya kogombania kiti cha uraisi katika nchi hii ya Tanzania.

ITAENDELEA KESHO

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

$
0
0

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara, Msanii wa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo Dawa na PETE za Bahati zenye uwezo mkubwa wa kuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.

Kutana na Sheikh Jumaa Bilal. Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki. 

Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. Sheikh Jumaa Bilal ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA-  Sheikh Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na Nje ya nchi.

Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nayasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.

Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudishaa alipote, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMBA, GARI..), Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali na UTAJIRI bila masharti na mengine mengi ya Siri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET)

*{لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّهُ بِاللَّغْوِ فِي أيْمَانِكُمْ وَلَٰكِنْ يُؤَاخِذُكُمْ بِمَا عَقَّدْتُمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِمَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ }* ﴿٨٩﴾

✨Wabillahhi Tawfiq Asallam  Alaikum

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa
nambari ya simu

+255 688 745 790
+255 672 861 042
Whatsapp :  0762 252 102

Serikali Yasitisha Ajira za wahudumu wa afya ngazi ya jamii

$
0
0
Serikali imesema imesitisha kuajiri wahudumu wa afya ngazi ya jamii kupitia mradi wa Global Fund na badala yake inaelekeza nguvu kuajiri watumishi kwenye sekta ya afya.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tamisemi, Josephat Kandege alisema hayo baada ya kuwapo kwa barua inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii inayotoka Tamisemi ikielekezwa kwa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Mbeya na Chunya, ikimtaka kusitisha ajira hizo.

Kandege alisema Wizara ya Afya inajenga vituo vya afya na zahanati nyingi vijijini na mijini, hivyo ina uhitaji mkubwa wa wahudumu wa afya.

“Tukiwaajiri wahudumu wa afya ngazi ya jamii huku zahanati na vituo vya afya tulivyojenga vina ubora na uwezo wa kutoa huduma kubwa ikiwamo upasuaji, ina maana tulichofanya itakuwa kazi bure,” alisema
 
Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Chunya mkoani Mbeya, Sophia Kumbuli alisema kulikuwa na mchakato unaendelea wa kutaka kuajiri watu wa kada hiyo, lakini suala la kusitishwa hana taarifa nalo.

Barabara ya Morogoro kwenda Dodoma kujengwa upya

$
0
0
Barabara ya Morogoro-Dodoma yenye urefu wa Kilomita 259 inasanifiwa upya ili ijengwa kwa viwango vya ubora unaoendana na mahitaji ya sasa.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa amesema mpango huo unafanywa katika mwaka wa fedha 2018/19 na mara baada ya usanifu kumalizika watapa michoro na kufahamu gharama halisi za ujenzi.

Naibu Waziri alisema hayo hivi karibuni mjini Morogoro alipofanya ziara ya ukaguzi wa matengenezo ya barabara katika maeneo mbalimbali kutoka Dodoma hadi Moropgoro yakiwemo ya Kibaigwa, Gairo na kuangalia shughuli za ujenzi wa mizani mpya ya kisasa eneo la Dakawa Magereza barabara ya Morogoro- Dodoma.

Alisema licha ya kuendelea kuihudumia barabara hiyo kuu serikali imekuja na mpango mwingine wa kufanya usanifu kwa mwaka wa fedha wa 2018/19 ili kupata michoro ambayo itaelezea gharama halisi ya kujenga barabara mpya katika kiwango cha ubora na mahitaji ya sasa.

Kwandikwa alisema serikali imekuwa ikitenga fedha nyingi kila mwaka kwa ajili ya ukarabati wa barabara kuu mbalimbali ikiwemo hiyo ya Morogoro-Dodoma ili ziweze kutoa huduma za usafirishaji wa abiria na mizigo na kwamba babrabara hiyo ni ya zamani kwani imejengwa zaidi ya miaka 30 iliyopita na sasa imechakaa na kuzeeka.

Makanga 3 Power, Dawa Bora Za Nguvu Za Kiume

$
0
0

Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.

Tupo dar es salam Buguruni

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348.

Serikali Yatoa Waraka MPYA wa kukariri darasa kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari nchini

$
0
0
Serikali imetoa waraka unaoelekeza utaratibu mpya wa kukariri darasa kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari nchini kuanzia Januari mwakani.

Waraka wa Elimu Namba 2 wa Mwaka 2018, kwa mujibu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, umetokana na kukithiri kwa malalamiko kutokea kwa wazazi na walezi wakilalamikia kutoshirikishwa ipasavyo katika kufanya uamuzi wa mwanafunzi kukariri. Pia kukosekana kwa uwazi na ushirikishwaji madhubuti kwenye maamuzi ya kukaririsha darasa wanafunzi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kaimu Kamishna wa Elimu katika Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk Edicome Shirima, maombi ya kukariri darasa la kwanza, pili na tatu yatashughulikiwa na halmashauri husika. Dk Shirika alieleza kuwa kukariri darasa kwa wanafunzi wa darasa la nne, tano na sita na wenzao wa kidato cha kwanza, pili, tatu na tano yatashughulikiwa na mkoa.

Aidha, kupitia waraka huo, Dk Shirima ameelekeza kuwa maombi ya kukariri darasa kwa wanafunzi wa darasa la saba na wale wa kidato cha nne na sita ambayo hayo ni madarasa ya mitihani ya mwisho ya kitaifa, maombi yao yataendelea kutumwa  kwenye ofisi yake.

Alisema iwapo mwanafunzi akikubaliwa kukariri darasa kwenye ngazi hizo atapewa fursa ya kukariri mara moja na endapo mamlaka inayohusika ikiona kuna umuhimu wa kukariri kwa mara ya pili ndio atapewa fursa hiyo.

Waraka huo umeelekeza kuwa mzazi wa mwanafunzi wa darasa la kwanza, pili na tatu ili mtoto wake akariri darasa atatakiwa kuandika barua ya maombi ya kukariri darasa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri husika. Kwa wanafunzi wa darasa la nne, tano na sita na kidato cha kwanza, pili, tatu na tano mzazi au mlezi atatakiwa kuandika maombi yake kwa Katibu Tawala wa Mkoa.

Kuhusu wanafunzi wa darasa la saba na wale wa kidato cha nne na sita, Dk Shirima alisema mzazi anatakiwa kupitisha maombi kwanza kwa mkuu wa shule na mkurugenzi wa halmashauri husika kabla ya kuyawasilisha kwenye ofisi yake.

Aliongeza kuwa kwenye maombi yao hayo kila barua inapaswa kuwa na picha mbili za mwanafunzi husika aina ya pasipoti saizi, namba ya kuandikishwa shule pamoja na nyaraka zozote muhimu kulingana na sababu ya ombi la kukaririshwa darasa kwa mwanafunzi. 

Pia kwenye waraka huo ameelekeza kuwa kukariri darasa kwa wanafunzi wanaoshindwa kufikia viwango vya ufaulu vilivyowekwa na shule hasa kwa wanafunzi wa darasa la nne na kidato cha pili, bado wanakuwa na sifa ya kumaliza ngazi husika ya elimu bila ya kukariri.

Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA , Salum Mwalimu Akamatwa na Jeshi la Polisi Iringa

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA (Zanzibar), Salum Mwalimu, leo Jumapili, Desemba 16, 2018 amekamatwa na polisi Mafinga mkoani Iringa akiwa anaelekea kwenye kikao cha ndani cha chama chake.

Ofisa habari wa Chadema, Tumaini Makene amesema Mwalimu alikamatwa akiwa katika gari akielekea katika kikao hicho, akitokea Kanda ya Nyasa.

Waziri Akerwa na Kitendo Cha Umeme Kukatika Mara Kwa Mara.....Aagiza Wakurugenzi Wawili Wavuliwe Nyadhifa Zao

$
0
0
Waziri wa Nishati Dr. Medard Kalemani ameagiza kuchukuliwa kwa hatua za kinidhamu ikiwemo kuwavua nyadhifa zao manaibu Wakurugenzi wa sekta ya uzalishaji na usambazaji wa Shirika la umeme nchini (TANESCO) kutokana na uzembe uliojitokeza kwenye gridi ya taifa na kusababisha umeme kukatika mara kwa mara nchi nzima.

Akizungumza jana jioni Jumamosi Desemba 15, 2018 baada ya kukutana kwa dharura na bodi ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Kalemani alisema katika kipindi cha miezi miwili Gridi ya Taifa imetoka mara nne kuanzia Novemba 28 hadi Desemba 14, 2018.

Alisema kitendo hicho ni hatari kwa usalama wa Taifa ikizingatiwa kuwa nchi ina ziada ya umeme wa wastani wa megawati 252


Alisema nchi inapokuwa gizani hata kwa sekunde moja maana yake hakuna usalama na kutoa maelekezo kwa bodi hiyo kuchukua hatua.

“Lazima kuchukua hatua kuhakikisha hilo halijitokezi. Mwenyekiti (wa bodi) unda timu mahsusi kuanzia leo ya kuchunguza na kufuatilia jambo hilo kwa kushirikisha tasnia na taasisi mbalimbali si Tanesco pekee.

“Ndani ya siku saba nipate matokeo ya nini chanzo cha tatizo hilo ili lisijirudie kabisa. Jambo hili linapotokea ina maana kuna uzembe katika usimamizi ama  kutofuatilia a maagizo ya Serikali.” Alisema

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) yatoa tahadhari ya mafuriko kwa baadhi ya mikoa

$
0
0
 Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari kwa wakazi wa baadhi ya mikoa nchini humo kutokana na vipindi vya mvua kubwa zinazotarajiwa kunyesha katika siku tano zijazo.

Hayo yameelezwa leo Jumapili Desemba 16, 2018 kati  taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na mamlaka hiyo.

TMA imewataka wakazi wa maeneo ya Kanda ya Ziwa, Kaskazini, Kusini na karibu na Bahari ya Hindi kuchukua tahadhali hiyo.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa kuanzia kesho Jumatatu Desemba 17, 2018 hadi Desemba 20, 2018 baadhi ya mikoa itaathiriwa na mafuriko jambo ambalo litafanya baadhi ya shughuli za kijamii kusimama.

“Hii inamaanisha kuwa mafuriko yatatokea katika maeneo mengi na kuathiri jamii nzima, kuvurugika kwa usafiri na barabara kubwa kutopitika, hatari kwa maisha kutokana na maji kujaa au yanayopita kwa kasi,” inaeleza.

Waitara: Barabara Mbovu Zisingoje Ziara Ya Kiongozi Ndio Zifanyiwe Matengenezo

$
0
0
NA TIGANYA VINCENT,TABORA
WAKALA wa Barabara za Vijijini na Mijini nchini (TARURA) ameagizwa kuhakikisha barabara zote zilizo chini yao zinapitika wakati  wote na sio kusubiri viongozi waje ndio zifanyiwe matengenezo.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali (OR TAMISEMI) Mwita Waitara mara baada ya kutembelea miradi mbalimbali na kukutana barabara zinakwenda katika miradi hiyo ziko katika hali isiyoridhisha.

Alisema ubora wa barabara sio kwa ajili ya viongozi pekee bali zinatakiwa kuwasaidia wananchi katika kujiletea maendeleo na kuchangia katika ujenzi wa uchumi wa viwanda.

Waitara alisema kuwa barabara ni lazima ziwasaidie wakulima kutoa mazao yao mashambani na kufikisha katika sehemu husika au sokoni kirahisi.

“Barabara lazima ziwe rafiki wakati wote kuwawezesha wananchi kwenda kupata huduma za matibabu kirahisi, wanafunzi kufika shule kirahisi na wakulima kutoa mazao yao mashambani bila vikwazo…barabara zinapitika sio kwa ajili ya viongozi bali ni kwa ajili ya wananchi wote…TARURA lazima muhakikishe barabara zenu zinapitika wakati wote” alisema.

Waitara aliongeza kuwa TARURA wamepewa jukumu la kuhakikisha wanasimamia barabara za vijiji na mijini wakati wanapokuwa ni lazima akili na nguvu zao wazielekeze katika kuboresha barabara.

“Kazi yenu ni barabara …mnapokuwa Ofisini ni barabara…mnapolala wazeni  barabara…mnapoamka ni barabara…kila mnapofanyakazi fikirieni barabara ndio kazi mliopewa”alisisitiza.

Alisema urahisi wa usafiri unaotokana na ubora wa barabara hasa za vijijini utasaidia kuharakisha malighafi kufika viwandani na masokoni na hivyo kuinua pato la mwananchi na maendeleo ya nchi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images