Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Video Mpya ya Alikiba - Kadogo

0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Alikiba ameachia video ya ngoma yake mpya ya Kadogo.

Wimbo huu wa ‘Kadogo’ umefanywa na Director Kevin Bosco Jr.. Utazame hapo chini

Jipatie Dawa ya Asili ya Kupunguza Maziwa, Kupunguza Tumbo,Kuongeza Unene, Kuongeza Maumbile ya Kiume na Kuondoa Chunusi

0
0
NATURAL BEAUTY PROD.
🍋🥑🍒OFFER ya X MAS na MWAKA MPYA🍉🍇

 Ofa hii itaisha tareh. 22/12/2018 wahi sasa jipatie bidhaa original kwa punguzo la bei.

 %%Bidhaa hizi zimetengenezwa kwa mimea na matunda hazina chemical wala madhara yoyote kwa mtumiaji.             Ukinunua bidhaa kuanzia mbili utapatiwa offer ya bidhaaa nyingine yoyote uipendayo wewe bureeee.

1. SHARK POWER--Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza maumbile ya kiume urefu na upana mpaka nchi 7.5 ilikua inapatikana kwa @170,000/= sasa ni @160,000/= tu

2. VIGA 84000---Hii dawa ya kuspray yenye uwezo mkubwa wa kuchelewesha wakati wa tendo la ndoa ilikua ni  @160,000/=. Sasa ni 150,000/= tu

3. HANDSOME UP ORIGINAL-- Hichi ni kifaa cha kuongeza maumbile kwa size uipendayo wewe pamoja na kuimalisha misuli kifaa hichi kilikua kinapatikana kwa @230,000/=. Sasa ni 210,000/= tu

4. MAXMAN CAPSULE--- Hii ni dawa ya vidonge ya kuongeza maumbile ya kiume urefu na upana pamoja na kuongeza nguvu za kiume kwa wiki mbili ilikua inapatikana kwa @200,000/=. Sasa ni 180,000/= tu

5. VIG RX---- Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza uume urefu na upana mpaka nchi 10 ilikua inapatikana kwa @190,000/=. Bei ya sasa ni 170,000/=

6. BODY BOOSTER---Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri ilikua inapatikana kwa @150,000/=. Sasa ni 140,000/=

7. BOTCHO MULT PLUS-- Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza (hips mapaja na makalio) kwa size uipendayo ilikua inapatikana kwa @200,000/=. Sasa ni 180,000/=

8. WHITE COLLECTION---- Ni vidonge vya kuwa mweupe mwili mzima pamoja na kuwa soft ilikua inapatikana kwa @150,000/= Sasa ni @140,000/= tu

9. BOTCHO HOLOGRAM CREAM--- Hii ni dawa ya kuongeza hips na makalio ilikua inapatikana kwa@180,000/= Sasa ni@160,000/=       

N.K

Wasiliana nasi kwa simu

NO:. +255 759029968  AU +255 659618585

Popote ulipo utapata huduma zetu.

Pia hakikisha unapatiwa risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ununuapo bidhaa kampuni hii.

WELCOME ALL

Simbachawene ataka taasisi za fedha zipunguze riba kwenye mikopo

0
0
Taasisi za fedha nchini zimetakiwa kupunguza riba kwenye mikopo inayotolewa kwa vikundi vidogo vidogo ili viweze kujikwamua kiuchumi.
 
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti George Simbachawene alipokuwa akifungua Mkutano wa 20 wa Chama cha kuweka na kukopa cha Walimu Mpwapwa, mjini humo.

Simbachawene ambaye ni Mbunge wa Kibakwe, alisema kwasasa kinachoonekana kwenye taasisi hizo ni kutoa mikopo yenye riba kubwa jambo linalosababisha ziweze kufa.

“Mkopo wenye riba kubwa hauna urafiki na masikini bali una lengo la kudidimiza wanyonge, hizi taasisi zinazotoa mikopo zinatoa kwa riba kubwa jambo linalosababisha zingine kufa, kufilisiwa mali zao,”alisema.

Alieleza kuwa lengo la vyama vya ushirika au vya kuweka na kukopa ni kuwasaidia wanyonge ambao wanakuwa wameunganisha nguvu kupambana na umasikini.

Mwenyekiti huyo alisema wilaya ya Mpwapwa inakadiliwa kuwa na walimu zaidi ya 1500 kama wangeingia kwenye chama chao wote kusingekuwa na haja ya kukopa kwenye taasisi za fedha bali wangetumia fedha za chama chao kusaidiana.

Awali, Mwenyekiti wa chama hicho Piniel Loilole alisema kwa mwaka 2018 kiasi cha Sh.Milioni 82.15 kilitolewa kwa wanachama kama mikopo ya dharura na ya kawaida.

Naye, Meneja wa chama hicho, Joackim Mokiwa alisema changamoto kubwa inayowakabili kwa mwaka huu ni hasara ya Sh.Milioni 6.68 iliyotokana na baadhi ya watumishi kugundulika kuwa na vyeti feki hivyo kukosa sifa ya kuwa wanachama huku wakiwa tayari wamechukua mikopo.

Muungano wa Baraza la Umoja wa Vyama vya Upinzani Nchini Waungana Kuupinga Mswada wa Vyama vya Siasa

0
0
Muungano wa Baraza la Umoja wa Vyama vya Upinzani nchini wamelalalamikia muswada wa sheria ya mabadiliko ya vyama vya siasa nchini kwa kile walichokidai kuwa muswada huo umelenga kuwabana vijana hao.

Wakizungumza jana na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam vijana hao wametishia kuuchana muswada huo pindi utakapofikishwa bungeni kwa ajili ya kujadiliwa.

Aidha katika Mkutano vijana hao kutoka vyama vya CHADEMA, CUF, NCCR - Mageuzi na CHAUMA  waliingia kwenye mkutano huo kwa kile walichoashiria kuwa ni majonzi waliyokuwa nayo juu ya muswada huo.

"Leo hii sisi tumevaa nguo nyeusi, hatuoni 'future',sasa basi vijana tunataka umoja tunapinga ili tuendeleea kuwa wamoja, Taasisi zote za vijana nchi hii kwa mara ya kwanza tutatangaza safari na tutauchana muswada ukiwa unataka kuingia bungeni," alisema Likapo Bakari ambaye ni Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ya ACT wazalendo.

"Muswada unampa mamlaka msajili kutoka kuwa mlezi wa vyama vya siasa, hadi kuwa  mdhibiti wa vyama vya siasa, hivyo basi baada ya kuutafakari kwa kina muswada huu, tumeona ndoto za vijana ziko hatarini kufa kabisa na hali ya vijana itakuwa mbaya zaidi kuliko hata ilivyo sasa, hatukubaliani nao hata kidogo," alisema Patric Ole Sosopi, Mwenyekiti BAVICHA.

Aidha Mwenyekiti wa JUVI-CUF taifa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mchinga mkoani Lindi, Hamidu Jabali, alisema kuwa mchakato wa vikao vya upembuzi wa muswada huo vinaendelea baada ya kila chama kutoa wajumbe wanne watakoingia katika timu waliyoiita ya ufundi ambapo watatoa tamko rasmi baada ya kumaliza mchakato huo.

Video Mpya: Kayumba - Maumivu

0
0
Video Mpya:  Kayumba - Maumivu . Itazame hapa

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

Kutana Na Dr Chikago Bingwa Na Mwokozi Kwa Waliosumbuka Na Magonjwa Bila Mafanikio

0
0
Ninauwezo wa kumrudisha mume, mke ,mchumba, hawara, mtu unaempenda ndani ya masaa mawili tu (2) na kumfunga asiwe na mtu mwingine zaidi yako na kumfanya akutimizie kilakitu unachokihitaji kutoka kwake hata km yupo mbali na atatulia kabisa

GALIMBO 3 MIX;  nidawa ya mitishamba iliyitengenezwa kwa kwa utabibu wa hali ya juu kwakuchanganya miti na matundatiba , Huogeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15 -85 ) , inakomaza zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakat wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaid ya Mara tatu bila ham kuisha wara kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-40.

YOLANI :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inch (6-8) na unene wa sm (3-4)

Matatizo haya husababishwa na mambo mbalimbali km upigaji wa punyeto, kisukali,  vidonda vya tumbo, tumbo kuunguluma na kujaa gesi, ngili, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani, maumivu ya mgongo ama kiuno, namengineyo mengi  (nk )

SUPER MBUKE :- nidawa inayotatua tatizo la kisukali na kupona kabisa Kwa mda mfupi sana na utakuwa na uwezo wakula chakula chochote chenye sukali baada ya kupona,

vilevile ninadawa ya uzazi kwa akina Mama na akina Baba, kurudisha mali iliyopotea kwamda mfupi sana, vidonda vya tumbo, kaswende,presha,chango la uzazi, gono,nyama uzembe, kusafisha nyota, kuzuia majini wachafu, kinga ya mwili, kuuza vitu bila kununuliwa, dawa za biashara, pesa nyingi (utajili)  mambo ya kes nk

Kwa huduma n msaada wasiliana na Dr CHIKAGO atakusaidia hatakama ulikata tamaa utarudisha furaha yako

Napatikana Dar es salaam  sm no 0743543944   /0620510598

Nb :km huna nafasi ya kufika ofisin huduma hii itakufikia popote ulipo kwawatu wa mkoani tunatuma kwanjia ya mabasi.

Kamishna wa zamani TRA Harry Kitilya na wenzake Kuendelea Kusota Rumande

0
0
Mwenyekiti wa kampuni ya Egma inayoshughulikia uwekezaji wa mitaji na dhamana, Harry Kitilya na maofisa wa zamani wa benki ya Stanbic, Shose Sinare na Sioi Solomon watamaliza mwaka wa 2018 bila ya shauri lao kuanza kusikilizwa baada ya mahakama kuambiwa jana kuwa upelelezi haujakamilika.

Kitilya, ambaye alikuwa kamishna mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Shose, ambaye alikuwa Miss Tanzania wa mwaka 1996 na Sioi, walifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa mara ya kwanza Aprili mosi 2016 na kusomewa mashtaka manane, likiwemo utakatishaji ambalo halina dhamana.

Wakili wa Serikali, Wankyo Saimon alisema jana kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na kumuomba Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kupanga tarehe nyingine.

Washtakiwa hao, ambao wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha fedha, wamerejeshwa rumande ambako wameshaishi kwa takribani miaka miwili sasa tangu wakamatwe.

Hakimu Shaidi alihirisha kesi hiyo hadi Desemba 28, 2018.

Washtakiwa wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya Machi 2013 na Septemba 2015 wakati wa mchakato wa mkopo wa dola 550 milioni za Kimarekani kwa Serikali ya Tanzania kutoka Benki ya Standard ya Uingereza.

Waziri wa Fedha Akiri Misaada ya Wafadhili Imepungua....Asema Nchi Inapitia Kipindi Kigumu Kwa Sasa

0
0
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango, amesema nchi inapita kwenye kipindi kigumu kutokana na wafadhili kupunguza misaada na ile iliyobaki imekuwa na masharti yakiwamo ya kukubali ushoga.
 
Dk. Mpango alitoa kauli hiyo jana jijini Dodoma alipokuwa akifunga mkutano kati ya wizara hiyo na watoa huduma za serikali katika kukusanya mapato.

Alisema misaada imeporomoka sana na hata ile iliyobaki ina masharti mengi ya ovyo.

“Mtakuwa mmesikia jinsi ambavyo sasa wanafika mahali, hata bila aibu, wanasema sisi tuvumilie ushoga, Mnakubali? Mnakubali niende kuomba hela ya nchi halafu kuchekelea ushoga hata mbuzi hawafanyi?

“Tukipeleka jeshi letu kudhibiti magendo, wanasema tunarudisha nyuma biashara ya usafirishaji hapa nchini. Inawezekana? Kwa hiyo ninachotaka kuwaambia ni nini? Marehemu Baba wa Taifa (Mwalimu Julius Nyerere) alitufundisha kwamba tumepata uhuru wa bendera, lakini tuna kazi ya kutafuta uhuru wa kiuchumi,” alisema.

Aliongeza kuwa:“Sasa hapo ndipo shughuli pevu lazima tujitegemee na ili tujitegemee serikali kuu, serikali za mitaa lazima zijielekeze kukusanya mapato ya ndani ndiyo maana yake hakuna nyingine.”

Dk. Mpango alisema serikali ikidhibiti madini wanasema wanafukuza wawekezaji na kwamba wamechukua miaka 57 sasa inatosha.

“Ninachotaka kuwaambia salamu zangu, kila Mtanzania popote alipo hasa nyie mliomo humu ndani kila mtu aweke Tanzania moyoni mwake. Ni lazima kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa nguvu zote na hasa kwa kutumia mfumo huu wa GePG (wa njia ya kielektroniki), lazima twende kisasa,” alisema.

Alisema mfumo huo utasaidia kupata mapato yote stahiki kwa ajili ya kuendesha serikali kuu na serikali za mitaa.

“Hakuna mjomba, mjomba anayekutakia ya ovyo ovyo namna hiyo hapana ‘enough is enough’ (inatosha). Kama mnaipenda Tanzania kila mtu akazane na kusimamia huo mfumo to the best of ability (kwa uwezo wake). Mzingatie mafunzo mnayopata, mzingatie sheria zote, tunaelewana? Nawasihi sana,” alisema.

Alibainisha kuwa taifa limechelewa, hivyo lazima maji yapatikane kwa ajili ya kinamama, elimu ya watoto na lazima kujenga misingi imara ya uchumi.

“Tutaweza kama tutaweza kukusanya ipasavyo na kudhibiti mianya ya uvujaji mapato. Bahati nzuri zamani tulikuwa tunatumia watu kutengeneza mifumo ya kielektroniki lakini siyo huu,” alisema.

Waziri Mpango alisema mfumo huo umetengenezwa na Watanzania kwa hiyo wale waliokuwa wanakula kula walipwe kwa kutengeneza mifumo mibaya na wakicheleweshewa malipo kwa siku moja, wanaharibu mifumo.

“Tunawataka wale wanaotengeneza mifumo wahakikishe wanatengeneza mifumo, tambueni hakuna atakayejenga nchi zaidi ya Watanzania wenyewe,” alisema.

Aliwataka kuendelea kuwa wazalendo kwa ajili ya mama Tanzania na wasiwe sehemu ya uharibifu wa hiyo mifumo.

“Kila mmoja hapa wizarani huwa nawaambia unapopewa jukumu la kuwatumikia watanzania tambua kuna watu milioni 58 kwenye mabega yako na wengi wao ni masikini.

“Utumwa sasa mwisho lazima tutembee kifua mbele. Mzingatie mafunzo haya kwenye kazi zenu ili tujidai sasa ni taifa huru linalojiendesha lenyewe,” alisema huku akisisitiza kuwa anatamani katika bajeti ijayo, Tanzania ijitegemee bila kukopa.

“Mungu atakaponipa nafasi nisimame nitamke kuanzia sasa serikali yetu itajitegemea tutatafuta mikopo labda ya kibinadamu kama matetemeko na mafuriko, hiyo ndiyo tutaenda kutafuta nje lakini vinginevyo tufanye wenyewe na tunaweza,” alisisitiza.

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

0
0

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara, Msanii wa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo Dawa na PETE za Bahati zenye uwezo mkubwa wa kuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.

Kutana na Sheikh Jumaa Bilal. Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki. 

Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. Sheikh Jumaa Bilal ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA-  Sheikh Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na Nje ya nchi.

Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nayasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.

Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudishaa alipote, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMBA, GARI..), Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali na UTAJIRI bila masharti na mengine mengi ya Siri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET)

*{لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّهُ بِاللَّغْوِ فِي أيْمَانِكُمْ وَلَٰكِنْ يُؤَاخِذُكُمْ بِمَا عَقَّدْتُمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِمَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ }* ﴿٨٩﴾

✨Wabillahhi Tawfiq Asallam  Alaikum

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa
nambari ya simu

+255 688 745 790
+255 672 861 042
Whatsapp :  0762 252 102

Benki Yafafanua Mbuzi Kufungwa Kwenye Tairi Ya Gari La Serikali

0
0
Benki ya TIB imetoa taarifa ya kusikitishwa kwake na kitendo cha dereva wa gari inayomilikiwa na benki hiyo yenye namba za usajili SU 38431 cha kubeba mbuzi kwenye tairi ya akiba iliyopo nyuma ya gari.

Kwenye taarifa hiyo ambayo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TIB Tawi la Mlimani City, imeeleza ni kwa namna gani dereva huyo ametumia mali ya umma vibaya, na pia kukiuka haki za wanyama.

Benki hiyo imesema itamchukulia hatua stahiki dereva huyo, ambaye alikuwa akiendesha gari hilo kutoka Mwanza kuelekea jijini Dar es salaam.

Kada wa CCM Ajitosa Kuwania Urais 2020

0
0
Kada wa CCM, ambaye mwaka 2015 alijitosa kuwania kupitishwa na chama hicho kuwania urais, Dk Muzzammil Kalokola ana mpango wa kuingia tena kwenye mbio hizo mwaka 2020, na hivyo kuwa mpinzani wa kwanza wa Rais John Magufuli.
 
Kada huyo Mkongwe wa CCM, amedai moja ya sababu kubwa ambayo imemfanya aweke wazi hilo ni Mwenyekiti wao wa chama Rais John Magufuli amekuwa akikiuka baadhi ya taratibu za chama hicho ikiwemo kuteua wapinzani katika nyadhifa mbalimbali.

“CCM tulijiwekea utaratibu wa kumuachia Rais kuwa mgombea pekee pale anapomaliza miaka mitano ili akamilishe mitano mingine ili kipindi chake cha miaka 10 kikamilike, lakini Rais Magufuli amekiuka misingi kwa hivyo hakuna sababu ya kumwachia, nitaomba ridhaa nipitishwe.” amesema Dk Kalokola.

“Haiwezekani mtu ambaye wakati wa kampeni za kuwania Urais mwaka 2015 alikuwa akimtukana na kutumia njia zote kuhakikisha Magufuli anakosa urais, leo ametangaza kuingia CCM, kesho jina lake linapitishwa kugombea ubunge, kesho kutwa anakuwa waziri,” alisema Dk Kalokola.

Licha ya Kada huyo kuonesha nia ya kuwania nafasi ya Rais Magufuli, mwingine ambaye alikuwa ametajwa ni aliyekuwa Mbunge wa Mtama, Bernard Membe lakini taratibu za chama hicho zinakataza mtu kutangaza kuwania nafasi ambayo tayari inaongozwa na kiongozi wa chama hicho.

Makanga 3 Power, Dawa Bora Za Nguvu Za Kiume

0
0

Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.

Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.

Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.

Onana na Dr shilindes shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.

Pia anaboresha akili kwa wanafunzi darasani, masomo na kufaulu mitihani pia kushinda bahati nasibu yeyote.

Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule, unaemtaka kimapenzi au kuoana, utampata na kumfunga asitoke nje ya ndoa daima na kutekeleza shida zako zote. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.

Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.

Tupo dar es salam Buguruni

Mawasiliano simu namba: 0784 460 348.

Polisi Dodoma Yapiga Marufuku Kula Mbuzi wa Ajali

0
0
Jeshi la Polisi Jijini Dodoma, limepiga marufuku kwa wananchi kula nyama ya mbuzi ambao walikufa kwenye ajali, iliyohusisha malori mawili hapo jana.

Marufuku hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi Dodoma, Gilles Murotto, na kusema kwamba daktari amewaambia kuwa nyama hiyo imeingia sumu baada ya kumwagikiwa mafuta ya dizeli, yaliyomwagika kwenye moja ya malori yaliyopata ajali.

“Hiyo ajali ilihusisha malori mawili ambayo moja lilikuwa limebeba mbuzi 150 likielekea Dar es salaam, na lingine likiwa ni la tanki la mafuta, yalivyogongana mbuzi 11 wamekufa na baadhi ya watu walijeruhiwa pia, hivyo tumetahadharisha watu kula nyama yake, kwanza ni ina dizeli na pia hata daktari kasema ina sumu ni hatari kwao”, amesema Kamanda Murotto.

Akielezea ajali hiyo Kamanda Muroto amesema imetokea jana majira ya saa 4 usiku jijini Dodoma, na majeruhi wote ambao walikuwa watano walikimbizwa kwenye hospitali ya Rufaa ya Dodoma, na hali zao zinaendelea vizuri.

Waziri Wa Kilimo Mhe Hasunga Aagiza Waliokopa Kwenye Saccos Kulipa Madeni Hayo Ndani Ya Miaka Mitatu

0
0
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Mtwara
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameagiza kurejeshwa ndani ya miezi mitatu madeni yote yaliyokopwa kwenye vyama vya akiba na mikopo (SACCOS).

Alisema kuwa mwananchi watakaoshindwa kutii maelekezo hayo katika kukamilisha deni lake ndani ya miezi mitatu hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

“ Nataka kila aliyekopa kwenye Saccos arejeshe deni lake kwa kufuata utaratibu wa makubaliano na kama wasipotekeleza ndani ya miezi mitatu niliyotoa serikali itaagiza wahusika wote kukamatwa maana dawa ya deni ni kulipa” Alisisitiza

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga ametoa agizo hilo tarehe 14 Disemba 2018 wakati wa kikao cha kazi katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara alipokuwa akizungumza na viongozi wakuu wa vyama vya Akiba na Mikopo (SACCOS) sambamba na Vyama vya Msingi vya Ushirika vilivyopo katika Mkoa wa Mtwara.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Kaimu Mrajisi wa vyama vya Ushirika nchini, Mkaguzi wa vyama vya ushirika na Saccos, Kaimu Mrajisi msaidizi wa mkoa wa Mtwara, Wenyeviti na watendaji wa SACCOS pamoja na vyama vya msingi vya ushirika vilivyopo mkoani Mtwara.

Mhe Hasunga amelitaka Shirika la Ukaguzi wa Hesabu za Vyama vya Ushirika (COASCO) kutimiza majukumu yake kwa weledi kwa kukagua na kuhakikisha vyama vyote vinafunga mahesabu huku akitaka vyama ambavyo sio hai kuchukuliwa hatua.
Pia ameagiza kila chama Tanzania kiwe na daftari la wanachama walio hai na wafu sambamba na kuhakikisha kuwa viongozi wote wawe na maadili na uwezo wa kuvisimamia vyama vyao ipasavyo.

Katika hatua nyingine alimtaka Mrajis wa ushirika Tanzania Bw Tito Haule kuwasilisha mpango kazi wa namna ya kukutana na wanachama wa ushirika nchi nzima katika kutatua changamoto zao. “ Na ni lazima taarifa itengenezwe ikionyesha idadi ya vyama mlivyokutana navyo na kueleza ni mambo gani mmezungumza kila mwezi” Alisema

Aliongeza kuwa Viongozi ni lazima kutoa mapendekezo ya mabadiliko ya sheria ya Ushirika itakayosaidia kuondoa usumbufu kwenye ushirika ili uendelee kuwa mkombozi wa wananchi. “Mje na mfumo wa namna ya kuwasaidia wananchi kupata pembejeo bila kuingia madeni yasiyokuwa na tija” Alisisitiza

MWISHO.

Tazama Hapa Majina ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza 2019

0
0
Tazama Hapa  Majina ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza 2019.

==>>Bonyeza Mkoa unaotaka kuona Majina hapo chini
  1.     Songwe
  2.    Arusha
  3.     Kilimanjaro-Wavulana
  4.     Kilimanjaro-Wasichana
  5.     Dar es Salaam
  6.     Tabora
  7.     Dodoma
  8.     Tanga
  9.     Morogoro
  10.     Pwani
  11.     Lindi
  12.     Mtwara
  13.     Ruvuma
  14.     Iringa
  15.     Mbeya
  16.     Singida
  17.     Rukwa
  18.     Kigoma
  19.     Shinyanga
  20.     Kagera
  21.     Mwanza
  22.     Mara
  23.     Manyara
  24.     Njombe
  25.     Katav
  26.     Simiyu
  27.     Geita
Mikoa mingine bado hayajawekwa...Tutaendelea kuweka kadri wanavyowekwa

Waziri Mkuu Majaliwa awatahadharisha wanaoharibu maeneo ya utalii

0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametoa tahadhari kwa vinara wanaojihusisha na uharibifu wa maeneo ya utalii, waache kufanya hivyo kwa kuwa hatua za kisheria zitazidi kuchukuliwa dhidi yao.

Pia amewataka watanzania watunze maeneo hayo kwa lengo la kukuza mapato kupitia utalii.

“Ningependa kuwakumbusha kuwa baadhi ya  vinara wanaojihusisha, kuharibu vyanzo, kuua wanyama na kufanya uharibifu wamaeneo ya utalii, adhabu zinaendelea kuchuliwa maana wapo baadhi ya watu wanaharibu maeneo ya kale bila kufahamu maeneo hayo ni Tunu ya nchi yetu, hivyo niwaombewatanzania waendelee kutunza maeneo haya ili yalete tija,” amesema.

Amesema kupitia Chaneli hiyo taifa litanufaika kwa kupata idadi kubwa ya watalii ambayo itatusaidia kuingiza mapato zaidi pia itasaidia kuonyesha watalii wa waliopo nje ya Tanzania vivutio vyetu na kuwavutia kuja nchini.

“Tukiimarisha utalii sekta hii itatoa ajira kwa watanzania zaidi ya milioni 1.5 cha muhimu tujiulize kwanini tunabaki nyuma wakati tuna vivutio vingi zaidi,”  amesema Waziri Mkuu.

Aidha amewataka watayarishaji wa vipindi vya runinga hasa vipindi vya utalii kuhakikisha vinavutia kama vile vinavyooneshwa katika chaneli za kimataifa na kwamba hawana budi kupambana na changamoto zitazojitokeza.

RC Makonda Atoa Onyo kwa wanaokamata wapiga picha katikati ya jiji la Dar es Salaam

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameagiza polisi wanaowazuia wananchi kupiga picha katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam kama kumbukumbu za maeneo hayo kuacha mara moja ili wasaidie kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo jijini.

Makonda ameyasema hayo leo Desemba 15, 2018 jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa chaneli ya Utalii iliyopewa jina la Tanzania Safari Chanel uliofanyika ofisi za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Makonda amesema kuwa sehemu maalum iliyozuiwa kupigwa picha za hivyo ni ikulu tu iliyopo Magogoni Jijini hapa.

“Inashangaza eti mtu anaona sehemu nzuri katikati ya jiji anapiga picha wanakuja wanamkamata, wasanii wanaigiza wanakamatwa,’’ anaeleza Makonda.

Hata hivyo amefafanua kuwa kwa kuwaacha watu wapige picha katika maeneo mbalimbali ya jiji hili kutasaidia kuinua utalii wa ndani na nchi kwa ujumla kama namna Marekani walivyoweza kutangaza utalii na nchi yao kwa ujumla.

“Marekani ni mfano mzuri kwani waigizaji wameifanya nchi yao kuwa ya kuvutia hadi kupelekea watu wengi watamani kwenda kuiona lakini inashangaza hapa kwetu wasanii wakienda kupiga picha wanakatazwa,” amesema Makonda.

Chaneli ya Tanzania Safari iliyoudhuriwa na viongozi mbalimbali nchini itapatika nakatika kisimbuzi cha Startimes namba 331.

Waziri Kigwangallah Atoa OFA Kwa Wasanii

0
0
Neema imewashukia wasanii nchini baada ya Waziri wa Maliasili na Utalii,Dk Hamisi Kigwangala kutoa ofa kwa wasanii wanaotaka kuandaa video za filamu ama za nyimbo zao katika maeneo ya utalii, kumuona yeye mwenyewe ili awape kibali cha kutumia vivutio hivyo vya utalii.

Kigwangala ameyasema hayo leo Desemba 15, 2018 katika uzinduzi wa chaneli ya Utalii iliyopewa jina la Tanzania Safari uliofanyika ofisi za Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) jijini Dar es salaam.

Dk Kigwangala amesema anafanya hivyo ili kukwepa urasimu mkubwa wanaopata wasanii wanapoomba kufanyia filamu ama video zao kwenye maeneo ya utalii nchini.

“Kila siku watanzania wanalalamika kuzuiwa kupiga picha katika baadhi ya maeneo na sasa hivi nimetoa ofa kwa wasanii wote wanaotaka kutengeneza video zao katika maene ya utalii wanione mimi moja kwa moja nitawapa vibali ili nawao watangaze vivutio vyetu,” amesema

Aidha amewatoa hofu watanzania wanaodhani Wizara ya yake haifanyi kazi ipasavyo wasiwe na wasiwasi kwani wamekuja na mkakati kabambe wenye lengo la kukuza sekta hiyo,

“Kwa sasa utalii unachangia asilimia 17.6 na tunasemwa sana kwasababu watanzania wanaona kama Wizara aifanyi kazi ipasavyo lakini nataka niwahakikishie kuwa tumejipanga na tuna mikakati mipya kabisa ya kuboresha sekta hii,” amesema

Waziri Mkuu Azindua Rasmi Channel ya Utalii Tanzania ....Awataka Waliopewa Dhamana Wazingatie Viwango Vya Kimataifa

0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amezinduaChaneli ya Taifa ya Utalii iitwayo Tanzania Safari Channel na amewataka watu wote waliopewa dhamana ya kuiendesha wahakikishe wanazingatia viwango vya kimataifa katika vipindi watakavyokuwa wanaviandaa.

“Vipindi vyenu ni lazima vivutie kama vile tunavyoviangalia katika chaneli za wanyama za kimataifa kama vile National Geographic, Discovery, Travel na zingine ili lengo lililokusudiwa wakati wa kuanzishwa kwake litime.”

Ameyasema hayo leo (Jumamosi, Desemba 15) wakati akizindua chaneli hiyo kwenye Ofisi za TBC, Mikocheni, jijini Dar es Salaam, ambapo ametoa wito kwa Wizara zote zinazohusika na uanzishwaji wa Chaneli hiyo kuhakikisha zinailea wakati ikijijenga kujiendesha kibiashara.

Amesema Tanzania ni moja ya nchi duniani zilizotenga moja ya tatu ya eneo lote la nchi kwa ajili ya uhifadhi, ambapo kuna tamaduni za makabila mbalimbali, ngoma za kuvutia, vyakula vya asili, sinema za maisha yetu na lugha adhimu ya Kiswahili.

“Hivyo, kwa kuanzishwa kwa chaneli hii inayotengeneza vipindi na kuonesha vivutio hivi ndani na nje ya Tanzania itasaidia watalii huko waliko kujua huu utajiri wetu na kuchagua kuja kutalii nchini. Ni matumaini yangu kuwa hii Tanzania Safari Channel ninayoizindua leo itaongeza thamani katika kuvutia watalii wengi zaidi kutembelea Tanzania.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ametaja faidazinazotokana na utalii ambazo ni pamoja na kuliingizia Taifa fedha za kigeni, ambapo kiasi cha Dola za Kimarekani bilioni 2.3 zimeingia kwa mwaka 2017. Fedha hizo ni sawa na sh. trilioni 5.04.

Pia sekta hiyo ya utalii inatoa ajira kwa Watanzania zaidi ya milioni 1.5 wanaojihusisha katika shughuli mbalimbali zikiwemo usafiri wa ndani kwa watalii, uongozaji watalii kwenye maeneo yenye vivutio, kuuza bidhaa kwa watalii kama vyakula, vinywaji, vinyago, nguo, zawadi.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema licha ya mafanikio hayo, lakini hatupaswi kuridhika nayo kwani Tanzania inapokea watalii milioni 1.3 kwa mwaka wakati nchi kama Misri na Afrika Kusini hupokea zaidi ya watalii milioni 10.

“Lazima tujiulize, ni kwa nini sisi tulio na vivutio vingi kuanzia hifadhi maarufu ya Serengeti, Ngorongoro, Mlima Kilimanjaro, hifadhi ya Ruaha, Sadani (Hifadhi pekee iliyopakana na bahari), Zanzibar ambako  kuna fukwe maridadi, malikale, maporomoko ya maji na vingine vingi na baadhi ya hivi vivutio vimewekwa katika kundi la maajabu ya Dunia tunapata watalii wachache.”

Aidha, Waziri Mkuu amesisitiza kuhusu uboreshwaji wa bustani katika barabara inayotokea Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, ambapo amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isac Kamwelwe asimamie jambo hilo pamoja na matangazo yanayowekwa katika barabara hiyo yaoneshe vivutio vya utalii vilivyopo nchini.

Kadhalika uzinduzi huyo ni utekelezwaji wa maagizo ya Rais Dkt. John Magufuli aliyoyatoa Mei 16 mwaka jana alipotembea TBC kuwa, pamoja na mambo mengine aliwataka waangalie uwezekano wa kuanzisha chaneli itakayotangaza hifadhi na vivutio vya utalii nchini.

Pia Uzinduzi wa Chaneli hiyo ya utalii ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM Ibara ya 29 iliyoielekeza Serikali kuweka mkakati wa kimataifa wa utangazaji wa utalii ili kuwavutia watalii wengi zaidi na kufikia idadi ya 2,000,000 ifikapo mwaka 2020.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Khamis Kigwangala. Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isac Kamwelwe pamoja na maafisa wengine wa Serikali.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images