Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Mabehewa TRL Yapandisha Vigogo 18 Kizimbani

$
0
0
Aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) sasa TRC, Kipallo Kisamfu na wenzake 17 wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kusomewa mashtaka 15 ya matumizi mabaya ya madaraka.

Kisamfu na wenzake ambao ni wahandisi na mameneja walipandishwa kizimbani jana Jumatano Desemba12, 2018 kwa kuingia mikataba ya zabuni ya ununuzi wa vichwa vya treni na kuipa zabuni hiyo kampuni ya Hindusthan Engineering and Industries Limited

Hayo yalielezwa na mwendesha mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Maghela Ndimbo mbele ya HakimuMkazi Mkuu, Wilbroad Mashauri

Mbali na Kisamfu washtakiwa wengine ni Gilbert Alfred Minja ambaye alisomewa mashtaka bila kuwepo mahakamani pamoja na Paschal John Mafikiri (Kaimu mhandisi mitambo mkuu).

Wengine ni Anthony Emmanuel Munishi (meneja usambazaji) Charles Ndenge (kaimu meneja wa usafirishaji), Ferdinand Soka (kaimu meneja msaidizi wa usambazaji), Muungano Kaupunda (kaimu mkuu wa kitengo cha ufundi).

Joseph Syaizyagi, Kedmond Mapunda, Lowland Simtengu, Ngoso Ngosomwile, Yonah Shija, Malumbo Malumbo, Stephan Kavombwe, Donatus Bandebe, John Charles na Ally Mwangila.

Katika shtaka la kwanza dhidi ya aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa TRL,  Kipallo Kisamfu inadaiwa Machi 21 mwaka 2013 huko katika makao makuu ya kampuni hiyo, alitumia madaraka yake vibaya kwa kusaini mkataba wa zabuni kwa Kampuni ya Hindusthan Engeering and Industries Limited bila kuhakiki  mkataba huo utatekelezeka kwa kuzingatia masharti ya mkataba.

Aidha imedaiwa, Kaimu Mhandisi Mkuu wa Ufundi, Paschal Mafikiri, anadaiwa kati ya Februari 21 na Agosti 15 mwaka 2013  alishindwa kutoa taarifa ya mkataba wa zabuni wa kampuni hiyo na kusababisha Kampuni hiyo ijipatie manufaa.

Pia inadaiwa, Mafikiri aliidhinisha michoro 274 ya mabehewa ya mizigo kwa Kampuni ya Hindusthan kinyume na mkataba wa zabuni.

Mshtakiwa huyo pia anadaiwa kwamba kinyume na mkataba aliidhinisha michoro ya mabehewa iliyoandaliwa na Kampuni ya Hindusthan.

Aidha mshtakiwa Kaupunda, kiwa Kaimu Mhandisi wa Ufundi na Mkuu wa Idara anadaiwa  Kuidhinisha mchoro wa mabehewa na mafuta iliyoandaliwa na kampuni hiyo.

Pia,  washtakiwa, Kaupunda, Syaizyagi, Mapunda na Simtengu  wanadaiwa kati ya Januari 10 na Februari 20 wakiwa waajiriwa wa TRL kwa nafasi zao za Mhandisi Mkuu wa Ufundi, Mchoraji Mkuu na Msaidizi Mkuu wa Meneja wa Usafirishaji wa Reli na wote wajumbe Kamati ya uthamini walitumia madaraka vibaya kwa kushindwa kufanya uchambuzi za zabuni.

Shtaka la saba kwa mshtakiwa Munishi , Meneja Mkuu wa Usambazaji, anadaiwa kuidhinisha usambazaji wa mabehewa 274 Febriaro11,2013 bila kuwasilisha ripoti hiyo kwenye bodi ya zabuni .

Washtakiwa Minja, Mafikiri, Massae,  Munishi na Ndenge, wanadaiwa Februari 20,2013 kwa kutumia madaraka yao vibaya waliidhinisha mapendekezo ya kamati ya uthamini katika mkataba wa Kampuni ya Hindusthan kusambaza mabehewa 274 .

Aidha,  mshtakiwa Ngosomwiles, anadaiwa Aprili 10 mwaka 2014 huko Katika maeneo ya karakana ya Tiljala India akiwa Kaimu Mhandisi Mkuu wa Ufundi alitumia madaraka vibaya kwa kuidhinisha uzalishaji wa mabehewa 50 bila kufuata masharti

Wakili Ndimbo amedai mshtakiwa Shija na Malumbo, wanashtakiwa kwamba Julai 16,2014 waliidhinisha Kampuni ya Hindusthan kuzalisha mabehewa 174 ya mizigo na shtaka la 11 linamkabili  Kavombwe na Bandebe wanadaiwa Septemba 4,2014 huko Santragachi India waliidhinisha kampuni hiyo kuzalisha mabehewa 50 ya matanki ya mafuta Shija na Malumbo wanadaiwa Julai 17,2014 waliidhinisha kusafirishwa kwa mabehewa 50, Pia mshtakiwa Kavombwe na Bandebe wanadaiwa kuidhinisha kusafirishwa kwa mabehewa 174 kuingia nchini bila kufuata masharti ya mkataba .

Pia washtakiwa Charles na Mwangila wanadaiwa kati ya Aprili 26 na 27 mwaka 2015 walitumia vibaya kwa kuidhinisha Kampuni ya Hindusthan kuingiza nchini mabehewa 50 ya mafuta na 27 ya mizigo bila kuwa na uhakika kwamba mkataba utatekelezeka .

Washtakiwa wote walikana mashtaka yao na wako nje kwa dhamana hadi Januari 18 kesi itakapotajwa. Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelekezi katika kesi hiyo bado haujakamilika

Ofa! Sale! Tumeshusha tena bei za Viwanja: Bunju na Mapinga

$
0
0
Ofa! Sale! Tumeshusha tena bei za Viwanja: Bunju na Mapinga

Kwa msimu huu wa sikukuu, tumeshusha sana bei za viwanja kwa Bunju na Mapinga ili kila Mtanzania mwenye uhitaji wa Ardhi (Kiwanja) apate kulipia haraka na kumilikishwa kiwanja chake. Ofa hii inaanza leo mpaka tarehe 30 dec

Kwa Mapinga vipo viwanja vifuatavyo:
sqm 400 (mita 20/20) kwa bei ya tsh 4,000,000/=
sqm 450 (mita 15/30) kwa bei ya tsh 4,500,000/=
sqm 800 (mita 20/40) kwa bei ya tsh 8,000,000/=
sqm 1120 (mita 32/35) kwa bei ya tsh 11,200,000/=
sqm 1364 (mita 35/38) kwa bei ya tsh 13, 640,000/=
sqm 1600 (mita 40/40) kwa bei ya tsh 16,000,000/=
sqm 1900 (mita 42/45) kwa bei ya tsh 19,000,000/=
sqm 2400 (mita 40/60) kwa bei ya tsh 28,000,000/=
sqm 3000 (mita 50/60) kwa bei ya tsh 34,000,000/=
Viwanja hivi viko umbali wa km 3 tu kutoka main road (Bagamoyo Road)

Kwa Bunju vipo viwanja 2 tu kama ifuatavyo:
sqm 600 kwa bei ya tsh 18,000,000/=
sqm 1700 kwa bei ya tsh 51,000,000/=
Viwanja hivi viko umbali wa km 1 tu kutoka main road (Bagamoyo Road)

Biashara hii haina dalali, mpigie mhusika: 0758603077, whatsap 0757489709

BAVICHA Waandika barua nzito kwa Jaji Mkuu

$
0
0
Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA (BAVICHA) wakiongozwa na Mwenyekiti wao Patrick Ole Sosopi, jana Desemba 12, 2018 wamewasilisha barua katika Ofisi ya Jaji Mkuu, Ibrahim Hamis Juma jijini Dar es salaam, wakilalamikia kukiukwa kwa haki kwenye mahakama.
 
Patrick Ole Sosopi amesema wamefikia uamzi huo kwa kuona hakuna sehemu nyingine wanaweza kupata haki kutokana na viongozi wao wa kitaifa kukosa badhi ya haki ikiwemo kuwaeleza wananchi maendeleo ya kesi zao mahakamani.

''Tumechukua hatua ya kumwandikia barua Jaji Mkuu Ibrahim Hamis Juma, kumweleza malalamiko yetu juu ya uonevu wanaofanyiwa viongozi wetu na vyombo vya dola na sasa vimefika mpaka mahakamani sasa ambapo viongozi wetu wana kesi mbalimbali lakini hawapati haki zao'', amesema Sosopi.

Aidha Ole Sosopi, ameongeza kuwa kuna mambo mengi yanayofanyika ambayo yanaenda kinyume na haki katika Mahakama ikiwemo kukamatwa na kupigwa kwa wanachama wa CHADEMA wanapokuwa kwenye majukumu yao ya kichama.

Pia amesisitiza kuwa barua hiyo haiishii kwa Jaji Mkuu pekee bali inakwenda pia kwa Mwanasheria Mkuu wa serikali Dkt. Adelardus Kilangi pamoja na  Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro.

Wimbo Mpya : Nedy Music - Zungusha

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Nedy Music anakukaribisha kusikiliza wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Zungusha. Isikilize hapa.

Video Mpya: Rich Mavoko - Wezele

$
0
0
Video Mpya: Rich Mavoko - Wezele

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

$
0
0

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara, Msanii wa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo Dawa na PETE za Bahati zenye uwezo mkubwa wa kuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.

Kutana na Sheikh Jumaa Bilal. Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki. 

Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. Sheikh Jumaa Bilal ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA-  Sheikh Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na Nje ya nchi.

Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nayasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.

Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudishaa alipote, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMBA, GARI..), Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali na UTAJIRI bila masharti na mengine mengi ya Siri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET)

*{لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّهُ بِاللَّغْوِ فِي أيْمَانِكُمْ وَلَٰكِنْ يُؤَاخِذُكُمْ بِمَا عَقَّدْتُمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِمَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ }* ﴿٨٩﴾

✨Wabillahhi Tawfiq Asallam  Alaikum

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa
nambari ya simu

+255 688 745 790
+255 672 861 042
Whatsapp :  0762 252 102

Dr Hindu: Bingwa Wa Tiba Asili .....Hutibu Matatizo Yafuatayo

$
0
0
NKURURU:-ni dawa inayotibu miguu kuwaka moto, kiuno tumbo kupooza kupoteza fahamu 

MALABALA; hutibu kisukari , uti wa mgogo, Change, pumu, busha, kaswende, kifua kikuu, muwasho sehemu ya siri 

NKURUNGU,: Ni dawa kutibu  N, B, G, POWER :-ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume ni vidonge 20 

MPERAMPERA:- ni dawa ya kurudisha Mke, mme, mpenzi,mchumba aliyekuacha /kuteseka, ni kwa mda wa siku 2 tu kusafisha , pia kuna dawa za kupunguza vitambi(nyama uzembe), maziwa makubwa,michirizi, mikovu makubwa, chunusi sugu. 

NR SIX POWER:-inatibu upungufu wa nguvu za kiume kwa wasio weza kumudu tendo la ndoa itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara 4 bila hamu Kuisha, inaboresha maumbile madogo na inaimarisha misuri iliyo legea na kusinyaa una pona kabisa, ndani ya siku 4 tu 

GASELA:-ni dawa ya maajabu (9) yaliyoshindikana. (1)-Kisukari, vidonda vya tumbo, tezi dume,walioshindikanika kupata watoto(ugumba),busha bila oparesheni, (2)zindiko Kali Katika biashara yako (chuma ulete) ndo kiboko yao kumkamata mwizi aliye kuibia vitu vyako pikipiki, gari, n, k( 2)zindiko la nyumba, mashamba, viwanja,.(4)kukutolea sumu uliyo ikanyaga (Mtego) (5)ujiamini kutumia dawa ya maajabu Saba (6)kutoa mikafara mfano ugomvi ndani ya nyumba kufukuzwa kazini bila sababu (7)kutabiri nyota na kung'arisha (8)kurudisha Mali iliyo potea mazingira ya kutatanisha, kushinda kesi uliyo sumbuka nayo mda mrefu. (9)kufukuza majini wachafu ndani ya mji,.

Haya yote yanawezekana kwa DR HINDU popote ulipo . Muone  DR HINDU,anatibu nguvu za kiume anarefusha na kunenepesha uume kwa saizi uipendayo kwa muda mfupi sana, pamoja na kuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa mara 4 bila hamu kuisha Na utachelewa kufika kileleni kwa muda wa dakika 40 bila kuchoka .

Angalizo usitume meseji wala kubipu..
 
You can get it in all East African countries,,our service is fast and easy... contact Whatsapp 0784,47,59,46. Dar es salaam, Mbagala Tanzania. ,..Dr. KANENGO 0744,92,29,82 / 0716608959...You are welcome. Yuko pia Khahama Mjini

Lugola Atoa Onyo Kali Kwa Wanaojipenyeza Kupitia Taasisi Za Dini Kuhubiri Siasa, Uchochezi

$
0
0
Na Felix Mwagara, (MOHA), MARA.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amesema wapo baadhi ya watu ambao wanajipenyeza kupitia mgongo wa taasisi za dini nchini kujifanya wahubiri kumbe ni wachochezi na wanajiingiza katika masuala ya kisiasa.

Amesema Wizara yake ipo makini katika kusajili Makanisa na Misikiti yote nchini na mpaka sasa wana maombi mengi ambayo yametumwa wakiomba kusajiliwa ambapo baadhi yao bado hayajasajiliwa kwasasababu wanahitaji umakini mkubwa katika kufanya uchunguzi wa kina kabla hawajatoa usajili ikiwa na lengo la kuepusha baadhi ya taasisi za dini zenye mpango mbaya na maendeleo ya  nchi.

Akizungumza na mamia ya wananchi wa Kijiji cha Sunsi, Kata ya Nampindi, Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, jana, Lugola ambaye ni Mbunge wa Jimbo hilo, alisema taasisi za dini zina mchango mkubwa nchini na uwepo wao ni muhimu katika maendeleo ya nchi, na serikali inawathamini mchango wao katika kuimarisha amani na pia kuwaweka watu pamoja lakini kuna baadhi ya dini hizo zinakiuka utaratibu wa usajili na kuvunja sheria za nchi kwa kuacha kuhubiri masuala ya kiroho wanajihusisha na masuala ya kisiasa pamoja na uchochezi.

“Serikali ya Rais Dk. John Magufuli ya Awamu ya Tano haitakua tayari kwa mwananchi yeyote kutumia mwavuli wa dini, au kufanya misikiti na makanisa kuwa kichaka kwa kufanya uchochezi katika nchi hii, kuhatarisha amani ya nchi hii, tupo makini na hatuwezi kuchezewa na mtu yeyote au taasisi yoyote,” alisema Lugola.

Lugola alitumia muda mrefu kutoa ufafanuzi huo baada ya kukaribisha maswali mbalimbali kutoka kwa wakazi wa kijiji hicho katika mkutano huo ili wananchi hao waweze kuuliza ndipo mmoja wao akauliza kuhusu uchelewashaji wa usajili wa kanisa.

“Taasisi hizi za Makanisa na Misikiti wanao mchango mkubwa sana kwa wananchi hususani waumini wao katika kuhubiri amani ya nchi hii, katika kukemea vitendo vya rushwa kwasababu hata katika maandiko rushwa imekemewe, rushwa imeonekana ni hatari katika vitabu vyote vitakatifu vya dini, lakini wapo baadhi ya watu wasiowaaminifu nchini wamejipenyeza na wanaendelea kujipenyeza katika taasisi hizo, na badala ya kuhubiri masuala ya kiroho, wanajihusisha na masuala ya uchochezi na uvunjifu wa amani,” alisema Lugola.

Lugola amesema Serikali haitakubali kuchezewa na kutokana na sababu hizo na nyinginezo Wizara yake inaendelea kuwa makini kuyafanyia kazi maombi ya taasisi hizo kwa kuomba usajili, na aliwataka ambao wametuma maombi yao kwa muda mrefu waendelee kusubiri wakati Serikali ikiendelea kuwa makini kuyafanyia kazi maombi yao.

“Serikali ya Awamu ya Tano haitakua tayari mwananchi yeyote kutumia mwavuli, kufanya misikiti na makanisa kuwa kichaka cha kufanya uchochezi, kuhatarisha amani ya nchi hii, Serikali ya Magufuli  ipo makini sana zaidi mnavyofikiria,” alisema Lugola.

Pia Lugola aliwataka wananchi nchini waendelee kutoa taarifa za uhalifu, taarifa majambazi, vibaka ili Jeshi la Polisi liweze kufanya kazi na waone makali ya Jeshi hilo katika utendaji wa kazi, kwasababu askari waliapa kulinda usalama wa raia na mali zao.

Waziri huyo aliwataka Watanzania waendelee kufanya shughuli zao kwa amani na utulivu kwa kuwa Jeshi lake lipo imara na linafanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa na amani.

Aidha, Waziri Lugola aliwataka wananchi wa jimbo lake waanze maandalizi ya kilimo cha mazao ya chakula na biashara ili kuepuka janga la njaa lisije liwakumba endapo hawata lima.

“Nipo katika ziara hii kwa lengo la kuwahamasisha mwezi huu wa Desemba muanze maandalizi ya kilimo cha mazao ya pamba, mahindi, mpunga, viazi na mengineyo ambapo ndani ya jimbo hili mnayalima,” alisema Lugola.

Lugola ameikamilisha ziara aliyoipanga kwa kutembelea Kata zote za Jimbo hilo kwa kuwapa elimu mbalimbali ya mipango ya miradi ya maendeleo jimboni humo na kuwaahidu kuyafanyia kazi changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Wema Sepetu Aitwa Kuhojiwa Tena

$
0
0
Bodi ya filamu imesema alichokifanya Wema Sepetu kutangaza filamu ya ‘Saa Mbovu’ sio sahihi kwa kuwa bado hawajamfungulia kujishughulisha na kazi za filamu.

Wema alitangaza filamu hiyo  katika ukurasa wake kwenye mtandao wa Instagram, filamu ambayo kacheza na Aunt Ezekiel wakiwa kama wahusika wakuu.

Mtendaji wa Bodi hiyo, Joyce Fisoo, amesema wamesikitishwa na kitendo hicho na tayari wamemuita kumhoji kwa nini amefanya hivyo na kwa nini asichukuliwe hatua.

Amesema kanuni za sheria ya filamu na michezo ya kuigiza namba 156 za Mei 2011, kifungu cha 50 kinaeleza kuwa kwa yeyote atakayetenda kosa kwa kukiuka masharti ya kanuni hizo atatozwa faini isiyopungua Sh5 milioni.

Amebainisha kuwa mbali na kumuita Wema, pia walikihoji kituo cha Azam kujua kwamba wao ndio walimpa kazi ya kutangaza filamu hiyo, ambao walikana na kudai kuwa wanatangaza kupitia mitandao yao.

Kuhusu kumalizika kwa adhabu yake, amesema bado yupo katika uangalizi hadi Aprili mwakani, ambapo amepewa kazi tatu kubwa za kufanya na endapo wataridhika watatangaza kwa umma ni hatua gani watazichukua dhidi yake.

Mahakama Yamwachia Huru Mama Anayetuhumiwa Kumuua Mwanae

$
0
0
Mahakama Kuu Tanzania Kanda ya Tabora, imemwachia huru mkazi wa Kijiji cha Minyinya Wilaya ya Kibondo, Ester Ndalaba (40), baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha kosa la mauaji ya mtoto mwenye umri wa miaka 8.

Akisoma hukumu hiyo, Jaji wa Mahakama hiyo, Julius Mallaba, alisema mshtakiwa huyo alikuwa ameshtakiwa kwa kosa la kumuua mtoto wake Magreth Gaudes kwa kumkata shingoni na kitu chenye ncha kali kwa kukusudia.

Upande wa mashtaka ulikuwa ukiongozwa na wakili wa serikali, Antia Julius, ambao ulipeleka mahakamani mashahidi watano na vielelezo viwili.

Jaji alisema upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha kosa hilo la mauaji, hivyo mahakama imemwachia huru mshtakiwa kwa sababu jukumu kubwa la kuthibitisha kosa dhidi ya mshtakiwa ni upande wa mashtaka na kama kuna upande wowote ambao haujaridhika na hukumu hiyo wakate rufani katika mahakama ya rufani.

Upande wa utetezi uliongozwa na wakili wa kujitegemea, Iginatus Kagashe.

Jaji Mallaba alisema mtoto huyo alikuwa ni wa mshtakiwa na alikuwa ni mlemavu wa kuongea, kutotembea na mikono na hadi kifo chake alikuwa na umri wa miaka 8 bila ya kuongea wala kutembea.

Alisema siku ya tukio Mei 4, mwaka 2010 ndipo alipofariki dunia kwa kukatwa shingoni na kitu chenye ncha kali.

Alisema mshtakiwa huyo alihusishwa na kitendo hicho cha mauaji kutokana na kifo cha mtoto huyo kuuawa kwenye chumba cha mshtakiwa huyo.

Credit: Nipashe

Ndege za ATCL Zaanza Kuhujumiwa Na Wafanyakazi....Waziri Atoa ONYO

$
0
0
Naibu  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye, amekemea tabia ya hujuma inayofanywa na baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya Ndege Tanzania-ATCL huku akikitaka kitengo cha masoko cha Kampuni hiyo kuhakikisha kinaangalia na kuondoa hujuma hizo.

Hujuma hiyo inatajwa kuwa ni ndege kusafiri bila kujaza abiria kwa manufaa ya ndege za mashirika mengine.

Naibu Waziri huyu alisema hayo jana wakati akifungua kikao cha tatu cha Baraza la Wafanyakazi wa ATCL, akisema hujuma hizo zinazofanywa na baadhi ya watoa huduma wa ndege hizo si nzuri na kwamba lengo la Serikali ni kuwekeza kwa Watanzania wote ambao utazaa matunda.

Alisema amekuwa akipokea simu kutoka maeneo mbalimbali kuwa ndege zinaondoka bila kujaa hasa za mikoa ya Kilimanjaro na Mbeya kutokana na baadhi ya watoa huduma hususan mawakala wa tiketi kuwa na tabia ya kuonwa na uongozi wa mashirika mengine ya ndege, hivyo kuacha kuuza tiketi za ATCL na kudai ndege imejaa na baadae ndege kuondoka na abiria pungufu.

“Baadhi ya mawakala huwa wanaonwa na viongozi wa ndege zingine na kudai ndege zao yaani ATCL zimejaa wakati hazijajaa ili ndege zingine zijae,” alifichua Nditite na kuongeza:

“Sasa najiuliza kwanini hawajali ajira na mshahara wao na kutegemea fedha za muda mchache, na hawana uzalendo na nchi yao, tunahitaji tija na sio hujuma.”

Aidha, alisema ATCL imepewa dhamana ya kuhudumia Watanzania wote na kwamba na ndege mpya zinatoa huduma nzuri, chakula na maji bure wakati ndege zingine hazifanyi hivyo.

Alisema, Serikali imeweka kipaumbele katika uendeshaji wa ATCL ambapo hadi sasa imeshapewa ndege nne ambazo ni Dash 8 Q400 tatu, Boeing 787 Dreamliner moja na hivi karibuni wanategemea kupeleka ndege nyingine mbili aina ya Airbus 220-300 huku wakitegemea kupokea ndege nyingine mpya ya Boeing 787 Dreamliner mwakani.

Hivyo alisema ni mategemeo ya Serikali kuona ATCL inafanya vizuri na kwa viwango vya kimataifa kwa kuwa ni fahari ya Tanzania.

Pia aliutaka uongozi wa ATCL kuimarisha kitengo cha biashara ili hujuma hizo zidhibitiwe mara moja.

Kadhalika, aliwataka viongozi na wafanyakazi kufanya kazi kwa weledi na bidii kubwa hasa katika kipindi hiki chenye changamoto nyingi na ushindani kibiashara kwa kuzingatia kutoa huduma bora, kuitii Serikali, kufanya kazi kwa uadilifu, kuwajibika kwa umma, kuheshimu sheria zilizopo na kutunza siri za Serikali.

Alisema ikiwa baraza hilo litazingatia kufanya kazi kwa weledi litaweza kwenda sambamba na soko lililopo ili uwekezaji wa Tanzania uliokusudiwa uweze kuzaa matunda.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Ladislaus Matindi, alisema watahakikisha kitengo cha masoko na usalama wa ndani kinakuwa salama katika mifumo mbalimbali na kuendelea kuchukua hatua kwa mujibu wa maelekezo ya Waziri.

Matindi ambaye pia ni Mwenyekiti wa baraza hilo, alisema, mikakati ya shirika hilo ni kufanya biashara kwa kutoa huduma za kuvutia wasafiri.

Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power

$
0
0
Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power Kwaajili Ya Nguvu Za Kiuume Na Promix Kwaajili Ya Kuongeza Maumbile;
Kwa mwanaume aliyekamilika na mwenye Afya njema ili kumridhisha mke au mpenzi anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara mbili hapo utamridhisha mpenzi wako ila ukiwa unapiga moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe 

Tiba Ya Tatizo Lako Ni Dawa Hiitwayo Simpo Power No, 1; dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge vya miti shamba na unga ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja :-1 itakufanya urudie tendo zaidi ya mara tatu 
2 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-20 kwa tendo la Kwanza 
3 huimarisha uume uliolegea na kusinyaa 

Je Una Mke Au Mpenzi Aliyebalikiwa Kuwa Na Kario Kubwa Au Mwili Mnene Na Wewe Mume Wake Una   Maumbile Mafupu?; tumia sasa dawa ya PROMIX dawa itakufanya umfikishe shemu nyeti maana inaboresha maumbile saizi upendayo.

Dawa zangu haziina madhara yoyote kwa mtumiaji 

MARKSU; ni dawa ya kisukari dozi siku 21 
MWARU; ni dawa ya uzazi,hufungua milija ya uzazi ata kwa Wale waliofungiwa uzazi  
MTUNDUU; ni dawa ya busha bila kupasua 
MAZANZA; ni dawa ya kisukar zipo dawa za miguu Kuuma,tumbo,kupunguza Matiti,kutoa minyama uzembe ngiri,vidondo vya tumbo  

FIKA OFISINI KWANGU BUGURUNI MALAPA KARIBU NA KOTA ZA POLISI AU PIGA  SIMU ULETEWE MAHALI ULIPO SIMU NO 0783185060,  0752348593  -DR AGU

Habari Njema Kwa Wenye Matatizo Yafuatayo.

$
0
0

(1).fikiria ulianzia wapi?je,ulifanikiwa au bado?
(2).upo tayari kupona kwa haraka?

TIBA ZITOLEWAZO NI,
NGORO 4 POWER;Huongeza nguvu za kiume yenye mfumo wa unga na vidonge dozi siku(6).

MELAMELA;hurefusha         na kunenepesha maumbile ya kiume  ipo katika mfumo wa unga dozi siku (4).

KASELA;Hurudisha mke,mme,mchumba na hawara ndani ya siku mbili tu,atatimiza mahitaji yote hata Kama yupo mbali na kumfunga asiwe na mtu mwingine.

DUDUMA;Huongeza hips,makalio na mguu wa bia.

SWASWA;Hupunguza maziwa makubwa, kitambi, nyama uzembe, michirizi na muwasho sehem za Siri,na harufu mdomoni.

KOOLA;Hutibu magonjwa sugu ya zinaa, tumbo kujaa gesi,kuuma chini ya kitovu, kiuno ,fangasi za miguu, na kuvimba miguu au miguu kuwaka Moto.

Kwa hayo na mengineyo mfatilie DR.MBALU kwani ana uwezo wa kuhudumia ndani na nje ya TANZANIA.Kwa Dar es salaam anapatikana BUGURUNI MALAPA pia KAHAMA anapatikana MARUNGA.

 Kwa wasio na mda wa kufika ofisini kwangu Nina vijana wa kukuletea mpaka ulipo kazini ama nyumbani kwako.OFISI ZINAFUNGULIWA SAA 07 :00 ASUBUHI NA KUFUNGWA SAA 18:00 JION

       CONTACTS ;

               0716608959  NA 0767171773

  "WOTE MNAKARIBISHWA".DR   MBALU NI SULUHISHO LAKO.

Mabadiliko ya Rangi Katika Bendera ya Taifa na Wimbo wa Taifa

$
0
0
Wizara  ya Mambo ya Ndani ya Nchi, imetoa maelekezo juu ya matumizi ya wimbo wa taifa na mabadiliko ya rangi ya bendera ya taifa kuwa itakuwa ya dhahabu na si manjano kama ilivyozoeleka.

Hayo yamebainika baada ya wizara kutoa maagizo kwa vyuo na taasisi kuhusiana na matumizi ya tunu hizo za taifa.

Pia barua hiyo ilisisitiza kuwa rangi sahihi za bendera ya taifa kuwa ni kijani, dhahabu, nyeusi na bluu na kusisitiza kwamba ni makosa kutumia rangi ya njano.

Maelekezo hayo yametolewa kwa wakuu wa vyuo vya ualimu, vyuo vya maendeleo ya jamii, wakuu wa vyuo vikuu na vyuo vikuu vishiriki na taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.

Kwa mujibu wa barua hiyo, iliyotolewa Novemba 23, mwaka huu na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambayo jana ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii, maelekezo hayo yameletwa kwa sababu imebainika kuwa taasisi za serikali zinatumia isivyo sahihi alama za taifa.

Ofisa Habari wa Wizara ya Elimu, Mwasu Sware, alithibitisha kwamba barua hiyo ni yao na kuomba watafute Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kwa maelezo zaidi ya kwa nini imesambaa mtandaoni.
 
Barua hiyo ambayo iliandikwa na wizara ikiwa na muhuri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ilisema Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, inaelekeza kuwa Wimbo wa Taifa utapigwa kwa dhifa za kitaifa pekee.

“Endapo hadhi ya sherehe haitambuliki, taasisi inalazimika kuomba kibali kwa waziri mwenye dhamana. Wimbo unatakiwa kuimbwa kwa ukamilifu beti zote mbili kwa kuzingatia ‘nota’ na maneno.

Kadhalika barua hiyo ilisema kuwa uwiano wa bendera ni theluthi katika urefu na upana.

Je Unapata Pesa Lakini Hujui Iendako Au umetupiwa Jini Chuma Ulete....Bofya Hapa Kupata Suluhu

$
0
0
Je Unapata Pesa Lakini Hujui Iendako Au umetupiwa Jini Chuma Ulete Na Tambua Jinsi Nyota Yako Inavyoweza Kutembelewa Na Watu Bila Wewe Kujijua:Kutana mganga wa tiba asili ambaye anatumia kipaji chake alichajaliwa na muumba wake... anatumia kioo cha asili kutibu magonjwa sugu yaliyoshindikana ata kama upo mbali 

Je Unauza Mali Zako Kama Vile Gari,nyumba,shamba,au Kiwanja lakini havihuziki? wasiliana na Mimi Leo uweze kuona nguvu ya maajabu ili mpaka vitu Mali iyo iwe ni yako halali isiwe na malalamiko hakika mungu atatia mkono wake. 

Je Umepotelewa Na Pesa Au Mali Yako Au Ndugu Yako Aliyepotea Kimiujiza Na Hujui Alipo? Acha kukata tamaa kipo kioo cha asili kitakulejea kile kilichopokea bila masharti magumu 

Je Unahitaji Kupata Mafanikio Bila Kutoa Kafara Au Unahitaji Pesa Za Majini?  acha kuogopa sasa wapo wengi waliokuwa hawaamini kama wewe ila kwa sasa wanamiliki pesa,majumba ya kifahar,maduka ya jumla,pamoja na viwanda kumbuka kuwa uwoga wako ndio umasikini wako na hakuna anayefanikiwa bila kuwa jasiri 

Je Umeachwa Na Mke Au Mme Au Unampenda Lakini Yeye Hakutaki ? onana Leo na chifu Ruyamba ili aweze kukupatanisha na mpenzi wako ndani ya Massa sita 6 tu atakuelewa 

Je Umegombana Na Bosi Wako Au Unataka Kupandishwa Cheo Au Wewe Ni Mpenzi Wa Kucheza Bahati Nasibu? acha kujiona mpweke utapatiwa Pete au saa itakayoendana na shughuli yako unamdai mtu ataki kukulipa au unakesi mahakamani ujui cha kufanya CHIFU RUYAMBA NDIO SURUHISHO WA YOTE .Hata kama ujawai pata mtoto uzazi wako utafunguliwa pia natibu kisukari,presha,busha bila kupasua,nguvu za kiume,na kuongeza maumbile ya kiume  saizi upendayo 

OFISI INAFUNGULIWA SAA MBILI ASubui adi saa mbili usiku na kwa sasa CHIFU RUYAMBA KAANZA  ZIARA MIKOANI PIGA SIMU 0764638796

Kutana Na Dr Chikago Bingwa Na Mwokozi Kwa Waliosumbuka Na Magonjwa Bila Mafanikio

$
0
0
Ninauwezo wa kumrudisha mume, mke ,mchumba, hawara, mtu unaempenda ndani ya masaa mawili tu (2) na kumfunga asiwe na mtu mwingine zaidi yako na kumfanya akutimizie kilakitu unachokihitaji kutoka kwake hata km yupo mbali na atatulia kabisa

GALIMBO 3 MIX;  nidawa ya mitishamba iliyitengenezwa kwa kwa utabibu wa hali ya juu kwakuchanganya miti na matundatiba , Huogeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15 -85 ) , inakomaza zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakat wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaid ya Mara tatu bila ham kuisha wara kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-40.

YOLANI :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inch (6-8) na unene wa sm (3-4)

Matatizo haya husababishwa na mambo mbalimbali km upigaji wa punyeto, kisukali,  vidonda vya tumbo, tumbo kuunguluma na kujaa gesi, ngili, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani, maumivu ya mgongo ama kiuno, namengineyo mengi  (nk )

SUPER MBUKE :- nidawa inayotatua tatizo la kisukali na kupona kabisa Kwa mda mfupi sana na utakuwa na uwezo wakula chakula chochote chenye sukali baada ya kupona,

vilevile ninadawa ya uzazi kwa akina Mama na akina Baba, kurudisha mali iliyopotea kwamda mfupi sana, vidonda vya tumbo, kaswende,presha,chango la uzazi, gono,nyama uzembe, kusafisha nyota, kuzuia majini wachafu, kinga ya mwili, kuuza vitu bila kununuliwa, dawa za biashara, pesa nyingi (utajili)  mambo ya kes nk

Kwa huduma n msaada wasiliana na Dr CHIKAGO atakusaidia hatakama ulikata tamaa utarudisha furaha yako

Napatikana Dar es salaam  sm no 0743543944   /0620510598

Nb :km huna nafasi ya kufika ofisin huduma hii itakufikia popote ulipo kwawatu wa mkoani tunatuma kwanjia ya mabasi.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

Majengo ya tume ya uchaguzi DRC Yateketea Kwa Moto.....Zilikuwa Zimesalia Siku 10 tu Kabla ya Uchaguzi Kufanyika

$
0
0
IKIWA Zimesalia Siku 10 kabla ya kufanyika Uchaguzi Mkuu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), vifaa vyote vya uchaguzi vilivyokuwa vimehifadhiwa kwenye ghala mjini Kinshasa vimetetea kwa moto hali inayozusha wasiwasi kuhusu kufanyika kwa uchaguzi huo Desemba 23, 2018

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa tume hiyo, moto huo ulianza kuwaka saa 8 za usiku kwa saa za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kuteketeza vifaa zaidi ya 7000 yakiwemo magari ikiwa ni siku 10 tu kabla ya uchaguzi.

Vyombo vya habari nchini humo vimeripoti kuwa, mashuhuda wa tukio hilo wameeleza kwamba kabla ya moto huo kuwaka kulisikika mlipuko ambao unaaminika ndio chanzo cha moto.

Uchaguzi wa Disemba 23 nchini DRC umegubigwa na vurugu za kila namna ambapo jana watu wawili waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa wakati Jeshi la Polisi likikabiliana na wafuasi wa mgombea wa upinzani Martin Fayulu katika Mji wa Kalemie.

Rais Joseph Kabila alisema kuwa ataondoka madarakani baada ya uchaguzi wa Disemba 23 wa kumtafuta mrithi wake, lakini akaeleza kuwa angebaki kwenye siasa na huenda akagombea tena huko mbeleni.

Mamlaka ya Rais Kabila aliyeiongoza DR Congo tangu mwaka 2001 baada ya kuuawa kwa baba yake, Laurent Kabila yalikoma mwaka 2016, lakini amekuwa akichelewesha uchaguzi, jambo ambalo limesababisha machafuko nchini humo.

Tume ya uchaguzi ilisema imekuwa vigumu kufanyika kwa uchaguzi kwa wakati nchini humo kutokana na changamoto za kuwaandikisha wapiga kura kunakochangiwa na uharibifu wa miundombinu na vita katika ukanda wa mashariki wa nchi hiyo.

Tangu ilipopata uhuru kutoka kwa Ubelgiji mwaka 1960, DR Congo haikuwahi kuwa na makabidhiano ya amani ya madaraka.

Kufuatia kuungua moto vifaa vya uchaguzi, watu wengi wanaamini kuwa tukio hilo linaweza kusababisha uchaguzi wa Disemba 23 kutofanyika tena kama ilivyopangwa, na Rais Kabila ataendelea kusalia madarakani.

Waziri Mkuu kuzindua chaneli mpya ya utalii

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa anatarajiwa kuzindua chaneli mpya ya utalii itakayojulikana kama ‘Tanzania Safari Channel’ iliyoanzishwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Mkurugenzi wa TBC, Dk  Ayub Rioba amesema Rais Magufuli aliwapa wazo hilo mwaka jana.

Uzinduzi huo utafanyika Jumamosi Desemba 15, makao makuu ya TBC, Mikocheni, Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa TBC, Dk  Ayub Rioba  akizungumza na waandishi wa habari leo Desemba 13 amesema chaneli hiyo itakuwa na vipindi vya vivutio mbalimbali vya utalii  nchini.

Amesema uzinduzi rasmi wa chaneli hiyo utafanyika Jumamosi ukiongozwa na waziri mkuu, Kassim Majaliwa.

"Vipindi hivyo vitakuwa vinatoka kwa taasisi na wadau mbalimbali ikiwamo wa utalii, watozi (producers) wa ndani wa TBC, watozi binafsi wa ndani na nje na vile vinavyotengenezwa kwa pamoja na vyombo vingine vya utangazaji vya utalii (co-production)” amesema.

"Mchakato wa kuanzisha chaneli hii ulihusisha pia mikutano na wadau wa sekta binafsi  ambao wanashughulika na masuala ya utalii,"

Amesema Rais John Magufuli alitoa wazo hilo alipotembelea makao makuu ya ofisi hizo mwaka jana ambapo uongozi wa TBC pia ilikuwa imeshaanza mchakato huo.

 "Chaneli hii itakuwa inatangaza vivutio mbalimbali vya utalii nchini na kwa kuanza itaonekana kwenye king'amuzi cha Startimes,” amesema.

Amesema mipango iliyopo ni chaneli hiyo kuanza kuonekana kwenye satellite kwani lengo ni kuonekana katika nchi nyingi duniani ili kuvutia watalii wengi wa ndani na nje ya nchi.

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 44

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588 
ILIPOISHIA   
   
Tukaingia katika awamu ya pili ya mazoezi ya taikondo. Mazoezi haya hakika ni magumu kuliko hata kukimbia katika msitu wa eneo hili. Zaidi ya masaa mawili saa Jojo na Danya wakawa wanatufundisha mazoezi haya ambayo hakika hadi tunamaliza wote watatu viungo vyetu vimeorojeka kwa kuchoka na kuapa majera kadhaa yaliyo tokana na kukosa umakini.
“Camila”
Nilimuita Camila huku tukiwa ndani ya chumba chetu, kwa maumivu niliyo nayo nikajikuta hata nikishindwa kulala kitandani.
“Mmmmm”       
“Mimi nahitaji kutoroka, siwezi kuendelea kukaa hapa”
“Mmmm…….”
“Ndio nahitaji kutoroka, maisha gani haya ya mateso naomba ujumuike nami mke wangu na tutoroke wote”
“Umewasahaua wale Simba na wanayama wengine humu msituni ehee?”

ENDELEA   
Nikakaa kimya huku nikimtazama Camila usoni mwake. Ukiachilia Simba na wanyama wengine ambao wapo katika msitu huu, ila kusema kweli hatufahamu ni wapi tulipo.
“Mume wangu wewe ni mwanaume, hakuna haja ya kukimbia mazoezi, tena ikiwa wewe ni mchezaji mpira, tena mchezaji ambaye dunia kwa sasa ina kutazama. Tafadhali nina kuomba mume wangu tuwe wavumilivu, siku na muda wa kuondoka utakapo fika basi tutaondoka”
 
“Nimekuja huku ili niwe mtalii wa kujua mambo mbalimbali ila si kuja kuwa mwanajeshi?”
“Jamani mume wangu, umesahau tabu na ngija ngija tulizo pata na kama ingekuwa si Ethan, haki ya Mungu nina apia leo sijui tungekuwa wapi?”
“Kwa hiyo unahitaji tuendelee kuwa wanajeshi wa hiyari ehee?”
“Sio wanajeshi wa hiyari mume wangu ila tunajilinda sisi wenyewe bwana”
“Sawa”
“Usiseme sawa kinyonge jamani”
Camila alizungumza huku akinikumbatia, ila kwa maumivu makali ya mwilini mwangu nikajikuta nikimsogeza pembeni kidogo.
 
“Nini”
“Mwili wote unauma bwana mke wangu”
“Hahaa hata nikikupa sasa hivi utashindwa?”
“Ndio”
 “Hahaa kweli umeshindwa mume wangu”
Camila alizungumza huku akicheka sana jambo lililo nifanya nimtazame kwa macho ya masikitiko. Usingizi ukanipitia taratibu, alfajiri na mapema kama kawaida tukaamshwa ili kufanya mazoezi kama kawaida.
“Yule jamaa yupo wapi?”
Nilimuuliza Jojo mara baaya ya kujikuta tupo wanne tu katika uwanaja wa mazoezi.
“Yupo kazini”
“Kazini kivipi?”
“Ni mfanyakazi wa moja ya benk katika hii nchi, ila siku mbili hivi atarejea”
“Sawa”
Tukaendelea kufanya mazoezi japo siku ya leo hayakuwa m agumu sana. Baada ya masaa mawili ya mazoezi tukaruhusiwa kuendelea kwa mamabo mengine binafsi.
“Ninaweza kuzungumza na baba yangu?”
 
“Kwa kutumia video call au?”
“Kama itawezekana”
“Sawa twendeni huku”
Jojo alizungumza huku tukianza kumfwata kwa nyuma. Tukaingia kwenye moja ya chumba kama ofisi, tukakuta moja ya computer kubwa kiasi. Akaiwasha na akaanza kufanya mawasiliano na baba Camila, baada ya muda kidogo akapokea msaidizi wa baba Camila.
“Hei Jonson”
Camila alizungumza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana usoni mwake.
“Hei Camila vipi upo  wapi?”
“Mmmm, nipo mbali kidogo. Ninaweza kumpata baba”
“Yupo kwenye kampeni ana hutubia kama upo karibu unaweza kuwasha televishion kumtazama jinsi anavyo hutubia”
“Ohoo inachukua muda gani?”
“Kama dakika ishirini hivi”
“Ninaweza kumsubiri nina hitaji kuzungumza naye sana”
“Sawa, akitoka basi nitamfahamisha na atawasiliana nawe”
“Sawa sawa”
 
Tukaendelea kukaa ndani ya ofisi hii kwa zaidi ya nusu saa, ndipo baba Camila akapatikana.
“Habari zenu vijana wangu”
Baba Camila alizungumza huku akiwa amejawa na furaha. Jojo akatoka ofisi humu na kutuacha sisi wawili.
“Salama tu baba, vipi kampeni zako zinaendaje?”
“Zinakwenda vizuri na kupotea kwenu kunazidi kuwapa wananchi hasira ya kuhitaji mimi niiingie madarakani ili niweze kukomesha utekaji ambao unaendelea”
“Mmmmm watu wana masikitiko?”
“Yaa wana masikitiko makubwa sana”
“Muheshimiwa samahani kidogo kwa kuwaingilia mazungumzo yenu”
“Hakuna shida Ethan, zungumza tu”
“Vipi familia yangua umeweza kuitembelea au kuwajulia hali?”
 
“Ndio nilizunguza na Mery pamoja na bi Jane Klopp na wapo salama na niliwaeleza juu ya usalama wenu”
“Nashukuru sana baba”
“Vipi Ethan mbona uso wako kama una kovu kidogo hapo usoni mwako”
“Baba huku tulipo yaani ni zaidi ya jeshini”
“Jeshini”
“Hapana baba Ethan ni uoga wake tu baba”
“Hapana baba yaani huku tunapewa mafunzo makali kiasi cha kujikuta ninapachukia huku sana”
“Baba, mume wangu na umahiri wake wote uwanjani ila anaogopa sana. Baba niamini tupo sehemu salama, naamini tukirudi tutakuwa fiti zaidi ya fiti”
Nikamaki nikimtazama Camila kwa macho ya mshangao, tukamaliza kuzunumza na baba yake kisha tukatoka ofisini humu. Tukakuta Dany aiwa amesha kifungua kinywa. Akatukaribisha mezani na tukaanza kupata kifunga kinywa.
“Leo jiandaeni tunakwenda kutembea”
“Wapi?”
Niliuliza kwa shahuku nikimtazama Dany usoni mwake.
“Nitawaambia baadaye ila mujiweke tayari kwa safari”
“Sawa muheshimiwa”
 
Tukamaliza kupata kifungua kinywa na kurudi chumbani kwetu. Camila akaanza kuvua nguo zake huku akiwa amenipa mgongo.
                                                                                                                     ***
    Tukakapewa nguo za kuondoka eneo hili kuelekea kwenye safari ambayo Dany alituahidi kwamba tunaweza kuondoka. Tulipo hakikisha  kwamba tumemaliza kujianda safari ya kuondoka aneo hili ikaanza.
“Tunaelekea wapi?”
“Kuna jambo moja nahitaji kulifanya kwa ajili ya kipaji chako”
“Mmmm”
“Camila mbona unaguna?”
“Kama tunakwenda kwenye uwanja wa mpira nahisi ni jambo la hatari  sana”
 
“Kwa nini?”
“Maadui zetu wanatuwinda”
“Mukiwa nasi hakuna adui yoote ambaye atawadhuru”
Jojo alitujibu huku akitugeukia.
“Kivipi?”
“Musijali nyinyi kuweni na amani tu”
Safari hii ikatugarimu saa moja na nusu hivi, tukafika kwenye moja ya mji mmoja wenye milima mingi na ulio jengeka vizuri kiasi.
“Hapa ni wapi?”
“Hili  eneo linaitwa Lushoto, kuna timu ya taifa chini ya miaka kumi na nane wamekuja kuweka kambi hapa kijiandaa na michuano ya kombe la dunia chini ya vijana wenye umri miaka kumi na nane.”
Dany alizungumza huku akisimamisha gari hili kwenye jengo moja la hoteli.
“Unahitaji mume wangu achezee timu ya taifa ya Tanzania ikiwa ana uraia wa Ujerumani”
 
“Ethan sio mjerumani ni Mtanzania halisi, baba na mama yake ni Watanzania. Ameishi Ujerumani kwa ajili ya matatizo ya hapa na pale”
Camila akanitazama usoni mwangu huku akiwa na masikitiko kiasi kwani kucheza mpira katika timu ya taifa ya Tanzania, basi sinto weza kucheza tena katika nchi ya Ujerumani na hii pia inaweza kuathiri kampeni za baba Camila kwa maana hata tangazo nililo lifanya la kisiasa linaashiria kwamba mimi ni Mjerumani.
“Dany samahani kidogo naomba tuzungumze”
Nilimuambia Dany huku nikisogea pembeni kidogo huku nikimtzama usoni mwake. Dany bila kujali umri wangu akanifwata sehemu nilipo simama.
“Ndio Ethan”
“Natambua kwamba mimi ni Mtanzania”
“Ndio”
“Ila kichwa changu hakina kumbukumbu yoyote kuhusiana na hii nchi hususani familia yangu. Sasa itawezekaje niweze kuichezea hii nchi ikiwa sijakua nchini hapa?”
“Kukua au kuto kulia katika nchi hii hilo sio tatizo”
“Ila”
 
“Ila fwata chimbuko la wazazi wako”
“Mimi sina kumbukumbu yoyote juu ya wazazi wangu, nitafwata chimbuko langu kivipi sasa?”
“Huna kumbukumbu za wazazi wako?”
“Ndio”
Jojo akatufwata hapa tulipo simama huku akiwa na sura ya tabasamu.
“Ethan”
“Mmmm”
“Huna kumbukumbu yoyote na wazazi wako?”
“Ndio”
“Unahitaji kufahamu ni kitu gani kilicho wapata?”
“Ndio”
Jojo akanisogelea na kunishika kichwani mwangu, nikahisi ubaridi mkali ambao taratibu katika ufahamu wangu wa akili nikaanza kuona ngurumo za radi huku mvua nyingi ikinyesha. Kumbukumbu zangu zikazidi kusonga mbele na kumuona mzee mmoja akiwa amezungukwa na kundi kubwa la vijana huku  wakimshambulia kwa kumpiga kwa magongo pamoja na mateke huku wakihitaji afariki dunia.

ITAENDELEA KESHO
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images