Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

TAKUKURU Yakomboa Mabilioni ya Pesa

0
0
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imedai katika kipindi cha hivi karibuni taasisi hiyo imefanikiwa kushinda kesi zake mbalimbali tofauti na ilivyokuwa kipindi cha nyuma ambapo kesi nyingi zilikuwa ikipigwa chini.


Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU nchini, Diwani Athuman, katika kipindi cha mwaka mmoja taasisi hiyo imeokoa Sh 70.3 bilioni zilizokuwa ziingie mifukoni mwa wala rushwa.

Diwani Athuman ameyasema hayo jana Jumanne Disemba 11, 2018 Jijini Dodoma katika ufunguzi wa mkutano mkuu wa makamanda wa taasisi hiyo wa mikoa na maofisa wake mbalimbali ambapo amesema mapambano dhidi ya rushwa bado ni vita kubwa inayohitaji ujasiri.

Aidha amesema katika kipindi cha mwaka mmoja kesi 495 zimefunguliwa na nyingi kati ya hizo wameshinda.

Diwani amesema katika uongozi wake wa miezi mitatu ndani ya taasisi hiyo amebadili mfumo wa utendaji na mtazamo, na kwamba anashirikiana na wenzake kuwapeleka watu mahakamani bila kuzingatia ukubwa wala muonekano wa nafasi zao.

Hivi karibuni Taasisi hiyo ilimuita kiongozi Mkuu wa Chama ACT - Wazalendo Zitto Kabwe kwa ajili ya mahojiano juu ya kutoa taarifa za rushwa na uhujumu wa miradi ya makaa ya mawe na chuma ya Mchuchuma na Liganga.


Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power

0
0
Okoa Ndoa Yako Sasa Kwa Kutumia Dawa Hii Iitwayo Simpo Power Kwaajili Ya Nguvu Za Kiuume Na Promix Kwaajili Ya Kuongeza Maumbile;
Kwa mwanaume aliyekamilika na mwenye Afya njema ili kumridhisha mke au mpenzi anatakiwa awe na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara mbili hapo utamridhisha mpenzi wako ila ukiwa unapiga moja au mbili hapo ujue umejilidhisha wewe 

Tiba Ya Tatizo Lako Ni Dawa Hiitwayo Simpo Power No, 1; dawa hii ipo kwenye mfumo wa vidonge vya miti shamba na unga ambayo hutibu matatizo matatu kwa pamoja :-1 itakufanya urudie tendo zaidi ya mara tatu 
2 itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-20 kwa tendo la Kwanza 
3 huimarisha uume uliolegea na kusinyaa 

Je Una Mke Au Mpenzi Aliyebalikiwa Kuwa Na Kario Kubwa Au Mwili Mnene Na Wewe Mume Wake Una   Maumbile Mafupu?; tumia sasa dawa ya PROMIX dawa itakufanya umfikishe shemu nyeti maana inaboresha maumbile saizi upendayo.

Dawa zangu haziina madhara yoyote kwa mtumiaji 

MARKSU; ni dawa ya kisukari dozi siku 21 
MWARU; ni dawa ya uzazi,hufungua milija ya uzazi ata kwa Wale waliofungiwa uzazi  
MTUNDUU; ni dawa ya busha bila kupasua 
MAZANZA; ni dawa ya kisukar zipo dawa za miguu Kuuma,tumbo,kupunguza Matiti,kutoa minyama uzembe ngiri,vidondo vya tumbo  

FIKA OFISINI KWANGU BUGURUNI MALAPA KARIBU NA KOTA ZA POLISI AU PIGA  SIMU ULETEWE MAHALI ULIPO SIMU NO 0783185060,  0752348593  -DR AGU

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH....Anatoa Pete za Bahati, Anasafisha Nyota, Anazuia Chuma Ulete na Mengine

0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam Shariff,  Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
 
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Adam Shariff Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. 

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Mawasiliaono: +255715971688  au +255756914036
 
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

LIVE: Rais Magufuli akitia saini kwenye mradi wa Stiglers Gorge

0
0
Rais Magufuli leo Jumatano, Desemba 12, 2018 anaaza safari ya kutimiza ndoto ya Mwalimu Nyerere kwa kusaini mkataba wa Mradi Stiglers Gorge. Tazama Live hapo chini akitia Saini.

Gwajima, Lusekelo Wamwaga Maombi IKULU

0
0
Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima na Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC), Anthony Lusekelo leo Jumatano Desemba 12, 2018 wameungana na Rais John Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.

Leo Rais Magufuli anasaini mkataba wa ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme katika Pori la Akiba la Selous wa Stiegler’s Gorge na viongozi hao wa dini wamekuwa miongoni wa viongozi mbalimbali wa dini waliohudhuria hafla hiyo.

Kabla ya kuanza kwa hafla hiyo, viongozi hao wa dini walianza kwa kufanya maombi kila mmoja.

Gwajima amemuomba Mungu awawezeshe  nguvu wote wanaofanya kazi na Rais John Magufuli, Makamu wa Rais, Samia Suluhu,  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, mawaziri na watumishi wote wa serikali.

“Nafunga kila kazi zenye kukwamisha mradi wa Stiegler’s Gorge, ukiwemo wizi, rushwa, maneno ya kuvunja moyo; nayazuia katika jina la Yesu na kila mmoja katika nafasi yake atiwe nguvu,” ameomba Gwajima

Kesi ya Kusambaza Picha za Uchi za Wema Sepetu kusikilizwa tena Januari 28, 2019

0
0
Kesi ya kusambaza picha za utupu inayomkabili Miss Tanzania 2016, Wema Sepetu imetajwa leo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam.

Upande wa Jamhuri umedai upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika.

Hayo yamedaiwa leo Decemba 12 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Wakili wa Serikali, Mosia Kaima, wakati kesi hiyo ilipotajwa mbele ya Hakimu Mkazi, Maira Kasonde kwa ajili ya kutajwa.

Kaima aliiomba mahakama ipange tarehe nyingine ya kuitaja ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la.

Hakimu Masonde baada ya kusikiliza maelezo hayo aliiahirisha kesi hiyo hadi Januari 28 mwakani, itakapotajwa tena.

Katika kesi hiyo, Wema anadaiwa kuwa Oktoba 15, mwaka huu katika maeneo mbali mbali ya jiji la Dar es Salaam alichapisha video ya ngono na kusambaza katika mtandao wake wa kijamii wa Instagram.

Taasisi za Umma Zashauriwa Kuwa na Akaunti za Makusanyo Kwenye Benki Zaidi ya Moja

0
0
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Taasisi za Umma zimeshauriwa kuwa na akaunti za makusanyo kwenye benki zaidi ya moja kati ya benki zilizoungwa na Mfumo wa Serikali wa Ulipaji wa Kielektroniki (GePG) ili kuwarahisishia walipaji wa huduma za serikali.

Ushauri huo umetolewa leo jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango wakati akifungua mkutano wa mwaka wa watumiaji wa mfumo wa GePG katika ukusanyaji wa fedha za umma uliozishirikisha taasisi za Umma zinazotumia Mfumo huo pamoja na timu ya GePG kwa ajili ya kujengeana uwezo wa namna bora ya kutumia mfumo huo.

Dkt. Mpango amesema kuwa utaratibu wa malipo kupitia GePG unatoa fursa ya kuwa na njia nyingi za kulipia fedha za umma pamoja na kuwapa walipaji wa huduma za serikali utaratibu rafiki na machaguo mengi ya kufanya malipo.

“Kwa kuwa malipo yote yanayopitia GePG hayatozwi ada za miamala na benki hizo hivyo kuongeza akaunti za makusanyo katika benki hakutoongeza gharama za miamala kwa taasisi za umma bali kufanya hivyo kutaondoa hatari ya Ofisi husika kukosa huduma ya malipo endapo benki inayotumika itashindwa kutoa huduma kwa sababu mbalimbali”, alisema Dkt. Mpango.

Dkt. Mpango ameongeza kuwa utaratibu huo wa makusanyo kupitia GePG unaenda sambamba na utekelezaji wa maelekezo mengine ya Serikali yanayohusu makusanyo ikiwemo yale yanayotaka akaunti kuu za makusanyo za taasisi za umma kuwepo benki kuu ya Tanzania (BoT).

Aidha, Waziri Mpango amezitaja baadhi ya faida za mfumo huo zikiwezo za kuongezeka kwa uwazi na udhibiti katika ukusanyaji wa fedha za umma, kupata taarifa sahihi na kwa wakati zinazohusu makusanyo pamoja na kuwa na viwango na utaratibu unaofanana katika ukusanyaji wa fedha za umma kwa taasisi zote za umma.

Vile vile, mfumo huo unachochea ubunifu katika ukusanyaji wa pesa za Serikali na sekta ya fedha kwa ujumla kwa kuweka mazingira rafiki na ya usawa kwa wakusanyaji, kutoa huduma bora na rahisi ya malipo ya fedha za umma pamoja na kusaidia fedha kufika haraka katika akaunti kuu za makusanyo za taasisi.

Amezikumbusha taasisi ambazo bado hazijajiunga na mfumo wa GePG kuwa ifikapo Juni 30 mwaka 2019 hakutokuwa na fedha yoyote ya umma itakayokusanywa nje ya mfumo huo, hivyo wakati wa kujiunga na kuunganisha mifumo yao na mfumo huo ni sasa.

Mnamo Juni 2017, Serikali iliifanyia marekebisho sheria ya Fedha za Umma (PFA) ya mwaka 2001 na kuiongezea kipengele kinachotaka fedha zote za umma zikusanywe kupitia Mfumo wa Government e-Payment Gateway (GePG), hadi sasa jumla ya Benki 11 na mitandao sita ya malipo kwa njia ya simu za kiganjani zimeunganishwa na mfumo huo.

Vigogo watano wa Chama Kikuu cha Wakulima wa Tumbaku (WETCU) Wahukumiwa Miaka Minne Jela

0
0
Na Mwandishi Wetu
Waliokuwa  vigogo watano wa Chama Kikuu cha Wakulima wa Tumbaku Kanda ya Magharibi (WETCU), wamehukumiwa kutumikia kifungo cha miaka minne kila mmoja, baada ya kutiwa hatiani kwa makosa mawili likiwemo la kukisababishia chama hicho hasara ya zaidi sh. milioni 109.

Hata hivyo, vigogo hao ambao walitiwa hatiani na Mahakama ya Wilaya ya Tabora, mbele ya Hakimu Mkazi, Tengwa Chiganga na kupewa adhabu hiyo, watatumikia kifungo cha miaka miwili gerezani kutokana na adhabu za kifungo zinakwenda sambamba.

Waliotiwa hatiani na kupewa adhabu hiyo ni  waliokuwa mwenyekiti wa chama hicho, Mkandala Mkandala, Kaimu Meneja Mkuu John Kusanja, Mhasibu mkuu Prosper Mbacho, Francis Mpeta na  Makamu Mwenyekiti Msafiri Ngassa ambao walipelekwa katika gereza la Uyui kuanza kutumia adhabu ya kifungo jela.

Wakati vigogo hao wakitiwa hatiani na kupewa adhabu hiyo, mahakama hiyo iliwaachia huru washitakiwa wawili katika kesi hiyo Hamza Kapela na mfanyabiashara Faraz Abbas ama Faraz Yaseen Abbasi, kutokana na upande wa jamhuri kushindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yao pasi na kuacha shaka yoyote.

Washitakiwa hao walikuwa wakikabiliwa na mashitaka manne ambayo ni kula njama ya kutenda kosa, kughushi, matumizi mabaya ya madaraka kwa kununua gari aina ya Toyota Land Cruiser V8 bila kupata kibali kutoka kwa Mrajisi wa Vyama vya Ushirika nchini na kukisababishia chama hicho hasara ya sh. 109,010,000 kutokana na kununua gari  hilo.

Akisoma hukumu hiyo mapema wiki hii, Hakimu Chiganga alisema wakati wa usikilizwaji wa shauri hilo upande wa jamhuri ulileta mashahidi 16 na vielelezo 16.

Alisema upande  wa jamhuri umeweza kudhibitisha mashitaka mawili bila ya kuacha shaka yoyote dhidi ya washitakiwa  Mkandala, Kusanja,  Mbacho,  Mpeta na Ngassa.

Hakimu Chiganga aliyataja makosa hayo kuwa ni  matumizi mabaya ya ofisi kwa kununua gari chakavu lenye thamani kubwa kuliko lililopitishwa na WETCU na kukisababishia chama hicho hasara.

Alisema kutokana na hilo, mahakama inawatia hatiani washitakiwa hao watano. Hata hivyo, alisema upande wa jamhuri umeshindwa kuthibitisha mashitaka dhidi ya washitakiwa Faraz na Kapela hivyo wanaachiwa huru.

Akitoa adhabu, Hakimu Chiganga alisema shitaka la kwanza la matumizi mabaya ya ofisi kila mshitakiwa atatumikia kifungo cha miaka miwili jela na la pili la kukisababishia chama hicho hasara  kila mshitakiwa atatumikia kifungo cha miaka miwili jela, adhabu ambazo zitakwenda sambamba.

Baada ya kutolewa kwa adhabu hiyo, upande wa jamhuri ukiwakilishwa na mawakili wa serikali waandamizi, Shadrack Kimaro, Juma Masanja na Wakili wa Serikali, Tumaini Ocharo walisema hawajaridhika na adhabu hiyo, hivyo waliwasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufani.

Washitakiwa hao katika kesi hiyo, walikuwa wakiwakilishwa na mawakili Hassan Kilingo na Kanani Chombala. Vigogo hao wa WETCU walikamatwa baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuamuru ambapo iligundulika walinunua gari chakavu kwa bei ya gari jipya na kinyume na uamuzi wa mkutano mkuu wa chama hicho ambao uliamuru kununuliwa gari kwa thamani y ash. milioni 40 na mrajisi wa vyama vya ushirika aliridhia.

Inadaiwa washitakiwa hao walinunua gari hilo kwa mfanyabiashara Faraz ambapo nyaraka za gari zinaonesha ni la mwaka 2008, lakini wao walighushi kadi na kuonesha la mwaka 2014 na likauzwa kwa sh. 269,010,000.

Machi 16, 2017, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alimuagiza  Kamanda wa Polisi, Mkoa wa  Tabora kuwakamata viongozi wanne wa Chama Kikuu cha Ushirika wa  Tumbaku (WETCU) na kufunga ofisi za chama hicho hadi uchunguzi wa tuhumaza ubadhirifu wa fedha za chama hicho utakapokamilika.

Pia, Waziri Mkuu alivunja Bodi ya WETCU na  Bodi ya Tumbaku Tanzania  – TTB kwa sababu ya kushindwa  kusimamia zao hilo pamoja na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Waziri Mkuu alitoa  maagizo hayo  katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Isike Mwanakiyungi mkoani Tabora, ambapo alisema  Rais Dk. John Magufuli ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa TTB, Vita Kawawa  na Mtendaji Mkuu wa Bodi hiyo  Wilfred Mushi.

Viongozi wa WETCU ambao Waziri Mkuu aliagiza wakamatwe ni Mwenyekiti Mkandala, Makamu Mwenyekiti. Msafiri Kassim, Mkaguzi wa Ndani na Mhasibu  Mkuu. Pia aliwasimamisha kazi watumishi wa kitengo cha uhasibu wa chama hicho hadi uchunguzi utakapokamilika.

“Kuanzia sasa watumishi wote wa kitengo cha uhasibu pamoja menejimenti nimewasimamisha kazi pamoja na Mrajisi wa mkoa wa Tabora Deogratius Rugangila. Kamanda hakikisha ofisi hazifunguliwi kuanzia sasa hadi hapo timu ya ukaguzi  itakapokamilisha kazi yake,” amesisitiza.

Waziri Mkuu alisema kwa muda mrefu wakulima wameteseka na zao hilo kukosa tija kwa sababu ya usimamizi mbovu wa viongozi wa ushirika na Bodi ya Tumbaku Tanzania jambo ambalo Serikali haiwezi kulivumilia.

“Hatuwezi kuwa na ushirika ambao hauwasaidii wanachama. WETCU walipokea sh. bilioni 15 ambazo walizikatia risiti na hazijaonekana. Pia waliwalipa wazabuni sh, bilioni 10 ambazo hawajazikatia risiti,”.

“Wakati wanachama ambao ni wakulima wakiendelea kutesema WETCU walinunua gari la sh. milioni 269 kinyume na na maelekezo ya Mkutano Mkuu wa wadau ambao ulipitisha zitumike shilingi milioni 40 tu,” alisema.

Waziri Mkuu alisema  chama hicho kimesababisha kupungua kwa uzalishaji kwa kiasi kikubwa kutokana nakuwa na menejimemti mbovu jambo ambalo limechangia wakulima wa tumbaku kukosa tija.

Amesema WETCU kimekithiri kwa matumizi mabaya ya fedha ambapo alitolea mfano suala la ukarabati wa ofisi tatu ikiwemo ya makao makuu ambayo ilipangwa ikarabatiwe kwa sh. milioni 33 wakatumia sh. milioni 170 na ofisi za Tabora na Urambo zilipangiwa sh. milioni tano kila moja na hazikukarabatiwa.

Je Unapata Pesa Lakini Hujui Iendako Au umetupiwa Jini Chuma Ulete....Bofya Hapa Kupata Suluhu

0
0
Je Unapata Pesa Lakini Hujui Iendako Au umetupiwa Jini Chuma Ulete Na Tambua Jinsi Nyota Yako Inavyoweza Kutembelewa Na Watu Bila Wewe Kujijua:Kutana mganga wa tiba asili ambaye anatumia kipaji chake alichajaliwa na muumba wake... anatumia kioo cha asili kutibu magonjwa sugu yaliyoshindikana ata kama upo mbali 

Je Unauza Mali Zako Kama Vile Gari,nyumba,shamba,au Kiwanja lakini havihuziki? wasiliana na Mimi Leo uweze kuona nguvu ya maajabu ili mpaka vitu Mali iyo iwe ni yako halali isiwe na malalamiko hakika mungu atatia mkono wake. 

Je Umepotelewa Na Pesa Au Mali Yako Au Ndugu Yako Aliyepotea Kimiujiza Na Hujui Alipo? Acha kukata tamaa kipo kioo cha asili kitakulejea kile kilichopokea bila masharti magumu 

Je Unahitaji Kupata Mafanikio Bila Kutoa Kafara Au Unahitaji Pesa Za Majini?  acha kuogopa sasa wapo wengi waliokuwa hawaamini kama wewe ila kwa sasa wanamiliki pesa,majumba ya kifahar,maduka ya jumla,pamoja na viwanda kumbuka kuwa uwoga wako ndio umasikini wako na hakuna anayefanikiwa bila kuwa jasiri 

Je Umeachwa Na Mke Au Mme Au Unampenda Lakini Yeye Hakutaki ? onana Leo na chifu Ruyamba ili aweze kukupatanisha na mpenzi wako ndani ya Massa sita 6 tu atakuelewa 

Je Umegombana Na Bosi Wako Au Unataka Kupandishwa Cheo Au Wewe Ni Mpenzi Wa Kucheza Bahati Nasibu? acha kujiona mpweke utapatiwa Pete au saa itakayoendana na shughuli yako unamdai mtu ataki kukulipa au unakesi mahakamani ujui cha kufanya CHIFU RUYAMBA NDIO SURUHISHO WA YOTE .Hata kama ujawai pata mtoto uzazi wako utafunguliwa pia natibu kisukari,presha,busha bila kupasua,nguvu za kiume,na kuongeza maumbile ya kiume  saizi upendayo 

OFISI INAFUNGULIWA SAA MBILI ASubui adi saa mbili usiku na kwa sasa CHIFU RUYAMBA KAANZA  ZIARA MIKOANI PIGA SIMU 0764638796

Kutana Na Dr Chikago Bingwa Na Mwokozi Kwa Waliosumbuka Na Magonjwa Bila Mafanikio

0
0
Ninauwezo wa kumrudisha mume, mke ,mchumba, hawara, mtu unaempenda ndani ya masaa mawili tu (2) na kumfunga asiwe na mtu mwingine zaidi yako na kumfanya akutimizie kilakitu unachokihitaji kutoka kwake hata km yupo mbali na atatulia kabisa

GALIMBO 3 MIX;  nidawa ya mitishamba iliyitengenezwa kwa kwa utabibu wa hali ya juu kwakuchanganya miti na matundatiba , Huogeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15 -85 ) , inakomaza zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakat wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaid ya Mara tatu bila ham kuisha wara kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-40.

YOLANI :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inch (6-8) na unene wa sm (3-4)

Matatizo haya husababishwa na mambo mbalimbali km upigaji wa punyeto, kisukali,  vidonda vya tumbo, tumbo kuunguluma na kujaa gesi, ngili, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani, maumivu ya mgongo ama kiuno, namengineyo mengi  (nk )

SUPER MBUKE :- nidawa inayotatua tatizo la kisukali na kupona kabisa Kwa mda mfupi sana na utakuwa na uwezo wakula chakula chochote chenye sukali baada ya kupona,

vilevile ninadawa ya uzazi kwa akina Mama na akina Baba, kurudisha mali iliyopotea kwamda mfupi sana, vidonda vya tumbo, kaswende,presha,chango la uzazi, gono,nyama uzembe, kusafisha nyota, kuzuia majini wachafu, kinga ya mwili, kuuza vitu bila kununuliwa, dawa za biashara, pesa nyingi (utajili)  mambo ya kes nk

Kwa huduma n msaada wasiliana na Dr CHIKAGO atakusaidia hatakama ulikata tamaa utarudisha furaha yako

Napatikana Dar es salaam  sm no 0743543944   /0620510598

Nb :km huna nafasi ya kufika ofisin huduma hii itakufikia popote ulipo kwawatu wa mkoani tunatuma kwanjia ya mabasi.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

Lugola: Ni Kosa Kisheria Kutokua Na Kitambulisho Cha Taifa, Wasiojisajili Ni Lazima Waende Ofisi Za Nida Wilayani

0
0
Na Felix Mwagara, (MOHA), Mara.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewataka wananchi wenye sifa ya kupata Vitambulisho vya Taifa nchini waende kujisajili katika ofisi za Mamlaka ya Vitambulisho hivyo (NIDA) zilizopo katika Wilaya wanazoishi kwakuwa ni lazima kila Mtanzania awe nacho.

Lugola alisema wapo wananchi ambao hawakujitokeza wakati usajili ulipokua unafanyika katika mitaa na vijiji vyao, na pia wapo ambao kipindi hicho walikua na miaka 17 na kukosa sifa ya kujisali, lakini kwasasa wamefikisha miaka 18, nao wanapaswa kufika ofisi za wilaya ili wapate huduma hiyo ya usajili.

Akizungumza na wananchi wa Mji wa Kibara, Jimbo la Mwibara, Bunda, Mkoani Mara, Lugola ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo hilo, alisisitiza kuwa, zoezi la kujisajili si la kupuuziwa kwa kuwa ni lazima kila mwananchi raia wa Tanzania awe na kitambulisho cha Taifa.

“Vitambulisho hivi ni muhimu kuwa navyo, nawaomba Watanzania msipuuze hili zoezi, na pia napenda kusisitiza kwa mara nyingine muelewe vizuri kuwa vitambulisho hivyo vitatolewa kwa watanzania wenye sifa tu ambao watapita katika mchujo ili kuepusha kutoa kwa wasio raia,” alisema Lugola.

Lugola aliongeza kuwa, NIDA ipo makini na pia watahakikisha kuwa wanasajili wananchi nchi nzima kwa umakini na pia kutoa elimu zaidi kuhusiana na kuwa na kitambulisho hicho kwasababu kuna baadhi ya watanzani bado hawajajua umuhimu wa kuwa na kitambulisho cha taifa.

“Ndugu wananchi wa hapa na Watanzania kwa ujumla, naomba ieleweke kuwa, hakuna mwananchi mwenye sifa atakayekosa kitambulisho cha taifa, kikubwa fuateni utaratibu baada ya kwenda Wilayani mkipata maelezo kabla ya kuanza kujisajili ikwemo pamoja na hatua zote mtakazo pitia mpaka mnakipata vitambulisho hivyo,” alisema Lugola.

Alisema moja ya hatua wanazozipitia Maafisa wa NIDA ni pamoja na utambuzi wa watu gani wanaweza kupata vitambulisho hivi, na pia katika utambuzi wanapaswa kuwa makini sana kwasababu wasijesije kupenyeza wasiokuwa raia na baadae zoezi hilo likaja kuwa gumu.

Lugola alisema baada ya hatua ya utambuzi, inafuata hatua ya usajili ambayo pia hatua hiyo nayo inahitaji umakini mkubwa zaidi na ikimalizika hatua hiyo majina yaliyosajiliwa yanarudishwa tena kwa wananchi kuulizwa kama waliosajiliwa wanatambuliwa katika sehemu wanazoishi, hatua hiyo ikiwa na lengo la kupata taarifa sahihi ya waliosajiliwa wanatambuliwa au hawatambuliwi na wazawa katika eneo husika.

“Endapo majina tulioyasajili na kuyaleta kwenu, nanyi mtayakataa basi hatutaweza kutoa vitambulisho kwa huyo au hao mliowakataa, na endapo mtayaridhia majina tuliyowaletea, basi tutaweza kuwatengenezea vitambulisho bila shaka yoyote, na endapo kuna mwananchi amekataliwa na Kijiji kuwa hatambuliwi, anayohaki ya kukata rufaa na kutueleza kwanini apewe kitambulisho,” alisema Lugola.

Jela Miaka Mitatu Kwa Kutoa Rushwa Ili Apate Ajira

0
0
Na Mwamvua Mwinyi, Mkuranga
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa ,Mkoa wa Pwani imemfikisha mahakamani Naziru Mwakangali aliyekuwa anafanya kazi kama kibarua katika mamlaka ya bandari Dar es salaam kwa makosa ya kuahidi kutoa rushwa ya sh.laki nne na kutoa rushwa ya kiasi cha shilingi 390,000,kinyume na kifungu cha 15(1)(b) cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa na. 11 ya nwaka 2007.

Mwakangali alifunguliwa kesi ya jinai namba. 4 ya mwaka 2018 katika nahakama ya wilaya ya Mkuranga, Mkoani hapo.

Akisoma mashtaka mbele ya hakimu wa wilaya ya Mkuranga Tumsifu Barnabas, mwendesha mashtaka wa TAKUKURU, Euphrazia Kakiko ,aliieleza mahakama kwamba mshitakiwa alitenda kosa la kuahidi kutoa rushwa laki nne kwa mtoa taarifa ili ampatie ajira katika kiwanda cha Knauf Gypsum Tanzania Limited wilayani Mkuranga.

Aidha aliieleza ,mahakama kwamba nshitakiwa alitoa rushwa sh. 390,000 kwa mtoa taarifa, jambo ambalo pia ni kosa kisheria .Mshitakiwa alikiri kutenda makosa yote mawili, ambapo alitiwa hatiani na hivyo kupewa adhabu ya kutumikia kifungo jela kwa muda wa miaka mitatu kwa kila kosa ambapo mahakama iliamuru vifungo vyote viende pamoja ama kulipa faini ya sh. 500,000 kwa kila kosa kwa mujibu wa sheria ya kanuni za adhabu, sura ya 16 ya sheria za Tanzania.

Vilevile, mahakama iliamuru fedha zilizokamatwa kwa lengo la kutolewa na mshitakiwa kama rushwa zitaifishwe kuwa mali ya umma kwa mujibu wa sheria.Hata hivyo ,mshitakiwa alilipa faini kama Mahakama ilivyoelekeza.

Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Pwani, Suzan Raymond anatoa wito kwa wananchi kuacha kujihusisha na vitendo vya rushwa na badala yake wafuate taratibu zinazotakiwa katika suala zima la utafutaji wa ajira .

Raia wa Ethiopia Ahukumiwa Kifungo cha Maisha Jela na Mahakama ya Mafisadi Baaada ya Kunaswa na Madawa ya Kulevya

0
0
Mahakama Kuu Kitengo cha Uhujumu Uchumi ‘Mahakama ya Mafisadi’ imemuhukumu kifungo cha maisha jela raia wa Ethiopia, Ana Moises Chissano baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kukutwa na dawa za kulevya aina ya Cocaine Kg 3.03.

Hukumu hiyo imetolewa na Jaji Lilian Mashaka ambapo amesema mshtakiwa huyo amefungwa chini  ya kifungu cha sheria cha 15(1)(b) cha sheria namba 5 ya 2015 cha sheria ya kuzuia na kupambana na dawa za kulevya.

Mahakama imeamuru dawa hizo ziteketezwe.

Tazama Hapa Alichokisema Rais Magufuli Baada ya Kutia Saini ujenzi wa mradi wa umeme wa Stiegler’s Gorge

0
0
Rais John Magufuli ameshuhudia utiaji saini wa ujenzi wa mradi wa umeme wa Bonde la Mto Rufiji wa Stiegler’s Gorge kati ya Serikali ya Tanzania na Misri, akibainisha kuwa mradi huo utasaidia kutunza mazingira tofauti na baadhi ya wanamazingira wanavyokosoa.

Akizungumza leo Jumatano Desemba 12, 2018 Ikulu Dar es Salaam katika utiaji saini huo ulishuhudiwa pia na Waziri Mkuu wa Misri, Mostafa Madbouly, Magufuli amesema mradi  ulipigwa vita kwa kisingizio cha kulinda mazingira na kusisitiza kuwa unalenga kutunza hayo mazingira.


"Lazima tujifunze kwa waliotutangulia, sisi tuna megawati 1500 wenzetu wa Misri wana megawati zaidi ya 25,000 na maji wanayotumia yanatoka Kagera, lakini kwetu hata hapo Kagera umeme hakuna.

"Nawaomba watanzania hasa wale wanaopenda kusemasema wasitumiwe na mabeberu, huu mradi hauna dini, si wa chama, huu ni mradi wa watanzania wote na ni kwa faida yetu sote watanzania, naomba wasitumiwe na mabeberu.
 
"Nawapongeza watanzania kwa kutekeleza mradi huu, ndio maana nasisitiza tulipe kodi. Kuamua ni kitu kigumu, nashukuru wabunge na watanzania kwa kuamua, tungeanza hata kutekeleza kidogo kidogo leo tusingefikia hapa au a kupata matatizo haya ya umeme.
 
"Mradi huu una baraka nyingi, nimekaa kwenye wizara ya ujenzi kwa miaka 23 na tulisaini miradi mingi lakini sijawahi kuona mradi ambao wakati wa utiaji saini kuwa na idadi ya viongozi wetu wa dini kiasi hiki, ndio maana nasema mradi huu umebarikiwa.
 
"Tulipoomba watukopeshe kwa ajili ya mradi huu wakakataa lakini tulipowaambia kuhusu kuingia ubia wakakubali, maana yake ubia ni biashara na wao ndio watatupangia bei, ukiona nchi imefikia hatua ya kupangiwa bei ujue tumekwisha, ipo siku watasema hatuwashi kabisa.

"Wakati tunakaribia kutia saini mkataba huu, Mhe. Rais wa Misri niliongea nae alisema atashindwa kuhudhuria tukio hili lakini ameniambia mradi huu ataubeba kama mradi wake.

"Tukikamilisha mradi huu, umeme utapatikana kwa bei rahisi, hata bidhaa za viwanda zitauzwa kwa bei ya chini, uchumi wa nchi utakua lakini pia uchumi wa mwananchi mmoja mmoja utakua.

"Wapo wanaosema kuwa mradi huu utaharibu mazingira, si kweli hata kidogo, Mradi huu ni rafiki wa mazingira kwasababu umeme wa maji ni rafiki wa mazingira, lakini eneo litakalotumika ni 1.8% hadi 2%.
 
"Mradi huu tuliona unafaa kwa sababu chanzo chake ni cha uhakika, gharama zake si kubwa kulinganisha miradi ya vyanzo vingine, lakini pia mito yake ni kutoka sehemu ambazo hupata kiasi kikubwa cha mvua kwa mwaka.

"Nimefurahi baada ya miaka 40 mradi huu unatakelezwa,  ni furahi zaidi unatekelezwa kwa fedha zetu wenyewe, utagharimu shilingi trilioni 6.558, wakati Yesu anawakimbia watesi wake alikimbilia nchi ya Misri, na sisi pia kwenye swala la umeme tumekimbilia Misri."Amesema Rais Magufuli

Mmiliki wa Mabasi Ya Princes Muro Akwepa Kwenda Jela....Alipa Faini ya Milioni 115

0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuhukumu mmiliki wa Kampuni ya mabasi ya Princes Muro Majid Kimaro kulipa faini ya Sh. milioni 115 au kutumikia kifungo cha miaka nane jela baada ya kukiri mashtaka yanayomkabili ya kutakatisha fedha na kuongoza genge la uhalifu ili kuiba mafuta katika bomba linalomilikiwa na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).

Pia Mahakama imeamuru gari aina ya Scania lenye namba za usajili T 856 ADH ambalo lilitumika kuiba mafuta hayo ambayo ni zaidi ya lita 26,875.25 ya dizeli na petroli litaifishwe na kuwa mali ya Serikali.

Akitoa hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba amesema kuwa mahakama inamtia hatiani mshtakiwa kwa makosa mawili baada ya kukiri.

Simba amesema katika shtaka la kwanza la kuongoza genge la uhalifu, Muro anapaswa kulipa faini ya Sh5milioni au kifungo cha miaka mitatu jela.

Katika shtaka la utakatishaji fedha mshtakiwa atatakiwa kulipa faini ya Sh110milioni  au kifungo cha miaka mitano jela.

Kabla ya kutolewa adhabu hiyo, wakili wa Serikali Simon Wankyo akisaidiana na Jacqueline Nyantori na Patrick Mwita wameiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa washtakiwa kwa sababu makosa hayo ya wizi husababisha kuathirika kwa uchumi na nchi kukosa mapato.

Pia ameomba gari hilo litaifishwe na kuwa mali ya Serikali kwa sababu ndio lililotumika kubeba mafuta baada ya kulitoboa bomba  na kuiba mafuta hayo.

Wankyo amedai katika kesi ya msingi, mshtakiwa anadaiwa kati ya Julai Mosi, 2016 na Januari 8, 2018 katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Kigamboni, Dar es Salaam na maeneo mengine akiwa pamoja na wenzake ambao hawako mahakamani,  kwa kujua aliongoza genge la uhalifu kwa lengo la  kutoboa bomba la mafuta la TPA na kuiba mafuta ili kupata faida.

Katika shtaka la pili inadiawa kati ya Julai Mosi, 2016 na Januari 8, 2018 walipata lita 15,950.3  za mafuta ya dizeli na lita 10,925.22 za petroli na kusambaza mafuta hayo kwenye vituo vyake vya mafuta ma kuyauza wakati akijua yametokana na makosa ya uhalifu.

Viongozi Kutoka Cuba Na Umoja Wa Mataifa Wafanya Ziara Za Kikazi Nchini

0
0
Viongozi kutoka nchini Cuba na Umoja wa Mataifa wanafanya ziara za kikazi nchini Tanzania zenye lengo la kuimarisha uhusiano na ushirikiano baina ya Tanzania na mamlaka hizo.

Naibu Waziri wa Kilimo wa Cuba, Mhe. Jose Miguel Rodriguez de Armas na ujumbe wake waliwasili nchini tarehe 12 Desemba 2018 na watakuwepo hadi tarehe 19 Desemba 2018.

Ziara ya Mhe. Naibu Waziri wa Cuba na ujumbe wake hailengi tu kukuza na kuimarisha ushirikiano wa kihistoria kati ya Cuba na Tanzania, bali  inalenga pia kufanya majadiliano na wadau husika, ya namna ya kuondoa changamoto zinazokikabili kiwanda cha Labiofam ili kiweze kufanya kazi kwa ufanisi. 

Wakati wa ziara hiyo, Mhe. Naibu Waziri anatarajiwa kufanya mazungumzo na viongozi wa juu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Wizara ya Kilimo na Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC).

Kiwanda cha Labiofam kimejengwa Kibaha mkoani Pwani kwa msaada wa Serikali ya Cuba kwa ajili ya kutengeneza viuadudu vya kuua viluwiluwi wa mbu wanaosababisha ugonjwa wa malaria.

  Kwa upande wa Umoja wa Mataifa, ujumbe wa Umoja huo ukiongozwa na Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya Misheni za Ulinzi na Amani, Bw. Jean- Pierre Lacroix na Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa MONUSCO utafanya ziara nchini tarehe 13 na 14 Desemba 2018.

Ziara hiyo ni sehemu ya kuadhimisha mwaka mmoja tokea shambulizi lililofanywa na waasi wa Allied Democratic Forces dhidi ya kombania ya Tanzania katika maeneo ya Simulike, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Askari 14 wa Tanzania walipoteza maisha katika shambulizi hilo.

Ujumbe huo unatarajiwa kufanya mazungumzo na viongozi wa Serikali na vyombo vya ulinzi na usalama akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga kuhusu kuboresha ushiriki wa Tanzania katika vikosi vya kulinda amani.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma
12 Desemba 2018

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Disemba 13

Kura ya kutokuwa na imani na Theresa May Yashindwa Kuzaa Matunda

0
0
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May ameshinda kura za wa-Conservative 200 dhidi ya 117 katika bunge la uingereza na sasa ataendelea na wadhifa wake

Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amenusurika kura ya kutokuwa na Imani naye na hivyo kuendelea na wadhifa wake na kuzuia changamoto nyingine kwa uongozi kwa mwaka mmoja. May ameshinda kura za wa-Conservative 200 dhidi ya 117 katika bunge la uingereza jana Jumatano.

Katika mkutano wa faragha na wabunge wa-Conservative kabla ya kura kuanza, May alisema atajiuzulu kama kiongozi wa Uingereza kabla ya uchaguzi uliotarajiwa kufanyika 2022 hatua ambayo huwenda imemsaidia kupata uungaji mkono wa baadhi ya wabunge ambao walikuwa hawajafanya maamuzi wakati wanakwenda kupiga kura ya siri. Tangazo la May la kutowania kuchaguliwa tena lilithibitishwa na waziri katika baraza la mawaziri, Amber Rudd na wabunge wa-conservative Alec Shelbrooke na Robert Buckland.

Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani Labor Party, Ian Lavery alieleza katika taarifa kwamba ‘mapungufu na kushindwa kwa May kumezuia kabisa serikali kusonga mbele katika wakati huu muhimu kwa nchi”.

Bado haijafahamika kama kura itamsaidia May kupata uungaji mkono anaouhitaji sana kwenye makubaliano ya Brexit ambayo anafanya majadiliano nao.

Uingereza inatarajia kujitoa kutoka Umoja wa Ulaya Machi 29 mwakani, ikiwa ni matokeo ya kura ya maoni ya mwaka 2016. Pande hizo mbili zilifanya kazi misingi ya kuachana baada ya mashauriano marefu, lakini lazima yaidhinishwe na bunge la Uingereza. Mapema wiki hii, May aliakhirisha upigaji kura uliopangwa ambao ulionekana ungefeli.
 
May amekuwa akijaribu mara kwa mara kuokoa mkataba kupitia mazungumzo na viongozi wa ulaya. Lakini maafisa wa EU wamekuwa thabiti kuhusu kutokuwa na hamu ya kufanya tena mashauriano kwa misingi hiyo.

Rais wa baraza la Umoja wa ulaya, Donald Tusk alisema baada ya kile alichokiita “mazungumzo marefu na ya wazi” na May siku ya Jumanne kwamba ni Dhahiri wanachama wengine wa EU wanataka kusaidia kutatua hali hii lakini “swali linakuja kwa njia ipi?”

Tusk ameitisha mkutano na viongozi wa EU hivi leo Alhamisi kuzungumzia Brexit ikiwemo uwezekano kwamba Machi 29 itafika na hakuna makubaliano yaliopo.

Mahakama Yamwachia Huru mfanyabiashara Gulamali

0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Singida imetupilia mbali kesi ya rushwa iliyokuwa ikimkabili mfanyabiashara, Haider Hussein Gulamali baada ya kutokuwa na kesi ya kujibu.

Uamuzi huo umetolewa jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Consolata Singano ambapo amesema amezingatia ushahidi wa mashahidi 9 wa upande wa Jamuhuri waliofika mahakamani hapo ambapo hakuna ushahidi unaomgusa Gulamali moja kwa moja.

Katika kesi hiyo ambapo Mawakili wa Gulamali alikuwa Godfrey Wasonga, Hakimu Singano amesema moja ya sababu ni kutofautiana kwa mashahidi watatu kuhusu bahasha iliyobeba fedha.

Amesema katika ushahidi wao kila shahidi ametaja rangi tofauti ambapo mmoja ametaja Kaki, mwingine nyeupe, huku wa mwisho akitaja Brown jambo ambalo mahakama imeshindwa kuelewa bahasha ipi ilibeba fedha.

Pia amesema hata hatua za ukamataji hazikuanishwa vizuri kwani hakuna mahali iliyoonyesha Pesa ziliwahi kutaifishwa hadi zilipofikishwa mahakamani, pia namna zilivyotunzwa mpaka kufikishwa kama ushahidi.

Kutokana na hatua hiyo, Hakimu Singano amesema anatupilia mbali kesi hiyo na kumfanya Gulamali ambaye alikuwa ni mgombea wa ubunge wa (CCM) Singida Kaskazini kuwa huru.

Katika kesi hiyo, miongoni mwa mashahidi hao ni Ofisa Usalama mkoa wa Singida, Kiseo Nzowa anayedaiwa kupewa rushwa hiyo ambapo amedai anafanya kazi kwa mujibu wa sheria.

Shahidi huyo amedai kuwa Gulamali alimpa Sh.Mil 2 ili amsaidie kupitisha jina lake kwenye kinyang’anyiro cha ubunge Singida Kaskazini na kwamba yeye hakuwa Mjumbe Kamati ya Siasa Wilaya.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images