Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 172 na 173 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA  
 
“Wasi wasi wa nani kwa manaa hata leo nikikamatwa wewe wala huto guswa na utaokolewa kama mke wa raisi”
“Mmmmm ila kumbuka wewe ndio baba”
“Ya……”
Sikumalizia senyensi yangu nikaanza kusikia mlio wa helicopter kwa haraka nikamuachia Hawa na kukimbilia dirishani, nikafungua pazia taratibu nikaona helicopter ya jeshi la kimarekani ikishusha wanajeshi wanao tumia kwene nyumba ya tatu kutoka hapa tulipo jambo lililo niogopesha sana kwani kama wameshuka kwenye nyumba ya tatu kutoka tulipo basi kutufikia sisi hapa ni haraka sana jambo ambalo ni hatari sana kwangu na watu wanao nisaidia mimi.

ENDELEA   
“Ni kina nani?”   
Hawa aliuliza huku akikimbilia sehemu nilipo naye akionekana kujawa na wasiwasi mwingi sana.
“Ni wanajeshi wa kimarekani.”
“Mungu wangu wamejuaje kama tupo hapa?”
“Tulia kaa hapo ulipo na usichungulie nje sawa”
“Sawa”
Nikatoka kwa haraka, nikamkuta Martin naye akipandisha ngazi akionekana kuwa na wasiwasi mwingi sana.
“Mkuu wanajeshi wamekuja?”   
“Nimewaona”
Nilizungumza huku tukishuka kwenye ngazi hizi kwa haraka sana. Tukawakuta Babyanka na wezake wakiwa sebleni huku kila mmoja ameshika silaha yake.
 
“Jamani kuna njia ya chini kwa chini ambayo tunaweza kutoroka katika hili eneo.”
Winy alizungumza huku akitutazama usoni mwetu.
“Tuonyeshe kwa haraka tuweze kuondoka na Winy wasiliana na Livna umuelezee hali halisi inayo endelea hapa sawa”
“Sawa kaka”
Winy alizungumza huku akichomoa simu yake mfukoni mwake na kuanza kuminya minya. Nikatoka nje na kuwakuta walinzi wa Livna wakiwa wamejificha kwenye maua yaliyopo humu ndani. Kwa ishara wakaniomba nirudi ndani, nikafanya hivi kwa maana sifahamu ni kitu gani walicho kiona hadi wakaniomba nirudi ndani. Nikarudi sebleni Martin akanikabidhi bastola mbili pamoja na magazine nne.
“Njia ipo katika chumba hichi”
Winy alizungumza huku akinyooshea mkono wake kwenye moja ya chumba.
“Wastue hao wasichana huko nje sawa”
“Pao”
Nikaanza kupandisha ngazi kwenda juu, nikaingia kwenye chumba na kumkuta Hawa akiwa amejibanza kwenye ukuta pembeni ya dirisha.
 
“Wanakuja huku”
Hawa alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.
“Twende huku”
Tukatoka chumbani humu na kuanza kushuka ngazi hizi kwa kasi sana, tukafanikiwa kufika sebleni.
“Livna amesemaje?”
“Amesema tutaonana katika sehemu ambayo tutatokea”
“Ni mbali na hapa?”
“Ndio”
“Poa, tangulieni na Hawa”
Nilizungumza, kwa haraka watu wote wakaelekea katika eneo la mlango wa chumba hicho huku walinzi wa Livna nao wakiwa ni miongoni mwao. Nikaifunga milango ya mbele ya hii nyumba kwa kutumia fungo zake, kishindo kikali nikakisikia kwenye geti ikionyesha mambo yamesha haribika.
“Mkuu twende?”
Martin alizungumza kwa sauti ya juu huku  akiwa amesimama mlangoni.
 
“Kichwa cha Donald kipo wapi?”
“Kipo kwenye begi, Winy ametangulia nacho”
Kwa kupipitia dirishani nikaona wanajeshi wa Marekani wakiingia kwa umakini huku wameshika bunduki zao. Nikakimbilia hadi kwenye mlango wa kuingilia katika chumba hichi. Tukasaidiana na Martin katika kuufunga mlango huu ambao ni mtizo kutokana na kutengezwa na chumba. Tukaanza kushuka kwa haraka kwenye ngazi zinazo enelea chini, tukawakuta Babyanka na wezake wakitubiria. Winy akaminya moja ya batani kubwa ya rangi ya kijani iliyopo ukutani na sehemu hii ya kuingilia ndani ikajifunga kwa ndani. Kisha kwa haraka akaminya batani nyekundu, mtetemeko mkubwa ukatokea hadi sisi tukajikuta tukianguka chini.
“Ni nini hicho?”
Niliuliza huku mapigo ya moyo yakinienda kasi sana.
“Nimeilipua nyumba yangu, na nilikuwa nimeitega mabomo kwa hiyo hapo walipo ndani wote wamekufa”
Sote tukabaki tumemtazama Winy kwani hichi kitu alicho kifanya kusema kweli ni kitu cha ujasiri mkubwa sana.
 
“Tuondokeni”
Winy alizungumza, tukaanza kumfwata Winy kwa nyuma kwa uzuri ndani ya hii njia ya chini kuna taa ndogo ambazo zinatusaidia kuweza kuona tunapo elekea.
“Jamani taratibu mwenzenu nimechoka”
Hawa alizungumza huku akiinama taratibu. Ikatulazima wote kusimama, nikamsogelea Hawa, na mimi kuinama.
“Unajisikiaje?”
“Hapa kunauma”
“Pole, jikaze tuondoke”
“Sawa mume wangu”
Hawa alizungumza kiuvivu huku taratibu akinyanyuka. Tukazidi kusonga mbele huku Winy akiwa ni kiongozi wa sehemu tunapo elekea. Tukajikuta masaa mawili yakikatika na kufika katika sehemu ya kutokea.
“Katazame juu”   
Nilimuambia Martin, kwa haraka akapandisha ngazi za zilizopo katika hii sehemu, akachungulia kwa muda huku kiwili wili chake kikiwa ndani. 
 
“Vipi?”
“Kupo salama”
“Inabidi tusubirie hapa hadi Livna atakapo fika”
“Unaweza kuwasiliana naye?”
“Naona simu yangu haishiki mtandao”
Winy alizungumza huku akiinyoosha nyoosha simu yake juu.
“Hapa ni hadi utokee huko juu”
Babyanka naye alizungumze.
“Ilete”
Martin alizungumza huku  akichungulia humu ndani, Winy akapanda kangazi kadhaa na kumkabidhi simu.
“Hembu ngojeni kwaza”
Msichana mmoja wa Livna alizungumza huku akitutazama.
“Mkuu hakuacha maagizo yoyote juu ya mawasiliano kati yenu na yake?”
“Aliicha”
“Basi ngojeni kwanza yeye mwenyewe anajua nini cha kufanya”
“Alafu ni kweli, mawasiliano yetu yanaweza kunaswa isitoshe sasa hivi mitandao ya simu itakuwa makini sana kwa kila simu zinazo ingia na kutoka katika mitandoa yao”
Babyanka alizungumza.
 
“Basi inabidi kuimarisha ulinzi huko nje. Martin mazingira yapo vipi?”
“Ni pori lenye miti mingi”
“Kuna dalili yoyote ya kuwepo na mtu?”
“Labda hadi nitoke ndio nitazame”
“Hembu chunguza hilo eneo  kwa dakika tano, zikizidi zaidi ya hizo tutatoka kukupa msaada”
“Sawa mkuu”
“Nitaongozana naye”
Msichana mmoja wa Livna alizungumza huku akinitazama usoni mwangu. Nikatingisha kichwa ikiwa ni ishara ya kumkubalia. Binti huyu kwa haraka akapandisha ngazi hizi za chuma zinazo elekea juu.
 
“Erick”
Babyanka aliniita huku akisogea pembeni na kujitenga nasi, nikamfwata taratibu huku nikimtazama usoni mwake.
“Unajua hatujawasiliana na waziri mkuu?”
“Ahaaa nimesahau kabisa, ila kwa hizi ngija ngija zilizo tokea kusahau ni lazima”
“Yaa kama itawezekana kule ndio kutakuwa sehemu sahihi ya sisi kuweza kijificha tukiacha hali hii ya hatari ipungue”
“Njia si unaikumbuka?”
“Ramani yake ninayo niliitunza”
Babyanka alizungumza huku akitoa kataratsi mfukoni mwake, akanikabidhi, nikaanza kuitazama vizuri na kukumbuka njia ambayo waziri mkuu aliweza kutochorea.
“Lucy mwanaye sijui itakuwaje?”
“Na tukienda pale pasipo mwanye anaweza hata atusipokee”
“Kuna mtu ndani ya NSS, ninamuamini sana ninaimani kwamba anaweza kutusaidia”
 
“Unamuamini sana?”
“Ndio”
“Basi unaweza kufanya naye mawasiliano”
Kabla hata dakika tano hazijafika, Martina akaingia ndani sehemu tulipo.
“Tunaweza kutoka eneo lipo salama na Livna amesha fika”
Kidogo nikajikuta nikipata amani ya moyo wangu, kwa haraka nikaanza kupandisha kwenye hizi ngazi nikachungulia kwa nje, nikaoga gari mbili nyeusi zikiwa zimesimama huku Livna akiwa anazungumza na wasichana wake. Nikatoka na kuanza kutembea kuelekea walipo simama.
 
“Dany pole sana kwa kurupushani zilizo tokea”
“Asante aisee vipi lakini?”
“Ahaaa umekuwa lulu mwanangu”
“Lulu kivipi?”
“Yaani wamarekani wametoa dau la dola milioni mia moja kwa yoyote atakaye fanikisha kukamatwa kwako, Yaani huko kote unapo pita ni Dany, Dany. Yaani umekuwa maarudu kwa masaa machache mshkaji wangu”
“Mmmmm”
“Yaani Osama mwenyewe hajatafutwa hivi khaaa?”
Maneno ya Livna kwa namna moja ama nyingine yananipa wasiwasi mwingi.
“Yaani laiti ningekuwa ni mtu wa tamaa ningekuuza rafiki yangu ila lengo letu ni moja, hapa ndio nilikuwa ninawaweka sawa vijana wangu  kwamba yoyote atakaye jihisi kwamba ana tamaa ya pesa, basi tamaa yake hiyo iishie moyoni mwake na asiitoe nje ya moyo wake kwani tunaweza kumuua muda wowote na popote atakapo kwenda Duniani lazima tutampata”
 
“Shukrani”
“Ingieni kwenye magari jamani, kwa sasa Dany hutakiwi kuishi kabisa kwenye ardhi”
“Una maanisha nini?”
“Twende nitajua ni wapi kwa kukupeleka”
Livna alizungumza, nikaingia naye kwenye gari moja. Taratibu safari ikaanza ya kuondoka katika eneo hili.
“Hivi wanajeshi wa kimarekani walijuaje kama nipo pale?”
“Wamarekani wana mitandao mingi ya kumtafuta mtu, hususani kwa kupotelewa na raisi wao, kwa hilo lisikushangaze sana”
“Wametambua kwamba sisi ndio tulihusika katika kutekwa kwa raisi wao?”
“Hapana ila wanatutilia mashaka tu hii ni kutokana na rekodi  kubwa ya kigaidi ambayo unayo”
 
“Mungu wangu”
“Usiogope Dany, huwa sipendi kubadilika badilika kama kinyonga, nimekuahidhi kukusaidia na nitakusaidia hadi dakika ya mwisho katila hili”
“Shukrani Livna kwa maneno yako ambayo unayazugumza”
Safari nzima ndani ya hili pori, akilini mwangu ninawaza kuhusiana na jinsi gani maisha yangu kwa sasa yalivyo magumu sana, taratibu nikajukuta nikijilaumu kumuacha hai kwanza K2 na kushuhulika na raisi wa Marekani.
“Dany”
“Naam”
“Usiwaze sana”
“Kuwaza nilazima rafiki yangu”
“Kwa sasa dunia inakutamua kama gaidi. Itabidi kuishi kigaidi gaidi na si kuishi kwa kufikiria kulipiza kisasi”
“Daaa yaani ninayakumbuka maisha ya nyuma sana, ya Mariam na mama yake”
“Duuu hivi huyo msichana yupo?”
“Sijui kwa kweli?”
 
“Mariammmmm lilikuwa tawi zuri la K2 na masiki ya Mungu alijikuta akiiua famili yako pasipo kufahamu kwamba ni familia yako”
“Yaa silaumu sana kwa hilo kwani lilikuwa ni jukumu la kazi yake”
“Yaa pia alifanya kwa kushinikizwa, mama yake aliwekwa kizuizini. Mara ya mwisho nilisikia kwamba yupo Somalia sijuia atakuwepo hadi sasa?”
“Hapana nilikitana naye hapo katikati kipindi ninamkimbia baba Hawa, baada ya hapo aliondoka na mume wake”
“Ahaaa ameolewa?”
“Yaa ameolewa”
“Mungu amsaidie kwenye maisha yake nina imani kwamba atakuwa anajutia maisha haya tunayo ishi sasa”
“Ni kweli, natamani hata itokee ndoto, miaka irudi nyuma. Na niishi yale maisha ya nyumba za kapanga kama vile nilivyokuwa ninaishi kwa mama Mariam””
 
“Ahaaa hilo jambo haliwezekani rafiki yangu, kikubwa ni kupambana hadi mwisho wa mwisho wa maisha yako”
“Nikimua K2 ninajisalimisha mikononi mwa serikali”
“Acha ufala wewe, ukimuua K2 tafute sehemu ukaishi na Hawa wako, leeni mtoto wenu mambo yatakuwa yameishi kiaina hiyo. Ila usiniambie kwamba utajisalimisha kwenye serikali ambazo hazijui ukweli wa mambo kwamba hao wanao waamrisha kufanya hivyo ndio magaidi namba moja”
Nikaka kimya huku nikimtazam Livna usoni mwake. Gari hizi zikafika mwisho wa msitu huu na kusimama, mbele kuna ufukwe mkubwa wa bahari.
“Majira ya saa mbili usiku kuna boti yangu itafika hapa itatuchukua hadi yalipo makao mkuu yangu”
“Sawa sawa”
“Nina imani kwamba siku zote ulikuwa unatamani sana kuweza kuyaona makao makuu yangu”
 
“Huko kwenye meli yako”
“Ndio, ila watu wako tutawafunga vitambaa vyeusi kwenye macho yao nisingependa wafahamu ni wapi wanaelekea”
“Sawa hilo kwangu halina shaka”
“Sawa, ila Dany kumbuka kwamba ninakuhitaji uishi kama gaidi, na niataka kukufanya uwe GAIDI mkubwa zaidi ya magaidi ambao walisha wahi kutokea duniani hapa, si Osama, si nani ila kwa sasa dunia nzima inakwenda kusikia jina la DANYYYY, na hata ukihitaji tuipike Marekani uwezo huo tunaoa na utaweza kuipiga nchi hiyo na yoyote itakayo jaribu kukusogelea ikiwemo Tanzania”
Livna alizungumza kwa msisitizo mkubwa sana huku akinitazama usoni mwangu, nikabaki nikiwa ninamshangaa kwani maneno anayo yazungumza hata siku moja sikuwahi kuyafikiria kichwani mwangu kwani kichwa changu hadi sasa kimetawaliwa na mtu mmoja ambaye ni K2 adui tunaye sakana miaka nenda rudi.

AISIIIII……….U KILL ME 173 

Tukazidi kusubiri masaa yazidi kusonga mbele huku wasichana wa Livna wakizidi kuimarisha ulinzi katika eneo hili. Marija ya saa mbili usiku kama alivyo zungumza Livna, boti moja ikafika katika fukwe hizi, wasichana wawili walio tokea kwenye boti wakafika hadi sehemu tulipo. Livna akaniomba tushuke kwenye gari. Nikashuka kwenye gari huku nikiwa makini sana, Livna akanitambulisha kwa wasichana hawa, kisha sote tukaingia kwenye boti hii.
“Haya magri”   
“Tunayeteketeza”
Livna alizungumza huku akitoa rimoti ndogo kwenye mfuko wake. Akaminya batani nyekundu gari hizi zikalipuka huku nasi tukiondoka eneo hili na kuzidi kutokomea baharini. Martin na wezake wote wakaanza kufungwa vitambaa vyeusi kwenye macho yao.
“Dany”
Livna aliniita huku nikiwatazama jinsi wezangu wanavyo fungwa vitambaa vyeusi na wasichana hawa walio kuja kutuchukua.
 
“Naam”
“Njoo”
Tukatoka eneo hili na kupanda juu kabisa ya boti hii, na kuanza kutazama jinsi maji haya ya bahari yanavyo changuka kila tunapo pita kwenye hii bahari.
“Kwenye maisha yangu huwa sipendi kufanya dhambi ikiwa nina haki ya mtu mikononi mwake”
“Sijakuelewa kivpivi?”
“Baba yako aliacha haki yake kwenye kikosi hichi ninacho kimilili, nimekaa nikafikiri na nilivyo kutana na Martin naye alivyo nishauri japo nilimpatia kichapo, nikaona hapana. Peke yako huwezi, nikaona kwamba nilazima niweze kukupatia msaada japo mimi na baba yako tulitengana kwa ubaya ila siwezi kuendelea ubaya wetu kwako”
 
Livna alizungumza kwa sauti ya upole huku akiwa ameinamia kwenye bomba zilizopo pembezoni mwa hii boti.
“Nashukuru kwa kuweza kuona hali ninayo pitia”
“Usijali kwa hilo Dany, hembu nieleze ukweli”
“Ukweli gani?”
“Kati ya Hawa na Yemi ni nani unaye mpenda?”
Nnikaka kimya kwa muda huku nikishusha pumzi taratibu.
“Ninampenda Yemi. Hawa imetokea kumsamehe kwa ajili ya kiumbe chake alicho kibeba tumboni na laiti ingekuwa sio hivyo ningemuua”
 
“Usimuue”
“Kwa nini?”
“Mpe nafasi ya kuzaa mtoto ambeye atakuwa ni msaada kwako, kwani tunamkuza kwenye mazingira kama walivyo kua wasichana hawa wengine ambao wote ni bikra kwa hiyo hawajua mwanaume. Wewe na Martin huko tuendapo munatakiwa kuwa makini sana musije mukanivunjia bikra za wasichana wangu.”
“Hahaaaaa, sasa hivi sio kit*** tena”
“Wapi, wakati umetukimbia kidogo, tukajua mwenzetu unakwenda kuua, umeturudia ukiwa umevaa boksa”
“Hahaaa hembu acha kunichekesha”
“Ila unatakiwa kuwa makini na Hawa, kama aliweza kukubadilikia mara ya kwanza basi hata mara ya pili anaweza kukubadilikia”
“Hilo nimelielewa, ila hata wewe inabidi usibadilike kama mara ya kwanza”
“Kwa sasa siwezi Dany, nipo tayari hata kuweka kiapo cha damu”
 
“Una uhakika?”
“Ndio hata ukihitajio niweke sasa hivi nitaweka”
“ Basi ninaomba tuweke”
Livna akanitazama kwa muda kisha akaniaga kushuka chini, hakuchukua muda mrefu akarudi akwia ameshika kisu kidogo, akasimama mbele yangu na taratiba akajichana sehemu ya kiganja chake cha kushoto, kisha akanikabidhi na mimi kisu.
“Nawe unaweza kufanya hivi nilivyo fanya”
Sikuwa na hiyana zaidi ya kuchukua kisu hichi na kujichana kwenye sehemu ya kiganja changu. Taratibu Livna akfungua kinywa chake na kunimba nimnyunyize vipande vya damu8 mdomoni mwake, nikafanya hivyo kisha akavimeza, na mimi akaninyunyizia vipande vya damu mdomoni mwangu na nikavimeza;
“Umeamini kwamba sinto weza kukusaliti?”
“Ndio, ulisha wahi kuweka kiapo kama hichi kwa mtu?”
“Hapana sikuwahi kufanya kwa mtu yoyote na wewe ndio mtu wa kwanza kuinywa damu yangu na mimi kunywa damu yako”
Maneno na vitendo vya Livna vikaanza kunioa ujasirina na kuanza kumuamini, japo si sana kwani kauli ya mama yangu ya kuniambia kwamba nisimuamini mtu bado inaendelea kuishi moyoni mwangu na ninaikumbuka kila ninapo anza kufanya kazi na mtu yoyote hususani yule ambaye alisha wahi kunisaliti kipindi cha nyuma.
 
“Kiapo chetu hichi nina ninakuomba kiwe ni kati yetu mimi na wewe ninakuomba usimuambie mtu”
“Sinto wesa kufanya hivyo nina imani kwamba una nifahamu vizuri”
“Yaa”
“Tutachukua muda gani kuweza kufika huko tuendapo?”
“Masaa kama manne, ni mbali sana”
“Duuu”
Safari ikazidi kusonga mbele huku tukiendelea kuzungumza mambo mengi na Livna huku akiendelea kunipa siri nyingi kuhuaisna na K2 na ili tuweze kumuangusha K2 nilazima kuna mizizi tunatakiwa kuikata kwani nikimuangusha yeye kama yeye basi wapo watu nyuma yake ambao watakuja kulipiza kisasi kwa ajili yake. Majira ya saa nane usiku tukafika kwenye meli kubwa ambayo katika maisha yangu ninaweza kuifananisha na meli ya Titanic iliyo zama miaka mingi ya nyuma, 
 
“Tumesha fika nyumbani kwanagu, hapa hakuna mtu anaye weza kuingia kuanzia chini ya maji, kwenye usawa huu wa maji hata angani, ndio maana ulijaribu kuitafuta sana hii sehemu ila ulishindwa”
Livna alizungumza huku tukishuka juu huku tulipo, boti hii ikasimama pembezoni mwa hii meli, tukashushiwa ngazi na taratibu tukaanza kupanda huku Martin na wezake wakifunguliwa vitambaa walivyo fungwa soni mwao.
Katika hii meli kuna wasichana wengi walio valia nguo nnyeusi zilizo wabana vizuri miili yao. Wasichana baadhi wakabaki wakinishangaa.
 
“Hao hawajawahi kumuona mwanaume uso wa kuso kwa maana tuliwachukua kuanzi walivyokuwa wachanga sana”
“Mmmmmm hiyo kazi aalikuwa anaifanya naani?”
“”Kazi gani?”
“Kazi ya kuwateka?”
“Hao watoto tuliwachukua hospitalini na wengine tulikuwa tunawachukua kwenye vituo va yatima”
“Huko hospitalini huwa munawawaiba au munawachukua tu?”
“Yaa huwa wanaibiwa kwenye vile vyumba vya kuhifadhiwa watoto baada ya kuazaliwa”
“Ahaaa”
Livna akatukaribisha sehemu maalumu ya watu kupata chakula kabla ya utambulisho alio niambia ataufanya mbele ya wasichana wake ambao ni wengi kusema kweli. Tukaanza kupata chakula taratibu, tukamaliza na Livna akaamuru msichana mmoja kuwasanya wezake haraka iwezekanavyo
Mlio maalumu akaanza kusikika.
 
‘Ni nini?”
“Hiyo ni kama kengele, hapo wanakusanyika katika kiwanja namba moja kilichopo gorofa ya kati”
“Hivi wapo wangapi hawa wasichana?”
“”Idadi yao ukitoa wasichana wenye umri kuanzia miaka tisa kushuka chini. Walio bakia wapo laiki moja na tisini elfu na hawa wasichana wadogo wapo kama elfu  kumi”
“Mmmmmmm Livna una hatari, sasa malezi wanayapata vipi hao wasichna wadogo?”
“Usijali kesho nitakutembeza sehemu muhimu kwenye hii meli ila nyengine hatuto weza kuzimaliza kwaaajili ya ukubwa wa hii meli?”
“Ukubwa wake si sawa na Titanic?”
“Weee Titanic ndogo katika hii, wajapani walio jenga meli hii, hawakujenga kwa ajili ya safari. Ipo husasni kwa uzalishaji wa wasichana ambao ni majasusi wa kufa mtu”
“Hivi si wapo ambao wanamjua K2 sasa wakiniona si inaweza kuwa ni shida?”
 
“Hakuna anaye weza kutoboa siri, hawa wasichana tunawafundisha mambo mengi sana moja wapi ikiwa ni kuwa ni utunzaji wa siri za kikosi hichi”
Tulizungumza huku tukipandisha ngazi kuelekea kwenye gorofa ya pili. Tukaingia kwenye ukumbi mkubwa ambao kusema kweli idadi ya wasichaana tulio wakuta humu ni wengi sana. Livna akakabidhiwa kipaza sauti na mmoja wa wakuu wa wasichana hawa. Akaanza kwa kuwasalimia wasichana hawa.
“Leo tuna ugeni ambao kwa sasa watakwenda kuishi nasi hapa kama ndugu zetu. Kikubwa ni heshima, ushirikiano. Ila kuna mmoja wenu nina imani kwamba mumwezeza kumsikia na kama si kumsikia basi mumeweza kumuona hata picha yake. Anaitwa Dany, nina imani kwamba mutakuwa munashangaa kumuona mwanaume hapa au kumuona yeye hapa, ikiwa ni mara kadhaa baadhi yetu niliwaagiza katika kumtafuta”
Livna akaka kimya kwa sekunde kadhaa huku akinitazama kwa jicho la kuiba.
“Japo alipandikiziwa mbegu ya kuonekana yeye ni mbaya, mbegu iliyo mfanya leo hii kuonekana kwamba ni gaidi ila si kweli na ukweli wa kila jambo mimi mkuu wenu ndio naufahamu. Nitaomba muheshimu yeye na timu yake aliyo kuja nayo, na siku za mbeleni nitawaeleza ni nini cha kufanya”
 
Katika kuwatazama tazama hawa viongozi nikamuona msichana mmoja ambaye alishikiriki katika kutuvmia mimi na Mariam kipindi tulipo agizwa kufanya kazi moja na baba yangu ytulivyokuwa nchini Japani. Livna akanikabidhi kipaza sauti kwa ajili ya kuwasalimia wasichana hawa, nikakohoa kidogo li kuliweka koo langu sawa kisha nikawasalimia wasichana hawa wote wakaniitikia kwa furaha kuliko hata walimvyo muitikia Livna.
“Ninaitwa Dany, ninaomba ushirikiano wenu katika kuishi hapa, kusema kweli nimependa usikivu wenu na ukarimu wenu kwangu. Ninawashukuru sana”
Baada ya kujitambulisha nikampatia Hawa kipaza sauti hichi naye akawasalimia, baada ya sote kusalmia na kujitambulisha mbele ya hawa wasichana, tukapelekwa katika vyumba vya kulala.
“Nitalala na Hawa kwa ajili ya kumuangalia”
Babyanka alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.
“Sawa hakuna tabu. Martin ninakuomba kwa muda tuzungumze”
 
“Sawa mkuu”
Martin akaingia chumba ninacho lala. Nichumba kizuri ambacho ukuta wake mmoja ni wa kioo kikubwa na kipo chini ya maji na baadhi ya samaki kwa usiku huu ninawaona wakikatiza katiza eneo la karibu.
“Umeyaonaje mandhari hapa?”
“Nimeyapenda kwa kweli watoto ni wazuri sana aisee”
“Wote hao unavyo waoana ni bikra”
“Bikra?”
“Ndio na hilo ndio jambo nililo kuitia. Tumekuja na hawa magube gube wetu ambao hapa ni mmoja tu ambaye nimeivunja bikra yake ambaye ni Hawa, hao wengine wala sifahamu bikra zao zimevunjwa na kina nani. Kitu ambacho ninahitaji kukusisitoizaia ni kuhusiana na hifadhi hii ambayo tumepewa”
Nilizungumza huku nikimtazama Martin usoni mwake kwa macho makali huku nikiendelea kuisoma tamaa na uchu wake wa mapenzi ulio mvaa baada ya kuwaona wasichana hawa.
 
“Wasichana wote ni bikra, wasichana wote hao wanajua kupambana kulilo unavyo fikiria, mziki wao ninahisi umeupayta kutoka kwa Livna aliyekuwa mke wako. Wewe m** Winy, Livna mwenyewe au Babayanka, ila nisije kusikia kwamba umevunja mtoto wa watu bikra sijui nitakufanya nini, kwa maana sisi huko nje ni wakimbizi na hii ndio hifadhi yetu ya  pekee ambayo tumekabidhi kwa hiyo hado hado bwana mdogo tusije kufukuzwa humu kwa tamaa zetu za ngono na ubaya mimi na wewe ndio wanaume kwenye hii meli hakuna wanaume wengine, sasa ishu ya mimba ikitokea kwa mmoja wao mimi na wewe tutawajibika sawa?”
 
“Sawa muu nimekuelewa sinto wagusa hao watoto wa watu jao nilisha anza kuwamezea mate kusema kweli?”
“Hayo mate yako yaishir tu mdomoni huku nje wala yasitoke”
“Sawa mkuu nipo kwa ajili ya kuifwata amri yako”
:Sawa nashukuru kwa hilo. Unaweza kwenda”
“Sawa mkuu”
Martin akasimama wima na kunipigia saluti kisha akageuka kikakamavu na kuanza kuelekea mlangoni.
“Unakwenda ku Winy?”
Martin akageuka na kutabaamu tu, hilo likawa jibu tosha ya swali langu, akafungua mlango na kutoka chumbani humu. Nikaanza kukichunguza chumba hichi  huku nikitazama mapamba yaliyo wekwa humu ndani. Nilipo jiridhisha na uchunguzi wangu nikapanda kitanda huku nikiwa nimevalia nguo zangu, Kutokana na ucovu mkubwa na kusahau hata kulala kwa siku kadhaa sasa, usingizi mzito taratibu  ukanichukua na kulala fofofo.
                        ***
      Asubuhi na mapema Livna akaingia kwenye chumba changu huku akiwa amevalia nguo za jeshi, kwa bahati nzuri akanikuta nami nipo kwenye harakati za kuamka kitandani.
“Vipi umepata usingizi mwanana?”
“Yaaa umeamkaje?”
“Nipo poa tu, nimekuja kukuamsha nikakuonyeshe eneo la mazoezi”
“Sawa”
“Kumbe hukupata nguo za kubadilisha?”
“Ndio”
“Ngoja nikakuletee, utaoga kisha utabadilisha nguo hizo”
“Sawa sawa”
 
Livna akatoka chumbani humu na kuniacha peke yangu, nikanyanyuka kitandani na kufungua mlango wa bafu na choo uliopo humu ndani. Nikavua nguo zangu na kuoga haraka haraka, nikarudi chumbani huku nikiwa nimevalia boksa, nikamkuta Livna akiwa ameweka kombati za jeshi juu ya kitandani huku yeye akiwa amesimama pembeni.
“Ngoja nitoke mie nisije nikaingia majaribuni”
“Ahaa wapi?”
“Ohoo Dany mimi nikitazama hicho kifua chako, kisimi kinanicheza sasa ya nini kumsaligti Hawa ikiwa yupo humu humu ndani?”
“Hawa mapenzi naye yamekwisha”
“Ahaa wapi, hadi kakubebea mimba unasema kwamba mapenzi yamekwisha?”
“Kweli vile”
“Kwa hiyo nikihitaji kidogo unanipatia?”
“Sio kdogo tu hata kingi nitakupatia”
Tukatazamana na Livna kwa macho yaliyo jaa mahaba, taratibu akausogele mlango na kufunga kwa ndani, kisha kwa haraka akanisogelea na kunishika mashavu yangu kwa viganja vya mikono yake na kaunza ku denda. Tukiwa katika harakati za kuvuana nguo, mlango ukagongwa kwa nguvu, sote tukajikuta tukiutazama mlango huu.
“Vaa”
Livna alizungumza huku akianza kueleka mlangoni, nikavua boksa hii na kuvaa boksa aliyo ni;etea Livna, nilipo vaa suruali yangu, Livna akafungua mlango.
“Mkuu kuna tatizo”
Nilisikia sauti ya msichana.
 
“Tatizo gani?”
Msichana huyu akamkabidhi Livna simu, akatazama kitu kinacho onyeshwa, nikamuona sura yake ikijaa makunyanzi baadhi yatokanayo na hasira, taratibu nikamsogela na kutazamaa anacho kitazama, nikaona wasichana wawili wakiwa wamefungwa gundi maalumu midomoni mwao huku wakiwa katika ulinzi mkali wa kikosi cha F.B.I kutoka nchini Marekani.
“K2 amewauza walinzi wangu nilio muachia kwa Wamarekanai, wakifa basi na yeye amekufaa poamoja na hao Wamarekani”
Livna alizungumza kwa msisitizo huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake akionekana kujawa na hasira kali dhini ya hili jambo lililo tokea kwa wasichana wake ambao hata mmoja akifarikia basi ni kosa kubwa sana kwa yule aliye msababishia mauti msichana huyo kwani naye ni lazima atakufa
 
ITAENDELEA
‘Haya sasa wasichana wa Livna wameingia mikononi mwa F.B.I je wasichana hao waliokuwa wakimlinda K2 je wanaweza kutoa siri ya sehemu kambi yao ilipo? Usikose sehemu inayo fwata ya hadithi hii ya kusisimua kutoka kwa muandishi mahiri Eddazaria G.Msulwa”

Msajili Apangua Hoja za Vyama vya Siasa Kuhusu Muswada Mpya

$
0
0
Msajili wa Vyama Vya Siasa  amevitaka vyama vilivyoitisha mkutano wa kuupinga Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vyaSiasa kuacha propaganda za kupotosha muswada huo kwa sababu hatua zote za mchakato wa maboresho walishirikishwa.

Ametoa kauli hiyo siku moja baada ya kufanyika mkutano wa vyama 15 vya siasa ambavyo pamoja na mambo mengine,vilitangaza kuupinga hadharani Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ya Vyama vya Siasa vikidai unatengeneza kaburi la vyama vya siasa na demokrasia nchini.

Akijibu hoja za viongozi wa vyama hivyo kwenye mahojiano yaliyofanyika  Dar es Salaam jana, Msajili Msaidizi wa vyamavya Siasa, Sisty Nyahoza alidai  kilichosemwa na viongozi hao ni upotoshaji na kutengeneza propaganda zauongo.

Alisema lengo la serikali katika sheria mpya ni kuhakikisha   vyama vya siasa nchini vinapata sheria bora inayokwenda na wakati ambayo itatoa nafuu kwa vyama vya siasa kuendesha shughuli zao kwa uhuru na kwa mujibu wa katiba za vyama vyao.

Alisema  hakuna kipengele ambacho kinampa mamlaka msajili kuingilia uamuzi wa ndani ya vyama vya siasa.

Kwa mujibu wa Msajili, ameshangazwa kusikia  marekebisho hayo yanakwenda kuua au kukandamiza vyama vya siasa wakati siyo kweli kwa sababu vyama hivyo vilitoa maoni yao wakati wa mchakato wa maoni mpaka hatua ilipofikia.

“Sasa kama wanaona muswada wa marekebisho ya sheria ya vyama vya siasa unakwenda kuua au kuvikandamiza vyama kwa nini walitoa maoni yao?.

“Kwa sababu tuliwashirikisha hatua zote pamoja na kuitisha mikutano ya kujadili, kama waliona kunà dosari kwa nini wasingesema mapema mpaka wamesubiri usomwe kwa mara ya kwanza bungeni.

“Waache unafiki,wasiwaaminishe wananchi kwa propaganda za uongo,” alisema Nyahoza.

Alisema  kilichofanyika kwenye muswada huo ni maboresho ya kawaida ambayo vyama na serikali wamekuwa wakifanya kwenye sheria au katiba zao  kuhakikisha wanapata sheria bora.

Alitoa mfano wa Chama Cha ACT-Wazalendo ambacho alisema kiliwahi kufanya marekebisho ya katiba yake, vivyo hivyo kwa msajili wa vyama vya siasa kufanya maboresho ya sheria zake.

Alisema hakuna kipengele ambacho kinaonyesha msajili anaweza kuingilia uamuzi wa vyama.

Alisisitiza hoja hiyo ni dhaifu kwa sababu kila chama kinaongozwa na katiba yake, hivyo  kuwaaminisha wananchi katika hoja hiyo ni kupotosha ukweli.

“Kwa mfano, sheria ya zamani inasema chama au mtu akifanya makosa iwe madogo au makubwa katika chama, chama hicho kifutwe,lakini muswada huu umesema chama au mtu katika chama akifanya makosa aonywe na msajili au kupewa adhabu ndogo ya kusimamisha kwa muda kutojihusisha na shughuli za siasa ama kulipa faini,” alisema.

Alisema katika muswada huo mpya hakuna kipengele kinachowazuia wanasiasa kuhama chama, kugombea   baada ya kuhama au kujiunga na vyama vingine, bali wanasiasa watafanya hivyo kwa mujibu wa katiba ya chama alichotoka au anachokwenda na   msajili hatahusika na lolote katika jambo hilo.

Alisema mpaka sasa  Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria bado inaendelea na mchakato wa kukusanya maoni.

Alisema kama wanaona kuna shida walipaswa kuwasilisha maoni yao na kuainisha vipengele ambavyo wanaona vina matatizo  viweze kufanyiwa marekebisho na siyo kuwadanganya wananchi kama walivyofanya.

Alisema kama wanadhani serikali ina nia ya kufuta vyama vyama vya upinzani au kuvikandamiza siyo kweli  kwa sababu serikali hiyo hiyo ndiyo iliyoanzisha mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 baada ya kuona kuna umuhimu wa kuwapo   vyama hivyo.

Msajili wa vyama vya siasa ni mlezi wa vyama hivyo na   ataendelea kufanya shughuli zake kwa mujibu wa sheria na katiba na si vinginevyo,  alisema.

Aliwataka wanasiasa na wananchi kwa ujumla wao kuusoma muswada huo  waweze kuuelewa jambo ambalo linaweza kuepusha upotoshaji.

Anayetuhumiwa Kumhonga Waziri Lukuvi Akutwa na Kesi ya Kujibu

$
0
0
Mfanyabiashara Mohamed Kiluwa (50) amekutwa na kesi ya kujibu katika mahakama ya Wilaya ya Ilala na ataanza kujitetea Desemba 17, 2018.

Uamuzi huo umetolewa leo Jumanne Desemba 11, 2018 na hakimu mkazi, Samuel Obasi  baada ya upande wa mashtaka kufunga ushahidi wao.

Kiluwa anakabiliwa na shtaka moja la  kutoa rushwa ya Dola za kimarekani 40,000 kwa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi,  William Lukuvi.

Akisoma Uamuzi huo baada ya upande wa mashtaka kufunga ushahidi wao leo,  Hakimu Obasi amesema "Upande wa mashtaka ulileta mashahidi sita pamoja na vielelezo vingi ikiwemo hati za Ardhi na CD.”

Hakimu Obasi amesema amepitia ushahidi wa mashahidi hao pamoja na vielelezo na kumuona  mshtakiwa kuwa ana kesi ya kujibu.

“Baada ya kupitia ushahidi na vielelezo hivi, mahakama yangu imemkuta Kiluwa ana kesi ya kujibu, hivyo chini ya kifungu namba 231(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, mshtakiwa anatakiwa kujitetea,” amesema Obasi.

Baada ya kueleza hayo wakili wa mshtakiwa, Omary Madega amedai upande wa utetezi watakuwa  na mashahidi wawili, akiwemo Kiluwa.

Awali, kabla ya hakimu kutoa uamuzi huo  upande wa mashtaka walikuwa na shahidi moja ambaye alitoa ushahidi wake dhidi ya Kiluwa.

Shahidi huyo,  Wilson Luge (39) ambaye ni Kaimu Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Wizara ya Ardhi, amedai kuwa yeye ndio aliyeshiriki zoezi la kuhakiki na kuhesabu fedha hizo Dola za 40,000 za Marekani ambazo zilikuwa katika bahasha ya kaki, juu ya meza ya waziri Lukuvi.

Akiongozwa na mawakili kutoka Takukuru, Maghela Ndimbo akisaidiana na Nikson Shayo, Luge ambaye ni shahidi wa sita katika kesi hiyo, amedai kuwa baada ya kuzihesabu fedha hizo walizianisha katika fomu maalum na kisha kuisaini fomu hiyo kama sheria inavyotaka.

Hakimu Obasi ameahirisha kesi hiyo hadi  Desemba 17,2018 itakapoendelea kwa upande wa utetezi kuanza kujitetea.

Je Unapata Pesa Lakini Hujui Iendako Au umetupiwa Jini Chuma Ulete....Bofya Hapa Kupata Suluhu

$
0
0
Je Unapata Pesa Lakini Hujui Iendako Au umetupiwa Jini Chuma Ulete Na Tambua Jinsi Nyota Yako Inavyoweza Kutembelewa Na Watu Bila Wewe Kujijua:Kutana mganga wa tiba asili ambaye anatumia kipaji chake alichajaliwa na muumba wake... anatumia kioo cha asili kutibu magonjwa sugu yaliyoshindikana ata kama upo mbali 

Je Unauza Mali Zako Kama Vile Gari,nyumba,shamba,au Kiwanja lakini havihuziki? wasiliana na Mimi Leo uweze kuona nguvu ya maajabu ili mpaka vitu Mali iyo iwe ni yako halali isiwe na malalamiko hakika mungu atatia mkono wake. 

Je Umepotelewa Na Pesa Au Mali Yako Au Ndugu Yako Aliyepotea Kimiujiza Na Hujui Alipo? Acha kukata tamaa kipo kioo cha asili kitakulejea kile kilichopokea bila masharti magumu 

Je Unahitaji Kupata Mafanikio Bila Kutoa Kafara Au Unahitaji Pesa Za Majini?  acha kuogopa sasa wapo wengi waliokuwa hawaamini kama wewe ila kwa sasa wanamiliki pesa,majumba ya kifahar,maduka ya jumla,pamoja na viwanda kumbuka kuwa uwoga wako ndio umasikini wako na hakuna anayefanikiwa bila kuwa jasiri 

Je Umeachwa Na Mke Au Mme Au Unampenda Lakini Yeye Hakutaki ? onana Leo na chifu Ruyamba ili aweze kukupatanisha na mpenzi wako ndani ya Massa sita 6 tu atakuelewa 

Je Umegombana Na Bosi Wako Au Unataka Kupandishwa Cheo Au Wewe Ni Mpenzi Wa Kucheza Bahati Nasibu? acha kujiona mpweke utapatiwa Pete au saa itakayoendana na shughuli yako unamdai mtu ataki kukulipa au unakesi mahakamani ujui cha kufanya CHIFU RUYAMBA NDIO SURUHISHO WA YOTE .Hata kama ujawai pata mtoto uzazi wako utafunguliwa pia natibu kisukari,presha,busha bila kupasua,nguvu za kiume,na kuongeza maumbile ya kiume  saizi upendayo 

OFISI INAFUNGULIWA SAA MBILI ASubui adi saa mbili usiku na kwa sasa CHIFU RUYAMBA KAANZA  ZIARA MIKOANI PIGA SIMU 0764638796

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

TFF Yatoa ufafanuzi tuhuma za Kutafuna Milioni 300

$
0
0
Shirikisho la soka Tanzania leo Jumanne ya December 11 2018 limeamua kutoa tamko kuhusiana na kilichoandikwa katika gazeti la ‘Tanzanite’ likilituhumu shirikisho hilo kutumiwa pesa kinyume na taratibu zaidi ya Tsh Milioni 300


Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Yawataka Wasimamizi wa Uchaguzi Kuzingatia Sheria na Taratibu za Uchaguzi

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi  (NEC) imewataka Wasimamizi wa Uchaguzi kuzingatia kanuni,sheria  na miongozo ya Uchaguzi wanaposimamia na kutekeleza majukumu ya uchaguzi.

Hayo yameelezwa na Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Mh. Jaji Mstaafu Mery Longway katika ufunguzi wa mafunzo kwa wasimamizi na wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi yaliyofanyika Mkoani Dodoma leo.

Ameeleza kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ndio yenye jukumu la kusimamia , kuendesha na kuratibu Uchaguzi , lakini wanaosimamia jukumu hilo kwa ukaribu zaidi ni wasimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo , Wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo, Wasimamizi wasaidizi ngazi ya kata pamoja na Watendaji wa vituo  vya kupigia Kura.

“Nawakumbusha kuzingatia kanuni, Sheria na Miongozo yote iliyotolewa na itakayotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ili kusimamia jukumu hili kwa ufanisi na mafanikio makubwa”. Amesema Mh. Longway.

Aidha amewakumbusha wasimamizi hazo wa Uchaguzi kuwa Uchaguzi ni Mchakato unaojumuisha hatua na taratibu mbalimbali za kufuatwa na kuzingatiwa ndio msingi wa Uchaguzi kuwa huru wa haki na kupunguza kama siyo kuondoa kabisa malalamiko au vurugu wakati wote wa Uchaguzi na hivyo kupunguza kesi mahakamani baada ya Uchaguzi.

Amesema kuwa pamoja na baadhi ya washiriki wa mafunzo kuwa wazoefu katika kuendesha Uchaguzi washiriki hao wametakiwa kuhakikisha wanazingatia maelekezo watakayopewa na wakufunzi wa Tume, haitokuwa vyema kutekeleza majukumu hayo kwa mazoea bali wanatakiwa kuzingatia matakwa ya Katiba, Sheria na Kanuni zinazosimamia zoezi la Uchaguzi

Washiriki wa Mafunzo hayo ni Wasimamizi wa Uchaguzi ngazi ya jimbo , Wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo, Wasimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Kata ambao watasimamia Uchaguzi Mdogo wa Umbunge Jimbo la Temeke na Udiwani katika kata 46  utafanyika Januari 19 mwaka 2019.

MWISHO

Kutana Na Dr Chikago Bingwa Na Mwokozi Kwa Waliosumbuka Na Magonjwa Bila Mafanikio

$
0
0
Ninauwezo wa kumrudisha mume, mke ,mchumba, hawara, mtu unaempenda ndani ya masaa mawili tu (2) na kumfunga asiwe na mtu mwingine zaidi yako na kumfanya akutimizie kilakitu unachokihitaji kutoka kwake hata km yupo mbali na atatulia kabisa

GALIMBO 3 MIX;  nidawa ya mitishamba iliyitengenezwa kwa kwa utabibu wa hali ya juu kwakuchanganya miti na matundatiba , Huogeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15 -85 ) , inakomaza zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakat wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaid ya Mara tatu bila ham kuisha wara kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 18-40.

YOLANI :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inch (6-8) na unene wa sm (3-4)

Matatizo haya husababishwa na mambo mbalimbali km upigaji wa punyeto, kisukali,  vidonda vya tumbo, tumbo kuunguluma na kujaa gesi, ngili, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani, maumivu ya mgongo ama kiuno, namengineyo mengi  (nk )

SUPER MBUKE :- nidawa inayotatua tatizo la kisukali na kupona kabisa Kwa mda mfupi sana na utakuwa na uwezo wakula chakula chochote chenye sukali baada ya kupona,

vilevile ninadawa ya uzazi kwa akina Mama na akina Baba, kurudisha mali iliyopotea kwamda mfupi sana, vidonda vya tumbo, kaswende,presha,chango la uzazi, gono,nyama uzembe, kusafisha nyota, kuzuia majini wachafu, kinga ya mwili, kuuza vitu bila kununuliwa, dawa za biashara, pesa nyingi (utajili)  mambo ya kes nk

Kwa huduma n msaada wasiliana na Dr CHIKAGO atakusaidia hatakama ulikata tamaa utarudisha furaha yako

Napatikana Dar es salaam  sm no 0743543944   /0620510598

Nb :km huna nafasi ya kufika ofisin huduma hii itakufikia popote ulipo kwawatu wa mkoani tunatuma kwanjia ya mabasi.

Nape Apinga Mfumo wa Serikali Kuhusu Malipo ya Korosho kwa Wakulima

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye ameibuka na kuwatetea wakulima baada ya serikali kutangaza hivi karibuni kuanza kutowalipa pesa wakulima wanaomiliki korosho walizozipata kwa kuzinunua kutoka kwa wenzao kwa mfumo wa 'kangomba' pasipo kuwa na mashamba.

Nape amesema kuwa mfumo huo unaoendelea sasa unawapa mateso wakulima na kupendekeza kuwa ili kumaliza tatizo hilo, ni vyema serikali kuviwezesha vyama vya ushirika kupitia Benki ya Maendeleo ya Wakulima (TADB) kulipa sehemu ya malipo kwa wakulima hao mara tu korosho inapofika ghalani.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Nape Nnauye ameandika, "dawa ya kangomba ni kubadili mfumo wa malipo ya korosho kwa wakulima, kwa kuviwezesha Vyama vya Ushirika kupitia TADB kulipa sehemu ya malipo mara tu korosho inapofika ghalani. Hiki kinachoendelea sasa hakiwezi kumaliza kangomba, ni mateso tu kwa wakulima!,"

Rais Magufuli wakati akitangaza uamuzi wa serikali kununua korosho za wakulima, Novemba 13 Jijini Dar es salaam alisema kuwa serikali itanunua korosho zote za wakulima kwa bei ya sh 3,300 kwa kilo baada ya wanunuzi binafsi kushindwa kutimiza matakwa ya serikali.

Hivi karibuni Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Rukia Muwango alisema kuwa wakulima wote waliouza zao hilo bila kuwa na mashamba, wajiandae kisaikolojia kwani hawatolipwa mpaka watakapoonesha mashamba waliyovuna korosho hizo.

Afrika Kusini Yang'aka Baada ya Rwanda Kumuita Waziri wake Kahaba

$
0
0
Afrika Kusini imemuita balozi wa Rwanda mjini Pretoria baada ya mtandao unaoipendelea serikali nchini Rwanda kumita "kahaba" waziri mmoja wa serikali ya Afrika Kusini.

Lindiwe Sisulu, waziri wa masuala ya uhusiano wa kimataifa nchini Afrika Kusini amekosolewa kwenye Twitter na afisa wa cheo cha juu wa Rwanda.

Msemaji wake aliiambia BBC kuwa matamshi hayo hayatakubaliwa na lazima yakome.

Bi Sisulu hivi majuzi alikutana na mkosoaji wa Rais wa Rwanda aliyeko uhamishoni Afrika Kusini na kuzua mzozo wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili.

Aliuambia mkutano wa wandishi wa habari mwezi ulipita kuwa alikutana na mkuu wa zamani wa majeshi nchini Rwanda Faustin Kayumba Nyamwasa, mjini Johannesburg.

Alisema alishangazwa kusikia kuwa Bw Nyamwasa ambaye amebuni chama chake nchini Afrika Kusini alikuwa na nia ya kuzungumzia mapatano na serikali yake ya zamani.

Bwana Nyamwasa amekuwa akiishi uhamishoni nchini Afrika Kusini tangu mwaka 2010 baada ya kutofautiana na rais wa Rwanda Paul Kagame.

Naibu waziri wa nchi za kigeni nchini Rwanda Olivier Nduhungirehe, alikosoa mkutano huo kwenye mtandao wa Twitter.

Alisema ikiwa afisa yeyote wa Afrika Kusini anataka kuzungumza na mhalifu ambaye alikuwa anaongoza vuguvugu yuko huru kufanya hivyo lakini kamwe asiishirikishe Rwanda.

Taarifa moja kwenye mtando wa habari unaoipendelea serikali ilikuwa na kichwa kilichomtaja Bi Sisulu kama "kahaba".

Msemaji wa Bi Sisulu, Ndivhuwo Mabaya, alisema balozi wa Rwanda huko Pretoria ameambiwa kuwa matamshi kama hayo hayatakubaliwa.

Alisema balozi wa Afrika Kusini mjini Kigali, George Twala, ameitwa kwenda Prerotia kwa mashauriano.

Mwaka 2014 Afrika Kusini iliwafukuza wanadiplomasia watatu wa Rwanda kufuatia shambulizi dhidi ya nyumba ya Bw Nyamwasa mjini Johannesburg. Rwanda ilijiubu kwa kuwatimua wanadiplomasia 6 wa Afrika Kusini.

Bw Nyamwasa alinusurika karibu mara mbili jaribio la kuuawa akiwa uhamishoni.

Wanaume wanne walikutwa na hatia mwaka 2014 na mahakama ya Afrika Kusini kwa shambulizi hilo la bunduki lililomuacha na majeraha ya tumbo. Bw Nyamawasa alilitaja shambulizi hilo kuwa lilichochewa kisiasa.

Uhusiano kati ya Afrika Kusini na Rwanda pia ulidhoofika baada ya aliyekuwa mkuu wa ujasusi kanali Patrick Karegeya, kuuawa katika hoteli yake mjini Johannesburg mwaka 2014.

Muda mfupi baada ya kuuliwa, Bw Kagame alisema: "Huwezi kuhujumu Rwanda na hukose kuadhibiwa. Yeyote hata wale ambao bado wako hai watavuna. Kila mtu."

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano ya Disemba 12

Bodaboda 20 wakamatwa na Polisi Dar kwa tuhuma za kushambulia kwa mawe Basi la Mwendokasi

$
0
0
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linawashikilia madereva 20 wa bodaboda kwa tuhuma za kulishambulia na kuliharibu basi la mwendokasi.

Wanadaiwa kulishambulia basi hilo baada ya mwenzao kugongwa na kufariki dunia.

Akizungumza jana Jumanne Desemba 11, 2018 Kamanda wa Kanda hiyo, Lazaro Mambosasa alisema Desemba 8, saa nane usiku eneo la Manzese Tiptop, dereva bodaboda akiwa anapita katika barabara ya mwendokasi aliligonga basi hilo na kusababisha vifo vya watu wawili.

Alisema watu wawili waliokuwa wamepanda bodaboda hiyo walifariki dunia pamoja na aliyekuwa akiendesha.

Alisema baada ya ajali hiyo madereva hao wanaoegesha pikipiki zao kando ya barabara hiyo walianza kulishambulia basi hilo kwa mawe na kusababisha uharibifu.

Mambosasa ametoa onyo kwa madereva wote wa vyombo vya moto hususan pikipiki kuacha mara moja kutumia barabara za mabasi ya mwendokasi ili kuepusha ajali ambazo zinagharimu maisha ya watu.

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

$
0
0

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara, Msanii wa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo Dawa na PETE za Bahati zenye uwezo mkubwa wa kuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.

Kutana na Sheikh Jumaa Bilal. Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki. 

Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. Sheikh Jumaa Bilal ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA-  Sheikh Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na Nje ya nchi.

Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nayasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.

Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudishaa alipote, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMBA, GARI..), Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali na UTAJIRI bila masharti na mengine mengi ya Siri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET)

*{لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّهُ بِاللَّغْوِ فِي أيْمَانِكُمْ وَلَٰكِنْ يُؤَاخِذُكُمْ بِمَا عَقَّدْتُمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِمَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ }* ﴿٨٩﴾

✨Wabillahhi Tawfiq Asallam  Alaikum

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa
nambari ya simu

+255 688 745 790
+255 672 861 042
Whatsapp :  0762 252 102

Amuua kaka yake kwa mganga wa kienyeji Kisha na Yeye Ajinyonga

$
0
0
Watu wawili wamefariki dunia Mkoani Morogoro baada ya mtu aliyedaiwa kuwa na ugonjwa wa akili kumuua ndugu yake na kisha yeye mwenyewe kujinyonga walipokuwa kwa mganga wa kienyeji kwaajili ya kupata matibabu.
 
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi wa Polisi Wilbord Mtafungwa amesema kuwa tukio hilo limetokea desemba 1, 2018 baada ya Lucian Kigolo (54) ambaye anamatatizo ya akili kumshambulia kaka yake Gerald Kigolo(60) kwa kumpiga na kitu kizito kichwani.

Aidha Kamanda huyo amesema baada ya kutenda tukio hilo, mtu huyo aliamua kujinyonga kwa kutumia kamba  nyumbani kwa mganga wa kienyeji ambaye ametambulika kwa jina la Luka Paulo (50), ambapo katika tukio hilo Jeshi la Polisi linamshikilia mganga huyo.

Rais Mstaafu Apigwa Marufuku Kukanyaga Marekani

$
0
0
Marekani imempiga marufuku Rais wa zamani wa Gambia, Yahya Jammeh kuingia nchini humo kutokana na historia mbaya ya utawala wake iliyohusisha vitendo vya rushwa na uvunjifu wa haki za binadamu.

Uamuzi huo umetolewa Disemba 10  ikiwa ni miaka miwili tangu Jammeh alipolazimishwa kukimbilia uhamishoni nchini Equatorial Guinea. Aliondolewa kwa nguvu madarakani na Jeshi la Umoja wa Afrika baada ya kukataa kuachia madaraka kufuatia kushindwa kwenye uchaguzi mkuu na Adama Barrow.

Marekani imeeleza kuwa Jammeh amezuiwa kuingia nchini humo pamoja na familia yake yote, na kwamba uamuzi huo unatokana na sheria za nchi hiyo kwa maafisa wa Serikali za nchi nyingine ambao wanaaminika kujihusisha na vitendo vya ufisadi na uvunjifu wa haki za binadamu.

Kwa mujibu wa Serikai ya Gambia inayoongozwa na Barrow, Jammeh aliiba zaidi ya $50 milioni za umma alipokuwa madarakani.
 
Kwa mujibu wa ripoti, Jammeh anamiliki majumba katika eneo la Potomac, Maryland nchini Marekani, Kilometa 24 tu kutoka Washington. Alinunua majumba hayo mwaka 2010 kwa $3.5 milioni kutoka kwa mwanamichezo wa Marekani, Calbert Cheaney.

Ajali ya Basi Yaua Watu 2 na Kujeruhi 21 Lushoto

$
0
0
Watu wawili wamefariki dunia na wengine 21 kujeruhiwa huku sita kati yao wakiwa na hali mbaya baada ya basi la Royal Classic waliokuwa wakisafiria, kuacha njia na kupinduka eneo la Kibaoni wilayani Lushoto jana Jumanne Desemba 11.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda waPolisi Mkoa wa Tanga, Edward Bukombe, amesema basi hilo lilikua likisafiri kutoka Tanga kwenda wilayani Lushoto.

Kamanda Bukombe amebainisha chanzo cha ajali hiyo ni utelezi uliotokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika eneo hilo.

“Majeruhi sita kati ya 21 hali zao ni mbaya na wamehamishiwa Hospitali ya Rufaa ya Bombo kwa matibabu zaidi,” amesema.

Waitara: Watumishi Wa Umma Msijiingize Kwenye Utumwa Wa Mikopo Ya Taasisi Zisizo Halali

$
0
0
Na Tiganya Vincent
Watumishi wa Umma wametakiwa kuacha kujiingiza katika mikopo inayowasababisha kuuza uhuru wao na kuwa watumwa kwa wakopeshaji wasio halali na ambao hawajasaliwa na Serikali.

Kauli hiyo imetolewa wilayani Nzega na Igunga na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR TAMISEMI) Mwita Waitara wakati wa vikao vya majumuisho na Watumishi wa Wilaya hizo.

Alisema baadhi ya wanawakopesha hawakusajiliwa na hawalipi kodi za Serikali na hivyo kuendesha biashara hiyo kinyume cha Sheria na taratibu za nchi.

Waitara alisema wakopeshaji hao wamekuwa wakikopesha kwa riba kubwa ambazo zimewafanya baadhi ya watumishi kuishi maisha magumu yaliyojaa utumwa ndani yake.

Alisema baadhi ya watumishi ambao ukopa wamekuwa wakikabidhi hata Kadi za kuchukua Fedha (ATM) kwa wakopeshaji na inapofika mwisho mwa Mwezi ndio upiga simu kwake ili waende kwenye ATM achukue fedha kwa ajili ya kulipa deni na kidogo za matumizi na baada ya hapo anarudisha kadi mdai wake.

Waitara alisema kitendo kinafanya taarifa za mshahara wa mtumishi kutokuwa siri kwake bali kuwa wazi hata kwa mkopeshaji jambo ambalo ni kuuza uhuru wake.

Aliwataka Watumishi wa umma kuishi kulinga na mishahara wanayolipwa na kujiepusha na tamaa ambazo zinaweza kuwasababisha kujiingiza katika matatizo.

Alikiba atangaza kuachia nyimbo mbili siku ya funga mwaka na King Kiba

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi Ally Salehe Kiba a.k.a Alikiba ameweka wazi kuwa December 19 mwaka huu ataachia nyimbo zake mbili.

Hiyo ni katika show yake kubwa ya kufunga mwaka, huku show yake na muimbaji maarufu Afrika,  Yvonne Chaka Chaka kutokea Afrika Kusini ikihairishwa hadi February 2019. 

Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;

"Kuelekea kwenye show yangu kubwa ya mwaka 'Funga Mwaka Na King Kiba' December 19, 2018 pale Next Door Arena, nitaachia “HITS” zangu mbili kabla mwaka haujaisha pamoja na kuizindua rasmi kinywaji changu cha Mofaya Energy Drink.

"Sema kuna mabadiliko ya tarehe ya show yangu na Mama Yvonne Chaka Chaka pamoja na King Of Best Melodies, Christian Bella christian  kutoka December to February 2019, the month of Love ❤"

Kwa sasa Alikiba anafanya vizuri na wimbo unaokwenda kwa jina la Mwambie Sina alioshirikiana na kundi lake la Kings Music ambalo pia kwa sasa linafanya vizuri na wimbo uitwao, Toto.

Marekani Yachukizwa Na Kitendo Cha Urusi Kutuma Ndege Hatari Za Kuangusha Mabomu Venezuela

$
0
0
Maafisa wakuu wa Urusi na Marekani wamejibizana baada ya ndege mbili kubwa za kuangusha mabomu za Urusi kutua nchini Venezuela, taifa linalopatikana Amerika Kusini.

Ndege hizo mbili zina uwezo wa kubeba silaha za nyuklia.

Ndege hizo za kivita aina ya Tu-160 zilitua Venezuela Jumattau katika kile kinachoonekana kama jaribio la kuonyesha uungaji mkono wa Urusi kwa rais wa Kisoshialisti wa Venezuela Nicolás Maduro ambaye amekuwa akikabiliwa na shinikizo.

Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Mike Pompeo amesema kitendo hicho ni sawa na "serikali mbili fisadi kufuja mali ya umma."

Serikali ya Urusi imesema maneno yake hayo "hayafai hata kidogo."
 
Ndege hizo mbili za kivita zenye uwezo wa kusafiri mwendo mrefu bila kutua zilitua katika uwanja wa ndege wa Simón Bolívar viungani mwa mji mkuu wa Venezuela, Caracas, zikiandamana na ndege nyingine mbili za Urusi.

Venezuela na Urusi zimekuwa marafiki kwa muda mrefu na ndege hizo mbili za kivita ziliwahi kutumwa tena taifa hilo mwaka 2008, zikiwa pamoja na manowari moja yenye uwezo wa kurusha makombora. Ndege hizo zilifika tena Venezuela mwaka 2013.

Kitendo cha sasa kimetokea siku chache tu baada ya rais Maduro kukutana na Rais Vladimir Putin mjini Moscow.

Waziri wa Ulinzi wa Venezuela Vladimir Padrino alisema ndege hizo ni sehemu ya mazoezi ya pamoja ya kijeshi kati ya Venezuela na mshirika wake Urusi.

"Hili tunalifanya kwa pamoja na marafiki zetu, kwa sababu tuna marafiki duniani ambao hutetea na kuheshimu uhusiano wa usawa."
 
"Tunajiandaa kuilinda Venezuela hadi hatua ya mwisho ikilazimu," alisema waziri huyo akionekana kurejelea tuhuma za mara kwa mara ambazo zimekuwa zikitolewa na serikali ya nchi hiyo kwamba yapo mataifa yanayotaka kupindua serikali ya nchi hiyo.
 
Rais Maduro alisema Jumapili kwamba kuna juhudi zinazoendelea kwa sasa "zikiratibiwa moja kwa moja kutoka White House (Marekani) za kuvuruga maisha ya kidemokrasia Venezuela na kutekeleza mapinduzi dhidi ya serikali iliyochaguliwa kikatiba, kidemokrasia na iliyo huru ya taifa letu."

Bw Pompeo alishutumu kitendo cha kutumwa kwa ndege hizo za Urusi kwenye Twitter.
 
Msemaji wa Rais wa Urusi Vladimir Putin, Dmitry Peskov, amesema tamko la Pompeo si la kidiplomasia hata kidogo.

Tazama Hapa tarehe na sehemu itakayofanyika Fiesta baada ya kuahirishwa

$
0
0
Uongozi wa Clouds media group umetangaza upya tarehe na sehemu itakayofanyika Fiesta kabla ya mwaka mpya baada ya mara ya kwanza kuahirishwa katika viwanja vya Leaders jijini Dar Es Salaam.

Ikumbukwe kwamba Fiesta ilifanyika karibia mikoa 15 nchini Tanzania lakini ilipofika wakati wa kufanyika hapa Dar Es Salaam ambayo ndio ilikuwa inafunga msimu mpya wa Fiesta ilisitishwa kwa madai kwamba sehemu ambako ingeenda kufanyika ingeleta taharuki kutokana na kelele zitakazojitokeza mahala hapo.

Uongozi wa CGM umetangaza tarehe mpya na sehemu ambako Tamasha hilo litafanyika

"Tarehe 22 Disemba kwenye Viwanja vya Posta DSM, Machampion wote wa nchi wanakwenda kutoa shukrani moja kubwa na kushangalia mafanikio ya mwaka huu. 

Ni mara 2 ya tulichokimiss: stage ya viwango, sound kubwa kuliko, bata la kihistoria na list ndefu ya machampion. . #TigoFiesta2018 ". Wameandika Clouds Media

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images