Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Baraza la Vijana CHADEMA Walalamika Wafuasi Wao Kukamatwa Mahakamani Wanapokuwa Wakifuatikia Kesi ya Mbowe

0
0
Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) limelalamikia  Jeshi la Polisi kuwazuia  wanachama wa chama hicho wanaofika mahakamani kufuatilia kesi zinazowahusu vigogo wa chama hicho.

Kufuatilia hali hiyo Bavicha wamemuomba Jaji Mkuu wa Tanzania na msajili wa mahakama kuingilia kati na kutoa tamko

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na viongozi wengine saba wanakabiliwa na kesi mahakamani, mara nyingi inapotajwa, wanachama na wafuasi wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania hujitokeza kwa wingi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa Desemba 7, 2018 mwenyekiti wa Bavicha, Patrick Ole Sosopi amesema jambo hilo alilodai linafanyw ana polisi ni uvunjwaji wa haki za msingi za raia kufuatilia mashauri mbalimbali mahakamani.

Amesema tangu kesi inayowakabili vigogo hao ilipoanza kusikilizwa Machi, 2018 baadhi ya wafuasi wanaojitokeza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Mahakama Kuu wamekuwa wakikamatwa na kuhojiwa.

"Bavicha tunachukizwa kwa kweli, jana polisi walitumia nguvu kubwa kuwazuia watu kusikiliza kesi za viongozi wetu na baadhi ya vijana wetu walikamatwa kwa saa kadhaa," amesema.

Sosopi amesema kufanya hivyo ni kuvunja sheria kwa kuwa wanaohudhuria kwenye kesi hizo si wafuasi wa Chadema pekee yao bali wapo wanaokwenda kwa ajili ya kufuatilia kesi za ndugu zao.

"Kwa mwenendo huu mahakama za kiraia zimegeuzwa kuwa Mahakama za kijeshi. Tunamtaka Msajili wa Mahakama na Jaji Mkuu kutoa tamko juu ya hali hii," amesema Sosopi.

Jiji la Dar es Salaam Kuongozwa na UKAWA, CCM

0
0
Na Christina Mwagala
UCHAGUZI wa Naibu Meya wa jiji la Dar es Salaam, umefanyika leo ambapo wajumbe wa Baraza hilo wamekubaliana kwa kauli moja kuwa na Manaibu wa wili kutoka Chama Cha Wananchi CUF  na mwingine  Chama Cha Chamapinduzi CCM.

Hatua hiyo imetokana na kuwepo kwa idadi sawa ya wajumbe kwa pande zote mbili ambapo Ukawa ulikuwa na wajumbe 12 huku CCM ikiwa na wajumbe 12.

Akizungumza wakati wakutangaza uamuzi huo ulioafikiwa   na wajumbe wa Baraza hilo, Mstahiki Meya  Isaya Mwita alisema kuwa kutokana na hali hiyo kila mmoja ataongoza kwa kipindi cha miezi mitatu hadi Juni 30 mwaka 2019.

Meya Mwita alieleza wajumbe wa baraza hilo kuwa, wamefikia uamuzi huo kwani viongozi wamechaguliwa kwa ajili ya kuleta maendeleo ya waanchi bila kujali vyama vyao.

Alisema kuwepo kwa viongozi wa vyama viwili tofauti haita wakosesha wananchi maendeleo kwakuwa wote wamechaguliwa kwa lengo la kuwatumikia wakazi wa jinnini hapa.

 Meya Mwita alitumia nafai hiyo  kuwasihi manaibu hao walioteuliwa kuonyesha ushirikiano mkubwa kwa ajili ya kuleta maendeleo jijini hapa kwakuweka itikadi ya vyama vyao pembeni.

“ Ndani ya ofisi hii kupata wasaidi kutoka vyama tofauti sio dhambi, lengo langu ni kulifikisha jiji sehemu ambayo inatakiwa, ninaimani kuwa walioteuliwa leo tutasaidiana bila kujali itikadi za vyama vyetu” alisema Meya Mwita.

 Kabla ya kufanyika kwa maamuzi hayo, Meya wa Manispaa ya Kinondoni Benjamini Sita alitoa hoja baada ya kuwepo kwa mvutano mkali kuwa baraza lijigeuze kamati ilikufanya maamuzi ambayo yatakuwa na maslahi kwa wananchi kuliko kuendelea na mabishano.

“ Ndugu mwenyekiti hakuna haja ya kuendelea kubishana ,wote hapa tunafanya kazi kwa ajili ya wanachi wa jijini hapa,ningeshauri tujigeuze kamati ili kufikia muafa wa jambo hili.

 Baada ya hoja hiyo kutolewa,wajumbe wa baraza hilo walikubaliana kuwa kamati ,ambapo baada ya nusu saa,walirudi kuwa baraza na hivyo  Meya Mwita kutoa maamuzi ya uchaguzi huo.

Uchaguzi huo umefanyika leo ikiwa ni baada ya aliyekuwa Naibu Meya Mussa Kafana kujiuzulu nafasi yake na kujiunga na CCM Septemba mwaka huu.

Mwishoo.

Aliyetakatisha Bilioni 188 kupitia mashine ya EFD afikishwa mahakamani

0
0
Mfanyabiashara Mustapha Kambangwa  mkazi wa Kongowe Mbagala, jijini Dar es Salaam amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, akikabiliwa na mashtaka manne likiwemo la kukwepa kodi na kujipatia Sh.bilioni 188.9 kupitia mashine ya kieletroniki (EFD).

Mwendesha mashtaka wa Serikali Mwandamizi, Christopher Msigwa, akimsomea mashtaka  mbele ya Hakimu Mkazi Janeth Mtenga, imedaiwa kuwa katika siku tofauti kati ya Juni Mosi, 2016 na Novemba 2, 2018  Kambangwa alijifanya mtu aliyesajiliwa kuwa mlipa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) na kukusanya kodi ya VAT  Sh.188,928,752,166 kwa kujifanya anakusanya fedha hizo kwa niaba ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Shtaka la pili, mtuhumiwa  amedaiwa kati ya Juni Mosi, 2016 na Novemba 2, mwaka huu, kwa udanganyifu alitumia mashine ya kieletroniki (EFD) yenye namba 03TZ842011315 iliyosajiliwa kwa jina la Kampuni ya Abraham’s Group LTD kukwepa kodi ya VAT yenye thamani kiasi hicho cha fedha.

Aidha mshtakiwa amedaiwa kuwa katika tarehe na kipindi hicho alijipatia au kujimilikisha fedha hizo alizozipata kutokana na makato ya kodi ya VAT ambazo zilipaswa kutolewa kwa Kamishna wa TRA, ikadaiwa mshitakiwa alitenda kosa hilo huku akijua kuwa fedha hizo ni zao la kosa tangulizi la ukwepaji kodi.

Aidha imedaiwa kuwa mshtakiwa kwa vitendo vya makusudi vya kukwepa kodi alitumia mashine ya EFD na huku akijua kwamba hajasajiliwa kama mlipa kodi ya VAT na aliisababishia hasara Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ya Sh. 188,928,752,166.

Hata hivyo, mshtakiwa hakuruhusiwa kujibu chochote  mahakamani hapo kwa kuwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi za uhujumu uchumi isipokuwa kwa kibali kutoka kwa DPP.

Wakili wa Utetezi, Shamo Shadrack,  aliiomba mahakama kupanga tarehe ya karibu ili kupinga  mashtaka hayo dhidi ya mshtakiwa na kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba 17 mwaka huu kwa upelelezi haujakamilika.

Kauli ya Mwandosya Baada ya Rais Magufuli Kumuondoa Kwenye Nafasi yake ya Ukuu wa Chuo cha MUST

0
0
Profesa Mark Mwandosya amezungumzia kuondolewa kwenye nafasi yake ya ukuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Mbeya, akisema ingawa alipaswa kumaliza mwaka 2020, bado anashukuru na kumpongeza aliyechukua nafasi yake.

Jana (Alhamisi Desemba 6), Rais John Magufuli alitangaza uteuzi wa nafasi mbalimbali, huku akimteua makamu mwenyekiti wa zamani wa CCM, Pius Msekwa kuwa mkuu wa chuo hicho badala ya Mwandosya.

Baada ya uteuzi huo mpya, Profesa Mwandosya aliyetangaza kupumzika siasa, aliandika kwenye akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Twitter akimpongeza Msekwa kwa kumpokea kijiti na kukishukuru chuo hicho kwa ushirikiano waliompa.

“Aprili 2014  Kikwete aliniteua mkuu wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya kwa kipindi kinachoishia 2020. Mheshimiwa Pius Msekwa anachukua nafasi hiyo kuanzia leo. Nampongeza. Nashukuru kwa heshima ya kuwa mlezi mkuu wa chuo,” ameandika Profesa Mwandosya.

Hivi karibuni pia, Mwandosya aliondolewa katika nafasi ya Uenyekiti wa bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere(MNMA) na nafasi yake kuchukuliwa na waziri na mbunge wa zamani wa Bunda, Steven Wassira.

Baada ya mabadiliko hayo, Profesa Mwandosya aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter akilezea shukrani zake huku akimnukuu Mwalimu Julius Nyerere kuwa alifundisha kushukuru kwa fursa yoyote unayopewa katika utumishi wa umma.

Zito Kabwe Awasilisha Ushahidi TAKUKURU

0
0
Leo Ijumaa Desemba 7, 2018 mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe amewasilisha vielelezo vya ushahidi katika ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Maelezo hayo ni kuhusu madai yake ya kampuni tatu za chuma kuwahonga baadhi ya viongozi wa Serikali.

Baada ya kauli yake hiyo,  Takukuru ilimuomba mbunge huyo afike ofisi za taasisi hiyo jijini Dar es Salaam ili kushirikiana kushughulikia suala hilo muhimu.

Katika mitandao ya kijamii Zitto anadaiwa kuandika kuwa amepata habari za kushtua kuwa kampuni tatu za China, Urusi na Uturuki zimewahonga baadhi ya watendaji wa Serikali kuchelewesha  mradi wa Mchuchuma na Liganga, lengo ni kuhakikisha nchi hizo zinapata soko la chuma chao.

Akizungumza leo baada ya kuwasilisha maelezo yake amesema, “Baada ya kupata taarifa hizo niliwaeleza kuwa ninaweza kufika leo. Nimefika na nimetoa maelezo ya sababu ninazoziamini za ucheleweshaji wa mradi huo kuwa ni za makusudi na zimefanywa na Serikali.”

Amesema ucheleweshaji huo ni kwa ajili ya kunufaisha kampuni zinazoingiza  bidhaa zinazotumika kwenye miradi ya chuma kama kampuni zinazojenga reli ya kati na kuagiza chuma kutoka nje badala ya kutoka ndani ili kukuza uchumi.

“Mradi wa Mchuchuma na Liganga ungekuwa umeanza mkandarasi asingeagiza chuma kutoka nje angenunua hapa ndani hata kwenye mradi wa bomba la mafuta mkandarasi naye angefanya hivyo.”amesema

Amesema baada ya maelezo yake hayo ameiomba Takukuru kuendelea kuchunguza uagizaji wa bidhaa za chuma ambazo viwanda vya ndani vina uwezo wa kutengeneza, lengo likiwa ni kupata ukweli wa jambo hilo na kwamba kesho atawasilisha tena maelezo yake.

Waziri Mkuu Atoboa Siri ya Kuvunjwa kwa bodi ya Shirika la Hifadhi ya Jamii NSSF.

0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Desemba 7, 2018, ametoboa siri ya kuvunjwa kwa bodi ya Shirika la Hifadhi ya Jamii NSSF.

Amtetoboa siri hiyo alipotembelea kiwanda cha kuzalisha sukari cha Mkulazi namba mbili kilichopo Gereza la Mbigiri wilayani Kilosa mkoani Morogoro leo.

Majaliwa amesema alikuwa akipata taarifa kutoka kwa uongozi uliopita kuwa mradi unaendelea vyema, lakini baada ya kuwatuma wataalamu mbalimbali kutembelea mradi huo ulionekana kusuasua, Serikali iliamua kuchukua hatua ya kuivunja bodi hiyo pamoja na idara nyingine zilizokuwa zikihusika na mradi huo.

Ameipongeza bodi mpya ya NSSF na Mkulazi kwa namna zinavyoshirikiana na Jeshi la Magereza katika kutatua changamoto zilizopo  pamoja na  kuwafikia wakulima wa nje wa miwa katika kiwanda hicho.

Waziri Mkuu ameziagiza bodi mbili zilizoteuliwa hivi karibuni za NSSF na ile ya Mkulazi, kufanya jitihada za kutosha kuhakikisha mradi wa kiwanda cha sukari cha Mkulazi namba mbili unakamilika kama ilivyopangwa.

Amezitaka kuimarisha mfumo wa  maji na kuangalia namna nzuri ya kuyadhibiti yanayopotea kipindi cha mvua ili yaweze kusaidia wakati wa kiangazi kwa nia ya kuzalisha miwa kwa wingi na isikauke kama ilivyo sasa.

Ametaka pia kuimarishwa kwa mashine za umwagiliaji, kutafuta nyingine mpya ili kuondokana na changamoto ya sasa ukosefu wa mashine mpya za kusaga miwa.

Pia amewaagiza wakuu wa wilaya za Kilosa na Mvomero kuwahimiza wananchi kulima miwa jirani na kiwanda hicho cha Mkulazi kinachoendeshwa na Serikali kupitia NSSF kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza.

Amesema kwa kufanya hivyo, viwanda vilivyopo vitazalisha sukari ya kutosha na kuondokana na utegemezi na gharama kubwa za uagizaji wa sukari toka nje ya nchi.

Mbali na kutoa maagizo hayo, Majaliwa amewataka watumishi wa serikali kuchangamkia fursa ya kulima mashamba yaliyo jirani na kiwanda hicho ili kujipatia kipato.

Mwenyekiti wa bodi mpya mbia ya Mkulazi Holding Company, Dk Hildelitha Msita amezungumzia namna walivyotekeleza maagizo ya waziri mkuu baada ya awali kusua sua kwa kiwanda hicho na changamoto zilizopo hasa umeme na ukame.

Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Kazi, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenister Mhagama amesema anaamini mradi huo utakuwa wa mfano na wabia wanatakiwa kukubaliana huku wakiongozwa na uzalendo na uaminifu.

Naibu waziri wa Kilimo Omary Mgumba kwa upande wake amemuomba waziri mkuu kusaidia kiwanda cha mkulazi namba moja nacho kianze uzalishaji .

Mahakama Kuu Yamwachia Huru Aliyemuua Mtu Aliyekuwa Akimbaka Mkewe

0
0
Jaji wa Mahakama Kuu kanda ya Tabora, John Utamwa amemwachia bila masharti mkazi wa kijiji cha Mahene Wilaya ya Nzega aliyekiri kumuua bila kukusudia mtu anayedaiwa kumbaka mkewe.

Kabla ya uamuzi huo upande wa Jamhuri ukiongozwa na wakili Tito Mwakalinga umedai Oktoba 12, 2016 mshitakiwa alisababisha kifo cha Mabula Ngassa kwa kumpiga  fimbo na kumsababishia majeraha mwilini.

Wakili Mwakalinga amesema siku hiyo mshtakiwa alirejea nyumbani kutoka katika harusi ya jirani yake na kukuta mlango wa nyumba yake umevunjwa huku sauti ya mkewe ikisikika akiomba msaada.

Ilielezwa kuwa mshtakiwa alikuta mkewe akibakwa huku watu wengine wawili wakiwa wamemshikilia, kuamua kutumia fimbo kumpiga aliyekuwa akifanya kitendo hicho.

Akitoa uamuzi wa shauri hilo,  Jaji Utamwa amesema  baada ya kusikiliza pande zote mahakama imezingatia kwamba mazingira ya mauaji yalitokana na mshitakiwa  kukuta mkewe akiomba msaada wake kwani alikuwa anabakwa.

Ameeleza kuwa mahakama imekubali maelezo ya wakili wa utetezi,  Chombala Kanani kwamba mshitakiwa alisababisha kifo kwa kwenda kufanya kosa kubwa la jinai ambalo hata adhabu yake ni kubwa kisheria.

Amebainisha kuwa mshtakiwa alikuwa anachukua hatua ya kumlinda mkewe  kwa kumtetea dhidi ya hatari aliyokuwa anakabiliana nayo ya kubakwa kosa ambalo lilikuwa linafanywa na watu ambao asingeweza kupimana nao nguvu.

Jaji  Utamwa amesema alitumia fimbo aliyoiokota eneo la tukio tena kwa kuirusha ikiwa ni njia ya kujihami kwa ikizingatiwa kuwa ilikuwa usiku.

Chombala aliiomba mahakama itoe adhabu ndogo  hata kwa kumwachia kwa masharti mshitakiwa kwani  ni mkosaji wa mara ya kwanza, ana familia   na watoto wanaomtegemea.

Pia wakili huyo alieleza kwamba mshitakiwa tayari alikiri tangu siku ya kwanza alipokamatwa na hakuisumbua mahakama hivyo amepunguza gharama na muda.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya Disemba 8


Video Mpya ya Davido: Wonder Woman

0
0
Msanii wa muziki kutokea nchini Nigeria, Davido anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Wonder Woman.

Video Mpya ya Tekno: On You....Itazame Hapa

0
0
Msanii wa muziki kutokea nchini Nigeria, Tekno anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la On You. Itazame hapo chini

Video Mpya: Chin Bees - Ladha

0
0
Msanii wa muziki Bongo, Chin Bees ameachia video ya wimbo wake unaokwenda kwa jina la Ladha. Itazame hapa.

Waziri Jafo: Mabosi Wengine Wana Roho Mbaya Kama Nyoka

0
0
Waziri  wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Selemani Jafo, amesema kuna baadhi ya watumishi na viongozi serikalini wana roho mbaya kama nyoka.
 
Amesema kuna baadhi ya watumishi ambao wamekuwa wakijijali wenyewe kuliko watumishi walioko chini yao na kusisitiza kuwa kama wapo katika wizara yake washindwe na walegee.

Aliyasema hayo juzi wakati wa utoaji tuzo ya utumishi iliyotukuka kwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mussa Iyombe, iliyotolewa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (Jica).

“Tuwe na upendo, tusiwe na tabia ya nyoka, maana nyoka namfahamu hata akiwa mfupi au mrefu lakini roho yake mbaya atamgonga nyati, kumla hawezi lakini basi tu,” alisema Jafo na kusababisha watu kuangua kicheko.

Jafo alisema kuna baadhi ya watumishi wanafanya mambo ya aibu na kuna baadhi ya mabosi wanaposafiri na madareva wao kwenda mikoani, wanakaa na pesa za mafuta badala ya kuwakabidhi madereva.

Alisema pindi mafuta yanapoisha mabosi hao ndipo wanatoa pesa na kuwapa madereva, lakini jambo la kushangaza wakati wa kufanya marejesho ya pesa madereva ndio wanahusika.

“Leo hii Katibu Mkuu (Iyombe) kuna watu wanafanya mambo ya aibu. Utakuta dereva wa kawaida unatoka naye safari hapa unaenda Geita. Mmetia saini pesa ya mafuta na posho lakini pesa ya mafuta ya dereva anakaa nayo bosi,” alisema na kuongeza:

“Yaani hadi taa ya mafuta inawaka dereva anachanganyikiwa anamuuliza bosi, bosi mafuta yameisha, bosi anaingia mfukoni anatoa pesa na kumpa dereva akanunue mafuta wakati pesa ya mafuta ametia dereva halafu retirement (ujereshaji masurufu) anafanya dereva. Hiyo ni roho mbaya iliyopitiliza katika maisha ya binadamu na mimi nasema kama hao watu wapo ofisini kwangu washindwe na walegee,” alisema Jafo.

Jafo alisema kuna baadhi ya idara ambazo watumishi wadogo wasiokuwa na sauti wananyimwa fursa pindi zinapotokea, huku baadhi ya watumishi wakipendelewa kwa kupewa fursa mara kwa mara na mabosi.

“Lakini kuna idara zingine watu wadogo kabisa wasiokuwa na sauti hata fursa ananyimwa, inatakiwa mtu apewe fursa achangamke, mtu anakuwa na watu wake hao hao anaowapa fursa, unakaa na watu ofisini watu wanamawazo wanaona kama wametengwa wanamsongo wa mawazo, hili ni jambo baya zaidi,” alisema.

“Jambo kama hili ndilo linasababisha watu wanakuwa na matabaka, kero, machungu, nendeni mkawe wema,” alisema Waziri Jafo.
 
Waziri Jafo aliwataka watumishi kubadilika na kuwa na roho nzuri na wanapaswa kujifunza kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara yake Musa Iyombe.

Aliyekuwa Mkurugenzi Halmashauri ya wilaya ya Sikonge Akamatwa na Jeshi la Polisi Kwa Kujifanya Usalama wa Taifa

0
0
Na.Alex Sonna,Dodoma
Jeshi la polisi mkoa wa Dodoma limefanikiwa kuwakamata watu wawili waliojifanya kuwa maafisa usalama wa Taifa waliojitambulisha kwa Mkurugenzi wa Utumishi Wizara ya Nchi ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kwa kutaka wapangiwe kazi idara ya elimu wakati siyo wafanyakazi. 
 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma Gilles Muroto amesema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa,na kuwataja watu hao ni Simon Ngatunga (38) mkazi wa Makulu Dodoma,na Razin Katundu (29) mkazi wa Yombo Buza Dar-es-Salaam.
 
Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi alisema kuwa Ngatunga aliwahi kuwa Mkurugenzi Halmashauri ya wilaya ya Sikonge  Tabora ambaye alitumbuliwa na Rais Dkt Magufuli.
 
Amesema kuwa Katundu (29) alikamatwa kutokana na kitendo chake cha kutaka kusaidiwa na Ngatunga ili aweza kumfanikishia kupangiwa kazi idara ya elimu ambayo imekuwa na safari nyingi za nje ya ofisi ambapo kwa upande wake angekuwa akijipatia kipato cha ziada.
 
Aidha jeshi hilo linamshikilia Salum Pwao (31) mkazi wa Tabata kwa kujifanya afisa wa PSSSF anayeshughulikia mafao ya wastaafu ili waweze kulipwa mafao yao.
 
“Huyu Pwao amekuwa na tabia ya kuwapigia simu waastafu wanaofuatilia mafao yao na kuwadai fedha kwa ajili ya kushughulikia mafao yao hayo ili yaweze kutoka kwa haraka huku akiwadanganya pia mafaili yao yapo mezani kwake”alisema.
 
Kamanda huyo wa polisi katika uperesheni yake hiyo inayoendelea ikiwemo na misako alisema kuwa pia imemkamata mtuhumiwa Yona Julias (32) mkazi wa Dar-es – Salaam kwa tuhuma za utapeli wa viwanja.
 
Alisema mtu huyo amekuwa akiwatapeli watu mbalimbali kwa kupitia kampuni yake anayoimiloki inayofahamika kwa jina la Vijana Kwanza Project inayojihusisa na upimaji wa viwanja.
 
Alisema kwa kutumia utapeli wake huo ameweza kuwaibia fedha wananchi wa mikoa ya Dar-es- Slaam,Arusha na Dodoma na kuwaahidi kuwapimia viwanja na kukamilisha kisha kutokomea.
 
Pia jeshi hilo katika uperesheni yake hiyo limefanikiwa kuwakamata watu wawili kwa kosa la kupatikana na bhangi na misokoto 40 eneo la kikuyu katika jiji la Dodoma.
 
Amewataja watu hao ni pamoja na Sham Jibrea (35)  na Meck Maula (40) wote wakazi wa mtaa wa Kinyambwa Kikuyu ambao watumiwa hao wamekuwa wakijihusisha na biashara ya madawa ya kulevya aina ya bhangi kwa kuwauzia wateja.
 
Hata hivyo kamanda huyo alitoa angalizo katika kipindi hiki cha kuelekea sikukuu ya Christmass na mwaka mpya madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani kwa kujiepusha na mwendo kasi.
 
Aidha watu wasijihusishe na uhalifu wa aina yoyote kwa kuwa uhalifu hauna nafasi na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi hili la polisi pindi wanapotilia shaka kwa vitendo vyovyote vibaya.

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 41

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA  
“Ethan ngoja kwanza usimuue”
Ethan alizungumza huku akinitazama.
“Kwa nini?”       
“Kwa kumtumia huyu basi tutahakikisha huyo mwana mama anaenguliwa katika kasi za kugombania uraisi na itazidi kumpa nguvu baba mkwe wako kushinda uchaguzi wa uraisi”
Ethna alizungumza kwa upole, kabla sijafanya chochote simu ya mwanasheria huyu iliyopo kwenye koti lake la suti ikaanza kuita, nikampasa kwa haraka na nikaitoa. Nikakuta namba hiyo ni ya mke wake, nikamuonyesha kisha nikaipokea na kuiweka sikioni mwangu.
“Mume fiki wapi mume wangu. Nipe habari njema”
“SIO HABARI NJEMA, NI HABARI MBAYA MUME WAKO AMEFARIKI DUNIANI”
Nilizungumza kwa sauti nzito na iliyo jaa mikwaruzo mingi sana na kumfanya mwana mama huyo kukaa kimya kwa sekunde kadhaa akisikilizia sauti yangu.

ENDELEA   
“JIANDAE NINAKUJA KWA AJILI YAKO”
Baada ya kumaliza kuzungumza maneno hayo nikakata simu huku nikimtazama mwanasheria wangu aliye amua kunisaliti kwa ajili ya mke wake.
“Ngoja nikachukue gari”
Ethan alizungumza huku akiondoka katika eneo hili. Mwanasheria hakuzungumza kitu chochote zaidi ya kuendelea kumwagikwa na machozi usoni mwake.
“Endapo nitagundua umefanya udanganyifu kwenye kitu chochote ndani ya kampuni yangu. Ninakuapia kwa jina la marehemu yangu. Lazima nitakua, umenielewa wewe mpuuzi”
Mwanasheria akazidi kulia kwa uchungu sana huku akionekana kujutia kwa maamuzi ya kijinga aliyo yafanya.
“Mke wako kwa nini amekuwa na roho mbaya kiasi hichi ehee?”
Camila alimuuliza mwanasheria, ila mwanasheria akaishia kumtazama Camila tu.
“Ila Mungu ni mwema, unakumbuka jana nilikuambia tuondoke pale hospitalini?”
 
“Ndio”
“Na nilikueleza kwamba yule sio mama yangu”
“Ndio”
“Niliustukia mpango wa huyu mzee. Yaani sijui ulikuwa unanichukuliaje. Kumbuka nimebakisha siku kumi tu kuingia umri wa miaka kumi na nane sasa wewe endelea kuleta ujinga wako mzee. Mimi sio mtoto na hata nikiwa katika umri huu huwezi kunidanganya. Mjinga wewe”
Tukamuona Ethan akisimamisha gari katika eneo lenye barabara. Akashuka na kutufwata sehemu hii tulipo. Akamnyanyua mwanasheria wangu na kumfunga pingu za mikononi mwake. Akampeleka moja kwa moja kwenye gari na kumuingiza siti ya nyuma huku nasi tukiwa nyuma yao.
“Mjini kwa sasa kila sehemu ina kaguliwa na askari kuwatafuta nyinyi mulipo, kwani habari ya kutekwa kwenu imesambaa kila mahali. Sawa”
 
“Sawa je wewe uungani nasi?”
Camila alizungumza huku akimtazama Ethan usoni mwake.
“Hapana mimi nitaondoka na hii pikipiki”
“Sawa”
“Ila angalizo, hakikisheni kwamba munampeleka katika sehemu ambayo itakuwa ni salama kwa nyinyi kumshikilia kwa kipindi chote katika kuhakikisha kwamba muna muangusha mke wake katika kumtoa katika kinyang’anyiro cha kuiongoza nchi hiyo.”
“Sawa nimekuelewa”
“Ila nitaendelea kuwalinda kwa ukaribu na sasa hivi Ethan hakikisheni kwamba kila hatua ya jambo linalo watatiza munaipiga na nitakuwa pamoja nanyi. Mumenielewa”
“Sawa”
“Shemeji safari jema”
“Nashukuru”
 
Tukaingia kwenye gari siti za mbele. Camila akaishika bastola yake na kumuelekezea mwanasheria aliye kalishwa siti ya nyuma. Nikawasha gari hili na kuanza kuondoka katika eneo hili kwa mwendo wa kasi. Kutokana gari hili lina GPRS haikuwa tabu kwa sisi kuusaka mji wa Berilin amboa ndipo tunapo ishi.
“Baby”
“Mmmm”
“Yule umesema anaitwa Ethan?”
“Ndio”
“Ni mtu kweli?”
Nikamtazama Camila usoni mwake, kisha nikatingisha kichwa nikimaanisha kwamba sio mtu. Camila akanielewa jibu langu huku akinitazama machoni mwangu.
 
“Ethan”
Mwanasheria aliniita kwa sauti ya upole na iliyo jaa unyenyekevu, nikamtazama kwa kupitia kioo kidogo kilichopo juu upande wangu wa kulia.
“Ehee”
“Vita ulio ingia ni kubwa sana mwanangu. Ninakuonea huruma kubwa sana”
“Pumbavu wewe nyamaza. Unahisi kwamba ninaogopa. Kama ulishindwa kuniua leo basi tambua kwamba hamuto niweze kuniua hata siku zijazo. Hata mukija watu laki, Mungu yu pamoja nami na hamutoweza kufanya lolote kwangu”
Nilizungumza kwa kujiamini sana huku nikiendelea kuendesha gari hili kwa kasi.
“Natambua hilo ila vita hii amekuachia baba yako mzee Klopp”
 
“Eti ehee?”
“Ndio, mali alizo zulimu, watu alio waua kipindi cha uhai wake. Damu zao zipo mikononi mwako, kwani wewe ndio mrithi wa mali zake. Leo hii umenionyesha na wewe una ukatili kama wa baba yako kwa maana umemuua dereva wangu ambaye hakuwa na hatia yoyote kwenye hili swala”
Nikayafumba macho yangu kwa sekunde kadha kisha nikafunga breki za gafla hadi Camila akashangaa. Nikashuka kwenye gari na kufungua mlango wa siti za nyuma, nimatoa mwana sheria kwa nguvu na kumbwaga chini. Nikaanza kumpiga mateke ya tumboni mwake huku nikimtukana matusi ya kila aina.
 
“Baby baby acha tafadhali”
Camila alizungumza huku akanisogeza pembeni kwani mateke niliyokuwa ninampiga mwana sheri kwa hakika yanaweza kumsababishia kifo.
“Mume wangu tuliza jazba kidogo. Kumbuka huyu mzee tunamuhitaji katika haya mapambano. Unavyo endelea kumpiga hivyo utazidi kumsababishia matatizo na mwishowe atakufa sawa mume wangu”
Camila alizungumza huku akiwa amenishika mashavu yangu. Akanibiga busu moja matata mdomoni mwangu, busu hili taratibu likazifanya hisia zangu za hasira kuanza kushuka taratibu na nikarudi katika hali yangu ya kawaida.
 
“Tambua nina kutegemea sana mume wangu. Tambua hii vita ni ya kwetu wote. Maisha ya baba yangu yapo hatiana na hata familia yangu kwa sasa ipo mashakani. Tafadhali ninakuomba mume wangu uwe mpole sawa baba”
“Nimekuelewa mke wangu”
Nilizungumza kwa upole kisha nikamnyanyua mwanasheria na kumuingiza ndani ya gari. Tukaendelea na safari hii huku akilini mwangu nikifikiria ni sehemu gani ambayo ninaweza kumpeleka huyu mwana sheria. Taratibu nikapunguz amwendo wa gari na kulisimamisha pembezoni mwa barabara. 
 
“Huyu mtu mjini hatuwezi kumpeleka mke wangu ni hatari”
“Kweli ni hatari mume wangu, nami nilikuwa ninaliwaza jambo hilo ila nikashindwa tu kukuanza”
“Hufahamu sehemu yoyote ambayo tunaweza kupata nyumba ya kumhifahdhi huyu shetani?”
“Mmmmm sifahamu”
Tukiwa katik ahali ya kujiuliza maswali ya hapa na pale, tukaanza kuona helicopter mbili za jeshi la nchi hii ya Ujerumani zikija mbele yetu. Nikakata kuwasha gari ila Camila akanizuia.
“Wamekuja kwa ajili yetu hawa”
“Una uhakika?”
“Ndio mume wangu, naamini kwa kutumia satelaiti wameweza kufahamu sehemu tulipo”
“Umejuaje?”
 
“Kumbuka hata kwa kupitia sura zetu tunaweza kutafutwa na kujulikana ni wapi tulipo na mbaya zaidi pale ulipo shuka kwenye gari na kuanza kumuadhibu huyu mzee nayo pia imechangia”
Camila alizungumza huku tukishuhudia helicopter hizo zikianza kusimama taratibu mita kadhaa kutoka sehemu ilipo gari letu. Wakashuka wanajeshi zaidi ya kumi na mbili, taratibu tukashuka kwenye gari hili. Wanajeshi hawa wakafika katika eneo hili.
“Ninaitwa Camptein Gudluck, kutoka jeshi la anga. Tupo hapa kwa ajili ya kuwaokoa.”
 
Mwanajeshi mmoja alizungumza huku akitupa mikono.
“Mumefahmu vipi kwamba tupo hapa?”
Nilimuuliza mwanajeshi huyu huku nikimkazia macho usoni mwake.
“Kupitia satelaiti”
Mwanajeshi huyu alizungumza huku akinionyesha alama ndogo inayo onekana kwenye simu yake aina ya iphone 6. Mapigo ya moyo yakanistuka mara baada ya kuona chata ndogo kwenye mkono wa mmoja wa huyu mwanajeshi. Chata hii ikanikumbusha vijana wa mwanasheria ambao aliwaagiza kwenda kunitafutia mama yangu nchini Tanzania.
 
‘Ohoo Mungu wangu, tumeingia tena mikono ni mwao’
Nilizungumza kimoyo moyo huku nikimkanyaga Camila kwenye mguu wake. Gafla helicopter moja ikalipuka na kutuchanganya watu wote katika eneo hili.
“Rudi kwenye gari”
Nilimuambia Camila kwa sauti ya ukali. Camila hakuhitaji kupoteza muda, kwa haraka akarudi kwenye gari huku nami nikirudi kwenye gari. Nikaliwasha gari hili na kuanza kulirudisha nyuma na kuwafanya wanajeshi hawa kuendelea kutushambulia kwa risasi.
 
“Mungu wangu ni kina nani wale!!?”
Camila alizungumza huku akiwa amejawa na mstuko mkubwa sana.
“Ni watu wa huyu mzee”
“Ohoo samahani mume wangu kwa kukuamisha kwamba ni watu wa serikali. Tukashuhudia helicopter nyingine nayo ikilipuka mlipuko mmoja mkali sana. Wanajeshi wanao tushambulia tukawashuhudia jinsi wanavyo anguka mmoja baada ya mwengine.
 
“Nilikuambia Ethan, hii vita si ndog….”
“Nyamaza nguruwe wewe”
Nilizungumza huku niligeuza gari hili kwa kasi sana, likayumba kidogo ila nikafanikiwa kuliweka sawa.
“Tupa hiyo simu ya huyo mzee”
Tuliisikia sauti ya Ethan akizungumza nasi, tukatazamana na Camila usoni mwetu. Nikaanza kujipapasa mifukoni mwangu na kuipata simu ya mzee huyu, nikashusha kioo kidogo na kuitupa dirishani na kuanza safari ya kutokomea sehemu ambayo kwa kweli hatuifahamu na hatujui ni nini hatima yetu na mwanasheria wangu huyu.

==>>ITAENDELEA KESHO

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 168 na 169 )

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   
   
“Laiti kama wangeweka bomu basi hii ingekuwa shabaha yangu ya pekee kuhakikisha kwamba K2 anakufa”
“Ni kweli, ila kama mtu mmoja simuoni katika walinzi wake ikiwa wasichana wengine nimewaona”
“Nani?”
“Livna Livba”
Hata kabla sijatazama vizuri, mlango wa hapa sebleni ukafunguliwa. Sote tukajikuta tukigeuka nyuma, tukamuona Martin akiingia humu ndani ila uso wake ukivuja damu na ametulia sana, akaingia na Winy naye jicho moja limemvimba, nikaishika bunduki yangu vizuri huku nikipiga hatua moja mbele. Martin akatingisha kichwa akishiria kunikataza kusogea mbele kwani kufanya hivyo inaweza kuwa hatari kwangu, kwani sifahamu ni nani aliyopo nyuma  yao.
   
ENDELEA   
Taratibu tukaona viatu vyeusi vya kijeshi, hatukamaliza hata sekunde moja, sura ya Livna ikasimama mbele yetu huku mikononi mwake akiwa ameshika  bastola mbili huku amewanyoshea Winy na Martin kwenye vichwa vyao.
“Halooo Dany”   
Sauti ya Livna haijabadilika kabisa, hata sura yake ni ile ile kabisa.
“Pigeni magoti nyinyi wajinga”
Livna alizungumza kwa kwa ukali, taratibu Winy na Martina wakapiga magoti chini jambo lililo anza kuniumiza akili yangu kwani siwezi kufanya chochote kibaya kwani kitahatarisha maisha ya hawa watu wawili ambao ni muhimu sana kwangu hususani Martin.
“Vijana wako bwana waliingia vibaya kwangu, sikuwa na jinsi zaidi ya kuwafanya hivi japo huyu mseng** hapa alikuwa ni mume wangu”
 
Livna alizungumza huku akimpiga teke la mgongo Martin.
“Sikuja hapa kukukamata ila nimekuja hapa kukusaidia”
“Kunisaidia?”
“Ndio kukusaidia, natambua kiu yako ni kumuua K2 si ndio?”
Nikakaa kimya kwa sekunde kadhaa huku nikimtazama Livna, taratibu akazichomeka bastola zake kwenye kiuno chake na kuanza kutembea hadi sehemu lilipo sofa na kukaa taratibu.
“Martin unatakiwa kujifunza zaidi maswala ya kupigana, na wewe dada nawe hivyo hivyo”
Uwepo wa Livna humu ndani ukazidi kunishangaza na hata maneno yake yanazidi kunishangaza. Kupigwa kwa Martin na Winy kwangu wala sishangai sana kwani hata mimi nilisha wahi kukutana na kipigo chake nilipo kuwa na Mariana kwenye meli nilipo kuwa ninatoroka nchini Tanzania.
 
“Mbona muna shangaa shangaa vipi nimekuwa kituko eheee”
“Martin mumefanya nini sasa?”
Nilimuuliza Martin huku nikimtazama usoni mwake.
“Samahani mkuu, nilitamani kuonana naye ndio yakatokea haya”
“Kwa nini mumemleta hapa?”
“Dany acha kumkoromea mwenzako. Mshukuru Martin amenishawishi sana kuweza kuungana nawe”
“Livna huwezi kuungana nami ikiwa uliweza kusaliti baba yangu na akafa, leo hii utaungana nami kivipi?”
 
“Baba yako alienenda tofauti na makubaliano yetu na pia K2 ameenenda kinyume na makubaliano yetu je wewe utaenenda kinyume na makubaliano yetu”
“Makubaliano yapi?”
“Moja nahitaji kizazi changu cha wasichana nilio wafunza mafunzo maalumu kubaki kama walivyo na sinto hitaji kuona kuna mkuu yoyote anaye hitaji kujimilikisha kikosi hicho kama alivyo fanya baba yako eti kisa anapesa. Na pia K2 ndivyo anavyo fanya, anawatumikisha wasichana wangu, wanajitolea maisha yao pasipo yeye kufahamu ni thamani gani hao wasichana walivyo na hata akifa msichana mmoja kwangu ni hasara kubwa inayo niumiza sana”
 
 “Mimi kikosi chako sina kisasi nacho na laiti wakihitaji kuendelea kumkumbatia K2 nitahakikisha kwamba ninawaua nao”
“Kuwaua unaweza, na mimi nitakuua kwa maana sishindwi kukuua Dany. Ila bado hujakomaa kwenye vita ambayo ungehitaji kuufanya kwani kumuua msichana wangu basi ineyagarimu maisha yako”
 
Livna alizungumza kwa kujiamini sana. Ili maisha yako yasiende bure nikaamua kukupa hii ofa, ili uweze kulipiza kwa yale yaliyo tokea kwa baba yako na familia yako kwa uzima”
“Una jambo jingine?”
“Ndio ninalo kwa nini nikose. Hakikisha kwamba unanipa orodha ya maadui zako wote sawa”
“Umezungumza ya kwako ngoja na mimi nizungumze yangu. Moja ofa yako nimeikubali. Mbili ukijaribu kunisaliti, nitakuaa, kwa maana Dany wa miaka ile si wa miaka hii ya sasa. Tatu maadui wangu ni watatu na ikiwezekana nitahitaji kabla ya masaa ishirini na nne yajayo wawe wamesha ondoka duniani sawa.”
 
“Sawa hilo ni jambo raisi. Oya bado hamjanyanyuka tu”
Martin na Winy wakanyanyuka, Babyanka akaanza kuwapa huduma ya kwanza kwani nyuso zao zimebadilika kwa kipigo walicho weza kukipata huko walipo toka.
“Jamani ninaombeni maji ya kunywa?”   
Livna alizungumza huku akikaa vizuri kwenye hili sofa. Babyanka akafungua friji na kutoa chupa ndogo ya maji ya kinywa na kukamabidhi Livna.
 
“Kuna sababu nyengine ya kumsaliti K2 zaidi ya hiyo ambayo umeniambia?”
“Sababu zipo ila ni ndogo ndogo sana”
“Kama?”
“Kujiachukulia tu wasichana nao wahitaji kwenye kikundi changu, kuto kuwalipa vizuri pia ni jambo ambalo kidogo limenifanya moyo wangu kila siku niwe na maumivu”
“Kweli?”
Nilimuuliza Livna huku nikiwa nimekazia macho usoni mwake.
“Ndio”
“Kwa nini ulishindwa kumuua ikiwa anaenenda kinyume nawe?”
 
“Sipendi kuua, na kikosi changu nilikiunda kwa sheria ya kulinda wale watakao lipa pesa kwa ajili ya sisi kuwalinda”
“Ilikuwaje K2 akachukau madaraka ya katika kikosi chako?”
“Baba yako na K2 ndio walikuwa walezi wa kile kikosi, walitoa pesa zao nyingi sana. K2 akamgeuka baba yako baada ya kuzidiwa kwa kutoa matumizi, akaamua kumuua, kwa kutumia watu wake wa karibu sana. Sasa yeye ndio akabaki kuwa na nguvu katika kikosi, ila mimi ndio niliachia kikosi hichi na muanzilishi tangu nikiwa mdogo sana.”
“Muanzilishi wa hicho kikosi ni nani?”
“Huwezi kumfahamu ni mama mmoja wa Kijapani na yeye ndio aliye nipatia mafunzo ambayo leo hii ninaweza kuwapatia wezangu”
“Sawa, sasa ninasikiliza mbinu zako ambazo tunaweza kuzitumia kumuangamiza K2, raisi Donald Bush na mke wa raisi bi Hawa Donald?”
“Hao wawili nao wameingia kwenye kumi na nane zako?”
“Ndio”
 
“Ilikuwaje?”
“Hupaswi kufahamu?”
“Basi kwa hao wawili nitajitoa kwa maana siwezi kufanya kazi pasipo kujua huyo ninayetakiwa kumuhudumia amefanya jambo gani kwako”
“Hawa alikuwa mke wangu”
“Ndio  uliye funga naye ndoa, kwa maana kidoleni una pete ya ndoa?”
“Hapana”
“Kwa hiyo alikuwa hawara?”
“Nilipokonywa na raisi huyo baada ya kunipeleka katika mission ambazo ni hatari kubwa. Moja ilikuwa ni kuvuruga kikundi cha Al-Shabab nchini Somalia na nilifanikiwa kukisambaratisha, mbili ilikuwa ni kukisambaratisha kikosi cha Boko haramu nchini Tanzania”
 
“Kweli Dany umebadilika vikosi vyote hiyo viwili uliweza kuvisambaratisha?”
“Niliweza kwenye Al-Shabab, ila kwenye hicho kikosi cha Boko  haramu nilikuwa jeneral wao, baada ya kuona nimesalitiwa na raisi Donald Bush. Nilimsamehe kwa kumchukua mke wangu, ila hakuona kama msamaha wangu una tija akatuma makomandoo wake waniangamize ila nilifanikiwa kuwaua. Nilipata mke mwengine niliye funga naye ndoa, wakaona haitoshi, mke wake akatuma watu wakamuua mtoto wa mke wangu isitoshe wakakisambaratisha kikosi kizima”
 
“Duuu kweli wanahaki ya kuuwawa. Si uliwasamehe kabisa baada ya kuchukuana wao?”
“Ndio”
“Hata kama ni mimi ningewaua”
“Natamani hata kwenda kuwaua leo nasikia wamelala hapo Serena Hoteli?”
“Nani kazungumza?”
Nikamtazama Winy ambaye tayari amefutwa futwa damu usoni mwake.
 
“Hapana hapo Serena wamelala wapambe wake tuu ila raisi na mke wake wapo katika manuari ya jeshi la Marekanani na huko si rahisi kwa mtu yoyote kuweza kuwafikia na kuwaua”
“Mmmmm”
“Ndio hivyo, ukihitaji kumua raisi wao labda kwneye hizo ziara zake anazo anza kesho”
“Anazianzia wapi?”
“Anaanza kutembelea daraja la Kigaoni kukagua kagua mradi huo”
“Sawa na ni saa ngapi?”
“Majira ya asubuhi tu”
“Dany”
 
Babyanka aliniita huku akinitazama, nikamsogelea sehemu alipo kaa kwenye kiti.
“K2 amekipata kichwa cha jamaa yake, na ujumbe ulio andikwa ameusoma tayari?”
Babyanka alizungumza huku akiirudisha video hiyo aliyo irekodi nyuma kidogo.
“Mbona analia K2?”
Livna aliuliza huku akisimama pembeni yangu.
“Tumemchinja mume wake.”
“Eheheee Dany umechokoza moto, mama anakwenda kuvaa gwanda leo”
 
“Shauri yake mkuki kwa nguruwe ndio mtamu ila kwa binadamu ni mchungu sana”
“Mmmm, sasa ilikuwaje mkamchinja jamaa yake?”
“Tulimkamata”
“Mkuu”
Martina aliniita, nikamgeukia na kumtazama.
“Hiyo ndio nafasi ya kwenda kumuua K2 kwa maana hapo amechanganyikiwa tayari”
“Hapana musimue sasa hivi”
“Kwa nini?”
“Kama unahitaji kumpata Donald na mke wake, hakikisha kwamba humuui K2, waue kwanza hao wawili kisha huyo ndio atafwatia na kifo chake kitakuwa ni cha taratibu”
Livna alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.
 
“Poa hapa kikubwa ni kupango wa kumuua Donald na watu wake”
“Usijali upo na injini ya kazi hapa, kesho dunia nzima unakwenda kuandika historia ya kugopesha wengi”
Masaa yote yaliyo salia tukayatumia katia kupanga mipango ya kuhakikisha kwamba raisi Donald na Hawa tunawaua huku Livna akiahidi kuongeza wasichana wake wanne ambao anawaamini na wana mfunzo ya hali ya juu anayo amini kwamba ni lazima maraisi hawa wataisoma namba.
 
Hadi kuna pambazuka kila kitu kikawa tayari katika mpango wake, wasichana wa Livna Livba nao  wakawa wamesha fika hapa nyumbani kwa Winy huku wakiwa na mavazi maalumu ambayo wanayatumia walinzi wa Marekani wanao mlinda raisi wao. Nikakabidhiwa suti nyeusi pamoja na jaketi maalumu ya kuzuia risasi ambayo nimeivaa nyuma kwanza kabla ya kuvaa shati langu juu. 
 
Nikavalishwa sura ya bandia ambayo imetengenzwa kwa haraka na mmoja wa wasichana wa Livna mara tuu baada ya kuniona. Sura hii uzuri wake ninaweza kuivaa na si hadi nifanyiwe upasuaji  maalumu(oparesheni).
Kikosi cha watu tisa kikakamilia huku sote tukiwa tumevaa vifaa maalumu vya kuweza kuwasiliana sisi kwa sisi, nikasimama kwenye kioo na kujitazama vizuri, kwa sura niliyo ivaa kusema kweli nimebadilika na si rahisi kabisa kwa mtu kuweza kunitambua. Kitambulisho changu pia kina sura hii, na ukikutana nami ni rahisi sana kuamini kwamba mimi ni mlinzi wa raisi wa Marekanani. Martin, Babyanka na Winy nao wakakabidhiwa vitambulisho vyao kwa ajili ya kwenda kuianza kazi hii.
“Dany ataenda na mimi. Husna utaenda na Winy pamoja na Martin, Babyanka utachukua walio salia”
Livna alipanga majukumu hayo huku tukkiwa tumesimama kwa mfumo wa duara.
 
“Sawa”
“Tukumbuke, mwanachi asife katika hii kazi hapa anaye takiwa ni raisi Donald na mke wake. Tuhakikisheni kwamba tunawaleta eneo hili wakiwa hai na sote tulindane kwenye hii oparesheni”
Livna alizidi kusisitiza huku akitutizama kwenye nyuso zetu.
“Sawa mkuu”
“Jamani nashukuru kwa umoja wenu, hii kazi ni ya kuhatarisha maisha yetu. Na nyote mumefanya kwa ajili ya kunisaidia. Endapo hatuto rudi kwa idadi hii basi ninaimani kwamba tutaonana kwenye dunia nyingine ambayo hakuna mtu aliye wahi kwenda”
Nilizungumza kwa sauti ya upole kwani kusema kweli katika hili swala laiti ningekuwa peke yangu basi siwezi kabisa kufanya hivyo.
 
“Usijali ninaimani sote tutarudi salama, na hakuna hata kati yetu atakaye kufa. Twendeni tukawatandike makalio yao sawa”
Livna alizungumza kwa msitizo ambao unampa hamasa kila mmoja eneo hili.
“Sawa mkuu”
Tukapeana mikono kisha sote tukaaanza kutoka sebleni hapa, kila mmoja akiwa na silaha za kutosha, na kila mtu anajua ni wapi ameingiza silaha hizo. Tukaingia kwenye magari manne yanayo tumiwa na walinzi wa Kimarekani ambayo yamekuja na wasichana wa Livna.
Safari ikaanza taratibu, tulipo fika barabarani gari zikatawanyika na kila gari likapita njia yake ila lengo kubwa ni kufika Kigamboni. Simu ya Livna ikaanza kuita mfukoni mwake, taratibu akaitoa na kuipokea.
 
“Muheshimiwa raisi”
Nikamtazama Livna huku nikiendelea kuendesha gari.
“Ziara imebadilishwa?”
Nikajikuta nikupunguza kasi ya mwendo wa gari.
“Ahaaa inaanzia hapo SPF Tower?”
“Sawa mkuu basi nitaimarisha ulinzi hapo”
Livna akakata simu yake na tukaanza kupeana taarifa watu wote juu ya ziara ya maraisi hawa kubalishwa. Ikatulazimu wote mpango kubadilika haraka inavyo wezekana. Mimi na Livna tukawa wa kwanza kufika katika magorofa haya mawili ambayo ni marefu sana kwenda juu na urefu wake ni sawa na mita 147  kwenda juu.
 
“Sijui wanafika saa ngapi hapa”
Nilizungumza huku nikiendelea kutazama ulinzi ulio imarishwa hapa. Hapakuwa na mtu wa kutukagua kwa maana tunavitambulisho.
“Watafika, siwezi kumpigia K2 simu na kumuuliza inaweza kumpa wasiwasi.”
“K2 alisha wahi kufahamu mahusiano kati yangu mimi na wewe?”
“Hapana hakuwah kufahamu”
“Ahaa sawa sawa”
 
“Tuelekee juu, kwa maana huku ndipo wanapo kagua kagua”
“Wanaanza gorofa gani kwa maana yapo haya mawili hapa?”
“Hili tulilopo ndio wanaanza”
“Babyanka na timu yako hakikisheni munakaa gorofa namba mbili.”
“Sawa”
Baada ya kutoa maelekezo hayo kupitia kinasa sauti maalimu nilicho kivaa, tukaanza kuingia ndani ya hili gorofa ambapo ndio mara yangu ya kwanza kuingia humu ndani. Baada ya lisaa ving’ora vikaanza kusikika, nikasimama kwenye moja ya dirisha na kuchungulia chini nikaanza kuona gari za raisi K2 zikifika katika hili eneo, walinzi wakazidi kuimarisha ulinzi.
“Jaribu kuizuia asira yako utakapo muona K2, tunaye muhiraji leo ni Donald na Hawa sawa Dany”
 
“Nimkuelewa”
Baada ya dakika tano mbeleni gari za raisi wa Marekani nazo zikafika katika eneo hili. Walinzi wote wa Marekani nao wakasogelea gari hili ambalo ni refu, wakamfungulia raisi mlango akashuka huku akipunga mkono. Taratibu nikaona gauni jekundu likianza kutoka ndani ya gari hili, kisha akashuka Hawa huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana usoni mwake, macho yangu nikayashusha hadi tumboni mwake nikaona ujauzito wake ulio nifanya nipatwe na uchungu mwingi sana hadi nikatamani kuanza kufanya mashambulizi nikiwa huku huku juu nilipo.
 
AISIIIII……….U KILL ME 169

“Dany tutafeli, unamuonaje malaya tu huyo na unakuwa na hasira kiasi hichi?”
Livna alizungumza huku akitazama mikono yangu jinsi inavyo tetemeka kwa hasira ambayo kusema kweli haina kipimo.
 
“Nahitaji kuwaua sasa hivi?”
“Piga picha ukiwaua sasa hivi kuna midomo mingapi ya bunduki kwa hawa watu na unahisi mwili wako unaonekana vipi. Utafanywa chujio kwa risasi acha ujinga”
Livna aliendelea kuzungumza kwa msisitizo hukua kinishika mkono wangu wa kulia ambao unazidi kutetemeka kwa hasira kali niliyo nayo.
“Tulia nitakuonyesha hii kazi jinsi inavyo fanywa”
“Sawa”
Tukaanza kutembea tembea kwenye gorofa tuliyopo huku tukiendelea kujifanya ni walinzi wanao imarisha ulinzi ila hatuna chochote katika hili.
 
“Hivi unahisi ni kwa nini niliamua kutembea na wewe?”   
“Sijakuelewa?”
“Yaani unatambua kwa nini nimeamua kuongozana nawe kwenye hii oparesheni hii?”
“Sijajua?”
“Kwa sasabu ninakujua vizuri Dany, unafeli kila misheni kwa ajili ya hasira za hapo kwa hapo, ukimuona adui sijui unakuwaje kuwaje. Na isitoshe humu ndani kuna watu wana ujuzi hadi wakuwasoma watu miguu yao jinsi  inavyo tembea wakikuona tembea yako haieleweki lazima wakudandie, sasa piga picha wakikustukizia na jinsi unavyo tafutwa watakufanya nini”
 
Livna alizungumza kwa sauti ya chini, tukasimama pembeni ya lifti inayo fika katika gorofa hili, wakaanza kutoka walinzi kisha akafwatia K2, alipo muona Livna akamkonyeza kama ishara ya urafiki. K2 na walinzi wake wakelea kwenye moja ya sehemu maalumu iliyo andaliwa humu ndani na hapa ndipo maraisi watakapo kutana ili kuanza kukagua gorofa hili lenye huduma mbalimbali.
Waandishi wa habari nao wakazidi kuwa bize kuhakikisha kwamba wanapata picha nzuri kwa raisi ajaye kupitia lifti hii. Tukiwa hapa gafla umeme ukakatika na giza totoro likatawala humu ndani, kelele zikaanza kutawala huku walinzi wakihakikisha kwamba wanamlinda K2 kwani kukatika kwa umeme hili jambo halikuwepo kwenye ratiba yao.
 
“Show time baby”
Livna alizungumza huku akinishika mkono, tutakasimama kwenye lifti hii na kwa haraka Livna akaanza kuifungua milango hii miwili, ambayo haikumpa tabu sana. Mara kwa mara macho yangu yanatazama sehemua lipo kuwa K2 ila kutokana na giza pamoja na wingi wa watu sikuweza kumuona.
“Tunashuka chini unaone lifti ile kule”
Livna alizungumza kwa nguvu huku akinionyesha lifti  iliyo kwama kwa mwanga wa simu yake nikaweza kuiona na lifti hii ndipo alipo raisi Donald pamoja mke wake pamoja na walinzi.
“Ile ni gorofa namba mbili  inabidi kushuka kwa hii kambi”
“Nimekupata”
Akaanza Livna kushuka kwa kasi na hii kamba ngum ili tengenezwa kwa nyanya ndogo dongo za chuma na zimaesukwa sehemu moja na kuifanya kama hii kuwa nene na ngumu sana.
 
Nikachomoa bastola zangu mbili na kuzifanya kama vishikizo katika kamba hii kwani nikishuka chini kwa kutumia viganja vyangu pekee, nikifika hadi lifi ilipo ni lazima viwe vimechubuka. Nikashuka kwa kasi sana hadi nikafika sehemu ilipo lifti.
Tukaanza kusaidiana na Livna katika kufungua mfuniko ulipo juu  ya lifti. Tulipo hakikisha  kwamba umefunguka Livna akamulika ndani na simu yake.
“Muheshimiwa raisi tupo kwa ajli ya kukutoa hapa salama wewe na mke wako”
Livna alizungumza, nikapata nafasi ya kuchungulia ndani, nikawaona walinzi wa raisi Donald wakiwa wamezielekezea bunduki zao kwa Livna.
 
“Sawa”
Livna akaingia kupitia uwazi huo, na mimi nikaingia pia kupitia katika uwazi huu. Cha kushangaza sijamkuta Hawa ila sikuhitaji kuonyesha tofati yoyote katika hili.
“Hii ni gorofa namba mbili, tusaidiane kufungua huo mlango na tumtoe raisi humu ndani”
Livna akawapa maelekezo vijana wa raisi Donald Bush.
“Sawa madam”
Tukaanza kusaidiana kufungua mlango hadi ukafanikiwa kufunguka, tukakuta lifti hii ipo katika usawa wa gorofa ya pili na ya tatu huku kukiwa na uwazi mdogo wa kupita katika  gorofa namba mbili kwani ndio ilikuwa inapanda kwenda juu.
“Unaweza kupita hapo muheshimiwa?”
 
“Ndio”
Wakaanza kupita walinzi baadhi, nikafwatia na mimi, kisha akafwatia raisi Donald, Livna na walinzi wengie wawili wa mwisho. Sote humu tunategemea mwanaga wa tochi wa simu ya Livna. Tukaanza kukimbia kwa haraka kwenye kordo hii kubwa huku kando kando  kukiwa na maduka makubwa ya simu ambayo sihitaji kuyatilia maanani.
“Mke wangu alielekea bafuni kidogo”
“Usijali muheshimiwa raisi tutampata tu. Yanka umesikia hiyo”
“Ndio”
Tuliisikia sauti ya Babyanka kupitia vinasa sauti ambavyo katika watu tulipo hapa tumevaa mimi na Livna tu na hata hawa walinzi wake wamevaa vinasa sauti vyao wanavyo wasiliana na wa watu wao. Tukaanza kushuka ngazi kuelekea chini huku raisi Donald Bush tukiwa tumemuweka katikati.
 
“Winy gari ziandaliwe kwneye magesho ya chini kabisa”
“Sawa”
“Raisi anaondoka na msafara mwingine?”
Mlinzi  mmoja wa raisi aliuliza huku  tukiendelea kushuka kwneye gorofa hii kwa kasi.
“Ndio, akiondoka na usafiri wake shambulizi lilizo pangwa kufanywa hapa ni lazima atashambuliwa kwenye gari”
“U…ume….sema shambulizi binti?”
Raisi Donald Bush aliuliza huku akihema sana kwani kasi tunayo mpeleka unaweza kuifananisha na wana riadha.
“Ndio muheshimiwa raisi”
“Nani huyo anaye hitaji kufanya shambulizi?”
“Ni Dany muheshimiwa”
 
“DANY…….Mwanaharamu mkubwaa, nitoeni hapa jamani akinikamata ataniua huyu”
“Usijali muheshimiwa upo salama, nitakulinda hadi dakika ya mwisho wa maisha yangu”
“Mke wangu, mke wangu jamani muokoeni”
“Yanka umefanikiwa kumpata mke wa raisi Donald?”
“Ndio tunaeleka naye kwenye maegesho ya magari”
“Muheshimiwa raisi mke wako utamkuta kwenye meegesho ya magari”
“Ila nyinyi ni kina nani, kwa maana mazungumzo yenu munayafanya nyinyi wenyewe?”
Mlinzi mwengine aliuliza 
 
“Sisi ni kikosi maalumu cha dharura alicho kiunda raisi K2”
“Ataunda vipi kikosi maalumu pasipo kushirikisha ofisi yetu?”
“Sisi ndio watu wa pekee tunayo ijua hii nchi, isitoshe muheshimiwa raisi amekuja kipindi ambacho nchi inamtafuta gaidi anaye itwa Dany, ninaimani unamfahamu na kama haumfahamu basi utakuwa umemsikia”
Livna aliendelea kujibu maswali ya hawa walinzi wa karibu wa raisi kiufasaha na laiti kama wangejua Dany mwenyewe nipo karibu yao wala wasinge dhubutu kabisa kunyanyua miguu yao.
“Tunahitaji kudhibitishiwa hilo na muheshimiwa raisi K2”
“Acheni ujinga nyinyi, tupo kwneye hatari nyinyi munataka kudhibitishiwa ili iweje, mule ndani ya lifti si mulikuwa mumechanganyikiwa na mukakosa la kufanya hadi huyu binti  akafika, eheeeeee?”
Raisi Donald Bush  aliuliza kwa kufoka huku akihema sana.
“Ila muheshimiwa raisi ni jukumu letu kukulinda kwa maisha yetu yote”
 
“Mimi ndio raisi wa Mareknani ninaye kupa amri wewe. Msikilizeni huyu binti  anacho kisema kuazia hivi sasa, nina imani kwamba nyote hakuna anye mjua Dany zaidi yagu, na kifupi Dany ni yule aliye isambaratisha kambi ya Al-Shabab, sasa piga picha akikutana na sisi sasa hivi nani atakate pona eheee?”
“Samahani mueshimiwa raisi”
Mlinzi huyu ikambidi kukaa kimya tu kwani ndio hivyo raisi amesha zungumza na ahitaji maoni mengine yoyote kusikia. Tukafika katika mlango wa kutokea nje, wote tukajibanza huku tukitazama nje, nikaona gari mbili tulizo kuja nazo zikiwa kwenye eneo la maegesho.
“Jamani tunatakiwa kuwa makini, hapa ni sehemu ya maegesho hatujui adui yupo wapi, kwa hiyo tunatakiwa kuwa makini sana”
“Sawa”
 
Baada ya Livna kuzungumza hivyo tukaanza kutoka katika eneo hili kuelekea lilipo gari, tukaanza kusikia kishindo cha kwanza cha mmoja wa walinzi wa raisi akianguka chini. Sote tukajibanza kwenye moja ya gari.
“N..nini jamani?”
“Shiiiiii…….”
Livna alimnyamazisha raisi kwani tayari woga umesham mtawala, hata mimi mwenyewe sijui ni kitu gani kinacho endelea. Hatukaa sawa mlinzi mwengine akaanguka chini huku  akitoa ukeleke. Nikataka kushambulia sehemu nilipo muona.
“Dany ni sisi tunakuona tumevaa night vision glass”
Niliisikia sauti ya Winy akizungumza jambo lililo nifanya niwe mpole na kuishusha bastola yangu chini. Kwani huu ni mpango ambao ninaimani Livna ameupanga ili kuwapagawisha raisi Donal Bush. 
“Hei, mumemuona mshambuliaji?”
Mmoja wa walinzi  alizungumza.
 
“Yaa yupo eneo lile”   
Kitendi cha mlinzi hutu kuzungumza hivyo akapigwa risasi ya kichwa na kuangukia miguuni mwa raisi.
“Yesu wangu…….!!”
Raisi Donald alizungumza kwa woga mwingi sana na ubaya wa washambuliaji wa hawa walinzi wamevaa miwani maalumu ambazo zinawafanya waone vizuri kwenye giza totoro. Walinzi walio salia wa raisi Donald wakaanza kuitoa kimaso maso ili kumzuia mshambuliaji. Mimi na Livna tukamshika raisi mikono yake na kuanza kukimbia huku tukiwa tumeinama, kitendo hicho kikawafanya walinzi wa raisi Donald wote kufa kwani tunamfanya Winy kuweza kuwadungua vizuri na bunduki yake haitoi mlio kwani ameifunga kiwambo cha kuzuia risasi hizo. Tukafanikiwa kufika kwenye gari tulilo waambia Winy na timu yake waliandae.
“Tuondoke tuondoke”
Linvna alizungumza na Martin akaliweka sawa gari hili na kuanza kuondoka kwa kasi eneo hili la chini.
 
“Mke wangu jamani?”
“Yupo gari la nyuma muheshimiwa”
Msichana mmoja wa Livna alimujibu raisi Donald aliye ishusha pumzi yake taratibu. Moyoni mwangu nikajikuta nikijawa na furaha kubwa sana ya kushangilia ushindi nilio upata kwa kusaidiwa na hawa wezangu.
“Muheshimiwa ni kitu gani mwilini mwako kinaruhusu satelaiti kukuona”
Livna alizungumza huku akiwa amemtazama raisi.
“Ni…..nina kimoja hapa mkononi”
Raisi Donald alizungumza huku akitetemeka sana. Kwa haraka Livna akaanza kukivua raisi Donald koti lake la suti kisha akakunja mkono wa shati lake hili jeupe.
“Naombeni kisu”
“Unataka kufanyaje!!?”
Raisi Donald alizungumza huku macho yakiwa yamemtoka kwa woga.
 
“Tunahitaji kukitoa hicho kifaa ni lazima Dany na timu yake watakufwata popote uendapo na ukumbuke upo Tanzania na si Marekani na yeye anaijua Tanzania vizuri kuliko unavyo fikiria”
“Sa..a…wa”
Livna akachukau kisu alicho kabidhiwa na mtu wake ambacho kina incha kali sana, pasipo uruma wala wasiwasi akaanza kupasua sehemu raisi Donald aliyo sema. Taratibu akatoa kidude kidogo sana, kilicho akafungua kioo cha gari na kukitupa.
“Una kingine ndani ya mwili wako?”
“Sina labda kiatu cha mguu wa kushoto”
Livna kwa haraa akamvua raisi kiatu hichi cha garama, akakitazama tazama kwa haraka kisha akaanza kuigandua kikanyagio cha soli kwa kutumia kisu hichi, alipo fanikiwa kukifunua, tukaona kifaa kingine kidogo kinacho wawezesha walinzi wa raisi hata wakiwa nchini Marekani kujua kwamba raisi wao yupo eneo gani. Livna akakitupa kifaa hichi na kumrudishia raisi Donald kiatu  chake huku kikiwa hakina kikanyagio cha soli.
“Una kingine?”
“Saa hii”
Raisi Donald akaivua saa yake akamkabidhi raisi.
“Huna kingine?”
“Hapana”
“Mke wako anacho?”
“Ahaa, mkufu alio uvaa”
“Yanka mvueni mke wa raisi mkufu wake na muutupe”
“Poa dakika sifuri”
 
“Ni wa garama sana, dola laki mbili?”
“Una garama kubwa kuliko maisha yako?”
Livna alizungumza kwa msisitizo hukua kimtazama raisi Donald Bush usoni mwake.
“Hapana”
“Acha utupwe na hii saa yako ya garama nayo ninaitupa”
Livna akafungua kioo kidogo na kuvitupa vitu hivi.
“Tunafanya hivi vyote ni kwa ajili yako la sivyo Dany atatuweka kati na akifanikiwa kufanya hivyo, muheshimiwa mziki wake hata mimi ninaujua”
Livn alizidi kuzungumza maneno ya kumtisha raisi Donald Bush juu yangu.
“Tunaelekea wapi?”
“Kwenye nyumba salama kwa muda, na baada ya hapo utaratibu mwengine utafwata”
Uzuri wa gari hizi zina ving’ora vinavyo fanya magari mengine barabarani kupisha njia, jambo linalo warahisishia madereva wetu kuzidi kutoroka. Tukiwa barabarani gafla gari moja jeusi linalo fanana na gari hili likaingia mbele yetu na kuongeza mwendo.
 
“Mkuu ni sisi”
“Sawa”
“Ni kina nani wale?”
“Ni kikosi kinazidi kuimarisha ulinzi”
“Ohooo asante Mungu wangu”
Raisi Donald alizungumza hukua kipiga ishara ya msalaba kwa ajili ya kumshukuru Mungu wake. Gari zote nne zikangia kwenye geti kubwa la jumba la Winy. Tukashuka kwenye magari na kwa haraka raisi Donald Bush na Hawa wakaingizwa ndani ya nyumba hii.
“D”
Livna aliniita baada ya kuniona nimeichoma bastola yangu kwa ajili ya kueekea ndani kuwamaliza maadui zangu. Nikasimama huku nikimtazama usoni mwake, akanisogelea karibu yangu na kunitazama kwa macho makali.
“Akilii, akilii ndio inahitaji usikurupuke, na kama kuwaua utawaua, ila tafuta kitu cha thamani kwao kwanza ndio uwaue”
 
“Sijakuelewa”
“Nenda ndani utaelekewa”
Baada ya Livna kuzungumza maneno hayo, akaondoka na kuanza kuwapa majukumu wasichana wake kuimarisha ulinzi wa hili eneo hili. Nikaanza kutembea kwa haraka huku nikifikiria jambo alilo niambia Livna, nikawakuta raisi Donald Bush na Hawa wakiwa wamekaa sebleni huku Babyanka na Win wakiwa wamewaandalia maji ili kusuuza makoo yao. Raisi Donald taratibu akamsogeza Hawa karibu yake na kumlaza begani mwake.
“Vipi hujapata mstuko wowote tumboni mwako?”
Raisi Donald alizungumza kwa sauti ya upole iliyo jaa mahaba mengi ndani yake.
 
“Hapana mume wangu, ni mstuko tuu, ila nipo sawa”
Nikachukua kiti kimoja na kukiweka mbele ya raisi Donald Bush pamoja na Hawa, taratibu nikaka huku bastoka nikiwa nimeishika vizuri. Nikawatazama kwa dakika kadhaa hadi wao wenyewe wakawa wananishangaa.
“Kijana mbona unatushangaa?”
Raisi Donald Bush alizungumza huku akiupeleka mkono wake wa kulia kwenye tumbo la Hawa na kuanza kulipapasa taratibu taratibu. Nikafungua kifungo cha shati langu, taratibu nikaiinamisha sura yangu chini, nikaanza kuvua sura hii ya bandia hadi ninaimalizia na kuinyanyua sura yangu na kuwatazama raisi Donald na Hawa, wote wakabaki wamenitumbulia macho hata mkao  wa kimahaba walio ukaa ukavurugika kila mtu akakaa jinsi anavyo jua yeye mwenyewe huku mwili wake ukiwa unawatetemeka, kwani yule wanaye muogopa na waliye mkimbia huko walipo toka yupo mbele yao. 
 
ITAENDELEA
“Haya sasa ule msemo wa USIYE MPENDA AMEKUJA, ndio ulio wakuta raisi Donald na Hawa. Dany yupo mbele yao unahisi ni nini kitakacho tokea na kuendelea katika story hii ya kusisimua?. Usikose sehemu inayo fwata ya hadi hii ya kusisimua kutoka kwa muandishi mahiri Eddazaria G.Msulwa”

Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH....Anatoa Pete za Bahati, Anasafisha Nyota, Anazuia Chuma Ulete na Mengine

0
0
Kutana na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam Shariff,  Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili ya Africa Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika
Anatibu kwa Njia ya Simu Ukiwa Nchi Yoyote / Mkoa wowote
 
..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Chief Sultan Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO NDANI YA SAA 12 TU(LIMBWATA). Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine?Una Mpenzi wako ana Pesa na Unataka kumkamata? Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao Endapo utafata Atakacho kuelekeza.
 
Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.
Adam Shariff Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..
 
Anatibu kwa Kutumia Vitabu vya QUR-AN Dawa za Asili za Africa,Dawa za Kiarabu na Majini.Anatafsiri Ndoto. Kushinda BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA,Hutoa PETE ZA BAHATI inayoendana na NYOTA YAKO. Mvuto wa Mwili na BIASHARA, Kinga ya Mwili,ZINDIKO za Nyumba.HUZUIA CHUMA ULETE NA KUKUPA DAWA YA KUONGEZA FAIDA KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA AU KUDHULUMIWA.MIGUU Kufa GANZI.Kufungua KIZAZI kwa wale walio fungwa kwa njia za KISHIRIKINA. 

Anakupa Jini la Mali kwa yule anaehitaji Utajiri BILA MASHARTI.Humaliza Kabisa Tatizo la Nguvu za KIUME na Kurefusha Uume kwa Saizi Unayotaka,HUMALIZA KESI YA AINA YOYOTE NDANI YA SIKU 14. na mengi zaidi

Mawasiliaono: +255715971688  au +255756914036
 
Tiba ni kwa Watu wenye Imani na Dini zote

Waziri Mkuu: Tumeanzisha Benki Ya Kilimo Ili Kutoa Mitaji Kwa Wakulima

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imeanzisha Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania kwa lengo la kuwasaidia wakulima wapate mitaji ili waongeze tija.

Pia amewataka wakuu wa wilaya za Kilosa na Mvomero mkoani Morogoro wahahakikishe wanawahamasisha wananchi katika maeneo yao kuchangamkia fursa ya kilimo cha miwa.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana jioni (Ijumaa, Desemba 7, 2018) alipotembelea shama la miwa Mkulazi na MbIgiri mkoani Morogoro alipokuwa njiani kwenda jijini Dodoma.

Alisema lengo la kuanzishwa shamba la mwa la Mkulazi ni katika jitihada za Serikali za  kuhakikisha mahitaji ya sukari nchini yanafikikia katika kiwango kinachohitajika.

Waziri Mkuu alisema Serikali imepanga kuzalisha sukari itakayotosheleza mahitaji na njia pekee  ni kuboresha kilimo cha miwa, kujenga viwanda vitakavyozalisha sukari ya kutosha.

Alisema shamba hilo linaendeshwa kwa ubia kati ya NSSF na Jeshi la Magereza, hivyo, aliiagiza Menejimenti mpya ya Mkulazi kuhakikisha shamba hilo linasimamiwa kikamilifu.

Waziri Mkuu pia, alimuagiza Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike apeleke wataalamu wengi wa kilimo katika shamba hilo ili wasaidie kusimamia kitaalamu.

“Nataka shamba hili lisimamiwe kitaalamu, uzalishaji uwe wa kitaalamu na liwe mfano na mashamba mengine, tusishindwe na watu binafsi,” alisema.

Kuhusu suala la maji hususan kipindi cha mvua ambayo huaribu shamba, Waziri Mkuu aliwataka watafute namna nzuri ya kuyahifadhi ili wayatumie kipindi cha kiangazi.

Kadhalika, Waziri Mkuu aliwataka watafute mashine nyingine zitakazotosha kumwagilia shamba hilo wakati wa kiangazi ili miwa isiharibike na iendelee kuwa ya kijani wakati wote.

Nae, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenistar Mhagama, alisema shamba la Mkulazi II ni miongoni mwa mashamba mawili yanayomiilikiwa na wabia wawili yaani NSSF na Jeshi la Magereza.

Alisema walikubaliana wao na Magereza wafanye kazi kwa kuongozwa na uzalendo, maadili ya utendaji wa kazi, uaminifu ili mwisho wa siku mradi huo uwe na tija na uweze kuwafikisha katika malengo yaliyokusudiwa.

Alisema wanaamini fedha zilizowekezwa kwenye mradi huo ambazo ni za wanachama zinatakiwa zirudishe faida kwa wanachama wenyewe na kujenga uchumi wa Taifa.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Kilimo, Omari Mgumba, alimshukuru Rais Dkt. John Magufuli kwa dhamira yake ya dhati ya kuhakikisha tatizo la upatikanaji wa sukari nchini linakuwa historia.

Alisema mbali ya shamba hilo la Mkulazi II pia kuna lingine la Mkulazi I ambalo ni kubwa zaidi, hivyo alishauri liendelezwe ili limalize tatizo la sukari nchini. Waziri Mkuu alimtaka ashughulikie shamba hilo kwa kuwa lipo Wizara ya Kilimo.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Mwanamke Apambana Na Jambazi Mwenye Silaha Akimuokoa Mumewe, Amuangusha Chini Amnyang’anya Silah... Waziri Lugola Amtembelea

0
0
Na Felix Mwagara, (MOHA) MARA.
Mkazi wa Kijiji cha Mahyolo, Kata ya Nyamihyolo, Wilayani Bunda, Mkoa wa Mara, Busimba Malegesi amemuokoa mumewe asiuawe na jambazi mwenye silaha ambaye alivamia katika nyumba yao na kuanza kumshambulia mwanaume huyo kwa kumkatakata mapanga mwili mzima.

Busimba alimrukia jambazi huyo kiunoni na kumuangusha chini na kufanikiwa kumnyang’anya panga pamoja na tochi ambazo alikua nayo wakati anamshambulia mumewe aitwaye Samson Malegesi (62).

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea saa 7:30 usiku wa kuamkia Ijumaa wakati familia hiyo ikiwa imelala ndipo jambazi huyo alivunja mlango na kuingia moja kwa moja chumbani kwa wanandoa hao na kuwasha tochi kumsaka Malegesi na baada ya kufanikiwa kumuona alianza kumshambulia kwa kumpiga mapanga kichwani, mikononi, kwenye mbavu na kusababisha damu nyingi kumwagika.

Wakati jambazi hilo akiendelea kumshambulia Malegesi, mkewe alikua naye anapambana kwa kumzuia asimshambulie mumewe, lakini jambazi hilo lilizidiwa baada ya mwanamke huyo kupata nguvu zaidi na kufanikiwa kumuangusha chini na kuhakikisha silaha aliyoishika mkononi akinyang’anywa kwa urahisi kutokana na kubanwa kwa juu na mwanamke huyo.

Mwanamke huyo wakati akipambana na jambazi huyo alikua akipiga kelele lakini sauti yake haikuweza kuwafikia majirani ili waweze kumpa msaada, hata hivyo jambazi huyo baada ya kuona anakosa nguvu baada ya kukandamizwa chini, akafanikiwa kupata upenyo ndipo akakimbia kutoka katika nyumba hiyo.

Hata hivyo, baada ya jambazi huyo kukimbia, mwanamke huyo alitoka nje kuomba msaada zaidi kwa majirani na walifanikiwa kufika na walimpeleka Hospitali ya Misheni ya Kibara Wilayani humo ambapo alifikishwa akiwa hajitambui na kuanza kupewa matibabu ya haraka ili kuokoa maisha yake.

Muuguzi wa Hospitali hiyo, Godliver Josephat alisema amempokea mgonjwa huyo akiwa na waaguzi wenzake, saa 9:00 usiku akiwa hajitambui na ndipo wakashirikiana na madaktari wakamuwekea dawa ya kuzindua uhai wa mgonjwa huyo na kufanikiwa kuzinduka na wakaendelea na tiba zingine ikiwemo kuzuia kutoka damu pamoja na kushonwa sehemu alizokatwa mapanga.

“Tumempokea mgonjwa huyo saa tisa usiku akiwa ana hali mbaya sana, jitihada zetu zilifanikiwa kumpa huduma ya kwanza kwa kumuwekea dawa ya kuzindua uhai wake na baadaye tukaendelea kumpa huduma zingine ikiwemo kuanza kumshona kwasababu alikatwa panga la kichwa, mikono yake yote miwili ilijeruhiwa, mbavu zake upande wa mgongoni alichimbwa kwa kukatwa na panga, hivyo hali yake ilikua tete, hata hivyo tumefanikiwa kumuhudumia kwa umakini mkubwa na sasa mnamuona anaweza kuzungumza,” alisema Godliver.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ambaye alikua katika ziara ndani ya jimbo lake ambapo tukio hilo limetokea, mara baada ya kupata taarifa ya tukio hilo alfajiri ya jana, alifika hospitalini hapo na kuelekea chumba cha upasuaji akakuta madaktari wakiendelea kumshona sehemu mbalimbali za mwili wake zilizojeruhiwa.

Lugola ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo hilo la Mwibara, aliwasili Hospitali hapo akiwa na Mkuu wa Kituo cha Polisi Kibara (OCS), Mkaguzi Boniface Mwalupale pamoja na madiwani na viongozi wa Halimashauri wa Wilaya ya Bunda ambao uambatana nao wakati akiwa katika ziara zake jimboni mwake.

“OCS hakikisheni hamlali mpaka mnalipata jambazi hili kwa kutumia njia zote za kiintelejinsia mulizosomea ili muweze kumsaka na kumtia mbaroni haraka iwezekanavyo, huu ni unyama na lazima akamatwe, mtafuteni usiku na mchana, msikae ofisini kunywa chai, hakikisheni huyu mtuhumiwa anakamatwa.” Alisema Lugola.

Lugola baada ya kutoa maelekezo hayo saa mbili asubuhi, alitoka hospitali hapo na kuendelea na mikutano ya hadhara jimboni humo na akasisitiza kuwa majambazi wasiibipu serikali kwa kuwa bado ipo macho kuhakikisha wananchi wake wapo salama, kutokana na tukio hilo Polisi watafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha mtuhumiwa anakamatwa.

“Nampongeza sana mwanamke aliyepambana na jambazi ili amuokoe mumewe, hakika kama sio ushujaa wa mwanamke huyo tungempoteza mumewe kwasababu jambazi huyo alidhamiria kumuua kwa kumkata mapanga zile sehemu ambazo ni hatari zaidi kwa uhai wa ubinadamu,” alisema Lugola alipokua anazungumza na wananchi wa Kijiji cha Busagara, Kata ya Chitengule, jimboni humo jana jioni.  

Kwa upande wa Mkuu wa Kituo cha Polisi Kibara, Mwalupale alisema baada ya kupata taarifa ya tukio hilo, tayari askari wapo katika msako mkali wa kumsaka jambazi huyo na wamemhakikishia Waziri Lugola pamoja na wananchi kuwa watamkamata mtuhumiwa huyo.

“Jambazi huyo alifanya uvamizi huo lakini hakuiba chochote ndani ya nyumba hiyo, inaonyesha kuwa, lengo la jambazi hilo alitaka kumvamia mtuhumiwa pekee. Ila tunaendelea kufanya uchunguzi kujua lengo la mtuhumiwa huyo kufanya tukio hilo la kinyama, na tutahakikisha tunamkamata na kumfikisha mahakamani,” alisema Mwalupale.

Hata hivyo, Waziri Lugola baada ya kumaliza mikutano yake jioni alirudi tena hospitalini hapo na kumkuta mgonjwa huyo ametoka chumba cha upasuaji na amepelekwa wodini kwa ajili ya kuendelea na matibabu.

Lugola alitoa pole kwa ndugu na wananchi waliokuwepo hospitalini hapo kutokana na unyama aliofanyiwa mwananchi huyo na kuhahidi Serikali ipo pamoja nao na watahakikishia jambazi hilo pamoja na wengine watakamatwa.

Dkt. Reginald Mengi amuandikia ujumbe mzito mke wake

0
0
Wiki hii ni siku ya kuzaliwa ya mke wa bilionea Dkt. Mengi, Jacqueline Mengi ambapo ndugu jamaa na marafiki wameitumia kumtakia mrembo huyo  maisha marefu yenye mafanikio katika maisha yake.

Mama watoto huyo wa Mengi ambaye alikuwa Miss Tanzania mwaka 2000, alipokea ujumbe mzito wa mahaba kutoka kwa mume wake huyo ambaye ni bilionea wa Afrika.

 “My love, my darling wife, my best friend, the holder of the key to my life, it is always “ better late than never” Happy Birthday my Baby. Thank you for giving me reason to live. I love you crazy @JNtuyabaliwe,” alitweet Mengi.

Naye Jacqueline Mengi aliamua kujibu ujumbe hao kwa kutweet

“This is so sweet hubby ❤️❤️❤️❤️I love you so much @regmengi I couldn’t have asked for a better man to be my everything.,”

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images