Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Ofa! Sale! Tumeshusha tena bei za Viwanja: Bunju na Mapinga Dar

$
0
0
Ofa! Sale! Tumeshusha tena bei za Viwanja: Bunju na Mapinga

Tumeamua kufunga mradi wetu wa viwanja vilivyopimwa; Mapinga na Bunju kwa kushusha bei maradufu ili kumfanya Mtanzania mwenye uhitaji wa Ardhi (Kiwanja) apate kulipia haraka na kumilikishwa kiwanja chake. Ofa hii inaanza leo mpaka tarehe 30 dec

Kwa Mapinga vipo viwanja vifuatavyo:
sqm 400 kwa bei ya tsh 4,000,000/=
sqm 450 kwa bei ya tsh 4,500,000/=
sqm 800 kwa bei ya tsh 8,000,000/=
sqm 1,120 kwa bei ya tsh 11,200,000/=
sqm 1,364 kwa bei ya tsh 13, 640,000/=
sqm 1,600 kwa bei ya tsh 16,000,000/=
sqm 1,900 kwa bei ya tsh 19,000,000/=
sqm 2,400 kwa bei ya tsh 28,000,000/=
sqm 3,000 kwa bei ya tsh 34,000,000/=
Viwanja hivi viko umbali wa km 3 tu kutoka main raod (Bagamoyo Road)

Kwa Bunju vipo viwanja 2 tu kama ifuatavyo:
sqm 600 kwa bei ya tsh 18,000,000/=
sqm 1700 kwa bei ya tsh 51,000,000/=
Viwanja hivi viko umbali wa km 1 tu kutoka main raod (Bagamoyo Road)

Biashara hii haina dalali, mpigie mhusika: 0758603077, whatsap 0757489709

Serikali Yaiagiza Bodi Ya Wataalam Wa Ununuzi Na Ugavi Kudhibiti Maadili Ya Wataalam Wa Ununuzi Na Ugavi

$
0
0
Na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Susana Mkapa, ameiagiza Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi nchini (PSPTB), kuhakikisha kuwa inadhibiti maadili ya wafanyakazi wa sekta ya ununuzi na ugavi ili fedha za serikali zinazotumika kwenye ununuzi ziwe na tija kwa wananchi.

Bi. Mkapa ametoa maagizo hayo Jijini Dodoma, katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Kaimu Naibu Katibu Mkuu ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mipango wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Richard Mkumbo, wakati akifunga kongamano la tisa la wataalam wa ununuzi na ugavi kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara.

Bw. Mkumbo amebainisha kuwa licha ya vitengo vya matumizi mabaya ya fedha za umma kupitia sekta ya ununuzi na ugavi, ikiwemo rushwa kuendelea kupungua, Bodi inatakiwa kuhakikisha kuwa vitendo vya rushwa vinadhibitiwa ipasavyo.

Amesema asilimia 75 ya fedha za umma zinatumika kupitia mchakato wa manunuzi ambao taarifa ya mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali (CAG) na Mamlaka ya Ununuzi nchini PPRA, umebaini kuwepo kwa viashiria vya rushwa katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya wananchi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi, Sister Dkt. Hellen Bandiho, amesema kuwa Bodi yake itahakikisha inasimamia kikamilifu maadili ya watumishi wa sekta ya ununuzi ili iweze kushiriki katika kukuza uchumi wa viwanda.

Kongamano hilo limewashirikisha wataalam wa ununuzi na ugavi wapatao 650 kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara

Mwisho

Video Mpya: Nay Wa Mitego – Michano

$
0
0
Msanii wa Bongo Fleva, Nay wa Mitego anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Michano. Itazame hapa.

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

$
0
0

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara, Msanii wa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo Dawa na PETE za Bahati zenye uwezo mkubwa wa kuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.

Kutana na Sheikh Jumaa Bilal. Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki. 

Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. Sheikh Jumaa Bilal ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA-  Sheikh Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na Nje ya nchi.

Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nayasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.

Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudishaa alipote, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMBA, GARI..), Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali na UTAJIRI bila masharti na mengine mengi ya Siri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET)

*{لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّهُ بِاللَّغْوِ فِي أيْمَانِكُمْ وَلَٰكِنْ يُؤَاخِذُكُمْ بِمَا عَقَّدْتُمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِمَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ }* ﴿٨٩﴾

✨Wabillahhi Tawfiq Asallam  Alaikum

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa
nambari ya simu

+255 688 745 790
+255 672 861 042
Whatsapp :  0762 252 102

Agizo La Waziri Lugola Kwa Wananchi Ambao Hawajapata Kitambulisho Cha Taifa Nchini

$
0
0
Na Felix Mwagara, (MOHA), MARA.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewataka Watanzania ambao hawajajiandikisha waende kujiandikisha ili waweze kupata kitambulisho cha taifa kwakuwa sio jambo la hiari bali ni lazima kwa kila Tanzania aliyeko ndani ya mipaka ya nchi kutambuliwa.

Akizungumza na wananchi wa Kata ya Nansimo, Mwibara, Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara, Lugola amesema katika Mkoa na mikoa mingineyo zoezi la kujiandikisha lilishakamilika ila wale ambao hawakuandikishwa kipindi kile ambacho Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wanaandikisha wananchi mitaani, wanapaswa kwenda katika ofisi Wilaya za Mamlaka hiyo ili waweze kujiandikisha.

“Wapo ambao kipindi kile NIDA wanaandikisha wananchi mitaani hawakuwepo hilo nalijua, na pia kuna wale ambao kipindi kile zoezi la kuandikishwa linafanyika walikua hawajafikisha miaka 18, hao wote ambao hawajaandikishwa wanapaswa sasa kwenda kujiandikisha haraka iwezekanavyo katika ofisi za NIDA katika Wilaya zao,” alisema Lugola.

Lugola ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara aliongeza kuwa, zoezi la vitambulisho vya utaifa ni lalazima kwa kila mtanzania aliye hapa nchini, ni kosa bwa kama wewe ni raia akaamua kukaidi ikiwa Rais Dk John Magufuli ameamua kutoa vitambulisho hivyo bure bila malipo yoyote nchini.

“Ndugu wananchi wa Mwibara na kote nchini, kupata kitambulisho ni jambo kubwa la nchi hivyo tusililinganishe na jambo lingine lolote na tusilichukulie kirahisirahisi tu, na ninawaambia baada ya mchakato huu kuisha tukamkuta mtu hana kitambulisho maelezo yake yatakuwa ni magumu kueleweka kama kweli yeye ni mtanzania halali,” alisema Lugola.

Lugola alisema kwa Mkoa wa Mara tayari zoezi lilikamilika na kinachofanyika sasa ni Kuhakiki, kuyafanyia kazi mapingamizi pamoja na Uchakataji, likikamilika zoezi hilo kwa wale waliojiandikisha na ambao wana sifa watapewa vitambulisho vyao.

“Hakuna Mtanzania mwenye sifa atakayekosa kitambulisho cha taifa, lakini lazima muwe na subira wakati zoezi la utambuzi wa watu gani wanaweza kupata vitambulisho hivi, na pia katika utambuzi tunapaswa kuwa makini sana kwasababu tusije tukapenyeza wasio raia wasiostahili na wao wakaweza kupata vitambulisho na baadaye tukaja kupata shida,” alisema Lugola.

Aidha, Waziri Lugola aliwataka wananchi wa jimbo lake waanze maandalizi ya kilimo cha mazao ya chakula na biashara ili kuepuka janga la njaa lisije liwakumba endapo hawata lima. Hata hivyo, kijiji hicho alichokitembelea, kwa mujibu wa taarifa ya mipango yao ya kilimo walisema kuwa wana upungufu mkubwa wa mbegu za mazao mbalimbali hasa zao la pamba.

Lugola anaendelea na ziara yake kwa kutembelea vijiji vyote jimboni kwake Mwibara akisikiliza kero za wananchi pamoja na kuhamasisha kilimo cha mazao ya pamba, mahindi, mpunga, viazi na mengineyo ambayo wakazi wa jimbo lake wanalima mazao hayo kwa wingi.

Filamu ya mwisho kucheza Marehemu Masogange kutoka December 15, 2018

$
0
0
Msanii wa Filamu Bongo, Rammy Galis anatarajia kuzindua filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la Hukumu.

Katika filamu hiyo Rammy Galis amecheza na aliyekuwa Girlfriend wake Marehemu Agnes Gerald maarufu kama Masogange.

Sio Masogange pekee yake bali waigizaji wengine wakubwa na wakali wameshiriki kwenye filamu hiyo itakayozinduliwa kwa mara ya kwanza December 15, 2018 City Mall, Dar es Salaam.

Agness alipata umaarufu mkubwa pindi alipotokea katika video ya msanii Belle 9 ambayo ilikwenda kwa jina la Masongange ndipo na yeye kuanza kutumia jina hilo. Masogange alifariki April 20, 2018 katika hospitali ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge, Dar es Salaam.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

Masha amiliki asilimia 68 ya hisa kampuni ya Fastjet

$
0
0
Waziri  wa zamani wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha, amenunua asilimia 64 ya hisa za kampuni ya ndege ya Fastjet Tanzania, hivyo kuongeza hisa zake kufikia asilimia 68 kutoka asilimia nne aliyokuwa akimiliki awali.
 
Ofisa Uhusiano na Masoko wa Fastjet, Lucy Mbogoro, jana alisema Masha alinunua hisa hizo ikiwa ni sehemu ya mpango wa kuimarisha na kuboresha kampuni hiyo, kuelekea katika mikakati mipya ya kuboresha huduma inayotarajiwa kuanza mwakani.

Alisema Masha ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti Mtendaji wa Fastjet amenunua hisa hizo ambazo ni asilimia 17 zilizokuwa zikimilikiwa na Kampuni mama ya Fastjet PLC ya Afrika Kusini na asilimia 47 ya hisa zilizokuwa zikimilikiwa na wazawa, ikiwa ni hatua ya kuifanya kampuni hiyo imilikiwe moja kwa moja na Watanzania.

“Kwa sasa ieleweke kwamba asilimia 68 ya hisa zote za Fastjet nchini inamilikiwa na Lawrence Masha na thamani halisi ya hisa hizo itatajwa baadaye, baada ya kuweka mambo yote sawa. Ila hii ni sehemu ya kuifanya kampuni hii imilikwe na Watanzania,” alisema.

Alisema ukitoa asilimia 68 ambazo sasa zinamilikiwa na Masha, ikiwa ni kiasi kikubwa kinachotoa nafasi ya umiliki wa kampuni hiyo, asilimia 32 zilizobaki bado zinamilikiwa na Haine Kaizer ambaye ni raia wa Afrika Kusini.

Mbogoro alisema pamoja na kununuliwa kwa hisa hizo, kampuni hiyo yenye ndege mbili kwa sasa ikiwa na safari mbili kila siku kati ya Dar es Salaam, Mwanza na Kilimanjaro pia safari moja kila siku kati ya Dar es Salaam na Mbeya iko katika mikakati ya kupanua huduma zake kwa kuongeza idadi ya ndege na safari hizo.

Alisema kampuni hiyo ambayo kwa sasa inamiliki asilimia 42 ya soko (kwa mujibu wa ripoti ya robo ya kwanza ya mwaka inayoishia Aprili) pia inatarajia kuongeza safari zake kati ya Dar es Salaam na Harare (Zimbabwe) na Dar es Salaam na Lusaka (Zimbabwe) ambazo zinafanyika mara tatu kwa wiki, pia kuongeza maeneo ya safari za ndani.

Kwa mujibu wa ripoti za umiliki wa soko, kufikia Aprili mwkaa huu Fastjet ilikuwa ikiongoza kwa asilimia 42 ikifuatiwa na Precision Air iliyokuwa ikimiliki wastani wa asilimia 35 ya soko na Air Tanzania ambayo iliongeza wigo wake kutoka asilimia 2.5 mwkaa 2016 hadi asilimia 20 mwanzoni mwa mwaka huu.

Fastjet Tanzania imekuwa kwenye mpango wa kununua hisa zote na kuifanya kuwa kampuni ya Kitanzania baada kampuni ya Fastjet PLC kutangaza kusitisha kutoa fedha kwa kampuni ya Fastjet Tanzania.

Fastjet PLC ni kampuni ya ndege ya kimataifa ikiwa na makao yake Afrika Kusini na Uingereza,i inayofanya pia usafirishaji Afrika kwa kujikita katika utoaji wa huduma kwa gharama ndogo.

Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) Yaitaka Belarus Imkamate Rais wa Sudan, Omar al-Bashir atakapotembelea taifa hilo

$
0
0
Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) imeaindikia Belarus na kuitaka kumkamata Rais wa Sudan, Omar al-Bashir atakayetembelea taifa hilo karibuni. 

Rais huyo aliyeko madarakani kwa miaka 29, anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu wa kivita, uhalifu dhidi ya binadamu na mauaji. 

Wauguzi Wanaovunja Maadili Ya Kazi Kukiona Chamoto

$
0
0
Na WAMJW - Nanyumbu, Mtwara
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe.Ummy Mwalimu ametoa onyo Kali kwa Wauguzi wote kwenye vituo vya  kutolea huduma za afya nchini wanaovunja maadili na miiko ya kazi za uuguzi ikiwemo matumizi ya lugha chafu kwa wagonjwa na wan&aowapiga akina mama wajawazito wakati wakijifungua.

Ameyasema hayo  wakati alipotembelea Hospitali ya Wilaya Nanyumbu, akiwa katika ziara yake Mkoani Mtwara ya kukagua hali ya utoaji huduma za Afya na uhamasishaji kwa wananchi juu ya umuhimu wa kujiunga na Bima ya Afya hasa katika msimu huu wa Biashara ya Korosho.

Waziri Ummy alisema kuwa Serikali kupitia Baraza la Uuguzi litawafutia usajili Muuguzi yeyote atakayegundulika ametenda kosa la kumpiga mama mjamzito au kumtolea lugha chafu wakati wa kujifungua.

"Tunataka kumjua huyo, ambae ni hodari sana wakupiga wanawake wajawazito, makofi wakati wakujifungua, kwa kweli huyo ni wa kumfukuza kazi, Mimi mkiniletea namfutia Leseni yake kabisa, hafanyi kazi Serikalini, hafanyi kazi Sekta Binafsi" alisema Waziri Ummy.

Pia, Waziri Ummy alitoa Maagizo kwa Mganga Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Wilaya ya Nanyumbu Mhe.Hamis Dambaya kuhakikisha  Wauguzi na Watumishi wote wanavaa vitambulisho vya kazi wakati wote wakiwa eneo la kazi ili wananchi wanaokwenda kupata huduma za Afya waweze kuwatambua majina yao.

"Tumewaambia wavae vitambulisho, ili mtusaidie kutaja jina la Wauguzi wanaovunja maadili ya kazi zao, hapa naomba nisiwahukumu wote, Mganga Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi mpo hapa, nikirudi tena nisisikie kuna Muuguzi anapiga makofi wajawazito wanaokuja kujifungua" alisema Waziri Ummy.

Kwa upande mwingine Waziri Ummy amesema kuwa Serikali kupitia Wizara ya Afya italeta mashine mpya ya kisasa ya digitali ya X-Ray ndani ya miezi mitatu itayosaidia wananchi wa Nanyumbu hasa kutokana na Wilaya hiyo kuwa katika Bara bara kuu ya kutoka Masasi hadi Songea.

Aidha, Waziri Ummy ametoa Rai kwa wananchi wa Nanyumbu kuhakikisha kabla ya kufika Disemba 31 mwaka huu, kaya zote katika eneo hilo lazima liwe limejenga na kutumia choo bora ili kupunguza magonjwa ya Bakteria yanayoigharimu Serikali pesa nyingi katika matibabu na Dawa.

"Ndugu zangu nendeni pale Hospitali, katika kila Wagonjwa 100, Wagonjwa 60 wana magonjwa ya kuhara,magonjwa ya tumbo, magonjwa yanayohusiana na kiwango duni cha usafi, nimekuwa nikiimba wimbo huu tangu nikiwa Waziri wa Afya, na hapa tulipofikia ni agizo la Waziri Mkuu pindi alipokutana na maafisa Afya wa Halmashauri na Mkoa jijini Dodoma" alisema Waziri Ummy

Waziri Ummy aliendelea kusema kuwa akiwa kama Waziri wa Afya kazi kubwa aliyonayo ni kuhakikisha anawakinga watu wasiumwe na pale wanapoumwa waweze kupata Huduma Bora za Afya, lazima niwe mkali kwenye kinga, mimi ni Waziri wa Afya sio Waziri wa Wagonjwa" alisema Waziri Ummy.

Huna Sababu Ya Kuaibika tena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0620510598  / 0743543944

Tovuti za Ngono Zafungwa Rasmi

$
0
0
Serikali chini Uganda kupitia Tume yake ya mawasiliano (UCC) imefungia mitandao inayoonyesha picha za ngono kwenye simu nchini humo.

Takriban tovuti 25 zinazoonyesha video hizo haziwezi kufunguka kwa sasa nchini humo kutokana na zuio hilo.

Mamlaka hizo zilifikia uamuzi wa kuzifungia baada ya kugundua kuwa tovuti hizo ni miongoni mwa tovuti 100 zinazotazamwa sana Afrika Mashariki.

Mwenyekiti wa Kamati ya kupambana na video za ngono nchini humo, Dr Annette Kezaabu amesema zuio hilo la tovuti kubwa za video za ngono limesaidia kushusha idadi ya watu wanaotazama kwa kipindi kifupi tangu lilipotangazwa.

"Mpaka sasa tunaendelea na mchakato wa kupitia majina mengine ya tovuti ambazo tutazifungia kutokana na video hizo. Tunafahamu kwamba watu watafungua tovuti zingine lakini huu ni mpango endelevu," amesema Dr Annette.

Zuio hilo nchini Uganda limekuja siku chache baada ya Mwenyekiti wa Baraza la Mitihani nchini Kenya kuiomba serikali ya nchi hiyo kufungia tovuti za video za ngono kwa lengo la kupunguza ongezeko la mimba za utotoni.

Lowassa ajibu madai ya kupongezwa na Kusifiwa mara Kwa Mara na CCM

$
0
0
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa amejibu madai ya kuonekana kiongozi pekee wa upinzani ambaye amekuwa akisifiwa mara kwa mara na viongozi wa Chama cha Mapinduzi CCM na serikali hali ambayo imeonekana kuzua sintofahamu kwa wadau wa siasa nchini.
 

Akijibu madai hayo Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa amesema “kuhusu madai ya mimi kusifiwa na viongozi wa serikali na CCM, naacha wananchi wahukumu na mimi naamini nina nia njema na nia njema itaendelea kuwepo, anayetaka kufikiria hivyo ni hiyari yake, huwezi kumnyima binadamu kufikiria, ila ninachosema mimi sina mpango wa kuondoka CHADEMA.”

Lowassa ambaye alishawahi kuwa mgombea Urais kwenye Uchaguzi Mkuu 2015, amekuwa ni kiongozi wa upinzani pekee ambaye amekuwa akionekana kwenye baadhi ya mikutano ya serikali ambayo Rais Magufuli amekuwa akishiriki, na mara kwa mara Rais amekuwa akiompongeza kiongozi huyo ambaye alikuwa mpinzani wake kwenye kinyang'anyiro cha urais.

"Maendeleo hayana chama, ndiyo maana Mzee Lowassa yupo hapa, nikushukuru kwa utulivu wako nilipokutupa chini baada ya uchaguzi ulikaa kimya, maana tuligombea mimi na wewe lakini wengine wanapiga kelele tu, kwakweli nikupongeze kwa uzalendo," alisema Rais Magufuli kwenye uzinduzi wa maktaba (UDSM) novemba 27, 2018.

Mbali na Rais Magufuli Lowassa pia alishawahi kupongezwa na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt Bashiru Ally akimtaka Mbunge wa zamani wa Mtama Bernard Membe kuiga mfano wa kiongozi huyo.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kwenye uzinduzi wa Maktaba alishawahi kunukuliwa kumsifia kiongozi huyo kuwa ni mtu ambaye anashiriki shughuli za maendeleo za serikali bila kujali itikadi za vyama husika.

Waziri Mkuu Awatoa Hofu Wakulima wa Korosho

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewatoa hofu wananchi hususan wakulima wa korosho nchini baada ya kuwahakikishia kuwa korosho zao zote zitanunuliwa.

Amesema Serikali kupitia Bodi ya Mazo Mchanganyiko itanunua korosho zote na hakuna korosho za wakulima nchini ambazo zitabaki bila ya kununuliwa.

Ameyasema hayo leo (Ijumaa, Desemba 7, 2018) alipozungumza na wafanyakazi wa kiwanda cha korosho cha Terra akiwa njiani kwenda Dodoma.

Waziri Mkuu amesema bodi hiyo inaendelea kufanya thamini na kujiridhisha kama kweli korosho hizo zimezalishwa nchini na kuangalia viwango vya ubora.

Amesema baada ya kujiridhisha kuhusu viwango vya ubora na mkulima aliyepeleka ndiye mwenyewe ndipo taratibu za malipo hufanyika.

Waziri Mkuu amesema Serikali iliamua kununua korosho baada ya wafanyabiashara kutaka kuzinunua kwa bei ya chini ambayo haikuwa na tija.

“Lengo la Serikali ni kuhakikisha mkulima ananufaika na ndipo Rais Dkt. John Magufuli alisitisha ununuzi baada ya kuona wakulima wanataka kudhulumiwa.”

Waziri Mkuu amesema kuwa hadi sasa tayari tani 181,000 zimeshakusanywa, hivyo amewataka wakulima wa zao hilo nchini waendelee kuiamini Serikali yao.

Kadhalika, Waziri Mkuu ameupongeza uongozi wa kiwanda hicho kwa kuunga mkono jitihada za Serikali kukuza uchumi kwa kupitia sekta viwanda.

Awali, Meneja Utawala wa kiwanda cha Terra, Peter Ngwale alisema uwezo wao ni kubangua tani 6,000 kwa mwaka, ambapo tayari wamebangua tano 3,000.

Pia aliiomba Serikali iwasaidie katika suala la ubora wa korosho kwa kuwa kiwango cha ubora kinachoandikwa kinakuwa tofauti na uhalisia wa korosho  yenyewe.

 (mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Polisi Kuanza Upya Zoezi la Uhakiki wa Silaha

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoani Mbeya, limetakiwa kufanya ukaguzi na uhakiki wa vibali kwa wamiliki wa silaha ili kudhibiti vitendo vya uhalifu, vinavyotokana na matumizi mabaya ya silaha hizo.

Agizo hilo limetolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila, wakati akizungumza na maofisa na askari polisi kwenye ukumbi wa mikutano wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU), muda mfupi baada ya kukabidhi msaada binafsi wa magari mawili yenye thamani zaidi ya milioni 20 alioutoa kwa jeshi hilo.

Alisema wapo watu wakiwemo wafanyabiashara wakubwa wanamiliki silaha kinyume cha taratibu na inawezekana matumizi yake yakawa mabaya pia, hivyo hiyo ikawa ni moja ya sababu inayochangia kuwa na ongezeko kubwa la vitendo vya uhalifu.

“RPC inakupasa kutangaza upya zoezi la uhakiki wa silaha, anzia Chunya ambako kuna machimbo ya madini, kila mwenye silaha aeleze anaimiliki kwa ajili ya shughuli gani na tuone kama vibali vyake ni halali maana wakati mwingine watu wanajisahau sana,” alisema Chalamila.

Agizo la pili, alilitaka Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na halmashauri kuhakikisha gari ndogo za kukodisha aina ya tax zinasajiliwa na kuwa na anwani ili kuondoa tax bubu kwenye maeneo yote ya mkoa huo.

Alisema agizo la tatu ni jeshi hilo kuweka mkakati wa muda mfupi wa kuruhusu magari makubwa ya mizigo na ya abiria yapite kwa awamu katika maeneo ya milima na miteremko mikali ili kupunguza ajali za barabarani ambazo ziliuandama mkoa huo siku za karibuni.

Pia aliliagiza jeshi hilo kwa kushirikiana na taasisi nyingine, kukomesha vitendo vya ukatili dhidi ya watoto ikiwemo ubakaji na ulawiti hasa katika Wilaya ya Chunya ambayo alidai vitendo hivyo vimekithiri.

Katika agizo lake la tano, Mkuu huyo wa mkoa aliwataka askari wa kikosi cha usalama barabarani kuwashughulikia madereva wanaokiuka sheria za usalama ikiwemo kujaza abiria kupita kiasi na kuendesha magari kwa mwendokasi bila kuchukua tahadhari.

Alisema vitendo hivyo vimeshamiri zaidi katika barabara kuu ya Mbeya – Malawi kupitia Kasumulu ambako alidai madereva wanahatarisha maisha yao na ya abiria.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei, alimshukuru Chalamila kwa msaada huo na kuahidi kuyatumia magari hayo kwa ajili ya kazi za doria na kukabidhiwa kwa  wakuu wa polisi wa Wilaya ya Mbeya Mjini na Wilaya ya Kipolisi ya Mbalizi.

Habari Njema Kwa Wenye Matatizo Ya Nguvu za Kiume, vitambi, nyama uzembe

$
0
0
HABARI NJEMA KWA MLIOATHIRIKA NA MAGONJWA YA MWILI NA AKILI.
Sasa dokta MBALU ana uwezo mkubwa wa kutibu magonjwa yaliyoshindikana,Kama umehangaika kwa muda mrefu bila mafanikio DK.MBALU Ni kiboko kabisaa.

TIBA ATOAZO NI:- (a)Vidonga vya tumbo,kilungulia,Tumbo kujaa gesi.
 (b)Kifua kikuu(TB),Pumu(ATHMA) na Rovu
(c)Miguu kuwaka moto,nyama za magoti kuuma,kiuno na mgongo.
(d)Uzazi na chango.
 (e)Nguvu za kiume,kurefusha na kunenepesha uume,busha,mshipa wa ngiri na tezi dume.
(f)Elimu mwanafunzi kuwa na uwezo mkubwa darasani na kufanya vizuri katika mitihani yake, kupandishwa cheo kazini, kulipwa madeni au mafao yako.
(g) kutoa ushauri nasaha kwa wenye matatizo ya kisaikolojia.

      AINA ZA DAWA.
NINJIWE:-,Hutibu vidonda vya tumbo,tumbo kujaa gesi,na kilungulia,vidonge 16 kwa muda wa siku nne na ya unga.
MPALAMA:-,Hutibu Kifua kikuu (TB), Pumu (ATHMA),na wenye tatizo la uvimbe katika koromeo yaani (ROVU),Huisha na kutorudi Tena.,dozi siku 6.

NKOLA:-,Hutibu miguu kuwaka moto,nyama za goti kuuma,kiuno na mgongo dozi siku 10.
MWATYA:-,Hutibu Uzazi au chango,dozi siku 30,na tatizo kupona kabisa.

LYONGO POWER:-,Hii ni dawa ya heshima kwa akina baba yenye uwezo wa kurefusha na kunenepesha uume kwa wale wenye maumbile madogo yaani (KIBAMIA).

NENGONENGO(4)POWER:-,Hutibu Nguvu za kiume na kuleta hamu ya tendo hivyo kuchelewa kufika kileleni na kuweza kurudia tendo zaidi ya mara (4),ina Nguvu mno Kama Ni muhanga wa tatizo hili   tumia NENGONENGO (4)POWER Ipo aina ya vidonge na unga dozi Ni siku 5 unapona kabisaa wahi Sasa.

NTUNDWA:-,Hutibu busha,mshipa wa ngiri na tezi dume,Busha dozi Ni siku (30),bila kufanyiwa operation,Mshipa wa ngiri dozi siku (4) na tezi dume dozi siku (10).

GWATA:-,kuuwa kesi na shauri kupangiwa tarehe za karibu zaidi na baadae kesi kufutiliwa mbali kabisaa.
NUGWANO:-, Humfanya mtu kuheshimika na kupandishwa cheo kazini pia kulipwa madeni au mafao kwa wakati muafaka.

NKOMA:-, Hurudisha mke,mme,hawara, mchumba ndani ya siku mbili atatimiza mahitaji yote hata Kama yupo mbali na kumfunga asiwe na mtu mwingine..

  Huduma zinatolewa ndani ya masaa 12,Saa moja asubuhi Hadi kumi na mbili jioni,DAR ES SALAAM NA KAHAMA wa mikoani unapata huduma kwa njia ya kusafirisha..na huduma yetu inakufikia ukiwa ofisini au nyumbani kwako..,CONTACTS 0767,  171  ,773
0716, 608  ,959


 OUR SERVICES ARE EASY.

BREAKING: Rais Magufuli Atangaza Msamaha Kwa Wafungwa 4,477

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu, Dkt. John Magufuli ametoa salamu za Kumbukumbu ya Miaka 57 ya Uhuru wa Tanzania Bara, leo Ijumaa, Desemba 7, 2018 Ikulu jijini Dar es Salaam.

Akituma salam hizo, Rais Magufuli kwa mujibu wa Ibara ya 45 Ibara ndogo ya 1 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ametangaza msamaha kwa wafungwa 4,477 waliyokuwa wamefungwa / kuhukumiwa kwenye magereza mbalimbali nchini ambapo  kati yao 1,176 wataachiwa Desemba 9, 2018 katika Sikukuu ya Uhuru.

“Wafungwa 1,076 watatoka siku ya Maadhimisho ya Uhuru yani December 9, 2018, msamaha huu utawahusu Wafungwa Wagonjwa, Wazee kuanzia miaka sabini na zaidi, Wafungwa wakike walioingia Gerezani wakiwa Wajawazito”

“Nimeamua Wafungwa waliotumikia robo ya adhabu zao wapunguziwe robo ya adhabu zao baada ya punguzo la kawaida la theluthi moja” -Rais Magufuli

“Msamaha hautawahusu Wafungwa wanaotumikia baadhi ya adhabu zikiwemo Kunyongwa, Kifungo cha maisha, biashara ya Dawa za kulevya, biashara za Binadamu, kukutwa na viungo vya Binadamu, Walionajisi, Waliowapa mimba Wanafunzi” -Rais Magufuli

Waziri Mkuu Amuaguza Mkurugenzi Mkuu wa EPZA Afuatilie KIbali WIzara ya Ardhi

$
0
0
*Ni cha ujenzi wa kiwanda cha nyuzi Chalinze
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Mkurugenzi Mkuu wa EPZA, George Simbakalia afuatilie Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuhusu kibali cha ujenzi wa kiwanda cha nyuzi kinachotakiwa kujengwa Chalinze.

Ametoa agizo baada ya Mkuu wa mkoa Pwani, Mhandisi Evarest Ndikilo kumuleza kuwa kuna muwekezaji wa kiwanda cha kutengeneza nyuzi cha H and J cha Chalinze ambacho ujenzi wake umekwama kutokana na mwekezaji kutopewa kibali cha ardhi.

Waziri Mkuu ametoa agzo hilo leo (Ijumaa, Desemba 7, 2018) alipozungumza na wafanyakazi wa kiwanda cha Keda kinachotengeneza marumaru aina ya Twyford kilichopo Chalinze mkoani Pwani akiwa njiani kwenda jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amesema ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kuwaunga mkono wawekezaji na kuwafanya wawekeze bila ya urasimu, hivyo amemuagiza kiongozi huyo wa EPZA kuhakikisha kibali kinapatikana.

“Nakuagiza Mkurugenzi ufuatilie kibali hicho na nikifika Dodoma nipate majibu. Hatuwezi kuchelewesha uwekezaji nchini kwa ajili ya urasimu, kila mtendaji ahakikishe anatekeleza majukumu yake ipasavyo.”

Akizungumzia kuhusu uwekezaji katika sekta ya viwanda kikiwemo na kiwanda cha Twyford, Waziri Mkuu amesema uwekezaji huo unafaida kubwa kwani licha ya mapato ya Taifa kuongezeka kupitia kodi pia wananchi wananufaika kwa kupata ajira

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema faida nyingine itokanayo na ujenzi wa viwanda ni pamoja na kutatua changamoto ya masoko ya mazao iliyokuwa ikiwakabili wakulima kwa muda mrefu, hivyo Serikali itaendelea kuhamasisha wawekezaji wengi zaidi.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu ametembelea mradi wa kiwanda cha matunda cha Sayona kilichopo katika kijiji cha Mboga, Chalinze mkoani Pwani na kusema kuwa uwekezaji huo unatija kwa kuwa wakulima wamepata eneo la kuuzia matunda yao.

Waziri Mkuu amesema kwa muda mrefu wakulima wa matunda mbalimbali kama mananasi, maembe katika mkoa wa Pwani na maeneo ya jirani walikuwa hawana soko la uhakika kwa ajili ya kuuzia matunda yao na kusababisha mengi kuharibika.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amewataka wananchi waliopata kazi katika viwanda mbalimbali wawe mabalozi wazuri kwa Taifa na wafanye kazi kwa bidii na uadilifu ili kuviwezesha viwanda hivyo viendelee na uzalishaji na wengine wapate ajira.

Kwa upande wake,Msaidizi wa Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Motisun Group, Aboubakary Mlawa amesema kiwanda cha matunda cha Sayona kimeajiri watumishi 470 kwa sasa huku matarajio ikiwa ni kuajiri watumishi 800.

Amesema licha ya ajira hizo pia mradi huo unawanufaisha wakulima zaidi ya 30,000 kutoka wilayani Bagamoyo kilipo kiwanda pamoja na maeneo mengine yanayolima matunda nchini kwani huuza matunda yao kiwandani hapo.

Akizungumzia kuhusu ujenzi wa mradi huo, Mlawa amesema umegharimu dola za Marekani milioni 55.5, pia kampuni ilitumia sh. milioni 500 kwa ajili ya uwekaji wa umeme mkubwa, uingizaji wa maji pamoja na ujenzi wa barabara kiwandani hapo.

Amesema kiwanda kina uwezo wa kusindika tani 18 za matunda kwa saa kwa line mbili ambazo tayari zimefungwa ila mpango wao ni kuongeza line zingine mbili ambazo zitakuwa na uwezo wa kusindika tani 48 kwa saa, hivyo kiwanda kuweza kusindika tani 66 kwa saa.

(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

NEC yatangaza uchaguzi Jimbo la Temeke na Kata 46 Tanzania Bara

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi  (NEC) imetangaza kufanyika kwa uchaguzi mdogo katika Jimbo la Temeke, Mkoani Dar es Salaam na kwenye Kata 46 za Tanzania Bara.

Akitangaza kufanyika kwa uchaguzi huo Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji (Rufaa), Semistocles Kaijage amesema kuwa uchaguzi huo utafanyika Januari 19 mwaka 2019 na fomu za uteuzi wa wagombea zitatolewa kuanzia tarehe 14 hadi tarehe 20 Desemba 2018.

“Uteuzi wa Wagombea utafanyika tarehe 20 Desemba, mwaka huu. Kampeni za Uchaguzi zitafanyika kati ya tarehe 21 Desemba, hadi tarehe 18 Januari, mwaka 2019 na siku ya uchaguzi itakuwa ni tarehe 19 Januari mwaka 2019,” amesema Jaji Kaijage.

Jaji Kaijage amebainisha kuwa Tume imetangaza uwepo wa nafasi wazi ya Ubunge kwenye Jimbo la Temeke baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Job Ndugai juu ya uwepo wa nafasi wazi ya Ubunge katika jimbo hilo.

Amesema kuwa Tume ilipokea barua kutoka kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye kwa kuzingatia kifungu cha 37(3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, aliitarifu Tume uwepo wa nafasi wazi ya Mbunge wa Jimbo la Temeke katika Halmashauri ya Wilaya ya Temeke Mkoani Dar es Salaam kufuatia Kujiuzulu uanachama wa Chama Wananchi CUF kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Maulid Said Abdllha Mtolea.

Kwa upande wa nafasi wazi za Udiwani Jaji Kaijage  amesema kuwa Tume ilipokea taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali ya Mtaa akiitaarifu  Tume juu ya uwepo wa nafasi wazi za Udiwani katika Kata 46.

“Tume imepokea Taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaaa mbaye kwa kutumia mamlaka aliyopewa chini ya Kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292, aliitarifu Tume uwepo wa nafasi wazi za Madiwani katika Kata 46 za Tanzania Bara,” amesisitiza Jaji Kaijage.

Ametoa wito kwa vyama vya siasa na wadau wote wa uchaguzi kuzingatia Sheria, Kanuni, Maadili ya Uchaguzi, Taratibu, Miongozo na maelekezo yote yatakayotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakati wa kipindi cha Uchaguzi mdogo.

Jaji Kaijage amefafanua kuwa kuwa uchaguzi huo mdogo utafanyika ndani ya Halmashauri 28 zilizopo kwenye Mikoa 14 ya Tanzania Bara.

Halamashauri na Kata zitakazokuwa na Uchaguzi ni pamoja na Ngorongoro (Sale,Misigyo,Malambo, Orgosorok na Olorien/Magaiduru), Arusha(Kimnyak), Kilwa (Kiranje ranje, Kikole, Pande Mikoana), Liwale (Kata Kichonda na Mlembwe), Babati(Dareda na Magara, Kiteto(Makame), Simanjiro(Loiborsiret, Ruvu Remit, Naberera), Kwimba(Walla), Sengerema(Nyampulukano), Ulanga(Msogezi), Mvomero(Mtibwa, Tchenzema, Mangae), Kilosa(Magomeni), Temeke(Keko), Kinondoni(Magomeni).

Halmashauri nyingine ni pamoja na Kasulu (kata ya Kitanga), Kasulu Mji( Kata za Kigondo na Msambara), Buhigwe(Mnyegera), Bukoba(Buhendagabo, Nyakato, Kikomelo), Misenyi(Kanyigo), Ngara(Nyamiaga), Mbinga(Utiri), Songea(Mpitimbi), Mbozi(Ilolo, Hasanga, Ihanda), Tandahimba(Nahyanga, Namikupa), Dodoma(Dodoma Makulu), Serengeti(Geitasamo), Bariadi(Nkundwabiye) na Bariadi Mji(Nyangokolwa).

Lugola Ambana Afisa Elimu Kwa Kukataa Kuandikisha Wanafunzi Darasa La Kwanza Mpaka Wazazi Wao Walipe Michango Wanayodaiwa

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia), akimsalimia Mkazi wa Kijiji cha Namalebe, Kata ya Chitengule, Jimbo la Mwibara, wilayani Bunda, Kaswanila Molore kabla ya kuanza mkutano wa hadhara na Wananchi wa Kijiji hicho. Akizingumza na wananchi wa Kata hiyo, Lugola amepiga marufuku wanafunzi wanaoanza darasa la kwanza kutokuandikishwa mpaka wazazi wao walipe michango wanaodaiwa katika shule mbalimbali jimboni humo. Na Mpiga Picha Wetu

………………………………………………………………………….

Na Mwandishi Wetu, MARA.

 WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amepiga marufuku wanafunzi wanaoanza darasa la kwanza kutokuandikishwa mpaka wazazi wao walipe michango wanaodaiwa katika shule mbalimbali jimboni kwake Mwibara, Wilayani Bunda, Mkoa wa Mara.

Lugola ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Mwibara, amemtaka Afisa Elimu wa Kata ya Chitengule, Jimboni humo, Thadeo Lukinisha kuruhusu shule za msingi zilizopo katika Kata yake kuandikisha wanafunzi hao bila kikwazo chochote kwakuwa elimu ya shule ya msingi ni bure nchi nzima.

Akizungumza na mamia ya wananchi wa Kijiji cha Nakatuba katika Kata hiyo, Lugola alipiga marufuku utaratibu huo ambao amesema hauna msingi wowote kwasababu unawaonea watoto ambao hawana kosa lolote hata kama kuna madeni ambayo wazazi wa wanafunzi hao wanadaiwa kutokana na watoto wao wanaoendelea na masomo katika shule zilizopo jimboni humo.

“Huu utaratibu sio sawa, haukubaliki, kipindi hiki wanafunzi wanaandikishwa kuanza darasa la kwanza waandikishwe bila kikwazo chochote ili waweze kupata elimu yao kama inavyostahili, michango yenu haihusiani na wanafunzi kuanza shule,” alisema Lugola.

Hata hivyo, Afisa Elimu huyo tukio hilo lipo lakini walifanya hivyo kutokana na baadhi ya wazazi kutolipa kiasi cha shilingi mia nne ambayo inachangwa kwa ajili ya kila mwanafunzi anachangia kwa ajili ya kumlipa mpishi pamoja na mafuta ambayo fedha hiyo inalipwa kwa mwaka.

Lugola alipata taarifa hiyo ya wazazi kukataliwa kuandikishwa watoto wao kuanza darasa la kwanza, baada ya mzazi mmoja kuulalamikia utaratibu huo na kuwafanya wazazi kutokuanidisha watoto hao kutokana na kudaiwa michango hiyo.

“Sitaki kusikia hili, Afisa Elimu huu sio utaratibu sahihi, lazima watoto waandikishwe kuanza masomo, na niwataka wazazi wote wahakikishe watoto wao wanaandikishwa haraka iwezekanavyo,” alisema Lugola huku akishangiliwa na wananchi waliohudhuria mkutano huo.

Kwa upande wake Afisa Elimu huyo baada ya kauli ya Waziri Lugola aliwaelekeza walimu wa shule zilizopo katika Kata hiyo waweze kaundikisha watoto wao bila kikwazo chochote.

“Napenda kutangaza kuwa, kuanza sasa wanafunzi waandikishwe bila kikwazo chochote katika shule ya Nakatuba na zinginezo ndani ya Kata hii ya Chitengule,” alisema Lukinisha.

Shule zilizopo katika Kata hiyo wanapewa chakula cha msaada na Shirika lisilokua la Serikali la PCI ambapo wazazi uchangia fedha kidogo ya mafuta na ya mlinzi hivyo uliwekwa utaratibu wa kila mwanfunzi katika shule hizo wachange shilingi 400 ili ziweze kuchangia huduma hizo.

Lugola anaendelea na ziara yake kwa kutembelea vijiji vyote jimboni kwake Mwibara akisikiliza kero za wananchi pamoja na kuhamasisha kilimo cha mazao ya pamba, mahindi, mpunga, viazi na mengineyo ambayo wakazi wa jimbo lake wanalima mazao hayo kwa wingi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images