Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 164 na 165 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA       
“Kwa nini umefunga kifaa hicho?”
“Niliamua tu kufunga kwa usalama wangu binafsi”
Waziri mkuu na Martin wakaingia ndani ya gari hili aina ya Toyota TX. Taratibu geti likafunguka nikaanza kutoa gari hili taratibu. Kabla hata sijakunja kona ya kuingia barabarani gari zipatazao nne kutoka katika kitengo cha NSS, nikaziona zikija kwa kasi jambo lililo nifanya nianze kufikiria kwa haraka ni kitu gani ninaweza kukifanya ili kuhakikisha kwamba ninawakimbia askari hawa wa kikosi cha NSS, mabao tayari wamesha gundua kwamba mkuu wao pamoja na waziri mkuu wapo mikononi mwangu jambo ambalo nina imani wanaamini kwamba ni hatari kwao.

ENDELEA   
“Wewe twende”   
Babyanka alizungumza huku naye akitazama gari hizi zinavyo kuja kwa kasi katika eneo hili, kwa taratibu nikaanza kuingia barabarani gari hizi nazo zikakatiza katika njia ambayo tumetokea, njia inayo elekea nyumbani kwa Babyanka.
 
“Mzee ni wapi tunapo elekea?”   
“Elekea hii njia ya Bagamoyo tukifika mbele huko nitakuambia ni wapi pa kuelekea”
Nikaanza kuongeza mwendo kasi wa hili gari huku nikikimbizana na muda ambao tupo nao kwani tayari hali ya hatari imesha tangazwa kwenye vyombo vya usalama na ninatambua ni lazima hadi  kuna pambazuka ni lazima kutakuwa na vizuizi vingi barabarani.
“Hembu simu yangu”
Babyanka alizungumza kwa haraka nikatoa simu yake mfukoni na kumkabidhi.
 
“Unataka kufanya nini?”   
“Nahitaji kufunga kila kitu wasinione kwenye satelaiti”
“Sawa”
Babyanka akaanza kuminya minya kioo cha simu yake, mimi kazi yangu ni kuhakikisha kwamba ninafika Bagamoyo mapema sana.
“Hawawezi kutufwatilia”
“Umezima?”
“Hapana nimeonyesha muelekeo tofauti na ninapo kwenda”
“Kivipi yaani?”
“Kwa sasa wanaona tunaelekea Mbagala”
“Haiwezi kulete hatari wakastukia?”
“Hapana hakuna mwenye ujuzi  huo ofisi nzima”
“Sawa”
 
Hadi inatimu saa kumi na mbili alfajiri tayari tukawa tumefanikiwa kufika mji Bagamoyo. Waziri mkuu akaanza kunielekeza kuelekea kuelekea katika shamba lake. Japo barabara sio nzuri ila gari hili kidogo linaweza kuhimili mashimo mashimo yaliyopo barabani.
“Kunja sasa kulia nenda moja kwa moja kwenye huo msitu”
“Sawa mzee”
Kusema kweli hii sehemu tunayo elekea kweli ni porini na wala sidhani kama kuna mtu yoyote ambaye anaweza kutupata kirahisi kwani kuna pori kubwa lililo jaa misitu  mingi sana.
 
“Waziri mkuu hivi huku kweli kuna dalili ya watu kiishi?”
Babyanka alimuliza waziri mkuu huku akigeuka na kumtazama siti ya nyuma.
“Wee acha huku nimepapata siku nyingi sana, hata kabla ya kuwa waziri mkuu”
“Mmmmm kazi kweli kweli yaani na hivi ninavyo jisikia ninajihisi kunyong’onyea kabisa”
“Tumebakisha kama kilomita moja hivi?”
“Mmmmmm, kilomota moja!!?”
Martin naye aliuliza kwa kushangaa, kwani hata mimi mwenyewe dereva ninahisi mikono yangu kuniuma.
“Ndio tuvumilie tu kidogo tutafika”
“Huku pia ni Tanzania?”
“Ndio ni Tanzania”
“Mmmmmm kweli Tanzania ni kubwa”
“Yaa”
 
“Ila Martin hata Nigeria ni kubwa”
“Sio kubwa snaa kama Tanzania mkuu”
Mazungumzo ya hapa na pale ndani ya gari, tukajikuta hata mawazo ya uchovu wa hii safari ya kipotea na watu wakazidi kuzoeana sana hususani kwa Martin. Hadi inatimu saa mbili na nusu asubuhi tukafanikiwa kufika eneo la shamba kubwa la huyu mzee, ambapo tumekuta nyumba moja ndogo iliyo tengenezwa kuta zake kwa mbao.
“Karibuni jamani”
Waziri mkuu alizungumza huku tukishuka kwenye gari. Taratibu nikaanza kujinyoosha viungo vyangu vya mwili.
“Karibuni ndani”
Waziri mkuu  alizungumza huku akianza kutangulia mbele, Babayanka akaanza kumfwata kwa nyuma.
“Mkuuu”
“Ndio”
 
“Hivi una waaamini sana hawa watu?”
“Asilimia kumi, vipi wewe?”
“Mini hata moja siwaamini, kwa maana sijajua ni kwa nini wamemaua kukubali kuungana nawe kirahisi hivi?”
“Ninawafahamu na wananifahamu, ila kwa watu ambao walipanga kuniangamiza sio rahisi kuwaamini”
“Jamani karibuni”
Waziri mkuu alizungumza kwa sauti ya juu huku akiwa amesimama nje ya mlango wa kijumba chake hichi. Tukaanza kutembea kuelekea walipo huku bunduki zetu tukiwa tumezishika vizuri sana.
Waziri mkuu akafungua mlango na taratibu tukaingia ndani, japo kuna giza kiasi ila mwanga unapita katika sehemu ndogo zenye uwezo.
“Itabidi tushuke huku chini”
Waziri mkuu alizungumza huku akiwasha iliyo tufanya tuweze kuona vizuri eneo hili la ndani mwa hii nyumba. Nyumba hii haina chumba chochote zaidi ya seble yenye viti viwili pamoja meza moja tu. Waziri mkuu akasogeza meza pembeni, Martin akamsaidia kusogeza viti hivyo viwili, akafunua kapeti zito, tukaona malango wa kuingilia chini, waziri mkuu akaufungua mlango huu na tukaonga ngazi zinzo elekea chini.
“Huku ndipo ilipo nyumba yangu”
Waziri mkuu alizungumza huku akianza kushuka chini, nasi tukaanza kumfwata kwa nyuma, akawasha taa iliyo tufanya tuweze kuona eneo zuri lililo pambwa kwa vitu vingi vya thamani.
 
“Kwa nini uliamua kujenga chini ya ardhi?”
Martina alimuuliza waziri mkuu huku akitazama eneo hili la hii seble.
“Nilipenda sana staili ya majengo haya niliipata nchini Ujerumani”
“Sasa walio jenga hivi ni kina nani?”
“Nilichukua mafundi kutoka nchini Ujerumani na wao ndio walio ifanya hii kazi iliwachukua miezi zaidi ya kumi na sita”
“Duuu”
Waziri mkuu akawasha tv kubwa iliyopo hapa sebleni.
“Hapa huduma zote za ndani zipo”
Taratibu Babyanka akakaa kwneye moja sofa huku akiwa ameshika tumbo lake. Nikamsogelea na kuchuchumaa mbele yake.
“Unajisikiaje”
“Tumbo langu kwa hapa linauma kidogo”
Babyanka alinionyesha sehemu ya chini ya kitovu chake.
“Pole. Mzee kuna dawa za kutuliza maumivu?”
“Ndio zipo?”
 
“Ninaomba umpatie Babyanka”
Waziri mkuu akaingia kwenye moja ya chumba na kutuacha hapa sebleni.
“Raisi Donald Bush anakuja saa ngapi Tanzania?”
“Leo saa moja moja hivi atakuwa amesha tua uwanja wa ndege”
“Tunatakiwa kumuangusha leo”
“Kivipi Dany?”
“Tunatakiwa kumuua raisi Donald, mke wake pamoja na K2?”
“Dany umechanganyikiwa, hivi unajua ni ulinzi wa wana usalama wangapi ambao wnaamlinda raisi Donald?”
“Hilo kwangu sio dili, ninacho kihitaji mimi ni kuhakikisha kwamba ninawaua”
“Hivi vitu Dany usichukulie hasira utafeli na wewe peke yako huwezi kukamilisha hilo unalo lihitaji kulikamilisha”
Babyanka alizungumza kwa msisitizo, waziri mkuu akatoka huku akiwa ameshika kisanduku chenye rangi nyeupe huku kikiwa na msalaba mwekundu.
 
“Unasikia maumivu sehemu gani?”
Waziri mkuu alimuuliza Babyanka ambaye akamuonyesha sehemu anayo hisi maumivu. Waziri mkuu akafungua kisanduku hichi na kuto sindano pamoja na kichupa kidogo cha dawa.
“Hii dawa itatuliza maumivu kwa kipindi fulani”
“Kwa muda gani?
“Masaa ishirini na nne hadi sabini na mbili”
“Sawa nichome tu”
“Mkuu”
martin alinita, nikamtazama kwa ishara ya kidole akanionyesha Tv na sote tukajikuta tukiitazama. Tukaona picha zangu na Martin zikitangazwa kwamba sisi ni magaidi tuliopo nchini Tanzania na atakaye fanikisha kukamatwa kwetu basi atazawadiwa dola milio moja sawa na bilioni mbili za Kitanzania. Sote tukakaa kimya huku tukiendelea kumtazama mtangazaji wa tangazo hili.
“Inabidi kumtoa madarakani kinguvu K2 amefanya mengi maovu”
 
Waziri mkuu alizungumza kwa msisitizo jambo lililo nifanya nimtazame kwa macho ya mshangao.
“Umetambua uovu wa raisi wako leo?”
“Kwa mfanyakazi wa kawaida kama mimi unahisi ni rahisi kuweza kufahamu kwamba bosi wangu yeye ndio gaidi?”
“Mimi ninafahamu”
Babyanka alizungumza huku akinyanyuka kwenye sofa alilo kalia.
“Una muda gani tangu ufahamu kwamba K2 ni gaidi?”
“Kabla hata hajawa raisi, mimi na Dany ndio watu wa pekee tuliye gundua uovu wake hadi akamuua raisi aliye pita ambaye ni kaka yake hii yote ni kwa uroho wa madaraka”
“Sawa ni kwa nini ukuzungumza kabla hajachukua hii nchi?”
“Unahisi maisha anayo ishi Dany kwa mimi mtoto wa kike ngingeweza kuishi.?”
 
Babyanka alizungumza huku machozi yakimlenga lenga. Waziri mkuu alibaki mdomo wazi lile alilo tamani kulizungumza alijikuta akishindwa kabisa kulizungumza.
“Nilikiongoza hichi kikosi cha NSS kwa amri kutoka kwa K2, na jana usiku kama ingekuwa ni kumkamata Dany ningeweza kumkamata kwa maana nilikuwa ni mtu wa kwanza kumuona tangu wakiwa kwenye fukwe za bahari ila kutokana mulikuwa mupo wawili nilihitaji akamatwe mwenzako ili wewe nije kukutana nawe”
 
“Kwa nini uliamua kunishambulia?”
“Kwa sababu ya waziri mkuu, sikuhitaji afahamu kujua kwangu kitu chochote kuhusiana na wewe”
Mimi na Martin tukatazama kwani maneno ya Babyanka kidogo yanaendana na ukweli ila sina imani naye kwa asilimia zote.
“Tuachane na melezo mengi. Tunahitaji kumuua K2”
“Kwa leo itakuwa ngumu”
“Kwa nini?”
“Walinzi wake wanao mlinda si NSS”
“Ni nani?”
“Kikosi chake cha wasichana wauaji, hao leo ndio wanamlinda”
Babyanka alizungumza huku akinikazia macho usoni mwangu. Wasichana hao ninawafahamu vizuri kwani Livna ndio kiongozi msaidizi.
 
“Kikosi cha wasichana?”
Waziri mkuu aliuliza kwa mshangao huku akimtazama Babyanka.
“Ndio, na kikoasi hichi kiongozi wao anaitwa Livna Livba”
“Nina mjua”
Nilizungumza huku nikimtazama Babyanka
“Yupoje huyo msichana?”
Waziri mkuu aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu
“Chotara fulani hivi”
“Hemb ngoja”
Waziri mkuu akakimbilia ndani kwake kisha akarudi na laptop yake mkononi, akaifungua, akaiwasha na baada ya muda akaanza kuminya minya batani za laptop hiyo kisha taratibu akatugeuzia.
 
“Msichana huyu?”
Waziri mkuu alizungumza huku akituonyesha picha ya Livna. Taratibu Martin akaanza kutembea huku akisogelea laptop ya waziri mkuu, taratibu akachuchumaa na kuitazama vizuri picha ya Livna.
“Martin vipi?”
“Ninamfahamu huyu  msichana”
“Unamfahamu vipi?”
Martin akanigeukia na kunitazama kwa macho ya yaliyo jaa wasiwasi mwingi hata swali langu ambalo nimemuuliza anashindwa kulijibu jambo lililo nifanya nijiulize maswali mengi juu ya hili.
“Martin mbona kimya?”
“Huyu msichana ni mke wangu wa ndoa”
Nikabaki nikimshangaa Martin kwani kwa kipindi chote ambacho nimeweza kumfahamu hajawahi kunieleza kwamba alisha wahi kuoa msichana yoyote isitoshe huyo msichana wake nillisha wahi kuwa na mahusiano naye ya kimapenzi miaka kadhaa nyuma.
 
AISIIIII……….U KILL ME 165

“Mke wako wa ndoa!!?”   
Nilimuuliza Martin huku nikimshangaa usoni mwake.
“Ndio nimemuoa miaka miwili iliyo pita, ila tulikuja kutengena”
“Kutengena kwa sababu gani?”
“Aligundua kwamba nipo katika kikosi cha Boko Haramu”
“Yeye alikuwa anafanya kazi gani?”
“Yeye alikuwa ni mwana chuo cha ualimu pale Lagos”
“Basi sio mwanachuo ni gaidi, tena gaidi kukushinda hata wewe, na ili tumpate K2 ni lazima kumpata Livna la sivyo hatutafanikiwa”
 
Nilizungumza huku  nikikaa kwenye moja ya sofa.
“Mimi ninajua jinsi ya kumpata”
Martin alizungumza huku akinitazama.
“Tutampataje?”
“Kama yupo Dar es Salaam ni lazima turudi Dar es Salaam”
“Dar ulinzi ni mkali kijana na kitendo cha kurudi ni lazima mutakamatwa na watanzania jinsi walivyo na njaa unahisi hiyo dola milioni moja watashindwa kutoboa siri pale watakapo waona?”
“Nitaenda nao, nitaweza kuwakinga pale nitakapo kutana na vizuizi”
 
“Kitambulisho chako unacho?”
“Ndio ninancho”
“Kama unacho unaweza kwenda nao”
“Wewe utakaa hapa?”
“Ndio sihitaji kurudi Dar es Salaam kwa sasa, nahitaji kupanga mipango ya kumpindua K2”
“Mipango hiyo utaipanga wewe mwenyewe?”
“Hapana ninategemea msaada wenu pia nitawawezesha huko muendapo kukutana na watu ambao  wanaweza kuwasaidia”
“Kwa mimi sihitaji mtu wa kutusaidia”
Nilizungumza huku nikimtazama waziri mkuu usoni mwake.
“Kwa nini?”
“Simuamini mtu hata wewe sikuamini mzee wangu, hii oparesheni nitaiendsha mimi na kijana wangu.”
Maneno yangu yakamFanya waziri mkuu kukaa kimya.
“Tutaondoka saa ngapi hapa mkuu”
Martin aliniuliza.
“Saa kumi na mbili jioni tutaianza safari kama kuna chakula mzee tunahitaji kuandaa”
“Njoo huku”
Waziri mkuu alizungumza huku akisimama, taratibu tukaingia kwenye moja ya chumba.
“Hapa ndio jikoni huwa marehemu mke wangu alikuwa anapenda sana kupatumia kupika pika vyakula vyake tukija mapumzikoni huku”
“Ninaweza kukuamini?”
“Unasema?”
“Mzee ninaweza kukuamini kama mwanao alivyo jitunza katika kuilinda bikra yake?”
Waziri mkuu  alinitazama usoni mwangu huku akinitumbulia macho.
 
“Ina maana umemtoa mwanangu usichana wake?”
“Ila ulisha wahi kuniambia hicho kitu “
“Kwamba?”
“Mwanao bado ni bikra, nihakikishe ninaitoa au umesahau”
“Wewe mwana haramu unadhani mwanangu anaweze kuishi na mwanaume kama wewe unaye tafutwa kila kona?”
“Analitambu hilo na nilimtahadharisha ila alikubaliana nami”
Waziri mkuu akatoa mchele kwenye moja ya droo ya kabati kubwa lililopo humu ndani.
“Hiyo si pete ya ndoa?”
“Ndio”
“Umeoa?”
“Ndio maana nimeivaa”
“Hakikisha mwanangu unamtoa mikononi mwa K2, na baada ya hapo ninakuomba uachane naye kabisa, sinto hitaji umuumize moyo kwa mambo ya kihuni huni sawa”
Waziri mkuu alizungumza kwa msisitizo huku  akiwanikazia macho.
“Mzee acha hasira mambo mengine hayahitaji hasira”
“Hapa ninazungumzia kuhusiana na mwanangu, kwenye hilo swala ni lazima niwe na hasira”
 
“Haya nimekuelewa mkuu”
Tukasaidia na waziri mkuu hadi tukamaliza kupika wali  maharage. Tukaandaa chakula hichi na kurudi nacho sebleni na kuwakuta Martin na Babyanka wakizungumza kwa kucheka sana wakionekana kuzoeana sana.
“Jamani nimeshindwa hata kuja kuwasaidia ikiwa mimi ndio mwanamek niliyopo humu ndani”
“Usijali tumesha korofisha msosi. Kuna jipya lolote lililo tangazwa kuhisiana na kupotea kwenu?”
“Mimi na waziri mkuu?”
“Ndio?”
 
“Hapana ila nyinyi ndio munatafutwa kila dakika mutatangazwa”
“Je simu umepigiwa?”
“Hapana simu nimeifunga na si rahisi kwa mtu kuweza kunipata hewani ila mimi ndio ninaweza kumpigia simu mtu”
“Poa”
Tukaaanza kula chakula hichi tulicho kiweka kwenye sinia kubwa. Hatukuchukua muda mwingi tukamaliza kula chakula. Waziri mkuu akaanza kutuchorea ranami na barabara ya kutokea huku shamhbani kwake kwani hata mimi siikumbuki vizuri. Akatupatia namba yake ya siri ambayoa naitumia huku porini. Tukaanza kuzishuhulikia silaha zilizopo kwenye begii kwa kuzisafisha na kuzipanga vizuri kwa ajili ya kazi ambayo tunaiendea mbele yetu.
“Dany hakikisha kwamba unampata Lucy na kunirudi naye huku porini”
 
“Sawa mzee”
“Niwatakie safari njema, na kazi njema na nina imani kwamba baada ya maasaa machache ninaweza kupata habari nzuri”
“Usijali nina imani  utakwenda kuwa raisi ajaye”
Nilizungumza kwa utani na kumfanya waziri mkuu kucheka kidogo kisha akatupa mikono ya kutuaga. Nikazichomeaka kiunoni bastola zangu mbili ambazo zina risasi za kutosha, kisha bunduki yangu kubwa nikaishika vizuri. Martin akabeba begi lenye silaha na tukaanza kutoka humu ndani. Waziri mkuu akatusindikiza hadi lilipo gari.
“Jamani umakini ndio kitu cha muhimu. Tumieni ujuzi wenu wote kuhakikisha kwamba munamuangusha K2 na nina imani kwamba mutaweka historia kubwa kwenye hii nchi”
“Shukrani mzee”
Tukaingia kwenye gari huku Babyanka akiwa amekaas iti ya mbele. Taratibu nikawasha gari na kuanza kuondoka hili eneo. Sikuweza kuendesha gari kwa mwendo wa kasi kutokana na kuwangalia angalia barabara hiii ambayo kusema kweli inachanganya.
“Jamani haya maharage yananipa usingizi”
Martin alizungumza huku akijinyoosha viongo vya mwili wake.
 
“Pole sana, lala tukifika barabarani nitakustua”
“Asante mkuu”
Safari ikazidi kusonga mbele huku  kazi ya Babyanka ni kunisomea ramani ya kutokea kwenye huu msitu. Hadi inatimi saa mbili usiku tukafnikiwa kutoka katika huu msitu na kuingia kwenye barabara ya lami. Safari ya kuelekea Dar es Salaam ikaanza.
“Dany”
“Naam”
“Uumeoa?”
Babyanka alizungumza huku akinitazama kidole cha upande wa kushoto cha mkono wangu wa kushoto.
 
“Ndio nimeoa”
“Mke wako yupo wapi?”
“Nigeria”
“Ahanafahamu uwepo wako huku Tanzania?”
“Ndio japo tumetengana kwa sasa”
“Kisa nini?”
“Maisha ya hapa na pale”
“Pole”
“Asante. Vipi wewe?”
“Nilibahatika kupata mtoto mmoja wa kike ila alifariki akiwa na miaka miwili”
“Ohoo pole aisee”
“Asante”
“Alifariki na nini?”
“Malaria ilichangia sana kifo chake”
“Pole sana”
“Kuna ukaguzi hapo punguza mwendo”
Nikatazama mbele nikaona kizuizi cha jeshi la polisi. Taratibu nikapunguza mwendo kasi wa gari. 
 
“Martin”
“Mmmmm”
“Amka jiweka sawa”
“Tumefika barabarani?”
“Muda mwingi sana”
Askari aliye valia koti jeupe alitusimamisha, taratibu nikasimamisha gari pembeni, sikushusha kioo upande wangu ila Babyanka aliweza kushusha.
“Njoo huku”
Babyanka alizungumza na kumfanya askari huyo kuzunguka upande alipo yeye, nikatazaama askari wengine waliopo kando kando ya barabara huku wameshika bundiki zao aina ya SMG.
“Habari yako”
Babyanka alizungumza huku akimtazama askari huyu.
“Salama, ninaomba vitambulisho vyeni”
Babyanka akatoa kitambulisho chake, nikamuona askari mmoja akilikagua gari letu akafika katika upande wa kioo changu, taratibu akagonga dirisha taratibu na kuniomba nifungue.
“Mkuu waambie dereva wako afungue kioo”
“Kwani kuna tatizo?”
 
“Tupo kwenye msako mkali wa kuwatafuta magaidi wawili hatari sana”
“Sasa mimi mwenyewe na kitengo changu cha NSS, tupo kwenye mpango wa kuwatafuta hao magaidi, kama umeona kitambulisho changu basi turuhusu tuondoke unatupotezea muda”
Babyanka  alizungumza kwa msisitizo huku akimtazama askari huyu.
“Mmkuu”
Askari huyu alimuita mkuu wake aliyopo pembezoni mwa barabara upande wa pili.
“Mart”
“Ndio”
“Umakini”
“Sawa mkuu”
 
Nilizungumza kwa sauti ya chini huku nikianza kuivuta taratibu bunduki yangu iliyopo pembeni yangu. Tukamuona mzee mmoja akija kwa mwendo wa haraka, akafika sehemu alipo askari wake, akamkabidhi kitambulisho cha Babyanka, mkuu huyo akatazama kitambulisho hicho kwa sekunde kadhaa, kisha akatoa simu yake mfukoni mwake na kuanza kiminya minya batani zake.
“Mkuu unataka kufanya nini?”
Babyanka alizungumza huku akimtazama kuu huyu wa polisi, ila cha ajabu mkuu huyu wa polisi ndio kwanza akasogea mbali kidogo na gari. Nikaminya batani maalumu ya kutoa ‘lock’ za milango, mlio wa lock za milango kufunguka ikawa ishara tosha kwa Martin kuelewa ni kitu gani kinacho takiwa kufanyika kwa wakati huu. 
 
Tukafungua milango ya gari na kushuka kwa kasi na kuanza kuwashambulia askari wote walio shika bunduki. Shambulizi letu halikuchukua hata dakika mbili tukawa tumewashambulia askari wote wenye silaha na kumbakisha mkuu wao aliye pata kiwewe na bumbuwazi kubwa huku simu yake akiwa bado ameishika mkononi mwake.
“Chukau simu yake”
Nilizungumza na kumfanya Martin kumpokonya mzee huyu simu yake akaikuta ipo hewani, nikaitazama jina la namba aliyo ipigia simu nikakuta jina lililo andikwa  ‘mke wangu’. Nikaminya batani ya kukata simu na kumtazama vizuri mzee huyu.
 
“Dany kwa nini mumewaua hawa?”
Babyanka alizungumza huku akishuka kwenye gari kwani hata hili shambulizi wala hakuhusina na kipindi linaendelea nina imani alikuwa anashangaa shangaa.
“Mzee amewaponza wenzake”
“Ulikuwa unazungumza na nani mzee?”
“Mmmm, mke wangu”
“Hembu simu”
Babyanka alizungumza huku akiichukua simu niliyo ishika, akaanza kuikagua. Nikaona sura ya Babyanka ikibadilika kidogo akionekana kama ana wasiwasi.
“Vipi?”
“Mzee ulikuwa unazungumza na mke wako kweli?”
“Ndio”
“Raisi ni mke wako?”
Babyanka alizungumza kwa msisitizo huku akimtazama mzee huyu. Hata kabla mzee huyu hajajibu kitu chochote simu yake ikaita na Babyanka akanigeuzia simu hiyo na kuiona namba aliyo  kuwa anazungumza nayo mkuu huyu wa polisi, taratibu nikaichukua simu hii na kuipokea.
 
“Mume wangu”
Sauti ya K2 ikanifanya nimgeukie mzee huyu na taratibu nikasimama mbele yake.
“Sikuhizi umeanzisha mahusiano hadi na wazee?”
“DAANY?”
“Waziri mkuu, na mkuu wa NSS hukuona thamani yao hata  nikiwaua kwako ilikuwa ni POA tuu, sasa huyu mume wako nitamuua kama nilivyo fanya kwa waziri mkuu wako”
Nilizungumza kwa msisitizo huku nikiichomoa bastola yangu moja kiunoni mwangu na kuielekeza kwenye kichwa cha mzee huyu aliye zidi kutetemeka hadi mikojo ikaanza kulowanisha suruali yake.
 
“Dany Dany ninakuomba, ninakuomba mpenzi wangu usimuue huyo mwanaumee tafadhalii…………………!!”
K2 alizungumza kwa sauti iliyo jaa woga na majonzi hapa ndipo nikagundua udhaifu wa K2 upo kwa huyu mkuu wa polisi ambaye kwa muonekano wa nje ni mbaya mbaya tu na sijui amempa nini K2 hadi leo hii analia kwa ajili yake.
 
ITAENDELEA
“Haya sasa Dany ameugundua udhaifu wa K2 ambao ni mkuu wa polisi... je Dany atamfanya nini mkuu huyu wa polisi, atamuua au atamuacha hai. Usikose sehemu inayo fwata ya hadithi hii ya kusisimua kutoka kwa muandishi mahiri Eddazaria G.Msulwa”

CCM Wazidi Kumkomalia Benard Membe....Katibu Mkuu Agoma Kujibu Jumbe zake za Mitandaoni

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally amekataa masharti yaliyotolewa na kada wa chama hicho, Bernad Membe katika ujumbe wake kupitia kitandao ya kijamii na kusema huo siyo utaratibu wa kukutana na wanachama wake.

Dk Bashiru amesema hayo leo Jumamosi Desemba 1, 2018 wakati akizungumza na wajumbe wa  mkutano mkuu wa CCM wilaya ya Bukombe mkoani Geita.

Amesema katika miaka 10 iliyopita CCM haikufanya vizuri kutokana kikundi cha wachache kujifanya ndiyo wenye nguvu na kudharau jambo lililosababisha chama kisipendwe na wapiga kura.

Amesema tangu achaguliwe kuwa katibu mkuu hajawahi kuonana na Membe na licha ya chaguzi zote zinazofanyika za kurudisha wabunge, Membe aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nje hajawahi kutoa mchango wowote wa mawazo.

Amesema Membe kama mwanachama mwingine hana nguvu zaidi ya chama hivyo bado anamhitaji afike kwake bila masharti yoyote.

"Sikumsema Membe kama mtu maarufu au mwenye nguvu bali nimemsema kama mwanachama wa kawaida, hana tofauti kabisa na wanachama walioingia leo, ila ana tofauti kwa kuwa amekuwa waziri na mbunge” amesema Dk Bashiru

“Namuhitaji sana (Membe), ningekuwa na namba yake ya simu ningempigia,” ameongeza.

Amesema CCM kipindi cha nyuma imeumizwa  na makundi, fitina, uongo na nguvu ya pesa mambo ambayo sasa hawapo tayari  kuyaendeleza.

Dk Bashiru ametoa kauli hiyo kujibu ujumbe unaodaiwa kuwa wa Membe aliyeutoa kupitia mitandao ya kijamii akijibu wito wa katibu mkuu huyo wa CCM kumtaka kufika ofisini kwake kujibu tuhuma zinazodaiwa kutaka kumkwamisha Rais John Magufuli.

Katika ujumbe huo ulioandikwa na mtu aliyejiita Bernard Membe unasema; Kufuatia taarifa za kwenye mitandao jioni (jana) hii na ujumbe mfupi unaotumwa kwake “Nimeamua kutoa ujumbe huu kwa wote wanaonitakia mema.”

“Usiku huu nimempelekea Katibu Mkuu wa chama chetu ndugu Bashiru ujumbe wa kukubali kumwona mara nitakaporejea kutoka nje ya nchi.”

“Nimeshangazwa kidogo na utaratibu uliotumika kuniita, lakini kwa sababu ya ugeni kazini na kwa sababu ninamheshimu, nitakwenda kumwona ofisini kwake,” amesema.


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya Novemba 2

Waziri Mkuu Azindua Mkakati Wa Kudhibiti Ukimwi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezindua Mkakati wa Nne wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI 2018/19 – 2022/23 ambao unatarajia kupunguza maambukizi mapya ya VVU kwa asilimia 75 ifikapo mwaka 2020 na asilimia 85 ifikapo mwaka 2023. 

Matokeo mengine yanayotarajiwa kufikiwa kutokana na mkakati huo ni kupungua kwa maambukizi mapya ya VVU miongoni mwa watoto kwa chini ya asilimia 5 ifikapo mwaka 2023 na chini ya asilimia 2 ifikapo mwaka 2030.

Waziri Mkuu amezindua mkakati huo jana (Jumamosi, Desemba 1, 2018) kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya UKIMWI duniani yaliyofanyika Kitaifa jijini Dodoma na kusema kuwa matayarisho yake yamezingatia matokeo ya mapitio ya Mkakati wa Tatu wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI 2013/14 – 2017/18. 

Alisema mbali na matokeo hayo pia mkakati huo utawezesha kupungua kwa vifo vinavyohusiana na ukimwi  kwa asilimia  50 ifikapo mwaka 2020 na asilimia 70 ifikapo mwaka  2023 na kupunguza unyanyapaa na ubaguzi ifikapo 2023 na kuelekea kutokomeza kabisa ifikapo mwaka 2030.

Hata hivyo Waziri Mkuu amesema mkakati huo umewianisha na kupanga programu mbalimbali zinazosaidia mwitikio wa Taifa zikiwemo afua zinazotekelezwa kupitia mpango wa dharura wa Rais wa Marekani wa uKIMWI (PEPFAR). 

“Pia Mfuko wa Dunia wa kudhibiti UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria (Globa Fund) na jitihada nyingine za makubaliano ya ushirikiano baina ya nchi mbalimbali na ili kupata matokeo mazuri tunapaswa kuimarisha mawasiliano na uratibu miongoni mwa wadau wote sambamba na kufuata na kutekeleza vipaumbele vilivyoainishwa.”

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema maadhimisho hayo husaidia kubaini changamoto, mafanikio na hivyo, kuja na mikakati ya kupambana na maambukizi ya VVU na UKIMWI. “Siku hii hutoa fursa kote Duniani kutafakari kwa mara nyingine kuhusu tulipotoka, tulipo na tunapokwenda katika mapambano ya UKIMWI kwenye jamii zetu.” 

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amezungumzia kuhusu faida za kampeni ya FURAHA YANGU aliyoizindua mwezi Juni mwaka huu, ambapo aliagiza mikoa yote kufanya uzinduzi wa kampeni hiyo kwenye ngazi za mikoa na hata wilaya.

Amsematakwimu zinaonesha kuwa wakati wa uzinduzi wa kampeni ya FURAHA YANGU katika mikoa yote nchini jumla ya wananchi 262,114 walijitokeza kupima VVU, wakiwemo wanawake 136,389 na wanaume 125,725.

 “Natoa wito kwa Mikoa na Wilaya zote kuwa kampeni hii iwe endelevu. Viongozi katika ngazi mbalimbali tuungane kwenye uhamasishaji wa jambo hili kwani vita dhidi ya VVU na UKIMWI inahitaji dhamira ya dhati na tafakuri ya kina katika kujilinda dhidi ya maambukizi mapya.”

Waziri Mkuu amewahakikishia kuwa kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli itaendelea kutekeleza na kuboresha huduma za upimaji wa Virusi Vya UKIMWI, kuzuia maambukizi ya kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, matibabu ya magonjwa nyemelezi na kupiga vita unyanyapaa wa aina zote kwa WAVIU.

Rais Magufuli awaonya wanaotaka kuzichonganisha Tanzania na Kenya

$
0
0
Rais wa Tanzania, John Magufuli amewataka wananchi wa Tanzania na Kenya kuendelea kushikamana na wasikubali kuchonganishwa katika masuala yanayolenga kuwatenganisha.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo jana Jumamosi Desemba 1, 2018 wakati wa uzinduzi wa kituo cha huduma za forodha kilichopo katika mpaka wa Namanga mkoani Arusha.

Alisema wananchi wa mataifa hayo wanapaswa kuungana na kuwa kitu kimoja wakishirikiana katika harakati za kuleta maendeleo kwenye nchi zao.

“Sisi ni wamoja hata mimi na (Rais wa Kenya, Uhuru) Kenyatta ni marafiki hivyo hakuna sababu ya kuchukiana endeleeni kupendana, kusaidiana na kushikamana.”

“Asitokee mtu wa kuwachonganisha ipo siku viongozi tutaondoka au kubadilika lakini nyinyi mtaendelea kuwepo,” alisema Rais Magufuli.

“Najua kuna watu wanachomoka na kusema vineno vya ajabuajabu ila nawaambia washindwe na walegee Afrika Mashariki ni moja,” aliongeza.

Kwa upande wake, Rais Kenyatta alisema ipo haja kwa nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki kuungana na kuweka mazingira bora ya kufanya biashara kinyume na hapo zitaendelea kuwa maskini.

“Tusipoungana nchi zetu zitaendelea kuwa maskini. Tuungane kwa kuwa na soko la pamoja litakalowezesha kuleta wawekezaji wakubwa ambao watakuwa kiini cha uwekezaji utakaozalisha ajira kwa vijana,” alisema.

Zitto Kabwe Matatani Tena.....TAKUKURU Wamtaka Afike Ofisini Kwao Haraka

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe, ameingia matatani tena safari hii akiitwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kuhusu mambo aliyoandika kwenye mitandao ya kijamii.

Taarifa iliyotolewa na Takukuru jana ilisema kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo, Brigedia Jenerali John Mbungo, amemtaka Zitto Kabwe kufika ofisini kwake akatoe ushahidi wa tuhuma alizotoa kuwa kampuni tatu za chuma kuwa zimewahonga baadhi ya viongozi wa serikali.

Takukuru katika taarifa yake hiyo ilisema wameamua kumwita Zitto baada ya kusoma kwenye mitandao ya kijamii taarifa aliyoisambaza juzi akitoa shutuma hizo.

Alifafanua kuwa taarifa hiyo ilikuwa ikielezea hisia za kuwapo kwa vitendo vya rushwa katika mradi wa uzalishaji wa chuma Liganga na Mchuchuma.

“Taarifa hiyo ambayo imewasilishwa kupitia ukurasa wa ‘Jamii Forum’ inasomeka kama imetolewa na Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini,” ilisema taarifa hiyo ya Takukuru.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kampuni tatu za chuma kutoka China, Russia na Uturuki, zimewahonga baadhi ya watendaji wa serikali kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji na Ofisi ya Rais kwa lengo la kuchelewesha ukamilishaji wa mradi wa Mchuchuma na Liganga hadi ujenzi wa mradi wa reli ya kisasa (SGR) utakapokamilika.

Taasisi hiyo ilisema baada ya kupokea taarifa hiyo, ilifanya jitihada za kuwasiliana na Zitto kwa njia ya simu bila mafanikio.

Ilisema lengo la kumtafuta lilikuwa kujiridhisha iwapo ni kweli yeye ndiye aliyetoa taarifa hiyo na pili ni kuhitaji ushirikiano wake katika kushughulikia suala hilo.

“Tunatoa taarifa hii kupitia vyombo vya habari kumwomba Zitto Kabwe afike ofisi za Takukuru Dar es Salaam mapema iwezekanavyo ili tushirikiane katika kulishughulikia suala hili muhimu kwa mustakabali wa maendeleo ya taifa letu,” ilieleza taarifa hiyo.

Aidha, Takukuru inaendelea kuwashukuru wananchi na wazalendo wa Tanzania ambao wamekuwa mstari wa mbele kushirikiana nao katika kufichua vitendo vya rushwa na ufisadi pamoja na wanaojihusisha na vitendo hivyo bila woga.

“Hatua hii inaonyesha uzalendo wa Watanzania kuunga mkono jitihada za Rais John Magufuli katika kutokomeza kero ya rushwa nchini. Tunasisitiza wananchi kutumia njia sahihi na rasmi za kuwasilisha malalamiko dhidi ya vitendo vya rushwa ili hatua stahiki za kisheria ziweze kuchukuliwa mara moja,” alisema.

Juzi, Zitto alidaiwa kuandika kuwa amepata habari za kushtusha kuwa kampuni tatu za China, Russia na Ururuki zimehonga baadhi ya watendaji wa serikali ya awamu ya tano kuchelewesha mradi wa Mchuchuma na Liganga. Lengo ni kuhakikisha nchi hizo zinapata soko la chuma chao.

Aliendelea kuandika kuwa kuhujumu mradi wa Mchuchuma na Liganga ni uhaini. Baadhi hawawezi kusahau hujuma hiyo na yoyote anayeshiriki atasakwa mpaka kaburini kwake ikibidi kuondoa kinga za watu ili iwe fundisho kwa uhujumu huu uchumi na uhai wa taifa letu.

“Msamaha wa kodi kwa bomba la mafuta kutoka Uganda ni mkubwa na hauna faida kulinganisha na mradi wa Mchuchuma na Liganga utakaotoa ajira za kudumu 35,000 kuingiza fedha za kigeni bilioni 4.6 kwa mwaka na kuifanya nchi yetu kuwa na viwanda vikubwa,” aliandika.

Zitto aliendelea kueleza katika ukurasa huo kuwa yote hayo yanafanywa chini ya uangalizi wa Rais Magufuli kiasi kwamba amelishwa matango pori dhidi ya mradi huo. Nchi yetu imegeuzwa dampo la kuagiza bidhaa za chuma kihayawani.

“Watendaji hao kutoka Wizara ya Fedha, Viwanda na Biashara na Ofisi ya Rais wamekula njama kiasi cha kuwezesha Bunge kutunga sheria kuondoa kodi zote kwa mataruma ya reli yanayoagizwa kutoka nje na kuzuia mradi wa Mchuchuma na Liganga kupata msamaha wa kodi kuwezesha mradi kuanza,” aliandika Zitto.


Diamond Platnumz: Nataka kuoa, imetosha....Nimefanya vitu vingi

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Diamond Platnumz amefunguka kuhusu mipango yake ya kuoa.

Muimbaji huyo akizungumza na Wasafi TV amesema ana kila sababu ya kuoa kwa sasa kwani ameshafanya mengi.

"Nataka kuoa sana mwaka huu, nina kila sababu ya kuoa, imetosha nimefanya vitu vingi sana, yaani nimefanya vitu vingi," amesema Diamond.

==>>Msikilize Hapo chini

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

$
0
0

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara, Msanii wa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo Dawa na PETE za Bahati zenye uwezo mkubwa wa kuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.

Kutana na Sheikh Jumaa Bilal. Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki. 

Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. Sheikh Jumaa Bilal ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA-  Sheikh Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na Nje ya nchi.

Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nayasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.

Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudishaa alipote, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMBA, GARI..), Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali na UTAJIRI bila masharti na mengine mengi ya Siri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET)

*{لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّهُ بِاللَّغْوِ فِي أيْمَانِكُمْ وَلَٰكِنْ يُؤَاخِذُكُمْ بِمَا عَقَّدْتُمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِمَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ }* ﴿٨٩﴾

✨Wabillahhi Tawfiq Asallam  Alaikum

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa
nambari ya simu

+255 688 745 790
+255 672 861 042
Whatsapp :  0762 252 102

Rais Magufuli Kuzindua Na Kuweka Jiwe La Msingi Mradi Mkubwa Wa Maji Jijini Arusha Leo

$
0
0
Na. Vero Ignatus, Arumeru
Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania mhe John pombe magufuli anatazamia kuweka jiwe la msingi katika mradi wa uboreshaji wa huduma ya maji safi na usafi wa mazingira jijini Arusha na baadhi ya maneo ya wilaya ya Arumeru

Mradi huo uliotiliwa saini hivi karibuni utazinduliwa katika kijiji cha kimyaki majira ya saa nne asubuhi na baadae kuzungumza na wananchi katika kijiji cha mringarimga

Wakizungumzia hali ya maji, mkazi wa eneo mringaringa Josephat Joshua amesema wakinamama wanalazimika kwenda kutafuata maji ya kunywa kutoka mringaringa kilometa mbili katika sehemu inayoitwa njoro au kwa wavii.Wakati mwingine sisi wakina baba tunabakia na watoto nyumbani.

'' Wakinamama wanafuata maji, hadi arudi nyumbani anakuwa tayari amechoka sana kutokana na kutafuta maji umbali wote huo bado majukumu mengine yanamsubiria"alisema Joshua.

Bi Miriam Zakayo amesema inawalazimu kutembea umbali mrefu na kushindwa kutimiza majukumu yao kwa wakati

'' Maji tunayoayatumia ni ya mto nayo yanachukua muda mrefu hadi kufunguliwa kwa sababu wengine tunayatumia katika mifugo, mashamba, hivyo tukitaka maji ya kunywa tunayafuata mbali"alisema Miriam.

Mkazi mwingine wa kijiji hicho Saning'o Lebang'ute Laizer amesema kwa ujio wa Rais Magufuli kwao ni neema kwani itawatatulia tatizo hilo sugu la maji safi, barabara na umeme

''Tunashukuru sana kwa kuja kutufikia kwetu ni neema, barabara, hii inawahudumia watu wa kimmyaki, Ilikiding' a na Sambasha, mradi wa umeme, ni fursa kwetu pia"alisema Laizer.

Operesheni Ya Uvuvi Haramu Yapaisha Mapato Serikali Kuu, Samaki Waongezeka

$
0
0
Operesheni za kudhibiti uvuvi haramu hapa nchini, zimeiwezesha serikali kuu kupata mrabaha wa Shilingi Bilioni 2.2 kuanzia Mwezi Desemba mwaka 2017 hadi Mwezi Novemba mwaka 2018, kutoka Shilingi Milioni 457.

Hayo yalibainishwa (01.12.2018) Jumamosi jijini Mwanza na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega wakati akiongoza kikao cha kufanya tathmini ya operesheni sangara kitaifa awamu ya tatu kwa mwaka 2018, kanda ya Ziwa Victoria, kikao kilichohudhuriwa na maafisa waliohusika katika operesheni hiyo, ambapo amesema kiasi hicho cha pesa kimeongezeka kutokana na mafanikio ya udhibiti wa mianya ya utoroshaji fedha.

“Mwaka 2017 mpaka tunafunga mwaka mwezi Desemba mrabaha wa serikali kuu kabla ya kufanya operesheni ulikuwa Shilingi Milioni 457, mwaka 2018 hadi Mwezi Novemba mrabaha wa serikali kuu ni Shilingi Bilioni 2.290, kutoka Shilingi Milioni 457 mpaka Shilingi Bilioni 2.290 unaweza kuona kwamba ni ongezeko la zaidi ya asilimia 200, hii maana yake kulikuwa na utoroshaji mkubwa wa fedha ambazo zingeingia katika mfumo mkuu wa serikali.” Alisema Mhe. Ulega.

Aidha, katika kikao hicho ambacho kilihudhuriwa na baadhi ya wafanyabiashara wa samaki, Mhe. Ulega alisema kabla ya kuanza kwa operesheni za kudhibiti uvuvi haramu, takwimu zilionesha uwepo wa samaki wachanga zaidi ya Asilimia Tisini, lakini baada ya operesheni hizo samaki walianza kuongezeka kauli iliyoungwa mkono na wafanyabiashara waliohudhuria kikao hicho ambao walisema samaki wakubwa wameanza kupatikana kwa wingi katika ukanda wa Ziwa Victoria.

Awali katika kikao hicho, akiwasilisha taarifa ya operesheni sangara kitaifa awamu ya tatu mwaka 2018 katika ukanda wa Ziwa Victoria, Afisa Mfawidhi wa kanda hiyo Bw. Didas Mtambalike alisema tangu kuanza kwa operesheni hiyo tarehe 18 Mwezi Oktoba Mwaka 2018 hadi tarehe Moja Mwezi Desemba Mwaka 2018 Shilingi Bilioni 1.172 zilipatikana kutokana na malipo ya faini walizotozwa waliojihusisha na mtukio ya uvuvi haramu.

Bw. Mtambalike pia alisema zoezi hilo limewezesha vyombo vingi vya uvuvi na biashara za bidhaa za uvuvi kusajiliwa na kupatiwa leseni kutokana na elimu ambayo wavuvi walikuwa wakipatiwa ili kufanya shughuli zao kwa kufuata sheria na taratibu za nchi.

“Kitu ambacho tumekibaini ni kwamba vyombo vingi sasa hivi vimesajiliwa vile vya uvuvi, vile ambavyo viko chini ya halmashauri vimesajiliwa lakini pia vile ambavyo viko chini ya serikali kuu vimesajiliwa ambavyo ni zaidi ya urefu wa mita 11.” Alisema Bw. Mtambalike

Baadhi ya wadau wa uvuvi ambao walipata nafasi ya kutoa maoni yao katika kikao hicho, walimuomba Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, uwepo wa bei elekezi kwa mazao ya samaki ili wavuvi waweze kuuza samaki kwa bei ya uhakika, pamoja na kulifanyia kazi ombi lao la kuendelea kuvua dagaa kwa kutumia taa zinazotumia mwanga wa jua kutokana na kusitishwa kwa ya taa hizo kwa shughuliza uvuvi hususana wa dagaa kutokana na uwepo wa madai ya samaki hao kuathiriwa na taa hizo, jambo ambalo Mhe. Ulega alisema serikali inalifanyia kazi.

Kikao cha tathmini ya operesheni sangara kitaifa awamu ya tatu mwaka 2018 katika kanda ya Ziwa Victoria kiliongozwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, ambapo kimefanya tathmini ya kutokomeza uvuvi haramu katika maeneo ya Singida, Sengerema, Ukerewe, Simiyu, Mwanza, Kagera, Geita na Mara ambayo yote yapo chini ya kanda ya Ziwa Victoria, ambapo kikao hivcho kimeridhishwa na mafanikio makubwa ambayo yamepatikana katika kudhibiti uvuvi haramu.

MWISHO:

Zitto Kabwe Ajipigia Promo ya Urais 2020....Asema Akiupata Wananchi Watakula Bata Mwanzo Mwisho

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama Cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe ameanza kujipigia chapuo kushika nafasi ya juu ya uongozi nchini, akitoa ahadi nono kwa Watanzania.

Mwanasiasa huyo ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Mjini, ameeleza kupitia Twitter kuwa endapo atapewa nafasi ya kuwa Rais wa nchi, wananchi wake wataishi kwa raha na kustarehe huku wakifanya kazi, kwa lugha ya mtaani ‘watakula bata’.

“Ninaamini nitakuwa Rais bora kwa uwezo wake Mola. Nitauona upinzani kama chachu ya Maendeleo badala ya kuwa na hofu nao. Nitarejesha taswira chanya ya nchi yetu mbele ya jamii ya kimataifa kwa kulinda Demokrasia na haki za binaadam. Mtachapa kazi, Lakini pia mtakula bata,” ameandika Zitto Kabwe.

Katika tweet nyingine, Zitto ameweka picha inayomuonesha akiwa na waziri wa zamani wa Mambo ya Nje, Bernard Membe na kuwataja baadhi ya vigogo wa upinzani pamoja naye akidai anawataka wafuate sera hiyo.

“Mbobezi Bernard Kamilius Membe Anawasalimu. Hata ikiwa yeye lazima #KaziNabata Au sio jamani? Jamaa yetu T A M Lissu aambiwe pia akiwa yeye #KaziNabata pia maana watu wamechokaaaa. Hata Mzee Edo akiwa yeye tena sisi tunataka #KaziNabata tu,” amendika.

Mwaka 2015, Zitto hakuweza kuwania urais kutokana na kuwa chini ya umri unaokubalika kisheria, lakini chama chake kilimsimamisha aliyekuwa Mwenyekiti wake, Anna Mghwira ambaye hivi sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi.

Hii inaweza kuwa ni ishara ya nia ya Zitto Kabwe kuingia kwenye kinyang’anyiro cha Urais mwaka 2020 kupitia ACT-Wazalendo.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Dr.Mjukuu wa kushosha : Pata Tiba Asili ya Tatizo la Uzazi, Kutopata Hedhi kwa Mpangilio, Nguvu za Kiume, UTI Sugu

$
0
0
SIX(6) power; Ni dawa ya Nguvu za kiume inayofanya kuchelewa kufika kileleni dkk 30 Hadi 46 unaweza kurudia tendo utakavyo,pia inarutubisha mbegu za kiume kwa wasio na sifa ya kupata mtoto,dozi Ni siku sita mabadiliko masaa manne.Tumia six(6) power ndio kiboko wa yote usisubiri kuhadithiwa.

SHOOLA 4 POWER; Wenye maumbile madogo (KIBAMIA) inanenepesha na kurefusha uume,kama tatizo Ni la kuzaliwa siku 12 Kama Ni la ukubwani siku 6.

MBUKE; Dawa ya Uzazi kwa aliyefungwa na kutofanikiwa kupata mtoto,kwa asie pata hedhi kwa mpangilio mzuri tatizo huisha kabisaa..Ni ya unga.

LYONGO;dawa ya mvuto wa mapenzi Kama umeachwa yote yatakwisha aliembali atakuhudumia mwenza wako atarejea ndani ya SAA 12 hata Kama yupo mbali.

HOLAZA; Ni dawa ya kumaliza matatizo mengi mengi Kama kesi,dhuluma,kushindwa kuuza eneo nyumba na Kama biashara haziendi.

TALIGULA;dawa ya kufungua kitu kilichofungwa kuchawi,kimizimu,majini wabaya mashuleni,kutokupata ajira,kuoa au kuolewa na Safari zilizofungwa
 
KASELA;Ni kiboko ya kusafirisha mizigo na kufika salama..iwe majini,migodini pia katika kilimo na ufugaji.

DR.Mjukuu wa kushosha asema kwanini usumbuke na maradhi mwilini wakati tiba zipo?? ,Amini tiba asilia Sasa maradhi yako yatakwisha .

Je,wewe una maradhi gani mwilini mwako??

(1)Sukari ya kupanda na kushuka(TUNDWA)Ni ya unga inayochemshwa ,dozi Ni siku 20.

(2)Presha ya kupanda na kushuka(NGADA) ni dawa ya unga dozi siku 14

(3)maleria sugu(NINJIWE) dozi siku 8 unapona kabisa

(4)U.T.I sugu(GUMO)Dozi siku 4 habari kwisha kabisa.

(5)Typhoid sugu(IKWATA) Dozi siku 3

(6)Kifua kubana,moyo,Figo(LUGALA)dozi siku 7

(7)Tezi dume(Dozi siku 8 - unga),ngiri,busha bila operation (SALIUNGU)dozi siku 14

(8)Miguu kuwaka moto (JIMYA) dozi siku 6

(9) kilungulia,kwikwi(INJACHI)dozi masaa 6.

(10)msongo wa mawazo.

(11) vidonda vya tumbo (MPALALA) Dozi siku 7.

Hizo Ndizo Huduma Zitolewazo Na Nyingine Nyingi,usitume Meseji Wala Kubip,nahudumia Duniani Pote Ulipo.

Ofisi Zipo Katika Mikoa Miwili Shinyanga Wilaya Ya Kahama Na Dar Es Salaam Wilaya Ya Ilala..Sehemu Zingine Nasafirisha..niulize Kwa Mawasiliano Yafuatayo...

     0744 922 982
     0716 608 959
     0784 475 946.

Vyama vya wafanyakazi Vyadai maoni yao hayakuzingatiwa wakati wa utungaji wa kanuni za Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA)

$
0
0
Vyama vya wafanyakazi vimedai maoni yao hayakuzingatiwa wakati wa utungaji wa kanuni za Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, lakini mamlaka ya usimamizi wa mifuko hiyo (SSRA) imesema hakuna haja ya kuzibadilisha.

Hivi karibuni umeibuka mjadala kuhusu mafao baada ya kanuni hizo kuondoa mfumo wa zamani wa kulipa asilimia 50 ya mafao ya mkupuo na badala yake mstaafu kuruhusiwa kuchukua asilimia 25 kwa mkupuo na asilimia 75 igawanywe ili ilipwe kama pensheni kwa kila mwezi kwa kipindi chote cha maisha ya mstaafu.

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu (THTU), Dk Paul Loisulie amesema pendekezo lao la kuboresha kikokotoo ilikuwa ni 1/540, miaka 15.5 na asilimia 50 ya fao la mkupuo na asilimia 50 inayobaki iwe pensheni ya kila mwezi.

Alisema walitoa mapendekezo mengi kuliko vyama vyote vya wafanyakazi na walipendekeza kikokotoo kiwe ndani ya sheria badala ya kuwekwa kwenye kanuni.

“Uzuri wa sheria inajumuisha maoni ya watu wote tofauti na kanuni ambazo zinaundwa na waziri,” alisema Dk Loisulie.

Alisema SSRA inaweza kuratibu kazi ya kupokea maoni ya wadau wote kwa lengo la kurekebisha kikokotoo kilicholeta taharuki na hivyo kutuliza wafanyakazi.

“THTU itawakutanisha wataalamu wa sekta ya hifadhi ya jamii ili kuandaa mapendekezo ya kina na kuyawasilisha SSRA na wizara husika kwa ajili ya mjadala na ufumbuzi,” alisema Dk Loisulie.

Naye rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Tumaini Nyamuhokya alisema walihangaika sana wakati kanuni hizo zikiundwa, lakini hawakufikia muafaka, na amewataka wanachama watulie kwanza.

“Vikao vya kisheria vitafanyika wiki ijayo, kelele ni nyingi kwa sasa wafanyakazi wanaona hatujatimiza wajibu wetu kwao,” alisema Nyamuhokya.

“Tuombe tu wawe na subira baada ya vikao hivyo, tutaeleza msimamo wetu.”

Alisema kabla ya kupitishwa kanuni hizo, mjadala baina yao na mamlaka husika ulichukua zaidi ya miezi mitatu na baada ya kikao cha wiki ijayo, wafanyakazi ambao ni wanachama wao wataelezwa hatua itakayofuata.

Mkurugenzi Mkuu wa SSRA, Irene Isaka alisema utoaji wa mafao mkupuo wa asilimia 50 unahatarisha uhai wa mifuko husika na hata iliyokuwa inafanya hivyo, utafiti uliofanyika ulibaini haiwezi kuwa endelevu.

“Uundwaji wa mifuko iliyokuwa inatoa mafao mkupuo ilikuwa na makosa tangu awali. Mfano mfuko wa PSPF ulikuwa na mwenendo mbaya kama usingeunganishwa, ulikuwa unahitaji marekebisho makubwa,” alisema Isaka.

Alisema kwa sasa haoni haja ya kubadilishwa kwa kanuni zilizopitishwa za kikotoo wala sheria, badala yake mamlaka itaongeza nguvu katika kutoa elimu.

“Watu wakitaka mafao ya mkupuo yawe asilimia 50, haiwezekani na hiyo itakuwa sio pensheni tena, labda tuiite mfuko wa akiba,” alisema Isaka.

“Hata hivyo, wengi wanaolalamika ni wale wa NSSF ambao mabadiliko haya hayawahusu na wengine wanaoleta malalamiko hapa ofisini si wachangiaji wa mfuko wowote.”

Uongozi Wizara Ya Viwanda Wawatoa Hofu Wakulima Wa Korosho

$
0
0
Kuhakikisha azma ya Serikali ya Awamu ya Tano inanunua korosho yote ya wakulima inatimia kabla ya kipindi cha masika hakijashika kasi, uongozi wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji umewatoa hofu wakulima wote wa mikoa ya kusini kuwa serikali inao uwezo wa kununua na kihifadhi korosho yote itakayonunuliwa.

Hakikisho hilo limetolewa na Katibu Mkuu, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Joseph Buchwaishaija wakati anahitimisha siku ya kwanza ya oparehseni ya ukaguzi wa maghala kwenye mikoa ya Lindi na Mtwara.

“Ziara ya ukaguzi wa maghala inatokana maagizo ya kikao cha tathmini ya Operesheni Korosho kilichoitishwa na Mwenyekiti wake Waziri wa Kilimo, Mhe. Japhet Hasunga, ambapo pamoja na mambo mengine kilibaini ufinyu wa maeneo ya kuhifadhia korosho kutoka kwa wakulima” anasema Prof. Buchweishaija.

Kwenye ziara hiyo Prof. Buchwaishaija pamoja na Naibu Katibu Mkuu (Viwanda) Ludovick Nduhiye na maafisa wengine waandamizi wa wizara hiyo walifanikiwa kukagua maghala ya korosho kwenye wilaya za Mtwara, Mtama, Masasi na Nachingwea na kubaini kuwa maghala makuu na yale ya uhifadhi yana nafasi ya ziada kuhifadhi korosho zaidi ya tani elfu arobaini na nane.

“Nachukua nafasi hii kuwatoa wasiwasi wakulima wote kwamba, maghala na sehemu za kuhifadhi korosho zetu sio tatizo tena, na tutahakikisha korosho zote ziliyopo kwenye AMCOS (vyama vya msingi) tunazisafirisha haraka iwezekanavyo kabla ya msimu wa mvua kuanza.” Anasisitiza Prof. Buchwaishaija.

Mbali na kukagua maghala ya kuhifadhi korosho, ziara hiyo pia ilikuwa na lengo la kukutana na makumpuni ya kubangua korosho ambayo yameonyesha nia na utayari wakati serikali itakapoanza kubangua korosho ilizozinunua moja kwa moja kutoka kwa wakulima.

Operesheni ya ukaguzi wa maghala  mikoa ya kusni inatarajiwa kuendelea kwenye wilaya za mkoa wa Ruvuma kesho.

Zari awajia juu mashabiki wanaomtaka ahame kwenye nyumba ya Diamond ya Afrika Kusini

$
0
0
Mjasiriamali  Zari Hassan ambaye pia ni mzazi mwenzie na Diamond Platnumz amejikiuta akishindwa kuvumilia maoni ya mashabiki wake mtandaoni wanaomtaka aondoke kwenye nyumba ya kifahari ya mzazi mwenzie,Diamond Platnumz
 
Zari kupitia ukurasa wake wa Intagram amesema kuwa hawezi kutoka kwenye nyumba hiyo, kwani yeye na watoto wake (Tiffah na Nillan) walinunuliwa nyumba hiyo ya kuishi.

Mrembo huyo kutoka Uganda ambaye makazi yake kwa sasa yapo Afrika Kusini, amesema kuwa kung’ang’ania kwake sio kwamba hana nyumba nyingine hapana anamiliki nyumba nne Afrika Kusini, bali anaishi kwenye nyumba hiyo kwani ni ya kwake na watoto wake.

Diamond na Zari wameachana mapema mwaka huu baada ya kuishi kwa takribani miaka mitatu kwenye mahusiano, wamefanikiwa kupata watoto wawili Tiffah ambaye ndio mtoto wa kwanza wa Diamond na Nillan.

Rudisha Heshima ya Ndoa Yako.....Pata Tiba Bora ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Wanaume wengi hawawaridhishi wake au wapenzi wao kwa kutokuwa na nguvu za kiume au uume mdogo? 

Kawaida mwanamke huwa anachukua dakika saba 7 adi kumi 10 ili aweze kufika kileleni na wakati wanaume wengi kwa sasa hutumia dakika tatu 3 hadi tano 5 ameshafika kileleni , hapo utagundua kabisa mke au mpenzi wako hujamtendea haki yake. Dr Nyalobi  anakuletea dawa imara na yenye nguvu tatu?

Simpo power; Hutibu matatizo yafatayo;

1.itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-20 kwa tendo la kwanza

 2. itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi mara nne 

3 Huimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa 

4 Hutoa uchovu pale umalizapo kufanya tendo

 Je kwa nini uzidi kuona aibu pale ukutanapo na mpenzi wako kwa sabubu uume wako mdogo na mwembamba? 

Promix; hii ni dawa ya kuongeza uume saizi upendayo.Dawa zetu ni za mitishamba na hazina madhara yoyote na ni tofauti na ulizowai kutumia ata wazee hutumia 

Mkuya; hii ni dawa ya kisukari dozi siku 21 

Mwaru; hii ni dawa ya uzazi hufungua mirija ya uzazi ata kama uzazi umefungwa

Markusi; ni dawa ya presha zipo dwa za korodani kuvimba,, vindonda vya tumbo, kupunguza kitambi, na minyama uzembe 

Fika ofisini kwetu Buguruni Malapa na Mwanza yupo wakala wetu au piga simu 0752348593 -Dokta Nyalobi

Huna Sababu Ya Kuaibika tena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0620510598  / 0743543944

Lazaro Nyalandu Awataka Watanzania Wamuombee Freeman Mbowe na Ester Matiko

$
0
0
Waziri wa zamani Lazaro Nyalandu leo Jumapili Desemba 2, 2018 amewataka Watanzania kuwaombea watu waliowekwa kizuizini nchini Tanzania akiwemo mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko.

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter, mbunge huyo wa zamani wa Singida Kaskazini ameandika, “Jumapili  ya leo tuungane sote kumwombea mwenyekiti Mbowe, Matiko na wote waliowekwa kizuizini popote Tanzania.”

“Kwa sababu moja, au nyingine imeandikwa haki huinua Taifa. Wenye Mamlaka wakaone fahari kutenda haki bila kukawia zaidi. Kama Taifa, tusimame pamoja nao.”

Mbowe na Matiko walifutiwa dhamana na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, anayesikiliza kesi hiyo Novemba 23, 2018 kutokana na maombi ya upande wa mashtaka yaliyodai wameshindwa kuhudhuria mahakamani bila sababu za msingi katika kesi yao iliyopangwa kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali.

Viongozi hao wamekata rufaa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam chini ya hati ya dharura wakipinga uamuzi wa Mahakama ya Kisutu kuwafutia dhamana katika kesi ya jinai inayowakabili mahakamani hapo.

Juzi, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ilisimamisha usikilizaji wa rufaa ya Mbowe na Matiko hadi rufaa ya Serikali itakapoamuliwa na Mahakama ya Rufani.

Joshua Nassary "Apewa Makavu" Mbele ya Rais Magufuli

$
0
0
Mbunge wa Viti Maalum CCM, Amina Mollel amedai tangu Joshua Nassari alipochaguliwa kuwa mbunge wa Arumeru Mashariki kwa tiketi ya Chadema, ametokomea kusikojulikana na hajui shida za wananchi waliomchagua.

Mollel ametoa madai hayo leo Jumapili Desemba 2, 2018 katika uzinduzi wa mradi wa uboreshaji huduma za maji safi na maji taka katika jimbo la Arumeru Mashariki uliofanywa na Rais Magufuli.

"Naamini walifanya makosa na hawatarudia tena 2020 na mimi niko hapa kwa ajili ya kuwasemea ili kuhakikisha shida zao zinatatuliwa," amesema Mollel. Katika uzinduzi huo Nassari hakuwepo.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema alisema Nassari yupo na wananchi wake na anafanya shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwamo katika sekta ya elimu na afya.

“Kuna kipindi Nasari alikuwa anasoma ila kwa sasa amemaliza na anaendelea na shughuli zake za Kibunge, Amina si msemaji wa wananchi wa Arumeru kazi hiyo ni ya wananchi wa Arumeru na kama alitaka kushitaki angewashitaki kwa Rais, mawaziri waliotajwa kutohudhuria vikao vya Bunge. 

Kwa upande wake mbunge wa Monduli, Julius Kalanga amemuomba Rais kuwasaidia kuondokana na shida ya maji kwa sababu wananchi wake wana hali mbaya.

Amesema hata akipewa nafasi kadhaa za kutoa maombi yake ili aweze kusaidiwa katika utekelezaji mara zote angetaja maji.

"Kama ulivyowakumbuka wenzetu wa Arumeru, tunaomba na sisi utukumbuke katika ufalme wako kwa sababu tuna shida kubwa ya maji," amesema Kalanga.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images