Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Taarifa Kwa Umma Toka Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Kuhusu Kusimamishwa Soko La Jumla La Fedha Za Kigeni (IFEM)

$
0
0
Soko la jumla la fedha za kigeni kati ya benki za biashara (IFEM) ni muhimu katika soko la fedha za kigeni. Hili ni soko la jumla ambalo linaziwezesha benki za biashara na taasisi za fedha kuuza na kununua (kubadilishana) dola za Kimarekani na Shilingi kati yao.

 Soko hili husaidia kuamua kiwango rasmi cha kubadilisha dola dhidi ya shilingi kwa siku husika. Benki Kuu ya Tanzania pia hushiriki kuuza na kununua fedha za kigeni pale ambapo inalazimu. 

Wakati mwingine huingilia soko ili kuhakikisha hakuna mabadiliko makubwa sana ya kiwango cha kubadilisha fedha.
 
Soko la Fedha za Kigeni kati ya mabenki (IFEM) lina kanuni na taratibu zake, ambazo zinaeleza kinagaubaga namna washiriki wote wanavyotakiwa kufanya biashara hiyo. Aidha, washiriki wote katika soko hilo wanatakiwa kutoa taarifa Benki Kuu ya Tanzania kuhusu miamala waliyofanya kwa siku.

 Washiriki wa IFEM ambao wanavunja kanuni na taratibu za soko hilo hufungiwa kushiriki katika kuuza na kununua kwenye soko hilo kwa kipindi maalum. Kufungiwa huko kunahusu tu ushiriki katika soko la fedha za kigeni kati ya mabenki na sio vinginevyo. 

Kwa hiyo, kusimamishwa kwa benki tano za Barclays, Exim Bank, UBA Bank, BancABC na Azania kunahusu ushiriki katika soko la jumla la fedha za kigeni kati ya mabenki tu, yaani IFEM na sio vinginevyo. 

Benki hizo zinaruhusiwa kushiriki katika soko la reja reja la fedha za kigeni, kwa mfano kuuza fedha za kigeni kwa wateja wake au kununua kutoka kwao.

Waziri Mkuu: Serikali Inafanya Mapitio Ya Leseni Za Uchimbaji

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali inafanya mapitio ya leseni zote za uchimbaji wa madini na zile ambazo zitabainika kuwa hazijafanya kazi kwa muda mrefu zitachukuliwa na kisha maeneo hayo hayo yatagawiwa kwa wachimbaji wadogo.
 
Amesema Wizara ya madini imeimarishwa  na sasa inatengeneza fursa kwa ajili ya wachimbaji wadogo ili waweze kunufaika na rasilimali hiyo muhimu inayopatikana katika maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na Mji Mdogo wa Katoro.
 
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Novemba 30, 2018) wakati akizungumza na wananchi katika Mji Mdogo wa Katoro uliopo kwenye Halmashauri ya wilaya ya Geita, akiwa kwenye siku ya mwisho ya ziara yake ya kikazi mkoani Geita.
Waziri Mkuu amewaambia wananchi hao ambao wengi wao ni wachimbaji wadogo kuwa waendelee kuwa na imani na Serikali yao ambayo imedhamiria kuhakikisha wachimbaji hao wanafanya shughuli zao bila ya kubugudhiwa.
 
“Jipangeni kwa kufanya kazi maeneo yapo na Serikali itawapa. Nawashauri mjiunge katika vikundi vitakavyosajiriwa na kutambilika kisheria ili muende kwenye mabenki mbalimbali na kukopa fedha za kununulia mitambo ya kisasa itakayowawezesha kuchimba kwa kutumia teknolojia ya kisasa.”
 
Kadhalika, Waziri Mkuu ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Geita ihakikishe kila kijiji kinakuwa na kisima cha maji ili kuwapunguzia wananchi kutumia muda mwingi kwa kutembea umbali mrefu kwenda kutafuta maji katika maeneo yasiyojulikana.
 
Kuhusu changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama inayowakabili wanachi kwenye Mji Mdogo wa Katoro, Waziri Mkuu amewataka waendelee kuwa na subira kwani Serikali imepanga kuwafikishia maji kutoka ziwa Victoria.

Waziri Mkuu amesemaSerikali kupitia Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani, itahakikisha wananchi katika maeneo yote nchini wanapata huduma ya maji safi na salama karibu na makazi yao.
 
Waziri Mkuu amesema mbali na kuimarisha huduma za maji  kwenye Mji Mdogo wa Katoro, pia Serikali imedhamiria kuboresha miundombinu ya kutolea huduma za afya na kikuwezesha Kituo cha Afya cha Katoro kiweze kuwa na maabara, chumba cha upasuaji, wodi ya mama na mtoto, chumba cha kujifungulia, wodi za wanawake na wanaume.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Madini, Doto Biteko amesema Serikali imeendelea kuwasaidia wachimbaji wadogo nchini wakiwemo na wa Mji Mdogo wa Katoro ili waendelee kufanya shughuli zao bila ya usumbufu wa aina yoyote.

Amesema katika kuhakikisha wachimbaji hao wafanya shughuli za uchimbaji kwa weledi, Serikali imeamua kujenga vituo vya mfano vyenye lengo la kutoa mafunzo kwa wachimbaji wadogo kuhusu namba bora ya uchimbaji kwa kutumia teknolojia ya kisasa

Amesema Mji Mdogo wa Katoro ni miongoni mwa maeneo ambayo Serikali imejenga kituo hicho katika eneo la Lwamgasa. Pia amesema wachimbaji wadogo kwa sasa wanaendelea na shughuli zao katika maeneo mbalimbali kwa uhuru na Amani yakiwemo ya Bingwa, Musasa, Nyamalimbe, Nyarugusu, Lwamgasa.

Naibu Waziri huyo ametaja maeneo mengine nchini ambayo Serikali inaendelea na miradi ya ujenzi wa vituo hivyo kuwa ni pamoja na Lindi, Chunya, Mpanda, Tanga na   Buhemba mkoani Mara.
 
Naye, Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amewahakikishia wakazi wa Mji mdogo wa Katoro na Buselesele kuwa maeneo yao yote ambayo hajaunganishiwa umeme wasiwe na wasiwasi umeme utawaka kabla ya sikukuu ya X-Mass. Amesema mkandarasi tayari ameshafika kwenye maeneo hayo na kuanza  kazi.

Dkt. Kalemani amesemaSerikali maeneo hayo yatasambaziwa umeme kupitia Mradi wa Nishati Vijijini (REA) na wananchi hawatowajibika kulipia gharama za nguzo wala fomu za maombi ya kuunganishiwa umeme kwani tayari gharama hizo zimeshabebwa na Serikali.

“Rais wetu Dkt. John Magufuli anataka kuona nyumba ya kila Mtanzania inapata umeme tena kwa gharama nafuu na ametenga fedha nyingi zitakazotosheleza kusambaza umeme katika vijiji vyote nchini. Gharama za kuunganishiwa umeme huo ni sh. 27,000 tu.”

Awali, Mbunge wa Busanda, Lolencia Bukwimba alimuomba Waziri Mkuu awasaidie kuwatatulia changamoto mbalimbali zinazowakabili zikiwemo za huduma za afya kwa kuwa kituo chilichopo hakitoshelezi mahitaji kwani watu wengi. Ameomba Serikali iwajengee hospitali na kuimarisha huduma za mama na mtoto kwa kuwa kwa mwezi wanazaliwa watoto 700.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Umenunua Flash Mpya Au Memory Card na Inakuandikia iko WRITE PROTECTED Kiasi kwamba Huwez Kuweka Kitu????....Tazama Hapa Ujifunze Jinsi ya Kuiondoa Hiyo Kitu

$
0
0
==>>Jinsi ya kuondoa WRITE-PROTECT kwenye USB FLASHDISK au MEMORY CARD..

Write-Protect ni ulinzi unaowekwa kwenye FlashDisk au Memory Card isiweze kufanyiwa mabadiliko yoyote kama kuongeza Data, Kufuta au Ku-Format. Bahati mbaya sana hiyo kitu wakati mwingine husababishwa na uwepo wa virusi kwenye hiyo flashi yako.
 
Kuna njia nyingi ambazo zinatumika kuondoa writeProtect, nitatoa njia kadhaa  tu  ambazo zinaweza kukusaidia.

1. Njia ya Kwanza: Hakikisha Flash yako au memory Card yako haina virusi. Njia rahis ya kulijua hilo ni kuiscan kwa kutumia Antivirus .Kama hiyo haitatibu tatizo, basi tazama hatua ya pili.

2. Njia ya Pili: Angalia Muundo wa flash yako. Kuna flash zingine zina switch ya kubonyeza kuruhusu au kuzuia Write Ptotection. Tazama hii picha. Kama hii pia  haitatibu tatizo, basi tazama hatua ya tatu.
Njia ya tatu: Tumia Window Registry.
Bongeza Start kwenye compunter yako; kisha andika Regedit.exe. ifungue hiyo kitu

Ikifunguka, nenda moja kwa moja hadi kwenye hii point;
Computer\HKEY_LOCAL_MACHINE\SYSTEM\CurrentControlSet\Control\StorageDevicePolicies

 Ukifika hapo utakuta value yake ni 1; Ibadili iwe 0.  Bonyeza Save kisha  chomoa flash au memory card  yako kisha iwashe upya computer yako yako.

Njia ziko nyingi saaana. Hapo nimeelezea Chache.

<<Ingia Hapa Kuona Njia zote>>

Hadi Hapo Utakuwa umefanikwa kuondoa WriteProtect kwenye FlashDisk yako.

Endelea kuwa nasi kujifunza mautundu mbalimbali kuhusu technology.

Usisahau kuinstall app yetu kwa habari motomoto. Ingia playstore kisha search MPEKUZI utaipata.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Disemba 1

Video Mpya: Shetta ft. Jux & Mr. Blue - Hatufanani

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Shetta anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake mpya uitwao Hatufanani ambao amewashirikisha Jux na Mr. Blue. Itazame hapa.

Video Mpya: Mwasiti Ft Roma – Fall in love

$
0
0
Video Mpya: Mwasiti Ft Roma – Fall in love . Itazame hapo chini

Tazama Hapa Shangwe la Wasafi Festival Iringa Lilivyokuwa Usiku wa Kuamkia Leo Iringa

$
0
0
Usiku wa kuamkia leo kulifanyika tamasha la Wasafi Festival mkoani Iringa likiwa na wasanii wote wa WCB na wengine wakali kibao. 

Tazama mwanzo mwisho mwa show hiyo, video kwa hisani ya Wasafi TV.

Picha kwa hisani ya John Bukuku

Video Mpya: Kings Music (Alikiba X Abdukiba, Cheed, Killy & K-2GA) - TOTO

$
0
0
Kings Music wanakukaribisha kutazama video ya wimbo wao mpya uitwao TOTO. Itazame hapa.

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

$
0
0

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara, Msanii wa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo Dawa na PETE za Bahati zenye uwezo mkubwa wa kuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.

Kutana na Sheikh Jumaa Bilal. Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki. 

Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. Sheikh Jumaa Bilal ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA-  Sheikh Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na Nje ya nchi.

Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nayasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.

Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudishaa alipote, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMBA, GARI..), Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali na UTAJIRI bila masharti na mengine mengi ya Siri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET)

*{لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّهُ بِاللَّغْوِ فِي أيْمَانِكُمْ وَلَٰكِنْ يُؤَاخِذُكُمْ بِمَا عَقَّدْتُمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِمَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ }* ﴿٨٩﴾

✨Wabillahhi Tawfiq Asallam  Alaikum

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa
nambari ya simu

+255 688 745 790
+255 672 861 042
Whatsapp :  0762 252 102

BREAKING: Rais George Bush afariki Dunia

$
0
0
Rais wa zamani wa Marekani George H.W. Bush (Baba yake na Rais Bush aliyemuachia Obama madaraka) amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 94 huko mjini Houston, msemaji wake Jim McGrath amethibitisha kifo chake.

Rais huyo wa zamani wa Marekani aliongoza kwa awamu moja tu akiingia madarakani mwaka 1989 na kuondoka 1993 hivyo kubaki kama Rais pekee aliyeiongoza Marekani kwa awamu moja.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Polisi Yaonya Wizi Mafuta Ujenzi Reli Ya Kisasa...."Tutakaye Mkamata Hatasahau Maisha Yake Yote"

$
0
0
Na Jeshi la Polisi.
Jeshi la Polisi nchini limetangaza kuanza kwa Operesheni kali ya kuwabaini na kuwasaka watu wote wanaojihusisha na wizi wa mafuta katika mradi wa  ujenzi wa reli ya kisasa (SGR)unaoendelea kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Operesheni Maalum za Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi DCP Liberatus Sabas wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wafanyakazi wanaofanya kazi katika mradi wa reli hiyo katika kambi ya ujenzi ya Soga mkoani Pwani  na Ngerengere wakati wa ziara yake katika mradi huo  kufuatia kuwepo kwa vitendo vya wizi wa mafuta.

Sabas amesema Operesheni hiyo haitamwacha salama yeyote atakayekutwa akishiriki na kufanikisha vitendo vya wizi katika mradi huo na kuwataka wafanyakazi hao kuwa wa kwanza kutoa taarifa pindi waonapo viashiria vya wizi katika maeneo yao ili mradi huo uwe salama.

“Polisi tutatumia kila aina ya nguvu zetu kuhakikisha kuwa mradi huu unakuwa salama na tukikamata mwizi wa mafuta katika mradi huu hatasahau maisha yake yote kwa kuwa kuhujumu mradi huu muhimu kwa taifa ni kosa kubwa hasa ukizingatia gharama kubwa ambazo Serikali inatua kufanikisha jambo hili” Alisema Sabas.
 
Katika hatua nyingine DCP Sabas amewaelekeza Makamanda wa Polisi wa mikoa ya Pwani na Morogoro kuweka mikakati kabambe kwa kushirikiana na Kikosi cha Polisi Reli ili kufanya doria za mara kwa mara katika vijiji vinavyozunguka mradi huo kwa kuwa ndipo kulikobainika kuuzwa mafuta ya wizi wa mradi huo.

Rudisha Heshima ya Ndoa Yako.....Pata Tiba Bora ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Wanaume wengi hawawaridhishi wake au wapenzi wao kwa kutokuwa na nguvu za kiume au uume mdogo? 

Kawaida mwanamke huwa anachukua dakika saba 7 adi kumi 10 ili aweze kufika kileleni na wakati wanaume wengi kwa sasa hutumia dakika tatu 3 hadi tano 5 ameshafika kileleni , hapo utagundua kabisa mke au mpenzi wako hujamtendea haki yake. Dr Nyalobi  anakuletea dawa imara na yenye nguvu tatu?

Simpo power; Hutibu matatizo yafatayo;

1.itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-20 kwa tendo la kwanza

 2. itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi mara nne 

3 Huimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa 

4 Hutoa uchovu pale umalizapo kufanya tendo

 Je kwa nini uzidi kuona aibu pale ukutanapo na mpenzi wako kwa sabubu uume wako mdogo na mwembamba? 

Promix; hii ni dawa ya kuongeza uume saizi upendayo.Dawa zetu ni za mitishamba na hazina madhara yoyote na ni tofauti na ulizowai kutumia ata wazee hutumia 

Mkuya; hii ni dawa ya kisukari dozi siku 21 

Mwaru; hii ni dawa ya uzazi hufungua mirija ya uzazi ata kama uzazi umefungwa

Markusi; ni dawa ya presha zipo dwa za korodani kuvimba,, vindonda vya tumbo, kupunguza kitambi, na minyama uzembe 

Fika ofisini kwetu Buguruni Malapa na Mwanza yupo wakala wetu au piga simu 0752348593 -Dokta Nyalobi

CCM Yatoa ONYO Kwa Wakuu wa Mikoa Wanaosaka Ubunge 2020

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally ametoa onyo la mwisho kwa wakuu wa mikoa  nchini Tanzania kuacha kuvuruga chama hicho kwa kufanya kampeni kimyakimya ya kusaka majimbo huku wakitumia rasilimali za Serikali.

Dk Bashiru ametoa onyo hilo jana Ijumaa Novemba 30, 2018 wakati akizungumza na wanachama wa CCM Mkoa wa Geita katika ziara mkoani humo.

Amesema wakuu hao wa mikoa, wameshindwa kutumia nafasi zao kutekeleza majukumu waliyokabidhiwa na Rais John Magufuli na kubaki kujiimarisha wao jambo ambalo hataki kuliona likiendelea.

Amewataka wateule hao wa Rais  kufanya kazi ya heshima na ya kikatiba ya ukuu wa mkoa, badala ya kuanza kuvuruga chama katika maeneo mengine.

“Nitawapeleka kwa aliyewateua, nimwambie awatafutie kazi nyingine waache kuvuruga chama, kwa sababu katika hatua za kutafuta ubunge, wanasababisha chuki na fitina katika majimbo, waache hapakaliki, sasa waache kumdharau aliyewateua.”

“Huwezi kujenga uongozi wa pamoja kama wateule wa rais na viongozi wa kisiasa hawana mtazamo wa pamoja,” amesema Dk Bashiru.

Diwani CCM Atupwa Ndani Saa 48

$
0
0
Diwani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kata ya Okaoni amejikuta akilala rumande kwa saa 48 kwa amri ya Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya baada ya kiongozi huyo kulalamikiwa na wananchi, kuwa amemiliki shamba lenye ukubwa wa heka 500  kwa muda mrefu bila kuliendeleza.

Akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara, uliofanyika Kijiji cha Nkwansira, DC huyo amesema mwekezaji huyo ambaye ni Diwani ameshindwa kuendeleza shamba hilo na kusababishia serikali hasara kwa kutokulipa kodi.

Aidha amesema mwekezaji huyo amekua akiwanyanyasa wafanyakazi katika shamba hilo na kuwanyima mishahara.


"Kuanzia leo nimetengua maamuzi ya kikao cha wajumbe 31 waliopitisha na kummilikisha shamba hili mwekezaji huyu hivyo, simtambui pamoja na shughuli zake zote ndani ya wilaya hii,"amesema Mkuu huyo.


Mkuu huyo amechukua hatua hiyo, baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wananchi wa Kijiji hicho wakimlalamikia mwekezaji huyo kutokana na matumizi mabaya ya shamba hilo ambalo ameshindwa kuliendeleza na badala yake kulibadilisha matumizi.


Pia, amesema amekua akikwepa kodi na hajawahi kuona kumbukumbu zozote za kulipa kodi kwa mwekezaji huyo na kwamba hamtambui.


"Sina kumbukumbu zozote za mwekezaji huyu na simtambui katika wilaya hi,"amesema Sabaya.


"Haiwezekani shamba hili ambalo amepewa na serikali kulima kahawa alitumie kulishia mifugo na kuotesha maharage,"amesema.

Hali ya kukamatwa kwa viongozi kwa upande CCM imekuwa mara chache kutokea kwa baadhi ya viongozi wa chama hicho, lakini imekuwa ni tukio la mara kwa mara kwa baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani ambao mara kwa mara wamekuwa wakituhumiwa kuvunja sheria.

Machi 2018 Mbunge wa Jimbo la Hanang, mkoani Manyara Dkt Mary Nagu (CCM) na Mwenyekiti wa CCM wilaya hiyo walishikiliwa na Jeshi la Polisi wilayani humo kwa amri ya Mkuu wa wilaya.

Magufuli, Kenyatta kufungua kituo cha pamoja cha forodha

$
0
0
Rais wa Tanzania, John Magufuli na Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta wanatarajiwa kufungua Kituo cha Forodha cha Pamoja (OSBP) eneo la Namanga upande Kenya na Tanzania kisha kufuatiwa na sherehe ya uzinduzi huo zitakazofanyika upande wa Tanzania.

Viongozi mbalimbali wakiwemo mawaziri, wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, wabunge na viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wapo upande wa Kenya kwa ajili ya uzinduzi huo unaofanyika leo Jumamosi Desemba 1, 2018.

Lengo la kuanzisha OSBP ni kurahisisha huduma na watu kuchukua muda mfupi kupata huduma za Forodha mpakani.

Kituo cha Forodha cha Namanga ni moja ya vituo vinavyotumika kutoka na kuingia Kenya mkoa wa Arusha, kituo kingine kidogo ni Osmolo kilichopo wilayani Ngorongoro.

Baba Mzazi Awaua Watoto Wake Watatu Akiwemo Wa Miezi 10,kisa Ugomvi Baina Yake Na Mkewe

$
0
0
Mkazi wa Kijiji cha Kunke wilayani Mvomero, Mkoa wa Morogoro, Salehe Masokola (22), amewaua watoto wake watatu kwa kuwanywesha sumu.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na alisema lilitokea Novemba 27, mwaka huu saa sita mchana katika maeneo ya Kibindu, Halmashauri ya Chalinze mkoani Pwani.

Kamanda Nyigesa, alisema mtuhumiwa huyo alikuwa na mgogoro na mke wake na wakati ukitokea watoto walikuwa wakiishi Kunke kwa mama mkwe wake.

Alisema baada ya mgogoro huo, mtuhumiwa huyo alisafiri hadi kwa mkwewe na kuwachukua watoto hao kwa kisingizio cha kutaka kwenda kucheza nao kisha baadaye angewarudisha.

Alisema baada ya maelezo hayo, mtuhumiwa huyo aliwapakia watoto hao katika baiskeli kutoka Kunke hadi Kitongoji cha Ditele Kibindu, Chalinze na aliwanywesha sumu ya twiga amine ambayo ni dawa ya kuulia magugu iliyopoteza maisha yao.

“Masokola alichukua sumu hiyo na kisha kuwachanganyia katika juisi na kuwanywesha watoto hao na kusababisha kupoteza maisha yao papo hapo na katika eneo la tukio tuliokota chupa mbili za juisi zilizotumika, chupa ya dawa na matapishi ambavyo vilichukuliwa kwa uchunguzi zaidi,” alisema.

Alitaja majina ya watoto waliofariki katika tukio hilo kuwa ni Shaila Salehe (6), Nurdin Salehe (4) na Sabrat Salehe aliyekuwa na umri wa miezi 10.

Pia alisema baada ya mtuhumiwa kufanya tukio hilo na yeye aliamua kunywa sumu kwa lengo la kutaka kujiua lakini ilishindikana kwa kuwa aliokolewa na wasamaria wema na kisha kukimbizwa katika Hospitali ya Mission ya Bwagala iliyopo Mvomero kwa matibabu lakini hali yake bado ni mbaya akiwa katika chumba cha wagonjwa mahututi chini ya uangalizi wa Jeshi la Polisi.

CCM Wamvaa Benard Membe Kwa Kumkwamisha Rais Magufuli....Katibu Mkuu Amuita Ofisini Kwake Akajieleze

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally amemtaka mwanachama wa chama hicho, Bernard Membe kufika ofisini kwake ili kutoa ufafanuzi wa tuhuma za kuandaa mpango wa kumkwamisha Rais John Magufuli.

Dk Bashiriu alitoa agizo hilo jana Ijumaa akiwa mkoani Geita kwenda kwa mwanadiplomasia huyo aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nje utawala uliopita na mgombea urais ndani ya CCM mwaka 2015.

Katibu mkuu huyo amesema Membe anatuhumiwa kuandaa mipango hiyo kimyakimya na tangu ameteuliwa kushika wadhifa huo hajawahi kuonana na Membe

“Kati ya wagombea wote wa CCM ni Membe peke yake ambaye sijakutana naye, namkaribisha ofisini, aje anieleze ninayoyasikia ni kweli au si kweli.”

“Kwani haya yanayozungumzwa nyie hamyasikii? nasema peke yangu? Mimi ndiyo katibu mkuu wa CCM aje ajitetee kwamba yeye si kikwazo,” alisema Dk Bashiru

“Iweje watu waseme kwamba wewe (Membe) unafanya vikao vya kutafuta kura za 2020, kwamba unataka kumkomesha Rais Magufuli, halafu unakaa kimya tu, sasa mimi nakualika uje ofisini kama ni mwanachama wa kweli aliyetoa ahadi ya uanachama wa CCM ya kusema kweli daima fitina kwangu mwiko njoo ofisini ueleze,” ameongeza.

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 39

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   
           
“Unaikumbuka sura ya mama yako vizuri?”
Swali la Ethan likanifanya nikae kimya kwa muda huku nikimtazama mama huyu.
“Hapana”
“Kwa nini umeamini kwamba huyu ni mama yako?”
“Ethan, moyoni mwangu, ninahisi kabisa sura ya mama yangu”
“Acha ujinga Ethan, ni watu wangapi weusi ambao una fanana nao, unataka kusema kwamba ni ndugu zako. Hapa umechezewa mchezo wa ajabu. Sasa ni hivi huyu sio mama yako, mumepumbazwa na unapo pelekwa ni kufilisiwa kila kitu chako na utabambikiwa kesi ya mauaji umenielewa”
Maneno ya Ethan kidogo yakanifanya nishikwe na bumbuwazi huku nikimtazama usoni mwake, kwani haya anayo nieleza sijawahi kuyafikiria kabisa kwenye akili yangu.

ENDELEA   
“Nani amepanga kunibambikia kesi?”
“Utajua, ila ukweli ni kwamba huyu si mama yako. Kitu kingine ninacho kihitaji Ethan sasa hivi usifanye maamuzi makubwa pasipo kunishirikisha. Muda mwengine ninakuja kukusaidia kwa sababu wewe ni rafiki yangu, ila nikiama kukaa mbali nawe basi nitakaa na utashindwa kwneye kila jambo. Umenielewa?”
 
Ethan alizungumza kwa msisitizo huku  akinitazama usoni mwangu.
“Nimekuelewa kabisa sinto rudia makosa”
“Yaa napenda kusikia hivyo. Sasa hivi nenda katafute hoteli, lala kesho urudi kambini”
“Sawa”
Ethana akapotea na kuniacha peke yangu katika chumba hichi. Nikamtazama mwana mama huyu kwa macho makali sana, nikatoka ndani humu na nikakutana na Camila mlangoni.
 
“Vipi mume wangu”
“Twende zetu hotelini”
“Hotelini tena?”
“Ndio, nahitaji kwenda kupumzika”
“Ila mbona kama unaonekana kama umekasirika”
“Twende nyumbani”
Nilizungumza kwa msisitozo mkali sana na kumfanya Camila kukubaliana na kile nilicho mueleza. Tukatoka katika eneo hili na walinzi wawili wakatangulia mbele yetu huku walinzi wengine wawili wakiwa nyuma yetu. Wakatufunguli mlango wa gari na  tukaingia ndani kisha taratibu tukaanza kuondoka katika eneo hili.
 
“Ethana mbona sijakuelewa kabisa, kwa nini umetaka tumuache mama pake yake kule hospitalini?”
“Sio mama yangu”
“Samahani, sijakuelewa?”
“Si mama yangu, hujanielewa nini?”
Nilizungumza kwa hasira kidogo na kumfanya Camila kukaa kimya. Camila akawaelekeza walinzi watupeleke katika hoteli nzuri na yenye ulinzi. Tukafika katika hoteli yenye hadthi ya nyota tano, Camila akatumia kadi yake maalumu ya malipo kulipia moja ya chumba cha kisasa kisha tukaelekea ndani.
“Ethan muda ule nilishindwa kuliongelea hili swala kwa urefu. Hembu niambie yule si mama yako kivipi, ikiwa ulisha sema ni mama yako?”
 
“Kuna mchezo ambao unachezwa hapa na wajinga”
“Mchezo gani?”
“Hadi hivi sasa mimi siukumbuki. Nimeweze kumtazama yule mama na kutafuta alama ambazo nilikuwa ninamuona nazo mama yangu, ila sijafanikiwa kuweza kuziona, hivyo wana nidanganya”
Ilibidi nimuongopee Camila.
“Mmmm ni kina nani hao lakini?”
“Si wale jamaa?”
“Jamaa wapi?”
“Mmoja wao ni yule mzee amabaye alinionyesha picha za huyu mwana mama akiniaminisha kwamba ni mama yangu ila ukweli ni kwamba si mama yangu”
 
“Mmmmm”
“Ndio Camila, kuna watu wana mpango wa kunifilisi na kunibamikia makesi ya ajabu. Endapo nitawajua haki ya Mungu nitafanya jambo moja baya snaa kwao”
“Mume wangu usiipe hasira nafasi ya kutawala moyo wako. Tafadhali na nakuomba uwe mvumilivu. Naamini huko mbeleni tutajua ni nani mbaya kwako na nani ni mzuri kwako. Ila tafadhali nakuomba uwe makini na kila mtu wa karibu yako”
 
“Ikiwemo wewe”
Jibu langu likamduwaza Camila, nikavua viatu na kujitupa kitandani. Mwili wangu kwa namna moja ama nyingine umechoka sana, toka asubuhi sikuweza kupata hata muda mzuri wa kupumzika. Camila taratibu akapanda kitandani huku akiwa mnyonge sana.
“Ethan”
“Mmmmm”
“Natambua ya kwamba una huzuni kubwa sana moyoni mwako. Natambua kwamba kitendo nilicho kufanyia hadi  sasa hivi bado hakijafutika akilini mwako. Ila tambua kwamba kila jambo nililo kuwa nimelifanya kwako kwa kipindi cha nyuma hazikuwa akili zangu. Nakuomba unisamehe Ethan”
“Nimekusamehe. Tule tulale”
 
Camilaakaandaa chakula huku akionyesha dhairi kwamba hana furaha kabisa. Tukapata chakula, tukaingia bafuni kwa pamoja, tukaoga kisha tukarudi chumbani na kulala pasipo hata mmoja kudhubutu kunyanyua hisia za mwezake.
    Asubuhi na mapema tukaanza safari ya urudi kambini. Msafara wa gari hizi tatu huku gari letu likiwa katikati, ukazidi kusonga mbele. Meseji ikaingia kwenye simu yangu. Nikaifungua na kukuta ikiwa imetoka kwa mwanasheria.
‘NIPO HOSPITALINI MADAKTARI WANADAI HAUPO MKUU, UPO WAPI?’
Nikaitazama meseji hii kwa muda, kisha nikampigia mwana sheria.
“Ndio mkuu za asubuhi?”
“Salama, sasa ni hivi”
“Ndio”
 
“Hakikisha unasimamia matibabu ya mwana mama huyo hadi anapona. Kisha arudishwe nchini Tanzania akaendelee na maisha yake”
“Ahaa….samahani mkuu, kwa nini umechukua maamuzi hayo?”
“Ni maamuzi yangu binafsi nahitaji akipona. Umpatie dola elfu hamsini, akaanzie maisha Tanzania. Mambo mengine nitakueleza muda ukifika wa kuyazungumza”
“Sawa mkuu nimekuelewa”
“Nashukuru”
Nikakata simu na kuirudisha mfukoni.
“Ethan”
“Mmmm”
“Haya maisha yetu ya kukaa kimya ya kuto kuzungumza, kununiana hakika mimi siyapendi mume wangu”
“Kwani Camila nimekununia?”
 
“Ndio, jana usiku, tumelala kila mtu amegeukia kwake. Leo asubuhi, tumeamka hata busu la hasubuhi hatukupeana, kila mmoja ameamua kufanya anacho taka kwa nini lakini”
Camila alizungumza kwa sauti iliyo jaa malalamiko, nikawatazama walinzi wawili walio kaa siti ya mbele huku mmoja akiwa ni dereva.
“Sijakukasirikia mke wangu, ila ninakasirika huu mchezo unao endelea”
“Sawa, ila tambua kwamba mimi ni mke wako”
“Natambua hilo na nitazidi kulitambua, ila na wewe unatakiwa kunibembeleza ukiniona nikiwa katka hali kama hii”
“Nitakubembeleza vipi ikiwa mwenyewe unanijibu vibaya”
“Sa…..”
 
Hata kabla sijaimalizia kauli yangu, dereva akayumbisha gari letu, huku akilikwepa gari la mbele lililo tutatungulia ambali, tunalishuhudia jinsi lilivyo paishwa angani kwa kulipuliwa na bomu moja kubwa na likatua chini na kusambaratika. Dereva wa gari letu akajitahidi kwa kadri ya uwezo wako kuliweka gari sawa, huku dereva wa gari la nyuma, akitutipa kwa kasi sana na kutangulia mbele yetu. Gari hizi mbili zilizo salia zikasimama, huku eneo hili tulilopo ni eneo la barabara za juu, katikati na chini. Ubaya wa barabara yuliyopo ni katikati, eneo ambalo huwezi kujirusha kwenda sehemu yoyote.
Watu walio valia nguo nyeusi, huku wakiwa na pikipiki kubwa, wakasimama mita kadha kutoka gari hizi zilipo na wakaanza kuzishambulia.
 
Walinzi kama jukumu lao la kutulinda, wakaanza kushuka kwenye magari haya na kujibu mashambulizi. Mimi na Camila miili yetu ina tetemeka kupita maelezo.
“Ohoo Mungu wangu”
Nilizungumza huku nikiendelea kushuhudia jinsi walinzi wanavyo zidi kupungua. Kwa haraka nikafungua mkanda wa siti niliyo kalia na kuahamia siti ya mbele ambayo mlinzi wake ameshuka kupambana na wavamizi hawa.
“Unafanyaje Ethan?”
Camila alizungumza huku akimwagikwa na machozi usoni mwake.
“Kaa hapo hapo”
Nilizungumza, huku nikikaa kwenye siti ya dereva ambaye tayari amepigwa risasi ya kichwa na kufa. Wavamizi wakazidi kutusogelea huku wakizidi kuwapukutisha walinzi wetu. Mlinzi aliye salia naye akapigwa risasi na kutufanya tubaki sisi kama sisi.
 
‘Lazima nifanye jambo hapa’
Nilizungumza kimoyo moyo huku nikifunga mlango ambao alishuka mlinzi. Nikaokota bastola moja ya dereva, kisha nikaufunga mlango kwa nguvu. Risasi zinazo pigwa kwenye kuelekea lilipo gari letu haziingii ndani ya gari kutokana gari hili limetengenezwa kwa mfumo wa kuto kuingiza risasi.
“Ethan unafanya nini mume wangu”
 
“Lala kwenye siti”
Nilizungumza huku nikilirudisha gari hili nyuma, mnikaligeuza kwa kasi sana hadi likakaribia kuanguka. Nikaingiza gia namba moja gari likanza kusonga mbele taratibu, nikazidi kuongeza gia za garihili na kulifanya lizidi kuongezeka mwendo. Kupitia kioo cha pembeni, nikashuhudia kuona wavamizi hawa wenye pikipiki zipatazo saba wakituandama huku kwenye kila pikipiki wakiwa wamepanda wawili wawili. Camila akajaribu kuchungulia ila kwa jinsi kioo cha nyuma kinavyo shabuliwa kwa risasi na kusababisha alama nyingi nyingi, nikajikuta nikimfokea Camila na kumuomba alale chini. Sikuwa na budi ya kukwepa magari ninayo kutana nayo, kwani barabara hii inaruhusu magari ya kwenda upande mmoja tu ambao tulikuwa tunauelekea.
“Ni kina nani Ethan?”
“Sifahamu Camila”
Risasi zikazidi kumiminika na mbaya zaidi watu hawa ni wataalamu wa kuendesha pikipiki, kisha cha kunifanya hata niendeshe gari vipi, wana zidi kunisogelea.
‘Ethan naomba msaada wako’
Nilizungumza kimoyo moyo, ila sikuweza kupata msaada wowote wa Ethan. Nikafika katika barabara ya kugeza ambayo inapita eneo la chini, nikakanyaga breki kidogo, huku nikikunja kona hii kali na kulifanya gari liserereke, na kujibamiza kwenye vymba vikubwa vilivyo jengewa pembezoni mwa barabara hii kisha likaa sawa na tukaondoka katika eneo hili kwa mwendo wa kasi.
“Ethan”
“Mmmm”
“Naomba bastola”
“Bastola ya nini?”
“Kuna hawa wanatusogelea?”
Camila alizungumza huku akijipangusa machozi usoni mwake. Nikatazama kioo cha pembeni yangu nan ikawaona wavamizi wawili wakiwa wanatukaribia kabisa. Nikafunga breki za gafla na kuwafanya mmoja wao kugonga pipiki hii kwa nyuma na kusababisha ajali moja mbaya sana.
 
“Njoo uendeshe”
Nilizungumza huku nikuhamia siti ya nyuma kwa haraka, tukapishana na Camila kama upepo kwani hapa tunapigania maisha yetu kama wapenzi. Akaka kwenye siti ya dereva kisha akaliondoa gari hili kwa kasi sana. Nikaikoki bastola hii vizuri huku nikitazama pikipiki zinazo kuja. Kioo hichi cha nyuma hakika kimejaa alama nyingi za risasi hadi zinasababisha kuto kuweza kuona vizuri nyuma na kimebakisha asilimia ndogo sana kitoboke na kuruhusu risasi kuweza kuingia ndani ya gari hili.
“Ongeza mwendo Camila”   
“Najitahidi”
 
Nikafungua kioo kidogo kisha nikautoa mkono wnagu wa kushoto ulio shika bastola na nikaanza kufyatua risasi kadhaa kuelekea nyuma.
“Ethana una fanya nini!?”
“Nawazui wasitukaribie”
“Ohoo Mungu wangu”
Camila alizungumza huku akijitahidi kufunga breki za gari hili hadi nikarumbishwa na kujipigiza katika siti pembeni yangu. Nikatazama mbele na kushuhudia lori moja kubwa sana likiwa limeziba njia na mbaya sana zaidi tupo kwenye barabara aina ya karabati na eneo hili linawashwa taa masaa ishirini na la sivyo kuna kuwa na giza moja zito sana.
“Ni mtego mpenzi wangu”
 
Nilizungumza huki nikikaa sawa, nikafunga kioo nilicho kuwa nimekifungua kidogo. Juu ya lori hili tukaona watu wawili nao wakiwa wamevalia nguo nyeusi huku mikononi mwao wakiwa wameshika mabomu aina ya bazooka ambayo laiti wakiyafyatulia kwenye gari letu basi, gari litanyanyuliwa kama vile lilivyo nyanyuliwa gari la walinzi wetu lililo kuwa limetangulia mbele.
 
“Camila”
“Mmmm”
“Usifanye kitu chochote hawa watu wanahitaji sisi tukiwa wazima”
“Ethan tuna kufa mume wangu”
“Hatuwezi kufa, niamini mimi na tutoke kwenye gari”
Nilizungumza huku nikishuhudia wavamizi wenye pikipiki wakisimamisha pikipiki zao nyuma yetu. Ubaya watu hawa wamejifunika sura zao jambo la kushindwa kumtambua nani ni nani. Wakatuamrisha kushuka kwenye gari huku mikono yetu ikiwa ipo juu. 

Nikamkonyeza Camila nikimuashiria tufanye kama tulivyo agizwa, kwa haraka Camila akaninyonya lipsi zangu huku machozi yakimwagika usoni mwake, taratibu na mimi machozi yakaanza kunimwagika. Nikazitoa lipsi zangu kwa Camila kisha nikafungua mlango wa gari hili na nikawa wa kwanza kushuka huku watu hawa wakianza kunisogelea kwa ukaribu sana, akafwatia Camila naye akashuka huku akitetemeka sana. Jamaa hawa wakatunyooshea mitutu yao ya bunduki, wakazikoki vizuri tayar kwa kutuua jambo lilizo tufanya tuzidi kujawa na hofu kubwa sana.

==>>ITAENDELEA

Huna Sababu Ya Kuaibika tena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0620510598  / 0743543944
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images