Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Video Mpya: Ben Pol ft. The Mafik - Sio Mbaya

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Ben Pol ameachia video ya wimbo wake mpya uitwao Sio Mbaya ambao amemshirikisha Ben Pol. Itazame hapa.

Video Mpya: Vanessa Mdee ft. Reekado Banks - Bambino

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Vanessa Mdee ameachia video  ya wimbo wake Bambino ambao unapatikana kwenye albamu yake ya Money Mondays akiwa amemshirikisha Reekado Banks kutokea  nchini Nigeria. Itazame hapa.

Wimbo Mpya: AY Ft. King Kiki - SAFARI

$
0
0
Wimbo Mpya wa  AY Ft. King Kiki - SAFARI

Alikiba Atangaza Kumleta Vyonne Chakachaka Katika Tamasha Lake La Kufunga Mwaka

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Alikiba amweka wazi kuwa atafanya show mbili za kufanga mwaka Dar es Salaam.

Moja ya show hizo mbili atakuwa na muimbaji Yvonne Chakachaka kutoka Afrika Kusini. 

Kupitia ukurasa wake wa Instagram  jana Novemba 29 aliandika.

"Ikiwa leo ni siku yangu ya kuzaliwa namshukuru Mungu kwa kuendelea kunibariki katika kila jambo na namshukuru kwa kunipa mashabiki wanaonipa support ya dhati kabisa. Shukrani zangu kwa mashabiki mwaka huu katika #FungaMwakaNaKingKiba zinakuja na show mbili kubwa ndani ya December 2018.

1st Edition ya Funga Mwaka Na King Kiba nitakuwa na Princess of Africa Mama Yvonne_ ChakaChaka itafanyika Serena Hotel Dar es salaam 22. December. 2018.

Halafu 2nd Edition ya Funga Mwaka Na KingKiba itatukutanisha pale Next Door Arena, Dar es Salaam tarehe 29. December.2018."

Nyimbo za Yvonne zilizotamba ni pamoja na I’m Burning Up, Thank You Mister DJ, I Cry for Freedom, Makoti, Motherland, Umqombothi na nyinginezo.

Mhadhiri Aliyesema Chuo Kikuu UDSM Kimekithiri Kwa Rushwa ya Ngono Aitwa Kuhojiwa

$
0
0
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Vicensia Shule ameitwa kwenye kamati ya maadili ya chuo hicho kuhojiwa leo Ijumaa, Novemba 30, 2018 mchana kuhusiana na taarifa yake aliyoitoa kwenye mtandao wa Twitter akimuomba Rais Dkt. John Magufuli kuingilia kati kukithiri kwa rushwa ya ngono chuoni hapo.

Kupitia mtandao wa Twitter, Vicensia aliandika;  "Baba @MagufuliJP umeingia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kufungua maktaba ya kisasa. Rushwa ya ngono imekithiri mno UDSM. Nilitamani nikupokee kwa bango langu ila ulinzi wako umenifanya ninyamae. Nasubiri kusikia toka kwako maana naamini wateule wako ni waadilifu watakwambia ukweli." 

Jana Alhamisi jioni aliandika kwenye Twitter kwamba amepigiwa simu na kutakiwa kufika mbele ya Kamati ya Maadili  UDSM.

"“My good people, a quick update. Leo Alhamisi 29 Nov jioni nimepigiwa simu kuitwa kwenye Kamati ya Maadili siku ya Ijumaa 30 Nov mchana. Nasubiri mwaliko rasmi kwa maandishi. For our dear sexual violence survivors, we are almost there, we will win, big time! #IStandWithDrShule,” 
Aliandika
Ingawa hakueleza ni rushwa ya aina gani iliyokithiri,  lakini katika  baadhi ya vyuo vikuu vingi kumekuwepo na tatizo la wahadhiri  kuwarubuni wanafunzi kwa rushwa ya ngono ili wawafaulishe na pindi wanapogoma hupigwa sup, carryover.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Rudisha Heshima ya Ndoa Yako.....Pata Tiba Bora ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Wanaume wengi hawawaridhishi wake au wapenzi wao kwa kutokuwa na nguvu za kiume au uume mdogo? 

Kawaida mwanamke huwa anachukua dakika saba 7 adi kumi 10 ili aweze kufika kileleni na wakati wanaume wengi kwa sasa hutumia dakika tatu 3 hadi tano 5 ameshafika kileleni , hapo utagundua kabisa mke au mpenzi wako hujamtendea haki yake. Dr Nyalobi  anakuletea dawa imara na yenye nguvu tatu?

Simpo power; Hutibu matatizo yafatayo;

1.itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-20 kwa tendo la kwanza

 2. itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi mara nne 

3 Huimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa 

4 Hutoa uchovu pale umalizapo kufanya tendo

 Je kwa nini uzidi kuona aibu pale ukutanapo na mpenzi wako kwa sabubu uume wako mdogo na mwembamba? 

Promix; hii ni dawa ya kuongeza uume saizi upendayo.Dawa zetu ni za mitishamba na hazina madhara yoyote na ni tofauti na ulizowai kutumia ata wazee hutumia 

Mkuya; hii ni dawa ya kisukari dozi siku 21 

Mwaru; hii ni dawa ya uzazi hufungua mirija ya uzazi ata kama uzazi umefungwa

Markusi; ni dawa ya presha zipo dwa za korodani kuvimba,, vindonda vya tumbo, kupunguza kitambi, na minyama uzembe 

Fika ofisini kwetu Buguruni Malapa na Mwanza yupo wakala wetu au piga simu 0752348593 -Dokta Nyalobi

Waziri Mkuu AMTUMBUA Mhasibu wa Halmashauri

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel amsimamishe kazi aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Mbogwe, Adam Nyoni kwa tuhuma za ubadhilifu wa sh. milioni 19.4 za Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).

Kadhalika Waziri Mkuu ameagiza Mhasibu huyo ambaye awali alikuwa wa Halmashauri ya wilaya ya Mbogwe na sasa amehamishiwa halmashauri ya wilaya ya Nyag’hwale arudishwe Mbogwe na asimamishwe kazi huku shauri lake likifikishwa katika vyombo vya sheria.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana jioni (Alhamisi, Novemba 29, 2018) alipozungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Masumbwe wilayani Mbogwe akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Geita.

Waziri Mkuu aliwataka watumishi wote wa umma wawajibike katika kufanya kazi kwa bidii na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano haitowavumilia watumishi ambao ni wezi, wabadhilifu, wavivu  na haitosita kuwachukulia hatua.

“Serikali hii haitamuhamisha wala kumuundia tume mtumishi atakayetafuna fedha za umma, ukiharibu tunamalizana hapo hapo. Naagiza mtumishi huyo aliyehamishiwa Nyang’hwale arudishwe hapa kwa kuwa kabla ya kuhamishwa kulikuwa na upotevu wa sh. milioni 19.4.”

Alisema watumishi wa umma wanapaswa wawatumikie wananchi bila ya ubaguzi wowote pamoja na kuacha kufanya kazi kwa mazoea. “Lazima mtambue kwamba msimamo wa Serikali ni kuwahudumia wananchi bila ya ubaguzi wa kidini, kiitikadi na kipato.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alimuagiza Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe, Martha Mkupasi kwenda katika ngoma za usiku za chagulaga na kuwachukulia hatua wanaume wote wanaowachagua wanafunzi wa kike kwa kuwa wanawaharibia maisha.

Alisema lazima wananchi washirikiane na Serikali katika kuwalinda wanafunzi wa kike ili wasipate ujauzito na kukatisha masomo yao kwa sababu kitendo cha kupata ujauzito kinawafanya wakatishe masomo yao jambo ambalo linakwamisha kufikia lengo lao kielimu.

Kadhalika, Waziri Mkuu alipiga marufuku kwa wanafunzi hao wa kike kuhudhuria kwenye ngoma hiyo ya usiku na badala yake watumie muda mwingi kujishughulisha na masuala ya masomo ili waweze kutimiza ndoto zao. “Wanafunzi wa kike msikubali kushawishika."

Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi wa wilayani Mbogwe kuhakikisha watoto wenye umri wa kuanzia miaka minne kuwapeleka shule ili waanze darasa la awali na kwamba hawatakiwi kutoa mchango kwa kuwa Elimumsingi inatolewa bure nchini.

Hata hivyo, Waziri Mkuu aliipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwekwa kutekeleza kwa vitendo agizo la Serikali la kujenga Zahanati katika kila kijiji kwa kuwa wilaya hiyo inaendelea na shughuli za ujenzi wa Zahanati katika vijiji 82 kati ya vijiji 86.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Serikali Yaagiza Doria Za Mara Kwa Mara Maeneo Ya Mipakani

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameziagiza Kamati za Ulinzi na Usalama kwenye maeneo ya mipakani kuendesha doria za mara kwa mara ili kuwabaini na kuwachukulia hatua watu wote wanaoingia nchini kinyemela bila ya kufuata taratibu.

“Suala la ulinzi na usalama ni muhimu, hivyo Idara ya Uhamiaji kwa kushirikiana na viongozi wengine wahakikishe wanasimamia sheria na kuimarisha ulinzi hususan maeneo ya mipakani ili kudhibiti watu mbalimbali wanaoingia nchini kinyemela.”

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana jioni (Alhamisi, Novemba 29, 2018) alipozungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa Stendi ya Ushirombo wilayani Bukombe akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Geita.

Waziri Mkuu alisema ni muhimu kwa viongozi wa maeneo ya kuwa makini katika kufanya ukaguzi kwenye maeneo hayo ili wazuie uingiaji wa wageni kiholela kwa sababu baadhi yao si watu wema. “Serikali haizuii wageni kuingia nchini ila wafuate taratibu zilizowekwa.

Kadhalika, Waziri Mkuu aliwaagiza wakuu wa wilaya akiwemo na mkuu wa wilaya ya Bukombe, Said Nkumba watangaze fursa za uwekezaji zilizopo kwenye maeneo yao kwa lengo la kuvutia wawekezaji wa sekta mbalimbali ikiwemo ya viwanda ili kukuza uchumi.

Alisema viongozi hao wawasiliane na Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na kuwaeleza fursa za uwekezaji zinazopatikana katika maeneo yao, ambapo alitolea mfano wilaya ya Bukombe ambayo ina mifugo mingi, watafute wawekezaji wa kujenga kiwanda cha nyama.

Pia, Waziri Mkuu aliwashauri wafugaji nchini kufuga kisasa na kujiongezea tija, badala ya kutembeza mifugo kwa umbali mrefu wafuge kulingana na ukubwa wa maeneo yao ya malisho na marufuku kwenda kulisha mifugo kwenye mashamba ya wakulima.

Mbali na kupiga marufuku wananchi kulisha mifugo kwenye mashamba ya wakulima, pia Waziri Mkuu amezuia wafugaji kuingiza mifugo katika mapori ya akiba kwa kuwa mapori hayo kwa sasa yapo katika hatua za mwisho kutangazwa kuwa mbuga za wanyama.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu: Tutaboresha Maslahi Ya Watumishi Wote Wa Umma

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kuboresha maslahi ya watumishi wote wa umma wakiwemo wa kada ya afya kupitia Bodi ya Mishahara na Motisha baada ya kukamilisha uhakiki wa taarifa za kiutumishi.

Amesema kukamilika kwa uhakiki huo wa taarifa za kiutumishi kwa watumishi wa umma kutaiwezesha Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli kupanga upya mishahara na motisha kwa watumishi.

Waziri Mkuu alitoa taarifa hiyo jana jioni (Alhamisi, Novemba 29, 2018) alipozungumza na watumishi wa Kituo cha Afya cha Ushirombo wilayani Bukombe baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi mradi wa uboreshaji miundombinu wa kituo hicho uliogharimu sh. milioni 500.

Alisema Serikali inaendelea kushughulikia maslahi ya watumishi, hivyo aliwataka waendelee kufanya kazi ya kuwahudumia wananchi bila ya ubaguzi wa aina yoyote. “Tunataka mwananchi akifika kwenye maeneo ya kutolea huduma apokelewe, asikilizwe na ahudumiwe.”

Kadhalika, Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuupongeza uongozi wa halmashauri ya wilaya ya Bukombe kwa kutekeleza kwa vitendo agizo la Serikali la kujenga Zahanati katika kila kijiji kwa kuwa wilaya hiyo imebakisha vijiji 2 kati ya 52 kumalizia ujenzi huo.

Waziri Mkuu alisema kwa sasa wananchi wa Ushirombo hawana sababu ya kusafiri umbali mrefu hadi Geita mjini au wilayani Kahama kwa ajili ya kufuata huduma za afya kwa kuwa huduma zote zitakuwa zikipatikana kituoni hapo.

Alizitaja huduma ambazo zitakuwa zikipatikana kwenye Kituo cha Afya cha Ushirombo kuwa ni pamoja na za mama na mtoto, huduma za upasuaji wa aina zote mdogo na mkubwa, maabara, chumba cha kuhifadhia maiti.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Bukombe, Dionis Myinga alisema ukarabati wa Kituo cha Afya cha Ushirombo ulianza Juni 22, mwaka huu na unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka huu.

Alisema lengo la mradi huo ni kukiwezesha Kituo cha Afya cha Ushirombo kutoa huduma bora za upasuaji wa dharura kwa akinamama wajawazito pindi wapatapo matatizo yatokanayo na uzazi. Majengo yote ya kipaumbele yamekamilika kwa asilimia 99.

“Mradi huu ambao tunaujenga kwa kutumia force account, pamoja na lengo la kutatua matatizo yatokanayo na uzazi kwa akinamama mradi huu utakapokamilika, Kituo cha Afya cha Ushirombo kitaweza kuhudumia watu wapatao 54,271.”

Mkurugenzi huyo alisema mradi wa ukarabati wa kituo hicho cha afya unakadiriwa kutumia sh. milioni 436.933 hadi utakapokamilika na sh. milioni 63.066 zilizosalia kwenye ukarabati huo zitatumika kujenga njia za kuunganisha wodi na kukarabati majengo ya zamani.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Wafuasi wa CHADEMA, CUF Watimuliwa Mahakamani Wakifuatilia Kesi ya Mbowe

$
0
0
Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Chama cha Wananchi (Cuf) wametimuliwa na polisi katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, baada ya kuanzisha kwa vurugu.

Tukio hilo limetokea mapema leo asubuhi Ijumaa Novemba 30, baada ya Jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi ndani na nje ya mahakama hiyo ili kuwadhibiti wafuasi hao kutokana na kesi kubwa mbili zinazotarajiwa kutolewa uamuzi leo.

Kesi hizo ni pamoja na ile iliyofunguliwa na viongozi wa Cuf, wakitaka kujua Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahimu Lipumba, ni mwenyekiti halali wa chama hicho au la.

Kesi ya pili ile ya maombi ya dhamana ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko ambayo inatarajiwa kutolewa uamuzi kuhusu pingamizi lililowasilishwa na upande wa  Jamhuri la kutaka rufaa itupwe ya kupinga kufutiwa dhamana kwa washtakiwa hao litupwe kutokana kutofuata vifungu vya kisheria.

Breaking News: Mahakama Kuu Yatupilia Mbali Mapingamizi Ya Serikali....Rufaa Ya Mbowe Kusikilizwa Saa Nane Mchana

$
0
0
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetupilia mbali pingamizi za serikali za kuzuia rufaa ya dhamana iliyokatwa na Mwenyekiti wa Chadema Mh.Freeman Mbowe na Esther Matiko isisikilizwe na hivyo imeamua kusikiliza rufaa hiyo leo saa nane mchana.

Mbowe, ambaye pia ni Mbunge wa Hai, sawa na Matiko wa Tarime Mjini, wamekata rufaa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam chini ya hati ya dharura wakipinga uamuzi wa Mahakama ya Kisutu kuwafutia dhamana katika kesi ya jinai inayowakabili mahakamani hapo.

Walifutiwa dhamana na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, anayesikiliza kesi hiyo Novemba 23 kutokana na maombi ya upande wa mashtaka yaliyodai wameshindwa kuhudhuria mahakamani wakati kesi yao ilipopangwa kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali bila sababu za msingi.

Endelea Kuwa nasi

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, TFF limesitisha michezo yote iliyopangwa kuchezwa usiku

Maofisa Sita Wizara Ya Ardhi Wasimamishwa Kazi

Mambo Bado Magumu kwa Mbowe.....Serikali Yawasilisha Kusudio la Kukata Rufaa

$
0
0
Hukumu juu ya maamuzi ya kupewa au kutopewa dhamana kwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Freeman Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko imeonekana kuwa ngumu baada ya upande wa Jamhuri kuwasilisha ombi la kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa awali wa Mahakama Kuu.

Jamhuri imetangaza nia hiyo  baada ya Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es salaam, kutupilia mbali baadhi ya hoja zao kwa kile alichokieleza kukosa msingi wa kisheria.

Upande wa Jamhuri uliwasilisha maombi ya kutosikilizwa kwa rufaa hiyo dhidi ya washtakiwa Mbowe na Matiko kwa kile walichokisema kuwa baadhi ya vipengele vya kisheria ambavyo vilitumika vinainyima sifa mahakama hiyo kusikiliza rufaa.

Kwa upande wa mawakili wa watuhumiwa Mbowe na Matiko walieleza kupinga taarifa hiyo ya rufaa kwa kile walichokidai kuwa upande wa jamhuri haujafuata baadhi ya taratibu za  mahakama.

Mbowe na Matiko ni miongoni mwa viongozi saba, ambao wanakabiliwa na kesi ya msingi ya kusababisha kifo cha aliyekuwa mwanafunzi Chuo Cha Usafirishaji cha NIT,  Akwilina Akwilini pamoja na makosa mengine ya uchochezi.

Mbali na viongozi hao, viongozi wengine wanaoshtakiwa kwenye kesi hiyo ya msingi ni Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt Vicent Mashinji, Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa, Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Zanzibar, Salum Mwalimu, pamoja na Mbunge wa Kibamba John Mnyika.

Jaji kaomba Nusu Saa Kuamua Hatima ya Dhamana ya Freeman Mbowe

$
0
0
Hatima ya usikilizwaji wa rufaa ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko iwapo itaendelea kusikilizwa na Mahakama Kuu au la itajulikana baada ya muda mfupi ujao.

Hatima hiyo itajulikana baada ya Jaji Sam Rumanyima kutoa uamuzi wa maombi yaliyotolewa na upande wa mashtaka ukiiomba Mahakama hiyo isimamishe usikilizwaji wa rufaa hiyo kwa madai kuwa haina mamlaka hayo.

Jaji Rumanyika ameomba kutumia muda wa nusu saa kuandika uamuzi huo baada ya kusikiliza hoja za mawakili wa pande zote mbili kuhusiana na uwepo rufaa ya Serikali katika Mahakama ya Rufani kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu kukubali kuendelea na usikilizwaji.

Breaking News: Freeman Mbowe, Ester Matiko Warudishwa Gereani

$
0
0
Wabunge Freeman Mbowe na Ester  Matiko warudishwa gerezani kusubiria uamuzi wa mahakama ya rufaa kuhusu dhamana zao.

Washtakiwa hao wamerudishwa mahabusu jioni hii baada ya mahakama kuu kusitisha kuendelea kusikiliza rufaa ya dhamana za wabunge hao.

Serikali Yawatoa Wasiwasi Wafanyabiashara Wa Uganda

$
0
0
Serikali imewahakikishia wafanyabiashara wa mafuta kutoka uganda kuwa imejipanga kutatua  changamoto zote zilizopo kwenye usafirishaji ili kupunguza gharama za uchukuzi  kati ya Tanzania na nchi hiyo.

Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Atashasta Nditiye, amesema hayo wakati wa kikao maalum kilichowakutanisha wafanyabiashara wa Mafuta wa Uganda na taasisi za Uchukuzi za Tanzania na kusema kuwa Serikali inatekeleza hayo kwa kuboresha miundombinu ili kuvutia wafanyabiashara wengi zaidi

“Niwahakikishie kuwa changamoto zote zilizoainishwa baada ya majumuisho ya ziara yenu ya siku 5 nchini tutazifanyia kazi”, amesema Naibu Waziri  Nditiye.

Aidha, Naibu Waziri Nditiye ameongeza kuwa Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ikiwemo upanuzi wa bandari,ukarabati wa reli na ukarabati wa meli ili mizigo inayokwenda Uganda kupitia bandari ya Dar es Salaam ifike kwa wakati.

Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Kampuni ya Meli, Eric Hamis amesema mpaka sasa tayari wamesafirisha zaidi ya tani elfu kumi na tano za Uganda kwa kutumia meli ya MV Umoja na kusema kuwa wamejipanga kusafirisha mzigo mkubwa zaidi kabla ya mwaka wa fedha kuisha.

Sisi kama Kampuni ya meli tuliifanyia ukarabati meli ya MV Umoja na imekuwa ikisafirisha mzigo wa Uganda na niwahakikishie kuwa kupitia ziara hii na jitihada nyingine tunazozifanya tutapata wafanyabishara wengine ambao watasafirisha mizigo yao kwa kutumia meli hii” amesema Hamis.

Kwa upande wake Mchumi Mwandamizi kutoka Wizara ya Ujenzi ya Uganda,  Gerald Akini,  amemwahidi Naibu Waziri Mhandisi Nditiye kuwa yale ya kisera yanayohusu Uganda atayafikisha katika ngazi husika ili yafanyiwe kazi ili kuimarisha ushirikiano uliopo kibiashara.

Bw Gerald ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa utayari wake wa kuwapokea wafanyabiashara na kuweka mazingira mazuri ili watumie bandari ya Dar es Salaam.

Aidha, ameipongeza Serikali kwa kuendelea kuboresha miundombinu ikiwemo kupunguza vituo vya mizani,ujenzi wa reli ya kisasa,uboreshaji wa bandari na kuahidi kuendeleza ushirikiano kwa kushawishi wafanyabiashara wengi zaidi kutumia bandari ya Dar es salaam.

Wafanyabiashara wa mafuta kutoka nchini Uganda wamefanya ziara ya siku 5 nchini ambapo wametembelea bandari ya Dar es salaam, Tanga,Mwanza pamoja na kukagua miundombinu ya reli na meli za kampuni ya meli na kuridhishwa na hatua zinazochukuliwa na Tanzania kuimarisha biashara baina ya nchi hizo.

Waziri Mahiga: Wadau wa maendeleo wana imani na Tanzania

$
0
0
 Ziara zinazofanywa nchini na viongozi mbalimbali kutoka nje ya nchi ni ishara ya wazi kuwa nchi rafiki na wadau wengine wa maendeleo wana imani kubwa na Tanzania.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga baada ya kufanya mazungumzo na viongozi wa nchi nne kutoka Ulaya na Amerika Kusini kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere tarehe 29 Novemba 2018.

Viongozi hao ni Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup; Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Yuri Pimentel Moura; Katibu Mkuu anayesimamia Maendeleo na Ushirikiano kwenye Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, Bi. Trine Rask Thygesen; Mjumbe kutoka China, Balozi Zhui Yuxiao, anayesimamia masuala ya Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) na Mkurugenzi wa Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Uswisi, Balozi Anne Lugou-Moulin ambaye alikutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro.

Wakati wa mazungumzo yake na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Dkt. Mahiga alieleza kuwa, licha ya Tanzania na Norway kuwa na uhusiano mzuri na imara wa kidiplomasia, kuna umuhimu wa kuongeza nguvu katika ushirikiano wa kiuchumi kwa manufaa ya nchi zote mbili. Dkt. Mahiga alitoa wito kwa Serikali ya Norway kushawishi sekta binafsi ya nchi hiyo kuchangamkia fursa lukuki za uwekezaji zinazopatikana nchini.

Alisema kuna kampuni 33 za kutoka Norway nchini Tanzania ikiwemo kampuni ya Equinor ambayo ipo katika mchakato wa kuwekeza katika gesi asilia mkoani Lindi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kusafirisha nje. “Uwekezaji huu ni mkubwa na unahitaji ardhi kubwa ambayo ishapatikana na utakapokamilika utatoa ajira za maelfu kwa vijana wa Kitanzania”. Balozi Mahiga alisema.

Balozi Mahiga aliishukuru Norway kwa misaada ya kimaendeleo inayoipatia Tanzania ikiwemo ya kusaidia kufanya mabadiliko ya kimfumo katika masuala ya ukusanyaji kodi, miundombinu, nishati ya umeme na mbolea.

Aidha, Norway inafadhili mafunzo ya vitendo kwa wahandisi wa kike ili waweze kuwa na sifa ya kusajiliwa na Bodi ya Usajili ya Wahandisi. Kutokana na ufadhili huo ambao kwa miaka minane iliyopita umegharimu Shilingi bilioni 4.2 na kuwezesha wahandisi wa kike 504 kusajiliwa na kupunguza pengo kubwa la uwiano la wahandisi wa kike na kiume ambapo uwiano wao kabla ya ufadhili huo ulikuwa ni 1:27 na sasa ni 1:10.

Waziri huyo kutoka Norway alimdokeza Dkt. Mahiga kuwa Mfalme wa Norway ana panga kufanya ziara nchini Tanzania mwaka 2019.

Wakati wa mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela, wawili hao walisisitiza umuhimu wa Tanzania na Venezuela kubadilishana uzoefu katika sekta ya mafuta na gesi ambapo Venezuela imepiga hatua na sekta ya madini ambapo Venezuela ingependa kujifunza zaidi kutoka Tanzania. Ili kurahisisha utekelezaji wa mazaungumzo yao, Mhe. Naibu Waziri amewasilisha barua rasmi ya maombi ya nchi yake ya kufungua ofisi ya ubalozi nchini jambo ambalo Balozi Mahiga aliahidi litafanyiwa kazi haraka iwezekanavyo.

Katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Dernmark, Waziri Mahiga alijulisha kuwa Kiongozi huyo alitaka kupata ufafanuzi wa hali ya mambo yanavyoendelea nchini badala ya kutegemea taarifa za vyombo vya habari ambazo wakati mwingine zinakuwa sio sahihi.

Baada ya ufafanuzi ambao ulimridhisha na hivyo kuihakikishia Serikali ya Tanzania kuwa Denmark haijasitisha misaada kwa Tanzania. Ilielezwa kuwa misaada ambayo inakwenda moja kwa moja katika sekta ambayo ina thamani ya Dola za Marekani milioni 550 inaendelea kutolewa. Msaada unaokwenda kwenye bajeti ya Serikali moja kwa moja wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 10 ambao mchakato wake umekamilika,  lakini kwa kawaida huwa unatolewa kwa pamoja na wadau wengine (Umoja wa Ulaya na Sweden) wanasubiriwa wakamilishe michakato yao ya ndani ili uweze kutolewa. Msaada huo kwa upande wa Sweden ni Dola milioni 9 na Umoja wa Ulaya ni Dola milioni 37.

Kuhusu mazungumzo na Balozi Zhui Yuxiao ambayo yalihusu mikakati ya utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa FOCAC uliofanyika Beijing mwei Agosti 2018. Balozi Zhui alishauri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki iteue mtumishi mmoja mwandamizi ili awe mratibu wa masuala ya FOCAC pamoja na kuteua kamati ya utekelezaji yenye wajumbe wa sekta mbali mbali lakini iratibiwe na Wizara ya Mambo ya Nje.

Kwa upande wa mazungumzo kati ya Dkt. Ndumbaro na Katibu Mkuu wa Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Uswisi, Balozi Anne Lugou-Moulin, wawili hao waliridhika na uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi zao ambao umedumu kwa miaka 98 tokea mwaka 1920.
 
Dkt. Ndumbaro alihimiza wawekezaji wengi zaidi kutoka Uswisi waje nchini kuwekeza kwa kuwa mazingira ya biashara yameboreshwa kwa kiasi kikubwa. Alisema hakuna mabadiliko ya sheria za uwekezaji isipokuwa mabadiliko ambayo yamelenga kuboresha zaidi yamefanyika katika sheria ya madini. Hivyo, aliwataka wawekezaji wasiwe na hofu yeyote kuhusu Tanzania.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar Es Salaam, Tanzania
Tarehe 30 Novemba 2018

Serikali Yajadili Uwekezaji Bora Zaidi Wa Misri Katika Sekta Ya Mifugo

$
0
0
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina ameongoza kikao cha wakuu wa idara zilizo chini ya wizara yake pamoja na wadau wengine wa sekta ya mifugo, kujadili namna bora zaidi ya serikali ya Tanzania inavyoweza kunufaika na uwekezaji katika sekta ya mifugo kutokana na nia ya serikali ya Misri kutaka kuwekeza katika sekta hiyo iliyooneshwa katika siku chache zilizopita.

Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika ofisi ndogo za wizara hiyo Jijini Dar es Salaam, Mhe. Waziri Mpina amewaambia wajumbe wa kikao hicho wakiwemo wawakilishi kutoka SUMA JKT, Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) na Dawati la Sekta Binafsi, kuwa na mikakati ambayo itasaidia uwekezaji huo uwe na tija kwa taifa.

Aidha Waziri Mpina amesema serikali inahitaji wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi, lakini ni muhimu yakaandaliwa mazingira bora zaidi ili uwekezaji huo uwe endelevu na kuleta tija kwa taifa na wananchi kwa ujumla.

Baadhi ya wajumbe waliohudhuria kikao hicho, wamemshauri Mhe. Waziri Mpina masuala mbalimbali yakiwemo ya kitaalam pamoja na vifungu vya kisheria ili mikataba itakapoandaliwa na kusainiwa kati ya serikali ya Tanzania na Misri iweze kuleta faida kwa nchi hizo mbili.

Hivi karibuni Kaimu Balozi wa Misri nchini Bibi. Neville El-Saeed na Mkuu wa kitengo cha Uchumi katika ubalozi huo Bw. Mohamed Ibrahim, walifika katika ofisi ndogo za wizara hiyo katika siku tofauti tofauti ambapo walipata fursa ya kuzungumza na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina kuhusu uwekezaji huo.

Maafisa hao pia walikutana na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel na kumkabidhi andiko la awali la nia ya serikali ya nchi hiyo kutaka kuwekeza katika sekta ya mifugo na kufungua fursa zaidi zilizopo katika sekta hiyo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images