Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

THRDC wamtaka Rais Magufuli ateue viongozi wa Tume ya Haki za Binadamu

$
0
0
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu nchini (THRDC), umemwandikia Rais John Magufuli waraka maalumu wa kumtaka kuteua viongozi katika ngazi mbalimbali ikiwamo Mwenyekiti, makamishna na makamishna wasaidizi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ambao wamemaliza muda wao januari mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano Novemba 28, Mratibu wa kitaifa wa THRDC, Onesmo Olengurumwa amesema tangu Januari mwaka huu hadi sasa viongozi hao muhimu hawako ofisini.

“Kwa mujibu wa Katiba ya nchi 1977 na sheria ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ya mwaka 2001, uwepo wa tume hiyo unajumlisha muundo wa uongozi ambao kwa sasa wamemaliza muda wake na ofisi kubaki bila watendaji hao,” amesema.

Pamoja na mambo mengine, Wakili wa Mtandao huo, Deogratius Bwire, alizungumzia hali ya kifedha kuwa si nzuri kutokana na matumizi ya tume hiyo.

“Katika bajeti ya mwaka 2016/17 ilikuwa ni Sh 1.17, kiasi ambacho ni kidogo ikilinganishwa na miaka iliyopita na mahitaji ya tume hiyo,” alisema Bwire.

Huna Sababu Ya Kuaibika tena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Serikali Yasema Zuio la wanafunzi wanaopata mimba Kuendelea na Masomo halihusu shule binafsi

$
0
0
Serikali imetoa ufafanuzi kuhusu hatua ya kuzuia wanafunzi wanaopata mimba kurejea shule kuwa suala hilo halizihusu shule binafsi.

Ufafanuzi huo umetolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwenda kwa Chama cha Wamiliki wa Shule na Vyuo Binafsi Tanzania (Tamongsco) ukiwataka kutofuata maelekezo ya awali yaliyotolewa Agosti Mosi, 2017.

Katika barua ambayo imeandikwa kwa Tamongsco na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na kuthibitishwa na katibu mkuu wa wizara hiyo, Dk Leonard Akwilapo imezitaka shule binafsi kuwaruhusu wanafunzi kuendelea na masomo kwani zuio hilo haliwahusu wao.

“Ni kweli tumewaandikia barua Tamongsco kwani ufafanuzi huo unatokana na maelekezo ya awali kuwachanganya na yalikuwa hayawahusu wao bali shule za umma,” alisema Dk Akwilapo.

Katibu mkuu huyo alisema badala ya maelekezo hayo kuyatuma kwa shule binafsi anuani zikakosewa na kutumwa kwa shule binafsi jambo ambalo limewafanya kuwatumia barua ya ufafanuzi kuwa zuio haliwahusu na wanaweza kuendelea na wanafunzi wanaopata ujauzito na hata Rais Magufuli alisema marufuku hiyo ni kwa shule za umma.

Alipoulizwa kama mwanafunzi atakayekuwa amepata ujauzito katika shule za umma ataruhusiwa kuendelea akihamishiwa shule binafsi, Dk Akwilapo alisema, “Ataruhusiwa na atakwenda kujiunga huko kwa kufuata taratibu ikiwamo kufanyishwa mitihani.”

Julai 22, 2017, Rais Magufuli akiwa Msata wilayani Bagamoyo mkoani Pwani alisema katika muda wote atakaokuwa madarakani hakuna mwanafunzi wa shule ya msingi na sekondari atakayepata ujauzito atakayeruhusiwa kuendelea na masomo katika shule za umma.

“Nataka niwaambie, katika utawala wangu hakuna mwanafunzi mwenye mimba atakayerudi shuleni. Yapo mambo mengi ya kufanya, wanaweza kwenda Veta au wakajifunza kushona, maisha yakaendelea,” alisema Rais Magufuli

Credit: Mwananchi

Viongozi, wanachama na wafuasi wa CHADEMA Wafurika Mahakamani Kusikiliza Rufaa ya Freeman Mbowe

$
0
0
Viongozi, wanachama na wafuasi wa Chadema na vyama rafiki wamefurika katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kusikiliza rufaa ya dhamana ya Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini (Chadema), Ester Matiko.

Mbowe ambaye ni Mbunge wa Hai na Matiko ambaye pia mweka hazina wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) wamekata rufaa Mahakama Kuu kupinga uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwafutia dhamana katika kesi ya jinai inayowakabili mahakamani hapo baada ya kupatikana na kosa la kukiuka masharti ya dhamana waliyopewa awali.

Walifutiwa dhamana hiyo Novemba 23 na Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kufuatia maombi ya upande wa mashtaka kwa madai ya kukiuka masharti ya dhamana kwa kutokufika mahakamani tarehe ambazo kesi yao ilipangwa kwa ajili ya usikilizwaji wa awali.
 
Mbowe na Matiko ambao wako mahabusu katika Gereza la Segerea walifikishwa mahakamani hapa mapema leo asubuhi 

Miongoni mwa viongozi wa vyama vya siasa waliofika mahakamani hapo ni Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vicent Mashinji, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema-Bara, John Mnyika, wabunge na madiwani.

Tazama Hapa Kilichoamuriwa Leo Mahakamani Kuhusu Rufaa ya Mbowe na Matiko

$
0
0
Jaji Sam Rumanyika anayesikiliza kesi ya pingamizi la rufaa ya kupinga uamuzi wa kufutiwa dhamana ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko, amepiga simu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akiamuru mwenendo wa kesi na uamuzi uliowafutia dhamana washtakiwa hao umfikie ofisini kwake haraka.

Jaji Rumanyika alifanya hivyo leo Jumatano Novemba 28, baada ya rufaa kukwama kusikilizwa kwa sababu nyaraka hizo hazikuambatanishwa na jalada lililomfikia.

Alipiga simu  kwa karani wa mahakama baada ya kukosa namba ya Hakimu

Baada ya simu kupokelewa Jaji Rumanyika alijitambulisha kwa majina huku sauti ya upande wa pili (sauti ya karani Comas) ilisikika akiitikia kumfahamu.

Jaji Rumanyika alimuuliza kama anaifahamu kesi Namba 112/2018 naye akajibu anaifahamu, kisha akauliza kwanini nyaraka zilizomfikia hazijakamilika, hakuna uamuzi wa mahakama na mwenendo wa kesi.

Karani alijibu kwamba bado hazijamaliziwa kuchapwa na Jaji Rumanyika alitaka ampelekee hivyo hivyo ziwe zimechapwa au zimeandikwa kwa mkono.

“Nenda unileee nakusubiri ofisini kwangu chumba namba 16… Nasubiri, “Jaji Rumanyika ilikata simu na kuzitaka pande zote mbili kusubiri hadi saa saba wajiridhishe kupata nyaraka hizo.

Rufaa hiyo itaanza kusikilizwa kesho Alhamisi asubuhi. Washtakiwa walirudishwa rumande.

Kubenea Apangua Kauli ya Makonda

$
0
0
Mbunge wa Jimbo la Ubungo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA), Saed Kubenea amefunguka juu ya tuhuma za Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda kumchonganisha na wananchi wake kwa Rais Magufuli.

Kubenea amesema kuwa kabla ya kutoa kauli ile mbele ya Rais alipaswa kumtafuta ili kujua ni kwanini hajafika katika hafla ile ya uzinduzi wa Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM).

Kubenea amesema kuwa amesikitishwa na kitendo cha kiongozi huyo kuzungumza bila kuwa na taarifa sahihi kuhusiana na sababu za kutofika kwenye uzinduzi huo.

"Imekuwa kawaida yake kuchonganisha watu bila kuwa na sababu za msingi, kama alifahamu ujio wa Rais pale alishindwa nini kunitafuta kabla?, Unajua unaweza sema neno juu ya mtu kumbe ana matatizo yaliyosababisha asifike", amesema Kubenea.

Kubenea amesema kuwa kilichomkwamisha kufika katika uzinduzi huo alikuwa katika kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Ubungo na hakufahamu kama itakuwa ni hafla ya muda mfupi na jiografia ya halmashauri iko mbali.

Jana katika hafla ya uzinduzi wa maktaba mpya katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM), Makonda alisema kuwa ameshangazwa na kutokuwepo kwa Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Saed Kubenea mahala ambapo Chuo kinapatikana katika Jimbo lake, pamoja na majirani zake ambao ni Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na Mbunge wa Kibamba, John Mnyika.

"Nashangaa hata wale wabunge wapinzani wa Dar es salaam ambao mara nyingi wanakuja vyuoni kuwarubuni wanafunzi wawapigie kura lakini hawatokei kwenye shughuli za maendeleo, kazi yao ni kukosoa tu", amesema Makonda.

DC Ilemela: Tumieni Mabaraza ya Wazee kuishauri Serikali

$
0
0
Wazee wa Ilemela pamoja na wazee wote nchini, watakiwa kuyatumia mabaraza yao yaliyoanzishwa kwa mujibu wa sheria  kuishauri Serikali katika kutekeleza mambo ya msingi ya kujiletea maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela jijini Mwanza Mhe. Severine Lalika wakati akizindua Baraza la Wazee la Wilaya ya Ilemela, ambapo amewataka wazee hao kuwa sehemu ya serikali sanjari na kuwa mwarobaini katika kufichua na kutafuta suluhu ya changamoto zote zinazokwamisha utekelezaji wa shughuli za kimaendeleo ikiwemo ukusanyaji wa mapato na mmomonyoko wa maadili.

"Nyie ni wadau wa maendeleo hivyo mnao wajibu wa kuishauri Serikali katika nyanja mbalimbali, zikiwemo za kisiasa, kijamii na uchumi,"Alisisitiza.

Aidha amewapongeza viongozi wote waliochaguliwa kuongoza baraza hilo sambamba na kuwahakikishia ushirikiano huku akiahidi kukutana nao tena haraka iwezekanavyo kwa ajili ya kujadiliana kwa pamoja juu ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo.

Akimkaribisha Mkuu wa Wilaya,  Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilemela Ndugu Said Kitinga alisema kuwa,  Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa na desturi ya kukutana na wazee na kubadilisha nao mawazo juu ya mambo mbalimbali ya kijamii katika awamu zote za uongozi  tangu kupata uhuru mpaka awamu ya sasa hatua inayodhihiridha juu ya umuhimu wa kundi hilo katika jamii.

Kwa upande wake mratibu wa baraza la wazee wilaya ya Ilemela Bi Neema Kavishe ametaja umuhimu wa kuanzishwa kwa baraza hilo ikiwemo kutumika na Serikali, wasiasa, watendaji na taasisi kama chanzo cha habari na sehemu sahihi  ya kupata takwimu za wazee kabla ya kupanga mipango ya kimaendeleo inayohusu wazee.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Wilaya ya Ilemela Shehe Mohamed Yusuph,  mbali na kuupongeza uongozi wa wilaya ya Ilemela kwa ushirikiano wanaoutoa kwa wazee hao, ameishukuru Serikali ya awamu ya Tano chini ya Mheshimiwa Rais Daktari John Pombe  Magufuli kwa kulithamini kundi hilo katika jamii na kuamua kuanzisha utaratibu wa kupata matibabu ya huduma za afya bila malipo kwa kutumia kadi maalumu huku akiahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kutekeleza shughuli za kimaendeleo.

Baraza la Wazee la Wilaya ya Ilemela liliundwa mnamo tarehe 22/09/2018 ambapo Shehe Mohamed Yusuph Hasan alichaguliwa kuwa Mwenyekiti huku , Makamu Mwenyekiti akiwa Bibi. Prisca Mwisijo, Katibu Ndibai Yukao, Katibu Msaidizi Jackson Kabote, Mweka Hazina Ndugu Daniel Makorere pamoja na wajumbe wawili wakiwakilisha upande wa wanaume na wanawake ambao ni Bwana Saulo Mihigo na Bibi Mary Masalu.

Taarifa Kwa Umma Kutoka Wizara Ya Elimu,sayansi Na Teknolojia


Walichozungumza Rais Magufuli na Rais Mstaafu wa Afrika Kusini Mhe. Thabo Mbeki Baada Ya Kukutana Leo Ikulu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 28 Novemba, 2018 amekutana na kufanya mazungumzo na Rais Mstaafu wa Afrika Kusini na Mwenyekiti wa jopo la ngazi ya juu lililoundwa na Umoja wa Afrika (AU) kushughulikia tatizo la utoroshaji wa fedha (ikiwemo utakatishaji, wizi, rushwa na biashara haramu) kutoka Afrika Mhe. Thabo Mbeki, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Mbeki amesema mazungumzo hayo yamemwezesha kupata taarifa na uzoefu muhimu kutoka kwa Mhe. Rais Magufuli kuhusu juhudi zinazofanywa na Serikali ya Tanzania kukabiliana na utoroshaji wa fedha katika maeneo mbalimbali yakiwemo sekta ya madini na rushwa, matatizo ambayo yanazikabili nchi zingine za Afrika.

“Ni wazi kwamba juhudi zinazofanywa na Tanzania zina umuhimu mkubwa kufanywa na nchi zingine za Afrika, kwa pamoja Waafrika tunaweza kukabiliana na utoroshaji wa fedha zetu kwenda nje ya nchi zetu, na Mhe. Rais Magufuli amezungumza kwa usahihi kabisa juu ya Matrilioni ya Dola za Marekani zinazopotea kupitia utoroshaji huo” amesisitiza Mhe. Mbeki.

Mhe. Rais Magufuli amempongeza Mhe. Rais Mstaafu Mbeki kwa kuongoza jopo hilo na kubainisha kuwa Tanzania ipo tayari kutoa ushirikiano utakaowezesha kunusuru rasilimali za Afrika, hivyo amemshauri kutenga muda wa kutosha ili apate taarifa za uhakika kutoka kwa viongozi na wataalamu katika mamlaka zinazodhibiti utoroshaji wa fedha hapa nchini.

Ripoti ya taasisi ya kimataifa iitwayo Global Financial Intergrity (GFI) ya mwaka 2014 kuhusu tatizo la utoroshaji wa fedha za Afrika inasema Afrika inapoteza Dola za Marekani kati ya Trilioni 1.4 na Trilioni 2.5 kwa mwaka kutokana na tatizo hilo, na kwamba kwa ujumla Afrika imepoteza Dola za Marekani Trilioni 95 kwa miaka 50 iliyopita, ikiwemo Tanzania iliyoripotiwa kupoteza dola za Marekani Bilioni 19 katika miaka 40 iliyopita.

“Na njia nyingi zinazotumika katika kutupotezea hizo fedha na kuibiwa, wanaweza wakaja kuwekeza lakini kila siku wakawa wanasema wanapata hasara kumbe hawapati hasara, wanatengeneza faida kubwa lakini kwenye vitabu wanawaandikia wanapata hasara, wanaweza wakaja kama wawekezaji na wakawa wanazidisha gharama za uwekezaji kuliko uhalisia” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway Mhe. Nicolai Astrup, Ikulu Jijini Dar es Salaam na kumshukuru kwa mchango mkubwa ambao Norway inautoa katika maendeleo ya Tanzania kwenye sekta mbalimbali zikiwemo elimu, kilimo, nishati na gesi.

Mhe. Rais Magufuli amemhakikishia Mhe. Nicolai Astrup kuwa Serikali ya Awamu ya Tano itaendeleza na kukuza zaidi uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Norway ikiwemo kushirikiana na kampuni ya Equinor ya Norway katika uwekezaji wa kiwanda cha kusindika gesi asilia (LNG) kwa manufaa ya pande zote mbili, na kushirikiana na kampuni ya Yara ya Norway katika kuwawezesha wakulima kupata mbolea bora na gharama nafuu.

Nae Mhe. Nicolai Astrup amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ya Tanzania kupambana na rushwa, kuongeza ukusanyaji wa kodi na kuimarisha uchumi, na kwamba Norway itaendelea kuunga mkono juhudi za Tanzania kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Mhe. Nicolai Astrup amebainisha kuwa pamoja na kufadhili miradi mbalimbali ikiwemo umeme vijijini (REA) na kuimarisha mifumo ya ukusanyaji kodi kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Norway itatoa Dola za Marekani Milioni 56 (sawa na shilingi Bilioni 127) kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro, Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Omary Mgumba na Balozi wa Norway hapa nchini Mhe. Elisabeth Jacobsen.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
28 Novemba, 2018

Waziri Mkuu: Serikali Imejipanga Kumaliza Tatizo La Maji Nchini

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imepanga kumaliza tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa kuchimba visima virefu na vifupi pamoja na kutumia maji ya maziwa na mito na kuyapeleka katika maeneo mbalimbali ya wananchi nchini.
 
Pia, Waziri Mkuu amewaagiza wakuu wa wilaya kusimamia uhifadhi wa maeneo ambayo yana vyanzo vya maji ili kuyafanya yaendelee kuwa chepechepe, hivyo kuhakikisha vijiji vyote vinapata maji ya uhakika. “Lazima maeneo hayo yatambuliwe na yahifadhiwe.”

Ameyasema hayo leo (Jumanne, Novemba 27, 2018) alipozungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Uwanja wa shule Sekondari Bugando kata ya Nzera wilayani Geita, wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi za siku nne mkoani Geita.

Waziri Mkuu amesemaSerikali kupitia Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani, itahakikisha wananchi katika maeneo yote nchini wanapata huduma ya maji safi na salama karibu na maeneo yao ya makazi.

Amesema Serikali imejipanga vizuri kuhakikisha kila kijiji kinapata huduma ya maji safi na salama, hivyo amewaagizawatendaji wote wa vijiji kuainisha maeneo yote yenye misitu na vyanzo vya maji na kuhakikisha yanalindwa.

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema mbali na huduma ya maji, pia Serikali imedhamiria kusambaza umeme katika vijiji vyote ambavyo bado havijaunganishiwa nishati hiyo nchini vitaunganishiwa katika awamu ya tatu ya Mradi wa Nishati Vijijini (REA).

“Rais wetu Dkt. John Magufuli anataka kuona nyumba ya kila Mtanzania inapata umeme tena kwa gharama nafuu na ametenga fedha nyingi zitakazotosheleza kusambaza umeme katika vijiji vyote nchini. Gharama za kuunganishiwa umeme huo ni sh. 27,000 tu.”

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema  wananchi hawatowajibika tena katika kulipia gharama za nguzo wala fomu za maombi ya kuunganishiwa umeme kwa sababu tayari gharama hizo zimeshabebwa na Serikali.

Naye, Mbunge wa jimbo la Geita Vijijini, Joseph Musukuma ameishukuru Serikali kwa utekelezaji wa miradi na ahadi zikiwemo na zile zilizotolewa za Rais Dkt. John Magufuli. “Nashukuru Serikali pia kwa kutuzindulia hospitali ya halmashauri ya wilaya ya Geita.”

Kuhusu suala la umeme, Mbunge huyo ameishukuru Serikali kwa kuwa vijiji vyake vyote vimeshaunganishiwa umeme isipokuwa vitongoji vichache, ambapo ameomba navyo viunganishiwe nishati hiyo muhimu kwa maendeleo ya wananchi.

Awali,Waziri Mkuu alikagua na kuzindua hospitali ya wilaya ya Geita inayojengwa katika kata ya Nzera na aliupongeza uogozi wa halmashauri ya wilaya ya Geita kwa hatua waliyofikia katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Jinsi ya Kubadili Picha yako na Kuwa Cartoon

$
0
0
Kama wewe ni mpenzi wa picha, utakuwa umeshasikia au kutumia baadhi ya programu za kuedit picha au hata kuzibadili kabisa na kuzifanya kuwa katuni. 

Katika makala hii fupi, tutaangalia programu mbadala za kubadili picha ukiacha ile maaarufu iliyozoeleka miongoni mwetu ya Adobe Photoshop.

Kwa muda mrefu uliopita kama ungemuuliza mtu ni ipi programu nzuri kwa kubadili picha sikuzote angesema Photoshop. Sawa nikweli Photoshop itaendelea kuwa programu kubwa na imara ila ni tabu kidogo kuitumia  maana ina mambo mengi na inahitaji ujuzi wa hali ya juu.

Hapo chini tumekuwekea Program mbadala ambazo zitakufanya u edit picha zako kwa wepesi zaid na pia zitakusaidia kujibadili na kuwa Katuni. 

#1. Be Funky
#2.Cartoonize
#3.Toonyphotos
#4.Cartoon photo 

Maelezo ya jinsi ya kuzipata au kuzitumia Progamu hizo yanapatikana hapa<<HAPA>>

Endelea kuwa nasi, tutaendelea kukuletea makala fupifupi kama hizi

Katibu Mkuu CCM Amtaka Zitto Kabwe Ahamie CCM

$
0
0
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Bashiru Ally amempongeza kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo na Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe kwa kuibua mijadala ya kiuchumi na kumkaribisha ajiunge na Chama chake cha CCM.

Akizungumza akiwa ziarani mkoani Iringa, Dkt. Bashiru amesema kuwa kiongozi huyo amekuwa akiibua mijadala mbalimbali ya kiuchumi na kumkaribisha kujiunga na chama hicho.

"Nampongeza kiongozi wa ACT-Wazalendo ndugu Zitto Kabwe kwa kuibua mijadala mbalimbali ya kiuchumi, nimtake na kumkaribisha ajiunge na CCM, chama cha ujamaa wa kweli", amesema Dkt Bashiru na kuongeza;

"Napenda kutumia hadhara hii kwa wote walioadhibiwa na wale waliosimamishwa uanachama milango ipo wazi kuomba msamaha na kusamehewa, tunajua walikosea ila hatutaendelea na visasi".

Katibu huyo ameongeza kuwa vyama vitakavyokufa kwenye uchaguzi ujao ni vyama vinavyoendeshwa kwa ajenda za matukio, vyama tegemezi vinavyotegemea mabepari, vyama vilivyochukua mafisadi na kuwaweka ngazi za juu.

"Hakuna mtu anayezuiliwa kugombea ila ni lazima afuate taratibu, atakayekiuka taratibu atakiona, baadhi wanatafuta Urais Zanzibar, wanapoteza muda Urais hauombwi, ni unaombwa. Hatuna urais wa udalali kwani ulipita toka mwaka 2015", ameongeza Dkt. Bashiru.

Hii Ndo Maktaba ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Iliyozinduliwa Leo na Rais Magufuli

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 27 Novemba, 2018 amefungua maktaba mpya, kubwa na ya kisasa ya Kikuu cha Dar es Salaam iliyojengwa katika Kampasi Mlimani (Mwl. Julius K. Nyerere) Jijini Dar es Salaam.

Maktaba hiyo kubwa Afrika Mashariki na Kati imejengwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 93.6 ikiwa ni msaada kutoka Serikali ya China na inakuwa maktaba kubwa kuliko maktaba zote ambazo China imezijenga barani Afrika.

Katika taarifa yake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Prof. William Anangisye amesema majengo ya maktaba hiyo yenye ghorofa mbili yamechukua eneo lenye ukubwa wa meta za mraba 20,000 yakiwa na uwezo wa kuhifadhi vitabu 800,000, kukalisha watumiaji 2,100 kwa wakati mmoja, yana kompyuta 160 zilizounganishwa na mtandao kwa ajili ya kusoma vitabu kwa njia ya kielektroniki, ofisi za wafanyakazi, eneo la wanafunzi wenye mahitaji maalum na ukumbi wa kisasa wa mihadhara wenye uwezo wa kuchukua watu 600.

Prof. Anangisye ameishukuru Serikali kwa mchango mkubwa uliosaidia kufanikisha ujenzi wa maktaba hiyo, ameishukuru Serikali ya China kwa kutoa msaada wa fedha za ujenzi huo na kampuni ya ujenzi ya Jiangsu Jiangdu ya China kwa kujenga majengo yenye ubora na hadhi ya hali ya juu.

Ameahidi kuwa Jumuiya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam itahakikisha majengo ya maktaba hiyo yanatunzwa vizuri na maktaba inatumika kuwanufaisha wanafunzi wa chuo hicho pamoja na wanafunzi wa taasisi zingine za vyuo na wananchi wa kawaida.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa namna anavyotoa kipaumbele kwa sekta ya elimu na ameahidi kuwa wizara yake itaendelea kuhakikisha taasisi zote zilizo chini ya wizara hiyo zinaendeshwa kwa kuzingatia maadili na matumizi bora ya rasilimali, pia amemshukuru Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke kwa kusimamia na kufuatilia kwa ukaribu ujenzi wa maktaba hiyo na kwa Serikali ya China kutoa shilingi Bilioni 50.8 kwa ajili ya ujenzi wa chuo cha elimu ya mafunzo ya ufundi stadi (VETA) Mkoani Kagera.

Akizungumza katika sherehe hizo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemshukuru Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke na kumuomba apeleke shukrani za Tanzania kwa Rais wa China Mhe. Xi Jinping kwa misaada ambayo China imekuwa ikiitoa kwa Tanzania, ikiwemo ujenzi wa Maktaba hiyo na Chuo cha VETA kitakachojengwa Mkoani Kagera.

Mhe. Rais Magufuli amesema urafiki wa China na Tanzania ulioasisiwa na Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Mwenyekiti Mao Zedong umeendelea kuleta manufaa makubwa na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano na itauendeleza na kuukuza uhusiano na ushirikiano huu mzuri.

“Jambo la kufurahisha ni kwamba misaada yao haiambatani na masharti. Wenyewe wakiamua kukupa wanakupa, walitujengea TAZARA, URAFIKI na pia wametusaidia katika maeneo mengine ya maendeleo” amesema Mhe. Rais Magufuli na kumhakikishia Mhe. Balozi Wang Ke kuwa Serikali itahakikisha kila msaada unaotolewa unatumiwa vizuri.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amempongeza Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Mstaafu Prof. Rwekaza Mukandala kwa kuandaa mpango wa ujenzi wa maktaba hiyo, na pia amewapongeza Jumuiya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kupata maktaba ambayo itawasaidia kuongeza kiwango cha ubora wa elimu.

Amewataka wana Jumuiya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuhakikisha maktaba hiyo inatunzwa vizuri na ametoa wito kwa Watanzania kujifunza lugha ya Kichina katika jengo mojawapo la maktaba hiyo litakalokuwa likifundisha lugha hiyo kwa kuwa kuna manufaa makubwa kwa Watanzania kujifunza lugha hiyo.

Sherehe hizo zimehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma, Mawaziri Wakuu Wastaafu Mhe. Jaji Mstaafu Joseph Sinde Warioba na Mhe. Edward Ngoyai Lowassa, Mawaziri, Mabalozi wa nchi mbalimbali na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
27 Novemba, 2018

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya Novemba 29

Tanzania Kujenga Bandari Na Meli Za Uvuvi

$
0
0
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega, amesema serikali ipo katika hatua nzuri ya kukamilisha hatua za ujenzi wa bandari ya uvuvi na kununua meli kwa ajili ya kuvua samaki kwenye eneo la bahari kuu pamoja na kuziwezesha meli nyingine kutia nanga katika bandari hiyo ikiwa ni lengo la Tanzania kwenda sambamba na nchi nyingine duniani kukuza uchumi kupitia sekta ya uvuvi.

Mhe. Ulega amebainisha hayo mara baada ya kuwasili nchini akitokea Mjini Nairobi nchini Kenya, ambapo hivi karibuni amehudhuria mkutano uliowajumuisha wajumbe zaidi ya elfu nne, kutoka mataifa mbalimbali, ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli amewakilishwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapindudi Dkt. Ali Mohamed Shein.

Mhe. Ulega amesema mchango wa sekta ya uvuvi hapa nchini bado ni mdogo hivyo mkutano huo umeongeza hamasa kwa Tanzania kutafuta namna bora ya ukuaji uchumi kupitia sekta ya uvuvi.

“Sisi tuko katika hatua nzuri ya kuweza kukamilisha ujenzi wa bandari ya uvuvi, tukishafanikiwa kujenga bandari ya uvuvi, maana yake ni kwamba meli zitatia nanga hapa kwetu, tutapata ajira, tutatengeneza pia vile vile  maeneo ya kuhifadhia samaki kwa wingi, tutachakata, tutakuwa na uwezo wa kuuza katika soko la ndani na soko la nje.” Alisema Mhe. Ulega

Aidha, amesema serikali imeshaanza hatua ya ununuzi wa meli zake zenyewe, hatua iliyoilazimu kulifufua Shirika la Uvuvi (TAFICO) ambalo tayari limeshaanza kufanya kazi.

“Ili uchumi wenyewe uwe endelevu ni lazima kulinda mazingira ya bahari, maziwa, mito, kulinda rasilimali zilizopo humo, ndio maana Tanzania inafanya kazi ya ulinzi wa rasilimali hizo ili ziwe endelevu hata kwa vizazi vijavyo viweze kukuta na kuzuia uchafuzi wa mazingira hayo pamoja na uvuvi usiofuata sheria.” Alisema Mhe. Ulega

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amesema pia katika mkutano huo wa ‘Blue Economy’ wenye lengo la kukuza uchumi kupitia sekta ya uvuvi uliofanyika Mjini Nairobi nchini Kenya, umebainisha kuwa sekta ya utalii ni muhimu katika uchumi endelevu, sambamba na ulinzi na usalama wa nchi, pia kuzuia uingizwaji wa dawa za kulevya ambazo zimekuwa zikiingizwa katika mataifa mbalimbali kupitia njia ya bahari.

Mwisho.
Imetolewa na: Edward Kondela
Afisa Habari-Wizara ya Mifugo na Uvuvi
28.11.2018

Mbatia Aweka Wazi Alichoteta Na Rais John Magufuli Wiki Chache Zilizopita

$
0
0
MWENYEKITI wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) na Mbunge wa Vunjo, James Mbatia amewamegea siri wananchi wa mji mdogo wa Himo juu ya mazungumzo yake na Rais Dk. John Magufuli, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Alidai alikwenda kumueleza malalamiko ya wananchi kuhusu amri ya Mkuu wa Wilaya ya Moshi ya kusitisha ujenzi wa barabara na kusababisha hasara ya mabilioni ya shilingi.

“Haya yote nimemueleza Mheshimiwa Rais (Magufuli) niwe mkweli, nilibahatika hapo katikati Mheshimiwa Rais akaniita akasema hivi, narejea sauti ya Rais aliniambia na ameshaagiza ofisi zake na wengine wameniita Dodoma, barabara za wana Vunjo atachangia yeye binafsi kama John Pombe Magufuli, pili serikali yake itachangia na tatu atakuja kama Amiri Jeshi Mkuu kufungua barabara hizi yeye mwenyewe kama John Pombe Magufuli,”alisema

Mbatia alikuwa akizungumza na wananchi wa Kata ya Makuyuni katika Mamlaka ya Mji mdogo wa Himo, Wilaya ya Moshi wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya ghalani. 

Mradi wa upanuzi na ujenzi barabara za vijijini kwa kiwango cha changarawe unaodaiwa kusisitishwa katika Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro, unahusisha barabara zenye urefu wa kilometa 389.3 ambazo zilikuwa zigharimu Sh. bilioni 12.077 kutokana na utafiti wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (Tarura) wa mwaka huu.

Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Kippi Warioba anadaiwa kusimamisha kazi ya ujenzi wa barabara hizo na hivyo kusababisha hasara.

Zaidi Mbatia alisisitiza: “Sasa tuone ni nani zaidi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na maendeleo ya watanzania, maendeleo hayana itikadi za vyama. Kwa nini amefanya hivyo, kwa sababu Jimbo la Vunjo tumekuwa wa kwanza Tanzania kuweza kujipanga wenyewe mpaka hatua tuliyofikia ya kujiletea maendeleo yetu wenyewe na tujipongeze wana Vunjo.

"Hizi barabara zikiwa vizuri si tunazitumia sote, barabara za Makuyuni zikiwa nzuri zitaendelea kutumiwa na watu wote hata kama Mbatia sitakuwa Mbunge…Mimi sijawahi kumtukana Rais, sasa atakuja yeye mwenyewe.”

Mbatia alikutana na Rais Magufuli na kufanya mazungumzo naye Ikulu, Novemba 13 mwaka huu akiwa pamoja na wanasiasa wengine Mh. John Cheyo (UDP), John Shubuda na mfanyabiashara Rostam Aziz.

Katika mkutano huo, Mbatia aliwaeleza wananchi hao kwamba amekopa fedha zaidi ya Sh. milioni 500 Benki ya CRDB kwa ajili ya kununua mitambo ya ujenzi wa barabara hizo.

“Mimi nimenunua mitambo sawa, mingine tunakodisha sawa lakini tukasema wananchi waanze kuchangia mafuta kwenye hiyo mitambo hiyo, kwa mfano Kijiji cha Mshihiri mpaka leo hii wameshachangia takribani Sh. milioni 26 lakini ukichanganya zote pamoja na za Ashira ni zaidi ya Sh. milioni 30 na kitu huko,”alieleza

Akijibu maswali ya wananchi kuhusu kukwama kwa ujenzi wa barabara za Samanga/Sembeti, Mbunge huyo alisema Mungu sio Athuman na akawataka wananchi hao kusubiri kwanza ili mdomo wake usiteleze kwa vile wana kesi mahakamani.

Wakati anahitimisha mkutano huo, Mbatia aliipongeza Kamati ya Maendeleo ya wana Vunjo (VDF) chini ya Askofu Mstaafu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini Dk. Martin Shao, mashekhe wetu, mapadri wetu na wachungaji na viongozi wote, akisema yeye binafsi toka sakafu ya moyo wake hana chuki na mtu yeyote na anamshukuru Mungu amesikia na Mheshimiwa Rais (Magufuli) amesikia dua zao.

Mwisho


Zaidi Ya Bilioni Tatu Zatafunwa......waziri Mkuu Aagiza Kuchukuliwa Hatua Kwa Watumishi Wote Waliohusika

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameagiza watumishi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyangw’ale waliohusika na ubadhilifu wa zaidi ya sh. bilioni tatu fedha ambazo zilitolewa na Serikali kugharamia miradi ya maendeleo wachukuliwe hatua.
 
Pia ameagiza kukamatwa na kuchukuliwa hatua kwa Mkaguzi wa Ndani wa halmashauri hiyo, Gavana Matesa kwa sababu ameshindwa kutoa kwa mamlaka husika kuhusu taarifa za wizi wa fedha za maendeleo zilizotafunwa.
 
Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo jana (Jumatano, Novemba 28, 2018) wakati akizungumza na watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Nyangw’ale akiwa katika ziara yake ya kikazi ya siku nne mkoani Geita.
 
Miongoni mwa miradi ambayo fedha zake zimepotea ni pamoja na sh. bilioni 1.2 za ujenzi ofisi ya halmashauri hiyo, sh. milioni 400 za ukarabati wa kituo cha afya Nyangw’ale, sh. milioni 611.230 za miradi ya maji.
 
Nyingine ni sh. milioni 536.119 za mpango wa malipo kulingana na huduma (EP4R), sh. milioni 125.914 za ushuru wa huduma, sh. milioni 31 za ujenzi wa ofisi ya mbunge na sh. milioni 109 za mfuko wa barabara.
 
“Wilaya ya Nyangw’ale ni mpya na Serikali imekuwa ikileta fedha nyingi lakini fedha zote zimetafunwa, Serikali ipo makini sana na moja kati ya vita kubwa ni dhidi ya mafisadi, wala rushwa ambayo ni endelevu hivyo tutashughulika na kila mmoja.
 
Tayari watu saba akiwemo aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Nyangw’ale, Carlos Gwamagobe na wenzake wamekamatwa. Wizi unatisha Nyangw’ale wilaya inatia aibu tutawaondoa watu wote waliohusika na tutaendelea kuwakamata.”
 
Hata hivyo Waziri Mkuu amewahakikishia wananchi wa wilaya hiyo kwamba Serikali itahakikisha miradi yote iliyoahidiwa kujengwa kwenye wilaya hiyo ikiwemo ya maji itatekelezwa kama ilivyopangwa, waendelee kuwa na imani na Serikali yao.
 
Kuhusua suala la watumishi, amesema wilaya hiyo lazima iwe na watumishi wasafi wenye weledi wa kufanya kazi na lazima wahakikishe fedha za miradi zinazotolewa katika halmashauri hiyo zinalingana na thamani halisi ya mradi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel amesema atahakikisha watumishi wote wa umma waliohusika na wizi huo wanachukuliwa hatua stahili na kwamba tayari baadhi yao wameshafikishwa kwenye vyombo vya dola.

Amesema halmashauri ya wilaya ya Nyangw’ale inaongoza kwa matumizi mabaya ya fedha za maendeleo kwa kuwa awali lilikuwa chaka kubwa la wizi, ambapo amesema ni bora watumishi wote wasiokuwa waadifu waondolewe na waletwe wengine.

Mkuu huyo wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Gabriel amesema tayari baadhi ya watumishi wanaotuhumiwa kuhusika katika ubadhilifu wa fedha za miradi mbalimbali wameshakabidhiwa kwa vyombo vya dola huku watumishi wengine wakiendelea kuchunguzwa.”Watumishi wote waliohusika na wizi huu watapata tabu sana”

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Dr.Mjukuu wa kushosha : Pata Tiba Asili ya Tatizo la Uzazi, Kutopata Hedhi kwa Mpangilio, Nguvu za Kiume, UTI Sugu

$
0
0
SIX(6) power; Ni dawa ya Nguvu za kiume inayofanya kuchelewa kufika kileleni dkk 30 Hadi 46 unaweza kurudia tendo utakavyo,pia inarutubisha mbegu za kiume kwa wasio na sifa ya kupata mtoto,dozi Ni siku sita mabadiliko masaa manne.Tumia six(6) power ndio kiboko wa yote usisubiri kuhadithiwa.

SHOOLA 4 POWER; Wenye maumbile madogo (KIBAMIA) inanenepesha na kurefusha uume,kama tatizo Ni la kuzaliwa siku 12 Kama Ni la ukubwani siku 6.

MBUKE; Dawa ya Uzazi kwa aliyefungwa na kutofanikiwa kupata mtoto,kwa asie pata hedhi kwa mpangilio mzuri tatizo huisha kabisaa..Ni ya unga.

LYONGO;dawa ya mvuto wa mapenzi Kama umeachwa yote yatakwisha aliembali atakuhudumia mwenza wako atarejea ndani ya SAA 12 hata Kama yupo mbali.

HOLAZA; Ni dawa ya kumaliza matatizo mengi mengi Kama kesi,dhuluma,kushindwa kuuza eneo nyumba na Kama biashara haziendi.

TALIGULA;dawa ya kufungua kitu kilichofungwa kuchawi,kimizimu,majini wabaya mashuleni,kutokupata ajira,kuoa au kuolewa na Safari zilizofungwa
 
KASELA;Ni kiboko ya kusafirisha mizigo na kufika salama..iwe majini,migodini pia katika kilimo na ufugaji.

DR.Mjukuu wa kushosha asema kwanini usumbuke na maradhi mwilini wakati tiba zipo?? ,Amini tiba asilia Sasa maradhi yako yatakwisha .

Je,wewe una maradhi gani mwilini mwako??

(1)Sukari ya kupanda na kushuka(TUNDWA)Ni ya unga inayochemshwa ,dozi Ni siku 20.

(2)Presha ya kupanda na kushuka(NGADA) ni dawa ya unga dozi siku 14

(3)maleria sugu(NINJIWE) dozi siku 8 unapona kabisa

(4)U.T.I sugu(GUMO)Dozi siku 4 habari kwisha kabisa.

(5)Typhoid sugu(IKWATA) Dozi siku 3

(6)Kifua kubana,moyo,Figo(LUGALA)dozi siku 7

(7)Tezi dume(Dozi siku 8 - unga),ngiri,busha bila operation (SALIUNGU)dozi siku 14

(8)Miguu kuwaka moto (JIMYA) dozi siku 6

(9) kilungulia,kwikwi(INJACHI)dozi masaa 6.

(10)msongo wa mawazo.

(11) vidonda vya tumbo (MPALALA) Dozi siku 7.

Hizo Ndizo Huduma Zitolewazo Na Nyingine Nyingi,usitume Meseji Wala Kubip,nahudumia Duniani Pote Ulipo.

Ofisi Zipo Katika Mikoa Miwili Shinyanga Wilaya Ya Kahama Na Dar Es Salaam Wilaya Ya Ilala..Sehemu Zingine Nasafirisha..niulize Kwa Mawasiliano Yafuatayo...

     0744 922 982
     0716 608 959
     0784 475 946.

Waziri Mkuu Achukizwa Na Wanafunzi Kukatishwa Masomo

$
0
0
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amechukizwa na vitendo vya watoto wa kike kukatisha masomo yao kwa kupata ujauzito wilayani Nyang’hwale ambapo jumla ya wanafunzi 72 wamepata ujauzo katika kipindi cha miaka mitatu cha kuanzia mwaka 2016 hadi 2018.

Kutokana na wilaya hiyo kuwa na idadi kubwa ya watoto wa kike wanaokatisha masomo kutokana na ujauzito, Waziri Mkuu amemuagiza Mkuu wa wilaya ya Nyang’hwale Hamim Gwiyama kufanya operesheni katika kila kijiji na kubaini waliowapa wanafunzi ujauzito na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria.

Waziri Mkuu aliyasema hayo jana jioni (Jumatano, Novemba 28, 2018) alipozungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Sabasaba, ,kijiji cha Kalumwawilaya ya Nyang’hwale, akiwa katika ziara yake mkoani Geita.

“Jambo lingine litakalowawezesha kukabiliana na tatizo la ujauzito kwa wanafunzi wa kike ni kuanzisha miradi ya ujenzi wa mabweni ili watoto wa kike waweze kusoma bila ya kupata vishawishi vinavyosababisha wao kupata ujauzito.”

Waziri Mkuu alisema Serikali haiwezi kuacha jambo hilo likiendelea, hivyo aliwataka wananchi washirikiane katika kuwalinda watoto wa kike na Serikali itawachukulia hatua watendaji wote ambao katika maeneo yao watoto wa kike watabainika kuwa na ujauzito.

“Watoto wa kike lazima waheshimiwe waachwe wasome bila ya usumbufu na atakayekatisha masomo adhabu yake ni kali. Tukikukuta umesimama na binti katika kona isiyoeleweka tutakukamata. Ole wenumtakaobainika kuwapa ujauzito wanafunzi, adhabu yake ni miaka 30 jela.”

Waziri Mkuu pia, alitoa onyo kwa wazazi au walezi watakaowaozesha watoto kike ambao bado ni wanafunzi na kwa upande wa wazazi watakaomsindikiza mtoto wao wa kiume kwenda kuoa mwanafunzi wote watachukuliwa hatua za kisheria.

Katika kuoneshwa kuchukizwa na jambo hilo, Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mwita Waitara ambaye anashughulikia elimu, amemueleza Waziri Mkuu kwamba Novemba 30, 2018 yeye arudi wilayani hapo kwa ajili ya kuwashughulia wote wanaokatisha masomo wanafunzi kike. Ametoa namba ya simu ili wananchi waanze kumpa taarifa za wahusika.

Katika hatua nyingine,Waziri Mkuu alisemaSerikali imedhamiria kusambaza umeme katika vijiji vyote ambavyo bado havijaunganishiwa nishati hiyo nchini vitaunganishiwa katika awamu ya tatu ya Mradi wa Nishati Vijijini (REA).

“Rais wetu Dkt. John Magufuli anataka kuona nyumba ya kila Mtanzania inapata umeme tena kwa gharama nafuu na ametenga fedha nyingi zitakazotosheleza kusambaza umeme katika vijiji vyote nchini. Gharama za kuunganishiwa umeme huo ni sh. 27,000 tu.”

Kuhusu suala la gharama za kulipia nguzo, Waziri Mkuu alisema wananchi hawatowajibika tena katika kulipia gharama za nguzo pamoja na zile za fomu za maombi ya kuunganishiwa umeme kwa sababu tayari gharama hizo zimeshabebwa na Serikali.

Awali, Waziri Mkuu alitembelea kiwanda cha kuchenjua dhahabu cha Nyamigogo ambapo alikagua miundombinu ya kiwanda hicho na kisha aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa kiwanda hicho, ambacho muwekezaji wake ni mzawa.

Rufaa Ya Mbowe na Ester Matiko Yaanza Kusikilizwa

$
0
0
Rufaa ya dhamana ya mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko imeanza kusikilizwa leo asubuhi Alhamisi Novemba 29, 2018 baada ya Jaji Sam Rumanyika kuingia mahakamani.

Hata hivyo,  upande wa mashtaka umewasilisha pingamizi la awali wakiomba rufaa hiyo itupiliwe mbali wakitoa hoja tatu za kisheria.

Kufuatia hilo mahakama imeamua kuanza kusikiliza pingamizi hilo kabla ya kuendelea na rufaa.

Mbowe na Matiko walipoingia  katika ukumbi wa Mahakama Kuu wafuasi na wanachama wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania walisimama kama ishara ya kuwapa heshima.

Mbowe ambaye ni mbunge wa Hai na Matiko wamekata rufaa Mahakama Kuu kupinga uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwafutia dhamana katika kesi ya jinai inayowakabili mahakamani hapo.

Tayari mawakili wa pande zote wameshaingia katika ukumbi wa mahakama ya wazi namba moja.

Wabunge mbalimbali wa Chadema akiwemo Godbless Lema (Arusha Mjini) na wanachama wanaendelea kumiminika mahakamani kufuatilia mwenendo wa rufaa hiyo.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images