Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?...... Tunazo dawa na PETE za bahati Zenye Uwezo wa Kubadili Maisha Yako

$
0
0

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara, Msanii wa Maigizo, Mwanamziki, ama mwanafunzi tunazo Dawa na PETE za Bahati zenye uwezo mkubwa wa kuyabadilisha maisha yako nakukupatia mafanikio makubwa ndani ya mda mfupi tu.

Kutana na Sheikh Jumaa Bilal. Yeye ni mtaalam na mtabibu wa nyota za binadam na bingwa wa tiba za asili Afrika mashariki. 

Wasiliana na mtaalam huyu kwani yeye ufaulu pale wote waliko shindwa na pia humaliza kazi zilizo shindikana ama zilizo achwa ndani ya siku1 tu. Sheikh Jumaa Bilal ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOASHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA-  Sheikh Sasa amezianza ziara zake za mikoani na atayatembelea maeneo mbali mbali ndani na Nje ya nchi.

Anatibu magonjwa sugu yanaojulikana nayasiojulikana kwakutumia QUR_AN MAJI , KIOO MAJINI NA MITISHAMBA.

Anazo dawa za mapenzi( Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu LIMBWATA) kumrudishaa alipote, kutoa Mikosi, Kutatuwa shida za chumaulete, mvuto wa biashara na sehem za kazi, kusafisha nyota, kurudisha mali zilizo ibiwa, zilizpotea, ama zilizodhulumiwa, kushika wezi na wachawi, Kutoa kinga ya mwili, nyumba, Biashara, kufukuza majini wabaya, KUUZA kwa haraka (shamba, NYUMBA, GARI..), Kuweka Zindiko ya mwili, nyumba, shamba, Gari, kupata Kazi na kupandishwa cheo, mali na UTAJIRI bila masharti na mengine mengi ya Siri. (Anazo Pia Pochi zisizo kwisha Hela MAGIC WALLET)

*{لَا يُؤَاخِذُكُمُ اللَّهُ بِاللَّغْوِ فِي أيْمَانِكُمْ وَلَٰكِنْ يُؤَاخِذُكُمْ بِمَا عَقَّدْتُمُ الْأَيْمَانَ ۖ فَكَفَّارَتُهُ إِطْعَامُ عَشَرَةِمَسَاكِينَ مِنْ أَوْسَطِ مَا تُطْعِمُونَ أَهْلِيكُمْ أَوْ كِسْوَتُهُمْ أَوْ تَحْرِيرُ رَقَبَةٍ ۖ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ ۚ ذَٰلِكَ كَفَّارَةُ أَيْمَانِكُمْ إِذَا حَلَفْتُمْ ۚ وَاحْفَظُوا أَيْمَانَكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ اللَّهُ لَكُمْ آيَاتِهِ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ }* ﴿٨٩﴾

✨Wabillahhi Tawfiq Asallam  Alaikum

Kwa tiba na ushauri wasiliana na ofisi kwa
nambari ya simu

+255 688 745 790
+255 672 861 042
Whatsapp :  0762 252 102

Mfumo mpya wa visa na vibali vya ukaazi vya kielektroniki kukuza diplomasia ya uchumi

$
0
0
Na. Immaculate Makilika – MAELEZO
Serikali imesema mfumo mpya wa visa na vibali vya ukaazi  vya kielektroniki unatajwa kuwa na faida lukuki kwa nchi ikiwemo kukuza sera ya diplomasia ya uchumi, sera ya viwanda, kusaidia ongezeko la watalii wanaokuja nchini pamoja na kuongeza ukusanyaji wa madurufu ya  Serikali.

Akizungumza jana, jijini Dar es salaam, wakati akizindua mfumo wa visa na vibali vya ukaazi vya kielektroniki, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa, alisema kuwa mfumo huu mpya unatarajia kufikia malengo ya Serikali  ya kukuza diplomasia ya uchumi, kuchochea kasi ya maendeleo na uchumi wa  viwanda, sambamba na hilo raia wa kigeni wanaweza kuomba huduma hiyo wakati wowote na mahali popote duniani.

“Ni imani yangu kuwa mfumo huu mpya utatatua  changamoto zote zilizokuwepo awali, lakini pia utarahisisha upatikanaji wa huduma kwa raia wa kigeni. Ni muhimu kwa mfumo huu kuunganishwa na mifumo mingine ya Idara ya Kazi, Kituo cha Uwekezaji,  Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), pamoja na Mfumo wa Malipo wa Kieletroniki Serikalini (GePG), ambayo itamsaidia mteja kupata  huduma kwa urahisi bila usumbufu wowote” alisema Waziri Mkuu

Waziri Mkuu Majaliwa, aliongeza kuwa mfumo huo utasaidia kutoa huduma kama ambavyo Serikali imekusudia, sambamba na kusaidia nchi katika masuala ya ulinzi na usalama.

Aidha, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga alisema kuwa mfumo huo utasaidia kukuza sekta ya utalii, ambapo kwa mwaka watalii milioni moja hadi mbili pekee wanafika  nchini, ambapo fedha za kigeni zinapatikana katika sekta hiyo ya utalii.

“Matarajio yangu kwamba mfumo huu mpya  wa  visa na vibali vya ukaazi  vya kielektroniki, utasaidia kuboresha na kuvutia wawekezaji,  sambamba na kuleta watalii nchini”

Pia, Waziri Mahiga alisema Wizara yake itaelimisha Jumuiya ya Mabalozi kuhusu huduma hiyo, ikiwa ni sambamba na kufanya diplomasia ya uchumi.

Kwa upande wake, Kamishna Mkuu wa Uhamiaji nchini, Dkt. Anna Makakala alisema kuwa mfumo huo mpya wa visa na vibali vya ukaazi  vya kielektroniki utasaidia kuimarisha usalama, uwekaji wa kumbukumbu, pamoja na kuwezesha Idara ya uhamiaji kupata taarifa na kuzifanyiakazi kabla ya mgeni kuwasili nchini, pamoja na kukusanya madurufu ya serikali bila upotevu

“Kuanzia Januari 31, mwaka 2018  hadi Novemba 25, 2018 jumla ya hati mpya za kusafiria za kielektroniki 55, 177 zimetolewa, ambapo zaidi ya shilingi bilioni 7 zimepatikana kutokana na malipo ya hati mpya za kusafiria za kielektroniki” alisema Kamishna Mkuu wa Uhamiaji

Aidha, ifikapo Januari 2019 huduma ya upatikanaji wa hati mpya za kusafiria za kielektroniki itapatikana katika balozi zote za Tanzania ili kuwarahisishia huduma watanzania au raia wa kigeni walioko nje ya nchi.

Mradi wa Uhamiaji Mtandao unaohusisha mfumo wa hati ya kusafiria ya kielektroniki,  mfumo wa visa na vibali vya ukaazi  vya kielektroniki ambayo ni awamu ya pili, pamioja na mfumo wa kuzuia na kudhibiti wahamiaji haramu wanaoingia nchini.

Emmanuel Mbasha Aandaa Siku Maalum Ya Maombi Kwa Ajili Ruge Mutahaba

$
0
0
Mwimbaji wa nyimbo za injili nchini Emmanuel Mbasha amesema mafanikio makubwa ya Muziki nchini Tanzania Mkurungezi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group Ruge Mutahaba anahusika.

Emmanuel Mbasha ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo ameweka siku Ijumaa ya November 30,2018  kwa ajili ya mkesha wa maombi ili kumuombea ili aweze kupona.

“Ijumaa hii nitakuwa kwenye mkesha wa kufunga na kufungua mwezi, na katika mkesha huu nitakuwa na maombi maalum ya kumuombea Ruge Mutahaba ambaye yuko nchini Afrika kusini kwa matibabu. Huyu ndugu binafsi tunafahamiana vizuri sana, maana alikuwa mtu wa karibu sana kwangu.”

“Najua wengi hawajui kuwa Ruge ndiye aliyekuwa meneja wetu aliyeisimamia albam yetu ya kwanza na ya pili wakati tunaimba na mke wangu, na hata baadhi ya nyimbo zetu ni yeye alisimamia kwa umakini mkubwa nikishirikiana nae kwa ukaribu sana, na kuzisimamia hadi zikavuma kila kona na kujulikana”

“Na kupitia usimamizi huu wa Ruge tulisaini mikataba mingi sana iliyokuwa ya faida. Hata katika ndoa yangu Ruge alipenda kunitia moyo na kuniambia kuwa “anafurahi kuona jinsi ninavyompenda mke wangu na kumsimamia vizuri, jambo ambalo ni gumu sana kufanywa na wanaume wengi wa kiafrika. Kwa kweli katika mambo yanayohusu tasnia ya muziki Tanzania kwa ujumla Ruge ana mchango mkubwa sana kwenye hii sanaa”

“Sio tu kwenye bongo fleva bali hata nyimbo za injili maana hadi leo hii ukitazama wanamuziki wengi wa nyimbo za injili ambao umaarufu wao umevuka ile mipaka ya kujulikana ndani ya kanisa tu, asilimia kubwa utakuta nyuma yao kuna support ya Ruge Mutahaba. Hivyo naamini hata katika ufalme wa Mungu huyu ni mtu wa faida sana. Na umuhimu wa wake umezidi kuonekana katika tukio la juzi la Fiesta, maana naamini kabisa endapo angekuwepo kila kitu kingeenda sawa”

“Nikiwa kama baba wa kiroho na mlezi mkuu wa waimbaji wote wa nyimbo za injili Tanzania, napenda kutoa rai kwa wasanii wote Tanzania, huu ni wakati muafaka wa kila mmoja kuweka pembeni tofauti zake za u team na tuungane kwa pamoja kumuombea dua njema ndugu yetu Ruge Mutahaba, na huu ndiyo moyo wa binadamu muungwana anaejua utu ni nini”

“Ila kwa yule atakaefurahia matatizo yake hakika atakuwa mchawi hata kama hajawahi kupaa na ungo. Maana ugonjwa ni hali inayompata mtu yeyote, leo kwake kesho kwako.
Asanteni….Get well soon brother ruge”

Kalulumila:Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
 BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO KALULUMILA.
----------------------------------------
Ni dawa pekee iliyojipatia umaarufu nchini na nje ya nchi kwa kufanya kazi mara 3, kwa wakati mmoja 1, kurefusha uume na kunenepesha saizi uipendayo kuongeza nguvu za kiume na inatibu matatizo na gerentii miaka 30. Na kuendelea haina madhara, inaimarisha mishipa ya uume iliyoregea na udhalishaji wa mbegu za kiume. 


---------NINI HUCHANGIA MATATIZO HAYA--Ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya ili kujua kwamba una ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya, ili kujua kama unangiri dalili zake ni kufika haraka kileleni wakati wa tendo la ndoa, 2)kushindwa kurudia tendo la ndoa. 3)kutoa choo kama cha mbuzi. 4)tumbo kujaa gesi na kuunguruma. 5)kukosa choo kabisa. 6)maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi. 7) korodani moja kuvimba 8)kutosikia hamu ya tendo la ndoa na maumivu ya kiuno wakati wa tendo la ndoa. 9)maumivu ya kiuno na mgongo pia tunatibu kisukari kwa siku7, presha, busha, bila kupasuliwa na magonjwa mbalimbali. 

---------------------------------------
TUPO TEGETA KWA NDEVU KARIBU NA MACHINJIO YA NGOMBE UTAONA OFSI IMEANDIKWA KALULUMILA HERBALIST CLINIC HOSPITAL SIMU .
----------------------------------------
-0655-557-182.
-0755-557182.
-0784-557-182.
PIA UTAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
---------------------------------------
KARIBUNI SANA.
----------------------------------------

TFS Yawasimamisha Kazi Watumishi 11 Kutekeleza Majukumu Yao

$
0
0
Kashfa ya uhujumu uchumi imetajwa kuwa chanzo cha  watumishi 11 wa Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) kusimamishwa kazi huku wengine wakifikishwa mahakamani.

Taarifa iliyotolewa  Jumatatu Novemba 26, 2018 na mkuu wa kitengo cha mawasiliano Wizara ya Maliasili na Utalii, Dirona Makaya amesema watumishi hao wamesimamishwa kazi kufuatia operesheni maalumu iliyofanyika kwenye vijiji na misitu na kubaini uvunwaji haramu wa miti aina ya Mkurungu.

TFS imezuia biashara ya mti wa Mkurungu kwa matumizi ya ndani au kusafirishwa nje ya nchi hadi taarifa rasmi itakapotolewa.

‘’Kufuatia uchunguzi uliofanywa, gari moja lilikamatwa likiwa na mbao 382 za mti wa Mkurungu na kuzuiliwa kwa uchunguzi ambapo watuhumiwa wawili walikamatwa,’’ amesema Makaya.

Amesema mbao 825 zilikamatwa zikisafirishwa kwa treni katika  stesheni ya Usule, Shinyanga na watuhumiwa sita  ambao ni watumishi wa reli wamekamatwa  kwa mahojiano.

Hata hivyo, majina na vyeo vya watumishi hao havikuwekwa wazi kwenye taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imeeleza mamlaka hiyo kwa kusirikiana na Kikosi cha Kuzuia Ujangili  (NTAP) wamezuia halmashauri kuendesha biashara ya miti bila idhini ya mamlaka husika.

Mkutano wa Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki (EAC) Kufanyika Jijini Arusha Ijumaa Novemba 30

$
0
0
Mkutano wa 20  wa wakuu wa nchi za Afrika Mashariki (EAC) unatarajiwa kufanyika Ijumaa Novemba 30, 2018 jijini Arusha.

Mkutano huo umetanguliwa na mkutano wa siku tatu wa baraza la mawaziri ulioanza jana Novemba 25, 2018.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo Jumatatu Novemba 26, 2018 na mkuu wa mawasiliano kwa umma wa Sekretariati ya EAC, Richard Owora  inaeleza kuwa miongoni mwa ajenda  za mkutano huo ni kupitisha itifaki mbalimbali.

Pia, kuidhinisha ripoti ya  umoja wa kisiasa ikiwa ni njia ya mpito kufikia shirikisho la kisiasa la Afrika Mashariki, mwelekeo wa haraka wa Sudan Kusini kujiunga EAC na kupitia maombi ya Somalia kujiunga kwenye jumuiya hiyo.

Mkutano huo utapitia ripoti yenye  mapendekezo ya kuona njia za kuchochea uundaji wa magari katika nchi za EAC ili kupunguza uingizaji wa magari kutoka nje pamoja na kuangalia kwa kina sekta ya viwanda vya nguo na ngozi ili kupunguza kuagiza bidhaa hizo.

“Katika mkutano wa kawaida wa wakuu wa nchi uliofanyika Kampala, Uganda Februari 23, 2018,  marais hao waliagiza baraza la mawaziri wa EAC kuchagiza uanzishaji wa kiwanda cha magari  ili kupunguza uagizaji kutoka nje na kuongeza ushindani katika kanda ya EAC,” anaeleza Owora.

Katika hatua nyingine mkutano huo utapitia mapendekezo ya baraza la mawaziri waliopendekeza EAC iwe na naibu makatibu wakuu wawili ambao watapatikana kupitia usaili na nafasi hizo zitakuwa za mzunguko kwa nchi wanachama.

Kwa sasa kila nchi mwanachama ina nafasi ya kuwa na naibu katibu mkuu anayeteuliwa na rais  wa nchi husika kisha jina lake kuidhinishwa na marais wenzake,

Pia mkutano huo utapitisha kuwa sheria miswada mbalimbali ambayo imejadiliwa na kupitishwa na Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) ambayo ni muswada wa kudhibiti bidhaa za nailoni wa mwaka 2016, muswada wa Utawala wa Mahakama ya Afrika Mashariki (EACJ) wa mwaka 2018.

Miswada mingine ni kuanzishwa taasisi ya Fedha ya EAC ya mwaka 2018 na muswada wa maboresho ya usimamizi wa forodha wa EAC.

Ray C: 'Rose Muhando anahangaika huko Kenya'

$
0
0
Msanii mkongwe wa Bongo Fleva Rehema Chalamila ‘Ray C’ amelitaka Baraza la Sanaa Tanzania(BASATA) likiwa chini ya Waziri Harrison Mwakyembe na Juliana Shonza kumsaidia Muimbaji wa Injili Rose Muhando.

Ray C ametumia ukurasa wake wa Instagram na kusema Rose Muhando ni Mtanzania, anahitaji msaada.

“Wasanii wenzangu na Watanzania kwa ujumla tunamsaidiaje dada yetu….Huyu ni wa kwetu sisi.Naamini kila mtu ana majukumu na shughuli za hapa na pale, lakini huyu dada ni mtanzania mwenzetu, ni dada yetu, ni ndugu yetu, anahangaika tu huko Kenya hana msaada..Waimba injili wote, wasanii wote na watanzania kwa ujumla tunamsaidiaje dada yetu”

“@basata.tanzania@harrisonmwakyembe @juliana_shonza……………..Naamini akipelekwa sehemu anayofaa kuwa atapata msaada,atapona na atasimama tena.Ushuhuda wangu Unatosha kuamini inawekazana.
1.Amepeperusha sana bendera yetu nje ya nchi kupitia muziki wake.
2.Ametupa amani ya moyo miaka na miaka kupitia muziki wake.
3.Ametusaidia sana kiimani kwa nyimbo zake.
4.Tulifarijika pindi tuskiapo nyimbo zake”

“DADA ROSE MHANDO,WEWE NI SHUJAA,NA SHETANI HAPENDI MASHUJAA,PIGANA NALO DADA,PIGANA NALO KIIMANI TU LITASHINDWA DADA.IMANI YAKO TU NDIO ITAKAYOKUSIMAMISHA TENA”

“BADO TUNAKUHITAJI SANA DA ROSE.🇹🇿”

Inaripotiwa kuwa Rose Muhando kwa sasa yupo nchini Kenya akiwa hana msaada na hii ni baada ya video yake kusambaa kwenye Mitandao ya Kijamii akionekana kuombewa.

Amber Rutty na Mpenzi wake waachiwa kwa dhamana

$
0
0
Msanii Amber Rutty na mpenzi wake Said Mtopari, wameachiwa kwa dhamama katika Mahakama ya Kisutu leo. Amber Rutty amedhaminiwa na ndugu yake huku mpenzi wake akidhaminiwa na Mchungaji Daudi Mashimo wa Kanisa la Emmaus Bible Church, Mbezi Luis DSM.

Amber Rutty na Said Bakary walifikishwa mahakamani hapo November 2, 2018 wakikabiliwa na kosa la kufanya mapenzi kinyume na maumbile.

Mbali na Amber Ruth na Said Bakary ambao walishindwa kudhaminiwa kwa mara tatu mfululizo mshtakiwa mwingine ni James Charles maarufu kama ‘James Delicious’ ambaye yeye alishadhaminiwa.

Makonda Ammwagia Sifa Lowassa, Amponda Kubenea

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema licha ya wabunge kuwatumia vijana kujipatia kura, wamekuwa nyuma katika kuhudhuria shughuli za msingi za maendeleo.

Makonda ameyasema hayo leo Jumanne Novemba 27, 2018 wakati wa uzinduzi wa maktaba ya kisasa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 2,100 kwa wakati mmoja na kuhifadhi vitabu 800,000.

Akizungumza katika uzinduzi huo unaofanywa na Rais John Magufuli, Makonda amesema alitarajia kuona wabunge wakiunga mkono juhudi za  maendeleo zinazofanywa, lakini wamekuwa wakikaa bila kuonyesha kuguswa kwao.

"Hata yule mbunge wa Ubungo (Saed Kubenea-Chadema) ambaye chuo hiki kipo katika jimbo lake sijamuona, kwa kweli nampongeza sana (Waziri Mkuu wa zamani, Edward) Lowasa kwa sababu anaoneka kukubali juhudi zako unazozifanya," amesema Makonda.

Mbali na hilo, Makonda amesema kabla ya Desemba makazi yote katika Jiji la Dar es Salaam ambayo hayana hati yatapimwa na hati zake kukabidhiwa kwa wamiliki.

Naye makamu mkuu wa UDSM, Profesa William Anangisye amesema milango iko wazi kwa wanafunzi wa vyuo vingine kwenda kujisomea katika maktaba ya kisasa ili kujiongezea ujuzi.

Akielezea sifa za maktaba hiyo, Profesa Anangisye mbali na kudai ndiyo maktaba inayoongoza kwa ukubwa Afrika Mashariki na Kusini. Pia, Maktaba hiyo imeunganishwa na umeme jua kwa kiwango cha kilovolt 280 zenye uwezo wa kuwasha taa na viyoyozi.

"Maktaba hii ni muhimu katika maendeleo ya chuo chetu hasa kwa wataalamu wake kujielimisha kupitia tafiti zilizotangulia," amesema Profesa Anangisye.

Pia, amesema ujenzi wa maktaba hiyo umegharimu Dola 41,280 milioni za Marekani huku chuo kikitoa Sh1.78 bilioni kwa ajili ya kugharamia nakala za vitabu na majarida.

Pia, maktaba hiyo ina ukubwa wa kilomita za mraba 4.4 huku ikiwa na kompyuta 160 zinazowezesha wanafunzi kusoma vitabu kwa njia ya mtandao.

"Tunatambua michango ya hali na mali inayofanywa na ubalozi wa China nchini katika kusaidia mambo mbalimbali ya kijamii na kiuchumi chuoni  kwetu inayotuletea maendeleo," amesema.

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala- Dar

Maajabu Ya Samli Katika Tiba Asilia Ya Kurefusha Na Kunenepesha Maumbile Ya Kiume.

$
0
0

Samli ina faida nyingi sana katika afya ya mwanadamu.

Moja kati ya faida za samli ni pamoja na kusaidia kuimarisha mifupa, kusaidia katika kupunguza uzito, kuboresha usagaji wa chakula mwilini na kutibu uvimbe kwenye ngozi.

Katika TIBA ASILIA samli  INA matumizi mengi sana.

Moja kati ya matumizi ya samli ni katika TIBA ya KUREFUSHA NA KUNENEPESHA MAUMBILE YA KIUME.

JINSI SAMLI INAVYO TUMIKA KATIKA TIBA YA KUREFUSHA MAUMBILE YA KIUME.

Katika TIBA ya KUREFUSHA na kunenepesha MAUMBILE ya kiume samli inatumika pamoja na mti ambao katika tiba asilia  unajulikana kama MWONGEZA.

Mti huu unaitwa Mwongeza kwa sababu karibu sehemu zote za mti  huu zinatumika katika tiba ya kuongeza vitu mbalimbali mwilini.

Mfano: Majani ya mti huu yanatumika katika tiba ya kuongeza hamu ya kula pamoja na kuongeza mwili wa mtu aliyedhoofika kwa maradhi kama kisukari n.k.

Mizizi ya mti huu hutumika kuongeza nguvu za KIUME.

Majani ya mti huu hutumika pamoja na majani mabichi ya mti wa mkwaju katika kuongeza maziwa kwa mama anae nyonyesha.

Katika TIBA ya KUREFUSHA na KUNENEPESHA maumbile ya KIUME magamba ya mti huu ndio yanayo tumika pamoja na mafuta ya samli.

JINSI YA KUTAYARISHA: Chukua magamba ya mti wa Mwongeza yakaushie kivulini (usikaushie juani ). Yakisha kauka yasage kisha changanya na mafuta ya samli halafu tumia kujichua kwenye uume Mara mbili kwa Siku kwa muda Siku thelathini.

Ni TIBA yenye Matokeo mazuri sana ambayo inaongeza na KUREFUSHA uume bila wasiwasi.

MAKALA HAYA YAMEANDALIWA NA DUKA LA NEEMA HERBALIST. DUKA LINALO JIHUSISHA NA UUZAJI WA DAWA MBALIMBALI ZA ASILI . TUNAPATIKANA UBUNGO JIJINI DAR ES SALAAM JIRANI NA SHULE YA MSINGI UBUNGO NATIONAL HOUSING NYUMA YA JENGO LA UBUNGO PLAZA.

WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA : 0693 005 189.

TOVUTI: www.neemaherbalist.blogspot.com

Rais Magufuli: “Lowassa washauri unaowaongoza la sivyo wataishia Gerezani”

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amempongeza Waziri Mkuu wa zamani na mjumbe wa kamati kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Edward Lowassa kwa kitendo cha kuhudhuria kuungana na serikali katika miradi ya maendeleo.

Rais Magufuli amefunguka hayo wakati akihutubia katika uzinduzi wa Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) ambapo amesema kuwa pamoja na kumshinda katika uchaguzi mkuu wa 2015 lakini bado hakuwa na kinyongo nae na kukaa kimya huku wasiohusika wakipiga kelele.


 “Siku zote huwa nasema, Lowassa umekomaa kisiasa, ndio maana unahudhuria katika shughuli za kimaendeleo, maendeleo hayana, chama, kabila, dini, wala rangi.

“Nakupongeza sana Lowassa kwa utulivu wako, Wewe ndo tuligombea Urais lakini nilipokutupa chini ukaenda ukapumzika Mzee wa watu wenye kelele wengine hata hawakugombea, Wewe unajua ktk mashindano yoyote kuna kushindwa.

“Vyama vyetu kamwe visiwe chanzo cha kututenganisha, nimeona nizungumze kwa heshima kubwa Mzee Lowassa ili wale unaowaongoza kule angalau ukawashauri otherwise wataishia kwenye Magereza”
,- Rais Magufuli


Hadi sasa, viongozi kadhaa wa upinzani, hasa Chadema waka kesi za aina tofauti katika mahakama mbalimbali nchini; baadhi wakishtakiwa kwa uchochezi, wengine kwa kutoa maneno yasiyofaa dhidi ya Rais na wengine kwa kufanya mikusanyiko bila ya kibali.

Wiki iliyopita, mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alifutiwa dhamana pamoja na mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko kutokana na kukiuka masharti ya dhamana katika kesi inayowakabili ya kufanya mikusanyiko kinyume cha sheria.

Lakini Lowassa, ambaye alikuwa kiongozi wa kwanza wa ngazi za juu kujivua uanachama wa CCM na kujiunga na upinzani, hajawahi kukumbwa na matatizo dhidi ya mamlaka, zaidi ya kuitwa kituo cha polisi kutoa maelezo.

Lowassa alihamia upinzani mwaka 2015 akipinga kitendo cha Kamati Kuu ya CCM kuondoa jina lake na la wagombea wengine wa urais na kujiunga na Chadema, ambayo ilimpa fursa ya kutimiza ndoto yake ya kugombea urais.

Katika harakati zake, Lowassa aliungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ulioundwa na Chadema, NLD, CUF na NCCR-Mageuzi na kushika nafasi ya pili, akiwa ameweka rekodi ya upinzani kupata kura nyingi. Alipata kura milioni 6.7, akiwa nyuma kidogo ya Rais Magufuli, aliyepata kura milioni 8.8.

Waziri Mkuu Aagiza Mradi Wa Maji Chato Ukamilike Kwa Wakati

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwaameweka jiwe la msingi mradi wa maji wa Imalabupina/Ichwankima wilayani Chato ambao una thamani ya sh. bilioni 8.28 na amewaagiza viongozi wa wilaya hiyo wahakikishe unakamilika kwa wakati.

Waziri Mkuu amesemaSerikali kupitia Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani, itahakikisha wananchi katika maeneo yote nchini wanapata huduma ya maji safi na salama karibu na maeneo yao ya makazi.

Ameyasema hayo leo (Jumanne, Novemba 27, 2018) alipozungumza na wananchi kwenye kijiji cha Nyamirembe baada ya kukagua na kuweka jiwe la msingi katika mradi huo wa maji wakati akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake mkoani Geita.

Amesema Serikali imedhamiria kuhakikisha wananchi wote nchini wakiwemo na wa wilaya ya Chato mkoani Geita wanapata huduma ya maji safi na salama karibu na makazi yao, hivyo amewataka waendelee kuwa na imaji na Serikali yao.

“Serikali ya Awamu ya Tano ina mikakati mizuri inayolenga kumaliza tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwenye maeneo mbalimbali nchini vikiwemo na vijiji vya wilaya ya Chato ili kuwawezesha wananchi kupata maji.”

Waziri Mkuu ameagiza mradi huo ukamilike kwa wakati kwa kuwa Serikali inahitaji kuona wananchi wakinufaika na huduma hiyo. Mradi huo ulianza kujengwa Mei, 2017 na ulitakiwa ukamilike Mei, 2018 ila kutokana na changamoto mbalimbali unatarajiwa kukamilika Februari 2019.

Awali,Mkuu wa wilaya ya Chato Mhandisi, Mtemi Simeon alisema mradi huo unatarajiwa kuhudumia watu takribani 59,609 katika vijiji 11 vilivyopo kwenye kata nne za Nyamirembe, Ichwankima, Kachwamba na Kasenga.

“Vijiji vitakavyonufaika na mradi huu ni Nyamirembe, Kalebezo, Nyambiti, Busalala, Imalabupina, Ichwankima, Kachwamba, Ipandikilo, Idoselo, Igagula na Mwangaza. Tayari vituo 240 vya kuchotea maji vimeshakamilika na matenki nane kati ya tisa yamekamilika pamoja na mabirika 10 ya kunyweshea mifugo.”

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Ajali Mbaya ya Gari Yaua Watu 16 Tarime

$
0
0
Miili ya watu waliofariki dunia katika ajali iliyohusisha magari mawili ya abiria jana Novemba 26, 2018 itazikwa katika eneo ilipotokea ajali hiyo kijiji cha Komaswa wilayani  Tarime Mkoa wa Mara.

Akizungumza leo Jumanne Novemba 27, 2918 mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima amesema uamuzi huo umechukuliwa na kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa kutokana na ushauri uliotolewa na kamati ya Taifa ya maafa.

Amesema hadi sasa majina  12 kati ya 16 ya waliofariki dunia yamejulikana licha ya miili yao kutotambulika kutokana na jinsi ilivyoungua.

“Isipokuwa miili miwili  ambayo ilitambuliwa ukiwemo wa dereva na mwingine uliotambulika baada ya kukutwa na cheni shingoni,” amesema Malima.

Amesema mazishi hayo yatafanyika kesho Novemba 28, 2019 saa nne asubuhi, kwamba mabaki yaliyotokana na miili kuungua yatakusanywa na kuzikwa eneo hilo.

Amesema baada ya mazishi eneo hilo utajengwa mnara kwa ajili ya kumbukumbu.


Rudisha Heshima ya Ndoa Yako.....Pata Tiba Bora ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Wanaume wengi hawawaridhishi wake au wapenzi wao kwa kutokuwa na nguvu za kiume au uume mdogo? 

Kawaida mwanamke huwa anachukua dakika saba 7 adi kumi 10 ili aweze kufika kileleni na wakati wanaume wengi kwa sasa hutumia dakika tatu 3 hadi tano 5 ameshafika kileleni , hapo utagundua kabisa mke au mpenzi wako hujamtendea haki yake. Dr Nyalobi  anakuletea dawa imara na yenye nguvu tatu?

Simpo power; Hutibu matatizo yafatayo;

1.itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-20 kwa tendo la kwanza

 2. itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi mara nne 

3 Huimalisha misuli iliyolegea na kusinyaa 

4 Hutoa uchovu pale umalizapo kufanya tendo

 Je kwa nini uzidi kuona aibu pale ukutanapo na mpenzi wako kwa sabubu uume wako mdogo na mwembamba? 

Promix; hii ni dawa ya kuongeza uume saizi upendayo.Dawa zetu ni za mitishamba na hazina madhara yoyote na ni tofauti na ulizowai kutumia ata wazee hutumia 

Mkuya; hii ni dawa ya kisukari dozi siku 21 

Mwaru; hii ni dawa ya uzazi hufungua mirija ya uzazi ata kama uzazi umefungwa

Markusi; ni dawa ya presha zipo dwa za korodani kuvimba,, vindonda vya tumbo, kupunguza kitambi, na minyama uzembe 

Fika ofisini kwetu Buguruni Malapa na Mwanza yupo wakala wetu au piga simu 0752348593 -Dokta Nyalobi

Diamond akabidhi rasmi kadi za bima ya Resolution kwa wakazi wa Tandale

$
0
0
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Nasib Abdul, Diamond Platinum ameshakamilisha ahadi yake ya kuwapatia kadi ya huduma ya bima ya afya wananchi wa Tandale.

Diamond aliwahi kutoa ahadi hiyo wakati wa sherehe yake ya kuzaliwa ya kuwa angewapatia kadi hizo wananchi 1000 wa eneo hilo ikiwa ni sehemu ya mchango wake kwao.

Wakazi hao wamepewa msaada huo wa bima ya afya kupitia kampuni ya bima ya Resolution Insurance ambapo Mkurugenzi Mtendaji wake Maryann Mugo alibainisha kuwa huduma hiyo ni kwa ajili ya watu wanne kwenye familia.

Alisema,”sisi tunapenda kuwahudumia wananchi kujipatia huduma nzuri za afya na kwa kile alichokifanya msanii Diamond kuwasaidia wakazi hawa huduma ya bima basi ni fahari kubwa kwetu”.

Kwa upande wake msanii Diamond aliyewakilishwa na dada yake Esma kwenye makabidhiano hayo aliwataka wananchi wa Tandale kutumia vema huduma za bima hiyo na kujiwekea akiba ya fedha ili mwisho wa siku huduma hiyo ya mwaka mmoja ikiisha waweze kujihudumia kama kawaida.

Rais Magufuli ahimiza matumizi sahihi ya misaada Inayotolewa na Nchi Mbalimbali

$
0
0
Rais Dk John Magufuli amesema ni wajibu wa kila mtanzania kuhakikisha anaitumia misaada inayotolewa na wafadhili ili ilete faida kwa vizazi vilivyopo na vijavyo.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Jumanne Novemba 27, alipokuwa akizindua maktaba mpya ya kisasa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambayo imejengwa kwa ufadhili wa serikali ya China kupitia kampuni ya ujenzi Jiangsu Jiangdu kutoka nchini humo.

Maktaba hiyo ina majengo mawili, moja likiwa maktaba yenyewe na lingine ni la Tasisi ya Conficius ambayo itakuwa ikifundisha tamaduni za kichina kwa wanafunzi wa UDSM na watanzania wengine, ukumbi wa mikutano wenye uwezo wa kukaa watu 600, inahudumia wasomaji 2100 kwa wakati mmoja na kuhifadhi vitabu 800, 000.

“Nitashangaa sana kama siku moja nitapita hapa na kukuta ukuta umechorwa chorwa  na makaratasi yamechanwa, maktaba hii itunzwe ili iwe ukumbusho kwa watanzania na wageni wanaokuja kututembelea lakini pia iwe kumbukumbu ya ushirikiano wetu na China, “ amesema.

Aidha pia Rais Magufuli ameipongeza Bodi ya ya Elimu ya Juu (HELSB) kwa kutoa mikopo kwa wakati ambapo asilimia 60 ya wanafunzi kwa mwaka wa kwanza ndio wamepata mikopo na kuwataka waendelee kufanya kazi kwa juhudi ili hao waliobaki wapate ziwasaidie  kupata elimu yao.

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 38

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA
“Ehee niambie”
“Mama yako amepatika”
“Kweli?”
Niliuliza kwa shauku iliyo ambatana na furaha kubwa sana.
“Ndio amepatika, ila…….”
Mwanasheria alizungumza kwa sauti ya upole na unyonge kidogo.
“Ila nini?”                   
Nilimuuliza mwanasheria huku furaha yangu ambayo nilikuwa nayo ikaanza kunipotea taratibu.
“Hali yake sio nzuri, katika harakati za kumkomboa kwa bahati mbaya alipunyuliwa na risasi ya kichwani mwake na kumfanya apoteze fahamu, na ninavyo zungumza hivi sasa, wapo njiana wanakuja naye nchini humu”
Nikajikuta nikinyon’gonyea na taratibu nikakaa chini na kumfanya Camila na watu wengine kunishangaa, kwa maana ni muda mchache tu wametoka kuniona nikiwa nimejawa na furaha sana

ENDELEA
Camila akachuchumaa kwa haraka, akaichukua simu yangu mkononi mwangu na kuiweka sikioni.
“Ni Camila ni nini kinacho endelea?”
Camila aliuliza kwa shahuku kubwa sana, huku akinitazama usoni mwangu. Habari aliyo ipata hata yeye mwenyewe akaonekana kumnyong’onyeza. Muongozaji wa tangazo hili akatufwata sehemu tulipo.
 
“Vipi jamani kuna tatizo?”
Camila akaibi kwa kutingisha kichwa huku akimtazama muongozaji huyu wa filamu.
“Nahitaji kwenda uwanja wa ndege sasa hivi”
Nilizungumza huku nikimtazama Camila usoni mwake.
“Hakuna tatizo Ethan”
Muongozaji wa tangazo hili alizungumza, taratibu Camila akaninyanyua akisaidia na muongozaji huyu wa tangazo, nikaingizwa ndani ya gari, kisha baada ya muda kidogo Camila naye akaingia ndani ya gari na safari ya kuondoka eneo hili ikaanza huku tukiwa tumetanguliwa na gari la walinzi wa mama Camila. Furaha na amani vikanipote kabisa moyoni mwangu. Akilini mwangu, akili yangu inamuwaza tu mama yangu ambaye hali yake ni mbaya sana.
 
“Mume wangu usijali kila jambo litakwenda vizuri sawa?”
Nikajibu kwa kutingisha kichwa tu na safari ikaendelea. Ikatugarimu kama lisaa moja kufika katika kiwanja cha ndege. Nikamkuta mwanasheria akiwa katika eneo hili akimsubiri mama yangu kufikishwa hapa.
“Itagarimu masaa ngapi kufika hapa?”
“Kama masaa lisaa moja na dakika aroboini na tano hivi. Na nimesha andaa magadaktari bingwa. Akipokelewa ataingizwa kwenye helicopter ya hospitali na atawahishwa hospitalini”
“Nashukuru kwa kila jambo”
Nilizungumza kwa sauti ya unyonge sana. Masaa yakazidi kusonga mbele huku kila baada ya nusu saa mwana
sheria aliwasiliana na vijana tulio wapa kazi ya kwenda kumkomboa mama yangu.
“Wapo wapi?”
 
“Kama baada ya dakika kumi ndege ikatua hapa”
Mwanasheria alizungumza huku akitazama saa yake ya mkononi. Madaktari wapatao wanne wakakaa tayari kwa ajili ya kumpokea mama. Ndani ya dakika kumi alizo niambia mwana sheria, ndege maalumu ya kukodi taratibu ikatua kwenye uwanja huu. Wahudumu wa maalumu wa uwanja huu, wakaanza kukimbilia kwenye eneo ndege hiyo ilipo simama huku wakiwa wameongozana na madaktari wote wanne walio beba kitanda maalimu cha kukunjua. Sikuona haja ya mimi kuendelea kuhushudia mambo kwa mbali, nikaanza kukimbia kuelekea kule walipo. Nikafika na kukuta wakimtoa mama yangu ndani ya ndege hii, macho yakanitoka sana, kwani ni miaka mingi sana sijawahi kumuona mwana mama huyu. Kumbu kumbu kadhaa zikaanza kujirejea kichwani mwangu juu ya maisha yangu na huyu mwana mama, ila kila nilipo jaribu kuzikumbuka vizuri, nikashindwa kabisa.
“Kitanda hichi kikaanza kusukumwa hadi kwenye gari la wagonjwa, likafungwa kwa haraka na kuelekea katika uwanja mdogo wa helicopter.
 
“Mkuu kina helicopter ya kampuni, ipo hapa unaja wa ndege tayari kwa kuelekea hospitalini”
Mwanasheria alizungumza huku akinitazama usoni mwangu.
“Sawa twende”
Tukaanza kukimbia kuelekea kwenye helicopter hiyo, huku Camila naye akiwa hayupo mbali nami. Tukaingia ndani ya helicopter hiyo na safari ya kuelekea hospiyalini ikaanza. Sikuzungumza kitu chochote hadi tukafika katika uwanja wa helicopter wa hospitali hii kubwa na nzuri. Tukashuka na kupokelewa na nesi mmoja na moja kwa moja tukaanza kupelekwa kwenye chumba cha upasuaji. Uzuri wa eneo hili la chumba cha upasuaji kuna kioo kikubwa ambacho mtu ukiwa nje ya chumba hichi unaweza kuona kinacho endelea ndani ya chumba. Tukawashuhudia madaktari jinsi wanavyo endelea na kuifanya kazi yao ya kuhakikisha kwamba wanayaokoa maisha ya mama yangu yanakuwa salama. 

Baada ya nusu saa mama Camia naye akafika katika eneo hili, kwa haraka akanikumbatia kwa nguvu huku akinipiga piga mgongoni mwangu taratibu. Machozi yakanimwagika na nikashindwa kujibu kitu chochote. Dada Mery naye akafika katika eneo hili, alipo tuona kidogo akaonekana kujawa na mshangao kwa maana toka nianzishe mchakato wa kumtafuta mama yangu, sikuwahi siku hata moja kumueleza dada Mery wala bibi Jane Klopp.
“Ethan ni kitu gani kinacho endelea?”
Dada Mery alizungumza huku akinisogelea karibu yangu. Akanitazama usoni mwangu kwa sura iliyo jaa wasiwasi mwingi.
 
“Ni mama”
“Mama yupi Ethan?”
“Mama yangu mzazi”
“Ohoo jamani?”
Dada Mery alizungumza kwa upole na unyonge mkubwa sana. Taratibu akanikumbatia huku akinibembeleza, Gafla tukawaona madaktari wakiwa katika harakati harakati nyingi ndani ya chumba hicho na wakanifanya niweze kukimbilia kwenye kioo hichi na kutazama ndani. Madaktari wengine wazee wakaingia ndani ya chumba hichi jambo lililo tufanya tujawe na wasiwasi mwingi sana.
Kitu kilicho zidi kutuchanganya ni mara baada ya mapazia ya kijani kufungwa kwenye vioo hivi na tukashindwa kuona kinacho endele ndani ya chumba hichi.
 
“Ni nini kinacho endelea?”
Niliuliza kwa sauti ya unyonge, hapakuwa na mtu aliye weza kunijibu. Camila akajikaza na kunikumbatia kwa nguvu.
“Nahitaji kuingia ndani humu”
“Ethan huwezi kufanya hivyo, kumbuka madaktari wapo kwenye kazi mume wangu”
“Nimesema ninataka kuingia”
Nilizungumza kw ukali sana huku nikimuachia Camila, kila mtu anaye nitazama akaonekana kunishangaa sana kwani maamuzi niliyo yafanya ni ya ukali sana. Nikafungua malango wa chumba hichi, manesi  wawili wakaniwahi kwa haraka hata kabla sijapiga hatua yoyote.
“Tafadhali, tunakuomba uweze kutoka humu ndani Mr Ethan”
“Nahitaji kuzungumza na mama yangu”
Nilizungumza kwa sauti ya unyonge ila iliyo jaa msisitizo mkubwa sana.
 
“Jinsi unavyo endelea kupoteza muda kuwemo ndani ya hichi chumba ndivyo jinsi unavyo zidi kuiweka hali ya mgonjwa katika wakati mbaya zaidi. Tafadhali toka ndani ya chumba”
“Ni mama yangu”
“Ndio tunajua, ila acha tufanye kazi yetu Mr Ethan”
Mwanasheria akanishika mkono na taratibu akanitoa ndani ya chumba hichi.
“Nahitaji kuzungumza nawe”
Nilimuambia mwana sheria huku nikimtazama usoni mwake. Nikaanza kuondoka katika eneo hili pasipo kumuaga mtu yoyote. Tukafika katika kordo ya kuelekea katika eneo la chumba cha upasuaji.
“Ndio mkuu”
“Endapo mama yangu atakufa, nahitaji kumuua mtu mmoja baada ya mwengine walio husika katika hili jambo. Umenielewa?”
 
Nilizungumza kwa hasira huku nikimtazama mwana sheria usoni mwake.
“Sawa mkuu nimekuelewa”
“Ninaweza kuzungumza na vijana wako?”
“Si kwa muda huu muheshimiwa. Inabidi tuweze kukaa hapa tufahamu hali ya mama ina endeleeaje”
“Nalijua hilo, ila ninataka kuhakikisha kwamba nao wanapitia magumu kama magumu haya ambayo ninayapitia mimi kwa muda huu”
“Nimekuelewa muheshimiwa”
“Nitengenezee mfumo wa kuhakikisha kwamba ninamfahamu adui yangu mkuu na timu yake nzima aliyo shirikiana nayo”
“Sawa mkuu”
Nikarudi katika chumba cha kusubiria huduma, Camila akanisogelea karibu na sehemu niipo simama na akanishika kiuno changu.
“Kila kitu kinakwenda kuwa salama mume wangu sawa”
“Nashukuru”
Nilimjibu Camila kwa ufupi, akanibusu mdomoni mwangu na wala sikuweza kuwa na hisia za aina yoyote kwake. Baada ya masaa mawili na nusu mlango ukafunguliwa na akatoka daktari mkuu wa oparesheni hii. Watu wote tukasimama mbele yake huku tukimtazama usoi mwake.
“Poleni sana kwa kusubiria”
 
“Tunashukuru”
Mama Camila alijibu kwa kujiamini.
“Tunashukuru Mungu upasuaji umeenda vizuri, na tumefanikiwa kutoa damu iliyo kuwa imeganda kwenye ungong”
“Ohoo asante Mungu”
Mama Camila alijibu kwa unyenyekevu mkubwa sana.
“Sasa hivi tutamtoa mgonjwa humu na kumpeleka katika chumba cha wagonjwa mahututi. Humo atakaa kwa muda hadi pale hali yake itakapo kaa vizuri”
“Je anaweza kuzungumza?”
Nilimuuliza daktari huku nikimtazama usoni mwake.
“Hapana, kwa sasa hawezi kuzungumza, na kuna mambo kadhaa tutayazungumza ofisini, au kama nyote hapa ni wana familia basi ninaweza kuyazungumza sasa hivi?”
“Wewe zungumza tu dokta”
Nilitoa ruhusa hii kwa maana tuliopo hapa wote ni watu ambao ni msaada mkubwa sana kwangu.
“Kuna matatizo yamempata mama, nitayaeleza kwa hali ya kawaida tu na si kitaaamu sana.”
 
“Wewe zungumza tu daktari”
“Mama hato kuwana uwezo wa kukumbuka mambo yaliyo tokea na wala hato kuwa na uwezo wa kuona tena labda tu zitokee baraka za mwenyezi Mungu tu aweze kurudi katika hali ya kawaida”
Mwili mzimza ukazizima, nikahisi kunyong’onyea miguu yangu, mwana sheria akawahi kunishika kabla sijaanguka chini.  Kitanda alicho lazwa mama kikatolewa humu ndani huku kitanda hichi kikiwa kimezungukwa na manesi sita.
Tukaongozana na manesi hawa hadi kwenye chumba kimoja kikubwa, wakatuomba tuwasubirie waandae chumba hicho vizuri kisha sisi nasi tuingie kumtazama. Baada ya dakika kama kumi na tano tukaruhusiwa kuingia ndani ya chumba. Nikaingai peke yangu ndani ya chumba hichi na kumkuta mama akiwa anapumulia amshine huku nesi mmoja akiwa amesimama pembeni ya kitanda hicho. Machozi yakazidi kunibubujika nikiwa ninamuangalia mama yangu, hali yake kwa kweli ni mbaya sana. Mwili wake ume dhohofika na anaonekana ni mwana mama amabt maisha yake yalikuwa ni mabaya huko alipo kuwaa kiishi.
 
“Mama”
Niliita kwa sauti ya unyonge kiasi huku nikijaribu kumshika mama mkono. Mama hakuweza hata kupepesa jicho lake, machozi yakaendelea kububujika usoni mwangu, nesi alipo ona hali yangu inazidi kuwa mbaya akaniomba niweze kutoka ndani ya chumba hichi. Sikuweza kubisha maamuzi ya nesi huyu, nikatoka ndani ya chumba hichi huku nikiwa nimejawa na dukuduku kubwa sana moyoni mwangu. Wakaiingia watu wengine nilio ambatana nao mmoja baada ya mwengine kumuona mgonjwa. 
 
“Mungu atamsaidia mama atapona sawa mwanangu Ethan”
Mama Camila aliniambia mara baada ya kutoka katika chumba cha ICU.
“Sawa mama”
“Inabidi uende kula chakula sasa”
“Mama sijikii kula”
“Jitahidi tu mwanangu sawa”
“Sawa”
“Ethanm nitakwenda nyumbani na nitamueleza mama hili lililo jitokeza sawa mdogo wangu”
“Sawa dada”
“Hakikisha unapata chakula kama alivyo kueleza dada hapa”
“Poa poa”
Dada Mery akaniaga na kuondoka zake. Mwanasheria akaniita pembeni kwa ishara, nikamfwata.
“Vipi mkuu nikuandalie chumba katika hoteli ya hapa karibu?”
Nikaa kimya kwa muda huku nikifikiria cha kuzungumza.
“Nahitaji kukaa hapa”
 
“Sawa ngoja nikakutafutie chakula”
“Hapana, sihitaji chakula kwa sasa, nipo vizuri”
“Sawa mkuu basi naomba na mimi niweze kuelekea nyumba nikapumzike kidogo”
“Sawa wewe chukua muda wa kutosha pale nitakapo kuhitaji basi nitakufahamisha uweze kuja hapa”
“Sawa”
Mwanasheria na yeye akaondoka eneo hili na kuniacha nikiwa na Camila.
“Mume wangu naomba nikaongozane na walinzi nikachukue chakula kisha nirudi hapa, nitakuwa nawe na sinto kuacha peke yako sawa mume wangu”
“Sawa”
Camila akaninyonya midomo yangu kidogo kisha akaondoka katika eneo hili. Ethan mwenzangu akakaa pembeni yangu huku akinitazama usoni mwangu.
 
“Vipi mbona una huzuni sana?”
“Kwani hujui kilicho tokea Ethan?”
“Sikuhizi hunishirikishi mambo yako rafiki yangu, hadi pale utakapo kuwa na shida ndio una nikumbuka”
“Sio hivyo Ethan”
“Ila?”
“Kichwa changu hakikuwa vizuri kabisa”
“Sio hakikuwa vizuri rafiki yangu, kwa swala dogo kama hili kweli ulishindwa kunishirikisha mimi, hadi umeamua kutumia garama nyingi sana kwa vitu hivi?”
Ethan alizungumza kwa kulalamika.
“Samahani kwa hilo”
“Njoo nikuonyeshe kitu”
Ethan alizungumza huku akinyanyuka hapa pembeni yangu. Nikanyanyuka na tukaingia katika chumba cha alicho lazwa mama.
 
“Huyu ni nani yako?”
“Ethan aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.
“Ni mama yangu?”
“Unaikumbuka sura ya mama yako vizuri?”
Swali la Ethan likanifanya nikae kimya kwa muda huku nikimtazama mama huyu.
“Hapana”       
“Kwa nini umeamini kwamba huyu ni mama yako?”
“Ethan, moyoni mwangu, ninahisi kabisa sura ya mama yangu”
“Acha ujinga Ethan, ni watu wangapi weusi ambao una fanana nao, unataka kusema kwamba ni ndugu zako. Hapa umechezewa mchezo wa ajabu. Sasa ni hivi huyu sio mama yako, mumepumbazwa na unapo pelekwa ni kufilisiwa kila kitu chako na utabambikiwa kesi ya mauaji umenielewa”
Maneno ya Ethan kidogo yakanifanya nishikwe na bumbuwazi huku nikimtazama usoni mwake, kwani haya anayo nieleza sijawahi kuyafikiria kabisa kwenye akili yangu.
                                                                                                       ITAENDELEA   

Huna Sababu Ya Kuaibika tena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images