Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Video Mpya Ya Rosa Ree- Banjuka

$
0
0
Rapper wa Kike Kutoka Tanzania anayefanya vizuri , Rosa Ree ameachia Video ya Wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Banjuka....

Unaweza Itazama Hapa Chini

Rais Mstaafu Benjami Mkapa Kuagwa Rasmi UDOM Kesho

$
0
0
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), ambaye pia ni Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, anatarajiwa kuagwa rasmi kesho chuoni hapo baada ya kumaliza kipindi chake.

Rais Mkapa amekuwa mkuu wa chuo hicho tangu kianze mwaka 2007 hadi sasa.

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo hicho (Taaluma), Prof. Peter Msoffe, akizungumza na waandishi wa habari, alisema ataagwa kwenye mahafali ya tisa yanayotarajiwa kufanyika Novemba kesho chuoni hapo.

Alisema kwa mujibu wa hati idhini ya chuo, Mkapa anatarajiwa kumaliza muda wake Machi 2019 na kwamba kwa kuwa ni mahafali yake ya mwisho, wameamua kumuaga kesho.

Alisema Mkapa ameshakitumikia chuo kwa kipindi cha miaka 11 zikiwa ni awamu mbili tangu kuanzishwa kwake.

Alisema UDOM itaendelea kuvuna busara zake hata baada ya kumaliza na amekuwa nguzo imara ya chuo hicho.

Aidha, Prof. Msoffe alisema katika mahafali hiyo ya tisa ya mwaka huu kutakuwa na jumla ya wahitimu 7,122 kwa ngazi mbalimbali.

Alisema mahafali hiyo itatanguliwa na kongamano la tisa la chuo hicho litakalofanyika leo na litakaloongozwa na Balozi wa India nchini, Sandeep Arya, ambaye atawasilisha mada juu ya maisha ya mwanzilishi wa Taifa la India, Mahatma Gandhi na mchango wake katika jamii.

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Yaanza Kupokea Rufaa za Mikopo 2018/2019

$
0
0
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inawafahamisha wanafunzi wote wa taasisi za elimu ya juu kuwa leo, Jumatano, Novemba 21, 2018 imeanza kupokea rufaa za mikopo kwa mwaka wa masomo 2018/2019 kwa kwa njia ya mtandao.

Dirisha la kuwasilisha rufaa hizo litakuwa wazi kwa siku tano, kuanzia leo hadi Jumapili, Novemba 25, 2018 na linapatikana kupitia http.olas.heslb.go.tz. Wanafunzi watakaokua wametimiza masharti na sifa watapangiwa mikopo kabla ya mwisho wa mwezi huu wa Novemba, 2018.

HESLB imefungua dirisha hili ili kutoa fursa kwa wanafunzi wahitaji ambao hadi sasa hawajapata mkopo au hawajaridhika na kiwango cha mkopo walichopangiwa, kuwasilisha maelezo na nyaraka kuthibitisha uhitaji wao. Maelekezo ya kina kuhusu namna ya kuwasilisha na nyaraka zinazohitajika yanapatikana kwenye mtandao (http.olas.heslb.go.tz).

Ili kuwasilisha taarifa na nyaraka zake za rufaa, mwanafunzi anapaswa kufungua mtandao huo, kusoma maelekezo na kutumia namba yake ya mtihani wa kidato cha nne aliyoombea mkopo kwa mwaka huu (2018/2019) kuingia na kuwasilisha taarifa zake kwa njia ya mtandao tu.

Hadi leo (Jumatano, Novemba 21, 2018), jumla ya wanafunzi 37,969 wa mwaka wa kwanza wamepangiwa mikopo na wanaendelea na masomo katika taasisi mbalimbali za elimu ya juu nchini.

Katika mwaka huu wa masomo, Serikali imetenga TZS 427.5 bilioni kwa ajili ya mikopo ya elimu ya juu ambazo zitawanufaisha wanafunzi zaidi ya wanafunzi 120,000wakiwemo 83,000 wa mwaka wa pili, tatu na kuendelea waliopo vyuoni ambao wamefaulu mitihani yao ya mwaka.

Imetolewa na:
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
DAR ES SALAAM
JUMATANO, NOVEMBA 21, 2018

Kwanini Baadhi ya Wanaume Wana Maumbile Mafupi na Upungufu wa Nguvu za Kiume? Suluhisho Hili Hapa

$
0
0
KWANINI BAADHI YA WANAUME WANA MAUMBILE MAFUPI NA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME... DR SITTA NDO SULULISHO LAKO

Tatiza, hili limekuwa likiwaathiri watu wengi sana kisaikolojia hasa baadhi yao kujiona wako tofauti na wanaume wengine. Kwa kawaida, mwanaume anatakiwa awe na uume, usiopungua nchi 6-7au-8 ,vinginevyo mtu huyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo... baadhi ni  upungufu wa vichocheo vya, HORMONES ZA CETROGEN .

SUPER MIZIZI, ni dawa inayozalisha HORMONES ZA CETROGEN,na kufanya, uume kukuwa na kuongzeka sazi utakayo na kuzibua mrija iliyosinyaa,

NSHOLA; ni dawa bora, ya kurudisha nguvu za kiume kwa kutibu kabisa  tatizo hilo na kukupa  hamu ya  kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara nne 4 bila kuchoka 

Pia  kuna dawa za kutibu presha ya kupanda na kushuka, kisukari , kuondoa mafuta  mwilini na maumivu ya mgogo kiuno, matazo, ya hedhi kwa wanawake, hedhi zisizokuwa na mpangilio.

NKANYA; ni dawa ya mvuto wa kimapenzi ,mchumba mpenzi aliyekuacha, mke, mme atakurudia .

NKOMA; Ni dawa kuongeza HIPS na mguu wa bia kwa wadada ,

NGAKAMA ,ni dawa ya kutibu miguu kufa ganzi na kuwaka moto, huduma zetu ,zipo ,vizuri, popote pale dawa utaletewa! 

DR SITTA, amebobea kwa tiba asilia 

Kwa DAR ANAPATIKANA MBAGALA ZAKHEM, SONGEA BOMBAMBILI, SHINYANGA- KAHAMA MJINI, 

KWA MAELEZO ZAIDI  PIGA SIMU; 0763172670/ 0715172670,/

WOTE  MNAKARIBISHWA... KAMA, UTAKUWA NA TATIZO, UTAHUDUMIWA,

TAKUKURU Yamtia Mbaroni Mchumi mwandamizi Jijini Mwanza

$
0
0
Mchumi mwandamizi wa Mwanza, Kaswalala Elisha anashikiliwa na Takukuru mkoani hapa kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa ya Sh300, 000 kutoka kwa mfanyabiashara.

Kwa kawaida Takukuru hutoa taarifa za watu wanaowashikilia kufanya makosa muda mfupi kabla ya kupelekwa mahakamani, lakini naibu mkuu wa Takukuru mkoa, Emmanuel Stenga alizungumzia suala la ofisa huyo wa Serikali bila ya kueleza atafikishwa mahakamani lini.

Stenga aliwaambia waandishi wa habari jijini Mwanza leo kuwa mtuhumiwa huyo alishirikiana na mtu mwingine kutenda kosa hilo Novemba 16, akiwa katika ofisi yake iliyopo katika majengo ya ofisi ya mkuu wa mkoa.

Alisema siku moja kabla ya kunaswa kwenye mtego uliowekwa na maofisa wa Takukuru, mtuhumiwa huyo pamoja na mwenzake ambaye bado anatafutwa walikuwa wakiwasiliana kwa njia ya simu na mfanyabiashara huyo anayejihusisha na uuzaji wa vifaa vya maabara (jina linahifadhiwa) aliyefikisha taarifa Takukuru.

“Pamoja na mambo mengine, watuhumiwa walimtuhumu mfanyabiashara huyo kukwepa kodi na kuiuzia Serikali bidhaa feki na hivyo kumtaka kutoa Sh5 milioni ili asichukuliwe hatua za kisheria,” amesema Stenga

Amesema kosa hilo ni kinyume cha kifungu cha 15 cha Sheria ya Takukuru ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007.

Kampuni ya Reginald Mengi Kuanzisha kiwanda cha kuunganisha magari Hapa nchini

$
0
0
Kampuni ya IPP Automobile Ltd imeingia ubia na Kampuni ya Youngsan ya Korea kusini kuwekeza katika sekta ya usafirishaji na uchukuzi kwa kuwa na kiwanda cha kuunganisha magari nchini.
 
Gari la mwanzo kutoka katika uwekezaji huo wa zaidi ya bilioni 22, litaingia sokoni kati ya Septemba na Oktoba mwaka 2019.
 
Kiwanda hicho kinachotarajiwa kuunganisha magari 1000 kwa mwaka kitatoa ajira za moja kwa moja kwa wananchi 500, idadi inayotarajiwa kuongezeka kadri ya muda unavyokwenda.
 
Kiwanda hicho kitajengwa eneo la Kurasini, ujenzi utaanza mwanzoni mwa mwaka ujao.
 
Makubaliano ya uanzishwaji wa kiwanda hicho yalitiwa saini jijini Dar es Salaam jana kati ya Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Reginald Mengi na Bw Thomas Choi Mkurugenzi na Mwakilishi wa Kampuni ya Youngsan Glonet ya Korea ambao ndio wawakilishi wa kiufundi wa kampuni ya Zyle Daewoo Commercial Vehicle na Hyundai Motor Corporation ya Korea Kusini huku tukio hilo likishuhudiwa na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Song Geum-young .
 
Katika mazungumzo wawakilishi hao na balozi walisema kuanzishwa kwa kiwanda hicho, kumelenga kuunga mkono juhudi za maendeleo nchini.
 
Akizungumzia hatua hiyo, Mwenyekiti Mtendaji  wa IPP,Dk. Reginald Mengi alisema kuanzishwa kwa kiwanda hicho, ilikuwa moja ya ndoto zake kama hatua ya kuitikia mwito wa Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais John Magufuli, inayosisitiza kasi ya ujenzi wa viwanda nchini.
 
“Hakuna kinachoshindikana ukiwa na nia, hata Rais wetu anapambana katika mambo ambayo wengi waliona yanashindikana, amenunua ndege na  kufanya mengine mengi..hii ni hatua kubwa katika kukuza maendeleo yetu,” alisema Dk. Mengi.
 
Alisema kiwanda hicho kikianza kazi, kitatoa ajira kwa Watanzania, pia kitasaidia kuongeza mzunguko wa biashara katika Afrika Mashariki na Kati na kuiingizia mapato serikali kupitia kodi mbalimbali.
 
Aidha, alisema mipango yake ya baadaye ni kuhakikisha wanajenga kiwanda chenye uwezo wa kutengeneza magari kuanzia mwanzo hadi inapokamilika kutoka katika hatua hiyo ya uunganishaji, jambo alilosema litazidi kuitangaza Tanzania.
 
Magari yanayotarajiwa kuunganishwa kupitia kiwanda hicho ni mabasi, malori na magari madogo, ambapo kwa mujibu wa Balozi wa Jamhuri ya Korea, Mh. Song Geum-young magari hayo ni ya kisasa.
 
Alisema Jamhuri ya Korea imepiga hatua kubwa katika uzalishaji wa magari na kwamba anaamini kuwa kuanzishwa kwa kiwanda hicho nchini, kutasaidia kuleta mapinduzi katika sekta ya viwanda na kuleta tija kimaendeleo na amewahakikishia Watanzania kuwa Korea ni wajuzi wa kutengeneza magari yenye viwango vya juu vya ubora duniani.
 
Magari yatakayotoka katika kiwanda hicho ni ya biashara ya tani 2.5; 3.6 na malori  ya tani 18 hadi 28; mabasi ya mita saba,9 na 12 na magari ya kujinafasi  (SUV) na magari madogo mengine.

Kilichoendelea Leo Mahakamani Katika Kesi ya Wema Sepetu

$
0
0
Upelelezi wa kesi inayomkabili mcheza filamu, Wema Sepetu katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu bado haujakamilika.

Hayo yameelezwa Leo Novemba 21 na Wakili wa Serikali Jenifer Masuri wakati kesi hiyo ilipotajwa mbele ya Hakimu Mkazi, Mwita Kasonde.

Wema alipanda kizimbani saa 3:30 asubuhi na kushuka kizimbani hapo saa 3:32 asubuhi.

Akiwa kizimbani hapo, wakili Masuri aliieleza mahakama kuwa kesi ilipangwa kwa ajili ya kutajwa upelelezi wake bado haujakamilika.

Hivyo akaiomba mahakama iipangie tarehe nyingine ya kuitaja ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la.

Baada ya wakili huyo kueleza hayo, Wakili wa Wema, Ruben Simwanza alidai kuwa hana pingamizi.

Hakimu Masonde baada ya kusikiliza Maelezo hayo aliiahirisha kesi hiyo hadi Desemba 12, mwaka huu.

Msanii huyo alipofikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza alitakiwa kutoweka video zinazohusiana na ngono wala Maneno yoyote yenye muelekeo huo katika mtandaoni wake wa kijamii wa Instagram

Mshtakiwa huyo alielezwa hayo na Hakimu Kasonde wakati akipatiwa masharti ya dhamana ya kuwa na mdhamini mmoja aliyesaini bondi ya Sh 10 milioni. Wema alifanikiwa kukamilisha masharti hayo ya dhamana na yupo nje.

Katika kesi hiyo Wema anadaiwa Oktoba 15, mwaka huu katika jiji la Dar es Salaam alichapisha video ya ngono na kusambaza katika mtandaoni wake wa kijamii wa Instagram.

Hata hivyo Wema baada ya kusomewa shtaka hilo alikana.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa pekee iliyotibu watu wengi nchini na nje ya nchini kwa kufanya kazi Mara 3 kwa wakati mmoja 1 ...kurefusha uume na kunenepesha saizi upendayo, kuogeza nguvu za kiume na inatibu matatizo , ikisha tibu aina madhara inaimalisha mishipa ilio regea na uzalishaji wa mbegu za kiume. TAHADHARI HAKIKISHA UNA MKE AU    MPENZI. 

NINI HUCHANGIA MATAZO HAYA . Ngiri ni chanzo Kikubwa cha matatizo,haya kujua kwamba una ngiri dalili zake ni 1.kufika haraka kileleni wakati  watendo la ndoa 
2.Kushindwa kulundia tendo la ndoa 
3.Kutoa choo kama cha mbuzi 
4. Tumbo kujaa gesi na kuunguruma 
5 kukosa choo kabisa 
6 Maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi 
7 korondani moja kuvimba 
8 kutosikia hamu ya tendo la ndoa
 9 maumivu ya kiuno na mgongo  

Pia tunatibu busha bila kufanyiwa opresheni .Umeachwa na umpendae na bado unamwitaji?

WASILIANA  NA MTALAM  CHALLO 0714 006521. YUPO MBAGALA.

Waziri Lugola Awaambia Mabalozi Nchi Ipo Salama.....Aahidi Kuendelea Kushirikiana Nao

$
0
0
Na Felix Mwagara, MOHA.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amefanya mazungumzo na Balozi wa Italia, Kenya na Afrika Kusini katika ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam, na kuwaambia ulinzi na usalama wa wananchi na mali zao nchini upo vizuri. 

Akizungumza katika kikao cha mabalozi hao waliofika ofisini kwake kwa nyakati tofauti leo, Lugola pia aliwaomba wawakilishi hao wa nchi zao hapa nchini waendelee kushirikiana na Wizara yake na nchi kwa ujumla.

Lugola aliwahakikishia Mabalozi hao kuwa Tanzania itaendelea kuwa salama kwa kuwa Wizara yake imejipanga vizuri kuendelea kuwalinda raia na mali zao pamoja na wageni wote waishio nchini.

“Mheshimiwa Balozi nashukuru sana kwa kunitembelea, najisikia furaha kwa ujio wako na karibu sana wakati wowote, Wizara yangu pamoja na nchi yangu kwa ujumla tutaendelea kushirikiana nanyi katika masuala mbalimbali,” alisema Lugola.

Hata hivyo, Balozi wa Afrika Kusini, Thami Mseleku alisema akiwa nchini anajiona kuwa yupo nyumbani kwasababu nchi yake ina historia kubwa ya ushirikiano na Tanzania.

Hata hivyo, Balozi wa Italia, Roberto Mengoni alimpongeza Waziri Lugola kwa kuteuliwa na Rais John Magufuli kuiongoza Wizara hiyo na pia alimuakikishia ushirikiano zaidi kati ya nchi yake na Tanzania.

“Hongera sana mheshimiwa Waziri kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani na pia nimefurahi kuja katika ofisini yako kufanya mazungumzo nawe,” alisema Balozi Mengoni.

Naye Balozi wa Kenya Nchini, Dan Kazungu alisema Tanzania ni nchi yake na anajisikia furaha kuwepo nchini kwasababu alishawahi kufanyakazi miaka kadhaa iliyopita hapa nchini, hivyo nchi yake itaendelea kutoa ushirikiano katika masuala mbalimbali Tanzania. 

Kama Unalikes FEKI na Followers Feki Instagram Basi Imekula Kwako

$
0
0

Kwa watumiaji wa mtandao wa Instagram ambao wanatumia Apps za kupata likes na followers feki kwenye akaunti zao, kwa sasa ujanja huo hautakuwepo tena kwani mtandao huo umeanzisha kampeni ya kufuta likes na followers wote ambao ni bandia.

Sheria hiyo mpya ambayo imeanza kutumika tayari na mtandao huo, itatumia mfumo wa Machine Learning ambao utaondoa followers na likes zote feki, pamoja na komenti ambazo zimetoka nje ya mfumo wa kawaida wa mtandao huo.

Mabadiliko hayo huenda ya kawa tishio kwa akaunti ambazo zinafanya biashara ya matangazo kwenye mtandao huo, kwani wengi wamekuwa wakiwahadaa wateja wao kuwa kurasa zao zinatembelewa na watu wengi kwa kuwaonesha likes, comments na followers wao na hata impression ya akaunti zao.

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 35

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA
Nikashusha pumzi taratibu, nikamsogelea mwana sheria na kumtaza usoni mwake.
“Hii ni vita ambayo tumesha ianzisha. Ni lazima damu za watu ziweze kumwagika. Nahitaji kuwa pamoja nawe kwenye kila jambo”
“Usijali mkuu, baba yako alinipa jukumu la kukuangalia nami nitakuangalia hadi mwisho wa maisha yangu”
“Sawa nashukuru kusikia hivyo. Huyo mwana mama tunamfanyaje?”
“Kwa sasa ngoja tumtafute kwanza mamam mzazi. Tukisha mpata tunamgeukia na yeye”
“Nashukuru”
“Huyu mzee mkuu tunamfanya nini?”
Kijana mmoja aliniuliza huku akinitazama usoni mwake. Nikamuonyesha ishara ya kuchinja, kijana huyu akachomoa bastoka yake na kumpiga risasi nne za kifua mzee huyu na kumfanya afe hapo hapo.
           
ENDELEA          
“Hakikisheni kwamba mwili wake hauonikani sehemu yoyote katika dunia hii. Ikiwezekana mumuingize kwenye pipa la tindikali”
Nilizungumza huku nikiwatazama vijana hawa.
“Sawa mkuu”
“Kitu kingine, naamini kwamba leo hii mimi na nyinyi ndio tumeonana. Naomba haya mambo yabaki humu ndani, juu ya nguvu zangu mulizo zishuhudia pia liwe jambo la siri sawa”
“Sawa mkuu, kati yetu hakuna mtu ambaye anatatoa siri yoyote. Tuamini katika hilo”
“Nafurahi na ninashukuru kusikia hivyo”
Mara baada ya kuzungumza hivyo nikaagana na vijana hawa. Kijana aliye kuja kutupokea akatuto na kutupeleka hadi sehemu ilipo helicopter tulio.
 
“Ninawategemea katika hii kazi”
“Usijali mkuu, tutaifanya katika muda mfupi snaa na kwa umakini wa hali ya juu kisha tutakueletea ripoti”
“Sawa”
Akafungua mlango wa helicopter hii, nikawa wa kwanza kupanda kisha akapanda mwanasheri. Mlango ukafungwa kisha rubani wetu taratibu akawasha helicopter hii na safari ya kurudi hotelini ikaanza. Ukimya ukatawala ndani ya helicopter hii, huku mwanasheria akionekana kujawa na mawazo mengi sana.
 
“Unawaza nini mzee?”       
“Nawaza jinsi ulivyo mnyanyua yule mzee na kiti chake hadi sasa hivi ninakosa jibu?”
“Hahaa usijali katika hilo, nina uwezo binafsi ambao Mungu amenijali”
“Kweli, Mungu ashukuriwe katika hilo”
“Wale vijana una waamini?”
“Asilimia mia moja wala usiwe na mashaka nao mkuu”
“Sawa, sinto penda kutokee matatizo kwenye hii kazi”
“Usijali”
 
Tukafika hotelini majira ya saa saba usiku. Nikashuka kisha mwanasheria akaondoke na kurudi kwake. Nikafika kwenye mlango wa chumba changu, nikaminya kengele, nikaisikia sauti ya Camila akiniuliza ni nani, nikaguna kidogo na baada ya sekunde tano mlango ukafunguliwa. Camila alipo     niona akanikumbatia kwa furaha sana
“Umenipa hofu mwenzako”
“Kweli?”
“Ndio, nimeshindwa hata kulala”
“Pole mpenzi wangu, ninamshukuru Mungu nimefanikiwa kulimaliza jambo lililo nipeleka kule”
“Vipi umemuona mzee?”
“Yaa nilimuona, amebananishwa kidogo na ametaja ni sehemu gani alipo mama yangu”
“Duuu sasa mama utampataje?”
 
“Kuna watu nimewakabidhi kazi ya kwenda kumleta, nina imani kwamba watafanikisha kumleta akiwa salama”
“Yupo nchi gani?”
“Tanzania”
“Ahaaa sawa mume wangu, twende bafuni tukaoge”
Camila alizungumza huku akinishika kiuno kwa nyuma. Tukaingia bafuni, akanivua nguo zangu zote kisha naye akavua nguo hizi za kulalia. Tukaoga kisha tukarudi chumbani, kutoka na uchovu nilio nao, sikuweza kufanya kitu chochote na usingizi uliwahi kunipitia. 

Asubuhi na mapema nikawahi kuamka na kumuacha Camila akiwa amelala, nikavaa nguo zangu za mazoezi kisha niakelekea uwanjani. Nikaanza kufanya mazoezi peke yangu hata kabla ya wachezaji wezangu. Baada ya nusu saa wachezaji wezangu wakajumuika nami katika kufanya mazoezi. Jinsi ninavyo cheza leo, kumewafanya wachezaji wezangu kunisifia kwani jana sikuwa sawa kabisa. Kocha akatupa mipango ya jinsi gani tunatakiwa kucheza mechi yatu ya kesho, kwani hadis asa hivi tunaongoza kundi letu kwa pointi sita.
“Tunatakiwa kushinda kila mechi iliyopo mbele yetu. Ethan nahisi hili ninalo kwenda kuzungumza sio jambo zuri kidogo, ila naomba ulivumilie kwa leo tu”
“Zungumza tu kocha”
“Leo naomba usifanye     chochote na bibie, asije akakumaliza nguvu sawa”
Mimi na wachezaji wezangu tukajikuta tukicheka huku tukimtazama kocha.
 
“Kweli vile, ninalo lizungumza lina maana Ethan”
“Usijali kocha”
“Haya sasa ni muda wa kupata kifungua kinywa”
Tukaondoka uwanjani hapa na kurudi eneo la hotelini, tukamkuta Camila akisiaidiana na wafanyakazi wa hapa katika kuandaa vifungua kinywa. Camila alipo niona akanifwata kunilaki, akanikumbatia pasipo kujali kama nina jasho liilo nilowanisha nguo zangu zote.
“Vipi, umecheza vizuri?”
“Ndio mke wangu na kesho nitafunga magoli kwa ajili yako”
“Kweli mume wangu?”
“Ndio”
“Utanifungia magoli mangapi?”
“Kama sita hivi”
“Huuhuhu, sita?”
“Ndio, kwani nashindwa?”
“Hamna hushindwi mume wangu, ila inabidi ufanye kazi kubwa. Tena leo inabidi nikubanie nisikupe utamu”
Camila alizungumza kwa kuninong’oneza sikioni mwangu na kunifanya nitabasamu.
 
“Sawa mama”
“Mbona umeitikia kinyonge?”
“Hamna mke wangu, mbona sijaitikia kinyonge”
“Kweli?”
“Ndio mke wangu”
“Nimeandaa kifungua kinywa kwa ajili yako, twende ukanywe.”
“Sawa”
Tukaa kwenye meza yetu pamoja na rafiki yangu Frenando. Tukapata kifungua kinywa kisha tukarudi mavyumbani mwetu.  Siku nzima hii ya leo, kocha alikaa nasi karibu sana huku akituhimiza sana tusipoteze mchezo ulipo mbele yetu kwani ana malengo makubwa sana nasi kwa maisha ya baadaye ya soka.
                                                                                                            ***   
Siku ya mechi ikawadia, tukaingia kwenye basi letu maalumu kwa timu hii kisha safari ya kuondoka nje ya mji ikaanza huku tukipewa usindikizaji wa gari mbili za polisi. Moja ipo mbele ya basi letu huku nyingine ipo nyuma ya basi letu. Daktari wa timu akampa Camila nafasi ya kuwa msaidizi wake, hivyo naye amejuimuika kuungana nasi katika basi hili.
“Utaimudu kazi ya udokta?”
“Ndio, kwa nini nishindwe”
“Hahaaa haya mwaya”
“Tena ukianguka wewe, nitakufwata na kukuhudumia hadi upone”
“Haya bwana mke wangu, ngoja nizungumze na wachezaji wangu”
 
Nikanyanyuka kwenye siti yanguna kusimama katikati ya basi. Wachezaji wezangu wote wakanitazama.
“Ni siku nyingine, tunakwenda kupambana, tukiwa pamoja. Ninawaomba tucheze kwa umoja, na tuhakishe tunashinda. Ninawategemea sana na kwa pamoja tutashinda sawa”
“Sawa kapteni”
Wachezaji wezangu waliitikia kwa pamoja kisha safari ikaendelea. Hadi kufika uwanjani, ilitugarimu masaa mawili. Tukashuka na kuwakuta waandishi wa habari pamoja na mashabiki wakiwa tayaru kwa kutupokea. Waandishi walipo niona ninashuka kwenye gari huku nikiwa na Camila, wakapiga shangwe ambayo hakika sikuitaraji. 
 
“Ethan na Camila tunawapenda”
Ni maneno yaliyo sikika katika kundi moja kubwa la wamashabiki wa kike. Nikagairi kuelekea ndani na kuwafwata mashabiki wangu hao huku walinzi na askari wakiwa wametangulia mbele yetu. Nikaanza hukuchua kalamu ya kila mshabiki, wapo wengine walihitaji niweke saini yangu kwenye mikono yao huku wegine wakihitaji niweke saini kwenye tisheti zao walizo zifanya. Camila naye aliweka saini kwa mashabiki wake wanao muomba kufanya hivyo.
 
“Ethan muda sasa umefika”
Mlinzi mmoja alizungumza pembeni yangu. Nikawapungia mkono na kuanza kuongozana na walinzi huku nikiwa nimeshika Camila mkono. Tukaingia katika chumba chetu cha kubadilishia nguo.
“Camila naomba clipbandeji”
“Ya nini mume wangu?”
“Nahitaji kujifunga kwenye mguu wa kulia, nahisi kama nyayo kidogo inavuta vuta kwa chini”
“Sawa”
Camila akaanza kunifunga mguu wangu kulia.
“Kaza kidogo”
 
Camila alafanya kama nilivyo mueleza. Akanivisha soksi, nikavua koti langu pamoja na suruali hii ya mazoezi niliyo ivaa, kisha nikavaa jezi yangu, ambayo mgongoni imeandikwa namba sana pamoja na jina langu. Kocha akaanza kupiga piga makofi, ikiwa ni ishara ya kutunyamazisha. Baada ya sekuende kadhaa kila mmoja akanyamaza na kumsikiliza kocha ni kitu gani ambacho anahitaji kuzungumza.
“Naamini kwamba kila mmoja anatambua nafasi yake si ndio”
“Ndio kocha”
“Kasi, na mashuti ya mbali ndio mchezo wa leo. Wamezoea kutuona tunacheza mchezo wa pasi fupi fupi, kumbukeni wezetu wana nguvu, wana kasi pia. Hivyo ni lazima tuweze kukubaliana na mwendo kasi wao la sivyo tutachemsha leo sawa”
 
“Sawa sawa kocha”
“Ethan, Pinto ninawategemea. Hakikisheni kwamba munayengeneza mfumo mzuri wa kushirikiana. Katikati, Chris na wezako hakikisheni hamtawaliwi. Chukueni mipira nyuma kisha muipeleke mbele sawa”
“Sawa sawa kocha”
“Tunadakika tano kabla ya kuingia uwanjani. Munaweza kuendelea na shuhuli zenu”
“Kocha suti ya leo imekutoa?”
Nilimtania kocha na kumfanya acheke kidogo.
“Nashukuru capten”
Camila taratibu akanifunga kitambaa cha ukapten katika mkono wangu wa kushoto.
“Hakikisha unaongoza timu na inashinda, sihitaji ushindwe mume wangu sawa”
“Sawa mke wangu
 
Camila akanipiga busu la mdomoni. Nikamuachia, kisha yeye na benchi la ufundi wakaanza kutoka katika chumba hichi. Taratibu tukaanza kutoka katika chumba chetu na kuelekea katika mlango wa kutokea, huku makaera man wakiwa makini sana kuhakikisha kwamba wana turekodi vizuri. Nikakonyeza kamera moja ambayo inanichukua kwa ukaribu sana usoni mwangu.  Refarii na wazaidizi wake wakasimama mbele yangu, katoto kamoja ka kike kaliko valia jezi ya timu yetu kakanipa mkono na nikakashika.
“Unaitwa nani?”
Nilimuuliza huku nikiwa nimeinama.
“Camila Alexander Diaz”
Kalinijibu kwa ufasaha kabisa huku akitabasamu sana.
“Kweli?”
“Ndio”
 
Nikatabasamu kisha nikasimama wima. Tukapewa ishara ya kuanza kuingia uwanjani. Taratibu tukaanza kutembea hadi uwanjani, uwanja huu una mashabiki wengi sana ambao wengi wao wameshika wabango yanayo nikaribisha tena uwanjani. Tukajipanga mstari mmoja ulio nyooka huku Camila Alexander Diazi akiwa amesima mbele yangu. Ukapigwa wimbo wa taifa wa timu ya Spain kisha ukapigwa wimbow a taifa wa nchi hii ya Ujerumani. Tukabadilsiahana bendera na kapteni wa timu ya wapinzani. Leo hii timu yangu inaanza katika goli Kaskazini mwa uwanja huu. Kila timu ikazunguka nusu duara katikati ya uwanja huu na tukapewa dakika moja ya ukimya kwa kuwakumbuka waalimu wa shule ya Camila walio chinjwa na kundi la kigaidi huko barania Afrika liitwalo Al-Shabab.
 
Dakika moja ilipo kwisha, filimbi ikapigwa na refarii, kisha wachezaji tukatawanyika, kila mtu akasimama katika nafasi yake. Wapinzani wezetu wakaanzisha mpira huu, huku wakionekana kuumiliki sana mpira huu. Hatukuchoka katika kuutafuta mpira ambao wapinzani watu wana umiliki kwa kupigiana pasi zinazo fika kwa kila anaye kusudiwa kupewa mpria.
Wapinzani wetu wakafanya shambulizi moja kali sana, ila Frenando akafanikiwa kuunyaka mpira huo. Frenando akaupiga mpira mbele.

 Lukas akautuliza vizuri kifuani mwake kishaa kauweka chini, akanitazama nilipo na kupiga pasi ndefu iliyo anza kuambaa ambaa hewani, nikaanza kukimbia kuelekea kwa wapinzani wangu, huku kila mara nikiutazama mpira huu. Wachezaj wawili ninao kimbizana nao hawakusita katika kuutazama mpira huo. Kitendo cha mpira kutufikia tulipo, nikauunganisha kwa shuti kali ambao liliambaa hewani kwa sekunde kadhaa na kugonga mwamba wa juu wa wapinzani, kisha mpira ukatoka nje. Uwanja mzima ulisimama na kushangilia kwani kama mpira huo ungeingia golini basi lingekuwa ni goli moja la kihistoria katika machuano haya.
 
Inadi ya wachezaji wanao nikaba kwa timu pinzani ikaongezeka, wakaanza kunikaba wachezaji wanne wanne jambo lililo nifanya nianze kuuona mchezo mgumu kwa upande wangu, kwani kila mpira ambao ninaletewa na wachezaji wezangu, siumiliki hata kwa sekunde nyingi wanakuwa wananipokonya. Kipindi cha kwanza kikaisha pasipo kufungana 
 
“Pole mume wangu”
Camila alizungumza huku akitembea pembeni yangu.
“Ndio mpira mpenzi wangu”
Nilizungumza huku tukiingia ndani ya chumba chetu. Kila mchezaji uso wake umetawaliwa na kuchoka, kwani mtandange huu ni wa kukata na shoka, yaani ni bora hata na mechi ya kwanza tulo cheza kwani tulifungwa na tulikuwa na hamasa ya kutafuta goli, ila mechi hii, karibia wachezaji wa timu pinzani wanakaba na wanaonekana hawana hata hamu ya kutafuta goli na itakuwa ni furaha yao wakiona tunagawana pointi.
 
ITAENDELEA   

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 156 na 157 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA
                       
Wahuzuriaji wa harusi hii ni watu wachache sana ambao hawazidi hata kumi na wote wanaonekana ni matajiri wakubwa sana kwani ni marafiki wa meja. Mchungaji hakuwa na mahubiri marefu juu yetu alicho kifanya ni kuingia katika ibada ya kufungisha ndoa hii. Tukavishana pete na Yemi na kuwafanya watu wote kufurahia. Tukakumbatia kwa nguvu na Yemi huku kila mmoja akiwa amejawa na furaha kubwa sana. Gafla kipande kimoja cha goroa la hoteli hii kikalipuka kwa bomu jambo lililo wafanya walinzi wote wa meja kukimbilia katika eneo tulipo na kuanza kututoa katika eneo hili kwa haraka sana kwani hatujui ni nani ambaye amefanya shumbulizi hili.
   
ENDELEA   
Heka heka za kututoa katika hili  eneo zikaanza huku walinzi hawa wakiwa makini sana. Kazi yangu ni kuhakikisha kwamba mke wangu anakuwa salama hata kama kutatokea jambo baya zaidi ila ni lazima kumuokoa Yemi.
“Huku huku”  
  
Mlinzi mmoja  alizungumza, na tukaanza kukimbilia ndani ya hoteli hii, huku meja na Martin wakiwa ni miongoni mwetu. Tukaingia kwenye moja ya chumba, tukakuta ngazi za kwenda chini, tukazidi kushuka chini huku tukiwa kasi. Tukakuta boti maalumu iliyopo katia eneo hili la chini ya hii hoteli ambayo inatumika kwa ajii ya dharura ya kutorokea, endapo kunatokea uvamizi kama huu.
“Ingieni kwenye hii boti itawapeleka moja kwa moja hadi nyumbani”
Mlinzi mmoja alizungumza, anaonekana yeye ndio mkuu wa hichi kikosi maalumu cha meja.
“Sawa hakikisheni munaniletea ripoti ya nani aliye sababisha hili shambulizi”
Meja alizungumza huku uso wake ukiwa umefura hasira hadi amekuwa mwekundu kiasi kwenye uso wake.
“Sawa mkuu”    
 
Wakaingia walinzi wawili na wengine wakabaki na kuondoka katika hili eneo. Mlinzi mmoja akawasha hii boti ya mwendo wa kasi na kuanza kuondoka katika hili eneo la hii hoteli ambalo lina maji ya bahari tukatoke katika usawa wa bahari. Meja ndani ya boti hii hakutulia kabisa, mara asimamae mara akae, mara asunye hii yote ni kuonyesha ni jinsi gani amekasirika. Muda wote Yemi usoni mwake machozi yanamtiririka, jambo lililo nifanya nimkumbatie pasipo  kuzungumza kitu chochote kwa maana ni jambo ambalo hakuna hata mmoja wetu ameweza kulitegemea.
 
Tukafika katika ukingo wa bahari lilipo jumba la meja, tukashuka sote na kupokewa na walinzi wengine, tukaingia kwenye gari lililo tufikisha moja kwa moja hadi kwenye jumba hili kwani kuna umbali kiasi. Yemi hakuzungumza kitu chochote zaidi ya kukimbilia chumbani na kunifanya na mimi kuelekea chumbani huko. Nikamkuta Yemi akiwa amelala kwenye kitanda huku akiendelea kulia kwa uchungu sana.
“Kwa nini, kwa nini sisi kila siku, hadi leo siku ya harusi badooo wanatundama jamaniii akhaaaa”
 
Yemi alilia kwa uchungu huku akikipi piga kitanda. Nikamnyua na kumkalisha kitako, nikaka pembeni yake na kumshika mikono yake yote miwili huku kigugumizi cha kuzungumza kikiwa kimenitawala mdomoni mwangu.
Dany mume wangu ni lini tunakuwa na furah, lini tunakuwa na amani jamanii”
“Ye….yemi”
Nilizungumza huku machozi ya hasira yakianza kunichuruzika kwenye mashavu yangu.
“Ndio mume wangu…….”
“Nitaitengeneza furaha ya familia yangu, nitahakikisha kwamba kila jambo kwenye maisha yetu linafikia mwisho sasa”
 
“Kwa nini jamani mume wangu, hawatuachi hata tukashangilia siku moja. Moja hii ya harusi akhahaaa”
Yemi aliendelea kulalamika kwa uchungu sana. Nikikipeleka kiganja changu cha mkono wa kulia kwenye shingo yake, taratibu nikakaanza kumnyonya mdomo wake, japo ana hasira na uchungu ndani yake ila Yemi hakuwa na hiyana kwangu, akanipa usihirikiano mzuri wa kunyonyana midomo yetu huku sote tukiwa katika hali ya huzuni na hasira ndani yake.
“Nitaua watu wote wanao niandama katika maisha yangu. Ninakuomba mke wangu ukubaline nami katika hili”
Nilizungumza kwa sauti nzito huku nikimtazama Yemi usoni mwake, Yemi machozi yakaendelea kumtiririka mashavuni mwake.
 
“Nipo tayari mume wangu waue woteee”
Baada ya Yemi kuzungumza maneno hayo nikamvutua tana kichwa chake na tukaanza kum midomo yake, safari hii  ukajawa na hisia kali za mapenzi,........Tukajikuta tukimaliza mzunguko wa kwanza huku wote tukiwa tumechoka sana. Nikashuka kitandani huku nikipepesuka na koo langu likiwa limekabwa na kiu  kikali cha maji.
 
“Ahahaa….Yemi leo umekula nini mke wangu”
Nilizungumza huku nikielekea bafuni, nikafungua maji ya bomba na kuanza kuyanywa taratibu kuhakikisha kwamaba nina kata kiu cha maji kilicho nitawala kooni mwangu.
“Hasira mume wangu, yaani hata mimi mwenyewe ninajishangaa”
 
Yemi alizungumza huku akinikumbatia nyuma yangu, tukajitazama kwenye kioo kilichopo mbele yetu.
“Namshukuru Mungu kwa kuweza kunipatia mwanamke kama wewe”
“Hata mimi mume wangu, ninakupenda sana Dany, japo ninakutana na mambo mengi ya kuniumiza kichwa changu, ila kusema kweli  una nifurahisha na kunifanya nijihisi mimi ndio mwanamke bora kuliko wote ulimwenguni. Umenipa dunia yangu peke yangu, ninakuomba sana Dany wangu uhakikishe kwamba dunia yangu hakuna mtu anaye weza kunipokonya”
Taratibu nikageuka, na kumtazama Yemi huku mikono yangu nikiipitisha kiunoni mwake.
 
“Nakuahidi mke wangu, nitahakikisha kwamba ninakulinda hadi mwisho wa maisha yangu”
“Asante mume wangu”
“Na kitu kingine ninahitaji kueleka Tanzania katika siku mbili hizi”
“Tanzania!!?”
“Ndio mke wangu, huko ndipo nyumbani kwetu sasa, hatuwezi kuendelea kuishia kwenye nchi hii wala kuishi kwa mtu ikiwa kwetu kupo”
“Nipo tayari kukufwata popote utakapo kwenda Dany wangu, utajiri wangu wote bila ya wewe si kitu kwangu, nina kupenda sana Dany wangu”
“Ninakupenda pia mke wangu kipenzi, ninakuomba usiniache peke yangu”
“Siwezi mume wangu, na hicho kitu wala usije ukakifikiria hata siku moja kama kinaweza kutokea kwneye maisha yangu”
 
Tukakumbatia na Yemi, kisha taratibu akayafungulia maji ya bomba la mvua yaliyo anza kutitirika kwenye miili yetu. Tukasimama kwa dakika zaidi ya tano huku tukiwa tumekumbatiana kisha taratibu tukaanza kuoga. Tukatoka bafuni huku huku tukiwa tumeshikana mikono               
“Yaani simaini kama sherehe yetu imeisha naamna hii”
Yemi alizungumza huku akijitupa kitandani.
“Kikubwa Mungu ametulinda na mpango mbaya ambao waliupanga juu yetu”
“Kweli mume wangu”
“Ngoja nikafwatilie tujua kwamba ni kina nani walipanga kutuangamiza?”
 
“Sawa hapa miguu yangu yote imechoka, leo umejua kunikoj...** hadi sina hamu kabisa”
“Huo mzunguko wa kwanza wa pili tutaendelea usiku muda wa kulala”
“Mmmmm utaniua mwenzio”
“Hufi”
“Ila chamoto nitakiona eheee”
“Yaa”
“Sawa mume wangu”
Nikavaa nguo zangu na kutoka chumbani kwangu, nikafika sebleni na kumkuta meja akiendelea kunywa mzinga wa pombe kali.
“DANNYYYYYYYYYYYYY…………”
Meja alizungumza huku akinyanyua mtungi huo juu.
“Karibu rafiki yangu”
Meja aliendelea kuzungumza kwa sauti ya ulevi huku akinitazama usonimwangu. Nikaka kwenye moja ya sofa huku nikimtazama.
 
“Kinywaji Dany”
“Hapana meja nipo vizuri”
“Samahani bwana rafiki yangu, hawa washenzi wamevuruga harusi yetuu bwana”
“Usijali meja natambua mambo kamaa hayo kwenye maisha yangu ni jambo la kawaida.”
“Kweli, ila hawa wana haramu kama ni wao hata mimi nitashiriki katika kuwaangamiza, potelea pote na mimi nikiwa gaidi”
“Meja aliendelea kuzungumza kwa sauti ya ulevi.
“Hapana meja, acha nishuhulike nao mimi mwenyewe”
“Njoo njoo”
 
Meja alizungumza huku akinyanyuuka kwenye sofa, akayumba kidogo ila akajihimili huku akiwa ameendelea kushika chupa yake.
“Kuna vitu vingi ninahitaji kukuonyesha rafiki yangu”
Meja alizungumza huku tukielekea nje, tukatoka na kuendelea kutembea kwenye jumba hili la kifahari.
“Kwenye maisha yangu siku zote niliishia kwa ajili ya kutafuta amani, niliishia kwa ajili ya kuwa mtu mwema, ila siku zote kwenye maisha maadui nao hujitokeza kama ilivyo kwenye maisha yako”
 
Nikaka kimya huku nikimsikiliza meja anacho kizungumza. Tukaingia katika moja ya chumba ambacho kipo katika jengo la nje, chumba hichi kimetawaliwa na michoro mikubwa iliyo jengewa kwa fremu za dhahabu.
“Kipindi nilipo kuw amdogo wazazi wangu waliipenda sana hii michoro na waliweza kuiweka kwneye jumba letu Calfoni nchini Marekani, na michoro hii unavyo iona kila mmoja una maana yake”
Meja akapiga fumba jingine la pombe kali kisha akainyooshea kidole picha moja. Kabla hajazungumza chochote simu yake ikaita, akaitoa mfukoni na kuipokea.
“Halooo”
“Wapo wangapi?”
“Waleteni hapa nyumbani”
Meja akakata simu na kunigeukia.
“Tumewakamata walio sababisha mlipuko wa pale hotelini, na wanaletwa hapa nyumbani”
“Wapo wangapi?”
“Wapo watatu”
 
Meja alizungumza huku akitoka chumbani humu, hata hamu ya kuendelea kunisimulia michoro hii aliyo nionyesha ikaishia hapo. Moja kwa moja tukaeleka katuka kiwanja cha helicopter ambapo ndipo meja alisema kwamba watu hao wanaletwa hapa.
“Watanitambu”
Meja alizungumza huku akiendelea kusunya sunya tu, haukupita muda mrefu helicopter ikatua katika hili eneo. Wakashushwa watu watu watatu ambao wamefunikwa nyuso zao na vigunia vidogo vyeusi. Meja akawatazama watu hawa, kisha akatoa amri kwamba wapelekwe kwenye chumna cha mateso. Watu hawa wakanza kupelekwa haraka haraka huku mikono yao ikiwa imfungwa na kamba ngumu ambazo sio rahisi kwa wao kuweza kuzifungua.
 
“Dany”
Nilimuona Yemi akija eneo letu huku akiwa anakimbia huku akionekana kuonekana ana wasiwasi mwingi sana usoni mwangu.
“Ni kitu gani kinacho endelea mume wangu”
Yemi alizungumza baada ya kutukaribia.
“Shemaji hakuna tataizo, ila tumewapata wale walio sababisha mlipuko kwenye harusi yenu na ndio wale wanao pelekwa kule”
Meja alinisaidia kujibu swali la Yemi alilo nikuliza. Yemi akawatazama watu hao, kisha akaachia msunyo mkali huku akionekana kukasirishwa sana.
“Nini?”
Nilizungumza huku nikimshika mkono Yemi.
“Wamenistua na mlio huu wa helicopter nikadhani tumevamiwa tena”
 
“Hapa kwangu shemeji hakuna ambaye anaweza kuingia, ila ulinzi kila sehemu”
“Naombeni na mimi niwaone hawa watu walio vuruga harusi yangu”
“Mke wangu……”
“Dany mimi pia ni muathirika katika hili, umeona ni uchungu gani ambao nimeupata kwa tukio lile”
Yemi alizungumza kwa msisitizo na kutufanya mimi na meja kumtazama kwa sekunde kadhaa, meja akatingisha kichwa akishiria kukubaliana naye ashiriki nasi kwenda kuwaona hawa watu.
“Sawa”
Niliitikia kinyonge kwani sina sababu ya msingi ambayo ninaweza kumzuia Yemi. Tukaanza kutembea kuelekea katika chumba walicho ingizwa watu hawa. Hatukuchukua muda mwingi kufika katika hichi chumba, tukaingia ndani na tukawakuta watu hawa wakiwa wamefungwa mikono yao huku wakiwa wamening’inizwa juu juu.
 
“Wavueni hivyo vitatambaa”
Meja alizungumza huku sote tukiwa tunawatazama watu hawa, akafunuliwa mtu wa kwanza, kwangu sura yake yake ni ngine, akafunuliwa mtu wa pili naye sura yake ni ngeni, ila nilipo yageuza macho yangu kwa Yemi akaonekana kama anawatambua kwani sura na macho yake yanaonyesha vizuri kwamba anawafahamu watu hawa. Mtu wa tatu kufuniliwa sasa hata mimi nikastuka kwa manaa huyu aliye funuliwa ni mume wa Yemi ambaye mara ya mwisho waliachana kwa ugomvi mkubwa sana ambao hata mimi nilishiriki katika kumpiga vibaya sana na kumpokonya mke wake ambaye nipo naye hivi sasa.                        

AISIIIII……….U KILL ME 157   


“Wee mwehu…..kk…umbe ndio umekuja kuvuruga harusi yangu”
Yemi alizungumza kwa kigugumizia huku akimsogelea mume wake huyu wa zamanai. Yemi akaongeza kasi na kumfikia, Yemi kwa harisa akaanza kumpiga vibao vya mashavuni huku akimtukana matusi mfululizo jambo lililo nifanya kwa haraka nimsogelee Yemi na kumtoa.
 
“Acha anipige hivi unahisi sijui kinacho endelea”
Jamaa huyu alizungumza kwa ukali huku akimtazama Yemi usoni mwake.
“Hata kama umejua kwamba ninaolewa, kwa nini uje kuvuruga harusi yangu, mimi na wewe mapenzi yalisha isha, nimepata mwanaume anaye niridhisha kuliko wewe”
Yemi aliendela kuzungumza kwa sauti hadi machozi yakaanza kumwagika mashavuni mwake.
“Acha ujinaga Yemi wanacheza na akili yako, unafurahi vipi ikiwa mtoto wetu yopo Mochari na amekufa kwa ajili ya huyo mwanaume?”
 
Macho yakatutika na tukabaki tumepatwa na mshangao mkubwa sana. Yemi akajitoa mikononi mwangu na kututazama mimi na meja kwenye nyuso zetu, nikatamani kuzungumza ila sijui hata nianzie wapi.
“Sijakuelewa unasema kwamba……..?”
“Mtoto wetu amekufa, na yupo mochwari hadi hivi sasa hivi ninazungumza. Unakuwaje na mwanaume ambaye amepelekea kifo cha mtoto wetu kwa mazambi yake?”
Mume wazamani wa Yemi alizidi kuzungumza maneno ambayo yalizidi kuniumiza ngumu. Nikastukia meja akimpita jamaa huyu chupa ya uso jambo lililo mfanya Yemi kupiga kelele za uchungu. Nikajaribu kumshika, Yemi akaitoa mikono yangu kwa nguvu huku akinitazama kwa jicho kali  sana usoni mwangu.
 
“Dany umenidanganyaa eheee”
Yemi alizungumgumza huku akinishika shati langu, na kulinyongorota maeneo ya kifuani.
“Ehehee Dany kwa nini unidanganyeeeee?”
Yemi akanisukumia hadi kwenye ukuta huku akiendelea kunikaba shiti langu, kusema kweli nguvu  zote zimenishia mwili mwangu, sijui hata nizungumze kitu gani kwa Yemi ambaye amekuwa na hasira kali kama samba jike aliye jeruhiwa katika zoezi la kuwakomboa watoto wake.
 
Yemi akanitandika ngumi ya tumbo iliyonifanya nijikuje huku nikisikilizia maumivu yake, akaninyanyua na kuniweka sawa.
“Nimeyatoa maisha yangu kwa ajili yako, nimetoa watu zaidi ya laki mbili kwa ajili yako na wamekufa kwa ajili yako nikijua nitakuwa na familia  bora na wewe leo hii umeamua kunisaliti, mwaanangu anakufa, unakaa kimya na kunifungisha ndoa nikirufahi nikujua mwanangu yupo sehemu salama kumbe unaniletea maswala ya kiku** na wewe”
Yemi aliendelea kuzungumza kwa hasira, kila ninapo jaribu kufikiria ni jambo gani ninaweza kuzungumza litakalo muweka Yemi katika mstari wa kueleweka na kuituliza hasira yake ila sina kabisa.
 
“Nimbie Dany mwanangu amekufaa eheeee”
Yemi alizungumza huku akinitingisha kifua changu.
“NIAMBIEEE WEWEEEEEEE”   
“NDIOOOOOO AMEKUFAA”
Nilizungumza kwa ukali huku akiniachia shati langu, akanitazama usoni mwangu kama mtu ambaye haamini kwa kile ambacho anakisikia. Akamgeukia mume wake wa zamani, kwa haraka akaanza kutembea hadi sehemu alipo fungwa, huku damu zikimwagika usoni mwake.
“Mfungueniiii”   
Yemi alizungumza kwa ukali, hapakuwa na mfanyakazi wa meja aliye weza kupokea amri ya Yemi.
“Nimesemamfungueni”       
“Hawawezi kukusikia pasipo amri yangu”
Meja alizungumza kwa sauti nzito hata ile sauti ya ulevi imemuaondoka sasa.
“Waambie hawa mende wako wamfungulie mume wangu la sivyo nitaua mtu”
 
Yemi alizungumza huku akiokota kipande cha chupa na kukishika mkono wake wa kulia. Meja akanitazama usoni mwangu, kwa ishara ya macho akaniuliza niwafungulie au laa. Nikamtazama Yemi usoni mwake,
“Wewe gaidi toa jibu, nanitaji mwanaume wangu afunguliwe, sio wewe mwanaume unayte taka familia yangu iishe kwa ajili ya matatizo yako”
“Yem…..”
Hata sikumalizia kuzungumza sentensi  yangu nikajikuta nikikwepa kipande cha chupa alicho kirusha Yemi na kikapiga ukutani. Nikamshuhudia Yemi akivua pete yangu ya ndoa niliyo mvisha masaa machache yaliyo pita na kunirushia miguuni mwangu jambo lililo mshangaza kila mtu humu ndani.
 
“Mimi na wewe basi, sikutaki Dany, wewe si mwanaume wa maisha yangu. Wewe ni gaidi, wewe ni muuaajiiii hufaiiii kuishi na mwanamke yoyoteee pumbavuuuuuu weweeeeee”
Taratibu nikachuchumaa na kuikota pete yangu huku machozi yakinitiririka usoni mwangu. Nikasimama na kumtazama Yemi usoni mwake. Taratibu nikaanza kusogelea huku nikiwa nimekazia macho, Yemi akabaki amesimama huku akinisubiria kufika sehemu alipo. 
 
Kitendo cha kumkaribia Yemi, akarusha kofi kwa mkono wake wa kulia, ila nikamdaka na kumshusha mkono wake chini.
“Huwezi kuvua peta yangu ya ndoa, ikiwa nilijaribu kwa uwezo wangu wote kuhakikisha kwamba wewe na mwanao munakuwa salama, nilijisalimisha mikononi mwa Wamarekani kwa ajili yako wewe na mwanao leo hii unaona kwamba msaada wangu hauna maana kwenye maisha yako eheee?”
 
Niliuliza kwa ukali huku nikimtazama Yemi usoni mwake.
“Nitolee sera zako za kisen** kujitoa kwako mimi kuna nihusu nini mimi eheeee?”
Yemi aliendelea kuzungumza kwa ukali. Nikamtazama mume wake huyu anaye enedeleka kuugulia maumivu ya uso wake ulio chanwa na mpasuko wa chupa iliyo tua usoni mwake.
“Siogopi kuua, na wala sihofii kuua na kama huyu msen** hapa ndio amekufa uvue pete yangu sasa nina muua”
Nilizungumza huku nikimuomba mlinzi mmoja wa meja bastola yake. Jamaa akachomoa bastola yake kiunoni na kunikabidhi, Yemi akanitolea macho huku akihema kwa hasira.
 
“Sikumuomba baba yako kuwa kiongozi wa kundi lake, sikukuomba wewe uwe mwanamke wake ila ni kwa ajili ya kufanya maamuzi yako ya kijinga ndani ya muda mchache baada ya kumfumania mume wako, nilitumwa kuwaua wewe na baba yako na huo uwezo nilikuwa nao na ningefanya ndani ya masaa machache tu. Ila nimakuacha leo  hii unavua pete yangu, unajua ni jisni gani ninavyo kupenda na nimeyatoa maisha yangu kwa ajili ya kusaidia mkund** wa baba yako na wako eheee. Hivi unahisi kwamba mimi ninawea kupigana na Marekanini, mimi nani? Osama Bin Laden, Gadafi eheeeeee?”
Nilzungumza kwa hasria huku nikiwa nimeishika bastola yangu, hasira niliyo nayo nina imani kwamba Yemi alisha wahi kuniona nayo siku ambayo alifahamu ukweli wa jina langu.
 
“Dany Dany”
Niliisikia sauti ya meja ikiniita nyuma yangu, nikageuka na kumtazama meja usoni mwake. Akatingisha kichwa akiniomba nisifanye kile ambacho ninahitaji kukifanya kwani yeye mwenyewe hajawahi kuniona katika hali kama hii.
“Maishani mwangu nimepoteza mtoto wangu, mama wa mtoto wangu, mama yangu mzanzi, baba yangu mzazi na mdogo wangu  wa kike na wote wamechinjwa leo hii unaona kifo cha mwanao kina thamani kubwa sana, kulilko damu za watu walio jitahidi kunifanya niwe Dany eheeee?”
 
Niliendelea kuzungumza kwa ukali hadi kukamfanya Yemi kutetemeka. Nikaishika pete aliyo ivua na kumnyooshea.
“Najua leo hii imevua pete mbele ya watu walio shuhudia jinsi nina kuoa, na niajua kwamba ipo siku utanisaliti mbele ya watu kwa ajili ya maamuzi yako ya kijinga. Chagua pete na mume wako mimi nitakuwa tayari kwa lolote”
“Dany Dany usifanye hivyo rafiki yangu?”
“Meja hapa hakuna mwanamke, acha afanye chaguo nipo tayari amesha niita gaidi unahisi kuna nini hapa?”
Yemi akanitazama usoni mwangu huku machozi yakimwagika, taratibu akamsogelea mume wake na kumkumbatia jambo lilio nistua hadi mimi moyoni mwangu, kwani ni maamuzi magumu aliyo yachuku Yemi.
 
“Ni bora niishi na mwanaume ambaye ni malaya kuliko kuliko kuishi na mwanaume gaidi na anaye hatarisha maisha ya familia yangu, kama kifo cha familia yako hakikuwa na thamani kwako ila kifo cha mwanangu kina thamani kubwa kwani si wewe uliye ibeba mimba yake na wala hujui uchungu wake”
Yemi alizungumza kwa sauti ya msisitizo huku machozi yakiendelea kumwagika usoni mwake. Nikamrudisha kijana wa Meja bastola yake nikakunja vidole vya kiganja kilicho shika pete ya Yemi kwa nguvu huku nikitingisha kichwa kwani nina hisi maumivu makali moyoni mwangu hadi ninahisi kwamba moyo wangu unaweza kupasuka muda wowote
 
“Meja ninakuomba uwasamehe na uwafungulie warudi Nigeria salama na wamchukue mtoto wao”
“Dany…”
“Meja nina kuomba kama rafiki yako, ninakuomba usiwashuhulikie kwa lolote”
Nilizunguza huku machozi yakinimwagika usoni mwangu, meja akanitazama kwa sura ya unyonge na iliyo jaa masikitiko. Nikamgeukia Yemi na kumtazama usoni mwake.
“Ninakuomba unisamehe Yemi kwani nilishindwa kukuambia ukweli kwa ajili ya kulinda furaha yako, ya kujiandaa kwa ajili ya harusi. Niwatakie maisha mema huko muendapo”
 
Nilizungumza huku machozi yakinimwagika usoni mwangu, hata uwe ni jasiri kiasi gani ila maumivu ya mapenzi kusema kweli yanaumiza na yanaweza kukuambisha kwa kumwaga machozi mbele za watu.
“Jamaa nisamehe kwa yale yote yaliyo jitokea, nisamehe kwa kushindwa kuyalinda miasha ya mwanao najua kama baba kweli ulistahili kufanya hivyo, ninakuomba unisamehe jamaa yangu”
Baada ya kamaliza kuzungumza maneno haya nikatoka katika hichi chumba na kumuacha Yemi akiangua kilio kwa sauti ya juu. Kila ninacho kiona mbele yangu ninakiona katika mtazamo wa ajabu ajabu jambo lililo nifanya nianze kupiga kelele huku nikihisi dunia kama ina vitu vya ajabu.
“Dany Dany Dany”
 
Niliisikia suti ya meja kama ya jitu fulani hivi baya ambayo ikanifanya nipike kelele huku nikijaribu kukimbia ila nikajikuta nikikamatwa na watu ambao nao nikiwatazama usoni mwao ninahisi kama ni majini fulani yaliyo kuja kunikamata.
“Mpelekeni ndani amechanganyikiwa”
Nilizidi kuisikia sauti nzito ya meja, iliyo nifanya nijiziba masikio yangu, nikanyanyuliwa juu, kila ninapo tazama angani na kuziona nyota ninahisi kama zipo usoni mwangu, jambo lililo zidi kunipagawisha.
“Mchomeni sindano ya usingizi”
“Sawa mkuu”
Nikahisi kitu chenye ncha kali kikiingia kwenye mkono wangu wa kulia, sikumaliza hata dakika mbili nikajikuta usingizi mzito sana ukinipitia na kulala fofofo.
  ***               
“Mkuu”
Niliisikia sauti ya Martin, taratibu nikageuza kichwa changu na kumtazama.
“Vipi?”
Nilimuuliza huku  nikijaribu kunyanyuka ila Martina akanizuia na kuniomba nilale.
“Mkuu bado afya yako haijawa sawa, tulia kidogo nina imani kwamba utakuwa unahisi kizunguzungu”
 
“Umejuaje?”
“Nimefahamu”
Nikayafumba macho yangu kwani ni kweli nina hisi kizungu zungu, nikayafumbua yena na kumuona Martina akinyanyuka na kufungua friji iliyopo humu ndani akatoa mfuko wenye barafu kubwa kisha akarudi sehemu nilipo lala.
“Naomba tu”
Nilizungumza mara baada ya muonoa Martin akihitaji kuniwekea mfuko huo wa barafu kichwani mwangu, nikauchukua mfuko huu na kujiweka upende wa kichwa ninapo hisi maumivu.
“Meja yupo wapi?”
“Ameelekea uwanja wa ndege”
“Kufanya nini?”
“Amemsindikiza Yemi na watu wake, wamaetokea hospitali kuchukua maiti ya mtoto”
Nikashusha pumzi taratibu huku nikimtazama Martin usoni mwake.
 
“Siwezi kumlaumu Yemi, yote ni kwa ajili yangu”
“Hapana Dany huwezi kujilaumu siku hata moja ikiwa wewe mwenyewe ulikuwa mikononi mwa wanajeshi wa Kimarekani na uliamua kujisalimsha wewe mwenyewe ili kuokoa maisha ya mtoto huyo”
“Nisingekuwa gaidi wala yasinge mkuta mtoto wa watu, isitoshe bado ni mdogo sana”
“Wewe sio gaidi Dany”
“Kwa nini unasema kwamba mimi sio gaidi, ikiwa hata mwanamke ninaye mpenda ameniita gaidi?”
“Yemi ninajua huko aendapo atakuwa anajutia kwa maamuzi yake na kinywa chake kwa kukuita gaidi, nina imani hatambui ni kutu gani kimetokea kwenye maish yako”
“Wewe una amini kwamba mimi si gaidi?”
“Asilimia mia moja mkuu nina kuamini kwamba wewe sio gaidi”
 
“Martin kwa nini huitaji kunisaliti mimi, ikiwa dunia nzima kwa sasa nina imani wananitafuta mimi?”
“Nilikuahidi kwamba tutakufa pamoja na pia tutaishi pamoja, na siwezi kukusaliti ni bora nife wa kwanza kuliko kukuona wewe unakufa wa kwanza”
Martin alizungumza kwa msitizo mkubwa sana, jambo lililo nipa matumaini makubwa sana. Taratibu nikaka kitako kitandani huku nikindelea kuugandamiza mfuko huu wenye barafu  kwneye kichwa changu na kidogo maumivu  na kizungu zungu kinacho nikabili vinatoweka.
“Dany sasa ni wakati wa kuimalizia kazi iliyopo mbele yetu, nina uchungu mkubwa sana kwa kuwapoteza rafiki zangu katika mashambulizi walio yafaya Wamarekani, pale ilikuwa ni nyumbani kwangu, pale palikuwa ni kwetu, nina imani kwa pamoja tunaweza kumungusha yule aliye pelekea vifo vya wapendwa wetu”
Martin alizungumza kwa msisitizo huku akinitazama usoni mwangu.
 
“Upo tayari katika hili?”
“Hata kama ni sasa hivi nipo tayari kuua, mapenzi kwa sasa mkuu wangu yaweke pembeni. Yatatufelisha kwenye mengi”
“Siwezi kupenda mwanamke yoyote kwenye maisha yangu, Yemi amesha nirudisha kwenye maisha ambayo kusema kweli damu ndio itakuwa kinywaji changu. Nitahakikisha kwamba wale wote walio niumiza na kuyapeleka kwenye maisha haya ni lazima niwaue tena kwa mkono wangu mimi mwenyewe”
“Hayo ndio maneno kaka yangu. Ninasubiria amri kutoka kwako mimi nitafanya”
Martin alizungumza kwa furaha huku akitabasamu, taratibu akanisaidia kushuka kitandani. Nikasimama wima huku nikitazama hichi chumba ambacho usiku wa siku mbili nililala na Yemi katika kitanda hichi.
“Maisha yanabadilika mdogo wangu”
 
“Kwa nini?”
“Jana tu nilitoka kumt** Yemi kwenye hichi kitanda leo ameondoka”
Martin akacheka chihi chini nina imani kwamba hakutarajia kwamba ninaweza kuzungumza maneno kama hayo. Tukatoka humu chumbani, tukakuta wahudumu wakiwa tayari wamesha andaa kifungua kinywa.
“Meja amesema anarudi saa ngapi?”
“Hajaniambia ila nina imani atarudi muda si mrefu”
Martin akaingiza mkono wake mfukoni na kutoa pete ya Yemi na kuniwekea karibu na sehemu nilipo kaa. Nikaitazama kwa sekunde kadhaa hii pete kisha nikaichukua hapa juu ya meza na kuiingiza mfukoni.
 
“Jana uliiangusha, nikakutunzia”
“Asante, nitaiweka kama ukumbusho kwa maana kwenye maisha yangu sikuwahi kuoa mwanamke kwa ndoa”
“Haito kuumiza hiyo pete utakapo iona?”
“Sijajua kwa kweli, nitajaribu kukaa nayo nikishindwa nitaitupa”
“Na hiyo ya kwako huko kidoleni?”
Kabla sijamjibu Martin malango ukafunguliwa, akaingia meja moja kwa moja akatufwata hadi tulipo kaa, akavuta kiti taratibu na kukaa.
 
“Vipi Dany?”
“Safi nimesikia umewasindikiza Yemi na mume wake?”
“Ndio ila ninahitaji kusikia neno la mwisho kutoka kwako, kwani ninahitaji kufanya kitu kwa ajili ya yule mpumbavu kwani amebadilisha hali ya hewa?”
“Kitu gani gani unacho hitaji kumfanyia?”
“Nimewapakiza ndege mbili tofauti na Yemi. Yemi amependa katika ndege yangu binafsi na mwili  wa mwanaye, jamaa na watu wake nao wamepanda kwenye ndege nyingine na wale wajinga wake watatu. Kwenye ndege waliyo panda, kuna bomu liliko tegwa, na nitahitaji maamuzi yako kwamba tuwalipue wafie hewani au tuwaache waendelea na maisha yao?”
 
Swali la meja likanifanya nitazamane na Martin, taratibu nikamtazama meja usoni mwake, huku nikikumbuka uwenda wazimu ulio nipata jana usiku kutokana na ukweli walio uzungumza mume mwenzangu kwa Yemi na kujikuta nikisikia sauti moyoni mwangu ikihitaji niweze kumuangamizaa jamaa huyu kwani amenipotezea mwanamke aliye nipa furaha maishani mwangu.
 
ITAENDELEA
“Haya sasa Dany amepata nafasi ya kumuua kivuruga wa amani ya maisha yake je nini nini kitakacho endelea. Usikose shemu inayo fwata ya kisa hichi cha kusisimua na kuburidisha.”

Kalulumila:Dawa Bora ya Nguvu za Kiume na Maumbile Madogo

$
0
0
 BORA YA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO KALULUMILA.
----------------------------------------
Ni dawa pekee iliyojipatia umaarufu nchini na nje ya nchi kwa kufanya kazi mara 3, kwa wakati mmoja 1, kurefusha uume na kunenepesha saizi uipendayo kuongeza nguvu za kiume na inatibu matatizo na gerentii miaka 30. Na kuendelea haina madhara, inaimarisha mishipa ya uume iliyoregea na udhalishaji wa mbegu za kiume. 


---------NINI HUCHANGIA MATATIZO HAYA--Ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya ili kujua kwamba una ngiri ni chanzo kikubwa cha matatizo haya, ili kujua kama unangiri dalili zake ni kufika haraka kileleni wakati wa tendo la ndoa, 2)kushindwa kurudia tendo la ndoa. 3)kutoa choo kama cha mbuzi. 4)tumbo kujaa gesi na kuunguruma. 5)kukosa choo kabisa. 6)maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi. 7) korodani moja kuvimba 8)kutosikia hamu ya tendo la ndoa na maumivu ya kiuno wakati wa tendo la ndoa. 9)maumivu ya kiuno na mgongo pia tunatibu kisukari kwa siku7, presha, busha, bila kupasuliwa na magonjwa mbalimbali. 

---------------------------------------
TUPO TEGETA KWA NDEVU KARIBU NA MACHINJIO YA NGOMBE UTAONA OFSI IMEANDIKWA KALULUMILA HERBALIST CLINIC HOSPITAL SIMU .
----------------------------------------
-0655-557-182.
-0755-557182.
-0784-557-182.
PIA UTAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO.
---------------------------------------
KARIBUNI SANA.
----------------------------------------

Majaliwa Akagua Kiwanda Cha Korosho Cha Buko Na Kiwanja Cha Michezo Cha Ilulu Mjini Lindi

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwaamewaagiza Warajisi Wasaidizi wa Ushirika katika Mikoa yote inayolima korosho nchini waandae semina kwa Maafisa Ushirika, viongozi wa vyama vya msingi (AMCOS), maafisa ugani na wakulima ili kuwawezesha kubaini na kupanga korosho katika madaraja kuanzia ngazi ya vyama vya msingi.

Amesema jambo hilo litasaidia mkulima aweze kujua korosho aliyoipeleka ina ubora gani akiwa huko kijijini na wanapoifikisha kwenye ghala kuu wafanye kazi ya kuthibitisha , kwa hatua hiyo itasaidia kuondoa malalamiko kuhusu madaraja .

“Zoezi hili licha ya kuthibitisha ubora itasaidia kuboresha uzalishaji kwani wakulima wataelimishwa namna ya kuimarisha na kuboresha uzalishaji wa korosho nchini ikiwa ni pamoja na matumizi bora ya viatilifu ’’

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatano, Novemba 21, 2018) wakati alipotembelea kiwanda cha korosho cha BUKO kilichopo kwenye Manispaa ya Lindi, ambapo ameshuhudia korosho zikipimwa ubora kwenye ghala kuu lilipo kiwandani hapo.

Ameagiza semina ifanyike mwakani ili maafisa ushirika baada ya kupata mafunzo wawasaidie wakulima kwenye msimu ujao watambue korosho walizopeleka kuziuza zina ubora gani.

Waziri Mkuu amesema katika semina hiyo wakutane maafisa kilimo na maafisa ushirika ili wapate taaluma hiyo itakayowawezesha kupima korosho na kuitenga katika madaraja na kuwaondolea shida wakati wa mauzo.

Kwa upande wake, Mrajisi Msaidizi wa Ushirika mkoa wa Lindi, Robert Nsunza amemuhakikishia Waziri Mkuu kwamba wataandaa semina hiyo kwa wahusika na kuanzia hapo wakulima wakuwa wakitambua ubora wa korosho zao kuanzia ngazi ya  kijijini.

NayeMkurugenzi wa Kampuni ya Nangomba Holdings, Ramadhan Katau ambaye ndiye mtunzaji wa ghala la korosho katika kiwanda cha BUKO amesema ghala hilo linauwezo wa kupokea na kutunza tani 10,000 za korosho, hadi sasa tani zilizopo ghalani hapo ni 6,370. Hali ya ukusanyaji wa korosho inaendelea kwa kuwa sasa ndio katikati ya msimu .

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Watu 6 Watiwa Mbaroni Kwa Tuhuma zaWizi Jijini Mwanza

$
0
0
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza tunawashikilia wezi sita wa makosa ya kuvunja nyumba usiku na kuiba na kupatikana na vitu mbalimbali vya wizi katika operesheni kabambe inayoendelea katika kata ya Igogo Wilayani Nyamagana na maeneo mbalimbali.

Operesheni hiyo kabambe ya kipindi cha wiki moja imefanyika, baada ya kupatikana kwa taarifa toka kwa raia wema kwamba katika mitaa ya Maruru na Bugarika iliyopo kata ya Igogo Wilayani Nyamagana kipo kikundi cha wezi wanaofanya kazi ya kuvunja nyumba usiku na kuiba. Baada ya kupatikana kwa taarifa hizo, kikosi maalumu cha askari wenye uweledi wa hali ya juu kilifanya operesheni kabambe katika kata hiyo na kupita chocho kwa chocho na kufanikiwa kuwakamata wezi hao sita wakiwa na vitu hivyo walivyoiba.

Wezi hao waliokamatwa katika operesheni hiyo ni;
  1.  Wilium Alex, miaka 24, dereva bodaboda, mkazi wa igogo
  2.  Peter Deogratius, miaka 22, Mkazi wa Bugarika
  3.  David Yusuph, miaka 18, dereva bodaboda, mkazi wa bugarika
  4.  Godfrey Joseph, miaka 28, mkazi wa bugarika.
Aidha watuhumiwa wawili ambao ni;
  1.  Rashid Ramadhan, miaka 32, mkazi wa maruru – Igogo na
  2.   Ester Izack, miaka 55, makazi wa maruru –Igogo, hawa wanashikiliwa kwa kosa la kupokea vitu hivyo vya wizi na kuviuza kwa watu mbalimbali.
Pia wezi hao walikamatwa na vitu vifuatavyo;
  1.     Pikipiki mbili aina ya SUN LG, ya kwanza ina namba T.758 CAG chassess namba LBRSPKB 57J9001020 na Engine namba KL1162 FMI12TG1309 na ya pili ina namba T.680 BTJ chassess namba LKIPCKL11E1043123 na Engine namba 162FMJD0003787.
  2.     Engine moja ya pikipiki aina ya Sun LG yenye namba SL162FMJ-2*18913674*
  3.     Fridge moj ya aina ya LG.
  4.     Flat screen mbili aina ya  Samsung inchi 32 na meza ya TV Moja
  5.     Laptop mbili aina ya dell na Aspires
  6.     Computer moja aina ya desk top na monitor yake.
  7.     Radio Sub wooffer moja  aina ya LG na speaker zake tano na deck yake
  8.     Radio Sub wooffer moja aina ya Greevox na speaker zake mbili
  9.     Speaker tatu za radio aina ya Seapiano
  10.     King’amuzi kimoja aina ya Continental na remote tatu
  11.     Pasi mbili aina ya zec na nippotec
  12.     Jiko la gas aina ya ORYX na mtungi wa gas aina ya ORYX.
  13.     Safuria kumi, Magodoro mawili moja aina ya Supper banco na lingine aina ya Tanform na mashuka mawili makubwa.
  14.     Radio moja aina ya Kenwood RXD.V890 yenye namba 71101776.
  15.     Mitungi miwili mikubwa ya gas aina ya ORYX.
  16.     Fridge moja na Freezer mbili.
  17.     Televisheni tatu, ya kwanza aina ya SONY Inchi 16, ya pili aina ya SAMSUNG Inchi 18 na ya tatu aina ya Star times flat screen inchi 21.
  18.     Radio Sub wooffer tatu na speaker zake sita.
  19.     Computer desk top moja na CPU yake
  20.     Majiko matatu ya gas
  21.     Mashine moja ya kupimaq presha
  22.     Nguo mbalimbali zilizofungwa kwenye mafurushi mawili.
  23.     Bidhaa mbalimbali za dukani, mzani mmoja wa dukani, chupa tupu za bia cret tano na pasi mbili
  24.     Deck aina mbalimbali sita na remote mbalimbali kumi na tano
  25.     Bomba la kutolea moshi la pikipiki, meza ndogo moja na meza ya TV.
  26.     Mashine mbili za kunyoa nywele, chupa ya chai moja kubwa na viatu pea moja.
Vilevile wezi hao pia walikamatwa na vifaa mbalimbali walivyovitumia kutendea uhalifu wa kuvunja na kuiba ambavyo ni;
  1.     Mtalimbo mmoja wa chuma
  2.     Nondo kipande kimoja kilichochongwa
  3.     Mkasi mmoja mkubwa wa kukata makufuli
  4.     Bisi bisi tatu na mapanga mawili.
Polisi tunaendelea na mahojiano na watuhumiwa wote sita, huku msako mkali ukiendelea katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Mwanza. Pindi uchunguzi ukikamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza, tunatoa onyo kwa wananchi wa Jiji na Mkoa wa Mwanza hususani vijana wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu kuwa waache mara moja kwani ni kosa la jinia na endapo watabainika hatua stahiki za kisheria zitachukuliwa dhidi yao. Sambamba na hilo tunaendelea kuwaomba wananchi waendelee kutupatia ushirikiano kwa kutupa taarifa za uhalifu na wahalifu ili waweze kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

 

Tanzania yashinda Tuzo ya Utalii nchini Urusi

$
0
0
Tanzania imeshinda tuzo ya utalii kwa kuonekana ni eneo bora zaidi la utalii duniani nchini Urusi kwa mwaka 2018 (The Best Destination to the World in the Category of Exotic Destination 2018).

Leo tarehe 21 Novemba 2018, Balozi wetu nchini Urusi Mhe. Maj. Gen. (Mst). Simon Mumwi atapokea Tuzo hiyo kutoka Jarida la kirusi la “National Geographic Magazine” jijini Moscow kwa niaba ya nchi.  

Tanzania imepata ushindi huo kutokana na kura zilizopigwa kwenye mtandao wa jarida hilo la “National Geographic Magazine” lililoshirikisha wapiga kura 263,000 kwa njia ya mtandao.

Hii ni mara ya tatu katika kipindi cha miaka saba tokea mwaka 2011, raia wa Urusi kupitia jarida hilo wanaichagua Tanzania kama eneo bora zaidi la utalii. Mwaka 2011, Zanzibar ilipata tuzo ya ‘Star Travel’ kama eneo bora zaidi la utalii wa ufukweni katika bara la Afrika na mwaka jana, Tanzania ilipata tuzo ya NGT na Tanzania ilishinda nafasi ya pili katika tuzo hiyo  katika kundi la eneo bora la utalii duniani.

“National Geographic Traveller Awards” (NGT Awards) ni tuzo ya kifahari zaidi katika sekta ya utalii nchini Urusi na hutolewa na Jarida la kirusi la “National Geographic Magazine”.

Mafanikio hayo yanatokana na jitihada zinazofanywa na Serikali ya Tanzania kupitia Ubalozi wetu Urusi, Wizara za Utalii za Tanzania Bara na Zanzibar, na Taasisi zote zinazosimamia masuala ya utalii za ndani na nje ya nchi katika kutangaza vivutio vya utalii kwa nchi mbalimbali duniani ikiwemo Urusi.

Kupitia juhudi hizi, idadi ya watalii wanaokuja Tanzania kutoka Urusi imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Kwa mfano, idadi hiyo imeongezeka kutoka watalii 4,021 mwaka 2012 hadi watalii 10,060 mwaka 2017. 

Wizara kupitia Ubalozi wetu itaendelea kuongeza juhudi za kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo Tanzania na tunategemea kwa kushirikiana na wadau wengine katika juhudi hizi, idadi ya watalii kutoka Urusi wanaokuja nchini itaongezeka zaidi.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
21 Novemba 2018

Tanzia: Askofu wa kanisa Katoliki Jimbo la Mbeya, Evaristo Chengula afariki dunia

$
0
0
Askofu wa Kanisa Katoliki jimbo la Mbeya, Evarist Chengula amefariki dunia leo asubuhi akiwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete alipokuwa anapatiwa matibabu ya moyo.

Askofu Chengula alifika jijini Dar es salaam jana, akitokea Mbeya ambako alikuwa hajazidiwa sana na alifikishwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili kitengo cha Moyo (JKIC).

Katibu wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Padre. Charles Kitima amesema kuwa marehemu alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo yaliyochangiwa na umri wake ambapo amefariki akiwa na miaka 78.

"Baba Askofu hakuwa anaumwa sana lakini alikuwa na tatizo la Moyo ambalo alikuwa analimudu kawaida na alikuwa anaendelea na kazi kama kawaida mpaka Alhamisi iliyopita ameongoza misa takatifu hali ilipobadilika ndipo alimtafta daktari wake", amesema Padre. Kitima.

Padre Kitima amesema kuwa Askofu Chengula atazikwa jijini Mbeya siku ya Jumanne katika kanisa alilokuwa akihudumia Askofu.

Mwezi Machi mwaka huu, Askofu Chengula aliwataka wakristo kote nchini kujipanga kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2019 wa Serikali za Mitaa akiwataka wananchi kumchagua mtu asiyewafanya waishi kwa kuogopaogopa.

Alitoa kauli hiyo Machi 30, 2018 alipokuwa akiongoza ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika kitaifa katika kanisa Katoliki la Bikira Maria wa Fatma lililopo Mwanjelwa mjini Mbeya.

Pia katika ibada hiyo, alitolea ufafanuzi ujumbe uliotolewa na maaskofu wakatoliki akisema ujumbe ulikuwa haumlengi mtu fulani bali uliwalenga wanafiki wanaodai ni Wakristo lakini hawana imani ya Kikristo ili waweze kubadilika na kuwa watu wema.
 

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi ya Novemba 22

Fid Q Avurugana na Mameneja wa Diamond Kisa Tamasha la Wasafi Festival

$
0
0
Msanii wa Hip Hop, Fid Q amejikuta kwenye wakati mguu mara baada ya kuanza kushambuliwa na Mameneja wa WCB, Babu Tale na Mkubwa Fella mtandao. Hii ni kutokana na Fid Q kufanya tangazo la Fiesta ambalo wamelitafsiri ni kama kijembe kwao (Wasafi Festival).

Mameneja hao wamekuwa wakimshambulia Fid Q kwa madai kuwa licha ya kufanya muziki ameshindwa hata kununua gari dogo tu.

Sasa Fid Q amejibu hilo kwa urefu zaidi kupitia ukurasa wake wa  Instagram kwa kueleza kuwa haoni kama ni busara kwa yeye kuchaguliwa watu wa kufanya naye kazi.

==>> Hiki ni kile alichoandika;

Keki ya taifa ni kubwa sana na ina vipande vingi vya kuwatosha wachakarikaji wote wenye kuistahiki. Na kwakua Allah ndio mtoaji riziki, mimi kama mimi sina hayo mamlaka au hata hiyo roho mbaya ya kutamani wachakarikaji wenzangu mkwame katika harakati zenu.

Ninasema hivi ni kwasababu siku zote huwa siamini kama nitapungukiwa kitu nyinyi mkifanikiwa na siamini hivyo kwa sababu  ninajiamini mimi ni mchakarikaji na kipande changu cha KEKI bado kipo mezani kinaningojea (cha muhimu ni PUMZI na DUA tu ).

Ni ukweli tupo kwenye tasnia moja na kila mmoja wetu anajaribu kufanya lile alionalo sahihi ili kusogea mbele, na iko wazi mmeshafanya na mnaendelea kufanya mengi makubwa, nami bila kusita siku zote nimekua ni mtu wa kuwapongeza iwe kwa njia ya mitandao au tukutanapo ana kwa ana, mie hufanya vile kiroho safi pasina chembe yoyote ya unafiki.

Nimeyasema hayo hapo juu ili tu uweze au muweze kupata picha halisi ya kilichomo moyoni mwangu na pia kuwakumbusha ya kwamba mimi pia ninao uhuru wa kufanya shughuli zangu za sanaa na yeyote ambaye nimeridhia nae kimaslahi pasina kujali kama jicho la pembeni yangu linaiona faida iliyopo au laah.

Sioni ni busara kwa nyie kuja na kujaribu kunipangia yupi nifanye nae au yupi nisifanye nae ili kuwaridhisha machoni/ mioyoni mwenu.. na kama mnaamini ni haki yenu ya msingi mimi kuyafuata hayo matakwa yenu basi naomba nikujuzeni ndugu zangu mtakua mmeonyesha UBINAFSI wa hali ya juu kwenye hili.

Pia kumbukeni mimi pia nishawahi kuwa na matatizo na MJENGO.. lakini nilijikuta ninapambana peke yangu hadi UTULIVU uliporejea pasina msaada wa mtu yeyote na sikupambana peke yangu kwasababu hamkua na taarifa, taarifa mlikua nazo lakini ninafikiri mlikua mmetingwa na shughuli zenu za ujenzi wa taifa kiasi kwamba hamkuona kama kuniongezea nguvu ingesaidia lile zoezi kuisha haraka.

Kiukweli yale maneno ya kwenye promo ya“MOJAKUBWA”sikutegemea kama yangekua na uzito huu uliopelekea ndugu yangu uchafukwe kiasi cha kunifungulia bomba la matusi humu Insta..

kwanza sikumbuki hata kama niliyatamka kwa nia ya kuleta msigishano huu lakini kama kweli nimewakwaza... Naomba mnisamehe kibinadamu kwa hilo, naomba tumuache SHETANI apite na mwisho naomba nimalize kwa kusema BURUDANI sio VITA.

Msanii wa muziki kutoka nchini, Nigeria, Mr. Eazi aomba kutumbuiza Wasafi Festival

$
0
0
Msanii wa muziki kutoka nchini, Nigeria, Mr. Eazi ameomba kutumbuiza kwenye Wasafi Festival.

Harmonize kutokea WCB ndio ameweka wazi mazungumzo yake na Mr. Eazi kupitia mtandao ambapo alikuwa akimueleza kuhusu nia yake ya kutaka kutumbuiza kwenye tamasha hilo.

Hivi karibuni akiwa hapa nchini Mr. Eazi alieleza kuwa ameshafanya ngoma na Harmonize na muda wowote itatoka. 

Pia mradi wake uitwao M Pawa ambao umelenga kuwasaidia wasanii wapya 100 barani Afrika, alipata ushauri kutoka kwa Harmonize, Diamond na Ben Pol.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images