Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

CUF Watoa Tamko Baada ya Mbunge wao Abdallah Mtolea Kuhamia CCM

$
0
0
Mkurugenzi wa Habari wa Chama cha Wananchi (CUF), Abdul Kambaya amesema hamahama ya ya wabunge na madiwani wa upinzani kwenda Chama cha Mapinduzi (CCM) wengi wao wanafuata maslahi binafsi na sio kumuunga mkono Rais John Magufuli.

Kauli hiyo ya Kambaya imekuja siku moja baada ya aliyekuwa Mbunge wa Temeke kwa tiketi ya CUF Abdallah Mtolea kujiuzulu ubunge na nafasi zote za uongozi alizokuwa nazo ndani ya chama hicho jana Alhamis Novemba 15, bungeni jijini Dodoma na kutangaza kujiunga na CCM.

Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya CUF leo Ijumaa Novemba 16, Kambaya amesema chama hicho hakina mpango wala hakijaitisha kamati ya maadili na nidhamu ili kumjadili mwanachama yoyote si wiki ijayo wala mwezi ujao hivyo Mtolea aliamua kwa utashi wake mwenyewe kuhama na sio kwamba amesikia anataka kufukuzwa.

“Kuwa na mgogoro na chama hakuwezi kufanya uache ubunge kwasababu unapochaguliwa unaenda kufanya kazi ya wananchi na si chama, hivyo Mtolea kahama mwenyewe asisingizie alikosa ushirikiano. 

“Wengi wao wanaohamia CCM wanautaka ‘uWaitara’ kwa maana kuwa wanataka kuchaguliwa kushika nyadhifa serikalini kama kuteuliwa kuwa Waziri au Naibu Waziri  kama alivyoteuliwa mbunge wa Ukonga Mwita Waitara kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi, “ amesema Kambaya.

Muswada wa Marekebisho ya Vyama vya Siasa Wasomwa Kwa Mara ya Kwanza Bungeni

$
0
0
Muswada wa Marekebisho ya Vyama vya Siasa wa mwaka wa fedha 2018 umesomwa kwa mara ya kwanza bungeni leo Ijumaa Novemba 16, 2018.

Katika muswada huo miongoni mwa mambo yanayopendekezwa ni kuongezwa kwa kifungu ambacho kitamwezesha Msajili wa Vyama vya Siasa kusitisha usajili wa chama cha siasa kitakachovunja masharti ya sheria.

Muswada huo umesomwa kwa mara ya kwanza bungeni ambapo Mwenyekiti wa Bunge Andrew Chenge amesema Spika wa Bunge, Job Ndugai ataipangia Kamati ya Bunge itakayofanya uchambuzi.

“Kifungu cha 19 kinapendekezwa kurekebishwa ili kumwezesha msajili wa vyama vya siasa kufuta usajili wa chama cha siasa kitakachobainika kuwa kilipata usajili kwa njia zisizo za halali,” sehemu ya sababu ya muswada huo imesema.

Pia, muswada huo unalenga katika kuzuia viongozi wa vyama vya siasa kutokuwa wajumbe wa bodi ya wadhamini.

“Muswada pia unapendekeza kufuta kifungu cha 21A na kifungu cha 21B kinapendekezwa kufanyiwa marekebisho ili kuliwezesha Baraza la Vyama vya Siasa kupata fedha kutoka katika bajeti ya Serikali na wafadhili,” amesema.

Muswada huo unapendekeza pia kuongezwa kwa vifungu ili kuainisha makosa na adhabu na kusitishwa kwa usajili wa vyama vya siasa vitakavyokiuka masharti ya sheria.

Pia, inapendekeza kufanyiwa marekebisho ili kumpa mamlaka waziri mwenye mamlaka ya kutengeneza kanuni za uandaaji wa taarifa za hesabu za vyama vya siasa na mambo yatakayojumuishwa katika katiba za vyama vya siasa.

Rayvanny na Diamond wairudisha video ya wimbo wao wa Nyegezi- Mwanza Youtube

$
0
0
Ikiwa ni siku mbili tangu msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Rayvanny achukue maamuzi magumu ya ku-block wimbo wake usitazamwe Tanzania baada ya kuamriwa kufanya hivyo na BASATA, hatimaye msanii huyo ameurudisha tena wimbo huo kwenye mtandao wa YouTube.

Mpaka sasa hakuna tamko lolote kutoka Basata wala kwa Lebo ya WCB ambayo inammiliki msanii Rayvanny kuhusiana na video hiyo.

Video ya Mwanza mpaka wakati huu ni Trending namba Youtube huku ikiwa na watazamaji zaidi ya million 2.4 kwa muda wa siku tano.

Mizizi 29 Power Ni Dawa Ya Nguvu Za Kiume Ambayo Imechanganywa Na Mizizi 29

$
0
0
Kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wanaume wazee hata na vijana kupungukiwa au kutokuwa kabisa na nguvu za kiume nanimekuwa nikipigiwa simu na wanawake wakilalamika ndoa zao zipo mashakani maana hawaridhishwi na Waume au wapenzi wao pale wanapoaza kushiriki tendo la ndoa 

Kwa Nini Ujione Mpweke Pale Ukutanapo Na Mpenzi Au Mke Wako Kisa Eti Hauna Nguvu Za Kiume? ;Tumia MIZIZI 29 POWER, hii ndio tiba itakayorudisha heshima ya ndoa yako . 

Dawa hii itakufanya;
 1 Uchelewe kufika kileleni mda wa dakika 15-25 kwa tendo la kwanza 
2 Dawa hii itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 
3  Dawa hii uhimalisha misuri iliyolegea na kusinyaa?dawa hizi hazina madhara kwa mtumiaji nani tofauti na ulizowai kutumia ata wazee wenye umri mkubwa wanapona 

NSONSOMA; Dawa hii itakufanya umridhishe  mke au mpenzi wako kwani uboresha uume saizi upendayo urfu wa nchi 5,6,7 na 8 na unene wa sentimita 2,3,4 na 5 dawa  hii ipo ya kupaka na kunywa 

NSHOLA; NI dawa ya uzazi kwa waliongaika mda mrefu bila kupata mtoto 

MWITA; Dawa hii humvuta meme, mke,au mpenzi mliyetengana pia umrudisha mtu kazini haliyefukuzwa, kumpatanisha mwajiliwa na bosi wake 

Tunatibu presha kisukari, busha ,vidonda vya tumbo tumbo kuunguruma kujaa gesi na kukosa choo 

MAHALI ILIPO OFISI; PANDA DALADALA SHUKA BUGURUNI MALAPA AU ROZANA NA MWANZA YUPO WAKALA PIGA SIMU 0752348593 DR NYAROBI .Kama hauna nafasi ya kuja ofisini utaletewa popote ulipo huduma hizi

Huna Sababu Ya Kuaibika tena............ Jipatie Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume, Maumbile Madogo Na Mvuto Wa Mapenz

$
0
0
Usikate tamaa ondoa maradhi yako, maana matatizo haya yamekua yakiasili watuwengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona wako tofauti sana na wengine kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamapunguvu katika mwiliwake.

Kunasababu nyingi sana zinazosababisha matatizo haya, chango hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngili :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli. Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na marakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kushindwa kabisa

MASISA 3POWER :- nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa mfumo wa vidonge, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka 15-90 , inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uludie tendo la ndoa zaidi ya mara nne (4) birahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya dk (20-30 )

YONINANI:- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwa mda mfupi sana,

SUPER MORINA :- nidawa inayotibu ama kutatua tatizo la kisukali kwawaliohangaika bila mafanikio, huondoa tatizo la kisukali na kupona kabisa, vilevile ninadawa ya magonjwa sugu km vile presha, vidondo vya tumbo, miguu kuwakamoto, muwasho mwilin, kaswende,uzazi nk.

LUGIMBA :- nidawa ya mvuto wa mapenzi, humtuliza mke, mme, mchumba, hawara au mtu yoyote umpendae na kumfanya akutimizie chochotekile unachokitaka kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu yoyote zaidi yako.

WASILIANA NA DR CHIPUPA NAPATIKANA DAR ES SALAAM KUMBUKA HUDUMAHII ITAKUFIKIA POPOTE ULIPO  0759208637 / 0622344969

Waziri Mkuu: Serikali Imetunga Sheria Kuongeza Udhibiti Sekta Ndogo Ya Fedha

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali iliamua kutunga Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha ya mwaka 2018 ili kuongeza udhibiti wa sekta ndogo ya fedha.

“Kwa muda mrefu sekta ndogo ya fedha haikuwa na udhibiti wa kutosha. Hali hiyo ilisababisha kuwepo na uendeshaji usio rasmi wa shughuli mbalimbali za kifedha kama vile, taasisi zinazochukua amana, vikundi vya fedha vya jamii na wakopeshaji binafsi,” amesema.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Novemba 16, 2018) bungeni mjini Dodoma wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa 13 wa Bunge. Bunge limeahirishwa hadi Januari 29, mwakani.

Amesema shughuli hizo ambazo nyingi ziliendeshwa katika utaratibu usio rasmi, ziliwaletea wananchi athari mbalimbali ikiwemo kupoteza mali zao zilizowekwa kama dhamana kwenye taasisi hizo.

Amesema baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu wamekuwa wakitumia mwanya wa kutokuwepo udhibiti wa kutosha kwenye sekta hiyo ndogo ya fedha kuendesha vitendo mbalimbali vya kihalifu ikiwemo utakatishaji fedha.

“Kutokana na sababu hizo, Serikali iliamua kutunga Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha ya mwaka 2018 kwa lengo la kuongeza udhibiti wa sekta hiyo ndogo ya fedha na kuiwezesha kuchangia ipasavyo katika kuimarisha uchumi wa nchi yetu na kulinda mali na fedha za wananchi wetu,” amesema.

Serikali iliwasilisha Muswada wa Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha wa mwaka 2018 (The Microfinance Act, 2018) ambao umesomwa kwa hatua zake zote na kupitishwa na Bunge, ukisubiri kibali cha Mheshimiwa Rais ili uwe sheria kamili.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema hali ya usalama barabarani bado ina changamoto nyingi licha ya takwimu kuonesha kupungua kwa matukio na vifo vinavyosababishwa na ajali hizo.

Akitoa mfano kuhusu matukio ya ajali nchini, Waziri Mkuu amesema katika mwaka 2016 matukio ya ajali za barabarani yalikuwa 9,856 ikilinganishwa na matukio 5,578 katika mwaka 2017 ambayo ni pungufu kwa matukio 4,278 sawa na asilimia 43.

Akifafanua zaidi, amesema katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Oktoba 2018, matukio ya ajali za barabarani yalikuwa 3,209 ikilinganishwa na matukio 5,578 katika kipindi cha kuanzia Januari hadi Desemba mwaka jana.

Amesema Serikali inachukua hatua mbalimbali kukabiliana na matukio ya usalama barabarani ikiwemo kuendesha operesheni za kuhakikisha sheria zote za usalama barabarani zinafuatwa kikamilifu.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, NOVEMBA 16, 2018.

Serikali Yatoa Sh. Bilioni 83 Kuimarisha Elimu.....Waziri Mkuu aonya wanaoshiriki wizi wa mitihani

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kati ya Julai na Oktoba, mwaka huu, Serikali imetoa jumla ya sh. bilioni 83.2 ili kuimarisha usimamizi na uendeshaji wa shule nchini.
 
Waziri Mkuu amesema, kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 38.6 zilipelekwa kwenye shule za msingi na shilingi bilioni 44.6 zilienda kwenye shule za sekondari ikiwa ni utekelezaji wa mpango wa elimumsingi bila malipo.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Ijumaa, Novemba 16, 2018) bungeni mjini Dodoma wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa 13 wa Bunge. Bunge limeahirishwa hadi Januari 29, 2019.

“Katika kuimarisha usimamizi na uendeshaji wa shule nchini, Serikali inapeleka fedha za elimumsingi bila malipo moja kwa moja shuleni. Kwa mfano, katika kipindi cha Julai hadi Oktoba, 2018 shilingi bilioni 38.6 zilipelekwa katika shule za msingi na shilingi bilioni 44.6 kwenye shule za sekondari,” amesema.

Amesema tangu kuanza kutekelezwa kwa mpango wa elimumsingi bila malipo, uandikishaji wa watoto wa darasa la awali na darasa la kwanza umeimarika na kwamba kumekuwepo na mwenendo mzuri wa ufaulu kwenye mitihani ya kumaliza darasa la saba.

“Kumekuwepo na mwenendo mzuri wa ufaulu katika mitihani ya kumaliza darasa la saba, ambapo mwaka 2016 ilikuwa wastani wa asilimia 70 na mwaka 2018 ilikuwa ni wastani wa asilimia 78. Hali hiyo, imeongeza mahitaji mbalimbali, ikiwemo miundombinu katika shule zetu za msingi na sekondari,” amesema.

Waziri Mkuu amesema katika kukabiliana na hali hiyo, Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu inaendelea na mikakati ya ujenzi na ukamilishaji wa miundombinu muhimu ya shule.

“Kwa mfano, kupitia programu ya Lipa Kulingana na Matokeo katika Elimu (EP4R), shilingi bilioni 53.4 zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya shule za msingi na sekondari.  Aidha, shilingi bilioni 9.2 zimeelekezwa katika uimarishaji wa miundombinu ya elimu kupitia programu ya kuboresha elimu ya shule za msingi (EQUIP-T),” amesema.

Amesema Serikali itaendelea kuimarisha miundombinu na kuweka mazingira mazuri katika mfumo mzima wa elimu nchini kwa kushirikiana na wadau wote.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amesema taasisi zote zinazohusika na usimamizi na uendeshaji wa mitihani ya taifa hazina budi kuhakikisha zinasimamia kikamilifu mitihani hiyo ili kuepuka udanganyifu.

“Natambua kuwa mitihani ya taifa kwa darasa la nne, kidato cha pili na kidato cha nne inaendelea. Hata hivyo, katika kipindi cha hivi karibuni kumezuka matukio ya kuvuja kwa mitihani.”

“Naziagiza taasisi zote zinazohusika na usimamizi na uendeshaji wa mitihani ya taifa kuhakikisha wanasimamia kikamilifu mitihani hiyo ili kuepuka udanganyifu. Itakapobainika kuwepo kwa udanganyifu wa mitihani, hatua stahiki zichukuliwe kwa mujibu wa sheria dhidi ya yeyote atakayehusika,” amesisitiza.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, NOVEMBA 16, 2018.

Waziri Mkuu: Maonesho Ya Viwanda, Biashara Na Madini Yanapaswa Kuigwa Na Mikoa Mingine

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema maonesho ya viwanda vidogo na biashara ndogondogo pamoja na yale ya teknolojia na uwekezaji katika sekta ya madini yanayofanyika nchini ni ubunifu muhimu na hauna budi kuigwa na mikoa mingine.

“Ubunifu huu wa kufanya maonesho ya viwanda ya kimkoa, kikanda na kitaifa ni jambo muhimu sana. Maonesho haya, yanatupa fursa ya kujitangaza na kutathmini hatua tuliyofikia katika utekelezaji wa ajenda ya ujenzi wa uchumi wa viwanda na kubaini changamoto zilizopo,” amesema.

Akizungumza wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa 13 wa Bunge leo (Ijumaa, Novemba 16, 2018) bungeni mjini Dodoma, Waziri Mkuu amesema maonesho hayo yanahamasisha wananchi wengi zaidi washiriki kwenye ujenzi wa uchumi wa viwanda.

“Napenda kuielekeza mikoa mingine iige mifano hiyo ya mikoa ya Pwani, Simiyu na Geita ili kuhamasisha wananchi na wadau wengine washiriki ipasavyo katika ujenzi wa viwanda na kuleta teknolojia mpya za viwanda na sekta ya madini,” amesema.

Amesema mbali ya kujifunza teknolojia mpya, maonesho hayo yanatoa fursa kwa wadau husika kukutana na kubadilishana utaalam na uzoefu mbalimbali.

“Napenda nitumie fursa hii kuwapongeza Wakuu wa Mikoa ya Pwani, Simiyu na Geita kwa ubunifu wao huo. Vilevile, niwapongeze sana wazalishaji wenye viwanda na madini pamoja na wadau wote walioshiriki kuonesha teknolojia mbalimbali na bidhaa mpya za kilimo na madini katika maonesho hayo.”

Amesema kupitia maonesho hayo, wachimbaji hao wadogo, pia waliweza kukutana na wataalamu wanaosimamia sekta ya madini na mabenki kwa lengo la kujifunza matumizi ya teknolojia mpya sambamba na kufahamu taratibu mbalimbali za kupata mikopo ya kuendesha shughuli zao za uchimbaji madini.

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwataka wananchi wajenge utamaduni wa kutumia bidhaa zinazozalishwa nchini ili kulinda viwanda vya ndani na kukuza uchumi.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Tanzania inakabiliwa na changamoto kubwa ya uharibifu wa mazingira na vyanzo vya maji na kwamba hatua stahiki hazina budi kuchukuliwa ili kudhibiti hali hiyo isiendelee.

Akitoa mfano Waziri Mkuu amesema: “Miradi mingi ya maji nchini imekwama au kutoleta tija kutokana na uharibifu wa mazingira na vyanzo vya maji. Hivyo, niwasihi Wabunge wenzangu muwahamasishe wananchi na wadau kutoa maoni yatakayosaidia kujenga na kuboresha vema sheria zinazokusudiwa kulinda mazingira yetu pamoja na vyanzo vya maji.”

Hata hivyo, Waziri Mkuu amebainisha faraja aliyoipata wakati alipofanya ziara ya kikazi wilayani Lushoto na kukuta mazingira yametunzwa vizuri na uoto wa asili umehifadhiwa, na akaagiza Halmashauri nyingine ziige mfano huo wa utunzaji mazingira.

“Katika ziara yangu ya hivi karibuni wilayani Lushoto, nilifarijika mno kuona jitihada kubwa zinazofanywa na wananchi wa wilaya hiyo katika kuhifadhi mazingira. Nitumie fursa hii kuwapongeza wananchi wa Halmashauri za Wilaya ya Lushoto na Bumbuli kwa utunzaji mzuri wa mazingira. Naziagiza Halmashauri nyingine nchini ziige mfano huo mzuri wa kuhifadhi mazingira,” amesema.

Bunge limeahirishwa hadi Januari 29, mwakani.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, NOVEMBA 16, 2018.

Vikundi Vya Upatu Kutosimamiwa Na Sheria Mpya Huduma Ndogo Za Fedha

$
0
0
Na Farida Ramadhani, WFM, Dodoma
Serikali imesema kuwa vikundi vya Upatu havitasimamiwa chini ya Sheria mpya ya Huduma Ndogo za Fedha ya Mwaka 2018 (The Microfinance Act, 2018) kwa sababu havijihusishi na biashara ya huduma ndogo za fedha.

Hayo yameelezwa bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) wakati akihitimisha hoja za mjadala wa Muswada wa Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha ya Mwaka 2018.

Dkt. Mpango alisema Sheria hiyo itahusisha taasisi kama vile Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo (SACCOS), Taassi za huduma ndogo za fedha zisizopokea na zinazopokea amana na vikundi vya kifedha vya kijamii, wakopeshaji binafsi na asasi za kijamii.

Alieleza kuwa Sheria hiyo pia inalenga kuwalinda wananchi wanaotegemea sekta ndogo ya fedha katika kuendesha maisha yao na shughuli za kiuchumi kwa ujumla na itasimamia na kudhibiti biashara ya huduma ndogo za fedha, kuwawezesha watumiaji na watoa huduma hiyo pamoja na kudhibiti changamoto zinazoweza kutokea katika sekta hiyo.

“Madhumuni ya Sheria hiyo ni kuwatambua watoa huduma ndogo za fedha kwa lengo la kuwasimamia, kupata takwimu, kuwalinda na kuwawezesha watumiaji wa huduma ndogo za fedha”,  alisema Waziri Mpango.

Dkt. Mpango aliongeza kuwa Sheria hiyo imeweka utaratibu wa kuiwezesha Benki Kuu kutoa elimu kwa watumiaji wa huduma ndogo za fedha hususan vikundi vya kijamii kwa lengo la kunufaika na fursa zilizopo.

Aliongeza kuwa wakati Benki Kuu itakapolazimika kusimamia Taasisi za huduma ndogo za fedha, taasisi hizo  hazitatozwa fedha kugharamia majukumu ya Benki Kuu.

Akizungumzia maoni wa wabunge kuhusu daraja la nne la Sheria hiyo linalohusu vikundi vya kifedha vya kijamii, wakopeshaji binafsi na asasi za kijamii, Waziri Mpango alifafafanua kuwa Sheria hii imebainisha kwamba kutaandaliwa kanuni na miongozo mahsusi kwa ajili ya kusimamia daraja hilo.

“Sheria hii inaainisha shughuli mbalimbali zinazoweza kufanywa na mabenki na taasisi za fedha zinazoweza kusaidia katika kulea na kukuza watoa huduma wa daraja la nne. Miongoni mwa shughuli hizo ni pamoja na utoaji mikopo yenye msharti nafuu na elimu ya fedha”, alisema Dkt. Mpango.

Alisema kuwa Serikali imejipanga kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa usimamizi wa daraja la nne. Mwongozo kwa ajili ya maandalizi ya bajeti ya 2019/20 umetoa maelekezo kwa Halmashauri zote kutenga fedha kwa ajili ya kazi hii.

Aidha, baada ya Waziri Mpango kuwasilisha hoja hizo, Bunge lilipitisha Muswada wa Sheria hiyo ambao umeundwa baada ya kujitokeza changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ndogo ya fedha ikiwemo Taasisi za huduma ndogo za fedha kutoa mikopo kwa wananchi kwa vigezo na masharti magumu na hivyo kusababisha madhara kwa wananchi ikiwemo mali zao kuuzwa pasipo kufuatwa kwa taratibu za kisheria.

Mwisho

Akamatwa Akimfanyia Mdogo Wake Mtihani Wa Kidato Cha Pili.

$
0
0
Na John Walter, Manyara.
WATU wawili wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa Manyara kwa kosa la kufanya udanganyifu kwenye mtihani wa Kitaifa wa kidato cha pili.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Kamanda wa polisi mkoani hapa Kamishna Msaidizi wa Polisi Augustino Senga alisema kuwa mitihani inaendelea vizuri isipokuwa  Novemba 12 mwaka huu lilitokea tukio moja la udanganyifu ambapo mwanafunzi ambaye tayari  amemaliza shule, aliamua kurudi shuleni kwa kushirikiana na  watumishi wa elimu wasio waaminifu.

Mwanafunzi huyo aliyemaliza masomo yake  aliweza kuingia darasani na  kufanya mtihani kwa kutumia jina la mdogo wake ambaye amekuwa mtoro  shuleni kwa kipindi kirefu kwa madhumuni ambayo anayajua yeye ama kuendelea na mafunzo ama elimu au kwa njia yoyote ili.

“Tukio hili llitokea  Novemba 12  mwaka huu ambapo Ofisa elimu kwa kushirikiana na polisi walipata taarifa kutoka kwa wasiri wetu kwamba kuna mwanafunzi ambaye ameingia kwenye chumba cha mtihani na hafahamiki na wale wanafunzi.

“Baada ya kufuatilia katika shule ya sekondari Qameyu iliyopo wilaya ya Babati mkoa wetu wa Manyara, kijana aitwaye Malkiad Massay mwenye miaka 18 alibainika akiwa katika chumba cha mtihani akifanya mtihani wa upimaji wa Kitaifa wa kidato cha pili huku akitumia jina la mwanafunzi aitwaye Martine Massay  wa kidato cha pili.

“Jina hili la kijana huyu amekuwa mtoro sana shuleni kwa kipindi kirefu na huyu mtuhumiwa Malkiad Massay ni kaka yake  wa baba mmoja na mama mmoja na kama nilivosema mwenye jina hilo amekuwa mtoro wa muda mrefu kwa hiyo kaka yake alitumia njia hiyo ya kuingia kwenye chumba cha mtihani ili aweze kufanya mtihani wa mdogo wake.

“Hii tunaamini walishirikiana na watendaji akiwepo mwalimu mkuu na watu wengine kwa sababu sio rahisi mwanafunzi akaingia pale bila kujua ambaye anajua mwanafunzi ni yupi anayetakiwa kufanya mtihani pale, kwa hiyo akawa amebainika akiwa ameshafanya mtihani mmoja ule wa kwanza.

“Basi kijana huyo amekamatwa lakini pia na mkuu wa shule hiyo anashikiliwa kwa mahojiano, mwalimu mkuu wa shule hiyo anaitwa Severine Umbaida mwenye miaka 58 ambaye pia ni mkazi wa Qameyu.

“Tukio hili ni la kufedhehesha ambalo  halina tija   kwenye elimu yetu na tunaamini katika uchunguzi wetu na wengine wote waliohusika na hili kwani hawa ni wa awali tu tutahakikisha tutawatia mbaroni na sheria itafuata mkondo wake.

“Tunataka watu wafanye mitihani kwa haki na kwa halali lakini  taarifa za awali zinaonyesha kwamba kijana huyu alishamaliza kidato cha nne na akafeli huko wilaya ya Mbulu mkoa hapa kwa hiyo alikuwa na nia ya kufanya mtihani huo labda apate kuendelea hapo ama mahali pengine na uchunguzi wetu utabaini kwa kadri tutakavoendelea na upelelezi”, Alieleza Kamanda Senga.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi ya Novemba 17

Benki ya Dunia Yaipatia Tanzania Bilioni 680 kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kuongeza ubora wa elimu

$
0
0
Benki ya Dunia imeridhia kuipatia Tanzania Dola za Marekani milioni 300 (Sh. bilioni 680.5) kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kuongeza ubora wa elimu ya sekondari.

Fedha hizo zinakusudiwa kutumika kujenga vyumba vya madarasa, mabweni, maabara, nyumba za watumishi na kununua vifaa vya kufundishia.

Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika, Dk. Hafez Ghanem, alisema hayo jana alipokutana na Rais John Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, Dk. Ghanen alisema pamoja na kuridhia kutoa fedha hizo, benki hiyo inaendelea kufadhili miradi mbalimbali ya maendeleo nchini yenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 5.2 (zaidi ya Sh. trilioni 13) na kwamba miradi hiyo inatekelezwa kutokana na uhusiano na ushirikiano mzuri kati yake na Tanzania.

Dk. Ghanem alisema katika mazungumzo hayo, walijadili juu ya maendeleo ya miradi hiyo na kazi nzuri ambayo inafanywa na Tanzania kuimarisha uchumi. Pia alimpongeza Rais Magufuli kwa matokeo mazuri katika mapambano dhidi ya rushwa na kuimarisha huduma za jamii.

Kwa upande wake, taarifa hiyo ilisema, Rais Magufuli aliishukuru Benki ya Dunia kwa ushirikiano na uhusiano mzuri na Tanzania na kuahidi kuwa serikali itaendeleza na kukuza uhusiano huo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha fedha zote zinazotolewa kwa ajili ya maendeleo zinatumika kwenye miradi iliyokusudiwa.

“Namshukuru Dk. Ghanem na Benki ya Dunia kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya miradi ya Tanzania. Hizo Dola Milioni 300 ambazo baadhi ya watu wasiotutakia mema walisema zimefyekelewa mbali, anasema zitaletwa.

“Pia Benki ya Dunia imetoa Dola bilioni 5.2 ambazo zinafadhili miradi mbalimbali ya elimu, nishati, barabara, kilimo, afya na maji, ni miradi mikubwa na mingi. Kwa hiyo amekuja kututhibitishia kuwa Benki ya Dunia haitatuacha,” alisema Rais Magufuli.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James, aliitaja baadhi ya miradi inayoendelea kutekelezwa kwa ushirikiano na Benki ya Dunia kuwa ni pamoja na uboreshaji wa bandari ya Dar es Salaam ambayo ujenzi wake umefikia asilimia 24.

Aliitaja mingine kuwa ni ujenzi wa barabara za juu katika makutano ya barabara eneo la Ubungo, jijini Dar es Salaam na ujenzi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka (BRT) kwa awamu ya kwanza na ya pili.

Mazungumzo kati ya Mhe. Rais Magufuli na Dk. Ghanem yalihudhuriwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Augustine Mahiga; Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi; Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako; Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu; na Mwakilishi wa Benki ya Dunia nchini, Bella Bird.

Vyama Vya Msingi Vya Ushirika 35 Vyanufaika na Malipo ya Korosho ya Rais Magufuli

$
0
0
Na Judith Mhina –Maelezo
Waziri wa Kilimo Japhet Asungwa amesema zoezi la awali la uhakiki  wa Wakulima , maghala na Vyama vya Msingi vya Ushirika vilivyopokea  korosho umekamilikana kuingiziwa fedha zao benki..

Waziri Asungwa amethibitisha hilo alipoongea na Waandishi wa Habari katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara jana jioni.

Waziri Asungwa amesema “Mpaka leo kuna jumla ya Vyama vya Msingi vya Ushirika 35 ambvyo vimekithi vigezo  vya kulipwa. Hivyo zoezi linaloendelea katika National Microfinance Bank – NMB na  kuingiza majina ya wakulima na wale wasio na account kufunguliwa na kuingize fedha  kulingana na koroshoalizowasilisha ghalani.

 Vyama hivyo  vya Msingi  kutoka  Tandahimba Newala Cooperative Union 10 – TAMECU, Tunduru Agricaltural Marketing Cooperative Union  6, TAMCU, Masasi, Mtwara na Nanyamba  Cooperative Union – MAMCU 15,  na Lindi  – Mwambao Cooperative Union 4  ambayo inashirikisha Lindi Mji na Lindi Vijijini.

Aidha Waziri Asungwa amefafanua kuwa fedha hizo zimeingizwa NMB na Tanzania Agricultural Development Bank – TADB kama agizo lilivyosema . Pia, wakulima watambue kuwa korosho zote zilizopo ghalani ni za msimu huu na zina daraja la kwanza hivyo zinastahilini kulipwa kwa kiwango alichotamka Rais Magufuli.

Tanzania ina jumla ya viwanda 23 Tanzania nzima ambapo vikifanya kazi vyote kwa ufanisi vinauwezo wa kubangua korosho 120,000  na kuleta ajira kwa Watanzania takriban. Hata hivyo kutokana na ukosefu wa malighafi katika viwanda vya ndani na mitaji midogo ya wawekezaji wetu korosho inayobanguliwa kwa sasa ni elfu 29 tu.Ameongeza Waziri Asungwa.

Katika kuonyesha umuhimu wa zao la korosho kwa Watanzania Waziri Asongwa alisema kuwa umla ya Kaya laki 750 zinalima zao la korosho na kuna jumla ya vyama vya Ushirika vya korosho 617, ambapo 503 vipo Mtwara lindi na Ruvuma, 98 vipo Mkoa wa Pwani na Tanga na 14.  

Akionya tabia iliyojitokeza kwa baadhi ya wakulima wasio waaminifu Waziri Asungwa amesema kuwa wapo wakulima wanaoleta korosho chafu katika maghala ambazo zimeshapoteza ubora wake na zinaonekana ni za mwaka jana na kuwaomba waache mara moja .

Pia kuna wakulima wasio waaminifu wanaoleta korosho kutoka nchi ya jirani ya Msumbiji ambapo wameona Tanzania ina bei nzuri ya korosho na kuwaagiza waache mara moja kwa sababu sheria za kimataifa za biashara haziruhusu.

Alipoulizwa kuhusu hatua zilizochukuliwa kwa korosho magunia 152 yaliyokamatwa yakitokea Msumbiji Waziri alisema magunia yote yametaifishwa.Pia, akawaomba wakulima watoe ushirikiano katika kutoa taarifa zozote zenye lengo la kuharibu zoezi zima la ununuzi wa korosho.

Mwisho Waziri aklitoa wito kwa wakulia kuwa waangalifu na fedha wanazoingiziwa wazichukue kwa mkupuo maana italeta madhara ya usalama wao na pia wajenge tabia ya kuweka akiba na kutumia kidogo kidogo wakikumbuka kuna madeni wanadaiwa na pia kuna msimu wa kilimo ujao unahitaji fedha kwa ajili ya kuzalisha korosho bora na nyingi zaidi kuliko mwak ahuu.

Katika kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ya kuacha asilimia kadhaa ya korosho hapa nchini kwa ajili ya kuhamasisha ubanguaji na kuinua ajira kwa wananchi 

Picha na MAELEZO; 

Askari Mmoja wa JWTZ Auawa Katika Makabiliano na Waasi DRC

$
0
0
Wanajeshi saba wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) wameuawa akiwamo askari mmoja wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika operesheni ya kijeshi iliyofanywa mashariki mwa nchi hiyo.

Msemaji wa Umoja wa Mataifa (UN), Stephane Dujarric amesema kati ya waliouawa sita  ni kutoka Malawi na askari mmoja wa Tanzania.

Askari hao waliouawa katika mapigano yaliyozuka karibu na mji wa Beni Kaskazini mwa Kivu, Mashariki mwa Congo eneo ambalo limeathiriwa zaidi na mlipuko wa homa ya ebola.

"Ripoti za awali zinaonyesha kuwa askari 10 walijeruhiwa na mmoja hajulikani aliko,” alisema Dujarric katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini New York, Marekani.

Duru za habari zinasema kikosi hicho cha kulinda amani kilikuwa katika operesheni ya kukabiliana na wapiganaji wa kundi la waasi la Allied Democratic Forces (ADF).

Taarifa zaidi zinasema walinda amani kadhaa wa jeshi la Congo nao pia wameripotiwa kuuawa au kujeruhiwa katika operesheni hiyo.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ametuma salamu za rambirambi kwa familia ya walinda amani waliouawa na kwa serikali za Tanzania na Malawi.

Vikosi vya waasi vimekuwa vikiendesha mapigano ya mara kwa mara nchini humo na tangu mwaka 2014 vimehusika katika mauaji ya mamia ya raia na askari 15 wa UN kutoka Tanzania waliouawa Desemba mwaka jana katika wilaya ya Beni.

Leo Ijumaa Novemba 16, 2018 akiwa mkoani Tanga, Mkuu wa Majeshi nchini Tanzania (CDF) Jenerali Venance Mabeyo amewataka Watanzania kuwa watulivu katika kipindi hiki ambacho askari wake ameuawa kwenye mapigano hayo.

Amesema tukio hilo halijalikatisha tamaa Jeshi la Tanzania bali limesababisha kutafuta mbinu nyingine za kuendesha mapambano

Rais Magufuli Kufungua Mkutano Wa 21 Baraza La Mawaziri Nchi Wanachama Wa Mto Nile

$
0
0
Rais John Magufuli, anatarajia kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano wa 21 wa Baraza la Mawaziri wa Maji katika nchi wanachama Bonde la Mto Nile zilizoko kwenye ukanda wa Maziwa Makuu (NESLAP).

Katika mkutano huo utakaofanyika Novemba 22, mwaka huu, jijini Dar es Salaam, baadhi ya mambo yatakayojadiliwa ni pamoja na kupitia utekelezaji wa masuala mbalimbali ya miradi, kupokea taarifa ya utendaji, hali ya ulipaji wa michango ya mwaka kwa kila nchi mwanachama na tathmini ya watumishi wa sekretarieti ya NELSAP.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Prof. Makame Mbarawa, alisema jana jijini hapa kuwa, Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano huo ambao ni wa kawaida wa kiutendaji.

"Baraza la mawaziri wa maji ndicho chombo cha juu kabisa cha uamuzi katika kusimamia na kuendesha shughuli za bonde la Mto Nile katika ukanda wa Maziwa Makuu na mkutano huu ufanyika mara moja kila mwaka kufuata mzunguko katika nchi wanachama," alisema Prof. Mbarawa.

Aidha, alisema mkutano huo utatanguliwa na vikao vya wataalamu vitakavyoanza Novemba 20 hadi 21, jijini Dar es Salaam.
 
"Vikao hivyo vya wataalam ambavyo ni vya kiutendaji hufanyika mara mbili kwa mwaka kufuata mzunguko katika nchi wanachama," alisema Prof Mbarawa.

Aliongeza kuwa, ushirikiano wa nchi za bonde la Mto Nile ni wa muda mrefu ambao ulianza tangu mwaka 1960 na ilipofika Februari 22, 1999 nchi wanachama ziliunda taasisi ya mpito iitwayo Nile Basin Initiative (NBI0).

"Malengo ya ushirikiano huu ni kufikia uanzishwaji wa kamisheni ya Bonde la Mto Nile ambayo mchakato wake unaendelea" alisema Prof. Mbarawa.

Aliongeza kuwa, Tanzania ni miongoni mwa nchi 11 za Bonde la Mto Nile zinazoshirikiana katika kusimamia na kuendeleza rasilimali za bonde la mto huo chini ya mwavuli wa NBI.

Alizitaja nchi zingine kuwa ni Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Misri, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Sudani Kusini, Sudan, Uganda na Eritrea ambayo ni mtazamaji.

Alisema ushirikiano huo una faida kubwa na nchi wanachama zinanufaika na maji ya Mto Nile kwa kuwa na haki sawa ya matumizi.
 
Hata hivyo, alisema katika mkutano huo, Tanzania ambayo ndiyo mwenyekiti kwa sasa itakabidhi kijiti hicho kwa Uganda.


Mikoa Minne Inayoongoza Kwa Kulima Bangi Yaanikwa Hadharani

$
0
0
Serikali ya Tanzania imewasilisha bungeni taarifa ya hali ya Dawa ya Kulevya nchini kwa mwaka 2017 ambayo inaitaja mikoa minane inayoongoza kwa kilimo cha bangi huku mkoa wa Mara ukiongoza.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama aliitaja jana Ijumaa Novemba 16, 2018 mikoa hiyo kuwa ni Mara, Arusha, Njombe, Tanga, Simiyu, Rukwa, Geita na Morogoro.

Hata hivyo, alisema kiasi cha bangi kilipungua kutoka tani 68.23 kwa mwaka 2016 na kufikia tani 52.19 kwa mwaka 2017.

Amesema ukamataji wa mirungi uliongezeka kutoka tani 21.6 kwa mwaka 2016 hadi kufikia tani 67.8 mwaka 2017 ikiwa ni ongezeko la zaidi ya mara tatu.

Amesema lakini idadi ya watuhumiwa ilipungua kutoka 2,397 mwaka 2016 hadi 1,797  kwa mwaka 2017 ikichangiwa na sababu ya watuhumiwa wengi kukamatwa na kiasi kikubwa cha mirungi na baadhi ya mirungi kukamatwa bila wahusika kuwepo baada ya kuitekeleza.

Mhagama amesema kiasi cha cocaine kilichokamatwa kilipungua kutoka kilo 18.52 katika mwaka 2016 hadi kufikia kilo 4.143 kwa mwaka 2017.

Amesema watuhumiwa waliokamatwa kwa kujihusisha na cocaine walipungua kutoka 263 kwa mwaka 2016 hadi kufikia 243 kwa mwaka 2017.

Hata hivyo, amesema kuna ongezeko la dawa za kulevya aina ya heroin zilizokamatwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya baada ya kuimarisha udhibiti wa dawa zinazopita mipakani na hivyo kupunguza uingizaji wa dawa nchini.

Amesema heroin ambayo ilikamatwa nchini katika mwaka 216 ni kilo 42.26  ikilinganishwa na kilo 185.557 zilizokamatwa mwaka 2017 ikiwa ni mara nne zaidi na kiasi hiki kikubwa kuwahi kukamatwa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Amesema idadi ya watuhumiwa waliokamatwa wakijihusisha na heroine iliongezeka kutoka watu 716 kwa mwaka wa fedha 2016 hadi kufikia watu 1,005 kwa mwaka 2017.

Aidha amesema mashamba ya mirungi ya ukubwa wa ekari 64.5 yaliteketezwa wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro.

Serikali Yasema Hakuna uthibitisho wa kisayansi kuwa kuku wa kisasa Wanasababisha Wanaume Kuota Matiti na Wanawake Kuota Ndevu

$
0
0
Serikali imesema hakuna uthibitisho wa kisayansi kuwa madawa na vichochezi vya ukuaji wa kuku na mayai ya kisasa yanasababisha wanawake kuota ndevu na wanaume kuota matiti.
 
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega alitoa kauli hiyo jana bungeni alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum(CUF), Zainab Mndolwa Amir.

Katika swali lake, Mbunge huyo alisema ziko aina mbili za ufugaji ambazo ni wa kienyeji na ufugaji wa kisasa.

"Ufugaji wa kuku wa kisasa hutumia dawa nyingine sana katika ukuzaji na hutumia muda wa wiki tatu hadi nne kutumiwa na binadamu. Je, kuku hao wana madhara gani kwa binadamu," alihoji.

Pia alihoji serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wafugaji wa kuku kutumia njia bora ya kisasa ambayo haina mashaka kwa watumiaji.

Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri Ulega alilihakikishia bunge kuwa, ulaji wa nyama ya kuku wa kisasa au mayai ya kuku wa kisasa hauna madhara.

Aidha, alisema ufugaji wa kuku wa kisasa hauendani na matumizi ya dawa kwa wingi.

Alisema vyakula vinavyotumika kulisha kuku wa kisasa huwa na viini lishe kama madini, vitamin, protini, na nishati pamoja na chanjo ambazo sio dawa na ni muhimu kwa ukuaji na afya ya kuku na havina madhara kwa afya ya mlaji.

Hata hivyo, alisema ukuaji wa haraka wa kuku wa kisasa unaofanya kuwa tayari kwa matumizi ndani ya kipindi kifupi cha wiki nne mpaka sita hutokana na ulishaji wa vyakula vyenye ubora pamoja na kuwapo kwa vinasaba kwa ukuaji wa haraka na siyo matumizi ya dawa au vichocheo.

"Pia hakuna uthibitisho wa kisayansi wa dawa na vichochezi kusababisha ukuaji wa haraka wa kuku," alisema.

Ulega alisema serikali imekuwa ikitekeleza mikakati mbalimbali kwa ajili ya kuwasaidia wafugaji wa kuku kudhibiti vimelea vya magonjwa ili kupunguza matumizi ya dawa katika ufugaji wa kuku wa kisasa.

Alitaja baadhi ya mikakati kuwa ni pamoja na kusajili na kusimamia mashamba ya kuku wazazi, na vituo vya kutotolesha vifaranga ili kuzalisha wasio na magonjwa, kushirikiana na wadau kuendesha mafunzo kwa wafugaji kuhusu ufugaji wa kuku unaozingatia usalama wa mazingira na mbinu za ufugaji bora wa kuku.

Ulega alisema pia serikali inaendelea na mkakati wa kusimamia na kusajili utengenezaji wa vyakula vya kuku vyenye ubora ili kupunguza usambazaji wa vyakula vyenye vimelea vya magonjwa.

"Serikali inasimamia Sheria ya Nyanda za Malisho na Rasilimali za Vyakula vya Wanyama Na 13 ya mwaka 2010 na kanuni zake zinazokataza matumizi ya dawa na vichocheo kwenye vyakula vya kuku ili kulinda afya ya walaji," alisema.

Serikali Yapunguza Udumavu, Vifo vya Watoto Chini ya Miaka Mitano kwa Asilimia 50

$
0
0
Na Jacquiline Mrisho
Serikali imeweza kufanya tahtmini na kubaini kuwa jitihada zilizofanyika zimeweza kupunguza udumavu na vifo vya watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano kwa asilimia 50.

Takwimu hizo zimetolewa jana jijini Dodoma na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alipokuwa akimuwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango katika uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii.

Waziri Ummy alisema kuwa katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na upungufu wa viwango vya matatizo ya lishe kwa baadhi ya viashiria ambapo moja ya viashiria vya kupungua kwa matatizo ya lishe ni kushuka kwa tatizo la udumavu, uzito pungufu pamoja na ukondefu wa mwili miongoni mwa watoto.

“Kama tunavyofahamu udumavu huathiri ukuaji wa mtoto kimwili na kiakili na kupunguza uwezo wa kufanya vizuri shuleni pamoja na kupunguza ufanisi wake katika maisha ya utu uzima, hivyo kutokana na juhudi za Serikali na wadau mbalimbali tumeweza kupunguza udumavu kwa kiwango cha asilimia 50 ambapo kwa sasa kuna wastani wa watoto watatu wenye udumavu kati ya watoto 10 walio chini ya umri wa miaka mitano,” alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy aliongeza  kuwa ingawa bado kuna changamoto kubwa miongoni mwa kundi la watoto kwa sababu ya idadi yao kuwa kubwa, kushuka kwa kiwango cha udumavu ni jambo la kujivunia kwani  hali hiyo inaonesha kuwa jitihada za kupambana na tatizo hilo zimezaa matunda.

Akizungumzia kuhusu machapisho hayo, Waziri Ummy amefafanua kuwa  Wizara ya Fedha na Mipango kwa kushirikiana na UNICEF walifanya uchambuzi wa bajeti katika sekta mtambuka ya jamii hususan katika Elimu, Afya, Virusi vya Ukimwi, Maji na Usafi wa mazingira na lishe kwa lengo la kuboresha upangaji na utekelezaji wa masuala ya Mama na Mtoto katika mipango na Bajeti.

Akimuwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa za Michezo, Susan Mlawa amesema kuwa machapisho hayo yanatoa Muhtasari wa Bajeti katika sekta mtambuka ya maendeleo ya jamii kwa kipindi cha kati ya mwaka wa fedha 2013/2014 na 2017/2018.

“Machapisho hayo yameelezea kuhusu kubaini kiasi cha fedha zilizotengwa na kutolewa katika bajeti kwa maeneo muhimu ya sekta ya jamii ambayo ni Elimu, Afya, Virusi vya Ukimwi na Ukimwi, Lishe, Maji na Usafi wa mazingira, kutoa Muhtasari wa Bajeti, kuishauri Serikali katika Sera, Mipango na bajeti yenye kuzingatia kuwapatia watoto makuzi bora na ulinzi kwa Mama na watoto katika jamii pamoja na kutoa elimu kwa wadau mbalimbali,” alisema Susan.

Akiwawakilisha wadau wengine, Mwakilishi kutoka shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Watoto (UNICEF), Maniza Zaman amesema kuwa shirika hilo limekuwa likifuatilia kwa karibu matumizi ya fedha za Umma zinazoelekezwa kwa watoto.

Zaman alifafanua kuwa katika kutekeleza na kuzingatia dira ya Serikali 2025 inayolenga ukuaji wa viwanda na kufikia uchumi wa kati, kumekuwa na hitaji la kuboresha huduma za afya, elimu pamoja na kuondoa changamoto zinazowakabili watoto na vijana nchini ili waweze kuimarisha afya zao pamoja na kuchangia katika maendeleo ya taifa hivyo mapendekezo yaliyotolewa katika machapisho hayo yanalenga kutekeleza lengo hilo.

Machapisho hayo yameandaliwa na Wizara ya Fedha na Mipango kwa kushirikisha Wizara za Kisekta; Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Tume ya UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC).

Spika Ndugai Amtoa Nje Suzan Kiwanga, Ampiga Marufuku Kuhudhuria Vikao Hadi Mwakani

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai jana alimtoa nje ya bunge, Mbunge wa Mlimba, Suzan Kiwanga (Chadema) na kumtaka kutohudhuria vikao vya bunge hadi Bunge la Bajeti  mwakani baada ya kuingilia hoja ya Mbunge wa Tandahimba Katani Ahmed Katani aliyekuwa akikanusha kujiuzulu ubunge.

Ndugai amemtaka Kiwanga kutohudhuria kikao cha mkutano wa bunge uliyobaki ambao, huku akimtaka kutoshiriki mikutano ya kamati za bunge na michezo ya bunge.

Ofa! ofa!, Viwanja vimeshuka bei: Bunju na Mapinga (Baobab Sec)

$
0
0
Ofa! ofa!, Viwanja vimeshuka bei: Bunju na Mapinga (Baobab Sec)

Kwa Bunju, tumeshusha bei kutoka tsh 35,000 mpaka tsh 30,000 kwa sqm moja. Bunju vipo viwanja vya (sqm 600 = tsh 18 mil), (sqm 1200 = tsh 36 mil) na (sqm 1700 = tsh 51 mil)

Kwa Mapinga, bei imeshuka kutoka tsh 15,000 mpaka tsh 12,000 kwa sqm moja. Hapa vipo viwanja vya (sqm 400 = 4.8 mil), (sqm 600 = tsh 7.2 mil), (sqm 800 = tsh 9.6 mil), (sqm 1400 = tsh 16.8 mil ), (sqm 1500 = tsh 18 mil), (sqm 2000 = tsh 24 mil), (sqm 2400 = tsh 28.8 mil) na (sqm 3000 = tsh 36 mil )

Viwanja vyote viko umbali wa km 3 tu kutoka main road (Bagamoyo Road) na Luksa kulipa kwa awamu. Huduma za maji na umeme ziko karbu sana.

Ukipata ujumbe huu mjulishe ndugu/jamaa/rafiki.

Hakuna dalali, contact mhusika: call 0758603077, whatsap 0757489709, email: menejadar@yahoo.com
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images