Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

AfDB Yaimwagia Tanzania Mabilioni Kutekeleza Miradi ya Maendeleo

$
0
0
Na Grace Semfuko-MAELEZO.
Serikali kupitia Wizara ya Fedha imesaini mikataba mitatu na Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB ya kuipatia msaada na mikopo ya masharti nafuu yenye thamani ya dola za Kimarekani 156.59 ambazo ni sawa na shilingi Bilioni 358.236 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Mikataba hiyo ya Mikopo na Msaada imesainiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Dotto James na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Dkt Alex Mubiru ambapo kwa upande wa mikopo Serikali ya Tanzania itailipa kwa kwa muda wa miaka 40 ijayo.

Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa njia ya kusafirisha Umeme wa Msongo Mkubwa wa 400kV kuanzia Nyakanazi Biharamuro Mkoani Kagera hadi Kigoma uliopata mkopo  wa dola za Kimarekani milioni 123.39, Mradi wa kudhibiti Sumu Kuvu kwenye mazao ya nafaka ambao umepata dola milioni 33 zikiwepo dola milioni 20 za msaada na dola milioni 13 za mkopo huku Bajeti ya Serikali ya mwaka 2018/2019 nayo ikiongezewa mkopo wa masharti nafuu wa dola milioni 56 sawa na shilingi Bilioni 128.28.

Akizungumza wakati wa utiaji saini wa mikataba hiyo mitatu ya mikopo na msaada kati ya Tanzania na Benki ya maendeleo ya Afrika AfDB, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw.Dotto James amesema Serikali itahakikisha miradi hiyo inatekelezwa kama ilivyokusudiwa ili kuwaletea maendeleo Watanzania.

“Ndugu zangu hii ni hatua kubwa na nzuri kwetu watanzania, hizi sio fedha ndogo, ni fedha nyingi ambazo ni mkopo wa masharti nafuu pamoja na msaada kwenye eneo la kudhibiti Sumu Kuvu za nafaka, tutalipa mikopo hii kwa muda wa miaka 40” alisema Dotto James Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango.

Kwa upande wake Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB Dkt Alex Mubiru amesema Benki hiyo inalenga kuimarisha maendeleo ya Watanzania kwani fedha hizo zinaingia moja kwa moja kwenye miradi ambayo itatumiwa na wananchi.

“Benki yetu ya Maendeleo ya Afrika AfDB inalenga kuimarisha maendeleo ya wananchi, tuna miradi mingi tunayofadhili kwa nchi za Afrika, kwa Tanzania pia tunayo miradi tunayoimarisha, lengo la mikopo na misaada hii ni koboresha maishaya watanzania” alisema Dkt Mubiru Mwakilishi Mkazi wa AfDB.

Zanzaibar ni miongoni mwa eneo litakalonufaika na msaada huo kutoka Benki ya AfDB kwa upande wa kudhibiti Sumukuvu kutoka kwenye mazao ya nafaka ambapo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bw.Ahmad Kassim Haji amesema watahakikisha wanalinda na kuhifadhi vizuri mazao yote ya nafaka na kwamba mradi huo utawawezesha kufanya shughuli hiyo kikamilifu.

Kususa Bungeni Kwawaponza Wabunge wa Upinzani

$
0
0
Kitendo cha Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, kususia kuapishwa kwa wabunge wanne wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambao walihama kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kujiunga na chama hicho tawala, kumewaponza upinzani baada ya kushindwa kusoma hotuba yao kuhusu Muswada wa Sheria ya Huduma Ndogo ya Fedha wa Mwaka 2018.

Pia kususa huko, kumewafanya wabunge wawili wa upinzani ambao walikuwa kwenye orodha ya kuuliza maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, kunyimwa nafasi hiyo.

Leo Alhamisi Novemba 15, asubuhi baada ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, kuingia kwenye ukumbi wa Bunge, alianza kwa dua kama kawaida baadaye kuwaaapisha wabunge hao James Millya (Simanjiro), Joseph Mkundi (Ukerewe), Pauline Gekul (Babati Mjini) na Ryoba Marwa (Serengeti).

Baada ya kiapo kumalizika, Spika alianza kuita watu wa kumuuliza maswali Waziri Mkuu ambaye jina la kwanza kutajwa lilikuwa la Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko (Chadema) na la pili lilikuwa la Mbunge wa Viti Maalumu, Suzan Lyimo (Chadema).

Spika alivyotaja jina jina la Matiko ambaye kwa wakati huo hakuwepo kwenye ukumbi wa Bunge ila Lyimo alivyotajwa alisikika akisema “Mheshimiwa Spika nipo…” hata hivyo Ndugai alisema “namfuta kwenye orodha kisha akaendelea na wauliza maswali wengine.

Baada ya kipindi hicho kwisha, aliita hati za kuwasilisha mezani ambapo wa kwanza alikuwa Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philp Mpango na wa pili alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti, ambaye naye aliwasilisha hati yake.

Alivyoita msemaji wa upinzani, hakuwepo kwenye ukumbi hivyo akaita wauliza maswali ya kawaida kuendelea na hata baada ya kipindi hicho ya maswali kwisha, Dk. Mpango alisoma kwa mara ya pili Muswada wa Sheria ya Huduma ndogo ya Fedha wa mwaka 2018 na kufuatiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, George Simbachawene aliyesoma maoni ya amati.

Baada ya pande mbili hizo kusoma hotuba zao, upinzani nao walitaka kusoma na ndipo Spika Ndugai akawaambia jambo hilo ni kinyume cha kanuni kwa sababu hawakuwasilisha hati zao awali kama kanuni zinavyotaka.

Suala hilo lilifanya Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (Chadema), kusimama na kuomba busara ya kiti itumike ili waruhusiwe kusoma hotuba hiyo.

Hata hivyo, baada ya Selasini kuzungumza hayo, Mnadhimu wa Mkuu wa Kambi ya Serikali, Jenista Mhagama, alisimama na kusema ombi la upinzani ni kinyume cha kanuni na Bunge siku zote huendeshwa kwa kanuni.

Kutokana na hali hiyo, Spika Ndugai alihitimisha mjadala huo na kusema lazima kanuni zifuatwe hivyo hotuba hiyo haiwezi kusomwa na badala yake akawaambia wabunge wanaweza kusoma hotuba hiyo wenyewe kwa sababu walishagawiwa.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa ya Novemba 16

Ofa! ofa!, Viwanja vimeshuka bei: Bunju na Mapinga (Baobab Sec)

$
0
0
Ofa! ofa!, Viwanja vimeshuka bei: Bunju na Mapinga (Baobab Sec)

Kwa Bunju, tumeshusha bei kutoka tsh 35,000 mpaka tsh 30,000 kwa sqm moja. Bunju vipo viwanja vya (sqm 600 = tsh 18 mil), (sqm 1200 = tsh 36 mil) na (sqm 1700 = tsh 51 mil)

Kwa Mapinga, bei imeshuka kutoka tsh 15,000 mpaka tsh 12,000 kwa sqm moja. Hapa vipo viwanja vya (sqm 400 = 4.8 mil), (sqm 600 = tsh 7.2 mil), (sqm 800 = tsh 9.6 mil), (sqm 1400 = tsh 16.8 mil ), (sqm 1500 = tsh 18 mil), (sqm 2000 = tsh 24 mil), (sqm 2400 = tsh 28.8 mil) na (sqm 3000 = tsh 36 mil )

Viwanja vyote viko umbali wa km 3 tu kutoka main road (Bagamoyo Road) na Luksa kulipa kwa awamu. Huduma za maji na umeme ziko karbu sana.

Ukipata ujumbe huu mjulishe ndugu/jamaa/rafiki.

Hakuna dalali, contact mhusika: call 0758603077, whatsap 0757489709, email: menejadar@yahoo.com

Aliyekuwa Mbunge Wa Temeke Abdalah Mtolea Aomba Kujiunga Na Chama Cha Mapinduzi (CCM)

$
0
0
Jana Novemba 15, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Temeke kwa tiketi ya Chama cha CUF Abdalah Mtolea alijivua uanachama wa CUF na kujiuzuru Ubunge wa Jimbo la Temeke, huku akieleza chanzo kikiwa migogoro isiyoisha katika Chama cha CUF kwa zaidi ya miaka miwili sasa.

Tukio la kujivua uanachama wa CUF na kujiuzuru ubunge lilitokea ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wakati akichangia hoja katika mjadala uliokuwa unaendelea 

Ndugu Abdalah Mtolea  jana hiyo hiyo alitangaza nia yake ya kuomba kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) akieleza msingi wa uamuzi huo ukiwa umejengwa katika ukweli kwamba wengi ya wapiga kura wake wamemshauri kujiunga na CCM.

Akizungumza katika kikao cha waandishi wa habari, watumishi na baadhi ya wanachama wa CCM katika Ofisi ya Makao Makuu ya CCM Jijini Dodoma, Ndugu Mtolea alieleza sababu zinazopelekea kuomba kujiunga na CCM na kuwa amevutiwa na Mageuzi makubwa ya Kiuongozi na kazi nzuri inayofanywa na CCM na Serikali yake chini ya Ndugu John Pombe Joseph Magufuli Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kikao hicho cha waandishi wa habari, watumishi na baadhi ya wanachama wa CCM kilihudhuriwa pia na Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM ambaye alimwelekeza kwenda katika tawi lililo karibu na makazi yake Wilayani Temeke, Jijini Dar es Salaam ili afuate utaratibu wa kuomba uanachama wa CCM.

Imetolewa na,
IDARA YA ITIKADI NA UENEZI CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
OFISI YA MAKAO MAKUU DODOMA

Spika Ndugai Amtoa Nje Suzan Kiwanga, Ampiga Marufuku Kuhudhuria Vikao Hadi Mwakani

$
0
0
Spika wa Bunge, Job Ndugai jana alimtoa nje ya bunge, Mbunge wa Mlimba, Suzan Kiwanga (Chadema) na kumtaka kutohudhuria vikao vya bunge hadi Bunge la Bajeti  mwakani baada ya kuingilia hoja ya Mbunge wa Tandahimba Katani Ahmed Katani aliyekuwa akikanusha kujiuzulu ubunge.

Ndugai amemtaka Kiwanga kutohudhuria kikao cha mkutano wa bunge uliyobaki ambao, huku akimtaka kutoshiriki mikutano ya kamati za bunge na michezo ya bunge.

Serikali Yapunguza Udumavu, Vifo vya Watoto Chini ya Miaka Mitano kwa Asilimia 50

$
0
0
Na Jacquiline Mrisho
Serikali imeweza kufanya tahtmini na kubaini kuwa jitihada zilizofanyika zimeweza kupunguza udumavu na vifo vya watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano kwa asilimia 50.

Takwimu hizo zimetolewa jana jijini Dodoma na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu alipokuwa akimuwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango katika uzinduzi wa machapisho ya uchambuzi wa bajeti katika sekta ya jamii.

Waziri Ummy alisema kuwa katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na upungufu wa viwango vya matatizo ya lishe kwa baadhi ya viashiria ambapo moja ya viashiria vya kupungua kwa matatizo ya lishe ni kushuka kwa tatizo la udumavu, uzito pungufu pamoja na ukondefu wa mwili miongoni mwa watoto.

“Kama tunavyofahamu udumavu huathiri ukuaji wa mtoto kimwili na kiakili na kupunguza uwezo wa kufanya vizuri shuleni pamoja na kupunguza ufanisi wake katika maisha ya utu uzima, hivyo kutokana na juhudi za Serikali na wadau mbalimbali tumeweza kupunguza udumavu kwa kiwango cha asilimia 50 ambapo kwa sasa kuna wastani wa watoto watatu wenye udumavu kati ya watoto 10 walio chini ya umri wa miaka mitano,” alisema Waziri Ummy.

Waziri Ummy aliongeza  kuwa ingawa bado kuna changamoto kubwa miongoni mwa kundi la watoto kwa sababu ya idadi yao kuwa kubwa, kushuka kwa kiwango cha udumavu ni jambo la kujivunia kwani  hali hiyo inaonesha kuwa jitihada za kupambana na tatizo hilo zimezaa matunda.

Akizungumzia kuhusu machapisho hayo, Waziri Ummy amefafanua kuwa  Wizara ya Fedha na Mipango kwa kushirikiana na UNICEF walifanya uchambuzi wa bajeti katika sekta mtambuka ya jamii hususan katika Elimu, Afya, Virusi vya Ukimwi, Maji na Usafi wa mazingira na lishe kwa lengo la kuboresha upangaji na utekelezaji wa masuala ya Mama na Mtoto katika mipango na Bajeti.

Akimuwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa za Michezo, Susan Mlawa amesema kuwa machapisho hayo yanatoa Muhtasari wa Bajeti katika sekta mtambuka ya maendeleo ya jamii kwa kipindi cha kati ya mwaka wa fedha 2013/2014 na 2017/2018.

“Machapisho hayo yameelezea kuhusu kubaini kiasi cha fedha zilizotengwa na kutolewa katika bajeti kwa maeneo muhimu ya sekta ya jamii ambayo ni Elimu, Afya, Virusi vya Ukimwi na Ukimwi, Lishe, Maji na Usafi wa mazingira, kutoa Muhtasari wa Bajeti, kuishauri Serikali katika Sera, Mipango na bajeti yenye kuzingatia kuwapatia watoto makuzi bora na ulinzi kwa Mama na watoto katika jamii pamoja na kutoa elimu kwa wadau mbalimbali,” alisema Susan.

Akiwawakilisha wadau wengine, Mwakilishi kutoka shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Watoto (UNICEF), Maniza Zaman amesema kuwa shirika hilo limekuwa likifuatilia kwa karibu matumizi ya fedha za Umma zinazoelekezwa kwa watoto.

Zaman alifafanua kuwa katika kutekeleza na kuzingatia dira ya Serikali 2025 inayolenga ukuaji wa viwanda na kufikia uchumi wa kati, kumekuwa na hitaji la kuboresha huduma za afya, elimu pamoja na kuondoa changamoto zinazowakabili watoto na vijana nchini ili waweze kuimarisha afya zao pamoja na kuchangia katika maendeleo ya taifa hivyo mapendekezo yaliyotolewa katika machapisho hayo yanalenga kutekeleza lengo hilo.

Machapisho hayo yameandaliwa na Wizara ya Fedha na Mipango kwa kushirikisha Wizara za Kisekta; Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Wizara ya Maji na Umwagiliaji, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Tume ya UKIMWI Tanzania (TACAIDS) na Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC).

Serikali Yawapandisha Madaraja Watumishi Wa Umma 113,520 Walioajiriwa Tangu Mwaka 2012

$
0
0
Serikali imewapandisha madaraja watumishi wa umma 113,520 walioajiriwa mwaka 2012 katika awamu tatu, ambapo ya kwanza walipandishwa vyeo Watumishi 28,049 waliokuwa wameidhinishiwa vyeo kabla ya zoezi la uhakiki wa watumishi hewa na uhakiki wa vyeti kuanzia mwezi Juni, 2016, awamu ya pili ilianza mwezi Novemba, 2017 na ilihusisha watumishi 59,967 ambao taarifa zao zilikuwa kwenye Mfumo Shirikishi wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara (HCMIS) kabla ya zuio na awamu ya tatu ilianza mwezi Aprili, 2018 na ilihusisha Watumishi 25,504 ambao barua zao zilikuwa hazijaingizwa kwenye Mfumo.

Ufafanuzi huo, umetolewa Bungeni jana na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Mary M. Mwanjelwa (Mb) wakati akijibu swali la Mhe. Joram Hongoli (Mb) kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora lililohusu watumishi wa umma walioajiriwa 2012 kutopandishwa madaraja mpaka hivi sasa.

Dkt. Mwanjelwa alisema, watumishi walioajiriwa Mwaka 2012 walistahili kupandishwa madaraja kuanzia mwaka 2016/2017 kipindi ambacho Serikali ilikuwa ikifanya zoezi la uhakiki wa watumishi hewa na uhakiki wa vyeti, hivyo mara baada ya kukamilika kwa zoezi hilo Serikali ilianza kuwapandisha watumishi hao kwa awamu hizo tatu kwa kuzingatia vigezo stahiki na kuongeza kuwa  watumishi wengine ambao wamekidhi vigezo wataendelea kukasimiwa katika bajeti ya mishahara ili waweze kupandishwa vyeo katika mwaka huu wa fedha 2018/2019.

Aidha, Dkt. Mwanjelwa aliainisha kuwa,  watumishi 31,188 walioajiriwa na TAMISEMI mwaka 2012,  kati ya hao watumishi 15,320 wamepandishwa vyeo na kubadilishiwa mishahara, na watumishi 3,349 waajiri wao wamewapandisha vyeo lakini majina yao yapo UTUMISHI kwa ajili ya kupitia taarifa zao kabla ya kuwabadilishia mishahara na  watumishi 1,064 waliopandishwa vyeo wamebainika kuwa na hoja mbalimbali ambazo waajiri wanapaswa kuzikamilisha na kurejesha majina yao UTUMISHI kwa ajili ya kuwaidhinishia mishahara.Watumishi 4,552 hawapo tena katika Utumishi wa Umma na watumishi 6,903 bado hawajapandishwa vyeo ambapo  Serikali inatarajia kuwapandishwa vyeo wakati wowote katika mwaka huu wa fedha 2018/19.

Suala la  upandishwaji vyeo kwa Watumishi wa Umma linazingatia vigezo mbalimbali ikiwa ni pamoja na utendaji kazi mzuri, kukidhi sifa zilizoainishwa katika Miundo ya Maendeleo ya Utumishi, uwepo wa nafasi wazi na bajeti iliyotegwa.  

Kwa mujibu wa Miundo ya Maendeleo ya Utumishi, mtumishi anapaswa kutumikia cheo kimoja si chini ya miaka mitatu kabla hajafikiriwa kupandishwa cheo. 

Aidha, iwapo mtumishi ameajiriwa kwa mara ya kwanza atapaswa kumaliza mwaka mmoja wa kuthibitishwa kazini kisha ndipo atumikie cheo hicho si chini ya miaka mitatu, hivyo  kwa kuzingatia sifa mtumishi anaweza kupandishwa cheo baada ya miaka 3, 4, 5 au hata saba kutegemea na kukidhi vigezo stahiki.

Imetolewa Na:
Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini
Ofisi Ya Rais (Utumishi)
Tarehe 15 Novemba, 2018.

Sakata la Korosho: Waziri wa Viwanda Joseph George Kakunda Awatumbua Wakurugenzi wawili

$
0
0
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, George Kakunda leo Novemba 14 amewavua ukurugenzi wakurugenzi wawili wanaosimamia viwanda na maghala katika wizara hiyo kwa madai ya uzembe uliosababisha kuzorota kwa viwanda vya korosho.

Kakunda aliyeteuliwa hivi karibuni akimrithi, Charles Mwijage amesema baada ya kutembelea viwanda hivyo jana kuanzia mkoani Lindi hadi Mtwara amekuta hali mbaya huku viwanda vingi vikiwa vimegeuzwa kuwa maghala.

"Nimeamua kumpunguzia majukumu ndugu Isaac Legonda, mkurugenzi wa maendeleo ya viwanda, ataripoti kwa Katibu Mkuu atapangiwa kazi nyingine ya uofisa," alisema Waziri Kakunda.

Aliongeza: "Nimemtafuta tangu juzi ili aweze kunipa habari za viwanda hayupo ofisini, Katibu Mkuu hana taarifa za kutosha huyu mtu yuko wapi. Katibu Mkuu atajua mwenyewe hatua zinazotumika katika kanuni za adhabu za utumishi."

Alimtaja pia Augustino Mbulumi ambaye pia ni mkurugenzi wa usimamizi wa maghala na kusema kwamba ametengua uteuzi wake kutokana na utendaji kazi hafifu na uzembe.

"Atateuliwa mkurugenzi mwingine ambaye atakuwa tayari kuwajibika vizuri zaidi. Hatuwezi kuwa na watu ambao hawaendi na kasi ya mheshimiwa Rais," alisema Kakunda.

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi Ya Novemba 15

Washitakiwa Watano NEMC Walioghushi Saini Ya January Makamba Wapewa Dhamana

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewapa dhamana washtakiwa watano wa Baraza la Hifadhi ya Mazingira (Nemc) baada ya kupata kibali kutoka Mahakama Kuu kitengo cha Uhujumu Uchumi.

Washtakiwa hao waliopata dhamana  ni Ofisa wa Mazingira Nemc, Deusdith Katwale (38) na mtaalam wa IT Nemc, Luciana Lawi (33) wote wakazi wa Ubungo Msewe, katibu muhtasi wa Nemc, Edna Lutanjuka (51) mkazi wa Mbezi Beach St Gasper, msaidizi wa ofisa ,Mwaruka Mwaruka (42) na ofisa mazingira Nemc, Lilian Laizer (27) wote  wakazi wa Ukonga Mombasa.

Wafanyakazi hao wamesota rumande tangu Oktoba 31 mwaka huu ambapo walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza na kusomewa mashtaka sita ya uhujumu uchumi likiwamo la kughushi saini ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Januari  Makamba katika vyeti vya tathmini ya uharibifu wa mazingira.

Akitoa masharti sita ya dhamana jana Novemba 14 yaliyotolewa na Mahakama Kuu Kitengo cha Uhujumu Uchumi, Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustina Mmbando alimtaka kila mshtakiwa kuweka fedha benki kiasi cha Sh. Milioni 13.3 au kuwasilisha mahakamani hapo hati ya mali isiyohamishika yenye thamani hiyo.

Pia Hakimu Mmbando ametaka kila mshtakiwa kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika kati yao mmoja awe mwajiriwa wa Serikali, wawe na vitambulisho vya Taifa watakaosaini bodi ya Sh2.5 milioni  kila mtu.

Hakimu Mmbando amewataka washtakiwa hao kutotoka nje ya Dar es Salaam bila kibali cha Mahakama pamoja na kuwasilisha hati zao za kusafiria mahakamani hapo.

Washtakiwa hao pia wametakiwa kuripoti kwa Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kama watakavyopangiwa.

Baada ya maelezo hayo washtakiwa wote walikamilisha masharti ya dhamana ambapo kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 28, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

Jipatie Dawa ya Asili ya Kupunguza Maziwa, Kupunguza Tumbo,Kuongeza Unene, Kuongeza Maumbile ya Kiume na Kuondoa Chunusi

$
0
0
NATURAL BEAUTY PROD. Tumeingiza mzigo mpya ni bidhaa zilizothibitishwa kiafya na kupewa kibali original cha kuuzwa hadharani.  Bidhaa hizi zimetengenezwa kwa mimea na matunda hazina chemical wala madhara yoyote kwa mtumiaji. Ukinunua bidhaa kuanzia mbili utapatiwa offer ya bidhaaa nyingine yoyote uipendayo wewe.

1. SHARK POWER--Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza uume urefu na upana mpaka nchi 7.5 inapatikana kwa @170,000/=

2. VIGA 84000---Hii dawa ya kuspray yenye uwezo mkubwa wa kuchelewesha wakati wa tendo la ndoa @160,000/=

3. HANDSOME UP ORIGINAL-- Hichi ni kifaa cha kuongeza maumbile kwa size uipendayo pamoja na kuimalisha misuli kifaa hichi kinapatikana kwa @230,000/=

4. MAXMAN CAPSULE--- Hii ni dawa ya vidonge ya kuongeza uume urefu na upana pamoja na kuongeza nguvu za kiume kwa wiki mbili tu bei yake ni @200,000/=

5. VIG RX---- Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza uume urefu na upana mpaka nchi 10 inapatikana kwa @190,000/=

6. BODY BOOSTER---Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri @150,000/=

7. BOTCHO MULT PLUS-- Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza (hips mapaja na makalio) kwa size uipendayo unaipata kwa @200,000/=

8. WHITE COLLECTION---- Ni vidonge vya kuwa mweupe mwili mzima pamoja na kuwa soft @150,000/= N.K  Wasiliana nasi kwa simu

NO:. +255 759029968  AU +255 659618585

Popote ulipo utapata huduma zetu.

Pia hakikisha unapatiwa risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ununuapo bidhaa kampuni hii.  WELCOME ALL

Korosho za magendo kutoka Msumbiji zakamatwa Mtwara

$
0
0
Zaidi  ya tani tisa za korosho zimekamatwa zikiwa zimeingizwa nchini kwa njia ya magendo kutoka Msumbiji.

Tani hizo (magunia 91 ya kilo 100 kila moja) zilikamatwa juzi mpakani mwa Tanzania na Msumbiji eneo la Newala wakati wa operesheni iliyofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Newala, Aziza Mangosongo.

Wiki iliyopita, Rais Dk. John Mafuguli alitangaza kuwa Serikali itanunua korosho zote kwa bei ya Sh 3,300 kwa kilo na akatahadharisha vyombo vya ulinzi na usalama kuwa makini kuhakikisha hakuna zitakazoingizwa kutoka nchi jirani.

Akizungumza jana kwa niaba ya mkuu wa wilaya, Katibu Tawala wa Wilaya ya Newala, Daniel Zenda, alisema Mtanzania mkazi wa Newala ndiye aliyekutwa na korosho hizo.

“Baada ya kuona rais ametangaza bei nzuri ya korosho, baadhi ya watu wameanza kutoa korosho za magendo kule (Msumbiji) kuja kuuza huku.

“Hizi korosho zilikutwa zikipimwa katika moja ya chama cha msingi kilichopo mpakani Masasi na huwa wanavusha kwa mtumbwi. Tulikamata pia trekta lililokuwa limezisomba,” alisema Zenda.

Katika hatua nyingine, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limewasili mkoani hapa na kuanza kukagua maghala ya kuhifadhia korosho wilayani Newala.

Wanajeshi hao walioongozana na Mangosongo, jana walikagua maghala matatu ambayo ni ya Micromix, Agro Focus na Chama Kikuu cha Ushirika cha Tandahimba na Newala (Tanecu). Zenda alisema walipokea ujumbe wa wanajeshi 20.

Alisema pia viongozi wa vijiji, kata na vyama vya msingi wanaendelea kupewa maelekezo ya namna bora ya kufanya kazi hiyo kwa lengo la kuzuia uingizwaji wa korosho kutoka nchi jirani.

Ofisa Masoko wa Tanecu, Juma Selemani alisema kwa msimu wa mwaka 2018/2019 wanategemea kukusanya tani 120,000 na hadi kufikia jana walikuwa wamepokea zaidi ya tani 38,000 ambazo tayari zimeingia katika maghala makuu.

“Korosho zinaendelea kuletwa na taarifa za wakulima zimeshaandaliwa na kuwasilishwa sehemu husika kwa ajili ya malipo,” alisema Selemani.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa alipokea magari matano ya JWTZ ambayo yatakuwa na kazi ya kupunguza korosho kutoka maghala makuu kwenda katika maghala yatakayotumika kuzitunza kwa muda wakati zikisubiri kubanguliwa.

Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea maghala, viwanda vya kubangulia korosho pamoja na kupokea magari hayo, alisema mkoa unatarajiwa kupokea magari zaidi ya 75 kwa shughuli ya korosho zitakazoanza kubanguliwa hivi karibuni.

Byakanwa alisema bado nguvu ya wananchi wengine itatumika kama ilivyokuwa kawaida.

Alisema mkoa umesambaza timu ya watu watano kila wilaya kuhakiki majina na akaunti za wakulima.

Byakanwa alisema tayari uhakiki wa majina umeshakamilika na wakimaliza uhakiki wa akaunti malipo yatafanyika mara moja ili kuruhusu kazi ya ubanguaji kuanza.


Makanga 3 Power, Dawa Bora Za Nguvu Za Kiume .

$
0
0
Kutibu nguvu za kiume dakika(10) na kupona muda wa siku tatu tuu. Kuimarisha misuli ya uume uliolegea, pia ipo Dawa ya kurefusha uume mfupi inchi NNE hadi saba na kunenepesha uume mfupi sentimita NNE.
 
Tiba ya kudumu kutibu maumivu ya mgongo,kiuno, tumbo kuunguruma na kujaa gesi, kupata choo vizuri, na kutibu uzazi, kutibu busha bila operesheni, kisukari, presha ,miguu kuuma, uzazi, fangas sugu, vidonda vya tumbo.
 
Ni docta bingwa wa kutibu magonjwa sugu, kutoa ndagu za utajiri kwa kutumia Pete, kazi ,cheni, mikufu maalumu ya bahati, una kesi umedhulumiwa Mali au pesa? Zitarudi muda wa Masaa matatu tuu.
 
Onana na Dr SHILINDE,  shida zako zote zitakwisha, anatoa Dawa za utajiri kwa wafanyakazi, wakulima, na wafugaji, wafanyabiashara na wachimba madini kwa kutumia pete, kazi kwa yeyote anaetaka kuwa na pesa nyingi.
 
Pia tunatoa Dawa kumrudisha Mume, mke, mpenzi, hawara, kwa muda wa SAA moja tuu, na kuomba msamaha kwa kukupigia magoti na yeyote yule. Kupunguza unene, kupunguza matiti makubwa, tumbo na nyama uzembe muda wa siku sita unapata saizi uipendayo.
 
Kutoa makovu mwilini, chunusi, upele na mabaka, pia tunayo Dawa ya kuongeza hipsi, makalio, mguu wa bia na kupata shepu safi kwa muda wa siku saba tuu.

Anapatikana Dar es Salaam maeneo ya Buguruni Sheli. 
 
Mawasiliano: 0784460348 au  0657 314701

Wa mikoani mtapata huduma popote mlipo.

Habari Njema Kwa Wenye Matatizo Ya Nguvu za Kiume, vitambi, nyama uzembe

$
0
0
(1).Fikiria ulianzia wapi? Je,ulifanikiwa au bado?

(2).Upo tayari kupona kwa haraka?

TIBA ZITOLEWAZO NI,

NGORO 4 POWER; Huongeza nguvu za kiume yenye mfumo wa unga na vidonge dozi siku(6).

MELAMELA; Hurefusha na kunenepesha uume ipo katika mfumo wa unga dozi siku (4).

KASELA; Hurudisha mke,mme,mchumba na hawara ndani ya siku mbili tu,atatimiza mahitaji yote hata Kama yupo mbali na kumfunga asiwe na mtu mwingine.

IKUMBUJA; Humfanya mtu  kupandishwa cheo kazini na kulipwa madeni au mafao yako pia na kumaliza kesi kabisa.

DUDUMA; Huongeza hips,makalio na mguu wa bia.

SWASWA: Hupunguza maziwa makubwa, kitambi, nyama uzembe, michirizi na muwasho sehem za Siri,na harufu mdomoni.

KOOLA;Hutibu magonjwa sugu ya zinaa, tumbo kujaa gesi,kuuma chini ya kitovu, kiuno ,fangasi za miguu, na kuvimba miguu au miguu kuwaka Moto.

Kwa hayo na mengineyo mfatilie DR.HINDU kwani ana uwezo wa kuhudumia ndani na nje ya TANZANIA.Kwa Dar es salaam anapatikana BUGURUNI MALAPA pia KAHAMA anapatikana MARUNGA.

Kwa wasio na mda wa kufika ofisini kwangu Nina vijana wa kukuletea mpaka ulipo kazini ama nyumbani kwako.

OFISI ZINAFUNGULIWA SAA 07 :00 ASUBUHI.

CONTACTS 0744 922 982(WhatsApp), 0716608959.

  "WOTE MNAKARIBISHWA".DR   HINDU NI SULUHISHO LAKO.

Swali la Kwanza la Charles Mwijage Bungeni Tangu Atumbuliwe Uwaziri

$
0
0
Aliyekuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage ameibuka na kuzungumza bungeni, kwa mara ya kwanza tangu atenguliwe nafasi yake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli wiki iliyopita.
 
Akizungumza Bungeni Jijini Dodoma kabla hajauliza swali kwa Wizara ya Nishati, Mwijage amelishukuru bunge hilo kupitia kwa Spika Job Ndugai wakati wote wa Uwaziri wake ndani ya Bunge, akisema,

“Nawashukru sana tangu mlivyokuwa mkiniongoza bungeni, kupitia kwako Mwenyekiti napenda kumshukuru Rais,  Makamu wa Rais na Waziri Mkuu kwa namna ambavyo waliniamini na kunisimamia kwenye majukumu ambayo waliyonipa."

Mbunge huyo huku akishangiliwa, alisema wananchi wake walipata mradi wa umeme katika jimbo zima lakini maeneo mengi yaliishia kuwekwa mambo bila ya kusimikwa kwa nguzo.

"Ni lini sasa Serikali itawaondolea kero ya umeme ili wananchi wale nao waanze kunufaika na miradi ya Rea," alisema Mwijage

Akijibu swali hilo, Waziri wa Nishati,  Dk  Medard Kalemani alisema miradi ya umeme katika wilaya ya Muleba itatekelezwa muda si mrefu na mkandarasi yuko katika maandalizi ya kupeleka nguzo.

Jeshi la Polisi Jijini Mwanza Laua Majambazi 7

$
0
0
Kamanda wa Polisi Mkoa Mwanza, Jonathan Shana amethibitisha kuawa kwa watu 7 wanaosadikika kuwa ni majambazi, katika eneo la kishiri kwenye majibizano ya risasi na jeshi la polisi.
 
Kamanda Jonathan Shana amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo mtaa wa Ihushi kata ya Kishiri wakati jeshi la polisi likifanya doria maalum mkoani humo.

“Hilo tukio la Kishiri limetokea majira ya saa 4 usiku wa kuamkia leo, na majambazi wote wameuawa wakati wa mapigano ya kurushiana risasi na jeshi la polisi na katika mapigano hayo tumekamata silaha mbili za kivita na risasi zaidi ya 71, majambazi wote wameuawa.”

Kamanda Shana amesema kabla kutokea makabiliano ya kurushiana risasi, polisi walifanikiwa kumtia mbaroni mtuhumiwa mmoja ambaye ndiye aliwaongoza hadi kwenye maficho yao na kuwakurupusha wengine ambao badala ya kujisalimisha walianza mashambulizi ya risasi yaliyojibiwa na polisi.

Hukumu ya Tido Mhando Kusomwa Disemba 18

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam Desemba 18 itatoa hukumu ya kesi inayomkabili aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Tido Mhando.

Tido ameshtakiwa kwa matumizi mabaya ya madaraka wakati akiongoza shirika hilo ambapo anakabiliwa na mashtaka manne ya kutumia madaraka vibaya na moja la kuisababishia Serikali hasara ya Sh887.1 milioni.

Hatua hiyo ilifikiwa leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya wakili wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai kuieleza Mahakama kuwa wamekwisha wasilisha majumuisho yao ya mwisho mahakamani hapo.

Wakili wa Tido, Dk Ramadhani Maleta aliitaarifu Mahakama kuwa wakili mwenzake, Martin Matunda amefariki dunia na kwamba na wao pia wamekwisha wasilisha hoja zao za mwisho.

Baada ya kueleza hayo, wakili Swai aliiomba Mahakama kuipangia kesi hiyo tarehe ya hukumu na hakimu Shaidi akapanga kutoa hukumu Desemba 18.

Alichokisema Lulu Michael Kwa Mara ya Kwanza Tangu Amalize Kifungo Chake

$
0
0
Mwigizaji Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, amefunguka kwa mara ya kwanza tangu alipomaliza kifungo chake Jumatatu iliyopita Novemba 12, 2018, kwa kusema ilikuwa akipitia kipindi kigumu.

Lulu ametumia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram kuelezea hisia zake baada ya kumaliza kifungo cha miaka miwili.

“Kilikuwa kipindi chenye maumivu, matusi, dharau, hukumu za wanadamu, maneno ya kulaaniwa, majina yasiyofaa na mambo mengine mengi ya aina hiyo, lakini namshukuru Mungu yote haya sikuyapokea kama yalivyokuja, bali niliyapokea kama somo/shule iliyojaa utukufu wake,” aliandika Lulu.

==>>Tazama hapo chini alichoandika

Mizizi 29 Power Ni Dawa Ya Nguvu Za Kiume Ambayo Imechanganywa Na Mizizi 29

$
0
0
Kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wanaume wazee hata na vijana kupungukiwa au kutokuwa kabisa na nguvu za kiume nanimekuwa nikipigiwa simu na wanawake wakilalamika ndoa zao zipo mashakani maana hawaridhishwi na Waume au wapenzi wao pale wanapoaza kushiriki tendo la ndoa 

Kwa Nini Ujione Mpweke Pale Ukutanapo Na Mpenzi Au Mke Wako Kisa Eti Hauna Nguvu Za Kiume? ;Tumia MIZIZI 29 POWER, hii ndio tiba itakayorudisha heshima ya ndoa yako . 

Dawa hii itakufanya;
 1 Uchelewe kufika kileleni mda wa dakika 15-25 kwa tendo la kwanza 
2 Dawa hii itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 
3  Dawa hii uhimalisha misuri iliyolegea na kusinyaa?dawa hizi hazina madhara kwa mtumiaji nani tofauti na ulizowai kutumia ata wazee wenye umri mkubwa wanapona 

NSONSOMA; Dawa hii itakufanya umridhishe  mke au mpenzi wako kwani uboresha uume saizi upendayo urfu wa nchi 5,6,7 na 8 na unene wa sentimita 2,3,4 na 5 dawa  hii ipo ya kupaka na kunywa 

NSHOLA; NI dawa ya uzazi kwa waliongaika mda mrefu bila kupata mtoto 

MWITA; Dawa hii humvuta meme, mke,au mpenzi mliyetengana pia umrudisha mtu kazini haliyefukuzwa, kumpatanisha mwajiliwa na bosi wake 

Tunatibu presha kisukari, busha ,vidonda vya tumbo tumbo kuunguruma kujaa gesi na kukosa choo 

MAHALI ILIPO OFISI; PANDA DALADALA SHUKA BUGURUNI MALAPA AU ROZANA NA MWANZA YUPO WAKALA PIGA SIMU 0752348593 DR NYAROBI .Kama hauna nafasi ya kuja ofisini utaletewa popote ulipo huduma hizi
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images