MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588ILIPOISHIA
Mungu mwenyewe ndio amenilete hapa. Nitahakikisha kwamba ninaongoza jeshi la Boko haramu kuwaangusha viongozi wote mafisadi, wala rushwa na ving’ang’anizi wa madaraka. Na vifo vya wanajeshi walio kufa hospitalini ni lazima wamarekani waweze kulipa hilo”
Nilizungumza kwa msisitizo huku nikiwatzama wanajeshi hawa.
“BOKO HARAMUUUUUUUUUU”
Nilizungumza huku nikinyoosha mkono wangu wa kulia juu, wanajeshi wote wakaitikia kwa sauti ya pamoja iliyo nipa matumaini na kujiamini kwamba nina uwezo wa kuongoza wanajeshi hawa katika kutimiza ndoto alizo kuwa nazo mzee Okocha na zikatimia.
ENDELEA
Mwanajeshi mmoja akanifwata na kuninong’oneza sikioni.
“Mke wako mkuu amezinduka, yupo katika chumba cha maiti”
“Ninakuja”
Nilizungumza kwa sauti ya chini na mwanajeshi huyu, kisha nikageuka na kuwatazama wanajeshi hawa.
“Ninaimani kwa pamoja tutasaidia katika kuhakikisha kwamba tunashirikiana kwa pamoja kuhakikisha kwamba kila lililo pangwa linakwenda sawa kama lilivyo pangwa, na uzuri ni kwamba nitaongoza opareheni hizo kwani bado damu yangu inachemka, ninacho waomba tuendelee na majukumu ya ulinzi huku tukifanya taratibu za mazishi ya wetu”
Baada ya kumaliza kuzungumza hivyo nikashuka katika jukwaa hili, kwa haraka nikaanza kutembea kuelekea ndani, moja kwa moja nikangoza hadi kwenye chumba chenye mwili wa mzee Okocha, nikamkuta Yemi akiwa amelaza kichwa juu ya kifua cha baba yake huku akilia kwa uchungu sana.
Sikutaka kumnyanyua zaidi ya kubaki nikiwa nimesimama huku nikimtazama tu. Jinsi Yemi anavyo lalamika kwa uchungu kunanifsanya nijisikie vibaya sana kwa maana. Taratibu nikatoka nje huku nikijifuta machozi yaliyo anza kunilenga lenga. Nikatoa simu yangu mfukoni, nikaitafuta namba ya meja kisha nikampigia, simu yake ikaita kwa sekunde kadha kisha ikapokelewa.
“Ndio meja”
“Dany video uliyo ituma kwa raisi, imeweza kukabidhiwa kwa FBI, na wamepewa jukumu la kukutafuta”
“Wananitafuta kisa nini?”
“Dany unatambua kwamba umewaua makomandoo, wa Kimarekani jambo ambalo nchi ya Marekani haito kusamehe katika hili”
“Meja natambua kwamba unaelewa kitu ambacho kinaendelea, jambo nilio lifanya ni kujilinda mimi na watu wanao nizunguka, na mbona nilisha kubali matokeo mbele ya raisi ila yeye akahataji kuniua sasa anacho hitaji ni kutengeneza uasama”
“Natambua hilo Dany, ila kwa mimi sina la kufanya zaidi ya kuweza kukutaarifu nyendo zao. Unacho takiwa ni kuhakisha kwamba simu unayo itumia mawasiliano yake yanakuwa hayawezi kunyakwa na mtandao wowote wa kipelelezi kwa maana kufanya hivyo inaweza kuwa ni kosa kubwa sana na usalama wako utakuwa ni mdogo”
“Na walifahamu vipi kwamba upo hospitalini?”
“Sijafahamu ila kuwa makini sana Dany”
“Nashukuru meja, ila kama raisi anahitaji kuingia katika matatizo na mimi, sinto baki chini na mimi atanilazimisha kuunyanyua mkono wangu katika kumshuhulikia”
“Sawa Dany”
“Nashukuru Meja”
“Peter?”
Niliisikia sauti ya Yemi nyuma yangu, kwa haraka nikageuka huku nikiingiza simu yangu mfukoni mwangu.
“Unauzungumza na nani?”
Yemi aliniuliza huku macho yake yakiwa yamejaa uwekundu kutokana na kulia sana.
“Njoo”
Nilizungumza huku nikimshika mkono Yemi, tukaingia kwenye moja ya chumba, ambacho baada ya kutazama kwenye kuta zake, nikakuta kikiwa na shelfu nyingi za kuhifadhia vitabu.
“Mke wangu, kuna kazi kubwa ambayo nitahitaji kuifanya baada ya msiba wa baba”
“Kazi gani?”
“Nitahitaji kumuangamiza raisi wa Marekani?”
“Nini…..unaakili kweli Peter?”
“Yemi, ninacho kizungumza nina maanisha. Marekani imekuwa ni nchi ambayo kila siku inajitahidi kujitanua katika kuhakikisha kwamba ina ishikilia dunia, na kuingilia uhuru wa baadhi ya nchi zikiwezo za bara la Afrika pamoja na bara la Asia.”
“Nikiwa kama kiongozi wa jeshi la baba yako kwa sasa, siwezi kuendelea kukaa na kuona kwamba kuna watu wangu wamefariki pale hospitalini na kama nisinge tumia akili mimi na wewe pia tungefariki. Je kwa yule aliye tuua angeshuhulikiwa na nani, angeshikiliwa na nani, ni nani ambaye angedhubutu hata kuigusa Marekani kwa ajili ya vifo vyeu?”
Nilizungumza kwa uchungu huku nikimtazama Yemi usoni mwake, akaka kimya kwa maana hana kitu cha kufanya.
“Wamarekani wanahitaji malaki ya wanajeshi wa baba yako wasambaratike, wafe. Je hawa wanajeshi wana hawana famili, hawana wake, hawana wazazi, hawana watoto. Je ni nani atakaye simamia familia zao. Je kuna ajira gani ya kiserikali ambayo itaweza kuwaajiri hawa wanajeshi?”
“Yemi nakuomba uniache niifanye hii kazi, baba yako aliniamini na kunifanya niwez kiongozi wa hili jeshi. Ninakupenda na nitakulinda sinto hitaji mtu yo……..”
Sikumalizia kuzungumza sentensi yangu, Yemi akanikumbatia kwa nguvu huku akininyonya lipsi zangu. Taratibu tukaanza kunyonyana huku sote machozi yakitumwagika usoni mwetu.
“Ninakupenda sana mume wangu”
Yemi alizungumza baada ya kuniachia mdomo wangu.
“Ninakupenda pia mke wangu. Ninaomba kwa sasa nikashuhulikie na mipango ya kumzika baba”
“Sawa mume wangu, nakuomba uwe makini kwa maana umepewa majukumu ambayo hakunamtu aliye weza kuyatarajia kama yatakukuta wewe”
“Nashukuru mke wangu, ukaribu wako kwangu kwa sasa nina uhitaji kuliko kitu chochote “
“Sawa mume wangu nipo kwa ajili yako”
“Sawa”
Nikatoka ndani ya chumba hichi, nikamuita mmoja wa wanajeshi ambaye nimemkuta akiwa amesimama sebleni.
“Ni nani ambaye ni makamu wa mueshimiwa”
“Ni meja Otomu, na yupo makao makuu kwa sasa”
“Kuna njia gani ambayo ninaweza kuwasiliana naye?”
“Kuna chumba cha mawasiliano, munaweza kuwasilina moja kwa moja kwa kuonana”
“Naomba mundae kikao hicho ninahitaji kuonana naye”
“Sawa mkuu”
Nikaongozana moja kwa moja hadi kwenye chumba maalumu cha mawasiliano, Tv kubwa iliyomo humu ndani ikawashwa na nikaka kwenye kiti kilichopo mbele ya Tv hii.
“Ndani ya sekunde kumi atakuwa hewani”
“Sawa”
Ndani ya sekunde kumi hizo meja Otomu, akaonekana kwenye Tv hii kubwa.
“Habari yako jenero Peter”
“Salama tu meja Otumu. Ninahitaji kusikai maoni yenu kuhusiana na mazishi yam zee wetu”
“Tulikuwa tunasubiria kauli yako, ila kama utakubalina nasi basi tutakuja kumzika mzee huku kwenye makao makuu ya jeshi”
“Siwezi kulikataa hilo kwa maana nyinyi ndio wenyeji wangu, ila kabla ya sisi kufanya maamuzi yoyote ya kijeshi inabidi kumshirikisha mke wangu kwa maana yeye pia katika hili anahusika kwa asilimia mia moja”
“Kwa hilo halina shida”
“Ninda kamuite mke wangu”
“Sawa jenerali”
Japo ni kazi ambayo ninaimudu, ila sikuwahi kuwaza kwenye maisha yangu kwamba ipo siku nitakuja kuwa kiongozi wa kijeshi tena jeshi la kigaidi linalo windwa na serikali yake ya nchi ambayo ni Nigeria na dunia nzima. Maisha yangu siku zote yapo katika wakati mgumu sana wa kuwindwa, na chanzo kikubwa ambacho kinaniingiza katika matatizo haya ni mapenzi ambayo yalianza kwa bosi wangu K2, mlango ukafungulia na kujikuta nikistuka kutoka kwenye msongamano huu wa mawazo, Yemi akaka kwenye kiti cha pembeni yangu huku macho yake akitazama kwenye Tv hii kubwa.
“Mke wangu hapa tunajadilisi kuhisina na sehemu gani ambayo tunaweza kumzika baba, na meja amependekeza baba azikwe kwenye makao makuu ya kambi”
Yemi akaka kimya kwa muda huku akinitazama usoni mwangu, taratibu akatingisha kichwaakikubaliana kwa kile ambacho nimemuambia.
“Mke wangu amekubaliana na hilo swala”
“Sawa jenero, basi nitatuma helicopter mbili, ndani ya dakika arobaini na tano zitakuwa zimefika hapo”
“Nitashukuru meja”
Tukamaliza mazungumzo haya na kutoka ndani ya chumba hichi huku nikiwa nimemshika Yemi mkono wake. Mwili wa mzee Okocha ukaandaliwa na madaktari na akavalishwa nguo zake za ujenerali wa hili jeshi.
“Mkuu helicopter zimesha fika, tunahatajia kuondoka sasa”
Nikatoka katika chumba hichi cha kuuandaa mwili wa mzee Okocha. Nikamkuta Yemi akiwa amesimama sebleni.
“Mke wangu tuondoke”
“Na baba?”
“Wanakuja naye”
“Sawa”
Tukaongozana na mwanajeshi huyu hadi kwenye helicopter zilio tua kwenye moja ya kiwanja kilichopo hili eneo, tukaoneshwa helicopter ya kuingia. Tukaingia na taratibu helicopter hii ikaanzza kuacha ardhi.
“Umeshawahi kufika makao makuu ya kambi ya jeshi la baba yako?”
“Ndipo nilipo kulia, kabla sijaondoka kuelekea Uingereza kusoma”
“Sawa sawa”
“Ila baada ya huu msiba kuisha nitaomba nikulezee ukweli kuhusiana na maisha yangyu pamoja na baba yangu”
“Sawa mke wangu”
“Ila ninakuomba usije ukaniacha”
“Kwa nini nikuache mke wangu?”
“Kwa sababu mimi na baba yangu hatukupata muda wa kukueleza ukweli wa maisha yetu”
“Usijali mke wangu, kila jambo linatokea kwa sababu”
Niliendelea kumfariji Yemi ili asizidi kuwa mnyonge. Tukafanikiwa kufika katika makao makuu ya boko Haramu, kwa akili yangu ya kawaida nilihisi kwamba inaweza kuwa ni sehemu ya maficho ila kusema kweli ni eneo lililo jengwa vizuri, mzee huyu aliweza kuwekeza pesa nyingi katika kuwekeza katika hili jeshi, japo ni porini na miimani, ilakumejengeka sana.
Tukapokelewa na meja Otumu, moja kwa amoja tukapelekwa kwenye eneo la kupumzi huku ikiwa imesha timu saa kumi na moja alfajiri.
“Tumepanga mazishi ya fanyike saa kumu alasiri”
“Kwa nini ratiba mumeipeleka mbele kiasi hicho?”
“Kwa maana kuna wageni wengine ambo walikuwa ni marafiki wa jenerali tumeweza kuwataarifu na wengi wameahidi kuweza kufika katika mazishi haya”
“Sawa hilo ninawaachia nyinyi ila usalama si upo wa kutosha?”
“Ndio upo wa kutosha”
“Basi ninaomba tupumzike kwa maana siku hii imekuwa ni ndefu sana kwetu”
“Hakuna tabu jenerali”
Meja akatoka katika chumba tulichopo mimi na Yemi. Nikaka kwenye sofa huku nikiwa na mawazo mengi sana.
“Mume wangu kweli utaweza kuongoza hili jeshi?”
“Kwa nini unaniuliza hivyo?”
“Nimekuuliza tu mume wangu, ninakuona una mawazo mengi sana”
“Usijali mke wangu nitaweza. Vipi sijasikia swala la mwanao kuweza kuhudhuria mazishi ya babu yake?”
“Yupo mbali na Nigeria hatoweza kuwahi mazishi?”
“Kwani yupo wapi?”
“Yupo Canada kwa sasa”
“Sawa mke wangu”
Kwa uchovu nilio kuwa nao, nikajikuta usingizi ukinipitia na kulala fofofo.
“Baby amka”
Niliisikia sauti ya Yemi akizungumza akizungumza na mimi. Nikafumbua macho yangu na kujikuta nikiwa nimefunikwa na shuka.
“Nimekufunika na shuka mume wangu, baridi ilikuwa kali?”
“Wewe hujalala?”
“Nimekosa usingizi kabisa mume wangu”
“Sawa, ni saa ngapi sasa hivi?”
“Ni saa nne asubuhi, wageni wamesha anza kufika, ila Meja anawapokea itabidi twende nasisi kuwapokea”
“Sawa mke wangu”
Kwa haraka nikajifunuashuka, nikasimama huku nikipiga miyayo ya uchovu mkubwa nilio nao.
“Ila inabidi kubadilisha mavazi kwa sasa wewe ndio jenerali wa jeshi”
“Zipo wapi nguo za kuvaa?”
Yemi akapiga hatua hadi kwneye moja ya kabati, akanitolea nguo za jeshi. Nikaanza kuvaa nguo hizi taratibu. Yemi akaanza kunivisha vyeo ninavyo stahili kwenye shati langu, nikavaa na kofia ya cheo changu ambayo ina rangi nyekundu. Nikavaa na buti za jeshi, kwa utani Yemi akanipigia saluti na kujikuta nikicheka sana.
“Umependeza sana mume wangu”
“Nashukuru mke wangu”
“Twende sasa mume wangu”
Tukatoka ndani ya chumba hichi, kila mwanajeshi niliye kutana naye akanipigia saluti ya kuniheshimu. Tukafika katika kiwanja cha helicoptwer, tukakuta helicopter moja ikiwa ndio inajiandaa kushuka. Taratibu helicopter hii ikasimama sehemu husika, wakashuka wasichana wawili walio valia suyo nyeusi huku kwenye nyuso zao wakiwa wamevaa miwani nyeusi. Sikuamini macho yangu baada ya kumuona K2 akishuka huku akiwa amevalia nguo za jeshi jambo lililo nifanya nibaki nikiwa nimemkodolea macho ya hasira iliyo changanyikana na matukio mabaya aliyo ifanyia familia yangu miaka kadhaa iliyo pita nyuma.
AISIIIII……….U KILL ME 143
K2 akaanza kutembea kwa kujiamini huku walinzi wake wakiwa wamenzunguka, mmoja akiwa upande wa kulia na mwengine akiwa upande wa kushoto. K2 akaanza kusalimiana na meja, huku wakipeana mikono na kuzungumza maneno mawili matatu na wanaonekana kufahamiana sana. Akasalimiana Yemi, kisha akanifwata mimi, macho yetu yalipo kutana akabaki akinishangaa kwa sekunde kadhaa, ili kuepusha watu kuona tofauti zilizopo kati yetu, nikampa mkono wa kulia huku nikimtazama usoni mwake, taratibu na yeye akanipa mkono wake kiwoga.
“Muheshimiwa raisi huyu ni mume wangu anaitwa Peter, kwa sasa ndio mkuu wa jeshi”
Yemi alizungumza baada ya kugundua kwamba sisi hatufahamiani.
“Nashukuru kwa kukufahamu jenerali Peter”
“Peter huyu ni raisi wa Tanzan, mtu wa karibu kabisa na baba na anaitwa K2”
“Nashukuru kukufahamu muheshimiwa raisi K2”
“Nawe pia”
Nikauminya kidogo mkono wa K2 kumuashiria kwamba bado bifu kati yetu lipo, kisha nikamuachia mkono wake, akaongozwa na wanajeshi wenye kazi hiyo ya kuwaongoza wageni rasmi kwenye sehemu husika wanayo takiwa kufikia.
“Wageni leo watafika wangapi?”
Nilimuuliza Yemi kwa sauti ya chini.
“Sijajua labda meja anafahamu ni wageni wangapi wanaweza kufika”
“Muite”
Kwa ishara Yemi akamuita meja, akatembea kwa mwendo wa ukakamavu hadi katika sehemu niliyo simama.
“Wamesalia wageni wangapi kuweza kufika?”
“Wamesalia wageni kumi na moja kufika na wote wapo njiani”
“Sawa kuna mgeni wa karibu munaye taratiji kuweza kufika hapa baada ya dakika kadhaa?”
“Mgeni tunaye mtaratajia kufika kwa sasa, atafika hapa baada ya robo saa”
“Sawa meja”
Meja akanipigia saluti kisha akarudi katika sehemu husika.
“Mke wangu naomba niende msalani, haja ndogo imenikamata”
“Sawa mume wangu, vipi tupate chai?”
“Hapana tutapata baada ya muda huyo mgeni anaye kuja kufika”
“Sawa”
Nikaondoka kwa mwendo wa haraka katika eno hili, sikuwa na haja ya kwenda msalanani ila haja yangu ni kwenda kuonana na K2.
“Raisi wa Tanzania yupo jengo gani?”
“Lile pale mkuu”
Nikaelekea katika jengo alilipo K2 nikakuta walinzi wake wakiwa wamesimama nje ya chumba hichi.
“Nahitaji kuonana na raisi wenu”
Mlinzi mmoja akaiingia ndani, baada ya dakika moja akatoka na kuniruhusu kuingia ndani. Nikaingia, na kuufunga mlango kwa ndani, nikamkuta K2 akiwa ameshika bastola yake huku amekaa kwenye sofa lililomo humu ndani na kuikunja miguu yake katika mfumo wa nne. Mkono wake wa kushoto ameshika sigara kubwa akivuta taratibu. Tukatazamana kwa sekunde kadhaa kisha nikaka kwenye sofa lililopo mbele ya sofa hili, huku kati yetu tukiwa tumetengenishwa na meza ya kioo.
“Naona una jeshi kubwa sana”
K2 alizungumza huku akitoa moshi mwingi wa sigara mdomoni mwake.
“Sijakuja kujadiliana na wewe, wala kujua nina jeshi au sina. Nimekuja kukuonya kwa kile ambacho utajaribu kukizungumza”
“Hahahaaa, Dany oohooo samahani. Jeneral Peter, mbona unajistukia sana? Mimi nimekuja kumzika rafiki yangu na kuondoka au unahisi kwamba nitazungumza ukweli kwamba wewe ni gaidi ninaye kutafuta kwenye nchi yangu na pia ni mpelelezi wa Marekani?”
“Ni nani aliye kuambia mimi ni mpelelezi?”
“Dany tambua kwamba mimi ni mkubwa kwako, kuanzia umri hadi akili. Ninatambua nyendo zako zote ambazo huwa unazifanya, na kama unahitaji kunipa vitisho, nitakwenda kuzungumza kila kitu mbele ya hawa wanejeshi na utaona ni kitu gani watakacho kufanya. Alafu wewe mjanja kweli umetumia uzuri wako kumt** mtoto wa watu hadi baba yake amekupa ujeneral ambao wapo watu ndani ya hili jeshi walistahili kuupata”
K2 alizungumza kwa kujiamini, huku taratibu akiendelea kuvuta sigara yake, nikaitazama bastola yake aliyo ishika.
“Bado nitakuwinda hata kama ukihitaji kuniharibia katika hili jeshi kwa manaa si chochote kwangu”
“Hahahaa Dany acha kupiga biti za kitoto, kumbuka hii ni Nigeria na sio Tanz kwamba utaweza kujificha kwenye vichochoro unavyo vijua. Sasa kama umenihitaji bifu lizidi kuendelea humu ndani ya hii ngome eti unayo imiliki, ninakupa masaa ishirini na nne ujivue madaraka ya ujenerali na upotelee unapo pajua, la sivyo utakufa ndani ya hii ngome”
“Siwezi kufa na siogopi kufa, kama ulishindwa kunikamata tangu ukiwa NSS, na umekuwa raisi na nikaka meza moja ya wewe tena ikulu pasipo kunifahamu, basi tambua huwezi kunipiga. Nakujua K2 udhaifu wako na nitaweza kuutumia kuhakikisha kwamba nina kuangusha chini”
Nilizungumza kwa kujiamini, kisha nikasimama na kuanza kupiga hatua kuelekea mlangoni. K2 akaanza kucheka kicheko cha dharau na kunifanya nisimame, nikageuka na kumtazama kwa macho makali sana huku nikikunja ngumi ya mkono wangu wa kulia, kitu kinacho nifanya nishindwe kumfwata K2 karibu ni bastola aliyo ishika mkononi mwake.
“Dany siku nyingine uwe makini unapo zungumza”
K2 akatoa simu yake mfukoni, na kunisikilizisha mazungumzo yote tulio kuwa tunatazungumza, kumbe kwa muda wote tulio kuwa pamoja alikuwa anayarekodi.
“Sasa kupitia hii utaniacha mimi niweze kuishi kwa amani ya bwana, na pia utafwata nilicho kuambia kwamba ndani ya msaa ishirini na nne ambayo nitaamua kukaa hapa, hakikisha kwamba ujivua ujenerali na usiwe hata kuruta ndani ya hii kambi. Bye”
K2 akanipungia mkono, kwa hasiri nikatoka ndani ya hichi chumba na kuubamiza mlango kwa nguvu hadi walinzi wake wakahawi kuingia ndani kumtazama mkuu wao. Moja kwa moja nikaelekea chumbani kwetu, nikapitiliza hadi chooni, nikasimama mbele ya kioo na kujitazama. Macho yangu yote yametawaliwa na uwekundu ulio sababishwa na harisa kali pamoja na kejeli za K2.
‘Lazima nimuue’
Nilizungumza kwa hasira na kujiikuta nikipiga ngumi kwenye hichi kioo hadi kikavunjika.
“Peter”
Nilisikia sauti ya Yemi nyuma yangu, nikageuka nikamkuta akiwa amesimama huku ameduwaa, kwa maana kioo chote kimavunjika vipande vipande.
“Mume wangu una tatizo gani?”
Yemi aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu, akautazama mkono wangu wa kulia, kwa haraka akanisogelea na kuushika.
“Mume wangu tazama unatokwa na damu jamani”
Yemi alizungumza huku akiuweka mkono wangu kwenye sinki la kunawia, akanichomoa kipande kidogo cha kioo kilicho nikita katika kidole changu. Kwa haraka Yemi akaanza kuiosha damu zinazo mwagika, akatoka bafuni humu kwa haraka, baada ya dakika akarudi na boksi dogo la kuhifahidhi vitu vya huduma ya kwanza, akaanza kuniosha na dawa ambayo ni ina maumivu makali sana, ila sikuyajali zaidi ya roho yanu kutawaliwa na roho ya mauaji.
“Peter mume wangu ninakuomba uniambie ni kitu gani ambacho kimekupata jamani”
Yemi alizungumza huku akinifunga bandeji yeupe.
“Nahitaji……..”
Nikaka kimya huku nikitafakari nizungumzae kitu kilichopo moyoni mwangu, ila nikaka nikaona Yemi hastahili kufahamu chochote kwani hii vita haimuhusu kabisa.
“Unahitaji nini mume wangu”
Yemi alizungumza huku akinishika mashavu yangu kwa viganja vya mikono yake miwili. Nikamtazama usoni mwake kwa sekunde kadhaa, kisha kwa haraka nikaanza kunyonya midomo yake.
“Nahitaji kukut**……..”
Nilizungumza huku nikimshika Yemi makalio yake na kuyaminya kwa nguvu, hakuwa na ubishi kwa maana mimi ni mwanaume ninaye mmiliki. Nikambeba na kutoka naye humu bafuni, nikamlaza kitandani, na kuanza kumvua nguo zake, huku na yeye akiwa na kazi ya kufungua vifungo vya shati langu.
“Ila mume wagu kuna wageni wata…….”
“Shiiiii……”
Nilizungumza huku nikimziba Yemi mdomo wake kwa kutumia lipsi zetu, tukaendelea kunyonyana lipsi zetu kwa nguvu. Nikaanza kuchezea ,
Tukamaliza mzunguko wa kwanza, taratibu tukajikuta tukikumbatiana kwa nguvu huku hasira ikiwa imenipungua kwa kiasi fulani. Tukashuka na kuingia bafuni, tukaoga haraka haraka na kurudi chumbani, tukavaa nguo zetu na kutoka chumbani humu.
“Inabidi mume wangu kwa sasa uwe na mlinzi wako”
“Kwa nini?”
“Ahaa wewe ni jenerali kuwa na mlinzi ni lazima na si mmoja bali hata wawili au watatu”
“Nahitaji wewe ndio uwe na walinzi sawa mke wangu”
“Sawa mume wangu”
Tukafika katika kiwanja cha helicopter, wageni kutoka mataifa mbali mbali wakazidi kufika, hadi inafika saa nane mchana tukawa tumemaliza kupokea wageni tulio kusudia kuweza kufika katika msiba wa mzee Okocha.
Tukaelekea kwenye sehemu ya kupata chakula na wageni husika, nikatambulishwa kwa wageni woge walio weza kufika katika eneo hili. Il kila ninavyo mtazama K2 ninahisi moyo wangu kuniuma kwani bado nina kinyongo naye.
Tukaendelea kupata chakula mchana huku sehemu husika ya mazishi ikiwa inaandaliwa na wanajeshi. Baada ya chakula cha mchana hatukuwa na muda wa kupoteza. Moja kwa moja tukaelekea katika kiwanja cha mazishi. Tukakuta wanajeshi wengi wakiwa wamejipanga, huku wote wakiwa wamefunga vitambaa vyeusi kwenye mikono yao ya kushoto.
“Jeneral kuna risala unatakiwa kusoma”
Meja alizungumza kwa kuninong’oneza huku akiweka katarasi kadhaa mezani mwangu.
“Risala, mbona hamkunijulisha mapema?”
“Ni kosa tu limejitokea, ila nitakuomba uipitie kwa dakika kadhaa kisha ukifika muda wa risasa nitakuomba uweze kuisoma”
Nikashusha pumzi yangu, nikaizipitia karatasi hizi nne, kisha nikatingisha kichwa kumkubalia Meja kwamba nitazisoma. Meja akarudi kwenye kiti chake na kunifanya nianze sasa kuisoma risasa hii, hatua hadi hatua.
“Wameiandaa vizuri?”
Yemi aliniuliza huku akininong’oneza
“Ndio ninaipitia hapa”
“Hembu niione kwa mana niliwapa maelezo na jinsi ya kuiandika”
“Sawa”
Nikamsogezea Yemi karatasi hizi, akaanza kuzipitia moja baada ya nyingine.
“Kuna vitu hawajaviweka, kama huto jali ninakuomba nikaisome hii risala”
“Sawa mke wangu, ila kuna vitu gani ambavyo hawajaviweka?”
“Historia ya baba wameikosea, upiganaji wake katika kuunda hili jeshi wameandika rasha rasha, sasa sijui ni nani aliye andika”
Kwa ishara nikamuita meja, akafika katika eneo tulipo, akanima chini taratibu.
“Meja hii risala mumeiandika tofauti mbona. Hichi sio kile nilicho waeleza watu wako asubuhi”
“Samahani mkuu, kama inawezekana ninaweza kuandaa nyingine”
“Hapana nitatoa kichwani mwangu, sawa”
“Sawa mkuu”
Yemi alizungumza kwa ukali kidogo, nikamruhusu Meja kuandoka na kubaki nikimtazama Yemi jinsi anavyo endelea kusoma risasala hii. Muda wa kusoma risasa ukafika, yemi akasimama na kusogela jukwa maalumu, akaanza kusoma risala ya baba yake huku akito historia ya baba yake. Hadi anamaliza machozi yakawa yanashuka kwenye uso wake nikasimama na kumsogelea hadi sehemu simama nikamkumbatia taratibu huku macho yangu yakiwaangalia wageni waalikwa. Macho yangu yakafika kwa K2 ambaye naye ananitazama, kwa ishara ya mkono akanionyeshaea ishara ya kunikata shingo yangu, jambo lililo nifanya nizidi kumchukia hadi nikahisi moyo wangu ukitaka kupasuka kwa maumivu haya ninao yasikia.
ITAENDELEA
“Je Dany atajiudhuru cheo chake cha jeshi la Boko haramu kama K2 alivyo muhitaji kufanya. Usikose sehemu inayo fwata.”