Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Boomplay, Universal Music Group Watangaza Ushirikiano Katika Usambazaji Muziki

0
0
Universal Music Group inakuwa kampuni ya kwanza kuingia mkataba na jukwaa linaloongoza kwa huduma ya kusikiliza na kupakua muziki barani Afrika.

Boomplay, huduma ya muziki inayoongoza upande wa kusikiliza na kupakua muziki na Universal Music Group (UMG), kampuni inayoongoza katika usambazaji wa muziki ulimwenguni, leo wanatangaza kusainiwa kwa makubaliano ya kibali cha kusambaza muziki katika masoko mengi ndani ya Afrika.

UMG ni kampuni ya kwanza ya muziki wa kupitisha leseni yake kwa Boomplay, ambayo inajulikana kwa huduma yake ya kusikiliza muziki barani Afrika. Chini ya makubaliano ya mkataba huu wa miaka mingi na ufanisi mara moja, Boomplay itasambaza muziki kutoka kwa UMG nchini Tanzania pamoja na Nigeria, Ghana, Kenya, Rwanda, Uganda na Zambia. Mpaka sasa, Boomplay ina nyimbo zaidi ya milioni mbili na maelfu ya video zinazopatikana kwa watumiaji wake zaidi ya milioni 36, na watumiaji karibu milioni mbili wanaoongezeka kila mwezi.

Watumiaji wa Boomplay sasa wanaweza kupata nyimbo za nyumbani na za kimataifa kutoka UMG wakiwemo wasanii kama Eminem, Tekno, Post Malone, Nicki Minaj, Lady Zamar, Lil Wayne, Bob Marley, Brenda Fassie, Wurld, J.Cole, Dr. Tumi, Nasty C, 6lack, Diana Ross, Hugh Masekela, Jon Bellion, Larry Gaaga, Tamia, Maroon 5, Aka & Anatii, TJAN, Jah Prayzah, Nonso Bassey, Mafikizolo, Cina Soul, Ella Mai, Mr. Eazi na wengine wengi.

Mapema mwaka huu, UMG ilitangaza uzinduzi wa Universal Music Nigeria, ikiwa na lengo la kuwapa wasanii fursa nyingi barani Afrika kwa ajili ya kufanikisha kazi zao kufika hatua za kimataifa. UMG inaendelea kusukuma gurudumu la lengo lao la kukuza mazingira ya muziki wa Afrika pamoja na kurekodi muziki, kuchapisha muziki, uzalishaji, matamasha, ushirikiano wa makampuni na jitihada za biashara.

Katika hili, Makamu wa Rais wa Universal Music Group, idara ya Maendeleo ya Masoko, Adam Granite alisema, "Tunatarajia kufanya kazi na Boomplay ambapo tutawawezesha wasanii wetu wa Kiafrika kuwa wabunifu, jukwaa la masoko na uendelezaji wa rasilimali ili kuharakisha kazi zao zinaendelea kukua barani Afrika. Mkataba huu utasaidia wasanii wa UMG kufikia watumiaji wapya, huku wakiongeza hamasa ya usikilizaji wa muziki wa Afrika ili watapate faida kuwafikia mashabiki wa muziki, wasanii wengine na wazalishaji muziki.

"Ushirikiano huu utaendelea kufikia watu wengi na kuhakikisha kazi za wasanii wetu zinawafikia mamilioni ya wapenzi wa muziki barani Afrika," alisema Ezegozie Eze Jr., Meneja Mkuu wa Universal Music Nigeria, "Tunafurahia kuwa kampuni ya kwanza ya muziki kushirikiana na Boomplay na tunatarajia kuleta ubunifu wa hali ya juu kwa wasanii wetu na kwa watumiaji wengi Afrika. "

Akizungumza pia, Mkurugenzi Mtendaji wa Boomplay, Joe He, alisema kuwa Boomplay itaendelea kuunda ushirikiano unaoimarisha mfumo wa kidigitali na kuunganisha wapenzi wa muziki na nyimbo wananazozipenda wakati wowote na mahali popote.

“Boomplay imejizatiti kuendelea kutengeneza shauku kubwa ya muziki wa kiafrika katika njia halali, hasa kwa watumiaji wa Boomplay kushirikiana na lebo kubwa za muziki duniani kama Universal Music Group inatoa nafasi nyingine kubwa kwa sisi kufanya hivyo ",
alisema.

App ya Boomplay ambayo kwa sasa inapatikana kwa watumiaji wa simu za Android, inatarajia kuzindua app kwenye jukwaa la iOS hivi karibuni. Kwa kuongeza, watumiaji wapya wa Boomplay wataweza kupata usajili wa miezi moja bila malipo pale watakapojiunga na kifurushi cha mwezi mmoja kinachojirudia.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na
 
Universal Music Group:
James Murtagh-Hopkins / +44 203 932 6822;  james.murtagh-hopkins@umusic.com

Boomplay:
Tosin Sorinola / +234 8166896617 tosin.sorinola@transsnet.com
 
Natasha Stambuli / +255 677007428 natasha.stambuli@transsnet.com
Kuhusu Boomplay
Boomplay ni app inayotoa uwezo wa kusikiliza na kupakua nyimbo, inayomilikiwa na kampuni ya Transsnet Music Limited. App hii ina mamilioni ya nyimbo na video, ikiwaunganisha mashabiki wa muziki na nyimbo wazipendazo muda wowote. Mpaka sasa, Boomplay ina watumiaji zaidi ya milioni 32, kati yao zaidi ya milioni 10 ni kutoka Google Play Store na wengine ni watumiaji wa simu za TECNO, Infinix na itel. 

Huduma hii inapatikana katika mtandao na hasa kwenye mfumo wa Android. App hii ambayo imewahi kushinda tuzo ya “Best African App” katika tuzo za “Apps Africa” mwaka 2017, inawezesha watumiaji wake kusikiliza na kupakua nyimbo pamoja na kujiunga na kifurushi kitakachokuwezesha ku-save nyimbo na kusikiliza bila kutumia data. 

Kwa muda mrefu sasa, huduma nyingi za malipo zimeanzishwa na hili limewarahisishia mashabiki wa muziki kulipia nyimbo kupitia huduma za pesa kwa njia ya simu, benki pamoja na kadi za Boomcoin. Lengo kubwa la Boomplay ni kujenga mfumo endelevu kwenye tasnia ya muziki. Bofya hapa kujua zaidi.

Kuhusu Universal Music Group
Ni kundi la kimataifa linaloongoza katika burudani, usambazaji wa kazi za muziki, kurekodi muziki, kuuza kazi za muziki na video katika nchi zaidi ya 60 duniani. Ikiwa na orodha ya kina kwenye kurekodi nyimbo za kila ladha,UMG hutambulisha na kuendeleza wasanii pamoja na kusambaza muziki uliopendekezwa sana kibiashara. 

Ikiwa imejikita kisanaa, ubunifu na ujasiriamali UMG inakuza maendeleo ya huduma, majukwaa na mifano ya biashara ili kuongeza fursa za kisanii na kibiashara kwa wasanii wa Afrika na kujenga uzoefu wa huduma mpya kwa mashabiki. Universal Music Group ni kampuni ya Vivendi. Pata maelezo zaidi hapa.


Bunge Kuanza Kesho Jumanne

0
0
Mkutano wa 13 wa Bunge utaanza kesho, huku miswada ya sheria mitano ikitarajiwa kusomwa kwa mara ya kwanza ikiwemo wa sheria ya vyama vya siasa ya mwaka 2018.

Spika wa Bunge, Job Ndugai  leo amesema miswada mingine ni wa maji na usafi wa mazingira, marekebisho ya sheria mbalimbali namba nne wa mwaka 2018, muswada wa mamlaka ya hali ya hewa wa mwaka 2018 na wa mamlaka ya usimamizi wa usafiri wa nchi kavu.

"Pia kuna muswada wa sheria za huduma ndogo za fedha wa mwaka 2018 ambao utasomwa katika hatua zake zote. Hati ya dharura ya mheshimiwa Rais nimeshaipokea na kamati ya uongozi imeridhia kusomwa katika hatua zake zote," alisema.

Aidha, alisema wabunge wanne watakula kiapo kesho ambao wote ni wa CCM,  Thimotheo Mzava (Korogwe Vijijini), Mwita Waitara (Ukonga), Julias Kalanga (Monduli) na Zuberi Kuchauka (Liwale).

Alisema pia katika mkutano huo mapendekezo ya mpango wa maendeleo wa mwaka 2019/20 utajadiliwa na sehemu kubwa mijadala itajikita katika mpango huo.

Ndugai aliongeza kuwa, maswali 125 yataulizwa na ya papo kwa waziri mkuu yatakuwa 16.

DC Muro Awatia Mbaroni Watuhumiwa Watatu Walioshiriki Kumtoa Mimba Mwanafunzi

0
0
Na Imma Msumba Arumeru,
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru kwa kushirikiana na Jeshi la polisi Wilaya ya Arumeru limewakamata watuhumiwa wa Tatu ambao wameshiriki kumtoa mimba mwanafunzi wa kidato cha nne kwa kutumia dawa za miti shamba suala ambalo linachochea mimba kwa wanafunzi na kuzorotesha elimu yao.

Dc Muro amesema kuwa wamebaini tukio hilo baada ya kuweka mtego na kuwabaini watuhumiwa hao pamoja na mtia mimba ambao wamefikishwa polisi kwa ajili ya kufikishwa mahakamani

Akielezea jinsi alivyopewa ujauzito na kisha ujauzito kutolewa aikaeli Pallangyo amesema ni kweli alipata ujauzito Kwa kurubuniwa na kijana wanaeishi nae Jirani nyumbani ambae alikuwa akimrubuni Kwa kumpatia fedha

Kwa upande wao watuhumiwa wa sakata hilo kijana aliempa mimba Binti,pamoja na mama Mzazi wa Aikaeli na mwanamke ambae ni ndugu wa Kijana aliempa mimba ambae anatajwa kuhusika na kumtoa ujauzito Binti wametoa sababu mbalimbali ambazo hata hivyo zimeonekana kukinzana zenyewe Kwa zenyewe Kutokana na mama wa Binti kukiri Kuwafahamu watuhumiwa wenzake na kuelezea tukio la Mchezo mzima ulivyokuwa

Akidhibitisha taarifa Za Binti huyo kuwa mjamzito na kutoa ujauzito, Mganga mkuu wa halmashauri ya Meru Daktari Cosmas kilasara amesema vipimo vya awali vilionyesha Binti kuwa mjamzito na vipimo walivyofanya tena vimeonyesha Binti sio mjamzito tena ambapo amesema hata hivyo Binti huyo ameendelea kupata dalili zote Za kuwa na ujauzito ikiwemo ya maziwa kutoka.

Kutokana na tukio hilo Mkuu wa Wilaya ya Arumeru amevigiza vyombo vya Usalama kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wote ambao wamehusika katika tukio hilo , ambapo pia amelitaka jeshi la Polisi kuhakikisha wanawakamata na wanawafikisha mahakamani watu wote waliohusika katika kuwapa ujauzito wanafunzi 57 Kwa kipindi Cha miaka miwili iliyopita.

Imetolewa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 26

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA  
 “Umesahau masharti yetu. Endapo utamueleza mtu yoyote kuhusiana na mimi basi nitakwenda kumuua huyo mtu pasipo huruma ya aina yoyote”
Ethan alizungumza huku mboni za macho yake zikibadilika badilika rangi, mara nyeusi, mara rangu ya blue na akazidi kutisha zaidi, zilipo badilika kuwa rangi nyekundu, huku machozi ya rangi nyekudu yakimwagika usoni mwake jambo lililo nifanya nijawa na woga mkubwa sana na wasiwasi.
“Najua uliniita sana, ila fkila jambo lililotokea kwa sababu ya huyu mwanamke wako. Kwa ajili yake yeye nilazima sadaka ya damu za wanadamu zitolewe ili furaha yako izidi kudumu zaidi na zaidi”
Ethan alizungumza kwa sauti nzito sana iliyo jaa utetemeshi mithili ya radi hadi nikajikuta mimi mwenyeweni nikiogopa sana kwani kila analo lizungumza linasababisha vitu vilivyomo ndani ya hichi chumba kupeperushwa na kuanguka chini.

ENDELEA
“Una maanisha nini?”
Nilizungumza huku nikiwa na wasiwasi mwingi sana. Ethan akaisogelea tv kubwa iliyomo humu chumbani, akainyooshea mkono wa kushoto na ikabadilisha matangazo ya kituo cha ESport niliyo kuwa nikiyatazama na kuonyesha kundi kubwa la wasichana walio valia sare za shule zinazo fanana na sare za shuleni kwa Camila.
“Hawa ni wasichana wezake ambao kwa sasa wapo nchini Somalia”
Ethan alizungumza kwa sauti ya kawaida na kusababisha hali ya upepeo humu ndani kutulia kabisa na hata mingurumo ya radi sikuweza kuisikia tena.
 
“Angalia”
Ethan aliniambia na nikazidi kutazama safari hiyo ya wanafunzi wezake Camila. Gafla basi walilo panda likazingirwa na gari nne ina za pick up zilizo jaa watu wenye silaha huku wakiwa wamevalia vitambaa kichwani huku wakiwa na mavazi ambayo si rasmi. Wakampiga dereva wa basi hilo risasi nyingi sana kisha wakaingia ndani ya basi hilo huku wakiwa na mitutu yao mikubwa ya bunduki.
“Laiti mpenzi wako angekusikiliza haya yasinge wakuta wezake”
“Ila Ethan si uliniambia asiende na hakwenda kweli?”
“Moyo…..Moyo wake ulisha dhamiria na safari ali ighairi mara tu ya kusikia wewe umetekwa, la sivyo angeenda”
Ethna alizungumza kwa msisitizo mkubwa sana.
 
“Naomba basi uwasaidie wasipate matatizo?”
“Kwa kosa hilo la mpenzi wako ni lazima wezake walipe kwa damu zao na hilo tukio linatokea sasa hivi nchini Somalia, na wote wanafunzi kumi na tisa na waalimu wao wanne lazima watauwawa kikatili sana”
Nikashuhudia mwalimu mmoja wa kiume akipigwa risasi kichwani mwake na kuanguka chini.
“Ethan fanya jambo rafiki yangu?”
“Snna uwezo wa kufanya jambo hilo, nimekusaidia ili uweze kuwa na furaha yako kwa maana huyu mwanamke ndio furaha yako laiti angekufa huyu usinge kuwa na furaha maisha yako yote”
“Je na wale wanao hitaji boksi jeusi ni kina nani?”
Mlango ukafunguliwa, akaingia Mery akiwa ameshika kifuko cha rangi ya kaki. Ndni ya sekunde tano kila kitu kikarudi katika hali yake na wala Mery hakuweza kuelewa ni kitu gani kilicho tokea humu ndani. Ethan akanitazama kwa sekunde kadhaa, kisha akapotea.
“Wifi amelala?”
“Yaaa nahisi alichoka na safari”
Mery akaka kwenye kiti kilichopo karibu kitanda hichi.
“Nimekuchukulia kuku wa kuchoma na ndizi za kuchoma kama unavyo penda”
 
“Nashukuru”
“Wifi amka ule”
Tartaibu Camila akaamka huku akipiga miyoyo mingi itokanayo na uchovu mwingi sana.
“Ehee nimechoka jamani”   
“Pole sana mke wangu”
Nilizungumza huku nikimtazama Camila usoni mwake, nikatupia macho yangu kwenye tv hii na kuona maandalizi ya mechi ya timu yangu ambayo inakwenda kuanza muda si mrefu. Nikatamani kumueleza Camila juu ya matatizo ambayo yanawakuta rafiki zake kwa muda huu ila nikashindwa kabisa kwani ataniuliza nimejuaje.
“Samahani kunwa wana usalama kutoka serikalini wanahitaji kuzungumza na Ethan tunaweza kuwaruhusu?”
“Kama ni maswala ya mahojiano waambie wamuache mume wangu ale kwanza”
“Sawa”
 
Daktari akafunga mlango na kutuacha, tukaendelea kula taratibu huku nikimtazama Camila usoni mwake. Mpira ukaanza, huku uwanja ukiwa umemimimika mashabiki wengi sana ambao wengi wao wameshika mabango yanayo nitakia afya njema na nipone haraka ili nirudi uwanjani.
“Watu wanakupenda sana mume wangu”
Camila alizungumza huku akinilisha kipande cha ndizi.
“Kweli”
“Sasa baadae inabidi ufanye mpango uwashukuru watu hao”
“Nitawashukuru vipi dada yangu?”
“Hata kwa kuwaandikia kwenye ukurasa wako wa Twitter”
“Sawa, vipi hali ya mama?”
“Mama yupo na nesi wake nyumbani, bado hali yake ndio ile ile”
“Habari ya kutekwa kwangu anaifahamu?”
“Sikuthubutu kumueleza kwa maana na uzee ule na hali aliyo nayo tungempoteza kabla ya siku zake”
“Sawa dada yangu nashukuru kwa hilo”
“Usijali”
 
Pinto akafunga goli la kwanza na kutufanya wote ndani ya hichi chumba kushangilia kwa furaha. Wachezaji wote wakajipanga mstari mmoja, kisha wakafunua tisheti zao na kila tisheti moja ina herufi moja zilizo anaindikwa ETHAN KLOPP. Nikajikuta nikijawa na furaha kubwa sana. Hadi wanakwenda kipindi cha kwanza wanaongoza goli moja. Walinzi wa wili wa Camila wakaingia chumbani humu.
“Unatakiwa kuondoka madam”
“Kuna nini!!?”
Camila aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana.
“Utakwenda kufahamu ukifika nyumbani, mzee anakuhitaji”
“Likini mpenzi wangu ana umwa jamani”
“Tunalifahamu hili madam ila ni amri kutoka kwa baba yako na hatuna la kufanya”
Camila sura yake dhairi ikaonyesha imejawa na masikitiko makubwa sana, akanitazama huku machozi yakimlenga lenga usoni mwake. Taratibu akaninipsi zangu, kisha akakumbatiana na dada Mery kidogo.
“Kesho pajapo majaliwa ya Mungu nitakuja sawa”
“Sawa mpenzi wangu”
Camila akatoka ndani huku na walinzi wake hao wawili ambao ninawafahamu na wamekuwa wakimlinda toka alipo kuwa shule ya msingi.
“Inabidi na wewe Ethan utafute walinzi”
“Wa nini dada?”
“Kwa ajili ya usalama wako, hembu tazama jinsi ulivyo tekwa, hadi sasa hivi sijajua huko wallikufanya kitu gani hadi kukuachia na kukutupa mbele ya hoteli”
“Usijali dada yangu usiwe na wasiwasi kila jambo litakwenda vizuri”
 
“Lini Ethan, unanipa wasiwasi mwenzio unajua?”
“Nalitambua ila wewe kuanzia leo inabidi uwe na walinzi wa karibu sana ambao watakulinda kila sehemu unayo kwenda”
Nilizungumza kwa msisitizo huku nikimtazama dada Mery usoni mwake.
“Watu walio niteka wanahitaji bosky jeusi, wanasema ni boksi ambalo ni mali yao na baba alilichukua”
“Boski jeusi, ndio lipi?”
“Hata mimi sifahamu hata lipo vipi, nashindwa hata kufahamu ninaanzia wapi kuwatafutia, isitoshe wanasema nisipo wapelekea tu, basi wanaanza kukuangamiza wewe”
“Ohoo Mungu wangu!!!”
“Ndio maana nahiyaji ulinzi uongezwe nyumbani. Maswala ya kwenda kwa shemeji sasa hivi hembu yakatishe kwanza, mimi nitawatafutia hili boksi kisha nitawapelekea”
 
“Ethan naogopa mwenzio”
Taratibu nikamshika dada Mery mkono wake wa kulia huku nikimtazama usoni mwake.
“Nipo kwa ajili yako, siwezi kukuacha wewe na mama mukapata tatizo lolote dada yangu umenielewa?”
Dada Mery alizungumza huku akitingisha kichwa chake akimaanisha kwamba amenielewa.
“Vizuri, naomba umpigie mwanasheria wa familia namuhitaji hapa hospitalini”
“Sawa”
Dada Mery akampigia simu mwanasheria huyu aliye ahidi atafika hospitalini hapa mara baada ya nusu saa. Tukaendelea kuangalia mpira huu,  kusema kweli timu yangu inacheza kwa umoja na mshikamano hadi wanamaliza kipindi cha pili, wakaibuka na ushindi wa goli moja bila.
“Kazi nzuri wamefanya”
“Yaa”
Mlango ukagongwa, nikamruhusu anaye gonga kuingia ndani. Mwanasheria wa familia akaingia ndani, tukamsalimia kutokana ni mzee sana. Akaka kwenye kiti cha pembeni, akaniomba nimsimulie ni kitu gani kilipelekea hadi mimi kutekwa. Nikamueleza kila kitu, kuanzia tulivyo kuwa ndani ya basi na wachezaji wezangu hadi pale nilipo jikuta nipo nchini Russia.
 
“Sasa wao wanahitaji hilo boksi jeusi, unalifahamu kweli?”
Mwanasheria akaka kimya huku akinitazama na macho yanayo maanisha kwamba anafahamu kile nilicho mueleza.
“Tafadhali niambie ukweli unafahamu hilo boski jeusi?”
“Ndio”
Nikashusha pumzi taratibu.
“Ila siwezi kukuambia lipo wapi kwa maana ni hatari sana hilo boksi Ethan”
“Kwa nini ushindwe. Maisha ya dada yangu, yangu na mama yangu yapo kwenye hatari. Walio niteka wanataka hilo boksi. Sema ni wapi lilipo ili tujue tunajitoa vipi kwenye huu mpango”
“Ni jambo la hatari sana kufanya hivyo Ethan. Ukiwakabidhi boksi hilo hakika dunia nzima itakwenda kuangamia kwa ajili yako”
Tukatazamana na dada Mery huku tukiwa na wasiwasi mwingi sana.
“Kivipi?”
“Samaani kwa kuwaingilia. Ninaitwa Agent Thomas. Ninamaswali kadhaa ninahitaji kukuhoji bwana Ethan”
Alizungumza mwanaume mmoja wa kijerumani, huku akituonyesha kitambulisho chake kinacho mtambulisha yeye kama mpelelezi mkuu kutoka katika kitengo cha Bundesnachrichtendienst  (BND).
 
“Bila sahamani”
Nilizungumza huku nikikaa vizuri kitandani.
“Wengine sijui munaweza kutupisha kwa muda”
“Mimi ni mwanasheria wake, kama ni maswala ya kiusalama unaweza kuzungumza nikiwemo nami ndani humu”
Mwanasheria wa familia alizungumza huku akimtazama bwana Thomas. Bwana Thomas akamtazama Mery kwa muda, dada Mery hakuhitaji hata kusemeshwa neno, akanyanyuka na kutoka chumbani humu na kutuacha sisi.
“Ilikuwaje mukatekwa?”
Nikaanza kuwaadisia jinsi basi lilivyo zuiwa na watekaji hao. Mwanasheria kwa ishara ya kidole akanikataza kuzungumzia kuhusiana na bosky jeusi.
“Je ni kitu gani walihitaji kwako hadi wakaamua kukuteka?”
“Hawakunieleza kitu chochote”
“Kweli Ethan?”
“Ndio hawakuniambia kitu cha aina yoyote ile”
“Je unaweza kuwakumbuka sura zao watu hao?”
“Mzee mmoja ninaweza kumkumbuka”
“Unaweza kuingi”
Bwana Thomas alizungumza kwa kutumia kinasa sauti kilichopo mkononi mwake. Akaingia mwana dada aliye valia miwani kubwa kidogo huku mkononi mwake akiwa ameshika laptop.
 
“Unaweza kumuonyesha picha za wale washutumiwa”
“Sawa mkuu”
Akafungua laptop yake kisha akaanza kunionyesha picha za wahalifu mbalimbali, hadi anafika mwisho hapakuwa na picha ya hata mualifu mmoja ambaye nina mfahamu.
“Je unaweza kumuelezea mzee huyo jinsi alivyo?”
“Ndio”
“Ehee muelezee”
Nikaanza kumuelezea mzee huyo jinsi anavyo onekana huku dada huyu akiwa makini katika kumchora kila ninacho kieleza, hadi ninamaliza kumuelezea mzee huyo, huyu dada naye akawa amemaliza na kunigeuzia picha aliyo ichora.
“Yupo hivi”
Nikajikuta nikishangaa sana kwani huyu dada ana kipaji cha hali ya juu, kwani mzee huyo amemtoa vile vile alivyo kuwa amenieleza.
“Ndio”
“Itume hiyo picha makao makuu na msako uanze kufanywa nchi nzima.”
 
“Sawa mkuu”
“Tunashukuru Ethan kwa muda wako, tutakapo kuwa na hitaji lolote basi tutakutafuta na kuzungumza nawe”
“Sawa sawa”
Thomas na dada huyu wakaondoka na dada Mery akaniingia ndani, nikamueleza dada Mery kile kitu ambacho nimehojiwa.
“Hii ishu ni kubwa sana, ndani ya serikali hii na dunia, hilo boksi jeusi linatafutwa. Na mtu pekee ambaye alikuwa anafahamu ni baaba yenu”
“Mbona hunyooshi maelezo, wewe si umesema kwamba unafahamu lilipo boksi hilo?”
“Ninacho fahamu ni njia ya kuweza kulipata boksi hilo seheu lilipo fichwa”
“Ni njia gani?”
Mwasheria akaka kimya kwa muda huku akitazama chini.
“Nakuuliza njia gani?”
“Njia ya kulipata ni wewe Ethan”
Maneno ya mwanasheria huyu yakatuacha mimi na dada Mery midomo wazi kwani sifahamu mimi nina njia gani ikiwa sifahamu hata muonekano wa boksi hilo jeusi.

==>>ITAENDELEA KESHO

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 138 na 139 )

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   
 
“Baba umefwata nini chumbani kwangu!!”
Niliisikia sauti ya Yemi Okocha akizungumza kwa mshangao, nikahisi labda yupo usingizini.
“Huyu ndio aliye kufanya umsaliti mumeo?”
Sauti nzito ya mwanaume ikanifanya nifumbue macho yangu, nikakutana na sura ya baba Yemi ambaye ni gaidi niliye tumwa kuja kumtafuta nchini hapa Ningeria, pembeni yake wamesimama wanajeshi wawili wakiwa na bunduki mkononi mwao, na mlangoni nikamuona mume wa Yemi Okocha akitutazama kwa hasira kali huku Yemi naye amekaa pembeni yangu huku amejifunika kwa shuka kuficha maungo yake ya ndani.
       
ENDELEA   
“Baba sio kosa la huju kijana kulala na mimi au kumsaliti huyo mshenzi hapo”
Yemi Okocha alizungumza kwa kujiamini sana huku akimtazama baba yeke usoni, mwili mzima ukaanza kunitetemeka kwa maana hili kosa ni saawa na kufuniwa na mke wa mtu.
“Mume wako amenieleza kila kitu, kwamba amekukuta na huyu kijana na mukamvamia na kumpiga kisha hapa mumelala pamoja”
“Ni muongo, baba unajua ni jinsi gani nilivyokuwa ninampenda Thomas, unatambua ni jinsi gani nilivyo yatoa maisha yangu kwa ajili yake, hadi hii hoteli alijenga kwa pesa yangu ambayo wewe umenipatia. Leo hii nimsaliti kirahisi pasipo yeye kuanza ujiang”
 
Yemi alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Sikuhitaji hata kujitingisha kwa maana kunaweza kuniletea matatizo na isitoshe kwamba nimepoteza ujasiri kabisa na sina uwezo wa kupambana kabisa.
“Baba mimi ni mwanao wa pekee. Haya ni mahusiano na maamuzi yangu binafsi, sinto penda wewe uyaingilie”
“Lakini mwanangu hii ni aibu, kulala na mwanaume mwengine namna hii”
“Baba yeye amelala na wahudumu wawili wa hoteli yangu, ninawalipa pesa yangu. Wamelala kwenye kitanda changu ambacho ni mali yangu. Hapo kweli kuna ubaya wa mimi kuamua kufanya maamuzi tofauti na yeye. Sinto jali baba kaishi maisha yangu mimi ukiendelea kunishawishi kurudiana na Thomas, simpendi na ukimuacha aendele kunisogelea ninakuahidi nitamuua”
Yemi Okocha alizungumza kwa ujasiri mkubwa huku akiendelea kumtazama baba yake, baba Yemi akashusha pumzi nyingi sana, akanitazama usoni mwangu kwa macho makali yaliyo nipa woga fulani.
“Kijana unaitwa nani?”   
“Peter”
Nilizungumza huku nikiendelea kutetemeka mwili wangu. Naamini kutetemeka huku pia kunanisaidia kuficha uhalisia wangu juu ya kazi ya upelelezi iliyo nilete hapa Nigeria.
“Vaa nguo zako”
“Baba Peter haondoki hapa pasipo mimi na kama unahitaji avae nguo zake wacha mimi nivae kwanza.”
“Yemi alizungumza huku akitaka kutoa shuka alilo lifunika, baba yake kwa haraka akageuka na kutupa mgongo kwani haitaji kuona maungo ya ndani ya mwanae.
“Acha kuvaa tafadhali. Wewe na huyo rafiki yako saa mbili usiku hakikisheni munakuja nyumbani kwa ajili ya chakula cha usiku ninahitaji kumfahamu zaidi ya hapa”
 
“Sawa baba”
“Na wewe uongozana na mimi”
Baba Yemi alizungumza huku akimnyooshea Thomas kidole, wakatoka kwenye chumba hichi na kunifanya nishushe pumzi nyingi huku jasho likinitoka usoni mwangu.
“Samahani kw ahili lililo tokea Peter”   
“Mmmm”
“Natambua unaogo ila usihofu juu ya hili, kila jambo litakwenda jinsi ninavyo weza isitoshe kwamba baba yangu ananipenda ndio maana ameweza kunisikiliza mawazo yangu juu ya maisha, kikubwa ninahitaji uwe na amani”
“Ila baba yako ni mwanajeshi ataniua mimi”
“Hawezi kufanya hivyo, namjua baba yangu ana roho njema, niamini Peter”
Yemi alizungumza huku akiwa amenishika mashavu yangu kwa viganja vyake viwili. Taratibu akanibusu mdomoni mwangu, tukatazamana kwa ukaribu sana wa nyuso zetu kwa sekunde kadhaa kisha tukajikuta tukianza kunyonyana lipsi zetu. 
 
‘Asante Mungu kazi yangu inakwenda vizuri’
Nilizungumza huku nikikilaza kichwa cha Yemi kwenye mtu, huku tukiendelea kunyonyana mdomo yetu. Woga na wasiwasi vyote vikanipotea, sikutaka kuwa mchoyo kwa Yemi kwa kumpa kile anacho kihitaji kwa asubuhi hii. Hatukuchukua muda mwingi tukajikuta sote tukimaliza mechi hii kwa pamoja.
“Asante Peter, sijui kwa nini siku zote sikuweza kukufahamu”
“Kivipi?”
“Wewe ni mwanaume ambaye umenionyesha ni jinsi gani mwanamke anatakiwa kut na mwanaume, sikutarajia kama siku ninaweza kukutana na mkuno ambao umeweza kunioatia jina usiku na leo asubuhi.”
“Kwani..aha…..mume alikuwa akufanyii hichi ninacho kufanyia?”
“Alikuwa hajiwezi, ila tuachane na hayo mambo sipendi kuyazungumzia sana. Ila tujiandae tukapate kifungua kinywa”
“Sawa”
“Au tupike humu humu?”
“Ni wewe tu”
“Ok sawa”
Tukashuka kitandani na kuingia bafuni pamoja, tukaingia katika sinki la kuga na taratibu tukaanza kuoga huku sote tukiwa katika furaha nzuri.
 
“Peter”
“Naam”
“Wewe ni mzuri”
“Hapana mimi wa kawaida sana”
“Nakuambia ukweli wewe ni mzuri, hivi umetokea wapi hapa Nigeria?”
Swali la Yemi likanifanya ninyamaze kimya kwa sekunde kadhaa huku nikimtazama usoni mwake. Kichwani mwangu ninapangilia ni sehemu gani ambayo ninaweza kuitaja kwa haraka haraka ili aweze kunielewa.
“Kwetu sio hapa Nigeria”
Nillizungumza kwa sauti ya upole kidogo na kumfanya Yemi kukaa vizuri kwenye sinki hili huku akinitazama kwa macho malegevu.
“Umetokea wapi?”
“Familia yangu ilikuwa nchini Kenya, na ndipo nilipo zaliwa. Nimesoma huko hadi nikamaliza, nikaajiriwa kwenye shirika moja la simu linaitwa Safaricom, nikafanya fanya kazi hapo ila baada ya mama yangu kufariki basi nikaamua kuja hapa Nigeria kwa maana mama aliniambia kwamba baba yangu ni mnageria na ndipo asili yangu ilipo, basi ikanibidi kuja hapa ili kumtafuta baba yangu”
 
Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga ili kuukamilisha uongo wangu vizuri sana. Taratibu Yemi akanisogelea na kunishika mashavu yangu.
“Shii….usilie mpenzi wangu. Je ulisha wahi kumuona baba yako?”
“Hapana sikuwahi muona kabisa wala hata kuja kwangu sidhani kama ninaweza kufanikiwa kwani aliondoka Kenya tangu nipo tumboni mwa mama yangu na wala baba yangu hakuwahi kujua kwamba ameacha mtoto nchini Kenya”
Nilizungumza uongo ambao hata tukisema tuanze kazi ya kumtafuta baba yangu basi itakuwa ni kibarua kigumu kwetu.
“Ohooo pole mpenzi wangu, sasa utaweza kweli kumtafuta baba yako?”
“Sidhani kwa maana sijui hata sura yake ipo vipi”
“Je jina mama alisha wahi kukutajia labada tunaweza kumtafuta”
Yemi aliendelea kuzungumza kwa suti ya upole huku akinishika mashavuni mwangu.
 
“Aliniambia anaitwa Popoola”
“Duuu kuna majina mengi ya watu wanaitwa Popoola, ila tutajaribu kufwatilia kwenye mtandao na tunaweza kupata japo mtu hata anaye weza kuendana nawe”
“Nitashukuru sana”
Yemi akanipiga busu la mdomoni, tukamaliza kuoga na kutoka bafuni. Tukavaa nguo zetu na kuanza kuandaa kifungua kinywa. Hatukuchua muda sana tukawa tumemaliza kuanda akifungua kinywa.
“Wanamitindo wezangu watafika saa ngapi hapa?”
“Sio wezako tena”
“Kwa nini?”
“Peter naomba uelewe, japo ni haraka sana kwa hili jambo. Ninakupenda, si kwasababu nimeachana na mume wangu, la hasha. Tangu nilipo kuona kwenye mashindano nilitokea kuvutiwa na wewe, ila nilijitahidi kuuzuia moyo wangu katika kukupenda kwa maana nilitambua nina mume wangu wa ndoa na ninaheshimu ndoa yangu. Haikuwa hivyo kama nilivyo tarajia ndoa yangu iwe, naamini wewe mwenyewe umeweza kuhushudia kila kilicho tokea””
 
“Yaaa, labda ni kitu gani kimekufanya unipende?”
“Hahaaa hilo swali utanieleza badae tunywe chai kwanza kisha kama huyo jali tutaingia gym kufanya mazoezi”
“Sawa, sasa sina nguo za mazoezi?”
“Itabid kwenda kufanya manunuzi ya nguo madukani, mazoezi tunaweza kufanya hata usiku”
“Hapo sawa, japo umesahau kwamba usiku leo baba yako anatuhitaji nyumbani kwake”
“Ohoo Mungu wangu, kichwa changu kimesahau kabisa jamani, daaa nauona uzee unanikabili”
“Haha sio uzee, mawazo tu, nitajitahidi kadri ya uwezo wangu kuhakikisha kwamba mawazo hayo yanakwenda kufutika kichwani mwako”
 
“Nitashukuru sana mpenzi wang”
    Tukajiandaa na kuanza safari ya kuelekea katika maduka ya nguo, kila tunapo pita Yemi hakusita kunishika mkono, jambo lililo nifanya niwe na wasiwasi mwingi sana kwani kwa kipindi hichi mitandao ya kijamii inarusha habari kwa haraka sana na ninaelewa ni lazima Hawa atakuwa anaifwatilia oparesheni hii kwa ukaribu wa hali ya juu. Umaarufu wa Yemi unazidi kuihatarisha kazi yangu kwani kila sehemua watu walimuomba kupiga picha nasi na aliweza kuwakubali.
“Baby”
“Mmmm”
“Huwa sipendi kupiga picha mbele za watu”
“Kwa nini mume wangu”
“Bado mapema sana kwa watu kuweza kufahamu kwamba mimi na wewe tuna mahusiano”
“Peter, tafadhali mpenzi wangu, nimesha fanya maamuzi yangu mimi mwenyewe niakuomba uwe na amani wewe kwa sasa ndio mume wangu”
“Sawa nalitambua hilo ila sinto penda kuishi maisha ya umaarufu”
 
“Kweli mume wangu?”
“Ndio”
Yemi akanipiga busu la mdomo, na baadhi ya watu walio tuzunguka wakapiga picha kadhaa kwa kutumia simu zao. Tukaingia kwenye gari tulilo jia na kuondoka eneo hili.
“Kwa nini hupendi kuishi maisha ya umaarufu?”
“Kwa sababu sikuzaliwa kuwa mtu maarufu”
“Kumbuka ulikuja kwenye shindano la uwana mitindo, na utambue kwamba video yako inaendelea kutazamwa na watu wengi duniani, umesha kuwa maarufu Peter”
Yemi alizungumza huku akikunja kona, tukaingia kwenye moja ya mtaa wenye maduka mazuri ya nguo za kiume.
“Nalitambua sana ila nilifanya hivyo kwa ajili ya kujaribu tu ili kuona kama na mimi ninaweza kuwa mwanamitindo na hata kama anikipata pesa basi zitanitosheleza katika kipindi chote nitakacho kaa hapa Nigeria nikimtafuta baba yangu.”
 
“Ohooo sawa mpenzi wangu, nimekuelewa”
Yemi akasimamisha gari kwenye moja ya duka lenye midoli ya kiume iliyo valishwa suti. Tukashuka kwenye gari na kuingia ndani ya duka hili, tukanunua suti nne zinazo nitosha kisha baada ya hapa tukaanza safari ya kuelekea hotelini.
    Japo ninatambua kwamba ni maisha ya muda mfupi ya kufurahia na Yemi ila kusema kweli ninafurahi sana kwa maana Yemi ana tabia ambayo nimeikosa kwa wasichana wengi katika maisha yangu. Kila muda Yemi kwake ni furaha, ananijitahidi kadri anavyo weza kunifurahisha.
“Unatambua ni nini Peter”
“Eheee”
“Tukifika nyumbani kwa baba yangu, ninakuomba ujiamini, ule woga wako kama wa asubuhi sinto hitaji kuuona leo usiku”
“Usijali”
“Sawa ngoja nikaonane na washiriki, hapa nimeambiwa kwamba wamefika. Kama unahitaji unaweza kujumuika nami?”
“Hapana nenda kaonane nao tu”
“Poa”
Yemi akanisogelea na kunibusu mdomoni mwangu, kabla hajatoka nikampatia namba yangu ya simu kisha naye akanipatia ya kwake na akatoka chumbani humu. Nikapiga hatua hadi kwenye moja ya dirisha niksimama na kuchungulia nje. Nikatoa simu yangu na kumpigia raisi Donald Bush. Simu yake ikapokelewa ila sikusikia akizungumza zaidi ya kusikia miguno ya mapenzi. Nikataka kukata simu ila nikasubiria kidogo kusikilia.
‘Nakojoaaaaa’
Niliisikia sauti ya Hawa na kujikuta nikistuka sana, mwili ukaanza kunicheza wivu wa mapenzi ukaanza kunitawala moyoni mwangu. Hasira kali ikazidi kunipanda na swali kubwa nikajiuliza ni kwa nini raisi amemua kunisaliti.
 
“Kwa penzi hili ulilo nipa nitahakikisha kwamba mume wako nina mshughulikia”
“Hapana muache Dany peke yake, upo na mimi hakuna haja ya kumfwatilia muache aendelee na maisha yake”
“Una uhakika na unacho kizungumza?”
“Ndio, kwa picha nilizo ziona leo, Dany akiwa na Yemi zina dhihirisha kabisa wapo kwenye mapenzi matamu, nimekufungulia moyo wangu muheshimiwa raisi, ninajitahidi kukupenda”
“Nashukuru Hawa, sikufamu kama wasichana wa kiafrika muna mapenzi matamu kiasi hichi”
“Ila na wewe hakikisha mke wako unamueleza ukweli kuhusiana nasi”
“Usijali nitamueleza ukweli sawa baby”
“Mbona kama simu yako ipo hewani”
“Shitii”
Simu ikakatwa, jambo lililo nifanya nijikute nikimwagikwa na machozi usoni mwangu. Taratibu nikaizima simu yangu na kuirudisha mfukoni mwangu.
 
‘Hawa kwanini unataka kutengeneza uadui mwingine juu yangu’
Nilizungumza kimoyo moyo huku machozi yakiendelea kunimwagika, kazi ambayo imenileta huku taratibu ninaanza kuichukia kwani mwanaume niliye muamini na kumpa jukumu la kumlinda mke wangu leo hii yupo chumbani na mwanamke wangu.
Mlango ukafunguliwa, kwa haraka nikafuta machozi yangu huku nikiwa ninatizama dirishani, nikageuka nyuma na kumkuta Yemi akiwa amesimama huku tabasamu pana limemjaa usoni mwake.
“Vipi mbona umerudi?”   
“Ahaa nimewapa maelekezo nimeona nije nitulie na wewe mpenzi wangu, vipi mbona kama unaonekana haupo sawa?”
“Kichwa kidogo kinaniuma”
“Ohoo pole sana”
Taratibu nikajikuta nikimsogelea Yemi na kumkumbatia kwa nguvu, machozi nikashindwa kuyazuia na kujikuta nikiangua kilio kikali sana hadi Yemi akabaki akishangaa ikambidi aanze kazi ya kunibembelea huku akiniuliza maswali ya kutaka kufahamu ni kutu gani kinacho endelea  kwangu.

AISIIIII……….U KILL ME 139
 
“Peter tafadhali ninaomba uniambie ni kitu gani kinacho kuliza mpenzi wangu?”
 
Yemi Okocha aliendelea kuniuliza kwa sauti ya upole na iliyo jaa unyonge ndani yake.
“Namkumbuka sana mama yangu”
Ilinibidi kuzungumza uongo.
“Shiii usilie mume wangu, kwa sasa nitakuwa mama, baba kwako nitakujali kwa kila jambo katika maisha yangu sawa”
“Nimekuelewa mke wangu ninashukuru sana”
“Vipi tutakula mchana?”
“Hapana nipo vizuri”
Taratibu tukaka kwenye sofa, Yemi akaniomba nilaze kichwa changu kwenye miguu yake na nikafanya hivyo.
“Mama yangu alikuwa ni mwanamke mpambanaji sana, kwenye maisha yake hakuhitaji kumtegemea mwanaume. Alijitahidi kuhakikisha kwamba ninapata elimu bora ili ije kunisaidie mbeleni”
Nilizungumza kwa sauti ya upole huku nikimtazama Yemi usoni mwake, na viganja vya mikono yake vinakazi ya kukatiza katiza katika mwili wangu.
 
“Mama alisumbuliwa na nini hadi akafariki?”
“Saratani”
“Daaa pole sana”
“Nashukuru, nilijaribu kumpeleka katika kila hospitali kubwa nchini Kenya ila ilishindikana na Mungu aliweza kumchukua”
Nilizungumza huku machozi yakinilenga lenga tena ili kuzidi kumpumbaza  Yemi Okocha.
“Kikubwa ni kumshukuru Mungu mpenzi wangu sawa baba”
“Sawa”
    Tukaanza kujiandaa kwa ajili ya kueleka katika nyumbani kwa baba Yemi. Nikavaa moja ya suti ambayo nimetokea kuipenda sana.
“Mke wangu kesho unikumbushe kuelekea katika hoteli niliyo toka nikachukue begi langu la nguo”
“Sawa hakuna tabu katika hilo”   
Imetulazimu kuondoka mapema kutokana na foleni kubwa iliyopo hapa katika jiji la Lagos Nigeria. Ikatuchukua saa moja na nusu kufika katika jumba kubwa la kifhari la baba Yemi. Nyumba hii inalindwa na wanajeshi wenye silaha kubwa zenye uwezo mkubwa katika upambanaji.
“Mkewangu tafahali usishuke kwanza kwenye gari”   
“Kwa nini?”
“Mbona kuna wanajeshi wengi hivi?”
“Baba yangu ni kamanda mkuu wa jeshi, ni lazima nyumbani kwake walinde wanajeshi”
 
“Huoni kama inaweza kuniletea shida kwangu kama anakuwa amejazwa sumu na mume wako uliye achana naye?”
“Baba yangu ni muelewa mkubwa sana na anapenda kunipa uhuru kwa kila jambo ambalo ninalotaka kulifanya kwa hiyo katika hili wala usiwe na wasiwasi mume wangu sawa?”
“Sawa”
Nikashusha pumzi nyingi huku nikishuka kwenye gari, tukapokelewa na wafanyakazi wawili wa kike na moja kwa moja tukaeelekea ndani. Tukaingia kwenye seble moja kubwa sana ambayo ukubwa wake kwa nchi yetu ya Tanzania unaweza kujenga nyumba hata ya vyumba vinne vya kulala.
“Waooo karibu mwanangu”
Baba Yemi alizungumza huku akinyoosha mikono yake na kumkumbatia mwanaye. Wakazungumza kilugha ambacho sikuweza kukielewa. Yemi akanigeukia na kunishika mkono wangu.
 
“Baba huyu anaitwa Peter ni mume wangu mtarajiwa”
“Peter huyu ni baba yangu Mzee Okocha”
“Nashukuru kukufahamu”
Mzee Okocha akanipatia mkono huku  akiutingisha na kunitazama usoni mwangu kwa macho makali ila anatabasamu. Tukakaribishwa kwenye meza ambayo imejaa vyakula vingi  vya kila aina huku kukiwa na majagi makubwa ya juisi. Wafanyakazi walio simama pembeni ya hii juisi nilisihi kwamba wanaweza kukaa nasi kwenye hii meza kubwa wajumuike kula nasi, ila hadi ninaanza kula sikuona hata mmfanyakazi mmoja akigusa kijiko kwa ajili ya chakula.
“Mwanangu laiti kwamba Peter asinge kuwa kijana mwenye muonekano basi ningekukatalia katu katu kuwa naye kimahusiano”
“Hahahaa, kwahiyo baba unapenda kijana mwenye muonekano mzuri?”
 
“Ndio, kwani mimi mbaya. Hata siku ambayo nilimpata mama yako nilikuwa nimevalia vizuri, sikupata shida ya kuzungumza maneno mengi, nilijikuta namchukua kiulaini sana”
Maneno ya Mzee Okocha yakatufanya tucheke sana kwani mbwembwe zake ni sawa sawa na marehemu baba yangu kwani nakumbua kwamba alisha wahi kuniadisia kwamba alimpata mama yangu kutokana na uzuri wake.
“Ila mama alikuwa mzuri sana”
“Ahaahaa ndio maana nikawa naye, wewe ulitaka awe mbaya ili nipate mtoto mbaya. Tazama wewe jinsi unavyo vutia naamini hata Peter umemependa mwanagu?”
“Ndio mzee”
Nilizungumza huku nikitabasamu, ila moyoni mwangu nina wasiwasi na woga mkubwa.
“Hicho ndicho nilicho kihitaji kutoka kwako Peter. Yule mshenzi Thomasi amekuja kunitoa hapa asubuhi asubuhi amenionyesha sikio lake nusu, nikakua kweli bwana kumbe ni mshenzi sana”
 
“Yaani baba laiti kama uneng’ang’ania niendelee kuwa na Thomas, basi muda kama huu ungekuwa umesha ipata maiti yake”
“Hahahaaa nililiona hilo mapema”
Mazungumzo ya Yemi na baba yake, kwa mtu mwenye uelewa wa hali ya juu, nilazima utahisi kuna jambo linalo endelea chini ya hii familia.
“Peter baada ya hapa ninahitaji kuzungumza na wewe maneno mawili matatu nje huko”
“Jamani baba munataka kuwa ninyi peke yenu?”
“Ahaaa kuna mambo mengine ninatakiwa kuzungumza na mkwe wangu peke yetu”
“Sawa”
Tukamaliza kula, mimi na mzee Okocha tukaanza kutembea kutoka katika hii nyumba. Tukatokea kwenye moja ya bustani kubwa na pembezoni kuna bwawa moja kubwa.
“Ahaa Peter wewe umetokea wapi?”
“Nimetokea Kenya mzee”
 
“Sawa sawa, unataka kuniambia kwamab wewe ni mkenya?”
“Ndio ila kwa historia ya mama yangu aliniambia kwamba uhalisia wangu ni hapa Nigeria kwa maana baba yangu alikuwa ni mnigeria”
“Ahaaa sawa sawa, sasa baba yako umeweza kuonana naye?”
“Hapana mama aliniambia kipindi baba anaondoka Kenya, alimuacha akiwa na mimba ya mwezi mmoja na baba wala hakuweza kulitambua hilo. Na kila alipo msubiria aweze kurejea baba hakurejea, hadi nikazaliwa na kuwa mtu mzima kabisa”
“Na mama yupo wapi?”
“Kwa sasa mama amesha fariki”
“Daaa pole sana, unajua kipindi ambacho mke wangu alifariki na kuniacha na Yemi, kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwa maana tulipendana sana na mama yake”
Mzee Okocha kwa jinsi anavyo zungumza unaweza ukamdhania kwamba ni mtu mwema sana asiye na tabu na mtu ila kwa historia ambayo niliipata yeye na kundi lake basi ni mtu mmoja gaidi sana.
“Thomas aliniambia uwezo wako wa kupambana je ni kweli?”
“Kivipi baba”
“Aliniambia kwamba unajua kurusha ngumi, mateke. Unajua jinsi ya kumzuia adui je ni kweli?”
“Kidogo japo sio sana”
“Sio sana!!?”
Mzee Okocha alizungumza huku akinitazama vizuri usoni mwangu.
 
“Ndio baba”
“Nitahitaji unionyeshe uwezo wako”
“Baba sio sana”
“Huo huo wa sio sana ndio nitahitaji unionyeshe kwa maana nahitaji kukujua wewe vizuri. Kwa maana binti yangu ni mzuri sana, anahitaji kupata mwanaume atakaye mlinda na kumpenda. Endapo mwanangu atakufa mikononi mwako basi nitahakikisha kwamba na wewe ninakuua. Na binti yangu akimuumiza na mimi nitahakikisha ninakuumiza.”
Mzee Okocha alizungumza kwa sauti nzito aliyo zungumza nayo asubuhi, nikabaki nikiwa nimemkazia macho.
“Sawa baba nimekuelewa”
“Na kitu kingine kuna mitihani yangu mitano nitakupatia ukifanikiwa kuipta hiyo basi utaishi na mwanangu na nitawapa kila kitu changu, ila ukishindwa basi nitakuua kimya kimya pasipo mtu yoyote kufahamu, umenipata Peter?”
 
“Ndio nimekupata mzee”
Tukafika kwenye moja ya kiwanja cha mpira wa mikono, mzee Okocha akaka kwenye moja ya kiti, nikataka kukaa akanizuia kwa ishara huku akinitazama usoni mwangu.
“Nahitaji kuuona uwezo wako wa kupigana”
“Ahaa mzee hapa mbona tupo sisi wawili tu nitapigana na nani?”
“Unaweza kupigana na upepo”
“Upepo!!?”
Niliuliza huku nikiwa nimeshangaa, bado nusu tu nimtukane mzee huyu kwani ninamuona ni mwenda wazimu japo nimetumwa kumpeleleza, nimeamua kuikatisha kazi hiyo kutokana na usaliti wa Hawa na raisi Donald Bush.
“Ndio”
Nikasimama huku nikimtazama mzee Okocha vizuri usoni mwake. Nikahisi hatua za mtu akija nyuma yangu kwa haraka nikageuka na kukutana na mwanajeshi mmoja mwembamba na ana urefu kama wangu.
 
“Huyo anaitwa upepo sasa unaweza kupambana naye”
Hapa ndio nikapata maana ya mzee huyu kuzungumza kwamba nitapambana na upepo, taratibu nikavua koti langu la suti pamoja na saa yangu ya kononi, nikaviweka kwenye moja ya kiti kisha nikamgeukia huyu mwanajeshi. Nikamtazama Mzee Okocha, akanikonyeza, nikstukia teke zito la kifua lililo niangusha chini mzima mzima, mwajashi huyu akaanza kunishambulia kwa kasi sana, uwezo wake unaweza kusema ni kama mchina aliye fuzu mafunzo ya kung fu.
Kila nilipo jaribu kujipanga, upepo aliweza kupangua mipango yangu. Sikuweza kurusha ngumi wala teke hata moja, sikuwa na ujanja zaidi ya kuanza kumsoma huyu upepo kuanzia urushaji wake wa mateke hadi ngumi. Kitu nilicho kigundua kwamba mikono yake ndio ina kasi sana kuliko miguu. 
 
“Kwa mtindo huo siwezi kukuachia mwanangu, mwanaume gani wewe”
Mzee Okocha alizungumza maneno ya kejeli huku akinitazama jinsi ninavyo jizoa zoa kunyanyuka chini nilipo anguka, shati langu lote jeuepe limeshafuka kwa fumbi la hichi kiwanja.
    Nikasimama kimtego upepo akajaribu kunikabili kwa mateke ya kuruka hewani, ila nikamkwepa na kumsindikiza kwa teke la mgongo lililo mfanya aanguke kifudifudi kama mzigo, upepo akanyanyuka kwa kasi, pasipo kufikiria kwamba nimemgundua siri ya upiganaji wake, akaanza kunishambulia kama mwanzo. Laiti kama kungekuwa na mashabiki pembeni wanao nishabikia basi wangeweza kunishabikia kwa nderemo na vifijo.
 
Huku si kupiga bali ni kumbuta mwanajeshi huyu anaye itwa upepo, kila alivyo jaribu kurusha ngumi, mimi nilicho kifany ni kuudaka mkono wake na kuhakikisha kwamba ninavunja japo kidole kimoja, upepe alijitahidi kujikaza kuonyesha ukakamavu mbele ya bosi wake ila mbinu na mipango yake yote nilisha itunza kwenye akili yangu.
 
“Khaaghaaaaaa……..”
Upepo alitoa ukelele mkali baada ya kumvuja mkono wake wa kulia hadi mfupa ukatoka nje, nikakamsukuma pembeni upepo na kumfanya mzee Okocha kubaki akiwa ameduwaa, kuona kijana wake anavyo garagara chini. Nikaanza kutembea kwa kujiamini hadi kwenye kiti alicho kalia mzee Okocha, huku nikiwa nimejawa na hasira kali. Nikameza funda zito la mate, taratibu mzee Okocha akasimama huku akiwa ameikunja sura yake.
 
“Usinijaribu tena na vijana wako nitawaua”
Baada ya kumaliza kuzungumza maneno hayo, nikabeba koti langu begani, kisha nikaichukua saa yangu na taratibu nikaanza kuondoka hili eneo, nikasikia mlio mdogo wa bastola inayo kokiwa, taratibu nikageuka na kumkuta mzee Okocha akiwa ameninyooshea bastola yake huku sura yake ikizidi kutisha kwa kukasirika.
“Wewe ni nani na unataka nini kwangu”
Mzee Okocha alizungumza kwa sauti nzito ambayo hainitishi kabisa, kwani nikiwa katika hasira huwa ninajiamini kuliko muda wowote ambao ninakuwa tofauti. Taratibu nikaanza kumsogelea mzee Okocha huku akilini mwangu nikitaka kumueleza ukweli kwamba mimi ni Dany na nipo hapa kuhakikisha kwamba ninamkamata yeye na kundi lake lote la boko haramu.
                                                                                     ITAENDELEA
“Je Dany atazungumza ukweli wa yeye ni nani, basi usikose sehemu inayo fwata ya kisa hichi cha kusisimu”

Video Mpya: Barakah The Prince - Mawazo

0
0
Msanii Barakah The Prince anakukaribusha kutazama video ya wimbo wake mpya uitwao Mawazo.  Itazame hapa.

Wimbo Mpya wa Bright X Nini – Kuna Nini

0
0
Wimbo Mpya wa  Bright X Nini – Kuna Nini. Utazame hapa

Wimbo Mpya: Prince - SAWA

0
0
Wimbo Mpya: Prince - SAWA . Utazame hapa

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne Ya November 6

Msemaji Mkuu wa Serikali: Serikali Imefanya Mambo Makubwa Sana Ndani ya Miaka Hii Mitatu

0
0
Na. Immaculate Makilika – MAELEZO
Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, imefanya jitihada kadhaa ikiwa ni sambamba na kutekeleza  sera mbalimbali ambazo zimeiwezesha nchi ya Tanzania kupata mafaniko makubwa ndani na nje ya nchi katika kipindi  cha miaka mitatu

Akizungumza  jana jijini Dar es salaam, Mkurugenzi wa Idara ya Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi, ametaja mambo 10 muhimu  yaliyofanywa na  Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika kipindi cha miaka mitatu na ambayo yameitangaza nchi ya Tanzania kimataifa.

Dkt. Abbasi alitaja mambo hayo kuwa ni uchumi unaoendelea kukua kwa kasi nzuri, ambapo  katika mwaka 2017/18 uchumi wa Tanzania ulikua kwa wastani wa asilimia 7.1 na kuongoza katika nchi zote za Afrika Mashariki, huku  ukiingia katika rekodi ya kuwa miongoni mwa nchi ambazo uchumi wake unakua kwa kasi zaidi duniani kama ambavyo  ripoti mbalimbali za kimataifa zimeeleza.

“Uchumi wetu ni wa tisa kwa ukuaji wa kasi duniani na katika Afrika, Kusini mwa Sahara ni wanne, hiyo ni kwa mujibu wa ripoti ya World Economic Forum ya mwezi  Machi, 2018 na kwa nchi za Afrika Mashariki  uchumi wa Tanzania unaongoza kwa ukuaji” alisema Dkt. Abbasi

Kuongezeka kwa mapato ya Serikali katika kipindi cha miaka mitatu, Rais Magufuli amethubutu kuziba mianya ya upotevu wa mapato na kuongeza kasi ya kukusanya kodi na hivyo kuongeza mapato ya kodi ya Serikali kutoka wastani wa shilingi  bilioni 850 kwa mwezi hadi kufikia wastani wa  shilingi trilioni 1.3 kwa mwezi.

Kufufuliwa kwa mashirika ya umma, Dkt. Abbasi alisema kuwa kutokana na ufuatiliaji, ubunifu, uwekezaji wa Serikali ya Rais Magufuli, mashirika mengi  mfano  Shirika la Mawasiliano Tanzania(TTCL), Shirika la Reli Tanzania (TRC) na Mamkala ya Maji Safi (DAWASA) na Bandari  sasa yameanza kuamka kuwa na ufanisi, kuongeza mapato na mengine kutengeneza faida.

“Baadaa ya Serikali kuchagiza mageuzi ya kiutendaji sasa  kwa mwaka TTCL  inakusanya shilingi bilioni 212 kutoka shilingi bilioni 102, Bandari imekusanya kutoka shilingi bilioni 703 hadi kufikia shilingi bilioni 838 kwa mwaka, TRC kutoka shilingi bilioni 23 hadi 36 kwa mwaka  na DAWASA shilingi bilioni 32.4 hadi shilingi bilioni 122.4 kwa mwaka “ alisema Dkt. Abbasi

Aidha, Dkt. Abbasi alisema kuwa katika kipindi hiki cha miaka mitatu Serikali ya Rais Magufuli imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika sekta ya  viwanda ambapo jumla ya  viwanda 3,306 viliandikishwa, na vingine vinaendelea kujengwa na baadhi vimekamilika. Halikadhalika viwanda hivyo vimeanza kutengeneza  bidhaa mbalimbali ambapo kati ya hivyo viwanda 251 ni vikubwa na vya kati ni 173.

Ambapo mchango wa ekta ya viwanda katika pato la Taifa umeongezeka kutoka asilimia 5.2 mwaka 2015 hadi 5.5 mwaka 2017. Kasi ya ukuaji wa Sekta ya Viwanda ilikua kutoka asilimia 6.5 mwaka 2015 hadi asilimia 7.1 mwaka 2017/18.

Akiendelea kufafanua mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Tano Dkt. Abbasi alisema kuwa Rais Magufuli amepambana na rushwa na ufisadi kwa pamoja na mambo mengine, sambamba na  kutimiza ahadi yake ya kuunda Makosa ya Uhujumu Uchumi maarufu kama Mahakama ya Mafisadi

“Mpaka sasa kesi mpya 41 zimefunguliwa, na  kuna maombi ya dhamana 346 yamewasilishwa katika Mahakama hii kati ya mwaka  2017 na 2018” alisema Msemaji huyo wa Serikali.

Katika sekta ya usafirishaji nako, Serikali ya Rais Magufuli imefanya mageuzi kadhaa, yaliyopelekea sekta hiyo kupata mafaniko  ya kuwa  na  ndege nne mpya zinazoendelea kuleta mageuzi katika usafiri wa anga nchini, abiria wanaotumia ndege za ATCL wameongezeka kutoka takribani abiria 4,000 kwa mwezi hadi abiria 30,000 kwa mwezi.

Aliongeza kuwa  ndege mbili   aina ya Air Bus zenye uwezo wa kubeba abiria watu 132 zitawasili nchini Disemba mwaka huu, na ndege aina ya  Boeing dreamliner ya pili inatarajiwa kuwasili nchini Oktoba mwaka mwakani.

Aidha, mradi wa umeme wa Stigler’s gorge utakapokamiika unatarajiwa kuzalisha  megawati 2,100, sambamba na mradi wa ujenzi wa reli kwa kiwango cha standarg gauge kutoka Dar es salaam hadi Morogoro na baade Dodoma, ambapo umefikia 33% ya ujenzi.

Mafaniko mengine ya Serikali hii yanaonekana katika katika sekta ya afya,  ikiwemo kujenga vituo vya Afya vya Kata 210 na kukarabati vingine vingi kufikisha idadi ya vituo vinavyotoa huduma hadi mwaka huu kuwa 7,746 kutoka vituo 7,014 mwaka 2014/15 sawa na ongezeko la asilimia 10.4.

 Dkt. Abbasi  alifafanua kuwa vituo hivi pia vina wodi za kina mama na vifaa vya kisasa. Aidha, ajira zaidi ya 6,000 za kada ya afya zimetolewa. Katika miaka mitatu Zahanati zimeongezeka kutoka 6,143 mwaka 2015 hadi 6,646 mwaka huu ikiwa ni sawa na  ongezeko la zahanati 503  ambapo baadhi zilijengwa na zingine kukarabatiwa sawa na ongezeko la asilimia 8.1.

Vilevile, Serikali ya Awamu ya Tano imefanya mageuzi ya kiutendaji ikiwemo kuongeza Bajeti ya Dawa na Vifaa Tiba kutoka shilingi bilioni 31 mwaka 2015 hadi kufikia shilingi bilioni 270  kwa mwaka huu wa fedha.

Ongezeko hilo limewezesha upatikanaji wa dawa muhimu katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini kufikia asilimia 89.6 kutoka asilimia 36 mwaka 2015/16. Aidha upatikanaji wa dawa muhimu umepanda kutoka wastani wa asilimia 35 tu hadi asilimia 93.

Sekta ya madini nayo, Dkt. Abbasi alisema kuwa “Serikali iliweka lengo la kukusanya shilingi bilioni 1.5 kwa mwaka kutoka kwa wachimbaji wadogo wa Tanzanite pale Mirerani. Hata hivyo kabla hata ya nusu ya mwaka huu wa bajeti kufika, tayari mapato eneo la Tanzanite yamefikia shilingi milioni 788.5 sawa na asilimia 52 ya lengo la mwaka 2018/19, hii inashadidisha kuwa uamuzi wa Mhe. Rais kujenga ukuta ulikuwa makini” alisema Dkt. Abbasi

Katika miaka hii mitatu licha ya matukio ya hapa na pale, Tanzania imeendelea, kusimama kama moja ya visiwa vya amani duniani na  Taifa limeendelee kushikamana kawa kuishi kwa amani na upendo.

Aidha, Dkt, Abbasi  alisema kuwa Rais Magufuli anasimamia misingi na Watanzania leo wako huru  kuamua mambo yao kama Taifa, huku akisisitiza  kuwa safari ya kujitegemea imeanza  na mataifa mbalimbali duniani  yanafahamu   azma ya Rais Magufuli kwa Taifa lake.

Habari Njema Kwa Wenye Matatizo Ya Nguvu za Kiume, vitambi, nyama uzembe

0
0
(1).Fikiria ulianzia wapi? Je,ulifanikiwa au bado?

(2).Upo tayari kupona kwa haraka?

TIBA ZITOLEWAZO NI,

NGORO 4 POWER; Huongeza nguvu za kiume yenye mfumo wa unga na vidonge dozi siku(6).

MELAMELA; Hurefusha na kunenepesha uume ipo katika mfumo wa unga dozi siku (4).

KASELA; Hurudisha mke,mme,mchumba na hawara ndani ya siku mbili tu,atatimiza mahitaji yote hata Kama yupo mbali na kumfunga asiwe na mtu mwingine.

IKUMBUJA; Humfanya mtu  kupandishwa cheo kazini na kulipwa madeni au mafao yako pia na kumaliza kesi kabisa.

DUDUMA; Huongeza hips,makalio na mguu wa bia.

SWASWA: Hupunguza maziwa makubwa, kitambi, nyama uzembe, michirizi na muwasho sehem za Siri,na harufu mdomoni.

KOOLA;Hutibu magonjwa sugu ya zinaa, tumbo kujaa gesi,kuuma chini ya kitovu, kiuno ,fangasi za miguu, na kuvimba miguu au miguu kuwaka Moto.

Kwa hayo na mengineyo mfatilie DR.HINDU kwani ana uwezo wa kuhudumia ndani na nje ya TANZANIA.Kwa Dar es salaam anapatikana BUGURUNI MALAPA pia KAHAMA anapatikana MARUNGA.

Kwa wasio na mda wa kufika ofisini kwangu Nina vijana wa kukuletea mpaka ulipo kazini ama nyumbani kwako.

OFISI ZINAFUNGULIWA SAA 07 :00 ASUBUHI.

CONTACTS 0744 922 982(WhatsApp), 0716608959.

  "WOTE MNAKARIBISHWA".DR   HINDU NI SULUHISHO LAKO.

LIVE | Mkutano wa 13 wa BUNGE Jijini Dodoma

0
0
LIVE | Mkutano wa 13 wa BUNGE Jijini Dodoma. Tazama hapo chini

Abdul Nondo: Nitaendelea Kupambana

0
0
Baada ya kuachiwa huru   na Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa, aliyekuwa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo, ameeleza magumu aliyopitia wakati akitetea wanafunzi huku akiwa anaendelea na kesi yake ya kudaiwa kujiteka.

Hukumu hiyo ya kesi ya jinai namba 13 ya mwaka 2018 ilitolewa jana na  Hakimu Mfawidhi, Liad Chemshana wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa.

Katika kesi hiyo  ilidaiwa kwamba Machi 7 mwaka huu akiwa Ubungo Dar es Salaam, Nondo  alichapisha taarifa hizo akitumia simu ya kiganjani yenye No. 0659366125 kinyume cha Sheria ya Makosa ya Mtandao na kusambaza katika mitandao ya jamii.

Akizungumza nje ya mahakama  baada ya hukumu hiyo, Nondo  alisema katika kipindi chote wakati anatetea haki za wanafunzi   na kuendelea na kesi dhidi yake, alipita kwenye nyakati nzito katika  maisha yake ila anamshukuru Mungu kwa vile  Mahakama imetenda haki.

Alisema pamoja na hali hiyo, kamwe hatorudi nyuma katika mapambano ya kutetea haki za wanafunzi nchini kwa kupaza sauti   mambo yanapopindishwa.

“Katika  kipindi  chote  ambacho  nilikuwa napitia mapito  haya  mazito  iwapo  ningekuwa sina  msimamo ningekuwa  nimerudi  nyuma na kukata  tamaa kukubali  kila  nilichoshinikizwa  niseme  niweze kuachiwa.

“…  lakini  sikuwa  tayari kwa hilo nilimtanguliza Mungu  ambaye leo (jana),  ameweza  kunipigania, namshukuru Mungu na Mahakama kwa kutenda haki.

“Pia naushukuru Mtandao wa  Watetezi wa  Haki za Binadamu (THRDC),  muda wote wamekuwa nami, asanteni sana mawakili wangu, asanteni Watanzania wote sitorudi nyuma kuwa mtetezi wa wanyonge,” alisema Nondo.

Alisema amepita  katika mapito mazito kwa ajili ya kupigania  haki za  wanafunzi na kamwe hataacha kuendeleza harakati za kupigania haki zao.

“Mungu ni mwema ametenda mema juu yangu na sitarudi nyuma, nawaombeni niwashukuru pia waandishi wa habari  nchini hasa Iringa ambao muda wote mlifika kufuatilia  kesi  yangu naomba leo (jana)  niishie hapa.

“Nitasema zaidi ila leo (jana) sipo vizuri nina furaha kubwa,” alisema Nondo huku akibubujikwa machozi

Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC), Onesmo ole Ngurumwa, alisema  Mahakama imeweza kutenda haki na uamuzi uliotolewa na mahakama hauna hata chembe moja ya upendeleo .

Katika  kasi hiyo, Nondo alikuwa  akitetewa na mawakili   wawili, Chance Luoga na Jebra Kambole  ambao walieleza imani kubwa  kwa mahakama kupitia hukumu hiyo.

Wakili Kambole alisema kuna uonevu mkubwa ambao  polisi walionyesha kumtendea mteja wao ambao mahakama  pia  imeuona.

Hukumu  hiyo  ilichukua    saa moja  kusomwa  huku  askari  wa  Kikosi cha  Kutuliza  Ghasia  (FFU)  wakiwa  wametanda nje ya mahakama  hiyo.

Jipatie Dawa ya Asili ya Kupunguza Maziwa, Kupunguza Tumbo,Kuongeza Unene, Kuongeza Maumbile ya Kiume na Kuondoa Chunusi

0
0
Bidhaa za NATURAL BEAUTY PROD ni bidhaa zilizothibitishwa kiafya na kupewa kibali original cha kuuzwa hadharani.

Bidhaa hizi zimetengenezwa kwa mimea na matunda hazina chemical wala madhara yoyote kwa mtumiaji
1. SHARK POWER--Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza uume urefu na upana mpaka nchi 7.5 inapatikana kwa @170,000/=
2. VIGA 84000---Hii dawa ya kuspray yenye uwezo mkubwa wa kuchelewesha wakati wa tendo la ndoa @160,000/=
3. HANDSOME UP ORIGINAL-- Hichi ni kifaa cha kuongeza maumbile kwa size uipendayo pamoja na kuimalisha misuli kifaa hichi kinapatikana kwa @230,000/=
4. MAXMAN CAPSULE--- Hii ni dawa ya vidonge ya kuongeza uume urefu na upana pamoja na kuongeza nguvu za kiume kwa wiki mbili tu bei yake ni @200,000/=
5. VIG RX---- Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza uume urefu na upana mpaka nchi 10 inapatikana kwa @190,000/=
6. BODY BOOSTER---Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri @150,000/=
7. BOTCHO MULT PLUS-- Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza (hips mapaja na makalio) kwa size uipendayo unaipata kwa @200,000/=
8. WHITE COLLECTION---- Ni vidonge vya kuwa mweupe mwili mzima pamoja na kuwa soft @150,000/=  N.K

 Wasiliana nasi kwa simu
NO:. +255 759029968
                      AU
           +255 659618585
Popote ulipo utapata huduma zetu.
Pia hakikisha unapatiwa risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ununuapo bidhaa kampuni hii.  
          WELCOME ALL

Wabunge wa CHADEMA, CUF Wasusia Viapo vya Wabunge wapya wa CCM

0
0
Wabunge wa Chadema na wa CUF upande wa katibu mkuu Maalim Seif wamesusia kushuhudia kiapo cha wabunge wanne wa CCM wakati wabunge hao walipokuwa wanaapishwa.

Mkutano wa Bunge umeanza leo asubuhi Jumanne Novemba 6, 2018 na kuongozwa na Spika Job Ndugai.

Mara baada ya kumaliza dua na wimbo wa Taifa, uliwadia wasaa wa kiapo kwa wabunge wanne waliokuwa upinzani ambao walijiuzulu na kuhamia CCM ambako waliibuka washindi.

Wakati wa shughuli hiyo ya kiapo, wabunge hao wa Chadema na CUF upande wa Maalim Seif hawakuwapo bungeni.

Aliyekuwa wa kwanza kuapishwa ni Julius Kalanga (Monduli), akafuatia Mwita Waitara (Ukonga), akaja Timotheo Mzava (Korogwe vijijini) aliyepita bila kupingwa akichukua nafasi ya marehemu Stephen Ngonyani ‘Majimarefu’ aliyefariki dunia.

Wa mwisho kuapishwa alikuwa Zuberi Kuchauka (Liwale) ambaye awali alikuwa mbunge kupitia CUF. Mara baada ya kumaliza kuapishwa, wabunge hao wa Chadema na CUF walirejea bungeni.

Alikiba Ajibu 'Kiaina' Mwaliko wa Diamond Wasafi Festival

0
0
Jana Novemba 5,  Diamond Platnumz alitangaza kuwa anatamani sana kumuona msanii mwenzake pia akiwa kama kaka yake kwenye muziki Alikiba awepo kwenye tamasha lake la Wasafi Festival .

Lakini baada ya Diamond kuongea hayo watu walianza kuzungumza mitandaoni na kuanza kusema Alikiba hawezi kukubali huku wengine wakisema Alikiba akubali tu, na hadi kufikia wengine kusema Alikiba atatoa jibu lake baya au la kizarau sana.

Sasa bila shaka taarifa hizo zimemfikia Alikiba ambapo muimbaji huyo ame-post picha ya mchekeshaji Mr. Bean ikiwa na maneno yanayosomeka; 'Thank you for listening, To my presentation', halafu chini ya post hiyo akaandika“Your welcome”

Mashabiki wengi wamechukulia kwamba hilo ndio jibu la Alikiba kwa Diamond kuhusu suala la yeye kushiriki Wasafi Festival ambayo itaanza November 24, 2018 mkoani Mtwara kisha kwenda Iringa na Morogoro.

TFF Yatangaza Tarehe Ya Uchaguzi Yanga

0
0
Kamati  ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imetangaza rasmi kuanza kwa mchakato wa uchaguzi wa klabu ya Yanga unaotarajia kufanyika Januari 13, mwakani.

Kumekuwa na mvutano tangu klabu hiyo kutakiwa kuitisha uchaguzi wa kuziba nafasi zilizoachwa wazi, huku baadhi ya wanachama wakitaka aliyekuwa Mwenyekiti wao Yusuf Manji arejee lakini hakuonyesha ushirikiano.

Hivi karibuni viongozi wa Yanga walikutana na Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo, Dkt Harrison Mwakyembe kujadili suala la uchaguzi  na baadae  Baraza la Michezo la Taifa, lilikuja na uamuzi wa kuitaka TFF isimamie klabu hiyo ifanye uchaguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ya TFF, Malangwe  Mchungahela, alisema  Yanga watafanya uchaguzi wa kujaza nafasi zilizoachwa ikiwamo ya mwenyekiti , makamu mwenyekiti na  wajumbe wake wa Kamati ya Utendaji.

Mchungahela alisema mchakato wa uchaguzi huo tayari umeanza na utasimamiwa na kamati hiyo, pamoja na kamati ya uchaguzi ya Yanga.

Alitaja utaratibu wa mchakato huo kuwa Novemba 5-7, mwaka huu, kutangaza mchakato wa uchaguzi, Novemba 8-13 wagombea wataanza kuchukua fomu, Novemba 14-17 ni  kikao cha mchujo wa awali.

Tarehe 18-20 ya mwezi huo, kuchapisha na kubandika orodha ya awali ya wagombea katika ubao wa matangazo, Novemba 21-24, kipindi cha kupokea na kuweka mapingamizi.

Alieleza kuwa Novemba 24-27 kupitia pingamizi zote na kufanya usaili wa wagombea, tarehe 28-30 kutangaza na kubandika matokeo ya awali ya usaili.

“Tarehe 1-4 Desemba sekretarieti ya TFF, kuwasilisha masuala ya maadili  katika kamati ya maadili ya TFF, Desemba 5-10 kipindi cha kupokea na kutolea maamuzi ya  kamati ya maadili, ” alisema.

Alifafanua kuwa mchakato huo utaendelea kwa kufuata hatua kwa hatua hadi Januari 6, mwakani kampeni zitakapoanza mpaka tarehe 13 ya uchaguzi.

“Mambo yote hayo yatasimamiwa na kamati ya uchaguzi ya TFF kwa kufuata Katiba kwa kuwa Yanga ni mwanachama wa TFF,” alisema Mchungahela.

Ajali Mbaya ya Gari Yaua Watu 6 Pwani

0
0
Na Mwamvua Mwinyi, Bagamoyo
Watu sita akiwemo mtoto mchanga wa jinsia ya kike wamefariki dunia na wengine saba kujeruhiwa katika ajali iliyotokea kijiji cha Msata, barabara kuu ya Segera/Chalinze mkoani Pwani. 

Akithibitisha, kamanda wa polisi mkoani Pwani Naibu Kamishna wa Polisi ACP Wankyo Nyigesa alisema kwamba ajali hiyo imetokea Novemba 5, 2018 majira ya saa moja usiku baada ya gari namba T. 124 DHW aina ya Toyota coaster ikitokea Mkata kwenda Mbezi -Dar es salaam kuligonga kwa nyuma lori namba KBV 746C/ZE2861 FAW iliyokuwa imeegeshwa barabarani kutokana na kuharibika.

Amesema dereva wa Toyota coaster iliyosababisha ajali ambae hajafahamika jina lake alikimbia baada ya kutokea ajali.

ACP Wankyo alieleza kuwa waliopoteza maisha ni wanaume watano wenye umri kati ya miaka 30-40 ambao majina yao bado kufahamika. Alisema ,watu saba walipata majeraha kwenye maeneo mbalimbali ya mwili yao .

"Waliopata majeraha ni pamoja na wanaume wanne na wanawake watatu ambao wote wamepelekwa zahanati ya jeshi Kihangaiko -RTS na kituo cha afya Lugoba kwa matibabu zaidi "alisema Wankyo, akiongeza kuwa  miili ya marehemu imehifadhiwa hospital ya wilaya ya Bagamoyo kwa uchunguzi wa daktari.

 Alitaja chanzo cha ajali, ni uzembe wa dereva wa gari namba T. 124 DHW aina ya Toyota coaster kujaribu kulipita bila tahadhari gari jingine lililokuwa limeegeshwa baada ya kuharibika na wanaendelea kumsaka.

Kamanda huyo alitoa rai kwa madereva kutii sheria za usalama barabarani na kuacha tabia za kuendesha vyombo vya moto kwa mwendo kasi ili kuepukana na ajali zembe. 

Wankyo aliwapa salamu madereva hao, kuwa hawatakuwa na muhali nao kwani watakamatwa na kuwachukulia hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa wengine.

Mizizi 29 Power Ni Dawa Ya Nguvu Za Kiume Ambayo Imechanganywa Na Mizizi 29

0
0
Kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wanaume wazee hata na vijana kupungukiwa au kutokuwa kabisa na nguvu za kiume nanimekuwa nikipigiwa simu na wanawake wakilalamika ndoa zao zipo mashakani maana hawaridhishwi na Waume au wapenzi wao pale wanapoaza kushiriki tendo la ndoa 

Kwa Nini Ujione Mpweke Pale Ukutanapo Na Mpenzi Au Mke Wako Kisa Eti Hauna Nguvu Za Kiume? ;Tumia MIZIZI 29 POWER, hii ndio tiba itakayorudisha heshima ya ndoa yako . 

Dawa hii itakufanya;
 1 Uchelewe kufika kileleni mda wa dakika 15-25 kwa tendo la kwanza 
2 Dawa hii itakupa uwezo wa kurudia tendo zaidi ya Mara tatu 
3  Dawa hii uhimalisha misuri iliyolegea na kusinyaa?dawa hizi hazina madhara kwa mtumiaji nani tofauti na ulizowai kutumia ata wazee wenye umri mkubwa wanapona 

NSONSOMA; Dawa hii itakufanya umridhishe  mke au mpenzi wako kwani uboresha uume saizi upendayo urfu wa nchi 5,6,7 na 8 na unene wa sentimita 2,3,4 na 5 dawa  hii ipo ya kupaka na kunywa 

NSHOLA; NI dawa ya uzazi kwa waliongaika mda mrefu bila kupata mtoto 

MWITA; Dawa hii humvuta meme, mke,au mpenzi mliyetengana pia umrudisha mtu kazini haliyefukuzwa, kumpatanisha mwajiliwa na bosi wake 

Tunatibu presha kisukari, busha ,vidonda vya tumbo tumbo kuunguruma kujaa gesi na kukosa choo 

MAHALI ILIPO OFISI; PANDA DALADALA SHUKA BUGURUNI MALAPA AU ROZANA NA MWANZA YUPO WAKALA PIGA SIMU 0752348593 DR NYAROBI .Kama hauna nafasi ya kuja ofisini utaletewa popote ulipo huduma hizi

Mbunge wa CUF Ataka Mwenge usikimbizwe Kwa Madai Kwamba Umepoteza Mvuto

0
0
Leo Jumanne Novemba 6, 2018, mbunge wa Temeke (CUF), Abdallah Mtolea ameuliza kama Serikali haioni kukimbiza Mwenge wa Uhuru kwa sasa hakuna umuhimu tena kwani umekuwa ukisababisha mambo mengi ikiwemo magonjwa ya zinaa ikiwamo HIV.

Akiuliza swali katika kikao cha kwanza, mkutano wa 13 wa Bunge unaoendelea jijini Dodoma, Mtolea alielekeza swali hilo kwa Waziri Mkuu kuwa kama Mwalimu Nyerere alisema anawasha mwenge ili uwekwe juu ya mlima Kilimanjaro kwanini serikali inaendelea kuutembeza.

Akijibu swali hilo kwa niaba ya Waziri Mkuu, Naibu Waziri wa Kazi Kazi, Vijana, Ajira na watu wenye ulemavu Anthony Mavunde amesema "kuwa lengo la mwenge ni kujenga misingi ya binadamu na utu wa mtanzania, pia umelenga kuhamasisha ukombozi wa bara la Afrika, kupitia utaratibu huu, mwenge ni chombo muhimu kwa kuimarisha nchi yetu.”

Mara baada ya majibu hayo Mbunge huyo wa jimbo la Temeke alidai mwenge huo kwa sasa unapokelewa na baadhi ya watumishi wa serikali, wakiwemo madiwani pamoja wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari pekee akidai kuwa wananchi wamechoshwa kuuona kila mwaka.

Kufuatia swali hilo la Nyongeza Spika Ndugai aliamua kumkatisha mbunge huyo wa Temeke kwa kile alichokisema kuwa swali lake halikuwa la msingi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images