Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu ya November 5


Habari Njema Kwa Wenye Matatizo Ya Nguvu za Kiume, vitambi, nyama uzembe

0
0
(1).Fikiria ulianzia wapi? Je,ulifanikiwa au bado?

(2).Upo tayari kupona kwa haraka?

TIBA ZITOLEWAZO NI,

NGORO 4 POWER; Huongeza nguvu za kiume yenye mfumo wa unga na vidonge dozi siku(6).

MELAMELA; Hurefusha na kunenepesha uume ipo katika mfumo wa unga dozi siku (4).

KASELA; Hurudisha mke,mme,mchumba na hawara ndani ya siku mbili tu,atatimiza mahitaji yote hata Kama yupo mbali na kumfunga asiwe na mtu mwingine.

IKUMBUJA; Humfanya mtu  kupandishwa cheo kazini na kulipwa madeni au mafao yako pia na kumaliza kesi kabisa.

DUDUMA; Huongeza hips,makalio na mguu wa bia.

SWASWA: Hupunguza maziwa makubwa, kitambi, nyama uzembe, michirizi na muwasho sehem za Siri,na harufu mdomoni.

KOOLA;Hutibu magonjwa sugu ya zinaa, tumbo kujaa gesi,kuuma chini ya kitovu, kiuno ,fangasi za miguu, na kuvimba miguu au miguu kuwaka Moto.

Kwa hayo na mengineyo mfatilie DR.HINDU kwani ana uwezo wa kuhudumia ndani na nje ya TANZANIA.Kwa Dar es salaam anapatikana BUGURUNI MALAPA pia KAHAMA anapatikana MARUNGA.

Kwa wasio na mda wa kufika ofisini kwangu Nina vijana wa kukuletea mpaka ulipo kazini ama nyumbani kwako.

OFISI ZINAFUNGULIWA SAA 07 :00 ASUBUHI.

CONTACTS 0744 922 982(WhatsApp), 0716608959.

  "WOTE MNAKARIBISHWA".DR   HINDU NI SULUHISHO LAKO.

Kidato Cha NNE Kuanza Mitihani Leo....Serikali Yatoa Onyo Kwa Watakaoiba Mitihani

0
0
Mtihani  wa taifa wa kidato cha nne unaanza leo, huku Baraza la Taifa la Mitihani (Necta) likitoa onyo kali kwa watakaobainika kujihusisha na vitendo vya udanganyifu.

Baraza hilo limesisitiza kuwa halitasita kukifutia matokeo kituo chochote cha mtihani ambacho kitabainika kujihusisha na udanganyifu.

Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa Necta, Dk. Charles Msonde, alipozungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mtihani huo ambao utawahusisha jumla ya watahiniwa 427,181.

Dk. Msonde alisema baraza linazitaka kamati za mitihani za mkoa, halmashauri kuhakikisha kuwa taratibu zote za uendeshaji mitihani ya taifa zinazingatiwa ipasavyo.

“Kamati zihakikishe kuwa mazingira ya vituo vya mitihani yapo salama, tulivu na kuzuia mianya yote inayoweza kusababisha kutokea kwa udanganyifu,” alisema.

Alisema wasimamizi wote wanatakiwa kufanya kazi yao kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu. Wasimamizi wanaaswa kujiepusha na vitendo vya udanganyifu kwani baraza litachukua hatua kali kwa yeyote yule atakayebainika kukiuka taratibu za uendeshaji wa mitihani ya taifa.

Dk. Msonde alisema kwa upande wa wanafunzi, baraza linaamini kuwa walimu wamewaandaa vizuri katika kipindi cha miaka minne ya elimu ya sekondari.

“Matarajio ya Baraza la Mtihani ni kuwa wanafunzi watafanya mitihani yao kwa kuzingatia kanuni za mitihani. Watahiniwa wote watambue kuwa kukiuka kanuni za mitihani au kufanya udanganyifu kutawafanya wafutiwe matokeo yao yote,” alisema.

Alisema baraza linawataka wamiliki wa shule wote kutambua kuwa shule zao ni vituo maalum vya mitihani, hivyo hawatakiwi kuingilia majukumu ya wasimamizi wa mitihani katika kipindi chote cha ufanyaji wa mtihani huo.

Dk. Msonde alisema hawatasita kukifutia matokeo kituo chochote cha mtihani endapo baraza litajiridhisha kuwapo na uhatarishi wa usalama wa mitihani ya taifa.

Aidha, alitoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano unaotakiwa katika kuhakikisha mitihani ya kidato cha nne inafanyika kwa maarifa, amani na utulivu.

“Wananchi wanaobwa kuheshimu eneo la mitihani na kuhakikisha kuwa hakuna mtu yeyote asiyehusika na mitihani anayeingia kwenye maeneo ya shule katika kipindi chote cha mtihani. Tukifanya hivyo, tutawawezesha watoto wetu kufanya mtihani kwa amani na utulivu,” alisema.

Dk. Msonde aliwataka wanafunzi, walimu na wananchi wote kutojihusisha na vitendo vyovyote vya udanganyifu wa mtihani huo.
 
Alisema baraza halitasita kuchukua hatua kwa yoyote atakayejihusisha na udanganyifu katika mitihani kwa mujibu wa sheria za nchi na kanuni za utumishi wa umma.

Aidha, aliwaomba wadau wote kutoa taarifa katika vyombo husika kila wanapobaini mtu au kikundi cha watu kujihusisha na udanganyifu wa mitihani ya aina yoyote.

Kwa mujibu wa Dk. Msonde, jumla ya watahiniwa 427,181 wamesajiliwa kufanya mtihani huo ambao utamalizika Novemba 23, mwaka huu.
 
Alisema kati ya watahiniwa wa shule ni 368,227 na watahiniwa wa kujitegemea ni 58,954.

“Kati ya watahiniwa wa shule 368,227 waliosajiliwa, wanaume ni 180,908 sawa na asilimia 49.13 na wanawake ni 187,319 sawa na asilimia 50.87. Watahiniwa wenye mahitaji maalum wapo 562 kati yao 372 ni wenye uoni hafifu, 44 wasioona, 109 wenye ulemavu wa kusikia na 37 ni wenye ulemavu wa viungo vya mwili,” alisema.

Matokeo ya Uchaguzi wa Simba SC

0
0
Club ya Wekundu wa Msimbazi Simba SC Jumapili ya November 4 2018 ilifanya mkutano wake mkuu sambamba na uchaguzi mkuu wa mwenyekiti na wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi wa kampuni ya Simba SC ambapo kura zilihesabiwa hadi alfajiri ya November 5 2018.

Simba SC sasa inahesabika kama kampuni baada ya kufanikiwa kuingia katika mfumo wa mabadiliko ya uwekezaji wa hisa, ambapo mfanyabiashara Mohammed Dewji ndio alishinda Zabuni ya uwekezaji ndani ya club ya Simba hivyo maamuzi ya timu hiyo kwa sasa yatakuwa yanajadiliwa ndani ya bodi.

==>>Tazama matokeo hapo chini


 Matokeo
Mwenyekiti-
Sued Mkwabi kura 1579 kayi ya 1628

Wajumbe:
Asha Baraka.        -1180
Hussein Kitta.       - 958
Dr Zawadi.              - 830
Seleman Harub.     -740
Mwina Kaduguda  -577
Elia Alfred Martin.  -530
Juma Pinto.            - 440
Jasmin Soud.         - 368
Patrick Rweyemam-349
Abubakar Zebo.       -301
Iddi Kajuna.              -270
Said Tully.                 -247
Ally Suru.                  -217
Chris Mwansasu    -186
Hamis Mkoma.      -174
Mohamed Wandwi-124
Abdallah Migomba -97

Washindi ni
1. Hussein Kitta
2. Dr. Zawadi
3. Haroub Seleman
4. Mwina Kaduguda
5. Asha Baraka

Sukari Ya Kupanda Ni Tatizo Linalo Weza Kudhibitiwa Kwa Tiba Asilia

0
0
Unasumbuliwa na tatizo la sukari ya kupanda kwa muda mrefu ? Umejaribu tiba mbalimbali bila mafanikio?

Kama jibu lako ni NDIO nasi hii ni HABARI NJEMA SANA KWAKO.

Ipo dawa ya asili ambayo inasaidia sana kutibu tatizo la.sukari ya kupanda.

Kazi za dawa hii ni pamoja na kushusha sukari iliyo panda pamoja na kudhibiti kiwango cha sukari mwilini.

Dawa hii pia ni nzuri sana.kwa wanaume wenye tatizo la.ukosefu wa nguvu za kiume ambalo linasababishwa na.sukari. Dawa hii inaanza kuonyesha Matokeo mazuri ndani ya Siku saba.

Mtumiaji wa dawa hii anashauriwa kupima sukari yake ndani ya Siku saba tangu alipoanza kuitumia dawa hii ili kujionea mwenyewe ufanisi wa tiba hii na kuweza kuona namna ambavyo sukari yake imeshuka na baada ya hapo anashauriwa kuwa anapima kila baada ya Siku tatu hadi sukari yake itakapo fika normal.

KWA WENYE SUKARI NA PRESHA :
Uzoefu unaonyesha kuwa watu wengi wenye kusumbuliwa na tatizo la sukari huwa wanasumbuliwa na tatizo la presha pia.

Kwa.mtu mwenye tatizo la sukari ya kupanda ambalo lina ambatana na presha ya.kupanda anaweza kutumia dawa mbalimbali za asili kutibu tatizo la presha.

Moja kati ya dawa hizo ni pamoja na majani ya ukwaju. Majani ya ukwaju yanawasaidia sana watu wenye presha ya kupanda.

Jinsi yanavyo tumika unachukua majani fresh ya ukwaju kiasi cha kujaa viganja viwili vya mkono una yatwanga kwenye kinu au kuyaponda ponda had yalainike kabisa halafu unachanganya na.maji nusu Lita kisha unakamua pamoja na maji kupata kimiminika chake. Utatumia kunywa robo Lita asubuhi na robo Lita nyingine unatumia kunywa usiku kwa muda wa Siku ishirini na.moja.

Kama utashindwa  kutwanga au kuponda ponda unaweza kutumia blender.

Majani hayo hayo ya ukwaju juisi yake inasaidia sana kuongeza maziwa kwa akina mama wanao nyonyesha. Inaongeza maziwa kwa kiasi kikubwa sana na kwa haraka sana.

Kupata dawa hii ya sukari fika katika duka la kuuza dawa za asili la Neema Herbalist.

Tunapatikana Ubungo jijini Dar Es Salaam jirani na.Shule ya Msingi Ubungo National Housing nyuma.ya jengo la Ubungo Plaza.

Kwa wateja wetu waliopo jijini Dar Es Salaam ambao hawana nafasi ya kufika ofisini kwetu, tunayo huduma ya kuwapelekea dawa mahali walipo ( Home & Office Delivery )

Na kwa wateja wa mikoani tunawatumia dawa kwa njia ya usafiri wa mabus mbalimbali.

Wasiliana.nasi kwa simu namba : 0693 005 189.

RC Makonda Alivyo Mwaga Machozi Akiombewa Kanisani

0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Mhe. Paul Makonda jana  Novemba 4, 2018 aliangua kilio kwa mara nyingine kanisani aliposhiriki ibada ya Jumapili kwenye Kanisa la Efatha lililoko Mwenge jijini Dar es Salaam.

Kiongozi huyo wa Jiji la Dar es Salaam aliangua kilio hicho baada ya kupewa nafasi na Mchungaji Kiongozi wa kanisa hilo, Josephath Mwingira ya kuwasalimia waumini.

Baada ya salamu, Makonda alianza kwa kueleza kuwa lengo la kufika kwake kanisani hapo ni kuwaomba waumini wa kanisa na mchungaji wake, kumsaidia kimaombi katika vita dhidi ya vitendo vya ushoga, usagaji na matukio mengine maovu yanayoendelea katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Alisema siri ya ushindi wake katika vita zote ambazo amekuwa kupambana nazo ni kumtegemea Mungu, akieleza kuwa anaamini hata katika vita hiyo atashinda kwa sababu amemkabidhi Mungu.

"Jambo ambalo ninaomba kwako mtumishi (Mwingira) pamoja na kanisa, wiki hii nimefikiria mambo mengi sana, pamoja na kwamba tunafanya kazi na kusimamia sheria lakini tunasahau kwamba na Mungu yupo," alisema Makonda na kuongeza: "Tunaweza kuwa na bidii sana ya kuhakikisha tunafanya mambo mazuri ya kumpendezesha Rais, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, lakini tukasahau Mungu ambaye hutupa nguvu na uwezo wa kufanya kazi hizo.

"Utaonekana umefanikiwa, umefanya kazi nzuri, lakini je, umefanya kazi ambayo Mungu alitaka ufanye ya kumpendeza?" 

Alisema kuwa pamoja na kufanya kazi ya serikali, kwa upande mwingine anapaswa kuhakikisha mkoa wake unakuwa ni sehemu safi na salama na kumpendeza Mungu kwa kuhakikisha hakukithiri maovu.

“Na ndiyo maana niliamua kuingia kwenye vita hata ya dawa za kulevya, ninyi mnajua kwamba ukipewa madaraka ya uongozi, Mungu anakutazama kwanza wewe kama ambavyo sasa hivi Mungu akiitazama Tanzania anamwona Rais John Magufuli, ndivyo ambavyo akiutazama Mkoa wa Dar es Salaam, anamwona Makonda," alisema.

“Mungu akinitazama anaangalia ushoga unaongezeka, akiangalia anaona mateja barabarani nao wanaongezeka, unafikiri Mungu atakuwa na furaha na mimi? Ndiyo maana nimekuja kuomba ‘toba’ kwa ajili ya mkoa wangu," alieleza zaidi Makonda huku akibubujikwa na machozi.

Makonda alidumu katika hali hiyo ya kububujikwa na machozi kwa takribani robo saa 15 na aliendelea kuzungumza katika hali hiyo, akiomba msaada na nguvu ya Mungu katika kufanikisha vita hiyo ya kuhakiksha Dar es Salaam inakuwa salama.

“Eee Mungu naomba toba kwa ajili ya mkoa wangu, nahitaji uniongoze, nahitaji nguvu, sheria zipo lakini watu hawaziangalii, watu wanafanya uzinzi wala hawaogopi, nahitaji mkono wa Mungu," sauti ya Makonda ilisikika akisali kanisani hapo. 

Baada ya kuanza kubugujikwa na machozi Makonda alipiga magoti, jambo ambalo lilimwinua Mchungaji Mwingira ambaye alianza kumwombea akishirikiana na waumini wake.

Katika maombi yake, mchungaji huyo alisema amebaini kiongozi huyo alikuwa anakabiliwa na makundi matatu ambayo yalikuwa yamepanga njama kumwangamiza.

“Siyo rahisi kwa kiongozi wa serikali kumwaga machozi mbele za watu, Mungu amesikia kilio chako, hata kama kulikuwa na makosa uliyoyafanya Mungu amekusaheme kwa sababu yeye husamehe," alisema Mwingira akiwa amemgusa kichwani Makonda.

“Na nimebaini kwamba kulikuwa na makundi matatu ambayo yalikuwa yamepanga njama ya kukuangamiza, lakini kwa maombi haya utakuwa salama, ulinzi wa Mungu uko juu yako." 

Baada ya kufanyiwa maombi katika kanisa hilo, Makonda alikwenda katika Kanisa la Victory Chiristian Center Tabernacle (VCCT) lililopo Kawe jijini ambako pia alimwomba mchungaji na waumini nao washirikiane naye katika maombi juu ya vita hiyo ya kuisafisha Dar es Salaam.

Makonda alisema vita hiyo aliyoianzisha ni ya Watanzania wa dini zote na si yake pekee, hivyo akaomba washirikiane naye.

 “Nataka ifike mahali hata wachawi waogope kukaa katika Mkoa wa Dar es Salaam, tunataka mkoa huu ubaki salama kwa ajili ya shughuli za kibiashara tu na si uhalifu wala uovu wa aina yoyote.

Na kwa taarifa nilizonazo ni kwamba tayari baadhi ya mashoga wameanza kukimbia kwenda nchi za jirani na mikoa mingine," alisema Makonda.

Wakati wa kampeni yake ya kupambana na matumizi na biashara ya dawa za kulevya, Makonda alilia hadharani Machi mwaka jana kwenye Kanisa la KKKT Kimara jijini  Dar alikokuwa akishiriki ibada ya Jumapili.

Jipatie Dawa ya Asili ya Kupunguza Maziwa, Kupunguza Tumbo,Kuongeza Unene, Kuongeza Maumbile ya Kiume na Kuondoa Chunusi

0
0
Bidhaa za NATURAL BEAUTY PROD ni bidhaa zilizothibitishwa kiafya na kupewa kibali original cha kuuzwa hadharani.

Bidhaa hizi zimetengenezwa kwa mimea na matunda hazina chemical wala madhara yoyote kwa mtumiaji
1. SHARK POWER--Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza uume urefu na upana mpaka nchi 7.5 inapatikana kwa @170,000/=
2. VIGA 84000---Hii dawa ya kuspray yenye uwezo mkubwa wa kuchelewesha wakati wa tendo la ndoa @160,000/=
3. HANDSOME UP ORIGINAL-- Hichi ni kifaa cha kuongeza maumbile kwa size uipendayo pamoja na kuimalisha misuli kifaa hichi kinapatikana kwa @230,000/=
4. MAXMAN CAPSULE--- Hii ni dawa ya vidonge ya kuongeza uume urefu na upana pamoja na kuongeza nguvu za kiume kwa wiki mbili tu bei yake ni @200,000/=
5. VIG RX---- Hii ni dawa ya kupaka ya kuongeza uume urefu na upana mpaka nchi 10 inapatikana kwa @190,000/=
6. BODY BOOSTER---Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza mwili pamoja na hamu ya kula vizuri @150,000/=
7. BOTCHO MULT PLUS-- Hii ni dawa ya kunywa ya kuongeza (hips mapaja na makalio) kwa size uipendayo unaipata kwa @200,000/=
8. WHITE COLLECTION---- Ni vidonge vya kuwa mweupe mwili mzima pamoja na kuwa soft @150,000/=  N.K

 Wasiliana nasi kwa simu
NO:. +255 759029968
                      AU
           +255 659618585
Popote ulipo utapata huduma zetu.
Pia hakikisha unapatiwa risiti yenye muhuri halisi wa NATURAL BEAUTY PROD ununuapo bidhaa kampuni hii.  
          WELCOME ALL

Mwanafunzi afariki kwa kukatwa mguu akichunga ng’ombe

0
0
Aliyekuwa mwanafunzi wa Shule ya Msingi Kisangura wilayani Serengeti, Mkoa wa Mara, Emmanuel Nyakitare, (15), amefariki baada ya kukatwa mguu kwa panga na mwanafunzi mwenzake wakiwa wanachunga ng’ombe.

Emmanuel alifariki wakati akisubiri matokeo ya mtihani wa darasa la saba, yaliyotangazwa hivi karibuni. Chanzo cha tukio ni kugombania eneo la kulisha mifugo baada ya mtuhumiwa, Charles Kaheke (13), mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Kisangura kumkata kwa panga marehemu kwa kumtuhumu kulisha mifugo eneo lisilo lake.

Ofisa Tarafa ya Rogoro, Gasper Richard, alisema tukio hilo lilitokea Oktoba 29, mwaka huu, baada ya wanafunzi hao kugombana na baada ya kutenda kosa hilo mtuhumiwa alikwenda shuleni bila mfuko wa madaftari kama ilivyo kawaida, mwalimu wake alipomuuliza kwa nini hakuwa na daftari akamjibu mwalimu kwamba amnunulie ampe.

“Siku ya tukio marehemu alikwenda kuchunga mifugo yao eneo hilo jirani na nyumbani kwa akina Kaheke, (mtuhumiwa) ambaye alipotoka shule kuja kupata chakula cha mchana alimkuta marehemu eneo hilo, katika kuzozana ndipo mmoja alimkata mwenzake kwa panga na kuvuja damu nyingi,” alisema.

Akielezea tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu, alisema lilitokea Oktoba 29, mwaka huu, kati ya saa 6 na saa 7 mchana, wakati wanafunzi hao wakichunga mifugo, ndipo ulipozuka ugomvi kugombania eneo la malisho, ndipo mtuhumiwa alikasirika na kumkata mguu mwenzake kwa panga, hivyo kuvuja damu nyingi na kusababisha kifo chake.

“Hata hivyo, baada ya kuona amesababisha kifo cha mwenzake alitokomea na kukimbia kwenda kusikojulikana na mpaka sasa haijulikani alipo na marehemu Nyakitare alikuwa akisubiri matokeo ya darasa la saba mwaka huu, baada ya kufanya mtihani,” alisema Babu.

Babu, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Serengeti, alisema baadaye wazazi wa mtuhumiwa walikwenda kwa familia ya marehemu na kuomba msamaha na kuahidiana mambo ambayo hayakuwekwa wazi, hivyo kulimaliza suala hilo bila kufika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwa hatua zaidi.

Masunzu Power Mix Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

0
0
🌸MASUNZU POWER MIX; ni dawa ya asilia yenye mchanganyiko wa mitishamba 7 yenye maajabu yafuatayo (1) inatibu upungufu wa nguvu za kiume Mara dufu na kuimalisha uume   uliolegea wakati wa tendo la ndoa 
(2) kurefusha uume uliorudi ndani nchi 5-8 
(3) kunenepesha uume sm4 ya upana itakufanya uchelewe kufika kileleni dk (15-20) kwa tendo la kwanza na utakuwa nauwezo wa kurudia tendo la ndoa Mara (2-4) bila hamu kuisha nainatibu kabisa. 

Dawa hii haina madhara yoyote kwa mtumiaji huanza kufanya  kazi baada ya dk 50 tu🌾🌾🌾🌾🌾🌾🌾🌾      

 MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA ;ngiri. au umejichua kwa muda mrefu. Punyeto kisukari. Presha. Tumbo kujaa gesi na kuunguruma chini ya Kitovu. Kutopata choo vizuri. Msongo wa mawazo. Kaswende. Gono. Haya yote husababisha kuwa na maumbile madogo na kukosa nguvu za kiume 

🌸SOSOMA DX. ni dawa ya kumvuta mme au mke au mpenzi wako arudi haraka na kuanza mapenzi mapya kama mlivyo anza mwanzo baada ya masaa 2 atarudi na kutulia ndani ya nyumba na kutimiza ahadi yako 

🌸GINDU EXTRA; ni dawa ya kutibu kisukari siku 14 unapona kabisa hata kama imepanda itashuka haraka Sana. Tunatibu busha bila upasuaji nk. 

Dar es salaam tunapatikana Buguruni chama au unaweza kuletewa popote ulipo wasiliana na tabibu ATHUMAN SIMU +255767104343 / +255653207272

Ugonjwa wa Zinaa wa Kisonono (gonorrhea) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga

0
0
Kati ya magonjwa yanayoathiri watu wengi sana duniani ni magonjwa ya zinaa. Haya ni magonjwa yanayoambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kupitia vitendo vya ngono. 

Vitendo hivi vya ngono vinaweza kuwa kujamiana, kupiga denda (kissing), vitendo vya ngono kwa kutumia mdomo (oral genital sex), kujamiana kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) iwe kwa mwanamume na mwanamke au kati ya wanaume wenyewe na hata wale wanaotumia vifaa vya kufanyia ngono (vibrators). 

Magonjwa ya zinaa huathiri sana watu walio katika umri wa miaka 15 – 24 lakini hata kwa watu wengine ambao wana umri chini au zaidi ya huu niliotaja pia yanaonekana kwa wingi.

Kuna magonjwa ya zinaa zaidi ya ishirini yanayotambulika duniani, baadhi ya magonjwa ya zinaa ni
  1.  Kisonono (Gonorrhoea – “Gono” kama wengi wanavyopenda kuita kwa kifupi).
  2.     Chlamydia
  3.     Kaswende (Syphillis)
  4.     Human papilloma virus (HPV)
  5.     HIV/AIDS (Ukimwi/Upungufu wa kinga mwilini)
  6.     Hepatitis B, C, A
  7.     Herpes virus
  8.     Trichomoniasis
  9.     Bacteria Vaginosis
  10.     Pubic lice (chawa kwenye nywele za kinena)
  11.     Chancroid
Magonjwa mengi ya zinaa yanatibika lakini kuna baadhi ambayo hayana tiba ya uhakika kama HPV, Hepatitis B na C, na HIV. Mengine yameanza kuwa sugu kutokana na matumizi ya dawa za antibiotics bila mpangilio, magonjwa hayo ni kama gono (gonorrhoea) na nk.
 
Visababishi vya magonjwa ya zinaa
  1. Vitendo vya ngono kama nilivyoeleza hapo awali
  2. Kuanza vitendo vya ngono mapema au wakati wa umri mdogo
  3. Kuwa na wapenzi wengi
  4. Kufanya mapenzi ambao sio salama
  5. Maambukizi kupitia michibuko au sehemu zilizokatika kwenye ngozi kwa kugusana na majimaji ya aina yoyote yanayotoka kwa mtu mwenye ugonjwa wa zinaa kama damu, shahawa nk. Hii inaweza kutokea bila mtu kujua kwani mara nyingi dalili za magonjwa ya zinaa zinakuwa hazionekani kwa wanawake na hata baadhi ya wanaume.
Watu wengi huhisi kitendo cha kula denda (kissing) ni salama lakini si kama wanavyofikiria kwani baadhi ya magonjwa kama kaswende, herpes nk, yanaweza kuambukizwa kupitia njia hii. 

Soma pia:Tatizo la Kutokwa na usaha Wakati wa Kukojoa 

Kondomu husaidia kupunguza maambukizi ya magonjwa ya zinaa kama gono, Chlamydia lakini sio kinga muafaka dhidhi ya magonjwa ya zinaa kama kaswende, genital herpes, genital warts, na magonjwa ya upungufu wa kinga mwilini (AIDS).

Kisonono (gonorrhea) ni nini?
Kisonono ni ugonjwa kati ya magonjwa ya zinaa unaosababishwa na bakteria aina ya Neisseria gonorrhoeae, bakteria ambao hukuwa na kuzaliana kwa haraka katika sehemu zenye unyevunyevu na joto mwilini kama kwenye shingo ya kizazi kwa wanawake (cervix), mirija ya kupitisha mkojo au shahawa (urethra), mdomoni na kwenye puru. Maambukizi mengi kwa wanawake hutokea kwenye shingo ya kizazi (cervix). 

Asilimia 75 ya ugonjwa wa gono hutokea kwa watu wenye umri wa miaka 15 – 29, wanawake walio katika umri wa miaka 15 -19 na wanaume walio katika umri wa miaka 20 – 24 wako kwenye hatari zaidi ya kupata ugonjwa huu.
 
Ugonjwa huu huambukizwa vipi?
Ugonjwa huu huambukizwa kupitia vitendo vya ngono kupitia uke, njia ya haja kubwa (anus), kupitia mdomoni (oral sex). Ugonjwa unaweza kujitokeza kwenye sehemu za kujamiana, kwenye mdomo na kwenye puru (rectum). 

Soma Pia: Ugonjwa wa Zinaa wa Kaswende (Syphilis) : Dalili Zake, Madhara Yake Na Jinsi Ya Kujikinga 

Ugonjwa wa gono huonekana sana kwa vijana, watu wenye maisha duni kiuchumi, watu wanaoishi mijini, watu weusi na watumiaji madawa ya kulevya.
 
Dalili za ugonjwa wa kisonono
Dalili za ugonjwa wa kisonono huanza kujitokeza kuanzia siku ya 2 hadi ya 7 baada ya mtu kupata maambukizi na huweza kuchelewa kwa wanawake. Dalili ni kama zifuatazo

Kwa wanaume
  1. Kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa (burning sensation)
  2. Kutokwa na majimaji ya njano au meupe au ya kijani kutoka kwenye uume yanayoambatana na maumivu makali sana
  3. Wakati mwengine maumivu au kuvimba kwa korodani (swollen testicles)
  4. Maambukizi yakiwa kwenye puru (rectum) huambatana na maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa, kuwashwa sehemu za haja kubwa, na hata haja kubwa inaweza kutoka ikiambatana na damu, hii inatokea kwa wanaume na wanawake.
Kwa wanawake
Dalili kwa wanawake huwa si nyingi lakini wanawake wengi hawaonyeshi dalili zozote
  1. Maumivu au kuhisi kama kichomi wakati wa kukojoa
  2. Kuongezeka kwa kutoka majimaji kutoka kwenye tupu ya mwanamke ambayo ni ya njano au yamechanganyika na damu
  3. Kutokwa na damu kupitia tupu ya mwanamke kabla ya hedhi kufika.
  4. Kutokwa na damu baada ya kujamiana au baada ya tendo la ndoa
  5. Kichefuchefu
  6. Homa (fever)
  7. Kutapika
Vipimo vya ugonjwa wa kisonono
  1. Swab for culture – Kipimo hiki hufanyika maabara kwa kupandikiza bakteria baada ya kufuta sehemu za siri kwa kutumia swab ili kuona kama kuna bakteria wanaosababisha gono.
  2. Polymerase Chain Reaction (PCR)– Kipimo cha kuangalia vina saba (DNA) ya bakteria, ni ghali sana.
Tiba ya ugonjwa wa kisonono ni nini?
Tiba ya gono inahusisha na tiba ya ugonjwa wa Chlamydia kwani mara nyingi magonjwa haya huambatana kwa pamoja.Tiba hutegemea na umri wa mgonjwa na kama mtu ni mjamzito au la. 

Tiba ya gono ambayo sio sugu iliyo kwenye shingo ya kizazi (cervix), urethra na puru, dawa zinazotumika ni aina za cephalosporin dozi moja pamoja na dawa za aina ya macrolide antibiotics (mfano azithromycin) na za jamii ya penicillin (mfano doxycyclin) ili kutibu ugonjwa wa chlamydia. Mara nyingi kwa wale chini ya miaka 18 na wanawake wajawazito, hutibiwa kwa kuchomwa sindano.

Soma Pia: Saratani ya tezi dume : Madhara Yake, Dalili Zake, Chanzo na Tiba Yake

Fuata ushauri wa daktari kabla ya kutumia dawa hizi kwani dawa nyingi zina madhara kwa wajawazito (mfano doxycyclin). Ushauri nasaha hutolewa kwa wapenzi wote wawili na ni vizuri wapenzi wote wawili kutibiwa hata kama mmoja hana dalili za ugonjwa huu.
 
Madhara ya ugonjwa wa kisonono
  1. Kutoweza kuzaa kwa mwanamke (tasa) au kutoweza kutungisha mimba kwa mwanamume (infertility)
  2. Huweza kuathiri moyo (heart valves), ubongo,ngozi nk ambayo ni hatari sana kwa mtu yoyote.
  3. Madhara kwenye sehemu za maungio au jointi (joint inflammation)
  4. Kwa wanawake wale ambao hawajatibiwa wanaweza kupata ugonjwa wa PID (Pelvic Inflammatory Disease) ambao huongeza asilimia ya mwanamke kuwa tasa.
  5. Wale wanawake ambao ni wajawazito na wameambukizwa gono wako kwenye hatari ya mimba kutoka au kuzaa mapema kabla mimba haijatimiza umri wake (preterm labor).
  6. Kwa wale wanaoambukizwa gono kipindi cha kukaribia kujifungua, wanaweza kuwaambukiza watoto wao na hivyo watoto kupata ugonjwa wa uti wa mgongo (meningitis), kuwa kipofu (blindness), homa ya mapafu (pneumonia) na ugonjwa wa mifupa (septic arthritis).
Kinga ya kisonono
  1. Kutumia kondomu wakati wa kujamiana
  2. Kuwa na mpenzi mmoja mwaminifu
  3. Kuacha vitendo vya ngono kama matumizi ya vifaa vya ngono hasa kwa wanawake mfano vibrators nk.
  4. Kwa wanawake wajawazito – Hakikisha unahudhuria kliniki mapema ili upate kuchunguzwa na kupatiwa tiba muafaka kama utagundulika na ugonjwa wa gono au ugonjwa mwengine wowote.
  5. Wanawake wajawazito wanashauriwa kujifungulia hospitali ili kama mtoto ameathirika na gono apate matibabu ya haraka baada ya kuzaliwa kuepusha kuwa kipofu.
  6. Epuka kufanya ngono na mtu aliyeambukizwa gono.

Breaking News: Mahakama Yamwachia Huru Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo

0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa imemuachia huru Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo leo Novemba, 5  baada ya upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha makosa mawili yaliyokuwa yanamkabili

Nondo alikuwa anakabiliwa  na mashtaka mawili; shitaka la kwanza ni kusambaza taarifa za uongo akiwa jijini Dar es Salaam kuwa ametekwa na kosa la pili ni kutoa taarifa za uongo akiwa mjini Mafinga kwa askari Polisi kituo cha Mafinga Wilayani Mufindi.


Kimewaka tena: Marekani Yaiwekea Vikwako Iran....Jeshi La Iran leo Kufanya Mazoezi Makubwa Kuonesha Ubabe Wao

0
0
Marekani imetangaza kuwa leo Nov 5 imeirejeshea vikwazo nchi ya Iran vitakavyolenga sekta ya mafuta na sekta ya kifedha.

Marekani imesema imeiwekea Iran vikwazo vigumu zaidi ambavyo haijawahi kuiwekea. Vikwazo hivyo vitalenga mauzo ya mafuta, usafiri kwa njia ya baharini na mabenki ambavyo vyote ni muhimu sana kwa uchumi.

Maelfu ya raia wa Iran wakiwa na mabango yaliyoandikwa  "Kifo kwa Marekani" wameandamana  wakiitaka serikali  yao kutofanya mazungumzo yoyote na Marekani.

Jeshi la Iran nalo limesema kuwa litafanya mazoezi ya kijeshi leo Jumatatu na Jumanne kuonyesha uwezo wake wa kijeshi.

Marekani imetangaza vikwazo hivyo  baada ya  Rais Trump kutangaza  kujitoa kwenye  mkataba wa mwaka 2015 uliolenga kupunguza mipango ya nyuklia ya Iran.

Marekani inasema inataka kuzima vitendo viovu vya Ina vikiwemo udukuzi wa mitandao, majaribio ya makombora ya masafa marefu na uungaji mkono wa makundi ya kigaidi mashariki ya kati.

Zaidi ya watu 700, kampuni, vyombo vya habari na ndege kwa sasa vimewekewa vikwazo, yakiwemo mabenki makubwa, wauza mafuta na kampuni za usafiri wa baharini.
 
Wakati hayo yakijiri, Uingereza , Ujerumani na Ufaransa ambazo ni kati ya nchi zilizo kwenye makubaliano ya nyuklia zote zimekataa vikwazo hivyo vya Marekani dhidi ya Irani.

Zimeahidi kuzisaidia kampuni za Ulaya zinazofanya baishara halali na Iran na kubuni njia mbadala za malipo ambazo zitasaidia kampuni kufanya bishara bila ya vikwazo vya Marekani

NEMC Yakifungia Kiwanda cha Nyama ya Punda

0
0
Baraza  la Usimamizi wa Mazingira nchini (NEMC), limekifungia kiwanda cha kusindika nyama ya punda kilichopo kwenye Jiji la Dodoma, baada ya ukaidi wa muda mrefu wa mmiliki kufuata taratibu sahihi za uhifadhi wa mazingira.

Barua iliyoandikwa na Kaimu Mkurugenzi wa NEMC, Dk. Vedast Makota,  imeeleza kwamba, kiwanda hicho ambacho kinashughulika na uchinjaji na usafirishaji wa nyama ya punda nje ya nchi, kwa muda mrefu sasa kimeonyesha kushindwa kuzingatia taratibu za uhifadhi wa mazingira, licha ya onyo na ukumbusho kadhaa uliofanywa na baraza.

“Kufuatia mlolongo huu wa uchafuzi wa mazingira, ambao umekuwa ni kero kwa majirani na ambao unaleta mashaka kwenye ubora wa bidhaa, Baraza limefikia hatua ambayo linakosa cha kushauri zaidi ya kufunga kiwanda,” imeeleza barua hiyo.

Kwenye maelezo ya ufungaji wa kiwanda hicho, Dk. Makota alisema: “Kwa mamlaka yaliyokabidhiwa kwa Baraza chini ya Kifungu cha 196(2) cha Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004, unaamuriwa kusimamisha shughuli zote za uzalishaji kuanzia siku ya agizo hili mpaka utakapochukua hatua kikamilifu za kutekeleza maagizo yote uliyopewa hapo awali,” ilieleza barua hiyo

Kiwanda hicho ambacho kinamilikiwa na kampuni inayofahamika kama Huwachen Company Limited, kimekuwa kwenye mvutano wa muda mrefu na Baraza pamoja na Wizara inayohusika na uhifadhi wa mazingira tangu Mei, mwaka huu, ambapo aliyekuwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Kangi Lugola, alitembelea na kueleza kutoridhishwa kwake na hali ya uhifadhi wa mazingira.

Ziara hiyo ya Naibu Waziri ilitokana na ukaguzi wa NEMC uliofanywa Agosti, mwaka huu kwa lengo la kutathmini hali ya uhifadhi wa mazingira kwenye kiwanda hicho kutokana na shughuli zake. Katika tathmini hiyo, suala la uchafuzi wa mazingira liliendelea kuonekana kuwepo.

Mambo yaliyoonekana kuwa ni tatizo ni pamoja na mabaki ya damu kwenye eneo hilo ambayo yalipelekea uwepo wa nzi wengi, kuziba kwa mitaro ya kupitisha maji machafu, kukosekana kwa utaratibu madhubuti wa kuhifadhi mbolea, kiwango duni cha shimo la kuhifadhia uchafu, harufu mbaya na ukosekanaji wa mpango endelevu.

Mapungufu hayo kwa mujibu wa taarifa hiyo ya Mkurugenzi wa NEMC yanakiuka vifungu kadhaa vya sheria ya mazingira ya mwaka 2004, hii ni pamoja na kifungu cha 106 (1) (2) na (6) pamoja na kifungu cha 187 (1) (b) na (C).

RC Makonda Afunguka Siri Ya Kumwaga Machozi Kanisani...."Watu Wanadhani ni Utani, Ila Mbinguni Wanajua"

0
0
Siku moja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kutokwa na machozi akiwa katika ibada katika kanisa la Efatha linaloongozwa na mtumishi wa Mungu Josephat Mwingira kiongozi huyo ameibuka na kutoa neno.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Makonda amechapisha video ambayo alionekana  anatokwa na machozi kanisani hapo na kuandika ujumbe ambao alibainisha watu wengi hawajui kilichotokea.

Makonda ameandika; “Powerful, very powerful watu hawaelewi nini kimefanyika Ila mbinguni wameelewa na wameandika, people think it’s a joke. Ila kwa Mungu hakuna mzaha, asante Mungu Kwa kusimama upande wangu”

Hivi karibuni Mkuu wa huyo wa Mkoa Dar es salaam alianzisha kampeni maalum ya kuwakamata watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja, na kuunda kamati maalum ya watu 17 ili ya kushughulika na suala hilo.

Jana kupitia ofisi ya Wizara ya Mambo ya Nje,  serikali ilisema zoezi linaloendeshwa na Mkonda  ni mawazo yake binafsi na si msimamo wa serikali.

Diamond Azindua Rasmi Wasafi Festival na Wasafi FM

0
0
Kampuni ya Wasafi Classic Baby (WCB) leo imezindua kituo cha redio cha Wasafi FM pamoja na tamasha la Wasafi litakalofanyika katika maeneo mbalimbali nchini.

Mkurugenzi wa WCB, Nassib Abdul 'Diamond Platnumz' amesema uzinduzi wa redio hiyo unalenga kutoa fursa kwa wasanii na Watanzania kwa ujumla kusikika.

"Siku ya leo redio yetu ya Wasafi FM itaanza kusikika kupitia masafa ya 88.9 katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani. Bado ndio tupo kwenye majaribio kwani mambo mazuri yanakuja na tumefanya hivi kwa sababu hata sisi wenyewe tulifanikiwa kwa sababu tulisapotiwa na vyombo vya habari," alisema Diamond.

Kuhusu Tamasha la Wasafi, Diamond alisema mbali ya kuburudisha, watafanya huduma za kijamii na kutangaza utalii.

"Licha kufanya tamasha, sisi tungependa kuonyesha kitu cha tofauti. Tutajitahidi katika kila mkoa tunaoenda kurudisha kwa jamii kile ambacho tunakipata kutoka kwao. Tutaangalia changamoto ya eneo husika kama itakuwa ni elimu basi tutatoa sare za shule, madawati na kadhalika. Pia tutatangaza utalii," alisema Diamond.

DC Jokate Mwegelo atembelea pacha waliotenganishwa Muhimbili

0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, Jokate Mwegelo akiwa na Ester Simon baada ya kumtembelea leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambako pacha walifanyiwa upasuaji wa kuwatenganisha kutokana na kuzaliwa wakiwa wameungana.

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo akisalimiana na Ester Simon baada ya kumtembelea wodini leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Muhimbili, Prof. Lawrence Museru akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo mara baada ya kuwatembelea watoto pacha leo.
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo Mwegelo akiwa katika picha ya pamoja na Prof. Museru na Sister Ester Mwambogoja.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa pekee iliyotibu watu wengi nchini na nje ya nchini kwa kufanya kazi Mara 3 kwa wakati mmoja 1 ...kurefusha uume na kunenepesha saizi upendayo, kuogeza nguvu za kiume na inatibu matatizo , ikisha tibu aina madhara inaimalisha mishipa ilio regea na uzalishaji wa mbegu za kiume. TAHADHARI HAKIKISHA UNA MKE AU    MPENZI. 

NINI HUCHANGIA MATAZO HAYA . Ngiri ni chanzo Kikubwa cha matatizo,haya kujua kwamba una ngiri dalili zake ni 1.kufika haraka kileleni wakati  watendo la ndoa 
2.Kushindwa kulundia tendo la ndoa 
3.Kutoa choo kama cha mbuzi 
4. Tumbo kujaa gesi na kuunguruma 
5 kukosa choo kabisa 
6 Maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi 
7 korondani moja kuvimba 
8 kutosikia hamu ya tendo la ndoa
 9 maumivu ya kiuno na mgongo  

Pia tunatibu busha bila kufanyiwa opresheni .Umeachwa na umpendae na bado unamwitaji?

WASILIANA  NA MTALAM  CHALLO 0714 006521. YUPO MBAGALA.

TFF Yamfungia maisha aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati yake ya Uchaguzi, Wakili Revocatus Kuuli

0
0
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kupitia Kamati ya Maadili limemfungia maisha kutojihusisha na soka aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati yake ya Uchaguzi, Wakili Revocatus Kuuli baada ya kukutwa na hatia ya makosa matatu ya kimaadili.

Mwenyekiti wa kamati ya maadili ya TFF, Wakili Hamidu Mbwezeleni alisema Kuuli akitambua nafasi yake ndani ya shirikisho hilo, alifanya makosa hayo matatu ambayo kimsingi yanastahili adhabu ya kifungo cha maisha kujihusisha na masuala ya mpira wa miguu.

Makosa matatu ambayo yamemtia hatiani Wakili Kuuli ni kusambaza nyaraka za shirikisho kinyume na kanuni na taratibu, kutoa maelezo yanayoonesha kuwa na mgongano wa kimaslahi kwa kuwapa watu wasiohusika na pia kufanya vitendo vinavyoshusha hadhi ya shirikisho.

"Uamuzi huu umechukuliwa kwa kufuata kanuni na taratibu. Hakuna aliyemuonea Kuuli niliweke hilo sawa," alisema Wakili Mbwezeleni.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMBO ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744391089  au  0653182109

Mzee wa Miaka 65 Mbaroni kwa Tuhuma za Kubaka Mtoto wa Miaka Mitatu

0
0
Mkazi wa Mburahati Motomoto, jijini Dar es Salaam, Mohamed Hassani (65) anashikiliwa na jeshi la polisi mkoa wa Kinondoni akituhumiwa kumbaka mtoto wa kike wa miaka mitatu.

Mama mlezi wa mtoto huyo, Hadija Saidi amesema siku ya tukio mtuhumiwa alimwita mwanaye kwenye chumba chake ili amtume dukani na alimwandikia kwenye karatasi dawa ya Diclopre na pipi ili akanunue.

Amesema hawakuwa na wasiwasi naye kwa kuwa mtuhumiwa alikuwa mtu mzima na mara nyingi amekuwa akimwita mtoto huyo ndani kwake na wakati mwingine akimtuma dukani.

"Huyu mzee ni mpangaji mwenzetu, hana mke na tulikuwa tunamheshimu sana wapangaji wote na tunamuita mjomba kutokana na uzee wake yaani sikuamini siku hiyo napigiwa simu na mpangaji mwenzangu akiniambia nirudi haraka nyumbani nikamwangalie mtoto amebakwa," amesema Hadija.

Hadija anasema wameshafungua jalada la kesi ya ubakaji yenye namba MBT/RB/5395/2018 ambapo mtuhumiwa ameshakamatwa hivyo wanasubiri afikishwe kwenye vyombo vya sheria.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kinondoni, Jumanne Muliro amesema tukio hilo lilitokea Oktoba 31, 2018 maeneo ya Mburahati Motomoto ambapo mtuhumiwa alimfanyia mtoto huyo kitendo akiwa kwenye chumba chake.

"Taarifa za kubakwa mtoto huyo tunazo tunazishughulikia kwa mujibu wa sheria na tutahakikisha mtuhumiwa anafikishwa mahakamani," amesema Muliro,
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images