Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Lugola Afanya Ziara Ya Kushtukiza Vituo Vya Polisi Tabata,Buguruni Na Kutoa Maagizo Ya Dhamana Kutolewe Saa 24

0
0
Na Felix Mwagara, MOHA
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amefanya ziara ya kushtukiza kituo cha Polisi Tabata na Buguruni vya jijini Dar es Salaam ili kujua kama maagizo yake aliyoyatoa katika vituo mbalimbali kama yameanza kufanyiwa kazi.

Waziri Lugola alianza ziara yake saa 2:45 jana asubuhi kwa kuibukia katika kituo cha Tabata na moja kwa moja alianza kuulizia mahudhurio ya wafanyakazi wote wa kituo hicho na kujua nani yupo kazini na nani hayupo na kwanini hajafika ofisini hapo kwa muda huo wa asubuhi.

Wakati alipokua kituoni hapo, pia Lugola alikichukua kitabu cha taarifa za watuhumiwa wote waliopo mahabusu na baadaye kuelekea katika mahabusu hiyo akiwahoji watuhumiwa kwa kuwaita kwa majina kujua makosa yao yaliyoyafanya wawepo kituoni hapo.

Lugola baada ya kumaliza katika kituo hicho, saa 5:27 alielekea kimyakimya katika kituo cha Polisi cha Buguruni, na aliwahoji watuhumiwa waliopo mahabusu katika kituo hicho na kujua makosa mbalimbali yanayowakabili huku polisi wapepelezi wa tuhuma zao wakiwepo katika tukio hilo.

Akizungumza mara baada ya kumaliza ziara yake, Lugola alisema, alitoa maagizo mbalimbali katika ziara zake nchini, hivyo anafuatilia kujua maagizo yake yameanza kufanyiwa kazi au bado baadhi ya vituo kama wameyapuuza.

“Lengo la hii ziara yangu ni kuboresha utendaji kazi wa vituo vya polisi nchini, sijaja kumuadhibu mtu mimi, hivyo msiwe na wasiwasi, bali kilichonifanya hapa nije nikufuatilia maagizo mbalimbali ambayo niliyatoa kama kweli mnayafanyia kazi,” alisema Lugola.

Maagizo aliyoyatoa mwezi miwili iliyopita katika ziara zake mikoa mbalimbali nchini ni kuhakikisha pikipiki zinaondolewa katika vituo vya polisi, dhamana zitolewe saa 24 ikiwemo Jumamosi na Jumapili, pamoja na polisi kutowabambikizia kesi wananchi.

Hata hivyo, Lugola alivipongeza vituo hivyo vya polisi vilivyopo wilayani Ilala na pia Kituo Kikuu cha Polisi Dodoma alichokitembelea wiki iliyopita, kwa kuanza kuyafanyia kazi maagizo yake aliyoyatoa zikiwemo baadhi ya bodaboda, zimeondolewa vituoni na zilizobaki zina kesi mahakamani.

“Nilifanya ziara ya kushtukiza pale Kituo cha Polisi cha Tabata, na pia nimekuja hapa Buguruni, kwakweli wameaanza kuyafanyia kazi maagizo yangu, pikipiki zote nilizozikuta zinasababu yakuwepo hapo, na si vinginevyo kama walivyokua wanaziweka kiholela hapo awali,” alisema Lugola.

Pia lugola aliwataka Makamanda wa polisi nchini kuwafuatilia askari wao kwa umakini ili kujua utendaji kazi wao, na pia Waziri huyo alisema atakua anafanya ziara kama hizo mara kwa mara hivyo vituo vya polisi nchini viwe sawa muda wote.

“Hamjui siku wala saa ambapo nitakuja, tufanye kazi, tuwahudumie wananchi, tusiwaonee wananchi, tujitume kufanya kazi kwa weledi, sitamvumilia mtu ambaye atavunja utaratibu,” alisema Lugola.


January Makamba: Nilitamani Kujiuzulu Ubunge Ili Kulinda Maslahi Mapana ya Wananchi

0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, January Makamba amesema kuwa mgogoro wa kiwanda cha Chai cha Mponde ulitaka kumfanya achukuwe uamuzi wa  kujiuzulu nafasi zake zote za uongozi kisiasa na kiserikali.

Hatua hiyo ilitokana na namna ambavyo viongozi wenzake walivyokuwa wamegawanyika katika namna ambavyo usuluhisho wa mgogoro huo ulivyokuwa ukionekana kutaka kuwanyima haki wananchi.

Waziri huyo alizungumza hayo jana Novemba 1 kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Mponde wilayani Bumbuli wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa hapo juzi.

Alisema alishadhamiria kuachana na nyadhifa zake baada ya kuona viongozi wenzake walitofautiana katika swala hilo wakidhani anamaslai nalo.

“Niliona ni wajibu wangu kusimamia haki za wananchi na maslahi yao hata kama ningetengwa na kunyanyaswa kwani naamini siku zote yule anayesimamia haki Mwenyezi Mungu hawezi kumtupa” alisema Waziri Makamba.

Amesema mgogoro huo ulileta mpasuko kwa viongozi wa ngazi ya mkoa hadi shina lakini imani yake kwa sasa ni kwamba wameelewa alichokuwa akikitetea na sasa wapo pamoja.

“Wananchi na Wakulima wa chai wameumua wamenyanyasika sana, wamedhulimiwa lakini siasa ninaimani kwa mikakati ya serikali sasa uchumi utaimarika” alisema Waziri huyo.

Hata hivyo aliiomba serikali kuwasaidia wakulima kufufua zao hilo kwa kuwapatia miche bora, pembejeo za kilimo ili kufufua zao hilo.

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa alisema kuwa serikali imekichukuwa kiwanda hicho na sasa wapo kwenye maandalizi ya kukifufua upya.

Alisema kwa sasa wanafanya uhakiki wa madeni yote pamoja na ukaguzi wa mashine na mitambo katika kiwanda hicho ili kujiridhisha kabla hakijaanza kufanyakazi tena.

Alisema tayari deni la kiwanda ni sh Bil 4.4 na kwa sasa anataka afahamu madeni yote mpaka ya wafanyakazi wa kiwanda hicho ili baada ya hapo wajipange kwa ajili ya ulipaji wa  madeni hayo ili kiwanda kianze upya.

Katika hatua hiyo Waziri Mkuu amemuagiza meneja wa kiwanda hicho, Stephen Wahome kuhakiki idadi ya wafanyakazi waliokuwepo awali kiwandani hapo kujua madai yao ya pamoja na idadi ya vifaa vilivyokuwepo kiwandani hapo.

“Watu wote waliokuwa wakidai kiwanda hiki serikali italipa madeni yao wakati tukiendelea na jitihada za kukifufua kiwanda hiki kiweze kurudi katika hali yake ya uzalishani na wananchi waweze kunufaika” alisema Waziri huyo.

Waziri Majaliwa alisema kuwa mgogoro wa kiwanda hicho ulianza Mara baada ya wakulima kuanzisha Umoja wa wakulima wa chai UTEGA na kuusajili kama Shirika la kijamii NGOs badala ya chama cha ushirika.

Alisema kuwa chama hicho kiliwabagua wakulima na kutoa upendeleo kwa baadhi ya wakulima hali iliyosababisha mgogoro huo.

Alisema kuwa mgogoro ulikuwa zaidi baada ya viongozi wa UTEGA nao kugeukana na kuuza kiwanda kwa mwekezaji bila ya kutoa taarifa kwa wakulima wala wanachama wao.

Hivyo kutokana na kasoro hizo huku maslahi ya mkulima yakiwa madogo ndipo serikali ilipoamua kuchukuwa kiwanda chake ili iweze kukiendesha mwenyewe kwa maslahi ya wakulima na wananchi.

BREAKING: Treni ya abiria Dar yapata ajali na Kujeruhi Watu 9

0
0
Treni ya abiria inayofanya safari zake kati ya Stesheni na Pugu, jijini Dar es Salaam imepata ajali baada ya mabehewa yake mawili kuanguka eneo la Karakata wilayani Ilala na kujeruhi watu 9, leo asubuhi, Ijumaa, Novemba 2, 2018.

Kamanda wa Reli nchini, David Mnyambuga amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema mabehewa hayo mawili yameharibika vibaya na kwamba majeruhi tayari walikimbizwa hospitali kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

BREAKING: Amber Rutty Afikishwa Mahakamani

0
0
Video Vixen wa video za wasanii nchini, Ruth Abubakar ‘Amber Rutty’, leo Novemba 2 amefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akiwa anachechemea na kushindwa kukaa hadi alipopatiwa huduma ya kwanza na askari mahakamani hapo

Amber Ruty na mpenzi wake wanatuhumiwa kufanya ngono kinyume cha maumbile na kusambaza picha/video zao  kwenye mitandao ya kijamii 

Habari Njema Kwa Wenye Matatizo Ya Nguvu za Kiume, vitambi, nyama uzembe

0
0
(1).Fikiria ulianzia wapi? Je,ulifanikiwa au bado?

(2).Upo tayari kupona kwa haraka?

TIBA ZITOLEWAZO NI,

NGORO 4 POWER; Huongeza nguvu za kiume yenye mfumo wa unga na vidonge dozi siku(6).

MELAMELA; Hurefusha na kunenepesha uume ipo katika mfumo wa unga dozi siku (4).

KASELA; Hurudisha mke,mme,mchumba na hawara ndani ya siku mbili tu,atatimiza mahitaji yote hata Kama yupo mbali na kumfunga asiwe na mtu mwingine.

IKUMBUJA; Humfanya mtu  kupandishwa cheo kazini na kulipwa madeni au mafao yako pia na kumaliza kesi kabisa.

DUDUMA; Huongeza hips,makalio na mguu wa bia.

SWASWA: Hupunguza maziwa makubwa, kitambi, nyama uzembe, michirizi na muwasho sehem za Siri,na harufu mdomoni.

KOOLA;Hutibu magonjwa sugu ya zinaa, tumbo kujaa gesi,kuuma chini ya kitovu, kiuno ,fangasi za miguu, na kuvimba miguu au miguu kuwaka Moto.

Kwa hayo na mengineyo mfatilie DR.HINDU kwani ana uwezo wa kuhudumia ndani na nje ya TANZANIA.Kwa Dar es salaam anapatikana BUGURUNI MALAPA pia KAHAMA anapatikana MARUNGA.

Kwa wasio na mda wa kufika ofisini kwangu Nina vijana wa kukuletea mpaka ulipo kazini ama nyumbani kwako.

OFISI ZINAFUNGULIWA SAA 07 :00 ASUBUHI.

CONTACTS 0744 922 982(WhatsApp), 0716608959.

  "WOTE MNAKARIBISHWA".DR   HINDU NI SULUHISHO LAKO.

BREAKING: Zitto Kabwe Afikishwa Mahakamani

0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini ambaye pia ni Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe  amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Jijini Dar es Salaam  leo Novemba 2 akisubiri kusomewa mashtaka yanayomkabili  baada ya kushikiliwa na Jeshi la Polisi tangu Oktoba 31, 2018

Waziri Mkuu: Nimefarijika Na Maendeleo Ya Viwanda

0
0
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema amefarijika na maendeleo ya ujenzi wa viwanda kwenye mkoa wa Tanga kwa sababu vitasaidia katika ukuaji wa uchumi na kuongeza ajira.

Aliyasema hayo jana jioni (Alhamisi, Novemba 1, 2018) alipotembelea kiwanda cha saruji cha Rhino na kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh, vyote vya jijini Tanga.

Waziri Mkuu ambaye jana alihitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani Tanga, aliwapongeza wawekezaji wa viwanda hivyo kwa kuunga mkono mkakati wa Serikali.

Alisema Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kukuza uchumi kutoka wa chini hadi wa kati ifikapo 2025 kwa kupitia sekta ya viwanda.

Akizungumzia kuhusu kiwanda cha Rhino, Waziri Mkuu alisema kiwanda hicho na vingine vya saruji nchini vitasadia kupunguza gharama ya saruji nchini na kurahisisha ujenzi.

“Serikali inaamini kwamba uwepo wa viwanda mbalimbali nchini si tu utawezesha ukuaji wa uchumi wa Taifa, pia utasaidia katika kumaliza changamoto ya ajira hususani kwa vijana.”

Akiwa katika kiwanda cha Tanga Fresh, Waziri Mkuu aliwataka wafugaji mkoani Tanga wabadili mfumo wa ufugaji na wafuge kwa kutumia njia za kisasa ili waongeze uzalishaji.

“Wafugaji lazima wakubali kubadilika watumie fursa ya uwepo wa kiwanda hiki kwa kufuga kisasa ili wapate maziwa mengi kwa sababu wana uhakika wa kuyauza kiwandani hapa”.

Kadhalika, Waziri Mkuu aliwataka wananchi walioajiriwa kiwandani hapo wafanye kazi kwa bidii, uaminifu na wawe waadilifu na wasijihusishe na vitendo vya wizi kwa kuwa havina tija.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, NOVEMBA 2, 2018.

Updates: Zitto Kabwe Kasomewa Mashitaka Matatu ya Uchochezi

0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe asomewa mashtaka matatu ya uchochezi,  yenye nia ya kuleta chuki kwa Watanzania dhidi ya Jeshi la Polisi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Hata hivyo ,Zitto  amekana kwa kusema sio kweli na muda huu yupo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akisubiri uamuzi wa dhamana. 

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

0
0
Ni dawa pekee iliyotibu watu wengi nchini na nje ya nchini kwa kufanya kazi Mara 3 kwa wakati mmoja 1 ...kurefusha uume na kunenepesha saizi upendayo, kuogeza nguvu za kiume na inatibu matatizo , ikisha tibu aina madhara inaimalisha mishipa ilio regea na uzalishaji wa mbegu za kiume. TAHADHARI HAKIKISHA UNA MKE AU    MPENZI. 

NINI HUCHANGIA MATAZO HAYA . Ngiri ni chanzo Kikubwa cha matatizo,haya kujua kwamba una ngiri dalili zake ni 1.kufika haraka kileleni wakati  watendo la ndoa 
2.Kushindwa kulundia tendo la ndoa 
3.Kutoa choo kama cha mbuzi 
4. Tumbo kujaa gesi na kuunguruma 
5 kukosa choo kabisa 
6 Maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi 
7 korondani moja kuvimba 
8 kutosikia hamu ya tendo la ndoa
 9 maumivu ya kiuno na mgongo  

Pia tunatibu busha bila kufanyiwa opresheni .Umeachwa na umpendae na bado unamwitaji?

WASILIANA  NA MTALAM  CHALLO 0714 006521. YUPO MBAGALA.

Updates: Zitto Kabwe Kaachiwa Kwa Dhamana

0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo) ameachiwa kwa dhamana  ya milioni 10 na  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na ametakiwa kufika tena Mahakamani Novemba 26, 2018. 

Zitto Kabwe alifikishwa mahakamani leo  November 2  na kusomewa mashtaka matatu ya uchochezi,  yenye nia ya kuleta chuki kwa Watanzania dhidi ya Jeshi la Polisi. Hata hivyo ,Zitto  alikana mashitaka yote.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMBO ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744391089  au  0653182109

James Delicious Kadhaminiwa....Amber Rutty Na Bwana Yake Wamekosa Dhamana na Kupelekwa Gerezani

0
0
Video vixen, Amber Rutty  amesomewa makosa mawili ikiwemo kufanya mapenzi kinyume na maumbile.

Mbali na Amber Ruty washtakiwa wengine ni Said Bakary Mtopali na James Charles maarufu kama ‘James Delicious’.

Kwa pamoja washtakiwa wamesomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustino Rwezire na wakili wa serikali Nassoro Katuga.

Wakili Katuga amedai kuwa kosa la kwanza ni kufanya mapenzi kinyume na maumbile ambalo linamkabili Amber Ruty.

Inadaiwa ametenda kosa hilo kati ama baada ya October 25, 2018 ambapo alimruhusu Said Bakary Mtopali kumuingilia kinyume na maumbile, kosa ambalo amelikana.

Pia kosa jingine la kufanya mapenzi kinyume na maumbile, linamkabili mshtakiwa wa pili Said Bakary Mtopali ambapo anadaiwa kati ama baada ya October 25,2018 jijini Dar es Salaam alifanya mapenzi na Amber Ruty kinyume na maumbile ambapo alisema si kweli.

Kosa la tatu la kuchapisha video ama picha za ngono, ambapo linamkabili James Charles ama James Delicious akidaiwa kati ya October 25,2018 alisambaza video za ngono kupitia magroup ya Whatsapp.

Kosa jingine la nne ni kusababisha kusambaa picha za ngono linamkabili Amber Ruty na Said Abubakary Mtopali ambapo wanadaiwa kati October 25,2018 walisababisha kusambaza picha za ngono kupitia makundi ya Whatsapp. Kosa ambalo wamesema si kweli.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, Wakili Katuga amedai kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika wanasubiri taarifa za Kitaalamu kuhusu picha hizo za ngono za minato.

Washtakiwa wamepatiwa masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini 2 kila mtu na kusaini bondi ya Shilingi Milioni 15.

Pia wadhamini wawe na vitambulisho vya taifa pamoja na kuwasilisha hati zenu za kusafiria na msitoke nje ya Dar es Salaam bila ruksa.

Hata hivyo mshtakiwa James Delicious aliyefanikiwa kutimiza masharti ya dhamana, huku Amber Ruty na Said Bakary Mtopali wameshindwa kutimiza masharti na kupelekwa gerezani.Kesi imeahirishwa hadi November 12,2018.

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 24

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   

‘Ethan nisaidie, nipe uwezo basi rafiki yangu’
Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiwatazama wachezaji wa timu pinzani wakishangilia goli hilo. Kwa dakika hizi kumi na tisa za hapa awali wachezaji wezangu wote wamechoka na wamechoka na wanaonekana kukata tamaa kabisa. Tukaanza tena mpira huku nikijitahidi kukimbia kidogo na mpira na kupiga katika goli la wapinzani, ila mipira yangu haikuweza kufika kwani mabeki ni mahiri kwa kuzuia mipira ya juu. Dakika ya ishiri na mbili tukafungwa goli la tatu. Dakika ya ishirini na nane tukafungwa goli la nne. Dakika ta arubaini na tano tukafungwa goli la tano ambalo liliyafanya machozi yangu kushindwa kujizuia na kuanza kutiririka machoni mwangu kwani mchezaji wa timu pinzani aliwapiga chenga mabeki wanne na akampiga tobo kiba na kufunga goli hili na kwa dharau ya ajabu akaanza kupiga piga kifua chake kwamba sisi na mashabiki wetu hatuna chochote mbele yao.

ENDELEA
Kitendo cha kuanza mpira, refarii akapuliza kipenga akiashiria ni muda wa mapumziko. Tarati bu tukatoka uwanjani huku nikiinamisha uso wangu chini, kwani nina huzuni kubwa kwa kweli. Tukaingia kwenye vumba vya kubadilishia nguo. Kila mchezi hakika amechoka na hakuna ambaye anaonyesha ana matumaini ya kufanya vizuri.
“Goli ni tano hadi sasa”  
      
Kocha msaidizi alizungumza kwa unyonge sana huku akitutazama.
“Kipa namba moja hali yake kidogo sio nzuri. Kipa namba mbili ninakuomba ujitahidi sana kuwapanga mabeki wako. Katikati munapotea sana, mipira haimfikii Ethan. Jaribuni kupanda na si kukaa tu nyuma kusubiria mashambulizi”
Kocha alizungumza kwa msisitizo. Nikanyanyaka na kuingia bafuni huku nikiwa nimejawa na hasira.
‘Kama ni urafiki wenyewe wa kuniacha kwenye matatizo peke yangu ni bora uishie hapa’
Nilizungumza kimoyo moyo nikiamini kwamba Ethan yupo ananisikia. Nikamuoa akiwa amesimama mlangoni huku akicheka sana.
‘Ni nini kinacho kuchekesha?’
‘Leo mumekula maharage ya wapi?’
‘Ethan tambua kwamba sipo katika wakati wa utani, tumedhalika kipindi cha kwanza’
‘Ni kweli mume dhalilika, maelfu ya mashabiki wenu wamekuwa hoiii. Imani yao imepotea kabisa kwenu’
‘Kwa hiyo, nipe basi njia nijue ni nini nafanya ili niweze kufanikiwa?’
 
‘Hahahaa. Njia ni moja tu’
‘Ipi?’
‘Vua hicho kitambaa cha timu kapteni na umkabidhi kipa wenu na wewe ubaki kama mchezaji huru’
‘Kwa kufanya hivyo tutashinda au?’
‘Unaniamini au huniamini?’
Nikakaa kimya kwa muda huku nikimtazama Ethan usoni mwake.
‘Fanya hivyo la sivyo, leo mutaoga mvua ya magoli hadi muone dunia chungu’
‘Poa’
Nikavua kitambaa hichi kabla ya kutoka humu ndani, Ethan akanigusa kifuani mwangu kwa mkono wake wa kulia, nikahisi msisimko mkubwa sana kifuani mwangu. Uchovu ambao ulitokana na kukata tamaa, ukanipotea hali ya kujiamini na munkari vikanitawala. Ethan akanitazama kwa muda kidogo kisha akatingisha kichwa kunirudi nitoke ndani humu. Nikatoka na kuwakuta wachezaji wezangu wakiwa tayari wamesha simama kujiandaa kurudi uwanjani. Nikamuita kipa na kumvisha kitambaa cha timu kapteni.
 
“Kwa nini kapteni”
Kipa aliniuliza huku akinitazama.
“Hii ni moja ya mbinu ya kuwapa kiburi wapinzani wetu. Wakikuona wewe umevaa hichi watajiamini na kujisahau sana”
Kocha akanitazama kwa muda kisha akakosa cha kuzungumza.
“Tunakwenda kushinda, mumenielewa”
“Ndiooo”
Wachezaji wezangu waliitikia huku wakionekana kujawa na matumaini ya kupambana upya. Tukarudi kiwanjani huku baadhi ya mashabiki wakianza kutuzomea kwa kushindwa kufanya vizuri kipindi cha kwanza. Wapinzani wakaweka mpira kati na refarii akapuliza filimbi na mechi ikaanza upya. Nikamfwata mchezaji mwenye mpira na kwa kasi nikampokonya mpira miguuni mwake na kuanza kukimbia huku nikiwapita mabeki wao kirahisi sana, nikapaki mimi na kipa. Kwa mguu wangu wa kushoto nikapiga shuti moja zito lililo mbabatiza kipa na kumuingiza golini yeye na mpira wake. 
 
Uwanja mzima ukafurika kwa shangwe, Wajerumani wote wakanyanyuka, kwenye viti vyao, tukapeana mikono ya kupongezana na wachezaji wezangu huku nikiwahakikishia kwamba ni lazima tushinde. Wapinzani wetu wakaanza mpira kwa kasi, ila kwa bahati mbaya wakaponywa na mmoja wa mchezaji wetu, alicho kifanya ni kupiga mpira mrefu, nikaruka juu na kuutuliza kifuani mwangu. Mabeki wawili wakanifwata kwa pupa. Mmoja nikampiga tobo huku mwengine nikimpitishia mpira juu yake, huwa tumezoea kuita kitendo hichi ‘Kanzu’. Nikaaza kukimbia kwa kasi, nikia mita chache kutoka golini, nikajikunjua mguu wangu wa kulia na kupiga shoti moja la chini ambalo kiba alibaki akisimama akiutazama mpira na kukaingia nyavuni.
Nikakimbia kwa kasi, kisha nikaburuzika kwa magoti yangu kwa mita kadhaa kisha nikalala chali na wachezaji wezangu wakaniangukia kwa juu huku kila mmoja akiwa na furaha kubwa.
 
“ETHAN, ETHA, ETHAN’
Jina langu lilitawala uwanja mzima. Wachezaji wezangu wakazidi kupata nguvu na matumaini.
“Tumebakisha goli tatu sawa”
“Sawa sawa”
Shangwe zikazidi kuwachanganya wapinzani wetu, kwani kila walivyo jaribu kushambulia, wakakutana na safu ya mabeki walio tulia na kila mchezaji wetu aliye pata mpira akiwa eneo la nyuma, alicho kifanya ni kuupiga mpira mbele. Wyne ambaye ni mchezaji namba nane katika timu yetu, akapata mpira mmoja kutoka kwa beki namba tano, akaanza kuwakimbiza wapinzani wetu hadi eneo la kona. Akaingiza krosi moja, na Pinto bila ya makosa akaruka hewani na kupiga kichwa kizito kilicho ufanya mpira kuingia nyavuni, na kuinua shangwe za mashabiki wetu.
 
Tukamkumbatia Pinto kwa furaha sana, kwani tayari mashabiki wetu tumesha washika sehemu ambayo hata wao wamesha jawa na hofu.
“Bado mbili”
Nilizungumza huku nikipiga makofi ili kuwahimiza wachezaji wezangu. Kocha wa timu pinzani akabadilisha mabeki wa wili na kuwaingiza wengine ambao wana miili mikubwa kulio hata walio anza toka.
“Pinto kuwa makini wale wameingia kuzuia tu na wapo tayari kucheza rafu hata kumvunja mtu. Sawa”
“Nimekupata kapteni”
Wapinzani wakaanza mpira katikati ya uwanja. Wakajaribu kuleta mashambulizi ila Lukas, akamzuia mpira na kunipigia pasi ya chini ambayo sikutaka kuiweka mguuni mwangu hata kwa sekunde mbili, nikampasia Wyne. Wyne kwa kasi aliyo barikiwa na Mungu akaanza kuwafwata mabeki wawili walio ingizwa katikati ya boksi la mabeki. Beki mmoja pasipo kujua ni nini maana ya Wyne kufanya hivyo akajikuta akimchota kwa miguu yake miwili na Wyne akaanguka chini. Refarii pasipo ubishi, akaweka penati huku beki huyo akionywa kwa kadi ya njano.
 
“Wyne piga”
Nilizungumza kwani mimi ndio nimezoeleka kupiga petani zozote zinazo toke. Wyne akaweka mpira kwenye kidura maalumu cha kupigia penati. Wachezaji wote tukajipanga nje ya boksi la makipa tukisubiria Wyne apige penati hiyo. Wyne akarudi hatua mbili nyuma huku akishika kiono chake kwamikono miwili, akisubiria refarii kupuliza kipenga.
Refarii akapuliza kipenga, Wyne akapiga penati hiyo kwa bahati mbaya ikapiga mwamba wa pembeni kisha ikarudi katika eneo nililo simama mimi. Nikampasia Wyen mpira huo na akamalizia kwa kuupigia nyavuni na kufanya ubao wa matangazo kusoma goli nne kwa tano. Nikatazama ubao wa matangazo unaonyesha ni dakika ya sabini na mbili.
“Tubadilisheni mfumo, tucheze ule nilio waambia jana usiku sawa”
 
“Sawa kampteni”
Mpira ukanza huku wapinzani wetu wakipoteana kwa mashaka makubwa sana. Nikaletea pasi moja nzuri sana na nikaanza kukimbia pembenozi mwa uwanja kila beki aliye nifwata alijikuta akishindwa kunizuia, nilipo fika karibu na eneo la kona, nikapika krosi. Kama kawaida ya Pinto akaruka hewani na kupiga kichwa kimoja kizito kilicho ingiza mpira huo golini na sasa tukawa tupo sawa kimagoli na wapinzani wetu.
“Mechi tunashinda hii Ethan”
Pinto alizungumza huku akinikumbatia kwa furaha sana.
“Ndio tunashinda”
“Sikieni bado goli tatu za mwisho”
“Dakika ni ya themanini na mbili”
“Ndio zinatosha, Pinto utacheza nyuma yangu. Wyne Lukas na wengine hakikisheni hakuna anaye panda huko kwetu sawa”
 
“Sawa”
Wapinzani wakaanza mpira, kwa kasi nikamfwata mwenye mpira, katika kukabana ili niuchukue mpira nikampiga kipushi kidogo akaweweseka na kuacha mpira, nikaanza kukimbia kwa kasi yangu yote, nikaanza kumchenga mchezaji wa kwanza, wa pili, wakaja wawili nikawapita, akaja wa tano, nikampita akaja mchezaji wa saba nikampita, kisha nikabaki mimi na kipa tu, kipa akajaribu kinifwata huku akiliacha goli mita kadhaa, nikampiga chenga na kukimbia hadi kwenye mstari wa goli hili nikaukanyaga mpira huku nikiwatazama wachezaji na mabeki wao wanavyo kuja kwa kasi huku wakionekana kujawa na hasira sana. Walivyo nikaribia nikaupiga mpira kwa kisigino na ukaingia nyavuni.
Nikaanza kujipiga kifuani mwangu huku nikirudia ishara za unyanyasaji alio ufanya mfungaji wao mmoja mara baada ya kutufunga goli la kwanza kipindi cha kwanza.
 
Uwanja ukafurika kwa shangwe, timu pinzani wakazidi kunyong’onyea. Wakajaribu kupiga shuti golini, ila kipa akadaka mpira wa kwanza toka tuingie kipindi cha pili. Kipa akapiga mpira mrefu na ukanikuta nipo mita chache kabla sijafika katikati ya uwanja. Nikamtazama kipa wao na kumuona yupo mbele kidogo kutoka lilipo goli lao. Nikapiga shuti moja refu lililo ambaa ambaa hewani kipa akajaribu kurudi nyuma ili kuunyaka mpira huo ila akajikuta akichelewa na mpira ukaingia golini.
Nikasimama sehemu hii hii na wachezaji wazangu wote wakanifwata na kunikumbatia, kwani magoli kama haya yanafungwa na wachezaji wachache sana duniani.  Hadi tunafika mwisho wa mechi hii, tukaibuka na magoli saba huku nami nikiwa nimefunga magoli manne na nikakabidhiwa mpira ikiwa nikama pongezi ya kufunga magoli zaidi ya matatu.
 
“Hongera sana Ethan”
“Asante kocha”
Tukakumbatiana na kocha kwa muda kidogo kisha tukaendelea kushangilia upande wa mashabiki wetu. Waandishi wa habari kadhaa wakanifwata kwa ajili ya kunihoji maswali mawili matatu.
“Ethan unazungumziaje goli lako la mwisho ulilo funga”
“Nimoja ya goli la ndoto yangu, nilitamani siku moja nifunge vile na nikafanikiwa”
“Kwa sasa wewe ndio mchezaji unaye ongoza kwa goli nne, je utazidi kupanda au utabaki hapo hapo?”
“Hayo yote ni ya kumuachia mwenyezi Mungu, unajua mpira unaweza kusama unapanda na kesho ukapata majeruhi na ukashindwa kufanya chochote”
“Hongereni sana kwa mchezo mzuri ulio uonyesha natimu yako”
“Tunashukuru”
Nikasogea pembeni na wachezaji wengine wakaendelea kuhojiwa na waandishi mbalimbali. Pinto akanimwagia maji ayaliyomo kwenye chupa aliyo ishika na kunifanya nifurahi.
“Hongera kaka”
“Asante”
 
“Sikutarajia kama inaweza kuwa hivi”
“Yaa tumefanya kazi nzuri hata wewe hongera”
Nikaanza kutembea kueleeka kwenye vyumba vya kubadilishia nguo, mashabiki wakazidi kunishangilia kila nilipo pita. Mechi yetu ya leo unaweza kusoma ni kama fainali kwani tunafuraha kubwa sana.
“Kaeni tupige picha”
Nilizungumza huku nikiishika simu yangu, tukapiga picha kadhaa na timu nzima.
“Ethan”
Kocha aliniita huku akinitazama”
“Ndio kocha”
“Kuna pongezi”
“Kutoka wapi?”
“Kwa baba mkwe wako, ametwitte kupitia akaunti yake hii hapa”
Kocha alinionyesha ujumbe wa baba Camila aliio uweka kupitia akaunti yake ya Twitter. ‘Ni furaha kuwa na mkwe kama Ethan, naamini mwanangu hajakosea kuwa naye. Hongera sana Ehan Klopp na hongereni sana shule ya CJD Christophorusschule Königswinter’
 
Nikajisikia kufarijika sana mara baada ya kusoma ujumbe huu wa baba mkwe wangu ambaye yupo katika kampeni za kugombania uraisi wa nchi hii kupitia chama cha Social Democratic Party of Germany(SPD) na kama atashinda basi atatawala nchi hii kwa miaka mitano ya mwanzo kabla ya uchaguzi kufanyika tena.
“Shukrani kocha kwa kunionyesha”
“Asante nawe pia. Jamani tukitoka hapa inabidi kuelekea hospitali kwenye kumuona rafiki yetu Frenando sawa jamani?”
“Sawa kocha”
Tukaingia kwenye mabafu na kuanza kuoga huku tukiwa tumejawa na furaha. Tukavaa nguo tulizo kuja nazo na safari ya kuekejea hospitalini ikaanza huku basi letu likipata uzindikizwaji wa pikipiki moja polisi. Simu yangu ikaanza kuita na kwa bahati nzuri ni namba inayo toka nchini Tanzania, nikaipokea kwa haraka huku nikiwa na shauku ya kuisikia sauti ya Camila. Camila akaanza kwa kunipatia mabusu mototomo ambayo yaliyo ufanya mwili wangu wote kusisimka kimahaba.
 
“Nakupenda sana Ethan wangu”
“Nakupenda pia mpenzi wangu”
“Yaani sikuamini kama unaweza kutoa timu yako kidedea hakika sijakosea kuwa nawe Ethan nakupenda sana, tena sana mpenzi wangu na ninakuomba tukimaliza masome unioe”
Camila alizungumza kwa hisia kali sana huku nikihisi machozi yakimwagika.
“Etha nakuomba unioe”
“Nitakua mpenzi wangu”
Kelele za gafla zikaibuka kwenye basi na wachezaji wezangu wakaanza kunifwata kwenye siti niliyo kaa huku basi likifunga breki kali sana na kunisababisha hofu na mashaka makubwa sana kwani sijua ni kitu gani kilicho sababisha dereva kufunga breki za gafla.

==>>ITAENDELEA KESHO

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 134 na 135 )

0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   

Ndani ya muda alio niambia dereva tukawa tumefika katika hoteli moja kubwa, nikakuta mlolongo wa vijana wakike na wakiume wakiwa wamepanga mistari kwa ajili ya kwenda kujisajili katika mashindano haya ya kutafuta wana mitindo, na mimi nikapanga mstari nikiwa ni mshirikia wa elfu moja na mia mbili. Muda ukazidi kwenda na foleni ikazidi kosogea, vijana walipo katika eneo hili wapo wengi wamependeza, nikajitazama mweyewe nilivyo vaa na kimoyo moyo nikajishauri na kujiambia kwamba nina vigezo vya kuweza kushinda katika shindano hili.
   
ENDELEA       
Vijana wengi walio ingia katika chumba cha usahili wengi walitoka wakiwa katika hali ya huzuni, huku wengine wakilalamika kwamba majaji wanaringa. Hali hii ikaanza kunitisha kwani kazi yangu iliyo nileta hapa ni kuhakikisha kwamba ninakuwa karibu na Yemi Okocha. Ikafika zamu yangu, na mimi nikaingia katika chumba cha ushahili, nikakuta majaji wanne watatu wakiwa wa kiume na mmoja akiwa ndio Yemi mwenyewe niliye weza kumuona kwenye picha niliyo onyesha kipindi nilipokuwa kwenye kambi ya jeshi ya Wamarekani nchini Somalia.
“Peter umetuletea nini leo”
Yemi alizungumza huku akinitazama usoni mwangu, swali la Yemi naamini kwamba hili ndio alio wauliza vijana wengi na wameshindwa kwani wengine wao ambao wameweza kushindwa wamevalia vizuri sana.
 
“Peter, Peter”       
Yemi aliniita baada ya kuniona nikiwa nimeduwaa kwa sekunde kadhaa huku nikijishauri ni kitu gani ambacho ninaweza kukijibu.
“Naam”
“Umetuletea nini kipya hapa kama mwanamitindo chipukizi”
“Nimewaletea mbinu na namna ambavyo walinzi wa tajiri wanavyo takiwa kumlinda tajiri wao pale anapo vamiwa”
“Mmmmm kivipi?”
Jaji mmoja wa kiume aliniuliza huku akionekana kushangazwa sana kwa kile ambacho nimekizungumza.
“Ningemuomba jaji mmoja”
Majaji wakatazamana, akasimama jaji mmoja wa kiume aliye jazia mwili wake, akapiga hatua mbili mbele, ila Yemi akasimama na kumuomba jaji huyo arudi alipo kuwa amekaa kisha akanisogelea yeye.
 
“Haya nionyeshe ni jinsi gani unavyo weza kunilinda pale ninapokuwa nimevamiwa?”
Nikatazama kamera zaidi ya sita zilizopo ndani ya hichi chumba na zote zinachukua tukio hili. Nikasimama nyuma ya Yemi, ambaye kusema kweli ameumbika, umbo lake limejazia makalio ya wastani, amebarikiwa urefu wa futi kama sita na nukta zake.
“Mwanamitindo anatakiwa kuwa mbunifu wa hali ya juu, hili ninalo kwenda kulifanya hapa nitakuomba uwe makini sana kwani kidogo ni hatari”
“Wewe kuwa huru tu”
“Kwa mfano adui anatokea mbele yako na mimi ndio mlizi na nipo nyuma yako. Ninatakiwa kufanya hivi”
 
Kwa haraka nikamshika Yemi Okocha mabega yake na kumgeuza huku nikiwa nimemshika, akaangalia nilipo kuwa mimi, kisha na mimi nikawa sehemu alipo kuwa yeye huku mguu wangu wa kulia nikiwa nimeunyoosha usawa wa kiuno changu, nikimaanisha kwamba nimeweza kumzuia adui mwenye kisu. Yemi akiwa katika kushanga shangaa, nikampiga mtama huku nikutangulia kulala chini na akaniangukia kifuani mwangu, na kwa haraka nikamgeuza na kumlaza chini, ila nikahakikisha kwamba nguo yake hata moja haigusi chini kwani mkono yangu ilijitahidi kumshika kiunoni mwake. 
 
“Hapa ni pale gaidi anapokuwa amefyatua risasi na mlinzi anatakiwa kuhakikisha kwamba bosi wake anaanguka chini kwa usalama”
Nikamnyanyua Yemi Okocha juu na kumfanya ashushe pumzi kwani matukio yote hayo nimeyafanya katika sekunde ambazo nina uhakika hazizidi sitini. Jaji mmoja akaanza kupiga makofi, na kuwafanya wezake kumtazama kwa mshangaa kwa maana hata Yemi Okocha na yeye yupo katika hali ya mshangao mkubwa.
 
“Peter una kitu kikubwa ambacho vijana wengine walio kuja hapa sijapata kukiona”
“Kitu gani wakati alihitaji kumuangusha jaji mkuu?”
“Hapana jaji Ode. Peter anambinu ambazo vijana wengi wa kiume hapa wameingia wamejazia vifua, wamejazia mikono na kukata matumbo yao na kuwa six pack, ila hakuna anaye weza kufanya kama hichi anacho kifanya Peter. Chifu mkuu Peter ni aina ya wanamitindo wachache ambao tunawahitaji, yaani kwa mfano mdogo tu kama tukisema kwamba tunamtengenezea filamu Peter, kampuni yako jaji mkuu ninaamini kwamba itakwenda kuwa mara dufu na na hapa tulipo”
Yemi akanitazama kwa sekunde kadhaa usoni mwangu, kisha taratibu akaanza kutembea kuelekea kwenye kiti chake, akaka huku akihema kidogo.
 
“Jaji mkuu hapa sijaona kitu chochote kutoka kwa huyu Peter”
“Jaji Ode hicho unacho kizungumza ni ufinyu wa fikra, kama hamuamini, fundi mitambo hembu rudisha hili tukio niamini kwamba mutakuwa mumelirekodi vizuri”
“Jaji mkuu hakuna haja ya kurudisha nyuma sijui tukio alilo lifanya, kuna watu wengine nje wanahitaji kuingia ndani”
“Jamani nasema hivi kama hamjaona kitu kutoka kwa Peter na mukashindwa kunielewa kwa kile ninacho kizungumza basi ninawaambia, mimi nitajivua rasmi sasa hivi kisha nitamchukua mimi na nitamtengeneza chini ya kampuni yangu na mutaona ni kitu gani ambacho jamaa ayakifanya”
Yemi Okocha akanyanyua mikono yake juu kidogo usawa wa meza ikiwa ni ishara ya kuwanyamazisha majaji hawa wawili wanao bishana kuhusiana na mimi.
 
“Fundi mitambo hembu rudisha tukio alilo lifanya Peter”
Watu wote humu ndani tukaigeukia Tv kubwa iliyopo kwenye moja ya ukuta. Tukio nililo lifanya likaanza kuonyeshwa tena likiwa limepambwa na mziki mdogo wa filamu. Kusema kweli unaweza kusema ni tukio fulani ambalo lipo kwenye filamu, kwani hata makamera mani waliweza kutingisha vichwa vyao kwa kubaliana na tukio hilo.
 
“Mumeona, mumeonaa. Tazama jaji mkuu pale jinsi ulivyo geuzwa, tazama ulivyo lazwa chini pasipo wewe mwenyewe kujijua na wala kijiandaa. Tazama jinsi alivyo kushika kwa nguvu, hakuna hata nguo yako iliyo husa chini. Sasa hapo munasema munataka mwana mitindo wa ina gani jamani ahaaaaa”
Jaji huyu ambaye hadi sasa sijamjua jina lake ameonekana kunikubali kwa asilimia kubwa sana.
“Peter”
“Naam jaji mkuu”
“Sijapata ona, una kipaji cha hali ya juu. Safi sana”
Yemi Okocha alizungumza na kumfanya jaji huyu mwengine anaye nishabikia kunyanyuka na kushangilia sana, akanifwata sehemu nilipo simama, akanikumbatia huku akinipiga piga mgongoni mwangu.
 
“Nilisema huyu ni genius. Ode ulitaka watu wanao tukatizia katizia miguu hapa huku wakidunda dunda hahahaaaa”
“Umeshinda Joo”
“Peter elekea mlango ule”
Yemi Okacha alizungumza huku akionionyesha mlango ambao ni tofauti na mlango wa kutokea. Nikawashukuru huku nikiwa nimetabasamu, nikaingia katika chumba nilicho onyeshwa, nikawakuta washiriki wengine walio shinda na kuchaguliwa, huku nao wakitazama matukio yanayo tokea kwenye chumba walipo majaji. Kila kijana humu alinitazama sana, nikatafuta kiti na kukaa huku nikiwa nimejawa na furaha ila moyoni mwangu nikijipongeza kwani kazi yangu sasa imesha anza.
 
Kila alipo toka mshiriki mmoja kwenye chumba cha majaji, kipande cha video ya tukio langu na Yemi Okocha kinaonyeshwa kwenye hii tv kubwa tuliyonayo humu ndani.
    Baada ya masaa manne washiriki wakawa wamekwisha, ndani ya chumba hichi kwa haraka haraka tupo wanamitindo thelathini, wanawake wakiwa ni kumi na sita huku wanaume tukiwa kumi na nne. Yemi Okocha na jopo lake la majaji wakaingia ndani ya chumba hichi huku wakionekana wakiwa wamechoka sana.
“Tunamshukuru Mungu tumeweza kumaliza mchujo wetu kwa usalama, pia ninawashukuru nyinyi nyote kwa kuweza kufika leo na kupata nafasi hii ya kuwa chini ya kampuni yangu”
 
Yemi alizungumza kwa sauti ya upole, kisha akaka kimya kidogo na kuendelea kuzungumza.
“Kwa leo mutaweza kulala katika hii hoteli, kesho tutaondoka hapa na tunawaambia ni wapi ambapo mutakwenda. Ila kumbukeni kwamba nyinyi ni wamaitindo ambao ni wabunifu kama rafiki yangu Peter hapo, hadi sasa kipande chake cha ubunifu wake alio nionyesha kimetazamwa na watu zaidi ya milioni kumi katika chaneli yetu iliyopo katika mtandao wa YouTube.”
Wamaitindo waote wakapiga makofi ikiwemo na mimi, ila akilini mwangu ninatambua kwamba ni jambo la hatari kwani maadui zangu tayari wamesha weza kugundua ni eneo gani ambalo nipo.
“Yaani sikutegemea sana, ndani ya masaa matano kupata watazamaji wengi kama hao. Wazo la jaji Joo kwamba tumepata mtu kweli hapa tumepata mwanamitindo”
 
Jaji Joo akanikonyeza huku akitingisha kichwa, akionekana akiwa anafurahia uwepo wangu uliopo katika eneo hili.
“Basi sisi tuawatkie usiku mwema, jaji Joo atawaongoza hadi kwenye vyumba vyenu na baada ya hapo mutapelekwa kwenye sehemu ya kula”
“Tunashukuru”
Jamaa mmoja alizungumza, tukatoka katika chumba hichi na kuongozana na jaji Joo, na moja kwa moj tuaanza kuonyeshwa kila mtu chumba chake.
“Peter”
Jaji Joo aliniita baada ya kuingia katika chumba changu huku mimi nikiwa ndio mtu wa mwisho kabisa kuonyeshwa chumba changu cha kulala.
“Ndioo Jaji”
“Hongera sana kwa kile ulicho tuonyesha, hivi ulitoa wapi wazo hili?”
“Ahaa nimefikiria kwa haraka haraka, nikaona mbinu hiyo kidogo inaweza kunisaidia na kweli imenisaidia”
“Kazi nzuri Peter, ninauhakika ukijitahidi tutatengeneza pesa nyingi sana kupitia wewe. Ila kitu cha kuangalia hakikisha kwamba unasimamia kwenye maslai mazuri pale unapo ingia mkataba”
 
“Nimekuelewa katika hilo”
“Basi tuelekee eneo la chakula”
“Sawa”
Tukaongozana na jaji Joo hadi kwenye ukumbi wa chakula ambapo nikawakuta wanamitindo wezangu wakiendelea kula taratibu.
“Kaa tu hapa”
Jaji Joo alizungumza, nikaka kiti cha pembeni yake, nikaletewa chakula nilicho kihitaji, taratibu nikaanza kula huku kazi yangu ikiwa ni kuwasoma tabia zao wana mitindo wote waliomo ndani ya hichi chumba. Nilipo jirizisha na upelelezi wangu wa kimya kimya pasipo mtu kuelewa nikanyanyuka kwenye meza niliyo kalia na kuanza kueleka chumbani kwangu kujipumzisha kwani nimesha maliza kula.
“Hei Peter”
Dada mmoja mwembaba aliniita huku akinyanyuka kwenye kiti alicho kalia. Nikasimama kumtazama jinsi anavyo nifwata.
“Ndio”
“Naitwa Calx, kusema kweli nimevutiwa sana na wewe”
“Ninashukuru Calx”
“Ahaa naweza kupata namba yako ya simu?”
“Nitakupatia asubuhi kama huto jali”
“Kwa nini isiwe sasa?”
“Sawa unaweza kunipatia namba yako ya simu kisha nikakutafuta mimi?”
“Ndio”
 
Calx akanipatia namba yake ya simu kisha nikaondoka eneo hili na kurudi chumbani kwangu. Nikaufunga mlango kwa ndani, nikazima taa ya chumbani kwangu na kutazama kwenye kuta zote kama kuna taa nyekundu ya kamera yoyote ambayo inaweza kutegwa humu ndani. Nikainama hadi chini ya uvungu wa kitanda kutazama kama kuna maera, ila sikufanikiwa kuona chochote. Nikawasha taa na kuanza kutafuta kama kuna kinasa sauti chochote cha kutegwa, kwani katika hoteli kubwa kama hizi hususani kwenye mashindao ya namna hii vitu hivi hutegwa kwenye vyumba vya washiriki ili kufwatilai nyendo zao. Sikuweza kufanikiwa kupata chochote, ikanibidi kuanza kukipanga vizuri chumba hichi kwani nikekichagua vibaya.
 
Nikataka kupiga simu Marekai ila nikasita kwani bado nafsi yangu inakataa kabisa kuweza kuamini hichi chumba kwani watu ninao shuhulika nao wana akili nyingi sana na pasipo kuwa mjanja basi ninaweza kujikuta nikistukiwa mapema sana.
Nikavua nguo zangu, nikachukua taulo na kujifunga kiunoni mwangu, nikaeleka bafuni na kuanza kuoga taratibu huku nikipanga ni jinsi gani ninaweza kujifanya nionekane bora na kuaminika mbele ya macho ya Yemi Okocha ili kuhakikisha kwamba ninafanikiwa kumteka kiakili na kufahamu kile kilicho nileta huku Nigeria.
 
Nikafungua mlango wa bafuni na kutoka, nikasimama mbele ya kioo kikubwa huku nikiwa sin nguo hata moja, taratibu nikaanza kujifuta maji yangu kwenye jogoo langu, huku nikiendelea kujitazama. Gafla taa ya chumbani kwangu ikazima, pasipo hata mimi kuizima, kioo cha dirishani kikavunjika na akaingia mtu aliye valia nguo nyeusi tupu huku ameficha sura yamebaki macho tu huku mkononi mwake akiwa amshika panga refu jambo lililo nifanya nijipange kwa kujihami haraka iwezekanavyo.

AISIIIII……….U KILL ME 135


Mtu huyu akaanza kupiga hatua za kunizunguka jambo ambalo lililo nifanya na mimi nianze kuzunguka taratibu taratibu. Mtu huyu akaanza kunishambulia kwa kasi sana jambo lililo nifanya na mimi nianze kumkwepa kwa kasi sana huku nikiepuka sana asinikate na panga lake alilo lishika.
Katika kurupushani hizi na mtu huyu nikafanikiwa kumpiga teke la kifua nililo mfanya aanguke chini kama mzigo huku panga lake likiangukia pembeni. Sikutaka kumpa nafasi ya kunyanyuka, nikamuwahi na kumpiga kabali ya shingo huku nikijitahidi kuhakikisha kwamba ninamvua kitambaa alicho jifunika uso wake. Nikakutana na sura ya kiume ambayo sikuwahi kuiona kabisa tangu niweza kufika nchini hapa Nigeria.
 
“Ni nani aliye kutuma”   
Nilimuuliza huku nikiendelea kumkaba kwa nguvu.
“Sii……..”   
Ikanibidi kuendelea kuminya shingo yake hadi akapoteza fahamu. Kwa haraka nikanyanyuka  huku jasho jingi likinimwagika, nikapiga hatua hadi swichi, nikawasha taa ya chumbani humu, mandhari ya chumba hichi yamebadilika sana kwani ni vitu vingi vimeanguka na kuchanguka changuka. Nikajikota hadi lilipo taulo langu nikajifunga na kuingia bafuni. Nikanawa uso wangu na maji ya baridi huku nikipikijitazama kwenye kioo.
Nikarudi chumbani, nikaichukua simu yangu aina ya samsung na kumpigia Calix.
“Peter hapa”
 
“Waooo Peter, mambo vipi?”
“Nahitaji msaada wako”
“Msaada gani?”
“Njoo chumbani kwangu”
“Chumbani kwako?”
“Ndio ninakuomba msaada wako”
“Upo chumba namba ngapi?”
“Ahaa ni chumba namba………”   
Nilizungumza huku nikitembea kuelekea mlangoni, nikafungua mlango na kuchungulia kwenye kordo, sikuona mtu yoyote, nikatazama namba ya mlango wangu na kukuta ni namba mia tatu na tatu
“Nipo chumba namba mia tatu na tatu”
“Ok ninakuja”
“Sawa”
Nikaufunga mlango na kusimama pembeni ya mlango huku nikimtazama jamaa huyu aliye lala chini. Hazikupita hata dakika tano, malango ukagongwa kwa nje.
“Nani?”   
“Calx”
“Ok”
Nikafungua mlango na Calx akaingia, akaanza kushangaa jinsi vitu vilivyo changuka humu ndani, akamshangaa na mtu ambaye amelala chini.
 
“Mungu wangu, Peter kimetokea kitu gani hapa?”
“Nimevamiwa na huyu mtu hapa”
“Hajakumiza”
Calx alizungumza huku akinishika mwili wangu, akauchunguza vizuri huku akionekana kunishangaa.
“Hapana hajaniumiza”
“Itabidi tuwasiliane na uongozi wa hii hoteli”
“Unaonaje tukawasiliana na majaji walio tuleta hapa kwa maana mtu huyu ni jambazi kwa kweli”
“Sawa tena nina namba ya jaji mkkuu Yemi Okocha”
“Ninaomba umpigie”
Calx akatoa simu yake mfukoni na kumpigia jaji Yemi ambaye kwangu yeye ndio mtu muhimu aliye nifanya mimi kuweza kufika hapa.
“Habari madam unazungumza na Calx”   
“Sahamani kwa kukupigia simu usiku”
“Kuna jamaa sijui ni nani amemvami Peter”
“Ndio chumbani kwake na alikuja na panga kabisa”
“Sawa madam”
 
Calix akakata simu na kunitazama usoni mwangu.
“Madam anakuja sasa hivi”
“Sawa nashukuru kwa kumpigia simu”
“Usijali maisha ni ni kusaidianana”
“Kweli kweli”
Haukupita muda mrefu Yemi na walinzi wake wakaingia ndani ya chumba changu, nao pia wakaonekana kushangaa kuona jinsi chumba kilivyo changuka na jamaa huyu aliye lala chini na hadi sasa hivi hajapata nafuu.
“Upo salama kweli Peter?”
“Ndio jaji mkuu nipi solama”
“Ahaa pole sana”
Yemi Okocha akawapigia simu uongozi wa hii hoteli, ambao nao pia hawakuchukua muda mwingi awkafika katika chumba changu.
“Huyu mtu mbona kama ninamfahamu”
Muhudumu mmoja wa hoteli alizungumza huku akimtazama mtu huyu usoni mwake. Sote tukamtazama mtu huyu.
“Unamfahamu vipi?”
 
“Anaishi mtaani kwangu na ninasikia sikia kwamba ni jambazi na leo kama hivi amekamatwa”
“Hili swala inabidi tuwashirikishe polisi kwa maana hakuna mtu ambate anafahamu kwamba washiriki wangu kwa leo wanalala hapa”
Yemi Okocha alizungumza huku akimtazama meneja wa hii hoteli. Meneja huyu taratibua kamshika mkono Yemi na kusogea naye pembeni, mazungumzo yao hapakuwa na mtu aliye weza kuyasikia, ila mimi kazi yangu ikawa ni kutazama lipsi zao za midomo na nikafahamu kabisa ni kitu gani wanacho kizungumza. Meneja anaonekana kumuomba sana Yemi Okocha asilifikishe swala hili kwenye vyombo vya sheria, kwani linaweza kuiweka hoteli katika hali ya uchunguzi. Yemi akaniangalia kisha akanita kwa ishara taratibu nikawasogelea sehemu walipo simama.
 
“Peter meneja hapa ana aombi kwako, japo ameniomba mimi ila nikaona si vyema mimi kulichukulia maamuzi moja kwa moja nikaona ni vyema kukushirikisha”
“Zungumza tu hakuna tatizo”
“Kaka natambua kwamba umeweza kumdhibiti huyu jambazi, ila hili swala kama ikitokea tukawakabidhi askari linaweza kutuletea hali ngumu ya kibiashara. Wageni wataogopa kulala hapa watahofia kwamba ulinzi wa hii hoteli ni mdogo sana”
 
“Na kweli ni mdogo, hivi meneja, inakuwaje mtu anatoka huko alipo toka hadi hapa chumbani kwangu tena na kuvunja dirisha hili la kioo pasipo kuwa na mtu ambaye yumo ndani ya hii hoteli yako na ametoa mchongo kwa huyu jamaa na akihahisi kwamba kuna pesa kwa hawa washiriki?”
 
Swali langu likamfanya meneja kupatwa na kigugumizi na akakopoteza ujasiri wa kunijibu kabisa.
“Isitoshe kabla ya mtu huyu kuingia humu ndani alizima taa ya hichi chumba akiwa kwa nje, na kwa uelewa wangu tu wa kawaida, katika mahoteli makubwa kama haya, lazima kuna chumba kimoja ambacho kinashuhulika na maswala yote umeme, na hapa inaonekana kwamba muhusika wa kupanga mpango wa mimi kuvamiwa yumo ndani ya hii hoteli yako ukubali ama ukatae”
Nilizungumza kw amsisitizo huku nikimtazama meneja huyu.
“Meneja naona hadi sasa hivi hujazungumza kitu cha muhimu kinacho weza kumshawishi Peter na mimi nikisema kwamba nikutete, unaweza kumfanya Peter kunifikiria mimi vibaya wakati mimi wala sipo hivyo”
 
“Kweli ni…nimeelewa hapa, ila ninacho waomba huyu mtu mumshuhulikie nyinyi wenyewe kama mutaweza”
“Ahaa mimi ni mwana mitindo sio askari wala sio mwanajeshi, na walinzi wangu hawawezi kuifanya hiyo kazi, sasa unavyo hitaji tumshuhulikie unakosea meneja”
Yemi Okocha alizungumza kwa msisitizo huku akimtazama meneja usoni mwake.
“Jaji mkuu huyu tunaweza kumuhoji humu humu ndani”
“Peter utaweza kufanya hivyo?”
“Ndio jaji mkuu”
“Sawa”
Tukarudi alipo lala huyu jamaa, mlango ukafungwa kwa ndani na watu wote wakawa na kazi ya kunitazama mimi kuona ni kitu gani ninakwenda kukifanya. Nikamkalisha mtu huyu kwenye kiti nikashukua upanga  wake na kuushika mkononi mwake. 
 
“Niletee maji ya baridi”
Muhudumu wa hoteli hii akakimbilia hadi sehemu iliyo na friji ndogo humu ndani, akachukua chupa ndogo ya maji na kurudi nayo nilipo kaa, nikachomoa mkanda wa suruali yangu na kumfunga mikono yake kwa nyuma jamaa huyu kwenye kiti alicho kikalia.
Nikaifungua chupa ya maji na kuanza kumwagia usoni mwake, jamaa akakurupuka kwa haraka huku akihema, ikajaribu kunyanyuka ila akashindwa, akanza kutazama mtu mmoja ndani ya hichi chumba, alipo fikisha macho yake kwa muhudumu ambaye alisema kwamba amemtambua akastuka sana. 
 
“Moses”       
Muhudumu huyu alimuuita huku akiendelea kumshangaa. Jamaa kwa aibu akajikuta akitazama chini.
“Hei Moses”
Nilimuita huku nikimnyanyua uso wake, akajaribi kukikaza kichwa chake, nikamtazama Yemi Okocha, akanikonyeza na kuniruhusu kutumia nguvu ili azungumze ni nani ambaye amemtua kuja kunivamia mimi. Nikamyanyua tena sura yake ili anitazame ila akakikaza kichwa chake, sasa hivi sikuhitaki kumbembeleza zaidi ya kutandika kofi zito la shavu lililo wastusha watu wote humu ndani ya hichi chumba. Nikamnyanyua kwa nguvu uso wake na kumtazama usoni mwake.
“Ni nani aliye kuagiza kuja kufanya uvamizi humu ndani?”
“Nenda ka....  mama yako”
Jamaa alinitukana tusi lililo nifanya nitazame chini kwa sekunde kadhaa huku nikishusha pumzi kwani hatambui ni wapi mama yangu alipo, nikanyanyua uso wangu huku ukiwa umejaa tabasamu panasana jambo ambalo natambua halikutegemewa na watu wengi ndani ya hichi chumba.
 
“Nashukuru, na nitafanya hivyo Moses. Hembu tuambie ni nani aliye kutuma?”
Moses akakaka kimya, nikalitazama panga lake nililo lichika mkononi mwangu. Pasipo na huruma nikalipitisha kwa nguvu kwenye paja lake la mguu wake wa kulia huku nikiyagandamiza makali ya upanga wake kwenye hili paja lake jambo lililo mfanya apige kelele, Calx na muhudumu wakabaki wakifumba macho yao ila Yemi, meneja na walinzi wawili wa Yemi wakabaki wakiwa wamemkazia macho Moses.
“Ni nani aliye kituma uje kunivamia  mimi?”
Moses akaendelea kulia kwa uchungu huku damu zikizidi kumwagika, nikazidi kumkata paja lake huku nikigandamiza panga hili kwa nguvu kadri niwezavyo.
 
“Ni nani aliye kutuma?”
“NI…….ME…E……NEJA”
Watu wote ndani ya hichi chumba tukamgeukia meneja aliye anza kushangaa shangaaa huku akionekana woga umemtawala usoni mwake.
“Meneja?”
Yemi Okocha alizungumza huku akimtazama meneja kwa macho ya mshangao. Kwnai hili lililo tokea hapa ni jambo lililo tushangaza sisi sote. Kwa haraka meneja akamkaba Yemi Okocha kabali kwa nyuma huku akitoa kisu kidogo mfukoni mwake na kumuwekea Yemi Okocha shingoni mwake.
“Mtu yoyote akinisogelea nitamuua jaji wenu”
Meneja alizungumza kwa msisitizo, walinzi wa Yemi wakabaki wakiwa ameduwaa tu wasijue ni nini cha kufanya kwa kitisho walicho patiwa na meneja huyu ambaye hadi sasa hivi hatujui lengo lake ni nini haswa.

==>>ITAENDELEA KESHO

Alichokisema Zitto Kabwe Baada Ya Kuachiwa Kwa Dhamana Mahakamani

0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini na kiongozi wa Chama Cha ACT – Wazalendo, Zitto Kabwe amedai makosa anayoshtakiwa yanafanana na makosa ambayo walishawahi kushtakiwa baadhi ya waasisi wa bara la Afrika.

Kwa mujibu wa Zitto Kabwe, amedai kuwa kesi za namna hiyo ndizo zilizowahi kuwakumba baadhi ya waasisi, akiwemo muasisi wa Taifa la afrika kusini, Nelson Mandela pamoja na muasisi wa  Tanzania Mwalimu Julius Nyerere.

Akizungumza mara baada ya kupatiwa dhamana, Zitto Kabwe amesema ; “kesi za namna hii wamefungwa wakina mandela, na mwalimu kwa hiyo sio jambo linalopaswa kuwatisha watu. Ila nasikitika sana jana sikushiriki kongamano la chuo kikuu cha Dar es salaam.

“Naamini lazima tuweze kutoa tafsiri mbadala juu ya kile kilichotokea jana, pia niwatake watanzania tuwe na mshikamano ili kuhakikisha nchi yetu inakuwa imara.”

Mbunge huyo wa Kigoma mjini anashtakiwa kwa makosa matatu ya uchochezi, ambapo katika kesi yake upande wa Jamhuri unawakilishwa na Wakili, Tumaini Kweka na upande mshtakiwa unawakilishwa na wakili Peter Kibatala.

Zitto alikamatwa na Jeshi la Polisi jijini Dar es salaam oktoba 31 mwaka huu kufuatia mkutano wake na waandishi wa habari ambapo alitoa madai ya kuawawa kwa zaidi ya raia 100 katika Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma.

Kesi ya Mbunge huyo inatarajiwa kuendelea tena Novemba 12 mwaka huu.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya November 3

Serikali Kutobinafsisha Shirika La Bima La Taifa

0
0
Na. WFM ,  Dodoma
Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuliimarisha Shirika la Bima la Taifa (NIC) kwa kuliondoa katika utaratibu wa ubinafsishaji ambao uliwekwa awali.

Hayo yamebainishwa na  Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi Susana Mkapa, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango, wakati wa ufunguzi wa mkutano wa tisa wa baraza la Wafanyakazi wa Shirika la Bima la Taifa  Jijini Dodoma.

Bi Susana alisema kuwa, hatua za kuliondoa Shirika la NIC katika utaratibu wa ubinafsishaji zimefikia hatua nzuri ambapo utahitimishwa kwa kuandaa hati ya kisheria.

“Wizara ya Fedha na Mipango imeongeza muda wa mikataba ya kazi kwa watumishi kwa miezi mitatu, hivyo mawasiliano rasmi kuhusu mikataba hiyo yatafanyika, nawaomba watumishi muendelee kufanya kazi na kuwajibika wakati taratibu hizi za kuliondoa Shirika katika ubinafsishaji zikikamilika”. Alieleza Bi. Mkapa.

Vilevile alisema kuwa, maamuzi ya Mashirika na Taasisi za Serikali kupata huduma za Bima kupitia Shirika la Bima la Taifa ni ya Kisera na yanahusisha mamlaka mbalimbali, hivyo amelitaka Shirika hilo liendelee kufanya kazi kwa ushindani, kuongeza ufanisi, ubunifu na kuondokana na fikra za kufanyakazi kwa mazoea.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa NIC Bw. Sam Kamanga alisema kuwa baadhi ya Taasisi na Mashirika ya Umma yanasita kutumia Bima za Shirika hilo kwa kuwa hakuna tamko rasmi ambalo linasimamia utekelezaji hivyo kuiomba Serikali  kutoa tamko hilo.

Pia ameiomba Serikali kuliongezea Shirika hilo mtaji kwa kuwa uliopo wa kiasi cha Sh. bilioni 2.9, ni mdogo na haukidhi katika kuimarisha Shirika hilo kwa utoaji wa bidhaa mbalimbali kulingana na uhitaji wa Soko.

Naibu Katibu Mkuu Bi Susan Mkapa alilipongeza Shirika la NIC kwa kuwa na Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi ambao utekelezaji wa matakwa ya sheria na kanuni zinazosimamia mahusiano kazini kati ya Menejimenti na wafanyakazi, na ushirikishwaji katika uendeshaji wa Taasisi, hivyo akawataka watumishi hao kuhakikisha wanatoa ushauri utakao imarisha taasisi hiyo na kusaidia kufanikisha malengo ya maendeleo ya Taifa.

Imetolewa na :
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedha na Mipango

Serikali Yataka UNESCO Kutoa Takwimu Za Mauaji Kwa Nchi Badala Ya Jumla

0
0
Na Ahmed Mahmoud Arusha
Serikali  imelitaka shirika la kimataifa ,Elimu ,Sayansi na Uchumi (UNESCO)kutoa takwimu sahihi juu ya matukio ya waandishi wa habari kufanyiwa vitendo vya unyanyasaji na mauaji kwa kila nchi tofauti na kutoa takwimu za jumla ili kuangalia ukubwa wa jambo hilo kwa kila taifa.

Waziri wa Habari,Sanaa,Utamaduni na Michezo,Dkt ,Harrison Mwakyembe ameyasema hayo katika mkutano wa kimataifa unaowashirikia waandishi wa habari kutoka nchi za ukanda wa kusini mwa jangwa la sahara (SADC)katika siku ya kutathmini vitendo vya unyanyasaji na mauaji dhidi ya waandishi wa habari dunia uliondaliwa na Unesco jijini hapa.

Amesema takwimu zilizotolewa na UNESCO zinazoonyesha kuwa waandishi wa habari wapatao 1010 waliuawa katika kipindi cha miaka 10 iliyopita,jambo ambalo halifafanui kiwango cha ukubwa kwa Kila nchi zilizokumbwa na Kadhia hiyo .

Aidha amesema kuwa Umoja wa mataifa umetenga siku ya Tarehe 2 kila mwaka kuadhimisha siku ya kupinga vitendo vya unyanyasaji,uzalilishaji na mauaji kwa wanahabari kote ulimwenguni lakini matatizo hayo yamekuwa yakijirudia bila kuyapatia ufumbuzi jambo ambalo ametaka takwimu za kila nchi zikabainishwa ikujua uwiano ili kupima ukubwa wa tatizo.

Awali akiongea kwenye mkutano huo Mkurugenzi wa Unesco Kanda ya Afrika mashariki Johnbosco Mayiga amesema kuwa katika kipindi cha miaka kumi jumla ya wanahabari wapatao 1010 waliuawa katika nchi mbali mbali duniani na hivyo kuongeza ukubwa wa vitendo vya ukatili kwa wanahabari kukosa uhuru na usalama wawapo katika utekelezaji majukumu yao.

Katika Mkutano wa Unesco uliofanyika mwaka jana jijini Nairobi uliazimia kila nchi kuangalia utaratibu gani wa kufanya ili kuwajengea mazingira mazuri ya utendaji kazi kwa waandishi wa habari ikiwemo kuwa na chombo cha kuwalinda.

Pamoja na Mambo mengine mkutano huu utalenga kuangalia utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa Nairobi ikiwemo ni hatua zipi ziweze kuchukuliwa katika kuhakikisha muandishi wa habari anatekeleza majukumu yake katika mazingira salama.

Kwa Upande wake Mkurugenzi wa chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania (Tamwa) Bi Edda Sanga amesema kuwa kitu alichokipenda katika mkutano huo ni mgawanyo wa  wa wajumbe na kuwa mwandishi si elimu pekee na ujuzi wa kazi utakaosaidia utendaji kazi wake

Amesema kuwa vyombo vya habari vina nguvu kubwa ya kutupeleka katika hatua kubwa ya maendeleo iwapo kutakuwa na mazingira mazuri kwa wanahabari na kutekeleza majukumu yao kwa weledi .

Waziri Mkuu: Tutahakikisha Wananchi Wote Wanapata Maji

0
0
*Aagiza vijiji vyenye shida ya maji Bumbuli vibainishwe

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali itahakikisha wananchi katika vijiji vyote nchini wanapata huduma ya safi na salama wakiwemo na wa jimbo la Bumbuli.

Pia, Waziri Mkuu amemuagiza Mhandisi wa Maji wa Halmashauri  ya Bumbuli, wilayani Lushoto, Charles  Boy afanye utafiti na kubainisha vijiji vyenye shida ya maji Bumbuli.

Amesema baada ya kuvibaini vijiji hivyo, anatakiwa aweke mpango wa kuhakikisha navyo vinapata huduma ya maji safi ili kuwaondolea wananchi tatizo hilo la ukosefu wa  maji.

Alitoa agizo hilo Alhamisi, Novemba 1, 2018 wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Mponde jimbo la Bumbuli, Lushoto.

Waziri Mkuu ambaye jana alihitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani Tanga, aliwapongeza wakazi wa wilaya ya Lushoto kwa kutunza mazingira na vyanzo vya maji.

Alisema Serikali ya Awamu ya Tano ina mikakati mizuri inayolenga kumaliza tatizo la upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo yote yenye changamoto hiyo nchini.

“Serikali kupitia Kampeni ya Rais Dkt. John Magufuli ya kumtua mama ndoo kichwani, itahakikisha wananchi katika maeneo yote nchini wanapata huduma ya maji safi na salama.”

Waziri Mkuu aliongeza kuwa upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi ni miongoni mwa vipaumbele vya Serikali, hivyo aliwataka wananchi waendelee kuiamini Serikali yao.

Awali,Naibu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso alisema Serikali imetenga fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi, ukarabati wa miradi ya maji, ambapo mkoa wa Tanga umetengewa sh. bilioni 13.

Aweso alitumia fursa hiyo kutoa rai kwa wakandarasi wanajenga miradi ya maji wazingatie viwango vya ubora kwa kuwa Serikali inatumia fedha nyingi katika kugharamia miradi hiyo.

“Serikali inatoa fedha kwa ajili ya miradi ya maji alafu mnazitumia kujengea majumba na kununua magari, safari hii mtazitapika tunataka miradi itekelezwe kwa kuzingatia viwango.”

Waziri huyo aliahidi kufuatilia kwa kina ujenzi wa miradi yote ya maji nchini ili kuhakikisha kama inalingana na thamani halisi ya fedha zinazotolewa katika miradi hiyo.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Maiti Zaendelea Kuokotwa Kando ya Reli Dar

0
0
Shirika la Reli Tanzania (TRC), limeeleza kushtushwa na maiti ambazo zimekuwa zikiziokota mara kwa mara kwenye njia ya reli.

Limesema kwa wiki iliyopita pekee zimeokotwa maiti mbili kwenye njia hiyo ya reli maeneo ya Gongo la Mboto, Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika hilo, Focus Sahani, alisema jana kuwa wahusika walizitupa maiti hizo kwenye reli kama ujanja kuonyesha kwamba watu hao waligongwa na treni.

Alisema shirika hilo limekuwa likiokota maiti kwenye reli hiyo kila mara vitendo ambavyo vinawashtua kwa kuwa hawajui wahusika wanafanya hivyo kwa lengo gani.

"Sasa hivi kumejitokeza matukio mengi tu unakuta wengine wamewekwa relini, watu wanamfanyia mtu kitu kibaya huko wanamtupa kwenye reli ionekane kama amegongwa na treni," alisema.

Alisema maiti hizo hadi sasa hazijafahamika zinatupwa na watu gani kwenye reli.

"Wanaua mtu huko wanamleta kwenye reli wanamuacha hapo ili kuonyesha kuwa amegongwa. Wanafanya hivi ili kuondoa ushahidi wiki iliyopita peke yake tumeokota maiti mbili na matukio ya aina hii yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara," alisema.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images