Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 23

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA 
 Kabla sijamjibu kocha simu yake ikaingia meseji. Nikaa kimya huku nikimtazama kocha anavyo soma meseji hiyo. Akashusha pumzi huku akinikabidhi simu simu yake ili niisome meseji hiyo.
‘Shule haito husika kwa chochote kwenye swala la mshahara wako wa ukocha, malezi na matumizi ya timu yako la sivyo jiudhuru ukocha tumuachie huyu mpumbavu timu tuoneka kama ataweza kuiongoza. Bili ya hotelini, leo ndio itakuwa siku yenu ya mwisho kukaa, nimeisitisha na muthithubutu kurudisha miguu yenu kwenye hiyo hoteli sawa Robert’
“Kocha ni nani huyu?”
“Mwalimu mkuu wenu”
Nikajikuta nikiachia msunyo mkali sana kwani sijui ni kitu gani mwalimu mkuu huyu anakifikiria kwenye ufahamu wake wa akili hadi kuamua kumshinikiza kocha kuacha ufundishaji wa timu hii.

ENDELEA
“Usijali, nakuomba usimueleze mchezaji yoyote kuhusiana na hili swala. Ngoja niwasiliane na dada yangu ili aweze kushuhulika na hili swala”
“Sawa”
“Ila ushindi wowote utakao patikana asilimia hamsini itakuwa yangu na zifwatazazo zitakuwa kwa ajili ya timu na hakuna hata asilimia itakayo ingia kwenye akaunti ya shule umenielewa?”
“Nimekuelewa”
Tukaingia kwenye gari na nikakaa kwenye siti aliyo kaa Frenando.
“Vipo kocha anasemaje?”   
“Ngoja tutazungumza tukipata muda”
“Sawa”
 
Nikatoa simu yangu mfukoni na kuingiza namba ya dada Mery kisha nikampigia. Simu yake ikaanza kuita na baada ya muda kidogo ikapokelewa.
“Ethan”
“Naimbie dada yangu”
“Safi, nasikia upo kwenye kiosi cha timu ya shule yako”
“Ndio dada. Upo wapi?”
“Mimi ndio ninajiandaa kutoka hospitalini hapa. Vipi?”
“Kuna jambo moja nahitaji kukuomba unisaidie”
“Zungumza tu mdogo wangu”
“Nahitaji uniwekee oda kwenye hoteli nzuri, nina idadi ya wachezaji ishirini na mbii pamoja na kocha mmoja”
“Ahaa sawa hilo halina shida kuna la ziada?”
“Hapana ni hilo tu, ila hoteli iwe ya kimichezo, viwepo viwanja vya michezo”
“Sawa sawa, nimekuelewa ndani ya dakika tano nitakupatia jibu lako”
 
“Poa”
Nikakata simu kisha nikasimama katikati ya basi hili, wachezaji wezangu wote wakanitazama.
“Naomba tusikilizane ndugu zangu”
“Kunzia hivi tunavyo toka hivi sasa. Hatuto rudi kwenye hoteli hiyo. Moja ni kutokana na maswala ya usalama wetu kwani kwa tukio la jana nina imani kila mmoja wetu emekuwa ni mtu mwenye wasiwasi na mashaka. Tumeamua kutafuta hoteli nyingine kwa garama zangu, na kila huduma ambayo timu kama timu itahitaji basi nipo tayari kugaramia”
Wachezaji wezangu wote wakapiga makofi na kushangilia
“Ngoja niwaeleza kitu kimoja. Ninawapenda sana”
“Hata sisi tunakupenda kapteni”
“Tunakwenda kupambana na tuhakikishe kwamba tunashinda sawa jamani”
“Sawa”
 
Wachezaji walitikia na mmoja wao akianzisha nyingo za kushangilia. Gari likafurika kwa shangwe huku kila mchezaki akipata munkari wa kwenda kucheza mechi iliyopo mbele yetu. Simu yangu ikaanza kuita, nikaipokea kuiweka sikio la upande wa kuhosto huku na nikiziba sikio la upande wa kulia ili niweze kumsikiliza dada Mery atazungumza kitu gani.
“Mbona makelele?”
“Utawaweza wachezaji, niambie umefanikiwa?”
“Ndio nimefanikiwa kupata hoteli moja ila ipo nje ya mji, ina kila sifa ulizo zihitaji”
“Hembu nitumie picha zake”
“Sawa, mechi munaanza kucheza saa ngapi?”
“Mida ya saa kumi na moja jioni”
“Ahaa sawa, nitafanikiwa kuiwahi kwa maana hivi sasa ninaelekea kwenye hiyo hoteli na wamehitaji kulipwa dola elfu ishirini na tano kwa siku”
“Sawa hilo halina tatizo, kikubwa iangalie na kama ipo vizuri muambie muhasibu atoe pesa hiyo kwenye akaunti yangu”
“Poa”
 
“Vipi mama?”
“Yupo vizuri hapa anategemea kuangalia mechi yenu”
“Poa badae basi”
“Poa”
Nikakata simu na kuzisubiria picha za hoteli hiyo. Baada ya muda kidogo picha hizo zikaingia kwenye simu yangu, nikamuonyesha Frenando.
“Duu hapa pazuri kaka”
“Eti ehee?”
“Yaa hapa pazuri kuliko hata pale”
“Poa poa”
Tukafika katika uwanja mkubwa wa mpira wa Olympiastadion Berlin ambao ndio shuhuli za ufunguzi wa kombe hili zinafanyika. Uwanja huu unaingiza mashabiki zaidi ya 74,475 kwa wakati mmoja. Basi letu likasimama katika eneo maalumu na sikuamini macho yangu baada ya kukuta idadi kubwa ya mashabiki ambao ni watu wazima wakiwa wamekusanyika kuipoke timu yetu. Waandishi wa habari ambao ni wengi sana wakaendelea kupiga picha mbalimbali huku wengine wakirekodi kila kinacho endelea. Tukashuka hutu nikuwa tumevaa makoti ya jezi zetu za shule.
 
“Ethan Klopp, Ethan Klopp”
Baadhi ya waandishi wa habari waliniita kwa ajili ya mahojiano. Nikasimama na wakanizunguka huku wakiniwekea vinasa sauti karibu na mdomo wangu.
“Kwanza poleni sana kwa kile kilicho tokea kwa kocha wenu”
“Tunashukuru sana”
“Je mumejiandaaje kwa mechi ya leo pasipo kuwa na kocha mkuu”
“Mimi na wachezaji wezangu tumejiandaa vizuri sana na nina imani kwamba tutawapa mashabiki wetu kitu kizuri kile wanacho kitarajia kutoka kwetu”
 
“Nimepata habari ya chini ya kapeti, ni kweli shule imejitoa katika kuihudumia timu kutokana na tukio la kukosekana kocha mkuu?”
Nikaka kimya huku nikimtazama muandishi huyu, nikatabasamu kidogo.
“Hapana ni uongo mtu. Kama shule ingejitoa katika kuhudumia timu basi leo hii tusinge kuwepo hapa”
“Mbona kuna hii meseji hapa imetoka kwa mwalimu mkuu wako, alininitumia na kudhibitisha kwamba shule imekata huduma zote juu ya timu yenu?”
“Kwa mimi hilo sifahamu na sina maoni juu ya hilo”
“Je mutafanikiwa kushinda kwa mbinu za kocha msaidizi?”
“Kija kitu ni mipango. Asanteni”
 
Nikaanza kuondoka na wakaanza kunifwata ila wakazuiwa na askari wanao imaeisha ulinzi katika eneo hili. Tukaingia kwenye vyumba vya kubadilishia mazoezi na kukuta jezi zetu zikiwa zimepangwa vizuri kila mtu kwenye sehemi yake. Tukabadilisha nguo, zetu na kuvaa jezi hizi na viatu.
‘Ethan’
Niliisikia sauti ya Ethan mwenzangu, nikaangaza macho ndani ya chumba hichi ila sikuweza kumuona.
‘Upo wapi?’
‘Siwezi kujitokeza kwenye kundi hili la watu’
‘Vipi?’
‘Leo jitahidi kwani timu pinzani ina mikakati mizito dhidi yenu na inaweza kuwa moja njia ya kuwadhalilisha’
 
‘Kutudhalilisha tena?’
‘Ndio’
‘Kivipi?’
‘Mutakwenda uwanjani utajionea’
‘Unanipa presha rafiki yangu’
‘Usijali’
‘Ethan’
Ethan hakuitika na ukimya ukatawala ndani ya nafsi yangu. Nikaendelea kumtazama kocha jinsi anavyo endelea kupanga mipango yake ya jinsi gani tuweze kucheza.
“Hei mbona unaonekana kama huna raha?”
Frenando aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.
“Hakuna ninawazia tu mechi”
“Usiwaze sana, tunakwenda kuwafunga hawa wajinga”
“Nakuomba usiruhusu goli Frenando”
“Usijali kaka”
 
Tukaendelea kukaa ndani ya chumba chetu hichi, tukisubiria maonyesho kadhaa yaweza kumalizika uwanjani. Saa kumi na moja kasoro kumi tukatoka ndani ya chumba chetu cha michezo na kuelekea katika mlango wa kutokea. Wachezaji wengi wa shule hii kutoka Italy ni warefu na wana miili mkubwa kiasi cha kuwafanya baadhi ya wachezaji wezangu kujawa na hofo. 

Kama timu kapteni nikaka mbele ya mstari huku nuyuma yangu akinifwatia Frenando na wengineo. Kocha msaidizi na madaktari wa timu wakatangulia uwanjani. Refa na wasaidizi wake wawili, wakasimama mbele kabisa na ilipo timu saa kumi na moja kasoro tano tukaanza kutembea na kutoka uwanjani humu. Uwanja mzima umejaa mashabiki wengi sana na katika maisha yangu sijawahi kucheza mpira kwenye wingi wa mashabiki wengi kama hawa.
 
‘Ehhh Mungu nisaidie’
Nilizungumza huku mapigo ya moyo yakiniende kasi. Hata mimi mwenyewe wasiwasi mwingi umenijaa moyoni mwangu. Tukapanga mstari mmoja, na sisi kama wenyeji, tukaanza kuwapa mikono marefa kisha tukafwatia wachezaji wa timu pinzani. Kila mchezaji ninaye mtazama naona ananizidishia wasiwai mwingi san. Baada ya kuwamaliza kuwapa mikono wapinzani wezetu, nikawaita wachezaji wezengu na kukusanyika duara moja.
 
“Hei jamani hawa wana ukuwa tu wa miili ila nina imani tunakwenda kushinda sawa”
“Sawa kapteni”
“Kapteni tayari kule”
Mchezaji mmoja alizungumza huku huku akinionyesha sehemu walipo simama marefarii. Nikakimbilia katika eneo hilo na kukuana na kapteni wa timu pinzani. Refarii akatuonyesha shilingi yenye pande mbili huku akituomba kila mmoja achague upande wake.
“Kichwa”
Nilizungumza huku nikimtazama refa, akairusha shilingi hiyo juu kisha akaibana na viganja vyake. Kwa bahati timu yangu inaanzia upande wa mashariki mwa uwanja huku tukupeleka mashambulizi kaskazini mwa uwanja.
 
“Asante”
Nilizungumza huku tukibadilishan nembo za shule na mpinzani wangu. Tukawa marefarii mikono pamoja na wasaidizi wao na kwa ishara nikawaomba timu yangu tuelekee upande wa mashariki. Tukapiga picha ya pamoja na kila mchezaji akatawanyika upande wake huku mimi nikisimama peke yangu katikati ya uwanja nikiwa na mpira kwa ajili ya kuanzisha mpira huu. Refarii akatazama saa yake ya mkononi na ilipo timia saa kimi na moja kamii akapiga kipenga cha kuanzisha mpira. 

 Nikampigia Pilo na taratibu tukaanza mchezo huu huku wapinzani wetu wakitufwata kwa kasi, kwa bahati mbaya mchezaji mwezetu mmoja akapokonywa mpira. Wapinzani wezetu wakimbia kwa kasi kuelekea golini kwetu na mmoja wao akapige shuti moja kubwa sana, Frenando akajaribu kulifwata kwenye pembe ya goli, ila akashindwa kuuzuia kwa mkono mmoja na mpira ukaingia nyavuni.
 
Robo ya uwanja wakanyanyuka na kushangilia, nikatazama saa kubwa hapa uwanjani ndio kwanza ni dakika ya pili. Nikastuka mara baaya kuwana mabeki wakiwa wamemzunguka Frenando, kwa haraka nikakimbilia hadi golini na kumkuta Frenando akilia kwa uchungu huku akiwa ameshika kiganja cha mkono wake wa kulia. Nikamvua gloves ya mkono huo, kidole kimoja cha mwisho cha Frenando kimefunjika jambo ambalo ni pigo kubwa kwetu kwani ndio kipa tegemezi naninaye muamini. Refarii akafika eneo hili huku madaktari wetu nao wakifika wakaanza kumpa Frenando huduma ya kwanza.
 
“Siwezi kuendelea”
Frenando alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake, jambo lililo nifanya na mimi machozi kunilengea lenga usoni mwangu. Nikatazama nje ya uwanja na kumuona kipa namba mbili akijiandaa na kipa huyu udhaifu wake mkubwa ni kunyaka mipira ya chini, huwa hajiwezi kabisa kuruka chini. 
 
‘Ethan upo wapi?’
Nilimuita Ethan mwezangu ila hakuweza kuitikia, nikajiona kwenye tv kubwa la hapa uwanjani jinsi nilivyo jawa na wasiwasi mwingi sana. Frenando akatolewa uwanjani hapa kwa kigari maalumu na kukimbizwa hospiyalini kwa matibabu zaidi. Akaingia kipa namba mbili anaye itwa Antoniyo Jr.
“Hakikisha huonyeshi udhaifu wako sawa”
Nilizungmza na kipa huyu huku nikimtazama usoni mwake.
“Sawa kapteni.”
 
Tukaanza mpira kwa kasi sana huku nikijitahidi kupeleka mashambulizi mbele, ila zaidi ya wachezaji wanne wananikaba mimi peke yangu na kunifanya nipate wakati mgumu wa kumiliki mpira hata kwa sekunde kumi. Kila nilivyo jaribu kutoa pasi kwa Pilo, hakuweza naye kutembea kwani kuna benki mmoja mkubwa anamzuia. Katika maisha yangu ya mpira leo ndio siku ambayo ninajihisi kukata tamaa mwanzo tu mwa mechi. 

Wachezaji wezangu hapo katikati ya uwanja wamepoteana kabisa, kwani wachezaji wanao cheza kati wa timu pinzani wana uwezo mkubwa, kwanza kumiliki mpira na pili kupiga chenga. Dakika ya kumi na tisa tukafunga goli la pili, tena kipa alipigiwa shoti lililo mchanganya akaruka upande mwengine na mpira ukaingia upande mwengine.
 
‘Ethan nisaidie, nipe uwezo basi rafiki yangu’
Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiwatazama wachezaji wa timu pinzani wakishangilia goli hilo. Kwa dakika hizi kumi na tisa za hapa awali wachezaji wezangu wote wamechoka na wamechoka na wanaonekana kukata tamaa kabisa. Tukaanza tena mpira huku nikijitahidi kukimbia kidogo na mpira na kupiga katika goli la wapinzani, ila mipira yangu haikuweza kufika kwani mabeki ni mahiri kwa kuzuia mipira ya juu. 

Dakika ya ishiri na mbili tukafungwa goli la tatu. Dakika ya ishirini na nane tukafungwa goli la nne. Dakika ta arubaini na tano tukafungwa goli la tano ambalo liliyafanya machozi yangu kushindwa kujizuia na kuanza kutiririka machoni mwangu kwani mchezaji wa timu pinzani aliwapiga chenga mabeki wanne na akampiga tobo kiba na kufunga goli hili na kwa dharau ya ajabu akaanza kupiga piga kifua chake kwamba sisi na mashabiki wetu hatuna chochote mbele yao.

==>>ITAENDELEA KESHO

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 132 na 133 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   
   
Mbele yangu kuna dada wa kizungu ameshika kioo kikubwa kiasi akijipamba nyusi zake, nikabahataika kupata upenyo mdogo wa kuangalia mtu aliye nyuma yangu, nikajikuta nikistuka baada ya kuona jamaa wawili wa kiarabu wenye ndevu nyingi wakiwa nao wamesimama kwenye hii foleni. Nikavuta kumbukumbu kwamba ni wapi nilipo waona jamaa hawa wawili. Kumbukumbu zangu zikaangukia katika kambi ya Al-Shabab, na mmoja kati ya hawa jamaa alikuwa ni mlinzi wa baba Hawa, sijafahamu ni wapi wanapo elekea ila mstari ambao nipo mimi sote tunapanda ndege moja, hapa ndipo nikaanza kupata wasiwasi mkubwa sana juu ya hawa jamaa kama hawapo hapa kwa ajili ya kutoroka basi wapo hapa kwa ajili yangu kwani mimi ndio muharibu mkubwa wa kambi yao.
           
ENDELEA   
Taratibu foleni ikazidi kusonge mbele, dada huyu wa kizungu akamaliza kujipamba uso wake na kurudisha kioo chake ndani ya pochi yake. Ikafika zamu yangu, nikakabidhi hati yangu ya kusafiria pamoja na begi langu, nikaliweka katika mkanda maalumu wa kukagulia mizigo.
“Karibu muheshimiwa”
Kijana huyu wa hapa uwanja wa ndege alizungumza huku akinikabidhi hati yangu ya kusafiria.
“Asante”
Nikachukua hati yangu ya kusafiria kisha, nikapiga hatua mbili mbele na kuchukua begi langu la mgongoni. Nikatembea kwa umakini hadi kwenye moja ya nguzo na kujibanza na kuwaangalia jamaa hawa. Nikawaona wakiwa wamesimama kwenye mlango maalumu wa kuelekea katika ndege. Kwa mauonekano wao hakuna hata mmoja ambaye ananifwatlia mimi. Taratibu nikaanza kupiga hatua hadi kwenye mlango wa ndege hii, nikajumuika na abiria wengine kuingia ndani.
 
“Karibu”   
Wafanyakazi wa shirika la hii ndege walitukaribisha kila abiria anaye ingia huku kila mmoja akionyesha tiketi yake. Nikaanza kutafuta herufi ya siti yangu ambayo na ‘J2’. Sikuchukua hata dakika moja nikawa nimefanikiwa kufika katika siti yangu, nikamkuta dada wa kizungu ambaye nilikuwa nimeongozana naye akiwa amesha kaa kwenye siti yake ambayo ni ‘J1”
“Mambo”
Dada huyu alinisalimia kwa lugha ya kingereza.
“Poa habari yako”
“Salama, ninaitwa Jane”
“Peter”
“Ahaa una jina kama la mdogo wangu wa mwisho”
“Yaaa tutakuwa tumefanana majina”
“Ninakwenda Nigeria wewe je?”
 
“Hata mimi pia ninakwenda Nigeria”
Nilizungumza huku nikiwatazama jamaa hawa wawili wakikaa kwenye siti zao ambazo zipo nyuma karibu na mlango wa kuelekea katika vyoo vilivyomo ndani ya hii ndege. Jane ni msichana mchangamfu sana kwani dakika kadhaa tangu nikae nae hapa amenizoea kwa haraka sana.
“Mimi ni dotka kutoka shirika la umoja wa mataifa, UN ninakwenda Nigeria kwenye semeni ya kidaktari wewe je?”
“Ahaa mimi ninakwenda kibiashara?”
“Labda biashara gani?”
Nikageuka nyuma na kuwaangalia jamaa hawa ambao hadi sasa hivi hawajanistulia kabisa. Jane na yeye akaangalia nyuma akitaka kuona nini ninacho kitazama mara kwa mara.
“Kuna tatizo?”
 
Jane aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.
“Hapana hakuna tatizo”   
“Unaonekana unawafwatilia sana wale jamaa, una wafahamu”
“Habari ndugu wasafiri karibuni katika ndege yetu. Tunakwenda kuianza safari dakika mbili mbeleni, tunawaomba muwezekufunga mikanda kwenye siti zetu tafahdali. Ninawatakia safari njema na Mungu atongoze”
Sauti ya kike ilisikika kupitia vipaza sauti vilivyomo humu ndani ya ndege, nikachukua  mkanda wa siti yangu na kujifunga vizuri kiuononi mwangu. Hata swali la Jane sikulikumbuka aliniuliza nini kwani akili yangu kwa sasa ipo juu ya hawa watu.
 
‘Lazima niawaue’
Nilizungumza kimoyo moyo kwani endapo nitawaacha hai watu hawa basi wanaweza kunigeukia mimi pale watakapo fahamu ukweli wote. Taratibu ndege ikaanza kuiacha ardhi huku abiria sote tukiwa kimya kila mmoja akimuomba Mungu wake kwa upande wake. Hadi ndege ilivyo tulia angani taartibu nikaanza kuona mtu mmoja baada ya mwengine akifungua mkanda wake.
“Huuu, hiili zoezi huwa silipendi sana”
Jane alizungumza huku akinitazama usoni mwangu
“Zoezi gani?”
“Zoezi la ndege kupaa au kutua, huwa ninapata mashaka sana na kuogopa”
“Hhaaha ila ni kawaida mbona”
“Yaa tangu nipo mtoto huwa sipendi ndege inavyo paa na kutua”
Nikatazama nyuma kidogo, nikamuona mmoja wa jamaa akifungua mkanda wake na kusimama. Nikamtazama Jane kisha nikajikoholesha taratibu.
 
“Ninakuja”
“Sawa”
Jane alizungumza huku akinitazama kwa macho ya mashaka kidogo, nikaanza kutembea katikati ya uwanzi ulio tengenisha siti hizi za pande mbele. Nikafika usawa wa siti aliuo kaa jamaa hawa, nikamtazama huyu mmoja kwa macho ya kuiba pasipo yeye kugundua lolote, nikaendelea kusonga mbele hadi kwenye vyoo vilivyomo humu ndani.
Nikausukuma mlango kwa nguvu na kuingia ndani, nikamkuta jamaa akiwa ameshika vipande vya bastola akiviunganisha, alipo niona akachomoa kisu mfukoni mwake, akajaribu kunirushia ngumi, ila nikaweza kumdhibiti kwa kumpiga kwa kutumia ubapande wa mkono wangu wa kulia ulio tua shingoni mwake na kumfanya awahi kulishika koo lake huku akijitahidi kupata pumzi. Nikampiga kabari moja nzito iliyo mfanya azidi kupoteza pumzi. 
 
Taratibu jamaa huyu akaanza kulainika na baada ya dakika moja, akawa ametebwereka kabisaa. Nikafungua moja ya mlango wa choo na kumkalisha kwenye choo cha kukaa kisha nikafunga choo hichi na kuweka kibao kidogo kilicho andikwa kwa maandishi ya rangi nyekundu ‘Choo kinafanyiwa matengenezo kwa muda’
Nikachukua begi ambalo lina silaha ambazo zinatakiwa kufungwa ili kukamilika, huku kuna mabomu sita ya machozi. Nikaiingiza bastola ndani ya begi aliyo kuwa ameanza kuifunga jamaa pamoja na kisu chake, kisha nikalifunga begi hili na kutoka katike eneo hili. Sikutaka kutoka na begi hili hadi walipo kaa abiria, nilicho kifanya ni kumuita muhudumu mmoja wa kike.
 
“Ndio kaka”
“Kwa jina ninaitwa Daniel, ninafanya kazi chini ya ofisi ya raisi wa Marekani bwana Donald Bush. Siku chache nyuma niliweza kuongoza oparesheni ya kuangamiza na kulifutilia mbali kundi la Al-Shabab na tulifanikiwa kuweza kumua mkuu wao. Sasa bado nipo kwenye oparesheni, na ndege yako leo hii ilitaka kwenda kutekwa na magaidi wachache walio salia, inavyo onyesha wanahitaji kulipiza kisasi kwa kile ambacho kimetokea siku chache zilizo pita”
 
Nikaanza kumuona dada huyu akianza kutetemeka mwili wake, naikamshika mkono na kumtuliza asitetemeke wala asizungumze neno lolote zaidi ya mimi nitakacho muambia.
“Ndani ya hii ndege yako kuna magaidi wawili wa Al-Shabab, mmoja nimedhibiti na mwingine bado yupo kwenye siti anasubiria mwenzake atoke ili waweze kufanya shambulizi, sasa ninacho hitaji kukuomba kwa sasa, wasiliana na rubani mkuuaombe kutua nchi yoyote kwa dharura ili kuwashusha hawa magaidi. Kumbuka hapa tunazungumzia roho za watu zaidi ya elfu mmoja tuliomo humu ndani ya hii ndege mukiwapa nafasi magaidi hawa, lolote linaweza kutokea sawa”
“Sawa”
“Na kama unahitaji udhibitisho wa kwamba kuna magaidi, silaha zao hizi hapa”
 
Nikafungua zipu ya begi kidogo na kumuonyesha dada huyu silaha zilizopo humu ndani, kwa haraka akachukua mkonga wa simu ya dharura uiliyopo kwenye moja ya ukuta humu ndani. Akameza mate kwa nguvu, ila kabla hajaminya batani yoyote, nikamshika mkono anao taka kuminya batani hizo.
“Ndani ya ndege hii hususani wafanyakazi wezako, kuna mmoja ni msaliti kwa maana silage hizi zimeingia hata kabla ya abiria kuingia na zimeweza kufichwa humu chooni, sasa unaweza kunieleza ni nani ambaye unaweza kumuhisi labda ana vijitabia hatarishi”
Dada huyu  akatingisha kichwa huku jasho likimwagika usoni mwake, nikamuachia mkono wake na kwa ishara nikamuomba ampigie rubani mkuu simu.
“Ndio mkuu, kuna tatizo”
“Kuna mtu anaitwa Daniel, anafanya akazi chini ya serikali ya Marekani, ameweza kukamata magaidi wawili weye silaha ndani ya hii ndege”
Dada huyu akanitazama kisha akautoa mkonga wa simu sikioni mwake na kunikabidhi mimi.
 
“Anahitaji kuzungumza na wewe”
Nikaupokea mkonga wa wasimu hii na kuuweka sikioni mwangu.
“Ndio rubabani?”
“Ni jambo gani ambalo unaweza kufanya hadi nikakuamini kwamba wewe ni mfanyakazi chini ya serikali ya Marekani na si gaidi?”
“Piga simu White House na uliza kwamba Dany ni nan? Hiyo ni moja mbili pasipo kukuvunjia heshima mkuu, hili ni tatizo linalo husu maelfu ya watu ndani ya ndege yako sasa ninakuomba kama utalizembea niwaachia magaidi hawa waanze kuua abiria mmoja baada ya mwengine na wewe utakuwa unafwata amri ya kila kitu watakacho kueleza na kumbuka kwamba hii lawama yote itakuwa juu yako, ninacho kuaomba, hakikisha kwamba unaomba kutua kwenye nchi yoyote tuwakabidhi hawa Magaidi kwenye vyombo vya usalama, ndege yoko ikaguliwe kisha safari hitaendelea na hii ni dharura”
 
Nilizungumza kwa msisitizo ambao nina amini kwamba umemfanya rubani wa hii ndege kunielewa.
“Nimekuelewa bwana Daniel”
“Nashukuru, gaidi mmoja bado yupo kwenye siti, nitafanya kila niwezalo kuhakikisha kwamba ninamuwekea uangalizi”
“Sawa bwana Daniel ngoja niombe kutua chini kwa dharura”
“Sawa muheshimiwa rubani”
Nikakata simu kuurudisha mkonga wa simu kutoka sehemu nilipo utoa, nikamkabidhi begi muhudumu huyu.
“Hakikisha unalitafutia sehemu salama unaliweka”
 
“Sawa”
Nikaanza kutoka katika eneo hili huku nikijiweka sawa. Nikatazama watu walikaa kwenye siti za karibu na huyu gaidi, wengi wao wamelala. Nikapiga hatua za umakini na kukaa kwenye siti ya gaidi aliye kuwa ameondoka na kumfanya mwenzake kushangaa.
“Una nikumbuka?”
Nilimuuliza huku nikimtazama machoni gaidi huyu, msangao wake ukanipa nafasi ya kumpiga kisukusuku cha kustukiza kwenye pua yake na kumfanya aweweseke kwa maumivu makali. Taratibu nikampiga kabali iliyo mpelekea kutulia kimya, na zoezi hili hapakuwa na mtu yoyote wala aliye weza kushushudia hili tukio, nikamfunga mkanda gaidi huyu huku nikimuweka vizuri kwenye siti, kisha taratibu nikanyanyuka na kurudi kwenye siti yangu.
 
“Umechelewa?”
“Yaa kidogo tumbo langu linanisumbua sumbua”
“Ohoo pole, kwa nini usiombe msaada kwa wahudumu?”
“Hapana nipo vizuri kwa sasa”
“Kweli?”
“Yaa kweli”
Nilizungumza huku nikitabasamu. Jane akaka vizuri kwenye siti yake huku naye akionekana kuwa na furaha ila ana onekana ana jambo anahitaji kulizungumza.
“Una kitu unahitaji kuzungumza?”
“Ahaa…yaa ila naona kwa sasa sio muda sahihi”
“Kwa nini?”
“Ahaa unajua ile mtu unaamuona kwenye ndege tu alafu unakwenda kuzungumza hisia zako za moyo kwa haraka namna hii anaweza kukuona kwamba ni malaya”
Jane alizungumza kwa sauti ya chini kidogo.
 
“Inategemea lakini”
“Habari ndugu abiria, tunawaomba kufunga mikanda yenu iliyopo kwenye siti, na ndege yetu itatua katika kiwanja cha kimataifa cha Bole Addis Ababa nchini Ethiopia, tunawaomba radhi kwa usumbufu ulio jitokeza na asanteni”
Sauti ya rubani wa kiume ikasikika masikioni mwa kila mmoja, na kuwafanya watu wengine walio lala kustuka. Kila mmoja ambaye alifungua mkanda wake, taratibu akaanza kuufunga kiuonini mwake, akisubiria ndege hii kutua.
“Kuna nini kinacho endelea?”
Jane aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.
“Sifahamu kusema kweli”
“Inabidi waweze kutuarifu tujue kwamba kuna kitu gani ambacho kinaendelea, kwa maana hawawezi kusema kwamba wanatua Ethiopia wakati sio ratiba ya ndege hii”
“Naamini kuna tatizo ambalo wanahitaji kulilinda ili abiria wasichanganyikiewe ngoja tuone itakavyo kuwa”
 
“Taratibu ndege ikaanza jutua ardhini, kupitia kidoo cha dirisha pembeni ya Jane, tukaona kundi kubwa la askari wenye silaha wakiimarisha ulinzi ardhini hapa.
“Kuna tatizo”
Jane alizungumza huku akitazama askari hao.
“Unahisi kuna tatizo gani?”
Nilimuuliza Jane huku sote tukitazama nje ya uwanja huu wa ndege.
“Sijajua kwa kweli”
Taratibu ndege ikaanza kusimama, gari za polisi zinavyo washa ving’ora vyao tukaona jinsi vinavyo izunguka ndege hii. Mlango ukafunguliwa kwa haraka wanajeshi wenye bunduki wakaingia ndani ya ndege hii huku wakiwa na silaha mikononi mwao. Muhudumu ambaye nilimkabidhi begi lenye silaha, akawaongoza wanajeshi hawa hadi kwenye siti ya gaidi ambaye sasa hivi ndio anastuka, kwani sikumuua zaidi ya kumzimisha tu. Wanajeshi hawa wakamtoa gaidi mwengine ambaye alikuwa chooni huku wakimbeba.
 
“Mr Dany tunakuomba uongozane nasi”
Mwanajeshi mmoja alizungumza na kumfanya Jane kunikazia macho, nikamkonyeza huku nikifungua mkanda wa siti yangu niliyo kalia. Nikashuka kwenye ndege nikiw ana muhudumu huyu wa kike pamoja na askari wengine.
“Munatupelekea wapi afisi?”
“Tunahitaji kuwahoji maswali mawali matatu kisha mutaendelea na safari yenu”
“Sawa”
Nikiwa hapa uwanjani nikaona ndege nyingine ikitua huku ulinzi ukiendelea kuimarisha walinzi mkali. Nikaona gari sita za kifahari zikiisogelea gari hiyo huku zikiwa na bendera ya Ethiopia pamoja na Tanz.
“Kuna kiongozi gani anaye kuja?”
“Ni raisi wa Tanza K2, ana Ziara ya siku mbili hapa nchini Somalia”
Mwanajeshi huyu aliniambia, nikajukuta nikikaza macho yangu kwenye mlango wa kushukia abiria, nikaona walinzi wakianza kutangulia kushuka kisha akaanza kushuka K2 huku akiwa na furaha sana na akipunga mikono kwa wenyeji wake wlaio fika kumpokea katika hili eneo jambo lililo nitamanisha kwenda kumvamia na kumuua ili mradi nilipize kisasi kwa kila kitu kibaya alicho nifanyia katika maisha yangu.
                                                                                    
AISIIIII……….U KILL ME 133
   
“Dany......Dany”       
“Ndio afande”
 
Niliitika huku nikistuka kwani kwa sekunde kadhaa nilitingwa na mawazo mengi kichwani mwangu nikimfikiria K2.
“Ilikuwaje hadi ukafahamu kwamba watu hawa ni magaidi?”
“Niliwafwatilia nyendo zao tangu walivyo kuwa wamepanga foleni na nina ustadi mkubwa wa kuweza kumsoma mtu”
“Wewe labda ni nani?”
“Afande nimefanya kazi niliyoifanya, kikubwa wahojini hao magaidi nina imani wataweza kuwaeleza mengi na lengo la kuiteka ndege ilikuwa ni nini”
Nilizungumza kwa ujasiri huku nikimtazama afande huyu. Akanitazama kwa sekunde kadhaa kisha akatingisha kichwa na kukubaliana nami kwa kile ambacho nimekizungumza.
“Ninaweza kwenda?”
“Ndio unaweza kwenda”
Nikaondoka katika eneo hili huku nikitazama gari za kifahari jinsi zinavyo ondoka katika eno hili. Nikaanza kupandisha kwenye ngazi za hii ndege na kurudi kwenye siti yangu niluyo kuwa nimekaa.
“Unaittwa Dany?”
Jane aliniuliza huku akinitazama usoni mwangu.
“Yaaa ni jina langu pia?”   
“Kwa nini uliniambia kwamba unaitwa Peter?”
“Naamini kila binadamu ana majina mawaili mawili si ndio?”
“Yaaa”
 
“Ok ukipenda unaweza kuniita Peter au Dany”
“Basi nitakuita Peter”
“Sawa”
Hatukuchukua muda mwingi katika uwanja huu wa ndege safari ya kueleka Nigeria ikaanza huku abiria wezangu kwa mara kadhaa walikuwa wakinitazama. Kadri muda ulivyo zidi kwenda ndivyo jinsi mazoea kati yangu na Jane yalivyo zidi kupamba moto. Kitu kikubwa ambacho ninajitahidi kukizuia katika mwili wangu ni hisia za mapenzi.
Baada ya masaa kadhaa tukafanikiwa kufika katika uwanja ndega wa Murtala Muhammed International(MMIA) Lagos nchini Nigeria, majira ya asubuhi.
“Una uwenyeji hapa Nigeria?”
Nilimuuliza Jane baada ya kutoka ndani ya uwanja huu wa ndege.
 
“Yaa nimesha wahi kufika, ila nimekuja kuchuliwa na shirika la kidaktari, kwa hiyo Mungu akibariki tunaweza kuonana”
“Sawa Jane”
Tukapena mikono na Jane kisha akaelekea kwenye gari aina ya Range Rover Sport na akaondoka eneo hili. Nikaanza kutazama eneo hili la uwanja, akanifwata kijana mmoja aliye valia kikoti maalumu lilicho andikwa dereva taksi.
“Unahitaji usafiri kaka?”
Nikamtazama kwa sekunde kadhaa kwenye macho yake, kisha nikatingisha kichwa na kumuambia ninahitaji. Tukaongozana na kuingia kwenye taksi yake aliyo isimamisha eneo maalumu ambalo kuna madera wengine ambao nao wamevalia sare za kufanana.
“Unaweza kunipeleka kwenye nyumba ya wageni ya bei raisi kabisa”
“Ndio ninaweza kukupeleka kuna nyumba nyingi za kawaida za kulala wageni”
“Napenda ambayo ipo katika mitaa mitaa ya watu wa maisha ya chini”
“Usijali kwa hilo kaka”
Safari ikazidi kusonga mbele, tukafanikiwa kufika katika mitaa iliyo jaa watu wa maisha ya chini, dereva akasimamisha gari mbele ya moja ya nyumba iliyo chakaa kiasi 
 
“Hii nyumba naamini itakufaa”
“Yaa tunaweza kushuka kwenda kuangalia”
“Yaa twende tu”
Tukashuka kwenye gari na kuingia katika nyumba hii ya kulala wageni, japo ninahitaji kuishi katika maisha ya kawaida sana ila hii nyumba ya kulala wageni inatisha, si kwa majengo yake tu ila ni kwa uchafu ambao unafanyika humu ndani. Watu wanafanya mapenzi kwenye kordo tea hii asubuhi ambayo watu wanatakiwa kuwa katika majukumu ya kufanya kazi.
“Kaka huna sehemu nyingine ambayo unaweza kunipeleka?”
“Si umehitaji sehemu ambayo ni ya bei rahisi, hii ndio ya bei rahisi”
“Hapana, ninakuomba tuondoke hili eneo, nipeleke katika hoteli nyi……”
Dada mmoja aliye shika ukuta huku mwanaume akiwa nyuma yake , akajaribu kunishika mkono wangu huku akiwa ameyalegeza macho, kwa haraka nikajikuta nikiiukwepesha mkono wangu kwa haraka huku nikiwa nimeikunja sura yangu.
“Tuondoke”
Nilizungumza huku nikitangulia kutoka nje huku nikiwa nimechoka kwa haya niliyo yaona humu ndani.
“Nipeleke hoteli yoyote ambayo ni kubwa sawa”
“Sawa bosi”
 
Safari ya kutafuta hoteli nzuri ikaanza, tukafanikiwa kupata hoteli iliyo tulia. Nikashuka kwenye gari, nikatoa noti ya dola mia na kumkabidhi dereva huyu.
“Nisubiri hapa nina baadhi ya mizunguko leo mjini”
“Sawa bosi”
Dereva huyu alizungumza kwa furaha, kwani ninaamini kwamba nimemlipa ujira ambao ni mkubwa sana kuliko hata pesa ambayo alitarajia mimi kumlipa. Nikaingia ndani na kusimama sehemu ya mapokezi .
“Habari dada?”   
“Salama tu za kwako?”
“Salama, ninahitaji kupata chumba”
Dada huyu akaanza kunitajia aina ya vyumba pamoja na bei zake. Nikalipia chumba cha bei ya kawaida kwa siku mbili, nikakabidhiwa funguo na  kuelekea chumbani kwangu, nikakichunguza chumba kizama kwa umakini sana nilipo hakikisha kwamba kina usalama wa kutosha, nikatoka kwenye chumba hichi huku nikiacha begi langu la nguo. Nikatoka na kuingia kwenye taksi, nikamuomba dereva anipeleke kwenye maduka ya simu.
Tukafika kwenye maduka ya simu, nikashuka kwenye gari, nikaingia kwenye moja ya duka simu, nikaanza kutafuta simu gani ni nzuri ambayo nitaweza kuitumia katika kazi yangu iliyo nileta hapa nchini Nigeria.
 
Nikanunua simu mbili, moja ikiwa ni iphone 6 huku nyingine ikiwa ni samsung note 4. Nikawaomba wanielekeze ni wapi ninapo weza kupata line za mitandao ya simu inayo tumika hapa hapa Nigeria, kwa bahati nzuri ndani ya duka hili kuna wakala wa moja ya mtandano. Nikampatia hati yangu ya kusafiria, akatoa nakala kisha akanirudishia.
“Itachukua muda gani dada?”
“Kama dakika tano hivi hadi kusajiliwa”
“Sawa”
Nikasubiri kwa dakika hizi tano wakawa wamemaliza kunihudumia. Niaweka salio la kutosha kisha nikatoka ndani ya duka hili. Nikaingia ndani ya gari na kumpigia simu meja.
“Ni mimi”
“Habari yako Dany?”
“Salama, nimefanikiwa kufika salama”
“Sawa hii ndio namba ambayo utakuwa unaitumia?”
“Ndio”
“Basi hakikisha unanunua kava ambazo zinazuia mawasiliano yako kunaswa na watu wa simu”
“Nitazipatia wapi meja”
“Uliza kwa hao wauzaji”
“Ngoja nijaribu”
“Sawa nitasubiria siku yako baada ya kuweza kupata hilo kava”
 
Nikashuka kwenye taksi na kurudi tena dukani, nikamfwata muhudumu aliye niuzia simu. Nikamtazama usoni kwa sekunde kadhaa.
“Samahani kwa usumbufu”
“Bila samahani”
“Kunakava fulani ambalo ukivalisha kwenye simu, basi mawasiliano unayo piga au kupigiwa yanakuwa salama je ninaweza kulipata”
Muhudumu huyu akanikazia macho huku akionekana anajiuliza maswali mengi sana kichwani mwake. Nikatoa noti ya dola mia na kumuwekea mezani kwake.
“Je ninaweza kulipata?”   
“Kwa nini unalihitaji, kwa maana kwa sheria ya hapa kuuza makava kama hayo unaweza kustakiwa na kupokonywa hata leseni ya usajili wa duka?”
“Ahaa mke wangu unajua ana wivu sana, sasa sihitaji afahamu nipo wapi?”
“Mke ndio anafanya ununue kava la simu yako kuto kunaswa na mawasiliano?”
 
“Yaaa, nisaidie kama unahitaji pesa nitakuongezea”
Kijana huyu akaka kimya akionekana kujishauri kichwani mwake, nikatoa noti ya dola mia nyingine na kumuwekea mezani. Akazichukua kwa pamoja na kuziingiza mfukoni mwake.
“Hembu simu yako?”
Nikatoa simu ya iphone 6, akaitazama kisha akaniomba nimsubiri. Nikaka eneo hilo kwa dakika kadhaa, baada ya muda akarudi akiwa kava hilo mikononi mwake.
“Ninakuomba uwe makini sana”
“Usijali, ila una uhakika wa kwamba hili ni kava halisi?”
“Ndio”
Nikalivisha kava hili kwenye simu yangu, kisha nikatoa dukani humu.
“Tunaelekea wapi bosi?”
“Turudi hotelini”
“Sawa”
Safari ya kurudi hotelini ikaanza, njia mzima nipo kimya huku nikifikiria ni kitu gani ambacho ninaweza kukifanya ili kazi yangu iende sawa. Tukafika hotelini, nikamlipa huyu dereva dola mia, kisha nikachukua namba yake na simu.
 
“Nitakupigia nikikuhitaji”
“Sawa bosi”
Moja kwa moja nikaingia chumbani kwangu, nikafunga mlango kwa ndani. Nikatoa simu na kumpigia meja.
“Mawasiliano kwa sasa yapo salama meja”
“Sawa hata mimi ninaona kwenye mtambo wangu hapa”
“Nahitaji kuzungumza na raisi”
“Sawa subiri kidogo niweze kumpigia, usikate simu”
“Sawa”
Nilizungumza huku nikiwa nimesimama pembeni ya dirisha langu nikitazama magorofa mengine yaliyopo karibu na hili gorofa.
“Dany unaweza kuzungumza sasa raisi yupo hewani”
“Muheshimiwa raisi habari yako?”
“Salama tu Dany nimeambiwa na meja kwamba umefika salama”
“Ndio muheshimiwa raisi nimefika salama, vipi mke wangu amefanikiwa kufika salama?”
 
“Ndio amefanikiwa kufika, na unaweza kuzungumza naye ndani ya muda mchache pale utakapo hitaji”
“Sawa nitashukuru sana muheshimiwa raisi. Ila muheshimiwa raisi kuna tukio liliweza kujitikeza njiani nilipo kuwa kwenye ndege”
“Jambo gani?”
“Kuna magaidi wawili wa Al-Shabab walihitaji kuiteka ndege ila niliweza kufanikiwa kuwadhibiti”
“Safi sana, ndio magaidi walio shushwa nchini Ethiopia?”
“Ndio hao muheshimiwa raisi”
“Nashukuru sana kwa kuweza kuwaokoa maelefu ya watu waliokuwa ndani ya hiyo ndege”
“Ni jukumu langu muheshimiwa raisi”
“Tena mke wako huyu hapa amesha fika ofisini kwangu unaweza kuzungumza naye”
“Dany”
Sauti ya Hawa ikanisisimua mwili mzima, moyo wangu ukajikuta ukijawa na furaha kubwa sana.
 
“Naa mke wangu”
“Umefika salama?”
“Ndio nimefanikiwa kufika, nahitaji kuanza kuianza kazi iliyo niletea huku”
“Kuwa makini mume wangu, na ninakuomba uweze kurudi salama”
“Usijali nitakurudi salama. Vipi unapata uangalizi mzuri katika hilo eneo?”
“Ndio tena raisi ameagiza watu wake, wananihudumia vizuri sana”
“Nafurahi kusikia hivyo mke wangu”
“Ninakupenda sana mume wangu, wewe ndio mwanaume wa maisha yangu”
“Hata wewe ndio mwanamke wa maisha yangu, nitakulinda kadri niwezavyo na nitahakikisha kwamba unajisifu kuwa na mwanaume kama mimi”
“Shukrani sana Dany wangu”
“Ok naomba umpatie simu muheshimiwa raisi”
“Sawa”
“Ndio Dany”
“Muheshimiwa raisi, ninahitaji kuianza kazi sasa”
“Mungu akutangulie katika hili”
 
“Shukrani sana”
Nikakata simu na kushusha pumzi taratibu, nikachukua rimoti na kuwasha tv, nikajitupa kitandani huku nikipangilia mipango ya jinsi gani ninaweza kumpata Yemi Okocha. Tangazo katika Tv hii likanifanya ninyanyuke kitandani na kukaa kitako. Yemi Okocha siku ya leo ana tamasha la kuchagua vijana wanao hitaji kujiunga kwenye maswala ya mavazi. Nikaandika eneo katika husika katika simu yangu kisha nikampigia dereva taksi, akaniahidi ndani ya dakika kumi atafika katika eneo hili. Nikasimama mbele ya kioo cha kabati kubwa lililopo hapa. Nikajitazama vizuri kuanzia chini hadi juu, nilipo ona nina vigezo kadhaa vya kuwa mwana mitindo nikashusha pumzi huku huku nikiwa nimejawa na furaha. Baada ya dakika kazaa simu yangu ikaita, nikaipokea.
“Bosi nimefika”
“Ninakuja”
Nikatoka chumbani kwangu na kufunga vizuri, nikashuka gorofani, nikaingia  kwenye gari nikamtajia jina la eneo ambalo ninahitaji kwenda.
 
“Tutachukua muda gani kufika”
“Hapo tutatumia dakika ishirini hadi kufika”
Ndani ya muda alio niambia dereva tukawa tumefika katika hoteli moja kubwa, nikakuta mlolongo wa vijana wakike na wakiume wakiwa wamepanga mistari kwa ajili ya kwenda kujisajili katika mashindano haya ya kutafuta wana mitindo, na mimi nikapanga mstari nikiwa ni mshirikia wa elfu moja na mia mbili. Muda ukazidi kwenda na foleni ikazidi kosogea, vijana walipo katika eneo hili wapo wengi wamependa, nikajitazama mweyewe nilivyo vaa na kimoyo moyo nikajishauri na kujiambia kwamba nina vigezo vya kuweza kushinda katika shindano hili.

==>>ITAENDELEA KESHO

Rais Magufuli: Sina mpango wa kutoa pesa kwa ajili ya katiba mpya

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk John Magufuli amewataka watu wanaotegemea atoe pesa kwa ajili ya kukaa vikao kujadili masuala ya kubadilisha katiba ya nchi waache kwa sababu hana mpango wala hategemei kutoa pesa kwa ajili hiyo.

Amesema kwa wale wenye fedha wanaotaka kusaidia mpango huo wampatie ili akamalizie mradi wa kujenga reli mpya ya kisasa ya Stiegler’s Gorge.

Ameyasema hayo leo Alhamis Novemba Mosi  alipokuwa akizungumza na washiriki wa kongamano la kuijadili hali ya siasa na uchumi wa nchi lililojumuisha maprofesa na viongozi kutoka katika sekta mbalimbali za serikali na Jeshi, lililofanyika ukumbi wa Nkrumah katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Rais Magufuli amesema amekuwa akipata ushauri kutoka kwa watu mbalimbali kuhusu kubadilisha Katiba mpya wasidhani hajui umuhimu wake ila kwa sasa hana pesa za kufanya hivyo.

“Sitegemei kutoa hela kwa ajili ya watu kwenda kujadili masuala ya kubadili katiba kama watu wana hizo hela watupe tukamalizie mradi wa Stieglers George,” amesema.

Rais Magufuli amesema hali ya uchumi ya nchi kwa sasa inakuwa kwa asilimia saba na  na Tanzania ni miongoni mwa nchi Tano za afrika ambazo uchumi wake unakua kwa kasi na mambo yakienda kama yalivyo pangwa itaendeleakukuwa na atasimamia hili ili ikue zaidi ya hapa.

“Nchi yetu ilifika katika hatua  kubwa sana ya rushwa na ndiyo maana  niliamua kujipa kazi kubwa ya kutumbua majipu kwa sababu nilitaka kufikisha nchi sehemu nzuri pamoja na changamoto zake niliapa lazima tutafika tu.

“Katika mambo makubwa ya msingi ni lazima tuyasimamie kwa pamoja kama watanzania bila kujali itikadi zetu za kisiasa na vyama na tusikubali kutumiwa,”amesisistiza Magufuli.

Zitto Kabwe Aondolewa Osyterbay na Kudishwa Mahabusu Mburahati

$
0
0
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe leo Novemba 1, 2018 ameondolewa kituo cha Oysterbay alikokuwa amehifadhiwa na kupelekwa Mahabusu ya kituo cha polisi Mburahati kilichopo Wilaya ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.

Uamuzi huo umekuja baada ya jeshi la polisi kufanya upekuzi nyumbani kwake kuanzia saa 2:20 asubuhi hadi saa 5:45 na kumrudisha tena kituo cha Oysterbay.

Wakili wa Zitto, Jebra Kambole amesema kwamba wapo kwenye mchakato wa kuwasilisha maombi ya dhamana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ili mteja wao apate dhamana.

“Tupo kwenye hatua za mwisho za kuwasilisha maombi ya dhamana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ili mgeja wetu aweze kupewa dhamana,” ameeleza Kambole.

Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi wa ACT, Ado Shaibu amesema hadi sasa kiongozi wake hajapewa dhamana badala yake anazungushwa kila kona.

“Hatuna jinsi tunafuata polisi wanavyotaka maana sasa hivi kiongozi wangu amerudishwa Mburahati," amesema Ado .

Zitto alikamatwa na polisi siku moja baada ya Polisi mkoani Kigoma kumtaka awasilishe vielelezo juu ya kauli aliyoitoa mbele ya waandishi wa habari Jumapili iliyopita Oktoba 28, 2018 kuwa ana taarifa za wananchi zaidi ya 100 kuuawa katika tukio la mapigano ya wananchi wa jamii ya Wanyantuzu na polisi wilaya ya Uvinza mkoani humo.

Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, Martin Ottieno amesema tuhuma za mbunge huyo hazina ukweli wowote na kusisitiza kuwa ni upotoshaji unaofanywa na wanasiasa.

Serikali Yamaliza Mgogoro wa Kiwanda cha Chai Mponde....Yaagiza mashine zichunguzwe, mitambo yenye hitilafu ikarabatiwe kazi ianze

$
0
0
SERIKALI imemaliza mgogoro uliodumu kwa miaka mingi kati ya wakulima wa chai wa wilaya za Lushoto na Korogwe na kampuni ya Mponde Tea Estate uliosababisha kufungwa kwa kiwanda cha chai cha Mponde baada ya kuagiza kiwanda hicho kianze kazi.

“Waziri Mwijage na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilomo Prof. Siza Tumbo hakikisheni kazi ya kukagua kiwanda na mitambo inafanyika haraka na kubaini mitambo ipi ni mizima na ipi ina hitilafu ili ukarabati ufanyike na kiwanda kianze kazi mara moja.”

Uamuzi huo wa Serikali umetangazwa leo (Alhamisi, Novemba 1, 2018) na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Kweminyasa kata ya Mponde, wilayani Lushoto baada ya kutembelea kiwanda hicho .

Waziri Mkuu amesema mwaka 1999 Serikali iliamua kuwapa wakulima wa chai na kiwanda hicho  kwa ajili kuwawezesha kuwa na sehemu ya kuchakata chai yao lengo likiwa ni kuwajengea uwezo wa kiuchumi. Imeamua kukirudisha Serikali baada ya kuwepo migogoro iliyoathiri uzalishaji kiwandani hapo.

Kuhusu suala la madeni ya watumishi, ameagiza watafutwe na madai yaorodheshwe kwa ajili ya malipo, amewahakikisha wananchi hao kuwa suala la ajira ambazo zilipotea baada ya kiwanda kufungwa zitarudi kwa sababu Serikali inataka kuona kiwanda kikifanya kazi.

“Serikali imeamua kukichukua kiwanda hiki ambacho awali ilikikabidhi wakulima wa chai na kwamba itahakikisha lengo lake la kuboresh kilimo linafanikiwa na  wakulima wanaendelea kulima zao la chai. Hatutaki kusikia masuala ya Utega wala Mponde hapa si mahali pake.”

Amesema wakulima hao walikosea kwa kuunda Umoja wa Wakulima wa Chai (UTEGA) ambapo katika kusajili badala ya kuanzisha ushirika wao walisajili NGO ambayo ilikuwa na wanachama wake, huku kiwanda kikiwa kimeanzishwa kwa ajili ya wakulima wote, jambo ambalo lilisababisha mgogoro baina ya wakulima na viongozi wa UTEGA.

Waziri Mkuu ameongeza kuwa wakati mgogoro huo ukiendelea kati ya UTEGA na wakulima wa chai wasiokuwa wanachama wa NGO hiyo, uliibuka mgogoro mwingine baina ya wakulima wote pamoja na muwekezaji ambaye ni kampuni ya Mponde Tea Estate baada ya kukabidhiwa kiwanda hicho  na uongozi wa UTEGA bila ya wao kushirikishwa.

Amewasisitiza wakulima wafufue mashamba yao kiwanda ni cha  Serikali  hivyo watakuwa wamepata sehemu ya uhakikika ya kupeleka chai ambayo itachakatwa. Pia ameagiza Mrajisi wa Ushirika aende kwa wakulima na kutambua idadi yao pamoja na kujua                               ukubwa wa mashamba yao.

Amesema baada ya kubaini idadi ya wakulima na ukubwa wa mashamba yao awasaidie katika kuunda vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) kisha kuunda ushirikia wao ambao watautumia katika kusimamia zao lao la chai na kuhakikisha mkulima ananufaika.

Waziri Mkuu amesema zao la chai ni miongoni mwa mazao makuu sita ya kimkakati, mengine ni korosho, kahawa, tumbaku, pamba na chikichi, hivyo amewataka wafufue mashamba yao na waendelee kuiamini Serikali yao ambayo imejidhatiti kuwahudumia.

Awali,Waziri wa Nchi Ofisi ya Makam wa Rais Muungano na Mazingira, January Makamba alisma Mgogoro huo wa kiwanda cha Mponde ulianza tangu mwaka 1999 na ilipofika mwezi Mei 2013, wananchi walimlalamikia kwa kushindwa kutatua tatizo hilo.

Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli aliwaomba wananchi hao waendelee kuwa na subira wakati suala lao likiwa linaendelea kushughuliwa na Serikali. “Mgogoro huo umesababaisha kudhorota kwa uchumi kwa sababu wananchi wengi waliacha kulima chai baada ya kiwanda hicho kufungwa miaka mitano iliyopita.”

HIvyo Makamba ameiomba Serikali iwasaidie wakulima wa zao la chai kuwapa miche mipya pamoja na pembe jeo kwa ajili ya kufufua zao hilo na kukiwezesha kiwanda cha chai MPonde kupata malighafi kama ilivyokuwa hapo awali.

Kwa upande wake, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage alisema kuwa  tayari amekuja na wataalam kwa ajili ya kukagua mashine zote zilizopo kiwandani hapo ili mchakato wa kukiwasha uanze  mara moja.

Mwijage alisema “mimi kama Waziri mwenye dhamana ya viwanda nawaambia wananchi muondoe wasiwasi tayari kiwanda kimeshafunguliwa maana sitaondoka hapa Bumbuli mpaka kieleweke.”

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, NOVEMBA 1, 2018.

Rais Magufuli: Upanuzi Bandari ya Mtwara utasaidia kupunguza gharama za usafirishaji wa mafuta

$
0
0
Rais Magufuli amesema upanuzi wa bandari ya Mtwara utasaidia kupunguza gharama za usafirishaji wa mafuta.

Pia utasaidia yashukie moja kwa moja mkoani mtwara tofauti na sasa ambapo inalazimu  yashushiwe jijini Dar es Salaam kisha yasafirishwe tena kurudi mkoani humo.

Akizungumza na washiriki wa kongamano la kujadili hali ya siasa na uchumi wa nchi ukumbi wa Nkrumah katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) leo Novemba Mosi ambapo amesema bandari ya mtwara itakuwa kituo cha biashara kwa mikoa ya Kusini na nchi za jirani.

“Hatuwezi kusafirisha mafuta kutoka Dar es Salaamvhadi Mtwara karibu kilometa 540 wakati tunaweza kushushia hukohuko na tukayasambaza lakini pia tumeamua kuipanua bandari ya Tanga nayo lazima tuipanue kwa sababu kuna kiwanda kinajengwa cha kuzalisha sarujii ambayo itauzwa ndani na nje ya nchi.

“Tumeamua kuunganisha nchi jirani za Rwanda na Burundi kwa reli ya kisasa ya Stiegler’s Gorge (SGR) ili wanapotumia bandari ya dar kwa ajili ya kusafirisha  bidhaa wapate urahisi nah ii itaiongezea nchi yetu pato kwa kukusanya kodi.

“Huwezi kuongelea kukua kwa uchumi kama hauna umeme wa uhakika na wa bei nafuu tukasema lazima tuwe na umeme wetu na ndiyo maana tukaanza na  mradi wa SGR kwasababu ni umeme wa maji na utakapoanza bei  ya umeme itashuka ”amesema.

Rais Magufuli amesema uwepo wa ndege binafsi ya Dream Liner utasaidia kukuza sekta ya utalii kwasababu watalii wataweza kutoka mataifa mbalimbali na kuja nchini.

“Watalii walikuwa hawaji nchini kwetu kwa sababu hatukuwa na ndege yetu binafsi, huwezi kutumia shirika la ndege la jirani ili kuleta watalii nchini kwako ndiyo maana sisi tukaamua kununua ndege zetu wenyewe na kufufua shirika letu la ndege na lengo kubwa ni  kuinua sekta ya utalii,” amesema.

Aidha Rais Magufuli amesema serikali imenunua rada zitakazofungwa katika jiji la Dar na maeneno mengine ya nchini ili kuongeza ulinzi katika safari za anga na iwe rahisi kujua inapotokea hatari yoyote ile.

Rais Magufuli: Kuongoza Nchi ni Kazi Ngumu Sana

$
0
0
Rais John Magufuli amesema hakuna kipindi anachopitia changamoto katika uongozi kama ilivyo sasa.

Amesema kuongoza nchi ni kazi ngumu na wakati mwingine anashindwa kulala kutokana na kukabiliwa na mambo mengi ya kufanya.

Ametoa kauli hiyo leo mchana Alhamisi Novemba Mosi, 2018 katika kongamano la uchumi na siasa lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

“Uongozi ni kazi ngumu sikutegemea ingekuwa ngumu hivi. Yaani ukiingia chumbani kwangu mafaili yamejaa hadi kitandani na kila moja lina umuhimu huwezi kulipeka kwa mtu mwingine,” amesema.

Pia, amezungumzia jinsi anavyopenda kuzungumza lugha ya Kiswahili akibainisha kuwa ndio lugha inayowaunganisha Watanzania.

“Nasikia watu wanasema hajui Kiingereza nimekuwa waziri nikasafiri nchi nyingi kwenye vikao huko nilikuwa napewa uongozi wakati mwingine wa mikutano mikubwa sasa nilikuwa nazungumzaje kama sijui, “ amesema.

“Ukiniambia kusafiri sijui wapi sijafika, nimetembea karibu dunia yote kwa sasa sina haja kwangu ni Utanzania kwanza na kipaumbele changu ni kuwatumikia Watanzania.”

Kesi ya Vigogo CHADEMA Yakwama...Mbowe ni Mgonjwa Yupo Afrika Kusini

$
0
0
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeelezwa kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ameshindwa kufika mahakamani kwa kuwa amepelekwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu, ambapo inadaiwa Mbowe anasumbuliwa na ugonjwa wa moyo na shinikizo la damu.

Kauli hiyo imetolewa mahakamani leo Novemba 1 na mdhamini wa Mbowe, Grayson Celestine aliyedai kuwa amepewa taarifa za ugonjwa wa Mbowe na mke wa mwanasiasa huyo.

"Kwa mujibu wa maelezo ya mkewe, Mbowe anasumbuliwa na matatizo ya moyo pamoja na shinikizo la damu na familia imeamua kumsafirisha afrika kusini kwa dharura lakini mimi sijaonana naye" amesema Celestine.

Aidha Celestine alimueleza Hakimu Mashauri kuwa “mshtakiwa Freeman Mbowe akirejea atawasilisha nyaraka za safari na matibabu, kwamba anaendelea kufanya mawasiliano ili azitume nyaraka kwa njia ya mtandao.”

Kufuatia maelezo hayo, wakili wa Faraja Nchimbi aliomba kutolewa kwa amri ya kumkamata Mbowe ili ajieleze sababu za kutofika mahakamani.

“Sisi upande wa mashtaka hiyo tunaona ni mwendelezo wa dharau ya mshtakiwa Mbowe kwa mahakama kwa kuwa alishapewa onyo, Mbowe ameamua kwa utashi wake kukiuka amri ya mahakama”, amesema Faraja Nchimbi.

Kiongozi huyo wa CHADEMA na viongozi wengine wanatuhumiwa kwa makosa mbalimbali ikiwemo kuratibu na kufanya maandamano yaliyosababisha kifo cha aliyekuwa mwanafunzi Chuo cha Taifa  Usafirishaji NIT, Akwilina Akwilini.

Lowassa Akwama Kumuona Zitto Kabwe Polisi

$
0
0
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amezuiwa kumuona kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe anayeshikiliwa na polisi tangu jana Oktoba 31, 2018.

Msaidizi wa waziri mkuu huyo wa zamani, Aboubakary Liongo amesema kuwa  leo Alhamisi Novemba Mosi, 2018 saa 9 Alasiri Lowassa alikwenda kumuona Zitto kutaka kujua hatima yake, kwani wako pamoja naye kuhakikisha haki inatendeka, lakini akaelezwa kuwa muda wa kumuona umeshapita.

Baada ya kufika kituoni hapo, msaidizi wa Lowassa alikwenda kuomba kibali cha kumuona Zitto lakini alielezwa kuwa muda umekwisha, ambapo Lowassa amenukuliwa akisema, “Huyu ni kiongozi mwenzetu huku upinzani lazima tushikamane kukabiliana na lolote lililo mbele yetu, tunahitaji kuwa kitu kimoja kuliko wakati mwingine wowote".

Zitto yupo kituo cha polisi Mburahati ambako amepelekwa leo  akitokea kituo cha Osterbay

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya November 2

Viwanja Vinauzwa Dar: Low, Medium & High Density plots for sale: Bunju na Mapinga (Baobab sec)

$
0
0
Low, Medium & High Density plots for sale: Bunju na Mapinga (Baobab sec)

Viwanja ni vikubwa sana na vinauzwa kwa bei nafuu sana na masharti nafuu.

Viwanja ambavyo vimepimwa na tayari vina hati viko kama ifuatavyo:
Robo Acre/eka (sqm 1000) ni tsh 15 milion
Nusu eka (sqm 2000) ni tsh 30 milion
Acre nzima (sqm 4000) ni tsh 60 milion

Pia vipo viwanja ambavyo process ya upimaji wake imeanza lakini haijakamilika (hati bado):
Robo eka (sqm 1000) ni tsh 8 mil
Nusu eka (sqm 2000) ni tsh 16 mil
Eka nzima (sqm 4000) ni tsh 32 mil

Na pia vipo viwanja vidogo (high density) kama ifuatavyo:
mita 10/20 bei mil 2
mita 20/20 bei mil 4
mita 20/30 bei mil 6
mita 20/40 bei mil 8

Viwanja hivi vyote viko Mapinga maeneo ya Babobab secondary, ni km 3 kutoka main road (Bagamoyo Road) na luksa kulipa kwa awamu.

Kwa Bunju B viko viwanja 3: kila kimoja kina sqm 600 na bei yake ni mil 20 tu

Ukipata taarifa hii mjulishe Ndugu/jamaa/rafiki.
Hakuna dalali. Mpigie mhusika. Call 0758603077, whatsap 0757489709, email: menejadar@yahoo.com

Kutana na Shekhe Yassin....Mtabiri wa Nyota, Pete za Bahati, Mimba Kutoshika au Mimba Kuharibika

$
0
0
Whatsap 0743313580....KUTANA NA SHEKHE YASSINI SAIDI
Ni Shekhe aliyejaaliwa karma nyingi kutoka kwa Allah Mwenye uwezo kutatua shida mbali mbali ziwapatazo wanadamu.


Anatibu na kuponya shida mbalimbali zilizo shindikana kwa wanadamu  na kwauwezo wa Allah atakutatulia shida zako inshaalah

Shekhe yassini Saidi anatibu kutumia qur an na rukaiyah pamoja na dawa za kiarabu na za kiafrika


Je? Una Mpenzi,mchumba,mume,mke, aliye kuacha na anaishi na MTU mwingine au anakuahidi ahadi alafu hatekelezi ahadi zake 


SHEKHE YASSINI SAIDI atakusaidia
 @shekhesaidiyasini anatumia picha, au jina la muhusika na kumaliza tatizo lako.

SHEKHE YASSINI SAIDI Anatafsiri ndoto kushinda bahati nasibu, nyota,mvuto wa mwili, Miliki Pete Yabahati Kutoka Falme Kuu bila Masharti Yoyote.

Pia kwa wenye tatizo la uzazi kutoshika mimba au ukishika mimba inaharibika tatizo la nguvu za kiume
Muone @shekhesaidiyasini inshaalla kwa uwezo wake Allah atakusaidia. 


Malipo Nikama Sadaka Na Utalipa Baada Ya Mafanikio.
Wasiliana nami
@shekhesaidiyasini
Whatsapp no +255 743 313 580
Piga no +255 743 313 580
Tigo +255 653 67 1650
Airtel 0683697810

Rais Magufuli Asema CCM hawakutaka amteue Dk. Bashiru Ally kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho

$
0
0
Rais  John Magufuli amesema kuna viongozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao hawakutaka amteue Dk. Bashiru Ally kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho.

Amesema moja ya hoja ya viongozi hao ni kuwa msomi huyo alikuwa anadaiwa kuwa mwanachama wa Chama cha Wananchi (CUF).
 
Rais Magufuli aliyasema hayo jana wakati wa kongamano la Hali ya Uchumi na Siasa nchini lililofanyika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa nchi, wasomi, wanasiasa na viongozi wa dini.

Rais Magufuli alisema Dk. Bashiru alipigwa vita na wanachama wa CCM kupewa nafasi hiyo, lakini aliamua kumteua.

"Hata Dk. Bashiru Ally wakati namleta CCM, alipigwa vita sana na wanaCCM, wakasema huyu ni mwanachama wa chama cha CUF," Rais Magufuli alisema na kuongeza:

"Ndiyo nawaeleza ukweli, hali ilivyokuwa wakati wa kumteua Dk. Bashiru. Na mimi nikasema nataka mtu wa CUF wa namna hii aje CCM. CCM hao hao hawakutaka mabadiliko na palikuwa na 'ka-syndicate' (kikundi cha watu waliokubaliana kuungana kufanya jambo) fulani. Na ndiyo maana namshukuru huyu mwanaCUF kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kunisaidia kufanya kazi nzuri ndani ya chama."

Dk. Bashiru ambaye alikuwa mhadhiri wa sayansi ya siasa katika chuo hicho, aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM Mei 29, mwaka huu, akichukua mikoba ya Abdulrahman Kinana aliyestaafu.

Mke wa Mchungaji Akutwa Amejinyonga Kanisani

$
0
0
Mke wa Mchungaji wa Kanisa la Last Church, Rusajo Mwambene (40), amekutwa amekufa kwa kujinyonga kwa kamba ndani ya kanisa hilo, katika Kijiji cha Shilinga Kata ya Ngulilo wilayani Ileje mkoani Songwe.

Selina Kayange, mkazi wa Ileje, alisema mwanamke huyo alikuwa na mtoto mchanga, ambaye alifariki dunia siku chache zilizopita.

Selina alieleza kuwa tangu kufariki dunia kwa mtoto huyo, mwanamke huyo alibadilika na alikuwa akienda makaburini kulia na baadaye hakuonekana nyumbani.

Alisema baada ya kutoonekana, waumini walipoingia katika kanisa hilo kwa ajili ya kufanya ibada, walimkuta akining’inia juu ya dari akiwa ameshakufa kwa kujinyonga kwa kamba.

Alisema hali hiyo ilizua taharuki kwa wakazi wa eneo hilo na wilaya kwa ujumla.

“Kitendo cha kuchukua maamuzi magumu ya kujiua kimeushangaza umma kutokana na kuwa ni mke wa mchungaji, lakini tumeshirikiana na viongozi kuuzika mwili huo baada ya uchunguzi wa kipolisi na kitabibu kukamilika,’’ alisema Kayange.

Ofisa Mtendaji wa kata hiyo, Nickodemus Yanga, jana alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo, na kusema alipata taarifa kutoka kwenye uongozi wa kijiji kisha alitoa taarifa kwa viongozi wa wilaya ambao walifika katika eneo hilo kwa ajili ya uchunguzi.

Sukari Ya Kupanda Ni Tatizo Linalo Weza Kudhibitiwa Kwa Tiba Asilia

$
0
0
Unasumbuliwa na tatizo la sukari ya kupanda kwa muda mrefu ? Umejaribu tiba mbalimbali bila mafanikio?

Kama jibu lako ni NDIO nasi hii ni HABARI NJEMA SANA KWAKO.

Ipo dawa ya asili ambayo inasaidia sana kutibu tatizo la.sukari ya kupanda.

Kazi za dawa hii ni pamoja na kushusha sukari iliyo panda pamoja na kudhibiti kiwango cha sukari mwilini.

Dawa hii pia ni nzuri sana.kwa wanaume wenye tatizo la.ukosefu wa nguvu za kiume ambalo linasababishwa na.sukari. Dawa hii inaanza kuonyesha Matokeo mazuri ndani ya Siku saba.

Mtumiaji wa dawa hii anashauriwa kupima sukari yake ndani ya Siku saba tangu alipoanza kuitumia dawa hii ili kujionea mwenyewe ufanisi wa tiba hii na kuweza kuona namna ambavyo sukari yake imeshuka na baada ya hapo anashauriwa kuwa anapima kila baada ya Siku tatu hadi sukari yake itakapo fika normal.

KWA WENYE SUKARI NA PRESHA :
Uzoefu unaonyesha kuwa watu wengi wenye kusumbuliwa na tatizo la sukari huwa wanasumbuliwa na tatizo la presha pia.

Kwa.mtu mwenye tatizo la sukari ya kupanda ambalo lina ambatana na presha ya.kupanda anaweza kutumia dawa mbalimbali za asili kutibu tatizo la presha.

Moja kati ya dawa hizo ni pamoja na majani ya ukwaju. Majani ya ukwaju yanawasaidia sana watu wenye presha ya kupanda.

Jinsi yanavyo tumika unachukua majani fresh ya ukwaju kiasi cha kujaa viganja viwili vya mkono una yatwanga kwenye kinu au kuyaponda ponda had yalainike kabisa halafu unachanganya na.maji nusu Lita kisha unakamua pamoja na maji kupata kimiminika chake. Utatumia kunywa robo Lita asubuhi na robo Lita nyingine unatumia kunywa usiku kwa muda wa Siku ishirini na.moja.

Kama utashindwa  kutwanga au kuponda ponda unaweza kutumia blender.

Majani hayo hayo ya ukwaju juisi yake inasaidia sana kuongeza maziwa kwa akina mama wanao nyonyesha. Inaongeza maziwa kwa kiasi kikubwa sana na kwa haraka sana.

Kupata dawa hii ya sukari fika katika duka la kuuza dawa za asili la Neema Herbalist.

Tunapatikana Ubungo jijini Dar Es Salaam jirani na.Shule ya Msingi Ubungo National Housing nyuma.ya jengo la Ubungo Plaza.

Kwa wateja wetu waliopo jijini Dar Es Salaam ambao hawana nafasi ya kufika ofisini kwetu, tunayo huduma ya kuwapelekea dawa mahali walipo ( Home & Office Delivery )

Na kwa wateja wa mikoani tunawatumia dawa kwa njia ya usafiri wa mabus mbalimbali.

Wasiliana.nasi kwa simu namba : 0693 005 189.

Mwanafunzi Atishia Kujinyonga Kisa Kulazimishwa Kwenda Shule

$
0
0
Mwanafunzi wa kike (15) aliyekuwa kidato cha kwanza Shule ya Sekondari Nsemlwa, Manispaa ya Mpanda, mkoani Katavi amenusurika kujiua kwa kujinyonga baada ya baba yake Bushiri Joseph, kumuwahi akiwa tayari amepanda juu ya kiti baada ya kulazimishwa kuendelea na masomo.

Mwanafunzi huyo pamoja mwenzake wa kiume mwenye umri wa miaka 16, anayesoma kidato cha pili katika shule hiyo, wanadaiwa kuwa watoro sugu na kutishia kujiua kwa kujinyonga kwa kamba au kunywa sumu iwapo wazazi na walimu wao wataendelea kuwalazimisha kuendelea na masomo.

Licha ya kuhojiwa na wazazi na walimu wao, wanafunzi hao hawakuwa tayari kueleza kinachowasababisha wakatae kuendelea na masomo na badala yake wamekuwa wakitishia kujiua kama watalazimishwa kurejea shuleni.

Inadaiwa kuwa wazazi wa wanafunzi hao wameshawafikisha kituo cha polisi bila mafanikio, wakiwa na msimamo wao wa kujiua.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Edgar Mwaisunga, aliwaambia waandishi wa habari kuwa mwanafunzi huyo alifikishwa na baba yake mzazi shuleni hapo kujiunga na kidato cha kwanza Januari, mwaka huu.

"Baba yake alikuwa amemnunulia kila kitu alichohitaji binti yake, lakini miezi miwili baadaye alianza utoro, tukimhoji alikuwa akidai kuwa hataki kuendelea na masomo...tulidhani kuwa ni mjamzito, lakini alipopimwa hakuwa na ujauzito,” alisema.

Alisema walimu walijitahidi kumsihi, lakini msichana huyo alikataa kata kata kuendelea na masomo...lakini alikuwa haelezi kwanini hataki kuendelea na masomo, huku akitishia kujiua kama atalazimishwa kuendelea na masomo," alisema.

Kwa mujibu wa Katibu wa Baraza la Kata ya Uwanja wa Ndege, Manispaa ya Mpanda, Salum Msimani, wanafunzi hao wawili ni miongoni mwa 17 wa Shule ya Sekondari Kasimba, Manispaa ya Mpanda, waliofikishwa katika Baraza la Kata na kufunguliwa mashtaka ya utoro shuleni.

"Wanafunzi hao msichana na mvulana waliokuwa wakisoma katika Shule ya Sekondari Nsemlwa, wakiwa na wazazi na walezi wao walifikishwa wiki iliyopita kwenye Baraza la Kata la Uwanja wa Ndege, Manispaa ya Mpanda na kusomewa mashtaka yao baada ya mkuu wao wa shule na bodi ya shule hiyo kuwasilisha malalamiko dhidi yao na wazazi wao kwenye baraza hilo," alieleza Msimani.

Msimami alisema wanafunzi hao wakiwa kwenye baraza hilo waliendelea na msimamo wao wa kukataa kuendelea na masomo, huku wakisisitiza kuwa kama watalazimishwa kuendelea na masomo watajiua kwa kujinyonga kwa kamba au kunywa sumu .

Alisema, walipotakiwa kueleza sababu zinazowafanya wakatae kuendelea na masomo hawakuwa tayari kuzieleza.

"Baraza hili limeshindwa kutoa hukumu dhidi ya wanafunzi hawa wawili na hata shuleni walikokuwa wanasoma walimu wameinua mikono, pia polisi wamefikishwa na wazazi wao, lakini imeshindikana wameng'ang'ania msimamo wao,” alisema na kuongeza:

“Kama Katibu wa Baraza hili la Kata natarajia kuonana na Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda kwa ushauri wa kisheria," alisisitiza.

Aidha, alieleza kuwa kamba aliyotaka kujinyongea mwanafunzi wa kike na kiti alichokuwa amepanda, vipo katika ofisi za baraza hilo.

Baba mzazi wa mwanafunzi huyo wa kike, Bashir Joseph, amedai kuwa hivi karibuni alipomlazimisha binti yake kwenda shuleni aligoma na kuingia chumbani kwake alikokuwa ametundika kamba ya kujinyongea na kumkuta akiwa amepanda kwenye kiti tayari kwa kujinyonga.

Naye baba mzazi wa mwanafunzi wa kiume, Sadok Isha, amedai kuwa pamoja kuchukua hatua mbalimbali za kumfanya kijana wake huyo aendelee na masomo, lakini imeshindikana baada ya kutishia kujinyonga.

Diwani wa Kata ya Uwanja wa Ndege, Stephano Asalile, alisema kwa tukio la wanafunzi hao wawili linaonyesha jinsi ambavyo baadhi ya wazazi wa wanafunzi wamekuwa wakipewa adhabu kutokana na utoro wa watoto wao, kumbe tatizo lipo kwa watoto wenyewe.

Tromex Power : Dawa Bora Na Imara Ya Nguvu Za Kiume

$
0
0
TROMEX POWER DAWA BORA NA IMARA ya   NGUVU ZA KIUME; Baada ya kufanyiwa utafiti na majaribio sasa imeingia sokoni 

Habari njema kwa tanzania pamoja na africa nzima mkombozi wa ndoa yako ni dawa anbayoitwa TROMEX. 

Dawa hii imeonyesha uwezo wa hali ya juu katka kutibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume ,dawa hii ni mpya na inapatikana katika clinic yetu 

Dawa hii ni dawa ya asilia ya mitishamba,mwaka juzi tuliipeleka nchini Ghana kwa ajili ya utafiti  katika utafiti ilishindanishwa na dawa zingine 4 kutoka nchi kenya, Uganda, msumbiji, pamoja na kongo, na imeonyesha asilimia 92 imeonyesha inauwezo mkubwa wa kutibu tatizo kwa mda mfupi sana 

Katika utafiti huo watu 1839 ambao walikuwa legelege walipewa dawa hii kwa ajili ya majaribio,baada ya kuitumia watu 1792 walipona kabisa na sasa wanaweza kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3 kwa wakati mmoja na watu 38 hawakupona kabisa pia watu 9 hawakurudi kuleta majibu 

Dawa hii ukiitumia itakufanya uwe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3 bila hamu kuisha

Dalili za upungufu wa nguvu za kiume ni kushindwa kurudia tendo la ndoa...Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa....Korodani moja kuvimba,tumbo kuunguluma na kujaa gesi, pia inazalisha homons za uzazi kwa mwanaume ambaye mbegu zake za uzazi ni nyepesi ambazo hazina virutubisho vya kuweza kumzalisha mwanamke 

Pia inauwezo wa kufanya maumbile yawe marefu kama yameingia ndani na kuwa mafupi sana, pia inatibu magonjwa zaidi ya 6 

Itumie sasa dawa hii inapatikana katika Clinic yetu iliyopo Kawe DAR mikoani tunatuma kwa njia ya mabasi 

Ukiwa nje ya nchi tunatuma kwa njia ya EMS ..maelezo zaidi 0756726865/ 0716096205 au tembelea    www.kihembehebalist.blogspot.com

Halima Kimwana: Ni Haki Yake Diamond Kubadili Wanawake Atakavyo

$
0
0
Dada wa hiari wa msanii Diamond Platnumz, Halima Kimwana amesema kuwa muimbaji huyo kubadili wanawake kila mara ni kitu ambacho hakimsumbui.

Akizungumza na Wasafi TV amesema mwanaume kubali wanawake ni jambo la kawaida hivyo hawezi kuona ni kitu cha tofauti.

"Mimi mdogo wangu akibadilisha wanawake siwezi kukasirika kwa sababu mdogo wangu ni mwanaume na mwanaume anatakiwa abadilishe wanawake," amesema.

"Mwanamke yeyote atakayekuja kwa mdogo wangu ni wifi yangu siwezi kumchagulia mwanamke," amesema.

Muimbaji Diamond Platnumz ameshakuwa na mahusiano na warembo kadhaa maarufu kama Wema Sepetu, Penny, Zari The Bosslady na Hamisa Mobetto.

Rais Magufuli Asimulia Alivyofunga Ndoa bila shamrashamra wala mbwembwe

$
0
0
Rais John Mafuguli amesimulia alivyofunga ndoa na mke wake Janeth bila shamrashamra wala mbwembwe kama ilivyozoeleka.
 
Akizungumza katika Kongamano la Siasa na Uchumi lililofanyika jana jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli alisema siku hiyo hakuvaa suti wala mke wake hakuvaa gauni la harusi.

Alisema siku hiyo alivaa suruali na shati la kawaida na hata pete aliyomvalisha mke wake Janeth alinunuliwa na Padri wa Kanisa la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambayo ilikuwa ya madini ya shaba.

“Nimefurahi kupata mwaliko wa kuja hapa, Chuo Kikuu ambacho nina historia nacho. Nimesomea hapa shahada yangu ya kwanza na nilikuwa nakaa bweni namba tatu baadaye nilikaa bweni namba moja jengo F,” alisema Rais Magufuli.

Alisema jambo kubwa analokumbuka ni pale alipofunga ndoa katika Kanisa la Chuo Kikuu na Padri Msemwa ambaye kwa sasa yuko mkoani Tanga ndiye aliyewafungisha.

“Kikubwa Chuo Kikuu nilifungia ndoa hapa na utofauti na ndoa mlizozizoea mimi sikuvaa suti na wala mke wangu hakuvaa shela, lakini tulifunga ndoa kwenye Kanisa la Chuo Kikuu. Tulikwenda kwa Padri nakumbuka siku hiyo pete alitununulia yeye na ilikuwa ya shaba na alitupa soda. Mimi nilikunywa Pepsi na mke wangu alikunywa Mirinda,” alisema.

“Si kwamba sikuwa na uwezo ila nilijua huo ndio utaratibu na kuanzia hapo hata watoto wangu watatu wamefunga ndoa nikiwa Rais na hamjawahi kusikia sherehe zao mpaka leo,” alisema.

Kwenye hotuba yake, Rais Magufuli alizungumzia mafanikio ya serikali yake yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitatu, tangu alipoingia madarakani Novemba 5 mwaka 2015.

“Uongozi ni mgumu, ukiingia chumbani kwangu hata leo utakuta mafaili yamejaa hadi mlangoni, hata wakati mwingine huwa najiuliza watangulizi wangu walikuwa wanafanyaje? Na kila faili lina umuhimu na huwezi kumpelekea mtu mwingine, kazi ya urais ni ngumu na inahitaji moyo,” alisema Rais Magufuli.

Alisema mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitatu ni mengi na kila mwezi serikali imekuwa ikipeleka Sh. bilioni 23 kwa shule nchini kuendeleza sera ya elimu bure na kwamba fedha hizo zinapelekwa moja kwa moja katika shule bila kupitia halmashauri.

Pia alisema serikali imeongeza bajeti katika mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu hadi kufikia Sh. bilioni 483.

Rais Magufuli alisema zaidi ya Sh. bilioni 660 zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa barabara za Jiji la Dar es Salaam, kupanua uwanja wa ndege namba tatu kwa kutenga Sh. bilioni 560.

Alisema wamepanga pia kununua rada zitakazofungwa katika maeneo yote ya nchi, ili ndege zitazokuwa zinapita katika anga ya Tanzania ziweze kulipia.

Masunzu Power Mix Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
🌸MASUNZU POWER MIX; ni dawa ya asilia yenye mchanganyiko wa mitishamba 7 yenye maajabu yafuatayo (1) inatibu upungufu wa nguvu za kiume Mara dufu na kuimalisha uume   uliolegea wakati wa tendo la ndoa 
(2) kurefusha uume uliorudi ndani nchi 5-8 
(3) kunenepesha uume sm4 ya upana itakufanya uchelewe kufika kileleni dk (15-20) kwa tendo la kwanza na utakuwa nauwezo wa kurudia tendo la ndoa Mara (2-4) bila hamu kuisha nainatibu kabisa. 

Dawa hii haina madhara yoyote kwa mtumiaji huanza kufanya  kazi baada ya dk 50 tu🌾🌾🌾🌾🌾🌾🌾🌾      

 MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA ;ngiri. au umejichua kwa muda mrefu. Punyeto kisukari. Presha. Tumbo kujaa gesi na kuunguruma chini ya Kitovu. Kutopata choo vizuri. Msongo wa mawazo. Kaswende. Gono. Haya yote husababisha kuwa na maumbile madogo na kukosa nguvu za kiume 

🌸SOSOMA DX. ni dawa ya kumvuta mme au mke au mpenzi wako arudi haraka na kuanza mapenzi mapya kama mlivyo anza mwanzo baada ya masaa 2 atarudi na kutulia ndani ya nyumba na kutimiza ahadi yako 

🌸GINDU EXTRA; ni dawa ya kutibu kisukari siku 14 unapona kabisa hata kama imepanda itashuka haraka Sana. Tunatibu busha bila upasuaji nk. 

Dar es salaam tunapatikana Buguruni chama au unaweza kuletewa popote ulipo wasiliana na tabibu ATHUMAN SIMU +255767104343 / +255653207272
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>