Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Uteuzi Mwingine Tena Uliofanywa Na Rais Magufuli Leo October 30


RC Makonda Afunguka Tena Sakata la Video Chafu za Amber Rutty

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda amefunguka tena kuhusiana na video chafu za mrembo Amber Rutty na mpenzi wake lakini pia kuhusiana na ongezeko la mashoga katika jiji la Dar es Salaam.

Akiongea na waandishi wa habari jana October 29, 2018, RC Makonda alisema kuwa Amber Rutty na mpenzi  wake bado  wapo lupango  wakati wanasubiriwa kupandishwa kizimbani na kuweka wazi kuwa adhabu yao ni kifungo cha  maisha jela au miaka 30 kama itatbitika wanafanya kinyume na maumbile.

"Tayari yule binti anayeitwa Amber Rutty pamoja na bwana yake wapo chini ya polisi tangu kipindi kile nilivyotoa maelekezo na niseme kuwa kosa lile liko wazi na sheria inasema ni aidha kifungo cha maisha au miaka 30, hiyo yote ni kuonyesha ni jinsi gani serikali isivyopendezwa na mienendo inayomomonyoa maadili ya taifa letu”. Alisema Makonda

Lakini pia RC Makonda alitangaza vita na mashoga wote ambao wanajihusisha na shughuli za kufanya mapenzi kinyume na maumbile;

"Naomba nitoe fursa hii kwa wakazi wa Dar es Salaam, namba yangu ya simu inafahamika .Nimepata taarifa kwamba kuna mashoga wengi sana kwenye mkoa wetu na mashoga hawa ndio kazi yao wanajinadi kwenye mitandao ya kijamii, kwa hiyo nawaambia wananchi kama kuna shoga yoyote unamfahamu leo mpaka jumapili napokea taarifa zao”.

Shahidi adai Mshahara na Posho za mhasibu Takukuru Ilikuwa Sh 334,175,332.05.

$
0
0
Ofisa  Uchunguzi Mwandamizi kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Naza Alawi (43), amedai mahakamani kwamba  aliyekuwa  Mhasibu Mkuu wa Takukuru, Godfrey Gugai, alifukuzwa kazi baada ya kukutwa na hatia ya kukosa uaminifu.

Kipato cha mshtakiwa huyo cha mshahara na posho katika kipindi chote cha ajira kilikuwa   Sh 334,175,332.05.

Shahidi huyo alidai hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba.

Akingozwa na Wakili wa Serikali Vitalis Peter, shahidi alidai majukumu yake kusimamia dawati la mishahara, kuandaa malipo, kulipa kodi mbalimbali na kutunza kumbukumbu ya daftari la watumishi waliokopa.

“Gugai alianza kazi Juni mwaka 2001 hadi Julai mwaka 2016 utumishi wake ulipokoma baada ya kufukuzwa kwa kukosa uaminifu.

“Alikutwa na mali ambazo hakuzitolea tamko kwenye tamko la mali, nilipewa maelekezo na mhasibu ya kuchambua mishahara ya Gugai kuanzia alipoanza kazi hadi alipofukuzwa, “alidai.

Alawi alidai mshahara wa Gugai alipoanza kazi Julai mwaka 2001 ulikuwa Sh 152,630, Februari mwaka 2004 ulipanda na kufikia Sh 191,822.15 ,hadi anafukuzwa kazi mshahara wake ulikuwa Sh 4,417,838.

Anadai posho za mazingira magumu Julai mwaka 2001, alikuwa analipwa Sh 45,000, Machi mwaka 2008 alilipwa Sh 341,784 na mpaka anafukuzwa posho hiyo alikuwa analipwa Sh 1,362,800.

Shahidi alidai posho ya matibabu alilipwa Sh 150,000 kuanzia Agosti mwaka 2006 hadi Juni mwaka 2003 na posho ya nyumba ilikuwa Sh 92,858.40 Julai 2007 na Mei mwaka 2009 ilipanda na kuwa Sh 142,450.

“Kwa kipindi chote cha ajira Gugai alilipwa   mshahara wa Sh 218,916,859.65, posho ya mazingira magumu  Sh 99,944,099.50, posho ya matibabu Sh 12,450,000 na posho ya nyumba j Sh 2,864,372.90.

“Jumla ya kipato chote cha Gugai katika kipindi chake cha ajira ni Sh 334,175,332.05,”alidai Alawi.

Shahidi huyo pia alichambua mshahara na posho za mke wa Gugai, Lina Francis, aliandikia ripoti ambayo alitaka kuitoa mahakamani kama kielelezo.

Wakili wa utetezi, Alex Mgongolwa alipinga kuwasilishwa   ripoti hiyo akidai kwamba muhusika hakuwapo  mahakamani.

Baada ya hoja hiyo mahakama iliahirisha kesi hadi leo kwa ajili ya kuendelea na ushahidi baada ya kujiridhisha kuhusu sheria inasemaje katika mazingira hayo.

Mbali na Gugai, washtakiwa wengine  ni George Makaranga, Leonard Aloys na Yasin Katera.

Katika kesi ya msingi, Gugai na mwenzake wanakabiliwa na makosa 43, kati ya hayo 19 ni ya kughushi, 23 ni utakatishaji fedha na moja ni kumiliki mali zilizozidi kipato halali.

Gugai anakabiliwa na shitaka la kumiliki mali kinyume na kipato chake, ambako alitenda kosa hilo kati ya January 2005 na Desemba 2015.

Inadaiwa   akiwa  Dar es Salaam kama mwajiriwa wa Takukuru alikuwa akimiliki mali za zaidi ya Sh bilioni 3.6 ambazo hazilingani na kipato chake cha awali na cha sasa huku akishindwa kuzitolea maelezo.

Tanzania Yashikilia Msimamo Wake wa Kutosaini Mkataba wa EPA

$
0
0
Waziri  wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi, ameongoza ujumbe wa Tanzania ulioshiriki mkutano  wa pamoja wa 16 wa mawaziri wa biashara wa nchi za Afrika, Caribbean na Pacific (ACP) na Umoja wa Ulaya (EU) uliofanyika  Brussels.  Ubelgiji.

Kwenye mkutano huo Tanzania ilisisitiza azma ya kutosaini mkataba wa EPA.

Mbali na mkutano huo, Profesa Kabudi alishiriki mkutano wa 21 wa Kamati ya Mawaziri wa Biashara wa ACP.

Taarifa   iliyotolewa jana, ilisema mikutano hiyo miwili ilitanguliwa na mkutano wa makatibu wakuu wa nchi za ACP wanaosimamia masuala ya biashara.

Ilisema katika mkutano huo, Tanzania ilisema mkataba wa EPA hauwezi kuwa nguzo au chachu ya maendeleo  kama ilivyo katika malengo yake kwa kuwa hautoi fursa kwa nchi za ACP kukuza sekta ya viwanda na biashara.

Ilisema badala yake mkataba huo una sura ya misaada kutoka EU kwenda ACP na umelenga nchi za ACP kuwa soko kuu la bidhaa za EU.

Taarifa hiyo ilisema mkataba huo una vikwazo vingi visivyo vya ushuru ambavyo husababisha nchi za ACP zishindwe kufanya biashara ya bidhaa na huduma na nchi mbalimbali za EU.

“Tanzania ilirejea msimamo wake wa awali wa kutosaini mkataba wa EPA hadi hapo utakapoboreshwa na kuwa na sura ya ushirikiano wa maendeleo ya uchumi.

“Baada ya Tanzania kutangaza msimamo wake, baadhi ya nchi nyingine za ACP ziliunga mkono hoja hii na kuhamasisha nchi nyingine zaidi za ACP zichukue msimamo wa Tanzania,” ilisema taarifa hiyo.

Ilisema katika mikutano hiyo   Profesa Kabudi aliongozana na Naibu Katibu Mkuu, Biashara na Uwekezaji kutoka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Dk. Edwin Mhede na wataalamu wengine waandamizi kutoka Wizara ya Viwanda, Viashara na Uwekezaji, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, na Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania jijini Brussels.

Tanzania ni miongoni mwa wanachama wa Nchi za  Afrika, Caribbean na Pacific (ACP)   tangu mwaka 1975. Nchi hizo za ACP zimekuwa na majadiliano na Umoja ya Ulaya (European Union – EU) kwa lengo na kukuza ushirikiano miongoni mwao.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa pekee iliyotibu watu wengi nchini na nje ya nchini kwa kufanya kazi Mara 3 kwa wakati mmoja 1 ...kurefusha uume na kunenepesha saizi upendayo, kuogeza nguvu za kiume na inatibu matatizo , ikisha tibu aina madhara inaimalisha mishipa ilio regea na uzalishaji wa mbegu za kiume. TAHADHARI HAKIKISHA UNA MKE AU    MPENZI. 

NINI HUCHANGIA MATAZO HAYA . Ngiri ni chanzo Kikubwa cha matatizo,haya kujua kwamba una ngiri dalili zake ni 1.kufika haraka kileleni wakati  watendo la ndoa 
2.Kushindwa kulundia tendo la ndoa 
3.Kutoa choo kama cha mbuzi 
4. Tumbo kujaa gesi na kuunguruma 
5 kukosa choo kabisa 
6 Maumbile kuingia ndani na kuwa mafupi 
7 korondani moja kuvimba 
8 kutosikia hamu ya tendo la ndoa
 9 maumivu ya kiuno na mgongo  

Pia tunatibu busha bila kufanyiwa opresheni .Umeachwa na umpendae na bado unamwitaji?

WASILIANA  NA MTALAM  CHALLO 0714 006521. YUPO MBAGALA.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

MWIFU: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0782682648  au 0656 551 093  au 0746473974

Angela Merkel atangaza kuachia ngazi 2021

$
0
0
Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel ametangaza kuwa hatagombea tena uongozi wa chama chake cha Christian Democratic Union -CDU, na kwamba muhula wa sasa wa ukansela ambao ni wa nne madarakani utakuwa wa mwisho.

Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya chama chake jijini Berlin, ambapo amesema kuwa muda umewadia wa kufungua ukurasa mpya.

Merkel mwenye umri wa miaka 64 amekuwa mwenyekiti wa chama cha CDU tangu mwaka 2000, na Kansela wa Ujerumani tangu mwaka 2005 ambapo katika kipindi cha miaka 13 kama Kansela, amekuwa pia mwanasiasa maarufu barani Ulaya.

Aidha, Merkel amegusia mivutano ya ndani ya vyama vinavyounda mseto wa serikali anayoiongoza, ambayo imesababisha mzozo baada ya mwingine, na kuhitimisha kwamba taswira inayotoka katika serikali hiyo haikubaliki.

“Kwa uamuzi huu najaribu kuchangia katika kuiwezesha serikali ya Ujerumani kujikita katika juhudi za uongozi bora, suala ambalo wananchi wamekuwa wakidai, kitu ambacho ni haki yao, hatua hii vile vile inakwenda sambamba na azma ya serikali ya Ujerumani kufanya tathmini ya nusu muhula, kuhusu ilivyotekeleza majukumu yake, kama ilivyokubaliwa na vyama vya CDU, CSU na SPD katika mkataba wa kuunda serikali ya mseto.” amesema Merkel

Hata hivyo, mwanasiasa huyo wa Ujerumani ambaye alikuwa akichukuliwa kama mwanamke mwenye nguvu zaidi duniani, na mwenye kauli ya mwisho katika Umoja wa Ulaya, alianza kupoteza ushawishi baada ya uamuzi wake wa kuruhusu wakimbizi zaidi ya milioni moja kuingia nchini Ujerumani mwaka 2015.

Masunzu Power Mix Dawa Bora Ya Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo

$
0
0
🌸MASUNZU POWER MIX; ni dawa ya asilia yenye mchanganyiko wa mitishamba 7 yenye maajabu yafuatayo (1) inatibu upungufu wa nguvu za kiume Mara dufu na kuimalisha uume   uliolegea wakati wa tendo la ndoa 
(2) kurefusha uume uliorudi ndani nchi 5-8 
(3) kunenepesha uume sm4 ya upana itakufanya uchelewe kufika kileleni dk (15-20) kwa tendo la kwanza na utakuwa nauwezo wa kurudia tendo la ndoa Mara (2-4) bila hamu kuisha nainatibu kabisa. 

Dawa hii haina madhara yoyote kwa mtumiaji huanza kufanya  kazi baada ya dk 50 tu🌾🌾🌾🌾🌾🌾🌾🌾      

 MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA ;ngiri. au umejichua kwa muda mrefu. Punyeto kisukari. Presha. Tumbo kujaa gesi na kuunguruma chini ya Kitovu. Kutopata choo vizuri. Msongo wa mawazo. Kaswende. Gono. Haya yote husababisha kuwa na maumbile madogo na kukosa nguvu za kiume 

🌸SOSOMA DX. ni dawa ya kumvuta mme au mke au mpenzi wako arudi haraka na kuanza mapenzi mapya kama mlivyo anza mwanzo baada ya masaa 2 atarudi na kutulia ndani ya nyumba na kutimiza ahadi yako 

🌸GINDU EXTRA; ni dawa ya kutibu kisukari siku 14 unapona kabisa hata kama imepanda itashuka haraka Sana. Tunatibu busha bila upasuaji nk. 

Dar es salaam tunapatikana Buguruni chama au unaweza kuletewa popote ulipo wasiliana na tabibu ATHUMAN SIMU +255767104343 / +255653207272

Waganga wafawidhi watakiwa kujadili sababu ya vifo vinavyotokea kwenye hospitali zao

$
0
0
Waganga  wafawidhi wametakiwa   kujadili sababu ya vifo vinavyotokea kwenye hospitali zao ili kuzifanyia kazi changamoto hizo na kurudisha taarifa Wizara ya Afya.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali watu Wizara ya Afya, Dk. Otilia Gowelle, wakati wa ufunguzi wa mkutano wa waganga wafawidhi nchini,  Dodoma jana.

“Waganga wafawidhi mnatakiwa kukaa vikao vya utabibu kujadili tiba pamoja na kujadili kifo cha kila mgonjwa  kujua changamoto iliyotokea na kuipatia ufumbuzi na kuandikia taarifa   kuondokana na vifo hasa vinavyotokana na uzazi,” alisema Dk. Gowelle.

Aliwataka wataalamu wa tiba kuzingatia vikao vya tiba na kufanyia kazi changamoto au maboresho ili kuzitolea taarifa na kuzitatua pamoja na kushirikisha wadau wengine.

Dk. Gowelle aliwataka pia waganga wafawidhi kuweka mifumo ya ufuatiliaji wagonjwa   na kupokea malalamiko  katika hospitali zao   kufanya maboresho ya huduma za afya wanazozitoa na kuchukua hatua zinazostahili.

“Kupitia kikao hiki, nawataka mkae kama timu na kuandaa mipango kazi ya kuanza kushughulikia kwa ukamilifu yale yote yaliyobainika katika taarifa hiyo.

“Lengo ni kuondokana na kero wanazokabiliana nazo wananchi wanapokuja kupata huduma katika hospitali zenu,” alisema Dk. Gowelle.

RC Makonda: Nimepokea meseji 5763 kati ya hizo kuna majina 100 ya mashoga wa Dar

$
0
0
Ikiwa ni siku moja toka Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda atangaze kampeni ya kuanza kuwakamata mashoga pamoja na malaya ambao wanajiuza kupitia mitandao ya kijamii, ameanza kupata mrejesho.

Hatua hiyo imekuja baada ya msanii wa muziki, Amber Rutty kuachia video chafu mtandaoni hali ambayo ilimfanya mkuu huyo kutoa tamko la kutaka akamatwe.

RC Makonda alisema kwa tukio ambalo amelifanya msichana huyo anapaswa kufungwa jela, kwani ni ukiukwaji wa sheria za nchi huku akiwataka Wanadar es salaam kumtumia majina ya mashoga pamoja na watu ambao wanafanya biashara ya ngono mtandaoni.

“Nimepokea msg zaidi 5,763 na majina ya Mashoga zaidi ya 100 hii inaonyesha Wana DSM hawataki laana ya mashonga. Naendelea kupokea majina ya Mashoga,” amesema RC Makonda kupitia taarifa aliyoitoa siku ya leo.

Mkuu huyo amesema msako mkali wa kamata kamata ya mashoga na watu wanaojiuza utaanza wiki ijayo kwani kwa sasa anakiandaa kikosi kazi pamoja na kupokea baadhi ya majina.

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMBO ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744391089  au  0653182109

Polisi,tra Kilimanjaro Wanasa Kiwanda Feki Cha Kutengeneza Pombe Kali.

$
0
0
Na Dixon Busagaga
JESHI la Polisi mkoa wa Kilimanjaro kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wamefanikiwa kukamata kiwanda  cha kutengeneza Pombe kali ambacho kimekuwa kikizalisha bidhaa hiyo bila ya usajili.

Moja ya dira za serikali ya awamu ya tano ni kufikia uchumi wa kati kupitia Viwanda ,hata hivyo baadhi ya wafanyabiahara wanatafsiri Dira hii tofauti kwa kuamua kuanzisha Viwanda bila ya kufuata matakwa ya Sheria na taratibu za nchi.

Hali hii imejidhihirisha mkoani Kilimanjaro katika mji mdogo wa Himo baada ya Polisi,TRA na TFDA kubaini uwepo wa kiwanda bandia kinachozalisha Pombe kali .

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Hamisi Issah amesema jeshi la Polisi litaendelea kushirikiana na idara nyingine za serikali kuhakikisha kodi ya serikali inapatikana pamoja na kuhakiki ubora wa bidhaa kwa ajili ya afya ya watumiaji.

Zoezi la kubaini uwepo wa viwanda bandia katka mkoa wa Kilimanjaro ambapo katika siku za karibuni viwanda vilivyogundulika ni vile vinavyotengeneza Pombe za kienyeji na Pombe kali ,baadhi  vikiwa katika wilaya ya Rombo.
 
Mwisho.

Mwenyekiti Wa CCM Rais Magufuli Aongoza Kikao Cha Kamati Kuu Ya Chama Hicho Jijini Dar Es Salaam Leo

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya CCM katika ofisi ndogo za chama hicho mtaa wa Lumumba jijini Dar es salaam leo Okotoba 30, 2018

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Makamu Mwenyekiti wake (Bara) Ndg. Philip Mangula na Katibu Mkuu Dkt. Bashiru Ally, baada ya kuongoza kikao cha Kamati Kuu ya CCM katika ofisi ndogo za chama hicho mtaa wa Lumumba jijini Dar es salaam leo Okotoba 30, 2018
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan baada ya kuongoza kikao cha Kamati Kuu ya CCM katika ofisi ndogo za chama hicho mtaa wa Lumumba jijini Dar es salaam leo Okotoba 30, 2018. 
 
Kati yao ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Ndg. Philip Mangula na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai

Dr Mengi Kuanzisha Kiwanda Cha Kutengeneza Simu za SmartPhone Hapa Nchini....Simu Zitakuwa na Uwezo wa Kukaa cha Chaji Wiki 2

$
0
0
Mfanyabiashara maarufu Tanzania, Dk. Regnald Mengi ametambulisha ujio wa kampuni yake mpya ambayo itakuwa ni ya kwanza Tanzania kwa kutengeneza bidhaa mbalimbali za Kielektroniki, ikiwa ni pamoja na simu za mikononi, simu janja (Smartphones), computers, Ipads, music bluetooth speakers, headphones, earphones .

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, Dk Mengi amesema simu ambazo zitatengenezwa zitakuwa zinakaa na charge kwa zaidi ya wiki moja zikiwa ni maalumu kwa mazingira yenye matatizo ya umeme hasa vijijini pia aina hizo za simu zitatumika kama power Bank kucharge simu zingine.

Aidha ameeleza kuwa wanatarajia kutoa ajira zaidi ya 2000 rasmi na zisizo rasmi na kampuni itatoa kipaumbele katika kuajiri wenye ulemavu, wenye sifa stahiki

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 22

$
0
0

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   

“Nimekuelewa kocha”
“Weweee mimi sio kocha ni kapteni”
Kauli yangu ikawafanya wanafunzi wachezaji wezangu kucheka. Gafla mlango wetu ukafunguliwa na sote tukastuka, akaingia daktari wa timu huku akionekana kujawa na wasiwasi.
“Kuna nini?”
“Njooni kocha amejinyonga”
Kauli ya daktari ikatufanya tutoke humu ndani kwa kasi sana na kikimbilia chumbani kwa kocha, kitendo cha kuingia ndani humu nikajikuta miguu ikiniishia nguvu kabisa kwani ni kweli kocha amejinyonga bafuni kwenye bomba kubwa la maji kwa kutumia tai yake.

ENDELEA
Tukiwa katika hali ya sinto fahamu, akaingia meneja wa hoteli hii huku akiwa ameongozana na baadhi ya wafanyakazi wa kiume. Wakaanza kufanya juhudi za kumtoa kocha kwenye bomba hilo, wakafanikiwa na kumlaza kocha sakafuni, daktari akainama na kuweka sikio lake katika kifua cha kocha, akatutazama.
 
“Bado mapigo yake ya moyo yanadunda”
Daktari alizungumza huku akianza kuminya kifua cha kocha. Wakaingia madaktari wakiwa na machela, wakampakiza kocha juu ya kitanda hicho, wakamfunga mikanda ya kitanda hicho ili asipate mitikisiko. Wakamuwekea mashine maalumu ya kupumulia na kuanza kukisukuma kitanda hicho kuelekea katika lifti za gorofa hili. Mimi na wachezaji wezangu tukaingia kwenye lifti nyingine na tukaanza kuelekea chini. Tukafika chini na kukuta madaktari wakimuingiza kocha kwenye gari la wagonjwa na kuondoka naye katika eneo hili huku gari hiyo ikiwashwa ving’ora vya kuashiria hatari. Gari mbili za polisi zikafika katika eneo hili la hotelini. Wakashuka askari kumi na kuelekea katika chumba ambacho kocha alijinyonga.
“Nani kiongozi wenu hapa”
Mmoja wa askari alizungumza.
“Mimi”       
Nilijibu huku nikimtazama askari huyu usoni mwake na kwa kujiamini.
 
“Unaweza kutuambia ilikuwaje?”
Nikashusha pumzi taratibu ili kuyarudisha mapigo yangu ya moyo kwenye mfumo wake wa kawaida, kwani wasiwasi na woga ndivyo vilikuwa vimenitawala.
“Tulikuwa chumbani kwangu na wachezaji wenzangu, daktari yeye ndio aliye kuja kutuita na kutuambia kwamba kocha amejinyonga”
“Daktari gani?”
“Daktari wetu wa timu”
“Anaitwa nani?”
“Ruben”
Kila nilicho kizungumza askari huyu anakiandika kwenye kijikitabu chake kidogo.
“Daktari yuppo wapi?”
“Amepanda gari la wagonjwa na ameambatana na mgonjwa”
“Sawa, wakusanye wezako ili tuweze kuwahoji mmoja baada ya mwengine?”
 
“Maeleo ambayo wao watakupa ndio niliyo kupa mimi, unavyo hitaji niwakusanye kwa pamoja ni kuzidi kuwapa presha na isitoshe kesho tuna mechi ya kwanza mchana. Sinto penda wachezaji wezangu wazidi kupatwa na presha”
Nilizungumza kwa kujiamini sana hadi askari huyu akanikodolea macho ya mshangao.
“Naomba ufanye hivyo kwa maana ni mahojiano ya kawaida kabisa”
Nikashusha pumzi huku nikitabasamu kidogo, nikaingia chumbani kwangu na bahati nzuri nikawakuta wachezaji wezangu wote. Frenando akanifwata huku mwili mzima ukimtetemeka.
 
“Ethan naogopa”
“Unaogopa nini?”
“Mimi naweza kutiwa hatiani kwa tukio hili?”
“Hakuna kitu kama hicho kwani wewe ndio ulimpa tai ajinyonge?”
Niliendelea kuzungumza kwa kujiamini japo kwa namna moja ama nyingine nami nina wasiwasi mwingi sana na kama ni kweli Frenando atahisiwa juu ya picha za nguno alizo mpiga kocha basi matatizo yanaweza kuwa makubwa sana.
“Futa picha hizo kwenye simu yako na ikiwezekana simu pia iviunje kabisa”
 
Nilizungumza kwa sauti ya chini sana pasipo wachezaji wengine kuweza kusikia na wote kila mmoja yupo katika hali ya majonzi na mashaka.
“Polisi wanahitaji kufanya mahojiano na sisi hivyo naomba mujiandae kila mmoja akajibu kitu sahihi kama atakavyo ulizwa. Mumenielewa?”
Wachezaji wezangu wakaanza kulalama huku wengi wao wakitetemeka. Hali hii ikaniogopesha sana kwa maana kesho ndio siku ambayo tunatakiwa kucheza mechi yetu ya kwanza na hali ndio kama hivi.
“Hei nawaomba mutulie musiwe na wasiwasi wa aina yoyote kila kitu kitakwenda kuwa sawa. Mumenielewa?”
Hapakuwa na mchezaji aliye weza kunijibu, nikafungua mlango na kuwatazama askari watatu ambao wananisubiria mlangoni hapa.
 
“Nitahitaji mutakapo wahoji wachezaji wangu, mimi mwenyewe niwepo?”
“Hilo sio jukumu lako kuwepo, tunacho hitaji ni kuzungumza na wacheji mmoja baada ya mwengine”
“Nimezungumza hivyo nikiwa nina maana kubwa sana na kama mutashindwa kukubaliana nami basi sinto ruhusu mchezaji wangu hata mmoja kuhojiwa na mahijiano mutayafanya pale atakapo kuja mwanasheria wa shule au mwalimu mkuu sawa”
Kujiamini kwangu kidogo kukateteresha msimamo wa hawa maaskari ambao walisha kazana kumuhoji mchezaji mmoja baada ya mwengine.
“Sawa”
“Mahojiano yatafanyika kwenye moja ya chumba ambacho wachezaji wangu wanakaa, tena chumba hicho hapo mbele yangu”
 
Nilizungumza huku nikiwaonyesha chumba kinacho tazamana na chumba changu.
“Tungehiji majina ya wachezaji wako yote”
“Nendeni mapokezi, mutaweza kuona majina hayo”
Majibu yangu dhairi yakaonyesha kuto wapendeza hawa askari. Tukamuona mkuu wa shule na mwanasheria wakifika katika eneo hili. Wakasalimiana na askari hawa na kuanza mazungumzo yao ambayo sikuhitaji kuyasikia kwani ninacho kihitaji hivi sasa ni akili ya vijana wangu kuweza kuwa sawa.
“Jamani mahojiano yamesimama kwa muda, ila nina jambo ninahitaji kuzungumza nawe, naomba tukusanyike”
Wachezaji wezangu wakanitiia na wote wakaanza kukusanyika na kunizunguka.
“Frenando yupo wapi?”
“Bafuni”
“Samahani nisubirini”
 
Nikapita katikati ya wezangu hadi bufani, nikamkuta Frenando akiwa amekaa kwenye sinki huku akilia kwa uchungu sana. Nikamtazama kwa muda kisha nikachuchumaa mbele yake.
“Hei Frenando”
“Mmmm”
“Unalia nini rafiki yangu”
“Ethan ninakwenda jela mimi”
“Nisikilize kitu kinacho itwa jela hivi sasa fanya kukisahau. Kumbuka kwamba hujahusika kwenye jambo la aina yoyote ile. Kumbuka kwamba maamuzi ya kujinyonga ni ya mtu mwenyewe na bahati nzuri kocha hajakufa, na hawezi kukutaja wewe katika hili swala kwamba umehusika na tukio lake. Umenielewa”
Frenando akaka kimya huku akinitazama usoni mwake.
“Pia mimi rafiki yako nina pesa, nitahakikisha hakuna jambo lolote ambalo linaweza kutoka kwenye maisha nakuahidi hivyo”
 
“Kweli Ethan”
“Niamini mimi rafiki yangu, ninaapa kwa jila la mwenyezi Mungu siwezi kukuacha upate matatizo.”
Frenando akanikumbatia kwa furaha sana huku akijipangusa machozi usoni mwake.
“Njoo tuwape wezetu mioyo ya kucheza mechi ya kesho. Ukiwa na huzuni wewe unahisi mimi nitafanya nini kwa hawa wachezaji. Tafadhali Frenando”
“Sawa kaka nimekuelewa”
Frenando akasimama nami nikasimama, tukakumbatia kwa sekunde kadhaa.
“Ulifuta zile picha?”
“Ndio na simu nimeivunja vunja na kuidumbukiza huku chooni”
“Sawa”
 
Tukatoka chumbani humu na kumkuta mkuu wa shule akizungumz ana wachezaji. Tukajisogeza katika eneo hilo.
“Kocha wenu ndio kama hivyo amepata matatizo hakuna haja ya kuendelea kuwemo katia mashindano haya ni vyema tukakubaliana kwa pamoja, mujitoe na mutashiriki mwakani. Hali zenu hapa wote mumejawa na wasiwasi mwingi sana. Ili kuto itia shule na taifa aibu basi ni vyema musishiriki”
Maneno ya mkuu wa shule yakanikere sana na kujikuta nikikatiza katikati ya wachezaji wezangu na kusimama mbele yake.
“Kwani kocha ndio anacheza uwanjani?”
Nilimuuliza mwalimu mkuu huku nikimkazia macho.
“Kocha ndio kiongozi wa timu sasa nyinyi kama nyinyi mutafanya nini?”
“Mkuu nakuomba katika timu yangu usiweze kuendelea kuzungumza ujinga na upuuzi wa kuwakatisha tamaa wachezaji wangu. Rudisha tumbo lako shuleni kule ukakae na walimu wezako mkacheke cheke. Sawa”
 
Mwalimu mkuu akanitazama kwa hasira kwani maneno niliyo yazungumza yana udhalilishaji ndani yake kwani ana kitambi kikubwa.
“Niachie timu hii nitaiongoza mimi mwenyewe na nitahakikisha kwamba siku moja inaweka heshima katika nchi hii na dunia. Huna taaluma ya kuongoza mpira sawa”
“Ethan tazama kinywa chako”
“Siwezi kutazama kinywa changu kwa ujinga na uzembe unao zungumza. Mimi hapa ni timu kampteni na sio mwalimu mkuu na sizungumzi kama Ethan, nazungumza kama kiongozi wa wezangu. Kama wao wamekuogopa kuzungumza kile wanacho kihisi katika mioyo yao, basi mimi nitakuambia ukweli kwanza ninakuomba uweze kutoka humu ndani”
 
“Unanifukuza?”
“Sikufukuzi, ila hatukuhitaji humu ndani”
“Sasa ninapiga simu kwa waandaaji wa hii michezo na ninawambia timu yangu inajitoa na wachezaji wangu haw…….”
Kabla ya mwalimu mkuu kumaliza kuzungumza jambo lolote nikajikuta nikimkaba kooni mwake na kumsukomia hadi ukutani na kumkazia machohuku nikiendelea kumtazama kwa hasira sana hadi wachezaji wezangu wakashangaa.
“Kwenye maisha yangu sipendi kuyumbishwa, sipendi mwanaume asiye jiamini kwa maamuzi yake. Uliamua timu ije kwenye michuano na si timu ije kuyumbishwa na mpuuzi mwenzako aliye jinyonga na kuanzia hivi sasa hatuhitaji kocha wa aina yoyote. Nitasimama kama kocha mchezaji umenielewa?”
 
Nilizunugmza huku nikiendelea kumkaba mwalimu mkuu koo lake, akatingisha kichwa akimaanisha kwamba amenielwa, nikamuachia taratibu na kumfanya anza kukohoa sana huku akihema kwani kama ningeongeza dakika mbili katika kumkaba koo lake basi angepoteza maisha.
“Potea ndani ya chumba chetu”
Mwalimu mkuu akatia amri niliyo muamuru na akatoka chumbani kwangu na kuwafanya wachezaji wangu wote kupiga makofi.
 
“Hatuwezi kuyumbishwa, sisi ni wanaume na hakuna mwanamke humu ndani, hakuna mseng** humu ndani. Tukiachana na swala zima la kuleta heshima ya shule, ila tucheze kwa ajili ya heshima zetu sisi wenyewe. Kesho na kesho kutwa tutajenga historia yetu sisi wenyewe. Historia ambayo haito jengwa na mwalimu mkuu, bali ni kwa juhudi zetu sisi wenyewe. Mawazo juu ya kocha yapotee, tufikirie mechi ya kesho na hata kocha msaidizi akifika kesho alfajiri hakuna haja ya kumpa nafasi ya kuvuruga kile tulicho kipanga. Mumenielewa?”
“Tumekuelewa kiongozi”
Nikanyoosha mkono wangu wa kulia katikati ya duara hili tulilo zunguka na kila mchezaji akanyoosha mkono wake na tukaiweka kwa pamoja ikiwa ni ishara ya mshikamano wetu na umoja wetu.
“Mechi ya kwanza hadi ya mwisho, tuhakikishe kwamba tunachezwa kwa ajili ya kuchukua kombe. Kila mmoja acheze kwa uwezo wake wote anao jua yeye. Siku moja mutanikumbuka mukiwa katika klabu kubwa za mpira. Hakuna siri ya mafanikio kama kujituma kwa juhudi pasiopo kukata tamaa. Mumenielewa?”
 
“Tumekuelewa kapteni”
Tukaachanisha mikono yetu. Nikawaruhusu wachezaji wote kwenda kulala. Nikajaribu kumpigia Camila ila nikakuta simu haipatikani.
“Hivi kocha alikuwa anafikiria nini hadi kujinyonga?”
Frenando aliniuliza huku akiwa amelala kwenye kitanda chake.
“Sifahamu kwa kweli. Ila kuna mambo yake mengine aliniambia kwamba anayatafajari, nahisi hayo ndio yamempekekea kuwa katika hali aliyo kuwa nayo”
“Mmmm, Mungu amsaidie apote tu”
“Ni kweli”
“Poa Ethan usiku mwema”
“Nawe pia ndugu yangu”
Nikajifunika shuka langu na kulala usingizi fofofo.
                                                                                                                     ***
Muda wa kueleka katika uwanja ambao ndio zinafanyika sherehe za ufunguzi wa mashindano ya kombe la bara la Ulaya kwa shule za sekondari. Kila mchezaji akabeba kifaa chake anacho hitaji kwenda kukitumia uwanjani.
“Ethan nakuomba”
Koch msaidizi aliniita kabla ya kuingia ndani ya basi. Tukasimama pembeni ya basi hili na kuwaacha wachezaji wengine waendelea kuingia ndani ya basi.
“Ndio kocha”
“Mfumo ambao umekubaliana na wezako kweli mutaweza kuuhimili uwanjani kwa maana timu munayo kwenda kukuata nayo inacheza mfumo wenu?”
Kabla sijamjibu kocha simu yake ikaingia meseji. Nikaa kimya huku nikimtazama kocha anavyo soma meseji hiyo. Akashusha pumzi huku akinikabidhi simu simu yake ili niisome meseji hiyo.
 
‘Shule haito husika kwa chochote kwenye swala la mshahara wako wa ukocha, malezi na matumizi ya timu yako la sivyo jiudhuru ukocha tumuachie huyu mpumbavu timu tuoneka kama ataweza kuiongoza. Bili ya hotelini, leo ndio itakuwa siku yenu ya mwisho kukaa, nimeisitisha na muthithubutu kurudisha miguu yenu kwenye hiyo hoteli sawa Robert’
“Kocha ni nani huyu?”
“Mwalimu mkuu wenu”
Nikajikuta nikiachia msunyo mkali sana kwani sijui ni kitu gani mwalimu mkuu huyu anakifikiria kwenye ufahamu wake wa akili hadi kuamua kumshinikiza kocha kuacha ufundishaji wa timu hii.

==>>ITAENDELEA KESHO

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 130 na 131 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA       

Kidogo nikajikuta nikishusha pumzi nikimshukuru Mungu kusikia kwamba Hawa hato jihusisha kabisa na oparesheni hii.
“Sawa mrs Dany ni maelekezo yapi hayo?”
“Kwa sasa siwezi kuyatoa, hadi niweze kuwa katika sehemu salama na ya kuaminika”
“Sehemu gani unahitaji kuwa Mrs Dany?”
“Ninahitaji kuishi kwa kipindi chote cha hii oparesheni ya mume wangu hapo ndani ya ikulu yako, naamini Dany atakuja kunichukulia hapo akimaliza kazi yake.”
Maeno ya Hawa yakatufanya mimi na meja kutazamana kwani sikutegemea kama Hawa anaweza kuomba kuishi katika ikuli ya raisi wa Marekani, ambayo inasifika sana kwa kuwea kulindwa kuliko ikulu yoyote Duniani.
   
ENDELEA   
“Hilo halina shaka mrs Dany, je kuna jingine zaidi?”
“Hapana ninashukuru muheshimiwa raisi kwa kuweza kunielewa”
 
“Sawa mpatie simu Dany”
Nikaichukua simu na kutoa loudspeaker, nikaiweka sikioni kwa ajili ya kumsikiliza muheshimiwa raisi.
“Dany najua kwamba kwa sasa upo katika wakati mgumu sana, ila ninakuomba uvumilie kwa kila kazi inayo kuja mbele yako”
“Muheshimiwa raisi ninalitambua hilo, ninakuomba umlinde mke wangu”
“Nitahakikisha hakuna baya linalo mpata na ataishi hapa ikulu kwa kipindi chote ambacho utahitaji aweze kuishi hapa”
“Nashukuru kwa kusikia hivyo”
“Basi kwa sasa mke wako anaweza kutueleza juu ya mtoto wa huyo kiongozi wa boko haramu na kuanzi hapo tunaweza kuianza kazi”
“Sawa muheshimiwa raisi”
“Siku njema”
Nikakata simu na kumrudishia meja.
“Tutawahitaji katika chumba cha maelezo baada ya nusu saa”
 
“Sawa meja”
Nikabaki na Hawa ndani ya chumba hichi, nikapiga hatua hadi mlangoni, nikaufunga mlango kwa ndani na kurudi kitandani. Nikamuinamia Hawa na kuanza kumnyonya midomo yake taratibu Hawa akaanz akuipitisha mikono yake nyuma ya mgongo wangu jambo lililo zidi kutufanya tuzidi kuzama kwenye dimbwi zito la mapenzi. Taratibu nikamchomoa Hawa sindano iliyo chomwa kwenye mkono wake inayo ingiza maji kwenye mishipa yake.
Nikavua tisheti yangu na kubaki kifua wazi.
 
“Dany”   
“Mmm!!”
“Naomba”
Hawa alizungumza kwa sauti iliyo jaa mahaba mengi ndani yake,  Nilipo hakikisha kwamba yupo vizuri taratibu nikaanza kula . Kila mmoja akajitahidi kuhakikisha kwamba anamridhisha mwenzake kwa kadri awezavyo yeye mwenyewe. Mechi yetu ikamalizika ndani ya nusu saa, na sote tukajikuta tukiwa tumeridhika kwa tulicho kifanya. Taratibu nishuka kitandani, nikamnyanya Hawa kutoka kitandani, nikambeba hadi bafuni ambapo ni humu humu ndani ya hichi chumba.
 
“Dany natambua kwamba hii kazi ambayo unayo iendea ni hatari sana, ila inabidi uwe makini mume wangu kwa maana bado ninakuhitaji na bado ninakutegemea kwenye maisha yangu. Kwa sasa wewe ndio baba, wewe ndio mama na wewe ndio ndugu”
“Usijali Hawa nitahakikisha kwmaba kila jambo linakwenda sawa kama tulivyo panga sawa mama”
“Sawa mume wangu, ila ninakuomba sana tena sana uwe makini, ukishindwa hii kazi ninakuoba urudi tu, tutatafuta hata sehemu ya kwenda kuishi wawili, hakutakuwa na haya ya wewe kuendelea na haya mambo, nahitaji uwe baba mzuri atakaye ilinda familia yake kwa garama yoyote itakayo jitokeza kwenye maisha yake”
 
“Nitakuwa baba mwema, nitahakikisha hizi kazi mbili ninazimaliza, na nikimaliza hapo nitaachana na kila jambo ambalo linauhusiana na kulipiza kisasi ama usalama”
“Nitashukuru mume wangu”
Taratibu Hawa akanikumbatia huku machozi yakimwagika, taratibu nikakilaza kichwa chake kifuani mwangu huku nikimbembeleza taratibu. Taratibu Hawa akaniachia huku akifuta machozi yake usoni mwake, akaizungusha koki ya bomba iliyopo pembeni, taratibu maji yakaanza kutumwagika mwilini mwetu. Tukaanza kuogeshana huku tukicheza baadhi ya michezo ikiwemo kutekenyana katika mbavu zetu.
 
“Hapo awali sikuweza kufahamu kwamba mapenzi yana raha. Baada ya kurudi Somali juzi, nikliona maisha yangu kwangu ndio basi tena, nilihisi kwamba sinto kuona tena, na baba yangu alinihitaji kukusahau ila haikuwa rahisi kama alivyo dhani. Nililia sana, nilijaribu kujiua kwa mara kadhaa, ila niliweza kuzuiliwa, ila jana nilivyo weza kusikia uwepo wako, sikuweza kuamini sana hadi pale nilipo kuona. Dany moyo wako ninakuomba usimpe mwanaume yoyote, tafadhali ishi na mimi, tafadhali linda pemzi langu, chochote kitakacho tokea kwenye maisha yetu nakuomba ukumbuke una mwanamke anaye jiheshimu na kukupenda katika maisha yake yote”
 
“Shukrani Hawa, nitakupenda na kukujali katika maisha yangu, na kama jana ungejiua na baba yako wala nisinge weza kuifikisha siku ya leo na mimi ningekuwa nimesha jiua”
“Ila Mungu hakupanga iwe hivyo”
“Kweli”
“Tumalize nahisi watakuwa wanatusubiria sisi”
Tukamalizia kuogo na kutoka bafuni, Hawa akavaa nguo zake wanazo vaa wagonjwa huku na mimi nikivaa kombati zangu za jeshi. Nikaufungua mlango, nikakutana na meja akiwa amesimama na inaonekana ni kwa muda mrefu alikuwa amesimama akisubiria tumalize kufanya tunacho kifanya ndani ya chumba hichi.
“Tunaomba dakika tano meja”
“Sawa”
 
Nikaurudishia mlango na kumsogelea Hawa, nikazishika nywele zake ndefu zinazo karibia kufika mgongoni, taratibu nikaziweka vizuri huku tukitazamana. Nikambusu mdomoni mwake, kisha na kumshika mkono wake wa kulia.
“Upo tayari kwa kutoka?”
“Ndio honey”
Tukatoka kayika chumba hichi, tukaongozana na meja hadi kwenye chumba kikubwa, tukakuta viongozi baadhi wa jeshi, pamoja na Tv kubwa.
“Tutawasiliana na raisi muda si mrefu”
“Sawa”
Tukaka kwenye viti viwili ambavyo tayari vilisha andaliwa kwa ajili yetu. Tv hii kubwa ikawasha na tukamuona raisi akiwa katika ofisi yake nchini Marekani. Akatusalimia wote kwa pamoja na sote tukaitikia.
 
“Nisiwapotezee muda mwingi sana katika hili tunalo kwenda kulijadili hapa, ila kitu kikubwa kwamba, jana tumefanikiwa kuangusha kundi moja la Al-Shabab hapo nchini Somalia, na kiongozi wao amaeweza kuuwawa.”
“Opareshini inayo fwata kwa sasa ni kuliangamiza kundi la Boko Haramiu, ambapo wiki iliyo pita tu, liliweza kuvamia shule ya wanafunzi wa kike nchini Nigeria na kuweza kuwaua mia moja na sita huku wanafunzi mia tatu hadi sasa havi serikali ya Nigeria wala sisi hatujui ni wapi wabini hao walipo”
 
“Opareshni hii, nimemkabidhi Dany, na yeye ndio atakuwa mpelelezi katika kuweza kufahamu ni wapi kundi hilo lililo na ni wapi wanafunzi hao wameshikiliwa, kwa maana kwa sasa hatujadilia maswala ya Marekani peke yake, ila tunajadili maswala ya dunia nzima kwa ujumla. Mrs Dany amekiri na kusema kwamba anaye mtu wa karibu sana na kundi la Al-Shabab, ambaye anaweza kutuongoza sisi kufahamu ni wapi lilipo kundi hilo. Sasa Mrs Dany ninakuomba uweze kuteleza ni wapi tunaweza kumpata huyo rafiki yako”
 
Sote tukamtazama Hawa, aliye nitazama na mimi kwa sekunde kadhaa kisha akamtazama raisi tunaye muona kupitia hii Tv kubwa.
“Rafiki yangu anaitwa Yemi Okocha, ni mwana mitindo mkubwa sana nchini hapo Nigeria, na kazi zake pia baadhia nazifanya nchini Marekani pamoja na South Afrika. Yemi Okocha sio jina lake la kuzaliwa, ila jina lake halisi anaitwa Tayana Mohamed Alade. Baba yake ndio kiongozi wa Boko Haramu, alikuwa ni mwajeshi aliye hasi inchi yake na kutengeneza kundi lake hilo kubwa, linazo zidi kupata umaarufu siku hadi siku.”
 
Mtaalamu wa maswala ya mitandao, kwa haraka aliweza kutuletea picha ya Yemi Okocha, kwenye kila Laptop iliyopo katika meza hii. Ni binti mzuri sana, mredu mwenye umbo zuri ana kila sifa ya kuitwa msichana mzuri.
“Makao makuu ya Yemi Okocha ni Victoria Island Lagos na jina la kampuni yake ni Y.O Entertiment. Hayo mimi ndio ninayo yafahamu kuhisiana na Yemi Okocha, ninamaini kwamba yatakuwa ni muongozo mzuri sana kwa Dany kuanza kuifanya kazi yake”
“Tunashukuru kwa msaada wako mkubwa Mrs Dany. Naamini mumesikia wote, sasa hapo ninacho hitaji ni kuweza kufahamu mchango wenu ni jinsi gani Dany anaweza kwenda na kuanza kuifanya hii kazi”
 
“Muheshimiwa raisi nianze kwa kuzungumza mimi mwenyewe, mpango mzima wa kwenda kuifanya hii kazi ningeomba uniachie mimi, japo ninaamini kwamba itachukua muda mrefu kiasi ila itabidi nifanye hi
vyo ili kazi yetu iweze kukamilika. Ninacho kiomba katika hili, ninaomba pesa ya kutosha na nitakwenda kama raia wa kawaida kabisa kwa maana katika hili hakuna haja ya kutumia nguvu ya jeshi kwani inaweza kwenda kuinua vita kubwa. Tukiweza kupata uhakika kwamba ni wapi kundi la Boko Haramu lipo basi hapo hata nguvu ya jeshi itahitajika”
“Sawa nimekuelewa sana Dany, je kuna mtu ana jambo la kuchangia katika hii oparesheni”
Watu takatazamana na hakuna aliye zungumza kitu chochote, ikimaanisha kwamba hakuna ambaye anahitaji kuchangia chochote. 
 
“Basi meja ninakuachia jukumu zima la kuhudumia hati za usafiri kwa Dany, pamoja na pesa atakayo hitaji basi aweze kupatiwa”
“Sawa muheshimiwa raisi”
“Kikao kimekwisha”
Tv ikazimwa, taratibu tukanyanyuka, nikamshika Hawa mkono na kutoka katika chumba hichi.
“Meja naomba unipatie simu niwasiliane na raisi moja kwa moja?”
“Kuna tatizo?”
“Hili ni jambo binafsi”
“Sawa”
Meja akanipatia simu yake ambayo tayari alisha mpigia raisin a simu ipo hawani.
“Ndio meja”   
“Hapana muheshimiwa raisi ni Dany hapa”
“Ndio Dany”
“Hatujazungumzia kuhusiana safari ya mke wangu?”
“Kuna private Jet ipo jiani inakuja kumchukua mke wangu, nilihitaji kukuambia hilo baada ikiwa imesha fika, naamini baada ya msaa manne itakuwa imesha fika hapo”
 
“Shukrani muheshimiwa raisi kwa kunijali katika hili”
“Karibu na nijukumu langu mimi kuweza kufanya hivyo”
“Basi ikifika nitakujulisha muheshimiwa raisi”
“Sawa”
Nikakata simu na kumkabidhi meja simu yake.
“Dany pesa, yote itaingizwa kwenye akaunti yako ambayo kwa sasa ipo katika hatua za mwisho kufunguliwa. Hati pamoja na vitu vyote vinatengenezwa, ila itabidi kwa sasa utumie jina tofauti na Dany”
“Jina gani?”
“Utatumia Peter Lukas Otieno, uraia wako utaonekana kwamba wewe ni Mkenya, hakikisha kwamba hilo unaliweka kichwani mwako”
“Nimekuelewa meja”
“Mrs Dany, utaongozana na nesi hapo, utaeleka chumba cha mavazi, utaandaliwa nguo zako za safari ndani ya muda mfupi ndege binafsi ya raisi itatua katika kiwanja chetu na safari ya Marekani itaanza”
“Sawa meja”
“Dany naomba unifwate”
Nikambusu Hawa kwenye paji la uso kisha tukaachana na mimi nikaongozana na meja hadi katika ofisi yake. Akanikaribisha kwenye sofa nzuri zilizopo kwenye hii ofisi, sote tukaka.
 
“Unahitaji kinywaji?”
“Hapana, sijapata chai hadi sasa hivi”
“Ohoo basi mukumbuke kupata kifugua kinywa hata kabla ya mke wako hajaondoka.”
“Sawa meja”
“Dany kitu ambacho ninakuomba, ninatambua kwamba unampenda sana mke wako, natambu hilo kwa muda mchache ambao tumekaa hapa”
“Ni kweli?”
“Kitu kikubwa ninacho kuomba katika hii oparesheni hakikisha unafanya jambo lolote ili hoyo msichana awe mikononi mwako, hata ikiwezekana tumia njia ya usaliti”
“Uma naanisha nini meja?”
“Hata kwa kutembea naye kimapenzi fanya hivyo, japo natambua utahatarisha ndoa yako ila hakutakuwa na jinsi nyingine ya kufanya ziaid ya kuwa na mahusiano na msichana huyo kwa maana una vigezo vyote vya kumvutia mwanamke yoyote, hata awe mke wa mtu ni lazima atavutiwa na wewe tu.”
Maneno ya meja yakanifanya nikae kimya huku nikishusha pumzi nyingi na maneno ya Hawa baadhi tuliyo yazungumza bafuni kuhusiana na kulilinda penzi letu yakaanza kunirudia kichwnai mwangu tarataibu.


AISIIIII……….U KILL ME 131

   
“Dany, Dany”       
Sauti ya meja ikanistua kutoka katika dibwi zito la mawazo ya maneno ambayo tuliyapanga mimi na Hawa.
 
“Naam”
“Natambua ya kwamba ni ngumu sana kumsaliti mke wako ambaye unampenda.Unajua kipindi nilipokuwa na umri kama wako, nilikuwa na mwanamke niliye mpenda sana japo kwa sasa ni marehemu, ila hadi leo ninaamini kwamba kifo chake nimekisababisha mimi ila sikuwa na jinsi”
Meja alizungumza kwa sauti ya chini huku akinitazama usoni mwangu.
“Basi nilimpenda sana Elistrida, tangu tulipokuwa shule ya msingi tulianzisha mahusiano hadi tukafikia umri wa kuona. Mipango ya harusi ilifanyika, mwezi mmoja kabla ya harusi yetu niliweza kupewa kazi ya upelelezi kwenda nchini Pakistani, nilipewa jukumu la kuweza kuchunguza ni wapi lilipo kundi la Alquida.”
 
Nikaanza kumuona meja machozi yakianza kumlenga lenga usoni mwake, ila nikazidi kujikausha kimya ili kuendelea kusikiliza kwa kile anacho nisimulia kwa muda huu.
“Nilipata mwanamke mmoja wa kipakistani, ambaye niliambiwa nihakikishe kwamba ninamueka mikononi mwangu hususani kimapenzi, kutokana kipindi kile nilikuwa kijana mzuri, bado uso hajajikunja na uzee huu, basi niliweza kufanya kama nilivyo fanya. Yule msichana alinipenda sana ndani ya muda mchache sana, aliweza kunipatia kila aina ya taarifa niliyo kuwa nina ihitaji. Nilipo fanikiwa kumaliza kazi yangu, basi niliondoka nchini Pakistani na kurudi Marekani pasipo msichana yule kufahamu.”
 
“Nikiwa sielewi ni kitu gani kinacho endelea nyuma yangu, siku ya harusi ikawadia, huku baadhi ya wakuu wangu wa kijeshi waliweza kufika kanisani. Tukiwa katikati ya ibada pale kanisani, Tv zote kubwa ndani ya kanisa, zikaanza kuonyesha video ya ngono ambayo nilikuwa na yule msichana, kumbe yule binti kila kitu tulicho kuwa tunakifanya alikirekodi pasipo mimi kufahamu”
Meja machozi yakaanza kumchuruzika kwenye mashavu yake, japo ni mzee wa miaka kama stini ila ameshindwa kabisa kuyazuia machozi yake mbele yangu.
 
“Mke wangu baada ya kuona vile, akachanganyikiwa kabisa, akaanza kukimbia kuelekea nje ya kanisa, nguvu ziliniishia, ila baadhi ya wanajeshi walijaribu kumshika, katika kurupushani za kumshika, akachomoa bastola ya kijana mmoja na kwa haraka sana aliweza kujipiga risasi ya mdomo na ikatokea nyuma ya kich……”
Meya akashindwa kumalizia hadithi yake na machozi yakazidi kumwagika usoni mwake, taratibu akanayanyuka kwenye sofa alilo kalia na kutemeba hadi katika kiti kilichopo hapa ofisini kwake. Kwa ishara akaniomba nitoke ndnai ya ofisi yake. Taratibu nikanyanyuka na kumtazama usoni mwake, akaendelea kunisisitizia kwa ishara nitoke ofisini kwake. Taratibu nikachukua kitambaa kilichopo juu ya hii meza, nikakikunja vizuri na kuwa kitambaa ambacho anaweza kujifutia machozi, kisha nikamuwekea juu ya meza yake na kutoka ofisini hapa.
 
“Nesi”       
“Ndio”
“Mke wangu yupo wapi?”
“Yupo katika chumba cha mavazi”
“Unaweza kunipeleka?”
“Hakuna shaka katika hilo”
“Sawa”
Nikaongozana na nesi hadi katika chumba cha mavazi, nikamkuta Hawa akipimwa pimwa vipimo vya nguo. Nesi akatoka na kuniacha nikimtazama Hawa na wapimaji hawa ambao nao ni wanajeshi wa kike ila wana fani ya ufundi.
“Dany nimepungua eheee”
Hawa alizungumza huku akinifwata usoni mwake akiwa amejawa na tabasamu pana.
 
“Sio sana”   
“Ila ni tofauti na mwanzo?”
“Yaa ila kwa hekaheka ambazo tumezipata kupungua ni lazima”
“Kweli vipi mbona unaonekana kama huna raha mume wangu?”
“Hapana, mke wangu, wanakushonea kitu gani?”
“Kuna suti mmoja wamenionyesha picha nikaipenda sana”
“Waoo sasa wanaweza kuimaliza kwa leo?”
“Sio leo tu yaani wataimaliza ndani ya dakika kumi na tano, yaani hawa wadada ni wataalamu sana”
“Duuu kazi kweli kweli”
Nilijaribu kujifurahisha ila kusema kweli woga umesha anza kuniingia katika moyo wangu, kwani historia ya meja, imenifanya nipoteze hata hamu ya kuifanya kazi iliyopo mbele yangu.
 
“Dany ninakujua vizuri sana mume wangu, ninakuomba uniambie ni kitu gani ambacho kinakusumbua akilini mwako?”
Hawa alizungumza huku akinitazama usoni mwangu kwa macho makali. Nikaka kimya kwa sekunde kadhaa, nikawatazama wadada ambao tayari wamesha anza kuishona suti ya Hawa wakishirikiana. Nikamshika Hawa mkono wa kulia, tukasogea hadi kwenye viti vilivyopo mbali kidogo na hawa wadada japo ni ndani ya hichi chumba.
“Niambie mume wangu una tatizo gani?”
“Baby ninaogopa kuifanya hii kazi”
Hawa taartibu akashusha pumzi huku akinitazama kwa sura ya masikitiko, taratibu akanishika mashavu yangu kwa viganja cya mikono yake. 
 
“Dany natambua unaogopa kwa maana sehemu unayo kwenda ni mpya na hakuna mtu hata mmoja ambaye unamjua au aliwahi kukufanyia ubaya. Ila kumbuka kwamba hii ni vita mume wangu. Dunia nzima, watoto wadogo, wanamama, wasichana ambao wanaishi katika mateso ya kukimbia vita kila siku wanakutazama wewe, wanakutegemea wewe. Hii ni nafasi ya pekee ambayo hata kwa Mungu ninaamini atakuandikia dhwawabu. Tafadhali Dany usiniangushe chini, nipo nyuma yako hakikisha kwamba unanifanya nijisifie mbele za wanawake na hata dunia kwa ujumla kwamba mume wangu ni mtu imara na mtu makini sana”
 
Hawa alizungumza kwa sauti ya upole iliyo jaa ushawishi na mahaba mazito ambayo taratibu nikajikuta nikiishiwa na wasiwasi ambao ulikuwa umeanza kunitawala moyoni mwangu.
“Ila mke wangu sielewi hii kazi ninaanza anzaje kuifanya hembu ninaomba unipe japo mwangaza kidogo, ili niweze kufahamu kwamba binti huyo anapendelea kitu gani?”
“Ahaa, Yemi anapenda sana kuogelea, nakumbuka kipindi tupo chuo, alikuwa hapitishi hata siku mbili kabla ya kwenda kuogelea, pia Yemi anapenda sana chocolate, hivyo ni vitu vikubwa sana anavyo vipenda”
 
“Chocolate!!?”
“Yaa mbona unashangaa mume wangu?”
“Hicho ni kitu cha kaiwada sana”
“Mume wangu hujatujua sisi wanawake hususani kwa sisi ambao tunatoka katika familia za kitajiri, huwa hatapendi vitu vikubwa kwa maana kila kitu tumekikuta kwenye familia zatu na si washamba sana wa kushadadia vitu vikubwa kama gari na mambo mengine kama ilivyo kwa kuwa kwa wasichana hawa wa kawaida”
“Sawa mke wangu, sasa daaaa.”
“Dany hii kazi ndio itakufanya wewe uwe juu zaidi ya hapa ulipo. Ifanye kwa moyo mmoja, hata siku mtoto wetu aje kujisifu kuwa na baba kama wewe”
 
“Nimekuelewa mke wangu nitafanya, Mungu aniongoze katika hili”
“Namini hakuna utakacho shindwa”
Maneno ya Hawa yakazidi kunifariji na kunipa moyo wa kuifanya kazi iliyopo mbele yangu. Katika muda huu tulio kaa hapa, washonaji hawa wakawa wamemaliza kushona suti ya Hawa. Wakamkabidhi, akaijaribisha na kwa jinsi Hawa alivyo penda suti yake iwe ndivyo ilivyo kuwa.
“Umependa mke wangu”
“Yaa siivui hii suti hadi Marekani”
“Hahahaa, usifanye hivyo mke wangu”
“Sikutanii honey, hapa ndio imetoka”
Malango wa chumba hichi ukafunguliwa, akaingia meja akiwa katika hali ya furaha hadi nikabaki nikiwa nimeduwaa.
“Mrs Dany umependeza sana”
“Nashukuru meja”
“Sasa ndege imesha fika, sijui upo tayari kwa safari tuelekee uwanjani?”
Hawa akaniangalia usoni mwangu na akabaki akiwa na kigugumizi kilicho nifanya nijibu mimi.
 
“Ahaa meja naomba nipate kifungua kinywa na mke wangu kisha baada ya hapo tutaelekea uwanjani”
“Sawa tuongozane katika bwalo la chakula”
Tukaelekea katika jengo linalo tumika kwa wanajeshi kuweza kupata chakula. Tukahudumiwa na wahudumu wa hapa.
“Kusema kweli Dany na mke wako mumeendana sana, sipati picha mtoto wenu atafananiaje?”
“Atafanana na baba yake?”
“Mmmm mimi nnataka mwanagu afanane na mke wangu?”
“Wapi atafanan na wewe kwa maana wewe ndio baba”
“Sasa akiwa wa kike unataka nifanane naye pia?”
“Tena ukifanana naye atakuwa bonge moja la mrembo kwa maana mmmmmm, mume wangu wewe mzuri. Ila ninakuomba kwamba huko unapo kwenda tafadhali ninaomba unilindie penzi langu, sinto taka kusikia wala kujua kwamba umeingia kwenye mahusiano na msichana yoyote mume  wangu sawa”
 
Tukatazamana na meja kwa macho ya kuiba, jambo ambalo Hawa hakulistulia kabisa. Nikatabasamu kidogo huku nikijiweka vizuri shati langu.
“Sasa kwa mfano ukajua mume wako ametoka kimahusiano na mwanamke mwengine inakuwaje?”
“Ahaa bora oparehsni ife kwa kweli, wanawake wa sasa wana magonjwa mengi, ninampenda mume wangu, nahitaji tujenge familia yenye afanya”
“Ila hujanijibu kwamba ukijua  kwamba imekuwa hivyo utafanyaje?”
“Huyo mwanamke kwanza nitashuhulika naye kwa kweli, ni bora nirudi katika hali yangu ya ugaidi kwa muda wa kumshuhulikia huyo mwanake kisha sasa hapo ndipo hali ya kawaida itaendelea”
Nikamuona meja akishusha pumzi taratibu taratibu huku akinitazama kwa umakini sana.
 
“Ahaa mke wangu hilo jambo haliwezi kujitokeza nakupenda sana”
“Natambua hilo mume wangu na ninakuamini katika hilo”
“Nashukuru kwa kuniamni”
Tukamaliza kupata kifungua kinywa, tukaingia kwenye gari la jeshi na moja kwa moja likatupeleka hadi uwanja wa ndege. Tukakuta mizigo ya mabegi ya Hawa, iliyo jazwa nguo ikiwa tayari imesha fikishwa kwenye uwanja wa ndege. Tukashuka kwenye gari na kuanza kutembea hadi ilipo ndege hii ya kifahari inayo milikiwa na raisi wa Marekanani. Nikamsaidia Hawa kuingiza mabegi ndani ya ndege hii inayo beba abiria wasiozidi wanne.
“Mke wangu unakwenda Marekani, ninakuomba uwe makini sana, ninakuomba uhakikishe kwamba unanitunzia penzi langu, sihitaji siku itokee nijue kwamba una mwanaume mwengine ndani ya ikulu, utanifanya nibadilike, utafanya zoezi hili lote libadilike na kuwa baya sawa mke wangu”
 
Nilizungumza huku nikiwa nimekumbatia Hawa, ndani ya hii ndege.
“Nimekuelewa mume wangu, siwezi kufanya hivyo, naytambua thamani yako. Natambua umuhimu wako kwangu, nakuahidi kamwe sinto weza kufanya ujinga wa aina yoyote wa kukuumiza wewe roho”
“Ninashukuru mke wangu”
. Taratibu tukaachiana huku sote tukilengwa lengwa na machozi.
“Nakupenda sana mume wangu”
“Hata mimi pia ninakupenda, ninakuomba ukae sasa uanze safari”
 
Taratibu nikamkalisha Hawa kwenye siti, nikamfunga mkanda wa siti, taratibu nikambusu kwenye paji la uso wake, kisha nikambusu kwenye midomo yake na taratibu nikaanza kushuka pasipo kuangalia nyuma kwa maana Hawa, alisha anza kuangua kilio.
Nikapiga hatua hadi alipo Meja, taratibu mlango wa ndege hii ukafunga, mlio wa ndege ukaanza kutawala kwenye masikio yetu, taratibu ndege hii ikaanza kuondoka eneo hili, hatukuhitaji kuondoka hadi tulipo ishuhudia inaicha ardhi ya Somalia nasi ndio tukajikuta tukitazamana.
“Mke wako yale aliyo yazungumza ana yamaanisha”
“Ni kweli meja, na Hawa akizungumza ujue amezungumza inabidi kuwa makini naye sana katika hili la sivyo tutajikuta tunashindwa kufanya kitu chochote kwenye hii oparesheni”
 
“Kweli Dany”
Tukaingia kwenye gari na safari ya kurudi kwenye majengo yetu ukaanza. Simu ya meja ikaanza kuita, akaitoa mfukoni mwake na kuipokea.
“Ndio”   
“Sawa tupo njiani tunakuja”
Akakairudisha mfukoni mwake na kunigeukia.
“Hati zako za kusafiria zipo tayari na utaondoka na ndege ya saa mbili usiku”
“Sawa meja, na jina nitakalo litumia ni Peter”
“Yaa, uraia wako ni Kenya”
“Sawa meja”
Tukafika ofisini kwa meja, nikakabidhi kila kitu pamoja na kadi ya benki ambayo inaonyesha jina langu pamoja na picha yangu.
“Kwenye akaunti yako ya beki kuna dola laki tano, nina amini kwa kipindi chote utakacho kaa Nigeria zitakusaidia na endapo zitakuishia, basi utawasiliana nasi”
 
“Sawa meja”
“Nguo zako zipo katika chumba kingine, huko huwezi kwenda na hizi gwanda, wasije wakakustukia bure wakakuua mapema”
“Kweli meja”
“Basi unaweza kupumzika, hadi saa moja moja tutaonana, na nitakusindikiza uwanja wa ndege”
“Nitashukuru meja”
Nikatoka ofisini kwa meja na kumuacha aendelee na majukumu mengine. Nikaingia katika chumba cha mavazi ya kiume ambacho kipo karibu kabisa na chumba cha mavazi ya kike. Nikachagua nguo chache za kuvaa niendapo, nilipo hakikisha kwamba nimepata nguo nzuri, nikaziweka katika begi dogo la mgongoni huku nikiwa nimezikunja vizuri. Nikahifadhi hati yangu ya kusafiria ila kadi yangu ya benki nikabaki nayo mfukoni.
 
Nikaanza kuzunguka maeneo ya kambi hii ya jeshi, ambayo kusema kweli imejengwa kwa ustadi wa hali ya juu na ina eneo ambalo ni kubwa sana, nikaanza kutazama jinsi wanajeshi wa Kimarekani wanavyo fanya mazoezi yao hususani ya kijeshi, nikafika kwenye moja ya kiwanja nikakuta wanafanya mazoezi ya jinsi ya kumlinda raisi pale anapo vamiwa kwenye msafara, kusema kweli nikajukuta nikufurahi sana, japo mimi mwenyewe nilisha wahi kuyajifunza nilipo kuwa nipo NSS, ila mafunzo yao yana ubora kulilo niliyo fundishwa mimi miaka kadhaa iliyo pita.
 
    Saa kumi na mbili jioni nikarudi kwenye chumba cha mavazi, nikaingia kwenye bafu lililopo hapa chumbani, nikaoga na kubadilisha nguo zangu. Nikavaa suruali ya jinsi yenye gengi yeusi pamoja na tisheti nyeusi iliyo nibana vizuri mwili wangu, nikava buti yeusi za kisasa, nikabeba begi langu la ranyi nyeusi, mgongoni kisha nikatoka katika chumba hichi. Nikaingia ofisini kwa meja, nikamkuta akipanga panga mafaili yake vizuri.
“Hapo upo vizuri, tunaweza kuondoka sasa”
“Sawa meja”
Tukaeleka kwenye gari binafsi la meja, tukapitia kwene moja ya nyumba anayo ishi humu ndani ya kambi, akabadilisha nguo zake na safari ikaendelea. Tukafika uwanja wa ndege wa nchini Somalia ulipo hapa Mogadishu. Kabla ya kushuka kwenye gari, meja akanipatia kibunda cha dola mia mia zilizo fungwa vizuri.
 
“Ni dola elfu kumi, utatumia kwa kuanzi maisha”
“Nashukuru sana meja”
“Nikutakie safari njema”
“Shukrani”
Nikashuka kwenye gari na moja kwa moja nikaanza kuelekea kwneye gari huku nikiwa makini sana. Nikapanga foleni kwenye mstari wa abiria wanao suburia kukaguliwa. Mbele yangu kuna dada wa kizungu ameshika kioo kikubwa kiasi akijipamba nyusi zake, nikabahataika kupata upenyo mdogo wa kuangalia mtu aliye nyuma yangu, nikajikuta nikistuka baada ya kuona jamaa wawili wa kiarabu wenye ndevu nyingi wakiwa nao wamesimama kwenye hii foleni. Nikavuta kumbukumbu kwamba ni wapi nilipo waona jamaa hawa wawili. Kumbukumbu zangu zikaangukia katika kambi ya Al-Shabab, na mmoja kati ya hawa jamaa alikuwa ni mlinzi wa baba Hawa, sijafahamu ni wapi wanapo elekea ila mstari ambao nipo mimi sote tunapanda ndege moja, hapa ndipo nikaanza kupata wasiwasi mkubwa sana juu ya hawa jamaa kama hawapo hapa kwa ajili ya kutoroka basi wapo hapa kwa ajili yangu kwani mimi ndio muharibu mkubwa wa kambi yao.

==>>ITAENDELEA KESHO

Habari Njema Kwa Wenye Matatizo Ya Nguvu za Kiume, vitambi, nyama uzembe

$
0
0
(1).Fikiria ulianzia wapi? Je,ulifanikiwa au bado?

(2).Upo tayari kupona kwa haraka?

TIBA ZITOLEWAZO NI,

NGORO 4 POWER; Huongeza nguvu za kiume yenye mfumo wa unga na vidonge dozi siku(6).

MELAMELA; Hurefusha na kunenepesha uume ipo katika mfumo wa unga dozi siku (4).

KASELA; Hurudisha mke,mme,mchumba na hawara ndani ya siku mbili tu,atatimiza mahitaji yote hata Kama yupo mbali na kumfunga asiwe na mtu mwingine.

IKUMBUJA; Humfanya mtu  kupandishwa cheo kazini na kulipwa madeni au mafao yako pia na kumaliza kesi kabisa.

DUDUMA; Huongeza hips,makalio na mguu wa bia.

SWASWA: Hupunguza maziwa makubwa, kitambi, nyama uzembe, michirizi na muwasho sehem za Siri,na harufu mdomoni.

KOOLA;Hutibu magonjwa sugu ya zinaa, tumbo kujaa gesi,kuuma chini ya kitovu, kiuno ,fangasi za miguu, na kuvimba miguu au miguu kuwaka Moto.

Kwa hayo na mengineyo mfatilie DR.HINDU kwani ana uwezo wa kuhudumia ndani na nje ya TANZANIA.Kwa Dar es salaam anapatikana BUGURUNI MALAPA pia KAHAMA anapatikana MARUNGA.

Kwa wasio na mda wa kufika ofisini kwangu Nina vijana wa kukuletea mpaka ulipo kazini ama nyumbani kwako.

OFISI ZINAFUNGULIWA SAA 07 :00 ASUBUHI.

CONTACTS 0744 922 982(WhatsApp), 0716608959.

  "WOTE MNAKARIBISHWA".DR   HINDU NI SULUHISHO LAKO.

Mtalaam Wa Magonjwa Yote Sugu Nayaliyoshindikana Kama Vile Pumu, Vidonda Vya Tumbo, Busha,

$
0
0
MTALAAM NA BINGWA WA MAGONJWA YOTE SUGU NAYALIYOSHINDIKANA KAMA VILE PUMU, VIDONDA VYA TUMBO, BUSHA, NGUVU ZA KIUME.

Tatizo la upungufu ukosefu wa nguvu za kiume, maumbile madogo ya uume limekuwa kubwa kwa lika zote hapa duniani

Matatizo hayo sio mageni kigeni ni ile tiba sahihi yakutibu na kuponya haya.chanzo cha hayo matatizo ni:KISUKARI, NGIRI,CHANGO, TUMBO KUUNGURUMA NA KUJAA GESI, KIUNO KUUMA, MAUMIVU YA MGONGO,MAGONJWA YA ZINAA, KORODANI KUVIMBANAKUUMA,VIDONDA VYA TUMBO, NK.

Tiba sahihi nabora ya tatizo la nguvu zakiume ni 3Power,Nidawa ya vidonge asilia vilivyotengenezwa kwa kiwango bora na salama kwa ajili yakutibu mojakwamoja tatizo la nguvu za kiume maradufu

1,hutibu nguvu za kiume mda mfupi sana kati ya umri wa miaka 18-85 naitakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20 hadi 40 tendo lakwanza bila kuchoka naitakufanya uwe nahamu yakuendelea na tendo la ndoa zaidi ya mara 5 bila hamu kuisha.

FINA Power; Nidawa yakuboresha maumbile ya kiume kwa kunenepesha na kurefusha kwa saizi uipendayo inchi 6,7 hadi 8 kwa mda mfupi sana.dawa hizi huanza kufanya kazi kwa mda wa dk 67 ukisha tumia guarantee miaka 55 ikishakutibu.

Pia tunatibu, PRESHA, UZAZI, NGIRI, PUMU,MALARIA SUGU, VIDONDA VYA TUMBO, CHANGO AINA ZOTE, BP, BUSHA BILA UPASUAJI NK.

ISHOSHA,Nidawa ya mvuto wa biashara,kazi,,humvuta mme,mke,hawara,mchumba,unaemhitaji au hakutaki hatimizi ahadi zako kwa dhati utampata kwa mda wa dk 45 tu naatatulia milele nakumfunga asitoke inje ya ndoa.

SHEPU EXRA,Nidawa ya yakupunguza matiti,unene tumbo,kitambi kwa akina baba,hutoa mafuta mabaya mwilini,makovu sehemu mbalimbali mwilini,chunusi sugu,minyama uzembe,michirizi mwilini,nakuongeza makalio hips,mguu wa bia nk.

HUDUMA HIZI NANYINGINE NYINGI MTALAAM BINGWA DR ZENGO.

Anapatikana  Dar es Salaam.

SIMU NO; 0784,47,59,46 / 0744,92,29,82 / 0652121197

NAKAMA NAFASI YAKUFIKA OFISINI HAIPO UTALETEWA HAPO ULIPO.

CCM Yasema Mwisho wa Kuwapokea Wanaohamia Toka Vyama Vingine ni Novemba 15....Tazama Hapa Maamuzi ya Kamati Kuu

$
0
0
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimewapitisha makada wake wanne kuwania nafasi ya ubunge katika maeneo yao kufuatia kikao cha kamati kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa kukutana leo jijini Dar es salaam.
 

CCM imewapitisha waliokuwa wabunge wa maeneo hayo kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), waliotangaza kujiunga na chama hicho kwa sababu mbalimbali ikiwemo kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli.

Wabunge hao waliopitishwa ni Pauline Gekui wa jimbo la Babati, James Milya jimbo la Simanjiro, Joseph Mkundi Jimbo la Ukerewe, na Marwa Ryoba ambaye atawania nafasi ya ubunge jimbo la Serengeti.

Aidha Chama hicho kimetaja tarehe 15 novemba kuwa ndio tarehe ya mwisho kwa Chama hicho kuwapokea maombi ya wenye nia ya kujiunga na Chama hicho na kupewa dhamana ya uwakilishi kupitia tiketi ya CCM kwa wabunge na madiwani kutoka vyama vingine.

Aidha taarifa hiyo imesema baada ya tarehe hiyo hakuna kiongozi yeyote atakayepewa nafasi ya kugombea uwakilishi wa Chama hicho katika uchaguzi wa marudio badala yake watakuwa wanachama wa kawaida.

Waziri Mkuu: Nimeridhishwa na Hatua za Awali za Uwekezaji Mkinga

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea eneo la mradi wa ujenzi wa viwanda 11 katika kijiji cha Mtimbwani wilayani Mkinga, ambapo amesema ameridhishwa na hatua za awali za uwekezaji huo.

Katika eneo hilo vinatarajiwa kujengwa viwanda mbalimbali kikiwemo cha saruji cha Hengya, kiwanda cha vioo, kiwanda cha vifaa vya kisasa vya ujenzi, uzalishaji wa umeme kwa kutumia makaa ya mawe.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Oktoba 30, 2018) wakati akizungumza na wananchi katika kijiji cha Mtimbwani wilayani Mkinga akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani Tanga.

Amesema uwekezaji huo unatarajiwa kulinufaisha Taifa na wananchi wakazi wa wilaya ya Mkinga kwa kuwa kinatarajiwa kuajiri zaidi ya watu 8,000, hivyo amewaomba wananchi hao waendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji hao.

Kuhusu wananchi ambao eneo lao limechukuliwa na wawekezaji na bado hawajalipwa fidia Waziri Mkuu amewataka wawe na subira kwa kuwa wote watalipwa. “Muwekezaji amenihakikishia kwamba atawalipa wananchi wote wanaodai fidia.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuuamewataka watumishi wa umma kutenga siku tatu katika wiki na kuwafuata wananchi waishio maeneo ya vijijini kwa ajili ya kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi.

Amesema Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kuwatumikia wananchi bila ya ubaguzi wa kidini, kisiasa, rangi  na kimapato, hivyo amewataka watumishi hao wafanye kazi kwa bidii.

Awali, Mbunge wa jimbo la Mkinga, Dastan Kitandula ameishukuru Serikali kwa niaba ya wananchi wa Mkinga baada ya Serikali kufuta hati ya shamba la moa na kuirudisha ardhi hiyo kwa wananchi, pia ameomba ifute hayi za mashamba mengine yaliyotekelezwa katika Tarafa ya Maramba.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, OKTOBA 30, 2018.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images