Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan Awataka Watanzania Kumuenzi Baba wa Taifa Kwa Kuwekeza Katika Viwanda

$
0
0
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kumuenzi baba wa Taifa hayati Mwl. Julius Nyerere kwa kuwekeza katika viwanda ili nchi irejee katika uchumi wa kutegemea uzalishaji unaotokana na bidhaa za viwandani.

Ameyasema hayo leo Jumatatu Oktoba 29, katika uzinduzi wa wiki ya maonesho ya viwanda yaliyofanyika katika viwanja vya Sabasaba Picha ya Ndege Kibaha mkoani Pwani na yatafungwa Novemba Nne mwaka huu ambapo wamiliki na wafanya biashara wa bidhaa zitokanazo na viwanda vya hapa nchini watapata fursa ya kuzionesha.

Amesema katika mkoa wa Pwani kuna viwanda 429 ambavyo kati ya hivo vipo vikubwa, vya kati na vidogo ambavyo vimejengwa na vingine vishaanza uzalishaji japo kuna changamoto za soko la bidhaa hizo kwasababu uzalishaji ni mkubwa kuliko uuzaji.

“Tunategemea maonesho haya yatakuwa endelevu kwasababu viwanda hivi vinatoa ajira kwa watanzania ni matumaini yangu kuwa wafanyabiashara mtatumia fursa hii kukuza biashara zenu,  tulipotembelea baadhi ya viwanda wamiliki wageni wanataka kuondoka na kuachia uongozi na uendeshaji kwa wazawa.

“Nasisitiza kuendelea kuwepo kwa mshikamano kati ya wizara ya viwanda na biashara na  sekta binafsi ili uwekezaji ukue zaidi ya hapa na bidhaa zinapouzwa nje na zikiwa na nembo yenye kuonyesha ni bidhaa zilizotengenezwa hapa nchini ni fursa yetu ya kujitangaza, ” amesema.

Aidha ametoa rai kwa Wizara ya na Ajira na sekta zinazosimamia masuala ya  Kazi kutembelea viwanda hivyo ili kujionea jinsi wafanyakazi wanaendesha kazi zao na kujua  kama haki zao za kisheria zinafatwa kwasababu kuna maeneo aliyotembelea watu wanafanya kazi zaidi ya masaa yaliyowekwa na serikali kikatiba.

Majanga Yazidi Kumwandama Wema Sepetu.....Chama cha Waigizaji Kinondoni (TDFAA) Nacho Chamfungia Miaka Miwili

$
0
0
Chama cha waigizaji mkoa wa Kinondoni (TDFAA) kimemfungia mwanachama wake Wema Sepetu kujihusisha na masuala ya filamu kwa muda wa miaka miwili.

Huo ni mwendelezo wa adhabu kwa muigizaji huyo kufuatia kusambaa kwa video inayomuonyesha akifanya vitendo vinavyokinzana na maadili ya Mtanzania.

Chama hicho kimekwenda mbali zaidi na kutaka Mamlaka za kiserikali zipuuze utetezi unaotolewa na muigizaji huyo kwa kuwa una lengo la kuvipumbaza visimchukulie hatua.

Msemaji wa chama hicho Masoud Kaftany ameeleza kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya kamati ya maadili kujadili suala hilo kwa kina.

Amesema kamati imeunga mkono hatua zilizochukuliwa na bodi ya filamu na imeliomba Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) kumuongezea adhabu itakayomzuia asijihusishe na shughuli zozote za sanaa kwa kipindi cha miaka miwili.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

MWIFU: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0782682648  au 0656 551 093  au 0746473974

Riwaya Kali: POWER - Sehemu ya 21

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA   
   “Usiseme Ethan kocha. Tambua nimebeba dhambi kubwa sana ya kumdanganya mke wako. Je dhambi hiyo mimi nina ilipaje eheee?”
“Ethan natambua nyinyi bado ni wadogo, ila muikingia kwenye ndoa mutaweza kujua ni nini kinacho tokea hadi wanaume tunaamua kuwa na wake wa nje”
“Wacha weeee”
Frenando alizungumza kwa kejeli huku akimtazama kocha usoni mwake. Gafla simu yangu ikaanza kuita ikiwa ndani ya kibegi changu mgongoni. Kocha akatoka na macho ya hasira kwani moja ya sheria tukiwa kambini ama shuleni haturuhusiwi kuwa na simu.
“Ethan kwa nini una simu?”
Kocha aliniulza kwa kunifoke sana.
“Acha upuuzi wewe mzee. Muache apokee simu la sivyo tunakwenda kuzungumza uchafu wote kwa mke wako na ushahidi wapicha ninao”
Frenando alizungumza kwa kujiamini na kumfanya kocha kumkodolea macho na kukosa jambo la kuzungumza kwa muda huu.

ENDELEA
Nikamtazama kocha kwa muda kisha nikachukua simu yangu ndani ya kibegi na kukuta ni namba kutoka nchini Tanzania. Nikaipokea kwa haraka na kuiweka sikioni mwangu.
“Haloo”
“Ethan”
 
“Niambie mke wangu”
Nilizungumza huku nikiwa nimejawa na furaha sana huku nikiondoka katika eneo hili na kumuacha Frenando na kocha.
“Safi Ethan wangu, samahani sana kwa kushindwa kuweza kuzungumza nawe mpenzi wangu baada ya kufika”
“Usijali mpenzi wangu, ila si mumefika salama?”
“Ndio tumefika salama na asubuhi ya leo tutaanza rasmi ziara yetu ya kimasomo”
“Sawa mpenzi wangu ila ninahitaji nikuombe kitu kimoja”
“Kitu gani tena mpenzi wangu?”
“Utanikubalia?”
“Ndio mpenzi wangu nitakukubalia wewe ni mume wangu lazima ninacho kuomba niweze kukubalia.”
“Ni jambo gumu lakini”
“Niambie tu Ethan, kumbuka mimi nipo kwa ajili yako mume wangu”
“Nakuomba mukimaliza ziara yenu nchini Tanzania, usiende nchini Somalia”
“Kwa nini?”
 
“Nahisi kuna hali ya hatari itakwenda kuwatokea huko mpenzi wangu”
“Usijali mume wangu, hapa nilipo tu kuna walinzi walitangulia wiki moja kabla ya kuja nchini hapa Tanzania kwa ajilli ya kunilinda na hata huko Somalia walisha tangulia walinzi kama mia moja hivi. Wapo kwa akili yangu mume wangu”
Camila alizungumza kwa kujiamini sana na kunifanya nishushe pumzi taratibu huku nikifikiria cha kumuambia.
“Usiwe na wasiwasi Ethan wangu, tamua nina lindwa sana na hakuna wa kuniletea ubaya wa aina yoyote sawa mume wangu”
“Sawa ila nakuomba ikiwezekana usiende”
“Usijali nitakuwa nikikujulisha kwa kila hatua ambayo nina fikia”
“Sawa mke wangu”
“Ngoja nijiandae kesho nitakupigia mchana tukiwa tuna rudi”
“Sawa sawa”
 
Camila akakata simu na taratibu nikashusha pumzi na kurudi alipo simama Frenando.
“Mzee wako anatetemeka, amesha ingia ndani ya gari”
“Kwani ushahidi wa picha unao kweli au?”
“Ndio cheki hizi hapa”
Frenando akanionyesha picha za kocha na muhudumu wa hoteli jambo lililo ishangaza sana.
“Umezipiga piga vipi?”
“Muda ule nilivyo mrudishia simu, niliingia kwa kunyata ndani kwao papiso wao kujijua kwani walikuwa wapo katikati ya dimbwi la mapenzi basi nikawapiga picha za kutosha kisha nikawastua”
Tulizungumza huku tukiingia kwenye basi la wachezaji wezetu. Safari ya kurudi hotelini ikaanza taratibu huku kocha wetu akiwa amekaa siti ya mbele kabisa akionekana sio mtu mwenye furaha kabisa.
“Frenando futa hizo picha”
“Kwa nini?”
 
“Isije baadae zikaleta matatizo si unajua tupo kwenye kipindi cha mashindano na mwalimu anahitaji furaha na akili yake iweze kutulia ili aweze kufanya kazi yake kwa umakini”
“Sasa Ethan unahisi huyu katika makocha kweli ni kocha. Tunacho kifanya uwanjani ni juhudi zetu tu. Acha kwanza tumpe tumbo joto akipata akili basi atanitafuta na kukaa nami kwa upole na kuniomba msamaha”
“Msamaha wa nini tena?”
“Si unamfahamu yule mwanaye wa kike?”
“Ndio”
“Mzee alinichimba biti siku moja, sikutaka kukuambia tu. Akaniahidi akiniona naye atanipiga risasi”
“Weee”
“Ndio hataki niwe mkwe wake”
“Ila vipi mwanaye anakupenda?”
“Ndio ananipenda, na hata yeye anajisikia vibaya sana juu ya baba yake kutukataza kuwa katika mahusiano”
“Duuu”
 
“Yaa mzee analeta swaga eti mimi Mmexco siwezi kumuoa Mjerumani”
“Ana wazimu, kwa hiyo mimi Mtanzania nisioe Mjerumani?”
“Ndio maana yake”
“Poa endelea kuzishikilia ila hakikisha kwamba simu yako hupotezi wala hakuna mtu mwengine wa kuziona”
“Poa poa”
Tukafika hotelini, tukaingia kwenye vyumba vyetu vya kulala. Tukaoga kisha tukaijiandaa kwa chakula cha usiku, ambacho tunakula kwa pamoja na siku inayo fwata tunaanza mechi yetu ya kwanza. Tukiwa katika eneo la chakula, kocha hakuwa na furaha kabisa. Hata mipango ya kupanga kesho tucheze mfumo gani kocha hazungumza kabisa jambo ambalo lilianza kuwashangaza hadi wachezaji wengine kwani si kawaida yake, kwani katika kipindi cha nyuma huwa hutumia muda wa chakula kuweza kupanga mipango na sisi wachezaji wake.
 
“Ethan”
“Mmmm”
“Hembu mfwate kocha kwa maana anaonekana hayupo sawa”
Mchezaji mmoja aliniambia kwa upole huku akinitazama usoni mwangu.
“Sawa”
“Tunakutegemea Ethan kumbuka wewe ndio timu kapteni”
Nikanyanyuka na kumfwata kocha alipo kaa, nikavuta kiti cha pembeni na kukaa huku nikimtazama usoni mwake.
“Kocha kuna tatizo gani?”
Kocha akanitazama kwa muda kisha akashusha pumzi nyingi.
“Kuna mambo ninatafakari”
“Mambo gani kocha, unaweza kunishirikisha”
Kocha akaingiza mkono mfukoni na kutoa karatasi nyeupe na kunikabdhi. Akanyanyuka kwenye kiti alicho kikalia na kunitazama.
“Hakikisha unawapa maelekezo wezako juu ya mchezo wa kesho”
 
Kocha baada ya kuzungumza hivyo akaondoka na kuniacha nikimsindikiza kwa macho. Nikafungua karatasi hii na kuoona ikiwa imeandikwa mfumo wa jinsi gani tunavyo takiwa kucheza kesho nani aanze na nani apumzike. Nikaikunja vizuri karatasi hii na kuiweka mfukoni mwangu.
“Mukimaliza kula tukutane chumbani kwangu wote”
“Sawa”
Wachezaji waliitikia kwa pamoja huku wakionekana kujawa na furaha.
“Dokta hembu kazungumze na kocha tujue ana sumbuliwa na nini?”
“Alisha nieleza anahitaji muda wa kupumzika kidogo ndio maana nilimuacha akae peke yake”
Kocha wa timu alinijibu huku akinitazama usoni mwangu.
“Kocha msaidizi anakuja lini?”
“Kesho asubuhi”
“Sawa”
Nikamfwata Frenando alipo kaa.
“Mzee sijui ni wewe ndio umemchanganya?”
“Kivipi?”
 
“Si umemuona leo alivyo nyeshewa na mvua”
“Ohoo pale nahisi anafikiria juu ya makubaliano tuliyo wekeana”
“Yapi tena?”
“Mara moja hii umesha sahau”
“Niambie”
“Nimemuambia, anipe mwanaye kiroho safi nami nifute picha hizi la sivyo tuna haribiana”
“Hiyo unahisi ni njia sahihi ya kuanzisha mahusiano na baba mkwe wako?”
“Ethan kuna njia gani nyingine zaidi ya hiyo. Mimi nimejitahidi kadri ya uwezo wangu kuhakikisha kwamba mzee ananikubali, ila wapi. Hata golini ninavyo jituma nisifungwe magoli, si kwamba ni kwaajili ya timu hapana. Nikwaajili yake, ili aone kwamba mkwe wake nina muhitaji mwanaye ila ananiletea upuuzi tu”
 
Frenando alizungumza kwa msisitizo mkali huku akinitazama usoni mwangu.
“Achagua moja tu, mtoto kunikabidhi au nizimwage kwenye mtandao na ikitokea nimeziachia kwenye mtandao basi ukocha anapoteza, ndoa inakufa. Hata huyo mwanaye anaye hisi kunibania pia atamkosa na kiulaini nitamchukua mwanaye”
Nikamtazama Frenando kwa muda kidogo jinsi anavyo ipanga mipango yake, nikajikuta nikicheka mwenyewe.
“Nini kinacho kuchekesha?”
“Mipango unayo ipanga ni ya mbali sana pasipo kufikiria madhara kwa upande wako”
“Upande wangu madhara yake yapo vipi?”
“Tambua akiamua kukufungulia hatua za kisheria anaweza kukufunga”
 
“Wapi, ana ushahidi gani kwamba mimi ndio nimefanya tukio hilo na akitaka kunistaki usihisi kwamba nitabaki mwenyewe”
“Una maana gani?”
“Wewe ni rafiki yangu naamini watakuchunguza na wewe wakiamini huu ni mpango wetu sisi wawili, ila ni wangu mimi kama mimi. Natambua kwamba wewe una makampuni mengi sana, sasa hii inaweza kuleta skendo kubwa kama mmiliki wa makampuni amehusika kwenye urushaji wa picha za nguno mtandaoni”
Maneno ya Frenando kidogo yakanistua sana na kunikasirisha kwa kiasi ila nikajaribu kuizuia hasira yangu kwa kutabasamu huku nikimtazama usoni mwake.
“Nakutania bwana Ethan, siwezi kukuhusisha katika maswala yangu haya ya kipuuzi. Kumbuka mama yako ni waziri mkuu Mexco hata likitokea la kutokea, kesi itakwenda kufunguliwa Mexco na si hapa”
“Sawa, maliza kula twende chumbani”
“Sawa kapteni”
 
Nilipo hakikisha kwamba wachezaji wezangu wote wamepata chakula, tukaelekea chumbani kwangu. Kutokana vyumba vyetu ni vikubwa, wachezaji wote waliweza kuenea ndani ya chumba hichi.
“Habari zenu”
“Safi kapteni”
“Kesho ndio tunaanza michuano yetu rasmi. Tukumbuke kwamba tuna maadui wengi sana kwenye haya mashindano. Maadui ambao wapo tayari kuhakikisha kwamba timu yetu inatoka mapema sana kadri wao wanavyo amani.”
“Ushikamano wetu, muunganiko wetu. Ujasiri wetu na kujituma kwetu ndio misingi kamili ya kuwaangusha maadui. Tumezoeleka kuwa na mifumo minne ya kimichezo. Mifumo ambayo makocha wengine wa timu nyingine ni lazima watakuwa wamesha ifanyia kazi na kujua ni nani na nani ambaye atakabwa ili timu isitembee”
 
Nilizungumza kwa upole huku wachezaji wezangu wote wakinisikiliza kwa umakini sana. Nikatoa karatasi ambayo alinikabidhi kocha nikaifungua mbele yao na kumkabidhi mmoja wao ili atazame nini kilicho andikwa na kocha kisha amkabidhi na mwenzake.
“Tutazame haraka haraka hiyo mifumo ndugu zangu”
Karatasi hiyo ikaendelea kupita kwa kila mchezaji na hadi mwisho ikarudi kwangu.
“Mfumo huo alio panga kocha, unafahamika sana kwa kila mmoja wetu. Pia kwa wachezaji wa timu pinzani. Jambo ambalo litatusababishia kutumia nguvu nyingi sana katika kutafuta magoli na inawezekana pia tukashindwa kupata magoli.”
 
“Ninahitaji mfumo ubadilike. Sisi sote humu ndani kila mmoja anaweza kucheza nafasi zaidi ya mbili si ndio?”
“Ndio”
“Tuachane na mfumo wa 4, 4,2 tucheze mfumo wa 4,3,1,2”
“Mchezo huu utawawezesha viungo kumpa mipira Lukas. Lukasi utasimama hapo kwenye moja, na kutokana una nguvu, kasi na unaweza kukaa na mpira muda mrefu, kazi yangu mimi na Pilo itakuwa ni kupokea mipira kutoka kwako na mipira usiilete kwa njia ya pasi za chini, wataizuia sana. Ilete kwa pasi za juu. Mimi ninaweza kuruka na kuichukua hata Pinto ni hivyo hivyo. Mabeki naamini munafahamu kazi yenu. Apite mtu mpira ubaki au upite mpira mtu abaki. Nyinyi viongo wa katikati, kazi yenu ni kuhakikisha Lukas anakuwa huru, kabeni watu wasielekee kwa mabeki. Kipa, sina wasiwasi na Frenando. Mumenielewa jamani”
 
“Ndio kapteni”
Wachezaji wezangu wakapiga makofi wakionyesha kukubaliana nami katika hili nilio waambia.
“Mwenye swali?”           
“Kampteni je mfumo huu ukituwia ugumu tunafanyaje?”
“Tutakuwa tunabadilisha mifimo ya uchezaji kila baaada ya dakika kumi. Tuanze na mfumo wa kawaida wa 4,4,2 kisha tutabadilika kadri mchezo unavyo zidi kwenda. Kikubwa ninacho kitegemea ni kasi, na Pinto yake mambo yako ya ubishoo wa kupiga chenga ukiwa golini ukitegemea penati sitaki kuyaona. Ukifika golini piga shuti golini, na kipa atajuana yeye mwenyewe na mpira wake. Sijui umenielewa Pinto?”
 
“Nimekuelewa kocha”
“Weweee mimi sio kocha ni kapteni”
Kauli yangu ikawafanya wanafunzi wachezaji wezangu kucheka. Gafla mlango wetu ukafunguliwa na sote tukastuka, akaingia daktari wa timu huku akionekana kujawa na wasiwasi.
“Kuna nini?”
“Njooni kocha amejinyonga”
Kauli ya daktari ikatufanya tutoke humu ndani kwa kasi sana na kikimbilia chumbani kwa kocha, kitendo cha kuingia ndani humu nikajikuta miguu ikiniishia nguvu kabisa kwani ni kweli kocha amejinyonga bafuni kwenye bomba kubwa la maji kwa kutumia tai yake.

==>>ITAENDELEA KESHO

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 128 na 129 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA- 0657072588
ILIPOISHIA     

Nilizungumza huku nikifunga kiwambo cha kuzuia sauti kwenye bastola yangu, nikajisogeza kwenye mti mwingine taratibu pasipo wao kuweza kuniona. Kitendo cha mwanajeshi mmoja kunyanyua simu yake ya upepo na kuhitaji kuwasiliana na wezake ikawa ni kosa kubwa kwangu kwani sikuwa na jinsi ya kufanya zaidi ya kumuua mwajeshi huyu kwa kumpiga risasi ya kichwa jambo lililo mfanya mwenzake kubaki akiwa ameduwaa asijue hata cha kufanya kwani mkononi mwake hana hata silaha ya kujitetea.
   
ENDELEA       
Nikajitokeza kwenye mti huu huku nikiwa nimeishika bastola yangu nikimuelekezea mwanajeshi huyu. Kwa ishara nikamuamrisha anyooshe mikono yake juu, akafanya hivyo tena kwa haraka sana, huku mwili mzima ukitetemeka.
“Weka vitu vyote mulivyo toa ndani ya hili begi”
 
Nilijaribu kuzungumza kisomali, japo ninachapia baadhi ya maneno ila nina imani mwajeshi huyu ameelewa nilicho muambia. Kwa haraka akaanza kuingiza kitu kimoja baada ya kingine nilipo hakikisha kwamba amemaliza kuviweka vitu hivi, nikamuomba begi langu. Akanikabidhi, taratibu nikalivaa mgongoni mwangu. Nimamtazama jinsi mikono inavyo lowanisha shuruali yake, roho ya huruma ikaanza kunitawala, ila nikimuacha hai huyu naye inaweza kuwa tatizo. Nikampiga risasi moja ya kichwa na kumfanya aanguke chini na kupoteza maisha yake hapo hapo.
“Dany kwa nini na huyo umemua?”   
“Sikuwa na jinsi muheshimiwa raisi, ninafanya kile ninacho kiona ni bora kwa hii opareheni”
“Sawa”
 
Nikaitazama PDA yangu na kuanza kuitafuta ramani ya kuelekea katika kambi ya Al-Shabab, kutoka hapa nilipo kuna umbali wa kilomita tano, ambazo nilazima nitembea ndani yam situ huu hadi kufika hapo. Nikaianza safari huku nikiwa makini sana kuhakikisha kwamba sikutani na wanajeshi wa serikali wanao fanya opareheni kwenye huu msitu ambao hata sifahamu jina lake. Saa yangu ya mkononi ikanionyesha ni saa kumi na moja kasoro alfajiri, nikazidi kusonga mbele ili kwamba nitumie muda mwingi sana katika kutembe ili hata kama asubuhi itanikuta kwenye huu msitu basi ninaami nitahakikisha kwamba ninakaa ndani ya huu msitu hadi usiku ili niendelee na uvamizi wangu katika kambi ya Al-Shabab, kwani kwenda mchana ni hatari kwa maisha yangu.
 
Hadi kuna pambazuka bado nipo ndani ya huu msitu ulio jaa vilima pamoja na mawe mengi, kwa mara kadhaa nilipumzika ili hata jioni ikifika nisiwe nimechoka sana. Katika siku ninayo ona masaa yanakwenda taratibu ni hii ya leo sikukuata tamaa zaidi ya kuzidi kusonga mbele.
“Dany umebakisha muda gani kuweza kufika katika ngome ya Al-Shabab?”
“Kama nusu kilomita muheshimiwa. Nitahitaji kufika usiku kwa maana mchana huu ni hatari kwangu”
“Sawa jukumu lote lipo juu yako, vikosi vya anga vinasubiria amri yako”
 
“Sawa muheshimiwa raisi”
    Pole pole ndio mwendo, kweli usemi huu kwa siku ya leo kwangu umeweza kukamilika, kwani hadi inafika usiku saa mbili, nikawa nimefanikiwa kufika jangwani ilipo kambi ya Al-Shabab, nikaanza kutemeba sasa kwa tahadari katika jangwa hili kwa maana katika ngome ya Al-Shabab kuna minara ya wanajeshi wanao kaa kwa juu na wanamuona mtu wa mbali sana anapo karibi kufika katika ngome yao. Nikafika kwenye moja ya kichuguu cha mchanga, nikapanda juu na kulala taratibu. Nikaitoa bunduki yangu moja kwenye begi na kuanza kuiunganisha kipande kimoja baada ya kingine. Ilipo kamilika, nikaifunga lensi ambayo inaniwezesha kumuona mtu wa mbali kwa ukaribu mkubwa sana. Uzuri lensi niliyo ifunga inatumika kuona mtu hata akiwa gizani, haina tofauti sana na miwani zinzo tumika usiku.
Nikafanikiwa kuona mmnara mmoja kwa sehemu ninayo tokea, huku taa kubwa likiwa lina mulika eneo zima huku likizunguka zunguka. 
 
“Muheshimiwa raisi oparesheni imeanza”
“Kazi njema Dany”
“Asante”
Nilipo hakikisha kwamba nimemuweka mwajeshi mmoja wa Al-Shabab katika tageti yangu, taratibu nikafunga kiwambo cha kuzia sauti, kisha taratibu nikavuta triga ya bunduki yangu na ninakiruhusu riasi kutoka kwa kasi, wala haikumaliza sekunde mbili mwajeshi huyu aliye kaa juu ya mnara kwenye kibanda kidogo akaanguka chini. Nikatazama eneo lote la karibu sikuona mwanajeshi yoyote, nikaishika bunduki yangu hii ambayo ni nzito kiasi, nikaanza kukimbia nayo huku nikiwa makini sana kitazama mbele. Nikafanikiwa kufika kwenye ukuta wa ngome wa hii kambi, nikatoa kamba yangu ndefu kwenye begi ikiwa na nanga ndogo yenye ncha zilizo kikunja tatu. 
 
Nikairusha juu ya ukuta kwa kutumia nguvu zangu zote, nikajaribu kuivuta, haikuweza kushuka chini, nikaiuvaa mkanda wa bunduki yagu mgongoni, huku beg langu nalo pia likiwa mgongoni, nikaanza kupanda ukuta huu mrefu kwa kasi ya ajabu huku nikiwa makini sana. Cha kumshukuru Mungu nikafanikiwa kufika juu kabisa ya huu ukuta. Nikachuchumaa kwa umakini sana huku nikitazama kwa ndani, wanajeshi wapo doria na nina imani hakuna hata mmoja ambaye anaelewa juu ya uwepo wangu humu ndani. Nikaanza kuivuta kamba yangu kwa haraka huku nikiikunja, ili kufuta ushahidi hata kama ikitokea wanajeshi wanao fanya doria nje ya hii ngome wasiikute.
 
“Nipo ndani muheshimiwa raisi, waambie timu ya wanajeshi mia moja wawe karibu kabisa”
“Sawa ndani ya dakika kumi na tano watakuwa maeneo ya karibu.”
“Sawa mimi ninaelekea moja kwa moja kwenye nyumba anayo ishi mkuu wao”
“Sawa”
Uzuri katika huu ukuta kwa huku ndani kuna ngazi za kushukia, taratibu nikaanza kushuka katika hizi ngazi, nikafanikiwa kufika chini pasipo mtu yoyote kueweza kuniona. Nikaanza kueleka katika nyumba anayo ishi baba Hawa, na uzuri ni kwamba eneo nililo ingia lipo karibu kabisa na ilipo nyumba ya baba Hawa.
 
Nikafika katika gorofa analo ishi baba Hawa, nikavua begi langu nikalificha kwenye moja ya maua mengi makubwa katika bustani iliyopo nyuma ya hili gorofa, nikabakiwa na bastola yangu pamoja na magazine za kutosha. Nikaanza kupanda kwa umakini kwa kutumia bomba la maji machafu lililo tengenezwa kwa chuma kizito. Nikafanikiwa kufika juu, taratibu nikasogeza dirisha hili la kioo, nikasikia miguno ya mapenzi ikitokea ndani ya hichi chumba. Nikachungulia vizuri nikamuona baba Hawa na Yudia wakila oroda huku mzee wa watu akijitahidi kuzungusha kiuno chake kwa utamu wa kum** anao pewa na Yudia. Nilipo muona mzee anazidi kuzungusha kiuno nikajua huu ndio wakati wa yeye kuweza kufunga goli hata la mkono. Nikaingia kupitia hapa dirishani ambapo ni dirisha la kioo na halina nando hata moja. Hadi ninasimama mbele ya kitanda chao ndio baba Hawa anamaliza kushangilia goli lake.
 
“Dany”       
Yudia akawa mtu wa kwanza kukurupuka kitandani baada ya kuniona, baba Hawa akajaribu kuiwahi bunduki yake iliyopo pembeni ya kitanda chake, nikampiga risasi ya baga na kumfanya aanguke chini.Yudia akatulia kimya huku mwili mzima ukimtetemeka.
“Musiye mpenda amefika, muna la kuzungumza?”
Niliwauliza kwa ukali huku baba Hawa, akijitahidi kunyanyuka chini alipo angukia.
 
“Dany nakuomba unisamehe, haikuwa dhamira yangu ku…..kuu”
Yudia alizungumza kwa woga sana kwani uwepo wangu ndani ya chumba chao hawakuutegemea kabisa.
“Dany tunawahitaji wazima wote wawili”
Niliisikia sauti ya muheshimiwa raisi akizungumza kwa upole, hapakuwa na mtu yoyote aliye weza kuisikia ndani ya hichi chumba zaidi yangu peke yangu.
“Yupo wapi Hawa?”   
“Umempa nini mwanangu mshenzi wewe”
Nikampiga risasi ya mguu baba Hawa na kumfanya agugumie kwa maumivu makali sana.
“Nimewauliza Hawa yupo wapi?”
 
“Ha…aha…awa. Nimemfu…ngia kwenye chumba chake”
“Muheshimiwa raisi, ninawaomba waingia, ila wahakikishe kwamba Hawa mtoto wa huyu firauni hapa wanamuoko”
“Nimekupata Dany, timu itaingia ndani ya dakika moja”
“Mshenzi unashirikiaana na wamarekani, wanakupa nini?”
Baba Hawa aliendelea kuzungumza huku akiwa ameyakaza meno yake kwa maumivu makali. Ndani ya dakika moja nikaanza kusikia milipuko huko nje pamoja na milio ya risasi ikirindima. Baba Hawa na Yudia wakazidi kuchanganyikiwa kwani kitu kinacho tokea hapa kinakwenda kuwashusha chini kwenye maisha yao yote.
Sikujaribu hata kukwepesha mboni ya macho yangu katika kuwaangalia baba Hawa na Yudia, ambao wote kwa pamoja wapo uchi kama walivyuo zaliwa. Galfa mlango ukafunguliwa kwa nguvu wakaingia wanajeshi wawili wa Al-Shabab, naamini wamekuja kwa ajili ya kumuokoa mkuu wao. Kwa haraka nikalala chini na kuwapiga risasi wakiwa katika harakati za kuingia ndani humu. Yudia akanirukia kutoka kitandani akiwa na kishu mkononi mwake. Kwa haraka kawahi kuishika mikono yake yote ili siku chake kisitue shingoni mwangu alipo kielekezea.
 
“Toka humu ndani mpenzi”
Yudia alizungumza huku akimuomba baba Hawa atoke ndani humu, ambaye taratibu akajitahidi kunyanyuka kutoka chini alipo kaa. Kusema kweli Yudia ana nguvu za mikono ambazo si rahisi kwa wanawake wengine kuwa nazo. Yudia akazidi kutumia nguvu katika kukishusha kisu chake, ila taratibu nikaanza kupata mafanikio ya kuigeuza mikono yake taratibu huku akinibana mbavu zake kwa miguu yake japo yupo uchi kabisa ila hakuna anaye jali utupu wake.
 
Nikamuona baba Hawa akitika katika chumba hichi huku akitembea kwa kwa kuchechemea, nikabana pumzi, nikaanza kunyanyuka chini nilipo lala chali huku Yudia akiwa amenikalia kiunoni mwangu. Nikafanikiwa kusimama nikatazama katika hichi chumba nikaona meza moja ya kiooa, nikatembea kwa mwendo wa taratibu huku nikiendelea kusikilizia maumivu ya mbaviu zangu zinavyo banwa na miguu ya Yudia aliyo izungusha kiunoni mwangu, huku mikono yangu ikiwa na kazi ya kukizuia kisu anacho hitaji kunichoma shingoni mwangu. Kwa Nguvu nikamshusha kwenye meza hii hadi ikavunjiaka na sote tukajikuta tukiwa tumeangukia kwenye hii meza ial Yudia ndio aliye tangulia chini kwa kuutanguliza mgongo wake. Yudia akapote nguvu ya kuhimili kukikamata kisu chake, ikawa ni rahisi kwa mimi kuweza kukishika kishu chake kwa mkono wangu wa kulia huku mkono wake wa kushoto ukiwa umeibana shingo yake kwa nguvu zangu zote.
 
“Imeisha sasa Yudia tutaonana ahera”
Kwa nguvu zangu zote nikakishusha kisu nilicho kishika kwenye sehemu zake za siri na chote kikazama ndani na kumfanya Yudia kutoa macho kwa maumivu makubwa. Sikutaka kuishia hapo nikachomoa kisu hicho kilicho jaa damu, nikakiandamiza kifuani mwake kwa nguvu, nikarudia kukishusha kwa mara nyinine ya pili. Mauaji ya familia yangu ya kikatili yakaanza kujirudia kichwani mwake.
“Ahahahahahahahahaaaaaghaaa”   
Nilijikuta nikipiga kelele kwa nguvu na uchungu mkubwa huku nikikata kichwa cha Yudia pasipo huruma ya namna yoyote, damu nyingi zikanimwagikia kuanzia usoni mwangu ila sikulijali hilo hadi nilipo hakikisha kwamba nimekitenganisha kichwa na mwili.
“Dany Dany Dany”   
Niliisikia sauti ya muheshimiwa raisi akiniita, sikumjibu kitu chochote zaidi ya mwili wangu kunitetemeka sana baada ya kuona nimekitengenisha kichwa cha Yudia na kiwiliwili cha mwili.
 
“Dany unatakiwa kutulia tafadhali, tulia Dany upo kwenye oparesheni unatakiwa kuiendelea, tafahdali tulia Dany”
Kumbukumbu ya Yudia jinsi nilivyo mkuta akicheza sebleni siku nilipo toka kulala hoteli ya mtendelea ikaanza kunijia kichwani mwake, uzuri alio barikiwa na mwenyezi Mungu ambao kusema kweli ulinipagawisha leo hii ndio umefikia mwisho tena kwenye mikono yangu. Nikajikuta nikizidi kutetemeka mwili wangu kwa woga sana, ni kazi rahisi kumuua mtu ambaye hujawahi kuwa naye kwenye mahusiano hata ya urafiki, ila ni ngumu sana kumua mtu ambaye ulisha wahi kuwa na mahusiano naye hata ya urafiki.
“Dany hadi sasa hivi tatufahamu ni wapi alipo mkuu wa Al-Shabab, tunakuomba uweze kurudi kwenye hali yako ya kawaida utusaidie kumpata huyu mzee”
“Muheshimiwa raisi”
Niliita taratibu huku machozi yakinimwagika usoni mwangu.
“Ndio Dany”
 
“Siwezi kuendelea na hii kazi”
“Hapana Dany, kumbuka kwamba hawa watu ndio walio kuulia wazazi wako, hawa ndio walimchinja dada yako Diana, hawa ndio walimchinja malaika wako mwanao Diana ambaye hakuwa na hatia yoyote, hawa ndio walio mchinja Mama yako na hawa ndio walio mteketeza mama wa mwanao, ni wakati wako sasa kuhakikisha kwamba wanalipa kwa damu za watu walio kufa pasipo makosa ya aina yoyote. Nyanyuka pambana, kumbuka uliniahidi kwamba uliniahidi kwamba utapambana hadi dakika ya mwisho na wala huto niangusha katika hili. Dany wewe ndio tegemezi langu kwa sasa, nimeiweka nchi yangu kwenye rahani ipo mikononi mwako. Akoa mamilio ya Wamarekani, okoa mabilioni ya Waafrika amba kila siku wanakufa kwa kunyanyaswa na majeshi wa kundi hili, watoto, wanamama wanakuwa wakimbizi kwenye nchi zao kwa ajilili ya hawa watu. Tafadhali Dany pambana”
 
Nilimsikia raisi anavyo zungumza kwa uchungu, huku sauti yake dhairi ikionyesha kwamba anamwagikwa na machozi. Nikaitazama bastola yangu iliyo anguka pembeni taratibu nikaichukua bastola yangu huku nikinyanyuka, nikazitazama damu zilizo mwagika chini za baba Hawa. Kwa haraka nikaanza kuzifwata sehemu zinapo elekea kwa kuzitazama kwa umakini. Damu hizi zikazidi kuniongoza, nikaanza kushuka chini kweneye ngazi za hili gorofa. Damu hizi zimeingia kwenye chumba kimoja, kwa haraka nikaupiga tege mlango wa chumba hichi na ukafunguka. Katika chumba hichi kuna ngazi zinazo elekea chini na kuna mwanga wa taa ndani ya chumba kilichopo chini ya ardhi. Kwa haraka nikaanza kushuka huku nikiwa bastola yangu.
Nikaona kordo ndefu iliyopo chini ya hii ardhi, michuruziko ya damu inaelekea mbele, nikaanza kukimbia huku nikiifwata kwa umakini sana.
 
    Nikazidi kuongeza kasi kukimbiza kuelekea mbele kuhakiksiha kwamba ninampata baba Hawa, na kichwani mwangu sifikirii tena kumpa nafasi ya yeye kuweza kuishi na nikimpata nitahakikisha kwamba ninamuua kama nilivyo fanya kwa Yudia. Nikajibanza kwenye moja ya kona huku nikisikilizia miguu ya watu wanao kimbia kusonga mbele, nikachungulia taratibu, nikamuona Stive, Hawa, baba Hawa pamoja na wanajeshi wengine wanne wa Al-Shabab wakisonga mbele. Huku wanajeshi hao mara kwa mara wakiwa wanatazama nyuma kuimarisha ulinzi, kwa haraka nikapiga ishara ya msalaba huku nikishusha oumzi nyingi. Nikajitokeza na kuanza kuwafyatulia walinzi wa baba Hawa risasi ambao kusema kweli hapakuwa na hata mmoja aliye weza kujificha kwa maana sehemu waliyo kuwepo kwenye hii kordo hakuna sehemu yenye kona inayoweza kuwafanya wajifiche na mtu ambaye ninaweza kujificha ni mimi kutokana nipo kwenye kona inayo niwezesha kujibanza.
 
Nikazidi kuwaangusha walinzi wa baba Hawa ambao hawakuna na namna yoyote zaidi ya wao kuwa kizuizi cha risasi ambazo ninazipiga kwa baba Hawa, kitu nilicho weza kukigundua ni kwamba Hawa katika zoezi hili hakuweza kushiriki kabisa na anavyo onekena ameshikiliwa mateka. Stive akajiweka mbele ya baba Hawa huku bunduki yaki ikiwa imemuishia risasi baba Hawa hana bunduki yoyote, taratibu nikaanza kuwasogelea huku nikiwa nimeshika bastola yangu. Sikumuonea huruma Stive zaidi ya kumpiga risasi ya kichwa, akaanguka chini na kufa. Baba hawa kwa haraka amashika Hawa huku akiwa amempiga kabali, kadri nilivyo zidi kuwasogelea ndivyo nilizo zidi kuweza kuiona sura ya Hawa akiwa katika masikitoko makubwa sana huku machozi yakimwagika usoni mwake. Taratibu Hawa akaanza kutingisha kichwa chake akioniomba nisiwasogelee, nikayashusha macho yangu hadi kwenye mkono wake wa kushoto sikuamini macho yangu kuona alivyo shika bumo la mkono ambalo akifyatua kipini chake basi yeye na baba yake wanakwenda kulipuka na kuchanguka vipande vipande na huo ndio utakuwa ni mwisho wa maisha yao.
 
AISIIIII……….U KILL ME 129 

  
“Dany nakuomba usije karibu”   
Hawa alizungumza huku akiendelea kumwagikwa na machozi mengi sana usoni mwake.
“Hawa, tambua kwamba huna makosa yoyote, baba yako ndio ninaye muhitaji hapa. Tafadhali mke wangu, ninakuomba usifanya hicho unacho hitaji kukifanya kwa sasa”
Nilizungumza huku machozi yakinimwagika usoni mwangu, sikutaka kusimama kama Hawa alivyo hitaji, nikazidi kutembea na kumsogelea ila bunduki yangu nikiwa nimeishika mkononi mwangu.
 
“Hawa nahitaji uishi karibu nami, nahitaji uwe mama wa watoto wangu, nahitaji tujenge familia, kumbuka fika mimi ndio mwanaume wako wa kwanza kuweza kuona mauongo yako ya ndani, ninafanya kila kitu kuhakisha kwamba ninakutunza, nina linda penzi lako, sina haja ya kuwa na mwanamke mwengine kama unanipenda ninakuomba usifanye chochote kibaya cha kukudhuru wewe”
“Hawa usimsikilize huyu ni muongo, lipua mwanangu bomu tufe”
Baba Hawa alizizungumza huku akiendelea kumkaba kabali Hawa, huku akiwa amejificha nyuma yake na ni ngumu sana kwa mimi kuweza kumpiga risasi baba Hawa kwani Hawa ndio kizuizi chake.
“Hawa kumbuka ni mangapi tuliyapanga, kwa nini unahitaji yaishe kwa namna hii, kwa nini unahitaji maisha yaende namna hii, tafadhali Hawa ninakuomba sana mke wangu”
“Mwanangu huwezi kufa mikononi mwa Wamarekani, anakudanganya huyo ni mjinga mshenzi, kumbuka mama yako hata huko mbinguni anasubiri kuwa pamoja nasi, lipua bomu”
 
Baba Hawa alizidi kuzungumza kwa msisitizo na kuzidi kumfanya Hawa amwagikwe na machozi mfululizo. Hawa akanitazama kwa macho yaliyo jaa huruma sana, kwa nguvu akamgeukia baba yake na kumkumbatia, mkono ulio shika bomu nikaona akiuingiza kwenye koti hili alilo vaa baba yake. Hawa akamsukumia baba yake pambeni na yeye akakimbilia upande wangu na sote tulalala chini huku nikiwa juu yake nikimfunika. Mlipuko mkubwa ukatokea huku vipande vya nyama nyama pamoja na damu vikiniangukia mgongoni mwangu.
Taratibu nikageuka na kutazama eneo alilo simama baba Hawa, nilicho kiona kimesalia ni kobazi alizo kuwa amezivaa tu, tena nazo zimekatika katika. Hawa akaka kitako huku akilia kwa uchungu sana, kwa nguvu nikamkumbatia huku nami machozi yakinimwagika.
 
“Yameisha mke wangu”
Nilizungumza huku nikimkumbatia kwa nguvu Hawa.
“Dany nimemuua baba”   
“Hapana baby ilibidi iwe hivyo tu”
Nilizungumza huku nikiendelea kumkumbatia Hawa kifuani mwake.
“Dany kazi nzuri”
Niliisikia sauti ya muheshimiwa raisi akizingumza nami. Taratibu nikasimama, nikamsaidia Hawa kusimama, kwa mikono yangu miwili nikambeba Hawa na kuanza kutembea naye kuelekea nje. Tukakutana na baadhi ya wanajeshi wa Kimarekani ambao tayari wamesha weza kuiweka ngome chini ya ulinzi mkali, huku wanajeshi wengi wa baba Hawa wakiwa wameuwawa. Mwanajeshi mmoja akanisaidia kumbeba Hawa na kumuwahisha katika gari la jeshi linalo shuhulikia wagonjwa.
“Muheshimiwa raisi unanisikia?”   
“Ndio Dany ninakusikia”
“Ninakuomba mke wangu Hawa umlinde kwa kila jinsi yeye ndio furaha yangu na wala siweza kuwa na furaha nyingine zaidi yake yeye”
“Nakuahidi Dany, nitahakikisha kwamba ninamlinda mpenzi wako, na hakuna jambo lolote litakalo mfika”
“Nashukuru muheshimiwa raisi, ninakuambini katika hilo”
Nikamtazama Hawa aliye lazwa kwenye kitanda cha wagonjwa, huku madaktari hawa wa jeshi wakiendelea kumpa huduma ya kwanza.
“Dany”
 
Hawa aliniita kwa sauti ya upole sana huku akinitazama usoni mwangu.
“Ndio mke wangu”
Nilizungumza huku nikiinama taratibu huku nikimtazama Hawa usoni mwake.
“Umefanya kazi kubwa sana”
“Bila ya wewe kuwa moyoni mwangu wala nisinge weza kuifanya hii kazi peke yangu, nimefanya haya yote kwa ajili yako mke wangu”
“Natambua hilo Dany, ninakupenda sana”
“Ninakupenda pia mke wangu”

“Dany, tunatakiwa kumpeleka mke wako hospitali kwa matibabu zaidi”
Mwanajeshi mmoja alizungumza huku akiwa amesimama mbele yangu, taratibu nikauchanisha mdomo wangu na mdomo wa Hawa.
“Munampeleka hospitali gani?”
“Katika kambi yetu ya Jeshi hapa Somali”
“Sawa”
 
Wanajeshi hawa wakambeba Hawa katika kitanda hichi cha wagojwa, wakamuingiza katika helicopter moja kati ya Helicopter nne za jeshi zilizopo katika hili eneo na taratibu ikaacha ardhi na kuondoka.
“Muheshimiwa raisi, oparesheni ya kufuta jeshi la Al-Shabab, imekwisha”
“Nashukuru Mungu. Dany sasa unaweza unaweza kwenda kwenye kambi ya jeshi la Marekani hapo Somalia”
“Sawa muheshimiwa raisi, ila inabidi kuendelea na opareshni ya kuwasaka Boko Haramu”
“Ni kweli ila unabidi upumzike kidogo”
“Sawa muheshimiwa raisi”
Nikaingia kwenye moja ya helicopter safari ya kuelekea katia kambi ya jeshi la Marekani hapa Somalia ikaanza. Sikuamini kwamba nimeweza kulipiza kiasi changu kwa asilimia ishirini na tano na hadi sasa hivi nimebakisha alisiliami sabini na tano ambazo bado sijafahamu kwamba ninazimaliza vipi. Hatukuchukua muda mwingi sana tukafanikiwa kufika katika kambi ya jeshi la Marekani hapa Somali.
“Ninahitaji kumuona mke wangu”
Nilimuambia mkuu wa hii kambi aliyo kuja kunipokea hapa.
“Sawa twende huku”
Tukapanda katika gari ndogo ya jeshi ambayo haijafunikwa kwa juu. Tukaondoka katika eneo hili la uwanja wa ndege za kijeshi. Kambi hii ina majengo mengi sana na ulinzi wake ni mkali sana.
 
“Umefanya kazi nzuri Dany”
“Nashukuru”
“Wewe utaifa wako ni Tannia?”
“Ndio”
“Kwa nini usichukue uraia wa Marekani, na ukafanya kazi chini ya Marekani?”
“Hahaaa, mimi ni muafrika na ni Mnzania halisi, kwa hiyo siwezi kubadilisha utaifa wangu”
“Sawa ni ombi tu niliko kuwa nina kuomba”
“Nimekuelewa meja”
Tukafika kwenye moja ya jengo, tukashuka kwenye gari hii, Tukaongozana hadi kwenye moja ya chumba. Meja akanifungulia mlango na nikaingia ndani kisha yeye akabaki nje, nikamkuta Hawa akiwa amelala kitandani huku ametundikiwa dripu la maji. Taratibu nikavuta kiti kilichopo karibu na kukaa karibu yake huku nikimtazama osoni mwake.
“Unaendeleaje mke wangu?”
“Safi tu”
Nikavua kinasa sauti sikioni mwangu na kukiweka mfukoni mwangu, nikavua pia kofia yangu na kuiweka pembeni.
“Pole honey”
“Asante mke wangu, vipi wamekuambia una tatizo gani?”
“Ni maji tu yamepungua mwilini mwangu, ila kila kitu kipo vizuri”
“Nafurahia kusikia hivyo”
“Vipi uliweza kumdhibiti Yudia?”
“Ndio, niliweza kumdhibiti, na kwa sasa amekufa”
Taratibu Hawa akashusha pumzi yake, akanishika mkono wangu wa kulia na kuuweka kifuani mwake.
 
“Moyo wangu kwa sasa una amani sana kwa sasa, umenifanya maisha yangu kubadilika. Kwa sasa Dany ninacho kifikiria ni kuwa mama, na  mimi nina hitaji kuwa mwanamke mwenye familia yangu, watoto wangu”
Hawa alizungumza kwa hisia kali sana huku akiwa amejawa na tabasamu zuri usoni mwake, lililo nifanya na mimi kujihisi furaha kubwa.
“Nashukuru kwa kulifahamu hilo mke wangu, nitahakikisha ninakulinda wewe hadi mwisho wa maisha yangu”
“Asante baby”
Nikambusu Hawa kwenye paji la uso wake na furaha kubwa ikazidi kutawala katika mioyo yetu na ninaamini kwamba ukurasa mpya wa maisha umefunguliwa katika maisha yetu. Hawa akaniomba nikilaze kifua changu kifuni mwake, nikafanya hivyo, usingizi kwa mbali ukaanza kunipitia na kujikuta nikilala fofofo.
“Dany, Dany”
“Mmmm”
“Kumekucha mume wangu”
Hawa alizungumza na kunifanya ninyanyue kichwa changu. Nikamkuta nesi akiwa amesimama pembeni yetu
“Umeamkaje mke wangu”
“Nipo poa, nesi anahitaji kunihudumia”
“Ahaa”
 
Nilizungumza huku nikinyanyuka, nikaanza kujinyoosha viungo vyangu kwa maana nimechoka sana kwa kazi ngumu niliyo ifanya kwa siku hizi nne.
“Nesi mke wangu hali yake vipi?”
“Yupo vizuri, ila maji tu ndio yalimpungua mwilini mwake”
“Sawa”
“Ila dripu hili ninalo muwekea ndio la mwisho baada ya hapa atakuwa salama”
“Sawa”
Nikasimama dirishani na kutazama nje, nikaona wanajeshi wakiwa katika mazoezi huku wengine wakikimbia mchaka mchaka katika mistari iliyo nyooka. Mlango ukafunguliwa akaingia meja wa jeshi aliye nipokea jana.
“Habari za asubuhi Dany”
“Salama”
“Kuna simu yako kutoka kwa muheshimiwa raisi”
“Naiomba”
Nikaichukua simu ya mkononi aliyo kuja nayo huyu meja, niakiweka sikioni mwangu huku nikimtazama Hawa usoni mwake.
 
“Muheshimiwa raisi”
“Habari za asubuhi kwa uko Somalia?”
“Salama muheshimiwa raisi”
“Sasa kazi ya kwenda nchini Nigeria imeanza ila nitahitaji uwende kama mpelelezi, na kazi ya kuhakikisha kwamba unagundua ni wapi makao makuu ya Boko haramu itakuwa mikononi mwako”
Taratibu nikashusha pumzi huku nikimtazama Hawa usoni mwake.
“Sawa muheshimiwa raisi”
“Ila Dany nina ombi moja?”
“Ombi gani?”
“Katika hii oparesheni, mke wako Hawa aweze kuhusika nina imani atakuwa anafahamiana hata na baadhi ya viongozi wa kundi hilo na itakuwa ni rahisi sana kwenu katika hii kazi”
“Ila muheshimiwa raisi, mke wangu kwa sasa hali yake sio nzuri sana ya kuweza kumfanya aifanye hii kazi”
“Dany”
Hawa aliniita huku akinitazama usoni mwake.
“Naomba nizungumze na muheshimiwa raisi”
“Sasa hivi?”
 
“Ndio”
Nikamtazama meja pamoja na huyu nesi, nikamsogela Hawa.
“Muheshimiwa raisi mke wangu anahitaji kuzungumza na wewe”
“Mpe simu”
Taratibu nikampa simu Hawa, akaweka loudspeaker na kutufanya sote tusikie mazungumzo yake na raisi.
“Muheshimiwa raisi sasa unazungumza na mrs Dany”
“Ndio Mrs Dany, nimemuomba mume wako muweze kuungana naye katika oparesheni ya kwenda nchini Nigeria, huko mutakuwa katika uchunguzi wa kufwatilia kundi zima la Boko Haramu, nina imani kwamba unaweza kufahamu baadhi ya viongozi ambao wanamiliko kundi hilo”
 
Nesi akatoka ndani ya chumba hichi na kutuacha sisi watatu.
“Nimekuelewa muheshimiwa raisi, ninamfahamu mtoto wa kiongozi mkuu wa hilo kundi, naamini kupitia yeye kazi inaweza kukamilika kwa kiasi fulani”
“Nashukuru kusikia hivyo mrs Dany”
“Ila mimi sinto kwenda, nitatoa maelekezo ambayo nina imani kwamba mume wangu anaweza kuifanya hii kazi pake yake”
Kidogo nikajikuta nikishusha pumzi nikimshukuru Mungu kusikia kwamba Hawa hato jihusisha kabisa na oparesheni hii.
“Sawa mrs Dany ni maelekezo yapi hayo?”
“Kwa sasa siwezi kuyatoa, hadi niweze kuwa katika sehemu salama na ya kuaminika”
“Sehemu gani unahitaji kuwa Mrs Dany?”
“Ninahitaji kuishi kwa kipindi chote cha hii oparesheni ya mume wangu hapo ndani ya ikulu yako, naamini Dany atakuja kunichukulia hapo akimaliza kazi yake.”
Maeno ya Hawa yakatufanya mimi na meja kutazamana kwani sikutegemea kama Hawa anaweza kuomba kuishi katika ikuli ya raisi wa Marekani, ambayo inasifika sana kwa kuwea kulindwa kuliko ikulu yoyote Duniani.

==>>ITAENDELEA KESHO

Wazee Wamfanyia Tambiko Dr Kigwangalla

$
0
0
NA ANDREW CHALE, NZEGA
 WAZIRI wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Jimbao la Nzega Vijijini la Mkoani Tabora, Dkt. Hamisi Kigwangalla amewashukuru viongozi mbalimbali wa dini Nchini kwa dua na maombi yao kwa kipindi chote alichopata ajali hadi sasa kupona na kurejea tena na majukumu yake.

Akizungumza katika mkutano wake wa pili uliofanyika katika Kata ya Lusu Tarafa ya Nyasa iliyopo kwenye jimbo lake hilo la Nzega Vijijini, jana Oktoba 28, 2018,  Dkt. Kigwangalla amewashukuru viongozi hao wa dini pamoja na Wazee wa Mila kwani wao wamekuwa chachu kwenye kupona kwake tokea alipolazwa Hospitali kwa zaidi ya miezi miwili kwa kuuguza majeraha ya mwili wake kutokana na ajali ya gari aliyopata Agosti 4, mwaka huu.

Amesema viongozi wa hao wa dini pamoja na  Wananchi kila mmoja kwa nafasi yake walikuwa ni wa kipekee na dua zao zimeweza kusaidia  na kwa sasa amerejea kutoa shukrani na kupokea dua zao hizo kwani kwa sasa ameanza kufanya kazi.

“Kwa sasa nimeanza kurudi kwenye majukumu yangu kama kawaida. Kwa hivyo nikaona kabla ya kuanza kuonekana nikiruka huku na kule kwenye majukumu ya kiwizara, nikasema hapana nirudi kwanza nyumbani nipate dua za wazazi wangu, dua za wazee na viongozi wa dini.

Kwa tukio lile kwa sisi tunaoamini,  ni mkono wa Mungu ulikuwa mahala pale” amesema Dkt. Kigwangalla.

Aidha, Dkt. Kigwangalla amewatoa hofu wananchi wa jimbo lake juu ya watu waliokuwa wakipitapita jimboni kwa lengo la kulinyemelea na kutoa maneno ya kumkatisha tamaa.

“Kwa waliokuwa wanatembea na wakikesha usiku kucha wakisubiri nife wameanguka. Mungu amesimama  mbele yangu, mimi ni mzima naendelea kutekeleza majukumu yangu mdogomdogo mpaka nitakapokuwa imara kabisa. Sasa naanza upya” amesema Dkt. Kigwangalla.

Pia amewahakikishia wananchi hao kuwa kazi za maendeleo ya jimbo hilo zinaendelea na wasaidizi wake wa ofisi ya Mbunge inaendelea kuratibu kwa ukaribu kabisa na  milango ipo wazi.

Katika hatua nyingine Wazee wa Mila na Watemi wakiongoza na Chifu Ng’wana Ng’washi wa Wasukuma walifanya tambiko la kichifu la kumtambikia ili akawe tayari kwa kazi za kulitumikia Taifa katika majukumu ya Kibunge na Uwaziri.

 Dkt. Kigwangalla yupo katika ziara ya kutoa shukrani na dua maalum kwa Wananchi wa jimbon lake hii ni tokea kurejea kutoka kuuguza majeraha ya mwili wake tokea kupata ajali Agosti 4, mwaka huu wakati akiwa katika majukumu yake ya kikazi Mkoani Manyara.

Mwakyembe Aagiza Wamiliki Na Wahariri Wa Gazeti la Tanzanite Wahojiwe

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb), amesema habari iliyochapishwa na gazeti la kila siku la Tanzanite la leo Jumatatu tarehe 29 Oktoba, 2018 lenye habari zenye tuhuma za kisiasa dhidi ya Viongozi kadhaa, haziakisi msimamo wa Serikali na ameagiza mmiliki na Bodi ya uhariri ya gazeti hilo waitwe mara moja Idara ya Habari (MAELEZO) kujieleza kuhusu msingi wa habari hiyo.

Dkt. Mwakyembe ametoa ufafanuzi huo leo mchana, mara baada ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuelezea kushtushwa kwake na mwenendo wa gazeti hilo kuchapisha habari zinazoibua tuhuma za kisiasa dhidi ya baadhi ya Viongozi nchini, wakiwemo Wabunge na kusababisha taharuki kubwa katika jamii.

Gazeti la Tanzanite linatolewa na kampuni ya CZ Information and Media Consultant LTD ya Dar es Salaam na leo katika toleo lake Na. 254 limeandika katika ukurasa wake wa mbele  habari yenye kichwa kinachosomeka “Vigogo 14 hatari kwa nchi watajwa” ambayo inawataja viongozi kadhaa wa kisiasa na wafanyabiashara.

TCRA Yatoa ONYO Kwa Wanaosambaza Picha na Video za Ngono Mitandaoni


Waziri wa Kilimo: Hatuwezi Kuendelea Kuagiza Sukari Wakati Tuna Uwezo Wa Kufanikisha Uzalishaji

$
0
0
Na Mathias Canal-WK, Dodoma
Serikali imeipa changamoto Bodi ya sukari nchini kutekeleza majukumu yake kwa weledi ikiwa ni pamoja na kusisitiza kuhuisha uzalishaji wa sukari kwa wingi ili kuondokana na uagizaji wa sukari kutoka nje ya nchi.

Kampuni mbalimbali za uzalishaji wa sukari nchini zimeitikia wito wa Serikali wa kuongeza uzalishaji wa sukari ili nchi iweze kujitegemea kwa bidhaa hiyo pendwa kwa matumizi ya nyumbani na viwandani na ziada jambo litalopelekea Bodi ya sukari kusimamia majukumu yake ipasavyo ili kuondokana na uagizaji wa sukari nje ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa leo jumatatu tarehe 29 Octoba 2018 na Waziri wa kilimo Mhandisi Dkt Charles Tizeba (Mb)  wakati akizungumza kwenye uzinduzi wa Bodi ya Sukari Tanzania (SBT) hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Mjini Dodoma.

Waziri Tizeba amemtaka Mwenyekiti wa Bodi ya Sukari nchini Bi Mwamini Juma Malemi na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania Prof Kenneth Michael Kitundu Bengesi Kudhibiti sukari inayoingia nchini pasina utaratibu huku akiwataka kusimamia kwa weledi ufanisi katika uongezaji wa uzalishaji wa sukari nchini.

Aidha, Dkt Tizeba alisema kuwa ufungashaji wa sukari kwenye ujazo wowote ule kwa kutumia vifungashio vya aina yoyote kama vile mifuko yenye nembo ya SUPER FINE lazima uzingatie Sheria ya Sukari Namba 26 ya Mwaka 2001 ambayo inazuia ufungashaji wa sukari bila kupata idhini ya Bodi ya Sukari Tanzania.

Alisema kuwa kwa mujibu wa Sheria hiyo ni marufuku kufungasha au kuuza sukari nyeupe kwa kuwa sukari hiyo ni kwa ajili ya matumizi ya viwandani kama malighafi na sio kwa ajili ya matumizi ya kawaida majumbani.

Alisisitiza kuwa Mtu yeyote atakayebainika kuvunja Sheria hiyo ya Sukari, atawajibika kulipa faini ya kiasi cha fedha kisichopungua Shilingi Milioni Kumi (10,000,000) au kifungo cha miaka mitatu (3) jela au vyote kwa pamoja.

“Kuna watu wanaolipa kodi ili wazalishe sukari lakini inapoingia sukari ambayo imepenya kinyemela hata ulinganifu wa soko madukani unakuwa mdogo kwa kuwa wanaoingiza bila utaratibu wanauza kwa kiasi cha chini kwa kuwa hawana uchungu wa kulipa kodi”

“Na hili sio jambo la hiara Bodi ni lazima isimame kidete kubaini mianya yote ya wafanyabiashara wanaoingiza sukari bila utaratibu” Alikaririwa Dkt Tizeba

Kuhusu sukari ya viwandani (Industial Sugar) Dkt Tizeba alisema kuwa, wafanyabiashara wamekuwa wakiomba kiwango kikubwa cha kibali cha uagizaji wa sukari lakini serikali ikihakiki kupitia kodi waliyolipa inakuwa haifanani na kiasi kilichoagizwa.

Waziri aomba radhi kuvuja kwa picha zake za ngono

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Afrika ya Kusini , Malusi Gigaba ameomba radhi mara baada ya video yake ya ngono kuvuja mtandaoni.

Waziri Gigaba amesema kuwa video hiyo ilirekodiwa kwa ajili ya matumizi binafsi ya yeye na mke wake ambapo video hizo zilivuja mara baada ya simu yake kudukuliwa na wahalifu wa mtandaoni mwaka jana.

Amesema video hiyo ilianza kusambaa mara baada ya wahalifu hao wa mtandaoni kumtaka atoe kiasi cha fedha alipochaguliwa kuwa Waziri wa fedha mwaka 2017.

Tayari taarifa juu ya wahalifu hawa zipo mikononi mwa sheria, hivyo uchunguzi wa kina unaendelea kufanyika.

Gigaba ameomba radhi kwa umma pamoja na familia yake hasa watoto wake, mama yake na mama mkwe wake kwa machungu na aibu kali aliyoisababisha kutokana na kusambaa kwa video yake akiwa faragha.

“Mke wagu na mimi tumesikitishwa na video hiyo ya ngono ambayo tulikuwa tuione sisi wawili tu kwani mawasiliano yangu ya simu yalidukuliwa mnamo 2016/17 na sasa inazungushwa miongoni mwa wanasiasa.

“Nachukua fursa hii kuomba msamaha kwa watu wengine wa familia yangu, hususan wanangu, mama yangu na wakwe zangu na wananchi wa Afrika Kusini kwa matatizo yatokanayo na jambo hili,” amesema Gigaba.

Katika video hiyo ya sekunde 13, Gigaba yuko peke yake akichezea uume wake kwa mkono na akisema: “Fikiria hiki kingekuwa mdomoni mwako.”

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya October 30

Rais Magufuli amteua Prof. Humphrey Mushi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya Ushindani- FCC

Ray Kigosi Amvaa Wema Sepetu Sakata la Video Chafu Mitandaoni

$
0
0
Muigizaji Ray Kigosi amesema Wema Sepetu anapaswa kutumia mitandao kuingiza fedha na sio kufanya mambo ya hovyo.

Ray akizungumza na Wasafi TV amesema alichofanya Wema hakuna ambaye amefurahaishwa nacho hivyo kumtaka kubadilika.

"Hakuna Mtanzania mwenye akili timamu atafurahia  yale matendo ambayo yamefanyika, huyo atakuwa ni tahira, una upungufu wa akili au atakuwa ni punguani," amesema Ray.

"Unamposti mpenzi wako mnakisi for what?, Wema ni brand kubwa abadilike asiwe na tabia ya kuomba msahaha na mambo yale yale yanajirudia atumie mitandao kuingiza pesa na sio kufanya upumbavu," ameeleza.

Hivi karibuni kulivuja video mtandao ya Wema Sepetu akiwa faragha na mtu ambaye aliwahi kutambulishwa kuwa ndiye mume wake mtarajiwa.

Video Mpya: Motra The Future ft. Marleen - Unikumbuke

$
0
0
Msanii wa muziki Bongo, Motra The Future anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake mpya uitwao Unikumbuke ambao amemshirikisha Marleen.

 Itazame hapo chini

Video mpya: Maryjane Ferdinand - KILA CHOZI LITAFUTWA

$
0
0
Tazama hapa  Video mpya ya  Maryjane Ferdinand - KILA CHOZI LITAFUTWA

Video Mpya Rudeboy ft. Efezino - Fire Fire

$
0
0
Msanii wa muziki kutokea nchini Nigeria, Rudeboy anakukaribisha kutazama video ya wimbo wake mpya mpya uitwao Fire Fire ambao amemshirikisha Efezino. 


Itazame hapo chini

Kutana na Shekhe Yassin....Mtabiri wa Nyota, Pete za Bahati, Mimba Kutoshika au Mimba Kuharibika

$
0
0
Whatsap 0743313580....KUTANA NA SHEKHE YASSINI SAIDI
Ni Shekhe aliyejaaliwa karma nyingi kutoka kwa Allah Mwenye uwezo kutatua shida mbali mbali ziwapatazo wanadamu.


Anatibu na kuponya shida mbalimbali zilizo shindikana kwa wanadamu  na kwauwezo wa Allah atakutatulia shida zako inshaalah

Shekhe yassini Saidi anatibu kutumia qur an na rukaiyah pamoja na dawa za kiarabu na za kiafrika


Je? Una Mpenzi,mchumba,mume,mke, aliye kuacha na anaishi na MTU mwingine au anakuahidi ahadi alafu hatekelezi ahadi zake 


SHEKHE YASSINI SAIDI atakusaidia
 @shekhesaidiyasini anatumia picha, au jina la muhusika na kumaliza tatizo lako.

SHEKHE YASSINI SAIDI Anatafsiri ndoto kushinda bahati nasibu, nyota,mvuto wa mwili, Miliki Pete Yabahati Kutoka Falme Kuu bila Masharti Yoyote.

Pia kwa wenye tatizo la uzazi kutoshika mimba au ukishika mimba inaharibika tatizo la nguvu za kiume
Muone @shekhesaidiyasini inshaalla kwa uwezo wake Allah atakusaidia. 


Malipo Nikama Sadaka Na Utalipa Baada Ya Mafanikio.
Wasiliana nami
@shekhesaidiyasini
Whatsapp no +255 743 313 580
Piga no +255 743 313 580
Tigo +255 653 67 1650
Airtel 0683697810

Tromex Power : Dawa Bora Na Imara Ya Nguvu Za Kiume

$
0
0
TROMEX POWER DAWA BORA NA IMARA ya   NGUVU ZA KIUME; Baada ya kufanyiwa utafiti na majaribio sasa imeingia sokoni 

Habari njema kwa tanzania pamoja na africa nzima mkombozi wa ndoa yako ni dawa anbayoitwa TROMEX. 

Dawa hii imeonyesha uwezo wa hali ya juu katka kutibu tatizo la upungufu wa nguvu za kiume ,dawa hii ni mpya na inapatikana katika clinic yetu 

Dawa hii ni dawa ya asilia ya mitishamba,mwaka juzi tuliipeleka nchini Ghana kwa ajili ya utafiti  katika utafiti ilishindanishwa na dawa zingine 4 kutoka nchi kenya, Uganda, msumbiji, pamoja na kongo, na imeonyesha asilimia 92 imeonyesha inauwezo mkubwa wa kutibu tatizo kwa mda mfupi sana 

Katika utafiti huo watu 1839 ambao walikuwa legelege walipewa dawa hii kwa ajili ya majaribio,baada ya kuitumia watu 1792 walipona kabisa na sasa wanaweza kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3 kwa wakati mmoja na watu 38 hawakupona kabisa pia watu 9 hawakurudi kuleta majibu 

Dawa hii ukiitumia itakufanya uwe na uwezo wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3 bila hamu kuisha

Dalili za upungufu wa nguvu za kiume ni kushindwa kurudia tendo la ndoa...Kutojisikia hamu ya tendo la ndoa....Korodani moja kuvimba,tumbo kuunguluma na kujaa gesi, pia inazalisha homons za uzazi kwa mwanaume ambaye mbegu zake za uzazi ni nyepesi ambazo hazina virutubisho vya kuweza kumzalisha mwanamke 

Pia inauwezo wa kufanya maumbile yawe marefu kama yameingia ndani na kuwa mafupi sana, pia inatibu magonjwa zaidi ya 6 

Itumie sasa dawa hii inapatikana katika Clinic yetu iliyopo Kawe DAR mikoani tunatuma kwa njia ya mabasi 

Ukiwa nje ya nchi tunatuma kwa njia ya EMS ..maelezo zaidi 0756726865/ 0716096205 au tembelea    www.kihembehebalist.blogspot.com

Kiboko Ya Matatizo Ya Nguvu Za Kiume,maumbile Madogo, Mvuto Wa Mapenzi ,magonjwa Sugu

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMBO ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744391089  au  0653182109

IGP Sirro Akutana Na Kikosi Maalum Kinachopambana Na Uhalifu Wilayani Biharamulo

$
0
0
Askari wa kikosi maalum kinachopambana na matukio ya uhalifu na wahalifu kama wanavyoonekana Pichani wakitekeleza majukumu yao katika eneo la Midaho wilayani Biharamulo mkoani Kagera jana 29/10/2018. Picha na Jeshi la Polisi.



Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akizungumza na askari wa kikosi maalum cha kupambana na matukio ya uhalifu na wahalifu katika eneo la Midaho wilayani Biharamulo mkoani Kagera jana 29/10/2018 wakati akiwa safarini  kuelekea wilaya ya Ngara mkoani humo kwa ziara ya kikazi. Picha na Jeshi la Polisi.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images